Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

Waziri Mwijage Atengua Uteuzi Wa Mkurugenzi Wa Wakala Wa Usajili Wa Biashara Na Leseni (BRELA)

$
0
0
Waziri Mwijage Atengua Uteuzi Wa Mkurugenzi Wa Wakala Wa Usajili Wa Biashara Na Leseni (BRELA)


Hii ni Habari Njema Kwa Wale Wote Waliohangaika na Matatizo ya Magonjwa Sugu Yaliyokosa Tiba

$
0
0
"HII NI HABARI NJEMA KWA WALE WOTE WALIOHANGAIKA NA MATATIZO YA MAGONJWA SUGU NA YALIYOKOSA TIBA" sasa usikate tamaa tiba imepatikanika kwa DK. ABDALA MUSSA anatibu matatizo kama yafuatayo:

Nguvu za kiume, uzazi, kisukari, tezi dume, vidoda vya tumbo, mgongo kuuma, miguu kuwaka moto na mataizo uliyonayo

1/ITAGULA- ni dawa ya mkosi kuosha nyota, kumvuta mpenzi, mke, mume, kuua kesi na kupata kazi haraka kama umeomba maombi serikalini au kampuni binafisi unaitwa ndani ya siku mbili 2/

NINJIWE- ni dawa inayomaliza matatizo ya wanaume heshima ndani ya ndoa, kuwa na nguvu za kiume milele na kukomaza mbegu na kuwa na uwezo kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila kuchoka kama umezaraulika na kufanya tendo na kusinyaa uume dawa ipo dozi yake siku sita vidoge 12 pia kuna na unga inayokomaza uume ndani ya siku 7 unapona kabisa.

3/MPALALA- ni dawa ya kutibu busha miguu kuwaka moto, kiuno, kisukari.

4/NGEKEWA- ni dawa ya kuvuta wateja kwenye biashara yoyote kuwa na wateja wengi katika biashara na kuzuia chuma ulete. 4/LINGWATA- ni dawa ya punguza unene, mafuta tumbo, matiti, miguu, hipsi na kutengeneza shepu dawa hii ni ya unga ukitumia utaona mabadiliko baada ya siku 3.

5/DUBISHO- ni dawa zindiko la mwili, majumba, gari, biashara, mteja wangu huduma utaipata mahali popote ulipo kuna wanasaplai mahali ulipo kama huna muda wa kufika osifini mkoa wa dar-es-salaam, iringa, kanda ya ziwa wilaya ya bunda. angalizo kwa wateja usitume sms wala kubipu huduma yangu ni kuanzia saa 12 asubui hadi saa 12 jioni kwa wateja wa dar-es-salaam ofisi ipo buguruni na mbagala zakhem na kwa wale walio nje ya mkoa dawa hizi mtazipata kwa njia za mabasi. punguzo la bei kwa wateja 5 wa kisukari na nguvu za kiume

KWA MAWASILIANAO ZAIDI WASILIANA NA DK. ABDALA MUSSA KWA SIM NAMBA 0767-171773/ 0716-608959 WOTE MNAKARIBISHWA:

Mahakama Yatoa Siku Sita Kesi ya Mpemba wa Meno ya Tembo

$
0
0
Mahakama Yatoa Siku Sita Kesi ya Mpemba wa Meno ya Tembo
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imewapa siku sita upande wa mashtaka, kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa maagizo waliyopewa na Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), katika kesi ya Yusuf Ali maarufu kama ‘Mpemba wa Magufuli.

Amri hiyo imetolewa  leo  Julai 20 na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Thomas Simba, muda mfupi  baada ya upande wa mashtaka kuieleza  mahakama kuwa upelelezi wa shauri hilo umekamilika na wanalifanyia kazi jalada la kesi hiyo, baada ya kupewa maelekezo na Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP).

Yusuph na wenzake watano wanakabiliwa na mashtaka manne, likiwamo la kujihusisha na biashara haramu ya meno ya tembo yenye thamani ya Sh 785.6milioni.

“Nimewapa siku sita kuanzia leo  Julai 20 hadi Jumanne ya wiki ijayo, muwe mmekuja na majibu, mmefikia hatua gani katika kesi hii,  sitawaelewa msipokuja na majibu," amesema Hakimu Simba.

Awali, Wakili wa Serikali Elizabeth Shekunde, alidai mahakamani hapo kuwa kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa, hivyo wanaomba tarehe nyingine ya kutajwa.

Baada ya upande wa mashtaka kueleza hayo, Wakili wa Utetezi NehemiaNkoko, alidai kuwa ahadi za upande wa mashtaka katika kesi hiyo ni za kawaida, hivyo wanaomba kujua washtakiwa hao watasomewa lini maelezo ya mashahidi.

“Tunataka kujua wateja wetu watasomewa lini maelezo ya mashahidi na vilelelezo, kwa sababu kila siku, upande wa mashtaka wanakuja na taarifa zile zile," amedai Nkoko.

Hakimu Simba baada ya kusikiliza hoja za pande zote, aliahirisha kesi hiyo hadi Julai 24, mwaka huu itakapotajwa.

Julai 5, Mwaka huu, upande wa mashtaka uliieleza Mahakama kuwa wanalifanyia kazi jalada la kesi hiyo, baada ya kupewa maelekezo na  Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP).

Upande huo wa mashtaka alidai kuwa limeshapitiwa na DPP na walipewa maelekezo ambayo wanayafanyia kazi na kwamba wapo katika hatua za kukamilisha maelekezo hayo.

Mbali na Yusuph, washtakiwa wengine katika kesi hiyo  ni Charles Mrutu, mkazi wa Mlimba, Morogoro, Benedict Kungwa, mkazi wa Mbagala Chamazi, Jumanne Chima, mkazi wa Mbezi, Ahmed Nyagongo, dereva na Pius Kulagwa.

Washtakiwa kwa pamoja wanakabiliwa na mashitaka manne ya kujihusisha na biashara haramu ya meno ya tembo yenye thamani ya Sh 785.6milioni na upelelezi wa kesi hiyo umekwisha kamilika.

Kutangaza Kuacha Muziki Haikuwa Kiki:-Q-Chillah

$
0
0
Kutangaza Kuacha Muziki Haikuwa Kiki:-Q-Chillah
Msanii mkongwe wa muziki, Q-chillah mefunguka na kuongelea swala lake la kutangaza kuacha muziki na baadae kurudi tena katika muziki kuwa sio kiki kama watu wanavyosema kwamba alitaa kufanya hivyo ili kutengeneza attention kwa mashabiki wake bali alikuwa ameamua kuachana na muziki ili kufanya kitu kingne na sio muziki tena.

Q-Chillah anasema kuwa kilicokuja kutokea ni baada ya kupokea simu kutoka nje na kuongea na moja ya watu waliwahi kuupenda sana muziki wake na kumwambia kuwa amekuwa akiona na kukijua kipaji chake siku nyingi hivyo haoni sababu ya yeye kuacha muziki bali anaomba kufanya nae kazi.

Q-chillah anasema kuwawat wengi wamekuwa wakija na kumsema kuwa alichofanya ilikuwa ni kiki lakini ukweli ni kwamba alikuwa akiona  jinsi ambavyo muziki wake ukimuendea pabaya,

kama niliweza kuomba ridhaa ya  watu wakati nataka kufanya muziki  ndio maana hata wakati nataka kuacha ilinibidi kuomba ridhaa ya kuacha haikuwa rahisi  rahisi kama inavyodhaniwa lakini pia haikuwa kiki kama watu wanavyofikiria.-Aliongea Q-chillah alipokuwa akiongea na waandishi wa habari wa Clouds tv 360.

Wema Sepetu Asipobadilika Atakua mtu wa Ajabu Sana- Albeto Msando

$
0
0
Wema Sepetu Asipobadilika Atakua mtu wa Ajabu Sana- Albeto Msando
Wakili wa wema sepetu Albert msando amedai kuwa iwapo wema hata badilika baada ya mahakama kumkuta na hatia na kuhukumiwa mwaka mmoja jela au kulipa faini ya shilingi millioni 2 atakuwa ni mtu wa ajabu.

Vilevile amedai kuwa amemsahauri wema awe balozi mzuri na kuwa na wajibu wa kuwa balozi wa kulisemea swala hili la madawa  ya kulevya na kulikemea na ameendelea lusema kuwa changamoto kubwa ya wasanii wanaigia na kujikuta hawana mambo mengi ya kufanya.

Amemalizia kwa kusema kuwa utofauti wa kesi ya wema na wakina TID ni kwamba swala la wema lilihitaji ushahid na kuthibitishwa ndio mana lmechukua muda mrefu hali kuwa swala la wakina TID wao walikubali moja kwa moja

Dudu Baya Baada Kuwashtumu Wasanii wa Dansi Wachafu Nyoshi Amjibu Hivi

$
0
0
Msanii wa dansi nchini Nyoso El Sadaat amemjibu Dudu Baya baada ya msanii huyo wa bongo fleva kuwajia wasaniwa dansi na kuwaambia kuwa wamefulia sasa hivi kwa sababu walizoea kuomba msaada kutoka kwa matajiri na kwa sababu hali ya uchumi sasa hivi kila mtu anajibana na ndio maana hakuna wanachofanya zaidi ya kufulia.

Dudu bata alisema “wasanii wa dansi sasa hivi ni wachafu sana , wamefulia tu hawana tena watu wa kuwaomba ela kabisa.Walikuwa wamezoea kuomba ela , awamu hii wa Magufuli watapata  tabu sana.

Hapo ndipo alipompanikisha Nyoshi na ndipo alipomjibu kuwa wao hawawezi kufulia hata siku moja kwa sababu mabosi wao mpaka sasa wapo na wanaendelea kutoa pesa na hakuna kitu kama icho kinaweza kutokea.

Mabosi wapo na hata uko kuwataja hakumaanishi kwamba tunawabebeleza watupe ela wao huwa wanatoa tu, kama kufulia tungefulia kwenye nguo mngeona tunavaa vibaya mbona tunapiga pamba kama kawaida tu hata hii miwani yangu kuna mtu kaniomba nimpe.

Raia wa Uganda Afumwa Gesti na Mwanafunzi wa Secondari

$
0
0

RAIA wa Uganda anayefanya kazi za kusafirisha watalii hifadhini aliyefahamika kwa jina moja la Peter anasakwa na jeshi la polisi baada ya kukutwa na mwanafunzi wa kidato cha kwanza jina limehifadhiwa.

Tukio la kufumaniwa kwa mwanafunzi na kijana huyo limetokea Majira ya saa 4 subuhi.

Mtandao huu wa DarMpya.com umefika eneo la tukio katika nyumba ya kulala wageni ya CK Lodge iliyopo eneo la Kijiweni na kumkuta mwanafunzi Hugo akiwa katika moja kati ya vyumba akiwa na chooni emejificha huku kijana huyo raia wa Uganda akitokea akifanikiwa kuwakimbia askari hao.

Pamoja kutokana na kukimbia kwa mtuhumiwa huyo polisi walimkamata rafiki take ambae pia ni Raia wa Uganda na kuondoka naye huku wakimtaka boss wao ambae ni mzungu kuhakikisha anampeleka kijana huyo polisi.

Kamanda wa polisi mkoa wa Iringa Juma Bwire amesema polisi wanaendelea kumsaka mtuhumiwa Hugo.

SUA yagundua mwarobaini tatizo la nguvu za kiume na Mvurugiko wa Mzunguko wa Hedhi

$
0
0

Chuo cha Kilimo SUA Kimefanya utafiti na kubaini kuwa mbegu za matunda zinaweza kutibu matatizo ya nguvu za kiume na mzunguko wa hedhi uliovurugika kwa mwanamke.

Katika miaka ya karibuni wanaume wengi wamekuwa wakisumbuliwa na tatizo la kukosa nguvu za kiume na kusaka tiba bila mafanikio huku wengine wakikimbilia kwa waganga wa kienyeji.

Hivyo wanafunzi wa SUA wakachukua fursa hiyo kuja na mbinu mbadala ya kukomesha tatizo hilo ambapo wamegundua kwamba mbegu za matunda kama tikitikimaji, maboga, alizeti, papai na matunda mengine zinaweza kutibu matatizo hayo.

Stewart Mwanyika ambaye ni Mtafiti Mwandamizi kutoka SUA amesema kiasili mbegu zina kiasi kikubwa cha madini ya zinki ambayo yanachangia kutengeneza homoni na chembechembe zinazohusika na utendaji bora wa via vya uzazi hasa vya mwanaume.

Hivyo ameshauri watu kutumia mbegu hizo mara kwa mara iwe tiba ya kudumu kwani madini ya zinki yanatengeneza haraka chembechembe nyeupe za damu ambazo ni kinga ya mwili na seli nyingine zinazohusika na via vya uzazi.

”Ukila matunda kama tikitimaji usitupe mbegu, tafuna meza na kama harufu inakukera unaweza kuzitoa na kuzikausha kisha oka ili kuongeza ladha kisha tafuna, mbegu za papai pia ukiweza kuzila ni vizuri lakini zina uchungu, ila kwa mbegu za alizeti na maboga kuzikaanga kisha unatafuna unameza” amesema Stewart.

Baraka The Prince ampa heshima Ali Kiba

$
0
0

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Barakah The Prince amempa heshima msanii mkongwe wa Bongo fleva Ali Kiba na kudai ni msanii mwenye experience kubwa Kwenye Bongo fleva. 

Barakah alikuwa chini ya Label ya Rockstar 4000 ambayo inaendeshwa na Ali Kiba lakini baada ya miaka michache ndani ya Label hiyo BAraka alitangaza kujitoa na kuanza kufanya Muziki wake mwenyewe. 

Baada ya kutoka Rockstar Baraka aliwatuhumu kwa kufanya njema mbali mbali za kumrudisha nyuma kimuziki ikiwemo mapema mwaka huu aliwatuhumu kwa kufuta nyimbo zake Youtube. 

Lakini sasa inaelekea Baraka amerudi katika nafasi nzuri na Ali Kiba kwani Kwenye Interview yake na kipindi cha refresh cha Wasafi Tv, Baraka amemtaja Ali Kiba kama mtu aliyemfundisha mambo mengi kwenye sanaa kutokana na experience yake; 

"Ali Kiba ni mkubwa na ana experience Kwenye Industry more than me kwaiyo muda ambao nilikuwa naye nilijifunza vitu vingi Kimuziki na kusema kweli nilikuwa niijua thamani yangu kama msanii na nilijua nini natakiwa kufanya ili kufanikiwa maana yeye ameshakula matunda ya Muziki wetu”.

Barakah amesema kwa sasa hana mpango wa kusainiwa chini ya label yoyote hapa Tanzania labda hapo baadae. 

Shoga wa Itali Aliyejibadilisha Kuwa Mwanamke Azuiliwa Kuingia Zanzibar

$
0
0

RAIA wa Italia, mwenye umri wa miaka 46 amezuiliwa Uwanja wa Ndege wa Abeid Amani Karume visiwani hapa na kurudishwa nchini mwake baada ya kubainika kuwa amebadilisha jinsia yake.


Mtu huyo aliingia Zanzibar wiki hii alibainika kubadilisha jinsia na kwamba katika hati yake ya kusafiria ilionyesha mwanaume, lakini yeye alionekana kama ni mwanamke baada ya kujibadilisha.

Akizungumza na Nipashe, Ofisa Uhusiano wa Idara ya Uhamiaji, Mlalama Amlima, alisema raia huyo ambaye alijulikana kwa Davide Katena alifanyiwa uchunguzi na kugundulika kuwa ni mwanaume ingawa alivaa mavazi ya kike.

Alieleza kuwa, walianza kumtilia mashaka baada ya kushuka uwanjani hapo na walipojiridhisha kuwa ni mwanamme akazuiliwa kuingia nchini na kulazimika kurejea alikitoka.

Aidha, alisema raia huyo ambaye alikuja Zanzibar na Shirika la Ndege la AAKIA majira ya saa tisa alfajiri ya kuamkia jumatano na tayari amesharejea nchini kwao.

Alisema kuwa raia huyo ni msanii na alikuja Zanzibar kwa ajili ya kufanya maonesho ya muziki.

“Tulipojaribu kumuhoji raia huyo pia alisema kuwa ana jina la kike ambalo ni Cristina Bugatty ambalo anatumia katika sanaa,” alisema.

Alieleza kuwa wamemzuia kuingia nchini kutokana na kitendo alichokifanya ni kinyume na sheria na taratibu za uhamiaji.

 “Ujio wa raia huyo ungevuta taswira ya ukahaba nchini kinyume na sheria, silka na desturi za jamii ya Kitanzania,” alisema.

Hata hivyo, alieleza kuwa hilo sio tukio la kwanza  kuwarejesha raia kama hao ambao wanajihusisha na mapenzi ya jinsia moja na wengine hufika Zanzibar kwa ajili ya fungate baada ya nchini kwao kufunga ndoa. 

Polepole Azindua Kampeni na Kumnadai Mgombea wa CCM Moshi

$
0
0

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole amewasihi wakazi wa kata ya Mawenzi mjini Moshi, kumchagua mgombea udiwani wa CCM, Apaikunda Naburi kwa maelezo kuwa atakuwa kiunganishi sahihi kati yao na Serikali inayoongozwa na Rais John Magufuli.


Polepole ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Julai 20, 2018 katika viwanja vya kituo kikuu cha mabasi mjini Moshi, wakati wa uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata hiyo, ambayo awali diwani wake, Hawa Mushi alikuwa akitokana na Chadema.


Hawa aliyechaguliwa kuwa diwani mwaka 2015 alifariki dunia mwezi uliopita na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kutangaza kufanyika kwa uchaguzi mdogo, sambamba na kata zingine 76 nchi nzima.


Polepole amesema maendeleo yanayoonekana katika mji wa Moshi yanatokana na sera nzuri za Serikali ya CCM, ambayo ndio imekuwa ikitoa fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo kwa asilimia 80.


Katibu huyo amesema kitakwimu, halmashauri ya manisapaa ya Moshi ina uwezo wa kukusanya mapato ya ndani yanayofikia zaidi ya Sh5 bilioni wakati bajeti kwa mwaka mzima ni Sh46bilioni.


"Hawa wenzetu (Chadema) wanasema wao ndio wameleta haya maendeleo mnayoyaona hapa Moshi. Nataka niwaambie leo, halmashauri mapato yake ni Sh5bilioni kwa mwaka lakini bajeti nzima ni Sh46 bilioni. Mwenye macho haambiwi tazama,"amesema Polepole.


Polepole aliwaomba wakazi wa kata hiyo kumchagua Naburi akisema ndio chaguo sahihi la kuwaletea maendeleo wananchi wa Moshi, ikiwamo kuboresha huduma katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro ya Mawenzi.


Mbunge wa Siha (CCM), Dk Godwin Mollel amesema ni upotoshaji mkubwa kudai  Rais Magufuli hapendi vyama vya upinzani wakati anaendelea kutoa ruzuku ya kila mwezi kwa Chadema ambacho kinajinasibu kuwa chama kikuu cha upinzani nchini.


Dk Mollel alikuwa mbunge wa Siha kwa tiketi ya Chadema kati ya Novemba 2015 hadi Desemba 2017, kabla ya kujiuzulu na baadae kuteuliwa na CCM kugombea ubunge jimbo hilo hilo na kushinda.


Kwa mujibu wa Dk Mollel, Chadema imekuwa ikipatiwa ruzuku ya Sh337 milioni kwa mwezi kwa fedha za Serikali ya CCM hivyo si sahihi kudai Rais Magufuli hapendi upinzani.


Dk Mollel amedai pamoja na chama hicho kupokea mamilioni hayo ya fedha kwa mwezi, kimeshindwa kuzitumia kwa maendeleo ya chama hicho na ndio maana hadi leo hakina ofisi yake ya kujenga.


Katika mkutano huo, CCM kiliwatumia makada wa zamani wa Chadema waliohamia CCM, kuwashawishi wakazi wa kata ya Mawenzi, kumchagua mgombea wa CCM.

Breaking News:Ali Kiba Kutambulishwa Kama Mchezaji wa Coastal Union

$
0
0

BREAKING NEWS : Imeripotiwa kuwa uongozi wa Coastal Union upo mbioni kumtambulisha Alikiba kuwa mchezaji wao tayari kwa msimu ujao.
Inasemekana tayari Alikiba ameshafanya makubaliano na uongozi huo na muda wowote kutoka sasa watamtangaza .

Amnesty wataka malkia wa urembo Kenya aondolewe hukumu ya kifo

$
0
0
Shirika la Amnesty International limetoa wito wa kubatilishwa kwa hukumu ya kifo iliyotolewa dhidi ya malkia wa urembo gerezani nchini Kenya Ruth Kamande.

Mwanamke huyo alihukumiwa kifo Alhamisi baada ya kupatikana na kosa la kumuua mpenzi wake miaka mitatu iliyopita katika mtaa wa Buruburu, Nairobi.

Bi Kamande, 25, amekuwa akizuiliwa rumande katika gereza kuu la wanawake la Lang'ata jijini Nairobi ambapo mwaka 2016 aliibuka kuwa malkia wa shindano la urembo lililoandaliwa humo gerezani.

Mkurugenzi mkuu wa Amnesty International nchini Kenya Irungu Houghton amesema mwanamke huyo anafaa kusaidiwa kujirekebisha badala kuhukumiwa kifo.


"Tunasikitika kwamba Kenya inaendelea kutoa adhabu hii katili, isiyo na utu na iliyopitwa na wakati. Hukumu hii ni pigo kwa rekodi nzuri ya Kenya ya kuendelea kubadilisha hukumu za kifo kuwa hukumu za vifungo jela," amesema.

"Hakuna ushahidi wowote wa kuaminika kwamba hukumu ya kifo huwazuia watu kutekeleza uhalifu zaidi ya adhabu za aina nyingine. Hukumu hii ya kifo inafaa kubatilishwa mara moja na Ruth Kamande asaidiwe kurekebisha tabia."

Ingawa huku ya kifo huendelea kutolewa kwa makosa ya mauaji na wizi wa kutumia mabavu nchini Kenya, haijatekelezwa kwa mfungwa yeyote nchini Kenya katika kipindi cha miaka 30.

Rais Uhuru Kenyatta na mtangulizi wake Mwai Kibaki walibadilisha hukumu ya wafungwa wengi waliokuwa wamehukumiwa kunyongwa katika kipindi cha miaka kumi iliyopita na kuwa vifungo vya maisha jela.

Wafungwa takriban 6,747 wamenufaika kupitia hatua hiyo.

Hukumu ya kifo iliondolewa katika mataifa 139 duniani lakini bado kuna nchi zinazotekeleza hukumu hiyo zikiwemo Marekani, China, Pakistan na Saudi Arabia.

Ni mataifa gani Afrika yanayoendelea kutekeleza hukumu ya kifo?
Amnesty wanasema hapana shaka kwamba familia ya marehemu Farid Mohamed ni lazima "itendewe haki" lakini suala kuu wanalopinga ni kutumiwa kwa hukumu ya kifo.

Wamesema nchini Kenya ni kawaida kwa kesi kutoendeshwa kwa njia ya haki na mtu asiye na makosa kujipata amehukumiwa.

Kuna mambo ya kuzingatia pia katika kesi ya Ruth Kamande, wameandika kwenye Twitter: "Alikuwa kijana, aliyekuwa ameathiriwa na wasiwasi na hatari ya kuambukizwa Ukimwi/Virusi Vinavyosababisha Ukimwi. Tangu wakati huo ameonesha nia ya kubadilika akiwa mahabusu. Ingawa haki ni lazima itendeke, hukumu ya kifo si moja ya njia za kufanikisha hilo."

Baadhi ya Wakenya mtandaoni wamekuwa wakikosoa hatua ya Amnesty International kutoa taarifa ya kuomba hukumu dhidi ya Bi Kamande ibadilishwe, wakishangaa iwapo ni kutokana na umaarufu alioupata kwa kuwa Miss Lang'ata Women Prison 2016.

Millard Ayo Afunguka Magumu Aliyopitia Mpaka Kupata Hii Gari...Atoa Shukrani Kwa Hawa

$
0
0

Kwa wenye uwezo hiki kinaweza kuwa kidogo lakini kwangu ni kikubwa sana, mwaka 2010/11 nilipoanza kuwa blogger vitendeakazi pekee nilimudu kununua/nilivyokua natumia vilikua laptop ya laki 3 na simu ya Blackberry torch niliyoitumia kama camera.
_
Leo namshukuru Mungu na kila binaadamu alieni-suport, nimepata gari ambalo ndani nimelitengeneza kama ofisi, litanisaidia kurahisisha kazi eneo la tukio kuliko awali na kurusha LIVE kutoka popote ambapo @vodacomtanzania wataniwekea Internet
_
Hata hivyo haikuwa rahisi kulipata, ilikua ni ndoto niliyoiwazia sana miaka mitatu na nikaitimiza mwaka wa 4, huko mitaani najua viko vichwa, wapo wenye uwezo wa kazi na mipango ya maana kwenye kutafuta pesa lakini wamekwama kwa kukosa mtu wa kuwashika mkono au kwa kukosa vigezo vya kupewa mikopo, hata mimi pia nilikosa mikopo mara 3 Bank lakini baada ya kukosa mikopo ambayo ingetimiza sehemu ya ndoto zangu ndani ya miezi minne, nilikubali njia pekee ya kujikomboa ni kukusanya kila senti na nikaanza kufanya hivyo kwa miaka miwili na nusu mpaka nikapata pesa ya kununua hili gari nikamuagiza @drisaacmaro Japan na ninamshukuru sana kwa kunichagulia gari zuri
_
Special Thanks kwa Maboss wangu CLOUDS @josephkusaga #RugeMutahaba, #Sheba na @sebamaganga kwa kuniruhusu kuishi ndoto zangu ndani ya ndoto zao, miongoni mwa pesa zilizonisaidia kwa kiwango kikubwa ktk kibubu ni zile za bonus ambazo Mtangazaji hupewa kipindi chake kinapofanya vizuri ktk mauzo, nina Brothers wengine WAWILI wa kuwashukuru SANA ktk hili, IPO SIKU YAO!
_
Lilivyofika TZ nili-design muonekano wa nje kwa kushirikiana na @jukaytzeedream ambae ndie MCHORAJI BORA wa logo ya @ayotv_ , idea ya nje na setting ya ndani ilikuwepo nikalipeleka garage kwa my Brother Thabeet @tttrautoupgrades nako likakaa kama miezi minne naa... nilipopata pesa kulikomboa ndio nikalifata, kisha Fundi mwingine (Dani) akamalizia, nikikumbuka wengine nita-edit
_
Nawakumbusha tu watu wangu tunaohangaika na hatuna wa kutushika mkono, anza na hichohicho kidogo ulichonacho haijalishi utachekwa au utaonekana umepoteza muelekeo, Asante kwa kila Mtanzania anae-support ninachofanya, naahidi kuyafanyia kazi mapungufu ili tupate bidhaa bora zaidi 🙏

Peter ndiye Baba Shujaa wa Patrick, Siyo Aliyekimbia Mimba. Wanaume Aina ya Peter ni Wachache

$
0
0

From @luqmanmaloto - DOOH MUNA! TUACHE TU PATRICK APUMZIKE

KUNA mwanamuziki wa Bongo Fleva mkubwa, naye alipatikana mfano wa mtoto Patrick kama alivyosimulia Muna. Mama yake akiwa mjamzito, alikutana na mwanaume ambaye alikubali kubeba majukumu ya mume na kuwa baba wa mtoto tumboni.

Mtoto alizaliwa. Yule mwanaume akawa baba rasmi. Cheti cha kuzaliwa kikaandikwa jina la yule mwanaume. Hata shule aliandikishwa kwa ubini huo. Mpaka leo, mwanamuziki huyo hamfahamu baba mwingine, isipokuwa huyo mwanaume aliyempokea mama yake na ujauzito.

Muna amesimulia kuwa alikutana na Peter Kosovo akiwa na ujauzito wa wiki mbili. Peter akamuoa Muna na mimba yake. Muna anasema, Casto Dickson ndiye baba wa mtoto, lakini aliikataa mimba. Peter akamchukua Patrick kama mwanaye kabisa. Hivyo, Patrick alizaliwa na kujikuta ana mama na baba rasmi ambaye ni Peter.

Thamani kubwa ya Peter ipo kwa Patrick. Mtoto anapozaliwa na kuona mama na baba yake wapo pamoja, humjenga kujiamini na kujiona amezaliwa katika mfumo rasmi. Hivyo, ilikuwa wajibu wa Muna na Peter kuendelea kubaki wazazi wawili wa Patrick bila kumvuruga.

Kitendo cha Peter kumng'ang'ania Patrick kina maana ya kumlinda mtoto asivurugwe kisaikolojia. Mtoto anafikisha miaka mitatu ndiyo anaambiwa baba mwingine aliyemkimbia akiwa mimba, aliyempokea na kumjua mpaka alipofikisha umri huo eti anakuwa si baba tena.

Kama yule mama wa mwanamuziki mkubwa wa Bongo Fleva na Muna, ndani ya familia nyingi hutokea. Baba na mama hukubaliana iwe siri yao chini ya falsafa ya "Kitanda hakizai haramu." Mtoto hukuzwa bila kuona tofauti yoyote kwa wazazi wake. Tatizo Peter alikosea mwanamke wa kutunza naye siri. Muna alistiriwa, yeye kajivua stara yote.7

Labda alidhani anamuumbua Peter, ila alijiumbua yeye na kumuumiza mtoto. Pengine Patrick katika ukubwa wake Mungu angemuweka hai, angemsema sana Muna na sinema zake zenye utoto mwingi kiasi cha kumdhalilisha. Thamani ya mtoto ni baba mmoja.

Peter ndiye baba shujaa wa Patrick. Siyo Casto aliyekimbia mimba. Wanaume aina ya Peter ni wachache. Hawazaliwi kila siku!

Ndimi Luqman MALOTO

Taarifa kwa Umma: Barabara ya Nelson Mandela Imefungwa kwa Siku 3 tangu Jana

$
0
0

Kuanzia jana  Ijumaa Julai 20, 2018 hadi Jumatatu Julai 23, 2018 watumiaji wa barabara ya Nelson Mandela jijini Dar es Salaam watakumbana na usumbufu kutokana na matengenezo yatakayoanza kufanyika katika barabara hiyo eneo la Ubungo.


Kufuatia matengenezo hayo, kuanzia  eneo la mataa ya Ubungo hadi Riverside (kama unatokea Mwenge kuelekea Buguruni), itafungwa kwa siku hizo, badala yake magari yatalazimika kupita upande wa pili wa barabara hiyo hiyo (inayotoka Buguruni kuelekea Ubungo).


Hayo yameelezwa katika taarifa iliyotolewa Julai 20, 2018 na kampuni ya CCECC inayojenga barabara za juu katika makutano ya Ubungo.


“CCECC inapenda kuwajulisha watumiaji wa barabara katika makutano ya Ubungo kuelekea Nelson Mandela (Riverside) kuwa siku ya Ijumaa Julai 20 kuanzia saa tano usiku hadi Jumatatu (Julai 23) ujenzi utakuwa unaendelea na watumiaji wa barabara hii watakuwa wanapita kama inavyoonekana kwenye mchoro huu,” imesema taarifa hiyo.

Polepole Aipukutisha CHADEMA Jimbo la Mbowe

$
0
0

Viongozi wote wa Chadema Kata ya Muungano, wakiongozwa na Godliving Emmanuel Kimaro ( Baba Diana) Mwenyekiti wa Kata ya Muungano na Ibrahimu Hamis Mkindi (Mparee) Mwenezi wa Chadema Kata Muungano kutoka Wilaya ya Hai wamejivua uanachama wa Chadema na kujiunga na CCM.


Viongozi hao wamepokelewa na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Taifa Kamaradi Humphrey Polepole kwenye Mkutano wa hadhara Moshi Mjini Kata ya Mawenzi wakati akimnadi Mgombea wa Udiwani wa CCM Kata ya Mawenzi Ndg. Apaikunda Ayo Naburi. 

TCRA yafichua sababu zinazopelekea kufungia wasanii

$
0
0

Ikiwa imepita siku moja tangu Mamlaka ya Mawasiliano TCRA) kuwapatia adhabu wasanii  Irene Uwoya na mwenzake wa mitindo, Msemaji wa TCRA, Semu Mwakyanjala amesema sababu ya Mamlaka kuwa inatoa adhabu ni kutokana na Kamati ya Maudhui ya mamlaka hiyo kuwa na hadhi ya kimahakama kisheria. 

Mwakyanjala amesema wakati ilipotaka kufahamu ni hatua gani zaidi ambazo Mamlaka hiyo itakuwa inachukua dhidi ya wasanii ambao watakuwa wanakiuka sheria hiyo ya mitandao na kanuni za maadili ya mwaka 2018 licha ya wasanii wengi kuonywa. 

Amesema kwamba licha ya kwamba wasanii wamekuwa wakipigwa faini, maonyo makali lakini pia maamuzi yanayotolewa huzingatia sheria za kimahakama kwa kuwa Kamati inamamlaka na ndiyo maana hutoa nafasi ya rufaa. 

"Ninachoweza kusema kwa sasa, wasanii wanaadhibiwa na sheria na pia wanapewa nafasi ya kukata rufaa ndani ya siku 21, baada ya hapo kama atakuwa ameridhika ndipo mambo mengine yanaweza kuongelewa. Hata jana waandishi hatukuweza kuwaruhusu kuuliza maswali kwa kuwa jambo hili bado lipo chini ya sheria, baada ya siku 21 kuisha vyote ulivyokuwa unataka kujua utafamu kwa kuwa itakuwa imeshajulikana kama wamekubaliana na adhabu au laa."  Mwakyanjala. 

Mnamo Juni 20, 2018, Msanii Irene Uwoya alichapisha picha kwenye mtandao wake wa kijamii ikiwa inamuonyesha maungo yake ya ndani huku yeye mwenyewe akidai alikuwa ufukweni ndio maana alifanya hivyo. 

Kamati ya maudhui ya mamlaka ya mawasiliano (TCRA) hivi karibuni imekuwa ikiwachukulia hatua wasanii wanaokiuka sheria za mitandao iliyotungwa 2010, ambapo kanuni zake zilianza kutumika 2018.

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

$
0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

Lugola Azungumzia Suti Zake Ambazo Zimekuwa Gumzo Mitandaoni

$
0
0
Baada  ya suti za Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, kuwa gumzo kwenye mitandao mbalimbali, mwenyewe amefunguka na kufafanua juu ya suala hilo.

Kwa muda sasa, tangu ateuliwe kushika nafasi hiyo, Lugola amekuwa akivaa suti zenye bendera ya Tanzania kwenye mifuko hali ambayo imesababisha mijadala kwenye mitandao ya kijamii.

Akizungumza na Michuzi, Lugola alisema anazo suti nyingi za aina hiyo na ni yeye mwenyewe aliyeamua zifanane kwa mwonekano.

Baadhi ya wachangiaji kwenye mitandao ya kijamii wamekuwa wakihoji iweje Waziri avae suti moja muda mrefu wakidhani kuwa amekuwa akiirudia.

Lakini mwenyewe jana alijibu na kueleza kuwa suti hizo ambazo ameziita kuwa ni za aina yake, anazo nyingi lakini ameamua zote zifanane.

“Hata ninapobadilisha suti hizi hakuna anayeweza kujua kwa sababu zote zimefanana,” alisema.

Mwonekano wa suti hizo umefanya watu wengine kuzishangaa kutokana na mifuko ya shati kutengenezwa kwa bendera ya taifa.
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live


Latest Images