Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Wanaume ni Viumbe Wabinafsi Sana na Wasiokuwa na Utu

$
0
0
Najitahidi sana kuamini kuwa wanaume ni wazuri ila kila kukicha naona hawa viumbe ni wanyanyasaji, wabinafsi, hawana utu, wauwaji, wabakaji, wanyaganyi, wauwaji, roho mbaya.

Nitaendelea kuamini wanawake ndiyo chachu ya maendeleo hasa kwa watoto wao.

Mtabishana a mimi lakini ndiyo ukweli wenyewe baba anatelekeza watoto anamwachia mama. Mama kwa kujali na upendo anaamua kupambana na baba atoe matumizi ya familia ada ya shule huku lijianaume likiwa libishi kuendekeza ufuska tu.

Leo hii nyie nyie wanaume mnakuja na viutafiti vyenu eti watoto wliolelewa na mzazi mmoja wanatatizo mfyuuu hata aibu hamna.

Asilimia kubwa ya watoto wengi ni mapambano ya mama kuvumilia uozo wote wa baba na kujitahidi kukufanya kama ulivyo mwisho wa siku mnajifanya kufanya utafifi.

Suluhisho kila mwanaume anayetia mwanamke mimba ahakikishe anakuwa bega kwa bega na mama hata kama unanyimwa papuchi, hata kama hupendi mama, matatizo yako na mama yasipelekee shida kwa watoto.

I real hate you men

Mtemvu: Umri wa Binti yangu Miss Tanzania ni Siasa za Wapinzani Wangu Ndani ya CCM

$
0
0
Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu amedai kwamba sakata la binti yake, Sitti Mtemvu, kudaiwa kuchakachua umri linachochewa na wapinzani wake wa kisiasa ndani ya CCM. Mtemvu alisema hayo wakati alipokuwa anamtetea binti yake ambaye amedanganya umri ili aweze kushiriki mashindano ya Miss Tanzania. Binti yake huyo anadaiwa kuwa kijeba lakini aligushi cheti cha kuzaliwa ili kupunguza umri uliomwezesha kushiriki mashindano ya u-miss.

Chanzo: Clouds Radio

MAONI YANGU
Waliozoea kuishi kwa uongo ukweli hawauwezi - Tundu Lissu

Sitta Afunguka na Kusema 'Mbunge Sugu Siyo Saizi Yangu'

$
0
0
Mwenyekiti wa lililokuwa Bunge la Katiba, Samuel Sitta amesema hakuwahi kukaa na kuuahidi upinzani serikali tatu.

Sitta alisema hayo jana ikiwa ni siku moja baada ya Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ kukaririwa na gazeti hili akisema kuwa, Sitta aliwasaliti wapinzani baada ya kuwafuata kuomba kura za uenyekiti wa Bunge la Katiba ili atetee serikali tatu lakini baadaye akawageuka.

Katika mchakato wa kumpata mwenyekiti wa Bunge hilo, Sitta ambaye pia alikuwa Spika wa Bunge la Tisa, alionekana kukubalika na pande zote; chama chake cha CCM na wapinzani jambo lililomfanya kushinda kiti hicho kirahisi kwa kupata asilimia 86.5 dhidi ya mpinzani wake Hashim Rungwe aliyepata asilimia 12.3.

Sugu alisema Sitta alimfuata na kumwomba ampigie debe kwa vijana ili akishinda atekeleze pamoja na mambo mengine, madai ya serikali tatu yaliyotolewa na wajumbe wa upinzani.

Akizungumzia suala hilo Sitta alihoji, “Sugu ni mtu gani kwangu mimi hata nimtafute? Nikitaka kuongea na Chadema nitamtafuta (Freeman) Mbowe au (John) Mnyika na si Sugu, hata sijui tulikutana wapi na yeye,” alisema Sitta.

Sitta ambaye pia ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki alisema hakuwahi kumwahidi mtu yeyote kitu chochote wakati wa kampeni zake ya kuwania uenyekiti wa Bunge hilo la Katiba.

“Mimi ni mtu wa kujitegemea na kusimamia haki na ndicho nilichofanya, sasa hayo anayosema huyo sijui katoa wapi,” alisema Sitta na kuongeza: “Nakanusha vikali kuhusu suala hilo analosema Sugu.”

Alisema kuna wabunge kama (Joshua) Nassari ambao walikuwa wanakubali sera zake na hivyo kumpigia kampeni za kuwania nafasi hiyo ya kuongoza Bunge la Katiba lakini si kama anavyosema Sugu hivi sasa.

Sitta alisema ni muhimu wapinzani wakaacha kupiga kelele na badala yake wasubiri Kura za Maoni ya Katiba Inayopendekezwa.

“Tusubiri Kura ya Maoni ndiyo waseme huko na si kupindisha mambo kwa kuwa wanaongea tu vitu ambavyo havipo,” alisema Sitta.

Vita Nzito Mbili Kubwa Hapa Mjini: Ali Kiba Vs Diamond na Clouds FM na Times FM

$
0
0
Stori: Erick Evarist, Musa Mateja na Chande Abdallah
MTIFUANO! Tamasha la Serengeti Fiesta 2014 limepita lakini nyuma yake limeacha vita nzito iliyowahusisha mafahari wawili, Nasibu Abdul ‘Diamond’ na Ali Kiba huku waandaaji wa tamasha hilo, Clouds FM wakisigana na Times FM kumgombea msanii wa Nigeria, David Adedeji Adeleke ‘Davido’, Risasi Mchanganyiko linakupa mchongo kamili.


TIFU LILIVYOKUWA
Kwenye shoo hiyo iliyofanyika wikiendi iliyopita katika Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar, mashabiki wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa Ali Kiba (Team Kiba), walipiga kelele za ‘buuu’ pale alipopanda Diamond kutumbuiza ili kumharibia.

CHANZO CHANENA
Chanzo makini kimedai kuwa, vurugu hizo hazikutokea kwa bahati mbaya bali zilipangwa na wafuasi wa Kiba ambapo inasemekana ziliandaliwa gari aina ya Toyota-Costa zipatazo 25 zilizokuwa zimejaa watu na kwenda kuwamwaga viwanjani hapo kwa shughuli mbili muhimu; kuzomea na kuhamasisha wengine wazomee pindi Diamond atakapopanda jukwaani.

“Ishu ilipangwa, Team Kiba waliibuka na Costa kama 25 hivi, wakajipanga katika maeneo tofauti ya uwanja huo lakini zaidi walikaa karibu na jukwaa ili kuweza kutimiza vizuri azma yao ya kuharibu pindi Diamond atakapokuwa akitumbuiza,” kilidai chanzo hicho.

WALIFANIKIWA?
Kwa namna moja mashabiki hao walionekana kufanikiwa kwani waliweza kuwashawishi watu wengi wazomee kiasi cha kumfanya Diamond ashtukie  na kuamua kutamka hadharani: “Jamani kuna uhuni unaendelea hapa.”


TEAM DIAMOND WACHARUKA
Madai yanasema mara baada ya Team Kiba kufanya vurugu hizo na kufanikiwa, baadhi ya mashabiki ambao waliaminika ni wa Diamond (Team Diamond), walicharuka na kusema hawakubaliani na uhuni huo ambao umefanywa hivyo watahakikisha wanapambana kulipiza kisasi kwa namna yoyote ile.
“Hatukubali, wao si walijipanga hapa kumharibia Diamond, sasa na sisi tutahakikisha tunalipiza kisasi kwa namna yoyote,” walisikika wakisema mashabiki wa Diamond.

TALE AKIRI KUSIKIA
Paparazi wetu aliwatafuta Diamond na Kiba ili kujua wanazungumziaje vurugu hizo. Baada ya kumtafuta Diamond bila mafanikio, alipatikana meneja wake, Hamis Taletale ‘Bab Tale’ ambaye alikiri kuwepo kwa maandalizi ya zomeazomea ambayo yalikuwa na lengo ya kumharibia msanii wake.

“Hizi kwetu tumezichukulia kama changamoto, tulisikia kwamba kuna watu wamelipwa kwa ajili ya kufanya fujo lakini hatukujali sana kwani lengo letu si kugombana na mtu, sisi tunafanya muziki mzuri ambao ndoto zetu ni kuufikisha katika levo za Kimataifa,” alisema Bab Tale.

KIBA ANAHUSIKA?
Alipotafutwa Kiba kuzungumzia suala hilo alikataa kuhusika nalo na kudai halina ukweli wowote kwani si rahisi kuwalipa pesa mashabiki wengi kiasi kile waliojitokeza uwanjani.
“Hiyo si kweli ni uzushi tu, sasa mimi nitawalipa nini hao mashabiki wote waweze kumzomea huyo Diamond? Siyo rahisi. Kwanza mimi nifanye hivyo ili iweje? Mimi si mtu wa kushindana na Diamond hata siku moja, nafanya muziki wangu, mashabiki wanauelewa, nashukuru Mungu kwa hilo,” alisema Kiba.

CLOUDS FM VS TIMES FM
Kwa upande mwingine, vita nzito ilizidi kutokota kupitia tamasha hilo baada ya msanii Davido kupanda jukwaani na kutumbuiza ilhali akiwa amewekewa pingamizi la kibali kutoka Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) sambamba na zuio la Mahakama ya Kisutu lililowekwa na Redio Times FM waliodai kuwa na mkataba wa kufanya shoo na msanii huyo Novemba, mwaka huu Bongo.

TIMES WANASEMAJE?
Mkurugenzi wa Redio Times FM, Rehure Nyaulawa alipotafutwa kwa simu kuhusiana na suala hilo alisema mahakama ilishaweka pingamizi, anashangaa kuona msanii huyo alipanda jukwaani lakini akasema hawezi kukaa kimya, atakwenda mbele zaidi ili haki itendeke.

CLOUDS JE?
Kwa upande wao, Clouds walipotafutwa hawakupatikana hewani lakini kimsingi na wao wana hoja zao ambazo zitabainika pindi kesi hiyo itakapoanza kusikilizwa.

Hata hivyo, kuna madai kwamba, zuio la Davido kutopanda jukwaani Leaders Club lilipelekwa na mahakama kwa Clouds Media Group wakati Tamasha la Fiesta linaandaliwa na Kampuni ya Primetime Promotion, kwa hiyo barua hiyo ilikuwa ‘missing in action’.

Baby Madaha 'Nawapanga tu Wanaume'

$
0
0
Stori: Gladness Mallya

MSANII wa muziki na filamu Bongo, Baby Madaha ambaye anadaiwa kuishi kinyumba na meneja wake Mkenya, Joe Kariuki wa Kampuni ya Candy n Candy Records, ametoa mpya baada ya kudai kuwa kutokana na kusubiri kwa muda mrefu ili apate mwanaume anayefaa kwa ajili ya kumuoa bila mafanikio, sasa ameamua kuwapanga foleni bila kujali idadi yao.

Akipiga stori na gazeti hili juzikati, Baby Madaha alisema amesubiri sana kuolewa lakini hajamuona mwanaume anayefaa, hivyo ameamua kuwapanga kama mafungu ya nyanya kama wao wanavyowapanga wanawake na ikitokea mmoja  ‘akamzingua’ anaachana naye na kumchukua mwingine.

“Mimi sasa hivi nawapanga tu wanaume maana sioni anayenioa ndiyo maana nimechukua uamuzi huu, wanaume wamezoea kutupanga sisi wanawake sasa mimi ndiyo nimewageuzia kibao nao waone utamu wake na ikitokea huyu amenizingua namuacha nahamia kwa mwingine,”alisema Baby Madaha.

Dida na Edzen Wakutana Coco Beach Laivu, Wachuniana kama Hawajuani

$
0
0
Stori: Mayasa Mariwata na Shani Ramadhani
WATANGAZAJI wawili waliokuwa wanandoa kabla ya kutengana hivi karibuni, Khadija Shaibu ‘Dida’ na Ezden Jumanne, mwishoni mwa wiki walikaushiana kama watu wasiofahamiana baada ya kukutana katika hafla iliyofanyika katika ufukwe wa Coco jijini Dar es Salaam.

Wawili hao walikutana wakati wa uzinduzi wa video ya wimbo wa Namchukua wa Zuwena Mohamed ‘Shilole’ ambapo mwanaume alikuwa mshereheshaji huku mke akiwa miongoni mwa wageni waalikwa.


Hata hivyo, Dida alionekana kuwa na mbwembwe zaidi huku akipiga ulabu na kuonekana kukolea kiasi cha kujiachia na kukata mauno mbele ya halaiki ya watu pasipo kujali uwepo wa mumewe huyo wa zamani, ambaye alikuwa mpole na aliondoka eneo hilo mara tu baada ya kumalizika kwa shughuli iliyompeleka.
GPL

Mahabusu Mwingine afariki Dunia Kwa Madai ya Kupigwa Askari Kituoni

$
0
0

Alfred aliyekuwa mkazi wa Sinza jijini hapa, alifikishwa kituoni hapo kwa kosa la wizi wa kuaminiwa na kuwekwa mahabusu wakati akisubiri kufikishwa mahakamani juzi(Jumatatu) ili kusomewa mashitaka yake.

Dar es Salaam
Mahabusi Daniel Alfred katika kituo cha Polisi Urafiki, eneo la Ubungo, amefariki dunia kwa madai ya kupigwa na baadhi ya askari wa kituo hicho.

Alfred aliyekuwa mkazi wa Sinza jijini hapa, alifikishwa kituoni hapo kwa kosa la wizi wa kuaminiwa na kuwekwa mahabusu wakati akisubiri kufikishwa mahakamani juzi(Jumatatu) ili kusomewa mashitaka yake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura jana alithibitisha kutokea kwa kifo hicho, huku akisema kijana huyo alikuwa akifanya fujo na kuwapiga wenzake wakati akiwa chumba cha mahabusu.

Kamanda Wambura alisema kuwa baada ya kifo chake waliupeleka mwili wake hospitali.

Wambura alisema ripoti ya daktari baada ya uchunguzi, ilionyesha kwamba mahabusi huyo alikuwa mgonjwa.

Shuhuda ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini, alisema alikwenda kituo hapo kumuona ndugu yake lakini alikuta askari wakimpiga.

“Mimi sijui kama alikuwa na matatizo ya kiafya, lakini niliona akipigwa sana na askari wa kituo hicho...yaani inasikitisha sana, jamaa alipigwa kama mpira wa gombania goli, mimi nilikuwa najua kituo cha polisi ndiko usalama wa watuhumiwa unapatikana kumbe hapana ndiyo maana nikaja kuwaeleza nilichokiona,” alisema mtoa habari huyo.

Alisema hata kama kijana huyo alikuwa mgonjwa, anaimani kuwa aliuawa na polisi kwa kipigo kikali.

Rais Jakaya Kikwete Kutunukiwa U-Profesa na Rais wa China

$
0
0
Chuo kikuu cha kilimo nchini China kinatarajia kumtunuku Shahada ya juu ya U-profesa Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete.

Bila shaka ni kwa kutambua mchango wake wake mkubwa kwa mapinduzi makubwa ya kilimo nchini.

Hongera PROFESSOR JAKAYA KIKWETE.

Naseeb Abdul maarufu kama Diamond anashikiliwa na Polisi

$
0
0
MSANII Naseeb Abdul (Diamond) leo anashikiliwa na polisi, siku moja tu baada Meneja wake Babu Tale kuhojiwa na kulala mahabusu kuhusiana na matumizi ya mavazi ya kijeshi katika onyesho la Fiesta mwishoni wiki.

Q Chief Afunguka Kuhusu Bifu la Diamond na Ali Kiba, Haya Ndo Mambo Makubwa Matatu Aliyoyasema

$
0
0
Mapya yanazidi kuibuka kuhusu ushindani wa Diamond na Ali Kiba amba ulianzia katika hitimisho la tamasha la Fiesta lililofanyika katika viwanja vya Leaders Club Dar. Mashabiki wa wasanii hawa wawili wanavutana huku kila mmoja akisema mwenzake ana kipaji na anamfunika mwenzake. Inasemekana kua kuna baadhi ya mashabiki walikodiwa kwa ajili ya kumzomea Diamond wakati akitoa burudani siku ya Fiesta na hilo lilithibitishwa na Babu Tale ambaye ni meneja wa Diamond.

Mwandishi : kwa sasa katika mziki wa BongoFlava kumekua kuna fitini nyingi wakati mwingine wasanii kwa wasanii wanachonganishwa na mwisho wa siku unakua ugomvi, kwa mfano sasa hivi bifu la Ali Kiba na Diamond. Je Q Chie unalizungumziaje hili?

Q Chief : Yote wanayopitia ni changamoto ambazo pengine hawakuwahi kuzania kwamba watapitia. Mi nmepitia situation ambazo zimenijenga kua sugu na Legendary ndio maana ya kua mkongwe unapitia situation ambazo watu wengine wanakufosi ufike huko. Hata kama upo level fulani wanakushusha kwa kufikiria kwamba wanaweza kukushusha. unapandishwa na watu, unapandishwa na mwenyezi Mungu, unashushwa na watu, unashushwa na mwenyezi Mungu. Mfano nimekua nikiangalia Fiesta kwenye TV sikwenda kwa sababu nlikua na mambo yangu Studio, hakuna kitu kigeni nlichokiona, nmeona msanii wa marekani anafunikwa na msanii wa Tanzania ambaye ni Ali Kiba. Nmeona Ali Kiba ambaye amekaa kimya kwa miaka mitatu bila Airtime na watu wamemzungumzia vibaya, vizuri na nini wamemkubali tena. Ikiwa ni mtu yule yule ambaye wamemkataa na wakumuweka mtu mwingine juu. Hakuna kitu kisichowezekana, matokeo uliyoyaona juzi ndio matokeo yanayotokea na yataendelea kutokea. Hakuna Mungu wa hii kazi, hakunaga mfalme wa hii kazi ila kuna masultan wa Hii Kazi.
~Credits:Bongoclan

Mwanamuziki Diamond Aachiwa Kwa Dhamana Baada ya Kukamatwa Kwa Kesi ya Kuvaa Nguo za Jeshi

$
0
0
Taarifa zinazomhusu msanii Diamond Platnumz kuhojiwa na jeshi la Polisi hii leo zimeenea sana kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, kuanzia jana (tarehe 21 Oktoba) meneja wa msanii huyo Babu Tale amekua akihojiwa na polisi mpaka alipoachiwa kwa dhamana mapema jana saa 5.
Vile vile msanii Diamond aliripoti polisi mapema jana kwa ajili ya kuhojiwa, ambapo baada ya kuhojiwa msanii huyo ameachiwa kwa dhamana .
Hii ni picha ikimuonesha msanii Diamond akitoka kuhojiwa na jeshi la polisi.

Lemutuz Acharuka 'Sitti Mtemvu Rudisha Taji uokoe Taifa Mimi Sina Shida na Ubunge wa Baba Yako'

$
0
0
Leo Asubuhi Mzee Mzima Lemuz Ameamka na Haya Kuhusu Miss Tanzania, Nanukuu Kutoka Kwenye Instagram yake @Lemutuz_nation

"Good Morning Instagram Nation....I mean cheti cha kuazaliwa umekipata mwezi uliopita infact siku 35 tu zilizopita leo.unaulizwa kwa nini cheti kile HAKIFANANI NA tarehe za kuzaliwa kwenye passport yako....unasema jawabu ni sikujipanga kujibu hayo maswali ya binafsi.....lakini kwenye stage ulijibu mpaka.Kifaransa? I mean to add salt to the injury Baba yako anasema tunaojaribu kuuliza aidha tunataka Ubunge wake au tunatumwa na wanaotaka Ubunge wake?......halafu Uncle Lundemga hajawahi hata mara moja kutangaza mshindi wa Miss Tanzania ilikuwaje siku ile.akapanda na kutangaza yeye? Na kuishia kutuletea Taifa huu mpasuko?.....halafu kwenye ile.press wote mnajibu kwa mahasira mmemkasirkia nani na mmelikoroga wenyewe sasa ni wakati wenu wa kulinywa......yaani sisi.wa Tanzania wote tumekubaliana KUKUCHUKIA Sitti? PLEASE HAYA MMEYATAKA WENYEWE HAKUNA MWENYE CHUKI WALA.WIVU NA WEWE......TAJI ULILOPEWA SIO.LAKO SIMPLY AS THAT KAMA NI LAKO ......huwezi leo.October ukaja na cheti cha kuzaliwa ulichopata just mwezi uliopita na hakifanani na passport...eti wabongo tunatakiwa kujua kuwa.huwa unasafiri sana kwa.hiyo tusishangae kusikia umepoteza cheti cha kuzaliwa hahahahahhaha......hivi siku hizi ukisafiri sana ni lazima upoteze cheti cha kuzaliwa basi Rais wetu atakuwa na vyeti vingi sana vipya vya kuzaliwa U know..... Mnasema uongo ambao.hata haukupimwa kabisa....SITTI THE RIGHT THING TO DO NI RUDISHA TAJI TU LIOKOE TAIFA NA THIS MESS mimi wala.sina shida na ubunge wa baba yako cause ninaishi Ilala U know! GUYS WE HAVE TO KEEP ON PRESSING KUANZIA LEO NINAMTAFUTA WAZIRI ALIYEHUSIKA NA KATIBU MKUU WA CCM MZEE KINANA NITAWAFAHAMISHA KINACHOENDELEA! ASUBUHI NJEMA LOVE U GUYS!" - Le Mutuz

T.I 'Tanzania ilikuwa Mzuka Sana, Sikuona Dalili yoyote ya Kuwepo Ebola

$
0
0
Baada tu ya kutua Marekani akitokea Tanzania, waandishi wa habari wa TMZ walimtime kwenye uwanja wa ndege na kumuuliza suala ya kusuluhisha beef ya Iggy Azalea na Snoop Dogg pamoja na show yake ya Dar es Salaam.

How was Tanzania man?” mwandishi wa TMZ aliuliza na T.I. kujibu: It was awesome man, it was an awesome experience.”

“Did you have to take any precaution about the Ebola stuff going on,? aliuliza mwandishi.

“I mean man for real, it never came up, I never saw any signs of it, I never saw anything me think of it, except for ignorant comments on my timeline,” alijibu T.I. akimaanisha comments za Instagram kuhusu Ebola.

See Video:
~Bongo5

Wema Sepetu Aponda Raha China Huku Diamond Akiugulia Machungu ya Fiesta

$
0
0
WAKATI bebi wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiugulia maumivu ya kuzomewa na mamia ya mashabiki wa muziki katika Tamasha la Fiesta jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wikiendi iliyopita, Wema Sepetu ‘Madam’ anaponda raha ya maisha nchini China, Amani lina full data.

Chanzo makini kilicho ‘kloz’ na muigizaji huyo nyota wa filamu nchini, kimesema Wema alipaa na ndege ya Emirates wiki iliyopita, siku chache kabla ya Tamasha la Fiesta, akiwa ameandamana na wanaume wawili, ambao ni meneja wake, Martin Kadinda na Petit Man, wote wakiwa wamekaa daraja la kwanza la dege hilo.

Chanzo hicho kilizidi kunyetisha kuwa gharama zote za safari hiyo zilibebwa na Madam mwenyewe na kwamba baada ya kufika katika jiji la Guangzhou nchini humo, Wema na wanaume hao wawili walichukua vyumba katika Hoteli ya Holiday Inn, inayotajwa kuwa moja ya hoteli ghali zaidi huko China.

“Yaani Wema jamani ana mambo, inavyoonekana lile rhumba la wakati ule ameshalisahau, amesahau kabisa kama alishafulia, sasa Mungu kamjaalia kapata pesa anavyoitapanya ovyo mpaka roho inauma. Wewe fikiria mtu amekwenda kuchukua vifaa vya biashara, unakwenda na hao wanaume wa kazi gani kama siyo kupoteza fedha tu,” kilisema chanzo hicho.

Inadaiwa kwamba kilichompeleka Wema katika nchi hiyo yenye watu wengi zaidi kuliko yoyote duniani, ni ununuzi wa vipodozi, kwani ana mpango wa kufungua duka kubwa katika eneo ambalo halijatajwa jijini Dar es Salaam.

Baada ya kufika huko, chanzo kinasema kuwa watu hao watatu wamekuwa wakiishi maisha ya starehe, wakila bata katika klabu mbalimbali za usiku, ambako wanajichanganya na watanzania wengine kuponda raha.

“Kwa matanuzi anayofanya kule, hata hiyo biashara aliyoifuata haina maana, angekuwa mtu mwenye nia ya biashara kweli, angetafuta tu hoteli ya kawaida ili kubana matumizi aweze kuja na mzigo mkubwa, sasa wewe mwenyewe fikiria, hii wiki ya pili sasa, tena na wanaume wawili wanakutegemea, hizo pesa si kuzitapanya tu jamani,” kilisema chanzo hicho kikionyesha kutofurahishwa na maisha ya staa huyo.
GPL

Majambazi Wavamia Benki ya Stanbic Tawi la Mayfair, Msasani na Kupora Kiasi Kikubwa cha Pesa

$
0
0
Benki ya Stanbic tawi la Mayfair, Msasani, Dar, leo imevamiwa na watu wanaodhaniwa kuwa majambazi na kupora kiasi kikubwa cha pesa. 

Wamekuja na Noah nyeusi wakapark kama wateja. Walikua wawili, mmoja akapanga msitari mwingine akaenda kujaza fomu za kuchukulia hela. Yule alopanga msitari akafunga mlango na yule Askari akakunjwa akanyang'anywa alarm. Yule alokuwa anajaza fomu kawambia wateja nyote lala chini, alikua anamjua mwenye ufunguo, wakasema Anna leta huo ufunguo. Akataka kugoma walipomnyoshea mtutu akatoa. wakaingia Kwenye chumba cha hela wakakomba hela zote wakapakia kwenye Noah. 

Wakawaaga na kusema iteni hao Polisi wenu. Hamna aliyeumizwa zaidi ya Askari kukunjwakunjwa alipotaka kubonyeza alarm.

In Kidhungu:

Today at stanbic mayfair plaza:

...Gang of armed robberies, arrest security guard, took the remote buton and proceed to strong room key custodian who was coming from wash room they open the strong room and ATM took all money Customers, USD 175,000/-, Euro 260,000, £190,Tzs 186mil. ATM 30mil....

Staff and our guard locked in strong room and they left keys at bank counter. Initial investgtn shows there was an inside job, why teller's didn't press alarm at first when security guard kept under arrest of robberies? They ran away by car...

all staff being sent to Police for statements.

Updates: Kesi ya Kulawiti na Kutuma Picha Katika Mitandao ya Kijamii inayowakabili Watu Wawili

$
0
0
SHAHIDI wa kwanza katika kesi ya kulawiti na kutuma picha katika mitandao ya kijamii inayowakabili wakazi wawili wa Mbagala, Dar es Salaam, alidai kwamba alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na mlalamikaji kwa miaka saba huku akiwa na mume wake ambaye ni mshitakiwa namba moja katika kesi hiyo.

Sanifa Sadick alidai mbele ya Hakimu Mfawidhi Saidi Mkasiwa kuwa mshitakiwa Erick Kasira (39) ni mume wake tangu mwaka 2006 na kwamba wana watoto wawili huku mshitakiwa wa pili, Juma Richard ni shemeji yake.

Alidai kwamba Agosti 23 mwaka huu, waliwasiliana na mlalamikaji huyo ili wakutane katika nyumba ya kulala wageni inayojulikana kama Maembe Bar & Guest House iliyopo Yombo Kiwalani kwa ahadi ya kusaidiwa Sh 100,000.

Akiongozwa na Wakili wa Serikali, Sylvia Mitanto, shahidi huyo alidai muda wa saa 7 mchana alimuaga mume wake kwamba anaenda kununua bidhaa za saluni.
Alidai kwamba alichukua usafiri wa pikipiki maarufu kama bodaboda huku mlalamikaji akimuelekeza kwa njia ya simu.

Sanifa alidai kwamba wakati anaelekea Yombo kulikuwa na mwendesha pikipiki ambaye alikuwa anamfuatilia kwa nyuma hadi eneo hilo.

Alidai kwamba alimkuta mlalamikaji akiwa peke yake na kuagiza kinywaji baadaye walichukua chumba namba sita na kuingia ndani; baada ya muda mlango wa chumba hicho uligonjwa ndipo alimuona mumewe akiingia pamoja na vijana watatu.

‘’Sikuweza kuwatambua wote lakini hawakuwa na silaha zaidi ya simu. Mpenzi wangu aliulizwa na mume wangu kuwa anafanya nini na mimi, naye alimjibu kuwa asiniache kwani atampa gharama yoyote ndipo waliandikishiana kutoa Sh 500,000 ,’’ alidai Sanifa.

Alieleza mlalamikaji kuwa alikuwa na kompyuta na kwamba alimwambia Erick akae nayo hadi atakapompatia fedha hizo walizoahidiana.

Alidai kwamba alikuwa amejificha chooni na kusikia kwamba wanaume hao wanamtaka mlalamikaji afanyiwe kinyume na maumbile na kwamba walimvua nguo zote huku aliyekuwa mwendesha bodaboda akiwa anapiga picha.

Alidai baada ya tukio hilo alikimbilia nyumbani na kukuta simu aina ya Tecno nyumbani kwake na kuiweka laini yake baadaye dada yake alimtumia picha ikimuonesha mlalamikaji akiwa utupu.

Alieleza kwamba mlalamikaji alimpigia simu Erick na kumwambia aende akachukue fedha alizoahidi kutoa wakati akifumaniwa na mke wa mshitakiwa huyo na kwamba mshitakiwa huyo aliondoka pamoja na ndugu yake Richard.

Alidai walipofika Tandika, waliwekwa chini ya ulinzi na Erick alimpigia simu mkewe kumtaarifu kwamba amekamatwa na polisi naye alipofika aliwekwa chini ya ulinzi. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Novemba 3 mwaka huu itakapoendelea kusikilizwa.

CHANZO: Habari Leo

Baraza la Sanaa (BASATA) Kumvua Taji Miss Tanzania 2014 kwa Kudanganya Juu ya Umri Wake

$
0
0
Sakata la lililojitokeza la mrembo wa Taifa wa mwaka huu 'Redd's Miss Tanzania 2014', Sitti Mtemvu kudaiwa kudanganya umri, limeingia katika sura mpya baada ya Baraza la Sanaa Tanzania (Basata) kueleza kuwa litamvua taji hilo endapo itabainika kweli alichakachua umri wake.

Katibu Mkuu wa Basata, Geoffrey Mwingereza, aliliambia NIPASHE jana kuwa baraza hilo linasubiri uchunguzi ukamilike na endapo watabaini kuna udanganyifu ulifanyika hawatakuwa na la kufanya zaidi ya kumvua taji.

Wakati Mwingereza akieleza hayo, viongozi wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wanatarajia kukutana leo jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujadili sakata hilo la Sitti.

Akizungumza na NIPASHE jana, Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Juma Nkamia, alisema serikali imesikia taarifa za mkanganyiko kuhusiana na mrembo huyo hivyo imeamua kuitisha kikao ili kuanza kulifanyia kazi.

Nkamia alisema kamwe serikali haiwezi kukaa kimya pale ambapo jina la nchi linatajwa vibaya.

"Siwezi kukuambia hatua gani zitachukuliwa, ila kesho (leo) tutakuwa na kikao, serikali haiwezi kukaa kimya, kuna vyombo vyake vinalifanyia kazi," alisema Naibu Waziri huyo.

Aliongeza kuwa yeye alikuwa nje ya Dar es Salaam, lakini tayari kuna maelekezo aliyoyatoa na yameanza kufanyiwa kazi na wizara hiyo.

Siku moja baada ya Sitti kutangazwa mshindi wa taji hilo, taarifa za mrembo huyo kuhusu umri wake zilianza kusambaa kwenye mitandao ya kijamii zikionyesha kuwa ana miaka 25, hivyo hana sifa za kushiriki shindano hilo hapa nchini.

Nakala ya hati ya kusafiria ya mrembo huyo ambayo ilitolewa Februari 15, 2007 na muda wake wa kumaliza kutumika ukiwa ni Februari 14, 2017 yenye namba AB 202696 inaonesha Sitti ambaye pia anashikilia taji la Kitongoji cha Chang'ombe na Kanda ya Temeke, alizaliwa Mei 31, 1989.Pia taarifa nyingine zinazoone sha mrembo huyo ana miaka 25 ni zilizokuwa kwenye Taasisi ya Explore Talent, ikimtaja kwamba anaishi Dallas, Texas, urefu wake ni 5'8, umbo lake ni la kati, asili yake ni Mwafrika na rangi ya macho yake ni kahawia.

Juzi, Kamati ya Miss Tanzania iliyoko chini ya Mratibu wa shindano hilo, Hashim Lundenga, ilisema kuwa Sitti amezaliwa Mei 31, 1991 katika wilaya ya Temeke jijini kwa mujibu wa cheti chake cha kuzaliwa alichokionesha.

Lundenga alionesha cheti cha kuzaliwa cha Sitti ambacho kimetolewa na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) Septemba 9, mwaka huu kikiwa na namba 1000580309 na kikimtaja baba yake ni Abbas Mtemvu Zuberi (Mbunge- Temeke) wakati mama ni Mariam Nassor Juma (Diwani- Temeke).

Hata hivyo, Lundenga alisema kuwa kamati yake inaendelea na uchunguzi kuhusiana na taarifa hizo na endapo watabaini kuwepo na udanganyifu watamchukulia hatua mrembo huyo kwa kushirikiana na Basata.

Pia Lundenga na Sitti, walikanusha taarifa za mrembo kuwa kuwa na mtoto na kusema kwamba mwenye uthibitisho wa jambo hilo anatakiwa aliwasilishe kwa kamati ili hatua zichukuliwe.

Sitti aliibuka kidedea katika shindano la urembo la taifa lililofanyika usiku wa Jumamosi ya Oktoba 11 kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini na kuwashinda washiriki wenzake 29 waliokuwa wanawania taji hilo.

CHANZO: NIPASHE

Msichana Kupata Mimba Bila Kukusudia ni Uzembe, Mwanaume Asilaumiwe

$
0
0
Kumekuwepo na malalamiko toka kwa wasichana kwamba kijana/mwanaume amenipatia mimba na anakwepa matunzo ya mtoto. Jambo la msingi hapa upatikanaji wa mimba mwenye kujilaumu ni msichana kwa kutokuwa makini. Sina maana kutetea wanaume wanaokwepa child support, ila najadili uzembe wa wasichana wengi kutokuwa makini na kushtukia wamepata mimba bila kukusudia.

Kuna mada moja ililetwa hapa  ikijadili jinsi wasichana wasivyo makini katika kutumia kinga (condom) wanapofanya ngono na wapenzi wao isipokuwa mwanaume ndiye ashughulikie. Hii inatoa picha jinsi wasivyo makini. Pengine kubana matumizi kwao kutaka kila kitu ashughulikie mwanaume matokeo it cost them, may be kisaikolijia ni inferiority complex ya wasichana kadhaa, lakini walio wengi wako makini sana.

Siku hizi hata wanandoa hupanga lini wapate mtoto na wanataka watoto wangapi, iweje msichana ajiachie kupata mimba bila makubaliano na mwanaume? Kama mpango ni kuoana kwa nini asihakikishe taratibu za kuoana zinakamilika ndipo wapate mtoto? Siku hizi hata mwanafunzi wa darasa la tano anajua tayari namna gani mimba inapatikana na namna gani awe makini kuepa kupata mimba tokana na elimu ya bayolojia shuleni.

Kuna uwezekano kupata mimba bila kuingiliana na mwanaume, hasa kwa romance s3x ambayo husababisha mwanaume kupata semen ejaculation na ikafika karibu na v@gna au kufikia v@gna wakati mwanamke eneo hilo la vagna liko wet dhahiri semen zinazobaba sperm zitakuwa zimepata reli ya uhakika kuingia ndani iwapo majira ni ya kuangua yai na ute ni ule laini, ukashangaa kwa vipi unapata mimba wakati hukufanya ngono kumbe mchezo wa romance umekubebesha mimba.

Urafiki mitandaoni nao hufanya marafiki kuwa karibu mno na kuzoeana hadi kufikia kufanya miadi ya kukutana na kufanya yale ambayo yanahatarisha kupata mimba tokana na kuhamasishana kwa online romance na hatimaye wakutanapo ni full mzuka wa patashika nguo kuchanika. Nakumbuka kulikuwa na mtandao mmoja wa BONGO  walikuwa na utaratibu wa kukutana ili kujuana na wengi walidandia na kudandiwa kwa mwendo huo wa kujuana hadi kupata watoto kama hawana akili na leo mzazi mmoja peke yake kabeba mzigo. Tuwe makini.

Akina dada jihadharini na mambo haya yafuatayo:
Ijue vizuri kalenda yako ya siku za kushika mimba.
Uelewe ute mzito usioruhusu semen kupenya na ute laini unaoruhusu semen kupenya.
Romance s3x hakikisha umevaa chupi pekee isiyopitisha majimaji kwenye vagna.
Usikubali kufanya ngono bila kinga.
Uwe mwangalifu mpenzio ambaye umemsababishia kupata ejaculation akishika sehemu yake ya siri kidole kikigusa vagna au nyeti yake kugusa eneo au karibu na vagna kuna uwezekana wa kushika mimba.
Jihadhari kulewa usije ukafanya ngono bila akili timamu kesho yake ukajilaumu akili ikikurudia, majuto ni mjukuu.
Usijiruhusu kujenga mazoea ya flirting ambayo yatakufikisha kufanya ngono sababu ya mhemuko wa kuzoeana.

Msichana ndiye mwenye nafasi ya kujiruhusu kupata mimba au kutopata, vinginevyo ni uzembe wa msichana mwenyewe. Hata hivyo inapotokea msichana kupata mimba kisha kuzaa mtoto mwanaume aliyesababisha mimba anawajibika kusaidia kutunza mimba na child support.

Aliyepigwa Risasi Tumboni Akiwa kwenye Gari Jana Magomeni Afariki Dunia

$
0
0
Juzi ilikuwa ya kwanza kuripoti tukio la mwanamme mmoja kupigwa risasi maeneo ya Magomeni Mikumi ambaye hakuweza kutambulika mara moja, lakini sasa amejulikana na kwa taarifa zilizotolewa na ndugu, jamaa huyo amefariki dunia jana afajiri akiwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Marehemu ametambulika kwa jina la Nyakiringa Stivin (39), mkazi wa Kibaha Picha ya Ndege na mwanamke aliyekuwa naye kwenye gari ameelezwa kuwa ni mkewe, Agness Lucas. Marehemu ni fundi wa sofa na imeelezwa na chanzo chetu kuwa alikuja jijini Dar kwa ajili ya kununua mahitaji yake ya ufundi

Alipopigwa risasi maeneo ya Magomeni alikuwa akitokea Access Bank Manzese ambako alitoa fedha kiasi cha shilingi 12M. Kwa mujibu wa mkewe, mkoba uliochukuliwa na majambazi ulikuwa na shilingi milioni 10 ambazo zilibaki baada ya kufanya manunuzi maeneo ya Manzese.

Boko Haram Noma Sana Yakiuka Makubaliano na Kuteka Wanawake Wengine

$
0
0
Taarifa iliyoripotiwa na shirika la utangazaji Uingereza BBC imesema kikundi cha wapiganaji cha Boko Haram kimefanya mashambulizi katika kijiji cha Adamawa kilichopo Kaskazini Magharibi ya Nigeria na kuteka wanawake na wasichana katika kijiji hicho.
Utekaji wa wasichana na wanawake hao unatokea ndani ya siku sita tangu serikali ya Nigeria na kikundi hicho walipofanya makubaliano ambapo Boko Haram waliahidi kuwaachilia huru zaidi ya wasichana 200 wanaoshikiliwa na kikundi hicho.
Japo Boko Haram wamekiuka makubaliano waliyoafikiana Ijumaa iliyopita, bado serikali ya Nigeria ina matumaini ya kuachiliwa huru kwa wasichana hao baada ya kikao kinachotarajiwa kufanyika muda wowote kuanzia sasa huko Chad.
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images