Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

Billnass Akanusha Kuwa Chanzo cha Steve Kususia Msiba wa Mzee Majuto

$
0
0

Msanii wa bongo fleva Billnass amekanusha taarifa kuwa yeye ndio chanzo kikubwa cha kumkwaza msanii wa bongo movies Steve nyerere kujihusisha na shughuli za msiba wa Mzee Majuto na misiba mingine itakayofuata kutokana na kashfa za kuwa anahujumu pesa za ubani zinazopatikana katika misiba.

Billnass na Stev Nyerere waliwahi kuingia katika majibizano yaliyopelekea wawili hao kuonekana kushushiana heshima hasa baadaya billnass kusema kuwa steve amekiwa akisubiri misiba ili apate ulaji, hata hivyo mara baada ya kutokea kifo cha mzee majuto billnass aliandika maoni katika moja ya post iliyozunguka sana katika mtandao ikisema kuwa kipindi hiki cha msiba wa mzee ndio kipindi cha Steve kukusanya pesa za ada ya watoto.


Hata baada ya maneno mengi, Steve Nyerere alisema kuwa kwa sasa yeye atakuwa kama waombelezaji wnegine lakini hawezi kujihusisha na kitu chochote katika misiba.

Billnass afunguka “sio kweli , mimi sio chanzo cha steve kususia msiba wa mzee,kwani mbona hata mimi aliniambia kuwa nina wafuasi kumi lakini sikuacha muziki.na atambue kuwa ni maneno tu kwaio asife moyo aendelee kujitolea.”

Hata hivyo maneno hayo ya kumkashifu msanii Steve Nyerere yaliwagusa wasaniiwengi na kuamua kuliongelea hilo huku wakionekana kutopendezwa na tuhuma hizo zinazoendelea juuu ya msanii mwenzao.

Baada ya Mkuu wa Mkoa Mbeya Kung'ang'ania Vyeo Viwili CCM Kumaliza Utata Huo

$
0
0
Baada ya Mkuu wa Mkoa Mbeya Kung'ang'ania Vyeo Viwili CCM Kumaliza Utata Huo
Baada ya kuwepo kwa mkanganyiko juu ya Mkuu mpya wa mkoa wa Mbeya Mh. Albert Chalamila kushika nyadhifa mbili ya Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa na Mkuu wa mkoa wa Mbeya, CCM imesema suala hilo litaamuliwa na Kamati Kuu ya chama hicho.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Ndugu Humphrey Polepole ameongea na www.eatv.tv na kueleza kuwa kila kitu kipo kwa mujibu wa Katiba ya chama hicho hivyo suala la Albert Chalamila kuwa na kofia mbili litaamuliwa kwenye mkutano wa kamati kuu unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni.

''Kanuni ya uchaguzi ya CCM inaeleza bayana mtu mmoja kofia moja, lakini pia kanuni imetoa mamlaka kwa kamati kuu ya chama kumwezesha mtu mmoja kushika kofia mbili endapo itaona inafaa na kamati chini ya Mwenyekiti Ndugu Magufuli itakaa hivi karibuni na itaamua kama aendelee na kofia zote au moja'', - amesema.

Chalamila aliteuliwa hivi karibuni na Rais John Magufuli pamoja na viongozi wengine wa mikoa na wilaya ambapo jana kupitia mkutano wake na viongozi wa dini mkoa wa Mbeya aliweka wazi kuwa hawezi kujiuuzulu uenyekiti wa wa CCM mkoa wa Iringa labda apokee maelekezo kutoka kwa Rais ambaye amemteua.

Chalamila sio kiongozi wa kwanza wa CCM kuwa na kofia mbili ambapo alitanguliwa na wengine kama Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi aliyeteuliwa na Rais Magufuli mwaka 2016 kuwa mkuu wa mkoa huo huku akiwa mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya. Hata hivyo, katika uchaguzi wa chama hicho mwaka jana, Zambi hakutetea kiti chake.

Kiongozi mwingine ambaye amewahi kushika nyadhifa mbili ni mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Kasheku ‘Musukuma’ ambaye alikuwa Mwenyekiti wa chama hicho mkoani Geita ambaye naye hakutetea nafasi hiyo katika uchaguzi wa mwaka jana

Uingereza Yaunga Jitihada ya Rais Magufuli... Yatoa Msaada wa Bilioni 307.5

$
0
0
Uingereza Yaunga Jitihada ya Rais Magufuli... Yatoa Msaada wa Bilioni 307.5
Uingereza imetoa msaada wa shilingi Bilioni 307.5 kwa Tanzania kwa ajili ya kuunga mkono juhudi za Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika elimu, mapambano dhidi ya rushwa na uboreshaji huduma za afya.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuonesha albamu ya picha Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Uingereza Mhe. Penny Mordaunt inayoonesha Shule ya Sekondari ya Ihungo iliyobomolewa kabisa na tetemeko la Ardhi mkoani Kagera lililotokea Septemba 10, 2016 ambayo imejengwa upya na serikali ya Uingereza kupitia mpango wake wa maendelo ya elimu kupitia UKAid/DFID.

Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Uingereza Mhe. Penny Mordaunt ametangaza msaada huo leo alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais Magufuli Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Penny Mordaunt amesema fedha hizo zinatolewa kwa ajili ya kuunga mkono vipaumbele vya Rais Magufuli ambapo kati yake shilingi bilioni 124.5 zitaelekezwa katika kuinua ubora wa elimu hususani kutoa fursa ya elimu kwa watoto wa kike na wenye ulemavu, shilingi Bilioni 23.5 zitaelekezwa katika kuunga mkono juhudi za kupambana na rushwa, na shilingi bilioni 160 zitaelekezwa katika kuboresha huduma za afya.

“Tunafanya hivi ili kudhihirisha dhamira yetu ya kuimarisha na kukuza zaidi uhusiano na ushirikiano wetu, tunataka kujielekeza katika kuhakikisha Rais Magufuli anafanikisha ahadi zake kwa Watanzania na tunafurahi kuwa wadau muhimu wa hilo” amesema Mordaunt.

Rais Magufuli amemshukuru Mhe. Penny Mordaunt kwa msaada huo na amemuomba kufikisha shukrani zake kwa Waziri Mkuu wa Uingereza Mhe. Theresa May kwa mchango mkubwa ambao Uingereza hutoa kuchangia bajeti ya Serikali na kufadhili miradi mbalimbali ya maendeleo huku akimkabidhi albamu ya picha za shule ya sekondari Ihungo mkoani Kagera iliyojengwa upya baada ya kuharibika kufuatia tetemeko la ardhi lililotokea Septemba 2016 ambapo shilingi Bilioni 6 zilizotumika kujenga majengo hayo zilitolewa na ubalozi huo.

Rais wa Korea Kaskazini Kim Jong-un Avua Nguo zote na Kubakiwa na Nguo ya Ndani Kisa Joto Kali

$
0
0
Rais wa Korea Kaskazini Kim Jong-un Avua Nguo zote na Kubakiwa na Nguo ya Ndani Kisa Joto Kali
Picha mpya zilizotolewa na vyombo vya habari vya Korea Kaskazini zinamuonyesha Kiongozi wa nchi hiyo Kim Jong-un akiwa amevua shati akibaki na nguo ya ndani , alipokuwa ametembelea kiwanda cha usindikaji samaki

Picha hizo , ambazo zilijaza kurasa mbili za kwanza za Gazeti la Serikali Rodong Sinmn, zinamuonyehsa kiongozi huyo akikagua kiwanda cha samaki

Si tu mtindo wake wa mavazi ulioeleza hadithi ya wenye nacho na wasionacho nchini Korea Kaskazini, lakini muda ambao ziara hiyo imefanyika unaonyesha namna pyongyang inavyoshughulikia changamoto ya chakula na joto kali mashariki mwa bara Asia.

Kim Jong-un akijadiliana na maafisa kuhusu usindikaji wa samaki
Bwana Kim aliwasili akiwa amevalia shati la rangi ya kijivu, kofia pana na suruali pana.


Kutokana na hali ya hewa ya joto kali iliyofikia 37.8, aliamua kulivua shati lake na kuendelea na ukaguzi wake akiwa na nguo ya ndani akiwa ameichomekea kwenye suruali yake ya kijivu.

Lakini wakati kiongozi huyo akipata akipozwa na namna hii ya nguo, maafisa wake wengine wakiwemo maafisa wa kijeshi na viongozi wa kiwanda walibaki katika sare zao.

Hiki Ndicho Kilichomfanya Rais Kabila Ang’atuke DRC

$
0
0
Hiki Ndicho Kilichomfanya Rais Kabila Ang’atuke DRC
Kukubali kung’atuka kwa Rais Joseph Kabila ni ishara nzuri, lakini bado ni mapema kufurahia uchaguzi huru na wa haki katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC).

Kabila ni mwanasiasa wa DRC aliyeiongoza nchi hiyo tangu Januari 2001. Alitwaa madaraka siku kumi baada ya kuuawa kwa baba yake, Laurent Desire Kabila aliyekuwa rais wa nchi hiyo.

Juzi, kiongozi huyo alivunja ukimya kwa kumtangaza waziri wa zamani wa Mambo ya Ndani, Emmanuel Shadary kuwania urais kupitia muungano wa vyama tawala wa Common Front for Congo (CFC).

Shadary aliwasilisha fomu zake za kuwania urais kwa Tume ya Uchaguzi juzi mchana saa chache kabla ya muda uliowekwa kuchukua na kurejesha kukamilika.

Uchaguzi Mkuu nchini humo unatarajiwa kufanyika Desemba 23, baada ya kuahirishwa kwa muda mrefu na kusababisha vifo vya watu kadhaa wakiwa wanaandamana kumpinga Kabila kuwania tena urais.

Kwa mujibu wa katiba ya DRC, Kabila hakupaswa kuwania muhula mwingine, lakini hilo halingemzuia kuahirisha uchaguzi huo ambao umekuwa ukibadilishwa kalenda tangu mwaka 2016.

Kumekuwapo na shinikizo kubwa kutoka jumuiya ya kimataifa na mashirika ya kiraia nchini humo kama vile Lucha na makundi ya kanisa yanayompinga Kabila kuwania muhula wa tatu.

Licha ya kuchelewa, lakini uamuzi wa kiongozi huyo ni ishara chanya hata kwa mataifa jirani. Ishara ya matumaini kwamba inawezekana kuzuia utawala wa maisha kwa njia za amani.

Hata hivyo, bado ni mapema kujua kama mgombea huyo ana ajenda yake mwenyewe ya mageuzi kwa ajili ya Taifa hilo lenye mikoa 26 ambalo ukubwa wake unazidi kanda nzima ya Ulaya ya Kati.

Tayari fununu zimeanza kuzagaa kwamba Shadary ni rafiki mkubwa wa Kabila ambaye ataendeleza sera zake na pia taasisi zote za kiserikali zipo kwa ajili yake na huenda hilo likawa jambo litakalomsaidia kutumia rasilimali za Serikali wakati wa kampeni za uchaguzi.

Ikiwa uchaguzi utafanyika Desemba 23, 2018 kama ilivyopangwa, kinyang’anyiro kinatarajiwa kuwa cha kukata na shoka kati ya Shadary na Jean-Pierre Bemba atakayepeperusha bendera ya chama cha upinzani cha MLC. Yeyote atakayeshinda kati yao atakabiliwa na changamoto nyingi kubwa.

Pia katika miaka ya utawala wa Kabila kumekuwapo na ongezeko la wakimbizi waliokwenda nchi za jirani na ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu vikiambatana na rushwa iliyokithiri, upendeleo, viwango vya juu vya ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana na umaskini uliopindukia.

Wananchi wa Kongo hawajui kinachoitwa uchaguzi huru na wa haki mpaka sasa tangu walipopata uhuru. Lingekuwa jambo jema wananchi wakayaona mabadiliko chanya na kwa rais ajaye kufanya kazi kwa manufaa ya raia na mustakabali wa Taifa.

Shadary amesema akichaguliwa atahakikisha kwamba wananchi wanaishi kwa amani na hali yao ya maisha itakuwa bora.

Ferdinand Kambere, naibu katibu mtendaji wa chama tawala cha PPRD, anasema kwamba uteuzi wa Shadary ni alama ya ushujaa wa demokrasia nchini humo.

Nguvu ya upinzani

Kwa upande mwingine, upinzani umeelezea kwamba uteuzi wa mgombea wa chama tawala ni hatua ya ushindi wa demokrasia kwa kuwa Kabila hagombei, lakini wanatarajia uchaguzi huru na wa haki. Martin Fayulu ambaye ni mgombea wa vuguvugu Dynamique de l’opposition anasema raia ndio wanaotakiwa kuamua kupitia uchaguzi na si vyombo vya Serikali.

Anasema hawana maoni yoyote juu ya mteule huyo anayetarajiwa kumrithi Kabila na kwamba, ni mambo yao ya ndani.

Anasema ikiwa Rais Kabila amepanga njama ya kurejea madarakani baadaye kama walivyofanya Rais Vladimir Putin wa Russia na rafikiye Dmitry Medvedev, hiyo ni haki yake, lakini akaonya kwamba wanachotaka ni uwepo wa uchaguzi huru, wa wazi na wa kidemokrasia ili kuruhusu raia kujichagulia viongozi wao.

Miongoni mwa wagombea wane wa upinzani ni pamoja na Jean Pierre Bemba, Vital Kamerhe na Felix Tshisekedi ambaye ni kiongozi wa chama cha UDPS.

Wagombea watatu ni wanawake ambao wawili wameishi ugenini akiwemo Monique Mukuna. Pia yumo Waziri Mkuu wa zamani na mshirika wa Rais Kabila, Antoine Gizenga (94).

Bado kuna tetesi kwamba upinzani nchini humo umepungua nguvu ikilinganishwa na awali na hii inatajwa kuwa sababu iliyomfanya Kabila kuachia madaraka kirahisi.

Bemba ambaye aliachiwa huru na Mahakama ya Uhalifu ya Kimataifa (ICC), kwa kufutiwa makosa yote aliyokuwa anakabiliwa nayo ya uhalifu uliotokea katika nchi jirani ya Jamhuri ya Afrika ya Kati kati ya mwaka 2002 na 2003, inadaiwa kwamba hana wafusi wengi kama ilivyokuwa awali.

Mgombea mwingine wa upinzani anayetajwa kwamba hana wafuasi wengi ni Felix Tshisekedi, kiongozi wa chama cha Union for Democracy and Social Progress (UDPS). Felic ni mtoto wa mwanasiasa maarufu nchini humo, Étienne Tshisekedi aliyefariki dunia mwanzoni mwa mwaka jana.

Pia yupo mgombea huru, Tryphon Kin-Kiey Mulumba aliyewahi pia kuwa waziri katika Serikali ya Kabila.

Nguvu ya upinzani imezidi kuporomoka baada Serikali kumzuia mfanyabiashara maarufu Moise Katumbi (53), kuingia nchini humo.

Mfanyabiashara huyo tajiri na gavana wa zamani wa Mkoa wa Katanga hakuwasilisha fomu zake za kuwania urais.

Katumbi amekuwa akiishi nchini Ubelgiji tangu Mei, 2016 baada ya kutofautiana na Rais Kabila.

Huyu Hapa Mshindi wa Miss Dar Atakaye iwakilisha Dar Miss Tanzania

$
0
0

Jana Tarehe 10 yamefanyika mashindano ya kutafuta mrembo wa Dar, Miss Dar na katika kinyanganyiro hicho ameibuka Mrembo Elithabeth Michael kuwa mshindi.

Elithabeth atawakilisha mkoa wa Dar katika mashindano ya Miss Tanzania 2018

Je kunyonyana ulimi au kula mate kunaweza kuambukiza VVU? 

$
0
0

Swali: 
Je kunyonyana ulimi au kula mate kunaweza kuambukiza VVU? 

Jibu: 
Njia ya mdomo inaweza kuchangia mtu kupata VVU kama mtu atakutana na mtu mwenye VVU mwenye vidonda au michubuko mdomoni nawe pia ukawa una michubuko au vidondamdomoni, ili kuweza kupata VVU kwa njia ya mate inabidi kulambamate lita 2 jambo ambalo ni gumu. 

Kauli ya Mambosasa Kuhusu Polisi Kumshambulia kwa Kipigo Mwandishi wa Habari

$
0
0

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema polisi imeanza uchunguzi wa tukio la kupigwa kwa mwandishi wa habari wa Wapo Redio, Sillas Mbise.


Mbise anadaiwa kushambuliwa na polisi juzi Agosti 8, 2018 wakati wa mchezo kati ya Simba na Asante Kotoko ya Ghana.


Video za tukio hilo zimesambaa katika mitandao ya kijamii, zikimuonyesha Mbise akishushiwa kipigo na polisi.


Akizungumza leo Ijumaa Agosti 10, 2018 Mambosasa amesema polisi wameanza uchunguzi wa tukio hilo kwa kufungua jalada la uchunguzi wa picha hizo za video.


Amesema hiyo inakwenda sambamba na kumtaka mtendewa wa kosa hilo la kupigwa kutoa taarifa kituo cha polisi ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa.


Amesema mtu yeyote anatakiwa kutoa malalamiko yake pale anapoona ametendewa vitendo ambavyo ni kinyume cha sheria.

Ongeza Hips, Makalio, Uume, Hamu ya Tendo na Nguvu za Kiume

$
0
0

Pata bidhaa hizi kwa bei ya ofa:-👇👇
1. kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @140,000/=
2. Kuongeza shepu (hips, makalio na mapaja) kwa (a)BOTCHO MULT-PLUS 10× @230,000/=
(b)Vidonge @230,000/=
3. Kuwa mweupe na softi mwili mzima bila sugu kwa:-
(1)Mafuta @140,000/=
(11)Vidonge @150,000/=
4. Kupunguza unene na manyama uzembe @150,000/=
5. Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa:-
(a) Gely ya kupaka @140,000/=
(b) Vidonge kwa ajili ya kuongeza nguvu hata kwa wenye kisukari na BP @140,000/= (c)Handsome up original>Kifaa kinachoongeza maumbile kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @230,000/=
6. Kuondoa mvi milele zisiludi tena @150,000/=
7. Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito pamoja na hamu ya kula @130,000/=
8. Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa:-
(a) Dawa ya kunywa au kupaka @140,,000/=
(b) Mkanda wa kawaida @100,000/=
(c) micro-computer belt unaovaibret @230,000/=
9 .Kupunguza maziwa na kuyasimamisha @130,000/=
10. Kushepu miguu na kuwa minene na kuondoa kigimbi @130,000/=
11. Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @100,000/=
12. kubana uke na kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa mwanamke @110,000/=

NB: Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.
Wasiliana nasi :-
(+255) 0767447444 na
0714335378
Follow us on instagram @Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr
#cosmetics
#hipsnamakalio
#bidhaaTz
#nguvuzakiume
#punguzauzitoTz
#shepuTz
#punguzamaziwaTz
#shepuBombaTz
Mwisho wa OFA ni tar 15/8

Uingereza yatoa msaada wa Tsh. Bilioni 307.5 kuunga mkono juhudi za Rais Magufuli

$
0
0

Uingereza imetoa msaada wa Sh bilioni 307.5 kwa Tanzania kwa ajili ya kuunga mkono juhudi Rais John Magufuli katika elimu, mapambano dhidi ya rushwa na uboreshaji huduma za afya.


Akitangaza msaada huo Ikulu jijini Dar es Salaam leo Ijumaa agosti 10, baada ya kukutana na Rais Magufulu, Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Uingereza, Penny Mordaunt amesema fedha hizo zinatolewa kwa ajili ya kuunga mkono vipaumbele vya Rais Magufuli ambapo kati yake Sh bilioni 124.5 zitaelekezwa katika kuinua ubora wa elimu hususani kutoa fursa ya elimu kwa watoto wa kike na wenye ulemavu.


Aidha, Sh bilioni 23.5 zitaelekezwa katika kuunga mkono juhudi za kupambana na rushwa na Sh bilioni 160 zitaelekezwa katika kuboresha huduma za afya.


“Tunafanya hivi ili kudhihirisha dhamira yetu ya kuimarisha na kukuza zaidi uhusiano na ushirikiano wetu, tunataka kujielekeza katika kuhakikisha Rais Magufuli anafanikisha ahadi zake kwa Watanzania na tunafurahi kuwa wadau muhimu wa hilo,” amesema Mordaunt.


Kwa upande wake Rais Magufuli amemshukuru Mordaunt kwa msaada huo na amemuomba kufikisha shukrani zake kwa Waziri Mkuu wa Uingereza, Theresa May kwa mchango mkubwa ambao Uingereza hutoa kuchangia bajeti ya Serikali na kufadhili miradi mbalimbali ya maendeleo.


“Namshukuru sana Waziri Penny Mordaunt kwa kutambua juhudi zetu za kuinua elimu, kupambana na rushwa na ufisadi na kuboresha huduma za afya, msaada huu utatusaidia kuongeza nguvu kwa sababu watoto wakipata elimu bora, tukikomesha rushwa na watu wetu wakiwa na afya njema tutaweza kujenga viwanda na kukuza uchumi wetu kwa kasi zaidi” amesema Rais Magufuli.


Hata hivyo, Rais Magufuli amemuahidi Mordaunt kuwa fedha zilizotolewa zitatumika vizuri na kwamba Serikali itahakikisha uhusiano wa Tanzania na Uingereza unazidi kuimarishwa kwa kuwa inatambua kuwa Uingereza ndiyo mwekezaji mkubwa hapa nchini na imekuwa ikitoa misaada mikubwa ya fedha za walipa kodi wa Uingereza kwa ajili ya maendeleo ya Tanzania.

Waziri Mpina ampiga Jokate 'Stop' kukamata mifugo

$
0
0

Siku chache baada ya mkuu wa wilaya ya Kisarawe Mkoani Pwani, Jokate Mwegelo kufanya oparesheni ya kukata mifugo katika maeneo ya hifadhi zilizopo wilayani humo, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina amepiga marufuku tabia ya ukamataji mifugo kiholela. 

Mpina ametoa marufuku hiyo wakati akifunga maonesho ya 25 ya Nane nane Kanda ya Mashariki inayojumuisha mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani na Morogoro katika viwanja vya Mwalimu JK Nyerere mjini Morogoro. 

Luhaga Mpina amepiga marufuku tabia hiyo ambayo imekuwa ikifanywa na baadhi ya watumishi wa umma na kusababisha mifugo mingi kufia mikononi mwa Serikali kwa kukosa huduma muhimu ikiwemo maji, malisho na matibabu hivyo kusababisha hasara kubwa kwa wafugaji na Taifa. 

Mpina amesema kuwa oparesheni hizo zinapofanyika ni lazima zihusishe pia maofisa wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi ili kuwa na uelewa wa pamoja wa jambo hilo na kuepusha mifugo hiyo kuteketea kwa kukosa huduma muhimu jambo ambalo ni kinyume na haki za wanyama. 

Aidha Mpina amefafanua kuwa utaratibu unaofanyika hivi sasa wa kukamata mifugo hovyo ni ukiukwaji wa sheria namba 17 ya Magonjwa ya Wanyama ya mwaka 2003 na, Sheria ya Ustawi wa Wanyama Namba 19 ya Mwaka 2008 ambazo zinataka mifugo inapokamatwa kuzingatia masuala ya magonjwa na ustawi wa mifugo katika kipindi chote inapokuwa imeshikiliwa. 

Rushwa yamtia Kifungoni Miaka Miwili Kalusha Bwalya

$
0
0

Fifa imebaini gwiji la soka Zambia, Kalusha Bwalya alihusika na kuchukua rushwa kutoka kwa kiongozi wa Qatar, Mohammed Bin Hamman. 

Hivyo imemfungia kujihusisha na masuala ya soka kwa kipindi cha miaka miwili. 

Bwalya ni gwiji la soka nchini Zambia na alikuwa kati ya watu waliokuwa wakituhumiwa katika sakata hilo lililochukua muda mrefu. 

Imeelezwa mwaka 2009, Bwalya alipewa kitita cha dola 50,000 kutoka kwa Bin Hamman na mwaka 2011 akaongezewa nyingine dola 30,000 ili amchague kiongozi huyo wakati akigombea uongozi, nafasi ya Rais wa Fifa dhidi ya Sepp Blatter.

Vanessa Kuweka Mipango Ya Ndoa na Jux Pembeni

$
0
0

Staa wa Muziki wa Bongo fleva Vanessa Mdee ‘Vee Money’ amefunguka kuhusu Mahusiano Yake na Msanii mwenzake Juma Jux.

Vanessa na Jux wamekuwa Kwenye Mahusiano ya Kimapenzi kwa miaka zaidi ya mitano lakini Vanessa amesisitiza kuwa hana haraka ya kuingia kwenye ndoa na mpenzi wake huyo.

Kwenye mahojiano na Kipindi cha Shilawadu cha Clouds Tv, Vee Money amesema hayo baada ya kuhojiwa kuhsuu mipango ya ndo n Jux ambapo ameweka wazi hivi sasa anafurahia Mahusiano Yake na Jux.

Vanessa na Jux wamekuwa Kwenye headlines kwa ajili ya Tour yao ya ‘In Love and Money’ ambayo imevunja rekodi kwa kuwa Tour ya kwanza kufanya na wasanii wawili ambao ni wapenzi na Kujaza mashabiki.

 

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

$
0
0

Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

Install Application ya Ud

Harmonize Alivyofichwa Msikitini Tanga Kuhofia Usalama Wake

$
0
0
Harmonize Alivyofichwa Msikitini Tanga Kuhofia Usalama Wake
Msanii wa muziki kutoka WCB, Harmonize aka Konde Boy amelazimika kufichwa ndani ya msikiti wa Chuda kwasababu za kiusalama kufuatia idadi kubwa ya watu kumzonga wakati mwili wa Mzee Majuto ulipokuwa ukiswaliwa.



Harmonize hii leo amefika kwenyemazishi hayo jijini Tanga mara baada ya Diamond kuonekana katika tukio la kuuaga mwili wa Mzee Majuto hapo jana Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Taarifa kutoka jijini Tanga zinaeleza kuwa, Harmonize ametolewa kwenye eneo hilo kupitia gari la Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigela.


Kocha Jose MourinhoAtibuana na Uongozi wa Manchester United

$
0
0
 Kocha Jose MourinhoAtibuana na  Uongozi wa Manchester United
LICHA ya kutoweka wazi juu ya mchakato wa ndani ulivyo lakini habari ni kuwa Kocha Jose Mourinho amekasirishwa na kitendo cha uongozi wa timu yake ya Manchester United kushindwa kumpatia fedha za usajili alizohitaji.



Dirisha la usajili lilifungwa juzi Alhamisi na kocha huyo bado alikuwa na matumaini ya kufanya usajili hasa wa beki wa kati, baada ya kukwama kote akataka kumsajili mkongwe wa Atletico Madrid, Diego Godin kwa pauni 18m lakini beki huyo akaamua kuendelea kubaki Hispania.



Licha ya kuzungumza na waandishi wa habari juzi akiwa na utulivu, habari za ndani zinaeleza kuwa kocha huyo alikuwa na hasira kali kabla ya mchezo wa jana ambapo timu yake ilicheza dhidi ya Leicester City kwenye Uwanja wa Old Trafford.



Mourinho alikuwa tayari kutumia hata pauni milioni 100 kufanya usajili wa beki wa kati lakini hilo lilipingwa na Makamu Mwenyekiti wa klabu, Ed Woodward. “Najua maneno mnayotaka niseme lakini
siwezi kusema chochote,” alisema Mourinho kabla ya kuivaa Leicester mara baada ya kuhojiwa na waandishi wa habari.



Kocha huyo amesema mashabiki wasubiri kuona Novemba au Desemba kuona mwelekeo wa timu yao utakuwaje. Mourinho alihitaji wachezaji watano baada ya msimu uliopita kumalizika lakini hadi dakika za mwisho akawa anahitaji angalau wawili lakini nao hakuwapata. Ndani ya miaka miwili aliyodumu klabuni hapo, kocha huyo ameshatumia pauni milioni 375 kwa ajili ya usajili.

Wizara Ya Mambo Ya Ndani Yatoa Tamko Kuhusu Akaunti Feki Ya Instagram Inayodaiwa Kuwa Ya Waziri Kangi Lugola

$
0
0
Wizara Ya Mambo Ya Ndani Yatoa Tamko Kuhusu Akaunti Feki Ya Instagram Inayodaiwa Kuwa Ya Waziri Kangi Lugola
Kumekuwepo na akaunti feki ya mitandao ya kijamii ya instagram ambayo imesajiliwa kwa jina la ‘‘kangilugola’’ na imekuwa ikitoa taarifa mbalimbali kwa jamii kuhusu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Wizara hii kwa ujumla.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi  inapenda kuujulisha Umma wa Watanzania kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mheshimiwa Kangi A. Lugola hana akaunti yoyote kwenye mitandao ya Kijamii  hivyo akaunti yoyote  iliyosajiliwa kwa jina la kangilugola ni feki.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi inatoa onyo kali kwa mtu yeyote anayejihusisha na kutumia jina la Kangi Lugola kusajili akaunti hiyo feki sambamba na kutoa taarifa za Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Wizara kwa ujumla kupitia akaunti hiyo feki, na yeyote atakayebainika kujihusisha na jambo hili hatua za kishera zitachukuliwa dhidi yake.

Aidha taarifa zote za Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi zitatolewa kupitia tovuti ya wizara kwa anuani ya www.moha.go.tz na twitter ya  Wizara kwa akaunti ya MsemajiMamboyaNdani.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Wizara ya Afya Yafunguka Kuhusu Mlipuko wa Ugonjwa wa Ebola

$
0
0
Wizara ya Afya  Yafunguka Kuhusu Mlipuko wa Ugonjwa wa Ebola
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inaendelea kutoa taarifa kuhusu mlipuko wa ugonjwa wa Ebola katika nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Nchi hiyo ya DRC imetangaza tena kuwa na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola mnamo tarehe 1 mwezi Agosti, 2018, ambapo jumla ya wagonjwa 26 na vifo 10 vilitolewa taarifa na wagonjwa 4 kati yao walithibitishwa kimaabara kuwa na ugonjwa wa Ebola. Wagonjwa hawa wametokea katika vijiji/Maeneo ya Mangina ikiwa ni kama km 30 tu magharibi mwa mji wa Beni kwenye jimbo la Kivu Kaskazini linalopakana na nchi ya Uganda ikiwa ni kama km 100 tu, na pia likiwa karibu sana na nchi ya Rwanda.

Huu ni mlipuko wa 10 wa ugonjwa wa Ebola kutokea nchini DRC, na umetokea wiki moja baada ya nchi hiyo kutangaza kuisha kwa mlipuko mwingine uliotokea mwezi Mei mwaka huu ambao ulikuwa katika jimbo la Equator, Magharibi mwa DRC, umbali wa zaidi ya km 2,000 kutoka eneo la huu mlipuko mpya uliotokea.

Ndugu wanahabari,
HADI SASA HAPA NCHINI TANZANIA HAKUNA MGONJWA YOYOTE ALIYEHISIWA AU KUTHIBITISHWA KUWA NA VIRUSI VYA EBOLA. Hata hivyo, kugunduliwa kwa ugonjwa huu kwenye jimbo la Kivu Kaskazini linalopakana na nchi za Uganda na Rwanda ni jambo la kutuweka kwenye wasi wasi kwani eneo hili liko karibu sana na nchi yetu kuliko eneo lingine lolote ambako ugonjwa huu umeshawahi kutokea kwenye nchi ya DRC. Hivyo nchi yetu ipo hatarini kuambukizwa ugonjwa huu kutokana na ukaribu na muingiliano wa watu, hasa kuhusiana na wasafiri wanaotoka na kuingia hapa nchini.

Kwa sababu hizi, watanzania hatuna budi kuchukua tahadhari ya hali ya juu ili kujikinga na kudhibiti na ugonjwa wa Ebola.  Hivyo Wizara inapenda kutoa tahadhari ya ugonjwa huu kwa wananchi wote katika Mikoa yote ya Tanzania, lakini hasa ile inayopakana na nchi jirani za DRC, Uganda na Rwanda. Mikoa hiyo ni pamoja na Mwanza, Kagera, Kigoma, Katavi, Rukwa na Songwe. Aidha tahadhari na hatua stahiki zichukuliwe katika maeneo yote ya mipakani ambapo abiria wanaingia nchini kutoka nchi jirani.

Ugonjwa wa Ebola

Ugonjwa wa Ebola husababishwa na virusi vya Ebola ambavyo huambukiza kwa njia zifuatazo;
 Kugusa Damu au majimaji kutoka kwa mtu aliyeambukizwa ugonjwa huo,
  Kugusa maiti ya mtu aliyekufa kwa ugonjwa huo,
 Kugusa wanyama (Mizoga na wanyama wazima) walioambukizwa kama vile Sokwe na Swala wa msituni.
Dalili za Ugonjwa
Dalili za Ugonjwa huanza kuonekana kwa mtu aliyeambukizwa baada ya siku 2 hadi 21 tangu kupata maambukizi. Dalili hizo ni pamoja na;
    Homa kali ya ghafla,
    Kulegea kwa mwili,
    Maumivu ya misuli,
    Kuumwa kichwa na vidonda kooni.
  Mara nyingi dalili hizo hufuatiwa na kutapika, kuharisha, vipele vya ngozi na pia figo na Ini kushindwa kufanya kazi.
  Kwa baadhi ya wagonjwa kutokwa na damu ndani na nje ya mwili.
Namna ya Kujikinga na ugonjwa wa Ebola:

Ugonjwa wa Ebola unaweza kuzuilika. Njia kuu za kujikinga na ugonjwa huu ni:-
Kuepuka kugusa au kuingiwa na mate, damu, mkojo, jasho, kinyesi, machozi na majimaji mengine yanayotoka mwilini mwa mgonjwa mwenye dalili za ugonjwa  wa Ebola
    Kuepuka kushughulikia maiti ya mtu aliyefariki akiwa na dalili za Ebola; badala yake watoe taarifa kwa uongozi wa kituo cha huduma za Afya kwa ushauri.
  Kuepuka kula nyama za Wanyama wa porini kama sokwe, swala na popo na pia kugusa mizoga ya Wanyama hao
  Kuepuke mila na desturi zinazoweza kuchelewesha kupata huduma muhimu na kuzidi kueneza ugonjwa wa Ebola.
  Kuzingatia usafi wa mwili
  Kutoa taarifa mapema kwa viongozi wa Serikali na wa huduma za Afya katika ngazi zote pale anapotokea mtu mwenye dalili za Ebola.
 Kuwahi katika vituo vya huduma za Afya pale mtu anapoona dalili za ugonjwa huu.

Hatua zilizochukuliwa na zinazoendelea kuchukuliwa na Wizara kufuatia kupatikana kwa taarifa ya Ugonjwa huu huko DRC

Kufuatia kuwepo kwa taarifa hizi tangu mwezi Mei 2018, hatua zifuatazo zinaendelea/zimechukuliwa na Wizara ili kujiandaa kukabiliana na mlipuko huo:
Kufanya tathmini ya utayari wa kukabiliana na ugonjwa wa Ebola nchini (Operational readiness assessment) kwa nchi nzima kwa kushirikiana na WHO na kuainisha mapungufu ambayo yanapaswa kufanyiwa kazi. Mapungufu hayo yanaendelea kuyafanyiwa kazi ili kujenga uwezo na utayari katika nchi yetu.
 Tumetengeneza mpango mkakati wa kujiandaa na kupambana na mlipuko wa Ebola endapo utatokea nchini (Costed Ebola Contingency Plan). Mpango huu umeandaliwa kwa kushirikiana na WHO. Mpango umeainisha maeneo ya kujenga uwezo kwa wakati huu wa kujiandaa, pamoja na hatua za kuchukua endapo ugonjwa utaingia ikiwa ni pamoja na gharama zake.
Tumefanya mafunzo ya Timu za dharura (Rapid Response Teams) ngazi ya Taifa na katika Mikoa ya Dar es Salaam, Songwe, Rukwa, Katavi, Kigoma na Kagera
Tumeimarisha ufuatiliaji wa wasafiri mipakani (travellers entry screening) kwa kutumia vifaa vya kupima joto la mwili (thermo scanners) na fomu maalum za wasafiri
 Wizara imepokea vifaa vya kukabiliana na Ebola kutoka WHO vikiwemo; Thermo scanners, Vifaa Kinga, au PPE, kama vile gloves, body bags, vifaa vya ufungashaji wa sampuli nk. Vifaa hivyo vimeanza kusambazwa mikoani kupitia MSD
 Uelimishaji wa umma umefanyika na unaendelea kufanyika kwa kupitia vyombo vya habari vya kitaifa na kijamii, na mitandao ya kijamii. Vile vile vipeperushi na mabango vinaendelea kuandaliwa
Vikao vya uratibu vimefanyika katika ngazi ya taifa na mikoa ambayo ipo katika hatari zaidi. Pia ufuatiliaji wa karibu unaendelea kupitia Kituo cha ufuatiliaji wa magonjwa ya dharura cha Wizara (Public Health Emergency Operation Centre is on “High Alert”)
Wataalam kutoka ngazi ya Taifa kwa sasa wako katika mikoa ya Kigoma Katavi Rukwa Kagera Kilimanjaro Mwanza Songwe na Mbeya kufanya tathmini ya utayari katika ngazi ya mikoa na Wilaya (Readiness Assessment)
 Maandalizi yanaendelea kwa ajili ya kutekeleza kazi nyingine kama ifuatavyo:
 Kufanya mafunzo katika mikoa iliyo salia ikiwemo Mwanza, Kilimanjaro na Mbeya ambayo imesalia katika ile mikoa nane iliyo katika hatari zaidi
 Mafunzo ya waandishi wa habari 30 (media orientation)
Zoezi la udhibiti wa matukio ya dharura (simulation exercise) katika ngazi ya Taifa
 Mafunzo kwa wasfirishaji wa sampuli kwenda katika maabara



Hitimisho
Nawaomba Wakuu wa Mikoa na Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri wote nchini kuchukua Tahadhari na kuendelea kuelimisha wananchi wote juu ya ugonjwa huu na kuwataka kutokuwa na hofu ila kuendelea kuchukua tahadhari za kujikinga na ugonjwa huu kwani mpaka sasa hakuna mtu aliyethibitishwa kuugua ugonjwa huu hapa nchini.

Aidha Wizara itaendelea kushirikiana na sekta mbalimbali katika kuimarisha ufuatiliaji na kuendelea kutekeleza mikakati ya kudhibiti ili ugonjwa huu usiingie nchini. Vilevile Wizara itaendelea kutoa taarifa pamoja na Elimu kwa Jamii kadri itakavyohitajika.

Imetolewa na
Ummy A. Mwalimu (Mb)
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto
10/08/2018

Mzee wa Miaka 70 Afunga Smartphone 11 Kwenye Baiskeli Ili Kucheza Game

$
0
0
Mzee wa miaka 70 afunga smartphone 11 kwenye baiskeli ili kucheza game
Mzee wa miaka 70 nchini Taiwan anayefahamika kwa jina la Chen San-yuan amefunga jumla ya simu 11 kwenye baiskeli yake ili aweze kucheza game kila anapokwenda.

San-yuan ambaye ni mkazi wa New Taipei hutumia saa 20 kucheza michezo ya Pokemon kabla ya simu na betri zake tisa hajaziweka kwenye baiskeli kuanza safari ya kutembea nazo.

Wakati, Feng Shui akisema kuwa hutumia kiasi cha pauni 1,165 kwaajili ya kulipia game hilo. Chen kwa sasa amepewa jina la utani akiitwa ‘Uncle Pokemon’.

Kwaupande wake amesema kuwa kucheza gemu kunamsaidia kusahau maradhi aliyokuwa nayo ya Alzheimer ambayo humsumbua lakini pia humuunganisha nawatu wengine wenye umri kama wake. Chen ametekwa na Pokemon baada ya kufundishwa na mjukuu wake namna ya kucheza gemu hilo mwaka 2016 .

Bill Nass: Mimi si Chanzo cha Steve Nyerere Kususia Msiba wa Mzee Majuto

$
0
0
Bill Nass: Mimi si Chanzo cha Steve Nyerere Kususia Msiba wa Mzee Majuto
Msanii wa bongo fleva Billnass amekanusha taarifa kuwa yeye ndio chanzo kikubwa cha kumkwaza msanii wa bongo movies Steve nyerere kujihusisha na shughuli za msiba wa Mzee Majuto na misiba mingine itakayofuata kutokana na kashfa za kuwa anahujumu pesa za ubani zinazopatikana katika misiba.

Billnass na Stev Nyerere waliwahi kuingia katika majibizano yaliyopelekea wawili hao kuonekana kushushiana heshima hasa baadaya billnass kusema kuwa steve amekiwa akisubiri misiba ili apate ulaji, hata hivyo mara baada ya kutokea kifo cha mzee majuto billnass aliandika maoni katika moja ya post iliyozunguka sana katika mtandao ikisema kuwa kipindi hiki cha msiba wa mzee ndio kipindi cha Steve kukusanya pesa za ada ya watoto.

Hata baada ya maneno mengi, Steve Nyerere alisema kuwa kwa sasa yeye atakuwa kama waombelezaji wnegine lakini hawezi kujihusisha na kitu chochote katika misiba.

Billnass afunguka “sio kweli , mimi sio chanzo cha steve kususia msiba wa mzee,kwani mbona hata mimi aliniambia kuwa nina wafuasi kumi lakini sikuacha muziki.na atambue kuwa ni maneno tu kwaio asife moyo aendelee kujitolea.”

Hata hivyo maneno hayo ya kumkashifu msanii Steve Nyerere yaliwagusa wasaniiwengi na kuamua kuliongelea hilo huku wakionekana kutopendezwa na tuhuma hizo zinazoendelea juuu ya msanii mwenzao.

Viewing all 104689 articles
Browse latest View live




Latest Images