Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live

Habari za Kuwa Ndege ya Dream Liner ni Mbovu....Mkurugenzi wa ATCL Afunguka

0
0

Mkurugenzi wa ATCL amekanusha taarifa kuwa, Dreamliner ni mbovu na kwamba ilisitisha safari yake ya Mwanza - Dar. Amesema, wamesimamisha safari ili ifanyiwe matengenezo kwani kwa sasa ipo katika majaribio. Ameeleza kuwa, itaanza safari za kimataifa mwezi huu kwenda Mum

Adhabu ya Viboko Kumbe Bado IPO Mashuleni...Ona Huyu Alivyochapwa Huko Arusha

0
0

ARUSHA: Mwanafunzi wa Kidato cha Kwanza katika Shule ya Sekondari Kinana ajeruhiwa mkono baada ya kupigwa fimbo 12 na Mwalimu wake

Inadaiwa kuwa sababu ya adhabu hiyo ni Mwanafunzi huyo kukosea kujibu swali.

Mwanafunzi amedai kwamba Mwalimu huyo aliyetajwa kwa jina la Mkama aliacha kumuadhibu baada ya kuona ameanza kujeruhika.
TOA MAONI YAKO HAPA

H Baba Amtetea Diamond na WCB Sakata la Rich Mavoko

0
0

Msanii anaefanya mziki wa dance nchini, H.Baba ameibuka na kumshauri Diamond baada ya taarifa kusambaa kuwa Rich Mavoco amejitoa WCB, huku sababu ya kujitoa kwake ikitajwa kuwa ni unyonyaji unaofanywa na lebo hiyo, kupitia ukurasa wake wa instagram H.baba ameandika ujumbe huo kama unavyosomeka hapo chini

"@diamondplatnumz #Polee sana ni muda wakujifunza maisha na watu ni vitu viwili tofauti #Umakini ulionao wewe sio wakila binadamu anaumakini huo #kujitambua kwako nakujipambania kwa uwezo wako nakumuomba Mungu sio Jambo la kawaida kwa mdharau Mwiba #kama kunatofauti yako na #Mr.mavoko limalizeni kiustaarabu naamini mnafahamiana vyema na Mr. Mavoko toka kitambo Mimi natoka mwanza nimewakuta kwenye game japokuwa siku ya kila mmoja kutoboa Mwenyezi Mungu ameiwekea siri kubwa ili ukate tamaa #Amkukata tamaa Kila mmoja akatoboa kwa njia yake Onyeshaneni upendo Sanaa inasiri kubwa #Kioo Cha jamii kwa msanii niinshu kubwa Sana ila tunachukulia poa jambo hili #Wekeni sawa swala lenu #Unyonyaji unaosemekana kuwa #WCB niwanyonyaji sio kweli #WCB hawanauwezo wakumnyonya msanii ila msanii anaouwezo wakuwanyonya #WCB Kwa sababu nyingi sana watazame kina #MBOSO #LAVALAVA je ninani anamnyonya mwenzie utagundua WCB wanautu #wcb niwapambanaji ila Kama upambani auwendani na Kasi ya #MR.KAUNGURUMA.. #Simbaaa #lazima utaomba poooo #Uvumilivu kwenye Sanaa ndio misingi ya sanaa yetu #Ukifata yawalimwengu utakuwa mtazamaji wa walimwengu #Ninamengi yakusema kwa Leo niishie hapa #lawama sio mzigo." H Baba

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

0
0

KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME DR SITTA NDO SULULISHO LAKO tatiza, hili limekuwa likiwaasili watu wengi,sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine, kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo zipo , sababu nyingi zinazosababisha, tatizo hilo baadhi ni (i) upungufu wa vichocheo vya HORMONES ZA CETROGEN ambazo mwanaume, anapobarehe vichocheo hivi, HORMONES hizo, husaidia ukuaji wa uume 

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mlija iliysinyaa, 

NSHOLA ni dawa bora, ya kurudisha nguvu, za, kiume bari inatibu ,kabisa kutoa tatizo hilo, na kukupa , hamu ya , kurudia tendo, la ndoa zaidi, ya mala nne 4 ,bila kuchoka atakama unaumli ,wa mika 80,! pia ana ,dawa za ,kutibu, presha ya kupanda ,na kushuka, kisukari kuondoa, mafuta , mwilini ,na maumivu ya, mgogo kiuno, dawa zipo, matazo, ya hedhi, kwa ,wanawake hedhi, zisizokuwa na, mpangilio, na kasonono, pia , vidonda ,vya, tumbo ,(STOMACHI UCLENS) IHUSHI ndoji lako. 

NKANYA ni dwa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi ariyekuacha, mke mme, atakuludia kwa, mda, wa msaa3 tu , ukishaitumia atarudi ,mwenyewe bila ,ugovi tena, NKOMA ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada . 

HERBON, ni, dawa, ya kuongeza, CD4, NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu ,miguu, kufaganzi, na ,kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! DR SITTA, amebobea, kwa tiba asilia 

DAR ANAPATIKANA MBAGALA, ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI SHINYANGA, KAHAMA MJINI, KWA MAELEZO ZAIDI , PIGA SIMU 0763172670 au 0715172670 

WOTE MNAKALIBISHWA, KAMA, UTAKUWA NA TATIZOUTAHUDUMIWA

Sallam SK: Uongozi wa WCB na Uongozi wa Alikib Tunakutana Mara kwa Mara

0
0
Sallam SK: Uongozi wa WCB na Uongozi wa Alikib Tunakutana Mara kwa Mara
Mmoja kati ya mameneja watatu wa Diamond Platnumz, Sallam SK amedai kwamba viongozi wa WCB huwa wanakutana mara kwa mara na uongozi wa Alikiba na kuzungumza mambo mbalimbali.


Jumatano hii meneja huyo akiwa Times fm akifunguka mambo mengi huku WCB pamoja na muziki ambapo pia alifunguka kueleza kwamba sio kweli kwamba Diamond ana bifu na Alikiba huku akienda mbali zaidi kwa kudai viongozi wa label hizo mbili hukutana mara kwa mara.



“Kati ya Ali na Diamond hakunaga bifu, na haijawi kutokea, na uongozi wa Alikiba na WCB huwa unakutana mara kwa mara kuzungumza,” alisema Sallam. “Bifu ilitengenezwa na sisi baada ya kuona watu wanapenda hivyo vitu tukavitumia kwaajili ya kupromote wimbo wetu,”

Marapa Tekashi69 na 50 Cent Washambuliwa kwa Risasi

0
0
Marapa Tekashi69 na 50 Cent Washambuliwa  kwa Risasi
MARAPA Tekashi69 na 50 Cent, wote wa Marekani, walipata taharuki juzi (Jumanne) wakati wakishuti video ya muziki eneo la Brooklyn, New York, ambapo mtu mmoja aliyekuwa katika gari aina ya  Porsche jeupe, alirusha risasi 11 usiku mnamo saa 4:30.

Hata hivyo, risasi hizo zilizokuwa zikitoka kwenye gari hilo, hazikumdhuru mtu yeyote.

Marapa hao walikuwa pia na wanamuziki Casanova na Uncle Murda katika kushuti video hiyo.


Polisi hawajamkamata yeyote aliyehusika na kitendo hicho, japokuwa kuna wakati mwanamuziki Chief Keef, aliwahi kurushiwa risasi baada ya kutokea bifu kati yake na Tekashi.

Odama Atoa Kauli Nzito Kwa Aliyemzushia Kifo

0
0
Odama Atoa Kauli Nzito Kwa Aliyemzushia Kifo
IKIWA ni saa chache baada mtu asiyejulikana kusambaza taarifa kwenye mitandao ya kijamii kwamba msanii wa filamu nchini, Jenifer Kyaka maarufu ka Odama amefariki dunia, msanii huyo ameibuka na kutoa kauli nzito kwa mtu aliyetenda jambo hilo.



Odama amesema inaonyesha mtu aliyemfanyia hivyo ana chuki binafsi na kusema anatambua kama ipo siku itafika atakufa kwani kila nafsi itaonja mauti huku.



“Kifo kipo na hakuna atakaekikwepa, kila binadamu ataonja mauti na kukamilika kwa maisha yetu hapa duniani. Lakini pia hata kama humpendi mtu unamchukia iwe alikutendea ubaya au umeamua tu kumchukia sio vizuri kumuombea kifo tena ukaona haitoshi basi unaweka matangazo mitandandaoni.



‘Nakushukuru wewe ulieamua kufanya hili, najua unaniongezea umri wa kuishi, na nikuambie tu kua mimi ni mzima wa afya na ninaishi kwa kudra za Mungu. Nitakufa tu pale siku yangu itakapofika mungu atakapoamua kunichukua lakini sio kwa kutaka wewe.



“Sijui nilichokukosea mpaka kufikia kunitangazia kifo. Nakuombea maisha marefu ili uendelee kuniona nikivuta pumzi ya mungu. Binadamu sisi laiti tungelijua kua si kitu kabisa tungeacha chuki zisizo na sababu. Asante mungu kwa kila kitu,” ameandika Odama.



Jambo la kuzushiwa vifo kwa mastaa na viongozi maarufu limekuwa likikithiri siku hadi siku, ikumbukwe kwamba enzi za uhai wake, Mzee Majuto aliwahi kuzushiwa kifo mara kadhaa na yeye kukanusgha, wengine ni Mzee Agustiono Mlema na wengine jambo ambalo si la kiungwana.

Katibu Mkuu CCM Asimulia Alivyokerwa na Swali la Mwandishi Aliyehoji Kuhusu Elimu Yake

0
0
Katibu Mkuu CCM Asimulia Alivyokerwa na Swali la Mwandishi Aliyehoji Kuhusu Elimu Yake
Siku mbili baada ya Katibu Mkuu wa CCM, Dk. Bashiru Ally, kufanya mkutano na waandishi wa habari na baadhi ya watu kudai kwamba sifa ya kuibua mijadala aliyonayo imeingia dosari kutokana na namna alivyojibu maswali ya wanahabari, mwanazuoni huyo ameibuka na kusema hajutii.

Katika mahojiano kwenye kipindi cha televisheni cha 360 kinachorushwa na Clouds Tv, Dk. Bashiru alisema alionyesha ukali na hajutii jambo hilo.

“Kuna yule (anataja chombo chake) alinikera kwa kuhoji elimu yangu, akisema kwamba sijaitumia vizuri kukidhi matarajio na kwamba mimejibu rojorojo, huko ni kuwatukana Watanzania ambao wamenisomesha.

“Anapohoji uwezo wangu kielimu anawahoji walionisomesha kwa vipesa vyao, kwa kuwa nimesoma katika shule za umma tangu mwanzo,” alisema.

Alisema yeye ni mwanataaluma ambaye hakuwahi kununua mtihani wala kushindwa popote, akiwa na maandiko yake ambayo mtu anaweza kuyakosoa, lakini yanakubalika ubora wake.

Dk. Bashiru alisema huenda sehemu ya maarifa hayo ndiyo yaliyompa nafasi aliyonayo sasa, kwahiyo si sahihi kuhoji rejareja kwa kuanza na swali linalokera.

Alisema Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe, alimpigia simu na kumweleza kuwa alipoulizwa swali hilo alipaswa kushuka badala ya kupanda na yeye akamjibu aliamua kupanda naye (mwandishi) na angepata nafasi angepanda naye zaidi.

“Lengo lilikuwa ni kutuma ujumbe kwamba wanapokusanyika kuzungumza, waheshimiane kwa sababu masuala ya mijadala yanahitaji kusikilizana,” alisema.

Alisema mijadala ni tofauti na porojo, kelele na mizaha katika mazungumzo, lakini mkutano wake na waandishi wa habari ulikuwa ni fursa muhimu kwao na yeye pia katika kuwasiliana na umma.

“Lakini mimi sikuridhika na naamini waandishi pia hawakuridhika,” alisema.

Kuhusu swali aliloulizwa kwamba kama CCM imeshindwa kuheshimu katiba yao ni vipi kitaheshimu ya nchi, alisema anamfahamu mwandishi aliyemuuliza swali hilo kuwa ni mwanachama wa Chama cha CUF na kwamba swali lake lilikuwa na mwelekeo wa kiitikadi.

“Hawa wanahabari walichukua mwelekeo wa kiitikadi na kuwakosesha watazamaji wasaa wa kupata ufafanuzi mzuri kwa namna swali linavyoundwa,” alisema.

Akizungumzia ustahimilivu wake kisiasa, Dk. Bashiru alisema anaweza kuvumilia jambo ambalo halimuui, lakini hawezi kuvumilia lile analoona linamuua na kwamba atakapoona anauawa atajitetea ili aendelee na mijadala.

Akizungumzia siasa za matusi, Dk. Bashiru alisema tatizo hilo la siasa za ugomvi, liliibuka katika vyama vyote wakati wa uchaguzi mkuu, lakini tatizo lilikuwa kubwa zaidi CCM.

Alisema pia wanachama wengi wa chama hicho waliondoka kwa sababu kilitengeneza mfumo ambao bila kuwa na fedha ni vigumu kupata uongozi na kwamba baadhi walitaka vyeo ili wapange safu zao.

Kuhusu kuhama kwa wabunge, madiwani na viongozi wengine wa upinzani na kujiunga na CCM, alisema vyama husika vijitathimini kwanini watu hao waondoke kwao.

“Iweje ndani ya muda mfupi vinakimbiwa na wanachama na kukimbilia mahala pengine?” alihoji.

Dk. Bashiru alipoulizwa kama anadhani ni muhimu nchi ikarudi kwenye mfumo wa chama kimoja, alisema; “wingi wa vyama siyo demokrasia, umadhubuti wa mfumo wa vyama vingi ndiyo suala muhimu.

“Bado mfumo wetu wa vyama vingi ni legelege na vyama havijakua kitaasisi, hata CCM bado inabidi kuimarishwa kuwa chama madhubuti.”

Alisema hata kama vyama vitapukutika na kubaki viwili, haoni kama ni faida au hasara kwa kuwa itategemea vinavyobaki vinatoa mchango gani na kwamba kinachohitajika ni wananchi kuamua.


Ray C, Koletha Mstari wa Mbele Kumshabiki Zari

0
0
Ray C, Koletha Mstari wa Mbele Kumshabiki Zari
Sio kila mmoja anawez akukuchukia vile anaweza kukuchukilia mwingine  vile kundi kubwa la watu wanvayoweza kukuchukulia wewe.pamoja na kwamba mwanadada Zari the bossy amekuwa akipata upinzani mkali sana instagram ahasa katika page mbalimbali za udaku lakini kuna watu bado wanampenda na wanamsifia kila kukicha.

Mwanadada Ray c amekuwa moja ya watu hao wanaomsifia na kumpongeza kila kukicha na kila anapofanya jambo zuri, wikiendi iliyopita mwanadada zari aliweka picha nyingi zinazomuonyesha akiwa katika mashindano ya u-miss huko nchini kwao, wapo waliomponda sana kuwa hajapendeza na gauni alilovaa lakini iemkuwa tofauti kwa mwanadada Ray c na Koletha akutoka bongo movies.

Wasanii hawa wawili wameonekana kutokuwa na team  zamitandao na kumpongeza zri kwa kupendeza huko, wa upande wa Rayc pia amekuwa moja ya watu wanaopenda sana kukosoa kila anapoona mtu mmoja anaingiliwa na kushambuliwa sana katika mitandao ya kijamii , kwa mfano aliwahi kumttetea na hata kumkosoa hamisa kutokana na mambo tofauti tofauti.

Casto Dickson Akana Kuitwa Mario kwa Tunda ''Unaniita Vip Miimi kibenten"

0
0
Casto Dickson Akana Kuitwa Mario kwa Tunda
Mtangazaji wa kipindi cha siz kitaa kinachorushwa na Clouds media Casto dickson amekana tuhuma za mashabiki kumuita yeye kiben ten na kwamba maisha yake ya mapenzi tangu yameanza na Tunda amekuwa akilelewa na Tunda hivyo kwa vijana wa mjini wanaitwa mario.

Casto anasema kuwa alichofata kwa tunda ni mapenzi lakini pia yeye na Tunda kila mtu anakaa kwake hivyo unawezaje kumuita yeye kiben ten ilhali yeye anafanya kazi yake na anakaa kwake na pia tunda anakaa kwake.

akiongea na Dizzim online tv, Casto anawazjibu waandishi na kusema ”  how can you call mimi kibenten wakati mimi nakaa kwangu na yeye anakaa kwake na kila mtu anajitegemea‘

Lakini pia Casto ametoa siri ya maisha yake ya mapenzi na kusema kuwa mapenzi yamemuhathiri sana kiasi kwamba endapo atakaa muda mrefu bila kuwa katika mahusiano basi anakuwa too rough.

Okwi Awatumia Salamu Kagera Sugar

0
0
Okwi Awatumia Salamu Kagera Sugar
MABAO mawili yaliyofungwa na Mganda Emmanuel Okwi yaliwafanya mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba kuibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Arusha United katika mechi ya kirafiki iliyopigwa kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid jijini hapa jana,-

ikiwa ni mechi ya mwisho kwa Wekundu wa Msimbazi hao kabla ya kuivaa Mtibwa Sugar Jumamosi.

Okwi alifunga bao la kwanza katika dakika ya saba akimalizia pasi ya Asante Kwasi, huku Ali Kabunda akifanikiwa kuisawazishia timu yake hiyo inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza dakika 10 baadaye akitumia makosa yaliyofanywa na mabeki wa Simba katika eneo la 18.

Bao la pili la Okwi lilipatikana katika dakika ya 29 na kuwafanya mabingwa hao wa Bara kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 2-1 kwenye mchezo huo ambao ulihudhuriwa pia na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.

Simba ilikosa bao la wazi katika dakika ya 42 baada ya Hassan Dilunga kupiga shuti pembeni na kupoteza pasi aliyopewa na Okwi, lakini kiungo huyo aliyetokea Mtibwa Sugar alilazimika kutoka nje na nafasi yake kuchukuliwa na Mzambia, Clatous Chama kutokana na kuwa na maumivu yaliyotokana na mchezaji wa Arusha United.

Timu zote zilifanya mabadiliko katika kipindi cha pili, lakini hakuna upande ambao ulifanikiwa kuliona bao la mwenzake huku wachezaji wa Arusha United ambao waliahidiwa zawadi ya Sh. milioni moja kwa kila bao watakalofunga walionekana 'kuamka', hata hivyo jitihada zao hazikuzaa matunda.

Kikosi cha Simba kinatarajia kurejea Dar es Salaam leo kwa ajili ya kujiandaa na safari ya kuelekea Mwanza kuwafuata Mtibwa Sugar katika mechi ya Ngao ya Jamii itakayopigwa keshokutwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba.

Simba: Aishi Manula, Nicholas Gyan, Asante Kwasi, Erasto Nyoni, Pacsal Wawa, Jonas Mkude, Hassan Dilunga/ Clatous Chama (dk 44), James Kotei/Mohamed Rashid (dk 56), Meddie Kagere/ Adam Salamba (dk 72), Emmanuel Okwi/ Rashid Juma (dk 81) na Shiza Kichuya/ Mzamiru Yasin (dk 76).

Fid Q Alilia Ufalme wa Alikiba

0
0
Fid Q Alilia Ufalme wa Alikiba
Kwa mpenzi wa burudani na shabiki wa Muziki wa Hip Hop Bongo hasa wa mwanamuziki Fareed Kubanda ‘Fid Q’, wimbo wake mpya uitwao Kiberiti aliomshirikisha Saida Karoli, mbali na kutoa burudani upande wake wa pili unasikitisha.

Unasikitisha kwa sababu ukiwa unasikiliza wimbo huo wakati una ‘enjoy’ vumbi la kiki, snea na vinanda utagundua Fid Q ameimba akiwa mwenye hasira, kuanzia ‘tone’ ya sauti yake mpaka ujumbe wa wimbo wenyewe! Bila shaka kuna mengi yanamuumiza kwenye ‘career’ yake na ndiyo amejaribu kuyaelezea kupitia wimbo huu. Nakuchambulia kwa kina;

YUPO KWENYE GEMU MUDA MREFU NA ANAPITWA!

Fid Q anatambua kwamba ni mkali na mwenye mashabiki wengi. Lakini asiye na heshima anayostahili. Ndiyo maana kwenye wimbo huu anapomuelezea mtu aliyemvika uhusika kufikisha ujumbe ambapo wazi ninaona alikuwa anajizungumzia mwenyewe anasema kwamba haonekani BET au MTV akitajwa na ni msanii wa muda mrefu anacheza tu!

Wengi wamemkuta kwenye gemu na wameondoka yuko palepale. Akitoa ngoma ni ‘hit song’ Bongo, lakini haifiki mbali zaidi wala hatajwi kwenye tuzo kubwa. Anajilinganisha na wanamuziki wengine ambao wamekuja baada yake na kufika mbali na ndiyo maana anajiona kwamba kwenye gemu anacheza.

LEGEZA KA’ WENZAKO ACHA KUTUKUZA MISEMO

Mstari huu unaonyesha kwamba kuna mengi yanagonga kichwani kwake kama sababu ya yeye kuwa alipo. Ndiyo maana kaandika mistari hii kwamba; “Tatizo lako hutaki kuuza maneno, legeza ka’ wenzako acha kutukuza misemo.” Fid Q anaona pengine sababu za kumfanya asifanye vizuri na kufika mbali ni aina yake ya uimbaji ya mistari ya kumfikirisha mtu.

IKICHORWA HIP HOP SIONI SURA YAKO KWA PICHA

Hapa inaonesha kwamba ndani au nje ya Bongo, wanaweza kuzungumziwa wanamuziki wakali wa Hip Hop Bongo na yeye asiwekwe kwenye listi.

Lakini kwenye listi hiyo wakawemo kina Bill Nas, Rosa Ree na wanamuziki wengine wa kileo na akaachwa yeye ambaye amekuwepo kabla na anakimbizana nao kwa sasa kwenye gemu na pengine yupo juu hata zaidi yao ukilinganisha kazi zao.

HUJAWAHI PIGIWA BUU UNAJIONA 2PAC Nimewahi kushuhudia Fid Q anaposhika kinasa sauti shangwe analoamsha si la kitoto. Si kwa nyimbo zake mpya tu, kuanzia nyimbo zake za mwanzoni alizotoa. Ni ukweli kwamba, hajawahi kupigiwa ‘buu’ lakini hii inatosha kujiona kwamba ana heshima kama ilivyokuwa kwa mwanamuziki kutoka Marekani, marehemu 2Pac Shakur!

AU TUPISHE USAHAULIKE, URUDI KUUZA MITUMBA LANGO

Fid Q amewahi kueleza mara kadhaa kwenye historia ya maisha yake kwamba kabla ya kutoka aliwahi kuuza mitumba kwenye Soko la Langolango.

Kwa wakazi wa Jiji la ‘Rock City’ Mwanza au mtu aliyetembea jiji hilo ambalo a.k.a yake siku hizi ni ‘Rap City’ watakuwa wamefika kwenye soko hili au wamesikia juu ya soko hili. Hili ni kama lilivyo Soko la Karume kwa upande wa mitumba. Alikuwa pale enzi hizo, sasa Fid Q anawaza kwa namna ‘career’ yake ilivyo apige chini muziki na arudi alikotoka?

ANAHITAJI UPENDO

Pengine uzalendo umemshinda na anahitaji ufike wakati aonyeshwe upendo na heshima aliyonayo. Siyo tu kwenye mistari yake mingi inayovutia na kufurahisha watu kama ilivyo rangi ya mistari ya pun-dam-ilia lakini hana heshima kama ya Ali Kiba ‘King- Kiba’ ambaye kwa namna moja au nyingine kuna watu wanamtambua kama mfalme wa Bongo Fleva.

Katika kufikisha hili, Fid Q amesampo baadhi ya mistari ya wimbo wa LL Cool J uitwao I Need Love alioutoa mwaka 1987.

Ukweli ni kwamba kuna mengi unaweza kuzungumzia kuhusu wimbo huu ukiusikiliza kwa makini. Itoshe tu kusema kwamba Fid Q anahitaji sapoti na heshima anayostahili, kweli ni mwanamuziki mkali na mwenye heshima yake.

Baraza la Sanaa (Basata) linaweza kufanya kitu kwa ajili yake. Ukijiuliza ni wanamuziki wa ngapi wa Hip Hop au Bongo Fleva wamepita kwa kufanya vizuri na mwisho wakaishia kupotosha kwa matumizi ya dawa za kulevya na vitu vingine vya ajabu, hakika ni wengi. Lakini Fid Q ameendelea kufanya anachokifanya. Amewavutia na kuwahamasisha vijana wengi kufanya Muziki wa Hip Hop.

Mbali na hayo yote anawasaidia vijana kutambua athari za dawa za kulevya na kuachana nazo. Kama Umoja wa Nchi za Ulaya EU uliutambua mchango wake na kumpa tuzo mwaka 2015 ya Champion of the 2015 Europe Year for Development in Tanzania, vipi kuhusu hapa nchini? Tusapoti vya kwetu na tumsapoti Fid Q

Chadema Yafunguka Kumpitisha Lowassa Kuwania Nafasi ya Ubunge Jimbo la Monduli

0
0
Chadema Yafunguka Kumpitisha LowassaKuwania Nafasi ya Ubunge Jimbo la Monduli
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimekanusha taarifa zinazosambaa kwenye mitandao ya jamii zikidai kuwa kamati kuu ya chama hicho imempitisha kuwania nafasi ya Ubunge jimbo la Monduli Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa.


Kamati Kuu ya (CHADEMA), imekutana katika kikao chake maalum jana Jumatano Agosti 15, 2018 kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali kuhusu chama hicho na taifa kwa ujumla.

Akizungumza na tovuti ya www.eatv.tv Katibu wa Chadema mkoa wa Arusha, Amani Golugwa amesema kuwa taarifa za kuteuliwa Lowassa hazina ukweli wowote kwani kufanya hivyo ni kumshusha hadhi Waziri Mkuu huyo mstaafu na kudai kuwa hadhi yake kwa sasa ni nafasi ya urais.

“Hayo sio mapendekezo ya kamati kama wanavyosema na hizo ni taarifa za uzushi na zinafanywa na wapinzani wetu kutaka kutuchafua, hakuna mgombea aliyepitishwa na mapendekezo yote yaliyotolewa ni ya awali,” amesema Golugwa.

Akizungumzia uamuzi wa Fred Lowassa kujiondoa kwenye kinyang’anyiro cha wanaowania kuteuliwa na chama hicho kugombea ubunge jimbo la Monduli, Golugwa amesema baada ya kushauriana, vikao vya uteuzi vilikubali kuondoa jina lake.

Fred ambaye ni mtoto wa Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa, alichukua fomu ya kuwania ubunge jimbo hilo wiki iliyopita lakini jana aliomba kujiondoa kwakile alichodai kuwa bado muda wake muafaka licha ya kuonekana kuungwa mkono na wanachama wengi awali.

Baada ya kujiondoa, Chadema kimempitisha diwani wa kata ya Lepurko, Yonas Masiaya Laizer kuwania ubunge wa jimbo hilo, kufuatia aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Julius Kalanga, kuachana na Chadema na kuachia ubunge na kuhamia CCM, ambapo Kalanga ameshateuliwa na CCM kugombea tena jimbo hilo.

Download Hapa Application ya Udaku Special Kwenye Simu Yako Kushuhudia Vimbwanga Mtaani na Stori za Mapenzi

0
0
Usipitwe na Habari zetu za Mapenzi na Udaku,kuzisoma kirahisi kupitia Application ya Udaku Special ambayo ipo Play Store kwa watumiaji wa Simu za Android

Bonyeza Hapa Chini Kuinstall/Kudownload :




Au Bonyeza Hii Picha Kujionea zaidi



Makalio Makubwa Yageuka Bunduki Kwa Mademu Wa Mujini....

0
0
Nimefanya kajiutafiti nikagundua wanawake wengi wa Kitanzania au kiafrica wamekuwa tegemezi sana kwenye silaha moja tu.

"MAKALIO YAO" Asilimia kubwa ya wanawake hasa wa mjini wamekuwa wakitumia makalio yao"Wowowo"Kuwanasa wanaume haswa maofisini n.k.
Nimejiuliza bila makalio mbinuko hawa watu wangetumia nini kutunasa?

We wafuatilie watembeapo huzungusha makalio, wapigapo picha hubinuwa makalio, walalapo kwa Bed huyaweka makalio yao juu juu.

Hivi ina maana makalio yenu yamegeka silaha yenu?
Na hii imewachangia baadhi ya wanaumme wawaze kuwatafuna utumbo mdogo a.k.a"T"
Unakuta mwanamke kwa sura mzuuriii..Lakini kama ni flat screen anapoteza confidence kabisa.

At the same time unaweza kumkuta demu sura nguumuu..Imekunjamana kama kalamba ndimu. Lakini kwa sababu kajaaliwa Makalio mbinuko anajiamini plus kiburi juu.

Makalio a.k.a Wowowo ni SMG kwenu?

Kujeni mjitolee tafsiri wenyewe mabibi na wazee wa Mikia.

Rafiki Yangu Ameniomba Nilale na Mume Wake Nipate Mimba Niwazalie Mtoto.....

0
0
Nina rafiki yangu lakini tunaishi nchi tofauti tunakutana mara 3-5 kwa mwaka hua mie nikienda nchi anayoishi anakuja kunitembelea na yeye akija ninakoishi anafikia kwangu.Yeye hajabahatika kupata mtoto mwaka wa 5 sasa tangu ameolewa, jana wakati tuna kula akaniomba tuonge kitu muhimu baada ya chakula, nikamwambia inshallah tutaongea.

Basi baada ya chakula na mambo mengine nikaenda kuwalaza watoto nikaenda chumbani kwake haya nimekuja tuongee, basi akanambia kama unavyojua sina mtoto na nimejaribu dawa zote unazozijua za kizungu na miti shamba sijafanikiwa kupata ujauzito sasa tumeshauriyana na mume wangu nikamwambia changua rafiki yangu yoyote mimi nitaongea nae ili atupatie mtoto.

Mie macho niliyatoa nakutetemeka juu, nikamwambia sijafahamu unamaanisha nini ukisema rafiki yako akupe mtoto je unataka nikupe mwanangu ule au vipi? Kasema NO nataka ulale na mumewangu nilimshangaa lakini sikutaka ahisi vibaya ilibidi nijikaze nikamwambia na ilikuwaje nikawa mie?

Kasema ndani ya moyo wangu nili wish mume wangu akuchague wewe na aliposema bora wewe ndio nikafurahi zaidi.Waungwana nilimpa maneno mengi yakumpa moyo lakini naomba nisema kua sijakubaliana na ombi lake na nimemwambia anisamehe sitoweza kufanya hicho kitu ila nitamsaidia kwa hali na mali.

Nitamuulizia kwa watu kama kuna tiba lakini kwa mimi siwezi na mumewe pia niliongea nae nikamwambia wanisamehe sitoweza, je nimekosea kuwakatalia?
Sijapenda lakini sina choice naipenda Family yangu sana na hata hili jambo silifikishi kwa Mr.

By Nimpendenani/JF...

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Wema Sepetu Ateswa na Kifo cha Mzee Majuto " Ameondoka na Ndoto Yangu"

0
0
Wema Sepetu Ateswa na Kifo cha Mzee Majuto " Ameondoka na Ndoto Yangu"
MUIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Wema Sepetu amefunguka kuwa nguli wa filamu za vichekesho marehemu Amri Athuman ‘King Majuto’ amefariki wakati akiwa hajatimiza ndoto naye aliyokuwa nayo.

Wema alisema, alipanga mwaka mmoja uliopita ilikuwa afanye kazi na mzee huyo lakini ilishindikana kutokana na maradhi yaliyokuwa yanamsumbua hivyo ikabidi avute subira lakini bahati mbaya Mungu alimchukua kabla hawajafanya kazi pamoja.

“Nilipopata taarifa tu ya msiba niliumia sana, nilijua wazi kabisa ndoto yangu imezimika na kile nilichokitarajia hakikuweza kufanikiwa kabisa nilitamani kujipima nione nikicheza filamu ya vichekesho na yeye ingekuwaje lakini ndiyo hivyo tena imeshindikana,” alisema Wema.

Lulu Diva; Kuondoka kwa Rich Mavoko WCB Sio Mwisho wa Penzi Letu

0
0
Lulu Diva; Kuondoka kwa Rich  Mavoko WCB Sio Mwisho wa Penzi Letu
MWANAMUZIKI wa kike anayekuja kwa kasi kwenye anga ya Bongo Fleva, Lulu Abbas ‘Lulu Diva’ amefunguka kuwa kuondoka kwa mpenzi wake Richard Martin’ Rich Mavoko’ kwenye Lebo ya Wasafi Classic Baby ‘WCB’, siyo mwisho wa penzi lao hata kama kwa upande wake ataendelea kuwa kwenye lebo hiyo.

Akizun-gumza na Showbiz Xtra, Lulu alisema kuwa amek-utana na maswali ya wengi ambayo yame-fanya afahamu kwamba wanahofu na penzi lao kwamba linaweza kuwa ni mwisho kwa sababu uhusiano wao ulianza wote wakiwa wapo kwenye lebo hiyo, lakini wafahamu kwamba penzi lao haliwezi kukatishwa na WCB.

“Watu wanahofia kwamba nitaachana na Mavoko kwa sababu ya kutoka WCB, hilo ni jambo lisilowezekana kwani tunapendana kweli na penzi letu halishikiliwi na lebo,” alisema Lulu ambaye inasemekana ni mjamzito.

Serikali Yaahirisha Mitihani ya Kitaifa

0
0
Serikali Yaahirisha Mitihani ya Kitaifa
Serikali kupitia Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto imesogeza mbele mitihani ya kitaifa katika vyuo vya Afya nchini kutokana na ratiba kuingiliana na sikukuu ya Idd El Haji.


Kupitia barua iliyotumwa kwa wakuu wa Vyuo vya Afya Tanzania Bara iliyosainiwa na Dkt. Otilia Gowelle, kwa niaba ya Katibu Mkuu Afya ambaye ni Dkt. Mpoki Ulisubisya imesema kuwa imesogeza mbele siku hiyo ambayo ilitakiwa kufanyika Agosti 22, 2018 ili kuhakikisha wanafunzi na watumishi wa sekta hiyo wanapata muda wa kufanya ibada na mapumziko.

“Mitihani ya vitendo iliyopangwa ifanyike tarehe 22 Agosti 2018, itafanyika siku inayofuata baada ya tarehe ya mwisho ya mitihani ya vitendo”, imesema taarifa.

Taarifa imeongeza kuwa kutokana na mapumziko hayo itakuwa imeongezeka siku moja kwenye ratiba ya ufanywaji wa mitihani hiyo kwa kada za Afya.
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live




Latest Images