Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live

Baraka The Prince Atoa ya Moyoni Kuhusu Daimond "Ndio Msanii Mwenye Mafanikio "

$
0
0
Baraka The Prince Atoa ya Moyoni Kuhusu Daimond "Ndio Msanii Mwenye Mafanikio "
Msanii wa muziki wa Bongo fleva anayefanya vyema kabisa na ngoma yake ya ‘Sina’ Barakah The Prince amefunguka na kumtaja Diamod kama Msanii Mwenye mafanikio ambaye yanaonekana.

Barakah amemtaja Diamond baada ya kuulizwa kuhusu wasanii mwenye mafanikio ambapo amekiri kuwa wasanii kadhaa wenye mafanikio sana lakini Diamond ndiye anayeonekana kufanikiwa zaidi.

Kwenye mahojiano na kipindi cha The Playlist cha Times Fm, Barakah amesema wasanii wenye mafanikio wapo wengi lakini hajui mkwanja wao benki au hawajionyeshi sana lakini Diamond anaonekana wazi kabisa:

Wasanii wengi wana mafanikio wakina Ali Kiba, AY, Joti, Masanja, sitaki kujudge kama Diamond ndio Msanii wa kwanza kwa sababu sijui akaunti yake lakini kwa nje kila mtu anaweza kuwa na mtazamo huo kwa sababu anafanya vitu vinavyoonekana katika jamii”.


Lakini hatuwezi kusema nani namba moja kwa sababu hatujui akaunti ya Sugu ipoje? Ommy Dimpoz, Profesa Jay, Juma Nature na wasanii wengineo”.

Msanii Chemical amewahi kumtaja Diamond kama Msanii Mwenye mafanikio na pesa zaidi Kwenye muziki wa Bongo fleva.

Moise Katumbi Azuiwa Kuingia DRC Kuwasilisha Nyaraka za Kugombea Urais

$
0
0
Moise Katumbi azuiwa kuingia DRC kuwasilisha nyaraka za kugombea urais
Moise Katumbi, kiongozi wa upinzani katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, amezuiwa kurudi nchini kugombea urais katika uchaguzi mkuu Desemba mwaka huu.

Serikali ya Congo imemzuia Gavana huyo zamani wa jimbo la Katanga anayeishi uhamishoni Afrika kusini kurudi nyumbani.

Katumbi aliomba ruhusa kuingia nchini leo asubuhi kuwahi kuwasilisha makaratasi yake ya uteuzi wa chama kuwa mgombea urais kwa tume ya uchaguzi nchini.

Sababu za Moise Katumbi kuanzisha Chama akiwa Afrika Kusinihttps://www.bbc.com/swahili/medianuai/2016/03/160308_katumbi

Maafisa wa polisi huko Lubumbashi wameweka vizuizi katika bara bara kuu na usalama umeimarishwa ndani na katika maeneo yalio karibu na uwanja wa ndege.

Kuna mipango ya kuzifunga njia za ndege kutua kuizuia ndege ya Katumbi isitue DRC.

Simba kuvaana na mabingwa wa Morocco leo

$
0
0
Simba kuvaana na mabingwa wa Morocco leo
MABINGWA wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba ya jijini Dar es Salaam wanatarajia kucheza mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya klabu ya Ittihad Riad de Tanger itakayofanyika leo Uturuki.

Mechi hiyo ya leo itajayofanyika kuanzia saa 10 jioni kwa saa za Tanzania ni ya pili kwa mabingwa hao baada ya kutoka sare ya bao 1-1 dhidi ya klabu nyingine kutoka Morocco.

Akizungumza jana jijini hapa, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Simba, Haji Manara alisema jana kuwa huo ni mwendelezo wa timu yao kupata mechi zitakazowaweka katika kiwango cha juu kuelekea msimu mpya.

Manara alisema kikosi chao kiko katika hali nzuri na benchi la ufundi linatarajia kuendelea kutoa nafasi kwa wachezaji wake wengi kuonyesha uwezo wao.

"Tuko katika mipango ya kuhakikisha timu yetu inapata mechi ya tatu kabla ya kurejea, mwalimu anasema yeye anaziita hizo mechi ni sehemu ya mazoezi, na timu itarejea nchini Jumapili alfajiri," alisema kiongozi huyo.

Naye Kaimu Rais wa Simba, Salim Abdallah alisema kuwa maandalizi ya Tamasha la Simba Day litakalofanyika Agosti 8 mwaka huu, yako katika hatua za mwisho na leo wanatarajia kumtangaza kiongozi ambaye atakuwa mgeni rasmi kwenye mchezo huo.

Abdallah alisema kuwa pia, klabu yake itatambulisha jezi mpya za klabu hiyo Jumapili pamoja wasanii ambao watatumbuiza katika Tamasha la Simba Day.Aliongeza kuwa katika mwendelezo wa wiki ya Simba, kesho wachezaji wakongwe wa timu hiyo watawatembelea wenzao wa Yanga katika malengo ya kudumisha umoja na ushirikiano kati ya klabu hizi mbili kongwe za hapa nchini.

Mabingwa hao wa Bara wamewaalika Asante Kotoko ya Ghana kucheza nao mechi ya kirafiki katika Tamasha la Simba Day.

Masikini Mzee Majuto Azidiwa Alazwa ICU

$
0
0
Masikini Mzee Majuto Azidiwa Alazwa ICU
MUIGIZAJI nguli nchini Tanzania, Amri Athuman maarufu kama Mzee Majuto amelazwa tena katika chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Jumanne ya wiki hii.

Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Hospitali ya Muhimbili, Aminiel Aligaesha ndiye aliyethibitisha taarifa hizo za kulazwa kwa Mzee Majuto.



Hii inakuwa mara ya pili kwa mchekeshaji huyo kulazwa katika Hospitali ya Muhimbili kwani mapema mwaka huu alilazwa Hospitalini hapo kabla ya kupelekwa India kwa matibabu zaid

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba, Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0



Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi?


Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Waziri Mkuu kuwa mgeni rasmi kwenye mchezo wa tamasha la 'Simba Day'

$
0
0

Klabu ya soka ya Simba leo imemtangaza Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa kuwa mgeni rasmi kwenye mchezo wa tamasha la 'Simba Day' dhidi ya Asante Kotoko ya Ghana Agosti 8, 2018.


Akiongea leo na wanahabari, msemaji wa timu hiyo Haji Manara, amethibitisha kuwa tayari Waziri mkuu ameshakubali ombi lao na kuahidi atakuwepo uwanjani kuwaongoza mashabiki wa Simba katika tamasha lao lenye shughuli mbalimbali ikiwemo kutambulishwa kwa wachezaji wapya.


''Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amekubali ombi letu, na ninaomba nitangaze rasmi kuwa yeye ndio atakuwa mgeni rasmi kwenye tamasha letu la 'Simba Day' akiongoza shughuli zote ambazo zitafanyika siku hiyo'', - amesema.


Mbali na kumtangaza mgeni rasmi, Manara amewataka mashabiki wa timu hiyo kutojihusisha na masuala ya kugushi tiketi kwani wao kama klabu wamejidhatiti kuhakikisha watu wa aina hiyo hawapati mwanya ndio maana suala la usimamizi wa tiketi uwanjani wamelikabidhi kwa Suma JKT.


Aidha Manara amesema kikosi cha Simba kitatua nchini Jumatatu ya Agosti 6 kikitokea Uturuki ambako kimeweka kambi ya maandalizi ya msimu wa 2018/19. Pia siku hiyo Simba watatambulisha jezi zao mpya za nyumbani na ugenini msimu huu.

Tazama Picha Jinsi Jokate Alivyoapishwa Kuwa Mkuu wa Wilaya

$
0
0

Mkuu mpya wa wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo ameapishwa leo huku akipewa onyo kuepuka wapotoshaji. Pamoja na Jokate, Zainab Kawawa naye ameapishwa kuwa mkuu wa wilaya ya Bagamoyo.


Jokate, ambaye aliwahi kuwa mlimbwende wa mashindano ya Miss Tanzania mwaka 2006, aliteuliwa kuwa mkuu wa wilaya ya Kisarawe, Julai 28 mwaka huu.


Jokate ameapishwa leo Agosti 3 huku ndugu, jamaa, marafiki na viongozi wa CCM wakihudhuria hafla za uapisho huo.


Akizungumza mara baada ya wakuu hao wawili wa wilaya kuapishwa, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Pwani, Ramadhani Maneno amewataka wateule hao waepuke wanaofika ofisini kutaka kuwapotosha katika utendaji wao.


Amewataka wakakae na makatibu tawala ili wakusanye mapato kwani mkoa wa Pwani una  viwanda.


“Kwa nafasi mlizopata hakikisheni mnakua karibu na viongozi wa chama hilo ni jambo kubwa. Wakati sasa mnaenda kuripoti kwenye wilaya mkaanzie kwenye ofisi za chama,”amesema.


Ameongeza: "Huko mnapoenda mtafute desturi na mila za maeneo yenu msizipuuzie, lakini mtafute yale yanayoendana na nyaraka zilizopo.”


Amesema anawakabidhi vitu vitatu, macho, masikio na mdomo ambavyo vitawasaidia kwenye utendaji wao wa kazi.


Pamoja na kuwepo kwa idadi ndogo ya waliohudhuria sherehe hizo za uapisho, hakuna msanii hata mmoja aliyeonekana.


Wengi walitarajia kuona wasanii wakijitokeza kwa wingi katika sherehe hizo kwa kuwa Jokate ni msanii wa filamu, muziki na ni mwanamitindo



Meya Boniface akomaa na ‘aliyemdanganya’ Rais kuhusu mapato

$
0
0

Siku chache baada ya Rais John Magufuli kuonesha kukwazwa na kiwango kidogo cha makusanyo ya mapato ya jiji la Dar es Salaamambayo alieleza kuwa yanazidiwa karibu mara mbili na ya jiji jipya la Dodoma, Meya waHalmashauri ya Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob ameibuka na kueleza kuwa Rais alipewa taarifa zisizo sahihi.

Rais Magufuli alieleza kuwa jiji la Dar es Salaam lenye watu zaidi ya milioni 5 lilikusanya Sh15 bilioni huku jiji la Dodoma lenye watu takribani milioni 2 likikusanya Sh24 bilioni na kuongoza.

Kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari, Jacob alisema kuwa jiji la Dar es Salaam lilikusanya zaidi ya Sh 139 bilioni ambazo ni sawa na asilimia 91.95 ya malengo iliyowekewa ambayo ni Sh 151 bilioni.

“Halmashauri zote za DSM walipanga kukusanya billioni 151,290,075,441 na wakafanikiwa kukusanya kiasi cha Billioni 139,118,756,519,90 sawa na asilimia 91.95. Swali ni Je, Billioni 139.118,756,519.90 ni ndogo kuliko billioni 24.4,” alisema Jacob na kusisitiza kuwa kiasi hiki ndicho kilichochangiwa na watu milioni 5 wa mkoa wa Dar es Salaam waliotajwa.

Akizichambua baadhi ya halmashauri za mkoa huo, alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam pekee ilipanga kukusanya sh16.4 bilioni lakini ilikusanya 16.8 bilioni ambayo ni sawa na asilimia 102, hivyo ilivuka lengo.


Aliongeza kuwa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni katika mwaka jana wa fedha ilipanga kukusanya 31.6 bilioni na ilikusanya 29.7 bilioni ambayo ni sawa na asilimia 94 ya malengo. Temeke ilipanga kukusanya Sh30.9 bilioni lakini ilikusanya Sh29.03 bilioni sawa na asilimia 94.


Halmashauri ya Ubungo ambayo anaiongoza, amesema ilikusanya Sh16 bilioni lakini ilikusanya Sh13.5 ambayo ni sawa na asilimia 81.8.

Akiendelea kumkosoa aliyempa taarifa hizo Rais, Meya huyo alisifu utaratibu aliouanzisha Rais Magufuli wa kushindanisha mapato ya Halmashauri zote nchini kwani utachagiza usimamiaji mzuri wa makusanyo ya mapato.

Boniface alikiri kuwa kuna mikono ya upigaji kwenye halmashauri za Dar es Salaam kama ilivyo kwa halhamashauri nyingine lakini akaeleza kuwa hata Waziri wa Tamisemi, Selemani Jafo anafahamu juhudi zinazofanywa na halmashauri hizo ambazo nyingi zinaongozwa na upinzani ikiwa ni pamoja na Jiji la Dar es Salaam likiwa chini ya Meya Isaya Mwita wa Chadema.

Kauli ya Rais Magufuli Juu ya Mkoa wa Dar Yamuamsha Makonda

$
0
0

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam,  Paul Makonda ameitisha kikao na wakurugenzi wa manispaa zote za mkoa kwalengo la kupitia takwimu za mapato na matumizi ya mkoa huo ili kujiridhisha kwanini wameshuka kimapato na kuzidiwa na jiji la Dodoma ambalo limepandishwa hadhi hivi karibuni.

Makonda ametoa kauli hiyo leo Agosti 3, 2018 katika hafla ya kuwakaribisha wakuu wa wilaya wapya na kuwaaga waliohamishwa vituo vya kazi, ambapo amemtaka katibu tawala wa mkoa kuipanga upya Idara ya Ardhi kwani ni maeneo yenye uongo mwingi na imekuwa na viongozi ambao wanachukuwa nyaraka za wananchi na kisha kuwapelekea matajiri na kuwanyima haki wanyonge.

“Haiingii akilini Mkoa wa Dar es Salaam kushuka kimapato pamoja na kuzidiwa ukusanyaji kodi wakati ni mkoa wa kiuchumi, kuna nyumba na viwanja vya serikali ambavyo vimechukuliwa na watu binafsi, mikataba ya unyonyaji ambayo imesainiwa na inaiminya serikali”, amesema

Makonda ameongeza kuwa viongozi wengi wa Dar es Salaam wanatoa taarifa nyingi za uongozi juu ya utendaji na utekekezaji wa miradi na mfumo wa biashara pia uangaliwe ili kuiwezesha kuwepo kwa mfumo rahisi ambao unarahisisha huduma za kitengo cha biashara kwani kumekuwa na urasimu uliopitiliza.

“Katika suala la ulinzi na usalama, wanaendelea na kuweka Camera katika maeneo mbalimbali ya jiji na baada ya hapo tutaruhusu ufanyaji wa biashara kwa masaa24”, ameongeza Makonda.

Agosti 1, 2018 wakati akizungumza na wakuu wa mikoa baada ya kuwaapisha viongozi mbalimbali aliowateua, Rais Magufuli alisema kati ya majiji yote, Dodoma inaongoza kwa makusanyo ya mapato ya Shilingi bilioni 24.2 ikiwa ni asilimia 123 ya makisio yao ya Shilingi bilioni 19.

Amesema Jiji la Dar es Salaam ambalo ni kongwe kuliko yote lilikusanya pesa kidogo tofauti na ukubwa wake ambapo lilikusanya kiasi cha Sh15.3 bilioni, Arusha (Sh10.3 bilioni), Mwanza (Sh9.3bilioni), Tanga (Sh9.1bilioni) na Mbeya (Sh4.2bilioni).

Kiboko ya Matatizo ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo, Mvuto wa Mapenzi na Magonjwa Sugu

$
0
0
KIBOKO YA MATATIZO YA NGUVU ZA KIUME MAUMBILE MADOGO MVUTO WA MAPENZI NA MAGONJWA SUGU Wanaume wengi wana upungufu wa nguvu za kiume na kuwa na maubile madogo ya kiume magonjwa kama kisukari presha ngiri korodani kuvimba busha, tumbo kuunguruma kujaa ngesi na kutopata choo vizuri, punyeto na NK huchangia kwa kiasi kikumbwa upotevu wa nguvu za kiume tumia dawa nzuri ya mitishamba ambayo haina madhara kwa mtumiaji ata uwe na miaka 80 inatibu na kumtuliza matatizo hayo


SUPER SHAFT NI DAWA YENYE UWEZO MKUBWA WA KUOGEZA NGUVU ZA KIUME MARA DUFU NA MAUMBILE MADOGO YA KIUME
(1) Itakufanya uwe na nguvu za ajabu ukiwa unafanya tendo la ndoa (2 ) Inaongeza hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka (3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni ndani ya dk 30 nakukupa nguvu zaidi
( 4)Itakupa nguvu za kusimamisha uume wako barabara kama msumari wakati wa tendo la ndoa

NYATI POWER INAREFUSHA NA KUNENE PESHA UUME SAIZI UTAKAVYO kuazia nchi 1 -8 unene sm 2-4 5) Itaimalisha milija ya uume iliyo legea au kusinyaa 6)lnasaidia kisafisha mishipa ya kwenye uume na hivyo kusaodia kuogeza kasi ya msukumo wa damu kwenye mishipa ya uume (7) Usaidia kuurudisha nje uume uliyoigia ndani
(8) Inasaidia kuogeza manii nyingi abazo vinaviini vya uzazi
( 9) Usaidia kutibu madhara ya punyeto, matumizi makali ya madawa ya kizungu milungi bangi na sigara

TUNATIBU MAGONJWA YOTE SUGU NGIRI KORODANI KUVIMBA BUSHA BILA KUFANYIWA OPRESHENI TENZI DUME KISUKARI PRESHA AINA ZOTE

UGONJWA WA MOYO STROKE KWIKWI, KICHOMI MIGUU KUFA NGAZI.NK

ANAPATIKANA MAGOMENI MIKUMI KARIBU NA KANISA KATOLIKI TUMAINI HEABRS CLINC NDIYO SULULISHO LA MATATIZO YOTE PIGA SIMU 0745495181 AU 0682644040

WOTE MNAKARIBISHA kama huna nafasi ya kufika ofisini kwetu huduma hii utaletewa mahali ulipo na wa mikoani mtaipata kirahisi

KWA MENGINEYO INGIA HAPAwww.tumainitibaasili.co.tz 

Mkurugenzi wa Twaweza Akalia Kuti Kavu ... Uhamiaji Washikilia Passiport Yake Azuiwa Kusafiri Nje

$
0
0
Mkurugenzi wa Twaweza Akalia Kuti Kavu ... Uhamiaji Washikilia Passiport Yake Azuiwa Kusafiri Nje
Idara ya Uhamiaji inaishikilia pasi ya kusafiria ya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Twaweza, Aidan Eyakuze na kumzuia kusafiri nje ya nchi.



Kwa mujibu wa kiongozi huyo wa TWAWEZA, pasi hiyo aliiwakilisha yeye mwenyewe baada ya kutakiwa kufanya hivyo na idara hiyo.

TFF Yatoa Msimamo Wake Kuhusu Alikiba

$
0
0
TFF Yatoa Msimamo Wake Kuhusu Alikiba
BAADA ya hivi karibuni baadhi ya watu kudai kuwa mchezaji mpya wa Coastal Union ya Tanga, Ally Salehe Kiba ‘Ali Kiba’ kuwa kanuni za Ligi Kuu Bara hazimruhusu kuitumikia timu hiyo katika ligi hiyo, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetoa msimamo wake.



Ilidaiwa kuwa kanuni za ligi kuu hazimruhusu Kiba kuitumikia Coastal katika ligi hiyo kwa sababu ni mwanamuziki jambo ambalo lilizua maswali mengi kwa baadhi ya wapenzi na mashabiki wa soka hapa nchini.



Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF, Salum Madai ameliambia Championi Ijumaa kuwa, hakuna kanuni yoyote inayomzuia Ali Kiba asiitumikie Coastal Union katika michuano ya kwa sababu tu ni mwanamuziki.



Alisema mchezo wa soka haubagui, kila mtu anaruhusiwa kucheza. “Kanuni zetu hazijasema mchezaji lazima awe na kazi moja tu, anaweza kuwa mcheza mieleka, mcheza kikapu na mchezaji wa soka la ufukweni na kusajiliwa kucheza soka.



“Kwa hiyo, Coastal Union wao kama wameona kuwa Ali Kiba anaweza kuwasaidia hiyo ni juu yao ila hakuna kanuni inayomzuia kutoitumikia timu hiyo kwa sababu ya kazi yake,” alisema Madadi.

Ninadaiwa na Rais Magufuli - Jokate

$
0
0
Ninadaiwa na Rais Magufuli - Jokate
Mkuu mpya wa wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani  Jokate Mwegelo ameapishwa rasmi leo tayari kuanza kuwatumikia wananchi  kwa nafasi ya ukuu wa wilaya, ambapo pamoja na mambo mengine amesema ana deni kubwa kwa Rais John Magufuli na wananchi wa Kisarawe.

Akizungumza na vyombo vya habari kwa mara ya kwanza tangu ateuliwe kuwa mkuu wa wilaya ya Kisarawe, Jokate amemshukuru Rais  Magufuli kwa na nafasi aliyompa ya kuongoza wilaya hiyo na kwamba ana deni
kubwa sana kwa vijana wengi ambao wanamuangalia yeye kama mfano.

Amesema “ sijaja kutengua torati  nimekuja kutimilisha, nimekuja kushirikiana na viongozi ambao wamefanya kazi nzuri sana katika wilaya hii ya Kisarawe. Kwa hiyo niseme tu ndugu zangu waandishi wa habari tukutane kazini tuendelee kumsaidia Mh. Rais kuweza kujua maendeleo ambayo tunayafanya kwa ajili ya wananchi tukiongozwa na ilani ya Chama
cha Mapinduzi”

Ni takribani wiki sasa jina la  Jokate Mwegelo limejiongezea umaarufu mkubwa katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii ndani na nje ya nchi baada tu ya jina hilo kutajwa katika orodha ya majina ya wakuu wapya wa Wilaya walioteuliwa na Rais Dkt. John Magufuli.

Ni wazi sasa Jokate Mwigelo ameanza safari yake ya kuwa mtumishi wa umma ambapo baada ya kuapishwa rasmi leo na mkuu wa mkoa wa Pwani Evarist Ndikilo anakwenda kuwaongoza wakazi 95.614 waliopo katika wilaya ya Kisarawe akiwa kama mkuu wa Wilaya.

Kim Kardashian Aliuza Gari Lake Kisa Hiki Hapa

$
0
0
Kim Kardashian Aliuza Gari Lake Kisa Hiki Hapa
MWANAMITINDO na mtangazaji wa televisheni maarufu nchini Marekani,  Kim Kardashian West analiuza gari lake aina ya  Land Rover Range Rover V8 kwa Dola 85,000 (Sh. milioni 194).

Staa huyo ameamua kwa sababu anazojua mwenyewe kuliuza gari hilo lenye aina kibao za anasa ndani yake ambalo lilikuwa likitumiwa na familia yake.

Steve Nyerere Awawakia Wanaomfananisha na Idriss

$
0
0
Steve Nyerere Awawakia Wanaomfananisha na Idriss
Mchekeshaji maarufu nchini  steve nyerere amefunguka na kusema kuwa watu wanakosea sana wanapotaka kumfananisha yeye na idrisa sultan kwa sababu hawawezi kulingana hata siku moja.

Wawili hao ambao wote ni wa tasnia ya uchekeshaji wamekuwa wakifanya vizuri comedy na kila mtu kwa style yake na huku kila mmoja akiwa na mashabiki wake.

Hata hivyo kutokana na jinsi idris amekuwa akitania sana wasanii wenzie katika mitandao ya kijamii na hata kutoa kituko cha skendo zinazondelea kumkabili steve nyerere, steve nasema kuwa haweiz kujibishana na idris kwa sababu wao ni watu wawili tofauti ni sawa na van dame na fransis cheka.

siwezi kushindana na idrisa maana kushindana na idrisa ni sawa na teke la van dame na fransis cheka, hivyo ni vitu viwili tofauti.

Baada ya Dar Kuzidiwa Kimapato na Dodoma Makonda Awabana Wakurugenzi wa Manispaa

$
0
0
Baada ya Dar Kuzidiwa Kimapato na Dodoma Makonda Awabana Wakurugenzi wa Manispaa
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam,  Paul Makonda ameitisha kikao na wakurugenzi wa manispaa zote za mkoa kwalengo la kupitia takwimu za mapato na matumizi ya mkoa huo ili kujiridhisha kwanini wameshuka kimapato na kuzidiwa na jiji la Dodoma ambalo limepandishwa hadhi hivi karibuni.

Makonda ametoa kauli hiyo leo Agosti 3, 2018 katika hafla ya kuwakaribisha wakuu wa wilaya wapya na kuwaaga waliohamishwa vituo vya kazi, ambapo amemtaka katibu tawala wa mkoa kuipanga upya Idara ya Ardhi kwani ni maeneo yenye uongo mwingi na imekuwa na viongozi ambao wanachukuwa nyaraka za wananchi na kisha kuwapelekea matajiri na kuwanyima haki wanyonge.

“Haiingii akilini Mkoa wa Dar es Salaam kushuka kimapato pamoja na kuzidiwa ukusanyaji kodi wakati ni mkoa wa kiuchumi, kuna nyumba na viwanja vya serikali ambavyo vimechukuliwa na watu binafsi, mikataba ya unyonyaji ambayo imesainiwa na inaiminya serikali”, amesema

Makonda ameongeza kuwa viongozi wengi wa Dar es Salaam wanatoa taarifa nyingi za uongozi juu ya utendaji na utekekezaji wa miradi na mfumo wa biashara pia uangaliwe ili kuiwezesha kuwepo kwa mfumo rahisi ambao unarahisisha huduma za kitengo cha biashara kwani kumekuwa na urasimu uliopitiliza.

“Katika suala la ulinzi na usalama, wanaendelea na kuweka Camera katika maeneo mbalimbali ya jiji na baada ya hapo tutaruhusu ufanyaji wa biashara kwa masaa24”, ameongeza Makonda.

Agosti 1, 2018 wakati akizungumza na wakuu wa mikoa baada ya kuwaapisha viongozi mbalimbali aliowateua, Rais Magufuli alisema kati ya majiji yote, Dodoma inaongoza kwa makusanyo ya mapato ya Shilingi bilioni 24.2 ikiwa ni asilimia 123 ya makisio yao ya Shilingi bilioni 19.

Amesema Jiji la Dar es Salaam ambalo ni kongwe kuliko yote lilikusanya pesa kidogo tofauti na ukubwa wake ambapo lilikusanya kiasi cha Sh15.3 bilioni, Arusha (Sh10.3 bilioni), Mwanza (Sh9.3bilioni), Tanga (Sh9.1bilioni) na Mbeya (Sh4.2bilioni).

Mbunge Bwege Ataka Kukamatwa Yeye Badala ya Zitto Kabwe

$
0
0
Mbunge Bwege Ataka Kukamatwa Yeye Badala ya Zitto Kabwe
Mbunge wa Kilwa kusini –CUF Suleiman Bungara maarufu Bwege ameingilia ugomvi wa Zitto Kabwe na Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola kwa kumtaka Waziri huyo amkamate yeye kwanza kwa kuwa yeye ndiye alimuita Zitto kwenye mkutano wake.


Waziri Kangi Lugola wa kwanza (kushoto), akifuatiwa na Mbunge wa Kilwa kusini –CUF Suleiman Bungara maarufu Bwege na mwisho kulia Munge Zitto Kabwe.

Kauli hiyo ya Bwege imekuja baada ya waziri wa mambo ya ndani Kangi Lugola kumtaka mbunge wa Kigoma mjini Zitto Kabwe kujisalimisha polisi mwenyewe kwa  kosa la kutoa  kauli za kichochezi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika jimbo la Kilwa kusini mkoani Lindi.

Akizungumza na www.eatv.tv  katika mahojiano maalum kwa njia ya simu, Bwege amesema " Mh Zitto mimi ndiye niliyemwandikia barua aje kwenye mkutano wangu, naona ni kukandamiza haki na uhuru wa wabunge siyo sahihi kumkamata Zitto Kabwe kwa sababu mimi ndiye niliyemuita kama kunikamata wanikamate mimi".

Amemtaka waziri wa mambo ya ndani ya nchi Kangi Lugola kujali na kufuata sheria za nchi katika utendaji kazi wake kwa kuwa Tanzania ni nchi ya demokrasia inaendeshwa kwa mujibu wa sheria na siyo kwa amri.

Bwege amesema Waziri Lugola ni mbunge aliyepata uwaziri, hivyo anamshauri kabla hajasema jambo lolote hadharani ni vema akawatumia wanasheria waliopo kwenye wizara yake kwa ajili ya kumshauri mambo muhimu ya kuongea hadharani badala ya  kuongea mambo ambayo kisheria hayapo.

Mbunge huyu ameongeza kuwa kwa upande wake amepigiwa simu na polisi mkoani Lindi wakimtaka kuripoti kituoni hapo na baada ya kufanya hivyo kutoka na maelezo yake amefunguliwa jalada la uchunguzi katika kesi ya uchochezi.

Aidha baada ya agizo la Waziri Kangi Lugola la kutaka Zitto Kabwe aripoti kituo cha polisi mkoani Lindi ndani ya siku mbili vinginevyo akamatwe popote alipo, jeshi la polisi kupitia kwa msemaji wake Barnabas Mwakalukwa lilitoa taarifa kuwa polisi wamefungua jalada la  uchunguzi dhidi ya kauli zilizotolewa na Mbunge Zitto Kabwe ambaye pia ni kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo.

Hata hivyo kupitia kwa  Katibu Kamati ya Uenezi na Mawasiliano  Ado Shaibu chama cha ACT Wazalendo kilitoa tamko rasmi kwamba baada ya kushauriana na wanasheria wa chama wamekubaliana kwamba kiongozi wao Zitto Kabwe hatakwenda kuripoti polisi kama waziri Lugola alivyoagiza kwa kuwa waziri huyo hana mamlaka kisheria ya kutoa agizo hilo na kwamba wenye mamlaka ni polisi.

Aidha mpaka tunaripoti habari hii Zitto hajaripoti kituo chochote cha polisi kama alivyotakiwa na waziri Lugola, kwa sasa anaendelea na mikutano yake ya kampeni za uchaguzi mdogo jimbo la Buyungu kama kawaida.

Wolper: Siwezi kudanga na siku nikikamata mmoja ni mimba tu

$
0
0
Wolper: Siwezi kudanga na siku nikikamata mmoja ni mimba tu
Msanii wa Filamu Bongo, Jackline Wolper amesema kitu ambacho hawezi kufanya ni kudanga. Wolper amefunguka hayo wakati akimjibu shabiki yake katika mtandao wa Instagram kufuatia mrembo huyo kuposti picha ya Rais wa Kenya na kuandika; My second home.

Sasa shabiki huyo alitupia comment yake kwenye post hiyo ambayo ilisomeka; "Siku Wakenya Watakukata ki******m ndo utajua ni second home au ni neighbor country we endeleaa tu kudangaaaa kwa waikikuyu"

Naye Jackline Wolper akajibu; "Siwezi kudanga na siku nikikamata mmoja ni mimba tu usijali, halafu kasome ujue maana ya kudanga.. na me kudanga siwezi, wanadanga watoto, am sorry".

Jackiline Wolper amekuwa nafari za mara kwa mara nchini Kenya kutokana na biashara zake hasa ile ya ushonaji kupitia duka lake la House of Stylish.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume, nasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0


TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za:

GUMBA POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.

NTINJE:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0754741788, 0715741788, 0783741788

-DR MAGISE

Paspoti ya Mkurugenzi wa Twaweza yashikiliwa na Uhamiaji

$
0
0

Idara ya Uhamiaji inaishikilia pasi ya kusafiria ya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Twaweza, Aidan Eyakuze na kumzuia kusafiri nje ya nchi. 

Kwa mujibu wa kiongozi huyo wa TWAWEZA, pasi hiyo aliiwakilisha yeye mwenyewe baada ya kutakiwa kufanya hivyo na idara hiyo.
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live




Latest Images