Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Bei ya Jezi mpya ya Ronaldo ‘Juventus’ Kufuru Tupu

$
0
0
Bei ya Jezi mpya ya Ronaldo ‘Juventus’ Kufuru Tupu
Imekuwa ni wiki yenye furaha kwa Mreno, Cristiano Ronaldo baada ya kuvuta mkwanja mrefu  kutoka klabu ya Juventus wakati mashabiki wa vibibi hao wa Turin wakimiminika kununua jezi za staa huyo.

Jezi halisi ya Ronaldo ambayo imetengenezwa na klabu ya Juventus ambazo ni za mechi za nyumbani zinagharimu kiasi cha dola 144.95 ambayo ni sawa na Tsh 329715.16.

Jezi hiyo hiyo ya nyumbani kwa upande wa wanawake inagharimu kiasi cha dola 94.95 ambayo ni sawa na Tsh 215977.78

Jezi hiyo hiyo ya nyumbani ya Ronaldo kopi yake ambayo siyo origino inauzwa kwa kiasi cha dola 104.95 sawa na Tsh 238687.62

Wakati kwa watoto jezi hiyo ya nyumani unaweza kuinunua kwa dola 79.95 ambayo ni sawa na Tsh 181,848.64.

Wakati mshahara wa mwalimu hapa nchini kima cha chini ni sawa na Tsh 331000 kwa mwezi.

Ronaldo mwenye umri wa miaka 33, ameingia kandarasi ya pauni milioni 105 kutua Juventus siku ya Jumanne akitokea Real Madrid.

Ronaldo alikutana na rais wa timu ya Juventus, Andrea Agnelli mchana wa siku ya Jumanne kwenye hoteli huko Greece ambapo alikuwa mapumzikoni na mpenzi wake pamoja na familia kabla ya kukubali dili hilo la miaka minne ambalo atavuna kiasi cha pauni 500,000 kwa wiki.

Hapo jana siku ya Alhamisi nyota huyo ameonekana akifurahia maisha na familia yake akiwa sambamba na marafiki zake akiposti picha kwenye instagram inayo muonyesha akipata chakula cha usiku.

Hawa Ndio Vinara wa Masomo ya Sayansi Kidato cha Sita

$
0
0
Hawa Ndio Vinara wa Masomo ya Sayansi Kidato cha Sita
Baraza la Taifa la Mitihani (Necta) limetangaza matokeo  ya kidato cha sita leo Julai 13 na kutoa orodha ya watahiniwa waliofanya vizuri zaidi kitaifa katika mtihani huo.

 Katibu Mtendaji wa Necta, Charles Msonde, ametangaza matokeo hayo akiwa visiwani Zanzibar leo.

 Watahiniwa waliofanya vizuri  zaidi kitaifa katika masomo ya Sayansi ni pamoja na Anthony Mulukozi, wa Shule ya Sekondari ya Mzumbe, Asia Jasho wa Tabora Girls, na Raphael Fanuel wa Ahmes, Pwani.

Wengine waliofanya vizuri ni pamoja na Godfrey Kawau, Uru Seminari, Kilimanjaro na Biubwa Hamis Ussi, wa shule ya Sekondari ya Sos Hermain Gmeiner, Mjini Magahribi (Zanzibar).

Wengine ni Fahad Rashid Salum, shule ya Sekondari Lumumba, Mjini Magharibi, Prince Walter Ngao, Marian Boys, Pwani, Victor Maghembe, Marian Boys, Pwani na Emmy Shemdangiwa, St Marys Mazinde Juu, Tanga na Vanessa Lodrick Shoo wa St Marys, Mazinde Juu.

Simba, Azam Kuonyeshana leo Fainali za Kagame CUP..... Hiki Hapa Kikosi cha Simba

$
0
0
Simba, Azam Kuonyeshana leo Fainali za Kagame CUP..... Hiki Hapa Kikosi cha Simba
Kikosi cha Simba SC kitakachoanza dhidi ya Azam FC, KAGAME CUP

1. Deo Munishi 
2. Nicholas Gyan
3. Mohammed Hussen
4. Paul Bukaba
5. Pascal Wawa
6. James Kotei
7. Mzamiru Yassin
8. Said Ndemla
9. Meddie Kagere
10. Mohamed Rashid
11. Marcel Kaheza

Kikosi cha akiba

12. Ally Salim
13. Ally Shomary
14. Jamal Mwambeleko
15. Abdul Hamis
16. Rashid Juma
17. Moses Kitandu

BASATA Haiwezi Kunilipa Huko ni Kunichafua- Steve Nyerere

$
0
0
BASATA Haiwezi Kunilipa Huko ni Kunichafua- Steve Nyerere
Msanii Steve Nyerere, amesema siyo kweli kuwa amepewa fedha na Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) ili aweze kuwashawishi wasanii wenzake juu ya mabadiliko mapya ya tozo yaliyotangazwa na baraza hilo siku za hivi karibuni ili wakubaliana nayo.

Steve amebainisha hayo wakati akizungumza na www.eatv.tv leo Julai 13, 2018 baada ya wadau mbalimbali wa filamu na muziki kumshambulia kupitia ukurasa wake wa kijamii kuwa amepatiwa fedha 'fungu lake' ndio maana anajifanya kutaka kukaa kikao na wasanii wenzake ili wapate ufumbuzi juu ya jambo hilo ambalo limekuwa gumzo kwa sasa.

"BASATA haiwezi kunipa fedha 'fungu' lolote kwa ajili yangu mimi huko ni kuichafua, mimi ni nina nguvu gani mpaka wanilipe. Lazima niwe upande wa wenzangu ambao ni wasanii na msema ukweli siku zote ni mpenzi wa Mungu, kiukweli milioni tano kwa msanii ni pesa nyingi sana hata ingekuwa milioni moja bado shida ingekuwepo", amesema Steve

Pamoja na hayo, Steve ameendelea kwa kusema "kama kweli BASATA walitaka kutusaidia walipaswa waanze kutupa kazi wao kwa kututengenezea mifereji ya kupata matangazo ili ndio watake hizo pesa walizozitaka. Kwa namna moja ama nyingine hayo makampuni yakikataa kutupa matangazo sisi na yakaenda kuwapa raia wa kawaida hao BASATA watakuwa wanapata nini zaidi ya hasara tu. Duniani kote msanii anapata fedha kupitia matangazo".

Mbali na hilo, Steve Nyerere ameitaka jamii kutoliingiza suala hilo katika mlango wa kisiasa licha ya kuwa yeye yupo ndani ya chama cha Mapinduzi (CCM).

Siku za hivi karibuni Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) liliweza kufanya mabadiliko mbalimbali katika tozo zao za utoaji wa huduma ikiwemo ya makampuni kulipa milioni tano kwa BASATA endapo watamtumia msanii kufanya tangazo la aina yoyote, jambo ambalo limekuwa likipingwa na wasanii wengi nchini wakidai kuwa kwa kitendo hicho watakosa kazi.

Kupitia kipindi cha Planet Bongo kilichorushwa Julai 10, 2018 na  East Africa Radio, BASATA ilitoa ufafanuzi juu ya suala hilo kuwa sio kweli kwamba msanii anatakiwa kulipa milioni 5 akifanya tangazo bali kampuni husika ndio inapaswa kufanya hivyo kwa kuwa wanaingiza kipato kikubwa kutumia tangazo hilo.

Wanawake Walioathiriwa na Jonsons Poda Watakiwa Kulipwa Bilion 4.7 za Marekani

$
0
0
Wanawake Walioathiriwa na Jonsons Poda Watakiwa Kulipwa Bilion 4.7 za  Marekani
Kampuni ya Johnsons & Johnsons imeamriwa kulipa fidia ya dola za Kimarekani bilioni 4.7 kama fidia na faini kwa wanawake 22 waliodai kuwa bidhaa za talc za kampuni hiyo zimewasababishia saratani ya ovari.

Baraza la Mahakama Missouri huko Marekani limeamuru walipwe dola za kimarekani milioni 550 kama fidia na wakaongeza dola bilioni 4.1 kama adhabu ya fidia.

Uamuzi huo unakuja wakati ambapo kampuni hiyo kubwa ya dawa ikipambana na kesi 9,000 zinazohusisha bidhaa yake maarufu ya poda.

Katika kesi hiyo iliyodumu wiki sita, wanawake hao na familia zao wamesema kuwa wamepata saratani ya ovari baada ya kutumia poda ya Johnsons na baadhi ya bidhaa zake za talc kwa miongo kadhaa.

Mawakili wa familia hizo wanasema kuwa kampuni ya Johnsons ilikuwa inatambua kuwa bidhaa yao ya poda ya talc ilikuwa na madini mabaya ya 'asbestos' tangu mwaka 1970 lakini ilikosa kuwaonya watumiaji kuhusu athari.

Kampuni hiyo ilikana kuwa bidhaa zake zimewahi kuwa na madini mabaya ya asbestos na walisisitiza kwamba bidhaa hizo hazileti saratani.

Kampuni hiyo kubwa ya dawa iliongeza kwamba tafiti mbali mbali zimeonyesha kuwa poda yao ni salama na wakasisitiza zaidi kuwa uamuzi huo ni matokeo ya uamuzi usiotenda haki.

Malipo hayo ndiyo ya juu zaidi kwa J&J kuwahi kuamriwa kulipa kama fidia kutokana na bidhaa zake na tuhuma kwamba huwa zinasababisha kansa.

Katika kesi iliyopita mwaka 2017 jopo la mahakama Calfonia liliiamuru kampuni hiyo kulipa tozo ya dola za kimarekani 417 kwa mwanamke ambaye alisema amepata saratani ya mayai ya uzazi baadha ya kutumia bidhaa za kampuni hiyo ikiwemo poda yake ya watoto (Johnsons baby powdwer)

Hata hivyo baadaye hakimu alibadiliuamuzi huo japo bado kampuni hiyo ina kesi kadhaa ambazo bado hazijatolewa uamuzi.

Adhabu za kulipa fidia mara nyingi huwa zinapunguzwa kwa hakimunwa kesi hiyo au kukata rufaa, na J&J imefanikiwa kubadili maamuzi ya kesi kadhaa huku baadhi ya hukumu hizo wakitoa vigezo vya matatizo ya kiufundi.

Mke na Mume Waachana Kissa Messi na Ronaldo

$
0
0
Mke na Mume Waachana Kissa Messi na Ronaldo
Moja kati ya stori za kusisimua katika soka barani Ulaya ni pamoja na hii stori ya mwanaume wa kirusi kuachana na mke wake wa ndoa aliyedumu nae kwa miaka 14 kutokana na mkewe kukosoa uwezo wa Lionel Messi wakati wa fainali za Kombe la Dunia.

Arsen mwenye umri wa miaka 40 na Lyudmila mwenye umri wa miaka 37 wameachana kufuatia mke wake kuwa shabiki mkubwa wa Cristiano Ronaldo na kupenda kumkosoa Lionel Messi ambaye anashabikiwa na mmewe Arsen.



“Kwa mara nyingine tena alipoanza kuzungumza maneno yake yasiofaa kuhusu Lionel Messi na kukosoa uwezo wake nikapata hasira na kumgeukia na akaendelea kueleza kila kitu ambacho kinasifia u-handsome wa Ronaldo”>>> Arsene



Arsen na Lyudmila kwa mara ya kwanza walikutana 2002 katika bar nchini Urusi wakifuatilia Kombe la Dunia na miaka miwili baadae walifunga ndoa, wote wawili ni mashabiki wa Club ya Moscow lakini nje ya hapo mumewe ni shabiki wa Barcelona na mkewe shabiki wa Real Madrid na Cristiano Ronaldo, wawili hao wameachana wiki iliyopita baada ya ugomvi wao mkubwa mkewe kukosoa uwezo wa Messi wakati wa Kombe la Dunia.

Makamu Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi Ajiunga CCM

$
0
0
Makamu Mwenyekiti wa  NCCR-Mageuzi Ajiunga CCM
Makamu Mwenyekiti wa chama cha NCCR-Mageuzi (Bara), Leticia Mosore leo Ijumaa Julai 13, 2018 ametangaza kujiunga na CCM

Amejiunga pamoja na wanachama wengine watano, akiwemo aliyekuwa mjumbe wa halmashauri kuu ya chama hicho, Mchata Mchata

Amesema “Kinachonikera kwenye upinzani ni kupinga kila kitu hadi mazuri wakati hayo ndio tulikua tunayasema, mpaka mwisho hatueleweki tunataka nini, Hivyo mtu mzima kama mimi nimeona bora nirud CCM”

“Niliamua kuhama CCM sababu utekelezaji wa ilani haukuwa wa kuridhisha, rushwa na ukosefu wa maadili vilikithiri. Upinzani wa wakati huo walisimamia hoja hizi, zilinigusa nikashawishika kuungana nao ili tunusuru nchi”.

Video: Dooh! Daimond Kiboko Acop na Kupesti Kila Kitu...... Wadau Wamtolea Povu

$
0
0
Baada ya mwanamuziki wa kizazi kipya Daimond Platinum Kuachia video ya ngoma yake iitwayo, Baila ambayo amemshirikisha Mshindi wa Tuzo za Grammy, Miri Ben -Ari wadau mbalimbali wameibuka na kumtolea povu msanii huyo kwa kile walichodai kuwa ame copy and paste vipande vingi vya ipande vingi kutoka kwenye wimbo Jab Tak Hai Jaan- Shah Rukh Khan ft Katrina Kaifwa kutoka India .

Hivi ni Baadhi ya vipande ambavyo daimond amedaiwa kuvichuku kutoka kwa msanii mwingine
vipo vipengere vingi ambavyo kama utaangalia wimbo mzima utakubaliana na maneno ya watu kuwa nguo ya mwanadada ambaye ni video qeen wake na huo wimbo wingine ni sawa kila kitu kuanzia rangi za nguo na  maeneo mbalimbali aliyotumia.




Hii ni Habari Njema Kwa Wale Wote Waliohangaika na Matatizo ya Magonjwa Sugu Yaliyokosa Tiba

$
0
0
"HII NI HABARI NJEMA KWA WALE WOTE WALIOHANGAIKA NA MATATIZO YA MAGONJWA SUGU NA YALIYOKOSA TIBA" sasa usikate tamaa tiba imepatikanika kwa DK. ABDALA MUSSA anatibu matatizo kama yafuatayo:

Nguvu za kiume, uzazi, kisukari, tezi dume, vidoda vya tumbo, mgongo kuuma, miguu kuwaka moto na mataizo uliyonayo

1/ITAGULA- ni dawa ya mkosi kuosha nyota, kumvuta mpenzi, mke, mume, kuua kesi na kupata kazi haraka kama umeomba maombi serikalini au kampuni binafisi unaitwa ndani ya siku mbili 2/

NINJIWE- ni dawa inayomaliza matatizo ya wanaume heshima ndani ya ndoa, kuwa na nguvu za kiume milele na kukomaza mbegu na kuwa na uwezo kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila kuchoka kama umezaraulika na kufanya tendo na kusinyaa uume dawa ipo dozi yake siku sita vidoge 12 pia kuna na unga inayokomaza uume ndani ya siku 7 unapona kabisa.

3/MPALALA- ni dawa ya kutibu busha miguu kuwaka moto, kiuno, kisukari.

4/NGEKEWA- ni dawa ya kuvuta wateja kwenye biashara yoyote kuwa na wateja wengi katika biashara na kuzuia chuma ulete. 4/LINGWATA- ni dawa ya punguza unene, mafuta tumbo, matiti, miguu, hipsi na kutengeneza shepu dawa hii ni ya unga ukitumia utaona mabadiliko baada ya siku 3.

5/DUBISHO- ni dawa zindiko la mwili, majumba, gari, biashara, mteja wangu huduma utaipata mahali popote ulipo kuna wanasaplai mahali ulipo kama huna muda wa kufika osifini mkoa wa dar-es-salaam, iringa, kanda ya ziwa wilaya ya bunda. angalizo kwa wateja usitume sms wala kubipu huduma yangu ni kuanzia saa 12 asubui hadi saa 12 jioni kwa wateja wa dar-es-salaam ofisi ipo buguruni na mbagala zakhem na kwa wale walio nje ya mkoa dawa hizi mtazipata kwa njia za mabasi. punguzo la bei kwa wateja 5 wa kisukari na nguvu za kiume

KWA MAWASILIANAO ZAIDI WASILIANA NA DK. ABDALA MUSSA KWA SIM NAMBA 0767-171773/ 0716-608959 WOTE MNAKARIBISHWA:

Steve Nyerere: BASATA haiwezi kunipa fedha

$
0
0

Msanii Steve Nyerere, amesema siyo kweli kuwa amepewa fedha na Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) ili aweze kuwashawishi wasanii wenzake juu ya mabadiliko mapya ya tozo yaliyotangazwa na baraza hilo siku za hivi karibuni ili wakubaliana nayo. 

Steve amebainisha hayo wakati akizungumza na www.eatv.tv leo Julai 13, 2018 baada ya wadau mbalimbali wa filamu na muziki kumshambulia kupitia ukurasa wake wa kijamii kuwa amepatiwa fedha 'fungu lake' ndio maana anajifanya kutaka kukaa kikao na wasanii wenzake ili wapate ufumbuzi juu ya jambo hilo ambalo limekuwa gumzo kwa sasa. 

"BASATA haiwezi kunipa fedha 'fungu' lolote kwa ajili yangu mimi huko ni kuichafua, mimi ni nina nguvu gani mpaka wanilipe. Lazima niwe upande wa wenzangu ambao ni wasanii na msema ukweli siku zote ni mpenzi wa Mungu, kiukweli milioni tano kwa msanii ni pesa nyingi sana hata ingekuwa milioni moja bado shida ingekuwepo", amesema Steve 

Pamoja na hayo, Steve ameendelea kwa kusema "kama kweli BASATA walitaka kutusaidia walipaswa waanze kutupa kazi wao kwa kututengenezea mifereji ya kupata matangazo ili ndio watake hizo pesa walizozitaka. Kwa namna moja ama nyingine hayo makampuni yakikataa kutupa matangazo sisi na yakaenda kuwapa raia wa kawaida hao BASATA watakuwa wanapata nini zaidi ya hasara tu. Duniani kote msanii anapata fedha kupitia matangazo". 

Mbali na hilo, Steve Nyerere ameitaka jamii kutoliingiza suala hilo katika mlango wa kisiasa licha ya kuwa yeye yupo ndani ya chama cha Mapinduzi (CCM). 

Siku za hivi karibuni Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) liliweza kufanya mabadiliko mbalimbali katika tozo zao za utoaji wa huduma ikiwemo ya makampuni kulipa milioni tano kwa BASATA endapo watamtumia msanii kufanya tangazo la aina yoyote, jambo ambalo limekuwa likipingwa na wasanii wengi nchini wakidai kuwa kwa kitendo hicho watakosa kazi. 

Kupitia kipindi cha Planet Bongo kilichorushwa Julai 10, 2018 na  East Africa Radio, BASATA ilitoa ufafanuzi juu ya suala hilo kuwa sio kweli kwamba msanii anatakiwa kulipa milioni 5 akifanya tangazo bali kampuni husika ndio inapaswa kufanya hivyo kwa kuwa wanaingiza kipato kikubwa kutumia tangazo hilo. 

Anusurika kifo kwa kutaka kufanya wizi wa Mtandao

$
0
0

Na manuel kaminyoge,Songwe, 
Kijana mmoja aliyefahamika kama Lusekelo Mwanjala (22) amenusurika kifo kutoka kwa raia wenye hasira kali baada ya kubainika akitaka kufanya wizi kwa njia ya mtandao kwa wakala wa tigopesa katika mtaa wa ilolo  mamlaka ya mji mdogo vwawa wilayani mbozi mkoani songwe. 

Kuwepo kwa mawasiliano ya mitandao mbalilmbali kumelaisisha mawasiliano katika jamii lakini kuna baadhi ya watu wamekuwa wakitumia vibaya mitandao hiyo kwa udanganyifu na kuwatapeli watu  kwa Njia ya mitandao hiyo.. 

Majira ya asubuhi katika mamlaka ya  mji mdogo  vwawa hali haikuwa nzuri kwa kijana lusekelo mwanjala (22)  ambaye amenusilika kifo kutoka kwa raia wenye hasira kali baada ya kubainika akitaka kufanya wizi  na udanganyifu kwa  njia ya mtandao kwa wakala wa tigopesa. 

Kufuatia tukio hilo baadhi ya wananchi na wafanyabiashara wa mamlaka ya vwawa wamesema kuwa wahalifu kama hao wachukuliwe hatua kali za kisheria huku wakitoa wito kwa jeshi la polisi kutowaachia huru watuhumiwa na utapeli. 

Kwa upande wake mwenyekiti  wa mamlaka ya mji mdogo wa vwawa  Ephrahim Mwakateba amewataka wafanyabiashara kuwa makini zaidi kwani matapeli wamekuwa wengi na wa aina mbalimbali huku afisa mtendaji wa kata ya ilolo Rehema Mwakilusya ametoa wito  kwa vjina kuachana na maswala ya wizi badala yake wajikite  kufanya kazi halali. 

Kwa upande wake  mkuu wa wilaya ya ileje ambaye ni kaimu mkuu wa wilaya ya mbozi Joseph Mkude amekemea uwepo wa wahalifu kama hao kwani wamekuwa wakiwaibia wananchi ikilinganishwa kuwa wengi wao hawana elimu juu ya  utapeli huo na kuwataka wananchi kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi. 

Baraza la Mtihani la Tanzania (NECTA) limezuia matokeo ya Kidato cha Sita

$
0
0

Baraza la Mtihani la Tanzania (NECTA) limezuia matokeo ya Kidato cha Sita

Katibu mtendaji wa baraza hilo Dkt. Charles Msonde.

Akitaja sababu za kuzuiwa kwa matokeo hayo, Katibu mtendaji wa baraza hilo Dkt. Charles Msonde wakati akitangaza matokeo hayo leo visiwani Zanzibar, amesema kuwa kuna baadhi ya watahiniwa walishindwa kukamilisha mitihani yao kutokana na sababu za kiafya na hivyo kufanya mitihani nusu, watapewa nafasi ya kurudia mwaka unaofuata.

Licha ya hiyo, Dkt. Msonde amesema kuwa ufaulu umeongezeka kutoka asilimia 96.06% mwaka 2017 hadi 97.12% mwaka huu, huku ufaulu katika masomo ya sayansi umeshuka ukilinganishwa na masomo ya sanaa na biashara.

“Jumla ya watahiniwa 83,581 sawa na asilimia 97.58 ya watahiniwa waliofanya mitihani ya kidato cha sita Mei mwaka huu wamefaulu huku wasichana wakiwa ni 34,358, na wavulana waliofaulu ni 49,223 pekee”, amesema Dkt. Msonde.

Dkt. Msonde ameongeza kuwa tathmini ya hali ya matokeo imeonesha kuimarika kwa ufaulu katika madaraja ya I,II na III ikiwemo kupanda kwa asilimia 1.80 kutoka 93.72 mwaka 2017 na kuwa asilimia 95.52 mwaka 2018.

Shule zilizofanya vizuri zimetajwa kuwa ni Kibaha, Kisimiri, Kemebos na Mzumbe, Feza Boys, Marian Boys, AHMES, St Mary's Mazinde Juu, Marian Girls & Feza Girls.

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0

KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME DR SITTA NDO SULULISHO LAKO tatiza, hili limekuwa likiwaasili watu wengi,sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine, kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo zipo , sababu nyingi zinazosababisha, tatizo hilo baadhi ni (i) upungufu wa vichocheo vya HORMONES ZA CETROGEN ambazo mwanaume, anapobarehe vichocheo hivi, HORMONES hizo, husaidia ukuaji wa uume 

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mlija iliysinyaa, 

NSHOLA ni dawa bora, ya kurudisha nguvu, za, kiume bari inatibu ,kabisa kutoa tatizo hilo, na kukupa , hamu ya , kurudia tendo, la ndoa zaidi, ya mala nne 4 ,bila kuchoka atakama unaumli ,wa mika 80,! pia ana ,dawa za ,kutibu, presha ya kupanda ,na kushuka, kisukari kuondoa, mafuta , mwilini ,na maumivu ya, mgogo kiuno, dawa zipo, matazo, ya hedhi, kwa ,wanawake hedhi, zisizokuwa na, mpangilio, na kasonono, pia , vidonda ,vya, tumbo ,(STOMACHI UCLENS) IHUSHI ndoji lako. 

NKANYA ni dwa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi ariyekuacha, mke mme, atakuludia kwa, mda, wa msaa3 tu , ukishaitumia atarudi ,mwenyewe bila ,ugovi tena, NKOMA ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada . 

HERBON, ni, dawa, ya kuongeza, CD4, NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu ,miguu, kufaganzi, na ,kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! DR SITTA, amebobea, kwa tiba asilia 

DAR ANAPATIKANA MBAGALA, ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI SHINYANGA, KAHAMA MJINI, KWA MAELEZO ZAIDI , 

PIGA SIMU 0763172670 au 0715172670 

WOTE MNAKALIBISHWA, KAMA, UTAKUWA NA TATIZOUTAHUDUMIWA

Amuua Mama Yake kwa Mapanga Kisa Mali za Urithi

$
0
0

MKAZI wa kijiji cha Ilebelebe wilayani hapo, Ngassa Mathias (24), anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga kwa tuhuma za kuhusika na mauaji ya mama yake mzazi, Nyawamba Dohoi (61), kwa kumcharanga mapanga kichwani hadi kufa.


Tukio hilo limetokea Julai 11, mwaka huu majira ya saa 10 usiku, wakati mama huyo akiwa amelala nyumbani kwake na wajukuu zake wawili.


Imedaiwa kuwa watu wasiojulikana waliingia ndani na kumshambulia mama huyo sehemu mbalimbali za mwili wake, ikiwamo kumkata kichwa kwa mapanga na kufariki dunia.


Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari jana, Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani hapo, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Simoni Haule, alisema chanzo cha tukio hilo ni kuwania mali za marehemu alizoachiwa na mumewe na mtoto huyo akidaiwa kutaka kuzimiliki.


“Tunamshikilia mtoto wa marehemu Ngassa Mathias kwa uchunguzi wa awali, inadaiwa ndiye mhusika mkuu wa mauaji ya mama yake mzazi kutokana na kutaka kurithi mali ambazo mama yake aliachiwa na mumewe na upelelezi ukikamilika na kubaini kufanya mauaji atafikishwa mahakamani,” alisema Haule.


“Natoa wito kwa vijana kujishughulisha katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo ikiwamo kilimo, na kuacha tabia ya kutaka mali za mirathi na kufikia hatua ya kutoa uhai wa wazazi wao,” aliongeza.


Aidha, Mwenyekiti wa kitongoji cha Kiloleli yalipofanyika mauaji hayo, Solo Bundala, alisema walibaini kufariki kwa mwanamke huyo majira ya saa tatu asubuhi na kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi.


Alisema kuwa katika kitongoji hicho kumekuwa kukitokea mauaji ya aina hiyo mara kwa mara.

Magufuli Atoa Agizo Hili kwa Baraza la CCM

$
0
0
Magufuli Atoa Agizo Hili kwa Baraza la CCM
Rais na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. John Magufuli amelitaka Baraza la Wadhamini la chama hicho kuhakikisha CCM inanufaika na mali zake na kuachana na utegemezi wa kuomba misaada kutoka kwa watu.

Dkt. Magufuli ametoa kauli hiyo wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na wajumbe wa Baraza hilo jipya ambao ni Anna Margareth Abdallah (Mwenyekiti), Ndg. John Zephania Chiligati, Jaji Mstaafu Mark Bomani, Balozi Mstaafu Daniel Ole Njoolay, Pandu Ameir Kificho, Christopher Gachuma, Dkt. Haruni Kondo na Hassan Omar Mzee, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

"Katekelezeni majukumu yenu ipasavyo, ikiwemo kusimamia mali zote za CCM na jumuiya zake, kufanya tathmini ya mara kwa mara ya mali za CCM na jumuiya zake, kutoa ushauri juu ya mabadiliko yoyote yanayohitajika katika umiliki wa mali za CCM na jumuiya zake na mutekeleza majukumu mengine ambayo nitakabidhiwa na Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa. Sitarajii kuona dosari za usimamizi wa mali za chama zikiendelea",amesema Magufuli.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa baraza hilo Ndg. Anna Margareth Abdallah amemshukuru Rais Magufuli kwa kuwaamini na kuwateua kuunda baraza hilo na kumuahidi kuwa watahakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa umakini na kwa maslahi ya CCM.

"Mambo hayatakuwa kama walivyozoea huko nyuma kwamba kila mtu anamiliki kipande chake cha mali za chama, hapana, mali zote za chama ni mali ya Baraza la Wadhamini wa Chama Cha Mapinduzi", amesema Anna.

Naye, Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Bashiru Ally amesema baraza la hilo ni la kwanza kuundwa baada ya kufanyika marekebisho ya katiba ya CCM, litasimamia mali za CCM pamoja na kusimamia utekelezaji wa mapendekezo ya tume ya kufuatilia mali za chama ambayo yeye alikuwa mwenyekiti.

Uwanja wa Ndege wa Mwanza Kufanyiwa Ukarabati wa Haraka Kwaajili ya Kupokea Ndege Mpya ya Boeing 787-8 Dreamliner

$
0
0
Uanja wa Ndege wa Mwanza Kufanyiwa Ukarabati wa Haraka Kwaajili ya Kupokea Ndege Mpya ya Boeing 787-8 Dreamliner
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isaack Kamwele ameuagiza uongozi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini (TAA), kuufanyia ukarabati wa haraka uwanja wa ndege wa Mwanza tayari kwa ajili ya uzinduzi wa safari za ndege mpya aina ya Boeing 787-8 Dreamliner Julai 29.

Mhandisi Kamwele ametoa maagizo hayo leo Julai 13 jijini Mwanza alipotembelea taasisi na kukagua miradi iliyoko chini ya Wizara hiyo.

Amesema Serikali pia itatekeleza ujenzi na ukarabati wa viwanja vingine tisa nchini kufikia viwango vya kuruhusu safari za ndege zote kubwa na ndogo.

Ametaja baadhi ya viwanja hivyo kuwa ni pamoja ni Songwe-Mbeya, Mtwara, Musoma, Kigoma, Songea, Shinyanga, Geita na Tabora.

Waziri huyo pia ameuagiza uongozi wa Shirika la ndege nchini (ATCL), kurekebisha mfumo wa ukataji wa tiketi, hasa kupitia kwa Mawakala ili kudhibiti ongezeko la bei kulinganisha ille inayotangazwa na shirikali hilo.

“Baadhi ya mawakala huwatoza wananchi kati ya Sh400, 000 hadi Sh500, 000 kwa safari kulinganisha bei inayotangazwa na shirika la Sh260, 000; nitoa muda wa wiki tatu mchezo huu ukomeshwe,” amesema.

Waziri huyo pia ametembelea bandari ya Mwanza pamoja na shirika la reli.

Hizi Hapa Sababu za Barack Obama Kupoteza Wafuasi Milioni Mbili Kwenye Twitter

$
0
0
Hizi Hapa Sababu za Barack Obama Kupoteza Wafuasi Milioni Mbili Kwenye Twitter
Watu mashuhuri walio na wafuasi wengi sana kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter wamepoteza mamilioni ya wafuasi baada ya kampuni hiyo kuanza kuondoa 'watu bandia'.

Rais wa zamani wa Marekani Barack Obama ni miongoni mwa walioathirika, ambapo amepoteza watu 2.1 milioni.

Bw Obama, ambaye babake alitokea Kenya, amepangiwa kuzuru tena taifa hilo la Afrika Mashariki Jumatatu 16 Julai, ziara yake ya kwanza tangu andoke madarakani.

Mwanamuziki nyota kutoka Marekani Katy Perry, ambaye ndiye mtu anayefuatwa zaidi kwenye Twitter, na Lady Gaga wamepoteza takriban wafuasi 2.5 milioni kila mmoja.

Twitter imesema imechukua hatua hiyo kutokana na juhudi zake ambazo zimekuwa zikiendelea za kujenga imani miongoni mwa wanaotumia mtandao huo.

Hii imetokea huku mitandao ya kijamii ikiendelea kuangaziwa kutokana na kueneza kwa taarifa za uzushi na watumizi feki wa mitandao ya kijamii.

Hatua mpya zilizochukuliwa na Twitter zinaathiri akaunt za Twitter ambazo zimefungwa kutokana na kutokea kwa shughuli zisizo za kawaida kwenye akaunti hizo.

Mfano wa shughuli hizi ni kufungiwa na watu, au kutuma ujumbe kwa wingi wakati mmoja mtandaoni. Aidha, kuna akaunti za watu ambao hawakujibu walipotumiwa ujumbe wa kuthibitisha utambulisho wao.

Akaunti hizi zote zinaondolewa kutoka kwenye hesabu ya watu wanaofuata akaunti mbalimbali.

Hili limeathiri watu kote duniani. Nchini Kenya, baadhi wamekuwa wakieleza idadi ya wafuasi waliowapoteza, ingawa kwa wengine idadi inashangaza.

Hatimaye Mke wa Ephraim Kibonde Azikwa Makaburi ya Kinondoni

$
0
0
Hatimaye Mke wa Ephraim Kibonde Azikwa Makaburi ya Kinondoni
Familia, ndugu, jamaa na marafiki wa karibu na mtangazaji Ephraim Kibonde wameuaga na kuuzika mwili wa marehemu Sara Kibonde ambaye ni mke wa mtangazaji Kibonde nyumbani kwake, Ubungo Kibangu na kisha baadae kuupumzisha mwili wake katika makaburi ya Kinondoni.

Sara na Kibonde wametimiza miaka 20 ya ndoa uku wakiwa jumla ya miaka 30 ya uhusiano ikiwa wameshawahi kuwa wapenzi miaka 10 kabla ya ndoa na kubahatika kupata watoto watati wawili wa kike na mja wa kiume.

Sara Kibonde amefariki dunia usiku wa Jumanne, Julai 10, 2018, katika Hospital ya Hindu Mandal akipatiwa matibabu.

Ongeza Uume, Nguvu na Hamu ya Tendo la Ndoa Hata Kwa Wenye Kisukari na Pressure

$
0
0

Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume au ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa limezidi kuongezeka kwa kasi duniani kote na limekuwa chanzo kikubwa cha ndoa nyingi na mahusiano kukosa uaminifu kutokana na wengi kutoka nje ya ndoa ili kupata mtu atakayemtosheleza na kumfikisha kileleni. Pia udogo wa maumbile ni tatizo kubwa na limekuwa likiwakosesha wanaume wengi uwezo wa kujiamini katika tendo na kusababisha tendo hilo kutokufanyika kwa usahihi. Hili pia huchangia kwa kiasi kikubwa wanawake wengi kwenda nje ya ndoa ( MAHUSIANO) kutafuta mbadala wake. 
BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:- 
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa 
☆Uume kusimama kwa ulegevu 
☆Kuwahi kufika kileleni 
☆Uume kusinyaa katikati ya tendo 
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati 
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa. 

Kwa kutumia mimea tiba na matunda bila kemikali sasa 
@markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:- 
1.HANDSOME UP ORIGINAL:- kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250,000/= 
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 5.5 hadi 6 @150,000/= 
3.VigRX CREAM:- ni gely iliyoboreshwa mahususi kwa ajili ya kuongeza maumbile kwa wastani wa inch 6.5 hadi 8 na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200,000/= 
4.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150,000/= 
5.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kuweza kurudia tendo ×3. @150,000/= 
BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA KIAFYA NA ZIMETHIBITISHWA 
NA SHIRIKA LA AFYA DUNIANI (WHO). 
KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :- 
@markson_beauty_pr 
@markson_beauty_pr 
@markson_beauty_pr 
WEB:www.markbeauty.org 
Wasiliana nasi Popote 
ulipo duniani kwa (+255) 
0767447444 na 
0714335378 
UTAPATA HUDUMA 
NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako. 
#OngezaUume 
#NguvuZaKiume 
#HandsomeUpOg 
#BidhaaTz

Wakili afungua kesi akihoji matokeo ya urais kutopingwa mahakamani

$
0
0

Wakili wa kujitegemea jijini Dar es Salaam, Jebra Kambole amefungua kesi katika Mahakama ya Afrika na Haki za Binadamu (AfCHPR), akiiomba iamuru matokeo ya urais nchini yapingwe mahakamani.


Kambole aliwasilisha maombi ya kufungua kesi hiyo katika mahakama hiyo Julai 4 na juzi ilimwandikia barua kumtaarifu kuwa imepokea maombi yake na kuyasajili kwa namba 018 ya mwaka 2018.


Naibu msajili wa mahakama hiyo, Nouhou Diallo alithibitisha jana kupokewa na kusajiliwa kesi hiyo.


Katika maombi hayo dhidi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kambole anapinga ibara ya 41 (7) ya Katiba ya nchi ya mwaka 1977 inayozuia matokeo ya urais yakishatangazwa kupingwa mahakamani.


Ibara hiyo inasomeka, “Iwapo mgombea ametangazwa na Tume ya Uchaguzi kwamba amechaguliwa kuwa Rais kwa mujibu wa ibara hii, basi hakuna Mahakama yoyote itakayokuwa na mamlaka ya kuchunguza kuchaguliwa kwake.”


Kambole anadai kitendo cha Serikali kuruhusu Katiba yenye ibara inayozuia mtu asiyeridhika na matokeo ya urais kuyapinga mahakamani kinakiuka ibara za 1, 2, 3 (2) na 7(1) (a) za Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu.


Anadai Serikali imeshindwa kutekeleza wajibu wake chini ya mkataba huo wa Afrika kama mwanachama wa Umoja wa Afrika, kutambua haki, wajibu na uhuru unaolindwa na mkataba na kuchukua hatua kulinda haki hizo.


Kambole anasema Tanzania ilipata uhuru mwaka 1961 na ni nchi mwanachama wa Umoja wa Afrika ikiwa mshirika katika Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu.


Anadai ukiukwaji anaoulalamikia wa haki ambazo zinalindwa na mkataba hadi sasa unaendelea kutokea katika mipaka ya eneo la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Anaiomba mahakama iamuru kwamba Serikali inakiuka ibara ya 1, 2, 3(2) na 7(1) ya Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na iweke kwenye Katiba na sheria hatua za kuhakikisha haki zinazotolewa katika mkataba huo zinalindwa.


Pia, anaiomba mahakama iiamuru Serikali kutoa taarifa mahakamani hapo ndani ya miezi 12 tangu kutolewa kwa hukumu, kuhusu hatua za utekelezaji wa hukumu na matokeo ya amri za mahakama.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images