Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Rais wa Liberia Kaamua Kumpa Tuzo Arsene WengerA

$
0
0
Rais wa Liberia Kaamua Kumpa Tuzo Arsene WengerA
Rais wa Liberia George Weah Jumanne ya August 21 2018 ameripotiwa kuwa ameandaa tuzo kwa kocha wa zamani wa club ya Arsenal ya England Mr Arsene Wenger.

George Weah amemualika kocha Arsene Wenger, Liberia katika jiji la Monrovia kwa ajili ya kumpa tuzo ya heshima kwani ni kocha ambaye amefanikisha yeye kufikia mafanikio aliyonayo sasa hivyo anaamini anastahili tuzo ya heshima.

Kama ufahamu George Weah ambaye ni Rais wa Liberia kwa sasa amewahi kufundishwa soka na kocha Arsene Wenger mwaka 1998 wakati alipomsajili katika club ya Monaco ya Ufaransa.

Weah ambaye anashikilia rekodi ya kuwa mchezaji pekee wa Afrika kuwahi kushinda tuzo ya mchezaji bora wa Dunia 1998, alistaafu soka mwaka 2003 na kuingia rasmi katika siasa, hivyo Ijumaa hii nchini Liberia, Wenger atakuwepo kukabidhiwa tuzo ya heshima.

"Wachungaji Muache Unafiki"- Nabii Daniel

$
0
0
"Wachungaji muache unafiki"- Nabii Daniel
Nabii Daniel Shilla ambaye amejipatia umaarufu mkubwa mtandaoni kwa kugawa pesa kwa waumini wake na watu mbalimbali, amesema sababu kubwa ya yeye kuwa karibu na wasanii wa filamu nchini ni kutaka kuwaweka karibu na Yesu huku akiwaponda wachungaji wengine kuwa waache unafiki.

Nabii Daniel amefunguka hayo alipokuwa anazungumza kwenye kipindi cha eNewz kinachorushwa na EATV, baada ya yeye kuonekana eneo la Mliman City jijini Dar es Salaam kwenye uzinduzi wa filamu mpya ya Duma inayoitwa nipe changu.

"Ili mimi niwakamate watu wa bongo movie na niwalete kwa Yesu ni lazima nikae nao karibu, siwezi nikaa nao mbali halafu nitegemee kuwavuta. Mimi Duma ni mtu ambaye nimemsaidia sana katika kazi zake za sana", amesema Nabii Daniel.

Pamoja na hayo, Nabii Daniel ameendelea kwa kusema "kuangalia filamu sio dhambi tena kuna wachungaji hao walokole wengine ni wanafiki wanaangalia nyumbani ila mimi nimeamua kuangalia 'live".

Mbali na hilo, Nabii Daniel amesema lengo kubwa ya yeye kujichanganya kwa watu mbalimbali ni kutaka kutangaza neno la Mungu, kwa kuwa hata Yesu alivyoshuka duniani alitembelea makundi mbalimbali na kujiweka kwa kila mmoja wao na kutangaza neno.

Sina Mpango Wa Kuoa- Dully Sykes

$
0
0
Sina Mpango Wa Kuoa- Dully Sykes
Msanii mkongwe wa Bongo fleva Dully Sykes amefunguka na kuacha watu vinywa wazi baada ya kuweka wazi kuwa hana mpango wa kufunga ndoa pamoja na kuwa na watoto kadhaa.

Kauli hiyo iliyotolewa na Dully iliwashangaza mashabiki zake kwani ilitolewa mbele ya kadamnasi ya mashabiki.

Dully alifunguka suala hilo wakati akiwa jukwaani akikamua kwenye Tamasha la Komaa, lililofanyika kwenye Viwanja vya Tanganyika Packers, ambapo akiwa katikati ya shoo alisema kwa nguvu.

Baada ya kauli hiyo swangwe ziliibuka kila kona na baadhi ya mashabiki walianza kuzungumza chini kwa chini juu ya kauli hiyo kwamba huenda Dully hana mpango wa kuoa kweli ndiyo maana kasema juu ya kauli hiyo.

Dully amekuwa akiulizwa kuhusu kufunga ndoa kwa miaka mingi sasa ambapo amekuwa akidai muda ukifika ataoa lakini mpaka leo bado hajaoa licha ya kuwa na watoto kadhaa.

Mbowe na Vigogo Wengine CHADEMA Wawekewa Pingamizi

$
0
0
Mbowe na Vigogo Wengine CHADEMA Wawekewa Pingamizi
Jamhuri imepinga maombi ya vigogo tisa wa Chadema, akiwamo Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, ya kutaka kesi inayowakabili iahirishwe hadi rufaa isikilizwe na kutolewa uamuzi kwa madai kwamba maombi hayo hayana msingi kisheria.

Hoja hizo za Jamhuri ziliwasilishwa jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri anayesikiliza kesi hiyo.

Wakili wa Serikali Mkuu, Faraja Nchimbi, aliomba mahakama hiyo iyatupilie mbali maombi hayo.

Mbowe na wenzake wanaiomba mahakama hiyo kuahirisha kesi ya jinai inayowakabili mahakamani hapo, kusubiri usikilizwaji na uamuzi wa rufani waliyowasilisha Mahakama ya Rufani Tanzania.

Mbowe na wenzake waliwasilisha maombi hayo kupitia wakili wao Peter Kibatala, wakiomba mahakama hiyo kuahirisha kesi hadi hapo Mahakama ya Rufani itakaposikiliza na kutolea uamuzi rufani watakayowasilisha  kupinga uamuzi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam wa kutupilia mbali maombi hao ya marejeo.

Pia, vigogo hao wamewasilisha maombi Mahakama ya Rufani wakiomba kusimamishwa kwa mwenendo wa kesi hiyo hadi rufani yao itakaposikilizwa na kutolewa uamuzi.

Nchimbi alidai wanapinga vikali hoja za waleta maombi (Mbowe na wenzake) kwa kuwa maombi yanakosa baraka za kisheria au yanakosa miguu ya kisheria ya kusimamia mbele ya mahakama.

Alidai maombi hayo hayana kitu kipya kwa kuwa mahakama hiyo ilishatoa uamuzi mdogo kutokana na maombi yaliyokuwa yamewasilishwa na Mbowe na wenzake ya kuomba kusitishwa kwa mwenendo wa shauri hilo.

“Hakuna chochote kipya kilichowasilishwa mahakamani kitakachoifanya mahakama hii itoe uamuzi wa kuahirisha mwenendo wa shauri la jinai,” alidai.

Alisema kifungu kilichotumika kuwasilisha maombi hayo na kesi mbili zilizotumiwa na upande wa waleta maombi huwezi kupata kile alichokiomba.

Kuhusu hoja ya hati ya kiapo kinzani, Nchimbi alidai ipo sahihi na kama ingekuwa na upungufu upande wa wajibu maombi wangewasilisha hoja ya kisheria.

Aliomba mahakama hiyo itupilie mbali maombi haya kwa kukosa misingi ya kisheria.

Wakili Kibatala katika maombi ya wateja wake, aliomba mahakama kuahirisha kesi kwa kuwa kuna rufani Mahakama ya Rufani na wamewasilisha maombi ya kusitisha usikilizwaji wa kesi hiyo.

Kibatala alidai wanaomba kuahirisha kesi hiyo ili kusubiri usikilizwaji na uamuzi wa rufani iliyoko Mahakama ya Rufani na maombi ya kusimamishwa kwa mwenendo wa shauri hilo kusubiri uamuzi wa rufani.

Alidai kifungu kilichotumika kuwasilisha maombi hayo kinaipa mamlaka mahakama hiyo kuahirisha usikilizwaji wa shauri la jinai kwa kipindi kisichozidi siku 15 kwa mshtakiwa ama washtakiwa walioko mahabusu na kwa kipindi kisichozidi siku 30 iwapo mshtakiwa ama washtakiwa wapo nje kwa dhamana.

Kibatala alidai mamlaka ya mahakama yapo wazi kabisa katika sheria, lakini pia yalisisitizwa na Mahakama ya Rufani katika mashauri mbalimbali.

“Ukichukua hati ya kiapo ambacho ameapa yeye kuunga mkono maombi hayo na hati ya kiapo kinzani, hakuna ubishi kwamba kuna maombi ya kusimamishwa kwa mwenendo wa shauri hilo yaliyoko Mahakama ya Rufani, hakuna ubishi rufani imeshawasilishwa na kusajiliwa.

“Maombi yaliyoko katika Mahakama ya Rufani yanagusa mwenendo wa kesi na kutokana na mchakato wa rufani ulivyokwenda haraka, tunaamini maombi ya kusitishwa kwa mwenendo wa kesi yatakwenda haraka.

“Mheshimiwa hakimu, tuna mashaka na uhalali wa hati ya kiapo kinzani kilichowasilishwa na upande wa wajibu maombi, hati tuliyopatiwa haina saini mwisho wa maelezo wala tarehe,” alidai Kibatala.

Alidai kutokana na hilo, hakuna hati ya kiapo kinzani iliyowasilishwa mahakamani hapo na kuomba maombi yao yakubaliwe.

Atiwa Mbaroni Kwa Tuhuma za Kumuua Mgoni Wake Aliyemfumania na Mkewe

$
0
0
Atiwa Mbaroni Kwa Tuhuma za Kumuua Mgoni Wake Aliyemfumania na Mkewe
Jeshi la Polisi mkoani Singida linamshikilia Jamal Makere (37) mkazi wa Utemini mjini Singida kwa tuhuma za kumuua mgoni wake, Ramadhan Athuman (27) anayedaiwa kwenda nyumbani kwa mtuhumiwa kwa lengo la kumfuata mkewe kimapenzi.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Sweetbert Njewike alisema tukio hilo ni la juzi kuamkia jana saa 6.00 usiku. Inadaiwa kijana Ramadhan akiamini Jamal hayupo nyumbani kwake, alienda kugonga mlango kwa lengo la kutaka kufanya mapenzi na mke wa Jamal, kwani ilikuwa ni mazoea yao kukutana usiku.

Hata hivyo, kutokana na usemi “Siku za mwizi ni arobaini,” siku hiyo mwenye nyumba alikuwepo na Ramadhan alipogonga mlango Jamal alitoka haraka, akamkuta ‘mwizi’ wake bado anamsubiri hawara (jina limehifadhiwa) kisha wakaanza kupigana hatimaye Ramadhan alielemewa. Kamanda Njewike alisema Ramadhan aliumizwa vibaya na kipigo hicho hivyo alikimbizwa hospitalini.

Hata hivyo juhudi za madaktari, hazikufua dafu na hatimaye aliaga dunia. Uchunguzi wa awali wa Polisi ulibaini kuwa mtu huyo alikuwa na mahusiano na mke wa mtuhumiwa na walikuwa na mazoea ya kukutana mara kwa mara nje ya nyumba ya mtuhumiwa.

Hili ni tukio la pili katika siku zisizozidi tano mkoani hapa, linalotokana na masuala ya mapenzi.

Agosti 15 mwaka huu, wanandoa wawili walipoteza maisha yao katika tukio lililohusishwa na wivu wa mapenzi.

Diamond Kuongeza Jumba Jingine la Kifahari Afrika Kusini

$
0
0
Diamond Kuongeza Jumba Jingine la Kifahari Afrika Kusini
Msanii wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz ameweka wazi kuwa ana mpngo wa kununua nyumba nyingine nchini Afrika Kusini.

Muimbaji huyo anayetamba na ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la Jibebe ametumia Insta Strory kueleza hilo.

"Still in love with my first South Africa house.... adding the new house in here before end of the year," ameeeleza Diamond Platnumz.

Nyumba ya sasa iliyopo Afrika Kusini ndipo inaishi familia yake, yaani mzazi mwenzie Zari The Bosslady na wanae wawili, Tiffah na Nillan.

Muone na Wasiliana na Dr Kanengo Bingwa wa Tiba Asili, Hutibu Magonjwa Haya

$
0
0

NKURURU:-ni dawa inayotibu miguu kuwaka moto, kiuno tumbo     kupooza/kuparalazi  kupoteza  fahamu  MALABALA  hutibu  kisukari , uti  wa  mgogo,  Change, pumu, busha, kaswende, kifua  kikuu, muwasho  sehemu  ya siri

POWER :-ni dawa ya kuongeza nguvu za kiume ni vidonge  20

MPERAMPERA:- ni dawa ya kurudisha Mke, mme, mpenzi,mchumba aliyekuacha /kuteseka, ni kwa mda wa siku 2 tu kusafisha, pia kunakuna dawa za kupunguza vitambi(nyama uzembe),  maziwa makubwa,michirizi, mikovu makubwa, chunusi sugu.

SIX POWER:-inatibu upungufu wa nguvu za kiume kwa wasio weza kumudu tendo la ndoa itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 4 bila hamu Keisha, inaboresha maumbile madogo na inaimarisha misuri iliyo regea na kusinyaa una pona kabisa, ndani ya siku 4 tu

GASELA:-ni dawa ya maajabu (9) yaliyoshindikana.    (1)-Kisukari, vidonda vya tumbo, tezi dume,walioshindikanika kupata watoto(ugumba),busha bila oparesheni, (2)zindiko Kali Katika biashara yako (chuma ulete)  ndo kiboko yao kumkamata mwizi aliye kuibia vitu vyako pikipiki, gari, n, k( 2)zindiko la nyumba, mashamba, viwanja,. ( 3 ) kurudisha mtu aliye kufa kiutatanishi (msukule) (4)kukutolea sumu uliyo ikanyaga (Mtego) (5)ujiamini kutumia dawa ya maajabu Saba (6)kutoa mikafara mfano ugomvi ndani ya nyumba kufukuzwa kazini bila sababu (7)kutabiri nyota na kung'arisha (8)kurudisha Mali iliyo potea mazingira ya kutatanisha, kushinda kesi uliyo sumbuka nayo mda mrefu. (9)kufukuza majini wa  chafu ndani ya mji,.Haya yote yana wezekana kwa DR KANENGO popote ulipo ukiniitaji nafika napatikana buguruni chama, mbagala zakhiem karibia na uwanja wa mkutano, na wilaya ya bunda musoma : mawasiliano  ni simu namba :-0767-17-17-73 na  0716-60-89-59

NI  KWA  WALIO  TUMIA  DAWA  ZA MATATIZO  MBALIMBLI  BILA  MAFANIKIO   uwezo  WA  kurudisha  mali  iliyopotea  au  kudhulumiwa    muda  mfupi  tu,  Na natoa  dawa  ya  utajiri  kwa  wafanya  biashara     wachimbaji  madini, wafaryakazi,  wakulima, wafugaji na  kwa yeyote  anayetaka  kuwa  na  pesa   nyingi  katika   maisha  yake,  Na  pia  anaunganisha  utajiri    kwa muda  mfupi  sana  pamoja  na  kuboresha  akili  kwa  wanafunzi  na  kumfanya  afaulu  mitihani  yote  au  intaview  yeyote  na  ana  uwezo  mkubwa  wa  kutibu  ugonjwa  wa  Uvimbe tumboni .  pia anarudisha  Mke, mme, mchumba,    hawara, kwa  muda  wa  saa  3  na  anatimiza mahitaji  yote  hata  kama  upo  mbali   kiasi  gani,  ahadi  zote  atatimiza  kwa  muda  mfupi  tu  Na  kumfunga  asiwe  na mtu  mwingine  kwa  nini  unaumiza  kichwa ?

Muone  ( DR  )KANENGO,anatibu  nguvu  za  kiume  anarefusha  na  kunenepesha  uume  kwa  saizi  uipendayo  kwa  muda  mfupi   sana, pamoja  na  kuwa  na  hamu  ya  kurudia  tendo  la  ndoa  mara  4  bila  hamu  kuisha   Na  utachelewa   kufika  kileleni  kwa  muda  wa  dakika   40  bila  kuchoka  hata  kama  una umri  mkubwa  kiasi  gani   Gerentii  miaka /=60    ukisha  pona  bila tatizo   kurudia  pia ana  uwezo  mkubwa  wa  kuongeza  hips na  makalio,  pia   anatibu  magonjwa  sugu  ya  zinaa  tumbo  kujaa  gesi,  kuuma  chini  ya  kitovu,vidonda vya tumbo,   kiuno,  miguu    kuwaka  moto  miguu,  kuvimba..Nk..Angalizo usitume meseji wala kubipu..
You can get it in   all East African countries, our service is fast and easy...

Contact Whatsapp 0767171773.Dar es salaam Tanzania. ..Dr. KANENGO 0716608959...You are welcome.

TFF Yawapiga Marufuku Simba Kumtumia Mzambia

$
0
0
TFF Yawapiga Marufuku Simba Kumtumia Mzambia
WAKATI leo Jumatano Simba ikianza kufungua pazia la Ligi Kuu Bara kwa kucheza na Tanzania Prisons, kikosi hicho kitamkosa kiungo wake fundi Claytous Chama raia wa Zambia, kutokana na kuendelea kukosa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) ambayo imechelewa kutoka kwa timu yake ya zamani ya Power Dynamos ya Zambia na hivyo TFF kuwaambia Simba wasimtumie.



Hii itakua mechi ya pili ya kimashindano ambayo kiungo huyo ataikosa kutokana na kukosa ITC baada ya wikiendi iliyopita kuwa nje kwenye pambano la Ngao ya Jamii dhidi ya Mtibwa.



Chanzo kutoka ndani ya Simba kimelidokeza Championi Jumatano kuwa kiungo huyo sambamba na mlinda mlango wao, Deogratius Munishi ‘Dida’, hawatakuwa sehemu ya mchezo kutokana na kukosa vibali vya kucheza, jambo ambalo limechangiwa zaidi na masuala ya kimtandao ambapo usajili wote umekuwa ukifanywa huko.

“Ishu ya Chama bado mambo ni magumu kwa sababu hadi leo (juzi) hatukuwa tumepata lolote juu ya kibali hicho na kusababisha kocha kumuondoa kwenye hesabu za watakaocheza dhidi ya Prisons.



“Suala lake limekuwa na mkwamo kwa sababu ya masuala ya kimtandao ambapo kila kitu kuhusiana na usajili kwa sasa kinafanywa huko, hivyo ndiyo maana mpaka sasa hakujapatikana nafasi ya yeye kupata kibali lakini sio yeye tu, hata golikipa wetu Dida naye bado hajapata kibali kitakachomruhusu kucheza mechi hii,” kilisema chanzo hicho.



Championi lilimtafuta Mratibu wa Simba, Abbas Ally ambapo alisema: “ITC zao bado hazijaja lakini tunaendelea kufuatilia, hilo ni suala la ‘system’, ndiyo maana unaona hadi sasa hawajapata, tunaendelea kufuatilia kwa karibu na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).”



Pia Championi Jumatano lilimuuliza Chama juu ya hali hiyo ambapo alisema: “Hakuna tatizo la kukaa nje, kama hunioni kwenye mechi jua kila kitu kinafuatiliwa na uongozi.”



Msemaji wa Simba, Haji Manara, amesema jana kuwa Fifa wamewaandikia barua Chama cha Soka cha Zambia kuhakikisha kuwa hadi kufikia leo Jumatano ITC ya Chama iwe imefika.

“Wamesema kama haitakuwa hivyo, watashughulika nao,”


Bobi Wine Aiajiri Kampuni ya Mawakili Kutoka Marekani Kumuakilisha Kwenye Kesi

$
0
0
Bobi Wine aiajiri kampuni ya mawakili kutoka Marekani kumuakilisha kwenye kesi
Mbunge asiye na chama nchini Uganda Bobi Wine ambaye anazuiliwa kwa mashtaka ya kumiliki silaha kinyume cha sheria ameiajiri kampuni ya mawakili ya Marekani kumwakilisha kwenye kesi, kwa mujibu wa wakili Robert Amsterdam.

Bw Amsterdam anasema kukamatwa mteja wake kumechochewa kisiasa na ni kitendo cha dhuluma na kuongeza kuwa ameteswa akiwa kizuizini.

Jeshi ambalo ndilo linamzuia Wine linasema kuwa hajateswa na Rais Yoweri Museveni ametupilia mbali madai hayo na kuzitaja kuwa bahari za uongo.

Amezuiliwa tangu wiki iliyopita pamoja na wabunge wengine kadhaaa. Walikuwa kwenye kampeni kali eneo la Arua kaskazini mwa nchi. Wine anaratarajiwa kufikishwa mahakamani siku ya Alhamisi.

Amsterdam anasema kuwa Marekani inastahili kuwawekea vikwazo maafisa wa Uganda akiongeza kuwa ni lazima wafahamu kuwa kuna majibu kwa ukiukaji huu wa haki za binadamu.

Sheria za Marekani zinazofahamika kama Magnitsky zinaruhussu bunge la Congress kuwawekea vikwazo wale wanaokiuka haki za binadamu popote pale duniani.

Polisi Kupambana na Walevi Siokukuu ya EID

$
0
0
Polisi Kupambana na Walevi  Siokukuu ya EID
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Murilo Jumanne Murilo amewaonya madereva kuacha kutumia vilevi huku wakiendesha vyombo vya moto kwa kutumia kigezo cha Sikukuu.


Murilo ametoa onyo hilo kwenye mahojiano na East Africa Breakfast ya East Africa Radio ambapo amesema kuwa Sikukuu zipo siku zote na zisitumike kama kigezo cha kufanya anasa zinazopelekea madhara kwa jamii, kama vile kutumia vilevi kupitiliza na kuacha watoto kutoka majumbani bila uangalizi.

“Sikukuu haimaanishi kwamba ndio mtumie pombe halafu muendeshe vyombo vya moto, haimaanishi mtoke majumbani wote ili mtoe mianya kwa wezi kuingia majumbani, au ndio kigezo cha kuwaacha watoto watoke peke yao, hii sio maana ya Sikukuu kwani vitu vingine sio vya lazima”, amesema Kamanda Murilo.

Kamanda Muliro amesema kuwa hakuna vituo vya Polisi vitakavyofungwa sababu ni Sikukuu bali viko wazi muda wote na atakayevunja sheria atakamatwa na kufikishwa mahakamani siku za kazi kama kawaida.

Takwimu za Jeshi la Polisi zinaonesha kuwa matukio mengi ya ajali zinazotokea siku za Sikukuu husababishwa na uzembe wa madereva kwa kisingizio kuwa ni siku ya kusherehekea na kunywa pombe.

Serena Williams Ndiye Mwanaspoti Mwanamke Mwenye Kipato cha Juu Zaidi

$
0
0
Serena Williams Ndiye Mwanaspoti Mwanamke Mwenye Kipato cha Juu Zaidi
Nane kati na wanaspoti 10 wa kike matajiri zaidi ni wa tenisi, huku bingwa mara 23 wa Grand Slam Serena Williama akichukua nafasiu ya kwanza kwenye Forbes.

Williams alilipwa dola 62,000 mwaka uliopita baada ya kuwa nje kwa miezi 14 kujifungua lakini alijizolea dola milioni 18 kutoka kwa matangazo ya biashara.

Mchezaji wa Badminton PV Sindhu na mwendesha magari Danica Patrick ndio wanaspoti wasio wachezaji tenisi walio katika orodha ya kumi bora.

Mwezi Juni Forbes iliwaorodhesha wanaspoti 100 wenye kipato cha juu zaidi lakini hakukuwa na mwanamke kwenye orodha hiyo baada ya Williama kukosa kuorodheshwa.

Mwanamasumbwi Mmarekani Floyd Mayweather alichukua nambari moja akifuatwana mchezaji soka Lionel Messi na Cristiano Ronaldo.

Mapato ya Williams yanamweka nafasi ya kwanza kwa mwaka wa tatu mfululizo.

Caroline Wozniacki yuko nafasi ya pili baada ya kushinda ubingwa wa Grand Slam kwenye mashindano wa Australia Open, ushindi uliompa dola milioni 3.1 na kuongeza kipato chake hadi pauni milioni 13.

Rais wa Urusi Sharapova alikuwa mwanaspoti wa kike aliyekuwa na kipato cha juu zaidi kwa miaka 11 mfululizo lakini kipato chake kimeshuka kufuatia marufuku ya miezi 15.

Dc Jerry Muro Amkaribisha Mkurugenzi Mpya wa Meru

$
0
0
Dc jerry muro amkaribisha mkurugenzi mpya wa Meru
Mkuu wa Wilaya ya Meru Jerry Muro amemkaribisha Mkurugenzi Mpya wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Emmanuel Mkongo.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Nd. Emmanuel Mkongo aripoti rasmi kwenye Halmashauri hiyo tayari kuanza uteelezaji wa majukumu yake.

Mkurugenzi Mkongo amewasili ofisini  baada ya kuteuliwa na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 13 Agosti 2017 .

Mkurugenzi Mkongo amepokelewa na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Jerry Muro pamoja na kaimu Mkurugenzi ambaye ni mkuu wa idara ya utawala na rasilimali watu Grace Mbilinyi
Mkurugenzi Mkongo wakati wa kikao cha kufahamiana na wakuu wa idara na vitengo ,aliweka bayana dira ya uongozi wake ni kuisimamia vyema Halmashauri hiyo kwa mujibu wa sheria na kujikita kwenye ukusanyaji wa mapato yatakayotumika kuiendesha Halmashauri hiyo na kuleta maendeleo kwa wananchi.

Mkongo amewaasa wakuu hao wa idara na vitengo kufanya kazi kwa ushirikiano na kutekeleza majukumu yao ipasavyo pamoja na kuwasimamia vyema watumishi walio chini yao sambamba na kuzingatia taaluma zao kutoa ushauri utakaoleta tija katika Halmashauri hiyo .“sitegemei kupewa taarifa isiyo sahihi na afisa wa Halmashauri hii” amesisitiza Mkongo.

Akizungumza kwa niaba ya wakuu wa idara na Vitengo Afisa elimu wa Sekondari, Mwl. Damari Mchome amempongeza Mkurugenzi Mkongo kwa kuteuliwa, pia ameeleza wapo tayari kumpa ushirikiano .

Kabla ya uteuzi wa Mkurugenzi Emmanuel Mkongo Halmashauri ya Wilaya ya Meru ilikuwa inaongozwa na aliyekuwa Mkurugenzi Ndg. Christopher Kazeri.

Mwanasheria wa Rais TRUMP Afikishwa Mahakamani

$
0
0
Mwanasheria wa TRUMP afikishwa mahakamani
Mwanasheria wa zamani wa raisi Donald Trump amefikishwa mahakamani na kukutwa na hatia ya matumizi mabaya ya fedha za umma na uvunjifu wa sheria za uchaguzi katika mahamakamya New York, ambapo hivi karibuni alikiri kuhusika na miamala ya fedha kwa mcheza filamu za ngono aliyekuwa na uhusiano na raisi ili kumziba mdomo.

Michael Cohen amekata rufaa katika mahakama ya Manhattan dhid ya madai juu yake kwamba alikiuka sheria za uchaguzi, na kudai kuwa alifanya hivyo kwa uongozi wa "mgombea", kwa lengo la kupisha uchaguzi salama.

Michael Cohen alikuwa chini ya uchunguzi maalum kutokana na tuhumza zilizokuwa zinamkabili za kuweko uwezekano wa udanganyifu dhidi yake juu ya masuala ya benki na ushuru.

Mamlaka ya shirikisho la Marekani lilikamata hati kutoka katika ofisi ya Cohen mnamo mwezi Aprili mwaka huu,kufuatia uchunguzi uliohumsisha mshauri maalumu Robert Mueller.

Anahusishwa na tuhuma za Urusi kuingilia uchaguzi wa na nafasi ya uraisi na ambao mpaka sasa umewagusa watu wapatao thelathini .

Uchunguzi huo mpaka sasa ume kwisha baini makosa matano, chanzo cha madai hayo hakijajulikana dhahiri mpaka sasa na hii haina maana kwamba bwana Cohen anakwenda kinyume na raisi Donald Trump.

Katika kipindi cha miaka kumi ya utumishi wake kama mwanasheia wa raisi, Cohen anatuhumiwa kuandaa malipo kwa mwigizaji wa senema za ngono , Stormy Daniels, mnamo mwaka 2016.

Mnamo mwezi wa tano mwaka huu, raisi wa Marekani alikiri kumpa pesa Cohen za malipo ya kutaka kumnyamazisha mwigizaji Stormy Daniels kuhusiana na suala la kuwa na mahusiana na mlimbwende huyo siku kadhaa kabla ya uchaguzi mkuu nchini humo.

Ingawa siku za hivi karibuni raisi Trump amekana kufahamu muamala wa malipo ya dola za kimarekani laki moja na selathini kama sehemu ya malipo ambayo hayajabainishwa.

Mwezi uliopita imefahamika pia kuwa bwana Cohen alimrekodi kwa siri raisi, wakati walipokuwa wakijadiliana ununuzi wa haki za umiliki mcheza filamu za ngono wa kulipwa mlimbwende Karen McDougal ikiwemo hadithi yake kutoka kwa kampuni dada la jarida la kitaifa la Enquirer.McDougal aliuza taarifa zake kwa jarida hilo wakati wa kampeni za uraisi.

Malipo yafanywayo kwa siri kwa niaba ya mwanasiasa ama mgombea yeyote yanaweza kuchukuliwa kama ukiukwaji wa sheria za kampeni za nchini Marekani.

Mwanasheria wa msanii huyo ambaye kwa pamoja anawashtaki raisi Trump na Cohen ameandika katika ukurasa wake wa twitter kuwa maamuzi ya leo yanaweza kumsaidi kushinda kesi yake dhidi ya raisi Trump.

Kama ilivyo ada ya raisi Trump, kutoa matamko kupitia ukurasa wake wa twitter, mpaka sasa hajaandika chochote kuhusiana suala hilo, ambaye kwa sasa yuko West Virginia. Kwenye ratiba zake za mikutano ya kisiasa,

Katika kesi ingine ya pili, iliyokuwa ikiendelea mjini Virginia, mahakama imemkuta na hatia ya mashtaka kumi na nane kutokana na udanganyifu wa kodi na masuala ya ki benki kampeni meneja wa raisi Donald Trump, Paul Manafort.

Lakini pia mahakama hiyo haijaafiki makubaliano juu ya mashtaka mengine kumi ambayo hakimu ametangaza wazi kuwa mbaya.

Bwana Manfort kwa muujibu wa tuhuma zinazomkabili anaweza kukabiliwa na kifungo cha muda mrefu gerezani.Rais Donald Trump ameonesha kusikitishwa kwake kutokana na hukumu hiyo lakini uchunguzi uliofanyika ni kama ulikuwa unamtafuta mchawi.

Raisi Trump alitoa kauli hiyo wakati alipokuwa anazungumza na katika mkutano wa hadhara huko West Virginia.Akiwa mjini humo rais amewaambia waandishi habari wazi kuwa anajisikia vibaya kutokana na yanayomkuta Paul, na kwamba kesi hiyo haina uhusiano wowote na kile kinachodaiwa udukuzi wa Urusi. Mwishoni mwa wiki iliyopita alimsifu Paul Manfort kuwa ni mtu mzuri na kwamba wanachomtendea inasikitisha na mwanzoni mwa wiki hii aliishutumu timu ya Robert Muller kwa kufurahia uangamizaji wa maisha ya watu na kuwaita wanaoaibisha taifa.

Mahakama pia imetoa muda mpaka tarehe 29 mwezi huu ili kujiridhisha ikiwa hakuna sababu ya kufungua mashtaka mapya dhidi ya uamuzi iliyoutoa.

Harmonize Ajibu Tuhuma za TID Kuhusu Kukopi Muziki wa Nigeria ''Hakunilenga Mimi Anitaje ili Asiingie Matatizoni na Wasanii W'engine

$
0
0
Harmonize Ajibu Tuhuma za TID Kuhusu Kukopi Muziki wa Nigeria  ''Hakunilenga Mimi Anitaje ili Asiingie Matatizoni na Wasanii W''engine
Msanii wa muziki Bongo, Harmonize amejibu tuhuma zilizotolewa na TID kuwa amekuwa akiinga muziki wa Kinigeria na kusahau Bongo Fleva.

Muimbaji huyo kutokea WCB akipiga stori na Wasafi TV amesema TID hakuwa ana mlenga yeye bali kuna watu alikuwa anataka kuwafikishia ujumbe huo.

"Mimi nafikiri TID ni kaka kabisa, ana namba yangu na nina yake pia, nadhani hakuwa ananilenga mimi kwa sababu angekuwa ana nilenga mimi  alikuwa ana uwezo wa kunipigia na kuniambia mdogo wangu hii haipo sahihi, usiimbe hivi," amesema.

"Naamini kuna watu alikuwa anawalenga lakini ili asiingie matatizoni na wasanii wengine akaona acha nipitie njia ya mdogo wangu Harmonize," amesema Harmonize.

Harmonize kwa sasa anafanya vizuri na wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la Atarudi.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa sulutani Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa sulutani Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na issa sulutani Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Issa sulutani Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi +255 622588038au 0679119679 au +255 764318107

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...


Mke wa rais wa Marekani, Melania Trump Aamua Kuja Africa

$
0
0

Mke wa rais Donald Trump wa Marekani, Melania Trump, atazuru bara la Afrika baadaye mwaka huu. Hata hivyo, kwa mujibu wa shirika la habari la AFP, ratiba rasmi ya ziara hiyo haikutolewa mara moja.

Hii itakuwa mara ya kwanza kwa Bi Trump kuzuru bara hilo.

Katika taarifa iliyotolewa na afisi ya Bi Trump, mke huyo wa rais anatazamia kujifunza kuhusu changamoto zinazowakabili watoto wa bara hilo.

“Ni wazo la kusisimua kwamba nitazuru Afrika na kujifunza kuhusu masuala ya watoto tamaduni na historia za bara hilo.”

Rais Donald Trump hajazuru bara hilo tangu aingie madarakani na ameshutumiwa kwamba alitoa maneno ya matusi mapema mwaka huu, yaliyoelekezwa kwa nchi za bara hilo.

Melania Trump hata hivyo amesema kwamba anaamini utengamano duniani ni muhimu na kwamba mazungumzo kati ya jamii mbalimbali yana manufaa makubwa kwani “yanachangia katika mchakato wa kujifunza kutoka kwa jamii mbalimbali.”

Msemaji wa Bi Trump, Stephanie Grisham, amesema kwamba White House itatoa ratiba rasmi na orodha ya nchi atakazotembelea katika wiki chache zijazo

Ni sakata la mwanaume, Wema Sepetu aomba kupumzishwa

$
0
0

Miss Tanzania na Muigizaji Wema Sepetuameonekana kukwazika na kinachoendelea kwenye mitandao ya kijamii kuhusiana na kile kinachodaiwa kuwa ame-comment kwenye page ya kijana aitwaye Rock Charles katika ukurasa wa instagram

Kupitia instagram account ya Rock Charlesaliandika caption inayosema imekuwa muda mrefu Tanzania, nakuja kumuona mke wangu mtarajiwa Wema Sepetu ” na baadae Wema Sepetu alionekana kujibu kwa kusema “karibu Mume”

Kupitia ukurasa wa instagram wa Wema Sepetuameweka wazi kuhusiana na hilo na kusema hamfahamu huyo kijana na kusema kuwa amechokwa kuandamwa ma kutukanwa kwenye mitandao ya kijamii na comment hiyo imetengenezwa hajahusika chochote na hicho.

“Aslaam Aleykum Hii kitu imekuwa ikisambaa sana and I know nothing about it… Natumiwa na watu wa karibu nabaki natoa macho… Jana nimeona ya kwanza nd I jus decided kupost those flowers na kuandika mnanitafuta Jamani huyo mtu hapo juu kwanza simjui And hizo edits mnazofanya za kuonesha nimecomment sio Mimi…

“Kwa wanaojua Instagram vizuri mtaona kabisa kwamba hio ni EDIT na sio original comment kama ya kawaida inavyokuwa nimesema mara moja na ntasema tena, Msione watu wamekaa kimya mkaanza kuwatafutia vijimambo vya ajabu vya kuzua zua nipumzisheni basi… Maana mmeshanisema mpaka”

“Mmetukana mpaka mmeninanga mpaka nimekaa kimya tu sasa this is a lil bit deep sipendi maneno maneno jamani… Kwani kipi kikubwa nimewakosea mpaka kila siku hamuachi kuniandama… Mbona nimekaa kimya tu na sina habari na mtu lakini kutwaaaa on my Case…. Sipendi jamani kuharibiana vibe za Eid tu SITAKI JAMANI NIACHENI Eid Mubarak my Loves”

Chadema Yaitumia Barua NEC

$
0
0
Chadema Yaitumia Barua  NEC
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeiandikia barua Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kikilalamikia kile kilichotokea Korogwe Vijijini, ambapo mgombea wa ubunge kupitia (CCM), Timotheo Mzava amepita bila kupingwa.


Barua hiyo imeandikwa na Katibu Mkuu wa Chadema, Dkt. Vincent Mashinji imekwenda kwa Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Dkt. Athuman Kihamia na msimamizi wa uchaguzi jimbo la Korogwe Vijijini, Dkt. George Nyaronga.

Dkt. Mashinji ametuma barua hiyo baada ya Dk Nyaronga kumtangaza mgombea wa CCM, Timotheo Mzava kupita bila kupingwa.

Barua imesema kuwa, “Rejea mazungumzo yetu ya simu awali leo (jana) saa 6:03 mchana na ukanirudia saa 06:06 kuhusu msimamizi wa uchaguzi Korogwe kutopokea fomu ya mgombea ubunge kupitia Chadema, Amina Ally Saguti ambaye alikuwapo muda wote leo (jana) kuanzia saa 4:00 asubuhi ofisi ya msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Korogwe Vijijini, jambo ambalo uliahidi kulighulikia,”

Dkt. Mashinji ameongeza kuwa, “Nilikurejea tena saa 09:47 jioni kukujulisha kuwa bado msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Korogwe Vijijini hajapokea fomu za mgombea kupitia Chadema na ukanirejea tena saa 09:55 ukinieleza kuwa unashughulikia”.

Katika barua hiyo, Dkt Mashinji ameendelea kusema, “Katika mazingira hayo, tunaitaka ofisi yako na Tume iingilie kati suala hili kubwa la uvunjifu wa sheria, kanuni na taratibu za uchaguzi ili mchakato urejewe kuruhusu mgombea wetu wa Chadema na wengine waliochukua fomu za uteuzi waweze kurejesha fomu hizo kwa ajili ya uteuzi”.

Akizungumza  msimamizi wa uchaguzi katika jimbo hilo ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Korogwe, Dkt. George Nyaronga amesema mgombea wa CCM ambaye ni Mzava amepita bila kupingwa baada ya muda wa mwisho wa kurejesha fomu leo Agosti 20, 2018 kuwa peke yake.

Jimbo la Korogwe Vijijini limekuwa wazi kufuatia kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Stephen Ngonyani maarufu kama Maji Marefu.

Gali Lililokuwa Linasafirisha Bangi Lapinduka Dereva Asakwa

$
0
0
Gali Lililokuwa Linasafirisha Bangi Lapinduka Dereva Asakwa
JESHI la Polisi mkoani Pwani, linamsaka dereva aliyefahamika kwa jina la Moshi Ramadhan Malinganya, mkazi wa Kisarawe kwa tuhuma za kusafirisha bangi misokoto 193, katika gari alilokuwa akiliendesha.



Kwenye gari hilo pia kumekutwa ndoo ndogo mbili za lita kumi, zenye bangi na kiroba kidogo chenye mbegu za bangi kilo mbili, zilizokuwa zimefichwa kwenye buti.



Akizungumza na waandishi wa habari mjini Kisarawe, Kamanda wa Polisi mkoani Pwani (ACP) Jonathan Shanna, ambaye anasubiri makabidhiano kuhamia Mwanza kikazi, amesema mtuhumiwa ametoroka baada ya gari alilokuwa akiendesha kupinduka wakati akiwakimbia polisi.

Kamanda Shanna ameeleza kuwa tukio hilo lilitokea jana, Agosti 21, majira ya saa 3:30 usiku eneo la shule ya sekondari Minaki, ambapo mtuhumiwa alikuwa anaendesha gari yenye namba za usajili T 801 AAF aina ya Toyota Mark II.

PICHA: Waziri Mkuu Atumia Usafiri Wa Boeng 787-8 Dream Liner Ya. ATCL Kutoka Mwanza Hadi Dar

$
0
0
PICHA: Waziri Mkuu Atumia Usafiri Wa Boeng 787-8 Dream Liner Ya. ATCL Kutoka Mwanza Hadi Dar

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakisafiri kwa Ndege ya Boeing 787-8 Dreamliner wakitoka Mwanza kwenda Dar es salaam kupitia KIA, Agosti 22, 2018.


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakiwa katika picha ya pamoja na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Phillip Mangula (watatu kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella (kulia) kwenye uwanja wa  Ndege wa Mwanza kabla kuondoka kuelekea Dar es salaam kwa ndege ya Boeing 787-8 Dreamliner Agosti 22, 2018.

Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images