Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live

Video:Diamond Platnumz Azidi kuwa Prove Wrong Team Ali Kiba..Ona Shangwe Alilopata Coco Beach Jana

0
0
Licha ya kupata zomea zomea wakati wa fiesta kijana diamond ameonekana kutojali na kuwa na confidence ya kupanda jukwaani tena bila kuhofia buu buu alizopata wakati wa fiesta na kufanya shoo ya kwa muda wa lisaa limoja na nusu kwenye viwanja vya Coco Beach.

Na muda wake wa kuondoka ulipofika ikabidi nguvu ya ziada itumike kuondoa mashabiki waliozingira gari lake kwa muda kadhaa wakitaka japo kumuona kijana huyo. 

Big up kwake kwa kuonesha kutovunjika moyo na kupata confidence ya kumiliki jukwaa.

VIDEO:


Mke wa Mtu Adakwa Akifanya Mapenzi na Mlinzi wake wa Getini

0
0
Is a pity that things like this still happen.The sad part of this episode is that her husband was said to have had accident on his way to visit his wife’s family and for months he has been recovering slowly. But the wife could not endure konji any more, she had to engage in some “rough play” with their security man.
Unfortunately for her, she was caught..Funny enough, the shameless housewife is said to be blaming the devil for her stupid act. “Devil don suffer”…

Mchawi Akutwa Amenasa Kwenye Chemba ya Maji Taka

0
0
Ni Jambo la Ajabu Kila Mtu alijiuliza huyu Mwanamke Ameingiaje Kwenye Chemba Hiyo , Tukio hilo limetokea Mjini Lagos Siku ya Ijumaa...

Inasemekana Mwanamke huyo alisikika akipiga kelele kutoka kwenye chemba hiyo ambayo ilikuwa haina sehemu ya kutokea bali matundu madogo ya kutolea maji na uchafu ...Watu walioshuhudia tukio hilo walibaki na maswali ameingiaje humo na wakati hakuna sehemu ya kuingia...ili kumtoa ilibidi wananchi watafute vifaa vya kukatia chuma ili kukata mifuniko ya chemba kumtoa..

Alivyotoka alisema meneno haya ,Jina langu ni Amudat Jimoh :

"Ni mungu ndio ameniweka huko kwenye chemba ili nitubu madhambi yangu nisije kufa...nahitaji maji ya kunywa tafadhali..Please help me.."


Kenya Wamtangazi Miss Kenya Atakaye Iwakilisha Nchi Hiyo Katika mashindano ya Miss World

0
0
It all started with the ”Miss County” competitions and it has been a long road for all the Kenyan Beauty queens. Machakos County brings out the lady who will be representing Kenya in the Miss World Competitions.

Miss Machakos- IDAH NGUMA, is 22yrs old marketing student from Tala…Isn’t she pretty????? She is now our Miss World Kenya....

Hongereni Kenya...Huku Kwetu ni Kidhungu Mkuti .....

Zitto Kabwe awabeza UKAWA na kawaita "Wasaka Tonge"

0
0

"Taifa limevimba. Wakulima Mahindi yanawaozea na Mpunga bei imeporomoka sababu ya mchele kutoka nje na usiolipiwa Kodi. Wahisani wamezuia misaada ( sababu ya kashfa ya #TegetaEscrow ) Kiasi Serikali haiwezi hata kujiendesha. Unapoona wanasiasa wanagawana vyeo katika nyakati kama hizi ujue Taifa halina Viongozi bali wasaka utawala. Wasaka utawala badala ya uongozi ni #WasakaTonge tu" Zitto Kabwe


Tanzania Yakataa Rasmi Mambo ya Ndoa za Mashoga na Wasagaji 'Ndoa za Jinsia Moja'

0
0
SERIKALI ya Tanzania imekataa rasmi kutambua ndoa za jinsia moja (ushoga) kama moja ya agenda za maendeleo katika malengo ya milenia 2015 mpaka 2030 katika mkutano wa Umoja wa Mataifa.

Akizungumza jijini Dar es Salaam kwenye mkutano wa majadiliano ya malengo ya milenia yanayotazamiwa kumalizika mwakani na kuanza malengo mapya, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy amesema serikali ya Tanzania imekataa kutambua ushoga kama moja ya agenda za maendeleo.

“tunatambua haki za binadamu, usawa wa kijinsia kati ya wanaume na wanawake na hata katiba yetu pendekezwa imetoa haki za sawa kati ya wanaume na wanawake lakini katika swala la kutambua ndoa za jinsia moja hilo tumekataa,” amesema Balozi Mushy

Amesema kwamba tumewaambia nchi zilizoendelea na wahisani wa maendeleo katika Umoja wa Mataifa kwamba swala la ndoa za jinsia moja (ushoga) si agenda ya watanzania na si agenda ya maendeleo.

Balozi Mushy aliongeza kwamba serikali ya Tanzania imeweka msimamo huo zaidi hivi karibuni na Rais Jakaya Kikwete aliagiza hivyo kwa maofisa wa Wizara ya Mambo ya Nje pamoja na Waziri husika kukataa shinikizo la kukubali swala ushoga kama agenda za maendeleo.

Amesema kwamba watanzania wanataka maswala yanayowagusa kama vile maji, elimu, huduma bora za afya, miundombinu ya umeme, ajira, umaskini na kuondoa umaskini wa kipato.

Balozi Mushy alifafanua zaidi kwamba mambo ya ushoga na ndoa za jinsia yanakwenda kinyume na maadili ya watanzania, maisha, historia, utamaduni, mila na desturi za mtanzania sinakataza maswala ya ushoga.

Amesema kwamba serikali inatambua kwamba sheria ya mwenendo wa makosa ya kujamiiana yaliwekwa na mkoloni mwingereza kabla ya uhuru na serikali ya Tanganyika imerithi kutoka kwenye serikali ya mwingereza.

Nzowa asema dawa za kulevya alizokamatwa nazo Chid Benz ni Heroine

0
0
Kamanda wa Kikosi cha Kuzuia na Kupambana na Madawa ya Kulevya Tanzania, Godfrey Nzowa amesema dawa za kulevya alizokamatwa nazo rapper Rashidi Abdallah Makwiro a.k.a Chidi Benz katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Ijumaa iliyopita (Oct. 24) ni aina ya Heroine.
Alikuwa na dawa Heroine kete 14″, amethibitisha Nzowa kupitia 255 ya XXL ya Clouds Fm. “na tunaendelea kumhoji tuone kama alipewa au nini kwasababu katika kupatikana iwe umepewa kwa hifadhi au kwa nini bado hiyo ya kupatikana inakutosha, kwasababu hakuna mtu anayepaswa kupatikana na dawa za kulevya. sisi whether unatafutwa siku nyingi hutafutwi siku nyingi kwa wakati huo huo tunapokukuta na hizo unakuwa in for it, na ndio maana sheria inasema hakuna hata defense…sisi tunashukuru kutokana kwamba amekamatwa kwasababu ni dawa hizo za kulevya imethibitika ni dawa za kulevya inatosha.”

Kamanda Nzowa ameongeza kuwa kwa sasa wanaendelea kumhoji na utaratibu utakapokamilika atapandishwa mahakamani.

Nahodha wa Bafana Bafana Senzo Meyiwa aliuawa akimuokoa mpenzi wake

0
0
Nahodha wa Bafana Bafana na Orlando Pirates Senzo Meyiwa aliuwa kwa risasi na majambazi alipokuwa akijaribu kumlinda mpenzi wake walipokuwa nyumbani kwa mpenzi wake huyo, karibu na Johannesburg, maofisa wamesema leo.

Mlinda mlango huyo wa Orlando Pirates aliuawa jana baada ya kupigwa risasi kifuani mbele ya mpenzi wake ambaye ni muimbaji na muigizaji. Katika tukio hilo, watu wawili waliivamia nyumba hiyo liyopo katika mji wa Vosloorus na kutaka wapewe simu, fedha na mali zingine.

“Senzo alitaka kumlinda Kelly sababu mmoja wao alikuwa amemwelekezea bunduki,” afisa mmoja aliwaambia waandishi wa habari. Polisi wanadai kuwa siku ya jana watu watu wawili waliingia nyumbani kwa Khumalo saa mbili usiku huku mwingine akisubiri nje na walipomaliza walikimbia.

Orlando Pirates,  imeandika kwenye Twitter: “@Orlando-Pirates family has learned with sadness of the untimely death of our number 1 keeper & captain Senzo Meyiwa.

Irvin Khoza, mwenyekiti wa club hiyo ameongeza: “This is a sad loss to Senzo’s family especially his children, to Orlando Pirates & the nation.”

Kina Mama Kuweni Waangalifu na Ma-House Girls Wenu Ndio Chanzo cha Kuharibika Ndoa zenu

0
0
Scenario No. 1
Kuna baadhi ya familia kuanzia baba hadi watoto kwa ajili ya kuogopa au usumbufu wa kuamka usiku kwenda kujisaidia walikuwa na makopo ndani kwa ajili ya huduma hiyo, basi cha kwanza dada akiamka asb ni kukusanya makopo vyumba vyote na kwenda kumwaga chooni. Is it fair jamani...... too bad aisee.

Scenario No. 2
Kuna baadhi ya familia hurundika chupi za week nzima, ikifika jumamosi Mama anakusanya chu.pi za familia nzima na kumkabidhi dada kwa ajili ya kuzifua. Kwa nini hivi?

Scenario No. 3
Kuna baadhi ya familia ambayo dada wa ndani haruhusuwi kula hadi member wengine wote wa familia wale ndio yeye afuate, ni mwiko kula na pamoja na member wengine wa familia na hata kula yeye anakula jikoni na si dinning kama wengine, na ni mwiko dada kukaa sebuleni. aiseee!

Wadau naomba tudadavue tatizo ni nini kwa nini wanawake walio wengi hushindwa kuishi vema na wadada wa kazi? (akina mama ndio huwa-control wadada hawa)

Kadhia hii ndiyo huweza kusababisha wadada hao kufanya malipizi yasiyofaa kama yale ya wao pia kulipiza kwa kuwatesa watoto na hata kuwadhuru kabisa.

Je ni kweli akina mama/dada walio wengi hawaelewi umuhimu wa wadada hao wa kazi?
Nasema haya kwa kurejea matukio mbalimbali ambayo nimepata kusimuliwa na kuona namna ambavyo akina mama/ dada wengi wanawafanyia wadada hao na hata kusababisha hata watoto wa familia hizo kuwadharau akina dada hao.

Naomba michango yenu wadau walau wengine wajifunze hapa namna bora ya kuishi na wadada hao ambao kwa kweli wanaachiwa dhamana kubwa ya kuwalea watoto wetu ambao hawana hata chembe ya undugu wa damu.

Nawapongeza wale ambao wanaishi na akina dada kama wanafamilia wengine kwa maana ya wanaishi kwa upendo na kuthaminiwa kama member wengine wa familia!

Mwandosya: Kumkejeli Warioba ilikuwa mbinu ya kupata ushindi

0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais asiye na Wizara Maalumu, Profesa Mark Mwandosya amesema kutumia lugha ya kejeli dhidi ya mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba ilikuwa mbinu ya kupata ushindi katika majadiliano wakati wa Bunge Maalumu la Katiba.

Mwandosya alitoa kauli hiyo jana alipozungumza na waandishi wa habari nje ya ofisi za CCM baada ya kuhudhuria kikao cha Halmashauri Kuu ya chama hicho ya Mkoa wa Mbeya.

“Katika eneo kama lile ni lazima utumie lugha ambayo ilikuwa siyo nzuri kwa Tume ya Warioba ili kuweza kusisitiza jambo fulani au ni njia ya ushawishi ili kuweza kupata ushindi,” alisema Mwandosya.

“Hivyo tunapaswa kuachana na maneno na maudhi yaliyofanyika wakati ule na kufuata misingi katika kuhakikisha tunapata katiba mpya kwa masilahi ya wananchi wetu.”

Alipoulizwa kuhusu Bunge hilo kutozingatia maoni ya wananchi kwa kuondoa vipengele vilivyokuwa katika Rasimu ya Katiba, alisema kuwa maoni ya wananchi yaliyotolewa, hayakuwa kura ya maoni.

Mwandosya alitetea kuwa katika vikao vya Bunge hilo hawakuwa na rasimu yoyote ambayo waliitumia katika kutafuta Katiba Mpya, zaidi ya ile iliyoandaliwa na Tume ya Warioba.

“Hapa naomba nifafanue vizuri kuwa hatukuwa na Rasimu yoyote ambayo tuliitumia nje ya Rasimu ya Jaji Warioba na ndiyo hiyo itakuja kwa wananchi kwa ajili ya kuipigia kura ya ndiyo au hapana,” alisema.

Kuhusu kuondolewa kwa vipengele ambavyo vinawapa wananchi nguvu ya kuwawajibisha viongozi wao, Mwandosya alisema wamefuatilia katiba zote duniani na kugundua kuwa wananchi wana haki ya kuwawajibisha wabunge wakati wa uchaguzi mkuu. Alisema wabunge wengi wamekuwa wakishindwa kwenye chaguzi kwa kuwajibishwa na wananchi.


Chanzo:Mwananchi

Jinsi Bilionea Wa Madawa ya Kulevya Bongo 'Chonji' Alivyokamatwa Huko Magomeni..

0
0
Stori: Makongoro Oging’ na Haruni Sanchawa
HII kali! Kukamatwa na polisi kwa mfanyabiashara bilionea jijini Dar, Mharami Mohamed Abadallah ‘Chonji’ (44) (aliyezungushiwa duara) hivi karibuni akidaiwa kukutwa na madawa ya kulevya ‘unga’ aina ya heroin yenye thamani ya shilingi 300,000,000 kumelitikisa Jiji la Dar, Uwazi limefuatalia hatua kwa hatua.


Mtikisiko huo umekuja kufuatia maeneo mbalimbali ya jiji kumzungumzia kwa namna mbili, wengine wakifurahia wengine wakisikitika, hasa wanawake wanaoishi maeneo ya Magomeni Kondoa, Dar  ambako mfanyabiashara huyo ndiko kwenye makazi yake.

AKUTWA NA SARE ZA JESHI
Tukio lingine liliwatikisa polisi wenyewe kufuatia upekuzi wa kina nyumbani kwake ambapo walimkuta pia na sare mpya za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) zinazofanana kwa sehemu kubwa na zile zilizomwingiza Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ kwenye mzozo na jeshi hilo.

AKUTWA NA BUTI
Mbali na sare kwa maana ya mavazi, pia mtuhumiwa huyo alikutwa na viatu vya jeshi hilo maarufu kwa jina la buti nazo zikiwa mpya!

BASTOLA NAYO
Katika hali iliyowatia shaka zaidi askari ni pale Mharami alipopekuliwa zaidi na kukutwa na bastola ambayo jeshi la polisi halijaitolea ufafanuzi inaitwaje na ilitengenezwa nchi gani!

VITU VINGINE
Vitu vingine vilivyokutwa kwa mtuhumiwa huyo ni jiko dogo la gesi na gundi ya plastiki, vyote vinaaminiwa kutumika wakati wa kutengeneza kete za unga tayari kwa kusafirisha.
Mharami, mbali na ishu zote hizo, anadaiwa kumiliki maghorofa mawili, Tandale na Magomeni Kondoa jijini Dar, mabasi na magari manne ya kutembelea mwenyewe.

ALIKAMATWA KAMA KWENYE SINEMA
Mharami alikamatwa Oktoba 21, saa saba usiku nyumbani kwake, Magomeni Kondoa lakini kwa mujibu wa mashuhuda, tukio hilo linasemekana kufananishwa na inavyokuwa kwenye sinema za Kimarekani.

Inadaiwa kuwa, awali askari zaidi ya 20 kutoka Kikosi cha Kuzuia na Kupambana na Madawa ya Kulevya Tanzania walifika kwenye nyumba hiyo kufuatia kutonywa kuwepo kwa unga na kumbana mtuhumiwa huyo akiwa na wenzake wanne ndani.Ikadaiwa kuwa, mtuhumiwa na wenzake walijaribu kutoroka  walipogongewa mlango na kukataa kufungua.

Chanzo hicho kiliendelea kudai kwamba baada ya Mharami kugoma kufungua mlango polisi walilipua mabomu ya machozi na kupiga risasi hewani ndipo alipokubali kufungua huku wenzake wakiwa wametawanyika kwa kupanda juu ya paa la nyumba ndogo kisha kupanda kwenye jumba  la ghorofa tano ambalo analimiliki mtuhumiwa huyo.

WATU WATOKA NA NGUO ZA KULALIA
Ikazidi kudaiwa kuwa, kufuatia milio ya mabomu na risasi, baadhi ya wakazi wa eneo hilo walitoka kushuhudia wengine wakiwa na nguo za kulalia tu.

ALICHOSEMA MJUMBE, MTENDAJI
Mjumbe wa Nyumba Kumi Shina Na. 2, Mwanamtama Sasamalo alipohojiwa na Uwazi alikiri kutokea kwa tukio hilo la kamatakamata ya askari kwa Mharami na wenzake.

“Ilikuwa kama saa saba usiku, polisi walinigongea nyumbani kwangu wakasema wanataka kumkamata mhalifu, tukafuatana hadi nyumbani kwa Mharami. Niliwakuta polisi wengine wakiwa na silaha wameizingira nyumba yake, nilichokishuhudia ni ungaunga ukiwa umesambaa chini, wahusika walikamatwa na kufuatana na askari,” alisema mjumbe huyo.

Naye Afisa Mtendaji wa Serikali ya Mtaa wa Makanya, Kata ya Ndugubi, Alex Mwisongo alipoulizwa alisema tukio hilo lipo, akaongeza kuwa vijana wengi wamekuwa mateja katika mtaa wake na wameathiriwa na unga ambao hajajua unakotoka.

KAMANDA NZOWA SASA
Naye Kamanda wa Polisi wa Kikosi cha Kuzuia na Kupambana na Madawa ya Kulevya Tanzania, SACP Godfrey Nzowa alipoulizwa na waandishi wetu ofisini kwake alisema Mharami alishawahi kukamatwa mwaka 2009 kwa kuhusishwa na madawa ya kulevya ambapo alikuwa chini ya uangalizi wa polisi na mahakama.

Aliwataja waliokamatwa naye safari hii kuwa ni Rehani Mursal (45), mkazi wa Mburahati (Dar), Abdul Abdallah (37), mkazi wa Mbezi Shamba (Dar), Tanaka Mwakasaburi (35), mkazi wa Magomeni- Makanya (Dar) na Maliki Zuberi (29), mkazi wa Magomeni Mwembechai (Dar).

Watuhumiwa hao wote walifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar, wiki iliyopita chini ya ulinzi mkali wa jeshi la polisi na askari magereza mbele ya Hakimu Janeth Kaluyenda na walipelekwa mahabusu ya Gereza la Keko, wanatarajiwa kurudi mahakamani Novemba 6, mwaka huu.
GPL

Jennifer Lopez Aonyesha Mwili Wake Akiwa Ndani ya Bikini..Miaka 45 Lakini Bado Chuma Mbichi

0
0
Mwanamuziki Jennifer Lopez Ameshare Picha Kwenye Instagram Profile yake Ambayo Inamuonyesha Akiwa Ndani ya Bikini akiwa na Umri wa Miaka 45 Sasa....

Changamoto kwa Mabinti..Hapa Bongo wengi Wakifisha 30 tu tayari Uzee na Minyama Uzembe...Chakua Hatua wacha Chips Kuku na Mibia ya Offer...Kidding lol

Hii Ndio Tofauti ya Wanafunzi wa Chuo wa Bongo na Wale Wa Ulaya Katika Picha

0
0
Nenda Google images andika Maneno Haya 'Wanafunzi wa Chuo'
Trust Me Zitakuja Picha nyingi za Aina hii Hapa Chini:



Halafu baada ya hapo andika ''University Students'' Zitakuja Picha za Aina Hii Hapa Chini:
Je Unaweza Sema Nini Kuhusu Picha hizo Hapo Mbili ? Je Wanafunzi wetu vyuoni Wanasoma Kweli? 

Penzi kwa Simu Linanoga, ila Nikimuona Penzi Nywiii

0
0


Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 24 naishi Dubai. Nimepata Mchumba ana umri wa miaka 37 na kakubalika nyumbani na tuko kwenye harakati za kufunga Ndoa.


Kwakweli huyu bwana ananipenda sana kupita kiasi . Ananijali na kunithamini na kuniongoza katika kila jambo na kunishauri mambo yake yote kuhusu maisha yake na kwa kila kitu kiasi ambacho kanisubiri muda wa Miaka mitano ili nimalize masomo ili anioe.

Kwakweli miaka yote hatuna tabia ya kutoka pamoja wala kuonana ila nimazungumzo kwenye simu tu kwa muda wa miaka miwili.

Anakuja kwetu kawaida na mie kwakweli namempenda huyu kwa jinsi anavyonipenda na kunijali na navutiwa naye sana nikiwa naongea kwa simu kiasi ambacho siwezi kukaa siku bila kuongea nae na siwezi kufanya jambo bila kumshauri yeye tu.

Lakini cha kunishangaza akija kwetu kuonana na mie Moyo wangu unabadilika nahisi kuwa kama sijampendaa huyu mtu!

Naomba usinielewe vibaya  kusema kweli  nikikaa nikifikiria kiakili nahisi  sijaimpenda sura yake kwakweli na kwajinsi nilivyo huwa inanijia kama tukitoka wote itakuwa vipi?

Ila moyoni nampenda sana na siwezi kumkosa kabisa. Kwakweli nahisi nachanganyikiwa sijui nijiamulie vipi niufate moyo wangu au akili yangu?

Naogopa sana ikaja ikawa tatizo kwenye ndoa yangu na kutompa furaha anayoitarajia au je hili halitokuwa tatizo nikioana nae kwa vile Moyoni nampenda ntakuja kumpenda na kutojali sura yake.

Naomba Ushauri

Waganda Nao Wacharuka Mitandaoni na Kusema Miss wao Mpya ni Mbaya Hakustahili Kushinda

0
0
Wakati Sitti Mtemvu akiwekwa kitimoto na Watanzania kwa kudanganya umri wake, Waganda nao katika mitandao ya kijamii wamecharuka na kuwakaba koo waandaaji wa Miss Uganda kuwa mshindi aliyepatikana Leah Kalanguka Miss Uganda 2014 ni mbaya na hakufaa kushinda taji hilo.

Kwa kumuangalia tu mrembo huyu, ni kweli hakustahili taji hilo?

TBC Yashika Nafasi ya Mwisho Kuangaliwa na Wananchi

0
0
Kwa hali ya kushangaza, kituo cha television cha matangazo cha tbc 1 kati ya vituo vinne maarufu vya matangazo ya habari nchini Tanzania kimeshika nafasi ya mwisho baada ya kufanyiwa utafiti,

Kwa habari za uhakika ni kwamba kituo kilichoongoza kuangaliwa na watazamaji wengi ni ITV kikifuatiwa na Star TV, nafasi ya tatu imeshikwa na Channel 10 na hatimaye TBC1.

Kwa utafiti uliofanya na na TCRA imebainika kuwa ni aibu kama kituo television ambacho ni cha Taifa na ni UMMA kushika mkia nyuma ya vituo binafsi jambo ambalo ni hatari.

Vyanzo vya kuaminika vinadai kuwa TBC1 imefikia hapi baada ya kugundulika inabagua baadhi ya habari ya vyama vya siasa na kutoa habari ya chama kimoja tuu jambo ambalo siyo sahihi katika utashi wa utangazaji na kutofuata uhuru wa kiutangazaji ndani ya uongozi wa shirika la habari la Tanzania, 

Utafiti umeonyesha kuwa ili chombo cha habri kiweze kuangaliwa na watu wote wa vyama vyote ni lazima chombo cha habari kitoe habari bila kubagua vyama vya siasa maana watazamaji wana misimamo tofauti na itikadi tofauti, na kama chombo cha habari kikiamua kutoa habari kwa chama kimoja cha siasa basi ujue hapo watakaoangali hizo taarifa za habari ni hao hao wa chama kimoja.

Watafiti pia walienda mbali zaidi na kukinyoshea vidole kituo cha taifa cha utangazaji kuwa ni chombo cha UMMA na kisipende kubagua baadhi ya taarifa za habari za vyama vya siasa kwa misingi ya kuelekezwa na wanasiasa au viongozi wa nchi maana madhara yake ni wananchi kushindwa kuangalia hicho kituo.

Mwisho wake kitashindwa kufanya biashara na hatimaye kutegemea tuu ruzuku serikalini na hapo ndo nchi itazidi kupata hasara badala ya kukiacha chombo kijiendeshe kwa uhuru. Wametoa mfano kama shirika la habari la Uingereza BBC lingefanya kama TBC inavyofanya basi nayo ingeishia kutazamwa tuu nchini uingereza na tena kwa watu wachache tofauti na ilivyo sasa BBC inatazamwa duniani kote.

Utafiti umeonyesha kuwa hivi vyombo vingine vya habari ITV, Star TV na Channel 10 vimepata watazamaji wengi kwa kuwa havibagui matangazo ya kada tofauti ya vyama vya siasa na hapo ndoo inasababisha waweze kupata watazamaji wa kutosha.

Mwanamuziki Chid Benz Kuendelea Kunyea Debe Mahabusu, Aingia Mahakamani Kavaa Mlegezo

0
0
MSANII wa Muziki wa Kizazi Kipya (bongo fleva), Rashidi Abdallah Makwaro (29), maarufa kama Chid Benz, amefikishwa mahakamani akikabiliwa na mashitaka matatu ikiwemo kukutwa na Dawa za kulevya aina ya Heroin yenye thamani ya Sh. 38,638, bangi ya Sh. 1,720 na vifaa ya kuvutia dawa hizo kijiko na kigae.
Chid Benz amefikishwa  mapema leo saa 3:00 asubuhi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kusomewa mashitaka yake. Saa 7:50 mchana alifikishwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Warialwande Lema aliyepangiwa kusikiliza kesi hiyo.
Hata hivyo, hakimu aliamuru msanii huyo kutolewa nje ili akave vizuri nguo baada ya suruali aliyokuwa amevaa mlegezo maarufu kama kata kei kuonyesha nguo yake ya ndani.
“Kwanza mtoeni nje aende akavae nguo hizo zinazodondoka…” aliamuru Hakimu.
Saa 7:54 alirejeshwa ndani ya chumba cha mahakama upande wa Jamhuri ukiongozwa na Wakili wa Serikali Mwanaamina Kombakono akisaidiana na Inspekta Jackson Chidunda, ulimsomea mashitaka yake.
Wakili Kombakono alidai kuwa Oktoba 24, mwaka huu katika uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, uliopo Ilala jijini Dar es Salaam, mshtakiwa alikutwa dawa za kulevya aina ya heroin isivyo halali zenye uzito wa gramu 0.85.
Katika shitaka la pili, ilidaiwa kuwa siku na eneo la tukio la kwanza, mshtakiwa alikutwa na gramu 1.72 za bangi isivyo halali.
Wakili huyo wa serikali alidai kuwa, siku na eneo la tukio la kwanza na la pili, mshtakiwa alikutwa akiwa na vifaa vinavyotumika kuvua dawa za kulevya aina ya heroin, kigae na kijiko huku akijua ni kosa.
Mshtakiwa alikana mashitaka yote na upande wa Jamhuri ulidai kuwa hauna pingamizi na dhamana dhidi ya mshtakiwa.
Hakimu Lema alisema mshtakiwa atakuwa nje kwa dhamana kwa masharti ya kuwa na wadhamini wawili wanaotoka kwenye taasisi zinazoamini na siyo walimu na dhamana ya Sh. Milioni moja.
Hata hivyo, mshtakiwa alishindwa kutimiza masharti hayo na amepelekwa mahabusu hadi Novemba 11, kesi hiyo itakapotajwa.

Ajali mbaya Jeti Lumo Mwisho wa Lami, Gari lenye Kontena Ladondokea Daladala

0
0
Kumetokea ajali mbaya  maeneo ya Jeti Lumo mwisho wa lami ambapo gari kubwa la mizigo limeangukia daladala iliyokuwa kituoni.

Ajali hiyo imetokea wakati gari hilo semi-trailer ikikata kona pale mwisho wa lami ambapo kontena lilianguka na kutua juu ya bodi ya daladala.

Kweli ni kontena imeangukia hiace sema hakuna majeruhi wala aliyepoteza maisha sema hiace imekuwa chapati.

Balotelli Anusurika Kutiwa Hatiani Baada ya Kumtukana Mwanamke Aliyekuwa Akipiga Picha ya Gari Lake

0
0
Jeshi la polisi nchini Uingereza halitomchukulia hatua za kisheria mshambuliaji kutoka nchini Italia na klabu ya Liverpool Super Mario Barwuah Balotelli kufuatia madai ya kumtolea maneno makali mwanamke mmoja aliyekua akichukua picha za gari lake.

Balotelli anadaiwa kufanya hivyo kutokana na kuchukizwa na kitendo cha mwanamke huyo ambae alionekana akichukua picha za gari lake aina ya Ferrari juma lililopita.

Taarifa za jeshi la polisi mjini Manchester zimeeleza kwamba hakuna uhalifu wowote uliotokea na kumuhusu mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 24 ambao umewasilishwa kwao ama kurekodiwa.

Hata hivyo imeelezwa kwamba mwanamke anaedaiwa kutolewa maneno makali na Baliotelli hakuwasilisha malalamiko katika jeshi la polisi na ndio maana ripoti ya jeshi hilo imeonyesha hakuna lolote linaweza kumfika Balotelli.

Jack Wolper Amwangukia Mkongo na Kumuomba Msamaha

0
0
BAADA ya hivi karibuni kumchana laivu Mkurugenzi wa Mwami Foundation, raia wa Kongo, Mwami Rajabu, staa wa Bongo Movies, Jacqueline Wolper Massawe anadaiwa kumwangukia jamaa huyo na kumuomba msamaha.

Kikizungumza na Risasi Mchanganyiko, chanzo makini kilidai kwamba baada ya gazeti ndugu na hili kuripoti habari ya Wolper kumchana Mkongo huyo huku akidai hana hadhi ya kuwa naye, wiki iliyopita alionekana kwenye Hoteli ya Double Tree iliyopo Masaki jijini Dar ambako ndipo alipofikia mwanaume huyo.

Kiliendelea kueleza kwamba mwanadada huyo alifika hotelini hapo kwa ajili ya kumuomba msamaha Mkongo na alikuwa akifanya jitihada kubwa ili asamehewe kwa kumtumia mwanamuziki wa FM Academia, raia wa Kongo, Patcho Mwamba amuombee msamaha.

“Nimemuona Wolper akiwa na huyo Mkongo kwenye hoteli hiyo aliyofikia ambapo kilichompeleka ni kuomba msamaha kutokana na maneno aliyozungumza kwenye gazeti,” kilisema chanzo hicho.

Baada ya kupata habari hizo kutoka kwa chanzo, kwanza alitafutwa Patcho Mwamba aliyedaiwa kusumbuliwa na Wolper akimtaka amuombee msamaha kwa Mkongo huyo ambaye ndiye aliyemuunganisha naye ambapo alikuwa na haya ya kusema:

“Siyo kweli kwamba Wolper anaomba msamaha mpaka sasa, kwani ameshasamehewa na wako vizuri kabisa kwani siku ile gazeti lilipotoka tu usiku wake tulikutana na Mkongo wakayamaliza.”

Kwa upande wa Mkongo alipoulizwa kuhusiana na habari hiyo alisema ni kweli Wolper alikuwa hotelini hapo akiomba msamaha huku akisema kwamba hakuwahi kuzungumza maneno kama hayo yaliyoandikwa gazetini hivyo aliamua kumsamehe.

“Nilimsamehe na sasa sisi ni marafiki wa kawaida tu siyo kimapenzi kwa sababu mimi nina mke na watoto sita na ninamuogopa sana mke wangu halafu hapa Tanzania sijaja kutafuta wanawake bali nimekuja kwa ajili ya biashara lakini nawashangaa hawa wasanii wa kike kunipakazia kwamba mimi nina uhusiano nao.

“Ipo siku nitafunguka mengi na watakoma kumendea waume wa watu,” alisema Mkongo.
Kujibu tuhuma hizo, Wolper alisema: “Watu wanasema sana lakini hakuna anayejua mimi na Mwami tukoje, kama ni bosi wangu au ni bwana wangu. Labda kama mtu aliniona nasalimiana naye akadhani nilikuwa naomba msamaha. Hakuna kitu kama hicho.”
GPL
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live




Latest Images