Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104745 articles
Browse latest View live

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume, Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0

TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 

FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 

NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Kamati ya mazishi ya Mzee Majuto yamtosa Steve Nyerere

$
0
0

Muigizaji Steve Nyerere ambaye amekuwa mstari wa mbele kuwaunganisha wasanii hasa katika kipindi cha misiba au matatizo yanayowatokea wasanii wenzao, ametoswa kwenye msiba wa Mzee Majuto. 

Hatua hiyo imekuja baada ya kuundwa kamati ya kushughulikia msiba huo ambayo imeundwa na Chama cha waigizaji Mkoa wa Kinondoni (TDFAA) pamoja na chama cha waigizaji Taifa. 

Kuondolewa kwa Steve ni kutokana na kutokuwa mwanachama  wa TDFAA,  hivyo hawezi kuteuliwa katika kamati. 

Mara baada ya Mzee Majuto kufariki, wajumbe wa kamati wakiongozwa na Simon Mwakifamba walifika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya taratibu za kuhifadhi mwili na wakatoa tamko kwamba taratibu zote za kuaga zitafanyika Muhimbili na baadaye kusafirisha kwenda Donge, jijini Tanga kwa maziko. 

Wakati hayo yakiendelea Steve Nyerere alifika Muhimbili saa 6.05 usiku, akija na utaratibu mwingine kuwa shughuli za kuaga zifanyike kwenye viwanja vya Karimjee kwa kuwa Majuto ni mtu maarufu na tayari walishaanza kukaa kikao na wasanii wenzake kwa ajili ya kuweka utaratibu wa kuagiwa kwenye viwanja hivyo. 

Hata hivyo, alipotoa wazo hilo, mmoja wa wanandugu alijitambulisha kwa jina la Ashraf, alimwambia kuwa lazima wawasiliane na ndugu wengine kwa hatua hiyo. 

Pamoja na wazo hilo kukubalika, Nyerere alibaki pembeni na hata alipoulizwa zaidi kuhusu utaratibu alikataa kwa kuwa si mwanakamati wa kamati ya maziko 

“Mimi sihusiki na chochote kwani nimekuwa nikitukanwa kwamba nakusanya fedha za rambirambi kisha nazitafuna,” anasema. 

Kamati ya mazishi ya Mzee Majuto yamtosa Steve Nyerere

$
0
0

Muigizaji Steve Nyerere ambaye amekuwa mstari wa mbele kuwaunganisha wasanii hasa katika kipindi cha misiba au matatizo yanayowatokea wasanii wenzao, ametoswa kwenye msiba wa Mzee Majuto. 

Hatua hiyo imekuja baada ya kuundwa kamati ya kushughulikia msiba huo ambayo imeundwa na Chama cha waigizaji Mkoa wa Kinondoni (TDFAA) pamoja na chama cha waigizaji Taifa. 

Kuondolewa kwa Steve ni kutokana na kutokuwa mwanachama  wa TDFAA,  hivyo hawezi kuteuliwa katika kamati. 

Mara baada ya Mzee Majuto kufariki, wajumbe wa kamati wakiongozwa na Simon Mwakifamba walifika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya taratibu za kuhifadhi mwili na wakatoa tamko kwamba taratibu zote za kuaga zitafanyika Muhimbili na baadaye kusafirisha kwenda Donge, jijini Tanga kwa maziko. 

Wakati hayo yakiendelea Steve Nyerere alifika Muhimbili saa 6.05 usiku, akija na utaratibu mwingine kuwa shughuli za kuaga zifanyike kwenye viwanja vya Karimjee kwa kuwa Majuto ni mtu maarufu na tayari walishaanza kukaa kikao na wasanii wenzake kwa ajili ya kuweka utaratibu wa kuagiwa kwenye viwanja hivyo. 

Hata hivyo, alipotoa wazo hilo, mmoja wa wanandugu alijitambulisha kwa jina la Ashraf, alimwambia kuwa lazima wawasiliane na ndugu wengine kwa hatua hiyo. 

Pamoja na wazo hilo kukubalika, Nyerere alibaki pembeni na hata alipoulizwa zaidi kuhusu utaratibu alikataa kwa kuwa si mwanakamati wa kamati ya maziko 

“Mimi sihusiki na chochote kwani nimekuwa nikitukanwa kwamba nakusanya fedha za rambirambi kisha nazitafuna,” anasema. 

Gari la Mbunge wa Chadema Lapata Ajali Mbaya

$
0
0

Gari la Mbunge wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Lucy Magereri lenye namba za usajili T 348 CSR limepata ajali eneo la Issuna wilaya ya Ikungi mkoani Singida ambapo Dereva aliyefahamika kwa jina la Thomas Maro amepoteza maisha papo hapo.

Katika gari la Mbunge alikuwepo dereva mwenyewe na alikuwa analitoa gari hilo Dodoma kulipeleka Shinyanga ndipo lilipogongana na Fuso lililokuwa linatoka Singida kwenda Dar es salaam

Aidha, dereva wa Fuso amepata majeraha madogo madogo huku mwili wa marehemu ukihifadhiwa katika hospitali ya mkoa wa Singida.

Hata hivyo, chanzo cha ajali hiyo ni dereva wa Fuso kuendesha gari upande ambao sio wake, na sasa amekamatwa yupo kituo cha Polisi kwa ajili ya mahojiano.

Mambo 5 Usiyotakiwa Kufanya Mara Baada ya Kula

$
0
0

Kiafya haishauriwi kufanya vitu vifuatavyo mara baada ya kula chakula hasa namba nne ni hatari zaidi kwa maisha yako, Kawaida mara baada ya kula chakula hasa cha usiku mtu hupendelea kujilaza au kukaa kwenye kiti, hii inatajwa kuwa ni kosa kubwa ambalo hutakiwi kulifanya mara baada ya kula, Kwa mujibu wa wataalamu wanasema kuwa kitendo hiko ni hatari sana na kinaweza kuweka afya yako katika hatari kubwa.

Kuvuta sigara

Kiafya mara baada ya kula chakula hairuhusiwi kuvuta sigara japo kuwa mvutaji wa siagara hupatwa na hamu kubwa  ya kuvuta mara baada ya kula tabia hii huhatarisha afya, hivyo inashauriwa kusubiri angalau kwa masaa kadhaa ndipo uvute endapo ni lazima sana kwani sigara ina miliki Nikotini kwa mujibu wa tafiti mbalimbali, madhara yanayotokea kwa kuvuta sigara mara baada ya kula chakula ni sawa na madhara yanayotokea kwa mtu aliyevuta sigara 10  kwa mara moja na hii huchangia mtu kupata kansa ya mapafu.

2. Kula matunda

Wanasayansi wamedhihirisha kuwa kiafya matunda yanatakiwa kuliwa kabla ya kula si mara baada ya kula kama ambavyo imezoeleka kwa watu wengi, Matunda yana enzymes na asali asili ambayo inahitaji kumeng’enywa ndani ya muda wa kutosha, hivyo kula matunda baada ya chakula inaweza kusababisha matatizo ya mmeng’enyo wa chakula pamoja na kiungulia.

3. kulala

Kulala mara baada ya kula ni kitendo ambacho hupendelewa kufanywa na mamilioni ya watu japokuwa tabia hii si nzuri kiafya, kwa mujibu wa tafiti zilizofanywa na wansayansi wa chuo kikuu cha Loannina Medical watu wanaosubiri kulala kwa kitambo kidogo mara baada ya kula wana nafasi ndogo ya kupata ugonjwa wa mshtuko na hii ndio sababu inashauriwa kukaa masaa mawili mara baada ya kula ndipo kulala.


4. kuoga

Kuoga mara baada ya kula ni moja ya kitu kibaya na hatari sana kwani kwa kufanya hivyo  unaweza kudhuru afya yako, Kuoga maji ya moto kunasababisha kuongeza kasi ya mzunguko wa damu kwenye miguu na kupunguza kasi ya mzunguko wa damu tumboni kitu ambacho kina madhara kwenye mfumo wa mmeng’enyo wa chakula.

5. Kunywa Chai

Chai ni afya lakini haitakiwi kutumiwa mara baada ya kula chakula, Kunywa chai baada ya kula inaweza kuingilia ufyonzaji wa madini wa chuma katika mwili wako kwani chai humiliki asidi  aina ya Tannic ambayo inakusanya pamoja madini ya chuma na protini kwenye chakula, matokeo yake ni kwamba 87% ya madini ya chuma hupungua kwa kiasi kikubwa hali inayopelekea mtu kukumbwa na magonjwa kama Anemia, kizunguzungu na kuchoka kutokana na kukosa madini ya chua mwilini.

Zitto Kabwe Azuiwa Kuhutubia Tarime..Mabomu Yapigwa

$
0
0

Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe jana alijikuta akikwama kumnadi mgombea udiwani wa Kata ya Turwa wilayani Tarime kupitia Chadema, Charles Mnanka,  baada ya Jeshi la Polisi kumzuia kuhutubia kwa kuusambaratisha mkutano kwa mabomu ya machozi. 

Zitto ambaye alialikwa kwenye mkutano huo pamoja na viongozi wa Chadema wakiwa kwenye eneo la tukio, alifika Mkuu wa Polisi Wilaya ya Tarime (OCD) na kuwamuru viongozi na wananchi   kutawanyika kwa sababu jeshi hilo halikuwa na taarifa ya kuwapo kwao. 

Akizungumza baada ya kutawanywa   mkutano huo na mabomu ya machozi, Zitto alilalamikia hatua ya  Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Tarime/Rorya akisema hatua hiyo ni ukiukwaji wa haki na sheria za uchaguzi. 

Alisema katika tukio hilo, zaidi ya watu 22 akiwamo Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko na mwandishi wa habari, wa Gazeti la Tanzania Daima, Sitta Tuma, walikamatwa na kushikiliwa katika Kituo cha Polisi. 

Zitto ambaye chama chake kimetangaza kuungana na Chadema katika uchaguzi wa marudio wa ubunge na udiwani unaotarajiwa kufanyika Agosti 12, mwaka huu, alisema hatua hiyo ya polisi kuvamia na kutawanya mkutano huo bila ya taarifa rasmi ni ukiukaji wa Katiba na taratibu za uchaguzi. 

“Mkutano wa hadhara wa kampeni wa sheria kwa mujibu wa Katiba na kwa mujibu wa sheria za uchaguzi, upo kwenye ratiba ya kampeni za udiwani za mgombea wa Chadema kwa mujibu wa katiba na sheria za uchaguzi,” alisema. 

Alisema alifika kuhutubia mkutano huo kwa mwaliko wa viongozi wa Chadema Mkoa wa Mara kupitia Katibu Wilaya na Mbunge Matiko na akiwa pamoja na viongozi wa ACT alifika kutimiza wajibu wake akitarajia kushirikiana na wenyeji wake. 

Akisimulia namna ilivyotokea, Zitto alisema baada ya kufika Tarime, alielezwa na viongozi wa Chadema mkoa kuwa walipata taarifa za ghafla walizopewa kwa mdomo kutoka polisi kuwa mikutano yote ya Chadema imezuiliwa kuanzia leo (jana Agosti 8) hadi Jumamosi Agosti 11 kwa sababu ambazo polisi wenyewe wanazijua. 

Alisema kwa kuwa huo si utaratibu, waliamua kufanya mkutano kwa kuwa ulikuwa umeshaandaliwa lakini polisi walivamia na kuuzingira. 

Alisema waliwazuia  kuendelea na mkutano huo wazungumzaji waliokuwa wameandaliwa ambao ni Zitto mweyewe, Mbunge wa Geita (Viti Maalumu Chadema) Peneza na Matiko (Tarime Mjini Chadema). 

Zitto alilaani kitendo hicho alichodai ni cha uvunjifu wa sheria kwa kuwa utaratibu uko wazi kwamba iwapo kuna tatizo linalolalamikiwa utaratibu unaelekeza msimamizi wa uchaguzi. 

Alisema msimamizi wa uchaguzi  anatakiwa kuwaita kwa maandishi viongozi wa kata/jimbo wanaohusika kwenye vikao vya kamati ya maadili, jambo ambalo halikufanyika, bali walichukua hatua ya kutumia polisi kuvuruga mkutano huo. 

“Kinachoonekana ni kwamba CCM wameshashindwa katika kata hii, hivyo wameamua kufanya makusudi kuvuruga uchaguzi kwa kuendesha vitisho kwa kutumia vyombo vya dola  kuwavunja moyo wananchi kushiriki uchaguzi, au kwa kufanya uchaguzi usiwepo au kuwavuruga wananchi wasijitokeze kupiga kura   wamtangaze wanayemtaka,” alisema. 

Alisema hata baada ya kukamatwa   watu 22 waliokuwa kwenye mkutano huo, yeye na mbunge wa Viti Maalumu, Upendo Peneza, walifika kituo cha polisi wanakoshikiliwa  kujua kinachoendelea na hali ya mbunge Matiko, katibu wake na mwandishi anayeshikiliwa, lakini walifukuzwa kituoni hapo. 

Alisema hadi jana jioni walikuwa wakiendelea kuwasiliana na wanasheria na viongozi wengine  kujua hatua wanazoweza kuchukua kutokana na tukio hilo. 

Zitto aliwataka wananchi wa Tarime watulie wakati wakiendelea kufuatilia na kuwasiliana na polisi makao makuu  kuhakikisha  amani haivurugiki na wananchi wanapewa uhuru na fursa ya kuchagua mgombea wanayemtaka na si anayetaka kuwekwa na CCM. 

Hata hivyo, muda mfupi baada ya kukamatwa, Sitta ambaye ni mwandishi wa gazeti la Tanzania Daima aliweza  kuandika ujumbe mfupi uliokuwa ukisomeka “Habari kaka Edwin. nipo Tarime nimekamatwa na polisi nikiwa natekeleza majukumu yangu ya uandishi wa habari. 

“Nimekamatwa baada ya polisi kuutawanya mkutano wa Chadema  wa kampeni kata ya Turwa Tarime kisha baadaye wakaanza kufyatua mabomu ya machozi. nikiwa napiga picha tukio la Mbunge wa Tarime mjini Ester Matiko ndiyo polisi wakanikimbilia na kunikamata”. 

Mwandishi na Mtetezi wa Haki za Binadamu,  Edwin Soko, aliandika barua kwa Jeshi la Polisi kumtambua  Tumma ni mwandishi na alikuwa katika eneo hilo akitekeleza majukumu yake . 

“Tuna imani Jeshi la Polisi lina weledi wa kutambua makosa ya jinai na taratibu za kushughulikia makosa ya jinai kadri sheria zinavyoelekeza. 

“Tuna imani IGP na RPC wa Tarime/Rorya watalishughulikia suala hili na mwandishi Tumma ataachiwa  aendelee na majukumu yake ya uandishi wa habari na kulinda uhusiano baina ya Jeshi la Polisi na waandishi wa habari,’’ ilieleza sehemu ya ujmbe huo kwenda Jeshi la Polisi Tarime

Maswali 10 yanayoulizwa mara kwa mara kwenye ‘Interview

$
0
0

Kujiandaa kwa kwenye usaili ni kazi nzito kwa watafutaji wengi wa ajira.

Yaani, unaanzia wapi? Unatazamia vipi maswali atakayokuuliza mwajiri?

Unajibuje maswali ya interview?

Wasiwasi wa kuwaza interview inasababisha wagombea wengi kuwa na hofu na hivyo kumfanya afanye kosa kubwa kabisa, kuongea bila mpangilio.

Njia moja ya kuzuia hii kutokea ni kufuatilia mfumo wa kujibu maswali.

Kwanza, toa mfano wa kazi uliyofanya na jinsi gani ilikusaidia kutatua tatizo linalo kumba hiyo kampuni hivi sasa. Kwa mfano, “kwenye ofisi yangu ya zamani, nilikuwa na changamoto la _ kilichokuwa na matatizo zinazofanana na hii.”



Baada ya hapo, elezea hatua ulizochukua kutatua tatizo hili.

Malizia kuelezea matokeo yake na jinsi gani ulichojifunza kwa kupitia hayo kitasaidia kampuni hiyo na changamoto zake.

Sasa, kwa kuwa unajua namna ya kujibu maswali, ujiandae na maswali yapi?

Yafuatayo ni orodha yetu ya maswali 10 yanayoulizwa mara kwa mara kwenye interview na maana yao:

Tupe maelezo mafupi kuhusu wewe

Hapa, mwajiri hataki kujua kuhusu maisha yako binafsi, familia yako au unachopenda kufanya nje ya kazini. Mwajiri anataka umueleze kwa ufupi kuhusu kazi ulizofanya. Ulifikaje hapa na unataka kufika wapi.

Kwa hili, andaa maelezo ya kazi ulizofanya isiyozidi sekunde 30 na jinsi gani kazi hizi zimekuandaa kwa nafasi hii.


Dokezo la ziada: Toa maelezo kwa kumhadithia uliyoyapitia. Usiseme “mwaka 1999 nilienda Chuo Kikuu cha Smith kusoma Masoko. Mwaka 2004 nikapata kazi yangu ya kwanza…”

Badala yake sema:

“Mapenzi yangu na masoko yalianza nilivyokuwa na miaka 12. Kuna tangazo la Coca Cola lililokuwa linaongelea kombe la dunia. Hapo ndipo nilipojua kwamba nataka kutumia maisha yangu kutoa hadithi zinazowaunganisha watu na makampuni, kwa hiyo nikajiunga na Chuo Kikuu cha Smith – yenye moja kati kozi bora ya shahada ya masoko nchini Marekani, na baada ya kumalizi nikapata kazi _. Baada ya kufanya kazi kwa muda mrefu pale, nilianza kutamani changamoto mpya ya kikazi. Ndio maana niko hapa leo”

Kwa nini tukuajiri?

Kama unataka kubaki kwenye fikra za mwajiri zaidi ya wengine, usiwape orodha ya sifa zako – mwajiri anazijua tayari kupitia CV yako. Badala yake, waambie utawasaidiaje kutatua matatizo na changamoto zao. Kutoa jibu kamilifu hapa, waeleze ni jinsi gani utawasaidia wao badala ya jinsi gani watakusaidia wewe.

Sifa yako kubwa ni nini?

Hii ni nafasi yako kuelezea sifa ulionayo ambayo unajua ni muhimu kwa kampuni hiyo na nafasi hiyo unayoitaka. Ila, usifanye kosa la kusema “mimi ni hodari kwa kuwasiliana”. Badala yake, toa maelezo kwa kuhadithia.


Kwa mfano:

“Sifa yangu kubwa ni ujuzi wangu kwenye kuwasiliana. Hii ilithibitishwa nilivyotakiwa kuonyesha maadili ya kampuni
kwenye soko jipya. Ilibidi ni fanye utafiti juu ya mahitaji na maadili ya wakazi wa eneo hiyo na kuandaa matangazo ya redio yaliyosisitiza maadili hiyo na kuonyesha namna gani kampuni hiyo ilihusiana na maadili hayo. Matokeo yake ni kwamba tuliongeza kwa 27% ndani ya mwaka mmoja. Sababu kuu ya hii ni kwamba tuliweza kuwasilisha ujumbe wetu kwenye mazingira ya pale nilipofanya tafiti.”

Upungufu wako mkubwa ni nini?

Hapa, waajiri wanataka kuona kama unajijua, kama unaweza kukubali kwamba una mapungufu na zaidi ya hapo, kama uko tayari kuzifanyia kazi.

Kwa hiyo, fikiria pungufu ambalo halina umuhimu mkubwa kwa kazi hiyo alafu ongelea hatua ulizochukua au utakazochukua kujiboresha hapo.

Usiseme kwamba huna pungufu lolote. Kila mtu ana pungufu au mapungufu.

Kwa nini unataka kufanya kazi hapa?

Hili swali pia halihusu jinsi gani kampuni itakusaidia wewe ila, jinsi gani utakuwa faida kwao.

Utafiti juu ya kampuni utakaokuwa umefanya ulivyokuwa unaandaa CV na barua ya kuomba kazi itakusaidia hapa. Fikiria jinsi gani nafasi hiyo unayotaka itasaidia kampuni na kwa nini una nia ya kufanya kazi hapo.

Waajiri wanatafuta watu wenye hamu ya kufanya kazi kwao na sio kwamba ni mtu anayetafuta ajira tu. Wanatafuta watu wenye shauku na mawazo. Huu ni muda wako wakuonyesha mawazo yako.


Kwa mfano:

“Nina nia ya kufanya kazi nanyi kwa vile nimetambua kwamba soko liko katika mabadiliko na ninataka kuwasaidia kuongezea ufanisi na kukua kwa kampuni. Najua kazi itakuwa ngumu lakini hiyo ndio changamoto ninayoitafuta hivi sasa.”

Kwa nini uliacha kazi pale ulipokuwa?

Usimseme vibaya mwajiri wala wafanyakazi wako wa zamani. Badala yake, sema tu kwamba unatafuta “changamoto mpya ya kikazi”, ila eleza zaidi kwa kuwaambia jinsi gani kazi hii itakupa changamoto ulizokosa kwenye kazi uliyoacha.

Unatarajia kupata nini kutokana na kufanyakazi hapa?

Ongelea unachotumaini kutimiza ila kuwa mkweli. Pia usiongee kwa ujumla. Chagua kitu maalum ambacho ni muhimu kwa kampuni halafu lenga hapo hapo. Ila, uwe wazi kwa kusema itachukua muda kujifunza zaidi kuhusu kampuni ili kufanikiwa zaidi.

Kwa mfano,

“Nikiwa mwalimu wa kiingereza, lengo langu ni kuongeza asilimia ya wanafunzi wanaofaulu mtihani wa taifa kuwa 85% ya darasa yangu. Najua itachukua muda kujua vizuri changamoto za wanafunzi ila, naamini nitafanikiwa”

Toa mfano ya tatizo ulilokumbwa nayo na ulichofanya kulitatua

Mradi umejiandaa kujibu hii swali, halitakupa shida.

Chagua mfano unaoonyesha ujuzi muhimu unaohitajika kwa kazi hii.

Unatarajia kupata mshaara wa kiasi gani?

Hakikisha unafanya utafiti juu ya viwango vya mishahara kwa nafasi hiyo na kwamba umeshafikiria hili. Ingia na viwango viwili, ya chini iwe unayoweza kukubali na ya juu iwe unayopenda.

Usipojiandaa na ukajaribu kuhisia, unaweza ukaishia kujionea.

Una maswali yoyote ya kutuuliza?

Mwishoni mwa interview, ni kawaida kwa mwajiri kuuliza kama una maswali kwao. Ukipewa nafasi hii, usiulizie mshahara na faida zingine. Badala yake, uliza:

Maadili ya kampuniAina ya uongoziWafanyakazi wenzakoChochote ambacho hukuelewa kuhusu kazi hiyo.Watakupa jibu baada ya muda gani?

Swali la ziada:

Baada ya miaka 5, unataka uwe umefikia wapi?

Mwajiri atakuuliza hili swali kujua kama utafuta ajira tu kupata mshahara au kama kweli unataka hii kazi kwa sababu umeipenda na inaendana na malengo yako ya kazi. Kwa hiyo, kwa kuwa wengi wetu hatujui kwa uhakika ni wapi tutakapofikia baada miaka 5, jaribu kufikiria hilo.

Tiba bora ya msongo wa interview ni kujiandaa

Ingawa interview inaweza ikakupa misongo mingi, ukijiandaa vizuri, kama chochote maishani, utashangazwa na mafanikio yako. Interview ni nafasi yako ya mwisho kumvutia mwajiri, na vidokezo vilivyoelezwa hapo juu zitakusaidia na hilo.

Kumbuka, hamna haja ya kuwa na wasiwasi ukiwa umejiandaa.

Ongeza Uume, Nguvu na Hamu ya Tendo la Ndoa Hata Kwa Wenye Kisukari na Pressure

$
0
0
Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume au ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa limezidi kuongezeka kwa kasi duniani kote na limekuwa chanzo kikubwa cha ndoa nyingi na mahusiano kukosa uaminifu kutokana na wengi kutoka nje ya ndoa ili kupata mtu atakayemtosheleza na kumfikisha kileleni. Pia udogo wa maumbile ni tatizo kubwa na limekuwa likiwakosesha wanaume wengi uwezo wa kujiamini katika tendo na kusababisha tendo hilo kutokufanyika kwa usahihi. Hili pia huchangia kwa kiasi kikubwa wanawake wengi kwenda nje ya ndoa ( MAHUSIANO) kutafuta mbadala wake.
BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Uume kusinyaa katikati ya tendo
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.

Kwa kutumia mimea tiba na matunda bila kemikali sasa
@markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL:- kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 5.5 hadi 6 @150,000/=
3.VigRX CREAM:- ni gely iliyoboreshwa mahususi kwa ajili ya kuongeza maumbile kwa wastani wa inch 6.5 hadi 8 na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200,000/=
4.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150,000/=
5.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kuweza kurudia tendo ×3. @150,000/=
BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA KIAFYA NA ZIMETHIBITISHWA
NA SHIRIKA LA AFYA DUNIANI (WHO).
KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
@markson_beauty_pr
@markson_beauty_pr
@markson_beauty_pr
WEB:www.markbeauty.org
Wasiliana nasi Popote
ulipo duniani kwa (+255)
0767447444 na
0714335378
UTAPATA HUDUMA
NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
#OngezaUume
#NguvuZaKiume
#HandsomeUpOg
#BidhaaTz

Ben Pol Afufua Penzi la Ebitoke

$
0
0
Ben Pol afufua penzi la Ebitoke
Msanii wa muziki wa kizazi kipya ambaye ilisemekana yupo kwenye mahusiano ya kimapenzi na muigizaji wa vichekesho Ebitoke, ameweka wazi juu ya mahusiano yao kwamba walishindwa kuwa wapenzi kutokana na mmoja wao kutokuwa muwazi kwa mwenzake.


Ben Pol amebainisha hayo wakati alipokuwa anazungumza kwenye kipindi cha KIKAANGONI kinachorushwa mubashara kupitia ukurasa wa kijamii wa facebook wa EATV, baada ya miongoni mwa shabiki zake waliokuwa wakimfuatilia, alipotaka kufahamu undani wa mahusiano yake na Ebitoke.

"Kiukweli sijawahi kuwa na mahusiano na Ebitoke na wala ile haikuwa kiki. Kilichotokea ni kwamba hatukufanikiwa kuwa na mahusiano licha ya wananchi au mashabiki zangu wenyewe kumpitisha kuwa mpenzi wangu kabla ya mimi sijamuona na kumkubali", amesema Ben Pol.

Pamoja na hayo, Ben Pol ameendelea kwa kusema "Ebitoke alikubarika hadi kwa wazazi wangu kutokana na yeye kuonekana kwenye vyombo vya habari akidai mimi ni mpenzi wake. Wazazi wakawa wanajua kwamba wameshapata mkwe wao. Hapakuwa na mapenzi ya kweli baina yetu ila tulikuwa tunafanya vile ili kuwaridhisha mashabiki zetu".

Mbali na hilo, Ben Pol amesema chanzo cha mapenzi hayo kushindwa kuendelea ni kutokana na Ebitoke kuogopa kusema ukweli.

Kati kati ya mwaka 2017, Ebitoke kwa mara ya kwanza aliweka hadharani hisia zake za kimapenzi juu ya msanii Ben Pol, lakini kwa bahati mbaya alishindwa kueleweka kwa haraka kwa jamii, kutokana na muonekano wake ambao watu walimzoea kumuona na kupelekea kudharauliwa huku wengine wakimshauri atafute mwanaume wa aina yake.

Juni 25 mwaka 2017, Ben Pol kupitia mitandao ya kijamii alimwagia sifa Ebitoke ikiwa kama ishara ya kukubali ombi la mwanadada huyo kuwa naye kimahusiano licha ya kuwa ukweli wa kila kitu walikuwa wanaufahamu wenyewe.

JB: Wasanii Hawakumtumia Ipasavyo Mzee Majuto

$
0
0
JB: Wasanii Hawakumtumia Ipasavyo  Mzee Majuto
Msanii wa filamu Jacob Steven (JB) amesema wasanii walichelewa kumtumia mzee Majuto kutokana na kipaji alichojaliwa

Akizungumza leo Agosti 9 wakati kuuaga mwili wa Mzee Majuto katika viwanja vya Karimjee, JB amesema pamoja na kuwahi kucheza naye filamu mbili, ikiwamo; ‘Shikamoo Mzee’ na  ‘Nakwenda kwa mwanangu’, lakini anaona bado wasanii hawakumtumia ipasavyo.

Amesema licha ya Mzee Majuto Mzee  kuigiza kwa miaka mingi lakini bado  hakuchosha machoni mwa watu na ndiyo maana filamu zake zote zilifanya vizuri.

JB amesema kifo cha Majuto kimemfunza mengi ikiwamo kuipenda sanaa kama kazi kwani ndizo zilizomfanya akapata mafaniko mbalimbali ikiwamo ya kufanya matangazo.

"Mzee Majuto ametufundisha kwamba tukiiheshimu kazi ya filamu tunaweza kuwa na mafanikio mengi kuliko tunavyofikiria na kubaki kulalamika kila siku, kwani vitu vingi alivyokuwa akivimiliki vya maendeleo vimetokana na Sanaa hii," amesema JB.

Polisi Yaanika Sababu za Kuzuia Mkutano wa Chadema Tarime

$
0
0
Polisi Yaanika Sababu za Kuzuia Mkutano wa Chadema Tarime
JESHI la polis limeeleza sababu za kumkamata  Mbunge wa jimbo la Tarime Mjini,Esther Matiko na wafuasi wake 16 akiwemo mwandishi wa habari wa Gazeti la Tanzania Daima,Sitta Tuma wakiwa kwenye mkutano wa kampeni za uchaguzi  unaoendelea ndani ya kata ya Turwa ya halmashauri ya Mji wa Tarime mkoani Mara jana kwenye viwanja vya mkuyuni kuwa ni kukiuka sheria ya uchaguzi ya mwaka 2015.

Akiongea na mwaandishi wa habari kamanda mkoa wa kipolisi Tarime/Roreya,Henry Mwaibambe amesema kuwa jeshi la polis linamshikilia Mbunge wa jimbo la Tarime Mjini,Esther Matiko Chadema na mwandhishi wa habari wa Gazeti la Tanzania Daima,Sitta Tuma na watu wengine 16 kwa kosa la kufanya mkusanyiko kinyume cha sheria.

Mwaibambe aliongeza kuwa polisi walipokea barua kutoka kwa msimamizi wa uchaguzi kata ya Turwa,Peter Julius  ikiwataka kwenda kusimamisha mikutano ya kampeni ya Chama cha demokrasia na maendeleo Chadema kwa siku Nne kuanzia Agosti,08 hadi Agost,11,2018 kutokana na sababu ya kukiuka kifungu cha sheria ya Taifa ya uchaguzi.

"Tulipokea barua kutoka kwa msimamizi wa uchaguzi kata ya Turwa,Peter Julius ambayo ilikuwa ikitutaka jeshi la polisi kwenda kusimamisha mikutano ya kampeni ya Chadema kuanzia Agosti,08 hadi Agosti,11,2018 na kuwa  chama cha NCCR Mageuzi pamoja na Chama cha mapinduzi wao wataendelea na kampeni za kuwanadi wagombea wao"alisema Mwaibambe.

Kamanda huyo pia alisema kuwa kuhusiana na mwandishi wa habari kukamatwa alikuwa sehemu ya mkutano na hakuwa sehemu ya kutekeleza majukumu yake kwasababu alikaririwa na kupigwa picha za video akiwa sehemu ya mwanaharakati sio kama mwandishi wa habari.

Kamanda Mwaibambe ameongeza kuwa bado polis wanafanya kazi yao pindi watakapokamilisha kazi ya upelelezi watuhumiwa wote watafikishwa mahakamani kujibu mashitaka yanayowakabili.

Kwa upande wake katubu wa Chama cha Demkorasia na maendeleo Chadema mkoa Mara,Chacha Heche alisema kuwa wao hawana taarifa yoyote ya kuwa mikutano yao imezuiwa na ndio sababu walikuwa wamejiandaa kwenda eneo la mkutano ndipi walishitukia polis wanakuja na magari na kuanza kutawanya wasikilizaji kwenye mkutano kituo cha Mkuyuni kata ya Turwa.

Kamati ya Mazishi ya Mzee Majuto Yamtosa Steve Nyerere Yamnyima Uongozi Kisa Hiki Hapa

$
0
0
Muigizaji Steve Nyerere ambaye amekuwa mstari wa mbele kuwaunganisha wasanii hasa katika kipindi cha misiba au matatizo yanayowatokea wasanii wenzao, ametoswa kwenye msiba wa Mzee Majuto.

Hatua hiyo imekuja baada ya kuundwa kamati ya kushughulikia msiba huo ambayo imeundwa na Chama cha waigizaji Mkoa wa Kinondoni (TDFAA) pamoja na chama cha waigizaji Taifa.

Kuondolewa kwa Steve ni kutokana na kutokuwa mwanachama  wa TDFAA,  hivyo hawezi kuteuliwa katika kamati.

Mara baada ya Mzee Majuto kufariki, wajumbe wa kamati wakiongozwa na Simon Mwakifamba walifika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya taratibu za kuhifadhi mwili na wakatoa tamko kwamba taratibu zote za kuaga zitafanyika Muhimbili na baadaye kusafirisha kwenda Donge, jijini Tanga kwa maziko.

Wakati hayo yakiendelea Steve Nyerere alifika Muhimbili saa 6.05 usiku, akija na utaratibu mwingine kuwa shughuli za kuaga zifanyike kwenye viwanja vya Karimjee kwa kuwa Majuto ni mtu maarufu na tayari walishaanza kukaa kikao na wasanii wenzake kwa ajili ya kuweka utaratibu wa kuagiwa kwenye viwanja hivyo.

Hata hivyo, alipotoa wazo hilo, mmoja wa wanandugu alijitambulisha kwa jina la Ashraf, alimwambia kuwa lazima wawasiliane na ndugu wengine kwa hatua hiyo.

Pamoja na wazo hilo kukubalika, Nyerere alibaki pembeni na hata alipoulizwa zaidi kuhusu utaratibu alikataa kwa kuwa si mwanakamati wa kamati ya maziko

“Mimi sihusiki na chochote kwani nimekuwa nikitukanwa kwamba nakusanya fedha za rambirambi kisha nazitafuna,” anasema.

Daimond Ashindwa Kujizuia Aamua Kubeba Jeneza la Mzee Majuto

$
0
0
Daimond Ashindwa Kujizuia Aamua Kubeba Jeneza la Mzee Majuto
Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Diamond Platnumz leo alikuwa miongoni mwa waombolezaji waliofika katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam kutoa heshima za mwisho kwa marehemu Mzee Majto.



Mwili wa msanii mkongwe wa filamu za Kibongo, Amri Athuman ‘King Majuto’, aliyefariki jana usiku, ulifikishwa Karimjee kuagwa kisha kusafirishwa kwenda nyumbani kwake Tanga kuzikwa.



Baada ya kuagwa katika Viwanja vya Karimjee, mwili wa marehemu umesafirishwa mpaka jijini Tanga kwa mazishi ambapo viongozi mbalimbali wamejitokeza kushiriki katika msiba huo.

Kisa Utoro Shuleni Baba Ampiga Mwanae Hadi Kifo

$
0
0
Mwanafunzi wa kidato cha nne katika Shule ya Sekondari ya Kata ya Sumbugu wilayani Misungwi  jijini Mwanza, Mariamu Tabu (18) amefariki dunia kwa kile kilichodaiwa ni kupigwa na baba yake mzazi baada ya kutohudhuria shuleni.

Akizungumza na wanahabari leo Agosti 9, Kamanda wa Polisi jijini humo Ahmed Msangi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba mtuhumiwa anashikiliwa na polisi kituo cha Misungwi na atafikishwa mahakamani kujibu mashtaka.

Kamanda Msangi amesema kuwa mama mzazi wa Mariam, Kija Mashauri amelieleza Jeshi la Polisi kuwa Agosti 6, mwanaye alikwenda shule lakini hakurudi nyumbani badala yake alirudi Agosti 7 jioni, ndipo baba yake aliuliza alipokuwa na kuanza kumpiga.

“Baba tayari tumemkamata kwa ushirikiano na wananchi, mara baada ya kutekeleza tukio la kumoiga mwanae alitaka kukimbia akazuiwa na wanakijiji, ambapo walimuwahisha mtoto katika zahanati ya kijiji kwakuwa alikuwa katika hali mbaya alifariki akiwa mapokezi”, amesema Msangi.

Juni 16, 2018 katika kilele cha siku ya Mtoto wa Afrika, ambayo kitaifa ilifanyika mkoani Arusha ambapo Tanzania ikitajwa kuongoza katika vitendo vya ukatili dhidi ya watoto kuliko uovu unaofanywa kwenye ujambazi, takwimu zilizowasilishwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto , Dkt. Faustine Ndugulile, zinaeleza kuwa watoto 41,000 walifanyiwa ukatili katika kipindi cha kuanzia mwaka 2012 hadi sasa, na kati yao 3,467 waliripotiwa kuanzia Januari hadi Disemba 2017.

Lakini pia, Idara ya Ustawi wa Jamii wizarani hapo, ilieleza kuwa asilimia 60 ya ukatili dhidi ya watoto unafanyika nyumbani, asilimia 33 ni shuleni na iliyobaki ni maeneo mengine.

NACTE yapata Mbinu ya Kuzuia Utitiri wa vyuo nchini

$
0
0
Baraza la Taifa la Elimu ya ufundi NACTE limesema tayari limetunga  kanuni na taratibu mpya ambazo zitadhibiti usajili na uendeshaji wa vyuo hapa nchini lengo likiwa ni kupunguza utitiri wa vyuo ambavyo vipo lakini badala ya kuweka mbele ubora wa elimu vimebaki kukimbizana kufanya biashara.

Naye Waziri wa Elimu ,Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako amealitaka baraza hilo kuvifungia vyuo vyote vinavyotoea huduma chini ya kiwango na hata kama kitakuwa ni chuo cha serikali.

Profesa John Kondoro ni Mwenyekiti wa Baraza la uongozi la NACTE ambaye anasema watasimamia sheria na kuhakisha vyuo vinatekeleza majukumu yake kwa misingi na sheria zilizopo.

Fahamu Njia Nne za Kulinogesha Penzi Lako Kwake Daima..!!!

$
0
0
KUPITIA safu hii uipendayo, leo ninakupa njia nne zitakazolifanya penzi lako liendelee kunoga, hata kama litakuwa limeanza kufubaa utaliamsha upya.

Wengi wamekuwa hawaelewi mambo mengi kuhusu uhusiano ndiyo maana huishia kulalamika kwamba wanapenda sana lakini mwisho wa siku huishia kutendwa.

Hakuna mtu ambaye hahitaji faraja, kila aliyekuwa na mpenzi wake anahitaji kuwa na furaha. Hakuna mtu ambaye anaingia kwenye mapenzi ili apate msongo wa mawazo, kila mtu anayediriki kuutoa moyo wake, kitu cha kwanza anachokitarajia ni faraja kisha furaha.

Ipo hivyo! Watu wengi wanakuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi huku wakiwa na matumaini kwamba hao waliokuwanao inawezekana watakuwa wapenzi wa maisha yao yote. Pasipo kujua, wakati mwingine kuna makosa hufanyika, mtu hajui afanye nini ili penzi alilonalo kwa mpenzi wake linoge, hajui ni njia zipi zitamfanya kupendwa kila siku.

Leo nitakutajia njia chache ambazo kama utazifanya, nakuhakikishia penzi lenu litashamiri zaidi ya lilivyo hivi sasa.

MPE UHURU KWANZA

Kila mtu anapenda kuwa huru, kuachwa afanye mambo yake anayoyapenda. Hakuna mtu anayependa kuingiliwa, hasa kwenye masuala ya kutumia simu yake. Kama kweli unahitaji penzi linoge, usitake kuingilia mambo yake hasa katika matumizi ya simu, unachotakiwa ni kumwambia muda ambao hupendi kuona akizungumza na simu na si kwamba kila unapoona simu yake inaita, unaichukua kwa nguvu.

Mapenzi hayapo hivyo, mpe uhuru mwenza wako. Haimaanishi mtu kama hajatulia basi kuchukua simu muda wote inapoita ndiyo kutamfanya kutulia, hapana, bali kwa kufanya hivyo utampa mbinu nyingine ya kuweza kupambana nawe. Unachotakiwa ni kumfanya kuwa huru, usimuingilie.

CHUKUA MUDA WAKO KUMTOA ‘OUT’

Wengi hukosea hapa, huwa hawapendi kwenda matembezi na wapenzi wao. Wengine hujifanya wapo bize, hata ukimwambia Jumamosi nataka tutoke out atakwambia anataka kufanya hili na lile.

Rafiki yangu, kila mtu anahitaji kuwa karibu na mpenzi wake, hakuna anayependa kuwa na mpenzi ambaye muda wote yupo bize tu. Mchukue, nenda naye sehemu. Kutoka mitoko ya mara kwa mara itawafanya muwe karibu zaidi, itawafanya muda wote mzidi kupendana, ila kama utajifanya upo bize, jua kuna mtu ataitumia nafasi hiyo kutoka na umpendaye.

PENDELEA KUFANYA UTANI

Hakuna mtu anayempenda mpenzi ambaye yupo siriazi saa ishirini na nne. Pata muda wa kukaa na kutaniana naye. Mchombeze kwa vineno vya utani, mpetipeti, mlaze kitandani na uanze kupiganapigana naye vibao vya kimahaba hata kwa kutumia mito ya kulalia.

Unapokuwa siriazi kila wakati inakuwa ni vigumu mwenzako kulifaidi penzi, pendelea kutabasamu inapobidi kila unapokuwa na mpenzi wako, siyo kila atakachokwambia wewe uso wako umekunja ndita kiasi kwamba ataonekana kukuogopa na kumtafuta mtu mwingine ambaye atahitaji kuliona tabasamu lake, atahitaji kuona akifanyiwa utani wa mahaba nk.

HEBU MSIFIESIFIE BASI

Wengi wanaogopa kuwasifia wapenzi wao, hawajui kama kila mtu duniani anapenda kusifiwa. Mpenzi wako anapovaa nguo nzuri zilizomtoa, usikae kimya, mwambie amependeza kwani hilo litamfanya kufurahi sana. Kama utakuwa na mpenzi halafu kila siku humsifii hata akifanya kitu gani, jua kwamba atajisikia vibaya, wakati mwingine atahisi hayupo sawa kwa kuwa tu hujawahi kumsifia.
Unapomsifia mpenzi wako kunamfanya kuongeza umakini katika kuvaa kwake, kununua manukato na hata jinsi atakavyosuka au kunyoa atafanya kwa ubora wa hali ya juu kwa kuwa anajua utamsifia

Kama Una Moyo Mwepesi Usisome Stori Hii, Wengi Wamelia Sana

$
0
0

Kama nilivyoanza mwanzo....usisome kama una machozi ya karibu...

“Nilipofika nyumbani usiku ule, mke wangu aliponitayarishia chakula, nilimshika mkono na kumwambia, Kuna kitu nataka nikwambie. Mke wangu alikaa chini na kula chakula kimya akiwa tayari kunisikiliza. Tena nikagundua macho yake yalionyesha anaumizwa.

Nilishindwa hata namna ya kuanza kufumbua kinywa changu. Lakini ilibidi nimwambie ili ajue nilikuwa nikifikiri nini juu yake.
Nataka kukupa talaka. Nilianza kusema kwa utulivu. Alionekana kutokereka na maneno yangu badala yake aliniuliza kwa sauti ya upole ‘kwa nini?’ Sikumjibu swali lake. Kutojibu kulimfanya akasirike. Akatupa kijiko na akanikaripia, ‘wewe si mwanamume!’ Usiku ule, hakukuwa na maongezi kati yetu. Alikuwa akilia kwa kwikwi.

Nilifahamu kwamba alitaka kujua ni nini kimetokea kwenye ndoa yetu. Lakini kwa hakika nisingeweza kumpa jibu wala sababu ya kuridhisha; alionekana si mali kitu kwangu penzi langu lilihamia kwa Mary. Sikumpenda tena mke wangu mawazo yote yalikuwa kwa Mary.

Kwa kweli nilimdharau mke wangu!
Huku moyo wangu ukijua wazi kwamba nafanya kosa, niliandika talaka ambayo ilionyesha kwamba yeye (mke wangu) angepata nyumba yetu, gari na atakuwa na hisa 30% ya kampuni yetu.

Aliangalia talaka ile na kuichana vipande vipande.
Mke ambaye tumeishi nami kwa miaka 10 alionekana mgeni machoni mwangu. Nilimuonea huruma kwa muda, rasilimali na nguvu alizopoteza lakini sikuweza kurudi nyuma kwa sababu Mary aliuteka moyo wangu kisawasawa.

Hatimaye mke wangu alilia kwa sauti mbele yangu, jambo ambalo kwa hakika nilitarajia. Kwangu mimi kilio chake kilinipa nafuu.

Wazo la kuachana na mke wangu limenisumbua kwa majuma kadhaa na sasa limeendelea kuimarika na kuwa jambo la hakika zaidi.

Siku iliyofuata nilikuja nyumbani kwa kuchelewa sana nikakuta mke wangu akiandika jambo mezani. Sikutamani hata kula chakula alichonipikia nilikwenda moja kwa moja chumbani na usingizi ulinichukua mara moja kwa sababu nilikuwa nimechoka baada ya kula raha za kufa mtu na Mary
Usiku nilishtuka usingizini mke wangu alikuwa bado akiandika.

Sikujali kabisa nikajifunika vyema shuka na kulala tena. Asubuhi yake alinikabidhi masharti ya talaka yake: hakutaka kitu chochote kutoka kwangu lakini alihitaji apate angalau mwezi mmoja wa kujiandaa kabla hajaachika. Akaomba kwamba katika kipindi hicho cha mwezi mmoja sote mimi na yeye tujitahidi kuishi maisha ya upendo au kawaida kwa kadiri itakavyowezekana.

Sababu yake ilikuwa ndogo lakini muhimu: mwanetu wa kiume alikuwa akikaribia kufanya mtihani katika mwezi uliofuata kwa hiyo hakupenda mtoto aathirike kisaikolojia kwa sababu ya kuachana kwetu. Hili halikuwa tatizo kwangu, nilikubali mpango wake. Lakini alikuwa na sharti la ziada, aliniomba nikumbuke jinsi nilivyombeba siku za fungate yetu hasa siku ya harusi yetu.

Akaniomba na kunisihi kwamba katika kipindi hicho cha mwezi mmoja niwe nambeba kutoka kitandani kwetu mpaka mlango wa kutokea kila asubuhi. Nilidhani anakaribia kuwa kichaa. Ili kufanya siku zetu za mwisho zisiwe na migogoro nilikubaliana na masharti yake ya ajabu.

Nilimsimulia Mary kuhusu masharti ya kuachana na mke wangu. Mary alicheka sana, aliona ni ujinga. ‘Hata akitumia ujanja wa namna gani talaka ni lazima’, alisema Mary tena kwa dharau. Mimi na mke wangu hatukuwahi kugusana tangu nilipomweleza dhamira ya kumtaliki. Kwa hiyo nilipombeba kwa mara ya kwanza sote tulinuniana. Mwanetu alifurahi sana na kupiga makofi nyuma yetu, ‘aah baba kambeba mama mikononi mwake’. Maneno yake yalinichoma moyoni moja kwa moja. Kutoka chumbani kwetu hadi sebuleni, halafu tena mpaka mlangoni, ni zaidi ya mita kumi nimembeba mke wangu. Alifumba macho na kusema kwa sauti laini na ya upole; usimwambie mwanetu juu ya talaka. Nilikubali kwa kichwa, ingawa nilijisikia vibaya.

Nilimuweka chini nje ya nyumba.
Alienda kituoni kusubiri basi la kazini kwake nami nikaendesha gari kwenda ofisini kwangu. Siku ya pili, zoezi lilikuwa rahisi kwetu sote. Aliegemea kifuani pangu. Nilisikia harufu nzuri ya uturi aliofukiza kwenye blauzi yake. Nikagundua kwamba sijamuangalia kwa makini mke wangu kwa kipindi kirefu sana. Nikagundua hakuwa binti tena. Kulikuwa na mikunjo usoni na nywele zake zilianza kuwa nyeupe! Ndoa yetu imekula urembo wake. Kwa dakika moja nikafikiri kwa nini namfanyia hivi.

Siku ya nne nilipombeba hisia za mapenzi kati yetu zilirejea. Huyu ni mwanamke aliyejitoa kuishi nami na tumeishi kwa miaka kumi sasa. Siku ya tano na ya sita ilikuwa wazi kwamba mapenzi yetu yalikuwa yakimea upya. Sikumwambia Mary kuhusu jambo hili. Kadiri mwezi ulivyokaribia kwisha niliona raha kumbeba mke wangu na zoezi likawa rahisi zaidi. Pengine kufanya kazi hii kila siku kuliniimarisha zaidi.

Alikuwa akichagua nini cha kuvaa asubuhi. Alichagua mavazi kadhaa hakupata linalomfaa. Kisha akaguna, ‘nguo zangu zote zimekuwa kubwa’. Nikagundua kwamba mke wangu amepungua sana, nadhani ndiyo maana niliweza kumbeba kirahisi. Ghafla jambo likanichoma... mke wangu ana uchungu na maumivu makuu moyoni mwake. Bila kujitambua nikamgusa kichwa chake. Mara mtoto wetu akatokeza na kusema ‘baba ni wakati wa kumbeba mama muende kazini’. Kwake kumuona baba akimbeba mama likawa ni jambo la furaha sana. Mke wangu alimuonyesha ishara mwanetu asogee karibu na akamkumbatia kwa upendo mkuu. Niligeuza uso wangu nisije nikabadili mawazo katika dakika ya mwisho. Kisha nikambeba mikononi mwangu kutoka chumbani, sebuleni halafu mpaka mlangoni. Mkono wake laini ulikuwa umeizunguka shingo yangu kwa upendo. Nilimkumbatia mwili wake; ilikuwa ni mithili ya siku ya ndoa yetu. Lakini wepesi wake ulinitia mashaka.

Siku ya mwisho nilipombeba nilipata shida hata kupiga hatua moja. Mtoto wetu alishakwenda shuleni. Nilimshika kwa karibu na kumwambia sikubaini kwamba maisha yetu yalikosa upendo. Nikaenda zangu ofisini…. Nikashuka garini hata bila kufunga mlango. Maana nilihisi nikichelewa tu ninaweza kubadili nilichoamua.... nikapand ngazi. Mary alifungua mlango nikamwambia, ‘Samahani, Mary, sihitaji tena kumtaliki mke wangu’. Akaniangalia kwa kustaajabu, halafu akagusa kichwa changu. Akaniuliza ‘Unaumwa?’ Nikaondoa mkono wake kichwani kwangu. ‘Samahani, Mary, nimesema sitaki kumtaliki mke wangu. Nadhani ndoa yangu haikuwa na furaha kwa sababu sikuthamini undani wa maisha yetu, mimi na mke wangu, si kwamba hatupendani. Nimetambua hilo tangu nilipombeba siku ya ndoa yetu nilitakiwa kumbeba siku zote za maisha yetu, nampenda mke wangu sitamuacha mpaka kifo kitakapotutenganisha.’
Ikawa kama Mary alizinduka usingizini. Akanizaba kibao cha nguvu, akajiegemeza mlangoni na kuanza kulia. Nikashuka ngazi na kuondoka zangu. Nikaingia kwenye duka la maua nikaagiza maua mengi mazuri kwa ajili ya mke wangu. Muuzaji akaniuliza aandike nini kwenye kadi. Nikatabasamu na kuandika “Nitakubeba kila asubuhi mke wangu mpaka kifo kitakapotutenga
nisha”. Jioni ile nilifika nyumbani na maua mikononi mwangu, tabasamu kubwa usoni nikakimbia mpaka chumbani, nikapokelewa na maiti ya mke wangu kitandani.

Kumbe mke wangu alikuwa akisumbuliwa na saratani kwa miezi kadhaa nami nilishindwa kubaini kwa sababu nilihamishia akili yangu kwa Mary. Alijua kwamba angekufa karibuni na alitaka asiniingize katika chuki na mwanetu kama ningelazimisha talaka mapema.
Angalau machoni mwa mwanangu naonekana ni mume mwema.
Mungu nisaidie Nisifike huku mimi.

Ukimuita Msichana Mwende Out Akaja na Marafiki zake Kadhaa Kukukomoa, Basi we Fanya Hili Kumfunza Adabu

$
0
0
Ukimuita Msichana Mwende Out Akaja na Marafiki zake Kadhaa Kukukomoa, Basi we Fanya Hili Kumfunza Adabu
Mwanaume mwenzangu, ukimwita msichana kwa ajili ya mtoko akaja na rafiki zake ili akukomeshe. Wewe wajali sana wale rafiki zake piga nao story, waonyeshe picha zako kadha wa kadha.

Washirikishe masuala yako ya kiofisi wape namba zako zote za simu hadi ile ya mezani. Muda wa kuondoka wapatie nauli ya kutosha kisha waelekeze unapoishi wewe na ikibidi hata wanapoishi wazazi wako.

#Myfriend! Next time ukimuita ataogopa hata kuja na mkoba atahisi utaujali mkoba zaidi yake yaani atakuja kama alivyo.

KUMWAGA Mbegu za Kiume Angalau Mara 21 Kwa Mwezi Hupunguza Hatari ya Kupata Kansa ya Tezi Dume

$
0
0
Kwa mwanaume unayehofia kuja kupata saratani ya tezi dume, kuna hatua angalau moja rahisi unayoweza kuichukua kukukinga dhidi ya hatari hii, na  urahisi wake ni kutokana na kujiondolea hatari ya kupata ugonjwa mkubwa kiasi hiki ukiwa chumbani kwako tu.

Tafiti nyingi zimehusisha utoaji wa mara kwa mara wa mbegu za kiume (manii) — kwa kufanya mapenzi, kupiga punyeto au ukiwa usingizini — na kupunguza kwa kiasi kikubwa hatari za kupata saratani ya tezi dume.

Jambo hili linaweza kuleta tofauti kiasi gani?

Kwa mujibu wa tafiti iliyochapishwa mwaka 2016 kwenye jarida la European Urology, tofauti ya kufanya na kutofanya hivi ni kubwa sana.

Wanaume 32,000 walifanyiwa utafiti kuanzia mwaka 1992 mpaka mwaka 2010 na matokeo waliyoyapata ni kwamba wanaume waliripoti kumwaga mbegu za kiume angalau mara 21 kwa mwezi walipokuwa na umri wa miaka ya 20 (20’s) maishani mwao walikuwa na asilimia 19 zaidi ya kutokutwa na saratani ya tezi dume ikilinganishwa na wale waliokuwa wakimwaga mara saba tu kwa mwezi mzima au chini ya hapo.

Kumwaga mbegu za kiume mara kwa mara ukiwa kati ya miaka ya 40 (40’s) pia inakupunguzia hatari ya kupata saratani ya tezi dume kwa asilimia 22, utafiti huo umeonesha.

“Ingawa matokeo ya utafiti wetu inabidi yathibitishwe na tafiti zinazochambua utendaji kazi wa kibaiolojia, bado matokeo haya yanasema kuwa kutoa mbegu za kiume na kufanya ngono salama katika ujana wako wote yawezekana ikawa ni mbinu yenye manufaa makubwa kwa mwanaume katika kupunguza hatari ya kupata saratani ya tezi dume,” amesema Jennifer Rider, kiongozi wa utafiti huo katika mkutano na waandishi wa habari.

Hakuna idadi maalumu kwa mwezi ambayo mwanaume anatakiwa anamwaga mbegu ili kupunguza hatari hiyo. Kilichobainishwa kutokana na utafiti huu ni kwamba huwa inategemea sana na mahusiano ya kingono kati ya wapenzi ambapo hatari ya kupata saratani hii inapungua sana endapo mwanaume anapata fursa ya kutoa mbegu za kiume mara nyingi zaidi.

Hii si mara ya kwanza kwa watafiti kuendesha utafiti kubaini ni kwa jinsi gani kutoa mbegu za kiume kuna uhusiano na kupunguza hatari za kupata saratani ya tezi dume. Mwaka 2003 timu ya watafiti wa nchini Australia walilinganisha idadi ya mwanaume kumwaga mbegu za kiume kwenye utafiti uliohusisha wanaume 2,300 — ambao nusu yao walibainika kuwa na saratani ya tezi dume. Matokeo yalionesha kuwa wale waliotoa mbegu za kiume mara tano hadi saba kwa wiki walipunguza hatari ya kupata saratani ya tezi dume kwa asilimia 36 wakilinganishwa na wale waliomwaga mara mbili au pungufu ya hapo kwa wiki.

Ingawa tafiti hizi zimekuwa zikileta matokeo yanayofanana, watafiti bado hajapata sababu maalumu ya kwa nini kumwaga mbegu za kiume mara kwa mara kunapunguza kwa kiasi kikubwa hatari za mwanaume kupata saratani hii.

Jennifer Rider aliliambia Shirika la habari la Reuters kuwa timu yake ilikuja na dhana moja inayoelezea uhusiano huo: kwamba “Utoaji wa mbegu za kiume mara kwa mara, kwa kiasi fulani, ni kielelezo cha afya bora kwa mwanaume kwa sababu wanaume waliobainika kumwaga mbegu mara chache zaidi kwenye utafiti wao — ambao hawakumwaga kabisa au walimwaga chini ya mara tatu kwa mwezi mzima — walikuwa na uwezekano mkubwa sana wa kukutwa na magonjwa mengine na pia walikufa mapema kutokana na sababu mbalimbali zaidi ya saratani ya tezi dume. Pamoja na matokeo haya, tafiti zaidi zinatakiwa kufanyika ili kuelezea uhusiano wa kibaiolojia unaohusika kupunguza hatari hii.”

Rais Magufuli Asisitiza Ushirikiano Imara kati ya Tanzania na Uganda

$
0
0
Rais John Magufuli amesema Tanzania na Uganda zitaendelea kufanya biashara kwa pamoja ili kuimarisha uchumi wa nchi zote mbili na kudumisha mshikamano kati yao.

Hayo yameelezwa leo Alhamisi Agosti 9, Ikulu jijini Dar es Salaam wakati Rais Magufuli akizungumza baada ya mazungumzo yake na  Rais Yoweri Museven ambaye aliambatana na viongozi mbalimbali kutoka nchini Uganda.

“Nimefurahia sana ziara ya mzee wetu Museven pamoja na ujumbe aliokuja nao hivyo ningependa Tanzania na Uganda tufanye biashara kwa pamoja na tuwe kama ndugu,” amesema Magufuli

Aidha rais Magufuli amesema wamekaa na Rais Museven na kukubaliana kutafuta namna ya kuzuia watu wenye lengo la kuharibu viwanda vya Uganda kutokana na hali hiyo kuwahi kutokea kipindi cha nyuma

“Kuna sukari iliwahi kuingizwa hapa nchini kumbe ilikuwa haijatengenezwa na viwanda vya Uganda bali ilikua na lengo la kuharibu viwanda vyao hivyo tumezungumza na rais Museven ili suala hilo lisijitokeze tena,” amesema Rais Magufuli

Rais Museven yupo nchini kwa ziara ya kikazi yenye lengo la kuimarisha ushirikiano na ujirani mwema uliopo kati ya Tanzania na Uganda.
Viewing all 104745 articles
Browse latest View live




Latest Images