Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104670 articles
Browse latest View live

Mamia Wamshambulia Wema kisa Jokate kuwa DC, Wadai Aendelee tu na Kiki za Insta

$
0
0

Wikiendi hii imekuwa ni ya nenda kwa usalama katika mitandao ya kijamii kutokana na habari kubwa kabisa ya mh rais kuteuwa viongozi mbalimbali wapya huku habari kubwa ya mastaa ikiwa ni kutokana na mwanadada jkate mwegelo kuteuliwa kuwa mkuu wa wilaya.

Watu wengi wamefuraha hasa kutokana  na uachapakazi  wa mwanadada jokate, alkini pia kutona ana moyo wake  wa kujitoa na kusaidia wengine.

Lakini wengi wamekuwa wakitoa mapovu kwa mwanadada Wema Sepetu huku wakisema kuwa inawezekana kabisa kuwa nafasi hii kubwa aliyopewa jokate hata yeye alipaswa kuwa nayo kutokana na ukweli kuwa hata yeye amekuwa katika siaisa miaka mingi .

Swala linalowafanya wamtukane na kumtolea mapovu ni kutokana ana tabia ya Wema ya kushindwa kujiheshimu , na kutokuwa na siri kwa kila kitu.amekuwa akijiingiza katika mambo ya hovyo yanayomuondolea sifa za kuwa na wadhifa mzuri.hizi n baadhi ya comment za mashabiki


Kidomo Domo Chawaponza Yanga Wachapwa Tena Kipigo cha Mbwa Mwizi na Gor Mahia

$
0
0
YANGA wameendeleza mwendo ambao siyo mzuri katika michuano ya kimataifa baada ya kuruhusu kupata kichapo kutoka kwa Gor Mahia cha mabao 3-2 kwenye mchezo wa hatua ya makundi wa Kombe la Shirikisho Afrika. Yanga wameshacheza michezo minne hadi sasa kwenye Kundi D ambalo lina timu nyingine ambazo ni USM Algers ya Algeria na Rayon Sports ya Rwanda, lakini hawajapata ushindi kwenye mchezo hata mmoja.

 Matokeo ya mchezo wa jana yanamaanisha kuwa sasa Yanga wamebakiza michezo miwili tu kwenye kundi lao na hawana matumaini ya kufuzu. Katika michezo miwili ambayo Yanga wamekutana na Gor Mahia hivi karibuni, wamefungwa jumla ya mabao saba, baada ya mchezo wa kwanza kufungwa 4-0 jijini Nairobi.

 Katika mchezo wa jana, kipa wa Yanga, Youth Rostand alifanya makosa kadhaa ambayo yalichangia mabao mawili ya mwanzo ya Gor Mahia.

Rostand alifanya kosa katika sekunde ya 35 tangu kuanzia kwa mchezo hu ambapo aliucheza mpira vibaya uliopigwa kichwa na George Ogutu na kujaa wavuni.

Hata hivyo, aliendelea kufanya makosa ya mara kwa mara ambapo dakika ya 41 kipa huyo aliudaka mpira akaurusha vibaya kabla haujaguswa na mchezaji mwingine akaudaka tena, mwamuzi akaamuru kuwa ni faulo ambapo Jacques Tuisenge aliifungia timu hiyo bao la pili.

 Dakika ya 55, Deus Kaseke, ambaye alicheza mchezo wake wa kwanza tangu asajiliwe na Yanga, hivi karibuni aliifungia timu yake bao moja baada ya kipa wa Gor Mahia, Boniface Oluoch kuutema mpira.

 Hata hivyo, matumaini ya Yanga hayakudumu kwani dakika ya 64, Gor Mahia walifunga bao la tatu kupitia kwa Haron Shakava baada ya mabeki wa Yanga kufanya uzembe. Dakika ya 75, Yanga walimtoa Rostand na nafasi yake kuchukuliwa Beno Kakolanya ambapo wakati anatoka mashabiki walikuwa wakimzomea.

 Dakika tano baadaye Raphael Daudi aliifungia timu hiyo bao la pili baada ya kipa kushindwa kukoa shuti lililopigwa na Ibrahim Ajibu. Hata hivyo, kocha wa Yanga, Mwinyi Zahera hakuonekana kwenye mchezo huo ambapo Noel Mwandila ndiye alikuwa anatoa maelekezo kwenye benchi.

Tunatibu Na Kuponesha Kabisa Upugufu wa Nguvu za Kiume, Busha, Kisukari na Vidonda vya Tumbo

$
0
0

TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO? BUSHA BILA KUPASUA KISUKALI NA VIDONDA VYA TUMBO? asilimia kubwa ya wanaume wanaupungufu wa nguvu za kiume NA maumbile madogo

NI NINI KINACHOSABABISHA UUME KUZIDI KUWA MDOGO NA WEMBAMBA 1 kuugua chango LA uzazi 2 unene kupita kiasi 3 kuvaa nguo au chupi za kubana 4 kupiga punyeto kwa mda mrfu ,NI NINI TIBA YAKE MAKAKANUA MIX nidawa ya mitishamba iliyochanganywa NA mizizi kumi NA mbili urfusha NA kunenepesha UUME saizi upendayo ich 5,6,7, NA 8 kwa urfu NA sentimita 3,4, na 5 ipo dawa ya kunywa na kupaka NI NINI KINASABABISHA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME 1 kupungukiwa kwa homoni ya testerone 2 kuhudhurika kwa Neva au uti wa mgongo 3 utumiaji holela wa madawa ya kizungu 4 usongo wa mawazo na asira 5 utumiaji wa vyakula vya mafuta mengi NI NINI TIBA YAKE MAPRO POWER NO 2 NDIO tiba tosha kwa sasa kwani utibu matatizo matatu kwa pamoja 1 itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15 adi 20 ,2 itakufanya urudie tendo zaidi Mara tatu 3 uhimalisha uume uliolegea na kusinyaa OKOA NDOA YAKO SASA ujihepusha na lawama ndani ya ndoa yako au pale ukutanapo na mpezi dawa hii itamfanya mpenzi wako hakueshimu na hasitoke nnje ya ndoa na ata wazee wenye umri mkubwa wanapona zipo dawa za kupunguza kitambi,minyama uzembe, presha ,kisukar mvuto wa mpezi au biashara FIKA OFISINI KWETU MBAGALA ZAKHEMU na wateja wa kanda ya ziwa yupo wakala wetu mwanza mjini au piga simu 0752348593

DR MABULA na utaletewa popote ulipo uduma hizi

Ali Kiba Huenda Akakosa Mechi Ya Kwanza Ndani Ya Coastal Union

$
0
0
Msanii wa Muziki wa Bongo fleva anayefanya vyema kabisa na ngoma yake ya ‘Mvumo wa radi’ Ali Kiba amedaiwa anaweza akakosa mechi muhimu kabisa ndani ya Coastal Union.

Ali Kiba ambaye alitangazwa kusajiliwa na timu hiyo ya mkoani Tanga wiki iliyopita, anasemekana kuwa ana aweza akakosa mechi yake ya kwanza ndani ya timu hiyo kutokana na shoo yake ya muziki.

Global Publishers wanaripoti kuwa Ligi Kuu imepangwa kuanza kutimua vumbi Agosti 22 lakini ratiba ya shoo ya Alikiba inaonyesha itaanza Agosti 17, 18 na 25, mwaka huu huko Toronto, nchini Canada katika shoo iliyopewa jina la The All Star Music.

Ratiba inaonyesha Coastal Union wataanza ligi, Agosti 22 dhidi ya Lipuli FC kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga hivyo Alikiba hatokuwa sehemu ya wachezaji watakaocheza mechi hiyo.

Meneja wa Coastal Union, Said Hilal ameweka wazi kuwa wanatambua majukumu ya kimuziki ya Ali Kiba hivyo hawana tatizo juu ya kukosa kwake mechi.

Tunajua AliKiba ana majukumu yake mengi na sisi kama klabu hatuwezi kumzuia kwenye hilo pale ambapo atakuwepo atafanya kazi na wenzake hivyo hakuna tatizo”.

Casto Aomba Maamuzi yake Yaheshimiwe, Sisikii lolote Kuhusu Tunda

$
0
0

Mtangazaji wa clouds media , Casto Dickson Amfunguka na kuwaomba watu wanaomsema na kumshangaa kwanini ana mpenda sana tunda wamuache na kuheshimu sana maamub=zi yake kwa sababu hapo ndipo alipofikia na ana mapenzi ya dhati na mwanadada tunda.

Akiandika katika ukurasa wake wa instagram, casto anasema kuwa tunda ndie mwanamke anampa ratiba zake za kila siku katika kazi zake katika maish yao.

respect my choice, she is the one who tells me casto its time to job,casto una ahadi ya kikao sehemu,unatakiwa kwenda kwenye hiki na hiki ila nyie majiran hamjui,yaacheni ya moyoni yabaki ya moyoni, nawaheshimu na nina wapenda sana, i love you mmachame wangu,

Tangu mahusiano ya catso na tunda yameanza kwa zaidi ya miezi sita sasa, mashabiki wamekuwa wakimsema sanacasto hasa kutokana na yale aliyowahi kuyafanya nyuma tunda, hata hivyo anachoamini casto kwa mwanamke wake ni kwamba hayuko kama zamani .

Faiza Ataja Sababu Ya Kuanika Ugomvi Wake na Sugu Mitandaoni

$
0
0

Muigizaji wa Bongo movie na mjasiriamali maarufu Kwenye mitandao ya kijamii Faiza Ally amedai sababu inayompelekea yeye kuanika ugomvi wake ni Sugu mitandaoni ni kukosa njia nyingine ya kuwasiliana naye.

Faiza na Sugu wamezaa mtoto mmoja anayeitwa Sasha na kwa muda mrefu wawili ho wamekuwa Kwenye migogoro na migogoro yao huwa Ikiwa Kwenye mitandao ya kijamii.

Kwenye mahojiano na gazeti la Risasi Jumamosi, Faiza amedai hana njia nyingine ya kumfikishia ujumbe mzazi mwenziye huyo zaidi ya kwenye mtandao wa Instagram kwani ndio sehemu pekee ambayo atasoma na kumuelewa kwa umakini na huwa anafanya hivyo kwa sababu hakuna anayeweza kumfikishia ujumbe mzazi mwenzie huyo kwa kuwa wanamuogopa.

Mimi sinaga namba yake na ndio maana huwa naandika Instagram sababu nahisi ndio sehemu sahihi kwani nikiwatuma watu wakamfikishie ujumbe huwa wanamuogopa nikaeleza kwamba aache kutumia watu mahitaji ya mtoto, alete mwenyewe mtoto amuone”.

Siku chache zilizopita Faiza amemuanika Sugu Mtandaoni na kudai amelogwa baada ya kukataa kumpa fedha za matumizi ya mtoto wao.

Lucy Komba Ammwagia Mapovu Irene Paul

$
0
0

Mwanadada Lucy Komba amemtolea povu msanii mwenzake irene paul kutokana na ukweli kwamba amekuwa akishindwa kumapa yeye credit na shukrani kwa kuwa yeye ndi ealimsaidia kutoka katika movie na wala sio wakina ray au kanumba ambao mara nyingi amekuwa akiwataja katika media.

Lucy Komba anasema kuwa  yeye ndie aliemfundisha irene kuigiza na kumpa nafasi katika katika movie ya cleopatra na fedheha ambapo ndipo kipaji chake kilianza kuonekana akiwa chini ya uangalizi wake yeye,.

Katika post yake lucy komba aliandika
Cleopatra  na NANI KAMA MAMA ni movie mbili zenye stori tofauti , utunzi wake ulikuwa wa kipekee kabisa na hakuna aliyeweza huu utunzi.na ni msanii mmoja tu aliyeweza kucheza party zote mbili katika nafasi tofauti tofauti.lakini pia hiyo ndip picha ya kwanza ya angelina jolie asietaka kujishusha.

Hata baada ya kuandika hayo waandishi waliamua kumtafuta Lucy ili kuelezea kwa undani maneno hayo na ndipo aliposema kuwa Irene  paul anasumbuliwa na kutokujielewa na kuvimbiwa ustaa wa bongo, na kushindwa kukumbuka kuwa yeye ndie alimuibua katika sanaa.

Lucy anasema amewatoa wasanii kama Jackline Wolper,Yusup mlela, Mzee chilo na hata Irene uwoya.

Tetesi za Barnaba Kurudiana Kimapenzi na Mama Steve, Ukweli Huu Hapa

$
0
0

Mzazi mwenza wa staa wa Bongo fleva anayefanya vyema na ngoma yake ya ‘Chausiku’ Barnaba Boy Classic, Zubeda amekataa kabisa Kurudisha Penzi kwa Baba watoto wake huyo.

Zubeda na Barnaba walikuwa Kwenye Mahusiano ya Kimapenzi kwa miaka mingi na hata kujaaliwa kuzaa mtoto mmoja wa kiume lakini penzi lao lilivunjika na kila mmoja kushika njia yake.

Siku chache zilizopita kulikuwa kuna tetesi kuwa wawili hao wameweka tofauti zao pembeni na kuamua kuwa pamoja tetesi ambazo Zubeda amezikataa na kudai hawezi kurudi kwa mzazi mwenziye kwa sababu kila mtu ana maisha yake mengine.

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Zubeda alisema kila mtu kwa sasa yuko kwenye uhusiano wa kimapenzi na wanaheshimiana katika hilo kilichobaki kwao kubaki kama wazazi na hakuna lingine zaidi ya hilo kwa sababu tangu wametengana ni muda mrefu sasa.

Watu wanadai tu kuwa nimerudi kwa Barnaba, lakini sio kweli kabisa yule ni mzazi mwenzagu tu na ataendelea kuwa hivyo na si kitu kingine kwa sababu nina mtu wangu na yeye ana mtu wake kilichobaki ni heshima tu ya mzazi mwenzangu”.

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

$
0
0

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

$
0
0


Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

Je, ni lini Wasafi FM itaanza kurusha matangazo hewani kama Wasafi TV? Diamond Platnumz atoa majibu

$
0
0
Diamond Platnumz amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusu ni lini kituo chake cha radio cha Wasafi FM kitaanza kurusha matangazo kama ilivyo kwa kituo chake cha Runinga cha Wasafi TV.

Habari nzuri ni kwamba Diamond amesema Wasafi FM itaanza kurusha matangazo yake mwezi Januari mwakani huku akieleza mipango yake ya kupanua wigo wa matangazo kwa Wasafi TV.
“Nimefungua Tv inaitwa Wasafi TV na inafanya vizuri sana na tupo katika mikakati ya kuhakikisha inapatikana bara zima la Afrika na ulimwenguni kote. Lakini pia mwezi wa kwanza au mwishoni mwa mwaka huu tunafungua pia Wasafi FM itakuwa hewani.“amesema Diamond Platnumz kwenye mahojiano yake na kituo cha radio cha Mayotte la 1ère cha kisiwani Mayotte alipoulizwa na moja ya matu waliopiga simu studio kumuuliza kama anamiliki vituo vya Radio na Runinga.

Wikiendi iliyopita Diamond Platnumz alikuwa Mayotte na alifanya show babkubwa kwenye visiwa hivyo vya Ufaransa. Tazama mahojiano yake na kituo hicho cha radio kwa lugha ya Kifaransa.

VIDEO:

Bongo5

Karen Aelezea Baba Yake Hakutaka Afanye Muziki, Ataja Mchango wa Jay Dee Kwake.

$
0
0
Msanii chipukizi wa bongo malkia karen amefunguka na kusema kuwa katika kufanya kazi ya muziki alipata upinzani mkubwa sana hapo mwanzo kutoka kwa wazazi wote wawili.karen ambae ni mtoto wa captain g habash anasema kuwa baba yake mara nyingi alikuwa akiogopa sana kuhusu maadili hasa kukaa vizuri sana mbele za watu.

Baraka zote zipo kutoka kwa wazazi wote wawili,mwanzoni ilikuwa ngumu sana kwa wote wawili na pia kwa uapnde wa baba ni kwamba kwa sababu yeye tayari ni nguli katika tasnia ya muziki kwaio alikuwa  anajua, kikubwa alikuwa  anakazania maadili tu,

Lakini pia Karen anakiri kuwa moja ya wat waliochangia sana kufika katika muziki na kufanikiwa ni mama yake mdogo Jay Dee ( ambae alikuwa akiishi na baba yake kwa ndoa) kutokana na kukaa nae vizuri lakini pia alikuwa akimlea vizuri na kumpa ushawishi mkubwa wa kufanya muziki.

Nilishawahi kukaa nae na alinilea vizuri sana hasa katika muziki,Kwakweli alini-inpire sana na katika nyimbo ninazozipenda ni ule wa faraja.

Waziri Lugola Kuyafuta Makanisa Na Misikiti Yenye Kuendeleza Migogoro Na Kutofuata Sheria Za Nchi

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amesema hatasita kufuta makanisa au misikiti inayoshindwa kutatua migogoro ya taasisi hizo.

Ametoa kauli hiyo jana Julai 29, 2018 katika Kanisa la Pentekoste la Leganga, lililopo Arumeru mkoani Arusha.

“Kuanzia sasa, kanisa lolote au msikiti wowote utakaokumbwa na migogoro na kushindwa kuitatua wenyewe; misikiti hiyo, makanisa hayo nitakwenda kuyafuta mara moja,” alisema.

Alisema hatua hiyo inalenga kuhakikisha yanakuwapo makanisa na misikiti inayohubiri amani na utulivu.

Waziri Lugola ameonya askari Polisi wanaowashusha jukwaani masheikh na wachungaji inapofika saa 12:00 jioni, akisema muda huo ukifika waimarishe ulinzi ili waumini wamalize ibada zao vizuri.

Vera Sidika na Otile Brown Wapigana Chini...

$
0
0
Such is Life can confirm that Otile Brown and Vera Sidika may have  broken up. Like O.V.E.R!

Singer Otile Brown and his lover Vera Sidika are no longer together at least according to their social media pages, or is it a publicity stunt? The two have been displaying their affection for each other in public to the annoyance of many but it last week, they pulled down all pics of each other on their social media accounts.

Mtoto wa miaka nane apata fistula baada ya kubakwa

$
0
0
Na John Walter -Babati

Mtoto wa Darasa la kwanza [jina tunalihifadhi] mwenye umri wa miaka nane (8) mwanafunzi wa shule ya Msingi Maganjwa iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Babati amefanyiwa kitendo cha ubakaji akiwa anaenda mashine kusaga unga wa ugali hali iliyomsababishia maumivu makali na kuwalazimu madaktari kumfanyia upasuaji.

Kwa mujibu wa mwenyekiti wa kijiji cha Maganjwa Petro Shauri alisema majira ya jioni mtoto huyo alitumwa mashineni kusaga mahindi kwa ajili ya chakula cha nyumbani na alipofika  msagaji alimwagiza arudi nyumbani kuchukua hela kwani alifika mashineni hapo akiwa hana hela na pia walikuwa wakidaiwa.

“Wakati akirejea nyumbani kumpa taarifa mama kwamba wanadaiwa ndipo alipokutana na mwanaume huyo na kufanyiwa kitendo hicho cha ubakaji’,.alisema Mwenyekiti

Aliendelea kusema ‘ilipofika usiku mama akastuka mbona mpaka sasa simwoni mwanangu ndipo  aliamua kwenda mashineni kumfuata na alipomuuliza Yule msagaji akamwambia nilishamuagiza muda mrefu aje umpe hela’.mwenyekiti alisimulia

Mwenyekiti alisema Mtuhumiwa alikamatwa usiku huo na kupelekwa katika ofisi ya kijiji hadi asubuhi na kupelekwa  kituo kidogo cha polisi Dareda.

Mama mzazi wa mtoto aliefanyiwa kitendo hicho Maria Domisiana amesema akiwa na majirani wakimtafuta alikumkuta mtoto wake akiwa na matope kichwani na alipomuuliza umepatwa na tatizo gani ndipo alipoanzanza kumsimulia kuwa alikutana   na Salao akamwambia twende tukachukue ndoo ya mama ana alipokataa akamkamata kwa na kmpeleka katika shamba la shule na kuanza kumvua nguo huku akimng’ata na kasha kumbaka huku akiwa amemziba mdomo.

Mganga mfawidhi wa hospitali ya Dareda Josef Lorry amesema kuwa mtoto huyo amepata ugonjwa wa Fistula kati ya sehemu yake ya haja ndogo na kubwa.

Lorry  amesema tukio hilo limemuathiri  mtoto huyo  kisaikolojia lakini pia athari za kihisia na kimaumbile kwa sababu ya kuharibiwa sehemu zake za siri.

Mtoto huyo kwa sasa yupo katika hospitali ya Wilaya, Dareda akiendelea kupata matibabu baada ya kufanyiwa upasuaji wa kumrudishia hali yake ya kawaida


Nandy Amwaga Radhi Jukwaani

$
0
0
KUONESHA mzuka umemkolea, msanii wa Kizazi Kipya zao kutoka Jumba la Kuibua Vipaji Tanzania (THT), Faustina Charles ‘Nandy’ amejikuta akishindwa kuzuia hisia zake mbele ya mashabiki na kulazimika kuvua ‘kuchojoa’ nguo ya juu pamoja na kiatu kimoja.

Ishu nzima ilijiri pande za Nyamongo, Tarime ambapo msanii huyo alikuwa akitumbuiza na baada ya kufika katikati ya shoo alisikika akiwaambia mashabiki wake kwamba avue nguo asivue ndipo akavua na kuwarushia akibakiwa na nguo moja ya ndani.

Baada ya muda tena aliwarushia kiatu mashabiki na kufanya umati uendelee kulipukwa kwa shangwe. Hata hivyo mara baada ya kushuka kwa shoo hiyo, Nandy aliingia katika mtandao wake wa Instagram na kuwashukuru mashabiki hao kwa kuandika; “Juhudi huzidi kipaji, asanteni sana Nyamongo

Saed Kubenea agoma kuhamia CCM, "Yakinishinda naacha Ubunge"

$
0
0

Mbunge wa Jimbo la Ubungo, Saed Kubenea amepinga taarifa zinazoenezwa kuwa anampango wa kuhamia CCM. Mbunge huyo ameongeza kuwa taarifa hizo zinatengenezwa na baadhi ya watu wa Chadema lakini yeye hawezi kuhama kwenye chama hiko anarekebisha mambo ila yakimshinda atasubiria amalizie muda wake wa Ubunge ataachana na kazi hizo na kuendelea na shughuli zake za uandishi wa habari. 

Hizi ndio Sababu za Wanafunzi kufeli

$
0
0

OFISA elimu wa Mkoa wa Shinyanga, Mohamed Kahundi, amesema uongezeko la sifuri katika shule za serikali husababishwa na usimamizi mbovu wa walimu wakuu katika vituo vyao vya kazi sambamba na kujihusisha na vitendo vya kufanya mapenzi baina yao na wanafunzi. 

Tusiposimamia ipasavyo elimu kwa kufuata misingi yake, shule za serikali zitaendelea kupata ziro kila mwaka hata kama tutakuwa na malengo mazuri, na kwamba shule za watu binafsi zitaendelea kutubeba kutokana na kuwa na usimamizi mzuri wa walimu wakuu na kuwahimiza walimu wao kufundisha. 

Kahundi aliyabainisha hayo juzi katika kongamano la kuongeza ufaulu wa jimbo la Ushetu na kutokomeza sifuri katika shule za sekondari, lilijumuisha walimu wakuu wa shule, maofisa elimu kata, walimu wa taaluma, wenyeviti wa kamati za shule pamoja na Mbunge wa jimbu hilo ambae pia ni Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias Kwandikwa. 

Alisema walimu wakuu wengi wamekuwa wakishindana kuvaa suti na kuzurura katika halmashauri badala ya kuwasimamia walimu wao kufundisha na wakati mwingine wamekuwa wakiwagawa walimu, hali ambayo imekuwa ikitengeneza matabaka baina ya walimu na walimu badala ya kufundisha. 

“Kushuka kwa ufaulu wa elimu katika shule zetu za serikali unatokana na usimamizi mbovu wa walimu wakuu sambamba na kujihusisha na vitendo vya 

mapenzi baina yao na wanafunzi, na ikishafikia hatua hiyo wanafunzi hawezi kusoma na badala yake atakwenda kufanya vibaya katika mitihani yake ya mwisho,” alisema. 

Aliongeza: “Mheshimiwa waziri unakuta msimamizi wa kituo anakuwa na makundi ya walimu na hali hiyo ndio inapelekea wale wanaopendwa na mwalimu mkuu kushindwa kuhudhuria vipindi vyao darasani, sasa nawaagiza walimu kuvunja makundi na tunataka kuona ufaulu wa wanafunzi unaongezekana. 

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Ushetu, Michael Matomora, alisema asilimia kubwa ya wananchi wa Ushetu ni wafugaji ambao wamekuwa na maisha ya kuhamahama na hali hiyo imekuwa ikisababisha baadhi ya wanafunzi kukosa masomo kutokana na wazazi wao kuhama na kutafuta malisho ya mifugo yao. 

Waziri Mkuu: Wanaowapa Ujauzito Wanafunzi Kupewa Adhabu Kali

$
0
0

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imeweka sheria kali zinazowalinda  watoto wa kike na watakaobainika kuwapa ujauzito na kukatisha masomo yao adhabu watakayoipata hawatoisahau maisha.


Aliyasema hayo jana (Jumapili, Julai 29, 2018) wakati akizungumza na wakazi wa kata ya Mwakizega wilaya ya Uvinza akiwa katika  ziara yake ya kikazi mkoani Kigoma.


Alisema Serikali itatoa adhabu kali kwa mtu atakayebainika kukatisha elimu ya mtoto wa kike iwe kwa kumuoa au kumpa ujauzo.


Alisema watoto wa kike wanatakiwa kuheshimiwa katika jamii na waachwa waendelee na masomo yao kwani elimu ni haki yao ya msingi.


 “Tukikukuta na mwanafuzni wa kike kwenye kona zisizoeleweka adhabu yake ni kifungo kisichopungua miaka 30 gerezani, hivyo vijana kuweni makini,” alisisitiza.


Pia Waziri Mkuu aliwataka wazazi na walezi kushirikiana na Serikali kuhakikisha watoto wa kike wanapelekwa shule na wanamaliza masomo yao.


Waziri Mkuu aliwaasa wanafunzi wote kusoma kwa bidii ili watimize ndoto zao na wasikubali kushawishika kwa kuwa watashindwa kufikia masomo yao.


IMETOLEWA NA:

OFISI YA WAZIRI MKUU,

JUMATATU, JULAI 30, 2018.

TFDA Yatakiwa Kusajili Jengo La Uzalishaji Chakula Ndani Ya Siku 10.

$
0
0

NA WAMJW- DAR ES SALAAM.

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeitaka Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) kutoa kibali cha kusajili jengo la kuzalisha bidhaa za chakula ndani ya siku kumi.


Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati wa kikao cha wadau kujadili mchango Taasisi za Serikali katika kuanzisha na kuboresha viwanda vya Chakula nchini leo jijini Dar es salaam.


"Naielekza TFDA kutoa kibali cha kusajili jengo la kutengeneza bidhaa za chakula ndani ya siku 10 pamoja na siku 30 za kusajili bidhaa husika ili kuleta chachu ya maendeleo ya viwanda nchini" alisema Waziri Ummy.


Aidha Waziri Ummy ameitaka TFDA kutoa mafunzo kwa wazalishaji wa bidhaa za vyakula kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa elimu ya sayansi juu ya uzalishaji bora wa vyakula na wenye tija kwa wananchi.


Kwa upande wake Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage amewataka TFDA kutopunguza viwango vyao vya ukaguzi wa bidhaa za vyakula ili kuleta sifa na ushindani kwenye soko la kimataifa.


"Nazitaka Taasisi za Serikali ikiwemo TFDA, TBS, MKEMIA MKUU WA SERIKALI na taasisi ya Mionzi kushirikiana katika kudhibiti ubora wa bidhaa nchini na kupunguza vikwazo kwa wawekezaji wa viwanda vya chakula nchini" alisema Waziri Mwijage.


Aidha Waziri Mwijage amewataka wajasiliamali wasibweteke katika kutengeneza bidhaa zinazokidhi viwango kwa mahitaji na zenye kulinda afya za watanzania.


Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA Bi. Agness Sitta Kijo amesema kuwa wamejidhatiti kuhakikisha hawatokuwa vikwazo kwa wawekezaji katika sekta ya uwekezaji kwenye viwanda vya chakula nchini.


Kwa upande Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania Dkt. Edward Sembeye ameipongeza TFDA kwa kupunguza malalamiko na vikwazo vingi kwa wajasiliamali na wawekezaji wadogo wa vyakula hapa nchini.


MWISHO.
Viewing all 104670 articles
Browse latest View live




Latest Images