Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104780 articles
Browse latest View live

Huu ndio Ugonjwa ulimuua Mtoto wa Muna

$
0
0

INAUMA sana! Ndiyo maneno unayoweza kutamka baada ya mtoto wa msanii wa filamu za Kibongo, Rose Alphonce ‘Muna’ anayejulikana kwa jina la Patrick (8) ambaye alikuwa maarufu sana mitandaoni na amecheza kwenye filamu kadhaa za wasanii mbalimbali kufariki dunia ambapo kilichomuua kimebainika, Risasi Mchanganyiko linakupa habari kamili. 

Mtoto huyo alifariki Jumanne jioni akiwa kwenye matibabu Nairobi nchini Kenya na kusababisha vilio kila kona; kwa wasanii hata kwa watu wa kawaida. 

KILICHOMUUA NI HIKI 
Akizungumza kwa njia ya simu ya mkononi kupitia mtandao wa kijamii wa WhatsApp kabla mwanaye hajafariki Muna alisema alikuwa akisumbuliwa na uvimbe kwenye ubongo. “Kinachomsumbua mwanangu ni uvimbe kwenye ubongo na hajaamka kwa siku sita huku akiwa amelazwa katika chumba cha uangalizi maalum ‘ICU’ hivyo tunasubiri aamke ndipo madaktari waangalie kama watamfanyia operesheni au la,” alisema Muna jana asubuhi na mwanaye huyo kufariki jioni. 

MAMA’KE AZIMIA 
Chanzo makini kilichopo Nairobi kilieleza kuwa mara baada ya mwanaye kufariki dunia, Muna alizimia kwa muda wa nusu saa kutokana na mshtuko huku anayedaiwa kuwa ni mchumba wake ambaye ni mwimbaji wa nyimbo za Injili, Joel Lwaga naye akiishiwa nguvu. 

DAKTARI AANIKA CHANZO CHA UVIMBE 
Akizungumza na Risasi Mchanganyiko, Dk Chale alisema uvimbe kwenye ubongo kitaalamu huitwa ‘Brain Tumour’ ambao unaweza kuwa wa kawaida au kansa na husababishwa na njia kuu mbili; moja ni ubongo wenyewe na pili kutokana na viungo vingine. 

Katika njia ya kwanza ni kwamba inawezekana ugonjwa huu ukarithi kutoka kwa familia kama baba au mama amewahi kuwa na matatizo hayo basi lazima na wengine warithi. Sababu nyinginezo ambazo zinachangia ni maambukizi ya virusi wa ugonjwa huo kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, sababu za kimazingira ambayo mtu anaishi, kemikali za viwandani, vipodozi, chakula, dawa na nyingine nyingi. 

Katika njia ya pili ya viungo vingine hutokana na kama mtu ana kansa ya mapafu, kizazi, matiti, figo, tezi dume hizi huweza kusa babisha uvimbe kwenye ubongo. Dk Chale aliendelea kufafanua kuwa uvimbe kwenye ubongo kwa upande wa watoto mara nyingi huwa ni kansa na siyo wa kawaida ndiyo maana huua haraka sana na hawawezi kupona maana uvimbe huwa chini ya ubongo na siyo kwa juu kama inavyokuwa kwa watu wazima. 

TUJIKUMBUSHE Kabla ya kukutwa umauti, Patrick alianza kuumwa mguu ghafla hali iliyosababishwa alazwe katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI) na kufanyiwa upasuaji mara tano. Baadaye, mtoto huyo alipata ahueni na kuendelea na maisha ya kila siku.

Jana (Jumanne) asubuhi mastaa mbalimbali walionekana wakimuombea mtoto huyo apone ambapo pia mtangazaji wa Wasafi TV, Zamaradi Mketema alianza kuchangisha kwani matibabu ya mtoto huyo kwa siku sita alizokaa huko ni zaidi ya milioni 22 lakini jioni ya siku hiyo mtoto huyo akaaga dunia. 

Biti Zito la Kangi Lugola "Mimi ni Ninja, Ole Wenu Mnaotaka Kuharibu Amani Ya Nchi"

$
0
0

Waziri  wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, amesema hatamwonea aibu kiongozi au mtu yeyote atakayetaka kuhatarisha amani ya nchi. 


Kutokana na hali hiyo, amesema kuanzia sasa, wanaotaka kuhatarisha amani, wajue kwa sasa ameuvaa uninja usoni.


Waziri Kangi aliyasema hayo jana mjini hapa alipokuwa akizungumza na viongozi wa taasisi, mashirika, mamlaka na taasisi za Serikali pamoja na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama, Mkoa wa Mbeya.


Katika maelezo yake, waziri huyo aliwataka viongozi wajiandae kwa uamuzi mgumu atakaoutoa baada ya kupokea taarifa kutoka kwenye mamalaka husika zinazojihusisha na usalama barabarani.


“Nilipokuwa bungeni, kuna baadhi ya watu walionekana kutaka kuharibu amani na mimi kulazimika kuvaa kofia ya kininja ambayo ilikuwa ya kitambaa.


“Lakini, kwa sasa nitalazimika kuvaa kofia hiyo ya chuma na nzito zaidi kwani ninaopambana nao ni makamanda wenzangu.


“Niliapishwa Jumatatu wiki hii kushika nafasi hii inayoyahusisha majeshi ya magereza, uokoaji,  idara ya uhamiaji, vitambulisho vya Taifa, wakimbizi, usajili wa vyama vya kijamii, makanisa na misikiti.


“Kwa kawaida, vyombo vyote hivyo ndivyo vinavyohakikisha amani ya nchi inakuwepo.


“Hivyo basi, wananchi wanapopata ajali mahali popote ikiwamo Mbeya na maeneo mengine ya nchi na wakati huo huo Serikali ikashindwa kuchukua hatua, basi nchi haitakuwa na amani wala utulivu.


“Kwa hiyo, sitanii bali nimeamua kuuvaa uninja nikimaanisha na sitamwonea haya mtu yeyote."

Msigwa: Sifikirii kuwa Rais, lakini 2020 Chadema tunachukua nchi

$
0
0

Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa amesema kuwa uchaguzi ujao wa mwaka 2020 anaamini kuwa chama chake kitakwenda kushinda kwa kishindo kikubwa.


Amesema kuwa CHADEMA imejipanga na ushindani wa mwaka 2020 katika uchaguzi mkuu ambapo amesema kuwa imani yake ni kuchukua dola.


Aidha, amesema wananchi wameona ni kwa kiasi gani walivyodanganywa na namna ahadi nyingi zilizotolewa zimeshindwa kutekelezwa hivyo anaamini kwamba hawataweza kufanya kosa la kuirudisha CCM madarakani.


“Ushindi wa Chadema 2020 utakuwa ni wa kishindo sana. Wananchi wamejionea kila mahali wanalia maisha magumu, yamekuwa ni mwiba kwao, na ushindi wetu utakuwa na kasi ya kimbunga,”amesema Msigwa


Hata hivyo, akizungumzia kuhusu suala la yeye kufikiria kuwa Rais siku moja kupitia chama chake, amesema kuwa bado hajapata maono hayo.

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0

KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME DR SITTA NDO SULULISHO LAKO tatiza, hili limekuwa likiwaasili watu wengi,sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine, kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo zipo , sababu nyingi zinazosababisha, tatizo hilo baadhi ni (i) upungufu wa vichocheo vya HORMONES ZA CETROGEN ambazo mwanaume, anapobarehe vichocheo hivi, HORMONES hizo, husaidia ukuaji wa uume 

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mlija iliysinyaa, 

NSHOLA ni dawa bora, ya kurudisha nguvu, za, kiume bari inatibu ,kabisa kutoa tatizo hilo, na kukupa , hamu ya , kurudia tendo, la ndoa zaidi, ya mala nne 4 ,bila kuchoka atakama unaumli ,wa mika 80,! pia ana ,dawa za ,kutibu, presha ya kupanda ,na kushuka, kisukari kuondoa, mafuta , mwilini ,na maumivu ya, mgogo kiuno, dawa zipo, matazo, ya hedhi, kwa ,wanawake hedhi, zisizokuwa na, mpangilio, na kasonono, pia , vidonda ,vya, tumbo ,(STOMACHI UCLENS) IHUSHI ndoji lako. 

NKANYA ni dwa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi ariyekuacha, mke mme, atakuludia kwa, mda, wa msaa3 tu , ukishaitumia atarudi ,mwenyewe bila ,ugovi tena, NKOMA ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada . 

HERBON, ni, dawa, ya kuongeza, CD4, NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu ,miguu, kufaganzi, na ,kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! DR SITTA, amebobea, kwa tiba asilia 

DAR ANAPATIKANA MBAGALA, ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI SHINYANGA, KAHAMA MJINI, KWA MAELEZO ZAIDI , 

PIGA SIMU 0763172670 au 0715172670 

WOTE MNAKALIBISHWA, KAMA, UTAKUWA NA TATIZOUTAHUDUMIWA

Zamaradi Awajia Juu Wanaomuingiza Katika Sakata la Muna na Aliyejitokeza Kuwa Baba Mzazi wa Patrick

$
0
0
Zamaradi Awajia Juu Wanaomuingiza Katika Sakata la Muna na Aliyejitokeza Kuwa Baba Mzazi wa Patrick
MTANGAZAJI Zamaradi Mketema aliyepewa jukumu kuratibu msiba wa mtoto wa Muna, Patrick ametaka yeye asihusishwe juu ya mvutano uliopo kati anayedaiwa kuwa ni baba wa mtoto, Peter Zacharia na aliyekuwa mkewe Muna Love.


Hatua hiyo imekuja baada ya siku ya jana kusambaa taarifa mtandaoni kwamba yeye anachangia mgogoro huo kuendelea wakati Muna akisema msiba uko kwake Mbezi Beach na baba akisema msiba upo kwake Mwananyamala huku wakiacha maswali kuhusu baba halisi wa mtoto huyo iwapo ni Peter au Casto.

Akizungumza kwenye Exclusive Interview na Global TV Online jana nyumbani kwake Mwananyamala Darajani jijini Dar, Peter alisema Zamaradi amefanya jitihada kubwa za kuokoa uhai wa Peter na kuongeza kuwa licha ya mtoto huyo kufariki, amemwachia jukumu la kuzungumza na Muna ili wanaweza kuumaliza mgogoro wao ili mtoto azikwe kwa taratibu zote.

Kupitia Ukurasa wake wa Instagram, Zamaradi ameandika;


Rais Trump Ashambuliwa Mitandaoni kwa Kukosea Kiingereza

$
0
0
Rais wa Marekani, Donald Trump amejikuta akishikwa na hasira baada ya wanaharakati mitandaoni kumsahihisha makosa ya kisarufi (grammatical Error) na kimaandishi (Typing error) kwenye Tweets zake huku wakimkebehi kuwa hajui hata kuandika kwa ufasaha kwa lugha ya Kiingereza.

Trump ambaye jana Julai 04, 2018 alitwiti mara moja na kisha kufuta twiti hiyo baada ya kushambuliwa kuwa alikosea kuandika, huku akidai mtandaoni kuna vyombo vya habari ambavyo haviangalii anachokifanya bali vinaangalia makosa yake ya kisarufi (grammatical error) mtandaoni.

“Nimeshawahi kuandika vitabu bora na vilivyouzwa zaidi, kwa hiyo huwezi kunipima kamwe kwenye uwezo wangu wa kuandika. Hii inaonesha wazi kuwa kuna vyombo vya habari vinatoa habari bandia (Feki) kwa kutumia muda mrefu kutafuta makosa kwenye tweet zangu,“ameandika Trump kwenye ukurasa wake wa Twitter.

Daktari Aanika Madhara ya Kukatwa Utumbo Kama Alivyofanya Wema Sepetu

$
0
0
Daktari Aanika Madhara ya Kukatwa Utumbo Kama Alivyofanya Wema Sepetu
KWA kipindi cha takribani wiki nzima sasa, gumzo kubwa katika ulimwengu wa mastaa ni kuhusu afya ya msanii maarufu Bongo, Wema Sepetu baada ya kusambaa video ikimuonesha akitoka kwenye hospitali moja jijini Dar ikidaiwa kuwa eti alikatwa utumbo ili kupunguza unene.



Video hiyo iliibua maswali mengi kuhusu kile kilichokuwa kikizungumzwa huku Wema akishindwa kujitokeza hadharani kueleza kilichompata na kama ni kweli alikatwa utumbo ili kupunguza unene ama ni maneno ya watu tu.



Aidha meneja wake, Neema Ndepanya alipoulizwa hivi karibuni kuhusu afya ya msanii wake huyo alipata kigugumizi licha ya siku chache nyuma kukiri staa huyo kusumbuliwa na tatizo la tumbo.

Hata hivyo, baada ya mengi kuzungumzwa, juzi Jumapili baada ya kupotea kwa muda mrefu, Wema aliposti picha ikimuonesha alivyo kwa sasa ambapo alionekana amepungua huku wengi wakimpongeza kwa muonekano wake.


Kufuatia upya huo wa Wema, baadhi ya wasichana waliomuona mtandaoni, walionesha kuvutiwanaye na wengine kudai kuwa, nao watafanya kila wawezavyo ikibidi kwenda kukatwa utumbo ili kupunguza unene.



“Jamani Wema kapendeza sana, licha ya kwamba kavaa dela (angalia picha ya mbele kushoto) lakini inaonesha kabisa amepungua tofauti na alivyokuwa huko nyuma. Sijui ndiyo huko kukatwa utumbo kama wanavyosema au kitu gani.



“Yaani ninavyotamani kupungua, na mimi nitafanya kila liwezekanalo ikibidi nitakwenda kukatwa utumbo maana naambiwa nayo ni njia mojawapo ya kupunguza unene,” alisema Sharika Sulle wa Sinza jijini Dar.



Baada ya kubainika kuwa baadhi ya wasichana walioona muonekano mpya wa Wema walishawishika kupunguza miili yao kwa kutumia njia zozote ikiwemo kukatwa utumbo, mwandishi wetu alimtafuta daktari maarufu jijini Dar, Godfrey Chale ambaye alifafanua kuhusu njia hiyo ya kupunguza unene.Kukatwa utumbo inakuwaje?



Kwa mujibu wa daktari huyo, njia hiyo ya kupunguza unene ambayo wengi huijua kama kukatwa utumbo kitaalum inaitwa Gastric Band ambapo sehemu ya tumbo la binadamu inabanwa ili kulipunguza ukubwa na kuruhusu kiasi kidogo cha chakula kuingia.



“Ni njia ya kitaalam ya kupunguza unene, kinachofanyika ni kupunguza ukubwa wa tumbo kwa kulibana katika sehemu ya juu ili mtu anapokula chakula kidogo tu ajisikie ameshiba. Hali hiyo humfanya kadiri siku zinavyokwenda kupungua unene,” alisema daktari huyo na kuongeza:

Image result for wema sepetu
“Ni njia inayoshauriwa kidaktari ya kupunguza unene lakini mbali na faida hiyo, kuna madhara yanayoweza kuwapata wanaofanya uamuzi huu.

“Kwa mfano, lengo lako linaweza kuwa ni kupungua lakini sasa ukakonda kupitiliza, hali ambayo pia kiafya siyo sawa. Lakini pia, tiba hii ya kupunguza unene inafanyika kwa kufanyiwa upasuaji ambapo damu nyingi inaweza kupotea na kusababisha madhara makubwa.


Madhara mengine yanayosababishwa na upasuaji huu, ni mwili kushindwa kuzikubali dawa za usingizi (Anasthetics) ambazo kwa kawaida mgonjwa yeyote anayefanyiwa upasuaji huchomwa kabla ya upasuaji. Hali hii ikitokea, maana yake ni kwamba mgonjwa anaweza kuzinduka wakati upasuaji ukiendelea na kusababisha kifo.

Matatizo mengine yanayoweza kusababishwa na upasuaji huu, ni mwili kupata mzio (allergy), kupata matatizo ya kupumua, damu kuganda kwenye miguu na kwenye mapafu, kuishiwa damu, kupata maambukizi kwenye damu na kupatwa na shambulio la moyo au kiharusi wakati wa upasuaji au baada ya kumalizika kwa upasuaji.

Pia kifaa maalum kinachowekwa tumboni baada ya upasuaji, kinaweza kuhama sehemu kilipowekwa au kikayeyuka na kusababisha madhara kwa mhusika, ambapo atalazimika kufanyiwa tena upasuaji. Utafiti unaonesha kwamba, kati ya asilimia 15- 60 ya watu waliofanyiwa upasuaji huu, hulazimika kufanyiwa upasuaji mwingine ili kurekebisha dosari zilizotokea awali.

Baada ya upasuaji, mhusika anatakiwa kufuata masharti ya vyakula, vinginevyo atatapika sana na kupatwa na tatizo la kutanuka kwa koo. Pia kifaa kinachoachwa tumboni, kinaweza kusababisha majeraha ya tumbo na viungo vingine vya ndani, husababisha kiungulia kikali, vidonda vya tumbo na maumivu makali ya tumbo.

Kutokana na madhara ya njia hiyo ya kupunguza unene, mastaa na watu wengine wanaotamani kupungua wameonywa kutoitumia ikiwa wana uwezo wa kutumia njia nyingine kama kufanya mazoezi, kufanya diet na nying

Hivi Ndivo Daimond Alivyovuruga Ndoa ya Zari na Maulid Kitenge

$
0
0
Hivi Ndivo Daimond Alivyovuruga Ndoa ya  Zari na Maulid Kitenge
 Imevuja! Baada ya hivi karibuni picha mbalimbali zikimuonesha Mtangazaji wa Kituo cha Redio cha EFM, Maulid Kitenge akijiachia nyumbani kwa mjasiriamali maarufu Afrika Mashariki, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ huko Afrika Kusini ‘Sauz’ na kufunguka kuwa ana mpango wa kumuoa, mpango huo umetibuka.

Aliyeutibua ni mzazi mwenzake na mwanamama huyo msanii Nasibu Abdul ‘Diamond’ ambaye amedaiwa kumzidi nguvu akinomanoma mtangazaji huyo, Amani linakujuza.

Chanzo makini kutoka Sauz kilieleza kuwa Kitenge alikuwa kwenye maandalizi ya kupeleka posa ili atimize alichomuahidi Zari, lakini mipango hiyo imeingia dosari, tulia ujuzwe zaidi.

“Unajua Kitenge alikuwa kwenye maandalizi na kwamba hivi karibuni posa ilikuwa ipelekwe na mipango ya ndoa ifanywe lakini upepo umegeuka baada ya Diamond kuonekana kupedwa zaidi na watu wa karibu na Zari wakiwemo mashabiki wa  mwanamama huyo ambaye ni raia wa Uganda,” kilisema chanzo hicho.

DIAMOND AMETIBUAJE?

Chanzo kiliendelea kutiririka kuwa Diamond anatajwa kutibua ndoa hiyo ya mama watoto wake na Kitenge kwa kuwa Waganda wanampenda sana na wanatamani yeye ndiyo amuoe Zari lakini siyo mwanaume mwingine yeyote.

“Huko Uganda ambapo ndipo alikozaliwa Zari, Diamond bado ana nafasi kubwa sana kwani anakubalika mno na jamii, kwa hiyo hawamtaki huyo Kitenge kabisa hali ambayo pia imemweka Zari njia panda,” kilitiririka chanzo.

WAGANDA WACHARUKA

Habari ziliendelea kuelezwa kuwa Waganda wamecharuka vilivyo baada ya kusikia Kitenge anataka kumuoa Zari jambo ambalo hawataki kabisa kulisikia kwani wao wanayemfahamu na kumkubali zaidi ni Diamond na siyo mwingine.

“Kumekuwa na maneno mengi sana kwenye mitandao ya kijamii, lakini kikubwa ni ishu ya zari kuolewa na Kitenge, wengi wamesema kuwa hawamshauri Zari asifanye hivyo na endapo atalazimisha wametishia kutomuunga mkono kwenye shughuli zake za biashara.” kilisema chanzo.

Msimamo huo wa mashabiki wake unatajwa kuwa umemtikisa mwanamama huyo kiasi cha kutojua nini cha kufanya ambapo chanzo cha karibu na Zari kimeliambia Amani kwamba The Boss Lady hana mpango wa kufunga ndoa na Kitenge.

KITENGE ANASEMAJE?

Ili kuujua ukweli juu ya suala la kukataliwa kwake ukweni, Amani lilimtafuta Kitenge ambaye alisema hajali chochote na mipango yake ya kumposa Zari iko palepale.

“Hao wanaosema maneno hayo kwamba nimekataliwa hivyo mpango wa kumposa Zari umeishia hapo ni waongo, ninachosema mimi ni kwamba niko kwenye mipango ya kupeleka posa muda wowote,” alisema Kitenge.

VIPI UPANDE WA DIAMOND?

Katika kuleta usawa wa habari gazeti hili lilimtafuta Diamond ili aeleze anazungumziaje suala hilo, simu yake ya mkononi haikuwa hewani.

Polisi Nchini Ethiopia Yalaumiwa kwa Kuwatesa na Kuwabaka Wafungwa

$
0
0
Polisi Nchini Ethiopia Yalaumiwa kwa Kuwatesa na Kuwabaka Wafungwa
Maafisa wa Polisi nchini Ethiopia wamelaumiwa kwa kuwatesa kwa vipigo na kuwabaka wafungwa wa kike, kwa mujibu wa ripoti mpya iliyochapishwa na shirika la kutetea haki za binadamu ‘Human Right Watch’ kuonesha kuwa wafungwa wa kisiasa walivyobakwa katika jimbo la Somalia.

Ripoti hiyo imewashutumu maafisa wanaofanya kazi katika jela ya Ogaden pamoja na maafisa wa kikosi cha Polisi cha Liyu, kwa kuwapiga na kuwabaka wafungwa wa kike wanaodaiwa kuwa waasi wa kundi la upinzani la Ogaden Liberation Front.

Human Right Watch ili wahoji wafungwa zaidi ya 100 waliokuwa wamefungwa katika gereza la Ogaden kati ya mwaka ya 2011 na 2018 huku wafungwa hao wakikaririwa kuwa walivuliwa nguo na maafisa wa gereza hilo kisha kubakwa.

Aidha katika ripoti hiyo imeonesha kuwa watoto wengi wamezaliwa kwa njia ya ubakaji huku wakiwa ndani ya 'seli' vyumba vya wafungwa bila huduma za kiafya.

Hata hivyo Waziri Mkuu mpya wa Ethiopia Abiy Ahmed, amekiri kuwa maafisa wa usalama wamewatesa wafungwa hao na serikali itafuatilia suala hilo na wote waliohusika watawajibishwa kisheria.

Rais wa zamani wa Club ya Barcelona ashutumiwa kumnunulia Abidal ini la magendo

$
0
0
Rais wa zamani wa Club ya Barcelona ashutumiwa kumnunulia Abidal ini la magendo
Leo July 4,2018 nakuletea stori hii kutoka huko nchini Hispania ambapo unaambiwa kuwa kwa mujibu wa ripoti za hivi karibuni zinasema kuwa Rais wa zamani wa Club ya Barcelona Sandro Rossell alimnunulia ini kwa njia ya magendo beki wake Eric Abidal mwaka 2012.

Hata hivyo taarifa hiyo imepingwa vikali na Barcelona pamoja na Abidal mwenyewe ambaye kwa sasa ndie Katibu wa Club hiyo.

Mwaka 2012 beki Raia Ufaransa Abidal alisumbuliwa na tatizo la ini lililomlazimu kufanyiwa upasuaji kwa ajili ya kumpandikizia ini jingine ambalo ndilo linalodaiwa kununuliwa kwa njia ambazo sio halali Rais huyo wa zamani wa Barcelona.

Aidha Shirika la upandikizaji wa viungo vya ndani ya mwili nchini hispania limeanzisha uchunguzi wa ndani likishirikiana na hospitali husika na shirika la upandikizaji la eneo la Catalan kubaini ukweli wa sakata hilo.

Baada ya Kutumbuliwa Mwigulu Akataa Kuongelea Mambo ya Siasa

$
0
0
Baada ya Kutumbuliwa Mwigulu Akataa Kuongelea Mambo ya Siasa
Mbunge wa Iramba Magharibi (CCM), Dk Mwigulu Nchemba amesema masuala ya siasa atayazungumzia jimboni kwake.

“Mambo ya siasa siongelei, ukitaka kuongelea nifuate jimboni tuongelee maendeleo ya jimbo langu,” amesema Dk Nchemba.

Alisema hayo jana Julai 4, 2018 baada ya kumalizika mechi ya michuano ya Cecafa Kagame CUP katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kati ya Simba na Singida United.

Dk Nchemba alikataa kuzungumzia masuala ya kisiasa baada ya kuulizwa swali na mwandishi wa Gazeti la Mwananchi.

Qeen Darleen Afunguka Sifa za Mwanaume Anayetaka Kutoka Naye Kimapenzi

$
0
0
Qeen Darleen Afunguka Sifa za Mwanaume Anayetaka Kutoka Naye Kimapenzi
Msanii wa Bongo Flava, Queen Darleen ameeleza vitu viwili ambavyo mwanaume akimfanyia kwenye mahusiano hasiti kuachana naye mara moja.

Mwanadada huyo kutokea WCB akipiga stori na Funiko Base ya Radio Five ametaja vitu hivyo ni uongo na usaliti.

“Darleen kwenye mahusiano ni mtu ambaye hapendi uongo, hilo la kwanza, na akikaa na mtu anakaa na mtu lakini yule mtu akigundua kama amemsaliti hawezi kumsamehe,” amesema.

“Yaani umenisaliti na nina uhakika hata kama nakupenda vipi na tumeishi miaka mingapi mimi naachana na wewe kwa sababu imani yake Darleen atakapokusamehe basi utaendelea kuwa na mtu mwingine,” amesisitiza Darleen.

Queen Darleen ambaye ndiye msanii pekee wa kike katika label ya WCB, kwa kipindi kirefu hajaweka wazi mahusiano yake kitu kilichopelekea hivi karibuni kutaniwa na Lava Lava katika mtandao kwanini hamuweki wazi shemeji watu wamjue.

Simba Yampokea Kimya Kimya Kocha Wao Mpya Raia wa Ubelgiji

$
0
0
Simba Yampokea Kimya Kimya Kocha Wao Mpya Raia wa Ubelgiji
Mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu uliopita, Simba imempokea kimya kimya kocha wao mpya raia wa Ubelgiji, Patrick Aussems ambaye amekuja kuziba nafasi ya Pirre-Lechantre ambaye ameachana na klabu hiyo mwishoni mwa msimu uliopita wa mwaka 2017/18.

Patrick Aussems mwenye umri wa miaka 53 ambaye aliwahi kucheza kama mlinzi enzi za uchezaji wake amekuja nchini mapema Jumapili ya wiki hii na kushuhudia mchezo wa pili wa Simba wa kombe la Kagame ambao waliifunga Rayon Sport 2-1 na jana pia alishuhudia mchezo ambao Simba ilitoka sare na Singida United.

Kocha huyo aliwahi kuzifundisha klabu kadhaa zikiwamo ES Troyes AC na Stade De Reims za Ufaransa pamoja na mabingwa wa kombe la Shirikisho la Afrika mwaka 2012, AC Leopards ya Congo Brazzaville .

Inaelezwa kuwa kocha huyo yupo katika mazungumzo ya mwisho na uongozi wa klabu ya Simba juu ya masuala ya mkataba kabla ya kumwaga wino rasmi kuitumikia klabu hiyo ambayo inashiriki michano ya kimataifa msimu ujao.

Historia yake kwa ufupi .

Jina lake halisi ni Patrick Winand Aussems , alizaliwa mnamo Februari 6, 1965 na alichezea baadhi ya vilabu vikubwa kadhaa barani Ulaya vikiwemo Standard Liege, KRC Gent na RFC Seraing za Ubelgiji, pamoja ES Troyes AC ya Ufaransa.

Mafanikio makubwa ambayo aliyapata ni kuiwezesha klabu ya AC Leopards ya Congo Brazzaville mwaka 2014 kuchukua ubingwa bila ya kupoteza mchezo wowote na kuifikisha katika nusu fainali ya kombe la Shirikisho ambapo ilipoteza mchezo huo mbele ya Sewe Sports ya Ivory Coast katika mwaka huo huo. Pia aliwahi kuifundisha timu ya taifa ya Nepal kati ya mwka 2015-2016.

Kikosi Timu ya Taifa ya Zimbabwe Yalala Mtaani Kisa Hiki Hapa

$
0
0
Kikosi Timu ya Taifa ya Zimbabwe Yalala Mtaani
Kikosi cha wachezaji wa timu ya taifa ya Zimbabwe ya mchezo wa Rugby wamelazimika kulala mtaani wiki hii nchini Tunisia baada ya kulalamikia huduma duni waliyopata kwenye hoteli waliyoandaliwa.



Picha kadhaa zimepostiwa kwenye mitandao ya kijamii zikiwaonyesha vijana hao wa Zimbabwe wakiwa wamelala kandokando mwa kituo cha mabasi nchini Tunisia wakati wakiwa kwenye maandalizi ya mchezo wao wa kufuzu michuano ya kombe la dunia dhidi ya wenyeji utakao pigwa Jumamosi ya wiki hii.



Mbali na kulala mtaani usiku wa vijana hao pia ulikuwa mmbaya baada ya kucheleweshwa kwenye uwanja wa ndege kwa saa sita nyakati za usiku kutokana na kucheleweshewa taratibu za Viza.

Baada ya Zimbabwe kuandika barua rasmi ya kulalamikia kitendo hicho mara tu walipofika kwenye hoteli hiy Shirikisho la Mchezo wa Rugby nchini Tunisia limeshtumu nchi hiyo kwa kitendo chake cha kuchua maamuzi ya kwenda kulala kwenye mitaa bila hata kuangalia uhusiano wa nchi hizo mbili.
Shirikisho la Mchezo wa Rugby Barani Africa limeomba radhi kwa jambo hilo lililotokea na kuwapangia hoteli nyingine.



Timu hiyo ya taifa ya Zimbabwe ambayo inashika nafasi ya nne ipo nchini Tunisia ambao ndiyo wandaaji wa mashindano hayo wakitafuta tiketi ya kufuzu michuano ya kombe la dunia.

Baada ya Kukabidhiwa Ofisi Lugola Aanza Kazi kwa Kuvunja Baraza na Kamati Zote za Usalama Brabarani

$
0
0
Baada ya Kukabidhiwa Ofisi Lugola Aanza Kazi kwa Kuvunja Baraza na Kamati Zote za Usalama Brabarani
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amelivunja Baraza la Taifa la Usalama Barabarani na Kamati zote za Usalama barabarani za mikoa na wilaya zote.

Julai 01, 2018, Rais Dkt John Magufuli alimteua Kangi Lugola Waziri wa Mambo ya Ndani akichukua nafasi ya Mwigulu Nchemba, huku akimtaka waziri huyo mpya kushughulikia sakata la Lugumi, ajali, sare za polisi, uingizwaji wa mizigo bandarini na mambo mengine ya usalama wa nchi.

Mfanyabiashara Peter Zakaria Afikishwa Mahakamani Kwa Kutaka Kuua Anyimwa Dhamana

$
0
0
Mfanyabiashara Peter Zakaria Afikishwa Mahakamani Kwa Kutaka Kuua Anyimwa Dhamana
Mfanyabiashara maarufu wilayani Musoma, Peter Zakaria, amepandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka mawili ya kujaribu kuua.

Zacharia amesomewa mashtaka hayo leo Julai 5, mbele ya Hakimu mkazi Mfawidhi Rahimu Mushi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Musoma, akidaiwa kuwapiga risasi Ahmed Segule na Isaac Bwire ambao hata hivyo hawakutajwa ni wakazi wa wapi wala kazi yao.

Baada ya kusoma hati ya mashtaka, Wakili wa Serikali Lukelo Samuel aliiomba Mahakama kuzuia dhamana ya mshtakiwa kwa sababu hali ya waliojeruhiwa bado ni mbaya na wamelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam kwa matibabu.

Maombi hayo yalipingwa na Mawakili wa mshtakiwa Kassim Gile na Onyango Otieno wakisema hayana msingi na kwamba dhamana ni haki ya mshtakiwa na shtaka linalomkabili linadhaminika.

Baada ya kusikiliza hoja za zote mbili, Hakimu Mushi ameahirisha shauri hilo hadi Julai 10 atakapotoa uamuzi wa kutoa au kuzuia dhamana. Mshatakiwa amepelekwa mahabusu kusubiri uamuzi wa mahaka

Juni 30, Mkuu wa mkoa wa Mara, Adam Malima aliwaambia waandishi wa habari kuwa waliojeruhiwa katika tukio hilo lililotokea mjini Tarime saa 2 usiku wa Juni 29 ni Maofisa wa Idara ya Usalama wa Taifa waliofika katika kituo cha mafuta kinachomilikiwa na Zakaria kwa ajili ya kujaza mafuta kwenye gari lao.

Vigogo NEMC Kortini Kwa Kughushi Saini ya Waziri Makamaba

$
0
0
Vigogo NEMC Kortini Kwa Kughushi Saini ya Waziri Makamaba
Watu wanne wakiwamo wafanyakazi wa Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka manane ya uhujumu uchumi ikiwamo kughushi saini ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), January Makamba katika vyeti vya tathmini ya uharibifu wa mazingira.

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Nassoro Katuga aliwataja washtakiwa hao jana mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Maira Kasonde kuwa ni Ofisa wa Mazingira NEMC, Deusdith Bulamire (38), Sekretari, Edna Lutanjuka (51) na mkulima Mwaruka Mwaruka (42).

Mwingine ni Mkaguzi kutoka ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali(CAG), Dawson Barwongeza.

Akisoma mashtaka yanayowakabili washtakiwa hao, wakili Katuga alidai washtakiwa hao kwa pamoja kati ya Machi 28, 2017 na Novemba 4, 2017 wakiwa Dar es Salaam walikula njama ya kutenda kosa la kughushi Vyeti vya Tathmini ya Uharibifu wa Mazingira (EIA).

Washtakiwa Bulamire, Lutanjuka na Mwarukwa wanadaiwa kuwa Oktoba 10, 2017 walighushi saini ya Waziri Makamba kwenye cheti cha EIA wakijaribu kuonesha sahihi hiyo ni ya waziri huyo wakati si kweli.

Kwa pamoja washtakiwa hao wote wanadaiwa kuwa kati ya Machi 28 na Novemba 4, mwaka jana walijipatia Sh30 milioni kwa njia ya udanganyifu kutoka kwa F1195 CPL Yohana Mtweve kwa madai kuwa wangeweza kufanya tathmini ya uharibifu wa mazingira na kumpatia cheti ambacho kinatolewa na NEMC kitendo ambacho si kweli.

Pia, wanadaiwa kuisababishia hasara ya Sh20 milioni NEMC.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo hawakuruhusiwa kujibu chochote kwa sababu Mahakama ya Kisutu haina mamlaka ya kuisikiliza wala kutoa dhamana kwenye kesi hiyo.

Washtakiwa wamepelekwa rumande na kesi iliahirishwa hadi Julai 18, 2018 kwa ajili ya kutajwa.

Nape Nauyo Atoa Maneno Mazito kwa Wanaomzushia "Watapata Tabu Sana Wanuka Maziwa"

$
0
0
Nape Nauyo Atoa Maneno Mazito kwa Wanaomzushia "Watapata Tabu Sana Wanuka Maziwa"
Mbunge wa Jimbo la Mtama, Nape Nnauye amewafungukia wanaosambaza taarifa kuwa  amesimamiswa uanachama wa Chama Cha Mapinduzi nakusema watapata tabu sana.

Nape ametoa kauli hii baada ya kusambaa taarifa katika mitandao ya kijamii kwamba barua ya Mbunge huyo kusimamishwa uanachama wa Chama chake imekwishamfikia mkononi.
“Kwa UZUSHI huu WATAPATA TABU SANA wanuka maziwa, ndio shida ya kudandia treni kwa mbele, unawakuta wenyeji unakuwa Mwenyezi kuliko….!” Nape Nnauye

Familia ya Muna Waungana na Peter Zacharia Mwananyamala Katika Msiba wa Mtoto wao Patrick

$
0
0
Ndugu wa Muna Waungana na Peter Zacharia Mwananyamala  Katika Msiba wa Mtoto wao Patrick
Kufuatia kifo cha mtoto wa Muna Love, Patrick aliyeaga dunia juzi Nairobi,Kenya akipatiwa matibabu, taarifa zenye mkanganyiko zimekuwa zikisambaa mitandaoni kuhusu nani ni baba halisi wa mtoto huyo huku wengine wakisema ni Casto na wengine wakidai ni Peter Zacharia.

MCL Digital ilifunga safari mpaka Mwananyamala nyumbani kwa Peter Zacharia Komu, anayedai kuwa ni mume wa ndoa wa Muna na ndiye baba mzazi wa marehemu Patrick, huku akieleza amekuwa akimhudumia mtoto huyo kuanzia matibabu yote, matunzo na ada ya shule.

Alidai kuwa yeye ndiye baba wa mtoto kwa kuwa vielelezo vya kumuhudumia mtoto anavyo huku akisema, alimkatia Bima ya Afya ya Jubilee.

Peter ameiambia MCL Digital kuwa yeye ni mume halali wa Muna walifunga ndoa kanisani mwaka 2010.


Alisema Patrick alipozaliwa miaka saba iliyopita, hakutaka kujitokeza hadharani kubishana na Casto ila aliwahi kumwambia asiingilie familia yake,na kumwambia Muna kuwa akakanushe anachoandika Casto kuwa Patrick ni mwanae.

Lakini tangu Kifo kitokee kumetokea na utata mkubwa katika msiba wa mtoto huyo kwani misiba imewekwa sehemu mbili kwa Peter ambaye anadai Patrick ni mtoto wake na kwa Muna anadai mtoto wa Casto.

Kutokana na hayo, Ndugu wa Muna ambao ni mama mzazi,dada yake,kaka yake,wajomba na mdogo wake wameungana na Peter na kudai wao wanachofahamu baba halali wa Patrick ni Peter, Casto wanamsikia mitandaoni tena baada ya Patrick kufikisha miaka mitano.

MCL Digital ilipata kuongea na mama yake Muna,ambaye hakuwa na hali nzuri kwani kila wakati alikuwa anazimia na kuishiwa nguvu.

 “Huyu Peter ndiyo baba halali wa Patrick navyojua mimi, ila sifahamu Muna amepatwa na nini, kwani kitu anachokifanya siyo sahihi kwa Peter,wakati ukweli anaujua kabisa. Sielewi,sielewi kabisa Muna kwanini yuko hivi,” alisema.

MCL Digital haikuishia hapo, ilizungumza na dada wa Muna naye amefunguka na kubainisha kuwa familia inafahamu mtoto huyo ni wa Peter na siyo Casto.

Chanzo: Mwananchi

Alichoongea Patrick Kabla ya Kufariki Akiwa Amelala Kifuani mwa Joel Waga “Daddy naumia”

$
0
0
Alichoongea Patrick Kabla ya Kufariki Akiwa Amelala Kifuani mwa Joel Waga “Daddy naumia”
Mtoto Patrick imewagusa wengi na still inaendelea kuwagusa wengi kila kukicha tukiwa tunasubiria kufahamu taratibu za mazishi AyoTV imekinasa kile alichoongea Patrick dakika chache kabla ya mauti kumfika.

Kwa mujibu wa Joel Lwaga ambaye alikuwa ana muuguza Patrick, Nairobi pamoja na Mama yake ameandika stori ndefu kidogo katika ukurasa wake wa instagram akieleza vile alivyokutana na Patrick mpaka akawa Baba yake wa kiroho nakufikia hatua ya kumjali kwa kila jambo na wakati umauti unamkuta alikuwa yupo nae.

Ameandika hivi Joel Lwaga “Hii ilikuwa ndio siku ya kwanza tulipoonana na since then u chose to call me Dady…Katika wakati huu muhimu ninaposhuhudia safari yako ya mwisho shujaa wa imani, nilikuahidi kutokukuacha and i made it to be there from the beginning of your illness till the time wen u said “Daddy…naumia” and i replied God is going to heal you son!”

“Hilo ndilo lilikuwa neno lako la mwisho kuniambia wakati ukiwa umelaza kichwa chako kifuani kwangu nakusinzia kisha ukaingizwa chumba cha wagonjwa mahututi ambapo haukurudi tena ukiwa hai nimekusubiri kwa siku tano pembeni ya kitanda chako lakini umeamua usirudi …ni zamu yangu kukwambia sasa naumia😭😭 naumia baba😭😭….” Joel Lwaga

Aliendelea kuandika Joel “Lakini wewe ni shujaa uliyerudi Nyumbani, an Amazing soul and a servant of God pumzika mwanaume, umeamua kujumuika na Bwana katika wingu la malaika….kama wanadamu tulitamani sana uendelee kuwepo ukue uwe mkuu na kumsaidia mama yako lakini imempendeza Mungu ukakae katika utukufu wake!”

“Pole mama @munalove100we are still together in this also, Mungu aujuaye Moyo wako na akupe Faraja ya kwel ipitayo ufahamu wa kibinadamu na akuvushe salama katika kipnd hiki kigumu R.I.P Hero! R.I.P @patdasmartboy#tillwemeetagainson”

Amehitimisha kwa kusema Bwana alitoa na Bwana ametwaa Jina lake na lihimidiwe
Viewing all 104780 articles
Browse latest View live




Latest Images