Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Nicki Minaj na Boyfriend wake Wamwagana? Boyfriend wake Afunika Tattoo ya Minaj

$
0
0
Wanasema dalili ya mvua ni mawingu, hivi ndivyo inavyoonekana katika uhusiano wa Nicki Minaj na mpenzi wake Safaree Sam ambaye alikuwa amejichora tattoo yenye picha ya Nicki na jina lake pia.

Wiki hii, Safaree ameonekana akiwa kifua wazi huku akiwa ameifunika tattoo ya picha ya Nicki na jina lake kwa michoro mingine. Tattoo nyingine aliyokuwa ameichora mkononi mwake inaonekana pia ikiwa imefifia sana ikiashiria kufutwa.

Hali hii imechochea kuni tetesi zilizoanza kusambaa kuwa wamepigana chini hasa baada ya Nicki Minaj kutweet, “Single and Ready to mingle.”

Tweet ambayo kwa mujibu wa Urban Islandz haikuwa na kwa ajili ya uhusiano wake bali alikuwa anazungumzia muziki wake kuwa anayo nafasi zaidi kwa mashabiki wake wakiume

Inaelezwa kuwa huenda Nicki hakutaka attention kama alivyofanya boyfriend wake huyo kujichora picha yake na ndio sababu ameamua kuifuta.

Itafahamika tu..endelea kutembelea tovuti hii tutakujuza.

Ampiga mawe binti yake hadi kufa kwa kosa la kufanya mapenzi kabla ya ndoa

$
0
0
Mfuasi mmoja wa kundi la ISIS la Syria ameungana na wanajeshi kadhaa wa kundi hilo kufanya mauaji ya kinyama kwa kumpiga mawe binti yake wa kumzaa hadi kufa baada ya kugundulika kuwa alizini.

Kundi la ISIS limeachia video inayoonesha tukio hilo la kusikitisha linaloelezwa kufanyika katika jiji la Hama nchini Syria.

Katika video hiyo iliyoripotiwa pia na mtandao wa Mirror wa Uingereza, msichana huyo anaonekana mnyonge akimuomba msamaha baba yake, “tafadhali baba….nisamehe.” Lakini baba yake anasikika akisema, “mimi sio baba yako tena.”

Aliongeza kuwa anatumaini adhabu anayompa binti yake itakuwa fundisho kwa wanawake wengine.

Baba huyo alioenekana akiwageukia wapiganaji wa ISIS na kuwapa ishara kuwa adhabu ianze, na mwisho yeye anaonekana akiwa na jiwe kubwa zaidi lililoutoa uhai wa binti yake

BonyezaHAPA kuona Video

Ni Wasanii Gani wa Bongo Walimshtua Davido kwa Shangwe kwenye Fiesta Dar es Salaam?

$
0
0
Unaambiwa weekend iliyopita kwenye Fiesta ya Dar es salaam mwimbaji Davido wa Nigeria alitumia dakika zake zote kutazama screen zilizokua zimewekwa nyuma ya stage ya Fiesta baada ya kusikia shangwe zilizokua zinapigwa baada ya Wakali wengine kupewa time ya kumiliki stage.
Alilazimika kutazama TV hizo kwa umakini baada ya kuona shangwe walilopata WEUSI ambapo mashabiki walikua wanaimba nyimbo zao kwa muda mrefu ambapo Davido kabla ya kuuliza alitumia muda mrefu kuwatazama kwa makini baada ya kushangazwa na shangwe walilokua wanapata WEUSI hawa.

Baada ya Wakali hawa kumaliza show Davido alianza kuuliza ni kina nani na wana umaarufu kiasi gani ambapo mmoja wa marafiki zake amesema stori hazikuishia uwanjani kwenye Fiesta bali mpaka Hotelini Davido alionyesha kushangazwa na shangwe la WEUSI na kuwaongelea tena.
Hii itafanya idadi ya Wasanii wa bongo wanaofahamika na Davido iongezeke manake alipokuja juzi Tanzania alihojiwa muda mfupi tu baada ya kutua kwenye uwanja wa ndege na kusema msanii pekee wa Tanzania anaemfahamu ni Diamond Platnumz.
Mengine aliyoyasema ni kwamba kwenye album yake mpya inayotoka mwanzoni mwa 2015 wameshirikishwa wasanii wachache kutoka Afrika ambao ni pamoja na Diamond na Mafikizolo na kwamba kuna wasanii wawili wakubwa wa kimataifa aliowashirikisha ambao hatowataja kwa sasa.

Mshiriki wa Tanzania Laveda Ndani ya Jumba la Big Brother Anaswa na Kamera Akipiga Puli Mbele ya Wenzake

$
0
0
Leo ni siku ya 20 tangu Big Brother Africa ya Mwaka huu ianze. Naamini kwa wale wanaoifuatilia wanaburudika vya kutosha na mambo yanayotendeka ndani ya jumba hilo.

Ni Shindano ambalo halikuanzishwa kwa lengo la kuenzi mila na desturi za kiafrika, bali lilianzishwa kwa lengo moja tu la kutoa burudani ya kutosha ambayo mwisho wa siku itawawezesha waanzilishi kujipatia pesa.

Turudi kwenye pointi yetu, kama ilivyo kawaida ya siku ya Ijumaa ndani ya jumba hilo, usiku wa kuamkia leo washiriki walikuwa wakiparty pamoja kwa kucheza na kunywa.

Baada ya burudani hiyo iliyosimamiwa vilivyo na Dj Izzy toka Botswana, dada yetu Laveda ambaye anaiwakilisha Tanzania katika jumba hilo alitoka na kuelekea kitandani.

Akiwa na mzuka wa kutosha, Laveda alijifunika shuka na kuanza kujichua( kupiga puli) pole pole.

Mtu wa kwanza kumshuhuda Laveda "akili PULINETI" ni mwana dada Mam Bea ambaye alistushwa na mnong'ono wa sauti za mahaba .

Ndipo mrembo huyo alipotoka na kuwajuza wenzake ambao hata hivyo hawakuonekana kumjali kwani "Pini" lilikuwa bado linaendelea!

Mam Bea aliendelea kuueneza umbea huo, hali iliyomfanya Idris( mshiriki wa kiume wa Tanzania) apandwe na hasira akitaka suala hilo liachwe kujadiliwa.

"Acheni Ujinga bana, mna ajenda gani,? Nini kigeni? Ntapiga mtu mimi!," Alifoka Idris akiwataka washiriki wenzake waliache suala hilo.

Hasira za Idris zilifanikiwa kudhibitiwa na Mr. 265 ambaye alimshika na kumsihi apunguze hasira.

" Yaishe mtu wangu, Hasira za nini kamanda? Achana nao!," alisikika Mr. 265 akimsihi Idris.

Ni ukweli usiopingika kuwa Idris ni mzalendo wa kweli na anaipenda Tanzania na ndo maana alipandwa na hasira baada ya kuona Laveda anazongwa zongwa.

Mangapi yanafanyika mle ndani? Watu wanaoga pamoja, tena uchi wa mnyama?

Eti leo hii mwenzao kaamua kupiga punyeto kupunguza hamu wanaanza kumsengenya!!? Hiyo sio haki. Safi sana Idris kwa kumtetea Mshiriki mwenzako na mtanzania mwenzako.

Laveda ni mtu mzima, ana hisia kama binadamu wengine. Pamoja na yote, bado ni mtu ambaye kimaadili anaongoza ndani ya jumba hilo. Kama huamini, tazama video za washiriki wanapokuwa bafuni uone ni jinsi gani anaoga.

Leo ni siku ya 20, nakuhakikishia hutaona video hata moja ikiyaanika maziwa yake hadharani. Ni mtu ambaye huoga na nguo tofauti kabisa na washiriki wengine.

Kesho jumapili, Mshiriki mmoja au wawili watayaaga mashindano hayo. Laveda ni miongoni mwa watu walioko hatarini kutolewa kesho.

Kura yako inahitajika sana kumfanya asitoke. Kuwa mzalendo, mpigie kura mtanzania mwenzako.

Matukio yote ya big brother yanaruka hewani mtandaoni kupitia www.bigbrotherafricans.com

Hukumu ya Kifo Yatangazwa kwa Wanawake Wanaojiuza Pamoja na Wateja Wao

$
0
0
Katibu wa maendeleo ya jamii katika jiji la Abuja Nigeria, ametangaza ‘kiama’ kwa wanawake wanaofanya ‘biashara ya kujiuza’ pamoja na wateja wao. 

Taarifa iliyochapishwa na Today Internet Newspaper imesema, katibu mkuu huyo Blessing Unoh amesema serikali imetoa amri ya kusitisha biashara hiyo ndani ya saa 48, kwa yeyote atakayekiuka hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Amri hiyo imetolewa saa chache baada ya katibu mkuu huyo kutembelea maeneo mbali mbali ambayo yamebobea kwa biashara hiyo ambapo amejionea hali halisi iliyopo.

Aidha amesema kwa yeyote atakekiuka amri hiyo na kukutwa na hatia ya kutenda kosa hilo awe tayari kukabiliana na hukumu ya kifo.

Baada ya kutemana na Edzen, Dida Amtambulisha Mchumba Wake Mpya Siku ya Birthday yake

$
0
0
SIKU chache baada ya kudai hawezi kuolewa kwa sasa, mtangazaji wa Kipindi cha Mitikisiko ya Pwani kupitia Radio Times FM, Khadija Shaibu ‘Dida’, ameonesha matumaini mapya ya kuolewa baada ya kumwanika mchumba’ke mpya.

Dalili za matumaini hayo mapya zilionekana usiku wa kuamkia Alhamisi iliyopita katika sherehe yake ya kuzaliwa (bethidei) iliyofanyaka nyumbani kwake, Mwananyamala jijini Dar na kuhudhuriwa na mastaa kibao Bongo.

Miongoni mwa wasanii waliohudhuria hafla hiyo ya kufuru ni pamoja na malkia wa Mipasho Bongo, Khadija Kopa na waigizaji; Chuchu Hans, Jacob Steven ‘JB’, Rose Ndauka, Salma Salmin ‘Sandra’, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’, Jeniffer Kyaka ‘Odama’, Maimatha Jese na wengine kibao ambao walimpa Dida kampani ya nguvu na kumtunza fedha na zawadi mbalimbali.



Kama hiyo haitoshi, kwenye hafla hiyo, kulitawaliwa na vinywaji vya kila aina huku kukiwa akichinja mbuzi watatu maalum kwa ajili ya sherehe hiyo sambamba na kuku kibao wa kienyeji, nyama za kila aina, msosi wa nguvu na pombe za kumwaga

Wakati sherehe ikiendelea, Dida aliibua minong’ono ya aina yake baada ya kutambulisha uwepo wa shemeji zake waliotoka Arusha ambao walimwakilisha mchumba wake katika pati hiyo.
“Jamani humu ndani kuna watu mbalimbali ambao wamefika kuniunga mkono, mkiwemo wasanii wanahabari pamoja na watangazaji wenzangu, lakini kikubwa zaidi napenda kutambua uwepo wa shemeji zangu waliofunga safari kutoka Arusha, wamekuja kuniunga mkono, nimefurahi sana,” alisikika Dida.

Ulipofika muda wa kutoa zawadi, mmoja wa mashemeji zake hao aliyejitambulisha kwa jina la Feisal alishika kipaza sauti na kusema alitinga kwenye hafla hiyo kumwakilisha ndugu yake (jina alilihifadhi) ambaye alimtuma amwambie Dida kuwa amemzawadia gari lenye thamani ya Sh. milioni 26 za madafu ambalo siku si nyingi litatua Dar.

“Hehee my new baby, huyo ndiye my new baby jamani na hawa ndiyo mashemeji zangu wa ukweli,” alipaza sauti Dida.


Alipoulizwa na mwandishi wetu juu ya mipango yake na mchumba huyo mpya, Dida alifunguka:
“Huyo ndiye mwanaume wangu wa sasa muda ukiwadia nitaanika kila kitu, bado mapema mno kuzungumza mengi,” alisema Dida ambaye kama ataolewa na mwanaume huyo itakuwa ndoa ya nne.

Dida aliyemwagana na Ezden Jumanne miezi kadhaa iliyopita, kabla ya hapo aliwahi kuolewa na wanaume wawili tofauti ambao alimwagana nao kwa talaka.

Waandishi: Mayasa Mariwata, Musa Mateja na Imelda Mtema

Lucy Nkya (Naibu Waziri wa zamani) arushiana risasi na mwanae

$
0
0


Naibu Waziri wa zamani wa Afya na mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki, Lucy Nkya, amerushiana risasi za moto na mwanae wa kumzaa, Jonas Nkya ndani ya ofisi zao mkoani Morogoro muda huu....Chanzo kinadai ni Mgogoro wa Kifamilia 

Boss wa Home Shopping Centre apewa Ubalozi wa Tanzania China

$
0
0
Msiniulize vetting ya yeye kupewa Ubalozi huko Guangzhou China ilifanya lini, na nani na criteria zipi alizokuwa nazo huyu mwarabu wa Yemen mpaka kupewa Ubalozi.



1. Huyu jamaa hakufayiwa vetting yoyote ile whatso ever na usalama wa Taifa kabla hajapewa hiyo nafasi.

2. Familia yake na biashara zao zimekuwa kwenye kashfa nzito nzito za kwa ukwepaji kodi 

3. Salaah hana elimu wala qualification yoyote ile ambayo ingemfaya apewe nafasi hiyo. As a matter of fact how can you give a diplomatic post kwa mtu ambaye kaishia standard 6? 

4. Kwa sababu za kiusalama aka national security hafai kupewa hiyo nafasi. 

5. Kwa sababu za national interest hafai kupewa hiyo nafasi

6. Foreign wapo watu wengi sana ambao wana qualify kupewa hizo nafasi na washapitia hiyo vetting na due dilligence

7. Salaah na familia yake hawana intergrity -both professionally and personally kuwa ma diplomats wa tanzania kokote kule duniani

Kuna vijana wengi wa Kitanzania ambao wamesoma,wazalendo na washafanyiwa vetting na usalama na wapo Foreign hawapewi 

Sasa cha kujiuliza hibi serikali ya nchi hii ina maana gani kusomesha watu wake na kisha kuwaweka benchi pale foreign halafu wanaenda kumteua huyu mshihiri wa Yemen ambaye hakusoma kuwa balozi wetu huko china?

Mbaya zaidi utashangaa jinsi mawaziri na viongozi wa juu wa serikali wanavyo mnyenyekea wakati kuna vijana wa Kitanzania ambao wasomi wanaendelea kusota pale wizarani na nafasi hizi hawapewi.
Source:JF

Shy-Rose Bhanji Ajitetea na Kukanusha Tuhuma za Kulewa na Kufanya Fujo Ndani ya Ndege

$
0
0
Mimi Shy-Rose Bhanji, Mbunge wa Afrika Mashariki-Tanzania, ninapinga vikali na kwa nguvu zote shutuma zilizotolewa dhidi yangu kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii.
Shutuma hizi hazina ukweli wowote na zinalenga, si kuniharibia, bali kuchafua sifa yangu na utendaji kazi wangu katika Bunge la Afrika Mashariki.
Lengo kuu la shutuma hizo ni kunivunja nguvu na ari ya kutetea maslahi ya nchi yangu na Watanzania wenzangu kwani daima nimekuwa kikwazo na mwiba kwenye ajenda zinazokiuka maslahi ya Tanzania.
Kwa mfano ardhi ya Tanzania kugawiwa kwa wana Jumuiya ya Afrika Mashariki ni kinyume na Sera ya Tanzania. Nimekuwa miongoni mwa wabunge wa Tanzania tulio mbele katika kulipinga suala hilo. Sishangai likinijengea uadui.
Isitoshe, kwenye ajenda ya kumuondoa madarakani Spika wa EALA, Dk. Margaret Zizziwa, nilisimama kidete kwa kutounga mkono kwa sababu halikuwa na maslahi ya Tanzania na yalikuwa kinyume na malengo ya ushirikiano wa Jumuiya nzima.
Hoja ya kumuondoa Spika ilikuwa ni sehemu ya ‘mchezo mchafu’ ya ajenda ya siri ya kumweka kwenye nafasi hiyo mjumbe mwingine kwa maslahi ya wachache.
Jaribio hili la kumuondoka Spika lilifanywa na kushindikana mara tatu baada ya kukosa sahihi za kutosha kutoka Tanzania, ikiwamo ya kwangu.
Baada ya kampeni ya kumwondoa Spika kushindwa, wabunge kadhaa walikuwa wanasusia vikao vya Bunge wakati wameshachukua posho za vikao. Kwa mfano kikao kilichofanyika hivi karibuni hapa Dar es Salaam.
Malumbano ndio yamekuwa yakitawala na kuinyima Bunge akidi ya kuendelea na ajenda za mtangamano. Huu ni usaliti wa wazi kwa nchi zilizowachagua na kuwatuma katika Bunge la EALA.
Ukijaribu kuwaasa kwamba mwenendo huo si sahihi, unageuka kuwa adui.
Na sasa wameamua kunitukana na kuzusha tuhuma kadhaa kupitia mitandao ya kijamii ambako yote ni utunzi wa kisanii usiokuwa na chembe ya ukweli, uhalali wala ushahidi.
Wahenga walisema ‘akutukanaye hakuchagulii tusi’. Walete ushahidi wa tuhuma zote dhidi yangu.
Kwa mfano, shutuma kwamba nililewa pombe ndani ya ndege, kuvunja chupa, kufanya fujo na kufungwa pingu wakati wa safari ya Ubelgiji si kweli hata kidogo.
Kama hizi tuhuma ni za kweli, kwanini hazikupelekwa polisi, serikalini au vyombo vingine vya sheria baada tu ya tukio?
Ijewe wamesubiri wiki mbili baada ya madai hayo ya tukio la kutunga ndipo wajitokeze wakati wa kikao kinachoendelea mjini Kigali, Rwanda? Kwanini wasubiri kikao cha Kigali ndipo uzushi huu utolewe?
Tuhuma kwamba nimewatukana marais wa nchi tatu hazina mashiko isipokuwa kuhalalisha kampeni ya wale wanaonichafua na kuibua chuki kwa maraisi na raia katika nchi za Kenya, Rwanda na Burundi.
Ninayo heshima kubwa sana kwa marais wa nchi zote tano na raia wa nchi wanachama ambako mara zote nimepokewa na kuishi kwa amani na upendo katika nchi hizo. Naahidi kuedeleza heshima hii.
Hainiingii kichwani ni wapi nilipoteza heshima hii isipokuwa kwa wale wasionitakia mema ambao wamekusudia kufanikisha ajenda zao.
Shutuma zote dhidi yangu zimetengenezwa na watu ambao hatushabihiani katika hoja zetu na sishangai kwa hilo.

Mimi ni Mtanzania na ni Mbunge wa Tanzania. Hivyo nina wajibu wa kulinda na kutetea maslahi ya Watanzania ili kuleta mtangamano wenye uwiano sawa kwa nchi zote wanachama.

Ninaahidi nitaendelea kuwatumikia Watanzania kwa nguvu zangu zote na kutoa ushirikiano kwa wabunge wengine wa EALA kwa manufaa ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Nimeyasema haya nikiamini kuwa: “Uongo ukiachwa usemwe mara nyingi unaweza kuaminiwa kuwa ni ukweli.”
Mungu ibariki Afrika MasharikiUmoja Wetu ni Nguzo Yetu

Diamond Atajwa Katika Orodha ya Wasanii Kumi Walioleta Mabadiliko Katika Muziki Afrika

$
0
0

Mkali wa Ngoma ya "Mdogo Mdogo" Diamond Platnumz ametajwa kwenye Orodha ya wasanii Kumi Afrika waliofanya Mabadiliko (Top10 Most Game Changers).

Orodha hiyo imetolewa week hii kwenye Kipindi cha Top10 Most kinachoendeshwa na Joketi Mwengelo na Ice Prince kutoka Nigeria, Diamond Platnumz ameshikilia namba 10 pamoja na Fally Ipupa. Hii ndio List nzima 
1. 2face Idiba 
2.Boom Shaka 
3.D banj  & Don Jazzy 
4.K'naan -
5.Banky W  & Psquare 
6.Dj Jimmyyat & Dj Waxxy
7.Tiwa savage  & Wizkid ayo 
8.Ice Prince - Nigeria & Naetoc 
9.Mafikizoro & Mr. Flavour
10.Diamond Platnumz & Fally Ipupa

Wakati Chid Benzi Akisota Polisi kwa Kosa la Madawa ya Kulevya..Ray C Afunguka Haya

$
0
0
"Pole kaka yangu Chidi Benz,Naumia kuona tatizo uliokuwa nalo bado haujalitaftia jibu unalijua la kutatua tatizo lako,Mimi ni dada yako na tumeshafanya kazi Pamoja,Tatizo ulilonalo na Mimi nilishakuwa nalo na niliweza kulitatua sababu nilijitambua na kutafuta suluhu,nimejaribu kila njia kukushauri badala yake ukaja na rungu la kimasai na kunitandika nalo nyumbani kwangu!nadhani janga hili lililokukuta litakuwa Kama jibu kwako kwamba unakoenda si salama kabisa kaka yangu ni bora ubadilishe njia ili uweze kuungana nasi kwenye tiba ya Methadone kwani ndio Kiboko ya madawa ya kulevya!!!!Kama Mimi mwanamke nimeweza najua Hata wewe utaweza!!!!Tanzania bila madawa ya kulevya Inawezekana !!Watanzania tusimyanyapae Msanii wetu kwani Uteja ni ugonjwa Kama ugonjwa mwingine na Unazuilika na Kutibika,Ana kipaji na Ana uwezo wa kurudi tena kwenye Sanaa,Tumuombee mema.........Tanzania Stand Up n Wish Him Luck............With Love,Ray C Foundation."

Taarifa Kuhusu Meseji Inayosambaa Kuwa Sitti Abbas Mtemvu Amejivua Taji la Miss Tanzania si ya Kweli

$
0
0
Jioni ya leo Imezagaa meseji ambayo imechukulikwa facebook page yenye jina la Sitti Abbas Mtemvu ikielezea kuwa Sitti Amejivua Taji la Miss Tanzania kutokana na Maneno ya Watu ...

Ukweli ni kuwa Hiyo Page si ya Sitti Mtemvu kwa uchunguzi wangu mdogo niliyofanya, Page inaonekana imetengenezwa tarehe 17 Mwezi Huu na ina Likes 1486 mpaka wakati huu..

Ijulikane kuwa Sitti Akiamua Kujivua Taji Hawezi Kamwe kusema kupitia Mitandao ya Kijamii bali itabidi ipitie katika kamati ya Miss Tanzania.......

Usidanganyike...

Naombeni Ushauri Kuhusu Huyu Mzungu

$
0
0
Ninae rafiki yangu mzungu wa Canada,huyu jamaa ananiambiaga nimtumie picha za watu walivyo maskini na nikiwa naongea nao,alituma pesa nikanunua Camera na laptop na huwa kila wiki ananitumia dola 50 nimemfanyia hii kazi kwa mwaka sasa na kuna wakati ananitumia hata dola 800 hata elfu moja ili niende mikoani.

Huyu mtu tulijuana kupitia biashara ya wadudu baadae akadai ameokoka kwamba ni mkristo na akaniuliza kwamba na mimi ni mkristo nikamwambia ndio amekuwa akiniuliza kuhusu bible na bible mimi siijui kwa undani sana japo ni mkristo na sijapata mda mzuri wa kujifunza.

Huyu mtu sijawahi kukutana nae face to face.Kusema kweli huyu mtu sijawahi kuumuulizaga madhumuni ya hizo picha japo yeye anadai anapenda kuwaona watu maskini kwenye picha ili awaombee.

Naombeni ushauri kwa watu wenye ujuzi zaidi na dunia.

~By Albosignathus JF

Kova ' Hatutambui Mkutano wa Ukawa Jangwani Leo'

$
0
0
Kamanda KOVA ametoa onyo kali kwa mkutano unaoitwa wa ukawa jangwani. kamanda KOVA amedai hana barua yoyote ya ukawa ofisini kwake.
AMETOA ONYO KALI UKAWA KUTOENDA JANGWANI. HUENDA KUKAZUKA BALAA KM AGIZO LITAPUUZWA.

Tanzania voted best safari country in Africa

$
0
0
Tanzania is the best place for a safari, according to a new poll.
First problem when considering a safari -- where to go. 

Zimbabwe has the majestic Victoria Falls, South Africa great boutique reserves.

Kenya offers chances to see big cats and Botswana is a leader in eco-friendly tours.

But you'd be best off selecting Tanzania, according to a recent poll on safaribookings.com.

The Netherlands-based website polled 1,000 safari tourists and 756 experts, including guidebook authors from Lonely Planet, Rough Guides, Frommer's, Bradt and Footprint, over two years.

The result: Tanzania is a clear favorite for novice and veteran safari-goers alike.

“Tanzania is home to Serengeti National Park and Ngorongoro Crater,” wrote Tim Bewer, a Lonely Planet guides author and one of the experts polled. “This alone makes a solid case for declaring it Africa’s best safari country.”

Also on CNN: Southern Africa's best boutique safari reserves

Adventure calls

Tanzania has seven UNESCO World Heritage Sites, including safari favorites the Ngorongoro Conservation Area and Serengeti National Park, home to millions of wildebeest that form one of the world's most spectacular sights as they migrate the area year-round.

The country is also home to Mount Kilimanjaro, the highest mountain in Africa.

Tanzania’s only drawback, according to Safari Bookings, is that there are “too many highlights to fit in one safari."

The news comes as welcome affirmation of the country as a tourist destination, after a recent bombing at a rally that killed two in Arusha. That event sparked anxiety among visitors.

Ratings out of 5 of Africa's top safari countries

As voted by tourists and safari experts

Tanzania - 4.84
Botswana - 4.75
Kenya - 4.66
Zambia - 4.58
South Africa - 4.55
Namibia - 4.54
Uganda - 4.16
Zimbabwe - 4.14

Dimond Kupiga Shoo ya Bei Ghali zaidi Kuwahi Kutokea Katika Historia ya Muziki wa Tanzania

$
0
0
Katika kile kinachoonyesha kwa wasanii wa bongo kuanza kujitambua na kutumia brand zao vizuri katika kujipatia kipato, Msanii kinara katika muziki wa Tanzania ambaye haishi kutajwa katika vinywa vya watanzania "Dimond platnumz" atapiga shoo ya bei ghali zaidi kuwahi kutokea(msaniiwa ndani) tangia Tanzania iumbwe maeneo ya Mlimani city.

Imefahamika kuwa wahuni wa zomeazomea waliotamba maeneo ya pale leaders hawatoweza kuhudhuria kwa kuwa bosi wao aliyewakodisha atashindwa kulipa viingilio ambavyo ni kati ya 50000 mpaka 70000 per kichwa.

Kitendo cha Dimond kupiga shoo za bei ghali kimewaamsha wasanii wengine ambao walikuwa hawatambui ukubwa wa brand zao hivyo basi na wao kuanza kudai hela nyingi katika shoo wanazopiga, ikumbukwe katika tamasha la Fiesta lililofanyika mwaka huu Dimond alipiga shoo mbili tu kutokana na mahitaji yake makubwa ya mtonyo katika shoo zake.

Dimond amebadilisha mfumo wa kinyonyaji uliokuwepo katika muziki wa Tanzania na sasa tunaona kumbe msanii wa Tanzania anaweza kutoa video nzuri, kumbe msanii wa Tanzania anaweza kujaza ukumbi kwa malipo ya shilingi 50000 kwa kichwa na yeye kunufaika na kazi zake.

Kabla ya Dimond walikuwepo wengi ila walikuwa hawafaidiki na kazi zao , kama Tanzania tukiwapata wakina Dimond hata wanne basi tasnia yetu itafika mbali, tuacheni majungu na wivu kwa shujaa wa muziki wetu ila tutengeneze mazingira mazuri ya kuwapata watu wengine kama Dimond.

Taarifa zaidi Kuhusu Naibu Waziri Kurushiana Risasi na Mtoto Wake..Mtoto Afunguka Kilichotokea

$
0
0

Taarifa zilizoenea mitandaoni saa chache zilizopita, zinahusiana na tukio la kurushiana risasi baina ya aliyekuwa Naibu Waziri wa zamani wa Afya na Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki Dk. Lucy Nkya na mtoto wake ambaye ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM Morogoro Jonas Nkya.

Tukio hilo ambalo limetokea leo Morogoro baina ya wanafamilia hao, limehusishwa na ugomvi wa kifamilia jambo ambalo limeamsha hisia tofauti.
Akizungumza na waandishi wa habari Morogoro, Jonas Nkya amekanusha taarifa za kurushiana risasi na kueleza kuwa tukio hilo ni tukio la bahati mbaya baada ya bunduki yake kudondoka na kupelekea risasi mbili kufyatuka.
Akizungumzia kuhusu tukio hilo, Jonas amesema, “.. silaha inakaa kiunoni, nakwenda kwenye gari nashuka pale ofisini pisto hii imeanguka imejipiga risasi mbili nje ya ofisi. Sasa nadhani majirani wakaogopa sijui mi sielewi, lakini kuna watu wanaishi pale. Sasa ndio ikafika hapo wakaja Polisi of course na nini.. tumejaribu kuwaeleza.. ndio hicho kilichotokea. Lakini mimi sijui.. wala sikujua kama mama yangu yuko ndani kwa sababu pale ofisini nimekwenda kufuata gari .”–Jonas
“.. Na ndio maana nasema kama mkipata muda na nyie mnaweza kwenda kumuuliza yule mama je tumegombana.. je kuna kitu kama hicho.. hiyo ndio habari iko hivyo.. hakuna ukweli kwenye hilo..”–Jonas

Maskini Mwanamke Aliyejinusuru Kubakwa na Kumuua Mbakaji, Ahukumiwa Kunyongwa

$
0
0
Reyhaneh Jabbari mwenye umri wa miaka 26 amehukumiwa kunyongwa baada ya kukutwa na hatia ya kumuua mtu mmoja ambaye alifanya jaribio la kumbaka.
Taarifa iliyoripotiwa na CNN inasema mwanamke huyo amenyongwa katika gereza la Tehrain, Iran ambapo alikuwa amefungwa baada ya kutenda kosa hilo mwaka 2007 wakati huo akiwa na umri wa miaka 19.
Mwanamke huyo amekutwa na hatia hiyo kutokana na kosa la kumuua aliyekuwa mfanyakazi wa wizara ya ulinzi na usalama nchini Iran, Morteza Abdolali.
Shirika la kimataifa la haki za binadamu Amnesty International limelaani kitendo cha Iran kutoa hukumu hiyo, ambapo mbali na jitihada ya kampeni mbali mbali zilizofanywa ikiwemo zile za kwenye mitandao ya kijamii katika kuipinga hukumu hiyo kuonekana kutozaa matunda.
Taarifa kutoka nchini humo zinasema mahakama ilitoa hukumu hiyo baada ya kutojiridhisha na utetezi alioutoa mahakamani kwamba alitenda kosa hilo akiwa anajilinda.
Utafiti wa Umoja wa Mataifa wa mwaka 2011 unaonesha Iran ni moja ya nchi zinazoongoza kwa ukiukwaji wa haki za binadamu ambapo nchi hiyo ina wastani wa kutoa hukumu ya kunyongwa mtu 1 kila baada ya masaa 8.

Wanaume Tuache Ubahili Tuwatunze Wapenzi Wetu

$
0
0
Kwanza nianze kwa kukili kua maisha ni magumu sana nadhani kila mtu anajua.

Na katika mahusiano ya mapenzi kati ya me na ke lazima kunakua na tofauti ya kipato, yaani Mara nyingi wanaume wanakua na hali mzur kimapato kuliko mwanamke.

Nieleweke vizur kua si maanishi kua wanawake wote wanakipato duni LA hasha.

Ningependa kuwashauri wale wenye wapenzi WA kike mambo haya yafuatayo:-

1 Ujue tofauti ya kuchunwa na kuhudumia unapokua na mpenzi ujue ni jukumu lako kumpendezesha anapopendeza watu watajua we ndio kidume uliemwezesha.

2 .Sio mpaka akuombe ndio umpe. jaribu kumfaam hali ya maisha na kipato chake ujue kukisia cha kumpa kwa matumizi yake.

3.Usiulize ya nini,ikitokea mpz amekuomba HELA usiulize ya nn ye ni MTU mzima awezi kukuomba HELA akaenda kuchambia.

4. Kutumia pesa nyingi sehemu ya starehe.
Kuna watu wanaenda mpaka hotel ya nyota 5 kustarehe akitumia zaidi ya laki tano.cha ajabu baada ya kutoka hotel anamwacha mpz wake 10000 ya nauli.
Huu ni ujinga bora ungeenda ata lodge ya nafuu ye ukamwacha na HELA ya kutosha.

5.Tenga ata 10% ya mshahara MPE yeye aangalie kama kuna kitu cha kurekebisha arekebishe.

NB.
APA ni kwa wale Wanaume wanaowazidi kipato wanawake wao sio wanawake wenye vipato vizur.

Tusiwe wataalamu wakutafuta Gspot wakati ukiombwa ata 1000 unanuna mapenzi ni pamoja na kupunguzia makali ya maisha.

Yeyote mwenye chochote anaweza kuongezea apo.

Kufuatia Kukamatwa Kwa Chid Benzi na Madawa ya Kulevya..Polisi Yatoa Onyo Kali

$
0
0
Kufuatia tukio la Msanii wa muziki Chidi Beenz kukamatwa na dawa za kulevya katika uwanja wa ndege wa Julius Nyerere Dar es Salaam, Kamanda wa Kikosi cha Kupambana na Dawa za Kulevya, Godfrey Nzowa aonya vijana kutokujihusha na dawa hizi kabisa.


Kamanda Nzowa amesema kuwa tukio la kukamatwa kwa msanii huyu mkubwa, ni nafasi ya jamii na vijana kujifunza na kuachana na dawa hizi ambazo madhara yake kwa jamii ni makubwa.

Chidi baada ya upekuzi alipatikana na kete 14 za dawa za kulevya kwenye mfuko wa shati lake na misokoto miwili ya bangi, tukio ambalo limeendelea kuzua maoni tofauti kutoka kwa watu mtandaoni wakati huu ambapo anasubiri hatua za kisheria kuchukuliwa dhidi yake.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images