Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

KUCHAPIWA...Nawaonea Huruma Wanaume Ambayo Hawaendi GYM na Wanawaruhusu Wake zao Kwenda Gym

$
0
0

Kuna gym hua naenda kufanya mazoezi hapo posta, yaani sipendi kuwaficha, huku gym wanawake hawa wanaliwa sana, mwanamme kama unafuga kitambi chako usiruhusu mke wako aje gym huku

Yaani kwa haraka haraka naona kama hawa wanawake wote members hapa wana vijana wa kuwaweka sawa(Nina marafiki wengi sana hapa so they tell me stuffs)

Ikifika mahali mwanamke ana mentality ya kua fit atatafuta a fit partner pia....

Ushauri wangu kwa wanaume ukiona mke au mpenzi wako anafanya mazoezi na diet ili awe vizuri afu wewe umekalia kufuga kitambi lazima utachapiwa tu hakuna namna yaani

Ni tahadhari tu maana I have seen enough

Kama Upo Kwenye Mahusiano Miaka 2 na Msichana na Hujaona Chozi lake, Huyo Hana Mapenzi ya Kweli

$
0
0

Leo nimeona nilete hili jambo, katika ujana wangu nimebahatika na kuwa na mahusiano ya kimapenzi na zaidi ya msichana mmoja ila kitu nilicho gundua hata wewe jalibu kufanya utafiti

kama upo kwenye mapenzi na mwanamke zaidi ya miaka miwili na hujabahatika walau siku moja
kuona machozi yake basi tambua huyo mwanamke hana mapenzi ya dhati kwako chamsingi
nikuchukua tahadhari mapema OVA.

Ukiamua Kuwa na Mahusiano na Mume wa Mtu Lazima Ukubali Kuwa Mtumwa wa Mambo Yafuatayo

$
0
0

Ukiamua Kuwa na Mahusiano na Mume wa Mtu Lazima Ukubali Kuwa Mtumwa wa Mambo Yafuatayo:

1. Baby samahani dakika moja,wife anapiga simu

2. Baby muda umeenda Sana mke wangu atanipigia, wacha niwahi kurudi nyumbani, Kesho saa 12 nitakuwa hapa

3. Bby nataka kuja kulala kwako mke Wangu amefiwa kaenda kwao

4. Baby sintaweza kuja Leo, wife kanibana... Pole kwa kuugua

5. Baby tangulia mbele, nitakukuta... Pale wanakaa shemeji zangu, wakituona pamoja watamuambia wife

6. Unaweza kimbiwa katikati ya sherehe usipewe hata nauli ya bodaboda, kesho unaambiwa sorry darling, si uliona wife alitokea ghafa

7. Mkiwa mnaongea kwa simu kwa mahaba mara unashtukia unaitwa Hamadi na kuagwa fasta.,baadae unaambiwa mke wangu alitokea ghafla nikawa sina jinsi

8. Unaweza pitwa barabarani na mvua inanyesha,kesho ukaambiwa nilikuona my love, Ila ningefanya nini.. ,nilikua na mke wangu

Ili mwisho wa siku ukija kupewa mimba na kuterekezwa usije na kauli zako za kusema wanaume wote ni mbwa😂😂na kama utafikia hatua ya kuwaita wanaume wote hivyo basi anza na kumtaja baba yako ili twende sawa maana sometimes huwa mnakuwaga na ukulunjuma mwingi sana dadeq

Mwanamitindo Mashuhuri wa Marekani Ajitangaza Ana Ukimwi

$
0
0

MAREKANI : Mwanamitindo Mashuhuri wa Marekani, Farren Jean Andrea anayejulikana zaidi kama Fucci ametangaza kuwa ni muathirika wa Virusi vya Ukimwi 'VVU.'
_
Fucci aliyepata umaarufu kwa kufanya kazi na Mwimbaji Rihanna, Bella Hadid, Jhene Aiko na miongoni mwa wengine wengi alitangaza uathirika wake kupitia ukurasa wake wa Twitter, Jumatano ya tarehe 25 Julai.

Mwanamitindo huyo mwenye umri wa miaka 25 aliweka ujumbe wenye taarifa hiyo ambapo alibainisha ilivyo kuwa ngumu kwake kuweka wazi hali hiyo ya VVU na kuomba watu wamuombee.

Mapokezi ya ndege mpya ya Boeing 787-800 Dreamliner Jijini Mwanza

$
0
0

Judith Ferdinand, BMG

Wakazi wa Jiji la Mwanza na maeneo jirani wametakiwa kujitokeza kwa wingi kushuhudia mapokezi (safari ya kwanza) ya ndege mpya  na ya kisasa aina yaBoeing 787-800 Dreamlineriliyonunuliwa na serikali ili kuimarisha shirika la ndege nchini ATCL.


Mkuu wa Mkoa Mwanza Mhe.John Mongella alitoa rai hiyo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari, na kubainisha kwamba ndege hiyo itatua katika uwanja wa ndege wa Mwanza jumapili Julai 29, 2018 majira ya saa moja asubuhi.


Mongella alisema tayari tiketi 244zimenunuliwa kwa ajili ya safari ya asubuhi na tiketi 158 kwa safari ya usiku hivyo wananchi pia wachangamkie fursa ya kusafiri na ndege hiyo kwa bei nafuu ambapo ina uwezo wa kubeba abiria 262 daraja la kawaida na abiria 22 daraja la biashara.


Kwa upande wake Msimamizi wa kampuni ya ATCL kituo cha Mwanza, Theonestina Ndyetabula  alisema shirika hilo limejipanga vyema na linazidi kuimarika na hivyo kuwahimiza wananchi kutumia ndege zake ikiwemo zile za Bombadier  Dash 8-Q400.


Ndyetabula alisema ndege za Boeing 787-800 Dreamliner pamoja na Bombadier  Dash 8-Q400 zinafanya safari zake mara nne kwa siku katika uwanja wa ndege wa Mwanza ambapo ndege ya  Dreamliner ya Mwanza – Dar kupitia Kilimanjaro ni saa 09:20 asubuhi hadi 11:40 asubuhi, Mwanza -Dar saa 20:20 hadi  21:40 usiku huku Bombadier Mwanza – Bukoba saa 11:15 asubuhi hadi 11:45 asubuhi na   Mwanza – Dar saa 13:15 mchana hadi 15:00 alasiri.

Serikali Yataja Sababu za Kumzuia Diamond Kwenye Nje ya Nchi Kufanya Shoo

$
0
0

Baraza la Sanaa nchini (Basata) limefafanua umuhimu wa kibali ambacho msanii Diamond alipaswa kuwa nacho kabla ya kwenda kufanya shoo nje ya nchi.


Haya yameelezwa jana Julai 27 baada ya  Diamond kuzuiwa kwa saa tisa katika uwanja wa ndege wa Julius Nyerere kutokana na kutokuwa  na kibali hicho alipokuwa akielekea visiwa vya Madagascar na Mayote.


Kaimu Katibu Mkuu wa Basata, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Fedha na Utawala, Onesmo Kayanda, amesema kibali hicho kinawasaidia kutunza kumbukumbu ya wasanii wanaokwenda nje ya nchi.


Jingine ni endapo atapatwa na tatizo lolote iwe rahisi kumsaidia na kuongeza kuwa kuna baadhi yao walishakumbwa na matatizo wakiwa nje ya nchi huku serikali ikiwa haina taarifa kama walisafiri.


Kibali hicho ambacho gharama yake ni Sh50,000, Kayanda amesema huchukua siyo zaidi ya dakika 20 kukipata isipokuwa tu  wasanii huzembea.


“Kuanzia sasa hivi tutakuwa wakali katika hilo bila kujali ukubwa wa jina la msanii, kwani ni kitu ambacho kipo kwenye sheria na ni kwa faida ya wasanii wenyewe na Diamond siyo wa kwanza kuzuiwa, wapo wengine labda kwa kuwa hawana umaarufu kama aliokuwa nao Diamond ndiyo maana haikuzungumzwa sana,” amesema.


Hata hivyo  kibali hicho baadaye kitaisaidia serikali kujua sekta ya sanaa inachangia pato la taifa kwa kiasi gani kwa wasanii kupata shoo za nje kwani katika hatua hiyo pia watapaswa kuweka na mikataba yao mezani ya mialiko kujua serikali nayo imepata nini katika suala zima la kodi.

Mabasi Mwendokasi Kufanyiwa Mabadiliko ya Ratiba zake

$
0
0

Kampuni  inayotoa huduma kwenye mfumo wa mabasi yaendayo haraka Dar es Salaam (UDART), imesema kuanzia Julai 30 mabasi yanayoanza na kumaliza safari zake katika kituo cha Ubungo Maji yataishia Ubungo Terminal.


Akizungumza na waandishi wa habari   Dar es Salaam jana, Mkuu wa Idara ya Mawasiliano, Deus Bugaywa, alisema mabadiliko hayo ni kutokana na shughuli za ujenzi wa daraja la juu kwenye makutano ya barabara za Morogoro, Nelson Mandela na Sam Nujoma.


Alisema  wamelazimika kubadili ratiba ya mabasi hayo yaliyokuwa yakianzia na kumalizia safari zake katika kituo cha Ubungo Maji, huku yakitumia njia moja na nyingine kutumika na magari mengine.


Alisema wakati wa asubuhi mabasi yanayotoa huduma ya ‘Express’  njia  namba 002 kutoka Ubungo hadi Kivukoni na njia namba 005 kutoka Ubungo mpaka Gerezani yatalazimika kuanzia safari zake kituo cha Ubungo Terminal badala ya Ubungo Maji.


“Nyakati za mchana na jioni mabasi ya njia hizo yataendelea na huduma za kawaida zisizokuwa express na hatua hii itadumu kwa miezi  miwili hivyo tunawaomba radhi wateja wetu kwa usumbufu utakaojitokeza.


“Wakati wa shuguli za ujenzi wa barabara hizo mabasi ya mwendo wa haraka yatakuwa yakitumia njia moja tu, ndiyo maana mabasi yetu yataishia Ubungo Terminal  kupunguza msongamano wa mabasi kituoni wakati wa kushusha abiria,” alisema Bugaywa.


Alisema  kutokana na mabadiliko hayo,  aliwashauri abiria waliokuwa wakitumia kituo cha Ubungo Maji hasa nyakati za asubuhi kutumia zaidi kituo cha Ubungo Terminal au Kibo kuondoa usumbufu.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya July 28

$
0
0

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya July 28

Pata Super Mkuyati Mpya Orjinal Inayo Imarisha Heshima ya Ndoa

$
0
0
SUPER MKUYATI MPYA ORJINAL INAYO IMARISHA HESHIMA YA NDOA

SUPER MKUYATI NI DAWA ILIYO KATIKA MFUMO WAJIDONGE NA UNGA IMETENGENEZWA KWA TEKNOLOJIA YA KISASA ILIYOFANYIWA UTAFITI WA KINA NA KUNDULIKA INAPAMBANA NA MAGONJWA SUGU YA KINA BABA DAWA HII INA GUVU (3)NA INAFANYA KAZI KWA PAMOJA (1) INAONGEZA NGUVU ZA KIUME 2 KWA UCHELEWE KUFIKA KILELEI KWA KWA WA DK 10-20 (3) INAZALISHA HOMONI KWA WINGI NA KUKUFANYA UWE NA MBEGU NYINGI ZENYE VIMELEO NYA UZAZI VILIVOKOMAA

MDINGO MIX NI DAWA INAYO LEFUSHA NA KUNENEPESHA MAUMBILE MADOGO YALIYOSINYAA KUNZIA NCHI
6-8 UPANA 3-4 INAZIBUA MILIJA YA UZAZI DAW HIZI HAZINA MADHARA KWA MTUMIAJI HATA KWA WAZEE WALIO NA UMRI WAMIKA 68-82 TUMIA LEO UONE MAJABU YAKE TIBA HIZI NIZAKUDUMU

DR GATUNDU ANAZO DAW ZAKISUKALI PRESHA HENIA NGILI YAKUSHUKA BILA UPADUJI VIDONDA VATUMBO KUPUNGUZA UNENE UZITO TEZI DUME NA KUPONA KABISA DAWA ZASILI

OFISI ZETU ZINA PATIKANA DR ZAKHEM KWA WALE WAMIKOANIi WATA TUMIWA KWA NJIA YA MABASI PASIPO NA MASHAKA


Piga Simu Namba 0768 408 794

Hatimae Yanga imetoa List ya Wachezaji Wake 2018/19

$
0
0
Club ya Dar es Salaam Young Africans ikiwa siku moja imepita toka dirisha la usajili lifungwe, leo imetaja list ya wachezaji wake itakaowatumia msimu wa 2018/2019, huku ikimteua nahodha wao Nadir Haroub Canavaro kuwa meneja mpya wa timu yao.

Yanga imewasajili jumla ya wachezaji wapya saba huku ikiachana na wachezaji wake wanne ambao ni Hassani Kessy aliyemaliza mkataba wake na kwenda kujiunga na club ya Zambia, Obrey Chirwa aliyemaliza mkataba wake na kwenda Misri.

Wakati kwa upande wa Geofrey Mwashiuya amemaliza nae mkataba wake na kujiunga na Singida United huku Mzimbabwe Donald Ngoma wakivunja nae mkataba kutokana na kuwa majeruhi kwa muda mrefu, Ngoma kwa sasa amejiunga na Azam FC

Wakala wa Samatta athibitisha safari ya La Liga

$
0
0

NA ELBOGAST MYALUKO
Nyota wa Tanzania anayekipiga katika klabu ya soka ya KRC Genk ya ligi kuu ya Ubelgiji Mbwana Samatta, huenda akatua kwenye ligi kuu ya soka ya Hispania kwa msimu ujao, baada ya klabu ya Levante kuonesha nia ya kuhitaji huduma yake.


Wakala wa Samatta Jamal Kasongo ameweka wazi hilo kupitia East Africa Television ambapo ameeleza kuwa tayari klabu hiyo imeshatuma ofa kwa klabu ya Genk ikimhitaji Samatta ambaye pia ni nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania.

''Ni kweli pande zote mbili zipo kwenye mazungumzo kinachoonekana kuchelewesha usajili huo ni gharama ambayo Genk wanahitaji na kiasi walichotoa Levante ambacho ni Euro milioni 4 zaidi ya shilingi bilioni 10 huku Genk wakihitaji Euro milioni 10 zaidi ya shilingi bilioni 26'' - amesema.

Kasongo ameongeza kuwa kuna ofa pia kutoka klabu ya CSKA Moscow ya Urusi lakini hawajaipa nafasi sana kutokana na ndoto ya Samatta ni kukipiga katika Ligi Kuu ya England, ambayo ndio chaguo lake namba moja na La Liga kama namba mbili hivyo yupo tayari kujiunga na Levante.

Akiwa na Genk ambayo alijiunga nayo mwaka 2016, akitokea TP Mazembe ya DRC, Samatta amecheza mechi 66 na amefanikiwa kufunga mabao 19. Tayari Samatta ameshacheza michuano ya Europa League msimu uliopita lakini timu yake ilishia hatua za awali.

Kauli ya Cannavaro Baada ya Kupewa Uongozi Yanga

$
0
0
NA ELBOGAST MYALUKO
Klabu ya soka ya Yanga imefanya mabadiliko kadhaa kwenye uongozi wake katika ngazi mbalimbali huku miongoni mwa waliopata nafasi ni nahodha na mchezaji mkongwe Nadir Haroub 'Canavaro' akiteuliwa kuwa meneja wa timu.


Mabadiliko hayo yametangazwa na Yanga kwenye kikao na wahahabari kiichofanyika mchana wa leo Julai 28, 2018, makao makuu ya klabu ambapo mkongwe huyo aliyewahi kunukuliwa na kipindi cha KIKAANGONI cha East Africa Television akisema kuwa lengo lake ni kuja kuwa kiongozi wa soka, sasa amepata fursa hiyo.

Baada ya kutangazwa, www.eatv.tv imemtafuta Nadir Haroub ili kujua atatumikiaje nafasi hizo mbili ya nahodha na meneja, lakini ameeleza kwa kifupi kuwa amepokea taarifa hizo bila kuwepo kutokana na kuwa nyumbaji kwao Zanzibar akimuunguza mama yake ambaye anaumwa.

''Nimechaguliwa kuwa meneja kweli nimesikia ila siwezi kusema chochote nipo namuuguza mama yangu na hayupo kwenye hali nzuri naomba tuongee baadae nitaeleza mapokeo yangu'', - Nadir.

Nadir anachukua nafasi ya Hafidh Saleh ambaye alikuwa akishikilia nafasi hiyo na sasa ameteuliwa kuwa mratibu wa timu. Yanga kwasasa inajiandaa na mchezo wake wa marudiano wa kombe la shirikisho barani Africa dhidi ya Gor Mahia. Mchezo huo utapigwa Jumamosi kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.

Kocha wa Senegal Apewa Mkataba Wenye Mtego

$
0
0

Kocha wa timu ya taifa ya Senegal, Aliou Cisse amepewa mkataba mpya kuendelea kuifundisha timu hiyo huku akipewa sharti zito kuelekea michuano ya mataifa ya Afrika mwaka 2019 nchini, Cameroon.

 
Katika mkataba huo mpya, Aliou Cisse amepewa sharti la kuifikisha timu hiyo katika fainali za michuano ya Afrika ili kujihakikishia nafasi ya kuendelea kwa miaka mingine.

Wakati wa hafla ya upokeaji wa taarifa ya kiwango cha timu hiyo katika michuano ya kombe la dunia iliyokwisha mwezi huu nchini Urusi kutoka kwa kocha, Rais wa shirikisho la soka la Senegal, Augustin Senghor amesema.

“Katika tathmini ya mkataba wake, tunaona amefikia mafanikio yake ya awali ya kuiwezesha timu kufuzu michuano ya kombe la dunia ambapo ulimwengu mzima umetambua kuwa alifanya juhudi za kuipeleka Senegal katika hatua kubwa “.

“Tunaona hakuna sababu ya kushindwa kuendelea naye, kwahiyo tumempangia kazi nyingine ya kuhakikisha anaifikisha fainali timu yetu katika michuano ya mataifa ya Afrika “. Ameongeza, Senghor.

Senegal iliweka rekodi kuwa timu ya kwanza kuondolewa katika hatua ya makundi ya kombe la dunia kwa sheria ya ‘Fair play’ baada ya kulingana kila kigezo na timu ya taifa ya Japan ambayo ilisonga mbele katika hatua ya 16 bora.

Aliou Cisse (42) alikuwa katika kikosi cha Senegal kwenye michuano ya kombe la dunia mwaka 2002 nchini Japan ambacho kiliifunga bingwa mtetezi Ufaransa na kilifika hatua ya robo fainali. Aliteuliwa kuiongoza Senegal mwezi March, 2015 baada ya kuiongoza timu ya vijana ya nchi hiyo katika michuano ya Olympic nchini Uingereza mwaka 2012.

Kutana na Sharifu Seif Mohammed Mtaalam wa Tiba za Asili Tanzania

$
0
0
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.



Sharifu seif Mohammed ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA(Rudisha Mahusiano yako Ndani ya Saa 12 tu)



Sharifu seif Mohammed ni Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFATA MAELEKEZO YAKE..) Je Unasumbuliwa na Mapenzi..?

Umeachwa na UMPENDAE Awe Mume/Mke na Bado Unampenda Je Umejaribu Sehemu Nyingi Bila Mafanikio? Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo.. Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu.

Je Umekimbiwa na Mumeo/Mkeo au Mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine..?

Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao (Mfarakano/Kimavi) Endapo Utafata Atakacho Kuelekeza.

Je Una Mpenzi wako ana Pesa na unataka Kumkamata? Muone Maalim khatibu Atamfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi.. Sharifu seif Mohammed Anatumia Jina La Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo..

Anatibu Kutumia QUR_AN DAWA ZA ASILI YA AFRICA, Dawa za KIARABU NA MAJINI..

ANATAFSIRI NDOTO. ANAPANDIKIZA NYOTA YA KUSHINDA BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUSKI NA VIFUNGO MBALIMBALI.

ZINDIKO ZA NYUMBA NA BIASHARA.. PETE ZA BAHATI.. HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA. HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA..

MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA..ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA  ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE..

Humaliza Kesi ya Aina Yoyote Ndani ya Siku 7 tu..

Hutoa Jini la MALI kwa wale Wanao Hitaji Utajiri Bila Masharti.. Kwa mawasiliano na ushauri zaidi



Mobile + 255 654 836970

WhatsApp +255 756 033670

NB: Ni vyema kupiga simu kuliko kutuma sms ili upate huduma kwa haraka

Wakulima Waonywa Kuchanganya Nafaka na Mchanga

$
0
0
WADAU wanaojishughulisha na ununuzi wa mazao mbalimbali mkoani  hapa  wamewataka wakulima kuacha tabia ya kuchanganya nafaka na mchanga kwa kuwa  hali hiyo imekuwa ikiondoa ubora  na thamani wa mazao.

Ushauri huo ulitolewa na Meneja wa kiwanda cha The Agro Processing Africa Purimui Suvuiiyu  baada ya kubainika baadhi ya wakulima wa zao la choroko kuwa na tabia ya kuchanganya  nafaka na mchanga kwenye magunia kwa lengo la kuongeza  uzito.

Akizungumza na waandishi wa habari mbele ya wanunuzi wakuu wa nafaka kutoka kampuni ya Export Trading LTD yenye makao makuu ya jijini Dar- es- salaam, meneja huyo alisema kuwa baadhi ya wakulima wamekuwa wakiongeza uzito kwa kuchanganya kwenye nafaka hizo kwa kuweka mchanga.

Alisema hali imekuwa ikishusha thamani ya zao hilo.

“Kiwanda chetu kinajishughulisha na shughuli za uchakataji wa choroko ambazo tunanunua kutoka kwa wakulima, kinachosikitisha baadhi yao siyo waaminifu wamekuwa wakichanganya mchanga na nafaka zingine ambazo siyo za choroko na kusababisha kiwanda kuingia kwenye hasara kubwa,”alisema.

Alisema kuwa kiwanda hicho kinauza choroko zake hadi nchi za nje hivyo kitendo cha wakulima kuchanganya zao hilo na vitu vingine vinaweza kushusha thamani  kwenye masoko ya  nje ambao wamekuwa wakinunua.

Naye, Meneja  Uhusiano wa Kampuni ya Export Trading Group, Fatuma Ally alisema choroko inayonunuliwa toka kwa wakulima wadogo wakati mwingine inakuwa haina ubora wa kutosha na kutokidhi vigezo kwenye masoko ya nchi za nje.

Alisema hukutwa choroko zimechanganywa na mchanga hivyo kusababisha ufanyaji wa kazi kubwa wa usafishaji kabla ya uchakataji na pia kupunguza kiwango cha choroko iliyonunuliwa.

Hata hivyo alisema kwa upande wao wa kampuni ya Export imekuwa ikinunua mazao mbalimbali kwa ajili ya kuwakomboa wakulima katika kujipatia kipato cha bei pamoja na soko.


Utata Mkubwa Waibuka Bethidei ya Tifah waibuka

$
0
0
Wakati mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akitangaza maandalizi ya kufuru ya bethidei ya mwanaye Tiffah (pichani), utata umeibuka baada ya upande wa pili wa mzazi mwenziye msanii huyo, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kudaiwa kuipotezea.

Mtu wa karibu na familia ya Diamond ameeleza kuwa, Zari hajakubaliana na ‘mbwembwe’ zinazoandaliwa na msanii huyo kwa ajili ya shughuli hiyo hivyo ameamua kukaa kimya.“Yaani unaambiwa mama la mama (Zari) kafura, kaamua kuichunia baada ya kupishana na Mond katika suala zima la maandalizi ya bethidei hiyo.

“Inaonekana kuna kitu hususan katika mambo yao ya kibiashara maana si unajua wale kwao kila kitu ni biashara sasa linapokuja suala la bethidei kuna makampuni ambayo yanajitokeza sasa mamaa asipokubaliana na kitu ndo’ maana unaona hivi,” alinyetisha mtu huyo. Kudhihirisha kwamba Zari ameipotezea bethidei hiyo hususan inayoandaliwa na Diamond, chanzo hicho kilieleza kuwa, mrembo huyo wa Kiganda mwenye maskani yake pande za Sauz amekuwa kimya na hasapoti chochote kinachowekwa na Diamond.

“Wewe ingia Insta (mtandao wa Instagram) utaona tu, Zari hasapoti chochote tangu Diamond ameanza mbwembwe za kuinadi bethidei. Hakomenti wala yeye haposti kuhusu bethidei ya Tiffah. Kama hiyo haitoshi, hata akaunti ya Tiffah yenyewe haiongelei chochote kuhusu bethidei yake,” kilidai chanzo hicho.

Amani liliingia kurasa za Zari na Tiffah katika mtandao wa Instagram na kujiridhisha kwamba akaunti za wawili hao, hazisapoti chochote kinachopostiwa na Diamond kuhusu bethidei hiyo kubwa inayoelezwa kuwa itasherehekewa kwa takriban siku sita mfululizo pande za Sauz.

Amani pia ‘lilifukua makaburi’ kwa kuperuzi bethidei ya mwaka jana ya Tiffah na kukuta, Diamond na Zari walikuwa wakisapotiana kuisherehesha sherehe ya Tiffah ambayo awali ilikuwa ifanyike katika Ukumbi wa Mlimani City lakini ikaahirishwa, ikafanyikia nyumbani.

UTATA MWINGINE
Chanzo hicho kilizidi kumwaga ubuyu kuwa, utata mwingine uliogubika bethidei ya Tiffah ni kitendo cha Diamond kutaka kuitelekeza bethidei ya mtoto wake aliyezaa na mwanamitindo Hamisa Mobeto, Dylan jambo ambalo limesababisha minong’ono ya chinichini kutoka kwa Team Mobeto.

“Watu wa Mobeto wameanza kumnanga Diamond na kumwambia haiwezekani amuache Dylan ambaye bethidei yake ni Agosti 8, halafu aende kufanya bethidei ya Tiffah Agosti 17, mwaka huu. “Tutapiga kelele kweli mitandaoni asitufanyie hivi kwani huyu Dylan sio mwanaye? Kwa nini wao wote kuanzia Diamond, Esma na mama yake Diamond wapendelee kule na si huyu wa mtoto wa huku nyumbani?” kilimwaga ubuyu chanzo hicho.

DIAMOND HUYU HAPA
Juzi, Amani lilimvutia waya Diamond akiwa nchini Marekani na kumuuliza juu ya utata ulioibuka ambapo kwa upande wake alisema haoni tatizo kwani wote ni watoto wake na Dylan atawakilishwa na mama yake (Mobeto) pamoja na bibi yake (mama Mobeto). “Mimi sioni tatizo. Nitakwenda Sauz sababu nitakuwa nimemaliza ‘tour’ yangu ya muziki lakini huko nyumbani, Mobeto ni mzazi mwenzangu pia, ataniwakilisha pamoja na mama yake Mobeto,” alisema Diamond.

Alichoandika Masanja Kuhusu Diamond Kuzuiwa Uwanja wa Ndege.

$
0
0
Alichoandika Masanja Kuhusu Diamond Kuzuiwa Uwanja wa Ndege.
Moja ya habari zilizosambaa sana katika mitandao ya kijamii leo ni habari ya msanii mkubwa tanzania, Diamond Platinumz kuzuiwa uwana wa ndege kwa kile kilichodaiwa kuwa alikuwa hana kibali vcha kwenda kufanya show nje ya nchi.

Na hata baaada ya mamlaka husika iliyomzuia kuulizwa walisema kuwa wamefanya hivyo kwa diamond ili kuwafunza wanamuziki wengine kufuata utaratibu kuhusu sheria mpya za BASATA.Kila mtu alipokea kwa hisia zake swala hio na mmoja aliyelipokea kwa masikitiko ni msanii wa vichelesho nchini masanja mkandamiza ambae katika akaunt yake ya twitter aliandika

Diamond ni moja kati ya vijana wanaojituma sana ili kufanikiwa na  kusaidia watu wengi kufanikiwa.huwezi kupendwa na kila mtu lakini hii sumu ya baadhi ya watanzania kufurahia mtu akipata tatizo au kumzushia upopompo anapofanikiwa au kuchukiwa mtu kupiga hatua inahitaji maombi ya kitaifa.

Zijue sababu za Watoto kukosa Hamu ya kula Chakula

$
0
0
Kukosa hamu ya kula ni tatizo la kawaida kwa watoto ambalo hupelekea wazazi wengi kuwa na wasiwasi juu ya afya ya watoto wao. Kuna sababu nyingi zinazoweza kusababisha  kukosa hamu ya kula na tatizo hili linapojitokeza tunatakiwa kuwa watulivu na kujaribu kuchunguza kwa makini ni kwa nini mtoto anakosa hamu ya kula. Baadhi ya sababu zaweza kutatuliwa na mzazi au mlezi lakini sababu nyingine kama zisababishwazo na magonjwa zitahitaji msaada wa wataalam wa afya.

Moja ya sababu kubwa ambayo huwakosesha watoto hamu ya kula ni aina mbalimbali za magonjwa. Magonjwa kama Malaria, kuhara, maumivu ya tumbo, maumivu ya kichwa, magonjwa ya kinywa na koo, homa na mafua au dalili nyinginezo ambazo humkosesha mtoto raha hupelekea watoto kukosa hamu ya kula.

Matatizo ya kifamilia na msongo ni sababu nyingine ambayo huwakosesha watoto raha na hamu ya kula. Kama walivyo watu wazima watoto pia hukumbana na matatizo ya kifamilia kama kupoteza ndugu au vitu wavipendavyo. Lakini pia watoto hukumbana pia na changamoto mbalimbali za kimaisha kama majukumu ya shule au pengine kukumbana na unyanyasaji kama kuzomewa na mambo mengine mengi yanayokiuka haki zao.

Kwa hiyo ili kumuepusha mtoto na ukosefu wa hamu ya kula, wazazi na walezi hawana budi kuwa makini endapo wataona mabadiliko yoyote ya kitabia ya mtoto. Kugundua na kuweza kuziondoa sababu zinazomsababishia mtoto msongo, tutaweza kuwarudisha katika hali ya kawaida na hamu ya kula itarejea tena.

Lakini pia wakati mwingine hali hii hutokana na ugonjwa wa kukosa hamu ya kula ujulikanao kitaalam kama Anorexia nervosa. Watoto wenye ugonjwa huu huweza kukaa muda mrefu bila kula ingawa hawana tatizo jingine, na endapo watapewa chakula huchagua aina fulani tu ya chakula jambo ambalo hupelekea kutopata mlo ulio kamili na hii hupelekea kupungua uzito pamoja na kudhoofu kwa afya zao .

Jambo hili linapojitokeza ni vyema kumpeleka mtoto kwa wataalam wa afya wa masuala ya lishe ambao watakuwa msaada mkubwa katika kumsaidia mtoto wako kurejesha tena hamu ya kula.

Kiwango kidogo cha ukuaji wa mtoto huchangia  kupungua kwa hamu ya kula. Katika mwaka wa kwanza wa maisha ya watoto, watoto hukua haraka lakini baada ya mwaka mmoja kiwango cha ukuaji hupungua na kiwango cha chakula wanachokula pia hupungua. Katika wakati huo, hali hiyo ni ya kawaida katika maisha ya watoto.

Sababu nyingine ambazo huchangia watoto kukosa hamu ya kula ni kama maudhi ya dawa, upungufu wa damu, uambukizi wa minyoo na matatizo ya mmeng'enyo mfano mtoto kutopata choo.

Maudhi ya dawa mbalimbali ambazo hutumika kutibu magonjwa kwa watoto yanaweza kuchangia watoto kukosa hamu ya kula. Mfano daktari akimwandikia mtoto dawa za antibiotiki, zaweza kusababisha tazizo la kukosa hamu ya kula. Kupoteza hamu ya kula kwa watoto wanaotumia antibiotiki ni maudhi ya dawa ambayo huwapata watoto wengi. Dawa nyingine pia zaweza kupelekea kupata maudhi ya dawa kama kichefuchefu na kutapika. Tatizo hili humalizika mtoto anapomaliza dawa na endapo atakuwa amepona.

Uambukizi wa minyoo huchangia tatizo hili. Minyoo huingia katika mfumo wa mmeng'enyo wa watoto na kusababisha upotevu wa damu. Minyoo hutegemea ufyonzaji wa damu kama chakula chao, na katika uambukizi sugu hupelekea kuvuja kwa damu,upungufu wa damu, kuhara, kichefuchefu, kutapika na kukosa hamu ya kula. Endapo mtoto ataonyesha dalili za umbukizi wa minyoo, ni vyema kuwaona wataalam wa afya ili kuweza kufanyiwa vipimo na kupatiwa matibabu.

Ugonjwa wa upungufu wa damu ambao kwa kitaalam hujulikana kama anemia, husababishia watoto tatizo hili. Kiwango kidogo cha madini ya chuma katika damu, huwapata watoto ambao hawapati lishe ya kutosha yenye madini haya. Lakini pia anemia yaweza kusababishwa na uambukizi wa minyoo au hata magonjwa mengine. Watoto wenye anemia huwa wadhaifu na wasio wachangamfu, na kama ugonjwa usipotibiwa utaathiri afya ya mtoto hata maendeleo yake shuleni. Ni vyema mtoto akafanyiwa vipimo vya damu endapo utahisi au ataonyesha dalili za ugonjwa wa anemia.

Kwa watoto hasa wadogo, kukosa choo hupelekea kukosa hamu ya kula. Kwa hiyo inapotokea basi ni vyema kupata msaada wa wataalam ili mtoto aweze kuondokana na tatizo hilo.

Wazazi na walezi wazingatie yafuatayo ili kuboresha hamu ya kula ya watoto wao:


Kuwa na ratiba nzuri ya kumpa mtoto chakula, na mtoto apewa chakula anapokuwa na njaa.
Usiwagombeze au kutoa maonyo makali kwa watoto wakati wa kula.
Kuwa na milo midogo kati ya milo mikubwa.
Mpe mtoto kiasi kidogo cha chakula lakini mara nyingi kwa siku na siyo kumshindilia kwa wakati mmoja.
Usimlazimishe mtoto kula kama hana njaa.
Hakisha mtoto anashiriki katika michezo, kwa kuwa michezo huusisha matumizi ya nishati ya mwili na kuboresha mifumo mbalimbali ya mwili.
Wakati mwingine mpe nafasi mtoto wa uchaguzi wa chakula akipendacho, lakini chini ya uangalilizi wa mzazi au mlezi ili afanye uchaguzi ulio sahihi.

Wakati wote  wazazi na walezi tukumbuke kuwa tatizo la kukosa hamu ya kula ni la kawaida kwa watoto wengi, na tatizo linapojitokeza hatuhitajiki kuwa na wasiwasi kila wakati. Kama mtoto wako ana afya njema, anapata usingizi vizuri na ni mwenye furaha, hauna sababu ya kuwa na wasiwasi. Lakini kama tatizo litaendelea kwa muda mrefu, basi hatuna budi kuonana na wataalam wa afya kwa msaada zaidi.

Nimelala na Mwanamke Mke wa Mtu Kitanda Kimoja Usiku Kucha ..........Tukajikuta Tume....

$
0
0

Ni mfanyakazi mwenzangu tumeenda nchi jirani kwa semina ya siku 5.Tulivyofika tu wakati tunacheki hotel ambayo ni nzuri bei kidogo ipo juu ila kampuni wametupa pesa za kutosha sana,Sasa wakati tunajadiliana jinsi ya kufanya yule sister akasema, Kwa nini tusichukue chumba kimoja tukashare ili tusave hizi pesa? Nilijua ananitania lakini akasisitisha kwamba yupo serious.

Tukachukua chumba kimoja chenye kitanda kimoja tukazama ndani.Ile kuingia tu ndani yule sister akasema anataka kuoga sababu ya uchovu wa safari akjifunga taulo kavua nguo kazama bafuni.Picha nyingi sana zikanijia ifikapo usiku itakuwaje? Sababu yeye ni mke wa mtu na mimi nina mke home.

Nikajiapisha sintofanya chochote na huyu sister kwanza tunaeshimiana sana. Nmimi nikaenda kuoga baada ya yeye kutoka nilivyorudi nikakuta ashavaa nguo. Story story kidogo tukashuka chini tukaenda pata dinner mpaka kwenye saa 5 usiku tukarudi room.
Kufika tu yule sister kavua nguo zake hii sasa alivua mbele yangu akapiga night dressing kajitupa bed.

Na mimi nikajipa moyo nikavua nikapiga bukta nikazama bed.Tukapiga story mbili tatu huku tukiwa tumejifunikia shuka moja.
Mara usingizi ukanipitia kushtuka nimemkumbatia ile mbaya nikijua ni wife home kuchek na yeye kanikumbatia na kaweka mguu juu yangu.Ki ukweli hali ilikuwa ngumu sana mpaka mapigo ya moyo yalibadilika.

Ki ukweli usingizi ulikata nikawa nimemkumabatia mpaka asubuh. Palipokucha yaani yule sister hana time akazama zake bafuni katoka kapiga suti yake na mimi nikazama bafuni kutoka tukaelekea kwenye hotel inapofanylika semina.

Jamani hii ndio siku ya kwanza kweli niatweza maliza siku tano bila kuingiza ndoa yangu matatani kwa style hii kweli.
Ila nimeapa kutofanya chochote na huyu sister.
Ee mungu nipe ujasiri.

By Manuu/JF

Majibu ya Ukimwi ya Diamond Gumzo, Msururu wa Wanawake Wawekwa Mezani

$
0
0
DAR ES SALAAM: Baada ya mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kuanika stika inyaoonesha amepima magonjwa yote, gumzo la aina yake limeibuka kwenye mitandao ya jamii huku kelele zaidi zikipigwa kwenye majibu hususan Ugonjwa wa Ukimwi.



Akiwa nchini Marekani katika ziara ya kimuziki hivi karibuni, Diamond aliweka ‘status’ kwenye akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Instagram inayomuonesha mkononi amefunga stika maalum ya hospitali inayoashiria amefanyia vipimo vya mwili na ndipo mjadala mkali uliposhika kasi kama moto wa kifuu.



TUICHAMBUE KWANZA STATUS

Kwenye status hiyo ambayo hukaa muda mfupi na kuondoka, stika aliyoivaa mkononi ilionesha jina lake (Nasibu Abdul), tarehe aliyozaliwa (Oktoba 2, 1988) aliyofanya vipimo hivyo yaani Julai 22, mwaka huu huku akiambatanisha na ujumbe wa maandishi kwa lugha ya Kingereza.

Kwa tafsiri isiyo rasmi sana, ujumbe huo uliashiria kwamba; “ni vigumu kupima na kuhakikisha anarudi nyumbani bila maambukizi kwa kupima mwili mzima (full body checkup),” mwisho wa kunukuu.



BALAA LAANZIA HAPO

Mara baada ya kuandika ujumbe huo ulioonesha kwamba amechekiwa mwili mzima, wachangiaji mbalimbali waliochangia mtandaoni humo, walianza kujiongeza kwa kujadili suala zima la matokeo ya vipimo hivyo na zaidi kwao haikuwa katika majibu kama ya Homa ya Ini, Malaria au Kifua Kikuu bali wengi walijikita kwenye Ukimwi kwenye eneo hilo.Wapo walionesha wasiwasi na kupinga kuwa haiwezekani akawa salama lakini wapo pia ambao walisema inawezekana.



MREMBO ASHADADIA ISHU

Baada ya Diamond kuweka status hiyo, mrembo aliyejitaja kwa jina la Kei, aliinasa picha pamoja na ujumbe wake huo na kuiweka fasta kwenye akaunti yake ya Instagram huku akiiambatanishia maneno yake kama ifuatavyo:

“Kama Mond kapima ngoma.. basi Ukimwi haupo..ngoja na mimi nikapime kesho…”Maneno hayo yaliamsha uchangiaji wenye mgongano wa hoja kwa baadhi ya marafiki wa msichana huyo ambapo wengi walimshambulia kwa kujaribu kutilia shaka vipimo vya afya alivyofanya Diamond huko Marekani.



“Mshamba tu wewe, kupima kwake kunakuhusu nini au na wewe amekupitia?” “Mi napita tu wajamani.”“Mambo ni moto, hana ngoma mzee baba…tehe.”“Kwi, kwiii, kwiiiiiii.” Hizi zilikuwa ni baadhi ya fleva za wachangiaji katika posti hiyo huko kwingineko nako hakukua shwari.



MSURURU WA WAREMBO WATAJWA

Waliokuwa wanaonesha wasiwasi, walikwenda mbali zaidi kwa kuweka mezani warembo ambao wamewahi kuwapitia’ mkali huyo wa Bongo Fleva hususan wale mastaa na kuongeza na wale wasiojulikana.



“Jamani tuwe wakweli, we msururu wa warembo alionao Diamond kweli anaweza kuwa salama?” Alihoji mmoja wa wachangiaji mtandaoni. Mchangiaji mwingine alizidi kushusha data kwa kuanika msururu wa warembo wanaodaiwa kutembea na Diamond na kuanzia na Wema Sepetu (muigizaji), Jokate Mwegelo (modo na muigizaji), Penniel Mungilwa ‘Penny’ (mtangazaji), Irene Uwoya (muigizaji), Hamisa Mobeto (mwanamitindo), Lynn (modo) na Rehema Fabian (miss), orodha hii ibaki kuwa mali ya wachangiaji mitandaoni na siyo ya Amani.



Kuwekwa mezani kwa warembo hao na wengine wakidai hao ni baadhi tu ya watu maarufu na kwamba wapo wengine pia wasiokuwa mastaa, bado wengine waliiponda orodha hiyo kwa kusema haina mashiko kwani suala la Ukimwi linabaki kwenye hoja ya kupata mchubuko kati ya watu wawili wanaposhiriki tendo la ndoa.



DAKTARI ANENA

Ili kupata uelewa mpana wa jambo hilo lililozua gumzo mtandaoni, Ijumaa lilizungumza na daktari maarufu jijini Dar, Dk Chale ambaye alieleza kuwa, maambukizi ya virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Ukimwi husababishwa na mambo mbalimbali. Alisema ngono zembe huchangia, mtu kushea vitu vyenye ncha kali na mtu mwenye maambukizi ya virusi vya Ukimwi kama sindano na wembe.



Mbali ya hilo, alisema upo uwezekano mdogo wa mtu kushiriki tendo la ndoa na mtu mwenye maambukizi na asipate maambukizi endapo hakutatokea mchubuko. “Lakini ni kwa asilimia chache sana mtu anaweza asipate mambukizi na ndiyo maana wataalamu mbalimbali wa masuala ya afya wanashauri kujikinga kwa kuvaa kondomu,” alisema dokta Chale.



MAJIBU YA DIAMOND YAKOJE?

Ijumaa lilimvutia waya juzi Diamond ili kutaka kujua anazungumziaje ishu hiyo na kama atakuwa tayari kuanika majibu ya vipimo vyake lakini simu yake ilikuwa haipatikani. Hata hivyo, mtu wa karibu na Diamond alieleza kuwa kwa wakati huo msanii huyo alikuwa safarini hivyo huenda ndiyo sababu ya kutompata kwa urahisi.



TUJIELIMISHE

Kama jamii suala la unyanyapaa ni la kupingwa na kila mtu, kwani haifai hata kidogo kunyoosheana vidole katika suala la Ukimwi kwani kufanya hivyo kunachangia kulikuza tatizo. Ifahamike pia kwamba mtu kuambukizwa Ukimwi hakutokani na wingi wa wapenzi alionao mtu bali kupuuza kutumia kinga katika kila tendo la ndoa, jambo ambalo kila mmoja anatakiwa kuwa na umakini nalo ili kulipiga vita gonjwa hilo.

STORI: MWANDISHI WETU, IJUMAA
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images