Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104745 articles
Browse latest View live

Mpishi Amchinja na 'kumpika' Mpenziwe

$
0
0
Mwanamume ambaye kazi yake ni ya upishi nchini Australia, anadaiwa kumuua mpenzi wake na kumkatakata vipande na kupika baadhi ya sehemu zake za mwili.
Aliyafanya unyama huo kabla ya yeye mwenyewe kujitoa uhai wake.
Marcus Volke, mwenye umri wa miaka 28, alijikataa koo yake huku akiwatoroka polisi waliokuwa wamekuja kufanya uchunguzi baada ya majirani zake kuripoti kuwepo harufu mbaya mfano wa nyama iliyooza iliyokuwa inatoka nyumbani kwa mwanamume huyo.
Maafisa wa polisi walipata sehemu za mwili wa mwanamke huyo zikitokota kwenye sufuria iliyokuwa imejazwa kemikali huku vipande vingine vikiwa kwenye karatasi za plastiki za takataka nje ya nyumba katika mtaa wa kifahari za Teneriffe.
Taarifa hii ni kwa mujibu wa jarida la Brisbane Courier Mail. Mwanamke huyo raia wa Indonesia bado hatajambulishwa rasmi.
Wapenzi hao waliokuwa wanaishi pamoja walikutana wakiwa wanafanya kazi kwa meli za kifahari na wote walikuwa wameajiriwa.
Wakazi wa mtaa huo waliambia vyombo vya habari kuwa harufu mbaya ilikuwa inatoka katika myumba ya Volke na ikazidi kuwa mbaya siku ziliposonga.
"nilipotoka nje harufu hiyo ilisababisha machozi kutoka machoni na hata kunifanya kujihisi mgonjwa,'' alisema mkazi mmoja. ''Ungedhani chakula cha Mbwa au nyama ilikuwa imeachwa nje kwa siku kadhaa.''
Polisi wangali wanafanya uchunguzi.

Ukiachika Kama Siyo Malaya Utakuwa Malaya! Kama ulikuwa Malaya Utakuwa Malaya Zaidi na Zaidi

$
0
0
Tumekushauri kuvumilia umekataa katakata 'siwezi kuishi na huyu mwanaume, ni malaya sana, ataniua bure na maradhi'. Umeamua mwenyewe kuachika, tena kwa maneno ya kejeli eti najimudi kiuchumi so maisha yataenda tu bila huyu mume.

Haya! ndg zako tumeamua kukuacha uishi utakavyo mwenyewe na maisha yako. Cha ajabu hata miezi sita haijafika na wewe unakazi ya kukitomb....tu!! tulidhani wewe utaendelea kutulizana, mbona sasa na wewe unakazi ya kuwapanga tu!! Bora hata ungekuwa na mmoja tungedhani pengine ndo unategemea awe hubby mpya, sasa huo msululu ndg yangu, si unatutia aibu hata sisi ndg zako!? Halafu sasa tukutofautisheje na ulichokimbia kwa mumeo?

My general rule: ukiachika kama hukuwa malaya basi utaanza kuwa malaya, na kama ulikuwa malaya basi ndo utakuwa malaya hataree.

Msinitusi tafadhali, ni kauzoefu wangu ktk kuishi na kuona na ku-experience mengi ya mahusiano.

Kumekucha : Maalim Seif Hamad Kujiuzulu Umakamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar...

$
0
0
Hali ya mambo visiwani Zanzibar siyo nzuri hata kidogo, (wala si ya kufurahia) toka jana jioni ilipotoka taarifa ya kufukuzwa kazi kwa Mwanasheria Mkuu wa SUK Athuman Masoud.

Kumekuwa na vikao usiku kucha kwa viongozi na wanachama wa CUF Zanzibar, na kuazimia pamoja na mambo mengine kufanya tathimini ya "KUJIUZULU" kwa makamo wa kwanza wa rais wa serikali ya umoja wa kitaifa. Maalim Seif.

Naam, mmoja wa vijana aliepewa kazi ya kupima upepo ambaye ni mwanasheria wa CUF, anaangalia swala hili kisheria (ikumbukwe kuna makubaliano ya kisheria katika kuongoza SUK).

Baadhi wamepewa angles tofauti na kutoa majibu mapema iwezekanavyo.
Ili Mheshimiwa achukue uamuzi Mgumu haraka leo.

Kama ikiwa ndio hivyo, kesho Media zote ni kujiuzulu kwa Sharif na si kupokeaji wa katiba.

My take:
Kama karidhia yeye mwenyewe Mh.Maalim, na iwe hivyo ila kama ni kupata attention ya media tu siyo.

Stay tuned...
Source:Jamii Forums

Wakamatwa na Polisi kwa Kulima Shamba Huku Wakiwa Uchi wa Mnyama

$
0
0
Watu wanne wa familia moja wamekatwa na polisi katika kata ya Busega, mkoani Simiyu baada ya kukutwa wakilima huku wakiwa uchi. Kaimu Kamanda ya Polisi mkoani Siminyu Venance Kimario amedhibitisha kutokea kwa tukio hilo baada ya polisi kufahamishwa na raia mwema katika kijiji cha Bushigwamala kilichopo Kivukoni wilayani Busega. 

Waliokamatwa ni baba mzani Makoye Gamoge (42), mama mzani Neema Kugela (31), mtoto wao wa kiume Juma Makoye (15) na mtoto wao wa kike Esther Makoye (12). Watoto hao wanasoma katika shule ya msingi ya Bushigwamala. Wote wanne hawakukimbia baada ya kuwaona polisi kwenye mida ya saa kumi na mbili za asubuhi. Waliendelea kulima huku wakiimba bila kuogopa uwepo wa polisi shambani hapo mpaka pale polisi walipowaamuru waweke majembe yao chini.

Kwa mujibu wa RPC baba mzani Gamoge amedai kuwa kitendo cha mtu kulima wakati akiwa uchi ni sehemu ya tamaduni za Wanyantuzu ambao ni sehemu ya kabila la Wasukuma na madhumuni yake ni kuleta mvua za kutosha na hivyo mavuno mazuri. Amesema kuwa walikuwa wanalima uchi kutoa heshima kwa nasaba zao. Gamoge aliongeza kwa kuwambia polisi kuwa familia yake ilishauriwa na mganga wa kienyeji aliyewahakikishia "mapinduzi ya kijani" kama kama wangefuata ushauri wa kulima mapema asubuhi huku wakiwa uchi

Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Othman Masoud Afukuzwa Kazi, Said Hassan Said Apewa Nafasi hiyo

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, amefanya Uteuzi wa Mwanasheria Mkuu wa Serekali ya Mapinduzi Zanzibar, kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya Kifungu 55(1)cha Katiba ya Zanzibar ya 1984.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi amemteuwa Mhe, Said Hassan Said kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Uteuzi huo umeaza leo 7,Oktoba 2014. Kabla ya uteuzi huo Mhe, Said Hassan Said alikuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serekali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Mhe, Said Hassan Said, anachukua nafasi ya aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Mhe, Othman Masoud Othman ambaye uteuzi wake umefutwa kwa mujibu wa Vifungu vya 53,54 (1) na 55(3) vya Katiba ya Zanzibar ya 1984 na kifungu 12 (3) cha Sheria ya Utumishi wa Umma Namba 2 ya 2011.

My Take:
Hii ni Kama: Nakufukuza kazi kwa sababu umetumia demokrasia yako vibaya kwa kupiga kura ambayo siitaki!

Wanawake Wenzangu Njooni Tuwatete Huku Hawa Viumbe, Funguka Kuhusu Maudhi ya Mume

$
0
0
Wanawake ni jeshi kubwa.
Hii mada itakuwa msaada mkubwa sana kwa wale wanaojiandaa kuingia katika ndoa, itasaidia kuwaanda kisaikolojia kupambana na maudhi ya mume maana kwa kweli ni mengi sana na usipoangalia yanaweza angamiza ndoa yako.

Karibuni tuyabainishe haya maudhi.

Mimi naanza.
kutoa maagizo kama anaongea na mtoto mdogo.
kurudi usiku huku yamelewa
hakutomasi tomasi kama mwanzo

Matusi ya Mama Wema..Kajala na Wema Sepetu Watoana Jasho Polisi

$
0
0
Kufuatia matusi ya mama wa staa wa sinema za Kibongo, Wema Isaac Sepetu, Miriam Sepetu kwenda kwa mwigizaji Kajala Masanja ‘Kay’, mastaa hao wamejikuta wakitoana jasho kwenye Kituo cha Polisi cha Kijitonyama almaarufu Mabatini jijini Dar mwishoni mwa wiki iliyopita.

DURU ZA ‘KIUBUYU’
Duru za ‘kiubuyu’ zilidai kwamba Kajala, baada ya kuchoshwa na matusi hayo ambayo yalianzia kwenye sherehe ya kuzaliwa kwa Wema, alijikuta akiishiwa na uzalendo kisha kuingia mzigoni ili kukomesha matusi hayo kwenye mitandao ya kijamii.

MATRIDA MBARONI
Ilidaiwa kwamba, Kajala akiwa na timu yake (Team Kajala) alifanikiwa kumtia mbaroni dada mmoja aliyetajwa kwa jina la Matrida akidaiwa kwamba ni mfuasi wa Wema (Team Wema).
Ilisemekana kwamba Matrida anayetumia jina la ‘Mat Kiboko Yao’ kwenye ukurasa wake wa Instagram ndiye ambaye amekuwa akiongoza jahazi la kumtusi Kay.

Ilizidi kunyunyizwa kwamba sakata hilo la kuanikwa Instagram lilianza siku mbili baada ya ile pati ya kuzaliwa ya Wema ambapo Mat Kiboko Yao alimtukana Kajala matusi ya nguoni (hayaandikiki gazetini) kupitia ukurasa wake kwenye mtandao huo.

KAJALA ACHOKA, AKIMBILIA POLISI
Ilidaiwa kwamba Kajala alipoona amechoka kutukanwa, alitafuta wataalam ili kujua namna ya kumkamata na alipomjua ndipo akakimbilia Kituo cha Polisi cha Mabatini kwenda kutoa taarifa.
RB
Gazeti hili lilifanikiwa kunasa namba ya jalada la kesi hiyo iliyosomeka KJN/RB/8854/2014-MATUMIZI YA MATUSI MTANDAONI.

Ilisemekana polisi walitumia mbinu zao na kufanikiwa kumkamata Mat Kiboko Yao na kumweka nyuma ya nondo za mahabusu kituoni hapo ndipo sarakasi za pande mbili zikaanza.

KWANZA
Mara tu baada ya Mat Kiboko Yao kukamatwa mishale ya saa 2:00 usiku, taarifa zilisambaa kama moto wa kifuu ndipo Team Wema ikaingia mzigoni kutaka kumtoa mwanadada huyo lakini wakagonga mwamba.

WEMA, PETIT MAN WATINGA MABATINI 
Ilidaiwa kwamba, baada ya Mat Kiboko Yao kutiwa mbaroni, Wema na jeshi lake akiwemo Petit Man walitinga Mabatini kwa ajili ya kumtoa mwanadada huyo lakini aligonga mwamba na kumuacha akilala kituoni hapo.

“Yaani ulikuwa ni usiku wa kutoana jasho na kupimana ubavu kwamba nani ni nani. Ilikuwa akitoka Kajala kuhakikisha kwamba mtuhumiwa wake aachiwi, Wema naye anatinga kituoni kwa mbwembwe kutaka Mat Kiboko Yao aachiwe kwa gharama yoyote.

“Hapo ndiyo ngoma ilikuwa nzito, kila mmoja alikuwa anamuonyesha mwenzake kuwa ni zaidi na ni maji marefu hadi kulipokucha muvi likaendelea,” alisema shuhuda aliyefuatilia sakata hilo kinagaubaga.

WAANDISHI WAPEWA UBUYU, WATINGA MABATINI   
Kulipokucha, waandishi wetu walipewa ubuyu huo ndipo wakatinga Mabatini kisha wakatega ‘rada’ zao na kuweka doria.

Wanahabari wetu, wakiwa kituoni hapo walimshuhudia Kajala akilinda kituoni hapo asitokee mtu yeyote akamtoa Mat Kiboko Yao.
Hata hivyo, alipoulizwa Kay kulikoni kuwa eneo hilo alisema alikuwa ameitwa kwa ajili ya kusuluhishwa badala ya kupoteza muda kwa jambo kama hilo.

KAJALA NA KUNDI LAKE
Awali Kay alionekana akiingia kituoni hapo na kundi lake la watu watatu akiwemo mwanaume mmoja ambapo yeye aliingia mpaka kwenye chumba cha mkuu wa kituo.

Kajala akiwa kwa mkuu wa kituo, haikujulikana kilichokuwa kikiendelea ndani kwani kulikuwa na kikao cha muda mrefu ambapo ghafla Kajala na mtuhumiwa wake waliyeyuka.

WEMA AINGIA MITINI
Wakati hayo yakiendelea kituoni hapo, si Wema wala jeshi lake waliofika kwa ajili ya kumtetea Mat Kiboko Yao ambaye ndiye kiongozi wa Timu Wema kwa kutukana.

Hata hivyo, baadaye alionekana mmoja wa marafiki wa karibu ambaye ni ndugu wa Mat Kiboko Yao aliyekuwa akihaha kumtoa mwenzake.

TUJIKUMBUSHE
Hivi karibuni Mama Wema alimtolea uvivu Kajala na kumtusi ndipo akafufua upya kile kidonda cha Sh. milioni 13 ambazo Wema alimlipia Kay asiende jela na kinachoonekana, bado fedha hizo ni tatizo kubwa.

Imeandaliwa na Hamida Hassan, Imelda Mtema, Mayasa Mariwata na  Shani Ramadhani.

Hali Bado Si Shwari Bongo Movies, Mastaa Wengine Watano Wajiondoa

$
0
0
Stori: Hamida Hassan na Imelda Mtema
HALI bado tete! Siku chache baada ya Mwenyekiti wa Klabu ya Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ kujiuzulu, upepo mbaya unaendelea kuitafuna klabu hiyo ambapo sasa wasanii wengine watano wamejiengua, Risasi Mchanganyiko linakupa mchapo kamili.

Kutokana na wasanii hao kujitoa, klabu hiyo inaonekana kupoteza muelekeo ambapo kwa sasa wanachama waliobaki kundini wanajipanga upya ili kuisimamisha upya.
Kwa mujibu wa chanzo makini, wasanii waliojiengua ni Halima Yahya ‘Davina’, Esha Buheti, Kajala Masanja, Flora Mvungi na  Salma Salmini ‘Sandra’ huku sababu kubwa ikitajwa kuwa ni kukithiri kwa vitendo vya ngono na ubaguzi wa kimaslahi.

Chanzo hicho kilizidi kumwaga ubuyu kwamba, hivi karibuni kulitokea safari ya wasanii kwenda mkoani Tanga lakini baadhi ya viongozi wamedaiwa kujichagua kwa ‘kapo’ bila kujali kuwa wapo wanachama wengine ambao wanatakiwa kwenda huko.

Kikifafanua madai hayo, chanzo hicho kilikwenda mbele zaidi na kuzinadi kapo hizo kama ifuatavyo:
Cloud 112 (Issa Musa) alidaiwa kuongozana na Coletha Raymond, JB (Jacob Steven) na Shamsa Ford, Rose Ndauka na Single Mtambalike (Rich) na wengine.

Baada ya madai hayo kutua kwa mapaparazi wetu, walianza kwa kuwatafuta walengwa ambao wamedaiwa kubaguliwa na kuamua kujitoa klabuni hapo. Mambo yalikuwa hivi:

Davina: 
“Mimi nimeamua kujitoa kwa sababu naona mambo mazuri wanachaguana mapatna tu sisi tunakumbukwa pasipo mazuri, kwenye pesa wanapeana wao wenyewe, mimi mpaka mume wangu alikuwa akiniuliza kwamba napata faida gani.”

Sandra: 
“Sijapata faida yoyote Bongo Movie, watu wanapeana mapatna inapotokea suala la safari na pesa.”

Esha Buheti:
“Mimi nimeamua kujitoa kwani watu wamekuwa na ubaguzi, sisi tunaitwa unapotokea msiba tu, nitafanya kazi zangu mdogomdogo, nitatoka tu.”

Kajala:
“Nimejitoa kwa sababu kule nilikuwa nikimfuata Steve Nyerere, sasa ameshatoka nafuata nini tena?”    
Jitihada za kuwapata wasanii wanaotajwa kuwa ni wabaguzi ziligonga mwamba kwa baadhi ya wasanii lakini alipopatikana Cloud 112, alikanusha taarifa hizo.

“Hakuna kitu kama hicho, sisi tunasafiri kulingana na matakwa ya waandaaji wa safari, waandaaji ndiyo wanaosema wanamtaka nani katika shughuli yao, wanaosema hivyo wamekosa la kuongea,” alisema Cloud 112.

Mwigizaji Cloud Akana Tuhuma Kumfitinisha Frank ili Asisafiri Kwenda Uingereza Kucheza Filamu

$
0
0
Stori: Mayasa Mariwata na Chande Abdallah
MSANII mkongwe wa filamu Bongo Issa Musa ‘Cloud’ amekana tuhuma zinazosambazwa mtandaoni kuwa alimfitini muigizaji mwenzake, Mohammed Mwikongi ‘Frank’ ili kumzuia asisafiri kuelekea Uingereza miezi michache iliyopita

“Mimi sikumfitini Frank, yule mtu alinifuata mwenyewe kwa makubaliano ya mdomo kuwa nikacheze filamu, sikuwa peke yangu, tuliongozana na kina Monalisa na Riyama, tatizo ni la huyo aliyenipeleka kule, nilifanya mambo kwa mazoea na ndiyo sababu anaamua kusambaza uongo dhidi yangu,” alisema mkongwe huyo wakati akizungumza na Global Tv.

Aliwasihi wasanii wenzake nchini kuacha kufanya kazi kwa mazoea bali wahakikishe wanaingia mikataba ya maandishi ili wawe na ushahidi wakati waliokubaliana nao kazi wanapoleta ujanjaujanja kama ilivyomtokea yeye katika safari hiyo ya Uingereza ambayo sasa inamletea uadui na Frank.

Ona Hawa Askari Wawili Wanavyo lizalilisha Jeshi la Polisi..Kama si Maigizo Haya Basi Hawafai Kabisa Hawa

$
0
0
Hivi hii picha wanafanya kweli au wako maigizo???? Yaan dah! Ukute hapo Wakisikia gari inakuja wanakurupuka kuwahi barabarani kuomba rushwa na mikwara kibao. Wakubwa tunaomba majina yao...

Tetesi za Edzen Kuwa Ndani ya Penzi Jipya Baada ya Kutemana na Mkewe Dida

$
0
0
"Couple" mpya mjini? Mtangazaji maarufu nchini @ezdee255 hivi karibuni ameonekana "benet" na msanii wa filamu na mfanya biashara @mozzah255 Katika mapozi yenye utata. Mtangazaji huyo hivi karibuni aliachana na aliyekuwa mkewe @didashaibu ambaye pia ni mtangazaji wa redio maarufu nchini kwa talaka "chungu" yenye kutawaliwa vyombo vya habari mpaka ikapelekea "Ezdee" kuongelea kwa undani masuala ya ndani ya mkewe na kumshutumu kwenye TV. Hata hivyo mashabiki wengi kwa pande zote hawakupendezwa na shutuma hizo za masuala ya ndoa kuanikwa hadharani namna ile. Mbali na kupiga picha na anayesemekana mpenzi wake mpya wa sasa, "Ezdee" amekana mara nyingi kwamba hawana mahusiano ya kimapenzi. Hata hivyo wengi wamewapongeza kuonesha kuwakubali japokuwa wachache bado wanaona ni mapema sana kujionesha kimapenzi wakati ameacha na mkewe karibuni. Haya sasa....sisi tunauliza, je hawa ni wapenzi au siyo wapenzi?

Mwanamke Mcharuko Awapa Watu Senema ya Bure, Kisa Mzuka wa Mziki

$
0
0
Kadri mapigo ya Vijana wa Masauti yalivyozidi kuchanganya, ndivyo midadi ya ‘mtu mzima’ ilivyozidi kupanda na kuanza kukata kiuno isivyo kawaida huku akichojoa kiwalo kimoja baada ya kingine.

Mzuka ulipokolea barabara, mama alijikuta akivua miwani yake ‘tintedi’ kwani ilikuwa ikimnyima raha kwa kutoona vizuri kwenye giza.

Baada ya miwani vilifuatia viatu, blauzi na kubakiza sidiria, huku chini akishusha ‘skini jinsi’ yake na kusababisha bikini na viungo nyeti kuwa nje nje mbele ya mwanaye aliyekuwa akiangalia pembeni kwa aibu kuu.

Mizuka ya mama huyo ilishindwa kutulizwa mpaka wasamaria walipoamrisha Vijana wa Masauti kuzima muziki ndipo mzazi huyo akatulia na kwenda kukaa huku watu wakimponda kwa kitendo chake cha kumwaga radhi mbele ya mwanaye. Baadaye alitimkia kusikojulikana huku mtoto akielekeza njia tofauti na walipoingia kwani mama ndiye aliyekuwa ‘dairekta’.

Siri wa Wabunge Kufurahi na Kucheza Bungeni Yajulikana

$
0
0
Baada ya "Rasimu ya Sitta" kupitishwa na Bunge maalumu baadhi ya wabunge walilipuka kwa furaha na wengine wakakata mauno hadharani, huku mbunge wa Njombe kaskazini Deo Sanga akicheza "Kitorondo" na kukata mauno mbele ya halaiki.

Pia kuna wabunge wengine walikua wakicheza kwa kufuatisha milio ya miziki iliyokua ikirindima kupitia simu
zao za mkononi. Watu wengi walihamaki kitendo cha wabunge kufurahia Rasimu hiyo hadi kufikia hatua ya kujitoa akili.

Hii hapa siri ya furaha ya Wabunge hao..
RASIMU YA WARIOBA ILIPENDEKEZA:

1. Mbunge akigombea vipindi vitatu basi, awaachie wengine.

2. Mbunge akivurunda ktk utendaji wake, wananchi wana
uwezo wa kumuondoa na kuchangua mwingine.

3. Hakuna mbunge kuwa Waziri, Mkuu wa mkoa, m/kiti wa bodi ya shirika etc. (kwanini vyeo vyote mjilundikie nyie?).

4. Elimu ya mbunge iwe angalau stashahada (diploma) na kuendelea.

RASIMU YA SITTA (ILIYOPITISHWA) IMEPENDEKEZA HIVI:

1. Ukomo wa Ubunge usiwe vipindi vitatu.. Hata wazee waliokaa bungeni miaka 50 kama Kingunge, waendelee tu kugombea. Vijana wanaotaka kuwa viongozi labda wakajaribu kwny SACCOSS sio UBUNGE.

2. Mbunge akivurunda wananchi hawawezi kumfanya kitu chochote hadi miaka mitano iishe na mbunge apewe pensheni yake (Mil.160).

3. Ruksa Mbunge kuwa waziri, Mkuu wa mkoa, DC, Mwenyekiti wa shirika, na vyeo vingine kadri anavyoweza
kujilundikia. Wanaosema mbunge asiwe na vyeo viwili au zaidi, wana "wivu wa kike" (according to Pius Msekwa).

4. Rasimu ya Sitta inasema si lazima mbunge awe na degree, diploma, au cheti. Si lazima mbunge awe na elimu ya sekondari. Si lazima
Mbunge awe amemaliza elimu ya msingi. Hata kama alisoma akaishia darasa la 3 lakini anajua kusoma na
kuandika RUKSA KUGOMBEA UBUNGE.

Sasa je katika mazingira haya wabunge wataacha kukata mauno na kucheza "kitorondo" kwa Rasimu hii kupita?

5. Ongezea kama kuna mengine

JIPU LIMEPASUKA, SIWEZI KUWA ADUI KWA KUSEMA
UKWELI...

Mbunge wa Kawe Halima Mdee Hastahili 'Kutendwa' Vile

$
0
0
Hata kama ni mambo ya kisiasa,twende taratibu. Jana, Mbunge wa Kawe (CHADEMA) na Mwenyekiti wa BAWACHA Halima Mdee alikosa dhamana na kuswekwa rumande. Ikatolewa sababu kuwa alishindwa kutimiza masharti ya dhamana. Sasa, hebu twende hatua kwa hatua. 

Kwanza Halima Mdee alikamatwa. Pili Halima Mdee akaachiwa kwa dhamana ya Polisi. Tatu Halima Mdee alifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kusomewa mashtaka yake. Nne, upande wa Mashtaka haukuwa na pingamizi juu ya dhamana ya Halima Mdee wala wenzake. Tano,Hakimu akatoa masharti ya dhamana. Sita, washtakiwa wote walikuwa tayari kuyatekeleza na kuachiwa kwa dhamana. Saba, upande wa Mashtaka ukataka kwenda kuhakiki wadhamini wa Halima Mdee na wenzake.

Umepagundua penye tatizo? Ni hapo pa kuhakiki wadhamini. Halima Mdee anajulikana. Wadhamini wake, ambao wengi ni Wabunge na Maafisa wa CHADEMA Makao Makuu wanajulikana. Kuhakiki kulikujaje? Wengine mbona hawafanyiwi hivyo? Kibaya zaidi,wahakiki hawakuenda mahali popote hadi Halima Mdee alipopandishwa karandinga na kwenda mahabusu. Wahakiki walitokomea kusikojulikana. Why?........Kwanini?

Nitoe rai kwa wahusika wote kufanikishadhamana ya Halima Mdee. Ingawa si wachama changu, hastahili kombolela lililochezwa jana. Hakuna haja ya 'kuipaisha' CHADEMA na viongozi wake kupitia Mahakama. We are suffering from that;it must end! Pole sana Halima Mdee.

Walio Kuwemo Kwenye Basi Hili Hawaita Isahau Siku Hiyo...Mambo ya Mlima Kitonga

$
0
0
Walio Kuwemo Kwenye Basi Hili Hawaita Isahau Siku Hiyo...Mambo ya Mlima Kitonga Hayo

One Word To these Student Who Shows off their Goodies Like This?

$
0
0
One Word To these Student Who Shows off their Goodies Like This? Ni wanafunzi wa Shule Moja Maarufu Bongo..Mmoja wapo alipost kwenye Instagram Profile

Baba Mzazi Adaiwa Kumchinja Mwanaye

$
0
0
Baba mzazi mkazi wa Sengerema anadaiwa kumuua mwanaye wa miaka minne kwa kumchinja koromeo na kumchoma kwa kisu kwenye kitovu na utumbo kutoka nje.

Mzazi huyo anadaiwa kufanya mauaji hayo juzi alfajiri baada ya kumchinja aliuchoma kwa kisu mwili wa mtoto huyo sehemu mbalimbali ikiwemo masikioni na kifuani.

Gazeti la MWANANCHI ambalo lilikua shuhuda limedai baada ya kufanya kitendo hicho alianza kufukuza wananchi waliokusanyika eneo hilo kwa kuwatishia kuwachoma na kisu.

Hata hivyo mtuhumiwa huyo alizidiwa nguvu na wananchi na kuanza kumshambuliwa kwa kipigo hadi alipookolewa na Mwenyekiti wa mtaa.

Mama mzazi wa watoto hao alisema kabla ya kutengana na mumewe huyo alizaa nae watoto watatu na kwamba ameshangazwa kupata taarifa za mwanaye kuuawa na baba yake.

Jeshi la Polisi linamshikilia kwa uchunguzi huku likisubiri taarifa ya hospitali kuhusu utimamu wa akili yake.

Breaking: Taarifa Mpya ya Kusikitisha Kuhusu Yule Mgonjwa wa Ebola Marekani

$
0
0
Thomas Eric Duncan mwanaume aliesafiri kutoka Liberia mpaka Marekani akiwa ameambukizwa virusi vya ugonjwa wa Ebola amefariki muda mfupi uliopita nchini Marekani baada ya kuwa kwenye hali mbaya.
Pamoja na hayo pia mamlaka husika zinaendelea na jitihada za kuhakikisha ugonjwa huo hausambai nchini humo na wanafahamu kabisa kwamba virusi vya Ebola vinaweza kuishi kwenye miili ya watu waliofariki ndio maana wakati wa kuizika ni watu pekee wenye mafunzo maalum tena wakiwa wamejikinga ndio wanaruhusiwa

Mwanamuzi Lady Gaga Sasa Amepitiliza, Atembea Uchi Mitaani, Watu Wapate Sinema ya Bure

$
0
0

Sio Bongo Tu Wasanii Wanatafuta Kiki Kwa nguvu Mbali Hata Huko Marekani Wasanii Wanatafuta kiki Kila siku ili Majina yao yabakie midomoni mwa Watu , Mwanamuziki Mkubwa Lady Gaga Ambae amezoeleka kwa kuwa na vituko vingi awapo jukwaani  sasa amehamishia vituko mtaani baada ya kunaswa akitembea akiwa amevaa T-shirt tu bila nguo chini kitu kilichofanya watu kumshangaa kila anapopita....

Halima Mdee 'Kama Serikali Walidhani Wamenikomoa Kunilaza Segerea ni Sawa na Bure, Kwasababu Nimekula ‘bata’, Ambao Sijawahi Kula'

$
0
0
Wakati Mbunge wa Kawe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo-Chadema (Bawacha), Halima Mdee, akiachiwa huru baada ya kulala mahabusu ya Segerea kwa siku moja, amesema kuwa alikula bata ambalo hajawahi kula maishani mwake akiwa mahabusu hiyo.

Mdee na wenzake wanane, waliachiwa huru na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,jijini Dar es Salaam jana baada ya kutimiza masharti ya dhamana katika kesi ya kupinga amri halali ya Jeshi la Polisi na kukusanyika isivyo halali kwa lengo la kwenda Ikulu.

Mbali na Mdee, wengine walioachiwa huru ni Rose Moshi, Renina Leafyagila, Anna Linjewile, Mwanne Kassim,  Sophia Fanuel,  Edward Julius, Martha Mtiko na Beatus Mmari.
Baada ya kuachiwa kwa dhamana Mdee alisikika akisema ‘people’s na wanachama hao walisikika wakiitikia ‘power’ hali iliyosababisha vurugu kubwa na kuwalazimu askari polisi wenye sare na askari kanzu kuanza kuwatawanya kutoka kwenye viunga vya mahakama.

Hata hivyo, Mdee alisimama ndani ya gari yenye namba za usajili T152 BSR aina ya Toyota V8 ya rangi nyeusi na kuwaambia waandishi wa habari kwamba, alilala mahabusu ya Segerea kimakosa.

“Kama serikali walidhani wamenikomoa kunilaza Segerea ni sawa na bure, kwa sababu nimekula ‘bata’, ambao sijawahi kula huko mahabusu…kama tulikuwa tunachechemea, sasa tunakimbia Chadema,” alisema Mdee nje ya mahakama baada ya kupata dhamana.

Mdee alitoa kauli hiyo huku viunga vya mahakama hiyo vikiwa vimefurika watu wanaodaiwa kuwa wafuasi Chadema, wakati huo huo ulinzi mkali wa askari polisi waliokuwa na silaha za moto, mbwa na gari lenye maji ya kuwasha ukiimarishwa.

Mdee na washtakiwa wenzake walipandishwa kizimbani mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Janeth Kaluyenda, kwa ajili ya kusikiliza masharti ya dhamana dhidi ya kesi inayowakabili, majira ya saa 6:17 mchana.

Mapema Oktoba 7, mwaka huu, Mdee na washtakiwa wenzake, walishindwa kutimiza masharti ya dhamana, baada ya nyaraka za wadhamini kushindwa kukamilika kufanyiwa uhakiki.
Upande wa Jamhuri jana uliongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Bernad Kongola, akisaidiana na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Salum Mohamed, na Wakili wa Serikali, Hellen Moshi.

Kongola alidai kuwa Oktoba 4, mwaka huu, katika Mtaa wa Ufipa, uliopo Kinondoni, jijini Dar es Salaam, isivyo halali, washtakiwa walikiuka amri halali ya Mrakibu wa Polisi (SP), Emmanuel Tillf, iliyowataka kutawanyika.

Ilidaiwa kuwa siku na mahali pa tukio la kwanza, washtakiwa walifanya mkusanyiko isivyo halali kwa lengo la kuandamana kwenda Ofisi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Washtakiwa wote walikana mashitaka hayo.

Upande wa Jamhuri ulidai upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na kuiomba mahakama tarehe ya kusikiliza maelezo ya awali.

Hakimu Kaluyenda alisema washtakiwa watakuwa nje kwa dhamana wakijidhamini kwa kusaini hati ya dhamana ya Sh. milioni moja, kuwa na wadhamini wawili wanaofanya kazi katika taasisi zinazotambulika.

Hakimu Kaluyenda alisema kesi hiyo itatajwa Oktoba 21, mwaka huu.

Viunga vya mahakama jana vilifurika na wanaodaiwa kuwa wafuasi Chadema, huku ulinzi mkali wa askari polisi waliokuwa na silaha za moto, mbwa na gari lenye maji ya kuwasha ukiimarishwa.
CHANZO: NIPASHE
Viewing all 104745 articles
Browse latest View live




Latest Images