Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104706 articles
Browse latest View live

Kiongozi wa Upinzani Nchini Zimbabwe "Jina la Zimbabwe Limelaaniwa Libadirishwe''

$
0
0
Kiongozi wa Upinzani Nchini Zimbabwe "Jina la Zimbabwe Limelaaniwa Libadirishwe'
Kiongozi wa upinzani Zimbabwe Nelson Chamisa ameapa kuwa atalibadilisha jina la nchi hiyo na kuwa "Great Zimbabwe" akieleza kuwa jina la sasa la nchi hiyo lina 'laana', kwa mujibu wa mtandao wa New Zimbabwe.

"Zimbabwe haiwezi kusalia kuwa Zimbabwe, kwasababu imegeuzwa kuwa gofu la Zimbabwe," Chamisa aliwaambia maelfu ya wafuasi katika mkutano wa kisiasa mashariki mwa mji wa Mutare.

"Jina la Zimbabwe limelaaniwa kama mnavyoona timu yetu ya taifa ya soka inashindwa kila saa katika mechi - kriketi tunashindwa, voliboli daima inashindwa," aliongeza kusema.

Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 40 ananuia kuwa rais katika uchaguzi mwishoni mwa mwei huu Julai 30 - uchaguzi ulio wa kwanza baada ya kiongozi wa muda mrefu Robert Mugabe kuondoka madarakani.
.

Zimbabwe ilijulikana kama Rhodesia kusini kati ya mwaka 1898-1964, ambalo ni jina la Mkoloni wa Uingereza Cecil Rhodes. Mapema 1960, however, raia wenye utaifa walianza kuliita taifa hilo Zimbabwe. Jina linalotokan ana maneno mawili "dzimba" na "dzamabwe" (yenye maana ya nyumba ya mawe) kwa lugha ya Shona inayozungumzwa pakubwa hivi leo Zimbabwe.

Amber Lulu Amuomba Daimond Kumsajili WCB "Mzee wa Vikuku si Niwe Msanii Wako au Unasubiri Uvae Kikuku cha Pili"

$
0
0
Ni kweli Amber Lulu anahitaji kusaidiwa na label ya WCB ya Diamond au alimua kumpiga dogo muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na video ya wimbo, Baila.


Muimbaji huyo ametumia picha ya Diamond iliyozua gumzo kwenye mitandao ya kijamii tangu juzi kama fursa ya kumwaga ombi lake hadharani ili limfikie Bosi huyo wa WCB.

Juzi, Diamond alizua tafrani mitandaoni alipoweka kipande cha video kinachomuonesha akiwa anapiga kazi jukwaani nchini Marekani lakini mguuni amevaa cheni, mtindo ambao ni maarufu kwa wakaazi wa Pwani kama Kikuku, na mara nyingi huvaliwa na warembo.


Hata hivyo, Diamond alikazia zaidi kwa kupost picha nyingine ikimuonesha ametulia baada ya kazi lakini ‘kikuku’ kilionekana kwa ukaribu zaidi mguuni kwake. Huenda Mkali huyo wa Baila alitumia mazingira sahihi kufanya kile ambacho ni kawaida kwa Wamarekani aliokuwa anawapigia show, lakini tafrani nyumbani. Wasanii kama Fabolous na wengine wamekuwa wakivaa Kikuku mara kwa mara wanapokuwa jukwaani.

Amber Lulu alitumia picha hiyo kumuomba Diamond kumpa nafasi ya kuwa Bosi wake na kumuomba ampe mkataba wa kuwa mmoja kati ya wasanii walio chini ya lebo ya Wasafi Classic Baby (WCB). Hakika alijua picha hiyo maarufu itabeba ujumbe wake na kuufikisha mbali.

“Sema mzee wa vikuku, si niwe tu msanii wako jamani kwani unasubiri mpaka uvae kikuku cha pili @diamondplatnumz,” ameandika Amber Lulu.

Amber Lulu ambaye wimbo wake ‘Jini Kisirani’ ulipata mafanikio makubwa zaidi katika muziki wake ukitazamwa zaidi ya mara 2,000,000 kwenye YouTube, sio msanii pekee mwenye kiu ya kujiunga na lebo ya WCB.

Related Articles

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume, nasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za:

GUMBA POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.

NTINJE:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0754741788, 0715741788, 0783741788

-DR MAGISE

Breaking News: Serikali Yatoa Ajira 4,840 za Walimu, Zisome Hapa

Kisa Kikuku Alichovaa Diamond, Vanessa Mdee Ampiga Mkwara Mkali Jux

$
0
0
Staa wa Muziki wa Bongo fleva Vanessa Mdee ‘Vee Money’ ameweka wazi kuwa amemchimba mkwara mzito mpenzi wake Jux kuhusiana na kuvaa kikuku.

Kwenye mahojiano na Wasafi Tv, Vanessa amefunguka kuwa uvaaji wa vikuku sio utamaduni wa wanaume wa Kitanzania hivyo hawezi pendezwa na utamaduni huo kwa madai umamshushia heshima mwanaume.

Kusema kweli Jux hawezi kuvaa kikuku  Sidhani kama inaendana na tamaduni zetu. Vikuku ni kwaajili ya wasichana, sipendi japo naona kuna watu wengi wanavaa”.

Vanessa aliongeza kuwa;

Kiukweli kuna msanii wa Marekani anampenda Jux anaitwa Fabulous, na yeye nahisi anavaa kikuku, nikasema nini hiki, nikamwambia ole wako na wewe uvae”.

Siku chache zilizopita Staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz alizua gumzo Kwenye mitandao ya kijamii baada ya kuonekana akiwa amevaa kikuku Kwenye mguu jambo ambalo watu wengi halikuwavutia.

Calisah Aongea Mazito Kuhusu Kuwapa Ujauzito Wadada wa Mjini "Ambao ni Wazuri Nawapitia Wabaya Nawapotezea

$
0
0
Kijana anaesifika kwa kazi yake nzuri ya modelling, Calisah amaefunguka na kusema kuwa amekuwa akiwapa mimba wadada wengi wa mjini mabao wamekuwa wakimuomba kufanya hivyo karibia kila siku.

Akiongea na mtangazaji wa Dizzim online , Calisah anasema kuwa wadada wengi wamekuwa wakimsumbua sana kufanya nao mapenzi ili wapate mimba yake na yeye hana kinyongo na hilo kabisa kwa kuwa anaamua kuwasaidia kama binadamu.

nimewatoa wadada wengi sana mimba na wengine wamekuwa wakinimba niwape, wako wanawake wengi sana  ambao wamekuwa wakiomba niwape mimba wanakaribia hat 25, hata nikikuomyeshea kwenye simu yang wapo wapo.(huku akifungua simu yake), na pia huwa naangalia mi mwenyewe kwa sababu hata mimi nina tamaa vilevile kwaio naangalia kama mzuri napita na wewe kama mbaya naachana na wewe.sina uwezo wa kuwalea wote hao  ila hata mimi niko kwenye mchakato so soon ntapata mtoto.

Mchepuko Adaiwa Kuwa Tishio Kwenye Ndoa Ya Dogo Janja na Uwoya

$
0
0

Mchepuko Adaiwa Kuwa Tishio Kwenye Ndoa Ya Dogo Janja na Uwoya
Ndoa ya staa wa Bongo fleva Dogo Janja anayefanya vyema na wimbo wake wa ‘Banana’ na Bongo Movie Star Irene Uwoya yadaiwa kupumulia mashine huku mchepuko akiwa chanzo.

Global Publishers wanaripoti kuwa ndoa Changa ya mastaa hao imedaiwa kuingia jini mkata kamba baada ya Mrembo anayeitwa Dayana kudaiwa kuwa na mawasiliano ya karibu na Dogo Janja.

Chanzo cha karibu cha couple hiyo kiliitonya GPL kuhusiana na tatizo katika Ndoa hiyo ya Dogo Janja na Uwoya:

Fuatilieni, Uwoya na Dogo Janja hawako sawa kabisa chanzo ni Dayana, nasikia wanawasiliana sana na mara kadhaa Dogo Janja ameshindwa kuvumilia hadi kumposti kimafumbo kwenye ukurasa wake wa Instagram”.

Baada ya Tetesi hizo Dayana alidaiwa ili kujibu tuhuma hizo lakini hakutaka kukubali wala kukataa lakini alimpa ujumbe mzito Uwoya:

Ningepanda sana kumshauri dada yangu Uwoya kuwa kwanza amsihi mumewe asiwe ananisumbua kwa simu kwa sababu mimi niko na mtu mwingine lakini najua atapata naye tabu sana kwa sababu Dogo Janja bado mdogo hivyo bado hajafika kwenye safari ya mapenzi.

Nafikiri ingekuwa vizuri kabisa Uwoya angemtafuta mtu ambaye analingana naye lakini hivi sio sawa atapata tabu sana ni bora kuwa na mtu mzima mwenzake”.

Baada ya GPL kuzungumza na Dayana, lilimtafuta Uwoya ili kusikia anamzungumziaje ‘mwizi’ wake ambaye pia amempa ushauri ambapo alipopatikana hakutaka kufunguka kwa kirefu zaidi ya kusema amepokea ushauri wake.

Sidhani kama kuna kitu kikubwa cha kusema ila tu nashukuru ushauri wake nimeupokea nitaufanyia kazi“.

VIDEO: Mabadiliko Shule ya Jangwani Walimu kuhamishwa, mlinzi nae OUT kisa kuwarubuni wanafunzi

$
0
0
Baada ya matokeo mabaya ya Kidato cha sita shule ya Wasichana Jangwani iliyopo jijini Dar es salaam, leo Julai 17 Waziri wa Nchi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Seleman Jaffo ametembelea shule hiyo na kutoa maagizo ikiwemo walimu wote waliofundisha mda mrefu (wahanga) kuhamishwa huku mlinzi ambae alikuwa anawarubuni wanafunzi nae kutolewa mara moja.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......USISAHAU KUSUBSCRIBE


Steve Nyerere Ampa Makavu Billnass "Kidogo Unaweka Matanga Watu Wameibiwa Wake Zao na Wanapambana na Hali Zao"

$
0
0
Steve Nyerere Ampa Makavu Billnass "Kidogo Unaweka Matanga Watu Wameibiwa Wake Zao na Wanapambana na Hali Zao"
Msanii wa bongo movie Steve Nyerere ameamua kumpa ukweli msanii wa bongo fleva  Bill Nass na kumwambia kazi sio kiki bali afanye kazi hii yote imetokea baada ya kumuona analalamikia wimbo wake kufutwa you tube.

Steve ametumia ukrasa wake wa instagramu kuandika Hivi:

 "Embu fanya mziki acha kulia lia mara nimeibiwa follows kwenye akaunt ya You tube yani unashindwa kuvumiliaaa watu wameibiwa wake zao na wanapambana na hali zao,Wewe kidogo tu umeweka na turubai daaaaaaaa .sasa ushauri wangu imba imba imba kijana wangu .unaskia baba fanya mziki kuwa kazi sio kiki sawa kijana kwa hii ngoma nimekusameee ata yaleee mambo

Kylian Mbappe Atoa Msaada Pesa Zote Alizozipata Kwenye Kombe la Dunia

$
0
0
Kylian Mbappe Atoa Msaada  Pesa Zote Alizozipata Kwenye Kombe la Dunia
Mchezaji wa timu ya taifa ya Ufaransa, Kylian Mbappe ameonyesha moyo wa kipekee baada ya kutoa msaada fedha zote alizopata kwenye michinuano ya kombe la dunia dola 550,000 sawa na bilioni 1.2 za Kitanzania kwa kituo kinachotoa huduma ya michezo kwa watoto wenye ulemavu.



Mbappe mwenye umri wa miaka 19 ametoa kiasi hicho cha dola za Kimarekani 550,000 ambazo zinatokana na posho pamoja na ‘bonus’ ya ushindi wa kombe la dunia mwaka huu 2018.

Mchezaji huyo amefunga jumla ya mabao manne kwenye michuano hiyo akiitumikia timu yake ya taifa ya Ufaransa ametoa fedha hizo kwenye kituo cha Premiers de Cordee kinacho husika na kutoa bure huduma za michezo kwa watoto wasio na uwezo wa kumudu gharama pamoja na wanamichezo watoto wenye ulemavu.

Kwa mujibu wa kituo cha habari cha L’Equipe kutoka nchini Ufaransa kimeeleza kuwa Mbappe hajabakiza hata kiasi kidogo cha fedha hiyo aliyopata kwenye kombe la dunia ambayo ni dola 22,500 kwa michezo iliyoshiriki timu ya Ufaransa na dola za Kimarekani 350,000 kama ‘bonus’ baada ya Les Bleus kushinda taji baada ya kuifunga Croatia jumla ya mabao 4 – 2.

Yanga Yajipanga Kupambana na Gor Mahia Kesho

$
0
0
Yanga Yajipanga Kupambana na Gor Mahia Kesho
Kikosi cha Yanga kinafanya maandalizi ya mwisho leo kwa ajili ya mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Gor Mahia FC utakaopigwa kesho jijini Nairobi, Kenya.

Yanga inaenda kucheza mechi hiyo ikiwa na kumbukumbu za kwenda suluhu tasa ya 0-0 dhidi ya Rayon Sports ya Rwanda ambayo wapo nayo kundi moja (Kundi D), mchezo uliopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mechi ya keshio itawapasa Yanga kuhakikisha wanapata ushindi kujiwekea mazingira ya kusalia kwenye michuano hiyo ambapo hivi sasa bado wana alama moja pekee katika msimamo wa kundi hilo.

Ikumbukwe Yanga ilipoteza dhidi ya MC Alger kwenye kibarua cha kwanza pia suluhu dhidi ya Rayon na kuwafanya kuwa kwenye mazingira magumu kunako kundi D.

Dawa pekee ya Yanga kujipa matumanini ni kuhakikisha inawafunga Gor Mahia kesho kisha kuanza maandalizi mengine ya mchezo wa mkondo wa pili utakaopigwa Dar es Salaam.

Yanga itashuka dimbani bila wachezaji wake mabeki Hassan Kessy na Yondani ambao imeelezwa wamebaki Dar es Salaam wakihitaji kuongezewa mikataba mipya.

Kigwangala Awaamrisha Polisi Kuwadaka Makada wa CCM

$
0
0
Katibu wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Wilaya ya Tarime, Newton Mongi na Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya chama hicho wilayani humo, Richard Tiboche wanashikiliwa na polisi kwa amri ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla.

Amri ya kukamatwa kwa viongozi na makada hao wa CCM ilitolewa na Waziri huyo jana Julai 16,2018 wakati wa ziara yake ya kukagua maeneo yenye migogoro kati Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (Senapa) na vijiji vya kata za Nyanungu, Gorong’a na Kwiwamcha wilayani Tarime.

“RPC (Kamanda wa Polisi mkoa) mtie mbaroni huyo kiongozi wa UVCCM kwa kuitukana Serikali. Mkuu wa mkoa mnakaaje na watu kama hawa; mwajiriwa anayelipwa mshahara wa CCM anawezaje kuitukana Serikali ya chama ambacho yeye ni mtumishi wake?” aliamuru Dk Kigwangala na kuongeza:

“Nimemsikia kwa maskio yangu akiitukana Serikali ya CCM ambayo yeye ni kada na kiongozi wake. Kamata na afikishwe mahakamani.”

Amri hiyo ilitekelezwa mara moja na askari polisi waliokuwepo kwenye msafara huo kwa kiongozi huyo kuwekwa chini ya ulinzi huku mwenzake ambaye hakuwepo eneo hilo wakati huo alikamatwa baadaye.

Hata hivyo, hakujulikana mara moja maneno yaliyotamkwa na viongozi hao wa CCM yaliyotafsiriwa na Waziri Kigwangala kama matusi kwa Serikali.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Mara, Athuman Mkilindi ambaye yuko kwenye ziara ya Waziri amesema hajui makosa yaliyosababisha amri ya kuwatia mbaroni makada hao wa chama kutolewa na kushauri atafutwe Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Tarime/Rorya, Henry Mwaibambe kwa ufafanuzi kwa sababu ndiko makosa yalikotendeka.

Mwananchi lilipomtafuta Mwaibambe alisema makada hao wanashikiliwa na uchunguzi dhidi yao unaendelea.

 “Ndiyo yuko kwenye uchunguzi lakini inadaiwa kuwa alimkashifu Waziri wa Maliasili,” alisem

Tunatibu Na Kuponesha Kabisa Upugufu wa Nguvu za Kiume, Busha, Kisukari na Vidonda vya Tumbo

$
0
0
TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO? BUSHA BILA KUPASUA KISUKALI NA VIDONDA VYA TUMBO? asilimia kubwa ya wanaume wanaupungufu wa nguvu za kiume NA maumbile madogo NI NINI KINACHOSABABISHA UUME KUZIDI KUWA MDOGO NA WEMBAMBA 1 kuugua chango LA uzazi 2 unene kupita kiasi 3 kuvaa nguo au chupi za kubana 4 kupiga punyeto kwa mda mrfu ,NI NINI TIBA YAKE MAKAKANUA MIX nidawa ya mitishamba iliyochanganywa NA mizizi kumi NA mbili urfusha NA kunenepesha UUME saizi upendayo ich 5,6,7, NA 8 kwa urfu NA sentimita 3,4, na 5 ipo dawa ya kunywa na kupaka NI NINI KINASABABISHA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME 1 kupungukiwa kwa homoni ya testerone 2 kuhudhurika kwa Neva au uti wa mgongo 3 utumiaji holela wa madawa ya kizungu 4 usongo wa mawazo na asira 5 utumiaji wa vyakula vya mafuta mengi NI NINI TIBA YAKE MAPRO POWER NO 2 NDIO tiba tosha kwa sasa kwani utibu matatizo matatu kwa pamoja 1 itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15 adi 20 ,2 itakufanya urudie tendo zaidi Mara tatu 3 uhimalisha uume uliolegea na kusinyaa OKOA NDOA YAKO SASA ujihepusha na lawama ndani ya ndoa yako au pale ukutanapo na mpezi dawa hii itamfanya mpenzi wako hakueshimu na hasitoke nnje ya ndoa na ata wazee wenye umri mkubwa wanapona zipo dawa za kupunguza kitambi,minyama uzembe, presha ,kisukar mvuto wa mpezi au biashara FIKA OFISINI KWETU MBAGALA ZAKHEMU na wateja wa kanda ya ziwa yupo wakala wetu mwanza mjini au piga simu 0752348593

DR MABULA na utaletewa popote ulipo uduma hizi

Lugola "Sitaki Kuona Wafungwa Wanakula Bure Bila Kufanya Kazi"

$
0
0

DAR: Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amewekea msisitizo kauli ya Rais Magufuli kuhusu wafungwa akisema hataki kuona wafungwa wanaishi kama ndege wa angani, akimaanisha kuwa wanakula bure bila kufanya kazi

Amesema Wafungwa wanatakiwa wafanye kazi na kujitafutia chakula wao wenyewe badala ya kusubiri kupewa chakula na Serikali

Amesema “Hata kama ni meno, lazima walimie meno, watatumia meno yao kulima mahindi, kulima maharage ili wajilishe, na nimemwambia Inspekta Jenerali wa Magereza, katika hili sitaki kisingizio cha aina yoyote"

Aidha, amewaagiza wasaidizi wake kupitia sheria vizuri na kumpelekea mpango mzuri wa kuwatumia wafungwa kufanya kazi za kilimo na ufugaji na kujitafutia chakula wao wenyewe

Ameongeza kuwa utoaji wa chakula bure gerezani umepelekea baadhi ya wafungwa kuona gerezani kama ndiyo sehemu ya kupumzika na kula bure bila kufanya kazi, hivyo hufanya makosa ya makusudi ili kurudi gerezani

Maiti Yazungumza Kabla ya Kuzikwa..Yamtaja Aliyemtoa Kafara

$
0
0

MACHAKOS. Watu wengi waliohudhuria mazishi walisalia vinywa wazi kusikia sauti kutoka kaburini, baada ya mwili wa msichana mmoja aliyekuwa kafariki katika ajali ya barabarani kumtaja mjomba wake kuwa ndiye aliyetumia kafara kumuua ili atajirike

Maeneo ya Masii, Machakos nchini Kenya, kilizuka kioja katika mazishi ya mwanadada huyo aliyefariki katika ajali ya barabarani. Inadaiwa kuwa mwanadada huyo mwenye umri wa miaka 27 alikuwa akiishi na mjomba wake mjini Voi kabla ya kifo chake.

Kulingana na kisa hicho kilichochapishwa katika gazeti la “Taifa Leo” la nchini humo, mwanadada huyo alifariki katika ajali ya barabarani na mwili wake kupelekwa katika mochwari ya eneo hilo na kwa muda wa mwezi mmoja mwili haukutambuliwa wala hakuna ndugu yeyote aliyejitokeza hapo.

Baadae wahudumu wa mochari hiyo waligundua baada ya mwezi mmoja kuwa maiti huyo alikuwa na kitambulisho mfukoni mwake, walitumia kitambulisho hicho kuwatafuta jamaa wake.

Limekuwa ni jambo la kustaajabisha wengi hasa majirani na ndugu zake huyo binti kwa sababu mjomba aliyekuwa akiishi na msichana huyo hakutoa habari zozote kuhusu kutoweka kwa msichana huyo.

“Licha ya kukosa kurudi nyumbani na kuwasiliana naye, mjomba hakushugulika kujua aliko hadi polisi walipowasiliana na familia yake,” Mmoja wa watu waliokuwa msibani aliongezea.

Watu walisalia kimya hadi siku ya mazishi huku kioja kikizuka wazi. Shuguli ya mazishi ilipoanza waombolezaji walishangazwa na sauti iliyokuwa ikitoka kaburini. Maiti alianza kuzungumza huku akieleza jinsi mjombake alivyopanga kifo chake kwa kutumia ndumba ili apate mali.

Alisema kuwa alikuwa ametolewa kafara jambo lililopelekea hasira kupanda kwa waombolezaji na kutaka kumvamia mjomba huyo, ijapo maafisa wa polisi walifika hapo upesi na kumuokoa.

Huwezi Amini Gwajima atuma pongezi kwa familia ya Makonda

$
0
0
Mwanasheria na kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Methusela Gwajima ,ameipongeza familia ya Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam  Paul Makonda kwa kupata mtoto wa kiume.

Gwajima ametoa pongezi hizo katika ukurasa wake wa Mtandao wa kijami wa INSTAGRAM  leo  na kusema kuwa mengi yalisemwa lakini Mungu ni anatosha.

"Hongera sana ndugu zangu kwa kupata zawadi ya mtoto mengi yalisemwa lakini  kwa hakika Mungu wetu anatosha kwani hujibu kwa wakati wake maombi daima ni silaha bora kwa aduizetu'. ameadindika Gwajima.

Itakumbukwa kuwa Gwajima  na Makonda ni marfiki wa muda mrefu wakati wa shida naraha ,marakwa mara amekuwa akiamini utendaji kazi wa Paul Makonda kuwa ni kiongozi ambaye ni mfano wa kuigwa  na  kusisitizakuwapuuza maadui wasiomtakia mema katika utumishi wakeulio tukuka.

Sheikh Kipozeo afunguka baada ya kusikia Diamond kavaa ‘kikuku’ (Video)

$
0
0
Sheikh Kipozeo ambaye amekuwa akitoa mawaidha katika mambo ya maadili, amefunguka ishu ya wanaume kuvaa cheni miguu ambapo amedai wanaume wanaojifanisha na wanawake kwa kuvaa cheni wamelaaniwa na Mwenyezi Mungu. Kipozeo amesema sio kwa Diamond tu wanaume hawaruhusiwi kuvaa vitu ambavyo vinavaliwa na wanawake.

VIDEO:

Fahamu Vigezo Sita Vikubwa Vinavyoweza Kumfanya Mwanamke Kukukimbia Au Kukuacha Kabisa...!!!

$
0
0
1. Wakikosa attention yako. Wasichana hupenda pale wanapofahamu kuwa unawasikiliza na unafahamu nini wao wanahitaji. Kama kutakosekana mawasiliano mazuri na atagundua hilo atauona uhusiano huo haumtimilizii haja zake. Hata kama kila kitu kinaenda sawa. Msikilize anapoongea. Kama akiona hapati penzi analolihitaji atatafuta mwingine ambaye yupo tayari kumtimizia.

2. Kumuheshimu. Msichana huwa anajitoa sana awapo katika mahusiano hivyo anategemea mvulana uheshimu hata kwa chochote kidogo anachokufanyia. Mfanye agundue kuwa umeheshimu kile ambacho amekufanyia.

3. Usaliti. Unaposaliti inamaanisha kuna kitu hakipo sawa katika mahusiano yako hata kama una uwezo wa kushughulikia lakini wewe unaona njia sahihi ni kutoka nje kuwa na mahusiano na msichana mwingine ukidhani ndio unarekebisha. Pale msichana wako akikukamata unamsaliti fahamu hawezi kuvumilia naye atakuacha.

4. Ukosefu wa hisia za kimapenzi. Msichana hupenda kuona kuwa wanapendwa wanathaminwa na wapenzi wao wanawajali sasa wakiona kuwa hakuna conection ya hisia za kimapenzi kutoka kwa mvulana wake huona kuwa hakuna mapenzi ya kweli katika uhusiano aliopo

5. Hawapendi kusikia kuhusu mapenzi mara kwa mara wasichana hupenda kutumia muda mrefu na wapenzi wao bila kusikia neno la kuwataka wafanye mapenzi kama ukiwa nao na ukawataka kimapenzi mara kwa mara watakuwa wanakuavoid hata utakapokuwa ukiwagusa.

6. Unapomcontrol sana
msichana humpenda mvulana atakayemlinda na kujiona yupo sehemu salama sio kumdhibiti kufanya mambo yake mengine anapenda uhuru.

Kwa Taarifa Yako Tu..Hiki Ndicho Ambacho Wanawake Huvutiwa na Kukipenda Kutoka kwa Wanaume ,Kama Huna Jitahidi Kuwa Nacho...!!!

$
0
0
Kama mwanaume lazima upate wakati wa kujua unatakiwa kufanya nini kwa ajili ya kulifanya penzi lako lizidi kuchanua.

USAFI BINAFSI

Asilimia kubwa ya wanawake wanapenda sana usafi. Ni aghalabu sana kukutana na mwanamke asiyejipenda. Ndiyo maana wanaitwa mapambo ya nyumba au la nyumba! Ni kwa sababu ya hulka yao ya kupenda sana usafi.

Mwanamke anavutiwa sana na mwanaume mtanashati. Usafi wako unamfanya ajiamini kuwa na wewe. Hata nyumbani kwako, lazima uishi katika nyumba safi. Hata anapokuja kukutembelea, anakuta mazingira masafi kuanzia sebuleni hadi chumbani.

Anapokukuta katika hali ya usafi, inakuwa rahisi zaidi yeye kuanzia hapo alipokukuta na kuendelea mbele.

KUJIAMINI

Mwanamke anajisikia salama zaidi akiwa na mwanaume ambaye anajiamini – mwenye uwezo wa kutetea hoja zake na kujieleza sawia. Siyo anayebabaika. Suala la msimamo binafsi, kwa mwanamke ni kubwa kuliko hata kumnunulia manukato mapya!

Mathalani unakuwa naye katika mtoko, angependa kukuona ukiwa katika hali halisi ya maisha yako, usiyeyumbishwa na mwenye kutoa maamuzi yasiyoyumba.

Wakati mwingine, mwanamke anaweza kukupima hata katika jambo ambalo amekosea yeye, ataangalia unavyotoa maamuzi yako, lakini pia atafuatilia kuona kama utakuwa mwepesi wa kuyabadilisha.
Anataka kuona msimamo wako muda wote. Mwenye kujiamini na mawazo yasiyo na matege wala makengeza!

KUJITETEA

Kipengele hiki hakina tofauti kubwa sana na kilichopita, lakini hapa ni kwenye upande wa kujitetea zaidi. Wakati unapodai haki yako mbele ya mwanamke wako, suala la kujitetea linapewa nafasi kubwa sana.
Wanawake hawapendi kuwa na wanaume ambao wapo tayari kuonewa. Wanataka wenye uwezo wa kusimama kidete kuona haki zao hazichukuliwi kirahisi.

Hili si suala la kutetea tu haki yako pekee kama mwanaume, bali inapobidi kusimamia haki ya mwanamke wako. Nisieleweke vibaya katika hili, lakini mwanaume imara ni yule ambaye ana nguvu – anafanya mazoezi na ambaye yupo tayari kwa lolote!

Inapowezekana, uwe na uwezo wa ‘kuzichapa’ ikiwa mtakutana na vibaka au watu wabaya wenye lengo wa kukudhuru/kuwadhuru au kumdhuru mpenzi wako.

Mwanaume aliye ‘fiti’ ni chaguo la wanawake wengi. Si mnyonge. Mpole kupitiliza na aliye tayari kuonewa! Huyu hana nafasi.

KUJALI

Wanawake wanapenda sana wanaume wanaojali. Wanawaona wao ni kila kitu na wanaotoa kipaumbele kwao. Kama huna tabia hiyo, ujue upo katika nafasi kubwa ya kumkwaza mpenzi wako. Mjali mpenzi wako kwa kila hali.

Kumjulia hali kila wakati na kutaka kujua maendeleo yake, kutakupa nafasi kubwa sana ya kuendelea kudumu katika uhusiano hai.

UKARIBU

Kati ya vitu vinavyowapa mshawasha mkubwa wanawake ni pamoja na kusogezwa karibu. Hapa ni kuwa naye katika mambo mengi unayoyafanya kila siku.

Ni vizuri kuwasiliana naye mchana, ukitaka kujua aina ya chakula alichokula siku hiyo au ikiwezekana mchagulie. Ni mambo madogo sana lakini yanayoongeza nakshi katika mapenzi.

Yapo mengi sana ambayo kwa kuyafanya utakuwa umemsogeza mpenzi wako karibu yako. Hebu tumia ubunifu wako ili uweze kuteka hisia za mwenzi wako kisawasawa!


KUMSIFIA

Wanaume wengi hupuuzia hili, huona kama ni jambo lisilo na maana sana kwao na wenzi wao. Hali ni tofauti sana kwa wanawake ambao hupenda kuwasifia wanaume zao. Nitakupa mifano miwili ya namna wanandoa wa jinsia mbili tofauti wanavyotambulishana kwa jamaa zao.

MWANAUME: “Peter kutana na mke wangu, anaitwa mama Diana. Nipo naye mwaka wa tatu sasa, tuna watoto wawili, huyo Diana na mwingine anaitwa Cris. Mama Diana, huyu ni Peter nilisoma naye A – Level, Tosamaganga Sekondari.”

MWANAMKE: “Suzan, huyu ndiye mume wangu mpenzi...anaitwa Elifaraja lakini mimi napenda zaidi kumuita Elly. Kiukweli nampenda sana mume wangu jamani, tuna mtoto wetu mmoja, anaitwa Agness. (Akimgeukia mumewe) Baby, huyu hapa ni rafiki yangu Suzan. Yaani tumekua naye mtaa mmoja huko Arusha.”

ANGALIA TOFAUTI

Bila shaka kwa namna wawili hao walivyotambulishana unaweza kuona tofauti kubwa. Mwanaume amemtambulisha mkewe kawaida kabisa, hajaonesha manjonjo au namna anavyompenda na kumthamini mwenzake, lakini mwanamke amefanya hivyo.

Sikia nikuambie, KUMSIFIA mwanamke, kuna nafasi kubwa sana kwake. Chunguza kwa makini, hata kunapokuwa na mgongano katika familia, halafu wakatokea wageni, baada ya utambulisho na mazungumzo ya hapa na pale, wageni wakiondoka kunakuwa na uwezekano mkubwa zaidi wa kumaliza mpasuko katika familia.

Jenga utamaduni wa kumsifia mpenzi wako, unamuweka katika kilele cha upendo. Anajiona kamili, peke yake na mwenye nguvu kwako. Anajiamini na unamfanya azidi kukupenda kwa kuwa anaamini yupo na mwanaume ambaye anajivunia kuwa naye.

MALENGO

Wanaume wengi wana ulemavu mmoja; hawapendi kuwashirikisha wanawake katika mambo yao. Wanapenda kufanya mambo yao kwa siri na wakati mwingine ikilazimika kumwambia mkewe basi kwa mshtukizo baada ya kukamilisha jambo husika.

Hii si sahihi. Dunia ya leo imebadilika rafiki zangu. Inawezekana wazee wa zamani walikuwa sahihi, maana ilikuwa ni suala la kununua ng’ombe na kuwaweka katika zizi kwenye kijiji cha jirani, halafu wanapewa malisho mazuri, baada ya miaka miwili wanazaliana, hapo ndipo anamweleza mkewe.

Siku hizi dunia imebadilika, kuna mambo mengi. Kuna suala la hasara katika biashara, utapeli n.k. Mkeo ndiye rafiki yako mkubwa kuliko wote, ndiye ndugu yako wa karibu zaidi kuliko yeyote. Yes! Mkeo ndiye ndugu yako maana umetengeneza naye familia. Mmeshirikiana kuzaa watoto na kujenga maisha pamoja.
Yeye anapaswa kujua mambo yako, ndiye mtetezi wako nambari wani. Mweleze juu ya malengo yako, wakati mwingine anaweza kukusaidia sehemu ambayo hukutarajia.

Hata hivyo, kumshirikisha katika malengo yako, kunampa nguvu na nafasi ya kujiona mama katika familia yenu. Msaidizi kamili wa nyumba yenu.

KIPAUMBELE

Kuna wakati wanawake huwa na mambo yao binafsi. Kazini au kifamilia. Inawezekana akatatizika katika eneo fulani ambalo kwa namna moja ama nyingine atahitaji usaidizi wako. Ikitokea mkeo akawa katika hali hiyo, msikilize.

Mathalani ana tatizo la kifamilia, amekuambia mmoja wa wazazi wake anaumwa, msaidie. Si lazima kifedha, lakini kuonesha kujali kwako tu, kutampa matumani kwamba anaishi na mtu sahihi. Acha kupuuza mambo yake; hata yale madogo, kama ya ‘mtoto wa dada amerudishwa ada shuleni’.

Msikilize, mshauri panapofaa kufanya hivyo na ukiweza msaidie hata kifedha. Katika upande wa pili ni hivyo hivyo. Labda una tatizo binafsi, kazini kwako au kifamilia, mshirikishe.

Unaweza kushangaa jambo ambalo uliamini unaweza kulimaliza peke yako, kwa kumshirikisha likawa jepesi zaidi na mambo yakaendelea vyema. Kipaumbele kwa namna yoyote ile, kunaongeza mapenzi zaidi kwa mwanamke.

TENDO LA NDOA

Hiki ni kipengele nyeti, kinachohitaji lugha nzuri ya kirafiki kukifafanua. Hakuna siri, tendo la ndoa ni moja ya kiwakilishi cha ndoa. Maana hata maandiko yanasema: “Mwanamke ataacha wazazi wake na kwenda kwa mumewe, nao watakuwa mwili mmoja.”

Kimsingi tendo la ndoa lina nafasi yake. Ni muhimu likaheshimiwa na kutengewa muda maalum wa kufurahia. Si papara. Kwa bahati mbaya wanaume huwa si wafuatiliaji sana wa kujua namna ya kuwafurahisha zaidi wenzao. Wenyewe wanajiwazia wenyewe. Wanafikiria namna ya kuwakomoa wenzao.
Si sahihi.

Tendo la ndoa halina maana ya kukomoana. Jenga mazoea ya kufanya maandalizi kamili kabla ya tendo. Sikiliza hisia za mwenzako. Ukiweza kumjulia mke wako katika eneo hili, ni wazi kwamba utazidisha upendo wake kwako, lakini pia atakuwa katika kuta za uaminifu. Akatafute nini nje wakati wewe ndiye mganga wake unayeweza kumtibu barabara?

Kuna kitu nimesahau kweli? Kama kipo nitafute pembeni, kwa hapa haya yatoshe kukufanya uelewe nilichotaka kukuelekeza. Nikuache na neno moja; uamuzi wa kuijenga ndoa yako upo mikononi mwako. Ukitaka iwe shaghalabaghala, pia ni wewe tu!

Wajue Wanaume wa Kiafrika na Hulka Zao Katika Maisha...!!!

$
0
0


1. Wanaume wakatili zaidi Afrika - Waangola, Warundi na Wanubi (Sudan). Ukiwakosea ni kipigo au kifo. Kwao hakuna msamiati uitwao "Msamaha".
2. Wanaume wanaojali zaidi familia zao Afrika - WaSenegal.

3. Wanaume wanaopigwa zaidi na wake zao - Wakenya (Kati ya wanaume 10 nchini Kenya 7 wanapokea kipigo kutoka kwa wake zao. Chama cha kutetea haki za wanaume hadi sasa kina wanachama laki 8).

4. Wanaume wanaosali zaidi Afrika - Wasomali (kati ya wanaume 10 wa kisomali, 8 huswali swala 5 kila siku. Hata katikati ya vita huwaachi kuswali).

5. Wanaume matapeli zaidi Afrika - Wanigeria (kati ya wanaume 10 wa Nigeria, 6 ni matapeli wa kutupwa. Hata kama ni Askofu ukijilengesha anakutapeli tu).

6. Wanaume wanaopenda dezo na kulelewa zaidi Afrika - Wakongo (hawa wakioa mwanamke mwenye pesa huhamia kwa mke. Wanaitwa "Mario").

7. Wanaume wasomi zaidi Afrika -Washelisheli (Sychelles). Kila wanaume 100, 40 wana degree. Tanzania kila wanaume 1000 watatu wana degree.

8. Wanaume washamba zaidi Afrika - WaEritrea (ukienda kanisani/msikitini na gari jipya wanaahirisha kusali washangae gari kwanza).

9. Wanaume wachawi na Washirikina zaidi Afrika - Wagambia (Rais wao Yahya Jammeh hutumia waganga na wapiga ramli kama sehemu ya walinzi wake).

10. Wanaume wenye mikwara mingi mdomoni lakini waoga kutake "action" - Watanzania.
Viewing all 104706 articles
Browse latest View live


Latest Images