Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Tazama VIDEO Julius Mtatiro Akitangaza Kujiunga na CCM na Kujivua Uanachama wa CUF

$
0
0
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha CUF Julius Mtatiro amejivua uanachama wa chama hicho nakujiunga na Chama cha Mapinduzi CCM huku akisema kuwa  huu ni wakati wake wakwenda kutumia vipaji vyake kikamilifu pia kuwa balozi mkubwa wa Rais Magufuli Ndani na nje ya Nchi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam amesema kuwa ameamua kuchukua uamuzi huo kwa kuwa jukwaa alilokuwa analisimamia katika siasa kwa miaka kumi limeshindwa kumpa nafasi yakuifanyie nchi yake maendeleo.

katika hatua nyingine baada ya kutangaza nia hiyo Mtatiro ametoa ahadi yakuwatumikia watanzania pamoja na kupambana na umasikini nakuongeza uamuzi alioufanya sio kwaajili yakutafuta cheo

VIDEO:


Rosa Ree Afunguka Kuhusu Gigy Money Kumfuata Kwenye Rap/ Mama Rosa Ataka Mwanae Aimbe Nyimbo za Dini

$
0
0
Rosa Ree Afunguka Kuhusu Gigy Money Kumfuata Kwenye Rap/ Mama Rosa Ataka Mwanae Aimbe Nyimbo za Dini

Tazama Video Amefunguka Mengi na pia mama yake ameongea


Bonge la Nyau Afunguka Sababu za Kutoka na Khadija Kopa

$
0
0

Msanii wa hip hop, Lameck Philipo maarufu kama 'Bonge la Nyau' ametoa sababu ya kufanya mziki na mkongwe wa muziki wa Taarab na anaeendelea kufanya vizuri, Khadija Kopa ambapo amesema lengo ni kuleta ladha tofauti na ile iliyozoeleka.

Bonge la nyau amefunguka kuwa ngoma hiyo inayotarajiwa kutoka hivi karibuni itawakutanisha mashabiki wa mziki wake na mashabiki wa Taarab na kuweza kufurahia kwa pamoja muunganiko huo. Akiongea na Mikito Nusunusu Nyauloso amesema

“Watu wanaweza kufikiri nimefanya Taarab pia kwenye kolabo yangu na Khadija Kopa, lakini si hivyo, tumefanya kitu tofauti na kitaleta matokeo tofauti kwenye gemu ambayo yatawashangaza wengi,” .

Kauli ya Nape Nnauye Baada ya Mtatiro Kujiunga na CCM

$
0
0
Kauli ya Nape Nnauye Baada ya Mtatiro Kujiunga na CCM
Mbunge wa Jimbo la Mtama Nape Nnauye  ametoa neno baada ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi CUF Taifa, Julius Mtatiro kukihama chama hicho, akisema kuwa hamahama hiyo itumike kama fursa ya kujenga upya demokrasia.

Nape ametoa maneno hayo kupitia ukurasa wake wa Twitter, ambapo amesema hamahama hiyo pia itumike kama fursa ya kujenga uimara wa CCM.

Hata hivyo, Nape amesema uimara wa CCM unategemea ubora wa upinzani huku akifananisha na ushindani wa timu za Simba na Yanga.

"Kama msomi wa Sayansi ya siasa, naona hii ni FURSA muhimu ya KUJENGWA kwa aina MPYA ya VYAMA na SIASA za upinzani nchini! Kwa DEMOKRASIA hamahama hii ni muhimu ITUMIKE kama FURSA ya kujenga UPYA! Uimara wa CCM unategemea ubora wa UPINZANI!{Simba/Yanga} " ameandika Nape kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Muone na Wasiliana na Dr Kanengo Bingwa wa Tiba Asili, Hutibu Magonjwa Haya

$
0
0
NKURURU:-ni dawa inayotibu miguu kuwaka moto, kiuno tumbo     kupooza/kuparalazi  kupoteza  fahamu  MALABALA  hutibu  kisukari , uti  wa  mgogo,  Change, pumu, busha, kaswende, kifua  kikuu, muwasho  sehemu  ya siri

POWER :-ni dawa ya kuongeza nguvu za kiume ni vidonge  20

MPERAMPERA:- ni dawa ya kurudisha Mke, mme, mpenzi,mchumba aliyekuacha /kuteseka, ni kwa mda wa siku 2 tu kusafisha, pia kunakuna dawa za kupunguza vitambi(nyama uzembe),  maziwa makubwa,michirizi, mikovu makubwa, chunusi sugu.

SIX POWER:-inatibu upungufu wa nguvu za kiume kwa wasio weza kumudu tendo la ndoa itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 4 bila hamu Keisha, inaboresha maumbile madogo na inaimarisha misuri iliyo regea na kusinyaa una pona kabisa, ndani ya siku 4 tu

GASELA:-ni dawa ya maajabu (9) yaliyoshindikana.    (1)-Kisukari, vidonda vya tumbo, tezi dume,walioshindikanika kupata watoto(ugumba),busha bila oparesheni, (2)zindiko Kali Katika biashara yako (chuma ulete)  ndo kiboko yao kumkamata mwizi aliye kuibia vitu vyako pikipiki, gari, n, k( 2)zindiko la nyumba, mashamba, viwanja,. ( 3 ) kurudisha mtu aliye kufa kiutatanishi (msukule) (4)kukutolea sumu uliyo ikanyaga (Mtego) (5)ujiamini kutumia dawa ya maajabu Saba (6)kutoa mikafara mfano ugomvi ndani ya nyumba kufukuzwa kazini bila sababu (7)kutabiri nyota na kung'arisha (8)kurudisha Mali iliyo potea mazingira ya kutatanisha, kushinda kesi uliyo sumbuka nayo mda mrefu. (9)kufukuza majini wa  chafu ndani ya mji,.Haya yote yana wezekana kwa DR KANENGO popote ulipo ukiniitaji nafika napatikana buguruni chama, mbagala zakhiem karibia na uwanja wa mkutano, na wilaya ya bunda musoma : mawasiliano  ni simu namba :-0767-17-17-73 na  0716-60-89-59

NI  KWA  WALIO  TUMIA  DAWA  ZA MATATIZO  MBALIMBLI  BILA  MAFANIKIO   uwezo  WA  kurudisha  mali  iliyopotea  au  kudhulumiwa    muda  mfupi  tu,  Na natoa  dawa  ya  utajiri  kwa  wafanya  biashara     wachimbaji  madini, wafaryakazi,  wakulima, wafugaji na  kwa yeyote  anayetaka  kuwa  na  pesa   nyingi  katika   maisha  yake,  Na  pia  anaunganisha  utajiri    kwa muda  mfupi  sana  pamoja  na  kuboresha  akili  kwa  wanafunzi  na  kumfanya  afaulu  mitihani  yote  au  intaview  yeyote  na  ana  uwezo  mkubwa  wa  kutibu  ugonjwa  wa  Uvimbe tumboni .  pia anarudisha  Mke, mme, mchumba,    hawara, kwa  muda  wa  saa  3  na  anatimiza mahitaji  yote  hata  kama  upo  mbali   kiasi  gani,  ahadi  zote  atatimiza  kwa  muda  mfupi  tu  Na  kumfunga  asiwe  na mtu  mwingine  kwa  nini  unaumiza  kichwa ?

Muone  ( DR  )KANENGO,anatibu  nguvu  za  kiume  anarefusha  na  kunenepesha  uume  kwa  saizi  uipendayo  kwa  muda  mfupi   sana, pamoja  na  kuwa  na  hamu  ya  kurudia  tendo  la  ndoa  mara  4  bila  hamu  kuisha   Na  utachelewa   kufika  kileleni  kwa  muda  wa  dakika   40  bila  kuchoka  hata  kama  una umri  mkubwa  kiasi  gani   Gerentii  miaka /=60    ukisha  pona  bila tatizo   kurudia  pia ana  uwezo  mkubwa  wa  kuongeza  hips na  makalio,  pia   anatibu  magonjwa  sugu  ya  zinaa  tumbo  kujaa  gesi,  kuuma  chini  ya  kitovu,vidonda vya tumbo,   kiuno,  miguu    kuwaka  moto  miguu,  kuvimba..Nk..Angalizo usitume meseji wala kubipu..
You can get it in   all East African countries, our service is fast and easy...

Contact Whatsapp 0767171773.Dar es salaam Tanzania. ..Dr. KANENGO 0716608959...You are welcome.

Bonge la Nyau Afunguka Kutoka na Khadija Khopa

$
0
0
Bonge la Nyau Afunguka Kutoka na Khadija Khopa
MWANAMUZIKI Lameck Philipo ‘Bonge la Nyau’ amefunguka kwamba siri ya yeye kuamua kufanya kazi na mwanamuziki mkongwe wa Taarab, Khadija Kopa ni kuleta ladha tofauti kwenye muziki mbali na vile watu walivyozoea.

Akipiga stori na Mikito Nusunusu, Bonge la Nyau alisema kwamba kwa ujio huo ambao siku yoyote kuanzia sasa atauachia atawapa nafasi mashabiki wa muziki wake na wale wa Taarab kufurahia muziki mzuri na kuona namna ‘chemistry’ ya Hip Hop na Taarab inavyoweza kufanya kitu ‘amaizing’.

“Watu wanaweza kufikiri nimefanya Taarab pia kwenye kolabo yangu na Khadija Kopa, lakini si hivyo, tumefanya kitu tofauti na kitaleta matokeo tofauti kwenye gemu ambayo yatawashangaza wengi,” alisema Bonge la Nyau.

Hii Hapa Sababu za Mtatiro Kutimkia CCM

$
0
0
Hii Hapa Sababu za Mtatiro Kutimkia CCM
Aliyekuwa naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi, (CUF) Julius Mtatiro ametangaza kuachana na chama hicho ambapo amesema kuwa amefanya hivyo ili kufanya siasa za maendeleo ili kumsaidia Rais Magufuli.

Mtatiro ametangaza kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM) leo Agosti 11, 2018 wakati akizungumza na vyombo vya habari ambapo amesema kuwa ameanza kwa kuzungumza na waandishi na kutangaza azma yake ambayo ameitafakari kwa muda mrefu kabla ya kuwataarifu viongozi wa CCM ambao amewaomba wampokee.

“Nawaambia Watanzania kwamba kuanzia leo nitaanza kufanya siasa za maendeleo ili kumsaidia Rais John Pombe Magufuli ", amesema Mtatiro.

Mtatiro ameongeza kuwa , "Nimejiridhisha kwa hitaji la nafsi yangu kwamba nijiunge na Chama cha Mapinduzi CCM, nawajulisha watanzania rasmi kuwa nimeanza mipango ya kutekeleza hili mara moja".

Mtatiro amesema kuwa masuala ya misimamo yake ya sera na ilani za CUF na misimamo ya CUF hayo yanabakia CUF, hivi sasa yeye ni  Mtatiro ambaye anajiandaa kujiunga na Chama cha mapinduzi CCM  kama mwananchi na anatumia haki yake kikatiba.

Wimbi la viongozi na wanachama wa upinzani kutimkia CCM, lilianza kushamiri mwaka jana ambapo mpaka sasa jumla ya wanachama milioni mbili wameshajiunga na chama cha mapinduzi kuanzia Januari mwaka 2017 hadi sasa kwa mujibu wa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Humphrey Polepole.

Private Jet ya Davido yatua Nigeria

$
0
0
Private Jet ya Davido yatua Nigeria
Staa Davido kutokea Nigeria anazidi kututhibitishia kuwa hela yake sio ya mchezo na hii ni baada ya kutuonyesha private jet yake kuwasili katika ardhi ya Lagos,Nigeria kupitia insta story yake na kuandika ujumbe wa kuthibitisha ujio wa ndege hiyo binafsi.

Kupitia Insta story ya Davido amepost ngazi za ndege hiyo na kuandika ujumbe unaosomeka “Tuko juu sasa hivi, ndio ndege yangu imeshawasili” ikiwa imeambatana na picha nyingine na kusema “Imefika”



Ikumbukwe tu May 11,2018 kupitia mtandao wa twitter Davido alitudokeza kuhusiana na ujio wa ndege hiyo binafsi na kusema kuwa itawasili hivi karibuni na itamsaidia katika ziara zake za muziki ndani na nje ya bara la Afrika.Ujio wa ndege hiyo ya Davido inamfanya kuwa miongoni mwa mastaa wachache wanaomiliki ndege binafsi duniani.


Hali ya Niyonzima Simba Yafika Pabaya

$
0
0
Hali ya Niyonzima Simba Yafika Pabaya
Upo uwezekano mkubwa wa kiungo mchezeshaji wa Simba Mnyarwanda, Haruna Niyonzima kutimka ndani ya kikosi hicho kutokana na maelewano mabaya na viongozi wake.

Niyonzima aliyejiunga na Simba msimu uliopita akitokea Yanga, amerejea nchini hivi karibuni akitokea kwao Rwanda, hakuwa kwenye kikosi cha timu hiyo kilichoweka kambi ya wiki mbili nchini Uturuki.

Kwa mujibu wa gazeti la Championi, kiungo huyo alitarajiwa kukutana na viongozi wa timu hiyo juzi Alhamisi jioni kwa ajili ya kujadiliana hatma yake Simba. Mtoa taarifa huyo alisema, kiungo huyo ameonekana hana mpango wa kuendelea kuichezea, ni baada ya kutofautiana kwenye baadhi ya makubaliano yaliyokuwepo kwenye mkataba.

“Uwezekano wa Niyonzima kubaki kuendelea Simba kwenye msimu ujao ni mdogo kwani yeye mwenyewe ameonekana hana nia tena kubaki kuichezea timu hiyo. “Hata kurejea kwake jijini Dar kumetia hofu ni baada ya kurejea pekee huku familia yake akiiacha nyumbani kwao Rwanda, hiyo inatosha kabisa kuthitibitisha hilo Niyonzima hataichezea Simba katika msimu ujao.

“Kuna baadhi ya vitu ametofautiana na viongozi katika masuala ya kimkataba ambayo wanayafanya siri, hivyo upo uwezekano mkubwa wa Niyonzima kuusitisha mkataba wake Simba na kurejea kucheza soka nyumbani kwao,” alisema mtoa taarifa huyo.

Alipotafutwa Niyonzima kuzungumzia hilo alisema: “Sipo kwenye nafasi nzuri kwa kuzungumzia hilo suala katika kipindi hiki, jana (juzi Alhamisi) nilitarajia kukutana na viongozi wa Simba kwa kuzungumza nao lakini hilo halikuwezekana. “Nitalizungumza hilo baada ya kukutana na viongozi wa Simba, kwani kichwa changu hivi sasa hakipo sawa kabisa nafikiria familia yangu ambayo ipo nyumbani Rwanda,” alisema Niyonzima.

Deusdedit Kakoko Athibitishwa Kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Bandari

$
0
0
Deusdedit Kakoko Athibitishwa Kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Bandari
Aliyekuwa kaimu mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA), Deusdedit Kakoko amethibitishwa  kuwa mkurugenzi mkuu wa mamlaka hiyo.

Akizungumza na wafanyakazi wa TPA jana Ijumaa Agosti 10, 2018 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe amesema amechukua uamuzi huo kutokana na utendaji kazi wake.

Amesema ni kawaida watumishi wa Serikali wanapoteuliwa kwenye nafasi kama hizo kukaimu ili kuangalia utendaji wao wa kazi na kama akiiridhisha mamlaka anathibitishwa.

“Kipindi  alichokaimu ameangaliwa na Serikali na bodi ya TPA kwa bahati nzuri bodi imenipa taarifa yake ya utendaji leo na nimemthibitisha,” alisema.

"Tafadhali tembo usilitie maji, nimekupandisha kwa sababu nimeona utendaji wako nina imani na wewe, usiniangushe.”

Kamwelwe alisema kuwa kuna wakati huwa anamuhurumia kutokana n kutumia muda mwingi kazini.

"Huwa nampigia simu hata saa nne  usiku na bado anakuwa yupo ofisini hadi namuuliza huwa unalala kweli. Watu kama hawa ndio tunawataka na wengine igeni mfano wake, kazi zinafanyika saa 24 ziendelee vivyo hivyo,” alisema.

Kwa upande wake, Kakoko alisema hatamuangusha waziri huyo.

Will Smithbna Mwanaye Wapanda Steji Moja

$
0
0
Will Smithbna Mwanaye Wapanda Steji   Moja
Rapper na Muigizaji mkubwa Will Smith, Alhamisi iliyopita amepiga show kwenye stage moja akiwa na mtoto wake Jaden Smith.

Will alipanda kwenye stage hiyo akiwa na mtoto wake huyo wakati wa tamasha la ziara yake ya KOD lililofanyika huko mjini Miami.

Kabla ya wawili hao kuanza show hiyo wakati wapo backstage, Will alikua anongea huku akitokwa na machozi.

Miongoni mwa  sentensi ambazo Simith alikuwa akizungumza ni kwamba, kama haya sio matunda ya baba na mtoto basi hawezi jua ni kitu gani tena hiko.

Wawili Hao walitumbuiza wimbo wao wa pamoja 'Icon' ikiwa ni kama remix ya wimbo wake mwenyewe na kuamsha hisia za mashabiki kibao walikokuwa wamehudhuria. Msanii mwengine ambaye aliwasha moto kwenye tamasha hilo ni rapper J Cole.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume, Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za:


FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.


NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Mwalimu afumaniwa akimfanyia mwanafunzi mtihani

$
0
0

Mwalimu mkuu wa shule nchini Burundi amekamatwa kwa kudanganya kuwa yeye ni mwanafunzi akiwa na lengo la kumfanyia mtihani mtu mwingine. 

Polisi waliingia kwenye ukumbi wa mtihani ambapo Benjamin Manirambona alikuwa akifanya mtihani huo. 

Hakufahamu kuwa polisi ambao walikuwa wamevalia nguo za raia walikuwa waemsubiri usiku kucha shuleni ili wamkamate. 

Bila ya kuwepo mahala pa kutorokea mwalimu huyo mkuu wa taasisi ya Butere alikiri papo hapo. 

Rais Buhari aunga mkono kufutwa walimu 20,000 kwa kufeli mitihani 
Bw Manirambona alieleza kuwa alikuwa akifanya mtihani huo wa niaba ya mwanajeshi aliyekuwa akihudumu nchini Somalia kama sehemu ya kikosi cha Burundi cha kulinda amani. Alisema mwanafunzi alihitaji alama hizo hizo ili apate kujiunga na chuo kikuu. 

Mwalimu huyo mkuu alisema mwanajeshi huyo alimuahidi kumlipa mara atakaporudi Burundi. 

Alikamatwa pamoja na wanafunzi wengine wanne ambao pia walishukiwa kudanganya 

"Kila kitu unachosema na uwongo, kwa hivyo tunakuchukua," alisema waziri wa elimu nchini Burundi Janvière Ndirahisha, ambaye aliwasili na polisi eneo kisa hicho kilitokea mjini Bujumbura. 

"Tutachunguza kwa sababu kulingana na habari ambazo tumepata sio mara ya kwanza unafanya kitendo kama hiki," alimuaabia Bw Manirambona. 

Alikamatwa pamoja na wanafunzi wengine wanne ambao pia walishukiwa kudanganya mmoja akilaumiwa kwa kuwaunganisha mwanajeshi na mwalimu huyo. 

Bw Manirambona sasa yuko kwenye kizuizi cha polisi. 

Nchini Burundi wanafunizi wanaofanya mitihani muhimu hupelekwa kufanyia shule zingine na ndiyo sababu Bw Manirambona hakuweza kutambuliwa na watu kwenye ukumbi wa mtihani.

DC Jokate Mwegelo Akubali Ombi la Mwanafunzi Darasa la 7 Aliyemwandikia Barua

$
0
0

Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo, amekubali ombi la mwanafunzi Mwanahamisi Yusufu wa darasa la Saba wa Shule ya msingi ya Chanzige B, Kisarawe ya kumtaka aitembelee shule yao.


Jokate ameandika katika ukurasa wake wa Instagram  leo Agosti 11 na kusema kuwa mwanafunzi huyo alimuandikia barua na akaipokea Jumanne, Agosti 7.


==>Huu ni Ujumbe wa DC Jokate Mwegelo.

"Siku ya Jumanne, tarehe 07/08/2018 nlipokea barua ya Mwanahamisi Yusufu Sakidukuli, mwanafunzi wa darasa la 7 - iliyodhaminiwa na Mwalimu Mkuu wake, kutoka shule ya msingi Chanzige B hapa Kisarawe. 

"Aliniomba nitembelee shule yake niongee na wanafunzi wenzake wa darasa la 7, kwa ajili ya mazungumzo juu ya changamoto mbali mbali shuleni hapo na elimu kwa ujumla hapa Kisarawe.

"Jana tarehe 10/08/2018 nikifuatana na Afisa Elimu- Msingi Wilaya na Katibu Tawala Wilaya tulifanikiwa kufika shule ya Msingi Chanzige, pamoja na matembezi katika mazingira ya shule, nilifanya vikao na Mwanahamisi, Wanafunzi wa darasa la 7 na Walimu. Tulijadili changamoto za Afya, Elimu na Miundo Mbinu. Nilifurahi jinsi Mwanahamisi alivyoweza kujipambanua na uthubutu alioonyesha. .

"Bado changamoto za masuala ya hedhi salama kwa Vijana Balehe ni kubwa, miundo mbinu ya elimu bado changamoto hususani makazi ya waalimu. 

"Changamoto ya maji tayari imetafutiwa suluhu kuna mradi unaendelea wa kuleta maji kutoka Ruvu Juu kuja Kisarawe wenye thamani ya Tsh Bilioni 10.8.

"Mimi, pamoja na Mwanahamisi, kwa kushirikiana na wadau mbali mbali wa masuala ya elimu, afya, mazingira na huduma nyingine za kijamii tumedhamiria kuleta mabadiliko kwenye changamoto hizi, ili kuhakikisha juhudi za Rais John Joseph Pombe Magufuli katika kuleta Elimu Bora, Afya Bora na Mazingira Salama ya kielimu Wilayani Kisarawe zinakua halisi.

"Nimshukuru Mwanahamisi, Wanafunzi na Uongozi wa shule ya Chanzige A na B kwa kushirikiana nami kujadili na kunia pamoja kuleta mabadiliko haya.

"Mwanahamisi ni mfano mzuri wa viongozi tunaowatengeneza leo kwa ajili ya kulijenga taifa letu. Lakini hasa ni mfano mzuri wa jinsi jamii inatakiwa kushiriki katika maendeleo yake na kutatua changamoto pamoja na serikali yake. .

"Niendelee kuwakaribisha Wilaya ya Kisarawe wadau mbali mbali wa masuala ya Afya ya Uzazi kwa Vijana Balehe, Wadau wa Elimu na Miundo Mbinu, pamoja tujadili na kuamua namna gani Serikali ya Awamu ya Tano inaweza shirikiana nanyi hapa Wilaya ya Kisarawe kuleta mabadiliko chanya katika sekta ya Elimu."

Walickosema Humphrey Polepole na Bashe Baada ya Julius Mtatiro Kutoka CUF Na Kujiunga CCM

$
0
0
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya CUF, Julius Mtatiro amejivua uanachama wa chama hicho nakujiunga na Chama cha Mapinduzi CCM leo Agosti 11, 2018.

Mtatiro ametaja mambo matano yaliyomfanya atoke CUF na kujiunga CCM  ambayo ni pamoja na, mosi kutoridhishwa na hali ya ushiriki na mchango wake kwenye siasa za CUF, pili ni mgogoro wa kiuongozi unaoendelea kukikumba chama hicho.

Jambo la tatu ni kutoridhidhwa na ushiriki wake kama kijana na kiongozi katika kuchochea maendeleo ya nchi. Wakati jambo la nne likiwa ni ajenda ya maendeleo ya nchi, huku jambo la mwisho likiwa ni mustakabali wake kuhusu masuala ya siasa.

Makada, Wabunge  wa CCM na baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani nchini wametoa maoni tofauti kuhusu uamuzi wa Mtatiro  kuhama CUF na kwenda CCM.

Mbunge wa Kigoma Mjini, (ACT-Wazalendo) Zitto Kabwe ameandika kwenye ukurasa wake wa Twita akisema:

“Huko wanakokutegea kukufukuza kila usemapo ukweli? Ninaamini kwenye maendeleo ndani ya Demokrasia na siyo maendeleo ndani ya udikteta. Ninaamini katika uhuru wa fikra na siyo mawazo ya kiimla.Ninaamini nchi yetu inahitaaji chama kingine kuirudisha kwenye reli. Nafasi ya CCM ni Museum (makumbusho)."

Ndipo Mbunge wa Nzega, (CCM) Hussein Bashe akaamua kumjibu Zitto Kabwe kwa kuandika;  “Ni rahisi kuleta mabadiliko ya haki, demokrasia na maendeleo ndani ya CCM) kuliko kutafuta mabadiliko nje kwa sababu kuna mgogoro wa kimawazo, kimuundo na kimadili huko nje. Kuna wanajeshi wachache wa ukweli.”

 Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole yeye kafunguka na kusema hata yeye kayakuta mtandaoni. ameandika;“Huu unaitwa uhuru wa kisiasa kwa mujibu wa katiba yetu, halafu wale wa ‘siasa za bei nafuu mseme kanunuliwa;” Hongera kaka, ndugu, kamaradi. Historia na Mungu pekee atakupa tuzo ya dhamira yako njema. Na mimi nimeikuta mtandaoni.”


Nape Nnauye atoa neno kuhama kwa Mtatiro....."Ipo Haja ya Upinzani Kujengwa Upya, Uimara wa CCM Unategemea Uwepo wa Upinzani"

$
0
0
Mbunge wa Jimbo la Mtama Nape Nnauye  ametoa neno baada ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi CUF Taifa, Julius Mtatiro kukihama chama hicho, akisema kuwa hamahama hiyo itumike kama fursa ya kujenga upya demokrasia.

Nape ametoa maneno hayo kupitia ukurasa wake wa Twitter, ambapo amesema hamahama hiyo pia itumike kama fursa ya kujenga uimara wa CCM.

Hata hivyo, Nape amesema uimara wa CCM unategemea ubora wa upinzani huku akifananisha na ushindani wa timu za Simba na Yanga.

"Kama msomi wa Sayansi ya siasa, naona hii ni FURSA muhimu ya KUJENGWA kwa aina MPYA ya VYAMA na SIASA za upinzani nchini! Kwa DEMOKRASIA hamahama hii ni muhimu ITUMIKE kama FURSA ya kujenga UPYA! Uimara wa CCM unategemea ubora wa UPINZANI!{Simba/Yanga} " ameandika Nape kupitia ukurasa wake wa Twitter.


Watu zaidi 21,000 Wahamishwa Kukimbia Moto Unaokaribia Kwa Kasi Califonia

$
0
0
Zaidi ya watu 21,000 wamehamishwa kutoka kwa njia ya moto unaokaribia kwa kasi Kusini mwa California.

Kuhama huku kwa lazima kulifuatia amri kutokana na kwamba moto huo kwa jina Moto Mtakatifu, ulitishia nyumba kadhaa kando mwa ziwa Elsinore kaunti ya Orange.

Moto huo ambao ni moja ya mingi kote jimboni humo umeharibu zaidi ya ekari 19,000 za msitu Kaskazini mwa San Diego.

Mwanamume mmoja anayeshukiwa kuanzisha moto huo mtakatifu amefikishwa mahakamani.

Forrest Clark alifoka mara kadhaa alipofikishwa kwenye mahakama ya Kaunti ya Orange mara nyingine akificha uso wake.

Kesi yake ilihairishw hadi tarehe 17 Julai Agosti na dhamana imewekwa dola milioni moja.

Mamlaka zinasema kuwa alianzisha moto huo makusudi siku ya Jumatatu bada ya muongo mmoja wa mvutano na majirani.

Kulingana na maafisa wa Kaunti ya Orange, Bw Clark alikuwa amemtumia barua pepe mzima mtoto wa kujitolea akitisha, "eneo hili litachomeka

Zaidi ya wazima moto 6000 wanapambana na moto huo ukiwa ni kati ya mioto 18 iliyo kwa sasa jimbo la California.

Moto unaofahamika kaam Mendocino Complex umetangazwa kuwa mkubwa zaidi kweny historia ya jimbo hilo na tarayi umechoma akari 290,692.

Maafisa wa moto wanaaminiwa moto huo kuendelea kuwaka kwa mwezi mzima.

Moto mwingine - tha Carr Fire ulio kaskazini, umewaua watu saba na kuharibu zaidi ya nyumba 1,500.

Kote jimboni humo takriban wazima moto 14,000 wanajikakamua kupambana na visa vingie vya kuzuka kwa moto.

Askari wa JWTZ Auwawa kwa Kupigwa Risasi

$
0
0
Watu wanaosadikiwa kuwa majambazi kutoka Burundi wamemuua kwa kumpiga risasi Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania aliyekuwa akishirikiana na wananchi kuwasaka majambazi walioteka gari la abiria.

Gari hiyo yenye namba za usajili T 757 AWG  Toyota Hiace ilikuwa ikitokea Mjini Kasulu kwenda Kijiji cha Nyamugari Wilayani Buhigwe na majambazo hao kupora vitu mbalimbali.

Akizungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wa vijiji saba vya Tarafa ya Muyama, baada ya kufanya msako, Mkuu wa wilaya ya Buhigwe, Luteni-Kanali MARKO NGAYALINA amepiga marufuku tabia ya baadhi ya wananchi kuwahifadhi raia wa Burundi kinyume cha sheria.

Luteni - Kanali NGAYALINA amesema wengi wa raia hao wa Burundi wamekuwa wakifanya vitendo vya uhalifu na kuondoka kutokana na wilaya hiyo kuwa mpakani.

Baadhi ya wananchi wa vijiji hivyo wamesema wamechoshwa na kuwepo kwa matukio ya mara kwa mara ya uvamizi unaofanywa katika maeneo yao.

Polisi - Acheni Kukabidhiana Silaha za Moto Kienyeji

$
0
0
Jeshi la Polisi mkoani Arusha limetoa angalizo kwa baadhi ya Makampuni ya Ulinzi kuwa makini na silaha za moto na kuacha mara moja tabia ya askari wake kukabidhiana kwa kupeana kienyeji badala yake wafuate utaratibu.

Agizo hilo limetolewa leo na Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ramadhani Ng’anzi wakati akiongea na wawakilishi wa Makampuni ya Ulinzi mkoani hapa katika kikao kujadili mafanikio na changamoto za Makampuni hayo kilichofanyika ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Polisi uliopo jijini hapa.

Kamanda Ng’anzi alisema baadhi ya askari wa Makampuni hayo wanapomaliza muda wa kuondoka lindoni wanakuwa na tabia ya kumkabidhi silaha askari anayeingia bila kuandikishana kwenye kitabu cha makabidhiano kitu ambacho si sahihi.

“Silaha ni Sensitive sana sio Muwa au Kanga unatakiwa utembee nayo wakati wote na hauwezi kuiacha popote au kukabidhi kienyeji kwani inapokwenda kwenye mikono ya watu hatari inaweza ikatumika vibaya na kuleta madhara makubwa, makabidhiano ya silaha yana taratibu zake”. Alilisitiza Kamanda Ng’anzi.

Alisema kwamba hali hii inaonyesha kwamba baadhi ya askari  wa Makampuni hayo wanahitaji mafunzo zaidi ili waweze kutambua umuhimu wa silaha na kuwaahidi kuwapatia wakufunzi watakaowapa mafunzo ya kutambua majukumu yao pamoja na haki zao.



Kamanda Ng’anzi alisema pamoja na changamoto kadhaa zilizopo ndani ya utendaji wa Kampuni hizo lakini zimekuwa msaada mkubwa katika masuala ya Usalama kwani mara nyingi wamekuwa wakifanya doria lakini pia kulinda katika maeneo mbalimbali.

Alisema Jeshi la Polisi mkoani hapa mara kwa mara limekuwa likishirikiana na Kampuni hizo kwa kupokea taarifa za uhalifu lakini pia kushirikiana nao katika kuimarisha ulinzi wakati wa Sikukuu kama vile Krismas na Mwaka Mpya ambapo Kampuni hizo zinajitolea kutoa Magari pamoja na askari wao.

Alizitaka kampuni ambazo zinamilikiwa na wazawa kuiga mifano ya Kampuni za nje ambazo zimewekeza nchini kwa kuzidi kuboresha viwango vya ubora, kuwa na vifaa bora na wabobezi katika sekta hiyo ili nazo siku moja ziweze kupata soko nje ya mipaka ya nchi yetu.

Akitoa historia fupi ya Makampuni ya Ulinzi, Mkurugenzi Mtendaji wa Chama Cha Sekta Binafsi ya Ulinzi nchini Bw. Isaya Maiseli alisema kwamba, Sekta binafsi ya ulinzi nchini mwetu imeanza toka mwaka 1988 mara tu baada ya ubinafishaji wa njia kuu za uchumi .

Alisema awali maeneo mengi ambayo sasa baadhi yao yanalindwa na Makampuni ya Ulinzi yalikuwa yanalindwa na Jeshi la Polisi na Polisi Wasaidizi na kubainisha kwamba, Kampuni ya kwanza kabisa kuanzishwa ilikuwa inaitwa Simba Security na baadae kufuatia Kampuni nyingine ambapo mpaka hivi sasa kuna jumla ya Makapuni 759 huku mkoa wa Arusha ukiwa na Makampuni ya Ulinzi 53.

Awali akimkaribisha Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha ambaye alikuwa mgeni rasmi katika kikao hicho, Mkuu wa Kitengo cha Polisi Jamii mkoani hapa Mrakibu Msaidizi (ASP) Edith Makweli alisema kwamba Makampuni hayo ya Ulinzi ni wadau muhimu sana kwa Jeshi la Polisi.

Alisema mara nyingi wamekuwa wakishirikiana nao katika masuala ya kiusalama na wao wana mchango mkubwa  katika kuimarisha utulivu wa mkoa huu, hivyo basi wataendelea kushirikiana nao na kuhakikisha Arusha inaendelea kuwa salama.

Jumla ya washiriki wapatao 40 walihudhuria katika kikao hicho ambapo mbali na Jeshi la Polisi mkoani hapa kuongelea mafanikio na changamoto za Makampuni hayo ya ulinzi lakini pia wawakilishi hao kwa mara ya kwanza walifanya uchaguzi na kufanikiwa kupata viongozi wao wa Chama hicho ngazi ya mkoa.

Vipimo vyawanasa vijeba Serengeti Boys

$
0
0
Zoezi la vipimo vya kuhakiki umri wa wachezaji wa timu shiriki kuelekea michuano ya kufuzu fainali za AFCON za vijana U-17 kanda ya Afrika Mashariki limekamilika huku wachezaji kadhaa waliozidi umri ‘Vijeba’ wakinaswa.


Madaktari wakimfanyia vipimo mchezaji wa timu ya Taifa ya Vijana ya Tanzania U17”Serengeti Boys” Ben Anthony Starkie anayecheza Leicester City U16 ya England.

Katika zoezi hilo lililofanyika katika hospitali ya taifa ya Muhimbili likisimamiwa na madaktari wa Shirikisho la soka barani Afrika CAF.

Miongoni walionaswa katika vipimo hivyo ni wachezaji wawili wa timu ya taifa ya vijana ya Tanzania, Serengeti Boys, Jafary Mtoo na Lenox Fred ambao wamethibitika kuzidi umri wa miaka 17.

Kwa mujibu wa taarifa ya Makamu wa Rais wa kamati ya tiba ya CAF, Dk Yacine Zerguini imewataja wachezaji wengine walioenguliwa ni Abdoul Intwari wa Burundi, Maxwell Mulili, Lesley Otieno na Abdulmalik Hussein Abdallah wa Kenya.

Wengine ni Simon Pitia Alberto wa Sudan Kusini, Gamel Abdul Kamal wa Sudan, Oluka George, Kafumbe Joseph na Elvis Ngonde wa Uganda.

Michuano hiyo ya vijana ya  kufuzu AFCON 2018 kanda ya  CECAFA inaanza leo Jijini Dar es Salaam kwa mchezo wa mapema kati ya Rwanda na Sudan na baadaye wenyeji Tanzania watamenyana na Burundi huku kiingilio kikiwa ni bure.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images