Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

Truth about Ebola 'Ukweli Kuhusu Ugonjwa wa Ebola'

0
0

From Ghana: Ebola is not real and the only people who have gotten sick are those who have received treatments and injections from the Red Cross

PermalinkNana Kwame wrote:

People in the Western World need to know what's happening here in West Africa. THEY ARE LYING!!! "Ebola" as a virus does NOT Exist and is NOT "Spread". The Red Cross has brought a disease to 4 specific countries for 4 specific reasons and it is only contracted by those who receive treatments and injections from the Red Cross. That is why Liberians and Nigerians have begun kicking the Red Cross out of their countries and reporting in the news the truth. Now bear with me

REASONS:

Most people jump to "depopulation" which is no doubt always on the mind of the West when it comes to Africa. But I assure you Africa can NEVER be depopulated by killing 160 people a day when thousands are born per day. So the real reasons are much more tangible.

Reason 1: This vaccine implemented sickness being "called" Ebola was introduced into West Africa for the end goal of getting troops on the ground in Nigeria, Liberia, and Sierra Leone. If you remember America was just trying to get into Nigeria for "Boko Haram" #BULLSHIT but that fell apart when Nigerians started telling the truth.There ARE NO GIRLS MISSING. Global support fell through the floor, and a new reason was needed to get troops into Nigeria and steal the new oil reserves they have discovered.

Reason 2: Sierra Leone is the World's Largest Supplier of Diamonds. For the past 4 months they have been on strike, refusing to provide diamonds due to horrible working conditions and slave pay. The West will not pay a fair wage for the resources because the idea is to keep these people surviving on rice bags and foreign aid so that they remain a source of cheap slave labor forever. A reason was also needed to get troops on the ground in Sierra Leone to force an end to the diamond miners strikes. This is not the first time this has been done. When miners refuse to work troops are sent in and even if they have to kill and replace them all, the only desire is to get diamonds back flowing out of the country.
Of course to launch multiple campaigns to invade these countries separately would be way too fishy. But something like "Ebola" allows access to an entire area simultaneously..

Reason 3: In addition to stealing Nigerian oil, and forcing Sierra Leone back to mining, troops have also been sent in to FORCE vaccinations (Deadly "Ebola" Poison) onto those Africans who are not foolish enough to take them willingly.3000 troops are being sent in to make sure that this "poison" continues to spread, because again it is only spread through vaccination. As more and more news articles are released as they have been in Liberia, informing the populous of the US lies and manipulation, more and more Africans are refusing to visit the Red Cross.Troops will force these vaccinations upon the people to ensure the visible appearance of an Ebola pandemic. In addition to this they will protect the Red Cross from the Liberians and Nigerians who have been rightfully ejecting them from their countries.

Reason 4: Last but not least, the APPEARANCE of this Ebola "pandemic" (should Americans not catch on) will be used to scare the countless millions into taking an "Ebola vaccine" which in reality is the pandemic.Already they have started with stories of how it has been brought to the U.S. and has appeared in Dallas, how white doctors were cured but black infected are not being allowed to be treated, etc.

ALL that will do is make blacks STRIVE to get the vaccine, because it appears that the "cure" is being held back from blacks. They will run out in droves to get it and then there will be serious problems. With all we have seen revealed about vaccines this year you would think we learned our lesson. All I can do is hope so, Because they rely on our ignorance to complete their agendas.

Ask yourself: If Ebola really was spread from person to person, instead of controlled spread through vaccination - then WHY would the CDC and the US Government continue to allow flights in and out of these countries with absolutely no regulation, Or At All? 

We have got to start thinking and sharing information globally because they do not give the true perspective of the people who live here in West Africa. They are lying for their own benefit and there aren't enough voices out there with a platform to help share our reality. Hundreds of thousands have been killed, Paralyzed and disabled by these and other "new" vaccines all over the world and we are finally becoming aware of it.

Now what will we do with all this information?

Huyu Binti Nimempata Mwezi wa Tatu Sasa Hajaniomba Hela Nimueleweje

0
0
Kuna binti mmoja umri miaka 23 sasa ni miezi mitatu tangu nimtokee cha kushangaza hajaniomba hata mia tano ya vocha na ni mwanafunzi sasa nimueleweje maana kwangu imekuwa kama muujiza, hao wanaofanya kazi tu tayari ni makamanda wa kikosi cha mizinga siku mbili tu ukiwa nae tayari atakuangushia jumba bovu

Binti ni mrembo sana na inaonekana anatoka familia ya kawaida sana ..Je Niwekeze hapa Kimoja naona dalili ya Mke mwema..Au bado naliliwa Timing?

Mwanamke Auawa kwa Kupigwa Risasi na Polisi Kwa Bahati Mbaya

0
0
Mwanamke mmoja mkazi wa Kijiji cha Iglansoni, ameuawa kwa kupigwa risasi kichwani kwa bahati mbaya na askari polisi waliokuwa katika jitihada za kumkamata mtuhumiwa wa ujambazi.

Aliyeuawa ni Joyce Maragabu (65), ambaye anadaiwa kupigwa risasi na askari hao waliokuwa wakijihami na kundi la watu waliotaka kuwavamia ili wasimkamate mhalifu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Geofrey Kamwela, alisema askari hao walikuwa wanataka kumkamata, Nkida Gwisu, anayetuhumiwa kumshambulia mtu mwingine, lakini kwa bahati mbaya risasi hiyo ikampiga kichwani mwanamke huyo aliyekuwa anafua nguo nyumbani kwake.

Kamwela alisema, tukio hilo lilitokea juzi Oktoba 16, saa 6 mchana.

Alisema askari polisi wawili ambao hakuwataja majina yao wa kituo kidogo cha polisi Ihanja, walifika katika kitongoji hicho ili kutoa ulinzi mnadani, lakini baadaye walipewa taarifa kuhusu mtuhumiwa huyo kumshambulia mmoja wa wanakijiji.

Alisema wakati wakiwa katika jitihada ya kumtafuta mhalifu huyo, alitokea mwananchi mmoja aliyedai kumfahamu mtuhumiwa huyo, hali iliyorahisisha kazi ya kumkamata na kumweka chini ya ulinzi.

Hata hivyo, alisema baadaye mtuhumiwa huyo alianza vurugu, hali iliyosababisha kundi kubwa la watu kwenda eneo hilo wakiwa na silaha za jadi ikiwamo mawe, pinde, mishale, fimbo na mapanga, na kuanza kumshambulia mmoja wa askari polisi aliyemshikilia mhalifu huyo.

Alisema kuwa katika hali ya kutaka kumwokoa mwenzake, askari aliyekuwa na bunduki alifyatua risasi moja ya moto hewani, lakini hata hivyo wakiwa kwenye purukushani, ndipo risasi moja ilifyatuka na kumpiga kichwani mwanamke huyo.

Kamwela alisema baada ya tukio hilo, wananchi waliokuwa na hasira waliichoma moto pikipiki ya askari hao, yenye namba za usajili PT 3242 –Yamaha na kuiteketeza.

Alisema kutokana na vurugu hizo, askari hao walijeruhiwa vibaya baada ya kupigwa na kundi hilo na tayari jeshi hilo linawashikilia askari hao kwa mahojiano zaidi. 

Chanzo:Nipashe

Baada ya Miss TZ 2014 Kuandamwa Mitandaoni, Miss TZ wa 2013 ameamua Kuvunja Ukimya

0
0
Kama na wewe unakerwa au haupendi jinsi ambavyo Miss Tanzania wa 2014 Sitti Mtemvu amekua akiandamwa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu umri wake na elimu yake baada ya kushinda taji hilo weekend iliyopita basi uko upande mmoja na Miss Tanzania wa 2013 Brigitte Alfred.
Kupitia page zake za twitter na Instagram Brigitte pamoja na mengine ameandika >>> ‘ Mazuri mengi yanawapita lakini inapotokea skendo mnajadili milele ndio maana hatuendelei, natamani tungeweka hizi nguvu za matusi kwenye vitu vya kujenga‘
Baada ya hiyo sentensi Brigitte alimuandikia Sitti kwa kusema ‘Sitti usiwaruhusu watu wakuandame sana, ikizidi warudishie tu taji lao’

Kwenye tweets nyingine za wiki hii baada ya Sitti kutangazwa mshindi Brigitte aliandika‘mngejua siasa za huko Miss World hata msinge jisumbua kumshambulia huyu msichana kiasi hicho, mtihani wa Miss Tanzania sio tu siku ya fainali ndio maana kunakua na camp ya siku 30′




Taarifa Kuhusu Wazungu Wawili Waliokutwa Wamekufa Chumbani Kwao Dar es Salaam

0
0
WAZUNGU wawili ambao ni mume na mke wanaodaiwa kuwa ni raia wa Afrika Kusini, wamekutwa wamekufa chumbani kwao katika nyumba waliyokuwa wakiishi maeneo ya Slipway, Masaki jijini Dar es Salaam Jumatano hii.Chanzo cha kuaminika kimeeleza kuwa wawili hao ambao walikuwa wakifanya kazi katika baa iitwayo Mashua iliyo ndani ya Slipway, huku mwanamke, aliyetajwa kwa jina la Hotsan, akiwa ndiye Meneja, walikutwa chumbani kwao wakiwa wamefariki baada ya kutoonekana kazini tokea Jumanne, siku ambayo Watanzania walikuwa wakikumbuka miaka 15 baada ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.
Inadaiwa kuwa baada ya kutotokea kazini katika muda wa kawaida, wafanyakazi wenzao walijaribu kupiga simu zao za mikononi, lakini zote zilikuwa zikiita pasipo kupokelewa karibu mchana kutwa na hivyo kuwapa maswali mengi yasiyo na majibu.
Siku iliyofuata, inadaiwa kuwa wafanyakazi wenzao walipojaribu tena kupiga namba hizo, simu zote mbili hazikupatikana.

Awali, walihisi huenda wenzao wameamua kuacha kazi baada ya kupata sehemu nyingine, lakini baadaye wakafikia uamuzi wa kuwafuatilia nyumbani kwao ili kujua kilichotokea.
Walipofika, walikuta milango ikiwa imefungwa kwa ndani, kitu kilichowafanya waamini kuwa walikuwa ndani. Kwa kushirikiana na majirani, wafanyakazi hao waliamua kuvunja mlango wa chumba wanacholala wanandoa hao na kuwakuta wakiwa kitandani wamelala, kila mmoja akiwa amegeukia upande wake.
Baada ya kuona tukio hilo la kushtusha, waliamua kuwaita Polisi ambao walipofika na kuiona miili hiyo, waliamua kuwaita wenzao wa kitengo maalum cha uchunguzi (Crime Investigation) ambao baada ya kufika, waliwataka raia na majirani waliokusanyika hapo kukaa mbali ili kuwapisha kufanya uchunguzi.

Askari hao walikaa na miili ya marehemu kwa zaidi ya saa tatu wakiwafanyia uchunguzi na baada ya kukamilika kwa zoezi hili, miili hiyo ilichukuliwa kupelekwa hospitalini Muhimbili.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataja marehemu kuwa ni Roxxana Hilari na Hainess Hilton William na kwamba uchunguzi zaidi juu ya kilichowaua unaendelea.

Utata kati ya Clouds Fm na Times FM Kuhusu Mwamamuziki Davido Kufanya Show Fiesta Leo Usiku

0
0
Leo Asubuhu kuna taarifa zimesambazwa na Times Fm kuwa Davido amezuiwa na mahakama ya Kisutu Kufanya Show ya Leo ndani ya Fiesta kwa kile walichosema kuwa tayari wao Times FM wanamkataba nae wa kuja kufanya show mwezi wa kumi na moja..Lakini wakati huo huo leo mchana uongozi wa Clouds FM kupitia Prime Times Wamewatambulisha wanamuziki watakao imba leo kwenye Show hiyo akiwemo na Davido kama unavyoona hapo kwenye picha...

Je nini Kinaendelea kati ya Radio Hizi Mbili ?
Na Je Davido Ataimba Kweli ama Amewekwa hapo kama Picha Tu ?

Pamoja na Zengwe Kubwa Davido Akamua Serengeti Fiesta Dar Usiku wa Jana

0
0


Clouds Noma ..Pamoja na zengwe kubwa alilowekewa msanii Davido Ambapo siku ya jana ilisemekana kuwa mahakama imetoa tamko kuwa asipofanye show ya Fiesta..Lakini Kwa mshangao wa wengi ambao walikuwa wanasubiri kuona nini kitatokea msanii huyo alipanda jukwaani kama kawa na kukata kiu kubwa ya mashabiki wake....hahahahh

Mama Mwenye Nyumba Ananitega Sana.

0
0

Nilipohamishiwa kanda ya ziwa kikazi toka Dar. nilimtafuta dalali ili anisaidie kunitafutia nyumba, kweli alipata nyumba ya mama mmoja hivi ambaye kiutamaduni ni mtani wangu na yy huwa ananiita mtani.

Sasa kwanza hana mume, mumewe alifariki mwaka jana mwezi wa 4 na ana watoto wakubwa tu wengine wapo vyuoni na mmoja anafanya kazi dar.

Toka mwezi huu uanze ameanza kunionyeshea tabia fulani fulani, kila nikitoka kazini anakuja ndani mwangu anakaa na wakati mwingine kumbe anakuja amefunga kanga tu.
Jana nimetoka kazini nikapita Hotelini kula nikakaa hadi saa 2 usiku nimerudi home aliposikia nafungua mpango tu huyo akaja na chakula nikamwambia nimeshiba nishakula, akanilazimisha kuwa chukua ule, nikapokea nikakiweka mezani then akakaa, akaniambia niwashe TV nikawasha.

Nikaenda kuoga kurudi naingia chumbani na yy huyo kafika akaniambia ngoja nikupake mafuta nikasema hapana sipaki mafuta usiku, aise si akakaa kitandani!! kumbe hakuwa na nguo ya ndani akabenua kanga mapaja hayo nje nje kweli nilipata mfadhaiko muda huo nikamwambia naenda sebuleni kuangalia kipindi fulani hivi cha ITV-KIPIMA JOTO, Akasema njoo kwanza nikarudi akaanza kunishika shika masikioni, nikamwambia nooo!! sipo tyr akauliza kwa nini? nikamwambia leo sijisikii kufanya hicho unachotaka, akaniuliza ina maana mi mbaya? nikasema hapana ila leo sina hamu kabisa ki ukweli nilikuwa na hamu sana ila nikimwangalia huyu mama ni mtu mzima sana ni above 50 na mimi mwenyewe ndo nipo above 27 nikasema hapana.

Akaniambia njoo angalau mara moja tu tux nikampa moyo kuwa subiri kesho yaani leo. Sasa ndugu zangu leo nitamdanganyaje tena?

Huyu mama sitaki kux naye coz ni kama mama yangu, pia, watoto wake japo wapo hostel chuoni kwao hapa hapa nahofia wakija jua kuwa namx mama yao na tunaheshimiana sana.

wazo la kuhama limenijia usiku ws leo sana.

nifanyeje

Kampeni za Urais CCM: Noti Zamwagwa Nec Dodoma

0
0
Baadhi ya makada wa wa CCM wanaotajwa kuwania urais kupitia chama hicho wanadaiwa kugeuza mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec), kuwa sehemu ya kampeni kwa wajumbe wa mkutano huo wakidaiwa kumwaga fedha usiku kucha.

Gazeti hili lilishuhudia kampeni hizo zikifanywa na wapambe wa wagombea hao nje ya Ukumbi wa Nec uliopo nje ya jengo la White House mjini Dodoma na baadhi ya watu wanaotajwa kuwania nafasi hiyo.

Wapambe hao kwa siku mbili za vikao vya Nec vilivyofanyika mjini hapa kuanzia juzi walionekana wakifika mapema, kusalimia, kujitenga katika makundi madogomadogo na wajumbe wa Nec tofauti na vikao vingine vilivyotangulia.

Harakati hizo hazikuishia katika viwanja hivyo, bali hata nje ambapo mmoja wa makada anayetajwa kuwania nafasi hiyo kutoka Kanda ya Ziwa ameonekana kukutana na makatibu wa CCM katika moja ya hoteli mjini hapa.

“Huyu jamaa amekutana na makatibu wa CCM mara nyingi katika kile kinachoelezwa kuwa ni kusaka wajumbe ili wasijiunge na kambi nyingine,” kilieleza chanzo chetu.

Alipoulizwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, alisema bado hajazipata taarifa hizo na kwamba kama kuna vitendo vya rushwa vinafanyika ni nje ya mazingira hayo.

Alisema katika mazingira kunapofanyika kikao cha Nec, si rahisi kuwapo vitendo hivyo.

“Sasa kama wanapeana barabarani mimi itakuwa ni vigumu sana. Mimi ninashughulikia na mambo ya humu ndani (kikao cha Nec),”alisema na kuongeza:

“Leteni taarifa nilikuta fulani anagawa ama fulani anapokea, haya maneno ya jumla hivi yanaweza kuwa ni mkakati wa kupaka chama matope,” alisema.

Alisema kama inagawiwa usiku wakati yeye akiwa amelala hawezi kufahamu.

Makatibu na wenyeviti wa CCM wa wilaya wanaingia katika Nec kwa mujibu wa vyeo vyao.

Tayari hali hiyo imelalamikiwa na baadhi ya wajumbe wa Nec, wakisema inakitia aibu chama.

Alichofanyiwa Diamond Fiesta...Nimeamini Maisha Bila Unafki Hayaendi

0
0

Nakumbuka miaka mitano iliyopita aliyekuwa nguli wa filamu Nchini Tanzania marehemu ""Steven Kanumba"" alienda kwenye jumba la Big Brother....

amini usiamini bila sababu yyte ya maana watanzania ndo walikuwa wa kwanza kuanza kumsema kuwa hajui kuvaa, nani alimchagua , hajui kiingereza mpaka kufikia kumuigiza!!! Walisahau hata watu maruufu kama Messi na wengine wengi hawajui kuongea kabisa lugha hiyo..

Baada ya kifo chake watanzania hawahawa wakaanza kusema alikuwa nguli aliyetuwakilisha vizuri nje ya nchi na kulia sana!!!kumbe wakati akiwa hai tulikuwa tunamshusha chini..

Miaka mitano baadae Tanzania imempata mtu anayeiwakilisha vizuri nje ya mipaka na kuitangaza vizuri nchi yake..

Pasipokuwa na sababu za msingi (chuki binafsi tu)anapangiwa njama za kuzomewa na kuabishwa katika ardhi ya nchi yake ambayo kwa namna moja au nyingine kuna watu wameifahamu sababu yake!! Ukiuliza sababu za wengi wao kumchukia ni mafanikio yake lakini hata kama humpendi mtu hivi ndo hadi umzomee kwa kiasi kile !!!

leo na kesho naye huyu akitoka utaskia hawahawa waliokuwa wanamzomea wanaanza kusema jamaa alikuwa anatuwakilisha vizuri sana , ametutangaza sana kimataifa!! lakini Watanzania wenzake ndio vinara wa kumuangusha..

Si lazima kila mtu ampende Diamond ila kutumia nguvu kubwa sana kumuangusha mtu ni ishara ya uwoga na Roho ya kimaskini...

Nimeamini ""maisha bila unafki hayaendi"

Sintah 'Lundenga Watanzania Wa Sasa Sio Wa Zamani Wakuburuzwa Buruzwa Tuu Ona Unavyoaibika'

0
0
Daah Ona jinsi Lundenga unavyoshusha hadhi ya mashindano haya, ona jinsi unavyoaibika na kutungiwa sms zinazosambaa mitandaoni yote hii ni kwasababu ya fitna iliyoendelea....
kwakweli hii Miss haijawahi kutokea Tanzania, wa Tanzania wa sasa sio wa zamani wa kuburuzwa buruzwa tuuuu, wanaelwa kila kitu, maneno mengi yameongelewa na Lundenga usijiaibishe katika kipindi hiki kigumu.... daaah inasikitisha but naamini  mtalifanyia kazi na kutujuza wa Tz maana ni mambo ya ajabu vitu vya ajabu, mara miaka 18, mara 23, mara 25 ilimradi kila mmoja anasema lake.

Lundenga hebu rudisha Miss Tanzania ya zamani watu wakisikia Miss Tanzania inakuja tunaanza kutafuta nguo mwezi mmoja maana lilikuwa moja ya shindano kubwa Tanzania, ila kwa sasa si apeche si aloloo.... jua umewaudhi sana watu tena sana, mbona kwa Briggite, Hapiness hawakusema?? iweje huyu?? kwa kipi haswa watu wamuonee wivu yeye?? Sitti anaweza akashindana na Ms Alfred kwa kitu chochote?? kwanini hawakuwasema hao waliopita wampinge yeye BIG NO Mr Mkurugenziii....

Sitti Mtemvu Umeshakuwa Maarufu Bongo Kwa Week Moja Rudisha Taji kwa Lungenga Umaarufu Uzidi

0
0
Nadhani katika Mtu aliyevunja rekodi ya kuwa maarufu na kuzumgumziwa kila sehemu kwa muda mfupi zaidi itakuwa ni huyu mrembo ambae ni Miss Tanzania 2014 Sitti Mtemvu..Yaani kwa sasa Wema Sepetu na Diamond Wamepumzika ..Ushauri wangu kwako tumia hiyo fursa kuwa maarufu zaidi ya hapo ..Rudisha Taji la Lundenga kwa hiari yako uone ..Najua itawashangaza wengi ila umaarufu utakuwa zaidi ya hapo na trust me Watanzania watakupenda....

Mfano mdogo tunaupata kwa Miss America 1984 Vanessa Williams ambae alivuliwa Taji la Miss America baada ya Picha zake za Uchi kuvuja Mitandaoni ..Surprisingly  the Huge shameless scandal did not bring her down , she actually emerged as THE most successful of any person ever chosen for the title of Miss America in the entire history of the organization's run. 

Tunasubiria...Wacha Trailer Iendeleee

Ukistaajabu ya Tanzania Hujayaona ya Kenya..Huyu Ndio Miss Kenya

0
0
Ukistaajabu ya Tanzania Hujayaona ya Kenya..Huyu Ndio Miss Kenya , Usipaniki tulia ana Miaka 19 tu , ana degree, masters na PHD...Beautiful Onyinye...LOL

Kizimbani Kwa Kucheza Ngoma ya Kigodoro Wakiwa Uchi

0
0
WAKAZI wa eneo la Masasi Mbovu katika Halmashauri ya mji wa Masasi mkoani Mtwara wamefikishwa kwa mara ya kwanza mahakamani kujibu shitaka linalowakabili la kucheza wakiwa watupu kwa staili ya vigodoro kwenye sherehe ya ndoa.

Jemima Jordan (22), Aziza Chukachuka (20), Anna Yohana (25) pamoja na mtoto mwenye umri wa miaka 17 (Jina linahifadhiwa) walifikishwa mahakamani hapo juzi mbele ya Hakimu Halfani Ulaya na kusomewa shitaka na mwendesha mashtaka Iddi Athumani.

Athumani alidai kuwa watuhumiwa hao walitenda kosa hilo Septemba 30 mwaka huu majira ya saa 12 jioni katika eneo la Masasi Mbovu huku wakijua kuwa kufanya hivyo ni kosa linalokwenda kinyume na maadili ya kitanzania.

Alidai kwa kuwa shauri hilo linamshirikisha mtoto aliye chini ya miaka 18, ni vyema Mahakama ikaahirisha kesi hiyo ili kupisha upelelezi wa kina kuhusu shitaka hilo linalowakabili washtakiwa hao.

Hakimu Ulaya alikubaliana na ombi la mwendesha mashtaka na aliahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 30 mwaka huu itakapotajwa tena. Watuhumiwa hao walio nje kwa dhamana hawakutakiwa kujibu lolote mahakamani hapo.

Diamond Platnumz Anaomba Kura yako Hapa ili Aweze Shinda Tuzo Nyingine ya MTV

0
0
Tafadhali naomba ubonyeze link hii kuweza ku ipigia kura kwenye tunzo za MTV Europe kama Masanii bora International toka Africa
Kupiga kura ni rahisi saana Bonyeza link hii kisha itakupeleka moja kwa moja hadi hapo kwenye picha... halaf utabonyeza ilo Neno VOTE chini ya jina langu http://base.mtvema.com/vote?category#cat=best-african
Kama Tuliweza kuichukua ile ya Marekani sasa hii itatushindaje....Tunaweza kupiga nyingi tuwezavyo Hadi ije nyumbani!!!

Shilole Atoa Makavu live 'Nuhu ni Mkubwa Ndio Maana Kajua Utamu wa Mwanamke na Ndo Maana Kaniganda'

0
0
Instagram imekua moja ya mtandao ambao umekua gumzo sana hasa hapa Tanzania. Wasanii wengi wameikimbia Facebook na Twitter na kuhamia Instagram ambako ndipo mara nyingi hutoa updates nyingi kuhusu maisha na kazi zao kwa ujumla. Kwa upande mmoja taarifa zitolewazo na wasanii hao hupokelewa vizuri na mashabiki wao na wakati mwingine hupokelewa vibaya.

Mfano mzuri ni pale mwanadada Shilole alipoamua kuweka wazi mahusiano yake na msanii mwenzake Nuhu Mziwanda, kuna baadhi walipokea vizuri na kuna baadhi walijitokeza waziwazi kupinga mahusiano hayo. Sababu kubwa ya wengi kupinga mahusiano hayo ni kutokana na kupishana kwa umri kwa wasanii hao, Shilole akiwa ni mkubwa zaidi kiumri kushinda Nuhu.



Ni mengi yameongelewa lakini inaonyesha ya kua Shilole amechoka maneno hayo na kwa sasa ameamua kufunguka rasmi kuhusu maneno haya. 

Kupitia akaunti yake ya Instagram Shilole aliandika 

"Huyo nuh mnaosema ni mdogo kwangu! Kwani hajawaona wadogo wenzie mpka kanipenda mm?? Mtt mdogo angekuwa analilia mapenz ! Siangekuwa analilia ziwa kwa mama yake ! But ni mkubwa ndo maana kajua utam wa mwanamke ndo maana kaniganda! Wenywe tumeridhiana! Wivu tu unawasumbua nikiwa na mtu mzima mtasema lol shilole bwanaake babu nikiwa na kijiana mwenzangu oooh kitoto kidogo mnikome! Mnakuepogi chumban muona udogo wake???"

Flora Mvungi na H-Baba Wamfunika Wema Sepetu Katika Mjengo

0
0
Stori: Gladness Mallya

HESHIMA! Wanandoa, muigizaji Flora Mvungi ‘H.Mama’ na mwanamuziki Hamis Ramadhan ‘H.Baba’ wamemfunika mwigizaji Wema Sepetu kwa kupanga ghorofa.

Akizungumzia mjengo huo walioupanga maeneo ya Mbezi-Jogoo, jijini Dar, H. Mama alisema yeye na mume wake wameamua kupanga nyumba hiyo si kwa sababu ya kumfunika mtu bali wanapenda kuwa huru na kuishi vizuri.

“Hatushindani na mtu katika maisha yetu bali cha msingi tunaangalia nafsi zetu zinataka nini, kuhusu gharama yake, niache kidogo,” alisema Flora.Wema amepanga nyumba ya kawaida maeneo ya Kijitonyama jijini Dar.

Mwanamuziki Linah Sanga na Mchumba Wake Watibuana, Kisa Hichi Hapa

0
0
Stori: Musa Mateja
MCHELE ulionyooka! Staa wa Bongo Fleva, mwenye sauti ya kumtoa nyoka pangoni, Estelina Sanga ‘Linah’ na mchumba’ke, Nangari Kombo wanadaiwa kutibuana, kisa kikidaiwa ni maneno ya wanafiki yasiyokuwa na ukweli.

Habari za chini ya kapeti zilinyetisha kwamba mtiti kati ya wawili hao ulijiri juzikati baada ya Kombo kudaiwa kuanza kumtuhumu Linah kuwa anapokuwa kwenye ziara za matamasha kama Fiesta huwa anamsaliti na wanaume wengine.

Chanzo hicho kilidai kwamba, kufuatia madai hayo Kombo alimuanzishia Linah bonge la tafrani na kujikuta kila mmoja anachukua hamsini zake.
Linah alipoulizwa kuhusu ishu hiyo alisema: “Ni kweli kulitokea kutoelewana but (lakini) tumeyamaliza, tupo vizuri sana.”
GPL

Meli ya MV Victoria ni Janga Linalosubiri Kutokea, Yapewa Jina la ‘Jeneza Linalotembea’.

0
0
Kwa muda wa wiki moja sasa, vyombo vya habari nchini vimekuwa vikiripoti hali mbaya kiusalama inayoikabili meli kongwe nchini, MV Victoria ambayo imekuwa ikisafirisha abiria na mizigo katika Ziwa Victoria kwa zaidi ya miaka 50 sasa. Tunaungana na vyombo hivyo vya habari kupaza sauti na kuihadharisha Serikali kuhusu janga la kitaifa linaloweza kutokea muda wowote kuanzia sasa, kutokana na meli hiyo kuzeeka kiasi cha kupata hitilafu mara kwa mara na kuhatarisha maisha ya abiria.

Hali hiyo inatokana na tukio la usiku wa kuamkia Jumamosi ya wiki iliyopita, ambapo abiria 381 waliokuwa katika meli hiyo ikiwa safarini kutoka Bukoba kwenda Mwanza walinusurika kifo. Habari zinasema meli hiyo ilipata hitilafu katika usukani na baadaye injini zake kuzimika zaidi ya mara mbili kabla ya kujikongoja hadi Bandari iliyo karibu ya Kemondo. Kwa muda mrefu sasa, zimekuwapo habari za matukio mengi ya kutisha ambapo meli hiyo imekuwa ikipata hitilafu ikiwa safarini kati ya Mwanza na Bukoba, kiasi cha kupewa jina la ‘jeneza linalotembea’.

Tunaambiwa abiria wanasafiri kwa hofu kubwa, huku roho zao zikiwa mikononi, kutokana na matatizo ya kiufundi yanayosababisha meli hiyo kuchelewa kufika bandari za Mwanza na Bukoba tofauti na ilivyokuwa zamani. Abiria wamekuwa wakiandamwa na matukio mengi yanayoleta hofu na kuashiria meli hiyo inaweza kuzama wakati wowote.

Tukio la mwaka 1996, ambapo MV Bukoba ilizama na kuua abiria zaidi ya 1,000 katika ziwa hilo halijasahaulika kwa wananchi wa Kanda ya Ziwa, ambao hivi sasa wanahoji iko wapi meli mpya waliyoahidiwa na Rais Benjamin Mkapa baada ya kutokea ajali ile. Vilevile, wanahoji wapi ilipo meli mpya waliyoahidiwa na Rais Jakaya Kikwete wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, hasa wanapotilia maanani kwamba amebakiwa na mwaka mmoja tu wa kuwa madarakani.

Kama Siyo Milion 58 Simba Ingefungwa Bao Tatu na Yanga

0
0
MATAJIRI wa Simba wamefurahishwa na matokeo ya suluhu waliyopata dhidi ya Yanga na kusema bila kambi yao ya nchini Afrika Kusini wangeweza kufungwa si chini ya mabao 3-0 na Yanga.

Kabla ya matokeo hayo ya juzi Jumamosi pale Uwanja wa Taifa, Simba ilikuwa Afrika Kusini ambako iliweka kambi ya siku nane kujiandaa na mchezo huo wa Ligi Kuu Bara ambao ulimalizika suluhu.

Akizungumza na Mwanaspoti, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Kassim Dewji ‘KD’, alisema kikosi chao  kilikuwa katika hali mbaya ya kuweza kupoteza vibaya mechi dhidi ya Yanga na wasingefanya jitihada hizo wangejikuta wanapata kipigo cha aibu.

Dewji ambaye ndiye aliyekuwa mmoja wa waratibu wa kambi hiyo, alisema Yanga kabla ya mchezo huo walikuwa katika morali nzuri kuliko Simba. Alisema kambi na gharama mbalimbali walizoziingia zimewagharimu zaidi ya Dola 350,000 ambazo ni sawa na Sh58 milioni.

“Hatukuwa katika hali nzuri, tulilazimika kutumia akili hiyo ya haraka kuinusuru klabu kupata kipigo cha aibu maana tuliangalia timu yetu kulinganisha na Yanga na kubaini endapo tusingeandaa ile kambi tungeweza kupata kipigo cha aibu cha si chini ya bao 3-0,”alisema Dewji.

Matokeo hayo yamewakera mabosi wa Yanga waliokuwa wanataka ushindi kuziba kelele za Simba huku wachezaji kilio chao ni kukosa Sh80 milioni walizoahidiwa endapo wangeshinda huku Simba nao wakikosa Sh100 milioni ambazo wangepewa kama wangeishinda Yanga.

“Tulipambana sana hasa sisi mabeki, lakini tatizo lilikuwa mbele katika umaliziaji tu, tulikuwa tunalala na fedha uongozi ulituletea Sh80 milioni taslimu na ukatuhoji nani akabidhiwe lakini ndiyo hivyo tumechemsha,” alisema kwa huzuni beki mmoja wa Yanga.
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images