Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104698 articles
Browse latest View live

Ladies: JE, kweli Kuwa Usipotongozwa Kama Wiki tu Hivi Wajisikia Vibaya?

$
0
0
Hivi dada zangu huwa mnaenjoy mkiwa mnatongozwa?

Ni kweli kuwa usipotongozwa kama wiki tu hivi wajisikia vibaya?

Najua kuna suala la umri hapa kwenye sanaa hii ya utongozwaji,

Lakini napenda tu nipate jibu la jumla,

Jamani huwa mnajisikiaje?

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya July 24

$
0
0

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya July 24

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa simba said Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Maalim Hussein Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Issa simba said Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA.

Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi +255 622588038au 0679119679 au +255 713101897

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Kimenuka..Kangi Lugola Amsweka Askari Mahabusu Arusha Kwa Kushindwa Kujibu Maswali Yake

$
0
0
Askari Polisi mmoja wa Kituo cha Utalii na Diplomasia Mjini Arusha, leo amejikuta akizindua mahabusu ya kituo hicho kwa kuwekwa mahabusu kwa agizo la Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola.

Kituo hicho kilizinduliwa na Rais John Magufuli mapema mwaka huu ambapo tangu wakati huo hakijawahi kupokea mahabusu yeyote.

Waziri Lugola, ametoa agizo hilo leo Jumatatu, Julai 23 alipotembelea kituo hicho cha kisasa, ambapo akiwa hapo alimuhoji baadhi ya mambo kadhaa ambayo askari huyo alishindwa kuyajibu kwa ufasaha.

“Nimeingia kwenye chumba cha mashtaka, nikamkuta askari nikamuuliza vitabu muhimu kwenye chumba hicho akabaki ameduwaa, nikamuagiza RPC (Kamanda wa Polisi) amuweke ndani. Lakini baadaye nikaamuru atolewe kwani yawezekana askari huyo hana elimu ya masuala ya utalii,” amesema.

Amesema kama kituo hicho hakijawahi kuweka mahabusu mtu, basi askari huyo amekuwa wa kwanza kukifungua kwa kukaa mahabusu,” amesema Waziri Lugola.
=

Muonekano wa Mpya wa Elizabeth Michael (Lulu)

$
0
0
Ni miezi mitatu imepita tokea muigizaji na staa wa filamu nchini Elizabeth Michael “Lulu” aachiwe huru na kubadilishiwa adhabu yake na Mahakama Kuu ya Tanzania na kwa sasa anatumikia kifungo cha nje.

Katika mitandao ya kijamii picha ya muonekano mpya wa Elizabeth Michael imekuwa gumzo  alipohudhuria tamasha la “Awe” liloandaliwa na muimbaji wa nyimbo za Gospel Paul Clement siku ya Jumapili July 22,2018.

Picha hiyo imesambaa sana katika mitandao ya kijamii ikiwa imepostiwa na watu mbalimbali lakini kwa upande wa instagram account ya Lulu mwenyewe bado hajapost picha yoyote mpya toka October 22 2017.

Makubwa!! Afisa aliyeshtakiwa kwa kumiliki magari 19 alianza kazi TRA akiwa nayo

$
0
0
Afisa Mchunguzi wa TRA, Tumaini Fadhir ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa Ofisa Msaidizi wa Forodha wa mamlaka hiyo, Jennifer Mushi anayekabiliwa na kesi ya kumiliki magari 19 yenye thamani ya Shilingi Milioni 197 aliajiriwa TRA na mali zake.

Afisa huyo ameyaeleza hayo wakati akiongozwa na wakili wa Jennifer, Fulgence Masawe kutoa ushahidi wake mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi.

Katika ushahidi wake, Fadhiri amedai yeye ni mchunguzi wa ndani wa TRA, huku majukumu yake ni kufanya uchunguzi wa malalamiko yote na kuhakiki mali za watumishi ili kudhibiti vitendo vya rushwa.

Fadhiri alipoulizwa na wakili Masawe kwamba anamfahamu Jennifer, alijibu kuwa anamfahamu kwa sababu aliwahi kumchunguza.

Pia aliulizwa kama anafamu idadi ya mali za Jennifer na thamani yake , Tumaini alijibu anafahamu.

Pia aliulizwa Jennifer alianza kazi lini TRA, alijibu kuwa tangu mwaka 2010, lakini awali aliajiriwa katika sekta binafsi.

Pia alipoulizwa kama Jennifer aliajiriwa TRA akiwa na mali zake, Fadhir alijibu ndio.

Pia alipoulizwa ametumia mfumo gani kubaini idadi ya magari ya Jennifer, amedai kuwa alitumia mfumo wa usajili wa magari lakini hajawahi kuyaona kwa macho.

Naye wakili wa serikali Peter Vitalis alimuuliza Fadhiri ni mali gani ambazo Jennifer anamiliki, amedai kuwa ni zaidi ya magari 10 na waliyabaini kwa sababu alishindwa kuorodhesha vitu hivyo.

Baada ya kutolewa ushahidi huo, Hakimu Shaidi ameahirisha kesi hiyo hadi August 16,2018.

Mushi anakabiliwa na kosa la kumiliki magari 19 ambayo anadaiwa aliyaingiza nchini kutokea Japan yakiwa na thamani ya shilingi Milioni 197,601, 207.

Makonda Ampongeza Rais Magufuli Kufanikisha Hatua Za Kuanza Kwa Ujenzi Wa Daraja La Salender

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mh. Paul Makonda amempongeza Rais Dkt,John Magufuli  kwa kufanikisha zoezi la utiaji saini baina ya serikali ya Tanzania na Korea Kusini.

Mh. Makonda ametoa pongezi hizo kupitia andiko lake alilolitoa saa chache mara baada ya zoezi hilo kukamilika ambalo liko hapo chini.

"Kwa niaba ya Wananchi wa Mkoa wa Dar es salaam napenda kumpongeza Rais wetu Mpendwa Dkt. John Magufuli kwa kufanikisha utilianaji saini Baina ya Serikali ya Tanzania na Korea Kusini kuashiria kuanza kwa ujenzi wa Daraja la Salender litakaloanzia Coco Beach hadi Agha Khan hospital kupitia bahari ya Hindi ambalo litasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza tatizo la msongamano wa magari lililokuwa likipelekea upotevu wa mabilioni ya shilingi.

"Rais Dkt. John Magufuli ameamua kutujengea Daraja hili la kisasa baada ya kujionea adha ya foleni inayowasumbua watumiaji wa Daraja lililopo sasa ambalo kimsingi ni finyu na haliwezi kumudu idadi kubwa ya magari yaliyopo sasa.

Mbali na *kupunguza foleni ujenzi wa daraja hili la kisasa litasaidia kuboresha mandhari ya Jiji letu la Dar es salaam huku wananchi tukiombwa kuendelea kutoa ushirikiano wakati wote wa ujenzi na kuendelea kuweka jiji letu safi kwani mji wetu Ndio kitovu cha biashara na uchumi wa taifa letu.

Ujenzi wa *Daraja la Salender utagharimu zaidi ya Shilingi Billion 250 ambapo itachukuwa muda wa miezi 36 hadi kukamilika na litakuwa na urefu wa Km 1.03 kwa upande wa baharini huku likiwa na uwezo wa kuhimili zaidi ya Tani 180 kwa wakati mmoja na magari zaidi ya 55,000 kwa siku.
HAKIKA HUU NDIO UTEKELEZAJI WA YALE ULIYOWAAHIDI WANANCHI KUPITIA ILANI YA CCM."

Mbunge Avuliwa Udiwani Kwa Kutohudhuria Vikao

$
0
0
Mkurugenzi wa Jiji la Tanga, Daudi Mayeji ametangaza Kata ya Ngamiani Kusini kuwa wazi  kutokana na Diwani wake ambaye pia ni Mbunge wa Tanga Mjini, Mussa Mbaruku (CUF), kutohudhuria vikao zaidi ya sita vya Baraza la Madiwani.

Mayeji amesema mbunge huyo amepoteza sifa kwa mujibu wa Sheria ya Mamlaka za Majiji.

“Sheria ya Serikali za Mitaa, Mamlaka ya Majiji Sura ya 228, kifungu cha 30B ndiyo imemuondoa, ni kwa mujibu wa sheria,” amesema Mayeji.

Mbaruku aligombea nafasi hizo za ubunge na udiwani katika chaguzi Mkuu mwaka 2015, kupitia Chama cha Wananchi (CUF) na kushinda zote.

Download Hapa Application ya Udaku Special Kwenye Simu Yako Kushuhudia Vimbwanga Mtaani na Stori za Mapenzi

Zitto Kabwe Aendelea Kuikosoa Serikali.."Ningekuwa Mimi Ningefanya Tofauti"

$
0
0
NingefanyaTofauti

Na Zitto Kabwe

KWA miaka mingi nimekuwa mtu ninayeamini katika kujipa muda wa upweke na kutazama dunia iliyonizunguka na kujiuliza maswali ama kunihusu mimi binafsi au kuhusu nchi yangu na Afrika.

Siku chache zilizopita, nilijipa muda huo wa utulivu kwa ajili ya tafakari. Swali kuu nililokuwa nikijiuliza ni hili; kwamba kama ningekuwa nimepewa mamlaka ya kuongoza Tanzania nini ningefanya tofauti na wanaoongoza sasa?

Hitimisho la tafakuri yangu likaangukia wilayani Ludewa mkoani Njombe. Kwenye utajiri ule wa chuma na mkaa wa mawe katika maeneo ya Liganga na Mchuchuma, nikaona kuna suluhisho la matatizo yetu yanayoendelea kiuchumi.

Mchuchuma na Liganga

Madini ya chuma na makaa ya mawe ndio msingi wa maendeleo ya viwanda duniani kote. Nchi yetu ina madini haya yote kwenye eneo moja, wilayani Ludewa mkoa wa Njombe.

Katika eneo la Mchuchuma kuna mashapo yenye tani bilioni 1.2 makaa ya mawe yenye uwezo wa kuzalisha Umeme 600MW kwa miaka 150. Makaa hayo pia hutumika kuyeyusha chuma na kuzalisha chuma cha pua. Vilevile eneo la Liganga lina mashapo ya madini ya chuma tani bilioni mbili ambayo ndani yake kuna madini yenye thamani kubwa ya Titanium na Vanadium.

Afrika nzima inajenga reli za kisasa na zote zinahitaji chuma kwa ajili ya kujenga njia za reli. Kenya na Ethiopia wamemaliza hatua za kwanza za reli zao ambapo Kenya imeshajenga kilometa 485 kutoka Mombasa mpaka Nairobi na Ethiopia kilometa 760 kutoka Addis Ababa mpaka Djibouti. Miradi yote hii mataruma ya reli yameagizwa kutoka nje na kuletwa Afrika na hivyo kuzalisha ajira huko kwenye nchi hizo (ambazo mataruma hayo yamezalishwa ).

Tanzania ingeamua, ingeweza kulisha miradi yote ya reli chuma kutoka Ludewa katika nchi za Kongo, Zambia, Angola, Uganda na Rwanda ambao wote wana miradi ya ujenzi wa reli na wamepanga kuagiza chuma kutoka China na kwingineko.

Bei ya tani moja ya chuma kwenye soko la dunia ni dola za Marekani 600 mpaka 1000. Kwa hiyo Tanzania ikizalisha chuma tani milioni moja tu kwa mwaka, inaweza kupata mapato ya fedha za kigeni kati ya dola milioni 600 mpaka dola bilioni moja kwa mwaka.

Jambo kubwa sana ambalo Tanzania imebahatika ni kwamba mashapo ya chuma yana madini mengine yenye thamani kubwa zaidi. Kwa mfano Vanadium ya Ludewa inauzwa tani moja dola 50,000 katika soko la dunia. Katika kila tani milioni moja ya chuma kutoka Ludewa, kuna tani 80,000 ya Vanadium. Tukiuza madini haya tunapata fedha za kigeni dola za kimarekani bilioni nne kwa mwaka.

#NingefanyaTofauti

Nchi yetu ina changamoto nyingi kiasi kwamba ni vigumu kuchagua ufanye ipi na uache ipi. Kiongozi mwenye maarifa huanza kutafuta fedha kwanza atekeleze majukumu mengine.

Viongozi wetu wa sasa wameamua kuanza kwa kutumia fedha za kodi au mikopo ghali yenye riba kubwa kutoka mabenki ya biashara ya nje. Wameanza na ujenzi wa reli wa dola bilioni saba, ununuzi wa ndege wa zaidi ya dola bilioni moja ( Dreamliner ‘Terrible Teen’) imenunuliwa kwa dola milioni 224 na hata ujenzi wa bwawa la kuzalisha umeme la Rufiji maarufu kwa jina la Stiglers Gorge litakalogharimu dola bilioni 3.5.

Ningekuwa na mamlaka ningeyafanya haya yote, lakini kabla ya kufanya hayo, ningeanza kwanza kwa kufanya jambo moja kubwa ambalo lingenipa fedha za kufanya hayo. Ningefanya tofauti.

Ningeanza na mradi wa Mchuchuma na Liganga kwa kuhakikisha kuwa uwekezaji unaanza mara moja na uzalishaji wa chuma na makaa ya mawe unafanyika bila kuchelewa. Ningehakikisha kuwa ndani ya miaka 2 tunaanza uzalishaji wa chuma, Vanadium na Titanium.

Mauzo ya Vanadium peke yake ni sawa na dola bilioni nne kwa mwaka ambapo kwa kuwa haya ni bidhaa ambatana na chuma maana yake 80% ya mapato haya yangekuwa ya nchi. Kwa hiyo mwaka wa kwanza tu wa uzalishaji ningeweza kupata dola bilioni 3.2. Kwa fedha hizo, tungejenga reli kuanzia Dar mpaka Dodoma kwa mara moja bila kuungaunga na kubakia na chenji ya dola bilioni moja ambazo ningeweza kujenga hospitali tano kubwa kama Mloganzila katika kanda tano za nchi; Mbeya, Mtwara, Mwanza, Kigoma na Arusha.

Ningeweza kujenga vyuo vya VETA kila Mamlaka ya Serikali za Mitaa nchini ( Wilaya, Miji, Manispaa na Majiji ) kwani unahitaji shilingi bilioni 750 tu kujenga vyuo hivyo vilivyokamili na vifaa vya kutosha vijana kupata mafunzo.

Ningeweza kujenga vyuo vikuu vipya vitatu aina ya UDOM kwani UDOM moja ina thamani ya shs bilioni 800 tu. Haya ni mapato ya mwaka wa kwanza tu. Kumbuka kuwa tunaweza kuendelea kuchimba chuma tani milioni moja kwa mwaka kwa miaka 2000!

Kwanini hatuwekezi Mchuchuma na Liganga?

Kungoza nchi kunahitaji MAARIFA. Hakika #NingefanyaTofauti

Maskini...Ndoto ya Wema Sepetu ya Kupata Ubunge Basi Tena

$
0
0
DAR: Hatma ya staa wa filamu Bongo, Wema Isac Sepetu katika midani za siasa nchini, imeingia dosari kutokana na hukumu ya kifungo cha mwaka mmoja jela au faini ya Shilingi milioni 2 iliyotolewa juzi na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu dhidi yake.

Wema ana ndoto ya kuwa mwanasiasa, hususan katika nafasi ya ubunge. Mwaka 2015 msanii huyo alienda mkoani Singida kugombea ubunge kupitia viti maalumu vijana, lakini alikosa.Pamoja na matokeo hayo, watu walio karibu na mrembo huyo, wamekuwa wakieleza kuwa bado ana ndoto ya kurudi kwenye kinyang’anyiro cha siasa katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Hata hivyo, hukumu iliyotolewa juzi dhidi yake baada ya kupatikana na hatia ya kukutwa na kutumia madawa ya kulevya aina ya bangi, imemwondolea sifa ya kugombea ubunge na kuwa kiongozi wa umma. Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kifungu 67 (2)c na d, inasema kuwa, ikiwa mtu amehukumiwa na Mahakama yoyote katika Jamhuri wa Muungano wa Tanzania na kupewa adhabu ya kifo au kufungwa gerezani kwa muda usiopungua miezi sita kwa kukutwa na hatia ya kosa lolote linaloambatana na utovu wa uaminifu, hataruhusiwa kugombea uongozi wa umma.

Katiba hiyo imebainisha pia kuwa ikiwa katika kipindi cha miaka mitano kabla ya uchaguzi mkuu kama mtu amepata kuhukumiwa na kupewa adhabu ya kifungu kwa kosa linaloambatana na utovu wa uaminifu au kuvunja sheria ya maadili ya viongozi wa umma hataruhusiwa kuwania uongozi.Mwanasheria maarufu nchini Emmanuel Elias alithibitisha kuwa kwa kosa na adhabu aliyopata Wema, anaweza asiruhusiwe kugombea uongozi wa umma kama atawekewa kipingamizi.

“Ninachojua kuna sheria inayozungumzia suala hilo, kwamba kama mtu amethibitika kufanya kosa na Mahakama ikamwadhibu kwa kifungo kinachozidi miezi sita atazuiwa kugombea uongozi, na hili ni suala la kikatiba,” alisema Elias.Ijumaa Wikienda lililokuwepo mahakamani siku ya hukumu ya kesi ya Wema, lilibahatika kunasa sauti ya jaji mmoja ambaye pia alieleza jinsi ambavyo kuna ugumu Wema kuwania nafasi za kisiasa.

“Yaani Wema ni kipenzi sana cha watu lakini kutokana na kuhukumiwa zaidi ya miezi sita basi amepoteza nafasi yake hiyo ambayo naamini kabisa mwaka 2020 angeweza kupata ubunge bila kipingamizi kikubwa,” alisikika jaji huyo akizungumza nje ya mahakama siku ambayo Wema alihukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela, lakini akalipa faini ya Shilingi milioni 2.

Hata hivyo, baadhi ya wanasheria wameleeza kuwa uzuri wa sheria ni kung’ata pande zote. Wakasema Wema anaweza akagombea tena kama atakata rufaa kupinga hukumu hiyo na kufanikiwa kushinda tena kesi hiyo.

Katika hatua nyingine, staa wa filamu Bongo, Kajala Masanja ametoa sababu za kutokuwa mstari wa mbele kumlipia faini staa mwenzake Wema Sepetu, kama Wema alivyomlipia yeye faini ya Shilingi milioni 13 ili asiende jela miaka saba miaka ya nyuma.

Akizungumza na Ijumaa Wikienda, Kajala ambaye kwa sasa yupo nchini Dubai, alisema kuwa kama angetakiwa kusaidia kumlipia Wema faini hiyo asingekuwa na tatizo, angemlipia.

“Ningejua na kuwa na hakika Wema hawezi kulipa hiyo faini, ningemlipia hata kama ni kwa kukopa hizo pesa, lakini mimi sikuwepo nchini wakati Wema anahukumiwa,” alisema.

Hata hivyo Kajala ameeleza kusikitishwa kwake na taarifa zinazosambaa kuwa amemtelekeza rafiki yake Wema akisema; “Jamani mimi naona watu wanasema sikuonekana mahakamani, lakini hawajui kama nipo au sipo, hata hivyo kama ingehitaji faini ambayo kubwa kwa kweli mimi nisingeshindwa hata ya kukopa ningemlipia.”

Kajala alisisitiza; “Sio kwamba sikuwa napenda kwenda mahakamani kuungana naye, kulikuwa na vitu vinaendelea kwa upande wangu hivyo ikaniwia vigumu.”

STORI: Imelda Mtema, DAR

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume, nasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za:

GUMBA POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.

NTINJE:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0754741788, 0715741788, 0783741788

-DR MAGISE

Diamond Acharukia Sakata la Kuhusishwa na Ushoga

$
0
0
KUFUATIA kusambaa kwa picha zikimuonesha akiwa ametinga kikuku mguuni kisha kushambuliwa akihusishwa na skendo ya ushoga, hatimaye staa wa Afro-Pop, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amevunja ukimya.

 Mara baada ya picha hizo kusambaa na kuibua gumzo huku baadhi ya watu wakimtolea povu, Diamond alianza kuitwa shoga, skendo ambayo ilikamata vilivyo hasa kwenye mitandao ya kijamii na kumjengea picha tofauti kwa mashabiki wake.

 MASHABIKI WAKASIRISHWA

Baadhi ya mashabiki hao kwenye mitandao hiyo walikasirishwa na kitendo hicho hivyo kummwagia matusi ya nguoni kutokana na kuchukizwa na kitendo hicho. Hoja kuu kutoka kwa mashabiki hao ilikuwa kwamba, jambo hilo haliendani na utamaduni wa Kitanzania na kwamba wanaofanya hivyo ni mashoga na lengo lake ni kuharibu vijaja wadogo wa Kitanzania.

 DIAMOND HAKUPEWA NAFASI

Katika hali kama hiyo, Diamond hakupewa nafasi ya kujitetea au kufafanua juu ya jambo hilo hivyo Ijumaa Wikienda lilijipa jukumu la kumtafuta ambapo alifichua siri ya kutinga kikuku hicho.

MAHOJIANO AKIWA MAREKANI

Katika mahojiano na gazeti hili akiwa kwenye ziara ya kimuziki nchini Marekani, awali Diamond alikuwa mkali akionesha kuchukizwa na jambo hilo alilodai ni baya mno na kwamba hata yeye anachukizwa na vitendo hivyo vichafu. “Kwanza sijui kama kile ni kikuku, nilivaa kama ninavyovaa mikufu au cheni.“Niliona ni urembo kama urembo mwingine na kwamba haiwezi kuwa ishu kubwa kama ilivyotokea,” alisema Diamond.

 Aliendelea kutirika kuwa, ni vyema ikafahamika kwamba, hata yeye anachukizwa sana na tabia ya ushoga kwa hiyo aliwataka wanamwita shoga kuacha mara moja. “Ninawaomba chondechonde waache kunihusisha na jambo hilo baya, ujue nyuma yangu kuna watu wengi mno wanatamani kuwa kama mimi hasa vijana wadogo.

 “Sasa wakiona ninahusishwa na jambo ambalo linapigwa vita nchini mwetu, wataacha kunifuatilia kama mtu wanayetamani kuwa kama yeye,” alisema Diamond na kuongeza: “Lakini unajua imekuwa ni kasumba kwa watu maarufu kuhusishwa na jambo hilo ili kuwajengea picha fulani kwa mashabiki au wafuatiliaji wake.
AMTAJA MICHAEL JACKSON, RONALDO

“Mtu kama marehemu Michael Jackson (aliyekuwa staa wa Muziki wa Pop duniani) alikuwa akihusishwa na ushoga, lakini hakuna aliyekuwa na ushahidi labda ilitokana tu na ishu za kujibadilisha mwili au sura. “Kwa hiyo si jambo geni kwa watu maarufu kusikia eti fulani ni shoga. Jambo hilo linaweza kuwa linatengenezwa na mpinzani wako.

 “Hata Cristiano Ronaldo (mchezaji wa Timu ya Juventus ya Italia aliyetua akitokea Real Madrid) amekuwa akihusishwa na ushoga, lakini amekuwa akipotezea na kuendelea kupiga hela. Kama nilivyosema si jambo geni lakini limenichefua sana.

AOMBA RADHI

“Najua mimi kama mtu wao nimewaudhi hivyo ninawaomba radhi na nisingependa waendee kunihusisha na dhambi hiyo.”

STORI: GPL

Lulu Diva 'Rich Mavoko Amebadili Maisha Yangu'

$
0
0
MWANADADA Lulu Abass ‘Lulu Diva’ amebonga kwamba miongoni mwa vitu vilivyombadilisha maisha yake hasa kwenye gemu la Muziki ni wimbo wake wa Ona aliomshirikisha Rich Mavoko.

Akichezesha taya na Star Showbiz, Lulu Diva alieleza kwamba nyimbo zake za nyuma zilikuwa ni nzuri na zilifanya vizuri lakini baada ya Wimbo wa Ona, umemfanya atambulike kwenye gemu la Bongo Fleva kama msanii mkubwa na kumpatia shoo za kila mara.

“Wimbo wa Ona umenipeleka kwenye levo nyingine kabisa kiukweli. Kwa sasa na mimi ni miongoni mwa wasanii wakubwa, shoo zimeongezeka na hata hadhi pia,” alisema Lulu Diva.

GPL

Mkapa Kumwakilisha Rais Magufuli Katika Hafla Ya Maadhimisho Ya Miaka 50 Ya Frelimo

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. John Magufuli amemteua Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa kumuwakilisha katika maadhimisho ya miaka 50 ya mkutano wa pili wa chama tawala cha Msumbiji (FRELIMO) .

Maadhimisho hayo yatafanyika tarehe 25, Julai katika jimbo la Niassa ambapo kutokana na majukumu mengine ya kitaifa Rais amemuagiza Mkapa kumuwakilisha ambaye ataongozana na Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (Bara), Philip Mangula.

Kupitia taarifa iliyotolewa leo na Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, imesema kuwa Mkapa na ujumbe wake wanatarajia kuondoka nchini tarehe 24 Julai, 2018 na kurejea tarehe 26 Julai, 2018.

“Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Mhe. Filipe Nyusi alimwalika Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kushiriki maadhimisho hayo. Kutokana na majukumu mengine ya kitaifa Mhe. Rais Magufuli hatoweza kushiriki”, imesema taarifa.

Aidha taarifa imeongeza kuwa Tanzania na Msumbiji zimeendelea kushirikiana katika masuala ya kiuchumi na biashara kwa kuzingatia ujirani na muingiliano mkubwa wa wananchi wa nchi hizi mbili, hususani katika Mikoa ya Ruvuma na Mtwara kwa upande wa Tanzania, na Majimbo ya Niassa na Cabo Delgado kwa upande wa Msumbiji.

Lema awaomba wakazi Arusha Kuipiga chini CCM na Kuchagua CHADEMA

$
0
0
Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema amewataka wakazi wa Arusha, kuonesha hasira zao za kuwa na maisha magumu kwa kuwachagua wagombea wa udiwani wa Chadema.

Akizungumza jana katika uzinduzi wa kampeni katika Kata ya Daraja Mbili, Lema alisema Chadema inaingia katika uchaguzi mdogo ili kuonyesha majaribu ambayo Taifa linapita kwa sasa licha ya hofu kutawala .

"Katika uchaguzi huu, hatupambani na (Prosper) Msofe (mgombea wa udiwani wa CCM) ambaye alikuwa diwani wetu na tulipambana na damu kumwagika ili awe diwani lakini amejiuzulu na kujiunga na CCM, sisi tunapambana kwa ajili ya maisha ya Watanzania," alisema Lema

Alisema hivi sasa hali ya maisha ni ngumu, biashara nyingi zimefungwa, migodi imefungwa na maisha ni magumu na hakuna sehemu ya kuonyesha hasira hizo zaidi ya kutowapigia kura CCM.

"Hivi sasa akina dada warembo wanakunywa konyagi ukiwauliza vipi wanasema eti wanapunguza mafuta mwilini, lakini hapana, tatizo hali ni ngumu ya maisha," alisema

Hata hivyo, alisema tatizo kubwa la Watanzania ni woga, hawataki kusimama na kutetea ukweli jambo ambalo madhara yake yataendelea kuwa makubwa.

Aliwaomba wakazi wa Kata ya Daraja Mbili, kumpigia kura mgombea wa Chadema, Masudi Sungwa ili aendelee kuwasaidia kutatua kero zao.

Kwa upande wake,  Masudi Sungwa aliomba kura kwa wakazi wa kata hiyo na kueleza kero zao atazishughulikia vyema akishirikiana na baraza la madiwani wa Jiji la Arusha ambalo linaongozwa na Chadema.

Hii Hapa Historia ya Mwanamuziki Michael Jackson..Inasikitisha !

$
0
0
Michel Jackson alizaliwa tarehe 29 August mwaka 1958, akiwa ni mtoto wa nane kati ya kumi wa mzee Joe Jackson na Catherine Jackson, alikuwa na madada wa 3 ambao ni Rebbie, La Toya na Janet, huku makaka zake ni Jackie, Tito, Jermaine, Marlon, Randy, na ndugu yake mwingine anayeitwa Brandon alifariki muda mfupi baada ya kuzaliwa.

Alianza kuimba akiwa umri wa miaka mitano akiwa na kundi la Jackson 5, kundi lakifamilia kwani waimbaji wote katika kundi hilo walikuwa ni ndugu zake wa damu, kundi hilo lilifanya vizuri sana nchini marekani na dunia nzima kwa ujumla.

Jackson hakuwa na mahusiano mazuri na baba yake Joe Joseph Jackson aliwahi kusema kuwa alikuwa na kawaida ya kumchapa Michael wakati akiwa mtoto, na Michael aliwahi kulalamika kuwa baba yake alikuwa akimnyanyasa kwa kumpiga hasa wakati wa Rehalse ingawa aliwahi kukiri kuwa baba yake alichangia kwa kiasi kikubwa yeye kupata mafanikio.

1968 Boby Taylor na The Vancouver waliligundua Kundi la Jackson 5 ambapo kundi hilo likasign na Motown Records na walifanikiwa kurekodi ngoma zilizotisha enzi hizo kama ABC, I want u Back, I’ll be there na nyinginezo, walirekodi album 14 na Motown na Michael alirekodi album nne za solo.

Jackson 5 walikaa na Motown mpaka ilipofika mwaka 1976 ambapo walidai wanataka uhuru wa kisanii na baada ya hapo wakaenda kusign na Epic, na kundi hilo lilibadilisha jina kutoka the Jackson 5 na kujiita The Jacksons na walirekodi album 6 kutoka 1976 mpaka 1984

1977 Michael alikutana na mtaarishaji wa muziki maarufu enzi hizo Quincy Jones chini ya Epic Records akarekodi album inayoitwa OFF THE WALL, ambayo ilifanya vizuri sana katika chart za nchi marekani.

1982 Wacko Jacko alirelease album ambayo inasemekana ni album ambayo imeuza sana kuliko album yoyote duniani, inaitwa THRILLER, ndani ya album hii kulikuwa na Single 7 ambaao zilihit sana dunia nzima, album hii iliuza copy milioni 50 dunia nzima, alifanya kazi na the best Producers na Directors na kufanikiwa kutengeneza Music video ya Thriller ambayo mpaka leo budget ya kutengeneza music video hiyo haijawahi kuvunjwa na msanii yeyote duniani.

1984 Wacko Jacko akavunja rekodi kwa kutunukiwa tuzo 8 za grammy ndani ya usiku mmoja, tuzo hizo zilitokana na Album yake ya Thriller na kitabu cha “T story book.”

Tarehe 9 December 1984 katika concert ya mwisho ya Jackson 5 iliyoitwa Jackson Victory Tour, Wacko Jacko akatangaza kuwa anajitoa kutoka kundi hilo na atakuwa anafanya kazi zake binafsi,

1987 Michael Jackson akarelease album yake iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu na mashabiki wake album inaitwa BAD na kuvunja rekodi ya Tour za msanii mmoja mmoja yaani Solo, kwani show zake zilikuwa zikihudhuriwa na malaki ya watu kila nchi aliyokanyaga..

1988 MJ kwa mara ya kwanza aliandika Autobiography yaani kitabu ambacho alizungumzia maisha yake kutoka utotoni na kazi yake ya muziki, Autobiography hiyo iliitwa MOON WALK.

Mwishoni mwa miaka ya 80 Mj alitajwa kama msanii wa Decade kutokana na mafanikio aliyoyapata katika Album zake za Thriller na Bad.

1991 MJ alisign mkataba na kampuni ya Sony Music, ambapo inasemekana ni mkataba mkubwa kuwahi kusainiwa na wanamuziki enzi hizo, MJ akatoa album yake ya nne Dangerous,

1992 akaanza kupiga Tour tena, na safari hii akazungukia nchi ambazo hazikuwahi kutembelewa na mwanamuziki yeyote wa POP na Rock , ambapo pia aliunda foundation ya kusaidia watoto maskini dunia nzima, iliitwa HEAL THE WORLD FOUNDATION, safari hii alifika mpaka nchini Tanzania kama mnakumbuka jamaa alifikia katika Hoteli ya Kilimanjaro jijini Dar es salaam.

1994 MJ alimwoa LISA MARIE PRESLEY. Mtoto wa Elvis Presly, na ndoa yao ilidumu kwa miezi 19 tu na kutalikiana mwaka 1996

1995 MJ akarelease Double album ambayo aliita History, nusu ya Album hii ilikuwa ni ngoma mpya na nusu iliyobaki ilikuwa ni Greatest hits.

1996 alioa kwa mara ya pili na safari hii bahati ilimwangukia Debbie Rowe ambae alikuwa na nurse na walikutana na MJ katika Hospitali aliyokuwa akifanya kazi Debbie na inasemekana MJ alienda kutibiwa Ngozi. Pamoja walifanikiwa kupata watoto wawili ambao ni Paris na Prince Michael.

1997 MJ alirelease remix album aliyoiita BLOOD ON THE DANCE FLOOR.

2001 MJ alisherehekea miaka 30 ya kufanya kazi kama Solo Artist na alipiga show jijini Newyork na wasanii kibao wa kizazi kipya ambao walirudia kuimba ngoma zake live, wasanii hao ni pamoja na Shaggy, Whitney Houston, Destinies Child, Usher Raymond na wengine kibao.

2001 MJ alitoa album nyingine INVICIBLE ndani yake kulikuwa na Single kama U ROCK MY WORLD, na CRY.

2003 MJ akaachia single mpya ONE MORE CHANCE.

2009 March MJ akatangaza Come back Tour ambayo ilitakiwa kupigwa 02 ARENA jijini London mwezi wa saba, ilipanga kupiga tour kwa siku 10 lakini wadau wakataka aongeze siku 50 za Tour, zaid ya Tiket laki saba na nusu ziliuzwa, na tiket zote hizo ziliuzwa dakika chache tu baada ya tangazo lake..

Tarehe kama ya leo June 25, mshumaa ukazimika ghafla kwa ugonjwa ambao kitaalamu unajulikana kama Cardiac Arrest, familia ya MJ ilitangaza kuwa the greatest Singer of all time amefariki dunia.

Tutakumbuka MJ kwa mchango wako ulioutoa kwa watu weusi dunia nzima, kwani baada yako kila mtu aliamini kuwa mtu mweusi anaweza kufanya chochote na kikapendwa dunia nzima bila kujalisha ni wa rangi gani..

Billnas Afunguka Kushindwa Kupata Mbadala wa Nandy

$
0
0
HITMAKER wa Ngoma ya Labda, William Lyimo ‘Bill Nas’ amefunguka kwamba anatamani sana kuwa kwenye uhusiano lakini kinachomfanya mpaka sasa kuwa ‘single’ ni kwamba hafahamu mwanamke yupi ni sahihi kwake.

Akipiga stori na Star Showbiz, Bill Nas ambaye aliwahi kuwa katika uhusiano na msanii mwenzake, Faustina Charles ‘Nandy’ alifunguka kwamba hahitaji kukurupuka, anachotamani ni kupata mtu sahihi ili aweze hata kufunga naye ndoa na si kuwa kwenye uhusiano ambao unaanza leo na kumalizika kesho.

“Watu wanaweza wasiamini lakini ukweli ni kwamba kwa sasa sina uhusiano wa aina yoyote ile. Kinachonikwamisha kuingia ni kwamba sioni bado mwanamke sahihi wa mimi kuwa naye. “Ninasubiri pengine Mungu anionyeshe, huyo nitakayempata ndiye atakuwa mke wangu na sihitaji uhusiano wa kuanza leo na kuvunjika kesho,” alisema Bill Nas.

BONIPHACE NGUMIJE

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

Ali Kiba Asajiliwa Rasmi Kuichezea Coastal Union, Kilichobaki ni Saini Yake Tu

$
0
0
Uongozi wa klabu ya Coastal Union ya jijini Tanga umethibitisha kutarajia kumsajili msanii wa muziki wa Bongo, Alikiba kwaajili kuitumikia timu hiyo msimu ujao wa ligi kuu soka Tanzania Bara.

Alikiba anayetamba na kibao chake cha Mvumo wa Radi huenda akaanza kuonekana kwenye mechi mbalimbali za ligi kuu kupitia na timu yake ya Coastal Union endapo usajili huo utakamilika.

Kupitia kipindi cha Esports kinacho ruka kwenye radio ya E FM, Mwenyekiti wa klabu ya Coastal Union, Steven Mguto amethibitisha kuwa kwenye mazungumzo na msanii huyo ili kupata huduma yake ya kukipiga katika kikosi cha wagosi hao wa kaya.

"Kiukweli siku zimebaki kidogo lakini na sisi kama zoezi letu limefikia ukingoni nafikiri mpaka kesho tutakuwa kwenye nafasi nzuri ya kueleza nani na nani tumemsajili.

"Kwa sababu kwa sasa ndiyo tunamalizia watu wengine maswala ya mikataba sasa sirahisi kuweza kumtaja mkataba bado haja saini mwisho wasiku anaweza akageuza nia na ikawa kitu kingine.

"Kwa kiasi kidogo kuna ukweli wa kutaka kumsaini Alikiba lakini pia mambo haya jakaa sana sawa lakini wenyewe mnamuona naye ni mchezaji ingawaje si wa kiwango cha juu kwasababu hana mazoezi ya mara kwa mara ya kucheza mpira hivyo kuwa katika mazungumzo ni kweli.

Alikiba ataweza kuisaidia Coastal Union licha ya uchezaji ndani ya uwanja lakini pia ataweza kuibeba klabu hiyo kupitia umaarufu wa staa huyo wa muziki nchini na bara zima la Afrika.

Klabu ya Coastal Union imepanda rasmi ligi kuu mwaka huu baada ya kuiyaga michuano hiyo msimu wa mwaka 2015/16.
Viewing all 104698 articles
Browse latest View live


Latest Images