Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104414 articles
Browse latest View live

Msanii Harmonize Achafua Hali ya Hewa Instagram

0
0

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Harmonize amekuwa gumzo mitandaoni kwa siku ya leo Tanzania baada ya kutangaza kuwa anaachia ngoma mpya.

Harmonize kupitia ukurasa wake wa Instagram amewaahidi kuwa ataachia video ya wimbo wake mpya endapo atatapata maoni (Comments) zaidi ya 2000.

Posti hiyo mpaka sasa imeshangaa masaa manne na tayari imefikisha comments 3000+ na views 102,000+ na kinachofuatia sasa ni mashabiki wake kumuandama mitandaoni mkali huyo wa Kwangwaru kuachia kichupa hicho.

Wengine waliotoa neno juu ya ujio wa ngoma hiyo ni mwanamuziki Barnaba na Eugy kutoka nchini Ghana ambao nao wamedai kuwa wimbo huo utakuwa ni moto wa kuotea mbali. || “Aiseee hili chuma, chuma naikumbuka mzee balaa sana ni chuma na nusuu,“ameandika Barnaba huku msanii wa muziki kutoka Ghana, Eugy akiandika “Let’s goooo!!“. || Ngoma hiyo mpya ya Atarudi ni ngoma ya tatu ya Harmonize kufanya kwa mwaka huu baada ya ngoma yake ya DM Chick na Kwangaru aliyomshirikisha Diamond Platnumz kufanya vizuri.

Je, Atarudi huenda ukawa wimbo mkubwa na mkali zaidi ya Kwangwaru na DM Chick???

BREAKING News: Dada yake Rais Magufuli, Monica amefariki Dunia leo

0
0

Leo August 19, 2018 Rais John Joseph Magufuli amefiwa na dada yake, Monica Joseph Magufuli aliyekuwa amelazwa katika hospitali ya rufaa ya Bugando jijini Mwanza. Bi. Monica amefariki leo asubuhi August 19 ikiwa ni siku moja tangu Rais Magufuli amtembelee katika chumba cha uangalizi maalum hospitalini hapo.

Hii ni kwa mujibu wa Mkurugezi wa kitengo cha Mawasiliano ya Rais, Gerson Msigwa kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Tunatibu Na Kuponesha Kabisa Upugufu wa Nguvu za Kiume, Busha, Kisukari na Vidonda vya Tumbo

0
0
TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO? BUSHA BILA KUPASUA KISUKALI NA VIDONDA VYA TUMBO? asilimia kubwa ya wanaume wanaupungufu wa nguvu za kiume NA maumbile madogo

NI NINI KINACHOSABABISHA UUME KUZIDI KUWA MDOGO NA WEMBAMBA 1 kuugua chango LA uzazi 2 unene kupita kiasi 3 kuvaa nguo au chupi za kubana 4 kupiga punyeto kwa mda mrfu ,NI NINI TIBA YAKE MAKAKANUA MIX nidawa ya mitishamba iliyochanganywa NA mizizi kumi NA mbili urfusha NA kunenepesha UUME saizi upendayo ich 5,6,7, NA 8 kwa urfu NA sentimita 3,4, na 5 ipo dawa ya kunywa na kupaka NI NINI KINASABABISHA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME 1 kupungukiwa kwa homoni ya testerone 2 kuhudhurika kwa Neva au uti wa mgongo 3 utumiaji holela wa madawa ya kizungu 4 usongo wa mawazo na asira 5 utumiaji wa vyakula vya mafuta mengi NI NINI TIBA YAKE MAPRO POWER NO 2 NDIO tiba tosha kwa sasa kwani utibu matatizo matatu kwa pamoja 1 itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15 adi 20 ,2 itakufanya urudie tendo zaidi Mara tatu 3 uhimalisha uume uliolegea na kusinyaa OKOA NDOA YAKO SASA ujihepusha na lawama ndani ya ndoa yako au pale ukutanapo na mpezi dawa hii itamfanya mpenzi wako hakueshimu na hasitoke nnje ya ndoa na ata wazee wenye umri mkubwa wanapona zipo dawa za kupunguza kitambi,minyama uzembe, presha ,kisukar mvuto wa mpezi au biashara

FIKA OFISINI KWETU MBAGALA ZAKHEMU na wateja wa kanda ya ziwa yupo wakala wetu mwanza mjini au piga simu 0752348593

DR MABULA na utaletewa popote ulipo uduma hizi

Calisah 'Nina Kampuni ya Kuwapa Wanawake Mimba'

0
0
MWANAMITINDO maarufu Bongo, Calisah, amesema kwa sasa anamiliki kampuni mbili,  moja ni ya kukuza wanamitindo wachanga Bongo na nyingine ni ya kuwapa mimba wanawake walioshindwa kupata mimba kwa wanaume zao.

Calisah amesema kwa sasa ameshawapa mimba wanawake 25 na anaendelea na biashara yake ambapo ukihitaji mimba unamtafuta mnasaini mkataba unamlipa kisha anakupa mimba.

WCB wafunguka ishu ya Rich Mavoko kujisajili upya BASATA

0
0

WCB imesema taarifa za Rich Mavoko kwenda kujisali Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) si sawa kwani tayari alikuwa ameshasajili kupita lebo hiyo mwaka huu.

Meneja kutokea WCB, Sallam SK amesema hayo alipokuwa akieleza ushirikiano uliyipo kati ya WCB na Baraza hilo kwa sasa.

"Suala la kusema hatushirikiani na BASATA hilo litakuwa si la kweli na sisi tunashirikiana nao sana kuna vitu vinatokea bahati mbaya. Lakini ukiangalia wasanii wetu wote wamesajiliwa BASATA na hamna yeyote ambaye hajawahi kujisajili," amesema.


"Hata juzi kati hapa ilisemekana kuwa Rich Mavoko ndio alienda BASATA akajisajili, hapana!, kashasajili kupitia WCB, actually mwezi wa saba mwaka huu," Sallam SK ameiambia The Playlist ya Times FM.

August 09, 2018 msanii Rich Mavoko alifika BASATA kwa kile alichoeleza alienda kujisajili na Baraza hilo lilithibitisha hilo pia.

Kwisa wa Shilawadu Achumbia..Hakuamini Alivyokubaliwa na Huyu ndio Mchumba Wake

0
0

From Kwisa
Siku ya Jumamosi ilikua ni siku kubwa Sana kwangu.. Nilifanya maamuzi makubwa Sana katika maisha maana nilijua itakua rahisi bt NO haikuwa Rahisi.. Nilienda mpaka kaburini kwa mama kwisa kuomba urahisi wa jambo hili na pia kuchukua baraka.. Nashukuru Mungu nilipo muomba MKE wangu matarajiwa Her hand in Marriage (Tuishi pamoja Milele) alinikubalia tena kwa furaha ya machozi juu (Hata mm nilikimbia chumbani kujifungia nilie kwanza, 😅😅 si unajua kidume kulia hadharani tena..) Asante Sana kwa kila rafiki, ndugu na jamaa mlioweza kufika... Nyinyi ni familia yangu.. Mlikua wengi sintoweza kutaja mmoja mmoja.. Ila asanteni sana sana... Happy Birthday @lauraally_ na Asante kwa kukubali kuishi milele na mm na watoto wetu.. Inshallah Jini mkata kamba yoyote asipite.. Damu itamwagika

Mwita Waitara "Naomba Chadema Waache Kunifatilia la Sivyo Ntamwaga Siri zao Hadharani"

0
0

Mgombea wa kiti cha Ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika Jimbo la Ukonga, wilayani Ilala mkoani Dar es Salaam, Mwita Waitara, amekionya Chama cha CHADEMA, kuacha kumfuatilia, la sivyo ataanika siri nzito zitakazokipasua kabisa chama hicho.

Huu ndio Mkoa Unaongoza Kwa Udhalilishaji

0
0

Jamii imetakiwa  irudi katika  dini zao pamoja na kurudisha malezi ya zamani kwa lengo la kupunguza au kuondoa kabisa  vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia.

Hayo yameelezwa na mkuu wa dawati la jinsia na watoto mkoa wa kusini Ali Mohammed Othmani  wakati akitoa elimu juu ya udhalilishaji wa kijinsia kwa wanafunzi wazazi,walezi pamoja na walimu huko makunduchi mkoa wa kusini unguja. 

Amesema kuwa takwimu zinaonesha kuwa  mkoa wa kusini unaongoza kwa kesi za udhalillishaji  ikiwemo kubaka,kulawiti  na mengineyo  jambo ambalo linarudisha nyuma maendeleo ya wanafunzi  na kushuka kwa kiwango cha elimu  pamoja na kushuka nguvu kazi ya taifa. 

Nae afisa wa  dawati la jinsia na watoto shuwekh Zuberi amefafanua madhara  ya ukatili ambayo yanaweza kumpata  muathirika wa tatizo hilo ni pamoja na kuathirika kisaikolojia, kupata ulemavu na hata kupata maumivu makali  katika mwili wake. 

Kwa upande wake diwani wa wadi ya makunduchi Zawadi Hamdu amewashukuru dawati la jinsia kwa kuja kutoa elimu na amewataka  wawe mstari wa mbele katika kushulikia kesi zao ili kuweza kupatiwa hukumu mapema.

Idadi ya waliohama Chadema, CUF kwenda CCM yafikia 138

0
0

Idadi ya madiwani na wabunge wa vyama vya upinzani, wengi wao wakiwa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Chama cha Wanachi (CUF) waliojiuzulu na kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM) imefikia 138 nchini Tanzania.

Takwimu zilizotolewa na gazeti la Mtanzania zinaonyesha tangu mwaka 2016 hadi 2018 idadi ya madiwani wa Chadema waliojiunga CCM imefikia 129 huku CUF ikifikia tisa.

Kwa mujibu wa gazeti la Mtanzania Jumapili, Kitengo cha Habari cha Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kimeeleza kuwa katika uchaguzi mdogo ujao utakaofanyika Septemba 16, unaojumlisha kata 23 Tanzania Bara, Chadema kina kata 15 za madiwani waliojiuzulu, akiwamo Diwani wa Monduli Mjini ambaye pia alikuwa ni Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Isack Joseph maarufu kwa jina la Kadogoo.

Hata hivyo, taarifa hiyo haikuwa na idadi ya madiwani waliojiuzulu na kusababisha uchaguzi mdogo uliofanyika Agosti 12, mwaka huu ukijumlisha kata 36 kutoka kata 77 zilizotangazwa awali baada ya madiwani 41 kupita bila kupingwa.

Akizungumza na Mtanzania Jumapili, Katibu Mkuu wa Chadema, Dkt Vicent Mashinji, alisema katika uchaguzi huo, idadi ya madiwani wao waliojiuzulu na kujiunga CCM walikuwa 54.

Kwa upande wa CUF, Naibu Mkurugenzi wa Habari na Uenezi (kambi ya Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad), Mbarala Maharagande, aliliambia Mtanzania hadi sasa idadi ya madiwani wao waliohama imefikia tisa.

Jumamosi gazeti moja la kila siku liliandika kuwa juzi pekee kulikuwa na madiwani saba kutoka kata za mkoani Pwani waliohamia CCM wakitokea vyama vya upinzani.

Gazeti hilo liliwataja majina na kata zao katika mabano kuwa ni Ally Mbwana (Ikwiriri), Abdul Omari (Kisiju), Sultan Waziri (Njia nne), Issa Salum (Magindu), Shabashaba (Ruvu), Hassan Mohamed na Hamis Mbonde.

Pia idadi aliyoitaja Maharagande inamjumuisha aliyekuwa Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Mussa Kafana, aliyekuwa Diwani wa Kata ya Kiwalani, aliyejiuzulu juzi na kuomba kupokewa CCM.

Kafana alipishana siku kadhaa na aliyekuwa Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala ambaye pia alikuwa Diwani wa Kata ya Vingunguti (CUF), Omary Kumbilamoto, aliyehamia CCM mwezi Julai, limeripoti Mtanzania.

Limesema kuwa sababu za madiwani hao kujiondoa Chadema hazitofautiani kwa sababu wamekuwa wakitoa hoja kuwa wanahamia CCM kuunga mkono utendaji kazi wa Rais Dk. John Magufuli.

Kwa mujibu wa gazeti hilo hadi sasa imebainika kuwa Mkoa wa Arusha ndio unaongoza kwa idadi kubwa ya kata zake kuondokewa na madiwani, huku Halmashauri ya Monduli pekee madiwani wake wanane walijiuzulu na kujiunga CCM.

Maandamano dhidi ya kukamatwa Bobi Wine yaendelea Uganda

0
0

Biashara zilisimama Jumamosi mjini Mukono, Uganda wakati maandamano yalipoanza kupinga kuendelea kuwekwa kizuizini Robert Kyagulanyi (Bobi Wine).

Bobi Wine ni mwanasiasa wa kambi ya upinzani nchini Uganda.

Maandamano hayo yalisababisha watu wenye silaha kupiga risasi za moto na kutupa mabomu ya machozi ili kuwasambaza waandamanaji hao.

Operesheni hiyo iliongozwa na Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Mukono Rogers Sseguya na maafisa wengine waliokuwa zamu wa vituo mbalimbali vya polisi wilayani Mukono.

Moses Kiwanuka ambaye ni mmoja wa wakazi wa eneo hilo amesema hawawezi kukaa na kutizama wakati serikali ikiwaweka kizuizini na kuwatesa watu.

Wakazi hao walianza kwa kufunga barabara ya Mukono-Kayunga na kisha wakaendelea kuzuia njia kuu ya Kampala-Jinja.

Mkuu wa polisi wa wilaya hiyo Sseguya aliagiza wenye maduka ambao waliacha waliendelea kufanya biashara kufunga maduka yao na kuwaambia kuwa biashara zao zitaangamizwa.

Ijumaa, polisi hao waliwakamata waandamanaji kadhaa pembezoni mwa mji huko Kamwokya.

Wakazi hao walikamatawa katika msako uliosimamiwa na mkuu wa polisi wa mkoa wa Kampala ya Kaskazini Michael Musana.

Maandamano hayo yalianza Alhamisi baada ya habari kuenea kwa kukamatwa kinyama, kuteswa na kuwekwa kizuizini Kyagulanyi na jeshi la nchi hiyo

Young Dee Akana Kutoka Kimapenzi na Rosa Ree, Adai Wana Wimbo Wamefanya Pamoja

0
0
Rapa Young Dee amezungumzia uhusiano uliopo kati yake na rapa wa kike the Goddess Rosa Ree, baada ya kuenea kwa tetesi kuwa huenda wawili hao wana uhusiano wa kimapenzi kutokana na ukaribu wao.

Akifunguka hivi karibuni kupitia The Playlist ya Times Fm, Young Dee alikanusha tetesi hizo, na kueleza kuwa hakuwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Rosa Ree, bali kinachowakutanisha ni muziki wao tu.

“Hatujawahi kudate mimi na Rosa Ree, tulikuwa washkaji tu. Ni kwa sababu yeye ni rapa na mimi ni rapa kwahiyo tunakutana kwa sababu ya kazi ya muziki… ni kama mimi na wewe kinachotukutanisha hapa ni hii kazi, hatuuzi vitumbua,” alijibu swali la Lil Ommy, mtangazaji wa The Playlist.

Hata hivyo, alipoulizwa kuhusu maswali ya wengi kuwa huenda wawili hao walikuwa wapenzi lakini sasa wameachana, Young Dee alisema bado hawajaachana [kama washkaji], na kueleza chanzo cha ukaribu wao.

“No, hatujaachana. Kwa sababu ni mtu ambaye anafanya kazi zake na mimi nafanya kazi zangu. Kilichotukutanisha ni kwasababu watu wote ambao sisi tulikuwa tunafanya nao kazi walikuwa watu wa karibu,” alifunguka.

Katika hatua nyingine, rapa huyo ambaye ameachia audio na video ya ‘Naoa’, alikiri kuwa kuna wimbo amefanya na Rosa Ree, lakini kwakuwa bado ni mapema, mengi kuhusu mradi huo yatajulikana muda utakapofika.

Rosa Ree ni rapa wa kike ambaye kwa hivi sasa anaonekana kuongoza mashambulizi ya mistari na mitindo ya kughani, akishika vichwa vingi vya habari na kuwavuta wasanii wengine wakubwa kufanya naye kazi.

Jionee Haji Manara Alivyowakera Mashabiki wa Yanga Baada ya Simba Kuibuka Kidedea Hapo jana

0
0
Wanasema kwenye msafara wa Mamba pia Kenge hawakosekani na ndivyo ilivyokuqa jana wakati wa mchezo kati ya Simba na Mtibwa pale Ccm Kirumba.

Kikundi kikubwa cha mashabiki waliovalia jezi za njano na kijani walikuwepo kuizomea Simba katika fainali hiyo lakini baada ya filimbi ya mwisho Haji Manara aliamua kuwakera kwa kufurahia ushindi mbele yao.

Jionee hapa hali ilivyokuwa


Manchester United Hakuna Kitu..Yatandikwa Kichapo cha Mbwa

0
0

Wakati Manchester United ikionja kichapo cha kwanza msimu huu baada ya kukubali kufungwa mabao 3-2 na Brighton & Hove Albion, ligi kuu ya soka nchini England EPL imeweka rekodi ya idadi kubwa ya mabao ndani ya siku moja.

Moja ya mabao kwenye mchezo wa Man United na Brighton.

Kabla ya Man United kufungwa na Brighton kwa mabao ya Glenn Murray 25', Shane Duffy 27' na Pascal Groß 44', EPL ilitanguliwa na ushindi wa majirani zao Manchester City ambao wameilaza 6-1 Huddersfield, hivyo kufanya kupatikana jumla ya mabao 16 ambayo ni idadi kubwa zaidi kwenye siku moja ya EPL ambayo ilihusisha mechi tatu au chini ya hapo.

Ukiacha mabao matano yaliyofungwa kwenye mechi ya Man United na Brighton, mabao mengine manne yamefungwa leo, ambapo Burnley wakiwa nyumbani walikubali kichapo cha mabao 3-1 kutoka kwa Watford. Hivyo ukijumlisha mabao yote katika mechi tatu za leo jumla yake ni 16.

Mbali na rekodi hiyo ya mabao pia Man United imeruhusu kwa mara ya 10 kufungwa goli 3 katika kipindi cha kwanza kwenye historia yake ya kucheza EPL. Mara ya mwisho kufungwa hivyo katika miaka ya hivi karibuni ilikuwa ni mwezi October 2015 kwenye mechi dhidi ya Arsenal.

Kwa upande wake Romelu Lukaku ambaye alifunga bao la kwanza la Man United dakika ya 34 kabla ya  Paul Pogba kufunga la pili dakika ya 90, sasa amezifunga timu 18 zinazocheza EPL msimu huu akifanya hivyo kwa misimu tofauti. Timu mbili pekee kati ya 20 ambazo hajazifunga ni Cardiff City na Wolverhampton.
 

Uhaba wa Saruji Nchini..Serikali yaingilia Kati

0
0

MWENYEKITI wa Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji,  Sadick Murad, amesema wanatarajia kukutana na serikali kutafuta mwafaka wa upatikanaji wa saruji  hususan iliyokwama njiani  kutokana na zuio lililowekwa.

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira, Sadick Murad (katikati), akizungumza na waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam jana, kuhusu mafanikio na changamoto mbalimbali walizokutana nazo baada ya ziara yao ya kutembelea viwanda zaidi ya 12 katika Mkoa wa Dar, iliyoratibiwa na Shirikisho la wenye Viwanda Tanzania (CTI).

Murad aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati akihojiwa na waandishi wa habari baada ya kutoa taarifa ya ziara iliyofanywa na kamati yake.

Alisema kamati itazungumza na serikali kuhusu saruji iliyokuwa njiani kwenda nje ya nchi ili kuona namna ya kuwasaidia wasafirishaji wa bidhaa hiyo wasipate hasara.

Alisema lengo la serikali kuzuia saruji hiyo kupelekwa nje ya nchi halikuwa na nia mbaya kwani inataka kutosheleza kwanza mahitaji ya ndani ndipo iruhusu kusafirisha nje ya nchi.

“Saruji itaruhusiwa kwenda nje iwapo mahitaji ya ndani yatajitosheleza. Tusije tukaanza kutafuta saruji kutoka nje ya nchi kukidhi mahitaji ya ndani wakati sisi wenyewe tunaweza kuzalisha ya kutosha,” alisema

Alisema kutokana na uhaba ambao ulijitokeza, serikali imetaka viwanda vyote vijitosheleze mahitaji ya ndani baada ya hapo itaruhisiwa kusafiri kwa  kuwa hilo zuio sio la kudumu.

Aidha, alisema wakati wakiwa kwenye ziara walijulishwa kuwa viwanda vya saruji vitatu vilifanya matengenezo kwa wakati mmoja na kusababisha uzalishaji kupungua.

“Pia  viwanda vililalamika kuwa havina magari ya kutosha ya kwenda kuchukua makaa, hivyo makaa hayaji kwa wakati na wenye magari wakasema hawana mkataba na wenye viwanda,” alisema Murad.

Alisema baadhi ya wenye viwanda walikuwa wanataka wapatiwe vibali ili waagize makaa kutoka nchini Afrika Kusini kwasababu hawakutaka kutumia makaa ya Tanzania.

Murad alisema tayari serikali ilikutana na wenye viwanda kwa ajili ya kuzungumza nao na huenda wakawa wamefikia suluhu.

Wiki hii serikali ilizuia saruji kusafirishwa nje ya nchi kutokana na uhaba wa bidhaa hiyo ambayo ilisababisha mfuko mmoja wa saruji kuuzwa hadi Sh. 18,000.

Jinsi Kibali cha Kuona Siri za Serikali Kinavyotolewa Marekani

0
0

Rais wa Marekani Donald Trump Jumatano alitengua kibali cha kuona siri za serikali cha Mkurugenzi wa zamani wa Shirika la Kijasusi la Marekani (CIA), John Brennan. Je, kitendo hicho kina maanisha nini?

Katika serikali ya Marekani kuna aina tatu za siri : Confidential, Secret na Top Secret. Vibali vya kuona ripoti za siri havimaliziki muda wake. Lakini, kibali cha Top Secret kina chunguzwa kila baada ya miaka mitano, kibali cha Secret kinachunguzwa kila baada ya miaka 10 na kibali cha Confidential kinachunguzwa kila baada ya miaka 15.

Nani wanapatiwa vibali vya kuona siri za serikali? 

Kwa mujibu wa ripoti ya ofisi ya serikali inayosimamia majukumu iliyotolewa mwaka 2017, kiasi cha watu milioni 4.2 walipatiwa vibali vya kuona ripoti za siri hadi kufikia mwaka 2015, wakiwemo maafisa wa jeshi, wafanyakazi wa umma, wafanyakazi walioingia mikataba na serikali.

Kwa nini kibali cha kuona ripoti za siri kinahitajika unapokuwa umestaafu?

Maafisa wa ngazi ya juu wa usalama waliostaafu na maafisa wa jeshi wanahitaji vibali vya kuona ripoti za siri iwapo wataitwa kutoa ushauri katika masuala nyeti. 

Je, rais anaweza kutengua kibali cha kuona ripoti za siri?

Anaweza kufanya hivyo. Lakini hakuna kumbukumbu ya kuwa rais amewahi kutengua kibali cha kuona ripoti za siri cha mtu yoyote. Kibali cha kuona ripoti za siri kawaida kinatenguliwa na idara ya serikali iliyomuombea kibali hicho mfanyakazi wake au mtu aliyeajiriwa kwa mkataba.

Idara zote za serikali kuu zinafuata orodha ya vigezo 13 vinavyo halalisha kutengua au kumnyima mtu kibali ambavyo vinaweza kuhusisha vitendo vya uhalifu wa jinai, kukosekana uaminifu kwa taifa la Marekani, tabia au hali ambayo inaweza kuhatarisha usalama wa taifa au uvunjifu wa usalama.

Kipigo cha Polisi Chaharibu Figo ya Bobi Wine..Madaktari Wajitolea Kumtibu

0
0

Mbunge wa Kyadondo Mashariki, nchini Uganda, Robert Kyagulanyi maarufu 'Bobi Wine' amepata matatizo ya figo na inaelekea kutokufanya kazi. 

Hii ni kwa mujibu wa Mawakili wake waliokwenda kumtembelea Mbuge huyo katika Kambi ya Jeshi ya Makindye anakoshikiliwa 

Kwa mujibu wa gazeti la Uganda la Daily Monitor, Madaktari hao hii leo kupitia Chama cha Madaktari nchini humo, (UMA), wako tayari kumpatia Mbunge huyo matibabu ya kitaalam ya hali ya juu ambaye sasa inaelezwa anapigania maisha yake katika kambi hiyo ya kijeshi 

Madkatari hao wametoa ombi hilo baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Mawakili wa Bobi Wine, wakisema mteja wao anahitaj haraka matibabu ya kitaalam ili kuokoa maisha yake. 

Hata hivyo wamesema hawawezi kutekeleza matibabu hayo bila kupata idhini kutoka Serikalini, kwa mujibu wa taarifa iliyosainiwa na Rais wa UMA, Dk. Ekwaro Obuku. 

Hayo yanajiri ikiwa ni siku chache tangu dereva wa Bobi Wine, kuuawa kwa kupigwa risasi katika vurugu wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Ubunge jimbo la Arua . 

Staa wa muziki nchini Uganda, Jose Chameleone amemuandikia barua ya wazi Rais wa nchi hiyo, Yoweri Museveni kwa lengo la kumuombea msamaha msanii mwenzake huyo ambaye anashikiliwa na Jeshi la Polisi hadi hivi sasa kwa tuhuma za uchochezi.

Shonza asifu ubunifu unaoneshwa na wasanii nchini

0
0

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza amesema wizara yake iko bega kwa bega na wasanii wa filamu ikiwemo kulinda haki zao na kuongeza kuwa haitamuacha pekee msanii yeyote anayehitaji msaaada wa kiserikali kwa kuwa fani hiyo imewapatia ajira vijana wengi hapa nchini. 

Shonza ameyasema hayo wakati akizindua filamu ya Nipe Changu yake msanii Duma katika ukumbi wa Mlimani City ambapo aliwasifu wandaaji wa filamu hiyo kutokana na ubora wa kazi yao lakini pia ubunifu ambao wameutumia katika kuandaa. 

Pia aliwataka wasanii hao kufanya kazi zao kiumakini ili kuwa na ubora wa kimataifa na kujizolea soko ndani na nje ya nchi ili wapate kunufaika na kipato.

Mfahamu Marehemu Dada wa Rais Magufuli

0
0

Aliyekuwa dada wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli, Bi. Monica Joseph Magufuli amefariki dunia asubuhi ya leo Agosti 19, 2018 katika hospitali ya Bugando Jijini Mwanza alikokuwa anapatiwa matibabu.

Kushoto ni Rais Magufuli na kulia ni Marehemu dada yake Monica Joseph Magufuli.

Jana Jumamosi Rais Magufuli alimtembelea dada yake kumjulia hali akiwa amelazwa chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum ICU, ambapo Rais Magufuli alisikika akiwaambia madaktari na wauguzi wa hospitali hiyo kwamba, hali ya dada yake ni mbaya.

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Gerson Msigwa ametoa taarifa za msiba huo kupitia mitandao ya kijamii ambapo ameandika, “Nasikitika kuwajulisha kuwa Dada wa Rais (John Magufuli) Monica Joseph Magufuli amefariki dunia asubuhi leo Agosti 19, 2018 katika hospitali ya Bugando jijini Mwanza alikokuwa akipatiwa matibabu,”.

Monica amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 63 (alizaliwa tarehe 25 Novemba, 1955) na ameacha watoto 9 na wajukuu 25.

Mtangazaji wa Clouds Diva the Bawse. Afunguka ya Moyoni Kuwa hawezi Kuzaa kisa Matatizo kwenye Uzazi

0
0

Mtangazaji wa Ala za Roho Clouds FM Diva the bawse Usiku huu Hajalala Na Katika ukarasa Wakae wa Instagram kaamua Kufunguka Kuwa Kwa Sasa Hawezi kuzaa Kutokana Na Mirija ya Uzazi kuziba kitu ambacho kinampa ugumu wa kupata mimba kwa njia ya Kawaida. Aomba Msaada kwa wasamaria wema Dola 7000 kwa ajili ya IVF (kuzibua mirija) nje ya Nchi

Part1: Nitachokiandika ni kitu ambacho kinaumiza sana Moyo wangu , Naandika Machozi yakiwa yananitoka , Sikutaka kuandika lakini Nahitaji kuandika ili nipate msaada zaidi, Sababu haya ni maisha yangu na naandika toka moyoni sitajali mtu atanifikiria nini au atawaza nini, hii situation is confusing sana na ndio maana nimeshindwa hata kulala yan nashindwa kulala kwa ajili ya hii issue sio tu kulala hata kula vizuri siwezi , Moyo wangu una maumivu mengi sana , Nimejiuliza maswali sipati, ila nimeamua kuandika hapa, Kwa muda sasa kama mwaka niliamua kutafuta mtoto, Nimekunywa kila aina ya dawa mnayoijua nyinyi, za hospitali ndio nimemeza mpaka ikafika kipindi nikachoka, hizo za kunywa ndio nimemeza mpaka nimechoka, nikaamua kuchukua likizo kwa ajili ya vipimo very deep kujua tatizo ni nini, In my life nishawahi kupata ujauzito lakini haukufika ata Miezi4 and i lost the baby, kiukweli ilivyotokea mimi mwenyewe nilishang'aa, ila kwa ajili ya mambo yaliyokuwa yanaendelea kwenye hio relationship na huyo mwanaume anaitwa Solomoni frank , niliona labda Mungu ana Mipango yake, too many lies, so i decided to step out n focus on me ,how i met him Sitaki hata kuandika hapa ila iko siku i will share , Hivyo Basi nikakutana na Madaktari wa TMJ hospital nikafanya kipimo kujua kwanini kupata ujauzito inakuwa mtihani sana. sababu vipimo vyote vilikuwa sawa nikaamua kufanya kipimo cha mirija, ambacho nilifanya 9th july 2018. kwa Mtu alieniona hii siku atagundua nilikuwa na maumivu sana , Nililia sana sijawahi lia kama hivyo katika maisha yangu, Nililia sana Nilikuwa na maumivu sina mfano wa kuyafananisha, went to see Dr, Msemo wa Sanitas hosp ambae pia anafanya kazi TMJ ili nijue hasa tatizo , Yeye ni Daktari wangu , Akaniambia majibu yapo umekutwa na Bilateral Cornual Block yaani mirija imeziba, ata kupata mtoto kwa njia ya kawaida inakuwa maajabu sana. alivyokuwa ananielezea Nilijikuta nalia Machozi yana teremka, nilishindwa drive i was in deep pain, nilitamani yule mtoto aliepotea arudi. at some point Sikuwa Pia naamini Mungu ana Exist , historia tu ya maisha yangu ilinifanya nitamani sana mtoto wangu mwenyewe afu the moment nahitaji sana ndio napewa haya majibu"

Anaendelea
Part 2: Basi nilijikuta nalia kupita maelezo ....had to call a friend called @qqtrends4u and gladly she was there for me wakati huu wote alikuwa yeye na @soudybrown ndio walini comfort 😭😭 i was heartbroken , tumeambiwa friends to keep ... hao ndio my friends to keep .. i love them sana sijui hata nieleze vipi hakuna maneno sahihi ya kueleza. 
Mungu Mkali sana Nilisema, Mimi Diva ambae natoa misaada , nasaidia, moyo wangu una utu imekuaje haya mambo yanitokee nilijiuliza sana ... sikuweza kulala wala kula mpaka nililazwa kwa kupata Presha, but Nikaanza kuomba kwa Mungu Nikasema hii ni mara ya mwisho naomba, Nikampigia doctor isaac nikamueleza akaniambia Gods Timing.... mambo yatakuwa sawa, nimeamua kuongea labda kuna wanawake pia wanapitia hii situation , ni situation inaumiza sana na kila ninapokutana na swali utazaa lini nakuwa naumia na hili swali sababu yan mimi Diva hata abortion sifanyi why on earth this imetokea, wakati wa ukuaji wangu nimeumwa sana na tumbo na naumwa sana na tumbo, nishawahi fanyiwa upasuaji, hivyo solution ilikuwa kuwa na mtoto ili tatizo la maumivu makali ya tumbo kuisha , hivyo naweza sema nimepitia machungu mengi in my life but stil leo usiku huu nimeamka na kuamua kuandika hivi nimemuomba sana Mungu nikasema Im going public with this. bila aibu wala uoga na ntasaidia wengine pia wapate msaada ninaohitaji mimi wakati huu sababu najua maumivu yake, naandika hii part 2 chozi au niseme machozi yananitoka. Everything happens for a reason right, i have my best friend called @iammelissa_1 nilikuwa nae kwa simu kwa muda akasema Diva Najua unachopitia, "I know it’s a sensitive subject and sad for you to talk about!
But maybe you should talk about it because you are a great influence in your country and have many fans that are maybe having the same trouble as you 
So you could help them too talking about it " hivyo nikakaa chini na kuamua kuandika Hivi ninavyoandika .. i believe God is real ... nikaamua kufungua a page ntaweka link on inaitwa Gofundme.com na kuanzisha Kampeni inaitwa ' Dreams , Hopes , Wishes . Nia is to have a donation ya $7000 kwa ajili ya ivf treatment in America. Namshukuru Daktari wangu alisema haya....

Part 3: mayai na kizazi chako vyote viko sawa , but unaweza fanya IVF treatment #ivfjourney nikaamua kuwatafuta madaktari wa nje ya nchi kujua nafanyaje, with the amount of money sababu kuna kuishi huko , kula, kwa siku kadhaa pamoja na kupata sperm donor hivyo hio amount inaweza kutosha. Guys ntaweka link hapo from gofundme , ili kama unaweza uchangie sababu mimi hizo hela sina siwezi danganya, thats alot of money, hivyo link apo juu wil help to support My Campaign called ' Dreams, Hopes, Wishes so that i can have My Miracle Baby baby of my own .... Daktari wangu amesema stil young can have it all done just pray , Nimeandika sababu It is completely sensitive I know but you can imagine the pain i feel everyday. nacheka nafanya kazi nafanya mambo mengine lakini Moyo wangu umevunjika ... Sina raha ... Niko kwenye huzuni kubwa sana maishani... hivyo ntafanya kazi sana na nita save for it ili nipate hio treatment ... Naamini Mungu yupo na anasikia kilio changu 🙏 hivyo Pia naomba Mniombee sana ... thanks💕 love you all 🙏 or you can send the money straight into my account , Diva Gissele AC/ 3007111473924 Equity Bank , or tigopesa 0656336919 Diva Loveness. thank You so much 🙏

NINI MAONI YAKO KUHUSU SWALA HILI

Mbwana Samatta sio Mwenzetu, Aendelea Kuwanyanyasa Wazungu..Atupia Mbili Usiku Usiku Uliopita

0
0

Club ya KRC Genk ya Ubelgiji inayochezewa na mtanzania Mbwana Samatta leo imeshuka tena uwanjani kucheza game ya 4 ya Ligi Kuu Ubelgiji dhidi Charleroi katika uwanja wao wa nyumbani Luminus.

Mbwana Samatta leo ameichezea KRC Genk game ya Ligi Kuu Ubelgiji dhidi ya Charlero kwa dakika 34, hiyo ni baada ya kuingia dakika ya 54 akitokea benchi na kwenda kuchukua nafasi ya Zinho Gano aliyecheza kwa dakika 54 za kwanza.

KRC Genk leo imevuna point tatu lakini hadi Mbwana Samatta anaingi game ilikuwa 1-1, Genk ikitoka kusawazisha goli dakika ya 45 kupitia kwa Jere Uronen, hiyo ni baada ya Charleroi kupata goli la kuongoza mapema dakika ya 27 kupitia kwa Cristian Benavente.

Mbwana Samatta alianza kuonesha makali yake dakika ya 77 baada ya kuifungia Genk goli la pili na baadae dakika ya tatu za nyongeza akafunga goli la tatu la Genk kwa mkwaju wa penati, hiyo inakuwa ni game ya tatu mfululizo kwa Mbwana Samatta kuichezea Genk na kufunga, Genk wapo nafasi ya pili kwa kuwa na point 10 nyuma ya Anderletch wanaoongoza Ligi kwa kuwa na point 12.
Viewing all 104414 articles
Browse latest View live




Latest Images