Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104687 articles
Browse latest View live

Makonda atimiza ahadi yake kwa Polisi, akabidhi tani 60 ya saruji Dar

$
0
0

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda leo Juni 24/ 2018 ametimiza ahadi yake kwa Jeshi la Polisi aliyoitoa hivi karibuni kwa kuwakabidhi shehena ya Mifuko 1,200 ya Saruji sawa na Tani 60 yenye thamani ya shilingi Milioni 14 kwa Askari Bora 12 waliochaguliwa na Jeshi la Polisi kutokana na utendaji kazi mzuri. 

Makonda amesema lengo la kutoa zawadi hiyo ni kujenga morali ya kazi kwa askari wanaojitoa kwa hali na Mali kulinda usalama wa Raia na Mali zao jambo linalopelekea Dar es salaam kuwa Shwari. 

Mifuko hiyo ya Saruji imetolewa na kampuni ya Nabis Cooperate Ltd iliyounga mkono jitiada za Makonda katika kugusa maisha ya Wananchi katika masuala mbalimbali. 

Aidha Makonda amesema pamoja na kuendelea kuliboresha Jeshi la Polisi Kama taasisi kwa kuwapatia vitendea kazi  Kama Magari, Pikipiki, Baiskeli na Computer pia ameona ni vyema kugusa maisha ya askari mmojammoja kwa kuhakikisha wanakuwa na makazi zao na familia  ili familia ijivunie kazi anayoifanya Baba au Mama. 

Hadi sasa Makonda amewezesha zaidi ya askari Polisi 800 kupata mikopo ya viwanja vya bei nafuu. 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kampuni ya Nabis Cooperate Ltd Eng. Thomas Wiso amesema kuwa wameamua kutoa saruji hiyo kuunga mkono jitiada za Makonda kujali wananchi wake na kuhakikisha hali ya Ulinzi na usalama inakuwa Shwari.

Dawa Bora za Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo la Ndoa

$
0
0

Baada ya utafiti wa muda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka sasa 

MWASELE HERBAL CLINIC. inakuletea suluhu juu ya matatizo haya kwa kutumia dawa za  

FULL POWER .ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu zakiume. dawa hii ina mchanganyiko wa kutosha kuzalisha vichocheo vingi vya hormone za gestrogen ziwemo vitamin B6&B1, vitamini E pamoja madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na muzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi na kuchelewa kufika kileleni zaidi ya dakika 20-30. ZAT 50 inarudisha maumbile ya uume yaani kurefusha na kunenepesha ulefu nchi 3-7, upana cm, 3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukitumia maumbile yatabaki kuwa hivyo siku zote . pia tunatibu matatizo mengine kama presha, kisukari , ngiri ,chango la tumbo,tumbo kujaa gesi, kutokupata choo vizuri,miguu kuwaka moto,matatizo ya uzazi, bawasili namagonjwa yazinaa kama kisonono nakaswende.  

Tunapatikana DAR ES SALAAM. SHINYANGA NA ZANZIBAR. kwa wakazi wa dar es salaam utaletewa huduma hii popote ulipo . wa mikoani tunawatumia kwanjia ya mabasi .  

Wasiliana nasi kwa sim no 0717702227 au 0754568767.DR . SAGUDA nyote mnakaribishwa

Hali ilivyo kwa Hamisa Mobetto Baada ya Kusikia Baba Mtoto wake Majizzo Anamuoa Lulu Michael

$
0
0

Msanii wa Bongo movie na mzazi mwenza wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Hamisa Mobetto ameweka wazi kuwa hana kinyongo na kutoa baraka zote kwa ajili ya ndoa ya Lulu na Majizzo.


Hamisa ambaye  amewahi kuwa kwenye Mahusiano na Majizzo siku za nyuma na  kuzaa naye mtoto mmoja ameweka wazi kuwa hivi sasa hana matatizo na Majizzo wala Lulu hivyo kwake ni Poa tu wakifunga ndoa.


Kwenye mahojiano na Risasi Jumamosi, Mobeto alisema kuwa hana kinyongo na Lulu kama ambavyo watu wanasema kwa kuwa mapenzi yake na Majizzo yalishakwisha siku nyingi.


"Mimi na huyo anayetaka kumuoa tulishamalizana, hivyo hakuna tena hata chembe ya mapenzi zaidi ya uhusiano wetu wa kulea mtoto.


"Kwa maana hiyo sina shida kusikia Lulu anaolewa na siku ya sherehe nikipewa kadi nitakwenda“.


Tangu Lulu atoke jela Kumekuwa na tetesi nyingi kuwa yeye pamoja na mpenzi wake Majizzo wanategemea kufunga ndoa hivi karibuni

Zuio la Mikutano ya Hadhara Yadaiwa Kuwa ni Piga kwa Wanawake...Hatuwezi Kupata Kina Halima Mdee Wengine

$
0
0

Baraza la Wanawake  Chadema (Bawacha) limesema uamuzi wa Serikali kupiga marufuku mikutano ya hadhara unarudisha nyuma juhudi za wanawake kufikia usawa wa asilimia 50 kwa wanawake kwa wanaume.


Kauli hiyo imetolewa jana Jumapili Juni 24, 2018 na makamu mwenyekiti wa baraza hilo, Hawa Mwaifunga wakati akizungumza na wanahabari katika mkutano wa kamati ya utendaji ya baraza hilo uliofanyika mjini hapa.


Mkutano huo wa siku mbili pamoja na mambo mengine unalenga kuwapa mafunzo, mbinu na ujasiri viongozi wa mikoa wa chama hicho.


Mwaifunga alisema wanawake wengi wamekuwa na hofu kutokana na uamuzi wa kuzuiwa kwa mikutano ya hadhara, jambo ambalo linawafanya wanawake washindwe kujitosa katika siasa.


Alisema uamuzi huo umewanyima fursa Watanzania kuwasikiliza wanasiasa ili baadaye waje wafanye uamuzi wa kuwachagua wagombea wa chama kinachofaa.


“Kwa sasa ni kutishana na kukamatwa na kuwekwa ndani. Kipindi cha nyuma watu walifanya siasa za kistaarabu sana, ndiyo maana tuliwapata akina Halima Mdee (mwenyekiti Bawacha), Paulin Gekul (Babati Mjini (Chadema). Walipatikana baada ya kuonekana majukwaani,” alisema.


Katibu wa Bawacha,  Grace Tendega alisema wataendelea kupambana  licha ya kuwa wanaoonekana kufanya siasa majukwaani wanakamatwa.


Alisema baraza hilo limejipanga kuhakikisha majimbo sita yanayoongozwa na wabunge wanawake wa Chadema yanalindwa.

Mtandao wa Twitter Wapumulia Mashine...Instagram na Facebook Vinara

$
0
0

Katika mitandao ya kijamii ambayo ni maarufu na inawatumiaji wenye mazungumzo mengi sana ni Twitter, lakini tatizo lake moja kubwa ni kwamba mtandao huu wa kijamii bado hautengenezi pesa za kutosha ukilinganisha na mitandao mingine ya kijamii. 

Mtandao wa Twitter ingawa inavutia mazungumzo mbalimbali kuanzia ya kisiasa, kiutani, n.k yanayohusisha hadi watu mashuhuri kama Rais wa Marekani wa sasa, wasanii na watu wengine mashuhuri kwa wadogo bado mtandao huu unapata shida katika kuvutia makampuni kutumia pesa kujitangaza katika mtandao huo. 

Mtandao wa Twitter bado upo nyuma katika kuvutia mapato yanayotokana na matangazo ukilinganisha na mitandao mingine kama vile Facebook na ata Instagram na Snapchat. 

Katika ripoti ya mapato na ukuaji ya kampuni uya Twitter iliyotoka Alhamisi hii inaonesha bado mtandao wa kijamii wa Twitter unapata shida kukuza idadi ya watumiaji, matangazo na mapato. 

Kwa mfano katika miezi mitatu ya mwisho ya mwaka 2016 Twitter ilikuwa na wastani ya watumiaji milioni 319 kwa mwezi, huu ni ukuaji wa asilimia 4 tuu ya watumiaji ukilinganisha na kipindi cha mwaka mmoja nyuma, pia namba hii ni ndogo ukilinganisha na mtandao wa Facebook. Facebook ina takribani wastani wa watumiaji bilioni 1.86 kwa mwezi. 

Twitter wanategemea kupata mapato ya dola milioni 91 tuu katika kipindi cha miezi hii mitatu ya mwanzo, hii ni chini sana ukilinganisha na pato la dola milioni 191 ambalo wengi waletegemea wafikie. 

Ingawa bado kibiashara mtandao huo upo katika hali ngumu ila ni uhakika bado hautaenda popote kwa sasa. Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Bwana Jack Dorsey anasema itaitaji muda mrefu kidogo na mabadiliko kadhaa ili kuweza kuona ukuaji wa watumiaji pamoja na mapato.

Zabibu Kiba Afunguka Uhusiano Wake na Jokate

$
0
0
DADA wa mwana-muziki maarufu Bongo, Ally Salehe Kiba ‘Ali- Kiba’, Zabibu amem-fungia mpenzi wa zamani wa kaka yake huyo ambaye ni mwanamitindo na mjasiriamali Jokate Mwegelo, na kusema kuwa hata kama hayupo ndani ya familia yao bado anamheshimu sana.

Akizungumza na Over Ze Weekend nyumbani kwao Kariakoo jijini Dar hivi karibuni, Zabibu alisema kuwa, Jokate kwake ni kama dada yake na wala hana tatizo naye na wanazungumza naye vizuri kama ilivyokuwa zamani na pia anamheshimu kwa sababu ni binti anayejielewa.

“Siwezi kuzungumzia kitu chochote kibaya kuhusiana na Jokate kwa sababu ni kama dada yangu kabisa ninamheshimu na ninampenda sana halafu pia tunaongea tu vizuri hatuna shida yoyote na ni msichana anayejielewa mno,” alisema Zabibu.

Haji Manara Awatolea Uvivu TFF

$
0
0
Haji Manara Awatolea Uvivu TFF
AFISA HABARI mwenye mbwembwe nyingi kuliko wasemaji wengine wa timu za hapa nchini, Haji Manara wa Simba, ameibuka na kuweka bayana kwamba Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limejipa mzigo mzito wa kuubeba msimu ujao kutokana na wingi wa timu ambazo zitashiriki ligi kwa msimu wa 2018/19.

TFF waliongeza timu am­bazo zitashiriki ligi kuu kwa msimu ujao kutoka 16 za sasa hadi 20 ambapo timu sita zilipanda kutoka Ligi Daraja la Kwanza msimu uliopita. Timu hizo ni JKT Tanzania, African Lyon na KMC za Dar, Biashara United ya Mara, Coastal Union ya Tanga na Alliance ya Mwanza.

Akizungumza na Championi Jumatatu, Manara amesema kwamba anaona TFF watakuwa na kazi kubwa kutoka­na na changamoto ya viwanja ambavyo vingi siyo rafiki kwa kuchezea sam­bamba na tatizo la ratiba ambayo ime­kuwa ikib­adilishwa kila mara.

“Kwangu naona kwamba kwa msimu ujao TFF watakuwa na kazi kubwa ya kufanya hasa baada ya kuongeza timu ambazo zitakuwa kwenye ligi kuu.

“Kuwa na timu 20 katika ligi siyo jam­bo dogo tena katika sehemu ambayo ina changamoto kubwa ya viwanja ambapo vingi vimekuwa siyo rafiki kwa wachezaji kucheza.

“Lakini kwa sasa tu tumekuwa tukiona juu ya hali ya upanguliwaji wa ratiba kwa kila mara tena zikiwa timu 16 sasa zinapokuja timu 20 si kutakuwa na matatizo zaidi, kwangu naona kama TFF watakuwa na kitu cha ziada ambacho wa­natakiwa wakifanye katika maeneo hayo ili ligi iwe nzuri,” alisema Manara.

Akon Azindua Sarafu Yake Apewa Ekari 2,000 na Rais wa Senegal

$
0
0
Akon Azindua Sarafu Yake Apewa Ekari 2,000 na Rais wa Senegal
Msanii wa muziki kutoka Marekani, Akon amezindua sarafu yake ya mtandaoni ( cryptocurrency) aliyoipa jina la ‘AKoin’ ambayo amedai kuwa miaka michache baadae itanusuru uchumi wa Afrika.



Akizungumza kwenye tamasha la ubunifu la Cannes Lions siku ya Jumatano iliyopita Akon amesema kuwa mradi huo wa sarafu unakuja na mpango wa kuanzisha mji maalumu ambao wakazi wake watatumia sarafu hizo.

Kupitia ukurasa rasmi wa sarafu hiyo wa akoin.io umeeleza kuwa mji huo utakuwa nchini Senegal na lengo kubwa na mji huo utabeba maudhui kama ya mji wa kusadikika uliooneshwa kwenye filamu ya Black Panther ‘WAKANDA’ .

Tayari Akon ameshakabidhiwa ekari 2000 na Rais wa Senegal, Macky Sall kwa ajili ya mradi huo wa kujenga mji mpya na eneo hilo lipo nje kidogo ya mji wa Dakar.

Mtandao huo umeeleza kuwa wakazi wa mji huo utakaojengwa na Akon watakuwa na uwezo wa kununua na kuuziana bidhaa kutumia sarafu hiyo ya AKoin kwa njia ya simu ili kulinda usalama wao.

Sarafu ya Akoin inakuwa sarafu ya pili ya kimtandao au kidijitali hii ni baada ya sarafu maarufu mtandaoni ya Bitcoin kuzinduliwa miaka 9 iliyopita.

Sarafu ya AKoin na Bitcoin ni sarafu ambazo matumizi yake hayaingiliani na mfumo wa kibenki kama zilivyo sarafu nyingine duniani.

Tayari sarafu hiyo imeanza kufanya kazi unaweza ukajisajili kupitia tovuti yao rasmi ya akoin.io  ili kupata maelezo yote kwa kina.

Mradi huo unakuwa wa pili kwa Akon kuuzindua baada ya mradi wake wa kwanza wa Akon Lighting Africa wenye lengo la kupeleka umeme jua vijijini kufanikiwa kwa kiasi kikubwa.


Recep Tayyip Erdogan Ashinda Muhula wa Pili wa Urais Uturuki

$
0
0
Recep Tayyip Erdogan ashinda muhula wa pili wa urais Uturuki
Tume ya uchaguzi nchini Uturuki imemtangaza Rais Recep Tayyip Erdogan kama mshindi wa nafasi ya urais katika uchaguzi mkuu uliofanyika June 24.

Erdogan ambaye aliingia madarakani 2014 ameshinda muhula wake wa pili kwa ailimia 53 ya kura zote zilizohesabiwa akiepuka kuingia mzunguko wa pili huku chama chake kikishinda wingi wa viti bungeni.

Mpinzani wake mkuu Muharrem Ince kutoka chama cha CHP tayari amempongeza Erdogan katika mitandao ya kijamii licha ya kushutumu uchaguzi huo kuwa haukuwa wa haki.

Muda mfupi kabla ya kura halisi kutangazwa Erdogan alizungumza kupitia televishen ya taifa akisema taifa lake limepata taarifa nzuri za yeye kuendelea kusalia madarakani licha ya kwamba hazikua bado za uhakika.

''Uchaguzi wa June 24 umeleta taarifa nzuri kwa nchi yetu, kwa watu wetu. Kwa taarifa nilizonazo licha ya kuwa sio za uhakika ni kwamba nchi yetu imenichagua kuendela kuwa rais, licha ya kuwa sio za uhakika. Pia chama cha AK kimeshinda uwakilishi wa viti vingi bungeni, ambapo tuna shughuli za kisheria.'' Alisema Erdogan.

Davido Ashinda Tuzo za BET 2018 Hii Hapa Orodha Kamili ya WashindI Wote

$
0
0
HAPA nimekuwekea orodha ya washindi wote wa Tuzo za BET 2018, zilizofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye Ukumbi wa Microsoft jijini Los Angeles.

Best Female R&B/Pop Artist Award
Beyoncé *WINNER
SZA
H.E.R.
Rihanna
Kehlani
Best Male R&B/Pop Artist Award
Bruno Mars *WINNER
Chris Brown
The Weeknd
Khalid
Daniel Caesar
Best Group Award
Migos *WINNER
A Tribe Called Quest
N*E*R*D
Rae Sremmurd
Chloe x Halle
Best Collaboration Award
Bruno Mars /Cardi B – “Finesse (Remix)”
DJ Khalid /Rihanna and Bryson Tiller – “Wild Thoughts” *WINNER
DJ Khalid /Jay-Z, Future & Beyoncé – “Top Off”
Cardi B /21 Savage – “Bartier Cardi”
French Montana f/Swae Lee – “Unforgettable”
Kendrick Lamar f/Rihanna – “Loyalty”
Best Male Hip Hop Artist Award
Drake
Kendrick Lamar *WINNER
DJ Khaled
Jay-Z
J.Cole
Best Female Hip Hop Artist Award
Cardi B *WINNER
Nicki Minaj
Remy Ma
Dej Loaf
Rapsody
Video of the Year Award
Drake – “God’s Plan” *WINNER
Cardi B – “Bodak Yello”
Bruno Mars /Cardi B – “Finesse (Remix)”
DJ Khaled /Rihanna and Bryson Tiller – “Wild Thoughts”
Kendrick Lamar – “Humble” Migos /Drake “Walk It Talk It”
Video Director of the Year Award
Benny Boom
Director X
Ava DuVernay *WINNER
Chris Brown
Dave Meyers
Best New Artist Award
SZA *WINNER
H.E.R.
Daniel Caesar
Gold
LinkA
Boogie Wit Da Hoodie
Dr. Bobby Jones Best Gospel/Inspirational Award
Lecrae / Tory Kelly – “I’ll Find You” *WINNER
Snoop Dogg / B Slade – “Words Are Few”
Ledisi and Kirk Franklin – “If You Don’t Mind”
Marvin Sapp – “Close”
Tasha Cobbs Leonard f/ Nicki Minaj – “I’m Getting Ready”
Best Actress Award
Tiffany Haddish *WINNER
Lupita Nyong’o
Issa Rae
Angela Bassett
Letitia Wright
Taraji P. Henson
Best Actor Award
Chadwick Boseman *WINNER
Michael B. Jordan
Donald Glover
Sterling K. Brown
Denzel Washington
Daniel Kaluuya
Young Stars Award
Yara Shahidi *WINNER
Ashton Tyler
Caleb McLaughlin
Lonnie Chavis
Marsai Martin
Miles Brown

Best Movie Award
“Black Panther” *WINNER
“Girls Trip”
“A Wrinkle in Time”
“Detroit”
“Mudbound”
Sportswoman of the Year Award
Serena Williams *WINNER
Venus Williams
Skylar Diggins-Smith
Candace Parker
Elana Meyers Taylor
Sportsman of the Year Award
Stephen Curry
LeBron James *WINNER
Kevin Durant
Dwyane Wade
Odell Beckham Jr.
Album of the Year Award
Kendrick Lamar – “Damn” *WINNER
SZA – “Ctrl”
Jay-Z – “4:44”
Migos – “Culture II”
Kendrick Lamar and Various Artists – “Black Panther: The Album”
DJ Khaled – “Grateful”
BET Her Award
Janelle Monáe – “Django Jane”
Lizzo – “Water Me”
Mary J. Blige – “Strength of a Woman” *WINNER
Remy Ma f/ Chris Brown – “Melanin Magic (Pretty Brown)”
Chloe x Halle – “The Kids Are Alright”
Leikeli47 – “2nd Fiddle”


Coca-Cola Viewers’ Choice Award
SZA / Travis Scott – “Love Galore”
Cardi B – “Bodak Yellow” *WINNER
Kendrick Lamar – “Humble”
Drake – “God’s Plan”
Migos / Nicki Minaj and Cardi B – “MotorSport”
DJ Khaled f/ Rihanna and Bryson Tiller – “Wild Thoughts”
The Best International Act Award
Booba (FRANCE)
Cassper Nyovest (SA)
Dadju (FRANCE)
Davido (NIGERIA) *WINNER
Distruction Boyz (SA)
Fally Ipupa (DR CONGO)
J Hus (UK)
NISKA (FRANCE)
Tiwa Savage (NIGERIA)
Stefflon Don (UK)
Stormzy (UK).

Mtoto Anyongwa kwa Kuvunjwa Shingo Akiwa Anachunga Mifugo

$
0
0
Mtoto Anyongwa kwa Kuvunjwa Shingo Akiwa Anachunga Mifugo
JESHI la Polisi mkoani Ruvuma, limewakamata watu wanaodhaniwa kumuua kwa kumnyoga kwa kumvunja shingo mtoto wa jamii ya kifugaji aliyetambulika kwa jina la Chanya Rugwashi (12).

Kamanda wa Polisi mkoani Ruvuma, Jemen Mushi, alisema  baada ya watu hao kutekeleza unyama huo, waliiba kondoo wawili na kuwachinja na kuondoka na nyama.

Kamanda Mushi alisema tukio hilo lilitokea Juni 20 katika eneo la mto Nampungu katika Kitongoji cha Matikiti Mashambani katika Kijiji cha Nambalapi.

Kamanda Mushi alifafanua kuwa marehemu Rugwashi alikutwa akichunga mifungo mingi wakiwamo ng'ombe, mbuzi na kondoo, lakini watu hao baada ya kufanya mauaji hayo waliiba kondoo wawili tu.

Kufuatia tukio hilo, Kamanda Mushi amewaomba wananchi ambao wanawafahamu watu waliotekeleza unyama huo kulisaidia Jeshi la Polisi ili kuwakamata haraka na kupisha vyombo vya sheria kutekeleza wajibu wake.

Kaka wa marehemu Rugwashi, Bundala Rugwashi, alisema kuwa mdogo wake alipotea Juni 20 na kwamba baada ya kubaini hali hiyo, walianzisha msako katika msitu huo na kufanikiwa kuupata mwili wake Jumamosi ukiwa umening'inizwa katika mti.

Alisema baada ya tukio hilo walitoa taarifa kwa viongozi wa serikali ya Kata ya Masonya na baadae kituo cha polisi.

Taarifa ya uchunguzi wa mwili wa marehemu Rugwashi iliyotolewa na Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Tunduru, Dk. Vitaris Lusasi, inaeleza kuwa chanzo cha kifo hicho ni kuvunjika shingo.

Badri Mwimbaji Rap Asimamishwa Kazi

$
0
0
Badri Mwimbaji Rap Asimamishwa Kazi
Kasisi mmoja wa kanisa Katoliki nchini Kenya aliyepata umaarufu kutokana na mtindo wake wa kutumbuiza kwa kutumia muziki wa kufoka amesimamishwa kazi.

Paul Ogalo aka 'Sweet Paul' amekuwa akitumia muziki wa rap kama njia ya kuwavutia vijana wengi kufika kanisani.

Alikuwa amesema muziki ni njia mwafaka sio tu kuwavutia vijana bali pia kueneza Injili.

Mistari ya nyimbo zake huwa kwa mfano: "Kujeni church kuna baraka, kujeni church kuna baraka..." au "Father Paul, niki-lock kwenye mic, Nduru inafuata, mamanze go tipsy, vijana ruka ruka swag ya kunguru, au sio"

Lakini hatua yake hiyo inaonekana kutowafurahisha viongozi wa kanisa Katoliki magharibi mwa Kenya ambao wamemsimamisha kazi kwa mwaka mmoja ili "ajitafakari".

Askofu wa jimbo la kanisa Katoliki la Homa Bay Philip Anyolo amesema padri huyo ni lazima achague kati ya kuwa „rapa na kuwa padri".

Amesema kasisi huyo hataruhusiwa kuongoza ibada ya misa kwa kipindi cha mwaka mmoja ingawa anaruhusiwa kushiriki ibada, na pia anaruhusiwa kufanya ibada ya misa lakini faraghani.

Trump Ataka Wahamiaji Haramu Watimuliwe Haraka Marekani

$
0
0
Trump Ataka Wahamiaji Haramu Watimuliwe Haraka Marekani
Rais wa Marekani Donald Trump ametoa wito wa kuharakishwa kwa shughuli ya kuwatimua wahamiaji haramu nchini humo bila hata kufuata utaratibu wa mahakama.

Amefanya hivyo kupitia msururu wa ujumbe kwenye Twitter.

"Mtu anapoingia ndani, ni lazima mara moja, bila majaji na kesi mahakamani, tuwarejeshe walikotoka," Trump ameandika.

Amesema hayo siku chache baada yake kubatilisha sera ya kuwatenganisha watoto wa wahamiaji na wazazi wao baada ya sera hiyo kushutumiwa vikali Marekani na nje ya nchi hiyo.

Takwimu zinaonesha watoto 2,300 walikuwa wametenganishwa na wazazi wao kati ya Mei na Juni mwaka huu.

Kuanzia mwezi Mei, wahamiaji wanaovuka mpaka wa Marekani na kuingia nchini humo kinyume cha sheria wanakabiliwa na hatari ya kufunguliwa mashtaka ya jinai chini ya sera ya Trump ya kutowavumilia wahamiaji.

Rais Trump hajatofautisha kati ya wahamiaji wa kiuchumi na wale wanaotafuta hifadhi kutokana na mateso na kudhalilishwa mataifa yao.

Rais huyo amekuwa akishutumiwa hata na viongozi wa chama chake cha Republican kwa lugha kali aliyoitumia kwenye Twitter.

Aliposema awali kwamba wahamiaji wanatishia "kufurika na kuiambukiza nchi yetu, mbunge mwanamke wa chama cha Republican Ileana Ros-Lehtinen alimjibu kwenye Twitter akisema tamko lake halina msingi, "linakera" na linadunisha wale wanaotafuta maisha mazuri.

Maafisa wa uhamiaji Marekani wanasema watoto 2,342 walitenganishwa na wazazi 2,206 kati ya 5 Mei na 9 Juni.

Mnamo 20 Juni, Trump aililegeza msimamo wake wa kuunga mkono sera hiyo kali na badala yake akatia saini agizo la rais la kusitisha hatua hiyo ya kuzitenganisha familia.

Sanaa Hailipi Tena Umachinga ndo Unaniokoa- Mwanaheri

$
0
0
Sanaa Hailipi Tena Umachinga ndo Unaniokoa- Mwanaheri
MUIGIZAJI wa Bongo Muvi, Mwanaheri Ahmed amefunguka kuwa umachinga anaoufanya nje ya uigizaji umemsaidia kwa sababu isingekuwa hivyo maisha yangekuwa ni magumu kwani sanaa hailipi tena kama ilivyokuwa awali.

Akizungumza na Over Ze Weekend, Mwanaheri ambaye kwa hivi sasa amefungua duka lake la kuuza madera Tandika jijini Dar, alisema amefanikiwa hilo baada ya kuuza nguo mojamoja mtaani mpaka kufikia hatua ya kufungua duka lake mwenyewe baada ya kuweka aibu pembeni.

“Mimi ningejifanya naona haya basi nisingefikia lengo hata kidogo lakini kwa sababu niliweka mambo ya ustaa pembeni nikachagua kufanya maisha ndio maana mpaka sasa hivi Mungu kanibariki siwezi kusema nitakosa hata hela ya kula, ningesubiria filamu zangu ziuze basi ningekuwa kwenye wakati mgumu sana,” alisema Mwanaheri.

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0


KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME DR SITTA NDO SULULISHO LAKO tatiza, hili limekuwa likiwaasili watu wengi,sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine, kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo zipo , sababu nyingi zinazosababisha, tatizo hilo baadhi ni (i) upungufu wa vichocheo vya HORMONES ZA CETROGEN ambazo mwanaume, anapobarehe vichocheo hivi, HORMONES hizo, husaidia ukuaji wa uume

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mlija iliysinyaa,

NSHOLA ni dawa bora, ya kurudisha nguvu, za, kiume bari inatibu ,kabisa kutoa tatizo hilo, na kukupa , hamu ya , kurudia tendo, la ndoa zaidi, ya mala nne 4 ,bila kuchoka atakama unaumli ,wa mika 80,! pia ana ,dawa za ,kutibu, presha ya kupanda ,na kushuka, kisukari kuondoa, mafuta , mwilini ,na maumivu ya, mgogo kiuno, dawa zipo, matazo, ya hedhi, kwa ,wanawake hedhi, zisizokuwa na, mpangilio, na kasonono, pia , vidonda ,vya, tumbo ,(STOMACHI UCLENS) IHUSHI ndoji lako.

NKANYA ni dwa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi ariyekuacha, mke mme, atakuludia kwa, mda, wa msaa3 tu , ukishaitumia atarudi ,mwenyewe bila ,ugovi tena, NKOMA ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada .

HERBON, ni, dawa, ya kuongeza, CD4, NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu ,miguu, kufaganzi, na ,kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! DR SITTA, amebobea, kwa tiba asilia

DAR ANAPATIKANA MBAGALA, ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI SHINYANGA, KAHAMA MJINI, KWA MAELEZO ZAIDI ,

PIGA SIMU 0763172670 au 0715172670

WOTE MNAKALIBISHWA, KAMA, UTAKUWA NA TATIZOUTAHUDUMIWA

TCRA na Jeshi la Polisi kula sahani moja na wezi wanaotumia mitandao ya simu

$
0
0

Serikali imesema kuwa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa kushirikiana na Polisi watahakikisha wanafanya kazi kwa ukaribu kuhakikisha wote wanaotapeli kwa njia ya mitandao wanakamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria.


Mbunge wa Mchinga, Hamidu Bobali akiuliza swali leo Bungeni jijini Dodoma

Hayo yamebainishwa na kupitia Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye, Bungeni Jijini Dodoma Wakati akijibu swali la Mbunge wa Mchinga, Hamidu Bobali aliyehoji; “Kumekuwa na wimbi sasa limeibuka la wizi wa kutumia mitandao ya simu wakiwa wanatuma sms kuwa umeshinda ‘Tatu Mzuka’ mara umeshinda Tigo, tuma pesa kwenye namba hii,kumekuwa na desturi hiyo sasa hivi. Nilitaka kupata majibu kutoka kwa Waziri TCRA imechukua juhudi gani wizi wa kutumia simu kwenye mitandao unakomeshwa na kuhakikisha wahusika wanakamatwa?

Kama mnaona tumekonda, leteni show tunenepe – Ruby

$
0
0


Msanii wa muziki Bongo, Ruby amefunguka kuhusu stori zinazodai kwa sasa mwili wake umepungua (amekonda) ukilinganisha na hapo awali.

Muimbaji huyo anayetamba na ngoma ‘Niwaze’ ameiambia FNL ya EATV kuwa picha zilizokuwa zikisambaa kwenye mitandao hajui zimetokea wapi.

Ruby alienda mbali zaidi kwa kueleza kuwa picha hizo zimefanyiwa editing na wale wanaoeneza stori hilo wampe kazi (show) ili anenepe.

“Halafu kitu kingine basi wawe wanaleta shows, kazi ili tunenepe, hivyo ndio vitu vya kuongea. Kama mnaona tumekonda, mnataka tunenepe, mnaleta shows, kazi,” amesema Ruby.

Ruby alikuwa kimya kwa kipindi kirefu katika muziki mara baada ya kuzinguana na menejimenti yake ya zamani. Wimbo wa kwanza kutoa kwa mwaka huu ni Niwaze aliowashirikisha kundi la The Mafik.

Watu 12 wamefariki dunia na 3 kujeruhiwa katika ajali Mkuranga

$
0
0

Watu 12 wamefariki dunia na wengine 3 wamejeruhiwa baada ya Gari dogo aina ya Toyota Hiace kugongana uso kwa uso na Lori la Mchanga lenye namba za usajili T 439 DCC  katika kijiji cha Dundani wilayani Mkuranga. 

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga Dkt.Steven Mwandambo amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na zoezi linaloendelea kwa sasa ni kuwanasua baadhi ya majeruhi walionasa katika magari hayo. 

JE, Ronald Leo Ataweza Kuonesha Kuwa ni Mbabe wa Kutikisa Nyavu Kombe la Dunia?

$
0
0

Michuano ya Kombe la Dunia nchini Urusi inaendelea tena leo katika viwanja vitatu ambapo nyota wa Ureno Cristiano Ronaldo atakuwa dimbani kuiongoza timu yake ya taifa kukipiga dhidi ya Iran katika mchezo wa Kundi B kwenye uwanja wa Mordovia kuanzia saa 3 kamili usiku.

Nyota wa Ureno Cristiano Ronaldo aliyenyoosha kidole akiwa na nyota wa England, Harry Kane.

kuelekea mechi hiyo, Ronaldo anapewa nafasi kubwa ya kuonesha ubabe wake wa kutikisa nyavu baada ya kutikisa kamba za wapinzani mara nne katika mechi mbili alizocheza.

Endapo Ronaldo atafunga bao moja dhidi ya Iran atakuwa amemzidi nyota wa England, Harry Kane aliyefikisha mabao matano katika mashindano hayo.

Mechi nyingine zitakazopigwa ni Misri ambao wameshaaga mashindano watakamilisha ratiba dhidi ya Saudi Arabia majira ya saa 11 jioni huku pia Uruguay wakikipiga na wenyeji Urusi muda huohuo wa saa 11.

Kauli ya Serikali Kuhusu Walimu Waliohamishwa Bila Kulipwa

$
0
0

Serikali imesema walimu wote waliohamishwa kabla ya tamko la Rais John Magufuli aliyeagiza wote wanaohamishwa kupewa kwanza stahiki zao, watalipwa fedha zao kwa kuwa madai yao ni halali.


Kauli hiyo imetolewa leo Jumatatu Juni 25, 2018 bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Joseph Kakunda wakati akijibu swali la mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Susan Lyimo.


Katika swali lake Susan alitaka kujua ni lini walimu waliohamishwa watalipwa madai yao ikiwemo waliobadilishiwa vituo vya kazi kutoka ualimu wa sekondari na kuwa walimu wa shule za msingi.


Akijibu swali hilo, Kakunda amesema zoezi la kuwahamisha walimu kabla ya kupewa malipo lilisitishwa baada ya kauli ya Rais hivyo madeni yaliyopo ni waliokuwa wanahamishwa bila malipo na kwamba  baada ya tamko la Rais, hali ni nzuri.


Awali mbunge wa Mbagala (CCM), Issa Mangungu alihoji ni kwa nini Serikali ilifuta posho za kufundishia na lini itazirudisha ili kuwatia moyo walimu waweze kufundisha zaidi.


Naibu Waziri amesema posho hiyo haikufutwa bali iliongezewa katika mishahara ya walimu kwa lengo la kuongeza mishahara na pensheni wakati wa kupata kiinua mgongo.
Viewing all 104687 articles
Browse latest View live




Latest Images