Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

Museveni Awawekea Ulinzi Wabunge

$
0
0
Museveni Awawekea Ulinzi Wabunge
 Katika juhudi za kukabiliana na wimbi la hivi karibuni la mauaji ya watu mashuhuri, wabunge wataanza kulindwa na askari wa Jeshi la Ulinzi wa Watu wa Uganda (UPDF), imefahamika.
Uamuzi huo ni matokeo ya makubaliano yaliyofikiwa Jumanne katika mkutano wa ndani kati ya wabunge na Rais Yoweri Museveni.
Katika mkutano huo, wabunge wakionekana kushtushwa na wimbi la hivi karibuni la mauaji ya watu mashuhuri hususan tukio la Juni 8 la kuuawa kwa kupigwa risasi Mbunge wa Manispaa ya Arua Ibrahim Abiriga, walimwambia Museveni kwamba wamekuwa wakipokea vitisho vya kifo kupitia simu za mkononi na majukwa ya mitandao ya kijamii.
Habari zinasema Rais Museveni alimwagiza Mkuu wa Jeshi la Ulinzi (CDF), Jenerali David Muhoozi, kukutana na Kamanda wa Polisi wa Bunge Mrakibu wa Polisi Anabella Nyamahoro kushughulikia mchakato wa kuongeza usalama wa wabunge. Nyamahoro alikuwa katika mkutano huo.
Wizara ya Fedha itatakiwa kukokotoa gharama za utaratibu huu wa maandalizi ya usalama.
Jenerali Muhoozi, Mkaguzi Mkuu wa Polisi, Martins Okoth-Ochola na Mkurugenzi wa Upelelezi (CID) Grace Akullo pia walihudhuria mkutano huo.
Vyanzo vya habari vinasema Rais aliagiza kwamba wabunge watakuwa wakisindikizwa na askari baada ya wabunge kuonyesha kutoridhishwa na walinzi wa kikosi cha polisi cha kupambana na ugaidi.
Wabunge, ambao waliunga mkono muswada wa marekebisho ya katiba uliopitishwa Desemba 2017 ili kuondoa ukomo wa umri wa rais, walipewa walinzi kutoka kikosi cha polisi cha kupambana na ugaidi kwani wapigakura waliokasirishwa na hatua hiyo walitishia kuwadhuru.
Mbunge wa Jimbo la Obongi, Hassan Kaps Fungaroo, ambaye alipuuza wito wa upinzani wa kususia na akahudhuria mkutano na Rais alisema wabunge wa chama tawala cha NRM walimwambia Rais Museveni kwamba wanapendelea kulindwa na UPDF badala ya polisi na pia waliomba magari ya kuwasindikiza.
"Kazi hii itafanywa zaidi na UPDF. Polisi waliokuwa wakiwalinda wabunge walikuwa wakikimbia (kwa sababu) walikuwa wanafikiria kazi ya kuwalinda wawakilishi wa wananchi ni hatari. Kwamba mazingira ya kazi yao (walinzi) ni hatarishi kwa maisha yao," alisema Fungaroo.
Walinzi hao watafanya kazi kwa muda wa miezi sita, kipindi ambacho Museveni anatarajia mapendekezo yake ya kuboresha usalama wa taifa yatatekelezwa.

TCRA Yavipiga Faini ya Milioni Sita Vituo Viwili vya Redio

$
0
0
TCRA Yavipiga Faini ya Milioni Sita Vituo Viwili vya Redio
Kamati ya maudhui ya mamlaka ya mawasiliano (TCRA) imevitoza faini ya Sh6 milioni vituo vya redio vya Magic Fm na Rasi Fm kwa kukiuka kanuni za maudhui.

Akisoma hukumu hiyo Juni 29, 2018 Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo Joseph Mapunda amesema Magic Fm cha Dar es Salaam, imetozwa faini ya Sh4 milioni kwa kosa la kukiuka kanuni za utangazaji kwa kushindwa kuweka mizania wakati wakichambua bajeti ya wizara ya mifugo.

Kupitia kipindi chake cha ‘Morning Magic’ kilichorushwa Mei 18 mwaka huu mtangazaji alieleza kuhusu kufilisika kwa kampuni ya uvuvi ya Taifa (Tafico) na kampuni ya ranchi za taifa (Narco).

Kwa mujibu wa kamati hiyo, watangazaji walitoa taarifa bila kupata maoni ya upande wa serikali na vilevile hawakuwa na uhakika wa taarifa walizozitoa.

Kwa upande wa Rasi Fm cha Dodoma, kilikutwa na hatia ya kukiuka kanuni za utangazaji kwa kurusha maudhui ya ngono katika muda ambao wasikilizaji wake wengi ni watoto.

Mapunda amesema Juni 6 mwaka huu saa tano asubuhi mtangazaji alizungumzia kuhusu ngono na uangaliaji wa filamu za ngono jambo linalowahamasisha vijana na watoto kuwa na tabia mbaya.

Kutokana na hilo kituo hiki kimekutwa na makosa mawili ikiwamo kushindwa kuwalinda watoto na kuweka mada za wakubwa muda ambao wasikilizaji ni watoto.

Kila kosa lilitozwa faini ya Sh1 milioni zinazotakiwa kulipwa ndani ya siku 30 kuanzia leo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Rasi Fm Ramadhan Mkotsollah amesema ameridhishwa na uamuzi huo kwa kuwa kweli kosa lilifanyika.

"Ni kweli kulingana na taratibu hilo ni kosa na mie binafsi sikufurahishwa na kitendo hicho ndio sababu tumechukua hatua,"amesema

Viongozi wa Ethiopia na Eritrea Wamekubaliana Kukutana

$
0
0
Viongozi wa Ethiopia na Eritrea Wamekubaliana Kukutana
Viongozi wa Ethiopia na Eritrea wamekubaliana kukutana kwa mara ya kwanza katika muda wa takribani miaka 20 ishara ambayo haikutegemewa ya kuanza upya uhusiano wa kidiplomasia kati ya mataifa hayo mawili jirani kwenye pembe ya Afrika.

Waziri wa mambo ya nje wa Ethiopia, Workneh Gebeyehu aliliambia shirika la habari la Associated Press-AP siku ya Alhamis kwamba mkutano huo utajenga msingi bora wa kurejesha amani. Aliongeza kuwa muda na mahala ambako mkutano utafanyika bado haujajulikana.

Mwanadiplomasia wa juu wa Ethiopia alizungumza wakati ujumbe wa Eritrea ulio-ongozwa na waziri wa mambo ya nje, Osman Saleh kumaliza ziara ya siku tatu ya kihistoria huko Ethiopia.

Mahusiano mabaya ya nchi hizo mbili yalianza wakati vita vya mpaka vilipotokea mwaka 1998 miaka mitano baada ya Eritrea ilipojinyakulia uhuru wake kutoka Ethiopia.

Baba Amuua Mwanaye Kisa Parachichi

$
0
0
Baba Amuua Mwanaye Kisa Parachichi
Polisi nchini Kenya linamsaka Mr. Morris Kirema kwa kosa la kumuua Mtoto wake mwenye miaka 12 na kumjeruhi Mtoto wake mwingine mwenye miaka 8 kwa kutumia panga na mateke akiwashutumu Watoto hao kula maparachichi kutoka katika shamba la jirani yao.

Mr. Morris anadaiwa kutumia mateke, ngumi pamoja na panga kuwaadhibu Watoto hao baada ya kula maparachichi kutoka katika shamba la jirani yao na kupelekea Mtoto wake huyo wa kiume mwenye miaka 12 kufa hapohapo.

Kwa upande wa Mtoto wa kike mwenye miaka 8 yeye amejeruhiwa vibaya sana pamoja na Mama yake ambao wanapatiwa matibabu katika hospitali moja nchini humo.



Inadaiwa kuwa mwenye shamba ambalo Watoto hao waliiba maparachichi hayo alidai alipwe kutokana na kitendo walichokifanya Watoto hao na ndipo Mr. Morris alipokasirika na kunuia kuwa lazima atawaua Watoto hao wakirudi kutoka shule.

Aidha duru za kuaminika zinasema kuwa Mwanaume huyo anasumbuliwa na uraibu wa michezo ya bahati nasibu na amekuwa akiwa mchungu akiombwa pesa na Mke wake

Habari Njema Kwa Wanaume Wote Wenye Matatizo ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

Next: Mdada Aliyekwambia kujua Kuzungusha Kiuno ndo Tiketi ya Kupata ndoa Kakudanganya.. 17:33 Mapenzi Kila mwanamke anavitu vyake alivyojiwekea, ambavyo anataka mwanaume wa ndoto zake awe navyo. Ikitokea akampata Mwenye hivyo vitu basi huona kamaliza kila kitu, anajisahau, anafurahia vile anavyoviona kwa nje na kitandani, badala aanze kumsoma huyo Mwanaume. Kama ni husband material. Wanawake ndio wanaongoza kwa kulizwa Sana kwenye mahusiano kuliko wanaume, kwasababu mwanamke akishampata mwanaume aliyekuwa anamtaka basi atampenda kwa kila kitu, moyo na mwili wake wote kwa haraka wakati yeye mwanaume hakupi vyote anakuangalia kwanza mpaka atakapoona kweli ndio kitu anachokitaka ndio ataanza kukupenda kwa ukweli sasa. Lakini akiona hakuna kitu atakuchukulia poa poa na baadaye anakupotezea, sasa wewe uliyekufa na kuoza lazima upate ugonjwa wa moyo. Mwanamke usiende kwenye mahusiano kwa kuangalia picha ya nje, anza kwanza kumwangalia Kama anaweza kuwa Mume na je unampenda kweli, ukijihakikishia hapo anza kuwa wife material msaidie mwanaume hata kwa mawazo tu sio unakaa tu kazi yako wewe ni kuzungusha kiuno tu. Inatakiwa ukiingia kwenye maisha ya mwanaume mwenyewe anakiri hakuna mwanamke Kama wewe. Unambadilisha hata Kama hakuwa muoaji ajue umuhimu wa mke na kutaka kukuoa. Install Application ya Udaku Special Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi =>BOFYA HAP
$
0
0
Je unawahi hufika mapema kileleni? Je uume wako hausimami imara ipasavyo? Je hupati hamu ya kurudia tendo la ndoa? Je unamaumbile madogo ya uume?

Sasa ipo tiba sahihi inayomaliza kabisa tatizo la nguvu za kiume na maumbile madogo kwa wakati.

- NGAKWA ni dawa bora ya asili inayotibu tatizo la nguvu za kiume nakulimaliza kabisa bila tatizo tena kujirudia.

- NKOMA ni dawa ya asili inayokuza na kunenepesha maumbile ya uume yaliyo madogo au kusinyaa kabisa wastani (Inch 6-7)

- Pia tunatibu matatizo mengine ya mfumo wa uzazi kwa mwanaume na mwanamke kama Ngiri, Kuvimba Korodani, Kushika au Kutia mbimba, Fangasi Sugu, Uvimbe kwenye kizazi Nk.

Dr FARU anapatikana Buguruni Dar es salaam, Piga Namba - 0755996494

HUDUMA ITAKUFIKIA POPOTE PALE ULIPO.

Mdada Aliyekwambia kujua Kuzungusha Kiuno ndo Tiketi ya Kupata ndoa Kakudanganya.. 17:33 Mapenzi Kila mwanamke anavitu vyake alivyojiwekea, ambavyo anataka mwanaume wa ndoto zake awe navyo. Ikitokea akampata Mwenye hivyo vitu basi huona kamaliza kila kitu, anajisahau, anafurahia vile anavyoviona kwa nje na kitandani, badala aanze kumsoma huyo Mwanaume. Kama ni husband material. Wanawake ndio wanaongoza kwa kulizwa Sana kwenye mahusiano kuliko wanaume, kwasababu mwanamke akishampata mwanaume aliyekuwa anamtaka basi atampenda kwa kila kitu, moyo na mwili wake wote kwa haraka wakati yeye mwanaume hakupi vyote anakuangalia kwanza mpaka atakapoona kweli ndio kitu anachokitaka ndio ataanza kukupenda kwa ukweli sasa. Lakini akiona hakuna kitu atakuchukulia poa poa na baadaye anakupotezea, sasa wewe uliyekufa na kuoza lazima upate ugonjwa wa moyo. Mwanamke usiende kwenye mahusiano kwa kuangalia picha ya nje, anza kwanza kumwangalia Kama anaweza kuwa Mume na je unampenda kweli, ukijihakikishia hapo anza kuwa wife material msaidie mwanaume hata kwa mawazo tu sio unakaa tu kazi yako wewe ni kuzungusha kiuno tu. Inatakiwa ukiingia kwenye maisha ya mwanaume mwenyewe anakiri hakuna mwanamke Kama wewe. Unambadilisha hata Kama hakuwa muoaji ajue umuhimu wa mke na kutaka kukuoa. Install Application ya Udaku Special Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi =>BOFYA HAP

$
0
0

Kila mwanamke anavitu vyake alivyojiwekea, ambavyo anataka mwanaume wa ndoto zake awe navyo. Ikitokea akampata Mwenye hivyo vitu basi huona kamaliza kila kitu, anajisahau, anafurahia vile anavyoviona kwa nje na kitandani, badala aanze kumsoma huyo Mwanaume. Kama ni husband material.

Wanawake ndio wanaongoza kwa kulizwa Sana kwenye mahusiano kuliko wanaume, kwasababu mwanamke akishampata mwanaume aliyekuwa anamtaka basi atampenda kwa kila kitu, moyo na mwili wake wote kwa haraka wakati yeye mwanaume hakupi vyote anakuangalia kwanza mpaka atakapoona kweli ndio kitu anachokitaka ndio ataanza kukupenda kwa ukweli sasa. Lakini akiona hakuna kitu atakuchukulia poa poa na baadaye anakupotezea, sasa wewe uliyekufa na kuoza lazima upate ugonjwa wa moyo.

Mwanamke usiende kwenye mahusiano kwa kuangalia picha ya nje, anza kwanza kumwangalia Kama anaweza kuwa Mume na je unampenda kweli, ukijihakikishia hapo anza kuwa wife material msaidie mwanaume hata kwa mawazo tu sio unakaa tu kazi yako wewe ni kuzungusha kiuno tu.

Inatakiwa ukiingia kwenye maisha ya mwanaume mwenyewe anakiri hakuna mwanamke Kama wewe. Unambadilisha hata Kama hakuwa muoaji ajue umuhimu wa mke na kutaka kukuoa.

Install Application ya Udaku Special Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi
=>BOFYA HAP

Mambo Ambayo Mwanaume Anafanya Kumtest Kama Msichana Anafaa Kuwa Mke Wake

Previous: Mdada Aliyekwambia kujua Kuzungusha Kiuno ndo Tiketi ya Kupata ndoa Kakudanganya.. 17:33 Mapenzi Kila mwanamke anavitu vyake alivyojiwekea, ambavyo anataka mwanaume wa ndoto zake awe navyo. Ikitokea akampata Mwenye hivyo vitu basi huona kamaliza kila kitu, anajisahau, anafurahia vile anavyoviona kwa nje na kitandani, badala aanze kumsoma huyo Mwanaume. Kama ni husband material. Wanawake ndio wanaongoza kwa kulizwa Sana kwenye mahusiano kuliko wanaume, kwasababu mwanamke akishampata mwanaume aliyekuwa anamtaka basi atampenda kwa kila kitu, moyo na mwili wake wote kwa haraka wakati yeye mwanaume hakupi vyote anakuangalia kwanza mpaka atakapoona kweli ndio kitu anachokitaka ndio ataanza kukupenda kwa ukweli sasa. Lakini akiona hakuna kitu atakuchukulia poa poa na baadaye anakupotezea, sasa wewe uliyekufa na kuoza lazima upate ugonjwa wa moyo. Mwanamke usiende kwenye mahusiano kwa kuangalia picha ya nje, anza kwanza kumwangalia Kama anaweza kuwa Mume na je unampenda kweli, ukijihakikishia hapo anza kuwa wife material msaidie mwanaume hata kwa mawazo tu sio unakaa tu kazi yako wewe ni kuzungusha kiuno tu. Inatakiwa ukiingia kwenye maisha ya mwanaume mwenyewe anakiri hakuna mwanamke Kama wewe. Unambadilisha hata Kama hakuwa muoaji ajue umuhimu wa mke na kutaka kukuoa. Install Application ya Udaku Special Uweze Pata Habari Kirahisi Zaidi =>BOFYA HAP
$
0
0


1. Ukienda kwake ukutane na vyombo vichafu na nguo chafu zimejazana usidhani ni mvivu, ni kamtihani anakupa.

2. Ukiingia kwake ukaona anampigia simu yule dada wa usafi anayekujaga mara moja kwa wiki aje afanye usafi alipwe usidhani eti anajali kihivyo. Anakutest aone kama utasema "Acha baby, ntakufulia mpenzi wangu".

3. Ukikuta kwake amefanya shopping ya vyakula vya kupika kama unga, mchele, na vingine halafu akakwambia mwende ule mgahawa fulani mkapate dinner usidhani eti ana hela kibao ya kutumia! Anakutest aone kama utamwambia mbaki kwake mpike mle. Uko chumba cha mtihani!

4. Siku kakuahidi kukutoa out halafu unafika kwake unakuta kajikunyata kama mgonjwa anakwambia mama ake kapiga simu anaumwa anaomba atumiwe hela. Halafu anakwambia hela aliyo nayo na ukipiga mahesabu unaona ni kama ile ya kutumia mkiwa out. Anakuomba ushauri afanyaje. Wewe unamwambia "Baby twende out, suala la mama nina uhakika kaka zako na dada zako watalishughulikia, atawapigia". Woiyeeee! My sista hapo umejimaliza!!

5. Ukimtembelea kwake ukakuta anapika na kufanya usafi wewe Umekaa tu unaangalia muvi halafu ukitaka umsaidie anakwambia endelea kuangalia muvi karibu anamaliza na wewe kweli ukarudi ukakaa kuendelea na muvi yako! Siku zako zinahesabika!!

6. Ulishawahi kumwambia mpenzi wako aende kwenye ibada? Alipokataa ulimsisitizia? My sister, hata walevi wanapenda wanawake ambao wanawasisitiza kwenda kwenye ibada. Sio tule wale kila siku wanashinda baa na club.

7. Mara ngapi huwa unamkumbusha kuwapigia simu wazazi au ndugu zake kuwajulia hali mkiwa wote? Angalao akupe na simu na wewe uwasalimie? Huo ni mtihani mwingine huwa mnafeli sana.

8. Jifunze pia kusisitiza kujitunza kabla ya ndoa. Sio kila saa ukimtembelea ni kujiachia tu. Inaleta adabu na inawafanya mkazanie kufikia lengo kubwa la maisha.

9. Jaribu ukiwa unaenda kwake uwe unaenda na tuvitu kama nyanya, vitunguu, n.k. Hivyo vyote huwa wanaume ni shida kununua mara nyingi.

10. Wakati mwingine nenda kwake hata na CD za dini mpelekee msikilize. Sio kila ukifika kwake wewe ni rege, Eminem, Lil Wayne na kina nani sijui. Ukiwa hivyo hataona tofauti kati yako na wale macho juu anakutana nao club kila wikiendi.
11. Jenga na tabia ya kumnunulia tuzawadi tudogo tudogo. Sometimes unakuja na boksa au kavesti au kadodoranti. Hiyo kwa wanaume inaonyesha unaweza kujipa majukumu na kuyasimamia.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za:

GUMBA POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.

NTINJE:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0754741788, 0715741788, 0783741788

-DR MAGISE

Bunge Lahairishwa Rasmi Leo Hadi Septemba

$
0
0
Bunge Lahairishwa Rasmi Leo Hadi Septemba
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametoa hoja ya kuahirishwa kwa mkutano wa 11 wa Bunge la Bajeti ulioanza Aprili 3 na kumalizika leo Ijumaa Juni 29, 2018.

Akiwasilisha hoja hiyo leo bungeni, Majaliwa amesema maswali 530 ya msingi na 1705 ya nyongeza yameulizwa na wabunge.

Pamoja na mambo mengine, Majaliwa amezungumzia masuala mbalimbali, zikiwemo halmashauri zote nchini kutenga asilimia 10 ya mikopo kwa ajili ya vijana, wanawake na wenye ulemavu na zisaidie uundaji wa Saccos shirikishi za makundi.

Kuhusu uchangiaji damu, amewaomba wananchi kujenga utamaduni wa kuchangia damu ili kuwezesha upatikanaji wa damu kwa wingi kwa wenye uhitaji.

Akizungumzia Virusi vya Ukimwi na kampeni ya upimaji Ukimwi ya Furaha Yangu, amesema hadi kufikia Machi, 2018 watu wanaoishi na VVU walikuwa milioni 1.02, kati yao watu milioni 1.0 walikuwa wanatumia dawa za kufubaza virusi hivyo.

Kwa upande wake, Spika wa Bunge Job Ndugai amesema, “tumemaliza Bunge hili maarufu la korosho na kuliwaka kweli kweli, Serikali imetuambia tuiamini na nafikiri mambo yatakwenda muswano.”

Serikali Yamtaka Prof. Jay Kufanya Jambo Hili

$
0
0
Serikali Yamtaka Prof. Jay Kufanya Jambo Hili
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga amemuagiza Mbunge wa Mikumi (CHADEMA) Joseph Haule ‘Prof. Jay’, kupeleka ushahidi kutokana na kuwa na madai ya kupotea watu 40 katika kata ya Luhembe, jimboni kwake.

Naibu Waziri Hasunga ametoa agizo hilo wakati akijibu swali la Mbunge wa Mikumi lililohoji, kuwa anaomba ufafanuzi kwa serikali juu ya kupotea kwa watu 40 jimboni kwake na hawajulikani walipo na tabia ya watumishi wa TANAPA kuwachukua wakazi wa Mikumi na kuwatesa.

Akijibu swali hilo Hasunga amesema, "Mheshimiwa Mbunge naomba ulete ushahidi wa kupotea kwa wananchi ili kutanabaisha taarifa hizo na serikali itashughulikia suala hilo maana serikali ipo kwa kulinda usalama wa wananchi”.

Naibu Waziri ameongeza kuwa serikali tayari imetatua mgogoro wa mpaka kati ya wakazi wa Mikumi na maeneo ya hifadhi.

Diwani Chadema anayedaiwa kumbaka mwanafunzi aendelea kusota rumande

$
0
0
Diwani wa Kata ya Kia (Chadema), Yohana Laizer ameendelea kusota rumande baada ya hakimu anayesilikiza kesi yake kutokuwepo mahakamani, ikielezwa kuwa yupo likizo.

Diwani huyo anatuhumiwa kwa makosa mawili ya kumbaka na kumpatia ujauzito mwanafunzi wa shule ya msingi Obrieni iliyopo Kata ya Kia Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro.

Leo Juni 29, 2018 kesi hiyo namba 152 ya 2018 ilipangwa kusikilizwa katika mahakama ya Wilaya ya Hai, lakini imeahirishwa kwa mara ya tatu kutokana na hakimu kutokuwepo mahakamani.

Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Wilaya ya Hai,  Regina Mushi  ambaye kesi hiyo kwa mara ya kwanza ilitajwa mbele yake, amesema  hakimu mwenye mamlaka ya kusikilia kesi hiyo  yupo likizo,  kwamba yeye hana mamlaka ya kuisikiliza kesi hiyo mpaka pale hakimu huyo atakaporejea.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Julai 5, 2018 kwa ajili ya  usikilizwaji wa awali.

Tanzania Yaongoza Barani Afrika Kuwa na Wanyama Wengi

$
0
0
Tanzania Yaongoza Barani Afrika Kuwa na Wanyama Wengi
Imeelezwa kuwa jitihada za serikali za kulinda rasilimali za nchi na ushirikiano kutoka kwa wananchi zimesababisha ongezeko kubwa la idadi ya wanyama pori na kuifanya nchi ya Tanzania kuwa nchi yenye wanyama wengi barani Afrika.

Hayo yamebainishwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Juni 29, 2018 katika hotuba yake aliyoitoa Bungeni wakati wakuahirisha Mkutano wa 11 wa Bunge Jijini Dodoma na kusema ili kuitumia vema fursa ya kuwa na vivutio vingi ikiwemo wanyamapori wengi na kuleta tija kwa nchi, serikali itaendelea kuandaa utambulisho wa Tanzania Kimataifa (Destination Branding), lengo likiwa ni kuitambulisha Tanzania kama kituo mahsusi cha utalii duniani.

"Tunalenga kuvutia wageni wa kimataifa waje kuitembelea Tanzania, kuongeza wigo wa kutangaza vivutio na kufanya vivutio vya utalii vifahamike duniani. Pia, serikali inakamilisha mchakato wa kuanzisha Channel maalum kwa ajili ya kutangaza utalii", amesema Waziri Majaliwa.

Kwa upande mwingine, Waziri Mkuu amesema maandalizi ya kuanzisha studio ya kutangaza utalii kwa njia ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) yanaendelea vizuri, ambapo studio hiyo itawezesha kutambua, kufuatilia na kuwasiliana moja kwa moja na watu wanaofuatilia Tanzania na vivutio vyake.

Rais wa Zimbabwe Atembelea Bagamoyo.... Amwaga Dola Elfu 10

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe, Emmerson Mnangwaga leo asubuhi ametembelea iliyokuwa shule ya wapigania uhuru wa chama cha FRELIMO ambacho hivi sasa ni Chuo cha Kilimo na Mifugo cha Kaole kilichopo Bagamoyo Mkoani Pwani.



Rais Mnangwaga akiwa chuoni hapo amesema yeye ni mojawapo ya waanzilishi wa chuo hicho katika miaka ya sitini akiwa pamoja na viongozi wengine wa Chama cha FRELIMO na kwamba alikuwa kiongozi wa ulinzi wa chuo hicho na kwamba hawakuwa na dhumuni la kutafuta madaraka bali ilikuwa ni jitihada zilizosukumwa na uzalendo wa kuzipatia nchi zao uhuru,” Rais Emmerson Mnangwaga.

Rais Mnangwaga amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli kwa kumpa fursa ya kuitembelea Shule hiyo kwa kuwa ilikuwa ni shauku yake baada ya kuondoka shuleni hapo miaka 58 iliyopita na kuwashukuru wananchi wa eneo hilo kwa kumtunza katika kipindi chote alichoishi Bagamoyo na kwamba hata sasa anajisikia kuwa ni mmojawapo wa jamii ya watu wa Bagamoyo,” Amesema Rais Mnangwaga.

Pia Rais Mnangwaga ametoa kiasi cha Dola elfu kumi kwa mkuu wa chuo hicho kama shukrani yake ambazo amesema zitasaidia kutatua baadhi ya changamoto chuoni hapo.

Tumia Super Mkuyati Kuleta Heshima ya Ndoa

$
0
0

SUPER MKUYATI INAYOLETA HESHIMA YANDOA super mkuyati nidawa ya mitishamba iliyo sheheni miti mbalimbali na kugundulika ina pambana na magonywa sugu

SUPER MKUYATI inanguvu (3) nainafanya kazi kwapamoja (1) itakufanya uchelewe kufika kileleni ndani ya dk 15-20 bila kuchoka (2) ina zalisha homon kwa wingi na kukufanya uwe na mbengu nyingi zenye vimeleo vya uzazi vyilivyokomaa (3) inaongeza ume mdogo uliosinyaa,kunenepesha uume na kurefusha adi nchi 5-8 na upanda sm 2-3 dawa hii haina mazala kwa mtumiaji ata kwa wazee walionaumri 60-80

SUPER MKUYATI ponyo la maradhi yako tumia Leo uone mjabu yake OFISI YETU ZINAPATIKANA DR MTONI KIJICHI KAMAUNA NAFASI UTALETEWA POPOTE ULIPO KWALE WAMIKOANI UTATUMIWA

DR GATUNDU SM 0717777402/0768408794

'Saratani ni ugonjwa ambao unarithiwa siyo kuambukizwa'

$
0
0

Saratani ni ugonjwa ambao unaweza kuathiri kiungo chochote cha mwili, ikiwa utapata matibabu haraka, unaweza kupona, lakini ukikawia bila kupata matibabu, husababisha kifo, ni ugonjwa unaosababisha vifo vingi kutokana na gharama za matibabu. 

Saratani ni ugonjwa usiokuwa wa kuambukiza lakini unaweza kurithi kutokana na vinasaba, akizungumza na Eatv Dkt. Sarah Maongezi kutoka kitengo cha magonjwa yasiyo ya kuambikiza, Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto amezitaja saratani ya matiti kwa akina mama pamoja saratani tezi dume kwa wanaume. 

"Saratani haiambukizwi lakini unaweza kurithi na zinazoweza kurithika ni zile zinazotokana na vinasaba pekee ambazo ni saratani ya matiti kwa wakina mama na tezi tume kwa wakina baba”, amesema Dkt. Maongezi. 

Saratani nyingine za kawaida ambazo huwaathiri wanaume kwa wanawake ni saratani ya mapafu, utumbo, maini, mdomo na ngozi.

Maradona atenga kitita kirefu kumnasa aliyemzushia kifo

$
0
0

Nyota wa zamani wa timu ya taifa ya Argentina Diego Maradona ametangaza ofa ya dola 10,000 za Marekani (sawa na Tsh. Milioni 22,75) kwa mtu atakayefanikisha kumpata aliyesambaza taarifa kuwa amekufa. 

Kuenea kwa taarifa za uzushi wa kifo chake kwenye mitandao na vyombo vya habari kumekuja muda mchache baada ya mchezo kati ya Argentina na Nigeria Juni 26 ambapo Argentina ilinusurika kuondoshwa katika hatua ya makundi na timu ya Nigeria. 

Katika Mchezo uliokuwa wa ushindani mkubwa, Argentina ilipata goli la ushindi dakika za mwisho wa mchezo ikijikusanyia alama 3 kwa kupata magoli 2-0 dhidi ya Nigeria. 

Maradana amecheza kombe la dunia mara nne akisaidia timu yake kuchukua kombe hilo mwaka 1986, na baadae kuwa mkufunzi wa Argentina kwa miaka miwili.

Bombadier yaliongezea thamani shirika la ndege

$
0
0

Biashara ya shirika la ndege la AIR Tanzania Company Limited (ATCL) imepanda thamani kwa kipindi cha miaka miwili licha ya kuwa na abiria wachache waliotumia ndege zake kusafiria 

Mkurugenzi wa biashara wa ATCL Patrick Ndekana aliambia gazeti la Daily News kwamba biashara za shirika hilo la serikali iliongezeka kutoka asilimia 2.5 mwaka 2016 hadi asilimia 42.6 mwisho wa mwaka jana huku ikiwa na ndege mbili pekee zinazofanya kazi. 

Amesema kuwa wana matumaini kwamba biashara hiyo itaimarika zaidi baada ya kununuliwa kwa ndege mpya. 

''Mwaka huu biashara yetu itaongezeka hususan baada ya kuwasili kwa ndege ya tatu kubwa aina ya Bombadier Q-400s na baadaye kuwasili kwa Bombadier nyengine mbili za Cs 300s ambazo zitakuwa na viti vingi'', alisema. 

Kwa sasa shirika hilo linamiliki ndege tatu aina ya Q-400 katika maeneo 10 tofauti nchini, mbali na kuelekea Comoro. 

Mkurugenzi huyo alisema kuwa hadi kufikia mwisho wa mwaka jana, shirika hilo limekuwa likisafirisha abiria wachache na kufanya safari chache ikilinganishwa na washindani wao. 

ATCL inapanga kuleta ndege hizo mpya kupitia kuongeza safari hususan katika maeneo ya Kaskazini , magharibi kaskazini mashariki. 

Ndege hizo za serikali zinapanga kuanzisha safari za kuelekea Bujumbura, Burundi kupitia Kigoma na Entebbe, Uganda kupitia Kilimanjaro.

Gigy Money aeleza namna alivyomsamehe Mo Jay ‘nitamzalia hata watoto wanne’

$
0
0

Video vixen Gigy na muimbaji Gigy Money amesema kwa sasa yupo pamoja na baba mtoto wake Mo Jay ikiwa ni miezi kadhaa toka wagombane na kurushiana maneno ya kashfa kupitia mitandao ya kijamii. Gigy amesema kwa sasa yupo tayari hata kumzalia watoto kwa kuwa amegundua mtangazaji huyo wa Choice FM ni mwanaume makini.

VIDEO:

Bongo5

Maamuzi ya Rais Magufuli kuhusu sherehe ya mashujaa

$
0
0
Rais Dkt. John Magufuli ameagiza shilingi milioni 308 zilizotengwa kwa ajili ya maadhimisho ya siku ya kumbukumbu ya Mashujaa, zitumike kuboresha miundombinu ya barabara Jijini Dodoma.

Taarifa hiyo imetolewa na Waziri Mkuu jana Juni 29, 2018, wakati akizindua kituo cha Polisi kinachohamishika katika hafla iliyofanyika eneo la Kisasa, Jijini Dodoma na kusema Rais Magufuli ametoa agizo hilo ili fedha hizo ziende kukarabati miundombinu ya barabara pamoja na taa za kuongezea magari katika barabara ya kisasa na taa za barabarani kwenye barabara mpya ya Emmaus-African Dream yenye urefu wa kilomita 1.4, ambayo kwa sasa inajengwa kwa kiwango cha lami.

"Kutokana na msongamano uliopo ambao unaweza kusababisha ajali. Mheshimiwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu, Dkt. Magufuli ameamua fedha zote zilizoandaliwa kwa ajili ya maadhimisho hayo zitumike kuboresha barabara. Pia ameawataka watanzania wote waadhimishe siku hiyo ya kumbukumbu ya mashujaa kwa kufanya usafi katika maeneo yaliyo jirani na makazi yao pamoja na yale ambayo wamezikwa mashujaa ikiwa ni njia ya kuwaenzi", amesema Waziri Mkuu.

Kufuatia uamuzi huo, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewaagiza Wakuu wa Mkoa waratibu zoezi hilo kwenye maeneo yao.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ameliagiza Jeshi la Polisi lianze kujikita kwenye matumizi ya mifumo ya kiulinzi ya kielektroniki yaani 'City Surveillance Sytems' ili limudu kudhibiti hali ya sasa ya uhalifu.

Kila ifikapo Julai 25 ya kila mwaka Tanzania huadhimisha siku ya mashujaa kama sehemu ya kuwaenzi mashujaa hao ambao waliipigania nchi hii kwa namna moja ama nyingine.

Download Hapa Application ya Udaku Special Kwenye Simu Yako Kushuhudia Vimbwanga Mtaani na Stori za Mapenzi

Viewing all 104712 articles
Browse latest View live


Latest Images