Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live

Mchezaji Abdi Banda Aliyemuoa Dada wa Ali Kiba Awa Lulu Huko South Afrika

$
0
0
Kupitia jarida maarufu la habari ncini Afrika Kusini Soccerladuma limeripoti kuwa mlinzi mahiri wa klabu ya Baroka Fc Abdi Banda a.k.a Abdi “Van Djik” anawindwa na mabingwa wa msimu na mabingwa mara 8 wa ligi kuu Afrika kusini Mamelodi Sundowns.

Mabingwa Mamelodi Sundowns wapo katika harakati za kuimarisha kikosi chao baada ya kutwaa ubingwa msimu uliopita.



Taarifa kutoka Siya , Masandawana zinadai kuwa Abdi Banda anahitajika na klabu hiyo baada ya kufanya vyema na klabu yake licha ya matokeo ya kusuasua ya klabu hiyo ya msimu uliopita waliomaliza nafasi ya 2 kutoka mkiani wakiwa wameruhusu mabao 38.

Baroka FC watotto hawa wanaotumia uwanja wa Old Peter Mokaba huu ni msimu wao watatu kwenye ligi hiyo.

Hata hivyo huenda dili hili likawekwa kwenye wakati mgumu kutokana na klabu hiyo kuhitaji huduma za mlinzi huyo.



Morgan Mammila ambaye ni mkurugenzi wa klabu hiyo alisema kuwa klabu uake haitaruhussu mchezaji yeyote kuondoka na watapambana kumaliza nafasi nane za juu msimu ujao.

“Malengo yetu ni kucheza vyema na kuhakikisha hatutaruhusu mchezaji yeyote kuondoka. Tunahitaji kwanza kujua ni kivipi tutafuzu MTN8. Hivyo nafasi 8 za juu ni lengo letu kubwa.”

Msimu wa kwanza Baroka kumaliza nafasi 2 za mwisho kabla ya kushinda mchezo wa mtoano kwenye mchezo wa kuamua timu ya kushuka daraja.



Msimu uliopita walitawala mechi za awali kabla ya kuporomoka mpaka nafasi ya 14.

Mshambuliaji hatari wa zamani wa Kaizer Chief, Wedson Nyirenda ametwaa mikoba ya kuinoa klabu hiyo.


Banda alicheza michezo 28 kwa klabu hiyo. Kiwango chake ndani ya klabu yake, pamoja na kuitwa kwake timu ya taifa mara kwa mara kumefanya aanze kuwindwa na timu mbalimbi.



Kocha mkuu wa Mamelodi Pitso Mosimane anafahamu uwezo wa Banda vyema. Banda ndiye mchezaji bora ea Baroka msimu uliopita bila shaka. Baroka wana haki ya kumzuia lakini Mosimane pia anaweza kumshawishi Banda na kupata huduma zake. Kadi yake ya kwanza alipata dakika ya 59′ baada ya kunawa mpira kwenye mchezo dhidi yao na Kaizer Chiefs 1-0 Baroka FC ambapo katika mchezo pia alifunga bao lililoipatia Baroka sare.



Abdi Banda umri wake unamruhusu kwani amefikisha miaka 23 kwa mujibu wa transfermarket.com. inaonesha alizaliwa tarehe 20 mwezi Aprili 1993. Abdi Banda yupo chini ya wakala wa Siyavumi.

Hata hivyo klabu yao msimu imefanya usajili wa kutosha. Elvis Chipezeze, Tshediso Patjie, Bheki Maliba, Thabo Moseki, Bonginkosi Makume,Siseko Manana, Armand Gnanuillet, Ananias Gebhardt, Shabani Hussein, Shabani Hussein na Orebotse Mongae.



Klabu hiyo ya Baroka pia imekuwa unataratibu wa kutoa Mamiss. Shindano lao linajulikana kama Miss Baroka ili kuvutia zaidi mashabiki na kufanya uwekezaji. Simba na Yanga Vipi kuna uwezekano wa Miss kariakoo Derby???😀

Hata hivyo Abdi Banda alipewa tuzo ya kuwa mchezaji bora wa mwezi mei mwaka huu wa klabu ya Baroka

Bibi Amchoma Moto Mjukuu Wake wa Miaka Sita Mbeya

$
0
0
Bibi Amchoma Moto Mjukuu Wake wa Miaka Sita Mbeya
Jeshi la Polisi mkoani Mbeya linawashikilia watu wawili Judith Amoni Mwansansu(39) ambaye ni bibi wa mtoto na Aive Alex Swalo(17) shangazi yake, kwa kosa la kumfanyia vitendo vya ukatili mtoto, Daines Kefas Mwansasu(06) vya kumuunguza kwa moto na kumpiga.



Kamanda wa Polisi jijini humo, SACP Ulrich Matei, amesema tukio hilo lilifanyika Jumanne July 31, 2018 majira ya saa tatu usiku ambapo siku iliyofuata Jeshi la Polisi lilipokea taarifa za tukio hilo kutoka kwa raia wema kwamba mtoto huyo amejeruhiwa sehemu mbalimbali kwa moto.

“Inadaiwa siku hiyo ya Jumanne, Daines alikuwa ameenda kucheza na rafiki zake na aliporudi nyumbani majira ya jioni shangazi yake alimuadhibu kwa kumchapa na waya wa umeme sehemu mbalimbali za mwili wake na kumsababishia majeraha na maumivu makali mwilini”, amesema Kamanda Matei.

Kamanda Matei ameongeza kuwa  August 1, 2018 majira ya asubuhi, watuhumiwa (Shangazi akishirikiana na bibi wa mtoto) waliendelea kumfanyia vitendo vya ukatili mtoto huyo kwa kumuunguza kwa moto sehemu za miguuni na kwenye makalio.

Juni 16, 2018 katika kilele cha siku ya Mtoto wa Afrika, ambayo kitaifa ilifanyika mkoani Arusha na Tanzania ikitajwa kuongoza katika vitendo vya ukatili dhidi ya watoto kuliko uovu unaofanywa kwenye ujambazi, takwimu zilizowasilishwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto , Dk. Faustine Ndugulile, zinaeleza kuwa watoto 41,000 walifanyiwa ukatili kati yao 3,467 kwa kipindi cha Januari hadi Desemba mwaka jana.

Lakini pia, Idara ya Ustawi wa Jamii wizarani hapo, ilieleza kuwa asilimia 60 ya ukatili dhidi ya watoto unafanyika nyumbani, asilimia 53 ni shuleni na iliyobaki ni maeneo mengine.

Takwimu zinaonesha watanzania wengi hawajaweza kumlinda mtoto kwa mujibu wa sheria ya mtoto ya mwaka 2009, ambayo imetoa wajibu kwa kila mtu na adhabu kwa anayeshindwa kutekeleza jukumu hilo.

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

$
0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

Najiona Mwenye Bahati Sana Maana Haya Maisha Ninayoishi Sijawahi Kuyaota- Harmonize

$
0
0
Najiona Mwenye Bahati Sana Maana Haya Maisha Ninayoishi Sijawahi Kuyaota- Harmonize
Msanii wa muziki nchini Tanzania, Harmonize amedai kuwa katika maisha yake hajawahi kufikiria kuishi maisha yenye mafanikio makubwa kama anayoyaishi kwa sasa.

Harmonize amesema kuwa miaka mitano iliyopita alikuwa mtu wa kawaida na alikuwa akifanya biashara ndogo ndogo maarufu kama Machinga Kariakoo jijini Dar es salaam lakini kwa sasa amepiga hatua kubwa kimafanikio kwenye muziki.

“Miaka (5) iliyopita nilikuwa nafanya biashara za kudunduliza maeneo haya ya #Kariakoo kwa lugha nyengine nilikuwa #Machinga shida, tabu, shuruba, nilizokuwa nikizipitia , M/mungu peke ndie anayefahamu..!! Hata wimbo wangu wa #Matatizo 90% umebeba uhalisia wa maisha yangu sana. Sina utajiri wowote ila afadhali niliyoipata najihisi ni mwenye bahati  Sana.“ameandika Harmonize kwenye ukurasa wake wa Instagram baada ya kutembelea marafiki zake wa miaka ya nyuma katika mitaa ya Kariakoo.

“Maana maisha ninayoishi sikuwahi hata kuyaota, Nimshukuru M/mungu kwa kunipa Nafasi hii ya kukumbuka Ndugu zangu ambao nimewaacha katika, Eneo hili na kupata nafasi ya kuzungumza nao mawili ,matatu Ya kuwapa Moyo, faraja, Mungu anawaona na Maombi yangu yapo kwenu sitochoka Kuwa nanyi siku zote…!!! Na kidogo Au kingi changu kiwafikie kama fadhila ambazo ni ngumu Kuwafikia watu wote..!!! Ila nyie Mliobahatika kwa leo mkawe wawakilishi wa wengine M/mungu awabariki sana…!!! Ndugu zangu Changamoto, pandashuka, majaribu, zifanye kuwa motisha wa kukufanya uongeze juhudi…!! #MunguHajakuumbaUjeteseka..!! Ipo siku.“amemaliza Harmonize.

Harmonize ni moja ya wasanii ambao kwa sasa Afrika Mashariki wanafanya vizuri sana kwenye tasnia ya muziki.

DPP Atoa Maelezo Kesi Mke wa Bilionea Msuya

$
0
0
DPP atoa maelezo kesi mke wa Bilionea Msuya
MKURUGENZI wa Mashtaka (DPP), amekiri kupokea malalamiko kutoka pande zote mbili katika kesi inayomkabili mke wa marehemu Bilionea Erasto Msuya, Miriam Mrita na mwenzake dhidi ya mauaji ya dada wa bilionea huyo, Aneth Msuya.

Aidha, DPP ameeleza kupitia Wakili wa Serikali Mwandamizi, Patrick Mwita akitoa madai hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.

Mwita alidai kuwa jalada la kesi hiyo lipo mikononi mwa DPP kwa ajili ya utendaji zaidi wa kikazi.

“Mheshimiwa hakimu, DPP amekiri kupokea malalamiko ya pande zote mbili, anaomba mahakama imvumilie wakati analifanyia kazi jalada la kesi hiyo, ili maelekezo atakayotoa yawe ya haki,” alidai Mwita.

Wakili wa utetezi, Peter Kibatala, alidai kuwa hana pingamizi na hoja za Jamhuri na kwamba DPP apewe muda wa kutosha kutenda haki kwa pande zote mbili.

Hakimu alisema upande wa Jamhuri ufuatilie jalada hilo ili mahakama iweze kuendelea na kesi hiyo, Mbali ya Miriam, mshtakiwa mwingine ni mfanyabiashara, Revocatus Muyela.

Katika kesi ya msingi, washtakiwa wanadaiwa kuwa Mei 25, 2016 walimuua kwa makusudi dada wa marehemu Bilionea Erasto Msuya, Aneth Msuya.

Wanaotorosha Madini ya Tanzanite Kukiona Chamoto

$
0
0
Wanaotorosha Madini ya TanzaniteKukiona Chamoto
Waziri wa Madini Angellah Kairuki amesema Serikali itaaendelea kusimamia  ulinzi  na kudhibiti utoroshaji wa madini ya Tanzanite na watakaokwenda  kinyume na matakwa ya Sheria, kiama chao  kinakuja.

Waziri Kairuki aliyasema hayo tarehe 1 Agosti wakati wa ziara yake mkoani Manyara wakati alipotembelea migodi mbalimbali ya madini  ya tanzanite ndani ya ukuta wa Mirerani.

Alisema ziara hiyo ililenga kuangalia suala zima la ulinzi katika ukuta unaozunguka migodi  ya tanzanite, shughuli za uchimbaji madini  mengine zinavyofanyika na kuangalia namna uzalishaji wa madini ya tanzanite  unavyoendelea katika migodi husika.

Kairuki aliongeza kuwa, ziara hiyo ililenga  kuangalia namna Sheria ya Madini inavyotekelezwa, masuala ya Mikataba ya watumishi katika migodi  na namna migodi husika inavyolipa  kodi  mbalimbali za Serikali  yakiwemo masuala ya usalama sehemu za kazi na  wafanyakazi kwa ujumla.

“Utoroshaji madini hausaidii, fedha ni za haraka lakini zinawaadhibu watanzania walio wengi kwa kuwa, fedha hizo hizo zingeweza kutumika katika miradi mingine ya maendeleo. Hivyo, kila mtanzania awe mlizi wa mwenzake,” alisema Kairuki.

Awali, akizungumza  katika eneo Lemshuku kunakofanyika shughuli za uchimbaji wa madini ya Green Garnet, waziri Kairuki alisema kuwa, serikali inatambua mchango wa wachimbaji wadogo katika kuchangia pato la taifa kupitia shughuli za uchimbaji, hivyo akawaasa wachimbaji nchini kufuata Sheria, kanuni na taratibu ili kufanya shughuli halali ikiwemo kulipa kodi stahiki.

Akizungmzia suala la ruzuku kwa wachimbaji wadogo, waziri Kairuki alisema hivi sasa serikali imesitisha kwa muda utoaji rukuzu kwa kuwa inaandaa utaratibu wa wazi na endelevu ambao utawezesha wachimbaji  na serikali kunufaika kupitia rasilimali madini.

Aliongeza kuwa, serikali inaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa shughuli za uchimbaji mdogo wa madini ikiwemo kuhakikisha kuwa inawawezesha wachimbaji kutoka uchimbaji mdogo kwenda katika uchimbaji wa kati na kuongeza, “ tayari tumetenga maeneo zaidi ya 44 kwa ajili ya wachimbaji wadogo.

Akitolea ufafanuzi suala la vibarua katika migodi ya madini, aliwataka wale wote wanaofanya vibarua katika maeneo hayo kuhakikisha kuwa, wanapata mikataba yao kabla ya kuanza kazi.

Kuhusu masuala ya utoaji leseni za uchimbaji madini, Waziri Kairuki  alisema   ndani ya kipindi cha wiki 2 Tume ya Madini itaanza kutoa leseni kwa waombaji waliokidhi vigezo na kuongeza kuwa, kwa wanaomiliki leseni bila kuziendeleza watanyang’nywa na hivyo akawaasa wamiliki wasiokuwa na uwezo wa kuendeleza maeneo yao kutoa tarifa ili waweze kuunganishwa na wenye uwezo wa kuwekeza waweze kushirikiana.

Pia, waziri Kairuki alihamasisha kuhusu uwekezaji katika mashine za kukata na kunga’risha madini ili kuwezesha shughuli hizo kufanyika nchini na kuongeza kuwa, kupitia Sheria Mpya ya Madini  hairuhusu yoyote kusafirisha madini ghafi nje ya nchi.

Kwa upande wake,  Kamishna wa Madini, Mhandisi David Mlabwa, alisema  ni lazima Sheria, Kanuni na taratibu zizingatiwe wakati wa utekelezaji shughuli za uchimbaji madini na kuongeza kuwa, serikali inatambua mchango wa kila aina ya madini yanayopatikana nchini.

Naye, Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro, Tumaini Magesa ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Kiteto alisema kuwa, shughuli za uchimbaji katika eneo la Mirerani zinaendelea na hivyo serikali itaendelea kuboresha ulinzi na kuhakikisha kwamba unaimalika.

Tiba ya Ukarabati wa Uke ''Inaweza Kusababisha Hatari Kubwa''

$
0
0
Wanawake wanaonywa dhidi ya hatari za mchakato wa kubadili umbo la uke ama kuurejesha katika hali yake asilia.

Wataalamu wanasema "matibabu", yanayotolewa na baadhi ya kliniki za kibinafsi katika mataifa mbali mbali yakiwemo ya Uingereza na Marekani yanaweza kumsababishia mwanamke kuungua vibaya, kupata makovu na kupata maumivu ya mara kwa mara.

Wakati wa matibabu haya, kifaa huingizwa ndani ya uke kwa ajili ya kuchemsha kukata nyama ya uke.

Ingawa matibabu haya si ya upasuaji na yanaweza kufanyika kwa muda mfupi tu, wataalamu wanashauri kuwa ni muhimu kuwa salama.

Matibabu hayo kwa njia ya vifaa vya kuchoma seli yameidhinishwa kwa matumizi ya matibabu ya kuua seli za saratani ya mfuko wa uzazi ama nyama ya uke pamoja na masundosundo ya sehemu za siri (genital warts) , lakini hayajafanyiwa vipimo vya ukarabati wa mwili

Hatari kubwa

'Dogo Janja' Afunguka Kuhusu Bifu Lake na Young Killer, Young Dee

$
0
0
'Dogo Janja' Afunguka Kuhusu Bifu Lake na  Young Killer, Young Dee
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Abdul Aziz Chande maarufu kama 'Dogo Janja' amesema hana bifu lolote na wasanii wenzake ambao amekuwa akihusishwa nao kama, Young Killer na Young Dee huku akidai vitu hivyo vinavumishwa na watu, lakini wao ni marafiki na wala hawana ugomvi.


Dogo Janja amebainisha hayo wakati alipokuwa anazungumza kwenye kipindi cha KIKAANGONI kinachorushwa mubashara kupitia kurasa za facebook za EATV, baada ya kuulizwa swali Abdul Yunusi ambaye alikuwa anafuatilia kipindi hicho kwa kutaka kujua kama ana ugomvi wowote na Young Killer pamoja na Young Dee.

"Sijawahi kuwa na bifu na msanii yoyote hapa nchini kwasababu mimi napita kwenye njia yangu nasio njia ya mtu kwa hiyo ni watu ndio wanaamua kufanya hivyo kwa kuweka ule 'U- young' lakini hatuna ugomvi, sisi ni marafiki", amesema Dogo Janja.

Pamoja na hayo, Dogo Janja ameendelea kwa kusema "sisi nje ya muziki tuna maisha yetu, hivyo huwa tunakutana mara moja moja na tunataniana sana, ila hawaniwezi mimi kwa matani maana nina kera na wao wanafahamu hilo".

Mbali na hilo, Dogo Janja amedai hakuna changamoto yoyote anayopitia endapo maswahiba zake wakitoa nyimbo kwa kile alichokieleza kuwa wao wana-rap na yeye anaimba kawaida.

Dogo Janja amekuwa akihusishwa kwenye ugomvi huo kutokana na wasanii hao kila mmoja akifanyiwa 'interview' na chombo cha habari huwa lazima mmoja wao amponde mwenzake kwa jambo baya na kupelekea kujenga hoja ya bifu katika vichwa vya mashabiki zao. Lakini kwa kauli ya Janjaroo aliyoitoa tunaweza kusema bifu hilo kwa sasa limefikia tamati.

CHADEMA Yatoa Tamko Hatma ya Mbowe Ndani ya Chama

$
0
0
CHADEMA Yatoa tamko hatma ya Mbowe ndani ya chama
Baada ya kutolewa kwa taarifa kwamba Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Freeman Mbowe ndio chanzo cha Wabunge wawili kutimkia CCM hivi karibuni, Chama hicho kimetoa tamko na kueleza kwamba hakiwezi kupangiwa kubadilisha mwenyekiti wao na CCM au watu wanaondoka ndani ya chama hicho.

Tamko hilo limekuja siku kadhaa baada ya aliyekuwa mbunge wa jimbo la Ukonga Mwita Waitara, na mbunge wa Monduli Julius kulanga kudai kwamba moja ya sababu zilizowaondoa CHADEMA ni mgogoro kati yao na Mbowe kuendelea kung’angania nafasi ya uenyekiti ndani ya chama hicho, na kunyimwa kushirikikiana na serikali katika shughuli za maendeleo.

Akizungumza na www.eatv.tv katika mahojiano maalum, Mkurugenzi wa Itikadi, Mawasiliano na Mambo ya Nje- CHADEMA bwana John Mrema amesema watakaoamua kiongozi wao ni nani ni wanachama wa CHADEMA na viongozi wao kwa mujibu wa katiba ya Chama hasa ikifika nyakati za uchaguzi, hivyo kinachofanywa kwa sasa na wanasiasa hao ni propaganda.

Akiendelea jibu hoja ya aliyekuwa mbunge wa ukonga aliyetimkia CCM kwamba CHADEMA ni 'SACCOS' ya Mbowe, Mrema amemtaka Waitara kutoa sababu zilizomfanya akakimbia,lakini siyo hizo ambazo alizitaja kwa sababu Mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali (CAG) anakagua chama kila mwaka na kutoa ripoti yake ambayo inaonesha mapato, matumizi na mali za chama.

“Unapokuwa na kiongozi ambaye anashindwa hata kusoma ripoti ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali halafu anaishia kusema uongo kwa kweli ni fedheha, ni kiongozi ambaye unaona kabisa kwamba hakuwa amejiandaa kuwa kiongozi”. Amesema Mrema

Mwishoni mwa wiki iliyopita aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Ukonga (CHADEMA) Mwita Waitara, alitangaza kujiunga na Chama Cha Mapinduzi CCM akidai moja kati ya vitu vilivymuondoa ndani ya chama hicho ni ugomvi wake na Mbowe ndani ya chama,ambapo baadaye Mbunge wa Monduli –CHADEMA naye alijiunga na CCM kwa sababu zinazofanana na hizo.

Aidha katika  kipindi cha takribani miwili na nusu tayari wabunge watatu wa CHADEMA  wameshajivua nyadhifa zao, na kujiunga na CCM ambao ni dokta Godwin Mollel wa Sia, Mwita Waitara wa Ukonga pamoja na bwana Julius kalanga wa Monduli.

Alikiba Afunguka Kuhusu Kusajiliwa Coastal Union

$
0
0
nguka Kuhusu Kusajiliwa Coastal Union
Msanii wa muziki, Alikiba alikuwa kimya kwa muda mrefu toka atangazwe na klabu ya Coastal Union ya Tanga kwamba ni mchezaji wao na atacheza ligi kuu ya Tanzania Bara msimu ujao.

Alikiba akisilimiana na shemeji yake.

Kwenye mitandao ya kijamii kumekuwa ni gumzo kila mmoja akijiuliza muimbaji huyo atawezaje kujigawa kwenye mpira na muziki kwa muwa mpira unahitaji muda mwingi zaidi kukaa kambini.

Siku ya jana ilikuwa ni siku ya ndoa ya dada yake Alikiba, Zabibu Kiba ambapo MC wa sherehe hiyo MC Pilipili alimuuliza muimbaji huyo kuhusiana na kusajiliwa kwake katika klabu hiyo yenye makazi yake mkoani Tanga.

“Tutaongea Tanga,” alisema Alikiba.

Watu wake wa karibu wamedai kwamba kwa sasa muimbaji huyo hawezi kuzungumza chochote mpaka atakapofika kwenye timu yake hiyo na kuanza mazoezi.

Uongozi wa klabu hiyo ulitangaza kwamba umemsajili mchezaji huyo kwaajili ya kuimarisha safu yao ya ushambuliaji.

Surveyed plots for sale: Mapinga (Baobab Sec, km 5 kutoka Bunju-DSM)

$
0
0

Surveyed plots for sale: Mapinga (Baobab Sec, km 5 kutoka Bunju-DSM)
Viwanja ni vikubwa sana (Low density & Medium densiy plots). Viwanja viko umbali wa km 2.5 kutoka main road (Bagamoyo Road).
Ziko plots za sqm 3000, sqm 2400, sqm 1500, sqm 1400, sqm 1200, sqm 900, na sqm 800
Bei ya kila sqm ni sh 13,000 (negotiable)
Huduma za kijamii (maji, umeme) zipo na miundombinu yote iko vizuri (mradi wa kusogeza lami mpaka nyumbani umeanza). Ramani zote (Town plan & Deed plan) zipo tayari. Hati ya miaka 99 itapatikana ndani ya mwezi mmoja tu.
hakuna dalali, contact mhusika: call 0758603077, whatsap 0757489709

Muone na Wasiliana na Dr Kanengo Bingwa wa Tiba Asili, Hutibu Magonjwa Haya

$
0
0
NKURURU:-ni dawa inayotibu miguu kuwaka moto, kiuno tumbo     kupooza/kuparalazi  kupoteza  fahamu  MALABALA  hutibu  kisukari , uti  wa  mgogo,  Change, pumu, busha, kaswende, kifua  kikuu, muwasho  sehemu  ya siri

POWER :-ni dawa ya kuongeza nguvu za kiume ni vidonge  20

MPERAMPERA:- ni dawa ya kurudisha Mke, mme, mpenzi,mchumba aliyekuacha /kuteseka, ni kwa mda wa siku 2 tu kusafisha, pia kunakuna dawa za kupunguza vitambi(nyama uzembe),  maziwa makubwa,michirizi, mikovu makubwa, chunusi sugu.

SIX POWER:-inatibu upungufu wa nguvu za kiume kwa wasio weza kumudu tendo la ndoa itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 4 bila hamu Keisha, inaboresha maumbile madogo na inaimarisha misuri iliyo regea na kusinyaa una pona kabisa, ndani ya siku 4 tu

GASELA:-ni dawa ya maajabu (9) yaliyoshindikana.    (1)-Kisukari, vidonda vya tumbo, tezi dume,walioshindikanika kupata watoto(ugumba),busha bila oparesheni, (2)zindiko Kali Katika biashara yako (chuma ulete)  ndo kiboko yao kumkamata mwizi aliye kuibia vitu vyako pikipiki, gari, n, k( 2)zindiko la nyumba, mashamba, viwanja,. ( 3 ) kurudisha mtu aliye kufa kiutatanishi (msukule) (4)kukutolea sumu uliyo ikanyaga (Mtego) (5)ujiamini kutumia dawa ya maajabu Saba (6)kutoa mikafara mfano ugomvi ndani ya nyumba kufukuzwa kazini bila sababu (7)kutabiri nyota na kung'arisha (8)kurudisha Mali iliyo potea mazingira ya kutatanisha, kushinda kesi uliyo sumbuka nayo mda mrefu. (9)kufukuza majini wa  chafu ndani ya mji,.Haya yote yana wezekana kwa DR KANENGO popote ulipo ukiniitaji nafika napatikana buguruni chama, mbagala zakhiem karibia na uwanja wa mkutano, na wilaya ya bunda musoma : mawasiliano  ni simu namba :-0767-17-17-73 na  0716-60-89-59

NI  KWA  WALIO  TUMIA  DAWA  ZA MATATIZO  MBALIMBLI  BILA  MAFANIKIO   uwezo  WA  kurudisha  mali  iliyopotea  au  kudhulumiwa    muda  mfupi  tu,  Na natoa  dawa  ya  utajiri  kwa  wafanya  biashara     wachimbaji  madini, wafaryakazi,  wakulima, wafugaji na  kwa yeyote  anayetaka  kuwa  na  pesa   nyingi  katika   maisha  yake,  Na  pia  anaunganisha  utajiri    kwa muda  mfupi  sana  pamoja  na  kuboresha  akili  kwa  wanafunzi  na  kumfanya  afaulu  mitihani  yote  au  intaview  yeyote  na  ana  uwezo  mkubwa  wa  kutibu  ugonjwa  wa  Uvimbe tumboni .  pia anarudisha  Mke, mme, mchumba,    hawara, kwa  muda  wa  saa  3  na  anatimiza mahitaji  yote  hata  kama  upo  mbali   kiasi  gani,  ahadi  zote  atatimiza  kwa  muda  mfupi  tu  Na  kumfunga  asiwe  na mtu  mwingine  kwa  nini  unaumiza  kichwa ?

Muone  ( DR  )KANENGO,anatibu  nguvu  za  kiume  anarefusha  na  kunenepesha  uume  kwa  saizi  uipendayo  kwa  muda  mfupi   sana, pamoja  na  kuwa  na  hamu  ya  kurudia  tendo  la  ndoa  mara  4  bila  hamu  kuisha   Na  utachelewa   kufika  kileleni  kwa  muda  wa  dakika   40  bila  kuchoka  hata  kama  una umri  mkubwa  kiasi  gani   Gerentii  miaka /=60    ukisha  pona  bila tatizo   kurudia  pia ana  uwezo  mkubwa  wa  kuongeza  hips na  makalio,  pia   anatibu  magonjwa  sugu  ya  zinaa  tumbo  kujaa  gesi,  kuuma  chini  ya  kitovu,vidonda vya tumbo,   kiuno,  miguu    kuwaka  moto  miguu,  kuvimba..Nk..Angalizo usitume meseji wala kubipu..
You can get it in   all East African countries, our service is fast and easy...

Contact Whatsapp 0767171773.Dar es salaam Tanzania. ..Dr. KANENGO 0716608959...You are welcome.

Harmonize Akumbuka Alivyokuwaga Machinga wa Kutembeza Bidhaa Kariakoo, Awakumbuka Wenzake

$
0
0
Mchumia juani hulia kivulini - Huo ni msemo wa wahenga ambao umekuwa ukionekana kuwa na ukweli ndani yake kutokana na mambo yanavyoonekana katika masiaha.

Miaka mitano sita iliyopita hakuna aliyekuwa anamfahamu Harmonize wala kutegemea kama jina kama hilo litakuja kusikika kwenye Bongo Fleva. Inawezejana kipindi hicho ndio alikuwa anapiga mishe zake jijini Dar es Salaam za kuuza vinjwaji baridi.

Msanii huyo leo hii amekuwa staa mkubwa Bongo na kufahamika sehemu kubwa Afrika. Harmonize ameonekana kwenye video aliyoiweka Instagram akiwa amewatembelea wafanyabiashara ndogo ndogo mjini Kariakoo kwa kuwapa moyo katika kutafuta maisha pamoja na kugawia fedha kama zawadi.

Hit maker huyo wa Kwa Ngwaru hajaishia hapo, katika video hiyo ameandika ujumbe mrefu wa kuwapa moyo watu wasikate tamaa katika maisha. Kupitia mtandao huo, Harmo ameandika:

Miaka (5) iliyopita nilikuwa nafanya biashara za kudunduliza maeneo haya ya #Kariakoo kwa lugha nyengine nilikuwa #Machinga shida, tabu, shuruba, nilizokuwa nikizipitia 
M/mungu peke ndie anayefahamu..!! Hata wimbo wangu wa #Matatizo 90% umebeba uhalisia wa maisha yangu sana......!!!! Sina utajiri wowote....!!! ila afadhali niliyoipata najihisi ni mwenye bahati 
Sana...!!! Maana maisha ninayoishi 
Sikuwahi hata kuyaota, Nimshukuru M/mungu kwa kunipa Nafasi hii ya kukumbuka Ndugu zangu ambao nimewaacha katika 
Eneo hili na kupata nafasi ya kuzungumza nao mawili ,matatu 
Ya kuwapa Moyo...!! faraja...!!!!! Mungu anawaona na Maombi yangu yapo kwenu...!!! 🙏 sitochoka 
Kuwa nanyi siku zote...!!! Na kidogo 
Au kingi changu kiwafikie kama fadhila ambazo ni ngumu
Kuwafikia watu wote..!!! Ila nyie 
Mliobahatika kwa leo mkawe wawakilishi wa wengine M/mungu awabariki sana...!!! Ndugu zangu Changamoto, pandashuka, majaribu, zifanye kuwa motisha wa kukufanya uongeze juhudi...!! #MunguHajakuumbaUjeteseka..!! Ipo siku....!!! 🙏🙏

Anaetuhumiwa kutoa rushwa ya Milioni 90 kwa Lukuvi afikishwa Mahakamani

$
0
0
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ambapo imempandisha kizimbani Mkurugenzi wa Kampuni ya Kiluwa Steal Group. Co.ltd na Kiluwa Free Processing Zone, Mohamed Kiluwa (50) kwa tuhuma za kutoa rushwa ya Shilingi Milioni 90 kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi.

Mshtakiwa huyo amepandishwa kizimbani mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Huruma Shaidi na kusomewa shtaka moja la kujihusisha na vitendo vya rushwa.

Akisomewa shtaka hilo mbele ya Hakimu Shaidi, Wakili wa Serikali Mkuu kutoka TAKUKURU, Maghela Ndimbo amedai July 16,2018 kati ya saa 6 na 8 mchana mshtakiwa huyo akiwa Mkurugenzi wa kampuni hizo mbili alitoa rushwa ya Dola za kimarekani 40,000 sawa na Sh. Milioni 90 kwa Waziri Lukuvi.

Wakili Ndimbo amedai mshtakiwa huyo alitoa fedha hizo kwa lengo la kutowasilisha hati ya umiliki wa kiwanja namba 57 ‘Block B’ Kikongo na ‘Block D’ Disunyura kilichopo eneo la viwanda Kibaha mkoani Pwani.

Baada ya kusoma shtaka hilo, Wakili Ndimbo ameiomba mahakama kuwapangia tarehe ya kutajwa kwa shauri hiyo na kuongeza kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado unaendelea na hawana pingamizi kuhusiana na mshtakiwa huyo kupewa dhamana.

Naye Wakili Upande wa Utetezi Imani Madega amedai kuwa kwa kuwa upande wa mashtaka hauna pingamizi na dhamana dhidi ya mshtakiwa wanaiomba mahakama itoe dhamana kwa kuzingatia masharti.

Hakimu Shaidi amesema ili mshtakiwa huyo apate dhamana anatakiwa kuwa na wadhamini 2 na mmoja atoe fedha taslimu mahakamani hapo kiasi cha Sh. Milioni 45 na kama hana awasilishe hati ya mali isiyo amishika yenye thamani ya kiasi hicho cha fedha.

Masharti ambayo upande wa utetezi uli

Aua Mke Kwa Shoka, Ajinyonga Kisa Wivu wa Mapenzi

$
0
0
MWANAMKE mkazi Njage wilayani Kilombero Mkoa wa Morogoro, ameuawa kwa kukatwa kwa shoka kichwani na mumewe kwa kilichoelezwa kuwa ni wivu wa mapenzi.

Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro, Willibrod Mutafungwa, alisema hayo jana na kufafanua kuwa tukio hilo lilitokea Julai 28 majira ya asubuhi ambapo mwanamke huyo, Rose Mngwe (43),  aliuawa na mumewe, Jacob Kambo (45), mkazi wa Kijiji cha Njage.

Kwa mujibu wa Kamanda Mutafungwa, mwanaume huyo baada ya kumuua mkewe kwa kumkata kwa shoka kichwani, alikimbilia porini na kujinyonga kwenye mti kwa kutumia kamba.

Kamanda Mutafungwa alisema inadaiwa kuwa mwanaume huyo aliamua kufanya kitendo hicho baada ya kuona mkewe amempuuza alipomwambia kuwaondoa watoto wake wa kike aliowazaa nje ya ndoa.

Kamanda alifafanua kuwa alitaka waende kwa waliomzalisha  watoto hao kwa madai kuwa wanawanyima nafasi wakiwa hapo.

Alisema miili ya marehemu hao imeshakabidhiwa kwa ndugu zao kwa ajili ya kuendelea na shughuli za mazishi.

Katika tukio lingine, Leo Charles Mashaka (61), mkazi wa Kitongoji cha Igagafu wilayani Kilosa, ameuawa kwa kupigwa na kitu chenye butu kichwani na usoni na mtoto wake wa kumzaa, Emmanuel Leo Charles, sababu ikitajwa ni kudai urithi.

Kamanda Mutafungwa alisema tukio hilo lilitokea Julai 30, alfajiri katika Kata ya Lumuma Tarafa ya Idete ambapo Mashaka alimpigwa na kitu chenye butu kichwani na usoni upande wa kulia na kumsababishia jeraha na michubuko mgongoni, Alisema tukio hilo lilisababishwa na mgogoro katika familia kuhusu urithi.

Kamanda huyo alisema mtuhumiwa alikamatwa na atafikishwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika.
 

Pata Dawa ya Mtikulu, Dawa ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0


MTIMKULU NI DAWA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO.

Matatizo haya yamekuwa yakiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia inchi (68)vinginevyo mtu huyo anamatatizo zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo baadhi ni upungufu wa vichocheo hivi Hormones za Getrogen ambapo mwanaume anapo balehe vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chango hushambulia neva ambapo huathiri misuri ya uume. Ngiri ambayo huleta maumuvu ya tumbo kuunguruma na kujaa gesi korodani moja kuvimba kutopata choo vizuri

Sababu hizi na nyinginezo hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara kwa mara hupelekea kupungua kwa nguvu za kiume na hamu ya tendo la ndoa hukosekana na kuisha kabisa

(MTIMKULU) ni dawa inayozarisha hormones za Getrogen nakufanya uume kukua na kuongezeka

(ITEGESHA)ni bora ya kurudisha nguvu za kiume na kukupatia hamu tendo ndoa zaidi ya mara nne bila kuchoka zaidi (dk1520)kwa tendo moja na hazina madhara kwa mtumiaji pia anatibu kisukari, miguu kuwaka moto kutoshika mimba, na mvuto wa mapenzi karibuni sana



Kwa Mawasiliano DR MADINA +255655105260

Rostam Ataka Kuondoka Yanga Kocha Afunguka

$
0
0
Rostam Ataka Kuondoka Yanga Kocha Afunguka
KOCHA Mkuu wa Yanga, Mwinyi Zahera raia wa DR Congo, amefunguka kuwa alifanikiwa kuona kiwango cha Deus Kaseke kupitia mechi ya Simba, huku akisema Youthe Rostand ameomba kuondoka.



Hivi karibuni Yanga ilifanikiwa kumrejesha Kaseke kikosini kwao akitokea Singida ili kuongeza nguvu kwenye kikosi hicho ambacho kinasuasua.



Katika kudhihirisha kuwa hawakufanya makosa kumsajili mchezaji huyo, wikiendi iliyopita Kaseke aliifungia Yanga bao moja katika kipigo cha mabao 3-2 kutoka kwa Gor Mahia ya Kenya kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika uliopigwa katika Uwanja wa Taifa, Dar.



Akizungumza na Championi Jumatano, Zahera alisema kwa mara ya kwanza aliona uwezo wa Kaseke akiwa hotelini akiishuhudia mechi hiyo kwenye runinga na akaamua kufanya uamuzi wa kumsajili huku akiwa na matumaini ya kiungo huyo atakuwa msaada kikosini kwake.



“Kaseke kwa mara ya kwanza nilimuona kwenye mechi ya Simba na Singida, hapo nilikuwa hotelini naangalia mchezo huo kupitia ‘TV’ ndipo niliweza kumpigia simu kocha Mwandila (Noel) na kumuuliza yule mchezaji ni nani, akaniambia, nikasema namuhitaji kwenye kikosi changu, ndipo nikapata jibu kwamba aliwahi kucheza hapa.



“Lakini kwa kipindi hiki kifupi ambacho nimekaa naye, nimegundua ni mchezaji mzuri hasa kifiziki, akiendelea kupambana atafika mbali zaidi, kikubwa ni kuepuka yale makosa madogomadogo lakini atakuwa mchezaji tegemeo kwenye timu,” alisema Zahera.



Katika hatua nyingine, Zahera alisema jana Jumanne beki wake, Kelvin Yondani kwa mara ya kwanza alianza mazoezi na wenzake baada ya kukosekana kwa muda mrefu kutokana na mkataba wake kumalizika, huku akibainisha kwamba, kipa wa timu hiyo, Youthe Rostand hakutokea mazoezini huku taarifa zikidai alikutana na uongozi wa Yanga kuona uwezekano wa kuvunja mkataba wake ili aondoke kikosini hapo.

Kajala Apigwa Stop Kujirusha Kwenye Kumbi za Starehe

$
0
0
Kajala Apigwa Stop Kujirusha Kwenye Kumbi za Starehe
STAA mkali wa filamu Bongo, Kajala Masanja ameifungukia sababu ya kutojirusha kwenye kumbi za starehe hivi karibuni na kudai kuwa kwa sasa yupo kwenye himaya ya mtu ambaye hapendi kabisa mambo ya kutoka usiku.



Akizungumza na Amani hivi karibuni, Kajala alisema watu wengi wamekuwa wakimuuliza kwa nini haonekani kwenye kumbi mbalimbali za starehe lakini kikubwa ni kwamba anamheshimu sana mtu aliyenaye kwenye uhusiano kwa sasa na ndiyo maana ameamua kujituliza.



“Unajua kuna kipindi mambo yanabadilika kabisa na unafanya vitu vingi kulingana na wakati uliokuwepo, mimi sasa hivi nipo na mtu ambaye hapendi kabisa vitu hivyo vya kutokatoka usiku lakini pia hata mimi mwenyewe nimebadilisha maisha yangu siyo yale tena,” alisema Kajala huku akiahidi kumwanika mwandani wake siku zijazo.

Anaetuhumiwa Kutoa Rushwa ya Milioni 90 kwa Lukuvi Afikishwa Kizimbani

$
0
0
Anaetuhumiwa kutoa rushwa ya Milioni 90 kwa Lukuvi afikishwa Mahakamani
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ambapo imempandisha kizimbani Mkurugenzi wa Kampuni ya Kiluwa Steal Group. Co.ltd na Kiluwa Free Processing Zone, Mohamed Kiluwa (50) kwa tuhuma za kutoa rushwa ya Shilingi Milioni 90 kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi.

Mshtakiwa huyo amepandishwa kizimbani mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Huruma Shaidi na kusomewa shtaka moja la kujihusisha na vitendo vya rushwa.

Akisomewa shtaka hilo mbele ya Hakimu Shaidi, Wakili wa Serikali Mkuu kutoka TAKUKURU, Maghela Ndimbo amedai July 16,2018 kati ya saa 6 na 8 mchana mshtakiwa huyo akiwa Mkurugenzi wa kampuni hizo mbili alitoa rushwa ya Dola za kimarekani 40,000 sawa na Sh. Milioni 90 kwa Waziri Lukuvi.

Wakili Ndimbo amedai mshtakiwa huyo alitoa fedha hizo kwa lengo la kutowasilisha hati ya umiliki wa kiwanja namba 57 ‘Block B’ Kikongo na ‘Block D’ Disunyura kilichopo eneo la viwanda Kibaha mkoani Pwani.

Baada ya kusoma shtaka hilo, Wakili Ndimbo ameiomba mahakama kuwapangia tarehe ya kutajwa kwa shauri hiyo na kuongeza kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado unaendelea na hawana pingamizi kuhusiana na mshtakiwa huyo kupewa dhamana.

Naye Wakili Upande wa Utetezi Imani Madega amedai kuwa kwa kuwa upande wa mashtaka hauna pingamizi na dhamana dhidi ya mshtakiwa wanaiomba mahakama itoe dhamana kwa kuzingatia masharti.

Hakimu Shaidi amesema ili mshtakiwa huyo apate dhamana anatakiwa kuwa na wadhamini 2 na mmoja atoe fedha taslimu mahakamani hapo kiasi cha Sh. Milioni 45 na kama hana awasilishe hati ya mali isiyo amishika yenye thamani ya kiasi hicho cha fedha.

Masharti ambayo upande wa utetezi uliyatekeleza na mshtakiwa akaachiwa kwa dhamana. Kesi hiyo imeahirishwa hadi August 15,2018.

Aua mke kwa Shoka Kisha Kujinyonga Kisa Wivu wa Mapenzi

$
0
0
Aua mke kwa shoka, ajinyonga kisa wivu wa mapenzi
MWANAMKE mkazi Njage wilayani Kilombero Mkoa wa Morogoro, ameuawa kwa kukatwa kwa shoka kichwani na mumewe kwa kilichoelezwa kuwa ni wivu wa mapenzi.

Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro, Willibrod Mutafungwa, alisema hayo jana na kufafanua kuwa tukio hilo lilitokea Julai 28 majira ya asubuhi ambapo mwanamke huyo, Rose Mngwe (43),  aliuawa na mumewe, Jacob Kambo (45), mkazi wa Kijiji cha Njage.

Kwa mujibu wa Kamanda Mutafungwa, mwanaume huyo baada ya kumuua mkewe kwa kumkata kwa shoka kichwani, alikimbilia porini na kujinyonga kwenye mti kwa kutumia kamba.

Kamanda Mutafungwa alisema inadaiwa kuwa mwanaume huyo aliamua kufanya kitendo hicho baada ya kuona mkewe amempuuza alipomwambia kuwaondoa watoto wake wa kike aliowazaa nje ya ndoa.

Kamanda alifafanua kuwa alitaka waende kwa waliomzalisha  watoto hao kwa madai kuwa wanawanyima nafasi wakiwa hapo.

Alisema miili ya marehemu hao imeshakabidhiwa kwa ndugu zao kwa ajili ya kuendelea na shughuli za mazishi.

Katika tukio lingine, Leo Charles Mashaka (61), mkazi wa Kitongoji cha Igagafu wilayani Kilosa, ameuawa kwa kupigwa na kitu chenye butu kichwani na usoni na mtoto wake wa kumzaa, Emmanuel Leo Charles, sababu ikitajwa ni kudai urithi.

Kamanda Mutafungwa alisema tukio hilo lilitokea Julai 30, alfajiri katika Kata ya Lumuma Tarafa ya Idete ambapo Mashaka alimpigwa na kitu chenye butu kichwani na usoni upande wa kulia na kumsababishia jeraha na michubuko mgongoni, Alisema tukio hilo lilisababishwa na mgogoro katika familia kuhusu urithi.

Kamanda huyo alisema mtuhumiwa alikamatwa na atafikishwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika.

Viewing all 104756 articles
Browse latest View live




Latest Images