Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104431 articles
Browse latest View live

Aunt Ezekiel Naye Afunguka Kusuhu Kuspend na Waziri Lazaro Nyalandu Nchini Marekani

0
0
STAA wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel, amesema hakuna ukweli wowote wa yeye kutanua na Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu nchini Marekani, kwani alikutana naye ukumbini, akiwa amealikwa na blog iitwayo Vijimambo ambayo hutangaza utalii wa Tanzania nchini humo kila mwaka.Alisema wakati wa safari yake hakuelewa lolote kuhusu Waziri Nyalandu na anashangazwa na yanayozungumzwa hivi sasa kwani baada ya kumsalimia walipokutana,
hawakuwahi kuonana tena hadi aliporejea, kwani yeye alikuwa amepangiwa kwenye hoteli ambayo pia ndiyo ukumbi wa shughuli hiyo ulipokuwa

Tetesi:Polisi Waliofukuzwa Kazi Kwa Kunyonyana Ulimi Wakiwa Kazini Warudishwa Kazini

0
0
Polisi mahaba waliofukuzwa kazi kwa kosa la kunyonyana ulimi warudishwa kazini kwa agizo la IGP. Inasemekana hakuna sheria yeyote inayokataza watumishi wa serikali au askari kuwa na uhusiano wa kimapenzi kazini na sio kosa kutongoza au kuwa na mpenzi sehemu yako ya kazi ili mradi usilazimishe wala kutumia cheo chako kumshawishi mtu kimapenzi. Kwa maana hiyo askari aliyeisambaza ile picha ndiyo amepewa onyo kali kwa kosa la kuharibu faragha ya wenzake.

Huyu ndio Mwanamke aliyefia uwanja wa ndege Kenya kwa tetesi za Ebola.

0
0
Kila mmoja amekua na hofu akisikia au kukutana na mtu alietoka kwenye nchi zenye zilizoathirika kwa ugonjwa wa Ebola barani Afrika na ndio maana ubaguzi umeripotiwa katika nchi mbalimbali za Amerika, Ulaya na hata Afrika.
Ripoti mpya inasema Mwanamke mmoja wa Kenya amefia kwenye uwanja wa ndege Jomo Kenyatta Nairobi kwa tetesi kwamba alikua anaumwa Ebola au Marbug ambapo familia yake imeilaumu Serikali kwa kifo cha ndugu yao kwa kutelekezwa na wauguzi kwenye Clinic ya uwanja wa ndege waliokua na hofu ya kuambukizwa ugonjwa wa Ebola.
NTV Kenya wameripoti kwamba Marehemu ambae alikua mfanyabiashara aliondoka nchini Kenya na kuelekea Juba Sudan ambapo alipitia Uganda wakati mlipuko wa Marbug ulipotokea na alipowasili Juba alikua anavuja damu kwenye sehemu ya uzazi jambo lililofanya dada yake amrudishe Nairobi kwa ajili ya matibabu.

Baada ya ndege kutua tu Familia yake inasema hakuhudumiwa ipasavyo ambapo kwa muda wa dakika 120 Mama yake mzazi na rafiki yake walibaki kutazama tu hali yake ikiendelea kudorora na alikua akilalamika anaumwa kichwa na amemiss mtoto wake wa kiume.
Mama Wanjiku pamoja na rafiki yake pamoja na Marehemu waliwekwa kwenye chumba kimoja kwa zaidi ya saa tano kabla ya kuruhusiwa kuondoka ambapo Wanjiku alifariki dunia akiwa kwenye kiti cha magurudumu.
Mama mzazi na rafiki yake waliruhusiwa kuondoka kabla ya matokeo ya uchunguzi wa matibabu kutolewa, kama Marehemu alikua akiugua Ebola au Marbug basi kuachiliwa kwao kungepelekea kusambaa kwa ugonjwa huo kwa haraka….

Baada ya Kusota Mahabusu Halima Mdee Aliezea Mambo Matano Mazito Aliyokumbana nayo Segerea

0
0
Stori: Makongoro Oging’
MBUNGE wa Jimbo la Kawe jijini Dar na Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bawacha), Halima James Mdee ambaye aliwekwa Mahabusu ya Gereza la Segerea, Dar kwa saa kumi na mbili amesimulia mambo matano mazito aliyokumbana nayo hali iliyomfanya atokwe machozi.



Akizungumza na mwandishi wa habari hii mwishomi mwa wiki iliyopita, Mdee licha ya kuponda utendaji kazi mbovu wa serikali kuhusu mahabusu, aliyataja mambo hayo kama ifuatavyo:

HAUSIGELI NA KESI NDOGONDOGO
Alisema alipofika mahabusu aliwakuta wasichana wadogo ambao baadhi yao ni mahausigeli wakamlalamikia kwamba wamekaa ndani kwa muda mrefu bila kesi zao kusikilizwa.

Alisema kwa uchunguzi wake alibaini kuwa wasichana hao wa kazi za ndani, kesi zao zilifunguliwa kwa kubambikwa na mabosi wao pale wanapodai malipo, hivyo wao husingiziwa wizi au kosa lolote.

UBOVU WA CHAKULA
Pia Mdee alisema chakula cha mahabusu hakiridhishi kutokana na kupikwa bila kiwango na kuwa na michanga, wakati mwingine hakiivi.

MAHABUSU KUKAA MUDA MREFU BILA KESI KUSIKILIZWA
Jambo jingine alilodai kukumbana nalo Segerea ni mahabusu kukaa kwa muda mrefu kati ya miaka 4 hadi 7 bila kesi zao kusikilizwa kwa kisingizio cha upelelezi kutokamilika.

MACHANGUDOA KUWASHAWISHI MABINTI
Katika sakata lingine, Mdee alisema wanawake wengi waliokamatwa kwa makosa ya kujiuza usiku (machangu) wanaopelekwa mahabusu wamekuwa wakiwashawishi wasichana wadogo, hasa mahausigeli wanaofikishwa humo.

“Wasichana hao huwashawishi mahausigeli kiasi kwamba wanapotoka mle mahabusu na wao wanakwenda kujihusisha na ukahaba na biashara ya madawa ya kulevya kwa vile baada ya kutoka hawapewi nafasi na mabosi wao kuendelea na kazi,” alisema Mdee.

MAHABUSU WA KIKE KUADHIBIWA NA ASKARI WA KIUME
Jambo lingine aliloligundua Mheshimiwa Mdee ni kitendo cha askari wa kiume kutoa adhabu kwa maabusu wa kike badala ya kuadhibiwa na wanawake wenzao kitendo ambacho alisema kimekuwa kikiwadhalilisha mahabusu hao.

Hata hinyo, Mdee alimuomba Waziri wa Sheria na Katiba, Asharose Migiro kuanzisha utaratibu wa safari za kushtukiza magerezani na kuzungumza na mahabusu ili kusikiliza kero zao na kuzitatua.
Jumanne iliyopita, Mdee alifikishwa katika gereza hilo saa 11 jioni ambako alilala hadi kesho yake saa 1 asubuhi kwa madai ya kufanya maandamano haramu kwenda Ikulu ya Dar.

Rose Ndauka Afunguka 'Sitaki Kuwa na Mwanaume Tena

0
0

Siku chache baada ya uchumba wake kuvunjika, msanii wa filamu Bongo, Rose Ndauka amefunguka na kusema kuwa kwa sasa haitaji tena mwanaume kwani anajikita zaidi katika kufanya kazi. 

Akizungumza na mwandishi wetu, Rose alisema katika maisha yake ya uchumba alijifunza mambo mengi na anamshukuru Mungu amempa zawadi ya mtoto hivyo anafanya kazi kwa bidii ili aweze kumlea mwanaye vizuri.

Alisema hajutii kwa yaliyomtokea kwa mchumba wake Malik Bandawe, kwani makosa yaliumbwa makusudi ili watu wapate kujifunza, hivyo akili yake kwa sasa anaiwekeza katika kazi zake za sanaa.

Lady Jay Dee Ampiga Chini Umeneja Gardner, Huyu Jamaa Ndio Maneja Mpya wa Lady Jay Dee Kwa Sasa

0
0
Rapper Wakazi ndiye meneja mpya wa Lady Jaydee. Amechukua nafasi hiyo kutoka kwa Gadner G Habash..

Akizungumza na gazeti la Mtanzania Wakazi alikiri kwamba yeye ndiye meneja mpya wa Jaydee japo hakuwa tayari kueleza lolote kuhusu ndoa ya binamu yake Jaydee na Gardner kwa maelezo kwamba yeye si msemaji wao katika masuala ya mapenzi na ndoa yao.

“Mimi sijui chochote, maana nilipokwenda Marekani niliwaacha wakiwa wachumba, lakini nilipokuwa huko nikasikia wameoana, niliporudi nikawakuta tayari wapo katika ndoa na nimeanza kazi ya umeneja wa Jaydee si muda mrefu, hivyo sijui mahusiano yao ya ndani labda muwaulize wenyewe,’’ alisema Wakazi.

Lissu: Marehemu Amepiga Kura Katiba ya Sitta

0
0

MWANASHERIA wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu amesema mchakato wa kutengeneza katiba mpya ni wa kihistoria kwani jina la marehemu lilipiga kura.

Akifafanua kauli hiyo alisema jina la mjumbe Shida Salum aliyefariki dunia Julai mwaka huu, limo kwenye orodha ya waliopiga kura ya ndiyo wakati kupitisha Katiba inayopendekezwa.

Lissu alisema hayo mwishoni mwa wiki mjini hapa alipotoa mada kwenye mdahalo wa kujadili Katiba iliyopendekezwa inayosubiri kupigiwa kura na wananchi, ambako alihoji ni Katiba Mpya au katiba ya kiimla katika rangi ing’aayo.

“Aliyekuwa mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba kundi la 201 kila mmoja anajua kwamba alifariki dunia lakini ukiangalia kwenye orodha ya waliopiga kura (huku akiionyesha kitabu kwa washiriki), anaonekana amepiga kura ya ndiyo.

“…Hii inawezekanaje jamani, ndiyo maana nakubaliana na Rais (Jakaya Kikwete) kuwa hii katiba iliyopendekezwa ni ya kihistoria,” alisema Lissu ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA.

Mwanasheria huyo ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki, alisema kitendo cha baadhi ya wajumbe kupiga kura wakiwa hospitalini ni miongoni mwa matukio yatakayokumbukwa kwa kuweka historia kwani halijawahi kutokea sehemu yoyote ulimwenguni.

Mbowe: Rais Kikwete ‘Hasomeki’ Mambo Mengi Anafanya Kinyume

0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe amesema Rais Jakaya Kikwete haeleweki kwa sababu mambo mengi wanayokubaliana naye anayafanya kinyume.

Akizungumza Dar es Salaam jana kabla ya kuanza kwa kikao cha siku mbili cha Kamati Kuu ya Chadema (CC), Mbowe alisema Rais Kikwete si mtu wa kupanga naye ‘dili,’ na kutolea mfano makubaliano kati ya Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) na Rais kuhusu Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

“Tulikutana na Rais Kikwete katika kikao cha TCD na kukubaliana kuwa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ufanyike Februari mwakani ili tubadili sheria kwanza na kuboresha daftari la wapigakura.

“Cha ajabu kupitia kwa Waziri Mkuu, Serikali inasema uchaguzi utafanyika Desemba mwaka huu,” alisema Mbowe.

TCD inaundwa na vyama vya siasa vyenye uwakilishi bungeni ambavyo ni CCM, CUF, Chadema, NCCR-Mageuzi, UDP na TLP, huku vyama visivyo na uwakilishi bungeni vikiwakilishwa na chama cha UPDP kinachoongozwa na Fahm Dovutwa.

Kwa mujibu wa kanuni zilizotolewa na ofisi ya Waziri Mkuu ambayo kisheria ndiyo yenye jukumu la kusimamia uchaguzi huo, fomu ya mgombea uenyekiti wa kitongoji ina sehemu 12 ambazo mgombea anatakiwa kujaza, ikiwamo nembo ya chama chake cha siasa na nembo ya halmashauri aliyopo.

Wakati huohuo, wanachama tisa wa Chadema Mkoa wa Njombe akiwamo Diwani wa Kata ya Njombe Mjini, Aggrey Mtambo wamekamatwa na polisi kwa mahojiano ya saa nne baada ya kuingia eneo la Kituo cha Polisi kwa ajili ya kufanya usafi kwa kile walichoeleza kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 15 ya kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.

Tukio hilo lilitokea saa nne asubuhi jana na viongozi hao wa Chadema walishikiliwa hadi majira ya saa tisa alasiri walipowekewa dhamana.

Chadema walifika zilipo ofisi za polisi wilayani Njombe, kwa lengo la kufanya usafi katika kituo hicho, baada ya kufanya usafi katika Soko la Wakulima, Soko Kuu na Stendi Kuu ya Mkoa.

Mtambo aliliambia gazeti hili muda mfupi baada ya kuachiwa kwa dhamana kwamba, walikamatwa na kuwekwa ndani kwa kuwa walifanya usafi eneo la polisi bila kibali.

“Kwa mujibu wa polisi, wametukamata kwa kuwa tulienda kufanya usafi bila kibali na gari la taka tuliloenda nalo ni kama tulitaka kuteka kituo, , ” alisema Mtambo.

Mama Kanumba Akanusha Tetesi za Kutoka Kimapenzi na Serengeti Boy

0
0
Mayasa Mariwata
MAMA wa marehemu, Steven Kanumba, Flora Mtegoa amekanusha vilivyo taarifa zilizozagaa kuwa ana uhusiano wa kimapenzi na kijana mdogo ambaye amemzidi umri (serengeti boy).

Mama Kanumba ambaye pia amefuata nyayo za mwanaye kwa kujiingiza katika uigizaji, alifunguka hayo alipokuwa akizungumza na mwanahabari wetu mambo mbalimbali yahusuyo maisha yake binafsi na sanaa kwa jumla.

Lilipofika suala la tuhuma hizo ambazo zimewahi kuripotiwa na baadhi ya magazeti (si ya Globa Publishers Ltd) kwamba anatembea na dogodogo, mzazi huyo alisema taarifa hizo ni za kipuuzi na hazina ukweli wowote.

“Huo ni uongo tu kwa kweli, hakuna kitu kama hicho, mtu mzima kama mimi naanzaje kufanya vitendo kama hivyo? Heshima yangu itakuwa wapi?” alihoji mama Kanumba.

Mama hakusita kutoa ufafanuzi zaidi juu ya madai hayo kwenda mbele hadi kufikia hatua ya kudai kuwa anaonekana na dogodogo huyo katika maeneo tofauti.

“Wanasema nimekuwa nikionekana naye sehemu tofauti? Inawezekana akawa ni huyu mwanangu Hotma Peter ambaye nimekuwa nikishirikiana naye kwenye kazi mbalimbali kwa kuwa watu hawamjui na walizoea kuniona nikiwa na Seth Bosco (mdogo wa marehemu), ukweli sina bwana na wala sihitaji hata awe pedeshee wa aina gani,” alisema mama Kanumba.

Akizungumzia kuhusu kampuni ya Kanumba The Great Film aliyoiacha marehemu mwanaye, mzazi huyo alisema kampuni hiyo kwa sasa bado inaendeleza shughuli za filamu japo kipindi cha nyuma ilikuwa haipo bize sana kwa kuwa akili yake haikuwa sawa.

“Kampuni bado inafanya kazi, japo kwa sasa msemaji wa kampuni hiyo ni Hotma ambaye ni mtoto wa marehemu mdogo wangu, Seth kwa sasa yupo bize na mambo yake mengine japo tunashirikiana naye katika kuandaa kazi mbalimbali na tumefanikiwa kutoa filamu moja mpaka sasa.

“Ukweli ni kwamba Kanumba hakuacha kazi yoyote, kwa kuwa kazi zake zote hatimiliki walikuwa nazo Kampuni ya Steps Entertainment na ya Mtitu, ni vizuri wasanii wawe makini na hili angalau ziwepo na kampuni ambazo hazina utaratibu wa aina hiyo wa kumiliki haki zote za kazi ya msanii,” alifunguka bi mkubwa huyo.

Trafiki wa Mahaba Siri Nzito Zafichuka, Dili la Nipe Nikupe Lafichuka

0
0
Na Ojuku Abraham
BAADA ya kuvuja kwa picha katika mitandao ya kijamii wiki iliyopita, iliyowaonesha askari wawili wa usalama barabarani wakiwa ‘kimahaba niue’ ndani ya sare za kazi na kusababisha kupoteza ajira zao kutokana na kukiuka maadili, siri zaidi nzito zimezidi kuvuja kuhusiana na ishu hiyo na Amani limemuibua afande wa kike baada ya kumsaka sana.

Kwa mujibu wa vyanzo makini kutoka wilayani Misenyi mkoani Kagera, askari wa kike aliyeonekana kwenye picha hiyo chafu, WP. 8898 Veronica Mdeme, inadaiwa kuwa alipata uhamisho kutoka polisi mkoani humo na kupelekwa katika wilaya mpya ya Misenyi mwaka 2011 ambako mwaka mmoja baadaye, ndipo akapigwa picha hiyo iliyoleta gumzo kubwa ndani na nje ya Bongo.

Ilidaiwa kwamba, picha hiyo ilipigwa katika barabara ya lami iendayo Mutukura, umbali wa Kilomita 50 kutoka Misenyi na kwamba askari hao walikuwa katika Kituo cha Polisi cha Kyaka.
Nguzo ya umeme inayoonekana nyuma yao, ni zile zinazopeleka umeme nchini Uganda kutoka Bwawa la Umeme la Mtera, Tanzania.

ILIKUWA PICHA YA KISHKAJI TU LAKINI…
Habari zilidai kuwa, askari hao Veronica, F.7788 Mpaji Mwasumbi na PC Fadhil Linga, walikuwa zamu moja na kwamba picha hiyo ilipigwa katika mazingira ya kishkaji tu lakini baadaye ikaja kuzua balaa kubwa.

Ilisemekana kwamba, Linga ndiye aliyewapiga picha wenzake ambao habari zisizothibitishwa zilisema kuwa walikuwa na uhusiano wa kijamii.

Madai yalizidi kutiririshwa kwamba baada ya kupigwa kwa picha hiyo, Linga alibaki na nakala katika kamera yake kwa muda wa miezi kadhaa kabla ya kugundua kuwa kumbe ilikuwa ni dili.

AWAGEUZIA KIBAO
Ilidaiwa kwamba, katika hali isiyotarajiwa, Mpaji na Veronica hawakuamini masikio yao baada ya Linga kuwaambia kwamba alihitaji kupata ‘kitu kidogo’ kutoka kwao ili aweze kuendelea kuhifadhi siri ya picha hizo.

Ilisemekana kuwa afande huyo aliwaambia wawili hao kama ataivujisha picha hiyo kwenye mitandao ya kijamii, watapoteza kazi.

“Baada ya kuambiwa hivyo, jamaa walilegea kabisa. Mwanzoni walitia ngumu lakini walipoona jamaa amekomaa, hawakuwa na jinsi zaidi ya kukubaliana naye, hivyo akawa anapata kitu kidogo kila alipojisikia  na kuwa nipe nikupe na hakuna uhakika kama dada Vero alisalimika kwenye mambo mengine kwani naye alikuwa akitumia nguvu kubwa kuhakikisha mumewe hajui,” kilidai chanzo hicho.

WAAMUA KUJILIPUA, WAMSHTAKI
Ilielezwa kwamba, baada ya ‘kutolewa upepo’ kwa muda mrefu na kuonekana kama wangekuwa ATM ya kudumu ya Linga, Mpaji na Veronica waliamua kujilipua na kwenda kumshtaki kwa kigogo wa juu wa jeshi la polisi mkoani humo ambaye anatajwa kuujua mchezo mzima ulivyokuwa.

Ilisemekana kwamba, kiongozi huyo alilichukulia jambo hilo kwa uzito wake na kuwakalisha wote watatu ili kuzungumza nao.Iliendelea kudaiwa kuwa katika kikao kati ya askari hao na bosi wao, wawili hao walikiri kupigwa picha hiyo na kuomba msamaha, lakini wakamlalamikia mwenzao ambaye naye alikiri kufanya kitendo hicho, kwa kuwageuza kuwa ATM.

Ilidaiwa kuwa mkubwa huyo alimuamuru Linga kuzifuta picha hizo na kuwataka kusameheana, kwani kitendo walichokifanya ni kibaya na kinachoweza kuhatarisha ajira zao. Linga alikubali ‘kuzi-diliti’ picha hizo!

WAGAWANYWA, LINGA ARUDIA
Ikazidi kudaiwa kuwa ili kuwafanya waishi kwa amani, waligawanywa katika vituo tofauti vya kazi mkoani humo huku mmoja wao, Mpaji akipelekwa Dar ambako alikwenda kusoma Chuo cha Polisi Kurasini.

“Wakiwa katika vituo hivyo tofauti, Linga alitulia kwa muda mchache tu kabla ya kuanza tena usumbufu wake, hasa kwa Veronica ambaye anadaiwa kuwa mke wa mtu. Ni katika usumbufu huo wa mara ya pili, akina Mpaji wakaamua kumjibu jeuri jamaa, hawakuwa na uoga tena kwa vile suala lao lilishafahamika kwa wakubwa,” kilisema chanzo chetu.

Inaelezwa kwamba majibu ya jeuri kutoka kwa Vero na Mpaji yalimuudhi Linga ambaye kwa lengo la kuwakomoa, aliamua kuzitupa picha hizo katika mitandao mbalimbali ya kijamii ambako nako zilizagaa kwa kasi ya moto wa kifuu na kuwafikia watu mbalimbali, ikiwa ni pamoja na vyombo vya habari vilivyoamua kuripoti.

“Picha hiyo ilipoonekana mtandaoni, moja kwa moja polisi walijua imewekwa na Linga kwa sababu hakukuwa na mtu mwingine aliyefahamu kuhusu picha hiyo. Ndiyo maana wote watatu walifukuzwa kazi siku moja, hawakuwa na sababu ya kuhangaika kujua nani kaweka,” kilisema chanzo hicho.

PICHA YA MREMBO YAWA GUMZO
Baada ya kufukuzwa kazi kwa wahusika hao watatu, kumekuwa na picha za mrembo mkali ambaye amekuwa akifananishwa na Veronica huku kukiwa hakuna uthibitisho wa moja kwa moja kama kweli ni yeye (angalia picha ukurasa wa mbele).

Kwa mujibu wa maoni lukuki katika mitandaoni, kama kweli mrembo huyo ndiye huyo askari wa kike, basi jamaa aliyekuwa naye kimahaba, alistahili adhabu yoyote kuliko kukosa mahaba hayo.

“Ni kama walivyoimba wale watoto wa Yamoto Band, yaani nzi kufia kwenye kidonda siyo ufala bali kupenda. Huyu mtoto mashalaah,” ilisomeka sehemu ya maoni ya stori hiyo ambayo ndiyo habari ya mjini kwa sasa.

Juzi, Amani lilimtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Henry Mwaibambe ili kumsikia nini kinaendelea baada ya askari hao kufukuzwa kazi lakini hakuwa hewani.

Naye msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, Advera Senzo alipopigiwa simu na kuulizwa alisema walishafukuzwa kazi hakuna kingine lakini akaelekeza apigiwe simu Mwaibambe.

Raha ya Kutongozwa Kwa Wadada..Ni Kweli Kuwa Usipotongozwa Kama Wiki tu Hivi Wajisikia Vibaya?

0
0

Kina dada hili swala la kutongozwa mnalichukulia vp, mwanamke ni asili yake kutongozwa?

Kwa sababu nilishakaa na kusikiliza maongezi ya kinadada wengi once anapokuwa anakosa mtu anaemtokea l mean kumtongoza hujisikia hajakamilika, na akiwa ni mdada ambae wanaume wanapishana kumtongoza anajifeel perfect hii imekaaje.

Huku Uswahilini Kwetu unakuta mdada anakesha kwa mganga ili apate kismati cha kutongozwa, Unakuta mdada anaewafungisha tela wanaume kwa kutongozwa Wenzake wanamwonea kijicho mpaka hawaelewani..

Hivi dada zangu huwa mnaenjoy mkiwa mnatongozwa?

Ni kweli kuwa usipotongozwa kama wiki tu hivi wajisikia vibaya?


Mwigizaji Lulu Michael Amjibu Mkongo wa Wolper, Ampa Shule Jinsi ya Kutongoza

0
0

Siku chache baada pedeshee Mkongo, Mwami Rajabu kutangaza kuwa anamtaka staa wa sinema Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ kwa gharama yoyote, mwigizaji huyo ametoa jibu linaloonesha dhahiri kwamba alikuwa radhi kumkubalia.

Akizungumza na waandishi wetu mara baada ya habari ya Mkongo huyo kuandikwa gazetini hivi karibuni, Lulu alisema kilichomshangaza kutoka kwa mwanaume huyo ni kwamba hakutakiwa kuanika hisia zake katika vyombo vya habari kama kweli ana nia ya dhati, angemtafuta mwenyewe au kwenda kujitambulisha nyumbani kwao.

“Namshangaa sana huyo Mkongo kwa kweli  kama angekuwa na mapenzi ya kweli asingeyaeleza kwenye magazeti, angenitafuta au angekuja nyumbani kwetu hapo ningemuona kweli ananipenda,” alisema Lulu.

Staa huyo aliendea kumwaga chache kuwa, kama mwanamke, anahitaji kupewa heshima yake na kudai kuwa wanaume wengi wa sasa wamejisahau kupindisha mila za Kiafrika kufuata taratibu na badala yake wanatanguliza fedha mbele.

“Nadhani watu wamesahau mila za Kiafrika kabisa, huwezi kuwa na mapenzi ya dhati kwa mwanamke halafu utumie rafiki au vyombo vya habari umpate, hiyo inakuwa siyo heshima kabisa,” alisema Lulu.

GPL

Vijana Wakimya Wanabahati Sana ya Kupendwa na Wasichana

0
0

Nimekuja kugundua wanawake hawapendi sana mwanaume mjuaji. Kuna watu wakimya sana hata akilewa yeye huwa anatabasamu tu, basi wewe utaongeeaaa, utapiga storiii na kujifanya kila kitu unajua lakini utashangaa mwisho wa siku aliyeenda kugegeda ni jamaa aliyekua hajachangia hata sentesi moja kwenye kiringe.

Na wala huwezi jua amemtongoza huyo msichana saa ngapi, nimejaribu hii kitu imenishinda aisee, yaani Safari zikishafika tatu tu, yaani naongea mpaka mishipa ya kichwa inanitoka.

Kwa kweli ukimya ni kipaji.

Tumechokaaa na Story za Miss Tanzania ooh Hana Vigezo ooh Sijui Mkubwa Mara Nini na Nini

0
0

Tumechokaaa na story za miss Tanzania ooh hana vigezo ooh sijui mkubwa mara nini na nini .. Watz bwana hata angepewa nani hilo taji la miss Tanzania msingerizika mngemchamba tu ! Muacheni Mtoto wa watu apumue kama kushinda ndio kashashinda umri wake unaingiliana vipi na umiss? Hao ma miss wote mbona hua wanapunguza umri wao au mnaona wa huyu tu? Haya basi hao wadogo waliokwendaga kutuwakilisha wametuletea nini ?? Eeh nauliza hao wenye umri mdogo wanaoendaga huko wamerudi na nini?? Nenda We sitti katuwakilishe tena wewe unaakili sana na unajielewa Yani katika wale wenzako niliowaona hakuna mwenye akili kama zako hakuna anaeweza simama mbele akatuwakilisha yaani bora wewe ! Hao wachezaji mpira miaka yao mnaijua nyie wanapunguza miaka hadi wanalingana na watoto wao hamuoni hayo ! Bigbrother si mnaangalia nyie haya mmeona hizo nchi nyingine washiriki wao?? Wakubwa na wazee lakini ukiuliza miaka yao unapata kiwewe lakini ndio kwanza wanasapotiwa... Embu acheni ujinga na tumsapoti miss tz wetu ndio kashakua miss wetu tena atafanya wonders......go girl go sitti....

Mshiriki wa Kike wa Botswana Big Brother Ajilegeza Kwa Jembe Letu la Kiume ( Idris) Linaloiwakilisha Tanzania

0
0




Big Brother Africa: Mshiriki wa Kike wa Botswana AJILEGEZA Kwa jembe letu la Kiume ( Idris) linaloiwakilisha Tanzania ... Siku washiriki wa BBA Hotshots wanatambulishwa, mwakilishi wa Tanzania, Idris Sultan alimwambia mtangazaji IK kuwa cheche zake zipo kwenye masuala ya wanawake. Huenda sasa shughuli imeanza. Baada  ya  binti  mrembo  wa  Botswana( Goitse)  kumzingua  mshikaji ( Idris ) aliyekuwa  ametupa  jiwe kumtaka  awe  mpenzi  wake, hatimaye  Idris  jana alimnasa binti  huyo na kula  naye  dinner pamoja... Ni  kama  ndoto  vile!!....Dinner  hiyo  iliandaliwa  na  kufanikishwa  na  washikaji  zake  wa  karibu  Nhlanhla na JJ  ambao  walisaidia kupika chakula hicho  kuhakikisha kuwa wawili hao wanakuwa na mtoko utakaowafurahisha.

Diamond asema "Nipo tayari kumsaidia collabo Ali Kiba"

0
0

Akiongea na 255 ya XXL kupitia Clouds fm Diamond amesema yupo tayari kumsaidia Ali Kiba.

Aliulizwa je yupo tayari kufanya kazi na Kiba pamoja na tofauti zinazozungumzwa kati yao.

Akajibu.....

Namnukuu " kama akija kuniomba nipo tayari kumsaidia, kama nimeweza kufanya na wasanii wa nje itakuwaje nikatae kufanya na. wasanii wetu wa nyumbani......nimeshasaidia wengi so akija yoyote nipo tayari kufanya nae.

Kiukweli mimi nimeshafika level fulani ivyo ni rahisi ata kumtangaza mtu kimataifa,so ikitokea mtu anaitaji nimsaidie mi sina tatizo"

Wasanii wa kimataifa Diamond aliofanya nao collabo mpaka sasa 

Waje - Nigeria 
Mafikizolo - South Africa 
Kcee - Nigeria 
Don Jazzy - Nigeria

Kura ya Meghji Yazua Utata Mpya Katika Katiba Iliyopendekezwa

0
0
Dar es Salaam. Suala la Mjumbe wa lililokuwa Bunge Maalumu la Katiba, Zakia Meghji kupiga kura upande wa Zanzibar wakati wa kupitisha Katiba Inayopendekezwa, limechukua sura mpya baada ya uliokuwa uongozi wa Bunge hilo kusema, “hakuna sehemu yoyote iliyobainisha kwamba alikuwa mjumbe kutoka Bara.”

Utata wa kura ya Meghji uliibuliwa na Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata), Deus Kibamba ambaye alisema mjumbe huyo alitakiwa kupiga kura upande wa Bara kutokana na Tangazo la Gazeti la Serikali namba 29 la Februari 7, mwaka huu lililomtambulisha Meghji kama mjumbe kutoka Tanzania Bara lakini katika upigaji kura alipiga upande wa Zanzibar.

Hatua ya mjumbe huyo kupiga kura upande huo wa muungano inachukuliwa na baadhi ya wanaopinga mchakato wa Katiba Mpya kama moja ya mbinu zilizotumiwa na uongozi wa Bunge Maalumu kulazimisha upatikanaji wa theluthi mbili ya kura kutoka visiwani ili kupitisha Katiba.

Hata hivyo, Naibu Katibu wa Bunge hilo, Dk Thomas Kashililah alisema jana kuwa: “Mnajichanganya tu, katika hilo tangazo la Serikali halikubainisha kwamba Meghji ni mjumbe wa Bara sisi tulichoangalia ni originality (asili) yake ni wapi hata kama anaishi Bara,” alisema Dk Kashililah na kuongeza: “Kama ndiyo hivyo, mbona Hamad Rashid anaishi Bara lakini asili yake ni Zanzibar? Mbona hilo hamuulizi? Hapo hakuna hoja kama wanatafuta kitu hicho hakipo.

“Katika Bunge hilo kulikuwa na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, wajumbe 201 na wajumbe kutoka Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania… ieleweke kwamba mjumbe wa Baraza la Wawakilishi anaweza kuingia Bunge la Jamhuri lakini wa Jamhuri hawezi kuingia Baraza la Wawakilishi.”

Muda mrefu ambao Meghji amekaa Bara anaweza kufananishwa na ule ambao Mbunge wa Dole (CCM), Sylivester Maselle Mabumba ameishi Zanzibar lakini wakati akipiga kura kupitisha Katiba, asili ya Mabumba ambayo ni Bara haikuzingatiwa.

Taarifa katika tovuti ya Bunge zinaonyesha kuwa Mabumba alihitimu elimu yake ya msingi katika Shule ya Langoni, Dole – Zanzibar mwaka 1983 na mpaka sasa amekuwa akiishi Visiwani humo licha ya kwamba ni mzaliwa wa Kahama, Shinyanga.

Meghji alipopigiwa simu kuzungumzia suala hili, baada ya mwandishi kujitambulisha kwake alisema: “Unasema unaitwa nani, unasemaje”, kisha simu ikakatika na alipopigiwa tena alipokea lakini ilisikika sauti ikisema hasikii na alipotumiwa ujumbe wa maandishi hakujibu.

Asili yake

Mjumbe huyo ni mmoja wa wabunge wa kuteuliwa na Rais katika Bunge la Jamhuri ya Muungano na hakuna taarifa zozote zilizoambatana na uteuzi wake kuhusu ni upande upi wa muungano anakotoka. Taarifa rasmi zinaonyesha kuwa amekuwa akiishi mkoani Kilimanjaro ambako 1990 alikuwa mkuu wa mkoa huo, nafasi ambayo aliipata baada ya kuwa Mkuu wa Wilaya ya Moshi mwishoni mwa miaka ya 1980.

Meghji pia amewahi kushika nyadhifa mbalimbali za uwaziri akiongoza Wizara ya Maliasili na Utalii kwa miaka tisa, Wizara ya Afya kwa miaka minne na Wizara ya Fedha kwa miaka miwili.
Wizara hizo mara kadhaa zimekuwa zikiongozwa na mawaziri kutoka pande zote mbili za muungano, lakini pia ni nadra kwa kiongozi kutoka Zanzibar kushika wadhifa wa mkuu wa mkoa na mkuu wa wilaya upande wa Bara.

Wasemacho wengine

Mratibu wa Mtandao wa Wanaopigania Haki za Binadamu, Onesmo Ole Ngurumwa alisema kitendo kilichofanywa ni kuhalalisha uchakachuaji wa Katiba hiyo.
“Kama mtu ameteuliwa kutoka Bara hata kama ni Mzanzibari atatakiwa kupiga kura kama mtu wa Bara kwani kulikuwa na maana yake kuteuliwa upande mmoja.”

Mwanasheria Mwandamizi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Harold Sungusia alisema kuna vitu viwili vinatakiwa kutazamwa kwa makini; mosi ni uteuzi wake ulikuwa kutoka wapi na alipiga kura kama mjumbe wa wapi.

“Kama aliteuliwa kama mjumbe wa Tanzania Bara alitakiwa kupiga kura kama mjumbe wa Bara na kama aliteuliwa mjumbe wa Zanzibar angepiga kura kama Mzanzibari na si kuangalia asili yake na hili halina hata haja ya kuumiza kichwa kwani linaeleweka alipoteuliwa ndipo huko atapigia kura,” alisema Sungusia.

Chanzo:Mwananchi

Ukweli Kuhusu Umri na Elimu ya Miss Tanzania 2014 Sitti Mtemvu Huu Hapa ..Kubali Au Kataa !

0
0

MISS TANZANIA 2014 SITTI MTEMVU ANA MIAKA 23 NA SIO 18
Katibu wa kamati ya Miss Tanzania Bosco Majaliwa amesema kuwa mshindi wa Miss Tanzania 2014 Sitti Mtemvu amezaliwa mei 31 mwaka 1991 na umri wake sahihi ni miaka 23 na sio miaka 18 kama ilivyozagaa sehemu mbalimbali.
Katibu huyo aliongeza kuwa Sitti ana shahada ya ya uhusiano wa kimataifa na alimaliza masomo yake Desemba mwaka jana katika chuo kikuu cha North Texas kilichoko kwenye jiji la Dallas nchini Marekani.
Sitti Mtemvu bado hajasoma ngazi ya shahada ya uzamili (Masters) kwa sasa ila anatarajiwa kwenda kusoma ngazi hiyo huko nchini Marekani.

Miss Tanzania na Lundenga on Fire Watu Waendelea Kumchimba Sitti Mtemvu Watoa Vielelezo..Jionee

0
0

Watu leo Wamecharuka Mitandaoni hasa Instagram Kuhusu Miss Tanzania Aliyepatikana Jumamosi iliyopita Miss Sitti Mtemvu , Leo Watu Wamepata Passport na Leseni yake zote zikionesha amezaliwa Mwaka 1989  pia kuna picha inazunguka mitandaoni akiwa amepiga na mtoto ambaye inasemekana ni wake ....Ukweli Upo wapi ? Tunazidi Kuchanganyikiwa....Nadhani kwa Mahali haya mambo yalipofikia Lundenga na kamati yake Wanahitaji kutoa Tamko Rasmi ili tuache kuchanganyikiwa kwa habari Hizi.

We Unasemaje Kuhusu Hizo Picha Hapo juu ni za kweli ?

Kundi la ze Comedy Limekabidhiwa Nyumba 7 Walizonunua Kutoka NSSF

0
0
Kundi la ze Comedy linaloundwa na wasanii kutoka hapahapa Tanzania lenye kujihusisha na uchekeshaji limekabidhiwa nyumba 7 walizonunua kutoka NSSF.
nyumba hizo kila moja imenunuliwa kwa thamani ya shilingi milioni mia moja na ishirini za kitanzania (120)  ambazo ni jumla ya shilingi milioni 840.
Viewing all 104431 articles
Browse latest View live




Latest Images