Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

Ladies: True Love Means Give And Take..Tunawapenda Sana ila Msitugeuze Gari la Mshahara

0
0
Mimi ni mwanaume wa miaka kadhaa..Kilichonipelekea kuleta hii mada ni kwamba kila mwanamke ninayeamua kuwa nae ananipa majukumu mengi hata kabla sijamtamkia kwamba nimeamua kuwa nitamuoa, sikatai kwamba kumsaidia mpenzi wako ni jukumu ambalo haliepukiki lakini msaada unaotolewa usiwe ndo kigezo cha uwepo wa mapenzi yetu, kwa kipindi kirefu nimevumilia hili toka kwa wanawake kadhaa lakini sasa naona kama naelekea kushindwa, mimi binafsi najihisi kama nina mkosi vile kwa heshima yako naomba waeleze wasichana/wanawake kwamba wakati mwingine sisi wanaume tunakuwa na nia kabisa ya kuanzisha uhusiano imara wenye uwezo wa kuzaa ndoa,


Wanaume wengi unakimbizwa na "Mizinga" yao ya kila siku.katika mapenzi kuna kusaidiana, ila naona kama wenzetu wanawake wameona msaada pekee wa kupewa ni pesa, au wao pekee ndo wanastahili msaada,Wanawake wengi huwa wanaharibu uhusiano bila kujua, hakuna asiyekubali kwamba kusaidiana katika mahusiano ni jambo jema linalokubalika, lakini sasa imzidi jamani, si kila siku mtu unakuwa na pesa ya kukupa na pia ikumbukwe kwamba suala la kusaidiana katika mahusiano si la upande mmoja sote twawajibika kusaidiana, wanawake wengi baada ya kuwa katika mahusiano huamini kupata mtatuzi wa shida zake zote.

Mwanaume mwenye nia ya kweli na wewe akianza kukuona unaanza kumgeuza kitega uchumi, taratibu huanza kuzua visingizio vya kutoonana na wewe mwishowe anaishia zake.

Kitu kingine ambacho wanawake hawajui, si kila tatizo unampelekea mpenzi wako, mengine peleka kwa ndugu zako, hivi kila siku mnapotuomba pesa mwafikiri twazitoa wapi?

Sio wote wauza sembe, wanawake wengine wana kipato zaidi ya wanaume lakini bado hata kile kidogo tukipatacho mwataka, wewe kila kitu pesa, kwani mimi ndo nazitengeneza? hata kama unahisi ninazo nyingi, basi unadhani zote ni kwa ajili yako?

Hata mimi nina familia ya wazazi, wadogo zangu nk, nahitaji kuwahudumia, Tuhurumiane jamani, True love means give and take, twawapenda sana wake/wapenzi wetu lakini msitugeuze gari la mshahara

Najua tabia hii si kwa wanawake wote, lakini asilimia kubwa ndo hao, naomba kupitia blog hii tujaribu kuwekana sawa,kwa wale ambao wana tabia hizi na mnawajua, waelezeni,mnatuumiza, na ndiyo maana hatuishi kusikia vituko vya kina kaka kuwaachia bili wanawake katika sehemu za starehe,kujifanya wanaenda msalani,kumbe anakimbia kukwepa aibu,kwa maana hela ya kulipa hana

Rais Magufuli Asali Ibada Kanisa la Mtakatifu Petro Jijini Dar es Salaam Leo

0
0
RAIS MAGUFULI ASALI IBADA KANISA LA MTAKATIFU PETRO JIJINI DAR

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo Julai 1, 2018 ameungana na waumini wengine kusali Ibada ya Jumapili, Dominika ya 13, katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay jijini Dar es salaam.


Rais Magufuli akipokea mkate wa Sakramenti alipoungana na waumini wengine kusali Ibada ya Jumapili, Dominika ya 13, katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay jijini Dar es salaam.

Mmiliki wa mabasi ya Zakaria ahojiwa kwa tuhuma za kuwapiga risasi maofisa usalama wa Taifa

0
0
Mmiliki wa kampuni ya mabasi ya Zakaria, Peter Zakaria anashikiliwa na polisi kwa mahojiano kwa tuhuma za kuwajeruhi kwa risasi watu wawili wanaodaiwa kuwa ni maofisa usalama wa Taifa.

Ingawa mazingira ya tukio hilo na nini maofisa hao walifuata kwenye kituo cha mafuta kinachomilikiwa na mfanyabiashara huyo hayajajulikana, mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima alisema jana mjini Musoma kuwa, tukio hilo lilitokea saa mbili usiku wa Juni 29.

Malima alisema baada ya kuwajeruhi kwa risasi maofisa hao, Zakaria alidhibitiwa na maofisa wengine ambao walimfikisha Kituo cha Polisi mjini Tarime.

Akifafanua, mkuu huyo wa mkoa alisema kabla ya tukio hilo, maofisa usalama watano walifika katika kituo hicho cha mafuta kwa nia kujaza mafuta gari lao, ndipo wenzao wawili walishuka na ghafla kushambuliwa kwa risasi.

“Baada ya wenzao kujeruhiwa kwa risasi, maofisa wengine walifanikiwa kumdhibiti Zakaria na kumtia mbaroni na kumkabidhi kwa polisi wanaoendelea kumhoji,” alisema.

Kwa mujibu wa Malima, maofisa waliojeruhiwa wamelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Tarime kwa matibabu huku mmoja akidaiwa kuwa katika hali mbaya.

Kuhusu tukio la polisi kutumia mabomu ya machozi kuutawaanya umati wa wananchi waliokusanyika eneo la hospitali hiyo, kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Tarime/Rorya, Henry Mwaibambe alisema lililenga kurejesha utulivu baada ya wananchi kuhamaki wakitaka kuingia kumuona Zakaria kutokana na kuzagaa taarifa kuwa amejeruhiwa na kulazwa.

Akizungumza kwa sharti la kutotajwa jina, mmoja wa wafanyakazi wa kituo cha mafuta, alidai Zakaria alifyatua risasi ili kujihami baada ya kuhisi kuwa watu walioshuka kwenye gari wakielekea ofisini kwake walikuwa majambazi.

“Kwa kawaida muda ule bosi huwa anapokea fedha za mauzo kutoka sehemu mbalimbali za biashara zake ikiwamo mabasi na vituo vya mafuta. Kitendo cha watu watano kufika na wawili kushuka kuelekea ofisini kwake kiliibua hofu ya usalama kutokana na matukio ya ujambazi, ndipo akaamua kujihami,” alisema mfanyakazi huyo.

Alisema baada ya wenzao kujeruhiwa, watu watatu waliobaki kwenye gari waliteremka na kumkamata Zakaria huku wakijitambulisha kuwa maofisa usalama, hali iliyozua mvutano walipotaka kuondoka naye kwa sababu wafanyakazi hawakuwa na uhakika iwapo walikuwa wema au wahalifu.

Mvutano huo ulisababisha milio ya risasi na watu hao kuondoka na Zakaria kwa nguvu huku wakisababisha hofu kuwa huenda mfanyabiashara huyo ametekwa, jambo lililoibua taharuki mjini Tarime.

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

Neno (Naumia) Wakati wa Tendo la Ndoa Kutoka Kwa Mwanamke Lanitatiza

0
0
Kwakifupi ni hivi:-
Kila tufanyapo tendo la ndoa, mwenzangu hutoa kilio pasipo machozi, huku ameikunja sura yake na wakatihuo hutamka neno Naumia... Hii kitu imekua inanipa wakati mgumu na kunifanya nimuonee huruma mpenzi wangu na kumuuliza, nitoke? chakushangazi yeye hukataa na Kuniambia usitoe na huku anuonyesha kufurahia tendo.

Maswali:-
Je, hulia kwa kupata maumivu?
Je, hulia kwa kuhisi raha?
Je, nawengine wanaliaga kama wangu?
Je, hutoa kilio kwa mbwembwe tu?

Naombeni ushauri wenu wakuu

Rapa Mwingine Aiawa Kwa Risasi Marekani, ni Rafiki wa Damu wa Drake

0
0

Ikiwa zimepita siku mbili tu tangu Rapa Drake aachie album yake mpya ya Scorpion, mkali huyo kutoka Canada usiku wa kuamkia leo amepatwa na msiba mzito wa rafiki yake mkubwa nchini Canada ambaye pia ni rapa aitwaye Smoke Dawg. 

Imeelezwa kuwa rapa Smoke Dowg amepigwa risasi na watu wasiojulikana kwenye vurugu jijini Toronto na tayari Drake kupitia ukurasa wake wa Instagram amethibisha taarifa hizo. 

Ukaribu wa Rapa Smoke Dawg na Drake ulianza mwaka jana baada ya Rapa  kujizolea umaarufu nchini Canada kwa kufanya remix ya wimbo wa Trap House ya French Montana. Tazama video ya wimbo wake wa mwisho alioutoa wiki iliyopita. 

Habari Njema Kwa Wanaume Wote Wenye Matatizo ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

0
0
Je unawahi hufika mapema kileleni? Je uume wako hausimami imara ipasavyo? Je hupati hamu ya kurudia tendo la ndoa? Je unamaumbile madogo ya uume?

Sasa ipo tiba sahihi inayomaliza kabisa tatizo la nguvu za kiume na maumbile madogo kwa wakati.

- NGAKWA ni dawa bora ya asili inayotibu tatizo la nguvu za kiume nakulimaliza kabisa bila tatizo tena kujirudia.

- NKOMA ni dawa ya asili inayokuza na kunenepesha maumbile ya uume yaliyo madogo au kusinyaa kabisa wastani (Inch 6-7)

- Pia tunatibu matatizo mengine ya mfumo wa uzazi kwa mwanaume na mwanamke kama Ngiri, Kuvimba Korodani, Kushika au Kutia mbimba, Fangasi Sugu, Uvimbe kwenye kizazi Nk.

Dr FARU anapatikana Buguruni Dar es salaam, Piga Namba - 0755996494

HUDUMA ITAKUFIKIA POPOTE PALE ULIPO.

Gigy Money 'Mimi Ndio Staa wa Kike Mwenye Nguvu Kushinda Wote Bongo, Simjui Wema Sepetu'

0
0
Msanii wa muziki na video vixen, Gigy Money amedai kwa sasa yeye ndiye staa namba moja wa kike Tanzania mwenye nguvu na pia kutokana na deal mbalimbali ambazo anapata huku akidai kwamba hamjui Wema Sepetu...Adai Watu hawakubali tu ila yeye ndio staaa Mkubwa wa kike kuliko wote Bongo

VIDEO:


China inavyoitikisa Marekani kiuwekez

0
0

Haya ni baadhi ya masuala ya uwekezaji yanayoonyesha kuwa China taifa linaloibukia kuwa na nguvu zaidi duniani linainyemelea, kuinunua na kuimaliza  Marekani kiuchumi, kama ilivyoandikwa kwenye mtandao wa Industry Week.

“Sisi Waamerika kwa muda mrefu tunapuuza athari zinazotokana na  kuruhusu kampuni na mashirika ya kigeni kununua mali zetu ziwe kampuni, ardhi na maliasili nyingine.Tunauza uwezo wetu wa kuzalisha mali na utajiri kwa wageni kwa kuruhusu mashirika yetu mengi kununuliwa na wageni.Lakini si wageni tu ni mashirika ya Kichina , tena kampuni zinazomilikiwa na Serikali ya China .Ni hatari kwani China inatumia mashirika yake ya umma kimkakati kwa kujifanya kuwa ni kampuni binafsi zinazoendeshwa kwa nguvu ya ushindani wa soko na imetungiza mkenge na kutufanya tuonekane kama majuha wakubwa wanaodanganyika kwa wepesi hapa duniani.” Inasema taarifa ndani ya mtandao wa  ‘Industry Week’  kwenye makala iliyoandikwa Januari 2018.

Hivi ni nani aliyeguswa na taarifa za kuuzwa kwa kiwanda kikubwa cha kuzalisha bidhaa za nguruwe cha Marekani cha ‘Smithfield Foods,’kununuliwa na shirika moja la China mwaka 2013?

Wanahisa waliruhusu mauzo kwa mwekezaji kampuni ya Shuanghui International Holdings Limited, mwekezaji mkubwa na msindikaji wa nyama wa China.

Ni wachache waliotafakari wakati kampuni ya Hoover, ilipouzwa kwa kampuni ya kielektroniki ya Hong Kong, iliyoko China iitwayo Techtronic Industries, muamala uliofanyika mwaka 2006 , baada ya kampuni ya Maytag, iliyokuwa inamilika Hoover, iliponununuliwa na Whirlpool.

Hoover ni kampuni iliyokuwa inazalisha vifaa vya usafi vya kielektroniki. Mashine za kusafisha vitu mbalimbali kwa kutumia ‘presha’ yanayotumiwa kusafisha mazulia, viyoyozi, injini za magari na kompyuta,wakati Whirlpool ni kampuni ya kuzalisha vifaa vya jikoni kama majiko, friji na mashine za kuoshea vyombo.

Aidha, Januari mwaka 2014, ulianza kwa kampuni ya Motorola Mobility kuuzwa kwa kampuni ya kielektroniki na teknolojia za kompyuta ya Kichina ya Lenovo yenye makao makuu jijini Beijing.

“Hii inamaanisha kuwa taifa kubwa lililogundua utaalamu na uwekezaji wa simu za mkononi ambalo ni Marekani limetupwa nje ya ulingo wa kuzalisha simu hizi. Muamala huu na mauziano umeipa China, teknolojia babu kubwa na uwezo wa juu wa kuzalisha simu duniani. Lenovo hiyo ndiyo tena iliyoinunua kampuni ya kompyuta ya IBM’mwaka 2004.” Inalalamika makala ya Industry Week.

“Kwa kutumia mkakati huo wa serikali kufanya manunuzi ya kampuni zetu, China imejiwezesha kuwa taifa linalotuuzia vifaa na mahitaji yote ya kinishati . Kuanzia 2009, kampuni zake zimewekeza mabilioni ya dola kununua hisa za kampuni za nishati kama The AES Corp., Chesapeake Energy, Oil & Gas Assets. Katika mwaka wa 2010, Kampuni ya Mawasiliano ya Kichina ya China Communications Construction Co. ilinunua asilimia 100 ya kampuni ya Friede Goldman United, wakati mwaka 2012, kampuni ya nguvu za upepo ya A-Tech Wind Power (Jiangxi) ilinunua kwa asilimia 100 kampuni ya Cirrus Wind Energy.”

Mwaka 2016, hoteli  bora za Marekani za Starwood Hotels , zilinunuliwa na Anbang Insurance, kampuni ya bima ya Kichina, ambayo sasa imecharuka kununua hoteli za Marekani. Mwaka jana kampuni hiyo ya bima ilinunua hoteli ya kisasa iliyoko New York ya Waldorf-Astoria. Hoteli ya Starwood ikaongeza idadi ya hoteli zilizonunuliwa na China kufikia 1,300 kote duniani mmiliki akiwa ni kampuni hiyo ya Beijing ya Anbang.

Kampuni nyingine ya Marekani ambayo sasa iko mikononi mwa Beijing ni Ingram Micro, ilinunuwa na Tianjin Tianhai Investment Development Company, inayojihusisha na usafirishaji wa anga na vifaa vya aina na matumizi mbalimbali.

Nyingine ni General Electric Appliance Business, iliyonunuliwa na Qingdao Haier Co, wakati Terex Corp yenye miaka 83, iliyokuwa na makao yake makuu jijini Connecticut, ikizalisha mashine na vifaa vya ujenzi, kilimo na viwanda ilipigwa mnada na kununuliwa na  Zoomlion Heavy Industry Science ya Beijing.

China inanunua hadi masuala ya burudani inaelezwa kuwa imenunua kampuni ya Legendary Entertainment Group, ambayo awali ilikuwa ikishirikiana na wadau kudhamini na kufanikisha sinema kali duniani kama Jurassic Park, Godzilla na Pacific Rim, sasa ziko mikononi mwa Wachina ndani ya kampuni yao ya Dalian Wanda.

Dalian Wanda, ilinunua pia kampuni ya burudani ya AMC Entertainment Holdings, iliyokuwa kampuni ya pili kwa ukubwa ya Marekani ya kutengeneza sinema wakati inauzwa, leo imepanda ni ya kwanza kwa ubora.

CHANZO

“Nchi nyingi haziruhusu umiliki wa asilimia 100 wa kampuni zake kwa wageni , lakini Marekani haibabaiki. Tunaruhusu kampuni za Kiamerika kuuzwa kwa wageni , labda kwa zile ambazo zina masuala ya usalama na maslahi ya taifa. Lakini cha kushangaza hatuoni mataifa tunayoyauzia yakituuzia kampuni zake.

Serikali ya China inadhibiti na kuzuia kampuni za kigeni kumiliki viwanda vyake kwa asilimia 100. Inasisitiza ubia kwa kampuni na viwanda vyake kwa kila anayetaka kuwekeza.

Kinachowawezesha Wachina kununua mali zetu ni pengo kubwa la kibiashara baina yetu na China. Ndiyo maana wanajichukulia kidezo makampuni yetu kwa vile kila tunapouza bidhaa hatuwatoshelezi na wanahitaji zaidi, wakati sisi tunanunua kidogo kutoka kwao.

Kwa takribani miaka 20 sasa tumekuwa tukiuhamishia utajiri wa Amerika kwa Wachina tukiwatajirisha kwa mamilioni ya dola. Mwaka 1994,pengo la kibiashara  (trade deficit) kati ya Marekani na China lilikuwa dola bilioni 29.5 , na lilikua hadi kufikia dola bilioni 83.8 mwaka 2001 wakati China ikipewa makaribisho makubwa kwenye Shirika la Biashara Duniani (WTO) ikiheshimika kama taifa linalokubalika zaidi duniani.

Kwa miaka mingi pengo hilo limekua na kuongezeka na sasa ilipofika 2016 limefikia dola bilioni 347.

KUTOTUMIA SHERIA

Kwa nadharia Marekani ina uwezo wa kuzuia uuzwaji wa mashirika yake kupitia kamati ya kuishughulikia  uwekezaji wa kigeni ‘Committee on Foreign Investment in the United States- CFIUS.’

Kamati hii ina mamlaka kisheria kurekebisha, kukataa au kuidhinisha ununuzi wa mashirika na uwekezaji wowote wenye mashaka, lakini CFIUS haijatumika kudhibiti ununuzi huu.

Athari za kampuni za kigeni kununua mashirika ya Marekani zilitajwa na mwaka 2013 na Ripoti ya Baraza la Bunge la Juu (Congress) ya Mapitio ya Kiusalama katika uwekezaji baina ya China na marekani.

Ilionya kuwa:“China inawasilisha kitisho kipya kwa kamati ya CFIUS, kwa sababu uwekezaji unaofanywa na mashirika yake ya umma unaweza kuondoa ama kutatiza mipaka baina ya usalama wa taifa na wa uchumi na uwekezaji .”

China inatajwa kuwa ina kiasi kikubwa cha akiba ya fedha za kigeni kwenye benki kuu kikifikia dola trilioni  3.66 na inahofiwa kuwa zaidi ya asilimia 70 ni dola. Aidha ina mabilioni ya mali (assets) yaliyo kwenye ardhi,majengo, utaalamu na teknolojia vyote hivyo vikitikisa mahasimu wake.

Tanzania na Afrika zinaweza pia kujifunza kile kinachotokea miongoni mwa mataifa haya makubwa na kujipanga vizuri kwenye uwekezaji wa miradi ya kiuchumi.

Ratiba Ya Mechi Za Hatua Ya 16 Bora Kombe La Dunia 2018 Urusi

0
0

*Jumamosi, Juni 30*

1. 🇺🇾Uruguay🆚Ureno🇵🇹(11:00 jioni)

2. 🇫🇷Ufaransa🆚Argentina🇦🇷(3:00Usiku)

*Jumapili Julai 1*

3. 🇪🇸Hispania 🆚Urusi🇷🇺(11:00)

4. 🇭🇷Croatia🆚Denmark🇩🇰(3:00 Usiku)


*Jumatatu Julai 2*

5. 🇧🇷Brazil🆚Mexico🇲🇽(11:00Jioni)

6. 🇧🇪Ubelgiji🆚Japani🇯🇵(3:00 Usiku)


*Jumanne Julai 3*

7. 🇸🇪Sweden🆚Uswisi🇨🇭 (11:00 Jioni)

8. 🇨🇴Colombia🆚England🇽🇪(3:00 Usiku)

BREAKING NEWS: Ajali mbaya yatokea, Kontena laangukia daladala tatu

0
0

Habari zilizotufikia hivi punde, zinaeleza kwamba ajali mbaya imetokea muda mfupi uliopita, eneo la Mbalizi, Mbeya likihusisha lori la mizigo (kontena) lililopoteza mwelekeo na kuziangukia daladala tatu, Toyota Hiace na kusababisha madhara makubwa. 

Juhudi za uokoaji zinaendelea eneo la tukio na mpaka sasa bado haijafahamika idadi ya majeruhi na kama kunab taarifa za vifo. 

Kwa taarifa zaidi, endelea kufuatilia hapahapa. 

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME DR SITTA NDO SULULISHO LAKO tatiza, hili limekuwa likiwaasili watu wengi,sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine, kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo zipo , sababu nyingi zinazosababisha, tatizo hilo baadhi ni (i) upungufu wa vichocheo vya HORMONES ZA CETROGEN ambazo mwanaume, anapobarehe vichocheo hivi, HORMONES hizo, husaidia ukuaji wa uume

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mlija iliysinyaa,

NSHOLA ni dawa bora, ya kurudisha nguvu, za, kiume bari inatibu ,kabisa kutoa tatizo hilo, na kukupa , hamu ya , kurudia tendo, la ndoa zaidi, ya mala nne 4 ,bila kuchoka atakama unaumli ,wa mika 80,! pia ana ,dawa za ,kutibu, presha ya kupanda ,na kushuka, kisukari kuondoa, mafuta , mwilini ,na maumivu ya, mgogo kiuno, dawa zipo, matazo, ya hedhi, kwa ,wanawake hedhi, zisizokuwa na, mpangilio, na kasonono, pia , vidonda ,vya, tumbo ,(STOMACHI UCLENS) IHUSHI ndoji lako.

NKANYA ni dwa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi ariyekuacha, mke mme, atakuludia kwa, mda, wa msaa3 tu , ukishaitumia atarudi ,mwenyewe bila ,ugovi tena, NKOMA ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada .

HERBON, ni, dawa, ya kuongeza, CD4, NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu ,miguu, kufaganzi, na ,kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! DR SITTA, amebobea, kwa tiba asilia

DAR ANAPATIKANA MBAGALA, ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI SHINYANGA, KAHAMA MJINI, KWA MAELEZO ZAIDI ,

PIGA SIMU 0763172670 au 0715172670

WOTE MNAKALIBISHWA, KAMA, UTAKUWA NA TATIZOUTAHUDUMIWA

Ushamba chanzo cha kutoendelea Tanzania

0
0

Mwenyekiti Kamati ya muda ya uongozi wa Chama cha Wananchi  CUF, Julius Mtatiro amesema, Tanzania inaonekana kuchelewa kusonga mbele kutokana na ushamba wa viongozi na kutojali vizazi vijavyo ndiyo maana mpaka sasa hoja ya uraia pacha inashindwa kupitishwa.


Mwenyekiti Kamati ya muda ya uongozi wa Chama cha Wananchi  CUF, Julius Mtatiro.

Mtatiro amesema kwamba sheria zilizopitwa na wakati ndizo zinafanya sheria ya Uraia pacha kwenye Katiba kushindwa kufanyiwa marekebisho, na hata wakati wa mabadiliko ya katiba kulikuwa na ukiritimba wa ung'ang'anizi wa mambo ya kale yaliyopelekea isibadilishwe.

Mtatiro amesema kwa ajili ya maendeleo ya uchumi, Tanzania ilipaswa kuwa na Uraia pacha  ili kuwaruhusu watu wanaopenda kuwa na uraia wa Tanzania wapate na hiyo ingesaidia hasa pale ambapo wangeamua kufanya uwekezaji na hata katika suala zima la ulipaji kodi.

"Hizi siyo zama za kina Nyerere na Uhuru, hizi ni zama ambazo kila nchi serikali inajitanua kutumia rasilimali za ndani na nje kupanua uchumi wa nchi yake" Mtatiro.

"Roho mbaya, ukale na ushamba pamoja na kuwa na viongozi wasiokuwa na 'focus' kwa vizazi vijavyo ndiyo maana kama Taifa tunaonekana tumechelewa" ameongeza

Hata hivyo Mtatiro anashangaa kuona kwamba suala la usalama linahofiwa katika suala la uraia pacha, wakati kama mtu mwenye uraia wa nchi akiiba au akiua ataweza kukamatwa mahali popote alipo kutokana na teknolojia kukua duniani kote hivyo hakuna haja ya serikali kuhofu.

Rais Magufuli afanya uteuzi: Waziri Mwigulu atemwa, Lugola aula. Mbarawa ahamishiwa Maji na Umwagiliaji

0
0

Rais Magufuli amefanya uteuzi leo :

Kangi Lugola - Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi

Musa Ramadhani Sima - Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais

Omary Mgumba - Naibu Waziri wa Kilimo

Prof. Makame Mbarawa - Waziri wa Maji na Umwagiliaji

Mhandisi Isack Kamwelwe - Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Athumani Kihami - Katibu wa Uchaguzi NEC.

Stay tuned..

Jamani Naombeni Msinilaumu Kwa Uamuzi Huu Niliouchukua Kwa Mume Wangu

0
0
Mimi nimeolewa miaka 15 sasa na tumejaaliwa watoto 4. Ndoa yetu ilipofikisha miaka 4-5 mume wangu alicheat, nikamkamata through sms akapinga sana lakini baadae alikubali akakiri kosa na kuomba msamaha nikamsamehe

Tumeendelea kuishi na nilipopata mtoto wa tatu akanicheat tena, safari hii alikuwa nje ya nchi kimasomo, napo alikiri na kuomba msamaha, nikamsamehe

Wakati niko mjamzito mimba ya mtoto wa nne alinicheat tena, kibaya zaidi alinicheat na house girl wanga akampa ujauzito. kwa hivyo wakati mimi nina mimba na House girl naye mjamzito (japo sikujua kama house girl alikuwa mjamzito kwani aliondoka nyumbani) niligundua baadae kuwa mtoto wa aliyekuwa house Girl wangu ni wa mume wangu

Kama kawaida yake akaomba msamaha safari hii hadi kupiga goti na kulia ili nimsamehe...na mimi kwa kuwa bado nampenda na nimemvumilia kwa mengi nikaamua kumsamehe tena..ila tulikubailana masharti mengi na akakubali masharti yote niliyompa..mwanzoni alibehave vizuri sana akawa muwazi kwangu hanifichi chochote kuhusu huyo mtoto.. na tuliishi maisha ya furaha kwani alinijali mno na alionekana kweli amerigrate.
sasa cha kushangaza siku za karibuni amebadilika sana, amekuwa msiri na hasemi chochote kuhusu huyo mtoto wa nje..siku hizi anatuma hela kwa siri na pia anawasiliana na huyo mama wa mtoto kwa siri haniambii chochote..

Nilipoona mabadiliko niliamua kumuuliza imekuwaje tena mbona siri tena wakati tulikubaliana kila kitu kiwe open? hakunijibu isipokuwa alikuwa mkali na kufoka na kusema hilo swala tumeshamalizana nalo sitaki kulisikiasikia tena..

Nikajaribu tena siku nyingine kumuuliza na majibu ndio hayo hayo, kwa kifupi hataki na anakwepa kuzungumzia hilo suala kabisa...sasa najiuliza kwa nini anafanya siri? kama hakuna jambo lolote baya basi anaficha nini? ina maana kuna kitu zaidi ya mtoto.

Sasa jamani mimi nimeamua kama ifuatavyo:

1. Na mimi nimeamua kuwa na mahusiano nje ya ndoa, jamani msinilaumu nami pia nahitaji kuliwazwa na kufarijiwa kwa kifupi nimechoka na mastress yasiyo kuwa na mwisho, sikuwahi kumcheat mume wangu katika maisha yote ya ndoa. ila sasa atanisamehe tu hata akijua wala sijali, nipo tayari kwa lolote..

2. Sina mpango wa kuondoka kwenye nyumba tuliyojenga pamoja nitaishi hapa hapa kwani sipendi watoto wangu walelwe na mzazi mmoja..watoto hawajui kinachoendelea in fact hata ndugu na jamaa hawajui chochote kwani mimi sijawaambia na wala sijawahi kuwaeleza matatizo ya ndoa yangu..kwa nje tunaonekana familia iliyobarikiwa na ina furaha lkn wenyewe ndio tunaojua ndani kukoje

3. Kwa sababu sisemagi matatizo yangu kwa ndugu na marafiki nimeamua kuweka hapa labda nitapunguza kitu fulani kichwani kwani sometime naona kama nazidiwa mawazo vile

By Qeen Maleo

RPC Azungumzia Lema kupigana na askari, Lema naye azungumza

0
0


Leo July 1, 2018 Mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema anadaiwa kuwa amepigana na askari aliyejulikana kwa jina Inspector Antony baada ya kutaka amnunulie skafu kwa ajili ya mtoto wake.

Baada ya taarifa hizo AyoTV imempata Kamanda wa Jeshi la polisi Arusha Ramadhan N’ganzi ambaye amethibitisha kupokea taarifa hizo nakusema atazifanyia kazi na kwamba Lema ameshampigia simu akitaka waonane naye.


VIDEO:

Tumia Super Mkuyati Kuleta Heshima ya Ndoa

0
0

SUPER MKUYATI INAYOLETA HESHIMA YANDOA super mkuyati nidawa ya mitishamba iliyo sheheni miti mbalimbali na kugundulika ina pambana na magonywa sugu

SUPER MKUYATI inanguvu (3) nainafanya kazi kwapamoja (1) itakufanya uchelewe kufika kileleni ndani ya dk 15-20 bila kuchoka (2) ina zalisha homon kwa wingi na kukufanya uwe na mbengu nyingi zenye vimeleo vya uzazi vyilivyokomaa (3) inaongeza ume mdogo uliosinyaa,kunenepesha uume na kurefusha adi nchi 5-8 na upanda sm 2-3 dawa hii haina mazala kwa mtumiaji ata kwa wazee walionaumri 60-80

SUPER MKUYATI ponyo la maradhi yako tumia Leo uone mjabu yake OFISI YETU ZINAPATIKANA DR MTONI KIJICHI KAMAUNA NAFASI UTALETEWA POPOTE ULIPO KWALE WAMIKOANI UTATUMIWA

DR GATUNDU SM 0717777402/0768408794

"Wanampotosha Rais" - Silinde

0
0

Mbunge wa Mbozi  Magharibi, David Ernest Silinde amebainisha kuwa wasaidizi wengi wa Rais Magufuli  wamekuwa wakimpotosha kiongozi huyo kwa kutomwambia ukweli sehemu zenye mapungufu ili tu kumfurahisha.


Kulia ni Rais Magufuli, kushoto ni Mbunge wa Mbozi Magharibi David Ernest Silinde.

Akizungumza na www.eatv.tv amesema viongozi hao wamekuwa wakidhani kwamba kuwadhibiditi Upinzani watakuwa wanamfurahisha Rais na badala yake wanampotosha kwa kutosema ukweli.

Silinde amesema kwamba kuna maeneo ambayo Rais hashauriwi vizuri lakini kwa kuwa viongozi wake wanahisi kwamba kuzuia hotuba za upinzani ni suluhisho ndiyo maana kuna mambo yanaanzisha na yanagota kabla ya kufika mwisho.

Pamoja na hayo kiongozi huyo amesema ipo haja ya kuwa na mapendekezo ya mabadiliko ya kikanuni kusiwepo na mamlaka ambayo itaweza kuzuia  hotuba za kambi ya upinzani, kamati au hata zile za kiserikali kwani utaratibu wa sasa unatokana na kanuni hizo.

EATV

Jibu la Rayvanny iwapo Rich Mavoko ameondoka WCB

0
0
Jibu la Rayvanny iwapo Rich Mavoko ameondoka WCB By Peter Akaro | July 1, 2018 - 4:24 pm
Msanii wa muziki Bongo kutokea WCB, Rayvanny amefunguka kuhusu taarifa zinazodai kuwa Rich Mavoko hayupo tena katika label hiyo.

Muimbaji huyo amesema ingawa yeye si msemaji rasmi wa suala hilo ila Rich Mavoko bado yupo nao WCB na wamekuwa wakiwasiliana mara kwa mara.

Taarifa za Rich Mavoko kutokwepo WCB zilianza kuchipuka June 19 , 2018 baada ya muimbaji huyo kutoonekana katika mkutano na waandishi wa habari ambapo Diamond alizungumza na wasanii wote wa WCB walikuwepo. Hata hiyo Babu Tale alieleza kuwa siku hiyo Rich Mavoko alikuwa aki-shoot video ya wimbo wake.

“Ujue sisi tunachekiwa kwenye group, leo kuna tukio hili na hili, so ukiona huyo kakosa ni masuala ya uongozi sana labda angekuwepo Diamond au Babu Tale angeweza kuongea sana lakini Mavoko yupo Wasafi kila siku,” amesema.

“Anakuja, anajiunga kwenye vitu lakini yeye kutokuja siku ile sijui sababu, kama kuna vitu vinavyoendelea ni yeye na uongozi. Mimi siwezi kuongea sana kwa sababu Mavoko ni mwanangu tunaongea tunachati, tunarekodi ngoma zetu,” Rayvanny ameiambia Wasafi TV.

Rich Mavoko alijiunga WCB mwaka 2016 akiwa kama msanii wa tatu kusaini baada ya Harmonize na Rayvanny, wimbo wake wa kwanza kutoa chini ya label hiyo unakwenda kwa jina la Ibaki Stori. Akiwa WCB ameweza kufanya kolabo na Harmonize na Diamond pamoja na kushiriki katika wimbo ‘Zilipendwa’ ambao uliwakutanisha wasanii wote wa label hiyo.

Bongo5

Maradona Awatolea uvivu Argentina, Amfananisha Mbappe na Mchezaji huyu Mkongwe Duniani

0
0

Mshambuliaji wa zamani wa timu ya taifa ya Argentina, Diego Maradona amesema kuwa timu hiyo ya taifa kwa sasa haina maelewano uwanjani kwani wachezaji hawajui cha kufanya pale wanapopata mpira.

Maradona akiongea mapema leo na shirika la Habari la  teleSUR, amesema kuwa safu ya ulinzi ya Argentina imekuwa haina maelewano kabisa na hawajui cha kufanya pale walipokuwa wanapoteza mpira.

“Nimeona timu mbovu kabisa kuanzia ushambuliaji na viungo ukiachana na safu ya ulinzi ambayo naweza kusema imekuwa tenga linalozuia maji, kwani nimeona wote wakipanda lakini linapokuja suala la kuzuia wanafeli, mbele wanamuangalia mtu mmoja hii ni mbaya kwa timu kubwa kama Argentina japo lawama lazima apewe Sampaoli,“amesema Maradona.

Kwa upande mwingine Mshindi huyo wa kombe la dunia la mwaka 1986 amemfananisha mshambuliaji wa Ufaransa, Kylian Mbappé na mshambuliaji mwiba wa zamani wa Argentina, Claudio Paul Caniggia kwa spidi yake uwanjani.

“Nashangaa mabeki wa Argentina dhidi ya timu bora ya Ufaransa yaani kama hawajawahi kumuona Mbappe na wakajisahau wote wakawa wanapanda mbele huku wakimuachia nafasi mtu ambaye ni sura halisi ya Caniggia tena akiwa bado mdogo, wakijua hata mbio hawawezi, kusema ukweli nimeona mpira mbovu kuwahi kutokea katika historia ya timu yangu ya taifa.“amesema Maradona.

Timu ya taifa ya Argentina jana imetolewa kwenye michuano ya kombe la dunia kwa kipigo cha goli 4-3 dhidi ya Ufaransa.
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images