Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli Punda Afe Mzigo Ufike Muda wa Kucheka na Kuku Ulishapita– Afande Sele

$
0
0
Rais Magufuli Punda Afe Mzigo Ufike Muda wa Kucheka na Kuku Ulishapita– Afande Sele
Jana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli wakati akitoa hotuba kwa viongozi mbalimbali aliowaapisha siku hiyo, kuna baadhi ya maneno aliyoyasema ndani ya hotuba yake yalikuwa gumzo kwenye mitandao ya kijamii.



Hata hivyo katika hotuba yake,Rapa mkongwe nchini Tanzania, Afande Sele hakutaka kukaa nyuma aliguswa na kuamua kuchukua baadhi ya maneno aliyoyazungumza Rais Magufuli na kuyaweka katika mtandao wake wa Instagram. Afande ameandika “Dume La Simbaaaaa….Gusa Unase….Maendeleo sio lele mama ni kauli ya baba wa taifa mwlm Nyerere…No pain No gain…Punda afe mzigo ufike…ukicheka na nyani utavuna mabua…Ngosha kanyaga twende kama china kama North korea hadi kieleweke…muda wa kucheka na kuku ulishapita sasa kazi tuu…..Chuma kikoli moto….”



Utakumbuka Marchi 15, 2018, Afande Sele alingaza kujiunga na Chama cha Mapinduzi mkoani Morogoro mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.

Pia Afande Sele kabla ya kujiunga na CCM alishawahi kuwa mwanachama wa CHADEMA na Chama cha ACT Wazalendo ambapo mwaka 2015 alitangaza nia ya kugombea ubunge jimbo la Morogoro Mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo.

Watoto 12 Waliopotelea Pangoni Toka Juni 23 Wapatikana Wakiwa Hai

$
0
0
Watoto Waliopotelea Pangoni Toka Juni 23 Wapatikana Wakiwa Hai
Jumla ya watoto 12 pamoja na kocha wao wa Mpira wa Miguu ambao walipotelea pangoni tangu Juni 23 wameonekana wakiwa hai katika moja ya pango lililojaa maji Jimbo la Chiang Rai nchini Thailand.

Vijana hao wenye umri wa kati ya miaka 11 hadi 16 pamoja na kocha wao mwenye umri wa miaka 25  wameonekana mita 400 kutoka eneo ambalo walikuwa wakicheza baada ya kuingia katika pango moja wakati likiwa kavu na ghafla baada ya muda mvua kubwa ikanyesha na kuwazuia kutoka katika pango hilo.

Kikosi cha waokoaji wa vijana hao kimeeleza kuwa kiwango cha maji katika pango hilo ni kikubwa kiasi cha kuleta ugumu wa kuwatoa vijana hao kwa haraka zaidi lakini juhudi kubwa zinafanyika kuweza kufanikisha uokoaji kwa haraka iwezekanavyo .

Vijana hao waligunduliwa na kikosi cha uokoaji cha Uingereza usiku wa Jumatatu baada ya kuombwa kwenda kusaidia harakati hizo japo juhudi za kuwaokoa kwa haraka zimeshindikana baada ya njia ya kuyanyonya maji katika pango hilo kushindikana na endapo waokoaji wataamua kusubiri maji yakauke basi vijana hao watakaa kwa muda wa mwezi mmoja katika pango hilo.

Kwa mujibu wa jeshi la nchi hiyo, njia pekee inayoweza kuwanusuru vijana hao kwa haraka zaidi ni kujifunza namna ya kuogelea ili waweze kutoka au wasubirie mwezi mmoja upite ili maji yapungue katika pango hilo.

Bonde hilo la Tham Luang limekuwa na historia ya kujaa maji kipindi cha mvua ambapo mvua hizo huwa zinanyesha hadi miezi ya Septemba na Oktoba.

Ofisa habari wa APR Afunguka Tofauti yake na Haji Manara

$
0
0
Ofisa habari wa APR Afunguka Tofauti yake na Haji Manara
Ofisa Habari wa klabu ya APR ya Rwanda, Clever Kazungu, amefunguka na kumuelezea Haji Manara kama mtu mwenye kipaji cha aina yake katika uzungumzaji anapokuwa anawasilisha jambo.

Kazungu amemtaja Manara ambaye ni Ofisa Habari wa Simba akisema ana kipaji cha aina yake katika uzungumzaji huku akisema anamkubali kutokana na kazi anayoifanya kwenye klabu ya Simba.

Kiongozi huyo kutoka APR amemueleza Manara kuwa utofauti wake na yeye kuwa ana uwezo wa kuzungumza maneno mengi huku akisema wanaendana katika kuwasilisha ujumbe kwa umma.

Kazungu amesema Manara anastahili kuwa hivyo kutokana ukubwa wa klabu yake akiamini kuwa pale mtu anapokuwa msemaji wa timu kama Simba ni lazima uwe vile.

Ofisa huyo ambaye pia ni Mwanahabari mkongwe yupo hapa nchini kwa ajili ya michuano ya KAGAME ambapo jana timu yake iliweza kufungwa mabao 2-1 na Simba katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mikoa ya Kusini Mngefanya Fujo Kisa Korosho Ningewashughurikia kwa Kipigo na Ningeanza na Jimbo la Waziri Mkuu- JPM

$
0
0
Mikoa ya Kusini Mngefanya Fujo Kisa Korosho Ningewashughurikia kwa Kipigo na Ningeanza na Jimbo la Waziri Mkuu- Rais JPM
Rais John Pombe Magufuli amesema alikuwa akisubiri wakulima wa mikoa ya Lindi na Mtwara wafanye fujo kama jinsi ambavyo Wabunge wa mikoa hiyo walivyokuwa wakidai na kueleza kwamba angewashughulikia kwa kipigo na angeanza na jimbo linaloongozwa na Waziri Mkuu.

Rais Magufuli ameyasema hayo jana wakati alipokuwa akitoa hotuba yake baada ya kuwaapisha Mawaziri na viongozi wengine ambao aliwateua siku ya jana alipofanya mabadiliko madogo katika wizara yake.

"Watu wanataka popularity, wengine nilisikia wanasema watachomewa nyumba, nilimwambia Waziri Mkuu nataka nione wakifanya fujo.  Ningewapa kipigo. Tena ningeanza kwenye jimbo lake kama kuna shangazi zake ningeanza kupiga hao. Nasema ukweli wala sifichi"

Rais aliongeza "Lazima tufike mahali tuambizane ukweli, ndiyo maana nilimwambia Katibu Mkuu CCM, aende Dodoma siku ya kupiga kura. Wabunge wa CCM ambao hawakuwepo wachukuliwe hatua".

Katika kuonyesha kukasirishwa na kitendo ambacho kilifanya na Wabunge wa Mikoa hiyo ambo pia ni wa CCM, Rais Magufuli alisema anashangaa wanafanya nini mpaka saizi kwenye Chama Cha Mapinduzi  badala ya kuondoka.

"Watu wanashangilia uongo, tumechoka, nilimuuliza Waziri Mkuu kuna wabunge wangapi wa CCM, Mtwara na Lindi akasema wapo 17, nikasema bora waondoke wote, hata Waziri Mkuu ni wa huko naye angeondoka, bado tungeweza kuongoza nchi. Nilimpigia simu Katibu wa CCM tukae kwenye mpango huo. Wangeondoka,"

Pamoja na hayo, Rais Magufuli alisema "Siku ya kupitisha bajeti nikamwambia Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru nenda Bungeni ukaangalie wabunge wangapi wa CCM hawapo bungeni uwalime barua, na kweli amewaandikia barua wote. Japo wapo Wabunge waliokuwa na sababu za Msingi lakini kuna wale ambao wamelimwa barua. Prof. Kabudi alikuwa amelazwa lakini kapokea barua yake na ataambatanisha na vyeti vya hospitali"

Mbali na hayo Rais amempongeza Naibu Waziri Mpya wa Kilimo na Umwagiliaji kwa kuweza kupambana kuitetea serikali wakati wa hoja ya Korosho ilipokuwa imepamba moto.

“Nakupongeza Naibu Waziri wa Kilimo (Omary Mgumba) kwa kazi uliofanya Bungeni, huwa nafuatilia michango ya CCM, mwingine anasema tukienda hivi tutashindwa, kwa nini bado uko CCM, si utoke huko? Ulinyimwa nafasi ya kutetea hoja yako, mmoja akapewa nafasi ya kukupiga na mwingine tena akakupiga, hiki ulichokipata ndicho ulistahili, nakuomba ukashirikiane na wenzako Wizara ya Kilimo." Alisema

Yanga Yaweka Wazi Kuhusu Obrey Chirwa

$
0
0
Yanga Yaweka Wazi  Kuhusu Obrey Chirwa
Uongozi wa klabu ya Yanga umefunguka jambo kuhusiana na aliyekuwa mchezaji wake, Mzambia, Obrey Chirwa ambaye hivi sasa amejiunga na Ismailia ya Misri.

Kwa mujibu wa Hussein Nyika kupitia kipindi cha michezo, Radio One, amesema Chirwa alimaliza mkataba na Yanga hivyo wasingeweza kumzuia asifanya mazungumzo na timu zingine.

Nyika amefunguka kwa kusema yeye kama kiongozi wa Yanga na klabu kwa ujumla wanamtakia kila lililo jema huko alipo katika kazi yake ya mpira baada ya kufikia mwafaka na timu yake mpya ya Ismailia kuichezea.

Mbali na kuondoka kwa Chirwa Yanga, Nyika amesema mchezaji huyo alikuwa ni moja ya waliokuwa bora kwenye kikosi cha timu yao kutokana na mchango pamoja na umahiri wake ndani ya Uwanja.

Chirwa ameondoka Yanga akiwa amechangia kuipatia ubingwa wa Ligi Kuu Bara katika msimu wa 2016/17 mbele ya watani zao wa jadi Simba ambao waliambulia nafasi ya pili.

Rais Magufuli Awaalika Viongozi Wakuu Wastaafu Ikulu Lowassa, Sumaye nao Ndani

$
0
0
Rais Magufuli Awaalika Viongozi Wakuu Wastaafu Ikulu Lowassa, Sumaye nao Ndani
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John pombe Magufuli amewaalika viongozi wakuu wastaafu wote. Kufanya nao mazungumzo leo Jumanne, Julai 03, 2018 Ikulu jijini Dar es Salaam.


Viongozi walioarikwa ni Marais, Mhe. Makamu wa Rais, Mawaziri Wakuu, Maspika na Majaji Wakuu.


Hii ni mara ya kwanza kwa viongozi hao kukutana na Rais Ikulu.

 

Jaji Kiongozi: Madalali wa Mahakama Muache Kunung'unika

$
0
0
Jaji Kiongozi: Madalali wa Mahakama Muache Kunung'unika
Jaji Kiongozi, Dk. Eliezer Feleshi ambapo amewataka madalali na wasambaza nyaraka za mahakama kuacha kulalamika na kunung’unika badala yake wajenga hoja kuhusu changamoto zinazowakabili.

Dk. Feleshi ameyasema hayo wakati wa kuzindua mafunzo kwa madalali wa mahakama yaliyoandaliwa na Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) katika kituo cha mafunzo na habari kilichopo Mahakamani Kisutu.

Dk. Feleshi amesema madalali wanatakiwa kuwa na uwezo kukamata mali za aina yoyote na sehemu yoyote hata kama itakuwa nje ya nchi.

“Ndio maana yameandaliwa haya mafunzo lengo likiwa kuwapatia umahiri katika utekelezaji wa majukumu yenu,” amesema.

Dk. Feleshi amewataka madalali kuendesha mijadala na kutumia fursa vizuri katika mafunzo badala ya kulalamika na kunung’unika.

Mange Kimambi Amtolea Uvivu Casto Dickson "Hana Faida Yoyote Mariooo Hata Laki Mfukoni Hana"

$
0
0
Mange Kimambi Amtolea Uvivu Casto Dickson "Hana faida yoyote Yeye Mwenyewe Mariooo Hata Laki Mfukoni Hana"
Mwanadada mwanaharakati Mange Kimambi amemtolea uvivu na kumpa makavu yake Casto Dickson ambaye ameonekana akila bata na mpenzi wake Tunda huku mwanaye akiwa kwenye hali mbaya bila yeye kuonekana kuguswa na tatizo alilonalo mwanaye.

Kupitia mtandao wa instagram wa mange kimambi alianza kwa kumtolea uvivu casto kwa kumpa makavu na kuwataka watanzania wasipoteze muda kumtukana tu kwani mwanaume huyo hata laki mfukoni hana na kuwashawishi watoe michango kwaajili ya matibabu.

 Mange aliandika hivi " Ila watanzania tunapenda kupoteza muda na vitu ambavyo havina maslahi kwetu, hiyo nguvu mnayoitumia kumchamba Tunda na Bwanawake si muitumie kumchangia mtoto apate matibabu.....  hivi huyo kaka mnayemchamba eti akamuone mtoto anafaida gani
 hata akienda? Hivi huyu hata laki anayo mfukoni? si ataenda kujaza listi ya wageni tu huko hospitali, mtoto mwenyewe yupo kwenye coma sio kwamba hata yuko macho anamtaka babaake.... Ebu changeni Embu changeni pesa bwana acheni kupoteza mida na upumbavu. Mnamfatilia baba wa mtoto utasema ni mtu wa maana kwamba kuna Msaada anaweza kutoa. Haki ingekuwa labda ni Ruge, Dai, Majey sijui mkaka gani mwingine mwenye maisha yake mazuri haki ningesaidia kumchamba moaka atoe msaada ila huyu mariyooooo mnamchamba ili iweje?? Huyu kaka ni style za kina Petit wanaume suruali, elfu 10 mfukoni hana. Alafu Tunda mnamchamba yeye ndo mwenye mtoto? Au kamfunga kamba huyo Mariyoooo asiende? Na inawezekana huyo kaka hana hata nauli ya kwenda huko Nairobi. Labda mumchangie nauli na malazi🙄, au mlitaka Tunda ndo amlipie nauli na pocket money ampe? Mnampigia kelele baba mtu akamuone mtoto Nairobi wakati mtoto alilazwa Agha Khan wiki 3 na hakwenda kumuona. Hata senti moja ya matibabu hapo Agha Khan hakutoa leo ndio atatoa za Nairobi? Vitu vingine muwage mnajiongeza bwana. Embu tumchangie mtoto acheni kupoteza muda na watu ambao hawana faida yoyote na uponyaji wa huyo mtoto.  "




Muone Ustadhi Ashrafu Atimize ndoto yako..Anatumia Nyota na Nguvu za Asili Kutibu

$
0
0


Muone Ustadhi Ashrafu Atimize ndoto yako. yawezekana ulizaliwa nanyota yakitajiri ila watu wabaya wameikalia mpaka sasa ikawa hufahamu chochote. Mtafute ust Ashrafu Airudishe nyota yako yakitajiri kwakupitia pete inayoendana na nyota yako. Ust Ashrafu Ananguvu zamajini katika utendaji wake.

Anauwezo wakutoa Mali kwakupitia pete nakwakupitia majini wake. Na anauwezo wakuzirudisha Mali zilizopotea kwanjia zakichawi kwakupitia Pete yakifalme Ambayo inayong'aa muda wowote nakubadilikabadilika rangi. Ust Ashrafu Ametembea baadhi ya nchi kwakuwapatia watu huduma mbalimbali. Kama vile maradhi yakisukari, presha, ukimwi, bawasiri, tezidume, mwiliwote kupooza nakutetemeka, NK. Navilevile Amewapatia wengi huduma yamvuto wa kibiashara, nayamvuto wakimapenzi.

Nawengi wametoa shukrani zao kwa ust Ashrafu namna Alivyozirudisha Ndoa zao zilizo sambaratika kwamuda mrefu. Mtafute ust Ashrafu ili akusaidie juu yamambo yako. Nahuyu ust anasaidia matatizo yauzazi, nguvu zakiume, kuwashwa mwilini, kutokwa namapere usoni nasehemu za siri, NK. Na anadawa yakumtuliza mume asiesikia nakutulia inayoitwa limbwata. Na anadawa yakumrudisha mpenzi ktk mahusiano kwamda mchache.

Na amezipatanisha familia nyingi zilizogombana. Na anauwezo wakufarakanisha maadui waliokua pamoja.

Mtafute Ustadhi Ashrafu kwa no. 0768486717-0627423037 Au Mtafute kwa whasapp 0659438578

Hizi ndio namba zake mpigie muda wowote usiogope yupo kwaajili yako. Mpigie hupate muongozo wa bure naushri. Ustadhi Ashrafu huduma zake hupatikana mahala popote utakapo muhitaji, ila sehemu kuu anapatikana Bagamoyo.

Msaada Please, Mpenzi Wangu Ananing'ata Tukiwa Sita kwa Sita Mpaka Natoka Damu

$
0
0
Wakuu nifanyeje juu ya sweetie wangu huyu. I really love and Am dying for her ila hili tatizo nahisi ipo siku nitachoka
Tatizo ninapomdinya nashtukia ghafla kaning'ata,nimebadili style,nikapiga doggy kajipinda hadi kang'ata paja , yaaani huku shingoni nimejaa alama alama , wengine wanasemaga ni love bite ila hii yangu imezidi kipimo , sometimes mpaka damu zinanitoka na kuuguza kidonda..

Wakuu what should I do

Kina Kaka Acheni Ujinga, Hakuna Mwanamke Asiyetaka Kuhongwa! Shauri Lako

$
0
0
Wakaka acheni ujinga, ukitaka dem wa peke yako basi jua kugharamia. Nakwambia wanawake asilimia kubwa hukumbuka fadhila za mtu anayemgharamikia kuliko wanaume wa ai lavii yuu maneno.

Usidanganyike hakuna mwanamke asiyependa kuhongwa, kuna wanawake natural hawawezi kuomba,ila anakua anataka ujiongeze, sasa kama wewe ni wale ambao akikwambia "baby kifurushi kimekata" unajibu "basi mumy pls ukiweka nicheki" umekwishaaaa!!!

Anakueleza shida zake unasema "mpenz vumilia nakuombea upate kazi" kaka umeishaaa kabisaaaa aiseeee!!! Huna chako!!!
Ujue ulivyokata simu umefatiwa na bonge la msonyoooo ka sio tusi la nguoni basi la mwilini. Yani wewe kama ni wale wa baby mwezi huu mambo yangu hayako sawa, nakuapia unagongewa weeeeeeeeee . . . . mpaka ujute!!

Unamuona dem wako kasuka, kapendeza na hana kazi, we umekazana tu "beibi umependeza" . . . . . . Yaani wee boya ujue!! Mume mwenzio kaweka nguvu, so anapokua anatoa calendar za kukuona tulizana, service inakua kwa anayehudumia.
Hakuna dem wa siku hizi anayetaka kuambiwa nakupenda jumapili mpaka jumapili we mhonge tu uone heshima.

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME DR SITTA NDO SULULISHO LAKO tatiza, hili limekuwa likiwaasili watu wengi,sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine, kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo zipo , sababu nyingi zinazosababisha, tatizo hilo baadhi ni (i) upungufu wa vichocheo vya HORMONES ZA CETROGEN ambazo mwanaume, anapobarehe vichocheo hivi, HORMONES hizo, husaidia ukuaji wa uume

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mlija iliysinyaa,

NSHOLA ni dawa bora, ya kurudisha nguvu, za, kiume bari inatibu ,kabisa kutoa tatizo hilo, na kukupa , hamu ya , kurudia tendo, la ndoa zaidi, ya mala nne 4 ,bila kuchoka atakama unaumli ,wa mika 80,! pia ana ,dawa za ,kutibu, presha ya kupanda ,na kushuka, kisukari kuondoa, mafuta , mwilini ,na maumivu ya, mgogo kiuno, dawa zipo, matazo, ya hedhi, kwa ,wanawake hedhi, zisizokuwa na, mpangilio, na kasonono, pia , vidonda ,vya, tumbo ,(STOMACHI UCLENS) IHUSHI ndoji lako.

NKANYA ni dwa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi ariyekuacha, mke mme, atakuludia kwa, mda, wa msaa3 tu , ukishaitumia atarudi ,mwenyewe bila ,ugovi tena, NKOMA ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada .

HERBON, ni, dawa, ya kuongeza, CD4, NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu ,miguu, kufaganzi, na ,kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! DR SITTA, amebobea, kwa tiba asilia

DAR ANAPATIKANA MBAGALA, ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI SHINYANGA, KAHAMA MJINI, KWA MAELEZO ZAIDI ,

PIGA SIMU 0763172670 au 0715172670

WOTE MNAKALIBISHWA, KAMA, UTAKUWA NA TATIZOUTAHUDUMIWA

Mwili wa Prof. Majimarefu Kuagwa Kesho

$
0
0
Mwili wa Prof. Majimarefu Kuagwa Kesho
Aliyekuwa Mbunge wa Korogwe Vijijini (CCM), Steven Ngonyani maarufu kama Profesa Maji Marefu, ataagwa kesho na baadaye mwili kusafirishwa kuelekea jimboni kwake Korogwe kwaajili ya maziko.


Aliyekuwa Mbunge wa Korogwe Vijijini (CCM), Steven Ngonyani maarufu kama Profesa Maji Marefu,enzi za Uhai wake.

Akizungumza na eatv.tv Kaka wa marehemu, Hilary Ngonyani amesema kuwa taratibu za kuaga mwili wa marehemu zitatangazwa baadae, ikiwemo mahali itapaofanyika ibaada ya kuaga mwili wa marehemu Maji Marefu, pindi watakapokamilisha mawasiliano na ofisi ya Bunge.

“Mwili utabaki Muhimbili leo, hadi hapo kesho tutakapoaga katika viwanja ambavyo taarifa itatolewa badae baadaya ya kukamilisha mawasiliano na Ofisi ya Bunge, ambapo ataagwa na wakazi wa Jijini Dar es salaam pamoja na wabunge wenzake na baadaye tutaanza safari ya kuelekea Korogwe kwaajili ya shughuli ya Mazishi”, amesema Hilary Ngonyani.

Taarifa za kifo cha mbunge huyo ziliripotiwa usiku wa Julai 2, majira ya saa 3:20 na Ofisa Uhusiano wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Aminiel Aligaesha.

June 6, 2018 mbunge huyo alifiwa na mkewe, Mariam aliyekuwa akipatiwa matibabu hospitali ya taifa pia.

Roboti Sophia Afanya Mazungumzo na Waziri Mkuu wa Ethiopia

$
0
0
Roboti Sophia amefanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Ethiopia
Sophia ni roboti aliyepata umaarufu na kupewa uraia wa Saudi Arabia, kwa uwezo wake wa kuongea, kujibu maswali, ishara za uso, na kusoma hisia za watu anaoongea nao.

Amewasili bara la Afrika nchini Ethiopia kuonana na Waziri mkuu Abiy Ahmed siku ya jumatatu na kuongea kuhusu misaada ya ubunifu wa teknolojia. Ingawa alipata hitilafu kidogo ya vipande vya mwili wake kupotea Airport wiki iliyopita. Ikafikia hatua ya kuahirisha mkutano na chakula cha usiku na waziri mkuu ijumaa iliyopita.

Sophia atahudhuria maonyesho ya ICT yaliyo anza kuonyesha jumatatu nchini humo Ethiopia.

IGP Sirro Afanya Mabadiliko ya Makamanda wa Polisi kwa Baadhi ya Mikoa

$
0
0
IGP Sirro Afanya Mabadiliko ya Makamanda wa Polisi kwa Baadhi ya Mikoa
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Sirro amefanya mabadiliko ya makamanda wa polisi kwa baadhi ya mikoa.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo Julai 3, 2018  iliyosainiwa na Msemaji wa Jeshi la Polisi, Barnabas Mwakalukwa, inasema mabadiliko hayo yanalenga kuongeza juhudi za kuzuia ajali zilizotokea mara kwa mara katika baadhi ya mikoa.

Katika mabadiliko hayo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Deusdedit Nsimeki aliyekuwa makao makuu ya upelelezi Dar es Salaam anakwenda kuwa Kamanda wa Polisi (RPC) Mkoa wa Simiyu.

Aliyekuwa RPC Mkoa wa Morogoro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Ulrich Matei anakwenda kuwa RPC Mkoa wa Mbeya.

Katika mabadiliko hayo, aliyekuwa Kaimu RPC Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi wa Polisi, Mussa Taibu amehamishiwa makao makuu ya polisi Dar es Salaam.

Aliyekuwa RPC Mkoa wa Tabora Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Wilbroad Mutafungwa anakwenda kuwa RPC Mkoa wa Morogoro, nafasi yake ikichukuliwa na Kamishna Msaidizi wa Polisi, Emmanuel Nley kutoka makao makuu ya polisi Dar es Salaam.

Wengine waliohusika na mabadiliko hayo ni aliyekuwa Ofisa Mnadhimu Mkoa wa Geita Kamishna Msaidizi wa Polisi, Stanley Kulyamo anayekwenda kuwa Kamanda wa Polisi Kikosi cha Tazara.

IGP Sirro amewataka makamanda wa polisi wa mikoa nchini, kuendelea kuwajibika ipasavyo katika kuhakikisha ajali hazitokei katika maeneo yao na kuwachukulia hatua kali madereva watakaosababisha ajali kwa uzembe.

Kangi Lugola Atinga Ofisi Ndogo Wizara ya Mambo ya Ndani Kukabidhiwa Ofisi

$
0
0
Kangi Lugola  Atinga Ofisi Ndogo Wizara ya Mambo ya Ndani Kukabidhiwa Ofisi
Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amewasili katika ofisi ndogo ya wizara hiyo jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kukabidhiwa ofisi baada ya kuapishwa.

Lugola ambaye ni mbunge wa Mwibara aliapishwa jana Julai 2, 2018 Ikulu jijini Dar es Salaam akichukua nafasi ya Dk Mwigulu Nchemba ambaye ameachwa kwenye baraza la mawaziri la Rais John Magufuli.

Waziri Lugola amepokewa ofisini leo Julai 3, 2018 saa 5:20 na viongozi na watumishi wa wizara hiyo.

Baada ya kushuka ndani ya gari, Lugola alisalimiana kwa kukumbatiana na Masauni. Pia, alisalimiana na katibu mkuu na manaibu wake.

Raila Odinga Afanya Ziara Nchini India ya Kuiwakilisha Serikali ya Kenya

$
0
0
 Raila Odinga Afanya Ziara Nchini India ya Kuiwakilisha Serikali ya Kenya
Kiongozi mkubwa wa vyama vya upinzani nchini Kenya (NASA), Raila Odinga amefanya ziara ya kuiwakilisha serikali ya Kenya nchini India.

Odinga ambaye ameongozana na Mkewe, Mama Ida Odinga mapema leo wakiwa jijini New Delhi wamekutana na Waziri Mkuu wa India, Narendra Modi na kujadili mambo kadha wa kadha ya kimaendeleo baina ya nchi hizo mbili.

“Mimi na mke wangu Ida Odinga tumefurahi kupokelewa na Waziri Mkuu wa India, Narendra Modi, Kenye na India zimekuwa na urafiki wenye manufaa kwenye sekta mbalimbali kwa miongo mingi na ni imani yangu kuwa ziara hii itakuwa yenye manufaa kwa mataifa yote mawili.“ameandika Raila Odinga kwenye ukurasa wake wa Twitter.

Kwa upande mwingine Odinga amesema kuwa wamejadili ongezeko la wawekezaji kutoka India katika Sekta za afya nchini Kenya na jinsi ya kuimarisha usafiri wa majini baina ya mataifa hayo.

Hata hivyo, hatua hiyo imepingwa na baadhi ya wafuasi wa NASA ambao wanahoji kiongozi huyo ameenda India kama nani? ile hali hana nafasi yoyote kwenye serikali nchini Kenya ambayo inaongozwa na hasimu wake Uhuru Kenyatta.

Mkanganyiko huo pia umeenda mbali zaidi kuwa Rais Kenyatta tangu waelewane na Raila Odinga amekuwa hamtumii Makamu wake wa Rais, Wiliam Ruto kwenye baadhi ya mikutano mikubwa ya kimataifa na ziara muhimu za kikazi.

Odinga amewasili nchini India tangu wiki iliyopita na anatarajiwa kurudi Kenya wiki hii huku kukiwa na tetesi kuwa kiongozi huyo na Uhuru Kenyatta watampokea Rais wa Tanzania, Dkt. John Magufuli kwenye ziara yake nchini Kenya inayotarajiwa kuanza Ijumaa hii.

Kabula Ateswa na Uamuzi wa Q Chillah, Amuomba Hili

$
0
0
Kabula Ateswa na Uamuzi wa Q Chillah, Amuomba Hili
kupitia kipindi cha XXL cha Clouds Fm staa mkongwe katika game ya Bongo Fleva Q Chillah alizungumza kuhusiana na kuachana na  muziki maamuzi  ambayo yaliwagusa wengi kutokana na mchango mkubwa aliouweka katika tasnia ya muziki nchini.

Kupitia instagram account ya muigizaji wa Bongo Movie , Kabula ameamua kutoa ushauri juu ya maamuzi aliyoyafanya Q Chillah kuhusiana na kuachana na muziki.

Kabula ameandika “Wee unaanzaje kumuacha mtu kama huyu apotee kizembe ifike mahali Taifa lipaze sauti kwa vijana nguvu kazi Chilla ni dhahabu ya Tanzania alipotangaza kuacha mziki roho ilipasuka nikasema No bado anauwezo mkubwa wa kuipeperusha bendera ya Taifa letu”

“Wewe ni dhahabu kaka na dhahabu haiwezi ngaa bila kupita kwenye moto huwezi kuwa shujaa mpaka ukutane na mengi ya kukuumiza moyo na kukukatisha tamaa lazima udharauliwe ukataliwe na wakati mwingine kunenewa maneno ya uwongo ila ukiweza kutobowa hakuna anaweza kukushusha chini tena”

“Sisi ni mashujaa wa Taifa ata tukiondoka leo tutaacha histolia ktk vizazi vijavyo acha ya zamani yaende simama ukainuliwe kaka…Watanzania tunakupenda tuko pamoja🙏🙏🙏 Maisha na mziki Go chilla❤❤❤❤😍”

Zamaradi Ahamasisha Kuchangia Matibabu ya Mtoto wa Muna Love... Achangia Milioni 1 Wema Naye Atoa Mchango Wake

$
0
0
Zamaradi Ahamasisha Kuchangia Matibabu ya Mtoto wa Muna Love... Achangia Milioni 1 Wema Naye Atoa Mchango Wake
Mwanadada mpambamaji hapa nchini Zamaradi Mketema ni miongoni mwa Watanzania Walioguswa na hali aliyonayo mtoto wa Muna Love na kuamua kuhamasisha watu kupitia mitandao ya kijamii kuchangia fedha za matibabu ili kusaidia kuokoa maisha ya  mtoto huyo.

Mtoto wa Muna  yupo ICU katika hospitali ya nairobi  kwa siku ya sita sasa  na kupitia matibabu anayopatiwa hadi sasa gharama imefikia milioni 22 .

Kupitia ukrasa wake wa instagram Zamaradi ameandika hivi;

"Nimezaa naelewa unachopitia,

Wapenzi mwenzetu yuko kwenye mtihani mzito, anauguza mtoto wake na yuko Hospitali Nairobi huku mtoto akiwa ICU almost siku ya sita leo, tunaelewa kuuguza ni nini, hata kama una kitu bado hakitatosha, Dawa anayotumia mtoto kwa siku hizi sita mpaka sasa Bill ni milioni 22!karibu na bado inaongezeka, nimeongea nae kuhusu kusaidia pale tunapoweza na kakubali, na nimeomba ACCOUNT YAKE YA BENKI ambayo hela itamfikia moja kwa moja, hivyo kwa yeyote atakaeguswa kuna NAMBA ambazo asubuhi utazioata kupitia page yangu na ya @munalove100 ambayo ni ACCOUNT YA BANK ya mtoto mwenyewe na unaweza kutuma kiasi chochote moja kwa moja itamfikia.

Naomba nifungue dimba hili kwa kuchangia Milioni moja, na nimeongea na WEMA pia nae kachangia ya kwake ambazo tunatuma moja kwa moja kwenye account siku ya kesho, tunaomba na wewe utakaeguswa tafadhali usaidie kwa kiwango chochote utakachoweza, ndio maana ya kushirikiana kwenye matatizo. Kumbuka kabla ya hapa alimuuguza mwanae kwa muda mrefu sana hivyo ifike mahala tusaidie kuubeba huu mzigo, na namba ya account ni yake yeye hivyo itamfikia moja kwa moja.

#kutoanimoyosiutajiri"

Huyu Ndiye Mtu Anayevalia Nadhifu zaidi Afrika

$
0
0
Unamiliki suti ngapi, viatu jozi ngapi, kofia ngapi, mashati mangapi na mikanda mingapi na soksi pea ngapi? Ukihesabu bila shaka hautakosa kugundua kuwa ni mavazi ya kukuwezesha kusukuma wiki moja au mbili hivi bila kurudia.

Lakini kwa mwanamume mmoja mwenye makao yake jijini Nairobi, Kenya hilo si tatizo.

Ana mavazi mengi ajabu, yanayojumlisha suti kamili za rangi tofauti, viatu, kofia, mikanda, saa, pete na hata mifuko ya simu, mavazi ambayo anaweza kuyavaa kwa zaidi ya siku mia moja bila kurudia.

Kila ukikutana naye kwenye mkusanyiko wa watu, hutakosa kumtambua kutokana na mtindo wake wa kipekee wa kuvalia.

Mwavuli pia nao lazima ufuate mtindo wake
James Maina Mwangi ni mzaliwa wa Muranga kati kati mwa Kenya anasema aliondoka nyumbani kwao na kuelekelea jijini Nairobi kutafuta riziki akiwa na umri wa miaka 12 baada ya kusoma hadi darasa la sita.

Anasema alipata changamoto kubwa za kuweza kupata mavazi ya kutosheleza haja yake, hasa utotoni.

"Nikiwa mdogo nilikuwa na shati moja tu nililokuwa nikilivua likikauka ninalivaa tena, na kuna wakati nilikuwa nikiazima nguo kutoka kwa marafiki kama ninataka kwenda kutembea mahali, nikimuomba rafiki ananijibu vibaya labda ananitusi au ananicheka," anasema.

"Ndipo nikamuomba Mungu anipe taji ambayo watu wengine hawana, ndio wajue kuna Mungu tofauti na yule walikuwa wanamjua," anasema Mwangi



Mwangi anasema suti moja inaweza kumgharimu kati ya shilingi 10,000 pesa za Kenya au dola 100 na shilingi 80,000 au dola 800.

Hadi sasa Bw Mwangi anasema anamiliki zaidi ya suti 150, zaidi ya jozi 200 za viatu na kofia zaidi ya 300 mavazi ambayo amekuwa akiyanunua nchini Kenya na kuagiza mengine kutoka nchini za kigeni zikiwemo Afrika Kusini, Italia, Uhispania, Ufaransa na Ujerumani.

Anasema anamiliki suti za kila rangi inayopatikana duniani na huwa kawaida anavaa rangi moja kuanzia kofia, miwani, shati, tai, suti yenyewe, viatu ,soksi saa, rangi ya simu na hata nguo za ndani.

"Mimi ni kama kioo kwa wananchi, watu wakiniona nimevaa hivi hufurahi sana, wao hunisimamisha, hunisalimia na kuzungumza nami na kunipa moyo kuendelea kuvaa hivi, na pia kuniombea mema, nafikiri ni mimi ndiye mtu maridadi zaidi Afrika," Bw Mwangi anasema.

Anasema kuwa kuvaa nadhifu lilikuwa ni ombi alilomuomba Mungu tangu utotoni na anasema kuwa atazidi kuvalia hivyo hadi ile miaka Mungu atamruhusu kuishi ulimwengu huu.

Viewing all 104689 articles
Browse latest View live




Latest Images