Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Pacha walioungana tumbo Jijini Mwanza Wafariki Dunia

$
0
0

Watoto pacha walioungana tumboni na kifuani waliolazwa katika chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando jijini Mwanza wamefariki dunia leo Agosti Mosi.


Mkurugenzi wa Hospitali hiyo, Abel Makubi amesema watoto hao wamefariki kwa tatizo la upumuaji.


Pacha hao walizaliwa Julai 25 katika Hospitali ya Sekotoure na baadaye wakapelekwa Hospitali ya Bugando, walikolazwa ICU.


Akizungumzia hali za pacha hao wiki iliyopita Dk Makubi alisema watoto hao Angelina Ramadhani (34) mkazi wa Nyakato jijini Mwanza, wameungana sehemu ya kifua na tumbo.


 “Baada ya jopo la madaktari kuwafanyia uchunguzi, limebaini kwamba wanachangia moyo mmoja, mshipa mmoja unaorudisha damu kwenye moyo (inferior venacava), ini moja na kwamba viungo vilivyobaki kama mapafu, figo, tumbo kila mtoto ana vyake.”amesema Dk Makubi.

Ukiwa na Mpenzi Mwenye Haiba hii, Kujenga Uhusiano Imara ni Mashaka

$
0
0
Wataalamu wa tabia na mienendo ya binadamu wanasema, kuna Makundi kadhaa ya haiba. Wana maana kwamba, binadamu wamegawanyika katika Makundi kitabia.

Je, wewe uko kwenye kundi lipi?

Hiki ndicho ninachotaka kuwasaidia siku ya leo.

Lakini leo ningependa kuwazungumzia watu wenye haiba ya ukamilifu. Hawa ni wale watu ambao wanaamini kwamba, hawapaswi kukosea. Kwao, wanaamini kuwa, mtu anatakiwa afanye kwa usahihi na ukamilifu na kukosea kuna maaana ya udhaifu mkubwa na unyonge.

Nguvu kubwa ya watu hawa iko kwenye usahihi, ukamilifu na kurekebisha makosa. Iko kwenye kufanya ambavyo mtu angetakiwa kufanya, na kufanya mambo kwa usahihi.

Watu hawa wenye haiba ya usahihi huko ndani mwao kuna sauti (little voices) ambazo zina nguvu sana kwao, zenye kuwaamuru wafanye mambo bila kukosea. Lakini, sauti hizi zinakosoa na kuwadhibiti wahusika kwa njia yenye kuwaumiza. Huwa ni sauti zenye kuzalisha mashaka. Kushtakiwa na dhamira na hofu.

Kwa sababu ni watu wanaoamini katika “nzuri na sahihi,” inakuwa ni vigumu sana kwao kuishi na watu wengine kwa amani. Mbaya zaidi ni kwamba, wapenzi wao hupata shida sana kuendana nao. Hii ni kwa sababu, wanataka mambo yaende kwa njia yao, yawe sahihi. Kuna, “ingetakiwa iwe hivi,” nyingi sana.

Watu hawa huwafanya wengine wanaohusiana nao kuhisi kama vile wanatembea juu ya maganda ya mayai.

Kwa nini?

Ni kwa sababu hawa watu wenye haiba hii, hujiona wanaweza kuliko wengine na wanastahili kuliko wengine. Watu hawa wana tabia ya kusema au kumwambia mtu ukweli moja kwa moja kwa njia yenye kukera sana. Hali hii huwasononesha watu wanaoambiwa ukweli.

Watu ambao wameoa au kuolewa na wenye haiba hii, huwa wanatamani kuona mambo yakiwa tofauti kidogo. Wanajihisi kufungwa pumzi, kukaliwa kooni, kufungiwa kwenye dema na kushindwa kuona nafasi yao kama watu huru. Huhisi kuwa wao ni watoto, wanaokosea kila kitu, kwani ndivyo sauti za wapenzi wao zinavyowaambia kila wakati.

Inabidi mtu wa haiba hii ajifunze kukubali makosa, kwamba, kukosea siyo udhaifu, bali kujifunza. Ajue kwamba, kuna njia nyingi za kujifunza mambo, siyo njia moja tu ya “usahihi.” Kuna ya kukosea na kujifunza makosa, halafu ndiyo usahihi ufuate

Nataka Kupenda Kama Mjinga, Nizame Nipotee! Kama limbwata ni Kweli Lipo Basi Nilishwe Hata Hilo

$
0
0
It may sound strange but this has been my major wish for a while,

Nataka kupenda kama mjinga, yaani niwe zombiee, nizame mapenzini nipotelee huko. Kila nachoambiwa nione sawa niwe mjinga mjinga no reasoning.

Yale mapenzi usipowasiliana ama kumwona mtu wako for a day unajisikia mgonjwa, mapenzi ambayo unaongea na mtu wako for two or three hrs and you feel like its just 5 minutes na haujui mlikuwa mnaongea nini.

Yaani mapenzi ambapo nikiachwa au nililazimika kuacha basi nichanganyikiwe, nishindwe kula, nikose usingizi, nipungue uzito, nione kama dunia imekwisha shughuli zangu nishindwe kufanya, kichwa kigome kufukiri

Kama limbwata ni kweli lipo basi nilishwe hata hilo, haya mapenzi ya kupenda robo robo with a lot of reasoning sio nayotaka.

Natamani kupenda with all my heart, soul, mind, body and my everything, nataka kupenda kamili kamili, kwa kila kitu, mpenzi wangu awe kila kitu, awe ndio dunia na maisha yangu.

Trust me I want to love like nothing else,

Hivi ni mimi tu?

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Alhamisi ya Agosti 2

$
0
0

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Alhamisi ya Agosti 2

Tunatibu Na Kuponesha Kabisa Upugufu wa Nguvu za Kiume, Busha, Kisukari na Vidonda vya Tumbo

$
0
0
TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO? BUSHA BILA KUPASUA KISUKALI NA VIDONDA VYA TUMBO? asilimia kubwa ya wanaume wanaupungufu wa nguvu za kiume NA maumbile madogo

NI NINI KINACHOSABABISHA UUME KUZIDI KUWA MDOGO NA WEMBAMBA 1 kuugua chango LA uzazi 2 unene kupita kiasi 3 kuvaa nguo au chupi za kubana 4 kupiga punyeto kwa mda mrfu ,NI NINI TIBA YAKE MAKAKANUA MIX nidawa ya mitishamba iliyochanganywa NA mizizi kumi NA mbili urfusha NA kunenepesha UUME saizi upendayo ich 5,6,7, NA 8 kwa urfu NA sentimita 3,4, na 5 ipo dawa ya kunywa na kupaka NI NINI KINASABABISHA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME 1 kupungukiwa kwa homoni ya testerone 2 kuhudhurika kwa Neva au uti wa mgongo 3 utumiaji holela wa madawa ya kizungu 4 usongo wa mawazo na asira 5 utumiaji wa vyakula vya mafuta mengi NI NINI TIBA YAKE MAPRO POWER NO 2 NDIO tiba tosha kwa sasa kwani utibu matatizo matatu kwa pamoja 1 itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15 adi 20 ,2 itakufanya urudie tendo zaidi Mara tatu 3 uhimalisha uume uliolegea na kusinyaa OKOA NDOA YAKO SASA ujihepusha na lawama ndani ya ndoa yako au pale ukutanapo na mpezi dawa hii itamfanya mpenzi wako hakueshimu na hasitoke nnje ya ndoa na ata wazee wenye umri mkubwa wanapona zipo dawa za kupunguza kitambi,minyama uzembe, presha ,kisukar mvuto wa mpezi au biashara FIKA OFISINI KWETU MBAGALA ZAKHEMU na wateja wa kanda ya ziwa yupo wakala wetu mwanza mjini au piga simu 0752348593

DR MABULA na utaletewa popote ulipo uduma hizi

ACT WAZALENDO: Lazima ‘Tumnyooshe’ Kangi Lugola (+video)

$
0
0
Tazama LIVE Chama cha ACT Wazalendo wanatoa tamko kuhusu agizo la Waziri wa Mambo ya Ndani Kangi Lugola alilotoa kwa Zitto Kabwe la kujisalimisha kwa RPC Lindi…Bonyeza PLAY hapa chini kutazama

VIDEO:

Seven Kazungumza UKWELI Kuhusu Ugonjwa wa Ommy Dimpoz (Video)

$
0
0
Meneja wa Alikiba, Seven Mosha amezungumza kuhusu kile kinachomsumbua muimbaji Ommy Dimpoz ikiwa hivi karibuni ziliripotiwa taarifa za kuumwa kwa msanii huyo ambaye yupo nje ya nchi ambako ndipo alipofanyiwa matibabu.

Msikilize Seven akifunguka Ukweli kuhusu ugonjwa huo

Mmoja Atiwa Mbaroni Kwa Kujifanya Katekwa na Wasiojulikana

$
0
0
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza linamshikilia mtu mmoja, aliyejulikana kwa jina la Prosper Lema, aliyedai kutekwa na watu wasiojulikana na kuanza kutumia uongo kuomba fedha kwa ndugu zake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi, amesema, taarifa hizo za Bw. Lema zilipatikana baada ya ndugu zake mtuhumiwa huyo kwenda katika kituo cha polisi kirumba jijini humo kutoa taarifa ya ndugu yao kutekwa na watu wasiojulikana Julai 18, mwaka huu baada ya kuwatumia ujumbe akiomba fedha.

Kamanda Msangi amesema kwamba mtuhumiwa Lema aliomba fedha zaidi ya shilingi milioni tano kwa familia yake kwa kutuma ujumbe kwenye simu ili aweze kuachiwa huru na watu waliomteka.

Aidha ameongeza kwamba mtuhumiwa Lema atafikishwa Mahakamani pindi uchunguzi wa tukio hilo utakapokamilika.

Mbali na hayo, Kamanda Msangi amewatahadharisha wananchi kuwa makini na kutoa taarifa kwa vyombo vya dola pindi wanapobaini kuwepo kwa dalili zinazofanana na hizo.

Taarifa kwa Umma Kuhusu Kujiuzulu kwa Mbunge Julius Kalanga Laizer

$
0
0
Taarifa kwa Umma Kuhusu Kujiuzulu kwa Mbunge Julius Kalanga Laizer

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume, nasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za:

GUMBA POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.

NTINJE:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0754741788, 0715741788, 0783741788

-DR MAGISE

Uingereza Nayo Yaomba Kuandaa Kombe la Dunia 2030

$
0
0
Uingereza Nayo  Yaomba Kuandaa Kombe la Dunia 2030
Shirikisho la kandanda nchini Uingereza, FA lipo katika mipango ya kuomba nafasi ya kuandaa michuano ya kombe la dunia mwaka 2030.

 Kupitia kwa mwenyekiti wa chama hicho, Creg Clarke ambaye amethibitisha kuwa bodi ya chama hicho imefikia makubaliano ya kuanza kazi hiyo kuona kama itawezekana.

"Kazi hiyo itaanza rasmi katika msimu huu mpya na kwamba hakuna maamuzi yoyote yatakayofanyika hadi mwaka 2019". Ameongeza mwenyekiti huyo.

Michuano ya mwisho mikubwa ya soka kufanyika nchini Uingereza ni ya mwaka 1996 ambayo ni michuano ya mataifa ya ulaya, bingwa wa michuano hiyo akiwa ni Ujerumani baada ya kuifunga jamhuri ya Czech.

Ilishindwa kupata nafasi ya kuandaa michuano ya kombe la dunia ya mwaka 2018 iliyomalizika nchini Urusi, ambapo sasa ina imani kubwa ya kufanikisha azma hiyo kutokana na uwazi wa zoezi la upigaji kura lililofanyika hivi karibuni ambalo lilizipa tiketi nchi za Marekani, Mexico na Canada kwa pamoja kuandaa michuano ya mwaka 2026.

Nchi hyo pia inatarajia kupata upinzani kutoka kwa mataifa ya Argentina, Uruguay na Paraguay ambayo yanapanga kuomba nafasi ya kuandaa michuano hiyo kwaajili ya kuadhimisha miaka 100 tangu kuanzishwa kwake mwaka 1930.

Uingereza ina historia ya kushinda kombe la dunia mara moja mwaka 1966, michuano iliyofanyika katika ardhi ya nyumbani ambapo ilishinda kwa penalti 4-2 dhidi ya Ujerumani magharibi ambayo baadaye iliungana na Ujerumani mashariki na kuwa nchi moja.

Wasiojulikana Wamponza Lema, Atiwa Mbaroni

$
0
0
Wasiojulikana Wamponza Lema, Atiwa Mbaroni
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza linamshikilia mtu mmoja, aliyejulikana kwa jina la Prosper Lema, aliyedai kutekwa na watu wasiojulikana na kuanza kutumia uongo kuomba fedha kwa ndugu zake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi, amesema, taarifa hizo za Bw. Lema zilipatikana baada ya ndugu zake mtuhumiwa huyo kwenda katika kituo cha polisi kirumba jijini humo kutoa taarifa ya ndugu yao kutekwa na watu wasiojulikana Julai 18, mwaka huu baada ya kuwatumia ujumbe akiomba fedha.

Kamanda Msangi amesema kwamba mtuhumiwa Lema aliomba fedha zaidi ya shilingi milioni tano kwa familia yake kwa kutuma ujumbe kwenye simu ili aweze kuachiwa huru na watu waliomteka.

Aidha ameongeza kwamba mtuhumiwa Lema atafikishwa Mahakamani pindi uchunguzi wa tukio hilo utakapokamilika.

Mbali na hayo, Kamanda Msangi amewatahadharisha wananchi kuwa makini na kutoa taarifa kwa vyombo vya dola pindi wanapobaini kuwepo kwa dalili zinazofanana na hizo.

Dar Kuna Upigaji Tena wa Nguvu Lakini Viongozi Wapo tu! – Rais Magufuli

$
0
0
Dar Kuna Upigaji Tena wa Nguvu Lakini Viongozi Wapo tu! – Rais Magufuli
Rais John Magufuli ametumia hafla ya kuapishwa kwa wakuu wa mikoa, manaibu katibu wakuu na makatibu tawala wa mikoa kukumbusha majukumu yao katika maeneo ya utendaji ambapo amedai mkoa wa Dar es salaam umeshindwa kufikia malengo kwenye ukusanyaji wa mapato.

Rais ameusifu mkoa wa Dodoma kwa kuongoza kwa ukusanyaji mapato, ikiwa ni siku chache baada ya kupandishwa hadhi na kuwa jiji.

“Dodoma inaogoza kwa makusanyo mengi, Sh24.5 bilioni. Sasa unaweza kujiuliza, Dodoma kuna nini?” alisema Rais.

“Yule mkuu wa mkoa wa Dodoma, RAS (katibu tawala), mstahiki meya na wananchi wa Dodoma wana genes za namna gani ukilinganisha na Dar es Salaam ambayo ina population (idadi) ya watu 5.5 milioni?”

Alisema mkoa wa Dar es Salaam uliwekewa malengo ya kukusanya Sh12 bilioni lakini hauklufikisha.

“Sasa unaweza ukajua kwamba hapa Dar es Salaam kuna upigaji tena wa nguvu. Lakini viongozi wapo.”

Pia alisema hata wilaya ya Kinondoni ambaye aliyekuwa akiiongoza, Ali Hapi amempandisha cheo na kuwa mkuu wa mkoa, ilikuwa ya mwisho.

“Sasa nikawa najiuliza sijui nimtumbue hapa hapa au,” alisema Rais Magufuli huku akikuna kichwa.

“Kweli wala sifichi, nikasema wilaya ilikuwa ya upinzani ile. Lakini hivi vitu vinatia aibu.”

Huku akizungumzia majiji mengine, alikosoa pia jiji la Mbeya akisema limeshika nafasi ya mwisho kati ya majiji sita nchini.

“Yaani jiji nililotangaza miezi miwili mitatu iliyopita ndio linaongoza! Nimejiuliza sana, labda tuweke mikakati ya kufanya; jiji linaloshindwa kukusanya linashushwa chini. Utaitwaje jiji wakati hata hujui kukusanya?” alihoji.

Alizitaja pia halmashauri za Mbulu na Mbinga akisema zimekuwa za mwisho katika ukusanyaji wa mapato, huku akiwataka wakuu wa mikoa kusimamia kazi hiyo.

“Wakuu wa mikoa ni kila kitu, hakuna mahali popote panaweza kukukwamisha. You are everything,” alisema.

“Sasa mimi huku Rais ninakazania mapato huku, wewe rais wa mkoa ule unashindwa kusimamia mapato, kwa nini nisijiulize kwamba hufai?

“Survival ya nchi hii ni mapato, fedha zinazokusanywa ziende kwenye miradi ya maendeleo ili nchi iende mbele. Hapa Dar es Salaam, wala siyo siri, wakikutana kwenye vikao, madiwani kama wamekaa siku moja wanalipana siku nne. Kila mmoja anajua. Wakikutana siku mbili zitakazojazwa pale ni siku nne. PCCB wapo. Unategemea utapata hela gani kwa maendeleo?”

Alisema kutokana na hali hiyo kero za wananchi wakiwemo wafanyabiashara ndogo hukosa nafasi za kufanya biashara licha ya kuwepo kwa viongozi.

Uchaguzi Zimbabwe: Jamii ya Kimataifa Yatoa Wito kwa Zimbabwe Kukomesha Ghasia

$
0
0
Uchaguzi Zimbabwe: Jamii ya Kimataifa Yatoa Wito kwa Zimbabwe Kukomesha Ghasia
Matumizi ya nguvu ya serikali dhidi ya upinzani nchini Zibabwe baada ya uchaguzi wa Jumatatu yameichochea jamii ya kimataifa kutoa wito wa kumaliza vurugu.

Umoja wa mataifa na umoja wa ulaya kwa pamoja wamekemea juu vurugu zilizotokea na polisi kufyatua risasi kwa waandamanaji.

Makundi ya waandamanaji yalikuwa katikati ya mji huo tangu alfajiri lakini habari zilipozuka kwamba Zanu PF imeshinda viti vingi katika bunge na kwamba matokeo ya urais hayakuwa tayari , hali ilibadilika.

Uchaguzi wa Jumatatu ulivutia asilimia 70 ya wapiga kura. Chombo cha habari cha ZBC kimesema kuwa Zec itatangaza matokeo ya uchaguzi wa urais mwendo wa 12.30 za Zimbabwe.

Tume ya uchaguzi nchini Zimbabwe inasema asilimia 70 ya wazimbabwe walijiandikisha kupiga kura
.Katibu mkuu wa umoja wa mataifa amesema kuwa serikali ya Zimbabwe inatakiwa kuhkikisha kuwa vurugu hizo hazitokei.

Wakati huo huo shirika la kutetea haki za binaadamu la Amnesty International linaitaka serikali kufungua mashataka kwa polisi waliofyatua risasi kwa waandamanaji.

''vikosi vya usalama vinapoingilia uchaguzi ni kuwanyima haki wananchi ya kujieleza'' amesema katibu wa Amnesty.

Tume ya uchaguzi ya Zimbabwe(Zec) hadi sasa imetangaza ushindi wa viti 140 kwa chama tawala cha Zanu-PF, huku kile cha Muungano wa Upinzani MDC kikiwa na viti 58 , Kulingana na taarifa ya Shirika la Utangazaji la taifa ZBC . Kuna viti 210 Katika Bunge la Taifa la taifa.

Zaidi ya watu milioni tano walijiandikisha kupiga kura, na watu wengi walijitokeza kushiriki uchaguzi kwa kiwango cha 70%.

"Hakuna Mwenye Uhakika na Cheo Chake"- Magufuli

$
0
0
"Hakuna mwenye uhakika na cheo chake"- Magufuli
Rais Dkt. John Magufuli amesema hakuna mwenye uhakika wa cheo katika serikali ya awamu ya tano kwani hata yeye mwenye hana uhakika kama atakuwa Rais wa muda wote na kuwataka viongozi kushughulika na matatizo ya wananchi mapema na sio kumsubiri yeye kuyatatua.

 Dkt. Magufuli amesema hayo jana Agosti Mosi, 2018 wakati akihutubia mara baada ya kuwaapisha wakuu wa mikoa, makatibu tawala, makatibu wakuu na manaibu katibu wakuu hafla iliyofanyikia Ikulu Jijini Dar es Salaam.

"Hizi kazi sisi sote tumepewa dhamana. Mimi mwenyewe pia nimepewa dhamana, hakuna mwenye uhakika na kazi hizi hata mimi sina uhakika na kazi hizi kwamba nitakuwa Rais wa moja kwa moja. Hii ni kazi ngumu, Hii ni kazi ni ngumu, its terrible job. Leo tu mimi nimeamka saa nane usiku usiku mara IGP ananipigia simu anasema kuna watu wetu wamepata ajali mpakani, kuna mwingine anasema hivi....

Basi na nyinyi mteseke kama mimi ninavyoteseka, ili kusudi tuwasaidie hawa tunaowaongoza. Machozi yao tutakuja kuyalipa hilo hakuna njia ya kukwepa, kama mabaya yamefanyika katika Mkoa wako au wilaya yako. Wewe RC au DC lazima malipo yako utayapata", amesema Rais Magufuli.

Mbali na hilo, Rais Magufuli ameonesha wazi kabisa kuchukuziwa na kitendo cha jiji la Dar es Salaam kushika nafasi ya mwisho katika ukusanyaji wa mapato katika majiji sita.

"Nchi hii ya Tanzania imebarikiwa sana, ina kila kitu. Dodoma ndio inaongoza katika Majiji, Halmashauri, Manispaa n.k Tanzania nzima katika kukusanya fedha nyingi takribani bilioni 24.5. Nashindwa kuelewa ni kwanini jiji la Dar es Salaam lenye wingi wa watu takribani milioni 5.5, linashindwa kufikia malengo yaliyokuwa bilioni 12..Ambapo imeizidi Dodoma kwa 'population'. Sasa unaweza kujua kwamba hapa Dar es Salaam kuna upigaji tena wa nguvu lakini viongozi wapo tu", amesisitiza Rais Magufuli.

Kwa upande mwingine, Rais Magufuli amesema kwa jinsi hali inavyoendelea wataweka mikakati ya kushusha hadhi ya majiji ambayo yatakuwa yanashindwa kufikisha malengo yake ya kimapato yaliyowekwa.

Ebola Yasambaa Upya DRC

$
0
0
Ebola Yasambaa Upya DRC
Serikali ya Jamhuri ya Demokrasia ya Congo imetangaza kusambaa kwa ugonjwa wa Ebola katika maeneo mapya.

Hali ya wasiwasi imetanda katika maeneo mengi ya mashariki mwa Congo,baada y'a wizara ya afya kutangaza kugundulika kwa ugonjwa wa Ebola katika maeneo ya Beni mashariki mwa nchi hio. Serekali ya Kongo imetangaza hayo wiki moja tu baada ya shirika la afya duniani WHO na mamlaka za DRC kutangaza mafanikio na mwisho wa janga hilo la Ebola katika jimbo la Ecuador.

Wizara ya afya ya Nchini Kongo imetoa taarifa kwa shirika la afya duniani WHO kuwa, vipimo 4 kati ya 6, vimekutwa na virusi vya ugonjwa huko Kinshasa, bado vipimo vingine vinaendelea.


Maambukizi makubwa yameonekana katika eneo la Mangina ambapo ni kilomita 30 tu kutoka mji wa Beni.
Mkurugenzi wa WHO Dr Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema kuwa, ebola ni tishio kubwa nchini DRC, lakini uwazi na ukweli wa serikali ya Kongo katika kutoa taarifa za ugonjwa huo, ndio njia ya kwanza ya kuweza kufanikisha mapambano ya kumaliza Ebola DRC.

Mkurugenzi wa WHO kwa upande wa Afrika amesema ni rahisi kuanza mara moja jitihada za kuzuia Ebola kwasababu wametoka kupambana na tatizo hilo hilo, hivyo vifaa na wafanyakazi wako tayari.

Maambukizi makubwa yameonekana katika eneo la Mangina ambapo ni kilomita 30 tu kutoka mji wa Beni.

Nina wivu kwa mume wangu akitoka bila mimi lakini…- Mke wa Babu Tale

$
0
0
Nina wivu kwa mume wangu akitoka bila mimi lakini…- Mke wa Babu Tale
Wiki weekend iliyopita kwa mara ya kwanza meneja wa Diamond Babu Tale alitoka na mama watoto wake na kwenda kwenye arobaini ya mtoto wa Zamaradi iliyofanyika huko Bunju B.



Bongo5 ilifanya mahojiano na mke wa Babu Tale na kumuuliza anajisikiaje pale anapomuona mume wake akipiga picha na warembo mbalimbali wakati akiwa kwenye shughuli zake za kikazi.

“Wivu upo lakini unategemea upo kwa kiwango gani na wivu ukiuendekeza mtakwama,” alisema mama watoto huyo wa Tale.


Kwa upande wa Babu Tale alidai kwa kuwa yupo kwenye tasnia ya burudani kwa muda mrefu amejifunza hawezi tembea na mke wake kila sehemu.

“Leo sijaja kazini nimekuja kwenye shughuli ndio maana unaona niko na mke wangu,” alisema Babu Tale.

Related Articles

Picha ya Gadner na Mwanae Yazua Gumzo Mitandaoni

$
0
0

Picha ya Gadner na Mwanae Yazua Gumzo Mitandaoni
Kuna picha  aliweka Gadner akiwa amerepost kutoka katika akaunti ya binti yake Karen ikiwa inaonyesha akiwa amemkumbatia mtoto wake  huku wakiwa wamelala kwenye kochi, na kwa jinsi wao walivyochukulia ilikuwa ni kama mapenzi ya baba na mtoto.

Lakini baada ya picha hiyo kwenda katika mitandao ya kijamii ilileta gumzo na kusemewa maneno mengi sana huku wadau na baadhi ya mashabiki wakisema kuwa hayo sio maadili ya kitanzania hasa kwa baba na binti yake.

Huku wengine wakimtuhumu sana gadner na kusema kuwa hawamuamini sana kutokana na ukweli kwamba amekuwa akitoka kimapezni na wasichana wenye umri kama wa binti yake , hivyo hiyo inaleta picha mbaya kwa mashabiki wanaomuona akiwa anafanya hivyo.

Polisi Yashindwa Kumkamata Zitto Kabwe Yamfungulia Kufungua Jalada la Uchunguzi

$
0
0
Polisi Yashindwa Kumkamata Zitto Kabwe Yamfungulia Kufungua Jalada la Uchunguzi
Jeshi la Polisi limefungua jalada la uchunguzi dhidi ya kauli zilizotolewa na mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe.

Akizungumza leo Jumatano Agosti Mosi, 2018 msemaji wa polisi, Barnabas Mwakalukwa amesema kwa sasa uchunguzi unafanyika kuhusiana na tuhuma zinazomkabili mbunge huyo ambaye pia ni kiongozi wa ACT.

Mwakalukwa ameeleza hayo ikiwa imepita siku moja tangu Waziri wa Mambo ya Ndani,  Kangi Lugola kumtaka kiongozi huyo kujisalimisha polisi  kwa maelezo kuwa ametoa kauli za uchochezi.

Lugola amesema Zitto ametoa kauli za uchochezi na kuwatukana viongozi wa Serikali wakati akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika jimbo la Kilwa Kusini, mkoani Lindi.

Katika mkutano huo Zitto alialikwa na mbunge wa jimbo hilo, Seleman Bungara maarufu Bwege.

Mwakalukwa amesema kufuatia agizo hilo la Lugola tayari wamefungua jadala kuchunguza jambo hilo, kwamba uchunguzi ukikamilika na iwapo itaonekana mbunge huyo anahitajika, watamuita polisi.

Amesema polisi wanafanya kazi kwa mujibu wa taratibu na sheria, kwamba Zitto akihitajika ataripoti kwa kamanda wa polisi mkoani Lindi.

Jana, Zitto alijibu kauli ya Lugola ya kumtaka aripoti polisi akibainisha kuwa atakwenda ikiwa atapewa wito wa kisheria.

Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter Zitto amesema, “waziri hana hayo mamlaka. Kama polisi wananitaka watoe wito wa kisheria nitakwenda.”

“Naendelea na kampeni za ubunge wa Buyungu ambapo tunamuunga mgombea wa Chadema na madiwani wa ACT- Wazalendo kwenye kata kadhaa. Nashauri waziri ampate kwanza yule mbwa wa polisi bandari.“

Nafasi za Ajira zilizotangazwa Leo

Viewing all 104709 articles
Browse latest View live


Latest Images