Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

Barakah The Prince: Baada Ya Kusoma Biblia na Quran Nimeamua Kuwa Muislam Ili Kuwa Karibu na Mungu

0
0
Barakah The Prince: Baada Ya Kusoma Biblia na Quran Nimeamua Kuwa Muislam Ili Kuwa Karibu na Mungu
Msanii wa muziki wa Bongo fleva Barakah The Prince amefungukia uamuzi wake wa kubadilisha dini kutoka kuwa mkristo na sasa kuamua kuwa Muislamu.

Barakah amedai kuwa maamuzi hayo ya kubadilisha dini hawakuwa ya ghafla bali yalichukua  muda mrefu hadi kuyatekeleza.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Bongo 5, amesema kuwa amejitahidi kusoma Biblia na Quran na akaja kubaini kuwa Uislamu ndio dini yake pekee kwa sasa ambayo itamuweka karibu na Mungu.

Baada ya kusoma biblia sana na kusoma Quran sana kukawa kuna vitu nikawa nimeipenda dini ya kiislamu Lakini pia naamini Mungu ni mmoja na tunamuamini Mungu mmoja tofauti ni dini tu”.

Lakini pia Barakah ameweka wazi kuwa pamoja na kubadilisha dini na kuwa Muislamu na kuupenda zaidi Uislamu lakini bado anasoma biblia kwani anataka kumjua Mungu zaidi na kuwa karibu naye.

Siku za nyuma baada ya Barakah kubadilisha dini na kuwa muislamu kuna tetesi zilidai kuwa alibadili dini kwa ajili ya mpenzi wake Naj ambaye ni Muislam taarifa ambazo Barakah alizikataa.

Ninapambana Hadi Tone Langu la Mwisho- Duma

0
0
Ninapambana Hadi Tone Langu la Mwisho- Duma
Msanii wa filamu bongo, Daudi Michael maarufu kama 'Duma' amedai wasanii wengi wameshindwa kuendelea kuishi katika soko la filamu nchini kutokana na kuzoea kupewa fedha na baadhi ya wasambaji ili kusudi waweze kufanya kazi waliotumwa jambo ambalo kwa sasa watu hao hawafanyi tena.

Duma amebainisha hayo wakati alipokuwa anazungumza na www.eatv.tv baada ya kuwepo wimbi kubwa la wasanii kupungua katika soko la filamu, jambo ambalo wafuatiliaji na wapenzi wa tasnia hiyo kudai huenda bongo movie imekufa au kutolipa katika nyakati hizi.

"Ninapambana na nitaendelea kufanya hivyo hadi tone langu la mwisho, ili kusudi soko la filamu liweze kurudi kwenye 'chart' yake kama ilivyokuwa hapo awali. Sitoweza kukubali kushindwa katika hili", amesema Duma.

Mbali na hilo, Duma amefafanua baadhi ya mambo kuwa kinachowafanya wasanii wengi wa filamu kushindwa kutoa kazi zao kama ilivyokuwa hapo awali ni kutokana na ma-boss waliokuwa wanawapa fedha, sasa hawatoi tena.

"Ma-boss hawatoi fedha tena sasa hivi kutokana kutosheka na movie walizokuwa nazo,  wasanii waliowengi hawamiliki filamu za kwao binafsi bali wao wanakuwa kama vibarua tu wa kufanyakazi kutokana na bajeti walizopewa na watu hao", amesisitiza Duma.

Kwa upande mwingine, Duma anatarajia kuachia kazi yake mpya kesho inayokwenda kwa jina la 'nipe changu', ambayo imejumuisha wasanii mbalimbali pamoja na kuwa na maudhui ya kitofauti na jinsi watanzania walivyozoea kuzitazama.

Tunatibu Na Kuponesha Kabisa Upugufu wa Nguvu za Kiume, Busha, Kisukari na Vidonda vya Tumbo

0
0
TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO? BUSHA BILA KUPASUA KISUKALI NA VIDONDA VYA TUMBO? asilimia kubwa ya wanaume wanaupungufu wa nguvu za kiume NA maumbile madogo

NI NINI KINACHOSABABISHA UUME KUZIDI KUWA MDOGO NA WEMBAMBA 1 kuugua chango LA uzazi 2 unene kupita kiasi 3 kuvaa nguo au chupi za kubana 4 kupiga punyeto kwa mda mrfu ,NI NINI TIBA YAKE MAKAKANUA MIX nidawa ya mitishamba iliyochanganywa NA mizizi kumi NA mbili urfusha NA kunenepesha UUME saizi upendayo ich 5,6,7, NA 8 kwa urfu NA sentimita 3,4, na 5 ipo dawa ya kunywa na kupaka NI NINI KINASABABISHA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME 1 kupungukiwa kwa homoni ya testerone 2 kuhudhurika kwa Neva au uti wa mgongo 3 utumiaji holela wa madawa ya kizungu 4 usongo wa mawazo na asira 5 utumiaji wa vyakula vya mafuta mengi NI NINI TIBA YAKE MAPRO POWER NO 2 NDIO tiba tosha kwa sasa kwani utibu matatizo matatu kwa pamoja 1 itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15 adi 20 ,2 itakufanya urudie tendo zaidi Mara tatu 3 uhimalisha uume uliolegea na kusinyaa OKOA NDOA YAKO SASA ujihepusha na lawama ndani ya ndoa yako au pale ukutanapo na mpezi dawa hii itamfanya mpenzi wako hakueshimu na hasitoke nnje ya ndoa na ata wazee wenye umri mkubwa wanapona zipo dawa za kupunguza kitambi,minyama uzembe, presha ,kisukar mvuto wa mpezi au biashara

FIKA OFISINI KWETU MBAGALA ZAKHEMU na wateja wa kanda ya ziwa yupo wakala wetu mwanza mjini au piga simu 0752348593

DR MABULA na utaletewa popote ulipo uduma hizi

China Inafanya Mazoezi ya Kushambulia Vituo vya Marekani

0
0
China Inafanya Mazoezi ya Kushambulia Vituo vya Marekani
Kuna uwezekano kuwa jeshi la China linafanya mazoezi ya kushambuia vituo vya Marekani na vya washirika huko Pacific, kwa mujibu kwa makao makuu ya ulinzi ya Marekani.

Ripoti ya kila mwaka kwa Congress inasema kuwa China inaongeza uwezo wake wa kupeleka ndege za kivita kwenye visiwa vyake vya baharini.

Ripoti hiyo inazungumzia kuongezeka uwezo wa kijeshi wa China ikiwemo bajeti kubwa ya dola bilioni 190, thuluthi ya ile ya Marekani.

Onyo kuhusu mashambulizi ya angani ni moja ya malengo ya kijeshi na kiuchumi ya China.

"Kwa miaka mitatua iliyopita PLA [People's Liberation Army] limepanua maeneo yake ya kufanyia mazoezi bahrini, na kupata ujuzi wa maeneo muhimu ya baharini na kuna uwezekazo kuwa linafanya mazoezi kushambulia vituo vya Marekani na vya washirika," ripoti hiyo ilisema.

Marekani yaionya China kuhusu visiwa bandia baharini
Inaendelea kusema kuwa haijulikani ni kipi China inataka kudhibitisha kwa kufanya mazoezi kama hayo.

"PLA huenda linataka kuonyesha kuwa lina uwezo wa kushambulia Marekani na vikosi washirika kwenye kambi za jeshi magharibi mwa bahari ya Pacific ikiwemo Guam," ripoti hiyo iliongeza.

Watuhumiwa Sugu wa Unyang'anyi wa Kutumia Silaha Wakamatwa

0
0
Watuhumiwa Sugu wa Unyang'anyi wa Kutumia Silaha Wakamatwa
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam linawashikilia watuhumiwa sugu 13 kwa tuhuma za unyang’anyi wa kutumia silaha katika maeneo mbalimbali ya jiji na mikoa ya jirani.

Watuhumiwa hao ni BALIZANILA EZEKIEL (37) Raia wa Burundi, SHUKURU HASSAN (38), SAIDI SHABANI (34) HAJI SALUM (38) FRENK KALIKENE (32) na wengine 8.
Watuhumiwa hao wamekuwa wakiendelea na vitendo vya uhalifu wa kutumia silaha licha ya kuachiwa huru baada ya kumaliza vifungo vyao katika magereza mbalimbali hapa nchini.

Watuhumiwa hao walikamatwa wakiwa na bostola aina ya Chinese star iliyokuwa na risasi nne ndani ya magazine, pamoja na risasi nyingine tisa zikiwa zimehifadhiwa pembeni.
Oparesheni hii ni endelevu ya kupambana na wahalifu wote wanaofanya unyang’anyi ndani ya jiji la Dar es salaam na wanaokuja kujificha jijini Dar es salaam baada ya kufanya uhalifu kutoka mikoa ya jirani.

Bobi Wine Akutwa na Makosa ya Kumiliki Silaha Kinyume na Sheria..... Ashtakiwa kwa Uhaini

0
0
Bobi Wine Akutwa na Makosa ya Kumiliki Silaha Kinyume na Sheria.....  Ashtakiwa kwa Uhaini
Mbunge wa Kyaddondo Mashariki, Robert Kyagulanyi maarufu kama Bobi Wine ambaye alikamatwa Jumatatu mjini Arua pamoja na wanasiasa kadhaa wa upinzani ameshtakiwa katika Mahakama ya Kijeshi mjini Gulu kwa makosa ya kukutwa na silaha na risasi kinyume cha sheria.
Kwa mujibu wa taarifa ya msemaji wa jeshi iliyotolewa Alhamisi Brigedia Richard Karemire, mbunge huyo alirejeshwa mahabusu hadi Alhamisi ijayo.
“Ikiwa ni sehemu ya uchunguzi kuhusu matukio ya vurugu, polisi waliwakamata waandaaji wakuu na washiriki akiwemo Mheshimiwa Robert Ssentamu Kyagulanyi Mbunge wa Jimbo la Kyadondo Mashariki. Katika upekuzi uliofanywa na wapelelezi kwenye chumba chake cha hoteli alikutwa akimiliki bunduki kadhaa na risasi vitu ambavyo kwa kawaida humilikiwa na Jeshi la Ulinzi,” ilisema taarifa ya Brigedia Karemire.
“Kwa sababu hiyo, Mheshimiwa Kyagulanyi leo amefikishwa katika Mahakama ya Kijeshi mjini Gulu na ameshtakiwa chini ya makosa yanayoangukia S 119 (1) (h) ya Sheria ya Jeshi la UPDF, 2005 yanayohusu umiliki usiohalali wa silaha na risasi. Kisha amepelekwa mahabusu hadi Agosti 23, 2018”.
Alishtakiwa mbele ya wanasheria wake wawili; Asuman Basalirwa (Mbunge wa Manispaa ya Bugiri) na Medard Seggona (Mbunge wa Busiro Mashariki).
Kwa mujibu wa Basalirwa, ambaye alikuwepo kwenye chumba cha mahakama, uso wa mteja wake Kyagulanyi ulikuwa umevimba na hakuwa na uwezo wa kutembea wala kuongea.
Seggona alisema Kyagulanyi hakuweza hata kuandikisha maelezo kwa sababu alikuwa katika hali mbaya na amefungwa pingu.

Mzee Akilimali Aitaka TTF Kumuadhibu Mwenyekiti wa Kamati ya Utendaji wa Yanga

0
0
Mzee Akilimali Aitaka TTF Kumuadhibu Mwenyekiti wa Kamati ya Utendaji wa Yanga
Katibu wa Baraza la Wazee wa Yanga, Ibrahim Akilimali amelitaka Shirikisho la Soka Tanzania kumwadhibu Mwenyekiti wa Kamati ya Utendaji wa klabu hiyo kutokana na kuwa na cheo ambacho ni kinyume na katiba ya Yanga.

Akilimali ameibuka na kueleza hayo bada ya Makele kuteuliwa kuwa Katibu wa Kamati ya Uchaguzi Yanga ambayo tayari imeshaanza mchakato kuelekea uchaguzi ambao utajaza nafasi za viongozi walioachia ngazi.

Katibu huyo amesema Makele amekalia wadhifa ambao ni kinyume na katiba ya Yanga ilivyo akieleza kuwa haiwezekani akawa Mwenyekiti wa Matawi ya klabu nchi nzima huku pia akawa Katibu wa Kamati ya Uchaguzi.

Akilimali ameoneshwa kushangazwa zaidi na uongozi wa Yanga kumpa wadhifa huo Makele kitu ambacho amesema ni kuvunja katiba ambayo klabu inaitumia kwa shughuli mbalimbali kuijenga Yanga.

"Ujue mimi nashangaa sana, huyu Makele hakustahili kuwa na nyadhifa mbili Yanga, haiwezekani akawa Mwenyekiti wa Matawi na vilevile akawa kwenye kitengo cha kamati ya uchaguzi kama Katibu, Yanga wamekosea, amevunja katiba'' alisema.

Aidha, Akilimali amefunguka juu ya suala la Mwenyekiti akisema ni wakati mwafaka wa kumpata mbadala wa Yusuph Manji ambaye ameachia ngazi takribani mwaka mmoja na miezi miwili sasa.

Akilimali amezidi kushangazwa na uongozi Yanga ambao upo madarakani mpaka sasa ukiendelea kusema hautajaza nafasi ya Mwenyekiti kuelekea uchaguzi ujao na badala yake watahusika na Makamu pamoja baadhi ya Wajumbe wa Kamati za Utendaji.

Uamuzi wa Yanga kueleza wanamtambua Manji kama Mwenyekiti ameeleza ni jambo la kupoteza muda kwani tayari ameshatuma barua katika klabu, TFF na Baraza la Michezo Tanzania (BMT) juu ya kujizulu nafasi hiyo.

Licha ya kutaka Mwenyekiti mpya achaguliwe, Akilimali ameeleza kwa sasa hawezi kutaja wala kupendekeza jina la nani anapaswa kuchukua nafasi ya Manji kwa hofu ya kuonekana mbaya kwa wadau na wanachama wa klabu hiyo na badala yake atasema hapo baadaye.

"Hakuna haja ya kuendelea na mtu ambaye ameshatangaza kujizulu na sasa ni mwaka na miezi miwili hayupo klabuni, ifikie wakati nafasi yake ijazwe kuliko kuendelea kujiaminisha kuwa atarudi"

"Siwezi kumtaja nani anastahili kuwa mbadala wake kwa sasa maana ninaweza kuonekana mbaya kwa baadhi ya wanachama na wadau wa Yanga, nitafanya hivyo baadaye" alisema.

Wakati Yanga ikiwa katika mchakato wa kufanya uchaguzi, tayari TFF imeshatoa siku 75 kwa ajili ya uchaguzi huo ikiwa ni sawa na kwa watani zao wa jadi Simba ambao nao pia utawala wao uliopo madarakani umeshamaliza muda wake.

Download Hapa Application ya Udaku Special Kwenye Simu Yako Kushuhudia Vimbwanga Mtaani na Stori za Mapenzi


Tofauti ya Lugha Kwenye Bar baina ya Zama zile na zama Hizi za Vyuma Kukaza

0
0
Lugha maarufu enzi zileeee.....;

1. Lete Tulivyokaa

2. Muongeze 5 huyo

3. Mbona bia haziendi?

4. Usiulize, wee Ongeza tu

5. Mbona jikoni hawatusikilizi??

6. Aah,tunahudumiwa na dume?

7. Nimesema Mbuzi mzima!!

8. Wee hizi ni kilo 5 kweli?

9. Kuna watu wanabusu bia!

10. Hamishia opener hapa hapa?

ZAMA HIZI SASA....


1. Waruke wote, sijaja nao mimi

2. Mmh, kaongeza nyingine?

3. Bia zenu bei mbaya zaidi ya jirani yenu?

4. dada, uliza kwanza hata kabla ya kuleta toothpiki

5. Tumekula majumbani kwetu

6. Nitanunulia kaunta mwenyewe

7. Mna kongoro?

8. Lete supu tu bila finyango kwani shingap?

9. Siku hizi inashauriwa bia 2 tu kwa afya

10. Hebu toa mavituvitu yenu hapa yanatuzingua

11. Nilitee bili ya bia nilizokuagiza mimi nyingine sizijui...

DC Jerry Muro atoa mwezi mmoja kwa wanaume aliotelekeza watoto Arumeru!

0
0

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Jery Murro ametoa mwezi mmoja kwa wanaume waliotelekeza watoto wilayani humo kuhakikisha wanaanza kutafuta watoto wao na kuanza kuwahudumia.


Amesema kuwa baada ya muda alioutoa kuisha ataanza kuwakaribisha Wanawake wote wanaoishi wilayani humo waliotelekezewa watoto kupeleka Malalamiko yap ofisini kwake.

Aidha, ametoa agizo hilo wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya hali ya utelekezji wa watoto wilayani humo.

Vile vile ameongeza kuwa lengo la zoezi hilo ni kupunguza idadi ya watoto wanaoishi katika mazingira magumu ,hatarishi na wanaojihusisha na uhalifu na wale wanaozurura na kuzagaa mitaani kwa kukosa malezi ya wazazi wawili.



“Nichukue fursa hii kuwataarifu akinamama na akinadada waliozalishwa na kutelekezewa watoto na kuachwa wabebe Mzigo wa kuwahudumia watoto wao, Natoa mwezi mmoja kwa kila mwanaume anayejua ana mtoto Arumeru, aanze kuhudumia, amesema DC Murro

Hata hivyo, Muro amesema licha ya serikali kutangaza elimu bure kwa wanafunzi, wapo baadhi ya wanafunzi ambao wanakwenda shule bila sare ya shule, madaftari au viatu huku moja ya sababu inayochangia hali hiyo ikiwa ni kutelekezwa na baba zako

Muziki wetu wa BongoFleva kwa sasa umekuwa kama Bubble Gum (Big G) unakula na kutema – Lamar

0
0
Mwandaaji wa Mziki wa kizazi kipya kutoka hapa Tanzania ambaye kwa sasa anajishughulisha na vitu vingine nje na muziki kama vile kufungua kituo cha kuoshea magari (Carwash) pamoja na sehemu ya kupikia na kuuzia chakua (Restaurant)  Lamar,amefunguka na kusema kuwa muziki wa Bongo Flava kwa sasa hauna ladha.

Lamar ameongea hayo katika mahojiano aliyoyafanya na kituo cha habari cha Clouds Fm na kuongea yote jinsi anavyouona muziki wa sasa na muziki wa kipindi cha nyuma kidogo Lamar amesema:-

“Muziki wa sasa hivi uko Bubble Gum (Big G) unautafuna halafu unautema tofauti na muziki wa zamani akimaanisha kipindi cha nyuma ambao uko kimziki zaidi maana unaishi muda mrefu,hii ni kwasababu ya upangiliaji wa codes za muziki (akimaanisha mfumo) maana zamani walikuwa wacheza codes ambazo zinaishi muda mrefu tofauti na sasa hivi ambao hutumii codes bali watu wameurahisisha tu kwani umekuwa muziki wa kawaida tu”



Lamar amefunguka hayo kwa hisia sana kwani muziki wetu ulipotoka ni mbali na kuna baadhi ya kundi la watu wanataka kuupoteza muziki wetu mana wanaleta mambo ya kuiga zaidi.

Kinachochangia zaidi i aina ya waandaji (Maproducer) wa kipindi hicho cha nyuma kidogo na waandaji wa sasa hivi ambao wameufanya muziki kuwa rahisi.

By Ally Juma.

Mara ya Tatu Sasa Namwota Secretary wa Kazini Kwetu Nikifanya Nae Mapenzi

0
0
Kaushauri ndugu zangu; usiku wa kuamkia leo ni siku ya tatu siyo mfululuzo naota nafanya mapenzi na secretary mmoja ambae yupo kazini kwetu ila sipo nae ofisi moja.

Sijawahi kumtongoza, sina feelings zozote na yeye, wala sijawahi kufikiria kumtongoza. Hizo mara mbili nilivyomwota sikumwambia maana niliona kama ninaweza kujenga ukaribu ambao sijau-plan. Lakini mara hii ya tatu naona si vema nikae tu kimya maana siku hiz watu wana technic-know-how. Nitamweleza mbele za watu kuwa nimeota nimefanya nae mara tatu. Sina mazoea ya kuota kufanya mapenz ndotoni imetokea kwake tu ndo maana nimeona si kitu cha kawaida kwangu na pia bora angekuwa mtu hata nam-feel ningechukulia hivo. Naombeni Ushauri Kwa Wanaojua Mambo ya Ndoto

DALILI 7 Za Kuonyesha Anakucheat Na Mwingine..!!

0
0
Katika mahusiano huwa kuna changamoto tofauti tofauti. Kwa kawaida ni muhali kupata mahusiano ambayo hayana patashuka moja au nyingine. Inajulikana ya kuwa mahusiano huwa kuna migogoro, kutoelewana, kunyamaziana na mbaya zaidi...vita.

Anyway mambo kama haya huwezi kuyazuia kwa sababu wenyewe ndio wanayaita mapenzi. Utaskia mtu akilalamika kuwa amemiss kugombana ama kuteteshana na mpenzi wake, jambo ambalo huwa ni la kawaida.

Ok. tukija katika mada yetu ni kuwa nataka nikuulize maswali yafuatayo. Je hivi karibuni umeona kama mpenzi wako amekuwa mtu tofauti na ilivyo kawaida? Je mpenzi wako imekuwa muda mrefu tangu mfanye mambo yenu ya kawaida ambayo mlikuwa mkifanya? Je unamshuku kama amepata mwingine?

Kama majibu yako ni NDIO basi hili chapisho nimeliandika spesheli kwako na nataka umakinike kwa kusoma dalili zetu tulizoziandika na kama yote yanawiana na dhana yako basi ni wakati wa kumfungukia mpenzi wako na umwambie kweupe kuwa umechoshwa na tabia yake ya 'kutoka nje', na umuulize kama amechoshwa nawe ili ukate minyororo ya kuwa naye ili uwe huru.

Zama nami!

Dalili #7: Muda mwingi anajaribu kujirembua kuoneka vizuri

Kuvalia vizuri kila wakati si jambo baya la kufanya katika mahusiano, mwanzo wapenzi hupenda sana kuhakikisha ya kuwa wanampendeza mwenza wao.

Lakini, ukiona ya kuwa anamakinika zaidi na upande wa kujifanya aonekane mrembo, basi itakuwa anajaribu kumridhisha mtu mwingine kando na wewe. Kama umemgundua kuwa anajaribu kuvalia vizuri wakati anatembelea hizi sehemu basi weka ? katika mawazo yako: Kazini, supermarket, mkahawa, na hata gym!

Makinika: Zile sehemu zake za kawaida anazozienda kama amezijeuza kuwa fashion show itakuwa ni ishara ya kuwa anakucheat.

Dalili #6: Anakuwa msiri na simu yake, pakatalishi yake nk

Kila mtu ana haki ya kuwa na faragha yake. Mwanzo, watu wengi hawapendi faragha yao ishambuliwe na hata wapendwa wao. But ishu itakuja wakati ambapo anakuwa msiri kuhusu vitu vyake zaidi kuliko awali.

Hii inaweza kumaanisha kuwa kunakuwa na migogoro isioisha wakati ambapo umechukua kuangalia simu yake hadi ule wakati anaudhika wakati umeingia kwa chumba chake akiwa anatumia kompyuta yake. Ukiona mtu akianza kuwa msiri zaidi ni kuwa atakuwa anawasiliana na mchumba mwingine ambaye ako naye.

Dalili #5: Anapunguza hamu ya kufanya tendo la ndoa hadi kukataa asilani

Hata watu waseme nini, kufanya mapenzi ni sehemu muhimu inayohitajika katika mahusiano. Kama hamfanyi mapenzi, utajihisi ya kuwa unabezwa na kukatalika na mpenzi wako.

Wakati umri unaposongea, utagundua ya kuwa kiasi cha mapenzi mnachofanya huwa kinapungua. Hio ni kawaida, lakini kuna hatua nyingine neno 'ni kawaida' linaondolewa.

Kukataliwa katakata kufanya mapenzi ama kutoa visababu inaweza kumaanisha kwa njia rahisi kuwa hajiskii kufanya mapenzi na wewe. Wakati mtu anakucheat, huwa anapoteza ule muungano wa kihisia na wewe na atakuwa hana hamu ya kufanya mapenzi na wewe

Dalili 4: Kuna yule mtu kilinge (mysterious)

Wale watu kilinge ndio unaopaswa kuwaogopa zaidi. Wanaume na wanawake kwa kawaida watakuwa na marafiki wa jinsia ile nyingine, lakini kama utamwona mpenzi wako haachi kuongea kuhusu huyo mtu basi kuna tatizo.

Hata kama nia yake ni nzuri, anaweza kuwa na kitu ambacho ni zaidi ya kuwa marafiki. Kama hatakuruhusu ukutane na huyu mtu kilinge ambaye amekuwa akipoteza muda wake mwingi naye, basi kunaweza kuwa na kitu ambacho ni zaidi ya kuchat pekee.

Dalili #3: Anazozana na wewe zaidi ya kawaida

Kukefyakefya na kukufananisha na wengine ni jambo lisilokubalika katika usuhiano. Wakati ambapo hii itatoka kuanzia mzaha hadi kuwa serious, ni ishara ya kuwa anakucheat.

Mara nyingi, mpenzi akikosana na mwenziwe hujaribu kujitenga na majibizano. Lakini ukiona ya kuwa kila wakati anagombana na wewe kwa sababu ya mahusiano yenu basi ni ishara ya kuwa kuna mwingine ambaye anamwonyesha mapenzi ya dhati...na si wewe

Dalili #2: Anakutenga wewe na marafiki zako wa karibu

Wapenzi wawili ambao wamekuwa pamoja kwa muda mrefu huwa wanagawa marafiki pamoja. Hawa ni wale ambao nyinyi wawili mnawaingiza katika maisha yenu kadri miaka inavyosonga. Wakati umeona kuwa mpenzi wako anapunguza muda wa kuwa na wewe na anachofanya ni kuwatenga watu hawa, kawaida huwa kuna mtu anahusika.

Anaweza kuwa hana moyo wa kukabiliana na marafiki wa karibu na kuwadanganya kuhusu furaha anayopata katika mahusiano yenu. Hii inaweza kutokea baada ya muda mrefu ama akajitenga ghafla.

Dalili #1: Analijeuza neno ''tu'' hadi ''ni'' polepole

Neno ''tu'' katika mahusiano ni takatifu. Huu ni ule wakati ambao mwanaume na mwanamke wamewekeza shina la kuwa pamoja. Wakati mwingi, sana sana wanawake ndio huwa wa kwanza wa kubadilisha neno ''ni'' hadi ''tu'' halafu mwanaume akalizoea.

Hivyo katika mahusiano ukiona mpenzi wako ameanza kurudia kutumia neno ''ni'' itakuwa anajaribu kukutenga katika maisha yake, anajaribu kukufuta katika picha yake.


Mwisho ni kuwa kudanganya katika mahusiano ni swala zito ambalo linaibua hisia nzito, lakini dalili za kucheat zinaweza kutatiza zaidi.

Kukataa kufanya mapenzi ama kujaribu kujirembua inaweza kusababishwa na misongo ama kutojiskia shangwe yeye mwenyewe. Kabla ya kumlaumu kuwa anafanya mabaya, hakikisha ya kuwa kuna ishu inayoendelea, ama inaweza kuwa wewe ndiwe chanzo cha kufanya mahusiano yenu yavunjike

Mpaka Mwanamke Anaamua Kuchepuka Ujue Kuna Shida kwa Mumewe

0
0

Katika Utafiti wangu imegundua kuna tatizo kubwa katika mahusiano aidha ya kimapenzi au ya ndoa.Uaminifu umekuwa tatizo kubwa miongoni mwa jamii ya kizazi hiki! Kutoridhika imekuwa sehemu ya maisha ya sasa si kwa mwanaume au mwanamke kuchepuka ndiyo habari ya mujini kwa sasa hadi wale walioaminika kuwa viongozi wa dini maana hakuna mwenye kinga ya kutotenda dhambi hivyo imekuwa kujitwalia kadri tupendavyo nani atakuwa kiini cha mabadiliko katika wimbi hili linaoelekea kupoteza wengi.

Tatizo ni nini hasa kwa uzoefu wangu wa kuishi katika dunia hii na katika ndoa kwa muongo zaidi ya mmoja nimegundua mwanamke anaweza akatulizwa (walioko ndoani) tu endapo mume atakidhi mahitaji yote ya kiuchumi,zaidi kuwa na muda wa kutosha na mkewe bila kusahau kusaidiana kufikishana katika kilele cha maraha ambacho.Mungu aliona ni vema atupe wanadamu kama kitulizo ktk maisha yetu haya yenye adha nyingi.

Sasa cha ajabu kuna baadhi ya wanaume wamekuwa busy wakiamini magari,pesa na fahari ndiyo vitaziba uhitaji wa mke katika kukidhi haja ya upendo ndiyo maaana lawama haziishi watu wanachapiwa na kuishia kulalama eti wanawake hawaridhiki hata uwape nini mwanamke haswa alilyelewa vyema akihudumiwa bed na akapata mahitaji ya kiuchumi sina cha kufata nje hata kidogo.

Nina zaidi ya miaka 13 ya ndoa hivyo najua nisemacho sioni fahari wala sijawahi kufikiria kutoka na mtu nje ya mume wangu kwa muda wote huo ila kuna mazingira baadhi wanaume wanasababisha hadi mke unajiona mhitaji,mume hashikiki ndani kila siku kuja home late mvivu kitandani hayuko romantic nk unategemea mke afanyeje?

Ilihali naye ana damu inachemka(hapa siharalishi kuchepuka ila mke anakuwa katika upweke mkuu nani ampe faraja mpaka mke anaamua kutoka nje kuna tatizo kubwa hivyo chukueni tahadhari waume wenye tabia hizi zinajeruhi sana mioyo yetu (nasi tunapendwa sana huko nje uwezo wa kutoka kama mnavyotoka tunao sana..ila ni staha tu na hofu kwa Mungu muumbaji.Wanaume many sehemu yenu na wanawake pia ili tuishi kwa raha bila kuumizana.

Lava Lava Akumbwa na Skendo ya Kutelekeza Ujauzito...Queen Darling Ahaidi Kumlea

0
0

Msanii wa muziki kutoka lebo ya WCB Wasafi, Queen Darleen amedai kuwa yuko tayari kulea mtoto atakayezaliwa na 'Flaviana Lutakwa', mwanamke aliyedai kuwa ana Ujauzito wa msanii @iamlavalava.

Queen amejitokeza na kuonesha utayari wa hilo kwa kuandika kwenye uwanja wa Maoni wa #EXCLUSIVE Interview iliyofanyika #DizzimOnline juu ya malalamiko ya mwanamke huyo, baada ya kusikika akidai kuwa amebeba Ujauzito na anakumbana na Changamoto ya kupotezewa na Msanii hiyo.

Kikwete amtembelea tena Kingwangalla, Sasa kuruhusiwa muda wowote

0
0

RAIS Mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete amemtembelea na kumjulia hali Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla aliyelazwa katika wodi maalum kitengo cha Taasisi ya Mifupa MOI, hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam kwa mara nyingine tena. 

Hii inakuwa ni mara ya tatu kwa Kikwete kumtembelea Dk Kigwangalla ambapo awali alimtembelea Agosti 8, 2018 alipokuwa amelazwa Wodi ya Mwaisela akipatiwa Matibabu ya awali na juzi Agosti 15, 2018 katika wodi ya Taasisi ya Mifupa MOI. 

Akiwa hospitaini hapo mapema jana, Kikwete ameweza kumjulia hali na kubadilishana nae mawazo mbalimbali huku akimtakia unafuu aendelee na majukumu yake ya kila siku na akimpongeza kwa shughuli zake anazozifanya katika kuinua sekta ya Utalii pamoja na kulinda rasilimali za Maliasili. 

“Nikutakie kheri. Nashukuru kwa kukuta unaendelea vizuri sasa na nilikuja ukiwa upo unaongea ukiwa umelala kitandani na kwa sasa nimekuja tena umeweza kuimarika na hata kutembea na kukaa kama hivi hongera sana” alieleza Kikwete wakati akimjulia hali Waziri Kigwangalla wodini hapo. 

Tayari jopo la Madaktari bingwa wa MOI wamebainisha kuwa Dkt. Kigwangalla kwa sasa anaendelea vizuri na muda wowote anaweza kuruhusiwa kurejea nyumbani ambapo kwa sasa sehemu zilizobakia ni mkono wake wa kushoto ambao kila siku unaendelea kuimarika. 

Hata hivyo, Dkt. Kigwangalla amemweleza Kikwete kuwa kwa sasa hali yake inaendelea kuwa vizuri na muda wowote anaweza kuruhusiwa kurejea nyumbani huku akiendelea na mazoezi kidogokidogo.

Aidha, jioni ya jana Dkt. Kigwangalla ameweza kufanya mazoezi ya kutembea umbali wa zaidi ya kilometa moja kuanzia kwenye viunga vya Hospitali hiyo na kuzunguka maeneo yanayozunguka Muhimbili na baadae kupanda kwa kutumia ngazi katika jengo anapopatiwa matibabu kwa miguu mpaka gorofa ya sita.

Waziri Dkt. Kigwangalla alipata ajali ya gari mnamo Agosti 4, 2018 huko Manyara akiwa katika ziara ya kikazi ambapo katika ajali hiyo iliyokuwa na watu 6, Afisa Habari wa Wizara hiyo Hamza Temba alifariki dunia huku watano wakijeruhiwa akiwemo yeye anaendelea na matibabu Hospitalini hapo.

Papa Francis alaani unyanyasaji wa kingono uliofanywa na mapadre

0
0

Kiongozi wa kanisa katoliki Papa Francis amesema yuko katika upande wa wahanga wa zaidi ya mapadre 300 waliofanya unyama wa unyanyasaji  mkubwa kingono nchini Marekani wanaoshutumiwa kuwafanyia unyanyasaji zaidi ya watoto 1000. 

Unyama  huo ulifanyika  katika  kipindi cha  miongo saba, yameeleza  makao  makuu  ya kanisa  Katoliki mjini  Vatican. 

Wahanga  watambue kuwa  papa  yuko  upande wao, imesema  taarifa  ya  Vatican baada  ya  ripoti mbaya ya jopo la mahakama nchini  Marekani  kuchapishwa  siku  ya  Jumanne inayoelezea hatua za  kuficha madhila hayo zilizofanywa  na  kanisa Katoliki. 

"Kuna  maneno  mawili yanayoweza  kueleza  hisia zinazokabili uhalifu  huu  wa  kutisha, aibu  na  masikitiko. Papa anachukulia  kwa dhati  kazi  ya  jopo  la  mahakama pamoja  na  ripoti iliyotoa. Papa analaani  bila kiasi unyanyasaji kingono watoto wadogo. Unyanyasaji ulioelezwa  katika  ripoti  ni  uhalifu  na kiroho ni wa kukemewa. 

Vitendo  hivyo  ni usaliti  wa  imani  ambayo  imewapora wale waliofanyiwa utu  wao na, pia imani  yao. Kanisa  linapaswa kujifunza  somo  gumu kutoka  yale  yaliyopita, na kunahitajika kuwajibika kwa  wale  waliofanya  vitendo  hivyo  na  wale  ambao waliruhusu  unyanyasaji  huo  kutokea." 

Hayo  ni  maneno  katika  taarifa  ya   makao  makuu  ya  kanisa Katoliki  mjini  Vatican  iliyosomwa  na  msemaji  wa  kanisa  hilo Greg Burke.  "Wale ambao  wameathirika  ndio anaowapa  umuhimu wa  kwanza,  na  kanisa  linataka  kuwasilikiza ili  kuondoa maafa haya  ya  kutisha  ambayo  yanaharibu  maisha  ya  watu  wasio  na hatia,"  taarifa  ya  Vatican imesema. 

Tunatibu Na Kuponesha Kabisa Upugufu wa Nguvu za Kiume, Busha, Kisukari na Vidonda vya Tumbo

0
0
TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO? BUSHA BILA KUPASUA KISUKALI NA VIDONDA VYA TUMBO? asilimia kubwa ya wanaume wanaupungufu wa nguvu za kiume NA maumbile madogo

NI NINI KINACHOSABABISHA UUME KUZIDI KUWA MDOGO NA WEMBAMBA 1 kuugua chango LA uzazi 2 unene kupita kiasi 3 kuvaa nguo au chupi za kubana 4 kupiga punyeto kwa mda mrfu ,NI NINI TIBA YAKE MAKAKANUA MIX nidawa ya mitishamba iliyochanganywa NA mizizi kumi NA mbili urfusha NA kunenepesha UUME saizi upendayo ich 5,6,7, NA 8 kwa urfu NA sentimita 3,4, na 5 ipo dawa ya kunywa na kupaka NI NINI KINASABABISHA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME 1 kupungukiwa kwa homoni ya testerone 2 kuhudhurika kwa Neva au uti wa mgongo 3 utumiaji holela wa madawa ya kizungu 4 usongo wa mawazo na asira 5 utumiaji wa vyakula vya mafuta mengi NI NINI TIBA YAKE MAPRO POWER NO 2 NDIO tiba tosha kwa sasa kwani utibu matatizo matatu kwa pamoja 1 itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15 adi 20 ,2 itakufanya urudie tendo zaidi Mara tatu 3 uhimalisha uume uliolegea na kusinyaa OKOA NDOA YAKO SASA ujihepusha na lawama ndani ya ndoa yako au pale ukutanapo na mpezi dawa hii itamfanya mpenzi wako hakueshimu na hasitoke nnje ya ndoa na ata wazee wenye umri mkubwa wanapona zipo dawa za kupunguza kitambi,minyama uzembe, presha ,kisukar mvuto wa mpezi au biashara

FIKA OFISINI KWETU MBAGALA ZAKHEMU na wateja wa kanda ya ziwa yupo wakala wetu mwanza mjini au piga simu 0752348593

DR MABULA na utaletewa popote ulipo uduma hizi

Hali ya Bobi Wine ni Mbaya, Hawezi Kuongea Wala Kusimama.,...Bado Anashikiliwa na Polisi

0
0
Hali ya Bobi Wine ni Mbaya, Hawezi Kuongea Wala Kusimama.,...Bado Anashikiliwa na Polisi
Wanasheria wawili wa msanii wa muziki ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Kyadondo Mashariki Robert Kyagulanyi maarufu Bobi Wine, wamesema mwanasiasa huyo ana hali mbaya kiafya kwani hawezi kutembea wala kuzungumza.

Wakiwa pamoja na familia ya Bobi, awali wanasheria hao walizuiwa kumwona mbunge huyo aliyekamatwa Jumatatu mjini Arua pamoja na wanasiasa kadhaa wa upinzani. Alifikishwa katika Mahakama ya Kijeshi mjini Gulu ambako alishtakiwa Alhamisi kwa kosa la kumiliki isivyohalali bunduki na risasi.Lakini pia ushiriki wake kwenye machafuko katika eneo la Arua, yaliyochangia kushambuliwa kwa msafara wa magari ya rais Yoweri Museveni.

Hata hivyo, alishtakiwa mbele ya wanasheria wake wawili; Asuman Basalirwa (Mbunge wa Manispaa ya Bugiri) na Medard Seggona (Mbunge wa Busiro Mashariki).

Kwa mujibu wa Basalirwa, ambaye alikuwemo kwenye chumba cha mahakama, uso wa mteja wake ulikuwa umevimba na hakuwa anaweza kutembea wala kuongea. Seggona alisema Bobi Wine hakuweza hata kuandikisha maelezo kwa sababu alikuwa katika hali mbaya na alikuwa amefungwa pingu.

“Hali ya Kyagulanyi ni mbaya sana. Ana maumivu makali. Hawezi kuzungumza, na anapata shida sana hata kukaa. Uso wake umevimba na hawezi kuona kwa sababu ya mateso aliyopata kutoka kwa askari wa SFC. Hakuweza hata kuzungumza wakati akisomewa mashtaka na naamini hakuwa anajua kinachoendelea wala kuelewa mashtaka aliyosomewa,” alisema Seggona alipozungumza na wanahabari.

Familia yake haikuruhusiwa kuingia kwenye chumba cha mahakama kusikiliza kesi hiyo chini ya mwenyekiti Luteni Jenerali Andrew Gutti.

Barbara Itungo maarufu kama Barbie, ambaye ni mke wa Bobi Wine alianguka na kuangua kilio wakati wanasheria wa mumewe wakielezea namna alivyoteswa.

“Nikiwa mke na mama, uvumilivu wangu uko majaribuni. Serikali iniruhusu nimwone mume wangu. Nina wasiwasi na hali yake kwa sababu najua alipigwa sana na wanajeshi,” alisema huku akitokwa machozi

Chadema Yaanika Majina ya Wagombea Wake Uchaguzi Mdogo

0
0
Chadema Yaanika Majina ya Wagombea Wake Uchaguzi Mdogo
Chama cha Demokrasia na Maendeleo, (CHADEMA), kimetangaza majina ya wagombea wake watakaowania ubunge katika majimbo ya Ukonga, Korogwe Vijijini na Monduli kupitia kikao cha kamati kuu ya chama.

Katibu wa chama hicho kanda ya kaskazini Amani Golugwa ameiambia tovuti ya www.eatv.tv kuwa tayari chama hicho kupitia mkutano wake kimekwisha pitisha majina ya watakaopeperusha bendera za chama hicho katika uchaguzi mdogo wa Septemba 16, 2018.

Golugwa amewataja wagombea hao kuwa ni Amina Ally atakayegombea ubunge jimbo la Korogwe Vijijini, aliyekuwa Diwani wa kata ya Lepurko Yonas Masiaya Laizer atasimama jimbo la Monduli pamoja na Asia Msangi atakayeiwakilisha Chadema jimbo la Ukonga jijini Dar es salaam.

Hatua hiyo imechukuliwa baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kutangaza Uchaguzi Mdogo wa Ubunge katika majimbo matatu na wa udiwani katika kata mbili za Tanzania Bara utakaofanyika Septemba 16, mwaka huu.

“Tume ilipokea barua kutoka kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye kwa kuzingatia kifungu cha 37(3) cha sheria ya Taifa ya Uchaguzi, aliitaarifu Tume uwepo wa nafasi wazi za Ubunge katika majimbo matatu majimbo hayo kuwa ni Korogwe Vijijini, Mkoa wa Tanga kufuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo Stephen Hilary Ngonyani, Jimbo la Ukonga katika mkoa wa Dar es Salaam na Jimbo la Monduli mkoani Arusha baada ya waliokuwa wabunge wa majimbo hayo kujiuzulu uanachama wa CHADEMA hivyo kukosa sifa za kusalia wabunge”, ilisema taarifa ya tume.

Uchaguzi huo utafanyika ikiwa ni mwezi mmoja kupita tangu ufanyike uchaguzi mwingine mdogo katika jimbo la Buyungu wilayani Kakonko mkoani Kigoma pamoja na kata 79 nchini ambapo Chama cha Mapinduzi (CCM) kilishinda kwa asilimia 100%.
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images