Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104698 articles
Browse latest View live

Anashinda Whatsapp Masaa Yote, Ila Nashindwa Kumbwaga

$
0
0
Huyu dada nimemfahamu miaka mitatu iliyopita.

Ni mwanasheria kwenye firm fulani jijini Dar, nilikuwa nina mpango wa kumuoa haraka, ila mmoja wa marafiki zake wa karibu aliniambia nijitahidi kumfahamu kwanza kabla sijaamua kumuoa nadhani alihisi kitu.

Kufahamiana naye kwa muda tukaishia kupata mtoto mmoja wa kike ambaye sasa ana miaka miwili.

Ni mwanamke mzuri sana, ni gumzo kila anapopita au kufanya kazi, hata nilitaka nitoane macho na patina mmoja wa firm yake. 

Kwa kweli anaita kila jicho ana mengi mazuri, lakini pia ana mapungufu yaliyonipigisha breki kali juu ya tope.

Kwa sasa anaishi na wazazi wake, lakini mara nyingi saba tunalala kwangu. Nafahamika kwao kama mzazi mwenza, kwetu pia kaskazini wanamtambua.

Amekuwa ni mwepesi sana wa kupata marafiki wa kiume, ana hasira za karibu, kujiachiachia sana kwa wanaume imekuwa sehemu ya maisha yake, yeye anadai si wapenzi wake. Wanataniana tu hii ni moja ya sababu iliyonizuia kumuoa.

Nilihisi kama hajiheshimu.hayuko tayari kuishi kama mke wa mtu nikadhani nimwache kwanza ale maisha wakati nami nakula taratibu ingawa nahofu ya magonjwa.

Simu zake sijawahi ziona hata mara moja zikiita kwa sauti toka nimfahamu.anashinda watsapp 24/7. 

Facebook kwake ni kama oxgen, kila siku anaongeza wanaume, viber anatumiwa mioyo na mikisi ya wanaume, linkedin pia hayuko mbali.

Nahisi kweli atakuwa ananipenda, lakini kwa hayo nashindwa kuji commit, ila bahati mbaya nashindwa hata kumuacha, hasa ukizingatia nina mtoto naye. 

Yaani sijui nifanyeje, nimbwage.

Naona sio waifu matirio.

Ataniua jamani.

Ndoa ni DIRECT VISA To Hell Kama Ukiichukulia Poa, Ni Heri Usioe ama Kuolewa Kama Humaanishi

$
0
0
Kila mtu anataka Kuolewa lakini shida ni Vigezo vya Waoaji vikoje??Kila siku vigezo vinabadilika..Sasa hivi unaangaliwa sana uwezo wako wa mfukoni kabla hujaambiwa NDIO...Hela imekuwa ndo GREEN LIGHT,ukiwa hohehahe basi utazungushwa wee na utaambiwa kila siku,"IAM NOT READY FOR MARRIAGE"
Kuna watu wametoswa kisa Wallet hazisomi na ukashangaa wameolewa na watu kisa WANA HELA..
Hela ingekuwa kila kitu AMBER ROSE na WIZ KHALIFA wasingeachana..Wana kila kitu wale...
Hela ingekuwa jawabu NICK CANNON na MARIAH CAREY wasingeachana...
Hela ingekuwa kila kitu JASON DERULLO na JORDIN SPARKS wangekuwa happily married lakini Wapi...
Raha ya ndoa itoke Moyoni...Mpendane kwa jinsi mlivyo...Mpendane kwa hali yoyote mliyonayo na muelewane..
Kuna watu kula kwao ni kwa mbinde lakini ndoa yao ina amani na furaha mwaka wa 20 huu...Kuna watu wana kila kitu,Magari,Mashamba,Viwanja,Akaunti zilizonona lakini hata miaka 3 wameshindwa kufikisha...Wamekuwa WATALAKA VIJANA...
Ndoa ni DIRECT VISA to Hell kama ukiichukulia poa,ni heri Usioe ama kuolewa kama humaanishi...Maana ukiachana na mwenza wako ndani ya miaka 3 hiyo miaka mingine yoooteee UNAZINI TU...Mbingu utaisikia kwenye kipindi cha JAHAZI tu...
Jifunze kwa Wajane na Watalaka...Jua unachotamani na UJIPANGE!

By Seth

Obama:Tumekadiria Vibaya Nguvu za Wanamgambo wa Kiislam wa IS

$
0
0
Rais Obama amekiri katika televishen ya kitaifa kuwa Mashirika ya Marekani yalikosea katika kukadiria hatari ya wapiganaji wa dola ya kiislam, Islamic State nchini Iraq na Syria.
Amesema kuwa wapiganaji hao wenye uhusiano na Al Qaeda walitumia fursa ya kutokuwepo serikali thabiti nchini Syria na kuongezewa nguvu zaidi na vijana waliojiunga kupigania jihadi kutoka mataifa mengine.
Hata hivyo Obama amesema wapiganaji hao waliwahi kuvurumishwa huko Iraq na majeshi ya nchi yake yakishirikiana na kabila la Sunni.
Obama amekiri vyombo vya Ujasusi vya Marekani zilikadiria vibaya uwezo wa majeshi ya Iraq kupambana na wapiganaji wa kiislamu ambao wameteka maeneo mengi nchini humo.

TCRA Yaanza Kuwashughulikia Wanaotumia Vibaya Mitandao ya Kijamii

$
0
0
Mamlaka  ya mawasiliano Tanzania (TCRA) imeendelea kuwakumbusha wananchi  kutumia njia ya mawasiliano ipasavyo ili kujijengea heshima kwani kwa sasa hatua kali za kisheria zimeanza kuchukuliwa kwa wale wanaotumia vibaya mitandao ya kijamii.

Akizungumza na Times fm,  Meneja mawasiliano wa  (TCRA) Inocent Mungy amesema kuwa ipo haja kwa wasichana kujiheshimu kwani picha nyingi mbaya zinazoonekana kwenye mitandao hiyo  ni zao.

Naye Mkuu wa kitengo cha masuala ya watumiaji wa mitandao Isack Mruma amesema watu wanapaswa kuelewa matumizi  sahihi ya mitandao na lazima kuwe na usiri wa akaunti za mitandao ili kuweza kuepukana na matatizo ya usambazaji wa picha mbaya kwenye mitandao hiyo.

Amber Rose Alimfumania Wiz Khalifa Saa Nane Usiku, Wiz Asema Alifanya Makusudi

$
0
0
Uamuzi wa Amber Rose kutaka kutalakiana na mumewe Wiz Khalifa ulizua maswali mengi huku ‘uchepukaji’ ukitajwa kuwa chanzo cha yote.

Lakini kwa mujibu wa TMZ, Amber Rose alichukua uamuzi huo baada ya kumfumania Wiz Khalifa akiwa na mwanamke mwingine nyumbani kwake majira ya saa nane usiku.

Taarifa hizo zimeunganishwa na tweet ya Amber Rose inayoeleza kuwa anaendelea kulikumbuka tukio hilo.

Hata hivyo chanzo cha karibu na Wiz Khalifa kiliieleza TMZ kuwa rapper huyo aliwaambia kuwa alifanya makusudi kwa kuwa hataki tena kuendelea kuwa mume wa Amber Rose.

“I just didn't want to be married to her anymore.” Chanzo hicho kimemkariri Wiz Khalifa.

Inaelezwa kuwa hii ni moja kati ya sababu zilizomfanya Wiz Khalifa kutopinga uamuzi wa Amber Rose kudai talaka yake.

Taarifa za awali zilieleza kuwa Amber Rose na Nick Cannon walianzisha uhusiano wa mapenzi na kuwala kisogo Wiz na Mariah Carey lakini wote walikanusha taarifa hizo.

Sitta: Nyaraka Zinazosomwa Makanisani Kuhusu Bunge la Katiba ni za Kipuuzi

$
0
0
Mwenyekiti wa Bunge la Katiba,Samweli Sitta,bila haya wala kumungunya maneno,amethubutu kusema baadhi nyaraka zinazosomwa makanisani ni upuuzi kabisa.

Akiwakaribisha wageni ambao ni waumini wa makanisa bwana(sidhani kama anafaa kuitwa mheshimiwa) Sitta amesema na hapa namnukuu "muwe waangalifu huko makanisani kwani baadhi nyaraka zinazosomwa huko ni za kipuuzi".Huenda sijanukuu maneno yote kwa usahihi ila kikubwa amesema nyaraka hizo ni za kipuuzi!

Wadau,nafikiri wote mnankumbuka waraka wa jumuiya ya kikiristo Tanzania(CCT) uliokuwa unasomwa makanisani na waraka huo ulikuwa unapinga kuendelea kwa bunge hilo.

Sasa mdau tafakari mwenyewe mzee Sitta alikuwa anaongelea nyaraka gani na utapata jibu alafu jiulize mwenyewe athari ya kaulu kama hiyo kwa mchakato huu na Taifa kwa ujumla.

Alafu,hivi kila mwenye kuvaa suti na kuwa na mnvi anastahili kuwa kiongozi?

Wema Sepetu 'Watu Wenye Majungu Hawanisumbui Kichwa Kabisa Nabaki Nawatazama Tu'

$
0
0
Stori: Mayasa Mariwata
MADAMUUU! Beautiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ amecharuka na kudai anachukizwa kwa kiasi kikubwa na wasanii ambao wanapenda kumfanyia majungu kutokana na chuki zao binafsi.

Akipiga stori na paparazi wetu, Madam alisema anajua wapo wengi wanaomchukia kutokana na sababu zisizo za msingi kwa kudai kuwa anaringa na vyovyote vile wanavyojadili lakini hajali kwa kuwa hakuna ukweli wowote.

“Watu wenye majungu hawanisumbui kichwa kabisa nabaki nawatazama tu, sababu sina maringo wala majivuno kwa mtu yeyote, sasa cha ajabu wengine wanasema naringa, kwa staili hiyo hatutafika mbali maana wasanii wa nchi za wenzetu wana umoja hawana mambo ya aina hiyo,” alisema Wema.

Mbunge wa Mbeya Mjini Mh. Sugu amwagana na Mke wake…Mwanamke Afunguka Mazito

$
0
0

Mwigizaji wa filamu nchini FaizaAlly amemwagana na mwanamuziki mkongwe wa muziki wa kizazi kipya Joseph Mbilinyi maarufu kama Sugu …

Kupiia Instagram, Faiza ameandika maneno yanayoonyesha amemwagana na Mh.Sugu ambaye pia ni mbunge wa Mbeya mjini kupitia Chadema.


Masheikh Wakiislam Nao Waikataa Rasimu ya Sitta

$
0
0
SHURA ya Maimamu Tanzania imetangaza hatua za kuikwamisha Rasimu ya Katiba inayopendekezwa, kwa kwenda kuwaeleza waumini wa dini ya Kiislamu kupiga kura ya hapana.

Hatua hiyo imekuja baada ya Rasimu ya Katiba inayopendekezwa iliyowasilishwa mwishoni mwa wiki na Mwenyekiti wa Kamati ya Uandishi, Andrew Chenge, kuiweka kando Mahakama ya Kadhi.

Akizungumza na MTANZANIA jana mara baada ya kumalizika kikao cha maimamu wa 

nchi nzima, Msemaji wa Shura ya Maimamu Tanzania, Sheikh Rajabu Katimba, alisema hatua ya kupiga kura ya hapana ni moja ya azimio lililoafikiwa na kikao hicho.

“Msimamo wetu kwa asilimia 100 ni hapana, hatuungi mkono, tunalaani vikali jinsi mchakato huu wa Katiba ulivyovurundwa kwa sababu maoni ya Waislamu hayakuzingatiwa.

“Leo (jana) tulikuwa na kikao kilichojumuisha maimamu wote kutoka Tanzania na msimamo wetu katika hilo ni hapana,” alisema Sheikh Katimba.

Zawadi ya Gari Aliyopewa Wema Sepetu Siku ya Kuzaliwa Yaleta Kizazaa, Wadada Wamjini Wamecharuka

$
0
0
Juzi ilikuwa ni Siku ya Kuzaliwa kwa Mrembo Wema Sepetu, Kitu kilichovuta Hisia za Watu wengi ni zawadi ya Gari aliyopewa Wema Sepetu kutoka kwa Mpenzi wake Diamond Platnumz...Inasemekana huko mjini wadada wamechachamaa hawataki tena zawadi mchwara za maua , visimu ama saaa siku za sikukuu zao za kuzaliwa nao wanataka magari nao kutoka kwa Maboifriend zao.

Hili ni Tamko la Umoja huo wa Magelofurendi :

Mchungaji Aliyewalisha Waumini Majani Aja na Mpya..Sasa Awaponya Wagonjwa kwa Kuwakanyaga Kanyaga

$
0
0
Yule Pastor Mwenye Vituko Vingi Kutoka South Afrika anayejulikana kwa jina la Lesego Daniel amekuja na Mpya baada ya kuwalisha majani waumini na kubadilisha petrol kuwa Juice ya Apple , Sasa eti anawaponya Waumini wake ambao wanasumbuliwa na magonjwa kwa kuwakanyaga migongoni...Angali Picha Hapo Juu

Ninaachika Kila Mara Kwasababu ya Msimamo Wangu wa Kutokufanya Mapenzi Mpaka Siku ya Ndoa..Ushauri Pliz

$
0
0
Mpenzi wangu ambaye nimedumu naye kwa mwaka mmoja leo amenitamkia kuwa hawezi kuendelea kuwa na uhusiano na mimi, amesema ameshndwa kuvumilia kuwa na mpenz bila kufanya S3X.

Amesema hawezi kunifanya pambo awe ananiangalia tu, lakn wakat tunaanza uhusiano alinikubalia kuwa hatufanya S3X mpaka tukifunga ndoa lakini leo amenigeuka. Nimelia saaana toka asubuh mpk asahv lakn naona haina maana, NAOMBEN ushaur wenu jaman nimrudie nikubal kuS3X nae au? 

Manake mpaka leo tayari nimeshaachika kwa wanaume kama wanne yote chanzo ni S3X, sasa nitaachika mpaka lini? Manake inavyoonyesha ni kwamba wanaume hawawezi kukaa na mwanamke bila ku-s3x kama atakwambia yupo tayari kukaa na wewe hivyohivyo huwa wanakuwa na wanawake wengine wa nje wanao s3x nao.

Nilishaurini jamani, nimwambie nipo tayari ku-s3x nae au niachane nae tu? Ukweli nampenda sana .

Ile Video ya Izzo B ya Walala Hoi Iliyofanywa Kwa Mil 1.3 Hii Hapa, Embu Linganisha Hii na Zile za Mil 40

$
0
0
Week iliyopita Izzo B alifunguka Gharama za Video yake ya Wimbo wa Walala Hoi kwa Kusema Ameifanya kwa Milioni moja na Laki Tatu Pale kwa Director Nick Dizzo ...Sasa Embu Angalia Hii Video Alafu Uniambie Kama kweli Kuna Ulazima wa Kwenda Nje Kufanya Video za Milion 40.

Audio yake imefanywa na mikono ya producer Dupy kutoka Uprise Music navideo imeafanywa na Director Nick Dizzo ambaye ameshiriki kuongoza video kadhaa ikiwemo ya Nishike Mkono ya D Knob, My baby ya Quick Rocker.

Mchungaji TB Joshua Kushtakiwa na Serekali ya Nigeria Baada ya Jengo Lake Kuanguka na Kuuwa Watu 115

$
0
0
Serekali ya Nigeria Imesema Inaanzisha Uchunguzi wa Kina Kujua sababu za Jengo la Hotel ya Mchungaji TB Joshua Ambapo Waumini wake ufikia lililo anguka Tarehe 12 September na kuuwa zaidi ya watu 115, Source zimesema ikiwa itakuwa ni uzembe wa TB Joshua basi atashitakiwa kutoka na Sheria za Nchi hiyo

Video: Irene Uwoya na Mwigizaji Rich Wapigana Denda Live Live

$
0
0
Kama mpenzi wako ana ndoto za kuwa muigizaji wa filamu za hapa Tanzania, huenda ukabadilisha mawazo yako ukiona video hii ya Irene Uwoya na Single Mtambalike aka Rich wakibadilishana mate kwenye scene ya filamu yao mpya.

Je Unaipenda Facebook ? Mtandao Pinzani Umezinduliwa , Waja kwa Kasi ya Ajabu

$
0
0
Mtandao wa kijamii wa Ello unapokea maombi 31,000 ya watumiaji wanaotaka kujiunga kila saa moja hali ambayo inaibua ushindani mkubwa kwa mtandao wa Facebook.
Muanzilishi wa mtandao huo Paul Budnitz ameiambia BBC kuwa wakati mtandao huo unaazishwa ulilenga watu kuhudumia marafiki 90 tu.
Mtandao huu kwa mjibu wa muanzilishi umeanzishwa August mwaka huu ukiwa ambapo hauna gharama yoyote kwa mtumiaji iwe matangazo ama kulipia data.
Hata hivyo baadhi ya watumiaji wameubatiza kwa jina la Anti-Facebook mtandao huo, wakimaanisha kwamba ndiye mpinzani mkubwa wa Facebook.
Baadhi ya wataalam wa masuala ya kimitandao wamekosoa mfumo wa Ello kutotoza gharama yoyote wakidai kuwa katika siku za usoni huenda mtandao wa Ello utalazimika kutoza kiasi kidogo cha fedha kwa watumiaji wake.
Paul Budnitz mtengenezaji wa baiskel za kampuni ya Vermont ameiambia BBC kuwa wapo imara katika ushindani wa kimitandao na kujigamba kuwa ana wataalamu wa kutosha kukabiliana na makampuni pinzania.
Hata hivyo kuhusiana na baadhi ya watu kuuiita kwa jinala bandia la anti-Facebook mtandao huo yeye amesema wanajiendesha kama mtandao wenye mtazamo wake binafsi na si kutegemea mtazamo wa mtandao wa Facebook.

Kuachana kwa Jason Derulo na Jordin Sparks Kwamfanya Lulu Asiamini ‘Mapenzi’ Tena!

$
0
0
Kama uliumizwa au kushangazwa na kuachana kwa Jason Derulo na Jordin Sparks, basi hauko peke yake.

Elizabeth Michael aka Lulu, ni mmoja wa watu waliomuizwa na kuvunjika kwa uhusiano wa wanamuziki hao wa Marekani ambao kwa wengi walionekana kupenda sana. “Guys u broke my heart too, I dnt believe in love n relations anymore, Ths pipo wr sooo in love…wat happened..!!?,” aliandika Lulu kwenye picha ya wapenzi hao aliyoiweka kwenye Instagram.

Wakati ambapo Jordin Sparks bado hajazungumza chochote kuhusu taarifa za kuachana kwao, muimbaji huyo wa ‘Wiggle’ amezungumza tena kukanusha tetesi kuwa alimsaliti mpenzi wake.

“Though I think it is a private matter and intended to keep my break-up Jordin personal, due to bogus and irresponsible lies being reported by insensitive media outlets it became necessary for me to comment,” Jason aliiambia ABC News Sept. 26.

“I spent three great years with Jordin and she is one of the most amazing people that I have ever met. But as in all relationships there are ups and downs and at this time we have decided to amicably part,” he said, echoing an earlier statement he made on Minneapolis radio station KDWB, claiming that “everything is cool” and that their breakup was not “a bad situation. Infidelity, cheating or deceit played no part in our relationship or our break-up, and I hope that people respect our privacy as we move forward with our lives.”

Pic of The Day: Mwanamuziki Recho Katika Pozi Ofisini

$
0
0
Mwanamuziki Recho Katika Pozi Ofisini, Haikuweza Kufahamika ni Ofisi gani ila Mazingira yanaonesha ni ofisi fulani...Kivazi hicho Jamani Chanimalizaaa

Mkasi TV yamuhoji Gardner G. Habash… Aliyoyaongea ni Pamoja na Haya.

$
0
0
Mtangazaji Gardner G. Habash ni miongoni mwa Watangazaji hodari ambao Tanzania imewahi kuwa nao ambapo alianza kwa kusikika kupitia CloudsFM kwenye shows mbalimbali ikiwemo Jahazi kabla ya kuanza kazi.
Wakati huu ambapo kumekua na stori zilizoenea mtaani kuhusu yeye na ndoa yake pia kazi, show ya TV ya Mkasi inayoongozwa na mtangazaji Salama Jabir imepata nafasi Exclusive ya kuongea nae.
Zifuatazo hapa chini ni baadhi ya sentensi alizoziongea Captain G kwenye Mkasi on EATV.

Kwanza alianza kwa kuongelea jinsi alivyoingia kufanya kazi Redioni huku akimkumbuka Othman Njaidi aliemchukua na kumpeleka CloudsFM sio kama mtangazaji bali akajiunge na timu ya Marketing, akakutanishwa na Ruge Mutahaba aliekua General Manager wakati huo ambae alipoisikia tu lafudhi ya Gardner akasema huyu anafaa kuwa mtangazaji.

Staa aliefurahi baada ya kukutana nae ni D’Banj wa Nigeria, alifurahia uchangamfu wake…
Salama alipomuuliza kuhusu uhodari wake wa kutangaza habari za mastaa wa dunia… Captain G. akasema ‘nilikua nanunua majarida kwenye maduka yanayouza majarida kutoka nje, wakati Internet hamna kulikua na majarida mengi kidogo’

‘Mimi ni mchaga kabisa wa Baba na Mama lakini Wazazi wangu walihamia Tanga zamani alafu mimi nimezaliwa Ngamiani pale Hospitali na tukaishi Chumbageni muda mrefu kwa hiyo nilipata lafudhi ya Tanga pale, na hiyohiyo lafudhi ya Tanga ndio iliyonipa kazi kwenye Radio’

Salama akamuuliza ‘Unajisikiaje ukisikia mtu anatangaza kama wewe‘ >> Gardner akajibu ‘kuna baadhi ya watu kusema ukweli wanachukizwa sana na hicho kitu na wananilalamikia sana kwamba kuna Watangazaji wengi wamekua wanakuiga kwenye kutangaza Redioni na kwenye kutengeneza jingle kama za kwako lakini mimi nimeiona ni baraka kwangu, kama watu wamekupenda kiasi kwamba wanakuiga ni jambo la kufurahisha kwangu mimi linanifurahisha sana’

Kuhusu kitu kilichomfanya akaondoka kwenye Radio, Captain amesema ‘Nilifanya kazi miaka 9 akili ikawa imechoka nikafikiria lazima pia nifanye biashara watu wanakusifia kwamba una uhodari flani kwa hiyo unajipa challenge kwanini nisitengeneze kitu changu, ndio tukafungua biashara za chakula lakini zaidi nilikua nataka kupumzika’

Swali jingine kutoka kwa Salama likawa ‘nasikia kuna stori kwamba hivi karibuni pia unaweza kurudi kule ama ukaenda sehemu nyingine‘ Captain G. akajibu >>> ‘ni mmoja kati ya hao wawili, stori ni ya ukweli ndio maana naondoka, nimemaliza mkataba nimepata ofa nyingine kubwa naichukua’

Swali jingine lililokua linasubiriwa ni hili alilouliza Salama >> ‘kuna stori mtaani kwamba wewe na Lady Jaydee mmeachana’  Gardner akajibu ‘mimi sijawahi kupata interview muda mrefu sana… nadhani hii inaweza kuwa interview yangu ya kwanza, kwahiyo nilikua nataka nikuombe tuongee kuhusu mimi kwanza manake tukizungumzia kuhusu JayDee nitafunikwa hapa’

Hizi Ni Sababu Kuu Tano Kwanini Lowassa Anafaa Kuwa Rais 2015

$
0
0
Maisha ya watanzania yamekua magumu mno,sasa sukari ipo juu ikiwa ardhi na mabonde kama ruvu mtibwa na kageara tunayo, umeme usio wa uhakika wakati gesi ya mtwara na RUBADA, madawa hakuna hospitalini, viongozi wanatuziba masikio kwa vizungumkuti vya ESCROW huku madawati hakuna shuleni, vitendo vya kihalifu vimejaa kila kona watu wakisaka ridhiki kwa nguvu, tumaini la katiba mpya ni kizunguzungu kiasi kutuacha wakiwa Zaidi sisi masikini wakitanzania, huku tukijengewa chuki na serikali na watawala kwa upenyo wakushuka uzalendo na kiasi cha kusema watu kuikimbia nchi kwa vijana ni kawaida kutafuta maisha ughaibuni na kusema hii nchi sasa si ile ya NYERERE bali ni ya watawala makatili mno. Lakini kwa muktadha ule ule wa kidemokrasia ambao hata rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania awamu ya tatu Mh. Benjamin Mkapa aliyasema pale alipo chagiza kabla kuteuliwa Dk Jakaya Kikwete ndani ya CCM kuwa achaguliwe mgombea ambaye vijana na wapiga kura wengi wanamtaka kitu ambacho kilipelekea Dk. Kikwete kushinda kwa kishindo ndani ya chama na hata katika uchaguzi mkuu 2005. Sasa zifuatazo ni sababu ambazo Lowassa atapitishwa kugombea URAIS kwani wanachama na watanzania wanamuhitaji.


1.MRITHI SAHIHI WA MWL. NYERERE KATIKA VITA DHIDI YA UJINGA

Edward Lowassa ni mwana siasa Pekee ambae ndani ya CCM,anaefaham Vission ya Mwalimu Nyerere 1961 Mwalimu alitangaza maadui watatu (1)Ujinga (2)Maradhi (3) Umasikini. Mwalimu katika miaka yake 24 alisimamia swala moja Elimu ya Kujigetemea na baada ya kuondoka mfumo huu uliharibika,Ili kupambana na Adui hao Mwalimu alianzisha Vijiji vya Ujamaa,msingi hapa ili kuongea Uzalishaji,huduma ya afya na Shule, akajenga shule za msingi katika kila kijiji. Mwaka 2005 Edward Lowassa aliamua kufufua upya utekelezaji wa Dira ya Mwalimu nayo ni kuwekeza kwenye Elimu na Kupambana na maadui 3.Alisimamia Ujenzi wa Miundo Mbinu ya Elimu kila kata( sekondari),Kupanua elimu ya Chuo Kikuu, Kusukuma Ujenzi wa vyuo vya kada ya kati (Veta) ili kujenga Kada la kati ya wataalam wa Ufundi mbali mbali, Kupanua Vyuo vya Ualimu ili kuziba pengo la upungufu wa waalim,mambo haya hayana tofauti mapambano alianzisha Mwl Nyerere baada ya uhuru kupambana na maadui watatu. Elimu imekua Agenda kuu ya Edward lowassa,Anaamini katika hilo Jambo kuwa msingi wa kupambana na Umasikini,Elimu itasaidia Uzalishaji,Elimu Itapambana na Maradhi,Elimu Itaondoa Ujinga miongoni mwa Jamii yetu, hii ni sababu pekee itakayo ifanya CCM kumpitisha kurudisha taswira ya chama.


2. MAAMUZI MAGUMU NA MAKINI KATIKA UONGOZI

Kwa kipindi kirefu sasa ndani ya nchi yetu tuna tatizo la maamuzi katika utekelezaji wa sera za serikali, viongozi wamekuwa wazito mno kutekeleza makubaliano ya vikao vyao wakiogopana au hata rushwa kutawala miongoni mwao hivyo kushindwa kutekeleza maamuzi hayo. Edward Lowassa ni kiongozi ambaye kwa kipindi chake alicho kuwa madarakani ameonyesha kuwa si kigeugeu kwa maana ya kwamba mara zote ambazo baraza la mawaziri katika vikao vyake vya ndani walipo fika makubaliano yeye alitekeleza, Utekelezaji wa ujenzi wa chuo kikuu Dodoma. Taarifa za ndani za viongozi zilionyesha ugumu mno wa utekelezaji wa sera hii ya chama, Lowassa ilifikia hatua kuwaeleza viongozi mbalimbali waandamizi katika ngazi za maamuzi na utekelezaji kama yeyote anaona ujenzi wa chuo kile hauwezekani aandike barua ya kujiuzulu na akabidhi kwake ampatie Rais Dk.Jakaya Kikwete, kitu ambacho kiliongeza ujasiri wa utekelezaji wa sera na sasa tunaona watoto wa masikini wakipata elimu. Alivunja mkataba wa city water, mkataba ambao ulifanya serikali kushtakiwa lakini na hata kuleta nafuu katika upatikanaji wa majia ndani ya jiji la dar es salaam pia bila kusahau alivunja mkataba wa kimataifa katika usambazaji wa maji kanda ya ziwa kitu kilicho mfanya mpaka aogepeke na jumuia za kimataifa akiwa anatetea haki ya Mtazania kwa hakika ni mzalendo na mtu pekee ndani ya CCM hii ya DK. Jakaya na Kinana anaefaa kuipeleka dira ya taifa mbele.

3. MPAMBANAJI ALIAZIMIA KUFUTA UMASIKINI

Lowassa ni Mwana siasa Pekee ndani ya CCM ambae Anaamini UMASIKINI si sifaa bora kwa Mtanzania kujisifia,Umasikini si Sifa ya Kiongozi,Umasikini unaendana na udhalilishaji na Ujinga na Maradhi,ni mwana Siasa pekee ambae hasifiii umasikini kwani ni vita katika vita kuu za taifa hili tangu tunapata uhuru. Hii imekuwa hulka ya viongozi kadhaa hasa wabunge wetu hutuhadaa wakisema tuwape ridhaa ya kutuongoza kwa sababu wao ni masikini wenzetu, siasa sasa ya leo na kimataifa imebadilika mno tukiangalia mataifa makubwa hata madogo , viongozi ni wale wenye majibu sahihi katika kuufuta umasikini na si kujisifia kuwa wewe ni masikini tukupe ridhaa tena ridhaa ambayo utahakikisha kujinufaisha wewe na famia yako kwanza, na CCM sasa inataka kujenga uchumi imara uchumi ambao utafuta umasikini kwa kumpa Mtanzania Elimu, kuimarisha miundombinu na kufungua biashara tujifunze haya toka Kenya waungwana.Pia ni miongoni mwa sababu zinazo wavutia wana CCM kumpa ridhaa ya kupeperusha bendera.

4.ANAPENDWA NA WATANZANIA WOTE NA WANAMUHITAJI

Ni mtu ambaye ana mvuto mkubwa kwa watanzania na ana sifa ya kuwa muadilifu, mtendaji mzuri, mbunifu, huheshimu mawazo ya wengine, anaijua Tanzania, Mfuatiliaji wa kazi, anatabia ya kuwapa watu matumaini Mpambanaji (fighter) na anaheshimika kikanda na kimataifa. Ni Mtanzania pekee anayependwa na kukubalika Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar ndani na nje ya chama chake. Ni mtu ambaye ana Aura ya aina yake na huleta matumaini unapokaa naye na kusikiliza.Ni kweli kabisa..Edward Lowassa (is the chosen one) kaatika uhai wa siasa ya chama chochote inatakiwa kuwa na gombea anaye uzika, anayekubalika na ambaye ni tumaini la mahitaji wananchi husika, Lowassa amekidhi vigezo vyote na hakika anafaa ndani ya CCM na ndio chaguo sahihi kama chama kinahitaji uhai wa muda mrefu.

5.KIONGOZI ALIYEPITIA MENGI NA ANAYEIJUA NCHI.

Lowassa ni kiongozi alie pitia mengi kama rais wa awamu ya pili alhajj Ali Hassan Mwinyi kufikia hatua ya kujiuzulu na kuwajibika kama kiongozi ambaye anjua fika maadili ya kiongozi wa umma, Lowassa amengia katika mfumo wa chama na serikali tangu mwaka 1977 ambapo imepita miaka Zaidi ya 30 akipambana na shida na mahitaji ya watanzania, mwenyekujua nini Watanzania wanahitaji, mtu ambaye amepitia mengi na kuwa na ufahamu wa kutosha wa serikali na chama chake kiasi cha kufanya kuwa kiongozi pekee kwa sasa anayekijua chama na serikali. Chama cha Mapinduzi kimekosa mtu mwenye sifa hizi mtu ambaye amepitia mikiki mikiki ya kina katika kuwatetea wananchi, kiongozi ambaye amepambana mpaka na mahafidhina ndani ya chama na kiongozi ambae si rahisi kumpelekesha, kiongozi huyu ameweza kuwa adui mkubwa wa mahafidhina kwa sababu hana si ya woga dhidi yao, hawafumbii macho na naweza sema huyu ni kama TAKUKURU kwa mahafidhina sababu hafumbii macho machafu.

MWISHO.
Watanzania tunahitaji kiongozi ambae atakuwa mrithi sahihi wa serikali ya awamu ya tatu, mtu ambae atatuongoza katika kukabiliana na mahitaji yetu yaani nini watu wa namanyere, uvinza nantumbo na Tanzania kwa ujumla nini wanataka, Mtu ambaye atakuwa msikivu na mpambanaji wa mahitaji yetu , nashauri wote kwa pamoja tuwajadili watu wanaoweza kuiongoza nchi yetu bila kejeli, matusi au woga na aina yeyote ya kufumbia macho machafu , kuukuza uzalendo ni pamoja na kuukana woga wa kivuli chako. MUNGU IBARIKI TANZANIA.
Viewing all 104698 articles
Browse latest View live




Latest Images