Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live

Nuh Mziwanda Afunguka Mazito Kuhusu Mjengo wa Shilole "Mimi Nilichangia Kununua"

$
0
0
Nuh Mziwanda Afunguka Mazito Kuhusu Mjengo wa Shilole "Na Mimi Nilichangia Kununua Mjengo Wa Shilole"
Msanii wa muziki wa Bongo fleva Nuh Mziwanda ameibuka kuwa ana yeye pia aliweka mkono Kwenye kununua Mjengo mpya wa Shilole aliouanika Kwenye mitandao ya kijamii.

Ikiwa ni siku chache zimepita tangibly shilole aanikr Mjengo wenye thamani ya zaidi milioni 90 anaoujenga hivi sasa, aliyekuwa mpenzi wake Nuh Mziwanda amedai na yeye pia ana chake Kwenye Mjengo huo.

DCI Afunguka Sakata la Kumkamata Aliyekuwa Mkurugenzi NIDA

$
0
0
DCI Azungumzia Sakata la Kumkamata Aliyekuwa Mkurugenzi NIDA
Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Boaz amesema wanayafanyia kazi maagizo ya kumkamata mkurugenzi mkuu wa zamani wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), Dickson Maimu.

Maagizo hayo yalitolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola siku mbili zilizopita akitaka Maimu kukamatwa kwa kosa la tuhuma za kula njama na kuisababishia hasara Serikali ya Sh4.6 bilioni.

Mbali na Maimu, wengine waliotakiwa kukamatwa juzi kabla ya saa 12:00 jioni kwa kosa hilo ni mmiliki wa kampuni ya Gotham International Ltd, Gwiholoto Impex Ltd na Ms Aste Insurance Broker Company Ltd.

Wamiliki wa kampuni hizo tatu walikamatwa na polisi waliokuwa katika ofisi za wizara hiyo juzi. Maimu hakuwapo katika mkutano na waziri, bali alikuwapo katika mahojiano naye Agosti 3.

DCI Boaz jana alisema serikali inajitahidi kuhakikisha kuwa taasisi za umma zinaheshimu haki za binadamu na uzalendo kwa kutumia vyema mali zilizopo.

Alisema wale ambao wamekuwa wakifanya ubadhirifu wa mali za umma lazima wakamatwe na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

 Alisema Waziri ana dhamana ya Wizara na pia ni cheo cha kisiasa hivyo lazima aweke msimamo katika masuala hayo na akimwagiza yeye analenga kuwataka vyombo vya dola vitoe vijana wake kwa ajili ya kufanya kazi hiyo.

Alisema wakikamilisha utaratibu kuwakamata watuhumiwa, watafikishwa mahakamani kujibu mashitaka yao na endapo watapata dhamana wataendelea kufanya upelelezi na kwamba wakiendelea kushikiliwa, upelelezi utaendelea hadi kuwabaini waliohusika na ubadhirifu huo.

Alisema kuendelea kufanya uchunguzi wakati watuhumiwa wakiwa mahakamani kunalenga kupata uthibitisho wa kina na kukusanya vielelezo ili kujua ni nani aliyehusika.

‘’Suala la uhujumu uchumi wa fedha za serikali linakuwa na mtandao mkubwa ambao mara nyingi kuwapata waliohusika kwa asilimia 100 ni ngumu kwa sababu wanashirikiana na watu ambao kuwafahamu inahitaji uchunguzi wa kina na wa muda mrefu, kuwapata walioshirikiana na wakurugenzi hao kufanya ubadhirifu,’’ alisema.

Agosti 15, 2016 mtuhumiwa Maimu, Kayombo na wafanyakazi wengine NIDA, walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashitaka ya uhujumu uchumi na kuisababishia serikali hasara ya Sh bilioni 1.16.

Wafanyakazi hao wa Nida ni Meneja Biashara, Avelin Momburi, Benjamin Mwakatumbula (Kaimu Mhasibu Mkuu), George Ntalima (Ofisa Usafirishaji), Sabina Raymond (Mkurugenzi wa Sheria) na Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama), Joseph Makani.

Maimu na Mwakatumbula wanadaiwa tarehe tofauti kati ya Januari 15 hadi 19, mwaka 2010 makao makuu ya NIDA wilayani Kinondoni Mkoa wa Dar es Salaam, wakiwa watumishi wa umma kwa nafasi zao waliidhinisha malipo kwa Gotham International Limited (GIL) ya Dola za Marekani 2,700,00 bila ya kutumia viwango vya kubadilisha fedha za kigeni vilivyowekwa na Benki Kuu ya Tanzania, kinyume na kifungu 19.3 cha mkataba kati ya NIDA na GIL, hivyo kuifanya GIL kupata faida ya Sh 3,969,000.

Pia walidaiwa kati ya Juni 3 na 5, 2013 katika makao makuu hayo walitumia madaraka vibaya kwa kuidhinisha malipo kwa GIL ya Dola za Marekani milioni 1.8, bila ya kuzingatia viwango vya kubadilisha fedha, hivyo kuifanya GIL kupata faida ya Sh 106,346,000.

Pia Juni 20, 2014 katika makao makuu hayo, waliidhinisha tena malipo ya Dola za Marekani 675,000 kwa GIL bila ya kuzingatia viwango vya kubadilisha fedha, hivyo kuifanya kampuni hiyo kupata faida ya Sh 42,471,000.

Maimu na Mwakatumbula wanadaiwa kutumia madaraka yao vibaya kwa kupitisha malipo mengine ya Sh milioni sita kwa GIL bila ya kupiga hesabu kwa kutumia viwango vya kubadilishia fedha hivyo kuifanya kampuni hiyo kupata faida ya Sh 14, 661,676.76.

Inadaiwa tarehe tofauti kati ya Januari 15, 2010 na Mei 16, 2015 katika makao makuu hayo ya NIDA kwa kuidhinisha malipo kwa GIL ya Dola za Marekani bila ya kuzingatia viwango vya kubadilisha fedha za kigeni waliisababishia NIDA kupata hasara ya Sh 167,445,676.76.

Anadaiwa Aprili 16, 2012 katika makao makuu ya NIDA, Ndege akiwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Aste Insurance Broker ambayo imeingia mkataba na NIDA wa kutoa huduma za bima, kwa nia ya udanganyifu aliwasilisha hati ya malipo yenye taarifa za uongo NIDA akionyesha kampuni yake inastahili kulipwa Sh 22,582,281 kwa huduma za bima iliyoitoa huku akijua taarifa hizo za uongo na zilikuwa na lengo la kumdanganya mwajiri wake.

Mkurugenzi huyo wa NIDA, Mwakatumbula na Ndege, wanadaiwa katika tarehe tofauti kati ya Agosti 2012 na Januari 4,2013 makao makuu ya NIDA waliisababishia hasara ya Sh 55,312,800.

Maimu na Mwakatumbula wanadaiwa pia kati ya Januari 29 na 30, 2013 katika makao makuu hayo walitumia madaraka yao vibaya kuidhinisha malipo ya Dola za Marekani milioni mbili kwa IRS Corporation Berhad.

Ilidaiwa mapendekezo ya utaratibu mpya wa haraka wa upatikanaji wa vitambulisho na vifaa bila ya kufanya marekebisho ya mkataba ulioko kati ya NIDA na kampuni uliiwezesha IRIS kupata faida ya fedha hizo.

Mwakatumbula, Ntalima na Kayombo wanadaiwa kati ya Juni 4 na 6, 2013 makao makuu waliisababishia NIDA hasara ya Sh 45,515,961.

Maimu na Sabina wanadaiwa kati ya Agosti 3, 2010 na Novemba 7, 2011 katika makao makuu ya NIDA wakati wakitekeleza majukumu yao, walitumia madaraka yao vibaya na kuiwezesha GIL kupata faida ya Sh 901,078, 494 na kuisababishia NIDA hasara ya kiasi hicho cha fedha.

Trump Azikana Tuhuma za Kutumia Fedha Wakati wa Kampeni Kuwalipa Wanawake Ili Kuwanyamazisha

$
0
0
Trump Azikana Tuhuma za Kutumia Fedha Wakati wa Kampeni Kuwalipa Wanawake Wawili Ili Kuwanyamazisha
Rais wa Marekani amekana vikali tuhuma za kuhusika kwake katika kutumia fedha wakati wa mikutano ya kampeni kuwalipa wanawake wawili ambao wanasadikiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi naye.

Katika kesi iliyosikilizwa katika mahakama moja mjini New York mapema wiki hii , mwanasheria wa zamani wa rais Trump, Michael Cohen, amesema kuwa Trump alimpa maelekezo kutoa fedha kwa lengo kuu la kuwashawishi wanawake hao kukaa kimya wakati wa uchaguzi wa rais wa 2016.

Ingawa katika mahojiano na kituo cha runinga cha Fox News, Raisi Trump alitoa ufafanuzi kuwa malipo hayo yalitoka katika fedha zake binafsi na hazikuwa fedha za kampeni kama inavyodhaniwa.

Na kuarifu kuwa alikuja kutanabahi juu ya malipo hayo baadaye, ingawa hakubainisha kuwa miamala hiyo ilifanyika wakati gani.

Raisi Trump amekuwa akimshutumu bwana Cohen kwa kupika mambo dhidi yake kwa lengo la kupata huruma na kuepuka kifungo.

Ikulu ya white house, imesisitiza kuwa kuvunja sheria ya fedha za kampeni kwa Michael Cohen hakumaanishi kuwa basi Rais trump naye atawajibika, msemaji wa white house sarah sanders amekataa kusema ni lini Rais Trump alijua juu ya malipo ya wacheza filamu wawili wa ngono

''kama rais alivyosema katika matukio tofauti tofauti, hajafanya kitu chochote kibaya, hakukua na madai yoyote dhidi yake katika hili, na kwasababu tuu Michael Cohen amekiri makossa yake haimaanishi inamgusa rais''

Katika kukiri makosa yake siku ya jumanne bwana Cohen alisema kuwa ametumwa na Trump kufanya malipo hayo lakini white house imekataa madai haya.

Malipo yafanywayo kwa siri kwa niaba ya mwanasiasa ama mgombea yeyote yanaweza kuchukuliwa kama ukiukwaji wa sheria za kampeni za nchini Marekani

Shilole Awapa Somo Uwoya, Wema "Acheni Maisha ya Kuigiza Mitandaoni Pambaneni Kuitafuta Shilingi"

$
0
0
Shilole Awapa Somo Irene Uwoya na Wema Sepetu "Pambaneni Kuitafuta Shilingi  Acheni Maisha ya Kuigiza Mitandaoni"
Msanii wa muziki wa Bongo fleva na mfanyabiashara Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole amewapa somo wasanii wenzake Wema Sepetu na Irene Uwoya.

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Shilole amewataka mastaa hao wa kike kuacha maisha ya kuigiza mitandaoni ambapo wanaonekana wamependeza kwa kuvaa nywele zenye thamani ya shilingi milioni moja na zaidi huku wakiwa hawajafanya la maana litakalowasaidia maishani.

Nawasihi wasanii wenzangu wote siyo Wema na Uwoya tu, wapambane na waithamini shilingi mia moja maana unakuta mtu ananunua nywele za shilingi milioni moja na hana hata kiwanja hebu jiulize hapo angenunua mifuko ya simenti angepata mingapi, jamani wasanii wenzangu jitahidini kufanya mambo yatakayowasaidia katika maisha ya mbeleni.

Inashangaza sana kuona msanii anafariki msiba unaenda kufanyika kwa shangazi yake kwa sababu kuna nyumba nzuri, kwa nini tusijikwamue sasa hivi angali tuna nguvu ili baadaye tuwe na cha kujivunia jamani, inabidi tubadilike zama za kujianika mitandaoni na nywele za mamilioni zimepitwa na wakati”.

Lakini pia Shilole alitoa siri ya mafanikio yake iliyomuwezesha kujenga mjengo huo wa thamani:

Hii nyumba nimejenga kwa fedha nyingi ambazo mpaka sasa sijui jumla ni gharama kiasi gani maana sijajumlisha na fedha hizo nilikuwa kila nikipata hela kidogo nanunua simenti au mchanga na vifaa vingine hivyo mpaka nikae chini niangalie risiti nianze kuzijumlisha”.

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo

$
0
0

Breaking News: Mahakama ya Jeshi Nchini Uganda Yamuondolea Mashtaka Bobi Wine Aachiwa Huru

$
0
0
Taarifa za hivi punde kutoka Uganda ni kwamba mahakama ya jeshi imemuondolea mashtaka mbunge wa Kyadondo Robert Kyagulanyi.

Inaarifiwa kwamba mahakama hiyo ya jeshi inataka badala yake inataka kumkabidhi mbunge huyo kwa mahakama ya kiraia ajibu mashtaka ya uhaini pamojana wabunge wengine waliokamatwa.

Mbunge huyo ambaye aliwahi kuwa mwanamuziki nchini kwa jina maarufu Bobi Wine leo alitarajiwa kurudishwa katika mahakama ya kijeshi mjini Gulu kaskazini mwa Uganda.

Mawakili wake awali walijuzwa kuwa kesi itasikilizwa katika kambi ya kijeshi ya Makindye anakozuiliwa mjini Kampala.

Kumekuwa na shinikizo kubwa kimataifa la kutaka Bobi Wine aachiwe huru.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa sulutani Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH issa sulutani Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na issa sulutani Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU. Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Issa sulutani Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI. Nguvu za KIUME, Humaliza Kesi zilishindika ndani ya siku 14 tu..na mengi zaidi +255 622588038au 0679119679 au +255 764318107

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...

Watoto wa Mzee Majuto Wafukuka Kuhusu Tuhuma za Kumfukuza Mama Yao

$
0
0
Watoto wa Mzee Majuto Wafukuka Kuhusu Tuhuma za Kumfukuza Mama Yao
Siku chache baada ya mke wa marehemu Mzee Majuto, Aisha Yusufu kudai kufukuzwa na familia ya msanii huyo, ndugu wametoa msimamo wao kuhusiana na sakata hilo wakisema wamezisikia tuhuma hizo.

Madai hayo yanakuja ikiwa ni siku 15 zimepita tangu alipofariki msanii huyo maarufu wa vichekesho aliywahi kutamba na filamu kama Back From New York, Inye na Mzee wa Chabo.

Wiki iliyopita mwanamke huyo alizungumza na vyombo vya habari akidai kwamba baada ya kumalizika kwa shughuli za maziko, ndugu walimwambia aanze kujitegemea kwa kila kitu ikiwemo chakula, jambo ambalo alilitafsiri ni sawa na wamemfukuza.

Katika maelezo yake mama huyo wa watoto wanne, amesema ndugu hao walimwambia kwamba ataishi kwa fedha za pole ambazo waombolezaji mbalimbali wameendelea kumpa.

MCL Digital ilizungumza na Hamza ambaye ni mtoto wa kwanza wa Mzee Majuto kwa njia ya simu, ambaye alisema hayupo tayari kuongea kwa sasa hivi lolote juu ya suala hilo mpaka hapo itakapofika siku ya kufanya arobaini.

“Arobaini ni Septemba 15 mwaka huu, wewe naomba uje huku Tanga  Septemba 14 tutaongea kwa kirefu na utajua kwamba tulimfukuza au la ila kwa sasa siwezi kukuambia lolote kuhusu jambo hilo,” amesema msimamizi huyo wa familia.

Kwa upande wake mtoto wa tano wa Majuto, Abuu Athuman, amesema anachojua mama yao amekwenda Dar es Salaam baada ya kukosekana kwa watu wa kukaa naye katika kipindi chote cha eda kwa kuwa wengi wana shughuli zao.

Pia amesema kwamba vyakula vipo vya kutosha tangu kulipotokea msiba na tuhuma za mama huyo kwamba amefukuzwa sio za kweli kwani hawawezi kufanya hivyo kwa kuwa wanamtambua kama mama yao.

“Yule ni mama yetu, hatuwezi kumfukuza isitoshe ana watoto wadogo ambao tunatakiwa tuhakikishe wanalelewa kama enzi baba alivyokuwa hai ikiwemo kusoma.”

Naye mke wa Majuto alipotafutwa, amesema kwa sasa familia yake imemkataza kuzungumza na vyombo vya habari na  kusisitiza alichokisema awali ndio ukweli wenyewe.

Haji Manara Awatolea Povu Washabiki wa Simba Wasiolidhika na Ushindi wa Jana "Mpira ni Zaidi ya Daktari Kufanya Oparesheni ya Kichwa"

$
0
0

Haji Manara Awatolea Povu Washabiki wa Simba Wasiolidhika na Ushindi wa Jana "Mpira ni Zaidi ya Daktari Kufanya Oparesheni ya Kichwa"
Baada ya Simba kuanza vema kwa ushindi kiduchu wa goli 1-0 jana dhidi ya Prisons, afisa habari wa klabu hiyo Haji Manara amewafungukia mashabiki wanao beza ushindi huo katika mechi yao ya ufunguzi wa Ligi kuu bara.

Simba iliibuka na ushindi wa bao 1-0 ambalo lilifungwa mapema kabisa na Meddie Kagere mnamo dakika ya pili tu ya mchezo aliyesajiliwa kutoka Gor Mahia FC huku aliyekuwa straika wa Lipuli FC na sasa Simba, Adam Salamba kucheza takribani dakika 6 bila kufanya maajabu kama alivyozoeleka.

Manara kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii amefunguka kuwa anawashangaa wanaobeza na kulalamikia kiwango cha kocha wao na kudai kuwa hafai kukinoa kikosi hicho.

Manara ameandika; “Wakati mwingine najiuliza nini wanadamu wanataka? hasa washabiki wa mpira, nimetalii kidogo kwenye magroup machache ya wanasimba kwenye WhatsApp nimeshangaa baadhi yetu kutokuridhika na ushindi wa leo wa goli moja dhidi ya Prisons. Wengine kwenye Instagram wanafika mbali zaidi eti mfumo wa kocha haufai”.

Ameongeza kuwa “Mpira ni sayansi kubwa kuliko kwenda mwezini au daktari kumfanyia upasuaji wa kichwa mtu,ukubwa wa sayansi hii ni kwamba hujui mpinzani wako kajipangaje, hujui kama siku hyo wachezaji wako watacheza kwa kiwango gani lakini kubwa Sayansi hii haina jawabu la moja kwa moja kama hesabu au hisabati 3×3 ni tisa tu, hata ukokotoe vipi! Huku kwetu kwenye ndiki 3×3 inaweza kuwa bilioni nane”.

Baada ya Simba kuanza kwa ushindi huo jana, watani zao wa jadi Yanga, leo wanashuka dimbani kuwakaribisha Mtibwa Sugar kwenye Uwanja huohuo wa taifa saa 12 jioni, ambapo kuelekea mechi hiyo mwenyekiti wa kamati ya usajili na mashindano, Hussein Nyika, ameahidi kuwa Yanga itauwasha moto mkali.

Huu Hapa Waraka Aliouandika Museveni Kabla ya Bobi Wine Kuachiwa na Mahakama

$
0
0
Huu Hapa Waraka Aliouandika Museveni Kabla ya Bobi Wine Kuachiwa na Mahakama
Baada ya kimya cha muda mrefu, Rais wa Uganda Yoweri Museveni amejibu kwa marar ya kwanza maombi ya wasanii wa muziki nchini humo wanaotaka amuachie rapa Bobi Wine ambaye amekamatwa Jumatatu ya wiki hii mjini Arua kwa makosa ya kuchochea vurugu.

Rais Museveni amesema kuwa anachokijua kwa sasa ni kwamba wanasiasa wanatumia upungufu wa ajira kuwashawishi wananchi kuvunja amani na kitendo hicho kwenye nchi yake kwa sasa hawezi kukiruhusu kwani amani ndio msingi wa maendeleo.

Kwa upande mwingine Museveni amesema kilichopelekea hadi kujibu ishu ya Bobi Wine ni kutokana na rundo la maoni mtandaoni yakimtaka amuachie huru Bobi Wine.

I have read your comments in response to my earlier statement. I thank all of you for giving your views. This is a good and productive way of communicating; no need for violence and “fujo”.

There is, however, one element that people are not bringing out in these comments. This is the issue of the unemployed Bazukulu in the towns and villages. It is one of the elements, in fact the main element, the unprincipled politicians cynically (concerned only with one’s own interests and typically disregarding accepted standards in order to achieve them) use to lure our youth into demonstrations and riots.

Our unemployed youth are a problem but a good one given that we have already laid the basis for resolving unemploymentthrough the economic recovery programme ever since 1987. What proof do I have? Look at our import bill of US$5bn per annum. The other day, at Kololo, while graduating the 4,000 Bazukulu of my daughter Nakyobe’s girl child skilling programme, I gave the list of the haemorrhage (bleeding) of our hard earned dollars importing from outside products that should be made by you, the youth, here. Some of the items are the following:

1. Shoes- US$ 51m

2. Maize-flour -US$ 54m

3. Medicine -US$295m

4. Second hand clothes -US$ 73m etc etc

With the support of the Government, many youth can get work sites and equipment to make many of those items here- thereby, creating jobs for themselves and for others. I have already shown you how this can be done by supporting the youth and non-youth groups in Katwe (motor-mechanics etc), Nsambya (furniture), Najjera (metal fabrication), Wobulenzi (grain milling and animal feeds mixing), Rukungiri (furniture making, metal fabrication etc), Nakyobe girl child skilling programmes (shoes making, cloth weaving, knitting, embroidery, confectionery, beautician skills) etc etc. How are those groups doing – well or badly? If they are doing well, for the individuals involved and for the country, then these pilot projects should be turned into a national movement of import- substitution and export promotion.

Above, I just pointed out the areas that are easiest to move in. The areas that need more skills are:

1. Automobiles – US$ 292m

2. Electrical equipment- US$ 49m

3. Electronics (TV sets, mobile phones, computers etc) – US$ 200m etc etc.

These types of projects are being done or will be done by our educated youth (scientists), foreign investors or some of our local business people converting from importing to import- substitution and export promotion.

Then there are the really big projects like steel- making (in Tororo), phosphates fertilizers (Tororo), gold refinery (Entebbe), Copper and cobalt processing (Kasese) etc. These can only be done by either the foreign investors or by Government parastatals. All these are already in progress and we now have enough electricity, the roads are being worked on, the railway is planned.

Therefore, the unprincipled politicians who mislead our youth into rioting or actually pay them to riot or to commit arson must be condemned. Also to be criticized are the NRM leaders who do not engage these youth and squander resources in unnecessary foreign travels and other non- priority expenditures.

We now have the money, if prioritization is correct, to launch a serious assault on the poverty and hopelessness that renders our Bazukulu vulnerable to manipulation and exploitation by unprincipled politicians. I have proof of this which I will bring out at the right moment.

There is another area of jobs access which I do not like myself but it is better than nothing as of now- as we organize ourselves better. These are the foreign jobs. The Ministry of Labour is letting us down here by allowing businessmen to exploit our youth by charging each youth between Shs2 and 8million to be allowed to access a job outside. This is too much. I have already picked this up and I will resolve it. I, however, prefer local jobs.

Coming to the responses, therefore, I say the following:

1. I salute those who understood and appreciated my explanations for the unfortunate events in Jinja East, Bugiri and Arua. Those who were positive to my explanations were people like:Ssebandeke Yakoub, Amos Nkamuhaabwa, Ronald Kisseka , Aggrey Mugume, Ssebunya Shafique, Kyoyesiga Nobert, Hosea Luberenga, Prosper, Nelson Luyima, Abdi Ngurusi, Abenawe, etc etc.

2. There were others who were either sceptical or negative. These were people like: Noel Spears, Daddy’s gal, Watuwa Jim James, Dan Okello, Jerry Gitta, Richard Tuwangye, Walakira Moses, Edith Mwigiri, Brandon Raymond, Atugonza Jackson, Tumukunde Comfort, Andeman Daku etc etc.

I will get time to respond to their views. I am going to get time and answer some of these comments one by one. I am too ready to engage in the debate. These seem to say that the Government should not take a firm stand on the politically motivated attacks on women, children, adults, damage to property or rape because as Jajja I should ignore those acts. That opinion is wrong. 70% of the registered voters stayed away from voting in Arua because of that violence. A person died in Bugiri and another one died in Arua on account of that. That must stop. We need discipline so that we roll out our well-conceived and already demonstrated strategy of transforming Uganda.

Besides, peace is a right of every Ugandan. You have absolutely no right to trample over my Kiosk, damage my shop or my car or cause damage to my farm because of your political ambitions. Peace is a right and not a favour from anybody. If you want to make a political statement, work with the Police, walk peacefully to an agreed, non- populated point and give your views. In UK, they have Hyde Park. In Uganda, people can use Kololo or other rally points. After the rallies, the organizers should tell the followers to go home peacefully. Is that too much?

3. I must condemn in the strongest terms the shooting by the Police of one of our Bazukulu, Sekisivu, who was in a taxi, together with others, going to participate in football matches somewhere else. The Policemen involved will be punished. Fortunately, they were identified. It was either panicky actions on their part or even malice , aimed at spoiling the name of the NRM. These people were not part of the rioters in Mityana. Why shoot them? This is very much regretted.

4. However, we must not forget to condemn the Mityana rioters who were the original cause of this confusion and who looted the kiosks of the low income earners. I will visit them and support them. That riot was organized by people associated with the indisciplined MP, Hon. Zaake. The facts will come out.

5. I condemn in the strongest terms, the killing of somebody, in the Katwe area, whose name I have not yet been told by elements of the Security forces. When I asked the Police, I was told of a stray bullet being responsible for the death. A stray bullet (a bullet that goes away from the target) originally aimed at what and why?

I was told that the Kampala demonstrating groups of Monday were more of a nuisance than a menace- which the Arua groups were. The Monday groups were operating in small groups, burning tyres and, then, sending them to social media, working for those who pay them, to show that Uganda is unstable. The enemies of Uganda are now worried at the emerging strength of the economy of Uganda.

The Permanent secretary Ministry of Trade of Kenya , who was here with the Deputy President of Kenya, the other day, told me that for the months of January, February, March, April, and May(2018), Uganda exported more to Kenya than the other way round. The enemies of Uganda are really worried about the growing strength of this economy.

Therefore, our youth groups of Monday were more of a nuisance and psychological warfare than a menace, unless I get new facts. Why then, shoot at them, why fire tear-gas, why fire bullets? Those mobile, tyre burning groups, who are not attacking anybody, should simply be chased on foot, identified from light helicopters (206- Agusto type) or UAUs, arrested and be charged with appropriate offences. In such a situation the issue of stray- bullets does not arrive. A stray- bullet is fired horizontally at a target but misses and hits another person. When you fire up in order to scare, you cannot talk of a stray bullet. By the time the bullet falls back on the ground it will be like a stone. I doubt that it can kill. Unless I get new facts, I provisionally, condemn that act and demand investigations into the circumstances by the Police and other Agencies. The dead person should be identified so that we can assist the family.

6. I condemn, again, in the strongest terms the beating of journalists by elements of the Security forces. It is true that the journalists working for foreign interests or for our own local parasites tell lies, they do not do balanced reporting. On account of that you can block them because sometimes they interfere with the scene of crime. If they refuse, you arrest them and charge them with disobeying lawful command. Beating, however, is wrong because the Security forces do not have that power. People should not be beaten even as a punishment. They can be imprisoned, fined, hanged, etc according to the law and logic but they cannot, be beaten (flogged) except if the Police is dispersing a menacing mob threatening to kill people or damage property. In some countries, they use batons.

On the issue of releasing Bobi Wine and the others , the President of Uganda does not have such powers. Once somebody is arrested, charged and remanded, it is only two authorities who can release such people in any way: the Courts or the DPP withdrawing charges if the evidence is not enough. Let us therefore, wait for the Courts and see what they decide.

Richard Tuwangye mentioned that confronting the rioters may affect Tourism and will give a bad image to Uganda. Yes, in the short-run, it may. However, in the long- run it will pay because opportunists will stop playing around with the stability of the country. Tuwangye’s scepticism about importing voters by the opposition will be reversed once he sees the evidence in Courts.

Finally, the anti-riot SOPs(Standard Operational Procedures) give the whole spectrum of options: warning rioters using loud- speakers, using shields and batons, using tear gas, using rubber bullets, using water – cannons, using rifles but firing in the air and, finally, shooting directly at the rioter in self- defence( for the Security personnel), to stop him harming a mwanainchi or damaging property if they do not pay heed. Therefore, Bazukulu, do not be misled by those who are misusing you that the Security cannot use deadly force. It all depends on the circumstances.

Yoweri K. Museveni

Idriss Aamua Kupita Njia za Daimond Baada ya Kuwa na Wema Sasa Atoka Kimapenzi na Lynn

$
0
0
Idriss Aamua Kupita Njia za Daimond Baada ya Kuwa na Wema Sasa Atoka Kimapenzi na Lynn
Msanii wa Bongo movie na comedian maarufu Idris Sultan anadaiwa kuwa Kwenye Mahusiano ya Kimapenzi na Ex girlfriend wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

Kumekuwa na tetesi kuwa Video vixen ambaye hakauki vituko Kwenye mitandao ya kijamii Irene Geofrey maarufu kama Lynn ana banjuka na Idris Sultan.

Tetesi za Mahusiano ya wawili hao zilianza juzikati ambapo watu wengi walipigia mstari baada ya mwanadada huyo kuposti picha ya Idris huku akiandika maneno ya kimahaba yalisomeka; “Babyboo baby boo bae.”

Baada ya Tetesi hizo kupamba moto Kwenye mitandao ya kijamii gazeti la Risasi Vibes, lilimsaka Lynn ambaye mara moja alikana kuwapo kwa Mahusiano hayo:

Unajua muda mwingine unaweza kuposti kitu halafu maneno yakajiandika yenyewe, sasa ndicho kilichonitokea na mimi sikutaka kufuta kwa sababu watu wangesema ni kiki.

Lakini Idris ni mshikaji wangu wa karibu sana na ninampenda anavyochekesha, watu wasinitengenezee mambo ambayo hayapo jamani“.

Niva Atoa Wosia Mzito "Naomba Kuzikwa na Steve Nyerere"

$
0
0
Niva Atoa Wosia Mzito "Naomba Kuzikwa na Steve Nyerere"
Msanii wa bongo movies Niva amefunguka na kutoa wosia wake na kusema kuwa anaomba endapo atakufa basi msanii Steve Nyerere ashughulikie mazishi yake,Niva ambae siku hizi ameonekana kujigamba na kuongea kwa kujiamini mbele za watu amesema kuwa kwake haina shida na anatamani sana katika mazishi yake yasimamiwe na Steve Nyerere.

Niva anasema kuwa hata  kuna watu wanamsema vibaya na kusema anakula rambi rambi kwake wala hakuna shida ilimradi azikwe kwa heshima kama vile ambavyo Steve amekuwa akijituma kufanya kazi hiyo.

Hata hivyo niva amelaani vikali wale wanaomwita na kumsema Steve nyerere vibaya  na kuwaita wapuuuzi na hawajui wanachokiongea.

Kumekuwa na maneno ya kejeli ya muda mrefu , baadhi ya wasanii wanamsema vibaya Steve Nyerere na kusema kuwa amekuwa akijihusisha katika misiba kwa ajili ya kula pesa za rambirambi.

Ninja Agoma Kuitumia Jezi ya Can­navaro..... Bado Aiweka Kabatini

$
0
0
Ninja Agoma Kuitumia Jezi ya Can­navaro..... Bado Aiweka Kabatini
Jezi ya Yanga yenye namba 23 ambayo Nadir Haroub ‘Can­navaro’ alimkabidhi Abdallah Shaibu ‘Ninja’ aendelee kuitumia baada ya yeye kustaafu kucheza soka, jezi hiyo bado ipo kabatini.

Cannavaro ambaye ni meneja wa Yanga kwa sasa, hivi karibuni alitan­gaza kustaafu kucheza soka akiwa nahodha wa timu hiyo ambapo uongo­zi ulitaka kuistaafisha jezi yake, lakini yeye akakataa na kumkabidhi Ninja.

Ninja ambaye alisajiliwa na Yanga msimu uliopita, bado hajaanza kuitumia jezi hiyo na wikiendi iliyopita kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho dhidi ya USM Alger alivaa jezi yake namba 6 aliyokabidhiwa wakati anatua Yanga.

Kwa mujibu wa Gazeti la Championi, Ninja amesema jezi hiyo anasubiri kuan­za kuitumia kwenye Ligi Kuu Bara msimu huu ambao unaanza leo huku Yanga ikicheza ke­sho Alhamisi dhidi ya Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar.

“Unajua jezi niliyoachiwa na Cannavaro siwezi kuitumia kwenye michuano ya kimataifa kwa sababu kule natam­bulika ninaitumia jezi namba 6, lakini msimu wa ligi ukianza rasmi ndiyo nitaanza kuitumia.

“Ni jambo zuri kuo­na nimekabidhiwa jezi hii na mkongwe am­baye anaamini nitaitendea haki, hivyo nitajipanga kuhakikisha simuangushi,” alisema Ninja ambaye Ko­cha Mwinyi Zahera ameanza kumtumia kama kiungo lakini pia beki wa kulia.

Watanzania Hawajui Kutumia Mitanda Itunufaishe Tunatumia Kwenye Upuuzi- Ray C

$
0
0
Watanzania Hawajui Kutumia Mitanda Itunufaishe Tunatumia Kwenye Upuuzi- Ray C
Mwanamuziki mkongwe nchini Tanzania, Ray C amedai kwamba asilimia kubwa ya watanzania hawajui kuitumia mitandao ya kijamii ipasavyo ili iwaingizie fedha, na badala yake wanaitumia kwa kujadili mambo yasiyo na tija kwa mtu mwenyewe na taifa kwa ujumla.

Ray C ameeleza hayo wakati akizungumza na www.eatv.tv hii leo Agosti 23, 2018, na kusema watu wengi wamekuwa wakipoteza muda na fedha zao kuingia kwenye mitandao hiyo bila ya kufikiria ni jinsi gani itaweza kuwarudishia faida.

"Watu wengi mitandaoni wanapenda upuuzi, ukiweka kitu cha maana hakuna mtu ambaye ata 'comment' chochote katika hicho ulichokiweka, maana wanakichukulia poa lakini fanye kinyume chake hapo ndio utawajua walipo. Wenzetu Ulaya mitandao ya kijamii kama wakina Kim Kardishian na wengine wanatumia mitandao hiyo kuuza 'product' na kuonyesha kazi zao ili wapate pesa...

lakini sisi ndio tumekuwa wakutoa pesa kwa kununua bando ili tukaharibu, tena sana sana Tanzania hatujui kutumia mitandao ili itunufaishe na badala yake tunatumia kwenye upuuzi", amesema Ray C.

Mbali na hilo, Ray C amedai hasumbuki na maneno ambayo amekuwa akizungumziwa kwenye mitandaoo ya kijamii kwa kuwa ana wafahamu watanzania vizuri jinsi walivyo.

"Huwezi kuzuia watu kuongea wanachokifikiria, Nikiingia kwenye mitandao ya kijamii siendi tu kukurupuka na kuweka kitu chochote bila ya kuwa na uhakika wa jambo fulani. Lakini wenye akili pungufu wanaweza wasinielewe ninachokizungumza ila wale wenye akili timamu watakuwa wananielewa", amesisitiza Ray C.

Kauli hizo za Ray C zimekuja baada ya siku za hivi karibuni kushambuliwa kwenye mitandao ya kijamii, baada ya yeye kuonekana kimbele mbele katika kila jambo licha ya kutokuwa muhusika katika hilo, na kufanya watu wadai pengine anatafuta kiki ili aweze kuendelea kuwa gumzo kwenye midomo yao.

Breaking News: Bobi Wine Akamatwa Tena Muda Mfupi Baada ya Kuondolewa Mashtaka

$
0
0
Breaking News: Bobi Wine Akamatwa Tena Muda Mfupi Baada ya Kuondolewa Mashtaka
Mbunge wa Kyadondo nchini Uganda Robert Kyagulanyi maarufu Bobi Wine amekamatwa muda mfupi baada ya mahakama ya kijeshi kumuondolea mashtaka ya umiliki haramu wa silaha nchini.

Muda mfupi baada ya kuachiliwa huru, Wine alikamatwa tena na inaarifiwa kwamba anatarajiwa kushtakiwa katika mahakama ya hakimu mkuu kujibu mashtaka ya uhaini pamoja na wabunge wengine waliokamatwa.

Mbunge huyo ambaye pia ni mwanamuziki nchini kwa jina maarufu Bobi Wine leo aliwasilishwa katika mahakama ya kijeshi mjini Gulu kaskazini mwa Uganda.




Rapper 50 Cent Amsifia Nick Minaj Licha ya Kuchanwa Vibaya na Mrembo Huyo

$
0
0

Rapper 50 Cent amekuwa wa kwanza kujibu kati ya male rappers kadhaa waliochanwa kiutani na Nicki Minaj kwenye wimbo wake wa hivi karibuni 'Barbie Dreams' kutoka kwenye album ya QUEEN.

Kwenye mahojiano na 'Extra' kupitia Hip Hop N More, 50 Cent ameweka wazi hisia zake juu ya wimbo ule kwa kuupa alama 100. Alisema: "Nimeupenda ule wimbo, niliwahi kufanya wimbo unaitwa 'How to Rob' na aliwahi kusema mwenyewe (Nicki Minaj) kuwa alivutiwa nao sana." alisema 50 Cent na kumsifia Nicki kwa uandishi wake wa mtindo wa mtazamo tofauti yaani kinyume (reverse perspective)

Aliongeza pia kuwa 'Barbie Dreams' inaonesha wazi kabisa kuwa wanawake kwenye Hip Hop wameanza kuchukua nguvu kutoka kwa wanaume - Swipe kuona interview hiyo.

Kwenye dude hilo, 50 Cent alichanwa kwenye line isemayo: "I tried to fk 50 for a powerful hour, but all that ni*a wanna do is talk 'Power' for hours." alichana Nicki.

Wengine waliotajwa kwenye wimbo huo ni Drake, Meek Mill, DJ Khaled, na wengine kibao.

Tunatibu Na Kuponesha Kabisa Upugufu wa Nguvu za Kiume, Busha, Kisukari na Vidonda vya Tumbo

$
0
0

TUNATIBU NA KUPONESHA KABISA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME UUME MDOGO? BUSHA BILA KUPASUA KISUKALI NA VIDONDA VYA TUMBO? asilimia kubwa ya wanaume wanaupungufu wa nguvu za kiume NA maumbile madogo

NI NINI KINACHOSABABISHA UUME KUZIDI KUWA MDOGO NA WEMBAMBA 1 kuugua chango LA uzazi 2 unene kupita kiasi 3 kuvaa nguo au chupi za kubana 4 kupiga punyeto kwa mda mrfu ,NI NINI TIBA YAKE MAKAKANUA MIX nidawa ya mitishamba iliyochanganywa NA mizizi kumi NA mbili urfusha NA kunenepesha UUME saizi upendayo ich 5,6,7, NA 8 kwa urfu NA sentimita 3,4, na 5 ipo dawa ya kunywa na kupaka NI NINI KINASABABISHA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME 1 kupungukiwa kwa homoni ya testerone 2 kuhudhurika kwa Neva au uti wa mgongo 3 utumiaji holela wa madawa ya kizungu 4 usongo wa mawazo na asira 5 utumiaji wa vyakula vya mafuta mengi NI NINI TIBA YAKE MAPRO POWER NO 2 NDIO tiba tosha kwa sasa kwani utibu matatizo matatu kwa pamoja 1 itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15 adi 20 ,2 itakufanya urudie tendo zaidi Mara tatu 3 uhimalisha uume uliolegea na kusinyaa OKOA NDOA YAKO SASA ujihepusha na lawama ndani ya ndoa yako au pale ukutanapo na mpezi dawa hii itamfanya mpenzi wako hakueshimu na hasitoke nnje ya ndoa na ata wazee wenye umri mkubwa wanapona zipo dawa za kupunguza kitambi,minyama uzembe, presha ,kisukar mvuto wa mpezi au biashara

FIKA OFISINI KWETU MBAGALA ZAKHEMU na wateja wa kanda ya ziwa yupo wakala wetu mwanza mjini au piga simu 0752348593

DR MABULA na utaletewa popote ulipo uduma hizi

Ray C "Wabongo Mitandaoni Wanapenda tu Vitu vya Kijinga vya Maana Holla"

$
0
0

Mwanamuziki mkongwe nchini Tanzania, Ray C amedai kwamba asilimia kubwa ya watanzania hawajui kuitumia mitandao ya kijamii ipasavyo ili iwaingizie fedha, na badala yake wanaitumia kwa kujadili mambo yasiyo na tija kwa mtu mwenyewe na taifa kwa ujumla. 

Ray C ameeleza hayo wakati akizungumza na www.eatv.tv hii leo Agosti 23, 2018, na kusema watu wengi wamekuwa wakipoteza muda na fedha zao kuingia kwenye mitandao hiyo bila ya kufikiria ni jinsi gani itaweza kuwarudishia faida. 

"Watu wengi mitandaoni wanapenda upuuzi, ukiweka kitu cha maana hakuna mtu ambaye ata 'comment' chochote katika hicho ulichokiweka, maana wanakichukulia poa lakini fanye kinyume chake hapo ndio utawajua walipo. Wenzetu Ulaya mitandao ya kijamii kama wakina Kim Kardishian na wengine wanatumia mitandao hiyo kuuza 'product' na kuonyesha kazi zao ili wapate pesa... 

lakini sisi ndio tumekuwa wakutoa pesa kwa kununua bando ili tukaharibu, tena sana sana Tanzania hatujui kutumia mitandao ili itunufaishe na badala yake tunatumia kwenye upuuzi", amesema Ray C. 

Mbali na hilo, Ray C amedai hasumbuki na maneno ambayo amekuwa akizungumziwa kwenye mitandaoo ya kijamii kwa kuwa ana wafahamu watanzania vizuri jinsi walivyo. 

"Huwezi kuzuia watu kuongea wanachokifikiria, Nikiingia kwenye mitandao ya kijamii siendi tu kukurupuka na kuweka kitu chochote bila ya kuwa na uhakika wa jambo fulani. Lakini wenye akili pungufu wanaweza wasinielewe ninachokizungumza ila wale wenye akili timamu watakuwa wananielewa", amesisitiza Ray C. 

Kauli hizo za Ray C zimekuja baada ya siku za hivi karibuni kushambuliwa kwenye mitandao ya kijamii, baada ya yeye kuonekana kimbele mbele katika kila jambo licha ya kutokuwa muhusika katika hilo, na kufanya watu wadai pengine anatafuta kiki ili aweze kuendelea kuwa gumzo kwenye midomo yao.

Young Dee "Ile Gari Nimenyanganywa Haipo Tena Mikononi Kwangu"

$
0
0

Rapper Machachari Young Dee Ametoboa siri kuwa kwa sasa ile gari aliyoinunua kwa mil 25 haipo mikononi mwake kwani ilinunuliwa na Uongozi aliyokuwa nayo kipindi cha nyumba hivyo wamechukua gari lao

Young Dee akihojiwa ameweka wazi kuwa kwa sasa anataka kununua Lambogini kama mambo yakimwendea vizuri

Young kwa sasa anakampuni yake inayoitwa Dream City ambayo inasimamia kazi zake pia

Wanaharakati Kenya Waungana Kumpinga Rais Museven wa Uganda

$
0
0

Nchini Kenya wanaharakati pamoja na wanasiasa wamejiunga na wenzao wa Uganda kushinikiza utawala wa rais wa Yoweri Museveni kuzingatia sheria na kuwaachilia huru wafungwa wa kisiasa. Makundi ya kutetea haki za binadamu yamesema yatawasilisha kesi katika mahakama ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ili kuishinikiza serikali ya rais Museveni kuzingatia sheria dhidi ya wafungwa wa kisiasa.
Viewing all 104689 articles
Browse latest View live


Latest Images