Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli apokea barua kutoka kwa Rais wa China, Nkurunziza

$
0
0
Rais Magufuli apokea barua kutoka kwa Rais wa China na kwa Nkurunziza
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amekutana na Balozi wa China hapa nchini Wang Ke ambaye pamoja na kufanya nae mazungumzo amewasilisha barua kutoka kwa Rais wa China Xi Jinping.

Katika mazungumzo hayo Wang Ke amemueleza Rais Magufuli kuwa uhusiano na ushirikiano wa Tanzania na China umeendelea kukua kwa kasi kubwa hususani katika masuala ya kiuchumi, ambapo miradi mbalimbali ya maendeleo imetekelezwa na inaendelea kutekelezwa na kwamba katika kipindi cha miaka 6 iliyopita uwekezaji wa China nchini Tanzania umekuwa mara kumi kutoka Shilingi Trilioni 1.58 hadi kufikia Shilingi Trilioni 15.82.

Wang Ke amemhakikishia Rais Magufuli kuwa China itaendelea kuwa mshirika muhimu wa maendeleo ya Tanzania.

Kuhusu ombi alilolitoa Rais Magufuli wakati meli ya matibabu ya China ilipokuja hapa nchini mwezi Novemba 2017, Wang Ke amesema Rais Xi Jinping ameshafanyia kazi ombi hilo kwa kutoa udhamini wa masomo kwa madaktari 20 watakaosomea ngazi ya uzamili na uzamivu katika matibabu ya ini na uboho (bone marrow) katika Chuo Kikuu cha Shandong cha China, na pia nafasi 30 za wataalamu watakaohudhuria semina ya mafunzo ya usimamizi wa hospitali.

Rais Magufuli amemshukuru Rais Xi Jinping kwa kutoa nafasi hizo za masomo na kwa mchango mkubwa wa China katika maendeleo ya Tanzania, na amemuomba Wang Ke kufikisha ujumbe wake kwa Rais Xi Jinping kuwa Tanzania itaendeleza na kukuza zaidi uhusiano na ushirikiano wake wa kidugu na kihistoria na China.

Rais Magufuli ametoa wito kwa Wang Ke kuendelea kuwahimiza wawekezaji zaidi kuja kushirikiana na Tanzania katika uwekezaji kwenye maeneo mbalimbali kwa manufaa ya pande zote mbili na kwamba Serikali ya Tanzania itakuwa tayari kujenga mazingira mazuri ya uwekezaji na biashara.

Wakati huo huo, Rais Magufuli ameagana na Balozi wa Canada hapa nchini Ian Myles na Balozi wa Ubelgiji hapa nchini Paul Cartier baada ya Mabalozi hao kumaliza muda wao.

Baada ya mazungumzo hayo Mabalozi hao wameelezea kufurahishwa kwao na uhusiano na ushirikiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na nchi zao na wamempongeza Rais Magufuli na Serikali anayoiongoza kwa hatua kubwa za kuleta mageuzi ya kiuchumi, kuboresha utendaji kazi wa watumishi wa umma, kupambana na rushwa na kuboresha huduma za kijamii.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli amekutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi Ezechiel Nibigira ambaye amewasilisha barua kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Burundi Pierre Nkurunziza.

Aidha, Rais Magufuli amefanya mazungumzo na Nibigira, mazungumzo ambayo yamehudhuriwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Susan Kolimba na Balozi wa Burundi hapa nchini Gervais Abayeho.

Baada ya Yanga Kuwaomba Wanachama Wake Waichangie Timu Mzee Akilimali Aibuka na Kuwataka Wasichange

$
0
0
Baada ya Yanga Kuwaomba Wanachama Wake Waichangie Timu Mzee Akilimali Aibuka na Kuwataka Wasichange
KATIBU wa Baraza la Wazee la Yanga, Ibrahim Akilimali, amewataka mashabiki na wanachama wa Yanga kutokukubali kuchanga pesa zao kwa kuwa anaamini hazitokuwa katika sehemu salama.



Akilimali ametoa kauli hiyo ikiwa ni baada ya hivi karibuni klabu hiyo kutangaza mpango huo wa kuchangiwa na wanachama na mashabiki wa timu hiyo ya Jangwani.

Ikumbukwe pia, msimu uliopita Yanga SC ilianzisha mfumo huo wa kuomba michango kwa wanachama lakini hawakuwaeleza kuwa walipata shilingi ngapi.



Akizungumza na Championi, Mzee Akilimali alisisitiza kuwa si vyema kwa Yanga kuendeshwa kwa mfumo huo na badala yake viongozi waliopo madarakani kujiuzulu ili kufanya mabadiliko ya kiuongozi ambayo anaamini ndiyo suluhisho ya hayo yote.

“Nawaomba wana Yanga hasa wenye uchungu na kuipenda timu yao wasitoe hata senti moja kwa sababu hakuna usalama wa kile kitakachotolewa, nasema haya kwa akili sana na kwa uchungu sana.



“Ni bora viongozi walioko madarakani sasa wajiuzulu wote na kuipisha Yanga iingie katika uchaguzi wa viongozi wapya ambao mfumo huo wa kisasa umekuwa ukitumika na Yanga tangu mwaka 2008, hilo ndilo litakuwa suluhisho,” alisema Mzee Akilimali.

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

Ndoa Ya Abdu Kiba Yadaiwa Kupumulia Mashine

$
0
0
Ndoa Ya Abdu Kiba Yadaiwa Kupumulia Mashine
Ndoa ya staa wa Bongo fleva Abdu Kiba ambaye ni Kaka wa Ali Kiba imedaiwa kuwa katika hali mbaya na kuwa mbioni kuvunjika.

Global Publishers wanaripoti kuwa Ndoa hiyo na Abdu Kiba na mkewe Rwahida imeendelea kuwa matatani ambapo imesemwa kuwa Abdul Kiba mara nyingi amekuwa ni mtu wa kurudi nyumbani usiku na mara nyingi anashinda maskani maeneo ya Ilala Mtaa wa Arusha, kitu ambacho mkewe huyo amekiona kama sio sawa na pamoja na hayo bado anaona hakuna upendo ndani.

Baada ya Tetesi hizo gazeti hilo lilimsaka Abdu Kiba ili kupata ukweli wake lakini mara moja aliwataka wazungumze na Meneja wake ambaye mara moja alifunguka:

Hizo habari hata sisi tumezisikia kwamba watu wanasema hivyo lakini naomba kukuhakikishia hakuna ukweli wowote.

Unajua Abdul ni tofauti sana na Ally, yeye mara nyingi anapenda sana kuwa huru sana hivyo watu wakimuona pekee yake wanafikiria hivyo lakini sivyo au wengine wanasema kwa nini hamposti mkewe…”.

Lakini pia na mke wa Abdu Kiba, Rwahida amefunguka na kusema:

Hakuna ukweli wowote mimi na mume wangu tupo vizuri tu kama kawaida hakuna kitu kama hicho“.

Chid Benz Afunguka Kuhusu Bifu Lake na Harmonize

$
0
0
Chid Benz Afunguka Kuhusu Bifu Lake na Harmonize
Msanii wa muziki wa siku nyingi Chid benz amefunguka na kuongelea mahusiano yake na msanii anaefanya vizuri sasa hivi katika sanaa ya bongo fleva Harmonize na kusema kuwa hakuna tatizo kubwa kati yake na Harmonize .Na hata kama litakuwepo , anaogopa hata watu watamshangaa na kumuona kuwa yeye ana wivu.

Hakuna tatizo kati yangu na harmonize na sdhani kama kutakuwa na tatzio lolote,na kama kutakuwa na tatizo kati yangu na harmonize lazima watu watanishangaa.kama kutakuwa na ugomvi  kati yangu na yeye basi ujue kuwa watu wanaweza hata kusema kuwa mimi nina mawivu yangu tu.

Lakini pia ninachoshukuru  ni kwamba karibia wasanii wote  wananipa respect sana mimi,mimi sinaga ubaguzi na mtu yoyote , kwa sababu mimi naongea na kila mtu, na nina heshimu kila mtu pia.

Lakini pia Chid benz amefunguka na kusema kuwa yeye ni moja ya wasanii wasiopenda unafiki hata siku moja na ndio maana kila mtu anapofanya kosa huwa anataka kuonana na mtu husika na kumwambia moja kwa moja na wala hana kujificha wala kusema nje na pale ulipo.

OFA!OFA!OFA Je Umepungukiwa Nguvu za Kiume na Umetumia Dawa Bila Mafanikio?

$
0
0

OFA!OFA!OFA je umepungukiwa nguvu za kiume na umetumia dawa bila mafanikio? sasa utapona kwa sh 15000 tu ofa ni kwa watu kumi wakwanza kila siku ofa hii itadumu ndani ya wiki 2 baada ya hapo bei itakuwa nyingine na kama hujapona tunakurudishia hera yako ! 

Dawa hii ni dawa ya maajabu huwezi kuamini Ila wengi wameiamini, inatibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume na utapewa garantee ya mwezi mmoja dawa hii inapatikana hapo hapo ulipo nyumbani kwako na tutakupatia maelezo ya namna ya kuiandaa wewe mwenyewe na baada ya kuiandaa utakunywa Mara moja tu,na hautatumia dawa yoyote ya nguvu za kiume dawa hii inawafaaa watu kuanzia miaka 18 mpaka miaka 70 zaidi ya miaka hyo haitakusaidia ni dawa ya asilia haina madhara yoyote. 

Watafiti na waganga wameikubali pia hii dawa inawafaa hata wanawake wasiopata hisia za mapenzi pia tunaweza kukutumia dawa popote ulipo lakini c kwa bei ya ofa ukiitumia dawa hii unakuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 3 bila hamu kuisha na itakufanya uwe na uwezo wa kufanya tendo la ndoa muda wowote imesaidia watu zaidi yawatu 148 ndani ya mwakammoja tangu igunduliwe Dr kiboko mganga wa tiba za jadi toka kisiwani mafia pia tunatibu magonjwa mbalimbali kurudisha mpenzi aliye kuacha,biashara iliyoyumba, kuondoa mikosi, nyota na nk maelezo zaidi 

Wasiliana na Dr kiboko 0679923297 

Wale wa ‘ile hela tuma kwa namba hii’ 13 wamefikishwa Mahakamani

$
0
0

Leo August 7,2018 tunayo story kutokea Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambapo 
watu 13 wamefikishwa mahakamani hapo wakikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi ikiwemo utakatishaji fedha wa Shilingi Milioni 154.

Akiwasomea mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Kelvin Mhina wakili wa serikali mkuu, Nassoro Katuga amedai kuwa washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka 5 ambayo wameyatenda katika mikoa tofauti.

Katika kosa la kwanza la kula njama ya kutenda kosa linawakabili washtakiwa wote ambapo wanadaiwa wamelitenda kati ya March 2018 na June 2018 katika jiji la Dar es Salaam na mkoa wa Rukwa na katika maeneo mengine ya Jamhuri ya Tanzania.

Pia kosa jingine ni kusambaza taarifa za uongo kupitia mfumo wa kompyuta ambapo wanadaiwa wamelitenda March na June 2018 wakiwa Dar es Salaam na Rukwa ambapo walichapisha taarifa fupi za jumbe (Message) ili kujipatia kitu.

Wakili Katuga amedai kosa jingine ni kusambaza jumbe (message) kwa njia ya Elektroniki kati ya March na June, 2018 kwa nia ya kudanganya na kushawishi kati ya Dar es Salaam na Rukwa walisambaza kwenda kwa watu tofauti tofauti ili kuonyesha wana mamlaka hayo.

Pia katika kosa jingine la kusambaza jumbe fupi za Kielektroniki, wanadaiwa walilitenda March na June, 2018 kati ya Dar es Salaam na Rukwa walisambaza jumbe zisizotakiwa kwa njia ya Kielektroniki.

Katika kosa la mwisho wanadaiwa ni utakatishaji fedha ambapo wanadaiwa wamelitenda kati ya March na June 2018 katika maeneo ya Dar es Salaam na Rukwa.

Inadaiwa kwa pamoja walijihusisha katika ufanyaji wa muamala wa Sh.Mil 154,032,830 ikiwa ni zao la kosa la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo, Wakili Katuga amedai upelelezi haujakamilika ambapo Hakimu Mhina amesema kesi hiyo haina dhamana kwa sababu ni ya uhujumu uchumi, hivyo wataenda lumande ambapo ameahirisha kesi hiyo hadi August 21,2018.

Katika kesi hiyo washtakiwa Boniface Maombe, David Luvanda, Moshi Sungura, Amos Bosco, Lule Kadenge, Jofrey Kapangamwaka, William Nturo, Regius Mauka, Collins Basham, Francis Kapalata, Kasonde Kapela, Enock Mwandaji na Pascal Kiatu.

Ajibu 'atia doa' shughuli Yanga

$
0
0

WAKATI kikosi cha Yanga kikiwa Morogoro kujiandaa na mchezo wake wa kimataifa pamoja na Ligi Kuu Tanzania Bara, mshambuliaji nyota wa timu hiyo, Ibrahim Ajibu, hajaripoti kambini, imeelezwa. 

Ajibu hajajiunga na wenzake kwa kile kilichoelezwa kusumbuliwa na Malaria. 

Mratibu wa timu hiyo, Hafidh Saleh, alisema wachezaji wote wanaendelea vema na mazoezi, lakini Ajibu bado hajaungana na wenzake kwa kuwa ni mgonjwa. 

"Wachezaji wote wapo na wanaendelea vizuri na mazoezi, ila Ajibu bado hajafika kambini na taarifa iliyopo ni kwamba anaumwa Malaria," alisema Saleh. 

"Sifahamu lini atakuja ila kocha Zahera anaendelea na program yake ya mazoezi..., tunafanya mazoezi mara mbili kwa siku," aliongeza kusema. 

Alisema Zahera alipenda kuona wachezaji wake wote wawepo kambini ili kurahisisha program yake. 

Hata hivyo, Ajibu hakupatikana jana kuelezea hali yake na lini ataungana na wenzake wakati huu kikosi hicho cha Yanga kikiwa kimeweka kambi ya wiki mbili mkoani humo.

CHADEMA: Wabunge na Madiwani Mnaorubuniwa na CCM Ondokeni Haraka Mtupishe Tujenge Chama Chetu

$
0
0

CHADEMA: Wabunge na Madiwani Mnaorubuniwa na CCM Ondokeni Haraka Mtupishe Tujenge Chama Chetu


Naibu Katibu Mkuu wa Chadema (Zanzibar), Salum Mwalimu, amesema milango ipo wazi kwa wabunge na madiwani wa chama hicho wanaokubali kurubuniwa na kukikimbia chama.


Alisema wabunge na madiwani hao hawana dhamira ya dhati ya kuwatumikia wananchi, hivyo wanaweza kwenda wanakorubuniwa.


Alisema hayo mwishoni mwa wiki mjini hapa wakati akiwahutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara wa kumnadi mgombea udiwani wa Kata ya Bagara, Mathias Zebedayo.


"Kwa wale wenye njaa watakwenda, kwa wale wasio na hofu ya Mungu watakwenda na kwa wale ambao walikuwa hawana dhamira ya kweli watakwenda kwa kuwa walihitaji udiwani na ubunge, lakini wanaohitaji mapinduzi ya kweli watabaki,'' alisema.


Aidha, alidai Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilizoea kutumia nguvu za dola kuwaibia kura wapinzani wakaona mbinu hiyo haitoshi, sasa wameamua kuanza kuwanunua wabunge na madiwani.


Alisema Chadema inawaacha wabunge na madiwani wanaokubali kununuliwa ili waende kushirikiana na watu waliozoea wizi na ufisadi katika majimbo yao na halmashauri zao na kusababisha huduma za kijamii kukosekana.


Aliwaomba wakazi hao kumchagua mgombea udiwani wa Chadema ili waendelee kuleta maendeleo katika halmashauri hiyo kwa kuwa wameshaonyesha njia.


Alisema kwa mfano, wakati wanaichukua halmashauri walikuta makusanyo kwa mwezi ni Sh. milioni 700, lakini kwa sasa halmashauri chini ya Chadema inakusanya Shilingi bilioni mbili ambazo zinasaidia kuwaletea maendeleo.


Akimwombea kura za ndiyo mgombea wa Chadema, Mbunge wa Jimbo la Babati Mjini, Pauline Gekul, aliwataka wananchi kujipanga kulinda kura zao.


"Wale ambao wamezoea kutuonea kwenye uchaguzi na kutuibia kura zetu awamu hii tumeandaa wazee wa kimila, ili wakituhujumu kwa njia yoyote wafe mtaona watakavyolaliana hapa wakifa mmoja baada ya mwingine,'' alisema.


Mgombea udiwani wa Kata ya Bagara, Mathias Zebedayo, aliwaomba kumchagua ili aweze kuyaendeleza yale yote aliyoshindwa mtangulizi wake kwa miaka mitatu iliyopita na kutimkia CCM.

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

$
0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

Wezi wa Fedha Mtandaoni wale Tuma Kwa Namba Hii Wafikishwa Mahakamani

$
0
0
Wezi wa Fedha Mtandaoni wale Tuma Kwa Namba Hii Wafikishwa Mahakamani
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambapo
watu 13 wamefikishwa mahakamani hapo wakikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi ikiwemo utakatishaji fedha wa Shilingi Milioni 154.

Akiwasomea mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Kelvin Mhina wakili wa serikali mkuu, Nassoro Katuga amedai kuwa washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka 5 ambayo wameyatenda katika mikoa tofauti.

Katika kosa la kwanza la kula njama ya kutenda kosa linawakabili washtakiwa wote ambapo wanadaiwa wamelitenda kati ya March 2018 na June 2018 katika jiji la Dar es Salaam na mkoa wa Rukwa na katika maeneo mengine ya Jamhuri ya Tanzania.

Pia kosa jingine ni kusambaza taarifa za uongo kupitia mfumo wa kompyuta ambapo wanadaiwa wamelitenda March na June 2018 wakiwa Dar es Salaam na Rukwa ambapo walichapisha taarifa fupi za jumbe (Message) ili kujipatia kitu.

Wakili Katuga amedai kosa jingine ni kusambaza jumbe (message) kwa njia ya Elektroniki kati ya March na June, 2018 kwa nia ya kudanganya na kushawishi kati ya Dar es Salaam na Rukwa walisambaza kwenda kwa watu tofauti tofauti ili kuonyesha wana mamlaka hayo.

Pia katika kosa jingine la kusambaza jumbe fupi za Kielektroniki, wanadaiwa walilitenda March na June, 2018 kati ya Dar es Salaam na Rukwa walisambaza jumbe zisizotakiwa kwa njia ya Kielektroniki.

Katika kosa la mwisho wanadaiwa ni utakatishaji fedha ambapo wanadaiwa wamelitenda kati ya March na June 2018 katika maeneo ya Dar es Salaam na Rukwa.

Inadaiwa kwa pamoja walijihusisha katika ufanyaji wa muamala wa Sh.Mil 154,032,830 ikiwa ni zao la kosa la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo, Wakili Katuga amedai upelelezi haujakamilika ambapo Hakimu Mhina amesema kesi hiyo haina dhamana kwa sababu ni ya uhujumu uchumi, hivyo wataenda lumande ambapo ameahirisha kesi hiyo hadi August 21,2018.

Katika kesi hiyo washtakiwa Boniface Maombe, David Luvanda, Moshi Sungura, Amos Bosco, Lule Kadenge, Jofrey Kapangamwaka, William Nturo, Regius Mauka, Collins Basham, Francis Kapalata, Kasonde Kapela, Enock Mwandaji na Pascal Kiatu.

Basata Yakanusha Kuwaita Roma na Stamina ''Wamejifungia Wenyewe, Wanatafuta Kiki''

$
0
0
Basata Yakanusha Kuwaita Roma na Stamina
Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), limesema halijawaita wala kufungia wimbo wa Parapanda uliombwa na wasanii wa kundi la Rostam, Roma Mkatoliki na Stamina na kusema kuwa labda wameamua kujifungia wenyewe kwa lengo la kutafuta ‘kiki’.

Kauli hiyo inakuja ikiwa ni siku moja baada ya Roma kupitia ukurasa wake wa Instagram kuandika maneno ya kuilaumu Basata kwamba inaua vipaji na ubunifu wa wasanii na kuhoji wimbo wao huo una tatizo gani.Mbali na kuandika hayo pia alizungumza na baadhi ya vyombo vya habari na kudai kuwa amepewa
 wito wa kufika Basata.

Akilizungumzia hilo, Katibu wa Baraza la Sanaa, Godfrey Mngereza, amesema hawajaufungia wimbo huo na haujapitishwa mikononi mwao hadi sasa kwa ajili ya kuhaririwa.

"Labda kama wameamua kujifungia wenyewe ili kuufanya wimbo wao ujulikane na watu, lakini sisi hata hatujauona na kuupitia kama taratibu zetu zinavyotaka na mnajua tukifungia wimbo huwa tunatangaza sasa labda Roma awaonyeshe wapi tumesema hivyo," amesema Mngereza.

Wasanii hao, Agosti 2 waliachia wimbo huo Parapanda, unaoelezea masuala mbalimbali yanayoendelea nchini yakiwemo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii.

Wimbo huo ambao umeachiwa sauti tu (audio) katika mtandao wa YouTube, umesindikizwa na picha za hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na aliyekuwa mwanasiasa mkongwe marehemu  Kingunge  Ngombare Mwiru.

Hata hivyo, katibu huyo alikiri kuwa juzi wasanii hao wawili kufika katika ofisi za Basata kwa ajili ya kushiriki jukwaa la wasanii ambalo hufanyika kila siku ya Jumatatu katika ukumbi wao uliopo Ilala Gereji huku mada kuu kwa siku hiyo ilikuwa kuhusu kanuni mpya za sanaa zilizoanza kutumika Julai mwaka huu.

Katika jukwaa hilo anasema mmoja wa waandishi aliuliza swali kuhusu matumizi ya picha za waasisi wa  mbalimbali wa nchi hii katika sanaa, ambapo Mngereza anadai alimjibu kuwa msanii anapaswa kupata kibali kutoka kwa familia au Serikali.

"Huenda majibu haya labda ndiyo yalimfanya Roma akaondoka pale na tafsiri yake na kuandika hicho alichokiandika, lakini kiukweli hatujamfungia wala kumuita kumuhoji kuhusiana na wimbo hiyo," amesema Katibu huyo.

Hii Hapa Kazi ya Kwanza ya Jokate Kuifanya Baada ya Kuwa Mkuu wa Wilaya

$
0
0
Hii Hapa Kazi ya Kwanza ya Jokate Kuifanya Baada ya Kuwa  Mkuu wa Wilaya
Mkuu wa wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo amewataka wataalamu wa afya wilayani humo kutoa elimu ya njia sahihi za kunyonyesha watoto.

Amesema elimu hiyo itawawezesha kinamama kupata kizazi chenye afya bora na kushiriki vyema masuala ya uchumi na kijamii kwa siku zijazo.

Ameyasema hayo leo Agosti 7 muda mfupi mara baada ya kufunga maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji watoto duniani yaliyofanyika mjini humo kwa ngazi ya wilaya ya Kisarawe.

Hii ni kazi ya kwanza kwa Jokate tangu ateuliwe na kuapishwa kuwa mkuu wa wilaya ya Kisarawe.

"Uongozi wa Serikali kwa ngazi zote mnapaswa kuweka misingi imara na kuhamasisha jamii yetu ili itilie maanani kunyonyesha watoto kikamilifu."

Jokate amewakumbusha waajiri kuzingatia sheria za ajira zinazowataka kuwapa likizo ya uzazi ya siku 84 ili waweze kunyonyesha watoto wao kikamilifu.

"Hii si kwa upande wa kinamama pekee bali hata kinababa nao wanapaswa kupewa likizo ya uzazi ya siku tatu pindi wake zao wanapojifungua na hizo siku wanapaswa wazitumie kuwapa misaada mbalimbali wake zao ili waweze kunyonyesha watoto wao kikamilifu," alisema Jokate.

Awali mratibu wa lishe wilayani humo, Mwanaharusi Issa alisema takwimu zinaonyesha kuwa watoto wenye umri wa miaka mitano wenye utapiamlo mkali katika wilaya ya Kisarawe ni asilimia 0.7 huku wenye utapiamlo wa kadri ni asilimia 13.6.

Mwanaharusi amesema ili kupunguza tatizo la utapiamlo lililopo, wataalamu wa afya wanatakiwa kumuelekeza mama jinsi ya kumpakata mtoto na kumweka kwenye titi ipasavyo mara baada ya kujifungua.

Pia kumuelekeza mama aliyejifungua jinsi ya kukamua maziwa yake ili mtoto aweze kupatiwa pindi anapokua mbali.

Naye meneja wa mradi wa chakula na lishe kutoka shirika lisilo la kiserikali la Feed the Children, Silvia  Imalike  amesema takwimu za utafiti wa hali ya kidemografia na afya uliofanyika mwaka 2015 zinaonyesha kuwa asilimia 59 ya watoto wa umri wa miezi 0 hadi miezi 6 nchini wananyonyeshwa maziwa ya mama pekee.

Uhamiaji Yatoa Sababu za Kuzuia 'Passport' ya Mkurugenzi wa Twaweza

$
0
0
Uhamiaji Yatoa Sababu za Kuzuia 'Passport' ya Mkurugenzi wa Twaweza
Msemaji wa Idara ya Uhamiaji nchini, Ally Mtanda amesema kuwa wamezuia hati ya kusafiria 'Passport' ya Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi ya Twaweza Aidan Eyakuze kwaajili ya kukamilisha taratibu za uchunguzi.

Mtanda amesema kuwa wamekuwa wakifanya hivyo mara kadhaa, pindi wanapopata taarifa kutoka kwa raia wema kuwa kuna mtu wana mashaka naye.

Mtanda amefunguka hayo kupitia East Africa BreakFast ya East Africa Radio, kuwa lengo la kushikilia hati ya Eyakuze sio kumzuia kutoka nje ya nchi kama watu wanavyodai lakini ni taratibu za Idara ya Uhamiaji na watakapokamilisha uchunguzi atafahamu hatma yake ikoje.

“Ni utaratibu wa kawaida unapotuhumiwa kuwa sio raia wa Tanzania, huwa Idara ya Uhamiaji tunazuia 'passport' kwakuwa ni mali ya Rais kwa maana hiyo 'passport' ni mali ya serikali, tukikamilisha uchunguzi ukagundulika ni Mtanzania basi utarejeshewa lakini ikiwa sio utafuata taratibu zingine wanazotakiwa kufanya raia wa kigeni”, amesema Mtanda.

Kuhusiana na suala la kumzuia kutumia hati ya dharura ya kusafiria, Mtanda amejibu kuwa, “hakutumia njia sahihi ya kuomba hati ya dharura kwakuwa tulivyoshikiria 'passport' yake alitakiwa kuja makao makuu kutoa taarifa, lakini yeye hakufanya hivyo alienda kuomba kibali katika ofisi zetu za wilaya bila kujua kuwa taarifa zake tayari zipo mipaka yote kuwa hatakiwi kutoka nje ya nchi, na alifanikiwa kupata lakini alizuiwa Airport baada ya taarifa zake kuonesha hatakiwi kutoka nje ya Tanzania”.

Agosti 3, katika mkutano wake na wanahabari, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Twaweza, Aidan Eyakuze alitoa taarifa za kuzuiwa kutumia hati ya kusafiria ya dharura kwenda kuhudhuria mkutano wa kikazi jijini Kampala, baada ya Idara ya Uhamiaji kuzuia 'passport' yake.

Wanachama wa CCM Monduli Waandamana Kumkataa Mbunge Julius Kalanga Aliyetoka CHADEMA

$
0
0
Wanachama wa CCM Monduli Waandamana Kumkataa Mbunge Julius Kalanga Aliyetoka CHADEMA
Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Monduli wameandamana kwenye ofisi za chama hicho wakitaka aliyekuwa Mbunge wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA), Julius Kalanga aliyejiunga na chama hicho kufuata utaratibu ikiwemo hatua za uteuzi wa nafasi ya kugombania ubunge.

Aidha, Wakizungumza katika Ofisi hizo wamesema kuwa wamesikia taarifa za kuteuliwa kwake bila kufuata utaratibu ikiwemo kukaa vikao na wazee wa kimila Malaigwanani ili waweze kumpitisha.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Monduli amesema kuwa hajashiriki kwenye vikao na wazee wa kimila kama inavyodaiwa na baadhi ya wanachama hao na kwamba utaratibu utatumika katika kuwapata wagombea

“Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinataratibu zake, kina katiba, sheria ambazo zote zitafuatwa katika mchakato huu wa kumpata mgombea ubunge wa jimbo hili la Monduli,”amesema mwenyekiti wa chama wilaya ya Monduli, Wilson Lengima

Mkuu wa Mkoa Ataka Wahamiaji Haramu Wakamatwe Haraka na Kufungwa

$
0
0
Mkuu wa Mkoa Ataka Wahamiaji Haramu Wakamatwe Haraka na Kufungwa
Mkuu wa mkoa wa Kigoma Brigedia Jenerali Mstaafu Emmanuel Maganga ameiagiza Idara ya Uhamiaji kuanza msako wa kuwakamata wahamiaji haramu waliojificha kwenye mashamba na majumbani.

Alitoa agizo hilo jana Jumatatu Agosti 6, 2018 wakati akiwaapisha wakuu wa wilaya ya Kasulu na Buhigwe ambapo alisema wahamiaji haramu mkoani humo wanatakiwa kukamatwa na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria ili wahukumiwe kifungo.

Kaitka hatua nyingine RC Maganga alioomba mahakama kuhakikisha kesi zote za wahamiaji haramu zinapewa kipaumbele ili kupunguza msongamano wa mahabusu magerezani, ambao wanakula chakula bila kuzalisha.

Alisema kuna wahamiaji haramu na wakimbizi waliotoroka kambini wanaishi mitaani na kwenye nyumba za wananchi kinyume cha sheria, jambo ambalo halikubaliki.

Rais Wa Uganda, Yoweri Museveni Kufanya Ziara Nchini Agosti 9, 2018

$
0
0
Rais Wa Uganda, Yoweri Museveni Kufanya Ziara Nchini Agosti 9, 2018
Rais wa Jamhuri ya Uganda, Mheshimiwa Yoweri Kaguta Museveni atafanya ziara ya kikazi ya siku moja hapa nchini tarehe 09 Agosti 2018.

Lengo la ziara hiyo ni kuimarisha ushirikiano na ujirani mwema uliopo kati ya Tanzania na Uganda.

Mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, Mheshimiwa Rais Museveni atapokelewa na mwenyeji wake Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Akiwa nchini, Mheshimiwa Rais Museveni atakutana kwa mazungumzo ya faragha na Mheshimiwa Rais Magufuli yatakayofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.

Mazungumzo hayo yatafuatiwa na Chakula cha Mchana kilichoandaliwa na Mheshimiwa Rais Magufuli kwa heshima ya Mheshimiwa Rais Museveni.

Mheshimiwa Rais Museveni na Ujumbe wake wataondoka nchini siku hiyo hiyo kurejea Uganda.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma. 07 Agosti 2018

Tetemeko la ardhi latokea Rukwa na Congo

$
0
0
Tetemeko la ardhi latokea Rukwa na Congo
Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa  kipimo cha ritcher 4.4 na kina cha Kilomita 10 limetokea katika baadhi ya maeneo ya mkoa wa Rukwa na maeneo ya jirani usiku wa kuamkia leo Agosti 7, 2018 ambalo kiini chake kinaonekana kipo katika Ziwa Tanganyika, Kilometa 23 kutoka kata ya Kirando Wilayani Sumbawanga.



Aidha, katika tukio hilo hakuna madhara yoyote yaliyoripotiwa kutokea.

Kiboko ya Matatizo ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo, Mvuto wa Mapenzi na Magonjwa Sugu

$
0
0
KIBOKO YA MATATIZO YA NGUVU ZA KIUME MAUMBILE MADOGO MVUTO WA MAPENZI NA MAGONJWA SUGU Wanaume wengi wana upungufu wa nguvu za kiume na kuwa na maubile madogo ya kiume magonjwa kama kisukari presha ngiri korodani kuvimba busha, tumbo kuunguruma kujaa ngesi na kutopata choo vizuri, punyeto na NK huchangia kwa kiasi kikumbwa upotevu wa nguvu za kiume tumia dawa nzuri ya mitishamba ambayo haina madhara kwa mtumiaji ata uwe na miaka 80 inatibu na kumtuliza matatizo hayo


SUPER SHAFT NI DAWA YENYE UWEZO MKUBWA WA KUOGEZA NGUVU ZA KIUME MARA DUFU NA MAUMBILE MADOGO YA KIUME
(1) Itakufanya uwe na nguvu za ajabu ukiwa unafanya tendo la ndoa (2 ) Inaongeza hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka (3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni ndani ya dk 30 nakukupa nguvu zaidi
( 4)Itakupa nguvu za kusimamisha uume wako barabara kama msumari wakati wa tendo la ndoa

NYATI POWER INAREFUSHA NA KUNENE PESHA UUME SAIZI UTAKAVYO kuazia nchi 1 -8 unene sm 2-4 5) Itaimalisha milija ya uume iliyo legea au kusinyaa 6)lnasaidia kisafisha mishipa ya kwenye uume na hivyo kusaodia kuogeza kasi ya msukumo wa damu kwenye mishipa ya uume (7) Usaidia kuurudisha nje uume uliyoigia ndani
(8) Inasaidia kuogeza manii nyingi abazo vinaviini vya uzazi
( 9) Usaidia kutibu madhara ya punyeto, matumizi makali ya madawa ya kizungu milungi bangi na sigara

TUNATIBU MAGONJWA YOTE SUGU NGIRI KORODANI KUVIMBA BUSHA BILA KUFANYIWA OPRESHENI TENZI DUME KISUKARI PRESHA AINA ZOTE

UGONJWA WA MOYO STROKE KWIKWI, KICHOMI MIGUU KUFA NGAZI.NK

ANAPATIKANA MAGOMENI MIKUMI KARIBU NA KANISA KATOLIKI TUMAINI HEABRS CLINC NDIYO SULULISHO LA MATATIZO YOTE PIGA SIMU 0745495181 AU 0682644040

WOTE MNAKARIBISHA kama huna nafasi ya kufika ofisini kwetu huduma hii utaletewa mahali ulipo na wa mikoani mtaipata kirahisi

KWA MENGINEYO INGIA HAPA www.tumainitibaasili.co.tz

Maungo Yangu Yananipa Tabu Sana, Natongozwa Kila Kukicha

$
0
0
Mimi nimeolewa mwaka wa pili sasa ila ninakutana na vishawishi vingi kila siku, yani sina amani kila mwanaume anatamani anione nilivyo nikiwa mtupu, na hiyo ni kwa ajili ya umbo langu kiuno nyingi ila nina tako balaa na miguu mizuri, tena wanakuja kwa njia za pesa na magari lakini namuheshimu mume wangu sitoe mwanya hata kidogo japo ilinifanya nikafukuzwa hata kazi niliyokuwa nimeajiriwa baada ya kumkataa bosi



Wanawake wenzangu tujiheshimu hata kama unajijua wewe ni mzuri kama malaika muheshimu mpenzi wako usitumie kigezo cha uzuri wako kumdharau mpenzi wako na kumletea nyodo.

Mmenipataaa.

By Emily
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live




Latest Images