Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

Trump Amteua Brett Kavanaugh kuwa Jaji wa Mahakama Kuu

$
0
0
amemteua Brett Kavanaugh kuwa Jaji wa Mahakama Kuu
RAIS Trump wa Marekani amemteua Brett Kavanaugh kuwa Jaji wa Mahakama Kuu nchini humo kuziba nafasi iliyoachwa na Jaji Kennedy.

Video thumbnail

Kavanaugh aliwahi kufanya kazi chini ya  rais mstaafu,  George H.W. Bush,  na alishiriki majukumu mbalimbali akiwa mwanasheria wakati wa utawala wa rais mstaafu,  Bill Clinton.

Idadi ya Vijana Waliookolewa Kutoka Pangoni Thailand Yafikia 10

$
0
0
Idadi ya Vijana Waliookolewa Kutoka Pangoni Thailand Yafikia 10
Vijana wengine wawili  waliokuwa wamenasa pangoni wameokolewa mchana huu na hivyo kufanya idadi ya waliookolewa kufikia kumi tangu kuanza kwa operesheni hiyo Jumapili iliyopita.

Vijana hao wanapatiwa matibabu ya dharura kabla ya kusafirishwa kwa helkopta kupelekwa hospitalini kuungana na wenzao wanaoendelea kuchunguzwa afya zao.

Wawili kati yao wamegundulika kuwa na matatizo kwenye mapafu na tayari wameanza kupata matibabu.

Kuokolewa kwa vijana hao kunafanya vijana waliokwama kwenye pango hilo kubakia wawili na mwalimu wao.

Ufaransa na Ubelgiji Kuchuana Nusu Fainali Kombe Leo

$
0
0
Ufaransa na Ubelgiji Kuchuana Nusu Fainali Kombe Leo
Timu ya kabumbu ya Ufaransa kuchuana na timu ya Ubelgiji katila mechi ya nusu fainali ya kombe la dunia mwaka 2018 nchini Urusi

Timu ya kabumbu ya Ufaransa kuchuana na timu ya Ubelgiji katila mechi ya nusu fainali ya kombe la dunia mwaka 2018 nchini Urusi

Mchuano kabambe kati ya Ufaransa na Ugelgiji unasubiriwa kwa hamu kubwa usiku wa Jumanne  katika uga wa Saint Petersburg . Kipengo cha mechi hiyo kştapigwa saa tatu kamili majira ya Uturuki na kuoneshwa moja kwa moja  kupitia tovuti ya TRT1, TRT 4K na tovuti ya fifa2018.trtspor.com.tr 

Muamuzi wa mechi hiyo ni raia kutoka Uruguay Andres Cunha.

Pacha Walioungana Wawasili Saudi Arabia kwaajili ya Kutenganishwa

$
0
0
Pacha Walioungana Wawasili  Saudi Arabia kwaajili ya Kutenganishwa
Pacha wa Tanzania waliozaliwa wakiwa wameungana kifuani hadi miguuni mkoani Kagera mapema mwaka huu wamewasili nchini Saudi Arabia kwa upasuaji wa kuwatenganisha.

Anisia na Maryness Beautus waliwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mfalme Khalid mjini Riyadh wakiandamana na mama yao na kundi la madaktari.

Kisa cha pacha hao kimefananishwa na kisa cha pacha wengine walioungana waliogusa nyoyo za wengi nchini Tanzania Maria na Consolata. Hao hata hivyo hawakutenganishwa na waliishi wakiwa wameungana hadi walipofariki dunia tarehe 2 Juni mwaka huu.

Pacha hao Anisia na Maryness watafanyiwa upasuaji karibuni baada ya Mfalme Salman kutoa idhini ya kufanyika kwa upasuaji huo kwa gharama ya serikali ya Saudia.

Pacha hao walipokelewa na kikosi maalum cha wanajeshi walinzi wa rais na maeneo matakatifu ya Kiislamu katika uwanja wa ndege. Wanajeshi hao walisaidiana na wataalamu kutoka Kituo cha Misaada ya Mfalme Salman (KSRelief) ambao watasimamia matibabu yao na kuchunguza iwapo inawezekana kuwafanyia upasuaji wa kuwatenganisha.

Pacha hao wawili wenye miezi sita wameungana kutoka kwenye koo, tumbo na mfupa wa nyonga. Wana miguu mitatu na kwenye uzazi. Hata hivyo, kila mmoja ana moyo wake.

Wamekuwa wakihudumiwa na madaktari katika hospitali ya taifa ya Muhimbili nchini Tanzania na wamekuwa katika hali nzuri.

Mfalme Salman alitoa agizo la kufanikishwa kwa matibabu ya pacha hao Jumapili ambapo aliagiza pia kwamba Saudi Arabia ilipie gharama yote ya upasuaji huo.

Ujumbe kutoka kwa ubalozi wa Saudia nchini Tanzania ulikuwa umewatembelea pacha hao Muhimbili, Dar es Salaam awali na kupokea taarifa za kimatibabu kuwahusu pacha hao kutoka kwa mkurugenzi wa hospitali hiyo Dkt Lawrence Museru.

Pacha hao wa Tanzania walizaliwa mnamo 29 Januari mwaka huu katika zahanati ya St Thereza Omukajunguti wilayani Misenyi. Walisafirishwa hadi hospitali ya kanda ya Bukoba kabla ya mwishowe kuhamishiwa Muhimbili.

Baba yao Benatus Bernado, 28, alikuwa awali ameambia gazeti la serikali ya Daily News kwamba waikuwa wameshauriwa na madaktari Muhimbili kwamba wataalamu wa Saudi Arabia ndio waliokuwa na uwezo wa kuwatenganisha pacha hao.

Serikali ya tanzana imekuwa ikifanya mashauriano ya kufanikisha kuhamishiwa kwa pacha hao Tanzania kwa wiki kadha, mazungumzo yaliyomshirikisha balozi wa Saudi Arabia nchini Tanzania Mohammed Bin Mansour Almalik na Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania Dkt Augustine Mahiga.

JPM Aongoza Kikao cha Kamati Kuu ya CCM

$
0
0
JPM Aongoza Kikao cha Kamati Kuu ya CCM
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Ndg John Pombe Joseph Magufuli aongoza kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi kinachofanyika katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM Lumumba jijini Dar es salaam, leo tarehe 10th July, 2018.


Huna Sababu ya Kuaibika Tena, Jipatie Dawa Bora ya Tatizo la Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0

HUNA SABABU YA KUAIBIKA TENA........ JIPATIE DAWA BORA YA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO

Matatizo ya nguvu za kiume yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIFINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUPER MORISIS :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr CHILAMBO mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAUSHAURI NA TIBA WASILIANA NA DR CHILAMBO ATAKUSAIDIA MATATIZO YAKO, NIPO DAR ES SALAAM PIA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO NYOTE MNAKARIBISHWA.

0744 391 089 / 0622344969

Hatimaye Watoto 12 pamoja na Mwalimu Wao Waliokwama Pangoni Siku 18 Waokolewa Wote

$
0
0

THAILAND: Hatimaye Watoto 12 pamoja na Mwalimu wao wa mpira wa miguu walikuwa wamekwama kwenye pango lililokumbwa na mafuriko wameokolewa.

Watoto hao waliokwama mnamo Juni 23 walianza kuokolewa kwa makundi na hatimaye mchana huu kundi la mwisho limefanikiwa kutoka ndani ya pango hilo.

Watoto 8 waliokolewa siku ya Jumapili na Jumatatu huku wakiwa na afya njema ya akili na mwili

Wanajeshi wa Kikosi cha Maji walifanikiwa kuwapelekea chakula mara baada ya kutambua umbali walopo kabla ya juhudi za uokozi kuanza

Watoto hao walikwama umbali wa Kilomita 4 kutoka kwenye mdomo wa mpango hilo

Siku ya Ijumaa Mwanajeshi mmoja wa kikosi cha uokoaji alifariki dunia kwa kuishiwa na hewa ya Oksijeni wakati akiwa kwenye harakati za zoezi la uokoaji

Beka Flavor Amuweka Hadharani Mpenzi wake

$
0
0

Waswahili husema 'Penzi ni kikohozi kulificha huwezi' na huwenda @bekaflavour kashindwa kuficha na kuamua kupost picha ya mpenzi wake. "Nimejikuta nimeshindwa na kuamua kupost picha ya mpenzi wangu na hivi karibuni nitaitwa 'Baba' furaha niliyonayo haipimiki kwani huyu atakuwa mtoto wangu wa kwanza " ***Ameyasema hayo @bekaflavour

Tumia Super Mkuyati Kurudisha Heshima ya Ndoa

$
0
0
SUPER MKUYATI ILIYO IMALA HESHIMA YANDOA super mkuyati nidawa ya mitishamba iliyo sheheni miti mbalimbali na kugundulika ina pambana na magonywa sugu SUPER MKUYATI inanguvu (3) nainafanya kazi kwapamoja (1) itakufanya uchelewe kufika kileleni ndani ya dk 15-20 bila kuchoka (2) ina zalisha homon kwa wingi na kukufanya uwe na mbengu nyingi zenye vimeleo vya uzazi vyilivyokomaa (3) inaongeza ume mdogo uliosinyaa,kunenepesha uume na kurefusha adi nchi 5-8 na upanda sm 2-3 dawa hii haina mazala kwa mtumiaji ata kwa wazee walionaumri 60-80 SUPER MKUYATI ponyo la maradhi yako tumia Leo uone mjabu yake OFISI YETU ZINAPATIKANA DR MTONI KIJICHI KAMAUNA NAFASI UTALETEWA POPOTE ULIPO KWA WAMIKOANI UTATUMIWA DR GATUNDU 0717777402/0768408794

Tarimba Ajitoa Kamati Ya Kuisaidia Yanga, Afunguka Mazito

$
0
0

Aliyekuwa  Mwenyekiti wa Kamati Maalum ya Mpito ya kuivusha Yanga, Abbas Tarimba ametangaza kuachia ngazi kwenye wadhifa huo kwa madai kuwa hakuna maelewano baina yake na Makamu Mwenyikiti wa Yanga, Clement Sanga, ambaye ameivunja kimyakimya kamati hiyo ambayo ilipitishwa katika mkutano mkuu.


Kufuatia tukio la kuvunjwa kwa kamati, Tarimba amesema hawezi akawa na muda wa kuonana na Sanga kwa sababu ameivunja kamati, na hata kama asingefanya hivyo asingekuwa tayari kutekeleza majukumu ya kamati hiyo.


“Waachane na mimi, mimi sina muda wa kuonana na Sanga waachane na mimi, yeye kwanza kamati kaisha ivunja na hata kama wasinge vunja mimi nisingeweza kufanya kazi nao” alisema Tarimba.


Mbali na kauli hiyo, Tarimba amekanusha uwepo wa taarifa zilizokuwa zimeripotiwa kuwa kamati yake imelipa madeni ya fedha zote zilizokuwa ni malimbikizo ya madeni kwa wachezaji. Tarimba ameeleza kuwa hakuna ukweli kuhusiana na hilo akiwahusisha viongozi wa Yanga kuwa wamekuwa waongo hivyo na kuwaomba waache masuala ya usanii kwa kuwa klabu hiyo ni taasisi kubwa.


“Wanayanga mnadanganywa Yaani wanayanga mnadanganywa mchana kweupe, Yanga tuna tamaduni zetu sio hizi, viongozi ni waongo, nawaomba watulize akili zao wasaidie timu, wengine ni wakubwa wanaongoza mpaka bodi ya ligi, sasa watumie ukubwa huo kuipeleka Yanga mbele waache uongo uongo,” alisema.

Mwigulu amkabidhi Ofisi Lugola

$
0
0

Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Lameck Nchemba amemkabidhi ofisi Waziri Mpya wa Wizara hiyo, Kangi Lugola katika Makao Makuu ya nchi Jijiji Dodoma leo Jumanne, Julai 10, 2018. 

Kupitia ukurasa wake wa Twiter, Mwigulu ambaye pia ni Mbunge wa Iramba Magharibi ameandika; “Makabidhiano ya ofisi/kijiti hii leo Dodoma. Nimemtakia kila raheli Mh.Kangi Lugola katika utumishi wake kwa watanzania katika wizara hii.”

Aidha Mwigulu Nchemba mara baada ya kuenguliwa nafasi hiyo alifika jimboni kwake na kuongea na wanachi wake akisema kuwa sasa atapa nafasi ya kuwatumikia vyema wananchi wake. 

Julai 1, 2018 Rais John Pombe Magufuli alifanya mabadiliko ya Balaza lake la Mawaziri na kumteua Mbunge wa Mwibara na aliyekuwa Naibu Waziri wa Muungano na Mazingura, Kangi Lugola kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi akichukua nafasi ya Mwiguku. 

Kutana na Dr Mabula Kukutibu Matatizo ya Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0
TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO BUSHA BILA KUPASUA PRESHA VIDONDA VYA TUMBO :

Asilimia kubwa ya wanadamu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali na wapo waliongahika sehemu mbalimbali bira MAFANIKIO MABULA CLINIC ni kituo cha tiba asilia kilichopo mbagara zakhemu njia kuu ya JESHINI JE HUNAUPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME AU UUME WAKO MDOGO NA MWEMBAMBA?


MAPRO PAWER NO 2 ndio Tiba kwa sasa utibu matatizo matatu kwa pamoja itakufanya uchelewe kufika kilekeni dikika 15-20 kwa tendo la kwanza 2 uimalisha misuli iliyoregea na kusinyaa hasa kwa wale walio asirika na upigaji punyeto 3 itakufanya upate hamu ya kurudia tendo zaidi ya Mara tatu.

KWA NINI UJIONE MPWEKE PALE UKUTANAPO NA MPENZI AU MKE WAKO kisa unawai kukojoa au unakomea bao moja tu na huku dawa zipo

MAKAKANUA mix ni dawa iliyochanganywa na miti Shamba 9 na Kuwa na uwezo wa kuongeza uume saizi upendayo inchi 5-8 Kwa Urefu na unene sentimita 1-5 dawa hizi hazina madhara yoyote kwa mtumiaji ata wazee wenye umri mkubwa wanapona.

Zipo dawa za mvuto wa mpenzi mme au mke Kwa masaa matatu tu na kukupigia simu yeye mwenyewe mvuto wa biashara kutengeneza mwonekano mzuri wa mwili kwa wanawake yani shepu tunatibu ngiri miguu mgongo na kiuno kuumwa kupunguza kitambi minyama uzembe matiti na mwili mkubwa

TIBA NA USHAULI MUONE DR MABULA AU PIGA SIMU NO 0752348593 UDUMA ZANGU UTAZIPATA POPOTE ULIPO KAMA UWEZI KUFIKA OFISINI

Ahukumiwa Maisha Baada ya Kuwaua Wanafunzi Wanne kwa Kuwachoma Visu

$
0
0
hukumiwa Maisha Baada ya Kuwaua Wanafunzi Wanne kwa Kuwachoma Visu
ZHAO ZEWEI raia wa China anayesemekana ana umri wa miaka itapayo 28 amehukumiwa kifo na Mahakama ya Jiji la Yulin kwa kuwachoma visu wanafunzi wanne kulipiza kisasi katika kile alichoita manyanyaso aliyoyapata katika shule hiyo ya jimboni Shaanxi wakati anasoma hapo.

Mahakama imesema Zhao aliyefunguliwa mashitaka hayo mwezi Mei mwaka huu, amekata rufaa.

Kutokana na sheria ya kubana umiliki wa bunduki nchini China, raia wengi nchini humo hutumia visu na mashoka kufanya mauaji.

Mahakama Yashindwa Kutoa Hukumu kwa Mbumge wa Chadema

$
0
0
Mahakama Yashindwa Kutoa Hukumu kwa Mbumge wa Chadema
Mahakama ya wilaya ya Mbozi imeshindwa kutoa hukumu ya kesi inayomkabili Mbunge wa jimbo hilo, Ndg. Pascal Haonga (CHADEMA) baada ya kudaiwa kwamba mchakato wa hukumu haujakamilika kulingana na uzito wa kesi.

Hukumu hiyo imeahirishwa na Hakimu Mfawidhi, Nemes Chawi  anayeendesha kesi hiyo ambapo amepanga kuifanyia maamuzi Kesi hiyo namba 117 ya mwaka 2017 Agosti10.

Katika kesi hiyo Haonga na  Katibu wake Wifred Mwalusanya na Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kalasha, Mashaka Mwampashi wanakabiliwa na mashitaka matatu ikiwa ni pamoja na kufanya vurugu wakati wa uchaguzi na kuwazuia askari polisi kutekeleza majukumu yao tukio walilolifanya  Agost 28, 2017.

Naye  Wakili upande wa utetezi Bonifasi Mwabukusi ameishukuru Mahakama kwa uamuzi huo na kuamini kuwa mahakama itatenda haki.

Mwigulu Nchemba Baada ya Kukabidhi Ofisi Leo “Bodaboda Wanapata Tabu”

$
0
0
Mwigulu Nchemba baada ya kukabidhi ofisi leo “Bodaboda wanapata tabu”
Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dr Mwigulu Nchemba amekabidhi rasmi ofisi ya Wizara hiyo kwa Waziri mteule mpya Kangi Lugola mkoani Dodoma.

Nchemba ameongelea pia baadhi ya mambo ambayo kama Wizara ilianza kuyashughulikia na angetamani kuona yakitekelezeka ikiwemo ahadi ya uandaaji wa kanuni mpya ya utozaji faini kwa vyombo vya moto ikiwemo bodaboda.

Good News: Wavulana Wote 12 na Kocha Wao Waliokwama Pangoni Thailand Waokolewa Wakiwa Hai

$
0
0
Good News: Wavulana Wote 12 na Kocha Wao Waliokwama Pangoni Thailand Waokolewa Wakiwa Hai
Wavulana 12 wa timu ya soka Thailand na kocha wao wameokolewa salama kutoka ndani ya pango walimokuwa wamekwama kwa siku 17 kaskazini mwa Thailand.

Mkasa huu uliwagusa wengi duniani, waliofuatilia kwa makini jitihada za kuwakoa.

Kikosi cha wanajeshi wa maji nchini kilichosimamia operesheni hiyo ya uokozi wanasema wavulana hao a kocha wao wameokolewa salama na kukamilisha operesheni iliyokuwa ngumu na ya hatari.

Je wajua kwamba mtoto akipewa chakula kigumu mapema analala vizuri?

Mtoto wa miaka miwili ajiua kwa risasi Marekani

Pacha walioungana Tanzania wawasili Saudi Arabia kwa upasuaji

Kundi hilo la vijana wacheza soka walikwama ndani ya pango tangu Juni 23 baada ya mvua kubwa kunyesha na kusababisha pango kufurika maji.

Awali duru iliyokuwa ndani ya operesheni hiyo ya uokozi imeiambia BBC kwamba watu watatu wametolewa kutoka kwenye pango hilo leo.

Operesheni hiyo iliendelea leo wakati wavulana wanne, kocha wao na daktari na wanajeshi watatu wa maji wakiwa ndani ya pango hilo.

Gigy Money Achafua Hali ya Hewa..Adai Anataka Kuzaa na Diamond na Idriss Sultan

$
0
0

Natamani kupata mtoto na Diamond Platnumz na Idris Sultan kwa kweli maana mtoto atakuwa mzuri kweli kweli. Maana mimi napenda sana wanaume warefu. Siwezi kuwa kwenye mahusiano na Nay Wa Mitego. ***Ameyasema Hayo Gigy Money katika interview kipindi cha #ThePlayList ndani ya #TimesFM.

Sababu zinazoshawishi watu kupanda ndege mpya ya Dreamliner

$
0
0

NDEGE iliyotengenezwa na kampuni ya Boeing 787 ya Marekani ambayo ni moja ya ndege zilizonunuliwa na serikali ya Tanzania,  ni ndege ya kimapinduzi ambayo ina kila aina ya starehe katika safari zake kwa madaraja yote. 

Ni ndege ambayo haina kelele zozote ukiwa ndani, hii ni kutokana na injini zake zisizokuwa na makelele makubwa  kutokana na mfumo wa kuzuia sauti kuwafikia abiria. 

Baadhi tu ya zana za starehe katika ndege hiyo iliyotengenezwa Marekani na kuwekewa injini aina ya Rolls Royce za Uingereza ni viti vya kuvutia ambavyo ‘vinakunjulika’ na kulazwa kama kitanda, nafasi kubwa ya kunyoosha miguu na televisheni kubwa za inchi 23 zilizo mbele ya abiria. 

Miongoni mwa sababu kubwa za abiria kuipenda Dreamliner Boeing 787 ni: 

• Nafasi kubwa zilizomo ndani yake. Hii ni pamoja na madirisha makubwa na dari iliyo juu zaidi, hii huwapa fursa abiria wake kujiona wako mahali pa wazi zaidi na hivyo kutokuwa na woga wowote.  Hii ni pamoja na nafasi ya juu ya kuweka mizigo midogo ya mikononi. 

A flight attendant checks out the seating options of 
• Usingizi mzuri wakati wa safari. Kwa vile  787 huruka juu katika kiwango cha futi 6,000 kutoka ardhini badala ya futi 8,000, uvutaji wa pumzi unakuwa rahisi ambapo mapafu ya abiria yanapokea oksijeni zaidi na hivyo kulala vizuri zaidi, kuzuia maumivu ya kichwa na kuvuta pumzi vizuri. 

Kwa vile ndege imetengenezwa kwa mchanganyiko wa madini na vyuma mbalimbali badala ya ‘aluminum’, Boeing huongeza unyevu zaidi katika hewa kuliko ndege zingine.  Hivyo, njia ya hewa kupitia puani haiwezi kukauka kirahisi au kukuletea harara, hivyo hali hiyo hukufanya ulale vizuri zaidi. 

• Usariri usiokuwa na mitingishiko. Boeing 787 imeundwa kwa kila aina ya utaalam wa kisasa wa kuzuia mitingishiko wakati wa usafiri.  Hii ni tofauti na ndege za aina nyingine ambazo huwa na mitingishiko hususan zinapopita juu ya maeneo fulani. 

• Madirisha yenye mwanga maalum wakati wa kulala. Boeing 787 ina madirisha maalum yanayoendeshwa kielektroniki ambapo yanaweza kufanywa yakawa ya giza ili kuruhusu abiria kulala kama vile ni waati wa usiku, hivyo kukwepa kusumbuliwa na mwanga. 

• Maliwato murua. Maliwato ndani ya Dreamliner yana kila sifa nzuri; mabomba na zana za kusafishia uchafu kirahisi, sehemu ya kukalia inayojifunga na kufunguka kwa kutumia nyenzo zilizopo. 


• Mfumo mzuri wa matangazo.  787  ina mfumo wa vipaza sauti ambavyo ni rahisi kusikika na kueleweka. 

• Ndege yenye nakshi na burudani za kutosha.  787, hususan  787-9,  ambayo ina urefu wa futi 20 zaidi kuliko  787 ya mwanzo, inavutia kwa nakshi  na mapambo mbalimbali ndani yake kiasi cha kuwaliwaza kikamilifu abiria. 

Hii ndiyo Boeing 787 ambayo unaweza pia kutoa maagizo yoyote unavyotaka iwe ndani yake kwa kadiri ya utashi wako mnunuzi.

Mwanaume Mmoja Anaweza Kuwapa Mimba Wanawake Wote Duniani

$
0
0

Ni mara chache sana sayansi inakosea. Leo tuongeze jambo kidogo la kisayansi. 
Dunia mpaka sasa ina watu hai 7.625 Bilioni (today's clock). Katika hao, wanawake ni 3.77 Bilioni.

Mwanaume mmoja mwenye afya hutoa sperms milion 40-1.2 Bilioni kwa mkupuo mmoja. Katika maisha yote (assume atakufa baada ya miaka 75) huweza kutoa sperms bilioni 525. Hivyo ukizigawa sperms hizo zinatosha kuwaingia wanawake wote duniani na kuwatia ujauzito na za ziada zikabaki kwa ajili ya kuogea!!!

Be proud to be a man!!!

Mfahamu Samuel Umtiti aliyewafikisha Ufaransa fainali Kombe la Dunia

$
0
0
Ufaransa watakutana na mshindi kati ya England na Croatia kwenye fainali ya Kombe la Dunia nchini Urusi baada ya kuwashinda majirani wao Ubelgiji kwenye nusufainali mjini St Petersburg.

Mechi ya fainali itachezwa Jumapili uwanjani Lzhiniki mjini Moscow saa tatu usiku saa za Afrika Mashariki.

Ubelgiji wamesalia na mechi moja ya kuamua atakayemaliza wa tatu, mechi ambayo itachezwa Jumamosi.

Bao pekee la mechi ya nusu fainali lilifungwa na beki Samuel Umtiti baada ya kona iliyopigwa na Antoine Griezmann.

Mchezaji huyu aliyewavusha Ufaransa hadi fainali ni nani?
Samuel Yves Umtiti huchezea klabu ya Barcelona ya Uhispania.

Ni mchezaji wa miaka 24 ambaye alizaliwa mnamo 14 Novemba mwaka 1993 mjini Yaounde, Cameroon. Mamake ni Annie Ngo Um lakini babake hajulikani ni nani. Ana ndugu kwa jina Yannick Umtiti.

Yeye kwa kawaida huwa ni beki wa kati.

Ni mchezaji mrefu kwa kimo, kimo chake ni futi sita (1.83m) jambo ambalo huenda lilimsaidia katika kufunga bao la kichwa dhidi ya Ubelgiji ambapo alikuwa anakamiliana na mchezaji mwingine mrefu wa kimo anayefahamika sana kwa mipira ya kichwa, Marouane Fellaini.

Kutokana na kwamba alizaliwa Cameroon, ni mchezaji ambaye alikuwa na fursa ya kuichezea timu ya taifa ya Cameroon. Ana uraia wa Cameroon na Ufaransa.


Juhudi za Shirikisho la Soka la Cameroon na nyota wao wa zamani wa kimataifa Roger Milla za kumshawishi aiwakilishe Cameroon hazikufua dafu.

Alizaliwa katika maisha ya umaskini na alikuwa tu ndio ameanza kuzoea maisha ya Yaounde pale familia aliyokuwa anaishi nayo ilipofunganya virago na kuhamia Ufaransa katika viunga vya mji wa Lyon. Kutokana na ufukara mamake alikuwa amemkabidhi kwa jamaa aishi naye akiwa bado mdogo. Kuna utata hata hivyo kuhusu iwapo alisafiri na jamaa waliokuwa wanamlea au na mamake mara ya kwanza kwenda Ufaransa.

Baada ya kukaa miezi kadha Villeurbanne ambapo alilelewa katika jamii ya wahamiaji kutoka Cameroon, hatimaye walihamia Menival.


 Mwaka aliohamia Ufaransa, 1995, ilikuwa si muda mrefu sana baada ya Roger Milla kuvuma sana akichezea Cameroon jambo ambalo lilichochea wahamiaji wengi wa Afrika waliokuwa nchini Ufaransa kukumbatia kandanda. Ni kipindi hicho ambapo wachezaji nyota kama vile Paul Pogba, Raphael Varane na Romelu Lukaku walikuwa watoto.

Umtiti alianza kuonyesha ustadi wa kusakata gozi akiwa na miaka mitano hivi ambapo kwa makubaliano kati ya shule yake na mamake aliruhusiwa kuifuata ndoto yake.

Njiani kati ya nyumbani kwao na shuleni kulikuwa na uwanja wa klabu ya soka ya Menival FC na huko ndiko alipoanza kuchezea soka.

Jinsi Kylian Mbappe alivyofikia umaarufu wake
Rais wa zamani wa klabu hiyo Said Intidam anamkumbuka: "Alikuwa na miaka mitano tu lakini angeweza kucheza katika mchezo wa wachezaji 11 kila upande bila matatizo."

Rais wa sasa wa klabu hiyo Judi Bouzama anasema tofauti kati yake na wachezaji wengine ilionekana wazi.

Haki miliki ya pichaAFP
"Hakuwa mchezaji wa kiwango cha Menival, alikuwa i mchezaji wa klabu kubwa kama vile Olympique Lyonnais au Saint-Etienne," amenukuliwa na mtandao wa SportEnglish.

Alianza kwenda Lyon kujifunza soka akiwa na miaka tisa mwaka 2001 na kuibuka kuwa miongoni mwa wachezaji nyota katika kikisi cha wachezaji chipukizi.

Alianza kama mshambuliaji, baadaye akawa anacheza safu ya kati kabla ya mwishowe kuanza kucheza kama beki.

Baada ya kukaa miaka 11 akijifunza soka akademi ya Lyon, aliichezea timu kubwa ya klabu hiyo mara ya kwanza Januari 2012 na kufikia msimu wa 2015/16 alitawazwa mchezaji bora wa msimu na mashabiki wa klabu hiyo ambapo alimshinda Alexandre Lacazette ambaye kwa sasa huichezea Arsenal.

Alikuwa amewachezea mechi 170 za ushindani na kufunga mabao matano, na kusaidia ufungaji wa mabao mengine mawili.

Ni beki stadi ambaye kipaji chake kilitambuliwa na Barcelona na akanunuliwa €25 milioni (£21.2 milioni) Julai mwaka 2016 kutoka Olympique Lyonnais (Lyon) ya Ufaransa ambapo alikuwa mchezaji wa kutegemewa sana.

Umtiti alitafutwa na Barcelona kuimarisha safu yao ya ulinzi na zaidi kujaza pengo lililoachwa na nyota Carles Puyol baada ya Jeremy Mathieu na Thomas Vermaelen kuonekana kutoimudu vyema kazi hiyo.

Mashabiki wa Ufaransa wakisherehekea kufika fainali Kombe la Dunia katika barabara za Paris
Alichezea Barcelona mara ya kwanza 17 Agosti 2016 katika mechi ya Super Cup ya Uhispania ambapo walishinda 3-0 dhidi ya Sevilla. Aliwafungia bao la kwanza 4 Machi 2017 dhidi ya Celta de Vigo. Siku zilivyosonga, aliunda ushirikiano wa karibu sana na Gerard Pique na Jordi Alba katika safu ya ulinzi na alikuwa katika timu iliyofanikiwa kuandikisha historia kwa kujikwamua dhidi ya Paris Saint Germain Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya mwaka 2017 baada ya kushindwa 4-0 mechi ya kwanza lakini wakashinda 6-1 mechi ya marudiano.

Alishinda Copa Del Rey 2016-17 akiwa na wachezaji wengine kama vile Lionel Messi, Neymar, Luis Suarez Barcelona.

Kuichezea timu ya taifa
Umtiti aliitwa kuichezea timu ya taifa ya Ufaransa katika Euro 2016 ambapo Ufaransa walikuwa wenyeji ambapo aliwekwa kikosi na Didier Deschamps baada ya kuumia kwa Jeremy Mathieu.

Aliwachezea mara ya kwanza michuano hiyo hatua ya robofainali dhidi ya Iceland baada ya beki wao mwingine Adil Rami kupigwa marufuku kucheza mechi moja.


Uchezaji wake mzuri ulimfanya kuchezeshwa kikosi cha kuanza mechi na kwa kipindi kilichosalia michuano hiyo. Alicheza nusufainali dhidi ya Ujerumani na kwenye fainali waliposhindwa na Ureno.

Alikuwa ndiye mchezaji wa kwanza wa ndani uwanjani tangu Gabriel De Michele katika Kombe la Dunia 1966 kuchezeshwa mara ya kwanza katika timu ya taifa wakati wa michuano mikubwa.

Umtiti alijiunga na Barcelona mwaka 2016
Aliwafungia Ufaransa bao lake la kwanza 13 Juni 2017 kwa kuwasawazishia dhidi ya England mjini Paris katika mechi ambayo walishinda 3-2.

Kabla ya kujiunga na timu kuu ya taifa, alikuwa amecheza katika timu za taifa za wachezaji chipukizi mara 47 na kufunga mabao matatu.

Anasemaje kuhusu Cameroon?
Bado hajakata uhusiano wake na taifa hilo la Afrika.

Kwenye mahojiano na FranceFootball, alisema: "Bado nina jamaa Yaounde na bado huwa twawasiliana kwa simu, lakini sina kumbukumbu nyingi kuhusu maisha yangu ya miaka miwili huko Cameroon," alisema.

"Nimezuru huko mara mbili, ni sehemu ya miziz yangu. Shirikisho lao la soka liliniomba niichezee Cameroon mara kadha, washauri wangu walikutana na Roger Milla kutokana na ombi lake, kwa heshima. Walisikiliza maoni yangu, lakini hakukuwa na mabadiliko yooyte. Nilikuwa tayari nimefanya uamuzi wangu, nilikuwa nimeufikiria vyema.

"Tangu mwanzoni, nilitaka kuichezea Ufaransa. Sijui kama Cameroon walikerwa na uamuzi wangu, lakini niliufanya uamuzi wangu na lazima uheshimiwe, watu wapende wasipende."

Uhusiano na Mitandao ya kijamii
Mchezaji huyu bado hajafunga ndoa rasmi lakini anadaiwa kuwa na uhusiano na Alexandra Dualauroy mwenye asili ya Colombia.

Ruka ujumbe wa Instagram wa samumtitiMwisho wa ujumbe wa Instagram wa samumtiti
Umtiti ana wafuasi wengi kwenye mitandao ya kijamii na hasa Instagram ambapo kufikia sasa ana wafuasi 4.1 milioni.

Yeye huwapenda sana wanyama na ana mbwa kwa jina Osito ambaye mara kwa mara hupakia picha za video zake kwenye Instagram.
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live




Latest Images