Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live

Fahamu Madhara ya Kufanya Mapenzi Kipindi cha Hedhi kwa Mwanamke

$
0
0


Fahamu Madhara ya Kufanya Mapenzi Kipindi cha Hedhi kwa Mwanamke
Kufanya mapenzi wakati wa hedhi ni kitendo cha kujiusisha na mapenzi na msichana au mwanamke aliye katika siku zake za kisichana..Kuna madhara mengi yanaweza yakatokea na kwa kawaida si madhuri kwa afya ya wote wawili.Hivyo kwa ushauri huwa tunapenda watu wajari sana afya zao na si kuzidumaza na kuendekeza hisia kwani hiloo ndilo kosa kubwa la vijana wengi wa siku hizi...Zifuatazo ni baadhi ya madhara yanayoweza kutokea endapo wawili hawa wakafanya ngono wakati KE yupo katika siku zake{period}..

 MADHARA KWA MWANAUME.
1.Kupata maambukizi katika njia ya mkojo hadi kwenye kibofu.

 2.Maambukizi katika tezi dume(Prostetits) hii inaweza kuathiri mfumo wa uzazi wa mwanaume.

 3.Kuziba kwa njia ya mkojo.

 4.Utasa au ugumba.

 5.Ulegevu wa misuli ya uume na upungufu wa nguvu za kiume.

 6.Athari mbaya ya kisaikolojia kwa kuwa anafanya tendo katika mazingira machafu hali itakayompelekea kutolifurahia tendo kutokana na hali ya umaji maji,utelezi, au harufu kali na mbaya na hivyo kuona kuwa mwanamke ni mchafu.Pia hali hii ikizidi inaweza kuathiri hata hufanyaji wa tendo katika siku za kawaida sio za hedhi.

MADHARA KWA MWANAMKE.
1.Kupatwa na mambukizi viungo vya ndani vya uzazi kama vile shingo ya kizazi,mirija ya uzazi kwa ujumla wake anaweza kuwa na tatizo la PID( PELVIC INFLAMATORY DISEASES) tatizo ambalo linaweza kuathiri mfumo wake wa uzazi.

 2.Maumivu makali ya tumbo hasa kwa wale wanaopatwa na maumivu wakati wa hedhi.(Dysmenorrhea).

 3.Utokaji wa damu unaweza ukaongeza kuliko vile inavyotoka kwa kawaida yake.

 4.Utasa au Ugumba.

 5.Kuvimba kwa kuta za ndani za uke kwa kuwa wakati wa hedhi zenyewe huwa tayari zimevimba au kutanunuka hali pia itamsababishia maumivu kwenye uke wakati wa tendo la ndoa.

 6.Athari mbaya ya kisaikolojia:Mwanamke atahisi kuwa mumewe hamjali wala mpendi bali anajali hisia zake za kingono na kwamba yeye anatumika kingono tu.Pia kuona kuwa mumewe ajali afya yake pamoja na maumivu anayoyapata lakini bado huyu mume anataka KU-DO.
NOTE
 Hali hii ikizidi inaweza kuathiri hata hufanyaji wa tendo katika siku za kawaida sio za hedhi.

Tunatibu Na Kuponesha Kabisa Upugufu wa Nguvu za Kiume, Busha, Kisukari na Vidonda vya Tumbo

$
0
0
TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO? BUSHA BILA KUPASUA KISUKALI NA VIDONDA VYA TUMBO? asilimia kubwa ya wanaume wanaupungufu wa nguvu za kiume NA maumbile madogo

NI NINI KINACHOSABABISHA UUME KUZIDI KUWA MDOGO NA WEMBAMBA 1 kuugua chango LA uzazi 2 unene kupita kiasi 3 kuvaa nguo au chupi za kubana 4 kupiga punyeto kwa mda mrfu ,NI NINI TIBA YAKE MAKAKANUA MIX nidawa ya mitishamba iliyochanganywa NA mizizi kumi NA mbili urfusha NA kunenepesha UUME saizi upendayo ich 5,6,7, NA 8 kwa urfu NA sentimita 3,4, na 5 ipo dawa ya kunywa na kupaka NI NINI KINASABABISHA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME 1 kupungukiwa kwa homoni ya testerone 2 kuhudhurika kwa Neva au uti wa mgongo 3 utumiaji holela wa madawa ya kizungu 4 usongo wa mawazo na asira 5 utumiaji wa vyakula vya mafuta mengi NI NINI TIBA YAKE MAPRO POWER NO 2 NDIO tiba tosha kwa sasa kwani utibu matatizo matatu kwa pamoja 1 itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15 adi 20 ,2 itakufanya urudie tendo zaidi Mara tatu 3 uhimalisha uume uliolegea na kusinyaa OKOA NDOA YAKO SASA ujihepusha na lawama ndani ya ndoa yako au pale ukutanapo na mpezi dawa hii itamfanya mpenzi wako hakueshimu na hasitoke nnje ya ndoa na ata wazee wenye umri mkubwa wanapona zipo dawa za kupunguza kitambi,minyama uzembe, presha ,kisukar mvuto wa mpezi au biashara

FIKA OFISINI KWETU MBAGALA ZAKHEMU na wateja wa kanda ya ziwa yupo wakala wetu mwanza mjini au piga simu 0752348593

DR MABULA na utaletewa popote ulipo uduma hizi

MUSIC AUDIO Mpya: Diamond Platnumz X Lava Lava X Mbosso – Jibebe

$
0
0
WCB wamekuja pamoja kwa mara nyingine tena, ni baada ya Diamond Platnumz kuachia ngoma mpya 'Jibebe' ambayo amemshirikiana na Lava Lava pamoja na Mbosso. Isikilize hapa


Ijue Siri Ya Kuondokana Na Ukata wa Pesa na Umaskini

$
0
0
Siku ya leo katika pekua pekua zangu za kuongeza chakula cha ubongo nilikutana na kauli ambayo kiukweli ilifanya mishipa yangu ya ardenalini kuweza kushtuka kwa kasi kama vile nimeona kitu cha hatari sana.

Kauli hiyo ilikuwa na maneno mawili yenye kubeba ujumbe mzito ambao sina uhakika kama, ujumbe huo upo mzani ambao ataweza kupima kilo zake, hii ni  kutokana na uzito uliopo katika ulipo katika ujumbe huo,  labda ujumbe huo upimwe na kichwa cha mwanadamu mwenye mtazamo chanya ndio anaweza kuuelewa.

Ujumbe huo unasema “unachokiogopa ndicho kitakachokua” narudia kusema tena unachokiogopa ndicho kitakachokua. Kwa haraka haraka unaweza usielewe maana ya msemo huo ila pindi utulizapo fikra ya ujazo wa akili unaweza kuelewa.

Binafsi nilichokielewa katika kauli hii ni kwamba, moja kati changamoto kubwa ambayo huwazuia watu wake kutoweza kutimiza makusudio yao hapa dunia ni kitu ambacho tunachokiita ni woga.

Woga ndio ambao umekua tatizo sugu lilojengeka machoni mwa watu wengi hata kuwapelekea watu hao kuweza kufa maskini huku watu hao wana uwezo mkubwa wa kufanya mambo makubwa yenye kuleta mapinduzi ya kufikia kilele cha mafanikio yao.

Woga huu si mwingine ni ule woga wa kuthubutu kuweza kufanya mambo mbalimbali. Wapo watu ambao wanatamani kufanya biashara kubwa ila wakiwatazama watu ambao walifanya biashara hiyo na kuona ya kwamba walifeli basi nao hujikuta wanaogopa kufanya jambo hilo.

Achilia mbali biashara, wapo baadhi ya watu wanavipaji mbalimbali lakini watu hao wamekuwa ni waoga wa kuonesha vipaji hivyo machoni mwa watu wengine huku wakiamini ya kwamba watachekwa, watu wa aina hii mara nyingi hufa na ndoto zao.

Wapo baaadhi ya watu wanaogopa kujenga nyumba zao za kuishi huku wakisema, “kwa heshima niliyonayo nikijenga nyumba ya kawaida watu wengine wanatanishangaa” kwa kauli kama hizi basi hujikuta miaka inazidi kukatika bila watu hao kuweza kufanya kitu chochote cha maana.

Wapo baadhi ya wanafanzi wamekuwa wanaogopa kusoma masomo ya sayansi huku wakiamini masomo hayo ni magumu mwisho wa siku watu hao hujikuta wanafeli masomo hayo, kwa mtazamo wa aina hii ndipo ninapokubaliana na kauli ile ambayo nimesema hapo awali ya kwamba unachokiogopa ndicho kitakachokua.

Kabla sijamaliza kusema nawe siku ya leo nitakuwa ni mchoyo wa fadhira kama nitashindwa kutoa ufumbuzi wa tatizo hili, yawezekana ukawa na tatizo la aina hii ya kuogopa kufanya jambo fulani la maendeleo eti kwa sababu ya woga uliojengeke ndani mwako, unachotakiwa kukufanya ni kuhakakisha kila jambo ambalo unataka kulifanya, kabla hujaanza kulifanya jambo hilo hakikisha ya kwamba jambo hilo unalichunguza kwa makini  na sio kutanguliza woga mbele na ndiyo itakuwa siri ya kuondokana na ukata.

SOMO: If you're Afraid to Lose Money NEVER INVEST, Baki na Hela zako.

$
0
0

Sikia....

Mzee Mengi alikuwa na gazeti linaitwa ALASIRI. Halikuleta faida. Gazeti la Dar Leo vile vile. Ushindani wa magazeti mengine ulikuwa mkali. Wasomaji wakabadilika. Internet zikaingia nk.
Akaachana nayo. Afu wewe eti unataka ufundishwe biashara ambayo hutaki kupoteza hela. Kaa na hela zako tu kwa kweli.

Hivi unadhani Novida imeenda wapi. Kama Coca Cola wanakosa soko la bidhaa yao wewe je? Lakini CocaCola wamefilisika? Mengi amefilisika? No.

Okay, tufanye hivi, ule ukumbi wa Sinema pale Mwenge ITV ulikufa kifo cha fasta. Competition. Century Cinemax ilileta upinzani. Wenye mradi wakajifunza.

Kuna matajiri wengi tu walipoteza sana pesa. Mabasi ya Scandinavia yapo tena? Kuna maduka mengi tu Kariakoo yamefungwa kipindi hiki.
Ni kawaida kwenye ulimwengu wa biashara. Si uliona Landmark Hotel Ubungo ilibadilishwa ikawa hostel. Umeona jinsi ambavyo tayari amerejea na kuwa hoteli ya kisasa zaidi. Alishajifunza. Sijui unaelewa?

Dar Village hapo Rose Garden Kijitonyama haijajengwa hadi leo. Mradi wa mabilioni uliingia mdudu miaka zaidi ya 8 sasa. Wewe unataka utakachoanza nacho kisife. Hela zako hutaki zipotee. Aisee you're not an entrepreneur. Kaa tu na hela zako. Bora ukazinywee soda tu au kula nyama choma kama unataka. Umekuwa mtu wa kutaka mafanikio yasiyo na changamoto yoyote. Ndo maana unasubiri ukiambiwa aisee biashara ya Matikiti inalipa hatari huyo umo. Ukiambiwa mayai ya kware yanalipa huyo. Hutaki kutulia kwanza ujifunze.

Hakuna biashara isiyolipa. Ila kuna akili zisizo za kibiashara ambazo lazima kuzibadili zijue biashara faida na hasara ni kawaida kabisa. Wanasema SOMETIMES YOU WIN AND SOMETIMES YOU LEARN.

Sasa wewe hutaki kulearn utafikaje kwenye mafanikio kibiashara?

Trump mwenyewe alifilisika kabisa. NIL. Zero. Rock bottom. Licha ya kuanza kwa mtaji mkubwa. Kama haupo tayari kukosekana pesa basi kazinunulie nguo mpya sikukuu zikifika uvae.

Na hiyo ndo maana kuna matajiri wachache. Wenye moyo wa UTHUBUTU katika jamii huwa ni wachache tu.

If you're afraid to lose money NEVER INVEST. Baki na hela zako.

Hii Hapa Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo ya Uume

$
0
0
Tatizo hili limekuwa likiwaadhiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wapo tofauti sana na wengine kwa kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi 6-8 kwanza upungufu wa vichocheo hivi huchochea ukuaji wa uume chongo ambalo hushambulia nerve ambayo uharibu kabisa ukuaji wa uume, ngiri, punyeto, ambayo huathili misuli ya uume, ngiri huleta maumivu, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, korodani moja kuvimba, kutopata choo vizuri, sababu hizi hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara nyingi hata nguvu za kiume ( hamu ya tendo la ndoa) hupungua na kwisha kabisa

GEMBE :Ni dawa inayozalisha na kukufanya uume kukua na kuongezeka
NGEMO : Ni dawa bora ya kuongeza nguvu za kiume

Hukutia hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi mara4 nne bila kukinai au kuchoka pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk30-45 kwa mtumiaji pia tunatibu kisukari, bp, ngiri, miguu kuwaka moto KAMA HUNAMDA WA KUFIKA OFISINI KWETU UTALETEWA POPOTE TUPO MBAGALA RANGI TATU

 0753471612/ 0715249530
0623 386 305

DR KUZENZA

Alikiba Aimwagia Fedha Coastal Union

$
0
0
Alikiba aimwagia fedha Coastal Union
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Ali Saleh maarufu kama Alikiba ambaye kwa sasa ni mchezaji wa Coastal Union amekuwa mdhamini mkuu wa timu yake hiyo.

Kiba ambaye anatarajiwa kuichezea timu hiyo kuanzia msimu huu, amekiambia kipindi cha Nyundo ya Baruani cha Azam TV, amekuwa mdhamini wa Coastal kupitia kinywaji chake ya Mo Faya ambacho amekitambulisha sokoni mwaka huu.

"Baada ya kuona kutia nguvu hiyo ya kwamba mimi nitakuwepo katika uchezaji, vile vile nimekuwa mdhamini mkuu kwasababu ya kinywaji changu cha sasa hivi ambacho nimekitoa cha Mo Faya na hii watu watakapokuwa wanakuja kabisa kuangalia mpira wanaweza kupata na vinywaji uwanjani. Vinywaji pia vitakuwa vinauzwa na kusupport Coastal Union," amesema Kiba.

 "Wanajitahidi ni wapambanaji na wanatafuta tittle msimu huu japo kuwa kuna timu kongwe lakini wanasema mpira unadunda. Nimeona ninaweza nikajiunga na Coastal Union kwa sababu ya talent ambayo nipo nayo," ameongeza.

Steve Amekuwa na Mchango Mkubwa Kwa Wasanii Hasa Muda Wa Matatizo- Uwoya

$
0
0
Steve Amekuwa na Mchango Mkubwa Kwa Wasanii Hasa Muda Wa Matatizo- Uwoya
Muigizaji wa Bongo movie Irene Uwoya ameibuka na kumkingia kifua Msanii mwenzake Steve Nyerere dhidi ya tuhuma za utapeli na Kula pesa za Michango ya rambi rambi.

Stevw Nyerere alijikuta katika wakati mgumu baada ya kila mtu kumnyooshea kidole na kumnanga kuwa misiba ikitokea anakuwa mstari wa mbele na kuchanganya michango ambayo anaishia kuitumia.

Kwenye mahojiano na Wasafi Tv, Irene Uwoya amemtetea Steve na kudai mchango wake mi mkubwa sana kipindi cha matatizo kwani watu wanakuwa hawajui wafanye nini hivyo yeye huwapa mwongozo kama kiongozi.

Kama Steve asingekuwa mtu wa kujitoa na kusimamia hiyo misiba tusongekuwa tunatoa heshima za mwisho sasa imekuja imegeuzwa kuwa Steven anasubiria misiba ili afaidike kitu ambacho sio cha kweli kwa sababu akisimama Steve msiba umetokea anasimama kweli kwa sababu msiba ni kitu cha ghafla tunakuwa hatujajipanga kwaiyo Steve anakuwa na uwezo wa kushika simu na kufanikisha mambo mbali mbali”.

Irene Uwoya amesisitiza kuwa Steve ni mtu muhimu sana Kwenye jamii na kama akijiondoa katika shughuli za kujitolea kama hizo lazima atakumbukwa maana mchango wake ni mkubwa sana.

CCM Chakanusha Kumpitisha Juliasi Kalanga Jimbo la Monduli

$
0
0
CCM Chakanusha Kumpitisha Juliasi Kalanga Jimbo la Monduli
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Arusha, Loata Sanare amesema kuwa chama hicho bado hakijampitisha Julius Kalanga (aliyetoka Chadema) kuwa Mgombea wa katika Jimbo la Monduli kwenye uchaguzi wa mdogo unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni.



Aidha, Sanare amesema kuwa, kupitia CCM, ni Kalanga pekee ndiye amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya kuwania ubunge ambayo tayari imeshapelekwa kwenye ngazi za juu za chama hicho kwa ajili ya usaili na kupitishwa kama itawezekana.

Udhamini Ligi Kuu Bara Pasua Kichwa

$
0
0
Udhamini Ligi Kuu Bara Pasua Kichwa
Ligi kuu ya soka Tanzania bara msimu wa 2018/19 inatarajiwa kuanza bila kuwepo kwa mdhamini mkuu kutokana na pande mbili ambazo ni Shirikisho la soka nchini TFF na wadhaini waliowasilisha ofa kutofikia muafaka mpaka sasa.

Akiongea na www.eatv.tv mtendaji mkuu wa bodi ya ligi Boniface Wambura amethibitisha kuwa ligi hiyo itaanza bila mdhamini mkuu huku akiweka wazi kuwa maongezi na makampuni mbalimbali yaliyoomba kudhamini ligi kuu kwa msimu  ujao hayajakamilika.

''Kalenda ya mashindano imeshafika na ligi inatakiwa kuanza hatuwezi kusubiri mdhamini, akipatikana ataingia wakati ligi inaendelea ila kwasasa tutakuwa na wadhamini wengine wadogo kama tulivyowatangaza'', amesema.

Ligi kuu soka Tanzania bara imekuwa chini ya udhamini wa kampuni ya simu ya Vodacom kwa miaka kadhaa lakini mpaka sasa kampuni hiyo na TFF hawajafikia makubaliano juu ya kuendelea au kutoendelea. Hivi karibuni TFF ilisaini mkataba na Benki ya KCB kama moja ya wadhamini wa ligi msimu ujao kwa dau la milioni 420.

Ligi hiyo inatarajia kuzinduliwa Jumamosi hii, Agosti 18 kwa mechi ya Ngao ya jamii itakayowakutanisha mabingwa Simba SC na mabingwa wa kombe la shirikisho Mtibwa Sugar mchezo ambao utapigwa kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Ligi yenyewe rasmi itaanza Agosti 22 kwa mchezo wa ufunguzi kati ya Simba SC dhidi ya Tanzania Prison ya Mbeya. Yanga wao watafungua msimu Agosti 23, ugenini dhidi ya Mtibwa Sugar kwenye uwanja wa Jamhuri Morogoro.

TCU: Kesho Ndo Mwisho wa Kutuma Maombi ya Kujiunga Chuo Kikuu Shahada ya Kwanza

$
0
0
TCU: Kesho Ndo Mwisho wa Kutuma Maombi ya Kujiunga Chuo Kikuu Shahada ya Kwanza
Tume ya vyuo Vikuu Tanzania (TCU) imesema kuwa kesho Agosti 15, 2018 ndiyo mwisho wa kutuma maombi ya kujiunga na masomo ya shahada ya kwanza katika vyuo vikuu na taasisi za elimu ya juu nchini.

Dirisha hilo la kuwasilisha maombi lilifunguliwa Julai 20, 2018 kwa awamu ya kwanza.

Akizungumza leo Agosti 14, 2018 Katibu Mtendaji wa TCU Profesa Charles Kihampa amesema kuwa baada ya kufungwa rasmi kwa dirisha la udahili vyuo vitaanza kuchakata majina ya waombaji kulingana na vigezo vya udahili vilivyowekwa kwa kila programu ya masomo.

Udahili wa kujiunga na vyuo vikuu unahusu makundi makubwa matatu ambayo ni waombaji wa kidato cha sita, wenye sifa linganifu kama vile shahada  na waombaji wenye vyeti toka nje ya nchi vyenye sifa linganifu.

"Baada ya kuchakata majina, dirisha la waombaji litaidhinishwa, " amesema Kihampa na kuongeza:

"TCU jukumu lao ni kuhakiki kama waombaji waliochaguliwa na vyuo wana sifa stahiki na wanakidhi vigezo vya kujiunga na programu husika za masomo,"amesema Profesa Kihampa.

Amefafanua kuwa waombaji wote wa udahili wanapaswa kutuma maombi yao moja kwa moja kwenye vyuo wanavyopenda na kuchagua programu za masomo.

Amesema Tume imetoa mwongozo wa programu zilizoidhinishwa kudahili pamoja na vigezo vya udahili vinavyotakiwa kwa kila programu za masomo.

"Waombaji wote wa vyuo vikuu na taasisi ya elimu ya juu wanakumbushwa na kuhimizwa kuzingatia kalenda ya udahili iliyoidhinishwa na Tume,"amesema Kihampa  na kuongeza:

"Ili kuepusha usumbufu usio wa lazima, waombaji wote wanahimizwa kutumia muda uliobaki kukamilisha maombi yao.”

Kihampa amesema dirisha la kuwasilisha maombi ya kujiunga na vyuo vya elimu ya juu awamu ya pili litafunguliwa Septemba tatu hadi saba.

Mwakyembe Alitolea Ufafanuzi Sakata la Channel za Ndani ITV, CLOUDS, Channel Ten Kuondolewa

$
0
0
Mwakyembe Alitolea Ufafanuzi Sakata la Channel za Ndani ITV, CLOUDS, Channel Ten Kuondolewa
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Harrison Mwanyembe, amezitaka kampuni za visimbuzi za DSTV, Azam na Zuku kwenda kwenda Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) wapewe utaratibu wa kurusha chaneli za ndani za bure kama wamevutiwa na soko hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo Jumanne Agosti 14 Mwakyembe amesema licha ya mikataba ya kampuni hizo kutoruhusha kurusha chaneli hizo lakini wamekuwa wakizirusha na kuwatoza wananchi gharama ili kuzipata.

“Kama hawa wenzetu wana hamu sana na soko hili la ndani wasitumie njia za chini chini waende TCRA wapewe utaratibu wa namna wa kuupata,” amesema Mwakyembe.

Alizitaja baadhi ya chaneli ambazo zinapaswa kupatikana bure kupitia visimbuzi mbalimbali ni pamoja na TBC, Star TV, ITV, Channel Ten na EATV na kusisitiza kuwa TBC ni lazima irushwe na kila kisimbuzi bila malipo yoyote.

Dk. Mwakyembe amesema pamoja na ufafanuzi mzuri uliotolewa na Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi ameamua kulitolea ufafanuzi jambo hilo ili kuondoa sintofahamu kwa wananchi.

“Naomba nianze kwa kutamka kwamba maelezo yote yaliyotolewa na Waziri Isack Kamwelwe yanawakilisha majibu ya wizara yangu,” amesema.

Dk. Mwakyembe pia amesisitiza kuwa serikali haijafuta leseni za visimbuzi vya Azam, Zuku na Multichoice Tanzania bali wanawataka kuondoa chaneli ambazo zinatakiwa kurushwa bure kulingana na matakwa ya mikataba yao.

Rais Magufuli Aendesha Kikao Cha Kamati Kuu Ya Hlmashauri Kuu Ya CCM Taifa

$
0
0
Magufuli Aendesha Kikao Cha Kamati Kuu Ya Hlmashauri Kuu Ya CCM Taifa
Rais John Magufuli akisalimiana na mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM alipowasili katika ofisi ndogo za chama hicho zilizopo Lumumba jijini Dar es Salaam.


Ndugu John Pombe Joseph Magufuli Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) akiwasili katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM Lumumba kwa ajili ya kuendesha Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa.

Ndugu John Pombe Joseph Magufuli Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) akiwa katika ukumbi wa mikutano katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM Lumumba kwa ajili ya kuendesha Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa.

Wabunge Nchini Uganda Watiwa Mbaroni kwa Kushambulia Gari la Rais Museveni

$
0
0
Wabunge mbaroni kwa kushambulia gari la Rais
Baadhi ya wabunge nchini Uganda wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kushambulia gari la Rais Yoweri Museveni kwenye uchaguzi mdogo eneo la Arua.

Jeshi la polisi limeeleza kuwa linawashikilia watu 30 ikiwa ni pamoja na wabunge kutoka Kampala, Njiri na maeneo mengine ambao wanadaiwa kuhusika kwenye tukio hilo lililotokea jana na kusababisha kifo cha mlinzi wa mbunge aliyeuawa kwa kufyatuliwa risasi na askari polisi.

“Hadi tunavyoongea hivi sasa hao wote tunawashikilia kwenye selo zetu, hatujui kama kati ya hao kuna waandishi wa habari au la. Tukianza kuwachambua tutafahamu ukweli wa jambo hili,” msemaji wa polisi wa eneo la West Nile, Josephine Angucia aliiambia NTV.

Aliongeza kuwa watu hao waliokamatwa walikuwa kwenye kundi ambalo lilirusha mawe kupiga gari linalotangulia msafara wa Rais.

Akizungumzia kifo cha mlinzi wa mbunge, alisema kuwa kifo chake kilitokana na risasi iliyopigwa bila kumkusudia.

Rais Museveni alikuwa katika eneo hilo akimpigia kampeni mgombea wa chama chake cha National Resistance Movement, Nusura Tiperu.

Mbunge wa Kyadondo, Robert Kyagulanyi maarufu kama Bobi Wine alikuwa eneo hilo la Arua pia akimpigia kampeni mgombea binafsi, Kassiano Wadri. Mbunge huyo ni miongoni mwa wanaoshikiliwa.

CCM Yateua Wagombea wa Ubunge Katika Jimbo la Monduli, Ukonga na Korogwe

$
0
0
CCM Yateua Wagombea wa Ubunge Katika Jimbo la Monduli, Ukonga na Korogwe
Kikao cha Kamati Kuu Maalum cha Chama Cha Mapinduzi CCM kimefanya uteuzi wa wagombea wa CCM katika Uchaguzi Mdogo wa Ubunge:

Julius Kalanga Laizer – Jimbo la Monduli
Mwita Mikwabe Waitara – Jimbo la Ukonga
Timotheo Paul Mzava – Jimbo la Korogwe Vijijini

Qwisa wa Shilawadu Awatolea Povu Wanayemshambulia Mpenzi Wake ''Chambeni Weeeee Siachani Nae''

$
0
0
Qwisa wa Shilawadu Awatolea Povu Wanayemshambulia Mpenzi Wake ''Chambeni Weeeee Siachani Nae''
Mtangazaji wa Clouds Media aliyejipatia umaarufu wake kupitia kipindi cha SHILAWADU akiwa na mtangazaji mwenzake Soud Brown, baada ya kutangaza rasmi kuuaga ukapera baada ya wikiend hii kumvisha pete mpenzi wake na kujianda kwa ajili ya ndoa hivi karibuni. huko mtandaoni pamekuwa hapashikiki katika page zote za udaku kuanza kumchambua mwanamke wake kila kona kama vile yeye na mtangazaji mwenzake Soudy wanavyokuwa wakifanya katika kipindi chake cha shilawadu.

Kufuatia kitendo hicho Qwisa ameonekana kuchukizwa na kitendo hicho na kuamua kuwatolea povu wanaomchambua mpenzi wake na kusema kua wao wametoka mbali na anampenda hivyo hivyo na ubaya wake kwakuwa anajua utamu wa mkewe.

Kupitia ukrasa wake wa instagramu aliandika hivi ''Mama Kamanda akipakwa Wanja wake almaarufu.. Nagaramia, Nampenda Hivyo hivyo na Wanja wake na sura yake na umbo lake na sugu zake.. Chambeni weeeee #SiachaniNae''



Daimond, Rich Mavoko Wakutana Uso kwa Uso Basata

$
0
0
Daimond, Rich Mavoko Wakutana Uso kwa Uso Basata
MKURUGENZI wa Kampuni ya WCB, ambaye pia ni staa wa Bongo Fleva, Nasbu Abdul  ‘Diaomond Platnumz’ na Mameneja wake wawili, Hamis Taletale ‘Babu Tale’ na Sallam Sharraf wametinga katika ofisi za Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) kuitikia wito wa baraza hilo kuhusu malalamiko yaliyowasilishwa na mwanamuziki Rich Mavoko aliyedai kuwa mkataba wake na WCB ni wa kinyonyaji.
Akizungumzia hilo mmoja wa meneja wa Diamond, Sallam, amesema waliitwa na Basata na sasa wapo katika mazungumzo ya kutatua jambo hilo na kufikia mwafaka.
Sallam amesema ni vyema watu wakasubiria yatakayoamuliwa huko, ambapo wanaamini Basata itauambia umma nini kilichoafikiwa badala ya wao  kuwa wasemaji.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume, Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0


TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za:


FUUl POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.


NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Aina 10 za waume ambao wake zao wanakereka kuwa nao

$
0
0
1. Wanaojiona Kama Wafalme (King Husband).
HIi ni aina ya wanaume ambao hutaka kusujudiwa kama wafalme na hupenda kuwafanya wake zao kuwa kama watumwa. Hawafanyi chochote ndani ya nyumba kazi yao ni kutumatuma hata kama mke anaumwa atapaswa kuamka na kupika, wanataka waheshimiwe wao tu na mwanamke akikosea kidogo ni maneno au kipigo. Mwanamke hana kauli ndani na mume akiingia nyumbani ni kama bosi anavyoingia ofisini, wote kimya hakuna hata kuongea.

2. Wanaume Wanaojihisi Bado Hawajaoa (Bachelor Husband).
Hii ni aina ya wanaume ambao hawawashirikishi wake zao kwa chochote. Hufanya mambo kama vile bado hawajaoa, hutumia muda wao mwingi na marafiki zao wakifanya mambo ambayo mke hata hayajui mke anaweza kustukizia tu mume kanunua gari bila kumshirikisha na mume haonyeshi hata kujali kuweza kumshirikisha. Hajali kama ana mke na mda mwingi huutumia akiwa na marafiki kufanya mambo yasiyo na msingi ambayo hayana mnanufaa yoyote katika ndoa yake.

3. Wanaume Wenye Gubu (Acidic Husband).
 Hawa hukasirika kila mara tena bila kua na sababu ya misngi, mambo hayaishi, kosa la mwaka juzi anaweza kukukasirikia leo. Wamemuudhi kazini hataki kusemeshwa na mnanuniwa nyinyi, mwanamke akiomba hela ya chakula ni shida ni kununa kutwa nzima, wanahasira na nirahisi kumpiga mke.

4. Mume Wa Kila Mtu (Genarel Husband).
 Hawa wanajifanya wasamaria wema, wanajali kila mwanamke, wanajali marafiki wakike wa mke na wakwao kuliko wanavyowajali wake zao. Mke anaweza kuwa na shida akasema hana hela lakini rafiki akampa. Wana marafiki wengi wakike na mara nyingi huwa hawaachani kabisa na ma X wao, wakiwalalamikia wanawasaidia kuliko hata wanavyowasidia wake zao wakati wakiwa na shida.

5. Wanaume Wanaojifanya Wagumu (Dry Husband).
Hawa wanajifanya wagumu sana, hawana yale mambo ya kimahaba na wao hujua kuwa ndoa ni kuleta chakula tu na kushughulika kitandani. Hakuna kuongea na hawajali hata hisia za mke, mke akiongea kwao wala hawajali wanajifanya ni vidume sana na wanaona mambo kama vizawadi, kupiga simu, kutuma sms, kusema nakupenda, kununua maua ni mambo ya kike, yaani hawaonyeshi juhudi yoyote kuwafurahisha wekea zao.

6. Wanaume Wanaopenda Kutumia Wake Zao (Panadol Husband).
Hawa huwa wanaume pale tu wanapokuwa na shida, wanakuwa na wake wazuri wanaowajali lakini wao wala hawajali. Wanapomhitaji mwanamke, wanapotaka mwanamke awafanyie kitu flani basi huja na maneno mazuri na hata kuleta vizawadi, wanajua udhauifu wa wake zao na huutumia kuwalaghai kuwatimizia mahitaji yao lakini wanapotimiziwa tu basi husahau hata kama wanawake, hawajali tena.

7. Wanaume Ambao Hawataki Kukua (Baby Husband).
 Bado wanatabia za kitoto, hawawezi kufanya maamuzi yao wenyewe mpaka kuuliza kwa ndugu zao, mtu kaoa lakini kila siku humpigia simu Mama yake kuuliza hiki na kile. Yaani wakiongea kitu na mke nilazima aulize ndugu kwanza ndiyo kipitishwa na mke akifanya kosaa kidogo kazi nikulinganisha mke na ndugu zake, mbona flani alifanya hivi, flani anaweza fanya zaidi na mambo kama hayo. Kwakifupi hawawezi kufanya maamuzi na mkewe, ndugu zake hasa Mama yake anakuwa kama shemeu ya ndoa.

8. Mume Mtalii (Visiting Husband).
Hawa wanakuja nyumbani kama wageni vile, mume ataihudumia familia yake kwa kila kitu lakini hawezi kuipa muda wake. Akirudi mke na watoto wamelala ni kugonga na hana sababu za msingi za kuchelewa, hata mwisho wawiki hupenda kutumia na marafiki au ndugu lakini si na mke. Hakuna kitu cha pamoja ambacho anafanya na mkewe au watoto wake, kila akiingia tu anakua na safari ya kutoka yaani hata atoke akakae nnje tu lakini si kukaa na mke au watoto.

9. Wanaume Wanaofuatilia Kila Kitu (Stalking Husband).
Hii ni aina ya wanaume ambao hufuatilia kila kitu, huchunguza kila kitu mwanamke anachofanya na hawampi pumzi. Akienda sehemu atachunguza anaenda na nani na alikutana na nani, huwa na wivu wa ajabu ajabu na kila saa huhisi wake zao ni wasaliti. Kila mtu mwanamke anayeongea naye wa jinsia tofauti huhisi ni mchepuko na hata marafiki wa mke wakike pia huhisi wanamkuwadia, kwakifupi hampi pumzi mwanamke.

10. Mwanaume Mbahili (Miserly Husband).
 Huyu anaweza kuwa na hela lakini mbahili ajabu. Akimpa mwanamke hela atafuatilia matumizi yake mpaka senti ya mwisho, anafuatilia mpaka mambo ya jikoni. Sukari ikiisha naataka ajue iliisha ishaje na kila mara huhisi mke anamuibia hela labda akajenge kwao, huwa msumbufu sana na mgumu kutoa hela. Mwanamke akifikiria mchakato wa kuomba hela kwa mume hukata tamaa na wakati mwingine kuamua tu kukaa kimya na matatizo yake.

UTAFITI Mpya: Pombe ni Hatari kwa Moyo Wako, Fahamu Kiasi Usichopaswa Kuvuka..!!!

$
0
0
Ingawa tafiti kadhaa zilizopita ziliwahi kueleza kuwa ni vyema kunywa kiasi fulani cha pombe kwa afya yako, utafiti mpya umebaini kuwa pamoja na hayo, kuna hatari kubwa ya kuvuruga mwendo wa mapigo ya moyo kwa kunywa pombe.

Kwa mujibu wa utafiti huo uliofanywa na timu ya wataalam wa sayansi wakiongozwa na Profesa Peter Kistler wa Hospitali ya Alfred iliyoko Melbourne nchini Australia, pombe ina madhara mengi kwenye mwili wa binadamu ambayo yanaweza kuchangia katika kuvuruga mwendo wa mapigo ya moyo.

Imeeleza kuwa hali hiyo inaweza kuwa chanzo cha magonjwa ya moyo pamoja na stroke (kupooza).

Imeeleza kuwa kunywa pombe kunaweza kusababisha udhaifu katika moyo na inaweza kuharibu mfumo wa mawasiliano unaoweza kusaidia seli za misuli ya moyo pamoja na mfumo wa fahamu ambao unasimamia kazi nyingi za mwili.

Watafiti hao wamewashauri watu ambao hunywa pombe lakini wamekuwa wakisikia mwendo wa mapigo ya moyo hauko vizuri wasitishe ama kupunguza kwa kasi kubwa matumizi ya vilevi.

Wakizungumzia kiwango cha pombe ambacho kinamfaa mtu ambaye ameanza kusikia mapigo ya moyo hayako sawa, apunguze hadi chupa moja ya pombe yenye kilevi cha kawaida na ahakikishe anapata siku mbili kwa kila wiki kutotumia kabisa kilevi.

Kazi hiyo ya watafiti hao iliyochapishwa kwenye jarida la American College of College of ardiology, ilifanya marejeo ya tafiti zaidi ya 100 na iliwahusisha takribani watu 900,000.

Viewing all 104776 articles
Browse latest View live




Latest Images