Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Mwanamke Atiwa Mbaroni Kwa Kumuua Mwanae na Mwingi kwa Kumuwekea Mwiko Sehemu za Siri

$
0
0
Mwanamke Atiwa Mbaroni Kwa Kumuua Mwanae na Mwingi kwa Kumuwekea Mwiko Sehemu za Siri
Wanawake wawili wanashikiliwa na polisi mkoani Morogoro kwa tuhuma mbalimbali akiwamo mmoja aliyemuua mtoto wake wa kiume wa miaka 11 kwa kumpiga fimbo kichwani.

Katika tukio jingine mwanamke mwingine anashikiliwa na polisi akituhumiwa kumsokomeza mwiko sehemu za siri mtoto wa dada yake mwenye umri wa miaka sita.

Kamanda wa polisi mkoani Morogoro, Wilbroad Mutafungwa amesema hayo leo Agosti 14 wakati akitoa taarifa ya matukio mbalimbali ya mkoani humo kwa waandishi wa habari.

Kamanda Mutafungwa amesema matukio yote yametokea katika wilaya za Gairo na Manispaa ya Morogoro na kwamba watuhumiwa wote watafikishwa mahakamani mara moja.

Natamani Mwanangu Afuate Nyayo Zangu - Gigy Money

$
0
0
Msanii wa bongo fleva na 'video vixen' nchini, Gigy Money amesema atajisikia furaha na amani endapo mtoto wake wakike aliyempa jina la Mayra, kuja kuishi kama alivyokuwa yeye kwa madai 'role model' wa mtoto ni mama pekee nasio mtu baki.

Gigy ametoa kauli hiyo leo Agosti 14, 2018 wakati alipokuwa anazungumza kwenye kipindi cha eNewz kinachorushwa na tinga namba moja kwa vijana EATV, na kusema haiwezi ikatokea mtoto akawa na role model tofauti na mtu ambaye amemzaa.

"Kila mtoto yoyote 'role model' wake ni mama yake mzazi hata iwaje.  Uwezi kusema mwanao atakuwa 'role model' wa mtu mwingine. Hivyo mwanangu atakuwa tu vyovyote atakavyotaka kuwa mimi nitampa ushirikiano. siwezi kumlaumu hata akitaka kuwa kama mimi ila ndio ntazidi kufurahi", amesema Gigy.

Pamoja na hayo, Gigy ameendelea kwa kusema "siwezi kujutia kuzaa halafu kingine ni kwamba kujipanga utajipanga baada huko wala hupaswi kuwaza kuwa itakuaje nikifanya jambo fulani. Maisha ya siku hizi hayana hiyo kitu, Mungu yupo kila siku anatenda".

Hii si mara ya kwanza kwa msanii Gigy Money kutoa kauli kama hizo kwani hata Juni 27, 2018 alipokuwa kwenye kipindi cha KIKAANGONI alitoa kali ya mwaka kuwa hakumbuki idadi ya mimba alizowahi kutoa licha ya kudai jambo hilo sio ufahari, huku akisisitiza zaidi kuwa ana lengo la kuanzisha timu ya mpira kupita watoto wake.

Baada ya Dereva Wake Kuuwawa Mbunge Bob Wine Akamatwa na Polisi

$
0
0
Baada ya Dereva Wake Kuuwawa Bob Wine Akamatwa na Polisi
Mbunge nchini Uganda Robert Kyagulanyi maarufu kama Boni Wine amekamatwa na polisi saa kadhaa baada ya dereva wake kuuawa kwa kupigwa risasi na polisi akiwa ndani ya gari lake.



Mbunge huyo wa Kyadondo aliandika kwenye mtandao wa Twitter kuwa walikuwa eneo linalojulikana kama Arua kwenye kampeni wakati mauaji hayo yalitokea. Uchaguzi mdogo unatarajiwa kuandaliwa eneo hilo Jumatatu katika juhudi za kumtafuta yule atakayechukua nafasi ya mbunge aliyeuawa, Ibrahim Abiriga .


Bobi Wine na viongozi kadhaa wa upinzani walikuwa eneo hilo kumuunga mkono mgombea huru Kassiano Wadri. Mikutano hiyo ilienda vizuri siku yote kabla ya polisi kuanza kukabiliana na wafuasi wa Wadri. Wafuasi wa Wadri nao waliripotiwa kukabiliana na wale wa mgombea wa NRM Tiperu Nusura.



Bobi Wine pia aliandika kuwa hoteli yake ilizingirwa na polisi kufuatia visa hivyo. Hata hivyo polisi wanasema kuwa wafuasi wa upinzani watalaumiwa kwa kuuliwa dereva huyo wa Bobi Wine Yasin Kawuma. Msemaji wa polisi Emilian Kayima, anasema watu waliokuwa wamevaa shati za kampeni za mgombea Wadri, walianza kuurushia mawe msafara wa rais hali ambayo ilisababisha polisi kufyatua risasi.



“Mwendo wa saa kumi na mbili unusu jioni msafara wa rais ulishambuliwa na wahuni katika manispaa ya Arua wakati rais alikuwa anaondoka uwanja wa Boma ambapo alikuwa amefanya mkutano wa mwisho,” Kayima alisema.

Watu Zaidi ya 35 Wafariki Dunia Baada ya Daraja la Mwendo Kasi Kuvunjika Italia

$
0
0
Watu Zaidi ya 35 Wafariki Dunia Baada ya Daraja la Mwendo Kasi Kuvunjika Italia
Kazi ya uokoaji imeendelea kufuatia kuvunjika kwa daraja la barabara ya mwendo kasi huko kaskazini mwa Italia katika mji wa Genoa na kusababisha vifo vya watu wapatao 35.

Picha ya video inaonyesha upande mmoja wa mnara ulisababisha daraja kuanguka kutokana na hali ya hewa kuwa mbaya. Sauti za kuomba msaada kutoka kwa watu wanaosadikiwa kunaswa katika mabaki ya daraja hilo zimesikika usiku kucha.

Tazama daraja la magari lilivyoanguka na kuuwa watu 30 Itali
Wafanyakazi wa dharura wanajaribu kuwatafuta watu walioanguka na magari yao huku wakiwa wanasaidiana na mbwa wenye utaalamu kwa kunusa .

Waziri wa usafirishaji Danilo Toninelli ameliongelea janga hilo kuwa kubwa na Ufaransa nayo imehaidi kushirikiana pamoja na Italia katika janga hilo.

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ameandika ujumbe wa pole katika ukurasa wake wa Twitter kwa waitaliano na wafaransa pia.

Jackline Wolper Alizwa na Wezi, Aonyesha Masikitiko Yake

$
0
0
Jackline Wolper Alizwa na Wezi, Aonyesha Masikitiko Yake
Mwanadada Jackline Wolper ameonyesha kusikitishwa na kitendo cha watu wanaofanya kazi ya kuiba navyorudisha nyuma maendeleo na kumvunja mtu moyo katika kitu kikubwa alichotaka kuwekeza au kukifanya kwa wakati huo.

Pamoja na kwamna mwanadada huyo hajasema moja kwa moja ni kitu gani amekumbana nacho au ameibiwa nini na ni wapi kati ya nyumbani kwake ao ufisini lakini katika ukurasa wke wa instagram , ameandika caption iliyofanya ielewekek kuwa hivi karibuni Jackline alilizwa na wezi.

Jackline aliandika ‘I cant , Mungu nipe nguvu” huku akiweka picha hii katika ukurasa wake

Askari Mstaafu wa JWTZ Atiwa mbaroni kwa Tuhuma za kukodisha silaha kwa majambazi

$
0
0
Askari Mstaafu wa JWTZ Atiwa mbaroni kwa Tuhuma za kukodisha silaha kwa majambazi
Askari mstaafu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) anashikiliawa na jeshi la polisi Mkoani Morogoro kwa tuhuma za kukodisha silaha kwa wahalifu  zinazotumika kwenye matukio ya ujambazi.

Akizungumza jana Agosti 14, kamanda wa polisi mkoani Morogoro, Wilbroad Mutafungwa alisema watuhumiwa 39 wa matukio hayo walihusishwa kwenye matukio ya uhalifu ikiwamo kukutwa na silaha za aina tano, bangi kete 200, bangi misokoto 66, risasi 27, pamoja na pombe aina ya gongo lita 58.

Mtuhumiwa Lumi Guya maarufu kama Mbulu (67) mkazi wa Kingolwira alikamatwa kwa tuhuma za kukodisha silaha yake aina ya Shot Gun anayoimiliki kihalali kwa watu wanaofanya uhalifu.

Kamanda huyo amesema mtuhumiwa huyo ni mwanajeshi mstaafu wa JWTZ na hushirikiana na Miraji Jumanne(28)mkazi wa Kichangani ambaye inadaiwa aliwahi kuwa askari polisi na kufukuzwa kutokana na vitendo visivyofaa wakishirikiana na wenzao sita ambao wote wanashikiliwa.

Watuhumiwa wengine walikamatwa katika matukio ya wizi, uuzaji gongo, wafugaji kulisha mifugo kwenye mashanmba ya wakulima na wizi wa kutumia silaha.

Meneja wa Wema Sepetu Aingilia Bifu la Zamaradi na Mobetto..Ampa za Pua Mobetto

$
0
0

Sokomoko la Zamaradi Mketema na Hamisa Mobeto, muigizaji Neema Ndepanya ambaye pia ni meneja wa Wema Sepetu aamua kumkingia kifua Zamaradi. Neema amepost picha ya Zamaradi na kuandika ...
.
"Sometimes people will be mad at u because you are not a lying ass motherfu**ker as they are... @zamaradimketema don't let anyone get comfortable disrespecting u hunie!!NEVER!!
Kiki za kuchafuana zilishapitwa na wakati...hakuna kitu kibaya dunian kama kuwa MNAFKI..
MNAFKI ni MUUAJI...
DONT PLAY SMART BITCH!!!
Yani nachukia mtu anajifanya kila wakati anaonewa yeye...uonewe kwa kipi bwana??kama pumzi wote tunavuta bure na utafutaj kila mtu anatafuta kwa njia zake hata awe mama mpika mandazi kama mm...
Kama ni hivyo wamama wanaopanga mandazi yao barabaran wangetuchukia sana kisa leo nimebadili kwenda kununua kwa mwingine??
Em punguza utoto wa kipumbavu shubaamit!!
Wengine tushakuwa wazee mambo ya kutukanana mitandaon yamepitwa na wakat...
Umechelewa sana bidada enzi za kutafuta kiki kwa kumchafua mwenzako zishaisha...
Unapenda drama kuliko kazi..... ACHA TABIA YA KUJITILISHA HURUMA UONEKANE UNAONEWA WENZAKO WAONEKANE WAKOSAJI...UNAJIFANYA ETI HUJUI KUONGEA MXIUUUUUU UONGO UMEKUJAA MPAKA UNAONA HAYA KUANDIKA UKWELI UNAJIFANYA HUPENDI KUONGEA SHENZI!! TABIA CHAFU SANA HII

Nigeria Kama Bongo Vile...Waufungia Wimbo wa This is Nigeria

$
0
0

Baada ya takriban miezi mitatu toka Falz The Bad Guy kutoka This Is Nigeria ambayo ni cover version ya This Is America ya Childish Gambino, Nigeria Broadcast Regulator WAMEFUNGIA Rasmi wimbo Na Video ya Wimbo huo kuchezwa au kuonyeshwa kwenye vyombo vya habari Nigeria. .

Wimbo huu wa Falz umeongelea mapungufu yote ya nchi ya Nigeria na kuonyesha wazi ubaya wa nchi hio na watu wake kupitia mistari kama

“This is Nigeria, everybody be criminal.” 'Hii ndio Nigeria, kila mtu ni Muhalifu'. umepelekea NBC kuwa na mamlaka ya kufungia wimbo huo.

NBC wataweza kuzuia wimbo kwenye yombo vya habari ila sio mtandaoni sababu Youtube hawajaona kosa la rekodi hio, mpaka sasa video inawatazamaji milioni 13.

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

$
0
0

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Awataka Watumishi wa Halmashauri Kurudisha Milioni 41 Ndani ya Siku 15

$
0
0
Mukuu wa Mkoa wa Njombe Awataka Watumishi wa Halmashauri Kurudisha Milioni 41 Ndani ya Siku 15
Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Christopher Ole Sendeka, amewataka watumishi wa halmashauri ya wilaya ya Makete waliotumia vibaya fedha za miradi ya maendeleo wilayani humo zaidi ya milioni 41 zirudishwe kabla ya tarehe 30 mwezi huu.


Mkuu wa mkoa wa Njombe, Christopher Ole Sendeka.

Ole Sendeka, ametoa agizo hilo katika kikao cha madiwani wa halmashauri hiyo na kujadili hoja za mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali ambapo amewataka madiwani kusimamia na kuhoji fedha za miradi ya maendeleo ili kuwezesha fedha hizo kufanya kazi kama zilivyokusudiwa.

Katika mkutano huo kubwa lililoibuka ni upotevu wa miradi ya Afya katika halmashauri hiyo ziliztolewa kwa msaada wa shirika la kuhudumiwa watoto Duniani UNICEF, Shilingi milioni 41 ambapo baadhi ya wataalamu wamehusishwa na upotevu huo.

“Licha ya baadhi ya fedha kuokolewa na TAKUKURU lakini kuna baadhi ya fedha zinatakiwa kutolewa majibu ya kina juu ya matumizi yake lakini mpaka ifikapo tarehe 31 wawe wameshaziridisha fedha hizo”, amesema Ole Sendeka.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amewataka madiwani kujenga utamaduni wa kuwahoji wataalamu kuhusu fedha za miradi mbalimbali ya halmashauri.

June 9, 2017  wakati akifungua semina ya mtandao wa wabunge wa Afrika walio katika mapambano ya rushwa (APNAC) tawi la Tanzania, Waziri Mkuu  Kassim Majaliwa alisema serikali imefanikiwa kuokoa Sh bilioni 53.9 kutokana na uchunguzi na operesheni mbalimbali zilizofanywa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) katika mwaka 2016/2017.

Watano Wafariki dunia dereva Akikimbia Askari wa Doria

$
0
0
Watano Wafariki dunia dereva Akikimbia Askari wa Doria
Watu watano wamefariki dunia papo hapo na wengine watatu kujeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kutoka Busurwa mwambao wa Ziwa Victoria wilayani Rorya kwenda mjini Tarime kupinduka.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tarime na Rorya, Henry Mwaibambe amesema ajali hiyo ilitokea katika kitongoji cha Bukwe eneo la Mika alfajiri ya jana Agosti 14, 2018, ambapo uchunguzi wa awali umebaini chanzo cha ajali ni mwendo kasi uliosababishwa na dereva aliyekuwa akiwakimbia askari wa doria.

Kamanda Mwaibambe amesema dereva wa gari hilo aliyejulikana kwa jina la Athumani Masiaga ambaye ni miongoni mwa waliofariki dunia alikataa kutii amri ya kusimama iliyotolewa na askari wa usalama barabarani kutokana na kubeba samaki wanaosadikiwa kupatikana kutokana na uvuvi haramu.

Kamati Kuu ya Chadema Kukutana Leo

$
0
0
Kamati Kuu ya Chadema Kukutana Leo
KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) inakutana leo jijini Dar es Salaam kujadili mambo muhimu ikiwamo kufanya tathmini ya uchaguzi wa marudio uliofanyika Jumapili iliyopita.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa jana kwa vyombo vya habari na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Chadema, Tumaini Makene, kamati hiyo inakutana kujadili masuala mbalimbali muhimu kuhusu chama hicho na taifa.

Katika taarifa hiyo, Makene alisema miongoni mwa mambo makuu yatakayojadiliwa katika kikao hicho leo ni kupokea taarifa na kujadili juu ya uchaguzi wa marudio wa ubunge, udiwani na hali ya siasa nchini.

"Kikao kitafanyika jijini Dar es Salaam chini ya Mwenyekiti wa chama, Freeman Mbowe, kitajikita katika masuala mawili, kupokea taarifa na kujadili kwa kina juu ya uchaguzi wa marudio wa ubunge na udiwani na hali ya siasa nchini," alisema Makene katika taarifa hiyo na kuongeza:

"Wanachama wa Chadema na umma wa Watanzania kwa ujumla utataarifiwa kuhusu maazimio baada ya kikao hicho."

Mbali na wabunge na madiwani kujiuzulu na kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM), chama hicho kikuu cha upinzani nchini kimefanya vibaya katika uchaguzi wa Jumapili kwa kulipoteza kwa wapinzani wao hao Jimbo la Buyungu mkoani Kigoma.

Uchaguzi wa marudio umefanyika katika jimbo hilo kutokana na kufariki dunia kwa aliyekuwa mbunge wake, Kasuku Bilago (Chadema).

Vodacom Yajitoa Udhamini Ligi Kuu Bara

$
0
0
Vodacom Yajitoa Udhamini Ligi Kuu Bara
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) kupitia Bodi ya Ligi limeweka wazi kuwa ligi kuu msimu ujao itakuwa na wadhamini wawili ambao ni Azam Pay TV na Benki ya KCB baada ya kampuni ya mawasiliano ya Vodacom kumaliza mkataba wake.



Kwa mujibu wa barua iliyotumwa na Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi Boniface Wambura, inasema kuwa ligi hiyo itakuwa na wadhanini hao ambapo Azam watakuwa na haki ya matangazo wakati KCB wakiwa ni wadhamini wenza kwenye ligi hiyo.

Haji Manara: Nitaachia Ngazi Ndani ya Simba Endapo Timu Itapoteza Dhidi ya Arusha United Leo

$
0
0
Haji Manara: Nitaachia Ngazi Ndani ya Simba Endapo Timu Itapoteza Dhidi ya Arusha United Leo
Ofisa Habari wa Simba SC, Haji Manara, amesema ataachia ngazi ndani ya klabu hiyo endapo timu yake itapoteza mchezo dhidi ya Arusha United leo.

Manara ametoa kauli hiyo kuelekea mchezo wa leo wa kirafiki ambapo Simba itacheza na Arusha United kufuatia mwaliko maalum na Mkuu wa Mkoa huo, Mrisho Gambo.

Ofisa huyo amefunguka akiamini kuwa Simba haiwezi kufungwa na Arusha United huku akitamba kumuahidi kipigo Gambo katika kipute hicho.

"Kama Arusha United wakishinda leo mimi nitaachia rasmi ngazi ndani ya Simba, siamini kama wanaweza wakatufunga" alisema.

Aidha, uongozi wa Simba umesema utautumia mchezo huo kama sehemu ya kuiandaa na mechi ya Ngao ya Hisani dhidi ya Mtibwa Sugar.

Simba watakapiga na Mtibwa jijini Mwanza Agosti 18 ndani ya Uwanja wa CCM Kirumba ukiwa unaahsiria kufunguliwa rasmi kwa pazia la Ligi Kuu Agosti 22 mwaka huu.

Alikiba Achafua Hali ya Hewa... Awaweka Mashabiki Zake Njia Panda

$
0
0
Alikiba Achafua Hali ya Hewa...  Awaacha Watu Njia Panda
Msanii wa BongoFleva mwenye 'hit song' ya 'Mvumo wa Radi', Alikiba amewaacha njia panda mashabiki zake baada ya yeye kuweka picha mfululizo kwa siku moja katika mtandao wake wa Instagram, jambo ambalo limewafanya kufikiri kuwa ni ujio wake mpya wa kutoa wimbo baada ya kukaa kimya kirefu.

Muda mchache kupita baada ya kuwekwa picha hizo, mashabiki hao walimiminika katika na kuanza kutoa maoni yao binafsi mbalimbali, huku wengine wakijaribu kumshauri kwa namna moja ama nyingine juu ya sanaa yake.

Miongoni mwa ujumbe zilizokuwa zikitawala chini ya picha hizo ni pamoja na;

"Naziona dalili zote za wimbo mpya yakufungia mwaka", ameandika barrish_holictz.

"The king always is different with other people kimawazo kifikra pia hata kwenye kufanya mambo yake. Huwa halazimishi kabisa kufanana na wengine 'like that guy'. Yani ni mtu makini sana na hana ushindani kwenye 'game' maana anaamini kipaji chake, wanao toa nyimbo 100 na yeye wimbo moja halafu wewe uliotoa moja inakua homa ya jiji kuliko waliotoa nyimbo 100", ameandika chii_beiby_quetface.

"Kwa mapicha picha haya bila shaka 'new hit is coming", ameandika prince_blessed

"Achia dude mzee baba", ameandika officialgerard_hero

"Nasikia harufu ya ngoma mpya", ameandika officia_topdenny251



Hii si mara ya kwanza kwa Alikiba kutumia njia ya aina hiyo kuweka 'attention' kwa watu kwani itakumbukwa mnamo mwezi Agosti mwaka 2017, alifanya vitu kama hivyo alipokuwa kwenye show yake mjini New York nchini Marekani na baada ya kupita siku kadhaa alitoa wimbo wake wa 'Seduce Me' ambao hadi sasa umetazamwa na takribani watu milioni 9.94 kupitia akaunti yake ya 'Youtube'.

Kwa upande mwingine, Alikiba siku ya Ijumaa anatarajia kufanya show katika mji wa Toronto nchini Canada ambapo atakuwa na wasanii wengine kama Yemi Alade, Falz the Bahd Guy, Sheebah, Dj Spinall, Zahara, Nonso Amadi pamoja na Nsoki.

Kikwete Amtembelea Kigwangwala Hospitalini Kumjulia Hali

$
0
0
Kikwete Amtembelea Kigwangwala Hospitalini Kumjulia Hali
Rais Mstaafu wa awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete jioni ya tarehe 14, Agosti 2018 amemtembelea na kumjulia hali Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangalla aliyelazwa katika wodi maalum kitengo cha Taasisi ya mifupa MOI, hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam.




Rais Mstaafu wa awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Andrew Chale ambaye ni Mwandishi wa Habari Maalum wa Waziri wa Maliasili na Utalii Dk Hamisi Kigwangalla. Kulia ni Dkt. Bayoum Awadhi Kigwangalla mke wa Waziri Dkt.Kigwangalla.



Hii inakuwa ni mara ya pili kwa Kikwete kumtembelea Dk Kigwangalla ambapo awali alimtembelea Agosti 8, alipokuwa amelazwa Wodi ya Mwaisela akipatiwa Matibabu ya awali. Kikwete amemtakia kila lakheri katika kipindi hiki kwa kuuguza majeraha ya mkono na sehemu za mwili ikiwemo mbavu ambazo kwa sasa hali yake inaendelea kuimarika kwa majibu wa Madaktari wa kitengo hicho cha mifupa MOI.



Awali tokea kufanyiwa operesheni ya mkono ameweza kufanya mazoezi taratibu ikiwemo kutembea mwenyewe katika viunga hivyo vya Muhimbili. Dkt. Kigwangalla alipata ajali ya gari mnamo Agosti 4, 2018 huko Manyara akiwa katika ziara ya kikazi ambapo katika ajali hiyo iliyokuwa na watu 6, watano walijeruhiwa na mmoja alifariki dunia ambaye alikuwa afisa habari mwandamizi wa Wizara hiyo, Hamza Temba.

Wema Sepetu Ampiga Vibao Chazi Baba Kisa Sajenti

$
0
0
Wema Sepetu Ampiga Vibao Chazi Baba Kisa Sajenti
KIBANO! Ndivyo unaweza kusema kufuatia kitendo alichofanya mwanadada kipenzi wa Watanzania, Wema Isaac Sepetu cha kumzaba vibao mpenzi wake wa zamani, Charles Gabriel ‘Chaz Baba’ kisa kikiwa ni msanii wa Bongo Muvi, Husna Idd ‘Sajenti’.

Mtiti huo ulitokea usiku wa kuamkia Jumatatu iliyopita kwenye ukumbi wa burudani wa The Club Legend (zamani Nyumbani Lounge), ambapo Bendi ya The African Stars ‘Twanga Pepeta’ ilikuwa ikikamua katika moja ya shoo zake za wiki.

ILIKUWA HIVI

Baada ya Chaz Baba kuburudisha jukwaani na wanamuziki wenzake, alishuka na kwenda maliwatoni, wakati akitoka huko alikutana na Wema njiani na baada ya mazungumzo machache, wapenzi wa burudani walishuhudia mlimbwende huyo aliyewahi kutwaa Taji la Miss Tanzania 2006 akimzaba makofi kadhaa Chaz Baba.

KALALA AMTOA

Wakati tukio hilo likizua taharuki ukumbini hapo, msanii mwenzake na Chaz Baba, Kalala Hamza ‘Junior’ ambaye alikuwa karibu, alimsogelea Wema na kumtoa nje ya ukumbi kwa kusaidiana na msaidizi wa karibu wa Wema aitwaye Agrey.

RISASI LAMVAA WEMA

Wakati Wema akiondoka Risasi Mchanganyiko, ambalo lilikuwa ‘busy’ kufuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea ukumbini hapo lilimvaa ili kufungukia kile ambacho kilikuwa kimetokea. Lakini baada ya kuulizwa, Wema alijibu kwa maneno mawili tu ya Kingereza; “No comment.” Risasi Mchanganyiko, lilijaribu pia kumbana lakini alikataa katakata kuzungumza lolote lile zaidi ya hapo.

CHAZ BABA AFUNGUKA

Kwa upande wa Chaz Baba, baada ya kufuatwa ili kuzungumzia tukio hilo, alisema kwamba hata yeye mwenyewe alishangazwa na kitendo alichokifanya Wema kwani hakukitegemea. “Tulikuwa vizuri tu maana jioni tulikuwa naye pamoja kwenye kikao cha kamati ya Miaka Ishirini ya Twanga maana na yeye ni mjumbe, tunategemea kusherekea naye siku hiyo kwa sababu itakuwa ni siku yake ya kuzaliwa pia usiku huo.

“Hakukuwa na shida yoyote. Sasa nimeshuka jukwaani naenda maliwatoni mara nikakutana naye akaanza kuniuliza kwa nini Sajenti ananiposti kwenye mitandao ya kijamii na kwa nini tupo karibu. “Mimi nilimjibu kuna shida gani kwa sababu nina uhuru wa kuwa karibu na mtu yeyote yule na yeye hawezi kunipangia masharti kwa sababu si mpenzi wangu.

“Nilipomjibu tu hivyo nilishitukia nazabwa makofi kadhaa usoni. Kalala alikuwa karibu ikabidi amtoe. Kiukweli ni kwa sababu ni mwanamke lakini angekuwa mwanaume mwenzangu pangechimbika,” alisema Chaz Baba.

Risasi Mchanganyiko, lilimuuliza kama amerudiana na Wema lakini alikataa juu ya hilo na kuongeza kwamba kuhusu Sajenti hawezi kuacha kuwa naye karibu kwa sababu mbali na kuwa si wapenzi lakini bado atabakia kuwa mzazi mwenzake.

Risasi Mchanganyiko lilijaribu kumtafuta Sajenti ili kumsikia anazungumziaje ishu hiyo lakini simu yake haikupokelewa hadi tunakwenda mitamboni.

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME DR SITTA NDO SULULISHO LAKO tatiza, hili limekuwa likiwaasili watu wengi,sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine, kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo zipo , sababu nyingi zinazosababisha, tatizo hilo baadhi ni (i) upungufu wa vichocheo vya HORMONES ZA CETROGEN ambazo mwanaume, anapobarehe vichocheo hivi, HORMONES hizo, husaidia ukuaji wa uume

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mlija iliysinyaa,

NSHOLA ni dawa bora, ya kurudisha nguvu, za, kiume bari inatibu ,kabisa kutoa tatizo hilo, na kukupa , hamu ya , kurudia tendo, la ndoa zaidi, ya mala nne 4 ,bila kuchoka atakama unaumli ,wa mika 80,! pia ana ,dawa za ,kutibu, presha ya kupanda ,na kushuka, kisukari kuondoa, mafuta , mwilini ,na maumivu ya, mgogo kiuno, dawa zipo, matazo, ya hedhi, kwa ,wanawake hedhi, zisizokuwa na, mpangilio, na kasonono, pia , vidonda ,vya, tumbo ,(STOMACHI UCLENS) IHUSHI ndoji lako.

NKANYA ni dwa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi ariyekuacha, mke mme, atakuludia kwa, mda, wa msaa3 tu , ukishaitumia atarudi ,mwenyewe bila ,ugovi tena, NKOMA ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada .

HERBON, ni, dawa, ya kuongeza, CD4, NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu ,miguu, kufaganzi, na ,kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! DR SITTA, amebobea, kwa tiba asilia

DAR ANAPATIKANA MBAGALA, ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI SHINYANGA, KAHAMA MJINI, KWA MAELEZO ZAIDI , PIGA SIMU 0763172670 au 0715172670

WOTE MNAKALIBISHWA, KAMA, UTAKUWA NA TATIZOUTAHUDUMIWA

Steve Nyerere Aongelea Kuhusu Post Aliyosema Ndoa ya Wema Sepetu Inakuja Hivi Karibuni

$
0
0
Steve Nyerere amezungumza na Ayo TV kuhusu post yake ambayo ilizua gumzo mtandaoni baada ya kupost picha ya Wema Sepetu na mwanaume anayefahamika kwa jina la Rahul ya kuwa ndoa ya hao wawili inakaribia. Steve aliweka picha hizo na kuambatanisha na caption iliyosomeka ‘Wedding is Coming soon”.

Ikumbukwe tu Wema Sepetu na Rahul wamekuwa wakidaiwa kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi licha ya kwamba wawili hao wamekuwa wakikataa kuthibitisha hilo na hata hivyo Ayo TV iliwai kufanya mahojiano na Rahul ambaye alisema kuwa Wema ni mshikaji wake wakaribu tu na siyo mpenzi wake.

Msikilize STEVE NYERERE akizungumza ni kweli WEMA ANAOLEWA HIVI SOON..? Bonyeza PLAY hapa chini.


Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images