Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live

Mzozo wa Kidiplomasia Waibuka Kati ya China, Taiwan na Swaziland

$
0
0
Mzozo wa kidiplomasia waibuka kati ya China, Taiwan na Swaziland
Mzozo wa kidiplomasia unazidi kuibuka kuhusu nchi ndogo iliyo kusini mwa Afrika ya eSwatini ambayo awali ilifahamika kama Swaziland.

Nchi hiyo ndiyo mshirika wa mwisho wa Taiwan aliyesalia barani Afrika.

China ambayo hairuhusu nchi yoyote kuwa na uhusiano wa kiserikali nayo pamoja na Taiwan kwa wakati mmoja imesema inataka eSwatini kuboresha uhusiano kati yake na Beijing.

Taiwan ambayo China inaitaja kuwa mkoa wake, imekuwa ikipoteza washirika wakiwa sasa wamebaki 17 tu. Siku ya Jumanne El Salvador ilikata uhusiano wake na China.

Taiwan iliapa Jumanne kupambana na tabia za China baada ya kupoteza mshirika wake El Salvador kwa China, ambayo ni nchi ya tatu kukata uhusiano wake na Taiwan na kujiunga na China mwaka huu.


"eSwatini haina uhusianoa na China kwa sababu ambazo kila mtu anazifahamu," naibu waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa China Cheng Xiaodong aliliambia shirika la habari la Reuters.

"Tuna matumaini kuwa nchi zote za Afrika huku moja ikiwa imebaki, zitashiriki katika kuwa na uhusiano mzuri kati ya China na Afrika," alisema.

Aika "Tuliwasaidia Kina Rosa Ree, Wildad na Celine ili Watoke Kimuziki"

$
0
0

Baada ya kuwaibua Rosa Ree, Wildad na Seline kwenye kiwanda cha Bongo Fleva kupitia music lebel yao The Industry, Aika amesema kuwa kwa sasa hawatasimamia wasanii kama ilivyokuwa hapo awali na badala yake watatoa msaada tu kwa wasanii wenye vipaji na ukifika muda sahihi watatangaza nia yao ya kurudi tena kuwasimamia.

“Kweli tulifanya hivyo kama kutoa msaada kwa wasanii ambao hawana uwezo wakulipia gharama za studio na sasa hivi tumewaruhusu kila mmoja kufanyakazi zake wenyewe, hatuwezi kuwa-sign wasanii wengine sasa hivi badala yake tutaendelea kutoa msaada kwao ni kitu ambacho hatuwezi kuacha”- alisema @Aikanavykenzo

Member huyo wa kundi la NavyKenzo amesema, kwa sasa wamewekeza muda mwingi kwenye miradi ya kundi lao na ameahidi kurudi kuonekana tena kwenye majukwaa ya muziki sehemu tofauti nchini.

Huyu Ndio Mwanamke Pekee Ambaye Yupo Nyuma ya Mafanikio ya Ali Kiba

$
0
0

Jina lake kamili ni Christine Mosha - ila aliamua kutumia jina la 'Seven' kutokana na kufundishwa kuhusu maajabu ya namba 7 - ikiwemo maajabu 7 ya ulimwengu na dhambi 7 kuu katika dunia. Hivyo anaamini namba saba ni yenye nguvu katika maisha yake.

Alizaliwa jijini Nairobi Kenya na kukulia nchini Tanzania. Maisha yake kwenye kioo yalianza kama mtangazaji wa kituo cha redio cha Clouds FM na baadae mwaka 2009 alitoka na kujiunga na MTV ambapo alihudumu kwa miaka kadhaa kupitia kitengo cha A&R yaani Artiste and Repertoire.

Baadae pia alihudumu katika kampuni kubwa ya muziki duniani Sony kwa muda na kisha baadae kusimamia tawi la Rockstar 4000 kama mkurugenzi wa vipaji na muziki.

Seven ndiye meneja wa kike pekee kwenye game ya Bongo fleva ambapo anasimamia kazi za Ali Kiba pamoja na Ommy Dimpoz kama meneja chini ya Rockstar 4000. Huu ni mwaka wa 7 - Seven anafanya kazi na Kiba, walikutana na mwimbaji huyo katika project ya One 8 wakati huo akiwasimamia wasanii wa Afrika Mashariki.

Ukaribu wao ukaanzia hapo hadi leo amemfanya 'KING Kiba' kuwa miongoni mwa wasanii wakubwa Afrika na dunia - akifanikiwa kutajwa kwenye tuzo kubwa nje na ndani na kushinda baadhi kama: MTV Europe Music Awards, KTMA, Sound City Awards na nyingine nyingi. Pia kufanya colabo na wasanii wakubwa nje na ndani ya nchi.

Huyu ndio Seven Mosha

Ndugu Wasusa Kumzika Aliyefia Mikononi mwa Polisi, Kamanda Afunguka

$
0
0

Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Polisi Tanzania na Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Temeke, Emmanuel Gabriel lukula ameeleza juu ya kifo cha Salum Juma Kindamba mkazi wa Chanika aliyefariki dunia katika hospitali ya Temeke  mara baada ya kupigwa risasi ya kiunoni na mguuni na Polisi.

Kamanda Lukula amezungumza hayo kufuatia suala ambalo limekuwa likiongelewa katika vyombo vya habari mbalimbali juu ya ndugu wa marehemu huyo aliyeuawa mikononi mwa polisi kususa kuuzika mwili huo.

Ambapo ndugu hao wamesusa kuzika mwili huo kutokana na sintofahamu ya mazingira ya kifo cha ndugu yao ambaye alipigwa risasi na jeshi la polisi katika mkoa wa kipolisi Temeke.

Kamanda Lukula amesema kuwa marehemu, Salum Kindamba aliuawa na polisi katika harakati za kukamata majambazi walioripotiwa na Mkuu wa Upelelezi wa Chang’ombe eneo la Kiwalani ambapo iliripotiwa kuwa watu wanne wasiofahamika wamefika katika eneo hilo wakiwa na silaha aina ya Pistol.

Hata hivyo kumekuwapo na taarifa juu ya matukio ya ujambazi katika maeneo tofauti katika mkoa wa kipolisi Jijini Dar es salaam, kufuatia matukio hayo ya ujambazi yaliyoripotiwa Kamanda Mkuu kanda maalumu ya Dar aliamuru kuundwa kikosi kazi cha kudhibiti matukio hayo.

Hivyo mara baada ya kusikia taarifa juu ya majambazi hao katika eneo la kiwalani kikosi kazi kilihamia huko kupambana na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa wanne na mfuko wenye silaha.

Dakika chache mara baada ya kuwatia mbaroni watuhumiwa hao akiwemo, Salum Kindamba alikurupuka na kufanikiwa kutoroka na mfuko ule wenye silaha aina ya pistol, pesa taslimu Sh. milioni 9 na simu aina ya Tecno.

Polisi walifanya jitihada zote kisheria kumtaka kijana huyo asimame bila kudhuliwa jitihada hizo ziligonga mwamba ndipo Polisi walipoamua kumpiga risasi ya kiunoni na  mguuni na kumkamata kijan huyo ambaye baadae alikimbizwa hospitali ya Temeke na kufariki dunia.

Taarifa hiyo imetolewa leo Agosti 22, 2018 kwenye vyombo vya habari kufuatia sintofahamu kwa ndugu wa marehemu ambao walikuwa hawafahamu kiundani juu ya mazingira yaliyopelekea ndugu yao kufikwa na mauti akiwa mikononi mwa polisi.

Walevi kukiona sikukuu ya Eid

$
0
0

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Murilo Jumanne Murilo amewaonya madereva kuacha kutumia vilevi huku wakiendesha vyombo vya moto kwa kutumia kigezo cha Sikukuu. 

Murilo ametoa onyo hilo kwenye mahojiano na East Africa Breakfast ya East Africa Radio ambapo amesema kuwa Sikukuu zipo siku zote na zisitumike kama kigezo cha kufanya anasa zinazopelekea madhara kwa jamii, kama vile kutumia vilevi kupitiliza na kuacha watoto kutoka majumbani bila uangalizi. 

“Sikukuu haimaanishi kwamba ndio mtumie pombe halafu muendeshe vyombo vya moto, haimaanishi mtoke majumbani wote ili mtoe mianya kwa wezi kuingia majumbani, au ndio kigezo cha kuwaacha watoto watoke peke yao, hii sio maana ya Sikukuu kwani vitu vingine sio vya lazima”, amesema Kamanda Murilo. 

Kamanda Muliro amesema kuwa hakuna vituo vya Polisi vitakavyofungwa sababu ni Sikukuu bali viko wazi muda wote na atakayevunja sheria atakamatwa na kufikishwa mahakamani siku za kazi kama kawaida. 

Takwimu za Jeshi la Polisi zinaonesha kuwa matukio mengi ya ajali zinazotokea siku za Sikukuu husababishwa na uzembe wa madereva kwa kisingizio kuwa ni siku ya kusherehekea na kunywa pombe.

Harmonize Ajibu Tuhuma za TID kuhusu kukopi muziki wa Nigeria

$
0
0

Msanii wa muziki Bongo, Harmonize amejibu tuhuma zilizotolewa na TID kuwa amekuwa akiinga muziki wa Kinigeria na kusahau Bongo Fleva.


Muimbaji huyo kutokea WCB akipiga stori na Wasafi TV amesema TID hakuwa ana mlenga yeye bali kuna watu alikuwa anataka kuwafikishia ujumbe huo.


"Mimi nafikiri TID ni kaka kabisa, ana namba yangu na nina yake pia, nadhani hakuwa ananilenga mimi kwa sababu angekuwa ana nilenga mimi  alikuwa ana uwezo wa kunipigia na kuniambia mdogo wangu hii haipo sahihi, usiimbe hivi," amesema.


"Naamini kuna watu alikuwa anawalenga lakini ili asiingie matatizoni na wasanii wengine akaona acha nipitie njia ya mdogo wangu Harmonize," amesema Harmonize.


Harmonize kwa sasa anafanya vizuri na wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la Atarudi.

Beyonce Ashinda Kesi ya Jina Lake Kutumika Kibiashara na Mtu Mwingine

$
0
0

Mwaka jana, Beyonce alihusishwa kuingia kwenye mgogoro wa kisheria na kampuni moja ya mjini Los Angeles ambayo ilijaribu kusajili kibiashara jina la 'Poison Ivy Park' jina ambalo linalandana na chapa ya bidhaa za nguo za Beyonce 'Ivy Park'
-
Sasa taarifa mpya ni kuwa The Queen Bey ameizima kesi hiyo kwa kushinda. Kwa mujibu wa mtandao wa The Blast, Beyonce amefanikiwa kushinda kesi hiyo dhidi ya kampuni (42/72 Inc.) ambayo ipo chini ya jamaa anayeitwa Mike Lin.

Baada ya kumalizika kwa shauri hilo, timu ya Beyonce ilitoa maelezo ya kwanini wameamua kufanya hivyo: Sababu kubwa ni kuondoa mkanganyiko kwa watu kwenye ishu za kibiashara.

Tatua Tatizo la Upungufu wa Nguvu za Kiume au Ukosefu wa Hamu ya Tendo la ndoa

$
0
0

Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume au ukosefu wa hamu ya tendo la ndoa limezidi kuongezeka kwa kasi duniani kote na limekuwa chanzo kikubwa cha ndoa nyingi na mahusiano kukosa uaminifu kutokana na wengi kutoka nje ya ndoa ili kupata mtu atakayemtosheleza na kumfikisha kileleni. Pia udogo wa maumbile ni tatizo kubwa na limekuwa likiwakosesha wanaume wengi uwezo wa kujiamini katika tendo na kusababisha tendo hilo kutokufanyika kwa usahihi. Hili pia huchangia kwa kiasi kikubwa wanawake wengi kwenda nje ya ndoa ( MAHUSIANO) kutafuta mbadala wake.
BAADHI YA DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI KAMA:-
☆Kukosa hamu ya tendo la ndoa
☆Uume kusimama kwa ulegevu
☆Kuwahi kufika kileleni
☆Uume kusinyaa katikati ya tendo
☆Kushindwa kurudia tendo kwa wakati
☆Kuchoka sana baada ya round ya kwanza na hata kukinai kabisa.

Kwa kutumia mimea tiba na matunda bila kemikali sasa
@markson_beauty_pr Tunakuletea suluhisho la matatizo hayo hata kwa wenye "KISUKARI NA PRESSURE" kwa:-
1.HANDSOME UP ORIGINAL:- kifaa chenye uwezo wa 99% kuongeza uume kwa size uipendayo na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @250,000/=
2.SHARK POWER ni gely ya kupaka inayoongeza uume kwa wastani wa inch 5.5 hadi 6 @150,000/=
3.VigRX CREAM:- ni gely iliyoboreshwa mahususi kwa ajili ya kuongeza maumbile kwa wastani wa inch 6.5 hadi 8 na kuimarisha misuli ya uume iliyolegea @200,000/=
4.Vidonge maalum kwa ajili ya kuongeza nguvu na hamu ya tendo la ndoa hata kwa wenye kisukari @150,000/=
5.Spray ya kuchelewesha kufika kileleni na kuweza kurudia tendo ×3. @150,000/=
BIDHAA HIZI HAZINA MADHARA KIAFYA NA ZIMETHIBITISHWA
NA SHIRIKA LA AFYA DUNIANI (WHO).
KWA BIDHAA HIZI NA NYINGINE NYINGI TEMBELEA UKURASA WETU WA INSTAGRAM :-
@markson_beauty_pr
@markson_beauty_pr
@markson_beauty_pr
WEB:www.markbeauty.org
Wasiliana nasi Popote
ulipo duniani kwa (+255)
0767447444 na
0714335378
UTAPATA HUDUMA
NB:Matokeo ni uhakika na garantii na hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii ili kukuhakikishia kufanikiwa kwako.

"Wachungaji Wenzangu Muache Unafiki, Mimi Kuangalia Filamu Mlimani City sio Dhambi" Nabii Daniel

$
0
0

Nabii Daniel Shilla ambaye amejipatia umaarufu mkubwa mtandaoni kwa kugawa pesa kwa waumini wake na watu mbalimbali, amesema sababu kubwa ya yeye kuwa karibu na wasanii wa filamu nchini ni kutaka kuwaweka karibu na Yesu huku akiwaponda wachungaji wengine kuwa waache unafiki.

 Nabii Daniel amefunguka hayo alipokuwa anazungumza kwenye kipindi cha eNewz kinachorushwa na EATV, baada ya yeye kuonekana eneo la Mliman City jijini Dar es Salaam kwenye uzinduzi wa filamu mpya ya Duma inayoitwa nipe changu.

"Ili mimi niwakamate watu wa bongo movie na niwalete kwa Yesu ni lazima nikae nao karibu, siwezi nikaa nao mbali halafu nitegemee kuwavuta. Mimi Duma ni mtu ambaye nimemsaidia sana katika kazi zake za sana", amesema Nabii Daniel.

Pamoja na hayo, Nabii Daniel ameendelea kwa kusema
"kuangalia filamu sio dhambi tena kuna wachungaji hao walokole wengine ni wanafiki wanaangalia nyumbani ila mimi nimeamua kuangalia 'live".

Mbali na hilo, Nabii Daniel amesema lengo kubwa ya yeye kujichanganya kwa watu mbalimbali ni kutaka kutangaza neno la Mungu, kwa kuwa hata Yesu alivyoshuka duniani alitembelea makundi mbalimbali na kujiweka kwa kila mmoja wao na kutangaza neno.

Mtazame hapa chini Nabii Daniel akifunguka zaidi.

PICHA: Waziri Mkuu Atumia Usafiri Wa Boeng 787-8 Dream Liner Ya. ATCL Kutoka Mwanza Hadi Dar

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakisafiri kwa Ndege ya Boeing 787-8 Dreamliner wakitoka Mwanza kwenda Dar es salaam kupitia KIA, Agosti 22, 2018.


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakiwa katika picha ya pamoja na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Phillip Mangula (watatu kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella (kulia) kwenye uwanja wa  Ndege wa Mwanza kabla kuondoka kuelekea Dar es salaam kwa ndege ya Boeing 787-8 Dreamliner Agosti 22, 2018

Ndege Boeing 787-8 Dream Liner ya shirika la ndege la Tanzania (ATCL) ikiwa Juu Ziwa Viktoria Mwanza ikijiandaa kutua katika uwanja wa Mwanza leo 22/Agosti /2018

Fid Q Amaliza utata Baina yake na Joh Makini

$
0
0
Rapa mkongwe Fid Q amefunguka na kuweka wazi kuwa tungo alizozitumia katika nyimbo yake ya kibiriti, hazimuhusu msanii yoyote yule kama baadhi ya watu wanavyofikiria katika vichwa vyao, bali wimbo huo una muhusu yeye kwa asilimia 100.


Fid Q amebainisha hayo alipokuwa anazungumza na Big Chawa ndani ya kipindi cha Planet Bongo kinachorushwa na East Africa Radio, baada ya watu kueneza uvumi kwenye mitandao ya kijamii kuwa wawili hao wana bifu la chini chini na ndio maana Fid ameamua kumuimba.

"Lahasha wimbo wangu wa kibiriti haumuhusu Joh Makini kwa lolote lile bali ni nyimbo ambayo inanihusu mimi asilimia 100, ambapo naongelea watu ambao wamekuwa wakiniponda kuhusiana na kazi zangu za kimuziki. Kwa hiyo nyimbo yangu ni makusanyo ya maneno yao pamoja kashfa mbalimbali zilizokuwa zinanilenga mimi moja kwa moja na wala sijamsema msanii mwenzangu, amesema Fid Q.

Mbali na hilo, Fid Q amedai kinachofanya watu wanamlinganisha yeye na Joh Makini ni kutokana na kazi zao nzuri ambazo zilikuwa za ushindani tokea walipoanza game ya kurapu.

Hii si mara ya kwanza kwa marapa hao wawili kuhisiwa wana bifu baina yao, na hayo yote yanatokona na wao kuwa washindani katika uwanja huo wa kurapu huku wengine wakiwashindanisha kwa vitu

EATV

Irene Uwoya Afungukia Mahusiano Yake na Mama Watoto wa Aslay

$
0
0

Msanii wa Bongo movie na mfanyabiashara maarufu Irene Uwoya amefunguka kuhusu ukaribu alionao na aliyekuwa mpenzi wa Aslay, Tessy Chocolate.

Siku za hivi karibuni Uwoya ameonekana akiwa kribu sana na Mrembo ambaye amezaa na staa wa Bongo fleva Aslay, Tessy na kujionyesha kama ni mashoga kwa sasa.

Kwenye mahojiano na Bongo 5, Ameongelea ukaribu wake na Tessy, Uwoya amepasua kuwa pamoja na kwamba wanaonekana na ukaribu mkubwa lakini wawili hao wakikutana hawana muda wa kuongelea mabwana kama wengi wanavyofikiri:

Ni mtu ambaye tukikutana tunazungumza mambo ya biashara, lakini ishu zake za mapenzi huwaga sizijui, pia ishu kuhusu mahusiano yake ni privacy, huwa nikikutana naye hatuzungumzi masuala ya mapenzi kwa kwa sababu kila mtu ana wake”.

Sijui kwa sasa yupo na nani kwanza hayanihusu kabisa”.

Tessy baada ya kuachana na Aslay amekuwa akisemekana kuwa Kwenye Mahusiano ya Kimapenzi na mfanyabiashara maarufu Kwenye mitandao ya kijamii kama Jembe ni Jembe, taarifa ambazo mwenyewe hajazithibitisha.

Kala Jeremiah Azianika Mbinu za Kushinda Urais..Amtetea Nikki wa Pili na Ndoto yake ya Urais

$
0
0
Ikiwa imepita siku moja tokea rapa Nikki wa Pili kuzua gumzo mitandaoni juu ya ndoto yake ya kuwa na rais wa nchi hii na kupigwa vikali na watu mbalimbali, msanii Kalajeremiah ameibuka na kumshauri mwenzake kuwa asife moyo na maneno ya watu kwani ipo siku atatimiza lengo lake.



Kala Jeremiah ametoa ushauri huo kupitia ukurasa wake wa kijamii wa instagram baada ya Nikki wa Pili kushambuliwa vikali kwa maneno juu ya jambo lake hilo, kwa kile kinachodaiwa kuwa hana sifa ya yeye kugombea nafasi kama hiyo kubwa huku wengine wakisema huenda ni kiki za wimbo wake mpya.

"Watu wengi hawajui maana ya ndoto, kwa hiyo wanamuangalia Nikki wa Pili kwa muonekano wa aliyo kuwa nao sasa, anafanya kazi gani, yuko karibu na nani na nani?. 'So' watu hawa wanakuweka moja kwa moja kwenye urais muda huu. Yani kwao ukisema una ndoto ya kuwa rais tafsiri yao ni kwamba unataka kuwa rais leo. watu hawa watakupinga tu",ameandika Kala Jeremiah.

Pamoja na hayo, Kala Jeremiah ameendelea kwa kusema kuwa
"watu wengi wanaogopa sana kuona mmoja kati yao anaendelea au ataendelea. Ukisema una ndoto ya kuwa rais watu waoga watakupinga sana kabisa maana wanajua mtu akisemacho kinaujaza moyo wake wanaamini utawazidi na hawataki uwazidi, huu uoga watu wengine wanauita wivu ila mimi naita uoga maana wivu ni ule wa kutaka maendeleo kama ya yule. Kwahiyo Nikk usijali kupingwa jali ndoto yako nami naamini itatimia. Weka mikakati songa mbele".

Mbali na hilo, Kala Jeremiah amempongeza rapa mwenzake kwa kuota ndoto kubwa na kudai imani siku zote inasema 'muota ndoto hafi kabla ya ndoto yake kutimia na kama muota ndoto hana imani na ndoto yake aweza kufa kabla ya kuitimiza'.

Mjadala wa kuwa Rais mara zote ukijitoka kutoka kwa watu ambao hawajafikiriwa au kudhaniwa kwa juu ya jambo hilo, siku zote huwa unazua mengi na kupelekea baadhi yao kuvunjika moyo kutokana na maneno ambayo ya ukatishwaji tamaa yaliyotolewa na watu fulani.

Rapa Kala Jeremiah pia yeye ni miongoni mwa wasanii waliowahi kujitangazia kuwa na lengo la kuja kuwa rais wa Tanzania hapo baadae, wakati alipokuwa anafanya mahojiano na chombo kimoja wapo cha habari lakini kwa bahati mbaya hakuweza kupata mapokezi mazuri kwa nyakati hizo na mwishowe akaambulia maneno ya kashfa na yenye kumkatisha tamaa.

EATV

Baada ya Muda Gani Unaruhusiwa Kufanya Mapenzi na Mkeo Baada ya Kujifungua?

$
0
0
Zoezi la kujifungua linafariji na kuchosha pia, ni la faraja sana kwa kuwa linakufanya uwe mama? Wiki 4 za mwanzo kwa mzazi zinaweza kuwa katika kumbukumbu zako kwa muda mrefu kwakuwa ni wiki za ‘majimaji’ tu – jasho, kunyonyesha na haja ndogo kutoa majimaji yote ya ziada mwilini mwako. Inashangaza hata kama mtu utakuwa na hamu ya kufanya mapenzi katika kipindi hicho.

Madaktari wanasema kuwa mwili wa mwanamke unahitaji wiki 6 kurudi kwenye hali yake ya kawaida. Katika kipindi hiki cha wiki 6, mfupa wa nyonga na uti wa mgongo hurudi kwenye hali yake ya awali. Homoni zako pia zinajirekebisha sambamba na misuli iliyopo kwenye sakafu ya nyonga kupumzika wakati ikirudi kwenye hali yake iliyokuwa nayo mwanzo kabla ya kazi kubwa iliyotoka kuifanya ya kumbeba mtoto na kusaidia kwenye kumtoa wakati wa kujifungua.

Kwahiyo, mpaka kitakapofika kipindi hiki cha wiki 6, unashauriwa kutofanya mapenzi, lakini haimaanishi kwamba huwezi kufanya mambo mengine kama kumbusu, kumshikashika, au kumnyonya mwanaume wako, na yeye kukufanyia hivyo hivyo. Wanawake wengine wanasema kuwa chuchu zao huwa na hisia sana kutokana na kunyonyesha kiasi kwamba wanaweza kufika kileleni kwa kushikwa chuchu tu.

Lakini kuhusu dawa za kuzuia kubeba mimba katika kipindi hiki, mnashauriwa muwe na tahadhari kuhusu kutumia njia yoyote itayoathiri mfumo wa homoni. Hii ni kwa sababu itaathiri sana kiwango na ubora wa maziwa na itamsababishia mtoto kutopata lishe inayotakiwa. Pia, vidonge vyenye oestrogen vimethibitishwa kusababisha kupungua kwa kiwango cha maziwa kwa mama anayenyonyesha, na mara nyingine hupunguza ghafla sana.

Shirika la Afya Duniani linasisitiza mtoto anywe maziwa tu kwa muda usiopungua miezi 6 kisha uendelee kumnyonyesha mpaka atakapofikisha miaka miwili. Wazazi wengi wanaona hii inawatesa na wengi wao wanasema kwamba miezi 6 ya mwanzo ni muhimu sana.

Unashauriwa uzungumze na daktari wako kuhusu muda gani unaweza kurudia kufanya mapenzi na njia za kutumia kujikinga na mimba ya haraka na pia umuulize hasa kuhusu kutumia dawa zenye progesterone na madhara yake kwako. Vidonge hivi vinaathiri maziwa (kwa wingi na ubora) kwa kiwango kidogo zaidi ukilinganisha na vidonge vyenye oestrogen.

Mwili wako umefanya kazi kubwa sana ya kuleta kiumbe duniani. Sio tu kwa sababu ni utambulisho wako na kukufanya uitwe ‘mama’ na chochote utachofanya kitakachokufurahisha, utashangaa jinsi ulivyo na sehemu nyingi zinazoweza kukufanya upate raha.

Nina Mimba ya Rafiki wa Mume Wangu, Nifanyeje?

$
0
0

Hi guys i hope mko poa,

Nimekuja kwenu kuomba ushauri kwa sababu najua hapa JamiiForums hatujuani tofauti na mitaani.

Mwezi uliopita mpenzi wangu alisafiri kikazi nje ya nchi na hata sasa hajarudi ila yuko mbioni kurudi.

Alipoondoka kama wiki hivi, rafiki yake alikuja kutuona tunaendeleaje, bahati mbaya watoto nilikuwa nimewapeleka kwa mama yangu wakashinde huko weekend yote hiyo, so shemeji alinikuta peke yangu.

Sijui tulianza anzaje, nilikua na feelings kali sana, nilitoa wine tukawa tunakunywa huku tukizungumza mawili matatu, as time went on tukaanza michezo michezo ya kutaniana, nasikitika mwisho wa utani huo kwa bahati mbaya shetani akatupitia tukawa tumezini na baadae tukahamia bedroom.

Hadi sasa tumeshafanya kama mara nane hivi, tumekua pia tuki meet katikati ya wiki, i accept that he is real good than my hubby.

On Tuesday niliamka na homa kali sana kama mtu mwenye Malaria hivi, nikaenda hospital kucheck Malaria but to my surprise naambiwa Niko pregnant, I was shocked, kwa sababu baada ya hubby kusafiri nilipata period, so kwa vyovyote itakuwa ya shemeji.

Nilikuwa najiuliza sijui niitoe kabla hubby hajarudi kwa sababu anarudi ndani ya siku 4 au 5 au nimsubiri aje nimsukumie yeye? Ila pia nina wasiwasi mtoto akija kufanana na shemeji itakuaje?

Nifanyaje?

Nina Mke Mzuri ila Nimekuwa Mtumwa wa Wanawake

$
0
0
Nimeficha ficha haya mambo ila najiona kabisa naangamia hivyo ni bora leo niombe ushauri maana hapa pana watu wazima, wanasaikolojia na viongozi wa dini.

Mkasa wangu ni wa hakika na bado nipo katika mateso hata sasa.

Wakati nipo balehe nilikutana na wasichana mbali mbali waliouteka moyo wangu na nikawaeleza hisia zangu, kwa bahati mbaya nilijibiwa karaha na kutoswa sababu ya maisha yangu ya dhiki.

Hali ilikwenda hivyo kwa muda mrefu mpaka moyo wangu ukajenga chuki na wanawake, niliwaona hawana usawa na sio wa kuwa nao karibu.

Katika utafutaji wangu wa maisha ghafla mambo yakabadilika na nikawa nina pesa na kuishi vizuri na nikaanza kujenga nyumba na pia nikawa na miradi pamoja na gari ya kutembelea.

Ni hapo ndipo wasichana wakaanza kuwa karibu na mimi na kunihitaji kimapenzi, na mimi nilishajenga chuki moyoni na nikapanga kuwakomoa, nikajikuta natembea na wanawake wengi tofauti kuanzia wanafunzi, walimu, wasichana tu wa mtaani, machangudoa na wapenzi wa watu.

Nikajikuta dhaifu mbele ya wanawake yaani siwezi kulala hata siku moja peke yangu bila mwanamke na pia mda mwingine nilifanya mapenzi na wasichana wawili tofauti kwa siku moja, haswa kama huyo wa pili aliyenitafuta ni mzuri sana.

Haya mambo sipangi bali najikuta tu inatokea na kila nikimaliza najuta na kusema ndio mara ya mwisho ila punde tu naingia katika vishawishi tena, nilioa mke safi kabisa ili niepuke hali hii ila tuliachana baada ya kunifumania mara kadhaa.

Sasa nina mke mwengine na safari hii nimeoa mke wa ndoto yangu mtoto mzuri sana shombe shombe kiasi kwamba marafiki wanasema kweli mwamba umepata kifaa.

Ila bado ninajikuta natembea na rafiki zake pia wasichana wa mtandaoni kama vile Jf, Badoo, Fb nk na pia nimekuwa maarufu madanguro mengi sana mpaka naona noma.

Mara kadhaa nasafirisha mademu wakali toka mikoa tofauti na kunifuata mimi, sihongi sana na wala sijatetereka ki uchumi na wala sijaathirika ila tu najiuliza nini kipo nyuma ya nguvu hii inayonishinda kujizuia?

Kilichonifanya nijione naingia katika hatari ni kwamba, juzi kushinda jana nilikwenda guest na msichana fulani nilikutana nae juu juu tu, tukafanya mapenzi na tulipomaliza wakati tunatoka kuna jitu la miraba minne lilikuwa likituangalia sana na yule msichana akashtuka sana.

Baadae nilipomuuliza akasema yule jamaa anafanya kazi na mume wake ni FFU kitengo cha doria.

Hakika nikaona hiki ni kifo cha wazi sasa na nimefikia pabaya, haya mambo sipangi ila imekuwa kama ulevi na siwezi kuacha.

Naombeni ushauri wa kunijenga wadau

Kutana na Sharifu Seif Mohammed wa Bagamoyo, Kijana Aliyezaliwa Katika Koo za Masharifu

$
0
0

KUTANA NA SHARIFU SEIF MOHAMMED WA BAGAMOYO, KIJANA ALIEZALIWA KATIKA KOO ZA MASHARIFU

SASA AMEKUWA GUMZO DUNIANI KOTE KUTOKANA NA DUWA NA TIBA MBALIMBALI ANAZOTOA,

SHARIFU SEIF MOHAMMED ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO WASAIDIA

Sharifu seif Mohammed ni Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili Tanzania na duniani kote,

ANATIBU KWA KUTUMIA KITABU CHA QUR'AN, DAWA ZA ASILI, NJIWA NA MAJINI

(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFWATA MAELEKEZO YAKE)

JE? Umeachwa na UMPENDAE Awe MME/MKE au MPENZI na Bado Unampenda? Mpigie Simu SHARIFU sasa Hivi Ujionee miujiza yake, Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA/ MAHUSIANO yako ndani ya saa 72 tu.
Hata kama mpenzi wako anaishi na mtu mwingine anauwezo wa hali ya juu ya Kusambalatisha Mahusiano yao (Mfarakano/Kimavi) na kumrejesha kwako,
Je Una Mpenzi wako ana Pesa na unataka Kumkamata? Muone SHARIFU SEIFU MOHAMMED Atamfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi, SHARIFU SEIF MOHAMMED Anatumia Jina La Muhusika au Picha Kumaliza tatizo lako, ANATAFSIRI NDOTO, ANAPANDIKIZA NYOTA YA KUSHINDA BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, ANATOA NUSKI NA VIFUNGO MBALIMBALI, ZINDIKO ZA NYUMBA NA BIASHARA, PETE ZA BAHATI ZINAZOENDANA NA NYOTA YAKO, HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME, HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA, HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA, MAGONJWA SUGU KAMA VILE MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA, TATIZO LA UZAZI KWA KINA MAMA, ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA  ALIE POTEA, ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE,

Humaliza Kesi ya Aina Yoyote Ndani ya Siku 7 tu, Hutoa Jini MALI kwa wale Wanao hitaji Utajiri Bila Masharti,

Kwa mawasiliano na ushauri zaidi:
Mobile + 255 654 836970
WhatsApp +255 756 033670

Ushauri: Ni vyema kupiga simu kuliko kutuma sms ili upate huduma kwa wakati

Simba Yafungua Ligi Vizuri Yaitandika Tanzania Prison Bao 1-0

$
0
0
Simba Yafungua Ligi Vizuri Yaitandika Tanzania Prison Bao 1-0
MABINGWA watetezi, Simba wameanza vizuri Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya kuichapa Tanzania Prisons ya Mbeya bao 1-0 katika mchezo uliofanyika usiku huu Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam.

Bao la Simba limefungwa na mshambuliaji kutoka Rwanda, Meddie Kagere aliyefunga dakika ya pili kwa shuti kali baada ya kupewa pasi na John Bocco kutoka upande wa kulia.


Kikosi cha Simba: Aishi Manula, Shomari Kapombe, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Pascal Wawa, Erasto Nyoni, Jonas Mkude, James Kotei, Hassan Dillunga/Nicholas Gyan dk82, Meddie Kagere, John Bocco/Adam Salamba dk83 na Shiza Kichuya/Muzamil Yassin dk67.


Tanzania Prisons: Aaron Kalambo, Benjamin Asukile, Laurian Mpalile, Nudrin Chona, James Mwasote, Jumanne Elfadhili, Salum Kimenya, Cleophace Mkandala, Kelvin Friday/Lambert Sabiyanka dk82, Salum Bosco/Ramadhani Ibata dk71 na Ismail Aziz/Hassan Kapalata dk79.

Mbunge Bobi Wine Kupandishwa Mahakamama ya Kijeshi Leo

$
0
0
Mbunge Bobi Wine Kupandishwa Mahakamama ya Kijeshi Leo
MBUNGE Robert Kyagulanyi maarufu kwa jina Bobi Wine leo anatarajiwa kurudishwa katika mahakama ya kijeshi mjini Gulu Kaskazini mwa Uganda. Taarifa hiyo imewashtua mawakili wake ambao awali walijuzwa kuwa kesi itasikilizwa katika kambi ya kijeshi ya Makindye anakozuiliwa mjini Kampala.
Wakati huo huo Mtandao wa haki za binadamu za wanahabari nchini Uganda umetoa saa 48 kwa jeshi kuwatambulisha askari wake waliowajumu wanahabari.


Kwa upande mwingine, Wanamuziki wakubwa wakiwemo Chris Martin, Angelique Kidjo na Damon Albarn, wametoa wito wa kuachiwa kwa Mbunge Bobi wine ambaye ana wiki sasa tangu kukamatwa kwake na mbunge mwezake na zaid ya watu 30. Wasanii hao wamejaza waraka wa kutaka mbunge huyo wa upinzani kuachiwa.
Wakili wa Bobi Wine anasema kuwa mteja wake ameteswa sana na jeshi, lakini jeshi kwa upande wao wamekanusha. Mbunge huyo anatarijiwa kufikishwa mahakamani kwa madai ya kumiliki silaha kinyume na sheria pamoja na tuhuma za wafuasi wake kuushambulia msafara wa Rais Museveni.

Baada ya Manji Kurejea Kwenye Nafasi Yake Maisha Ndani ya Yanga Yaanza Kuwa Mazuri

$
0
0
Baada ya Manji Kurejea Kwenye Nafasi Yake Maisha Ndani ya Ya Yanga Yaanza Kuwa Mazuri
MAISHA yamebadi­lika ndani ya Yanga, ikiwa leo ni siku ya nne tu tangu Mwenyekiti Yusuf Manji arejee rasmi kwenye uongozi Jumapili iliyopita.



Manji ambaye ni mtaalam wa biashara, aliibuka Ju­mapili na kuzungumza na wachezaji ndani nya Uwanja wa Taifa na USM Algiers ikakumbana na kipigo cha mabao 2-1 katika mechi ya Shirikisho.



Championi Jumatano limejiridhisha kwamba tan­gu Manji aonekane ndani ya klabu hiyo mambo yame­kuwa safi ambapo timu imekuwa na hamasa ya kutosha hali inayowafanya hata wachezaji waliokuwa hawajitumi kuanza kuamka kwani wana matarajio ya neema kubwa.





“Tangu ajitokeze Mwenyekiti wetu Manji na kututia moyo siku ya mchezo wetu na Waarabu, kuna matumaini makubwa kwetu wachezaji kuwa nee­ma itashuka muda si mrefu kwani hadi leo hii timu ipo kambini inaonyesha wazi kuwa mkono wake ulishaingia katika kuisa­poti timu kwani mwanzo tulikuwa tukisuasua kwa mambo mengi likiwemo suala la kuchelewa kuingia kambini mapema tofauti na ilivyo sasa.



“Hata wachezaji wa­mechangamka, huku ndani ya kambi gumzo ni yeye tu hadi wachezaji wageni wameanza kuuliza kuwa jamaa ana nini mpaka kila mtu anapagawa,” kilisema chanzo chetu cha kuaminika ndani ya kambi ya Yanga.



“Maneno ya Manji muda mfupi kabla ya mchezo wetu na Waarabu yaliji­tosheleza sana kwetu kuona kuna jambo zuri linakuja kutoka kwake,” kiliongeza chanzo hicho.



Yanga imeweka kambi yake kwenye Hoteli ya Island iliyopo Manzese jijini Dar es Salaam na inaelezwa kuwa kila kitu kimekuwa kikienda sawa tofauti na mwanzoni.



Timu hiyo ilikuwa ikikabiliwa na ukata kutokana na kutokuwa na vyanzo vya fedha, lakini ujio wa Manji umewapa faraja kutokana na moyo wake wa kujitoa haswa pale panapokuwa na jambo la dharura la fedha.
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live




Latest Images