Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104690 articles
Browse latest View live

Dawa Bora za Nguvu za Kiume na Kukosa Hamu ya Tendo la Ndoa

$
0
0
Baada ya utafiti wa muda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka sasa

MWASELE HERBAL CLINIC. inakuletea suluhu juu ya matatizo haya kwa kutumia dawa za

FULL POWER .ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu zakiume. dawa hii ina mchanganyiko wa kutosha kuzalisha vichocheo vingi vya hormone za gestrogen ziwemo vitamin B6&B1, vitamini E pamoja madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na muzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi na kuchelewa kufika kileleni zaidi ya dakika 20-30. ZAT 50 inarudisha maumbile ya uume yaani kurefusha na kunenepesha ulefu nchi 3-7, upana cm, 3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukitumia maumbile yatabaki kuwa hivyo siku zote . pia tunatibu matatizo mengine kama presha, kisukari , ngiri ,chango la tumbo,tumbo kujaa gesi, kutokupata choo vizuri,miguu kuwaka moto,matatizo ya uzazi, bawasili namagonjwa yazinaa kama kisonono nakaswende.

Tunapatikana DAR ES SALAAM. SHINYANGA NA ZANZIBAR. kwa wakazi wa dar es salaam utaletewa huduma hii popote ulipo . wa mikoani tunawatumia kwanjia ya mabasi .

Hivi Ndivyo Milioni 9 Zilivyomfanya Gigy Money Kumkimbia Mwanaye

$
0
0
Hivi Ndivyo Milioni 9 Zilivyomfanya Gigy Money Kumkimbia Mwanaye
Msanii wa muziki wa Bongo Flava na video vixen, Gigy Money amesema kutokana na utafutaji mara nyingi analazimika kutengana na mwanae.

Muimbaji huyo katika mahojiano na XXL ya Clouds Fm amesema ni vigumu yeye kulala nyumbani wakati hana fedha.

“Nilienda Nairobi nikakaa mwezi mzima na nilimuacha mtoto na mama yangu, hakuna mtu anaweza kuacha dola 4,000 (sawa Tsh. Milioni 9) kirahisi,” amesema Gigy Money.

Ameendelea kwa kusema analazimika kufanya hivyo kutokana anategemewa na familia yake. Gigy Money ni mama wa mtoto mmoja wa kike itwaye Mayra.

Rais Magufuli Amteua Jenerali Davis Mwamnyange Kuwa Mwenyekiti wa Bodi DAWASA

$
0
0
Rais Magufuli Amteua Jenerali Davis Mwamnyange Kuwa Mwenyekiti wa Bodi DAWASA
Rais John Pombe Magufuli amemteua Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Mstaafu, Jenerali Davis Mwamunyange kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira (DAWASA).

RC Makonda Asitisha Usafi Kila Jumamosi

$
0
0
RC Makonda Asitisha Usafi Kila Jumamosi
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda leo ametangaza rasmi kuondolewa kwa  kipengele kilichokuwa kikiwataka wafanyabiashara kufunga maduka siku Jumamosi hadi Saa nne asubuhi kwaajili ya usafi na badala yake jukumu amelikabidhi kwa zaidi ya Vijana 4,000 wa JKT.


Makonda ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na Vijana wa JKT na Mgambo, waliojitokeza katika usaili wa kuajiriwa ili kusimamia zoezi la usafi na kuhakikisha wanawawajibisha wanaochafua mazingira jijini, huku wafanyabiashara wakifungua maduka yao kama kawaida.

“ Wafanyabiashara kufunga maduka yao siku ya Jumamosi hadi Saa nne asubuhi, hilo halitakuwepo tena na badala yake nawakabidhi jukumu hilo na atakayekaidi zoezi la Usafi na kutupa taka ovyo akamatwe maramoja”, amesema Makonda.

Aidha Makonda amesema vijana hao watakuwa na jukumu la Kusimamia kampuni zilizopewa kazi ya Usafi kwenye maeneo husika, Kuwakamata, kuwatoza faini watupaji wa taka pamoja na kufuatilia kujua kila nyumba inapeleka wapi taka wanazozalisha ambapo ifikapo Jumanne ya Julai 10 itakuwa ndio mwisho wa usajili wa vijana hao.

Sajenti Aeleza Machungu Aliyonayo kwa Mtoto Patrick

$
0
0
Sajenti Aeleza Machungu Aliyonayo kwa Mtoto Patrick
STAA wa filamu kutoka Bongo Movie, Husna Idd ‘Sajenti’ ameeleza machungu yake kwa aliyekuwa mtoto wa msanii mwenzake ambaye ni rafiki yake wa karibu, Rose Alphonce, marehemu Patrick na kusema kuwa amemuachia kovu kubwa.



Akizungumza na Ijumaa, Sajenti alisema kuwa, Patrick enzi za uhai wake alikuwa ni rafiki mkubwa wa watoto wake na walikuwa wamezoeana sana hivyo alivyopata taarifa za kifo chake aliumia na hakuamini kwa kile kilichotokea kwa sababu ni mtoto aliyekuwa akimpenda na hata watoto wake walimzoea.



“Nilivyopata taarifa za kifo cha Patrick kwa kweli niliumia sana, nilijaribu kujiangalia nilivyomzoea nikajikuta huzuni kubwa ikinitawala, sikuweza kulala kabisa, kutwa nikilia kwa uchungu kwa sababu tu nilivyokuwa nimemzoea Patrick na hata watoto wangu,” alisema Sajenti.


Akiendelea kuzungumza na Ijumaa Sajenti, alisema kuwa Patrick amemuachia kovu kubwa ambalo haliwezi kupona milele anachofanya sasa hivi ni kumuomba Mungu, ampe subira mpaka atakapompokea mtoto huyo (jana au leo).



“ Hapa namuomba Mungu tu, anipe ujasiri niweze kupata nguvu ya kupokea mwili wake niamini kabisa hayupo nasi maana nina kovu kubwa ambalo haliwezi kukauka kwenye moyo wangu,” alisema Sajenti kwa masikitiko.



Mtoto Patrick alifariki Jumanne iliyopita jijini Nairobi alipokuwa amepelekwa na mama yake huyo kwa ajili ya kufanyiwa matatibu baada ya kugundulika kuwa na uvimbe kwenye ubongo.

Tozo za Basata Zamshangaza Nikki wa Pili

$
0
0
Tozo za Basata Zamshangaza Nikki wa Pili
Rapa Nikki wa Pili ameshangazwa na tozo za ada ambazo yanachajiwa Makampuni pale yanapotaka kufanya kazi na  wasanii wa muziki nchini Tanzania.


Nikki wa Pili kupitia ukurasa wake wa Twitter amesema kuwa tozo watakayolipa Makampuni itakuwa ni kilio kwa wasanii kwani hakuna kampuni itakayokubali kulipa shilingi milioni 5 kwa kufanya kazi  na wasanii.

“Matangazo yapo ya aina nyingi, kampuni inaweza mtumia msanii kuposti tangazo lao katika page yake, waka mlipa kwa post moja au mbili, sasa ukisema hapo kampuni ilipe basata milioni 5?? sasa kwani kwa post moja msanii hulipwa bei gani, kifupi hapo hizo dili zitakufa,“ameandika Nikki wa Pili.

Mnamo Julai 04, 2018 Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) Lilitangaza kuwa Makampuni yatakayotumia wasanii au sanaa kujitangaza (Branding) yatatozwa gharama ya shilingi laki 5 huku matangazo yatakayotumia wasanii kila tangazo/tukio litatozwa shilingi milioni 5.

Brazil Yaondolewa Kombe la Dunia kwa Kufungwa 2-1

$
0
0
Brazil Yaondolewa Kombe la Dunia kwa Kufungwa 2-1
USIKU wa  leo Ubelgiji imewashangza wadau wengi wa soka baada ya kutinga nusu fanali ya michuano ya Kombe la Dunia kwa kuiondosha Brazil kwa kuifunga mabao 2-1.


Ubelgiji ambayo ilikuwa haipewi nafasi kubwa ya kushinda mchezo huo, ilifanya maajabu hayo kwenye Uwanja wa Kazan mjini Moscow nchini Urusi. Kutokana na ushind huo, sasa Ubelgiji itakutana na Ufaransa waliowaondosha Uruguay kwa mabao 2-0 katika mchezo wa mapema wa robo fainali.


Mchezo wao wa nusu fainali utapigwa Julai 10, mwaka huu kwenye Uwanja wa St Petersburg. Mchezo kati ya Brazil na Ubelgiji ulianza kwa kila timu kumvizia mwenzake, lakini walikuwa Ubelgiji walioandika bao la kwanza kupitia kwa beki Mbrazili, Fernandinho aliyejifunga dakika ya 13 wakati akiwa katika harakati za kuokoa mpira wa kona.




Baada ya bao hilo kuingia, Brazil walikuja juu na kusaka bao la kusawazisha, lakini walijikuta wakipata tabu sana baada ya kufungwa la pili dakika ya 31 kupitia kwa staa wa Klabu ya Manchester City, Kevin de Bruyne kwa shuti kali akiwa nje kidogo ya 18 baada ya kupokea pasi murua kutoka kwa straika, Romelu Lukaku aliyewachekecha walinzi wa timu pinzani.



Bao hilo ni kama liliwaamsha usingizini Brazil kwani walipeleka mashambulizi makali langoni mwa Ubelgiji lakini umakini mdogo wa wachezaji wake kama Neymar, Phillipe Coutinho na wengineo
ulisababisha wajikute wanamaliza kipindi cha kwanza wakiwa nyuma kwa mabao 2-0.


Kocha wa Brazil, Tite alifanya mabadiliko kadhaa kikosini mwake ikiwemo ya kumtoa Willian na nafasi yake ikachukuliwa na Firmino, huku Renato Augusto akiingia badala ya Paulinho. Baada ya mabadiliko hayo, Brazil walikuja juu na kufanikiwa kupata bao la kwanza kupitia kwa Augusto dakika ya 76 akiunganisha kwa kichwa krosi iliyochongwa na Coutinho ambaye alikosa mabao mengi jana usiku.

Brazil itabidi wajilaumu wenyewe kwani walikosa mabao mengi ya wazi na kama wangekuwa makini basi wangepata ushindi mkubwa katika mchezo huo. Ubelgiji sasa itapambana na Ufaransa Julai 10 katika mchezo wa nusu fainali na mara ya mwisho timu hizo zilikutana mwaka 2015 katika mchezo wa kirafi ki ambapo Ubelgiji ilishinda mabao 4-3. Mafanikio ya mwisho kwa Ufaransa kwenye Kombe la Dunia ni kumaliza nafasi ya pili mwaka 2006 na Ubelgiji ni kutinga hatua ya robo fainali mwaka 2014.

Hivi Ndivyo Mapenzi Yalivyomnyoosha Amber Lulu

$
0
0
Hivi Ndivyo Mapenzi Yalivyomnyoosha Amber Lulu
MWANADADA kwenye gemu la Muziki wa Bongo Fleva ambaye pia ni muuza sura kwenye video za Kibongo, Lulu Euggen ‘Amber Lulu’, amesema kuwa mapenzi yamemnyoosha na kwa sasa ameamua kujiweka kando.



Amber, aliyewahi kuwa kwenye uhusiano na mastaa mbalimbali akiwemo staa wa muziki kutoka Kenya, Jackson Makini ‘ Prezzo’, alisema kuwa, amekuwa kwenye mahusiano mengi, lakini anaona ni kama anapoteza tu muda.



“Mapenzi yameninyoosha bora niyapige chini maana wanaume wengi wananipenda kwa sababu ya umaarufu wangu, lakini unakuta hawana mapenzi ya kweli kwangu. Ninaona tu huko ninapoteza muda na kuambulia maumivu, kwa hiyo bora nijiweke wazi tu, hakuna namna,” alimaliza

Ndoa ya Zabibu Kiba na Abdi Banda Yanukia

$
0
0

KAPO’ inayoonekana kuwavutia wengi mtandaoni ya mwanasoka Abdi Banda na dada wa staa mkubwa wa muziki Bongo, Ally Salehe Kiba ‘Alikiba’, Zabibu Kiba imekuwa gumzo baada kuonekana dalili kuwa, wawili hao wataoana mwezi Agosti, 2018.



Gumzo hilo limekuja baada ya Banda anayeichezea Timu ya Baroka FC ya Afrika Kusini kumposti mchumba wake huyo kwenye ukurasa wake wa Instagram kisha akaandika hivi; “Maamuzi sahihi, Get ready AUGUST. Unapenda tarehe gani?



Kufuatia swali hilo, wadau wengi waliamini Banda anaizungumzia ndoa yao hivyo wengi wakamshauri tarehe ya kufanya tukio hilo huku wengine wakiishia kuwaombea kila la heri ndoto yao ya kuwa mwili mmoja itimie.



“Mimi siku yoyote mtakayofunga ndoa ni poa ila iwe haraka jamani, naipenda sana kapo yenu,” aliandika mdau mmoja aliyejiita Kissbway.

Zabibu alipotafutwa kuzungumzia tarehe ya ndoa yake alisema, bado hawajapanga ila watu wanaweza kuendelea kupendekeza tu.

Najifunza Mengi Kupitia Kwenye Msiba wa Mtoto Huyu Patrick

$
0
0
Niseme machache kama wasiawangu kwa Jamii, Iyeleweke kua msiba hauzoeleki katika maisha ya kilimwengu, Ispokua msiba niwakujifunza kupitia kwa mwenzio, kama wasemavyo waswahili
MWENZIO AKINYOLEWA Basi nawe jiandae kwa kukosha nywele zako, Tunaiyamini sana misemo kwani huwendana nawakati,
NAOMBA NIREJEE PANAPO KUSUDIO LANGU

Dhumuni kuu nikujifunza bado angali tukiwa hai, Ukiwa kama Mzazi Baba Mama, Ama familia kwa ujumla tuna tambua uhai wa mwanadamu namwadamu hutambua uwepo wake katika Dunia, Wazazi huonyesha thamani ya mwana tangu yupo tumboni hadi kuzaliwa kwake, mama nababa huyang'aza macho yao kwa furaha kwa pendo jipya lamtoto, Huanza kuonyesha thamani yautoto kwamaanaya maadili Elimu zote mbili Pamoja na maradhi pindi mwana augupo, Jicho lathamani kwawazazi huwaza kua na papara nakupatwa nasinto fahamu yakujiuliza mengi kua nikipi kimemkuta kijanawao au binti yao, Hatimae huangaika hadi mungu kuurejesha uzima wake, hapo wazazi hurejesha furaha za myiyoyao nakuanza upya maisha.

UGOMVI
Wazazi wanapo gombana haimaniishi namtoto kagombana nawazazi, Iyeleweke kua mtoto hujifunza kityu kupitia ugomvi wawazazi, Natumaini kuzungumza hvyo inatosha kwakua naeleweka vyema,

MSIBA WA PATRIK
Najifunza sana kwamaranyengine pindi itokeapo misiba ya dizain kama hii, Iweje wazazi amandugu mlete mkanganyiko wa sinto faham ingali mwana Ashafariki, Hivi mnafahamu uchungu wakifo naje mwatambua hukumu yakuchelewa kuzika navipi hizi vuta nikuvute zatukazikie wapi, Ikiwa atazikwa mwananyamala atafukiwa katika shimo Akizikwa Kinondoni bado nishimoni masaki bado nishimoni Hata akizikwa Ulaya bado nishimotu litachimbwa na atazikwatu. Malumbano wekeni pembeni kamhifadhini huyu kija mkirudi kila bondia achukue nafasi yakurusha ngumi ama maneno, Vijembe havisaidii kwa wakati mgumu kama huu, Mama Patrik yatakiwa umpe thamani mumeo nasio kumjazia nzi kwakilamtu aone kane mbaya, Anahaki yamsingi kama baba,Na kuuchukua mwili nakwenda kuzika Nawe pia kadhalika, Lakin mwanamke unadaraja dogo sana juu yahili, Sawa basi mtueleze Patrik atazikwa ama hazikwi ili sisi majiranizetu ambao niwaajiliwa vibaruwa na wajasiliamali tujuwe moja, kama nikuwaacha mtazikawenyewe sawa kulikoni bumbuwazi lamacho, Kwani mtoto kakosa nini? au mlikua natatizo nae wakati yupo hai, Hivi tukimuamsha Patrik akikuta huu mvutano wenu hayo macho yenu mtayafumba kwa mtindo upi au mtamuomba vip radhi naje? kwa udhalili huo atatambuaje kama nyinyi niwazazi wake, Yaan kutoka Dar hadi Nairobi Kenya kwaku muuguza naleo anarudi Dar akiwa ni marehemu, Lakini bado kuna mkanganyiko mara marehemu ameletwa yupo uwanja wandege mara mama katangulia mtoto kababi kenya mara kapelekwa kanisani wazazi Fungeni mikaja Acheni vijembe, Baba funga msuli mama fuka kaniki muelekeo kuzika Kimaisha hayo simaadili mema, maana tuna watoto wetu pia wanajifunza kupitia msiba huu kwa kufatilia Taarifa mbali mbali kwenye vyombo vya habari kupitia mvutano wa msiba wakijana Patrik, Binafsi nimeulizwa na mtoto wangu Maswali haya.

KWANI BABA PATRIK ALIKUA NANI
NAMAMAYAKE ALIKUA NANI
NAKWANINI HAJAZIKWA
NAMBONA ANAJULIKANA SANA?
NABABAYAKE NINANI KWANI?

NILIMJIBU NNAVYO FAHAMU MIMI
Mwanangu nnavyo mfahamu patrik nimemfahamu kupitia kwenye mitandao Wala sijawahi kumuona, Nilikua namskia kupitia Radio nyingi kwenye vipindi vya dini yake navipindi vya watoto akishirikiana na wanafunzie wenzie na mengine mengi, Ama kuhusu mamayake Nimuigizaji hapa nchini kwetu, Hakuzikwa kutokana na mkanganyiko wa familia ya wazazi wake wote wawili, Ila atazikwa leo, Ndio anajulikana Msiba nitukio linalo unganisha watu wasio juana kuja kujuana kwani wote wanao shiriki sindugu wapo watu tofauti, Mfano Kuna wanao tafuta majina kupitia misiba kuna wanao jifanya wanamjua sana marehemu nawengine hujitokeza nakujifanya wanamdai marehemu bila kujua aliekufa ni mtumzima au mtoto, Hiyo ndio maana halisi ya msiba mwanangu, Hapa kwenye swala la baba yake sina jibu Msiri mkuu ni mamayake pekee kwani hata mimi huwenda nikawa sio baba yako siri yote yamaisha yako anaijua mama yako, Akataka kuuliza swali jengine nikamnasa kofi kisha ni kamtimua kwakua alipo kua akielekea si mahala pake,

Mwisho wazazi wa Patrik huyo nimwenenu muoneeni huruma ili akapumzike kwamaana kaumwa anahitaji pumziko lenye busara litakalo mfanya akutane na mola wake Why? mnamchelewesha?

Mwisho sina lakusema zaid nikusema
MOLA AILAZE NAFSIHII KATIKA MAZINGIRA SALAMA KWAPAMOJA TUITIKIE AAAAAAMIIIIIN

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

$
0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

Masikini! Muna Azidiwa Ghafla Alazwa Hospitali ya Agha Khani

$
0
0
Muna Azidiwa Ghafla Alazwa Hospitali ya Agha Khani
Mama mzazi wa marehemu Patrick, Muna Love asubuhi ya leo amelazwa ghafla katika hospitali ya Agha Khani kwa kuzidiwa na homa kali hii ni baada ya mwili wa mtoto wake kutolewa hospitalini hapo.

Tazama matukio mawili ya jinsi mwili wa Patrick ulivyotolewa Agha Khani hadi nyumbani kwa baba yake mzazi Mwananyamala kwa ajili ya kuuaga mwili wa mtoto Patrick.

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

$
0
0

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume, nasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

Yanga Yajipanga Kumpokea , Yusuf Manji

$
0
0
Yanga Yajipanga Kumpokea , Yusuf Manji WENYEVITI wa matawi ya Yanga kesho Jumapili watakutana na uongozi wa kwa ajili ya kupanga mikakati ya jinsi ya kumpokea aliyekuwa mwenyekiti wa klabu hiyo, Yusuf Manji ambaye anatarajiwa kurudi kuendelea kuiongoza klabu hiyo.



Mei 23, mwaka jana, Manji aliyeleta mapinduzi Yanga na kuifanya timu hiyo ishiriki hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika, alitangaza kuachia ngazi ya uongozi ndani ya timu hiyo kutokana na kukabiliwa na matatizo mbalimbali yakiwemo ya kiafya.



Hivi karibuni wanachama hao kwa pamoja katika mkutano wao mkuu waligoma kuridhia uamuzi huo wa Manji wa kujiuzulu na kudai kuwa bado wanamtambua kama mwenyekiti wao mpaka mwaka 2020 ambapo muda wake wa uongozi utamalizika hivyo wakautaka uongozi wa klabu hiyo kumpatia taarifa juu ya maamuzi yao hayo.



Habari za kuaminika kutoka ndani ya Yanga ni kwamba, baada ya uongozi kupokea majibu kutoka kwa Manji kuhusiana na maamuzi ya wanachama wa klabu hiyo kugomea kujiuzulu umepanga kufanya mkutano wa kujadili kwenye makao makuu ya klabu hiyo yaliyopo Mtaa wa Twiga na Jangwani jijini Dar.



“Hivi karibuni tumepokea ujumbe wa mwenyekiti wetu Manji kutokana na barua tuliyompelekea kuhusiana na maamuzi ya mkutano mkuu uliofanyika hivi karibuni ambapo wanachama wote waligomea suala la kujiuzulu kwake.



“Ujumbe huo ni mzuri na umefufua matumaini yetu yaliyokuwa yamepotea hapo awali, kwa hiyo Jumapili tutakutana na viongozi wa matawi kwa ajili ya kupanga mikakati ya jinsi ya kumpokea upya kiongozi wetu huyo,” kilisema chanzo cha habari.



Alipotafutwa Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Mkwasa ili aweze kuzungumzia hilo hakupatikana lakini ofisa habari wa klabu hiyo, Dismas Ten alithibitisha kuwepo kwa mkutano huo huku akidai hafahamu unahusu nini.

Meya Awaajili Warembo Katika Kitengo cha Usalama Barabarani Huku Akiwataka Wavae Nguo Fupi

$
0
0
Meya Awaajili Warembo Katika Kitengo cha Usalama Barabarani Huku Akiwataka Wavae Nguo FupiMeya wa mji wa Broummana nchini Lebanon Pierre Achkar amewaajili warembo wa vyuo vikuu katika kitengo cha maafisa usalama barabarani huku akiwapa mashariti ya kuzingatia.


Mabinti wa vyuo waliojiliwa na Jeshi la Polisi nchini Lebanon.

Pierre ametoa nafasi hiyo kwa mabinti wa vyuo vikuu kuajiliwa ili kufanya kazi na maafisa usalama barabarani huku akiwataka kuvaa nguo fupi kwa kile alichodai kuwa ni sehemu ya kuvutia vyombo vya habari, ndani na nje ya nchi.

"Sababu kubwa ya kuajili mabinti hawa ni kuongeza mvuto katika maeneo yetu ya mji na kuvutia vyombo vya habari ambapo tutapata namba kubwa ya watalii na kukuza uchumi wa nchi yetu”, amesema Pierre.

Hili ni agizo la pili kutoka kwa Pierre baada ya siku chache zilizopita kutoa agizo kwa walimu wa mazoezi ya viungo kufundisha mabinti pembezoni mwa barabara mjini Broummana ili kuwavutia watalii.

Waziri wa Afya Aionya TFDA "TFDA Isiwe Kikwazo Katika Juhudi za Rais Magufuli”

$
0
0
Waziri wa Afya Aionya TFDA "TFDA Isiwe Kikwazo Katika Juhudi za Rais Magufuli”
Waziri wa Afya, Maendelao ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amekabithi vyeti vya ithibati kwa kiwango vha kimataifa ambapo ameitaka Mamlaka hiyo kutokuwa kikwazo kwa wawekezaji nchini hususan viwanda vya kuzalisha dawa.

Hayo yamezungumzwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakati wa kukabidhi vyeti vya ithibati kwa kiwango cha kimataifa ISO 17025 kwa maabara ya chakula na maikrobailojia za TFDA.

“TFDA isiwe kikwazo kwa wawekezaji nchini hususan viwanda vya kuzalisha dawa ili kuunga mkono juhudi za Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli ya kuelekea uchumi wa viwanda.” amesema Waziri Ummy

“TFDA mnawajibu wa kuwawezesha wafanyabiashara kutoa bidhaa zao wanazozileta nchini mapema zaidi mara wanapokuwa wamejiridhisha na ubora unaokidhi afya za watanzania na kuwapa vibali mapema”, amesema Ummy.

TCRA yaagizwa kuzishughulikia kampuni za ving’amuzi

$
0
0
TCRA yaagizwa kuzishughulikia kampuni za ving’amuzi
Mamlaka ya mawasiliano nchini (TCRA) imetakiwa kuzichukulia hatua kampuni za ving'amuzi ambazo zinakiuka leseni kwa kuzuia matangazo ya chaneli za bure.

Agizo hilo limetolewa jana Julai 6 na Naibu Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi   Mhandisi Atashasta Nditiye wakati kamati ya bunge ya miundombinu ilipotembelea (TCRA).

Mhandisi Nditiye amesema serikali haitazifumbia macho kampuni zinazoleta michezo ya kijanja wakati zinafahamu fika maelekezo ya leseni zao.

"Hakuna kufumbia macho, kama kuna mtu nyumbani kwake hajalipia king'amuzi halafu amekatiwa chaneli za bure asisite atoe taarifa na hatua zichukuliwe haraka,"

Amesema kampuni za Star times, Digitek, Ting na Continental zinatakiwa kurusha bure chaneli tano za hapa nchini ili kuwapa fursa wananchi kupata taarifa. Chaneli hizo ni TBC, ITV, Channel ten, EATV na Star TV.

Nditiye pia ameziagiza kampuni za simu kuzingatia usajili wa laini kwa kutumia teknolojia ya biometriki ambayo inahusisha uchukuaji wa alama za vidole na picha ya mtumiaji wa namba husika.

Amesema mfumo huo wa usajili una lengo la kuhakikisha namba moja ya simu inatumiwa na mtu mmoja hivyo itasaidia kukabiliana na vitendo vya matumizi mabaya ya mawasiliano.

"Niwaambie watanzania kuwa changamoto ya watu kutumia vibaya laini za simu limeshapatiwa ufumbuzi na linakwenda kumalizika kabisa muda si mrefu kutokana na mfumo huu,”

“Sasa mtu akisajili namba lazima zichukuliwe alama za vidole na picha apigwe ili tujue kabisa namba fulani inatumiwa na nani,”

Kuhusu utapeli unaofanywa na wanaotuma meseji za kuelekeza fedha itumwe amesema tatizo hilo limeshatatuliwa.

Waziri wa Zamani wa Pakistani Ahukumiwa Miaka 10 Jela

$
0
0
Waziri wa Zamani  wa Pakistani Ahukumiwa Miaka 10 Jela
Mahakama nchini Pakistani imemhukumu aliyekuwa waziri mkuu wa nchi hiyo Nawaz Sharif kifungo cha miaka 10 gerezani kwa makosa ufisadi unaohusu majengo manne ya kifahari jijini London.



Nawaz Sharif,ambaye kwa sasa yuko London alihukumiwa akiwa hayuko mahakamani, na mwenyewe alisema kuwa hukumu hiyo ina mlengo wa kisiasa.

Jaji Mohammad Bashir amemtaka Sharif kutumikia kifungo cha miaka 10 kwa kosa la kumiliki mali yenye gharama kubwa kuliko kipato chake na mwaka mmoja kwa kutotoa ushirikiano na mamlaka inayopambana na vitendo vya rushwa, NAB.

Binti yake, Maryam Nawazi Sharif amehukumiwa kifungo cha miaka saba kwa kushirikiana na babaye kwenye uhalifu huo na mwaka mmoja kwa kutotoa ushirikiano kwa mamlaka za kiuchunguzi huku mkwewe Nawaz akihukumiwa kifungo cha mwaka mmoja kwa kutotoa ushirikiano.

Sharif na Maryam wametozwa faini ya pauni milioni 8 na pauni milioni mbili.Kwa sasa wote wako jijini London ambapo mke wa Sharif, Kulsoom Nawaz anapata matibabu kutokana na maradhi ya saratani.

Panama Papers zilizovuja mwaka 2015 zilitoa taarifa kuwa watoto kadhaa wa Sharif walikuwa na mahusiano na makampuni yaliyo nje, ambayo yalidaiwa kupitisha fedha kwa ajili ya kununua mali nje ikiwemo majengo ya anasa jijini London

Familia yake, hatahivyo, inasisitiza kuwa wanamilimiliki mali hizo kihalali. Katika sehemu ya hukumu, Mahakama imetaka mali hizo zitaifishwe kwa serikali.

Waandishi wa habari nchini Pakistani walikita kambi nje ya makazi ya Avenfield, ambako familia ilikuwa ikitazama kesi.

Simba Yasaka Mbadala wa WAWA

$
0
0
Simba Yasaka Mbadala wa WAWA
Simba ni kama imeshtukia vile ni baada ya benchi la ufundi la timu hiyo kuuomba uongozi umsajili beki mwingine wa kati mwenye uzoefu na uwezo mkubwa kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa Ligi Kuu Bara.

Timu hiyo chini ya mfadhili wake bilionea, Mohamed Dewji ‘Mo’, inataka kusajili beki mwingine ikiwa ni siku chache tangu imlete Muivory Coast, Pascal Serge Wawa anayeichezea timu hiyo katika michuano ya Kombe la Kagame.

Kwa mujibu wa gazeti la Championi, limeeleza kuwa timu hiyo huenda ikamshusha beki mwingine kutoka Ghana au Nigeria ambapo punde atakapotua tu atasaini mkataba moja kwa moja baada ya kujiridhisha.

Kwa mujibu wa chanzo cha habari kutoka ndani ya benchi la ufundi la timu hiyo, uongozi wa timu hiyo bado haujaridhishwa na safu yao ya ulinzi na haraka umechukua maamuzi ya kusajili beki mwingine mmoja wa kati kabla ya dirisha kufungwa Julai 26, mwaka huu.

Chanzo hicho kilisema, uongozi umejiridhisha hilo katika michuano ya Kombe la Kagame inayoendelea kwenye Uwanja wa Taifa, Uhuru na Azam Complex jijini Dar es Salaam.

“Benchi la ufundi limebaini upungufu kwenye safu ya ulinzi, hivyo ni lazima tusajili beki mwingine wa kati mwenye uzoefu na uwezo mkubwa kabla ya usajili wa ligi kufungwa.

“Kama unavyofahamu sisi Simba malengo yetu siyo ubingwa wa ligi pekee, tunataka kuona timu yetu ikifika mbali kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika tutakayoshiriki, mwaka huu mwishoni,” kilisema chanzo hicho.


Alipotafutwa kaimu kocha mkuu wa timu hiyo, Mrundi, Masoud Djuma kuzungumzia hilo alisema kuwa: “Mimi sihusiki katika kusajili, mimi nahusika katika kutoa mapendekezo pekee ambayo nilishayakabidhi kwa uongozi ambao wao wanayafanyia kazi hivi sasa.”
Viewing all 104690 articles
Browse latest View live




Latest Images