Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104414 articles
Browse latest View live

Baada ya Wema Sepetu Kumwaga Diamond, Mama Wema Afanya Sherehe

0
0
CHEREKO chereko! Siku chache baada ya supastaa ‘grade one’ wa sinema za Bongo, Wema Sepetu ‘madam’ kummwaga King of Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, mama mzazi wa mwigizaji huyo, Mariam Sepetu ameangusha sherehe ya nguvu kama ishara ya kuonesha ‘amekunwa’ na tukio hilo, Ijumaa Wikienda linashuka nayo mstari kwa mstari.

TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo makini, kutokana na mama huyo kutobariki uchumba wa mwanaye na Diamond ambaye pia anajulikana kwa jina la Dangote kwa muda mrefu, habari za uchumba huo kuvunjika zilipochapishwa kwenye Gazeti la Ijumaa ‘Kubwa’ toleo lililopita, moyo wake ulijawa na furaha.

“Mama Wema alichukizwa kwa kiasi kikubwa na mapenzi ya wawili hao kutokana na kile alichoamini kuwa, Diamond hakuwa na mapenzi ya dhati kwa mwanaye zaidi ya kutegemea nyota yake impe mafanikio ndiyo maana akafanya pati hiyo fupi nyumbani kwake Sinza-Mori, Dar,” kilisema chanzo hicho.

SHEREHE ILIVYOKUWA
Chanzo hicho kilizidi kumwaga unga kwamba, sherehe hiyo ilikuwa ni ya aina yake kwani mama Wema aliwaita mashosti zake, wakaandaa ‘menu’ ya ukweli kabisa, wakasherehekea lakini bahati mbaya Wema hakuhudhuria.

“Wema hakuweza kuhudhuria sherehe hiyo kutokana na kubanwa na majukumu mengine. Bi mkubwa aliwaita marafiki zake, wakafungua shampeni, wakala, wakanywa na kucheza muziki kufurahia Dangote kupigwa chini,” kilisema chanzo hicho.


MAMA NA CHUKI YA MUDA MREFU
Chanzo hicho kilizidi kumwaga ubuyu motomoto kuwa, mama Wema alipiga cherekochereko za kutosha siku hiyo kwani alikuwa akimchukia Diamond kwa muda mrefu.

“Mama Wema chuki zake kwa Diamond hazitaisha kamwe kwa kuwa hampendi tu kutokana na kuona mwanaye hasongi mbele kimaendeleo kama alivyo Diamond ambaye akiachana na Wema mambo yake hayamwendei vizuri kama anavyokuwa na mwanaye.”


MAMA WEMA ANENA
Baada ya wanahabari wetu kunasa maelezo hayo ya chanzo, walimvutia waya mama Wema ambaye alikiri kufanya sherehe fupi baada ya mwanaye kummwaga Diamond.
“Mimi naona huu ndiyo mwisho wa Wema na Diamond na siku zote nasema hakuna uhusiano ukadumu bila baraka za wazazi, niseme tu, sitaki kumuona ndugu yeyote wa Diamond kwangu, kama mahari wakatoe kwa Penny siyo kwa mwanangu,” alisema mama Wema.

TUJIKUMBUSHE
Kumwagana kwa Wema na Diamond safari hii, ni mara ya nne. Awali walimwagana, wakarudiana, wakamwagana tena, Diamond akatua kwa Jokate Mwegelo, wakarudiana tena na Wema, wakaja mwagana tena, Diamond akatambaa na Penniel Mungilwa ‘Penny’, wakamwagana, karudiana na Wema, sasa  wamemwagana tena.
GPL

Uvaaji wa Cheni ama Vikuku Kwa Mwanamke Miguu Yote Miwili

0
0

Unaweza kuta kavaa mguu mmoja au yote miwili wao wanaita (VIKUKU) huwa zina ashilia au kumanisha nini? 

Huku mtaani midume huwa tuna danganyana sana juu ya hii kitu Wengine husema ukimuona anazo pande zote huyo antoa kotekote, Ebu tupeni ukweli wana dada au ni urembo tu kama heleni....?

Sheria Ngowi Afunika Katika Maonyesho ya Mavazi Huko South Africa

0
0
Mbunifu wa kimataifa wa mavazi kutoka Tanzania, Sheria Ngowi amedhihirisha kuwa yeye ni nguli katika ubunifu baada ya kufinika katika onyesho la mavazi la kimataifa lijulikanalo kama Mercedes Benz Fashion Week Africa 2014 lililofanyika juzi Ijumaa mjini Johannesburg, Afrika Kusini.

Ngowi alionyesha mkusanyiko wa mavazi aliyoyaita 'PRIDE' yaani kujivunia,  kama moja ya njia za kumuenzi Baba wa Taifa, Mwl. Julius Nyerere pamoja na viongozi mashuhuri waliopigania uhuru Afrika.

Afrika Kusini ilizizima na kuduwaa kwa muda usiopungua dakika 15 pale ambapo mavazi mbali mbali yaliyobuniwa na Ngowi yalipokuwa yakioneshwa katika ukumbi wa Melrose Arch.

Sheria Ngowi alionyesha mkusanyiko wa mavazi aina ya suti yenye ubunifu na ueledi wa hali ya juu kwa kutumia vitambaa vya kisasa na kale vilivyonakshiwa kwa maua na rangi za kuvutia kama nyekundu, zambarau, machungwa, nyeupe na nyeusi  huku mengine yakiwa bila maua lakini yaliyong'aa kwa kutumia rangi imara kama blu, kahawia na kijivu.

Onyesho hilo la Mercedes Benz Fashion Week Africa 2014 lilihudhuriwa na watu mbali mbali wakiwemo viongozi wa umma kutoka Afrika kusini, Balozi wa Tanzania Afrika Kusini, Radhia Msuya, wabunifu wa mavazi kutoka nchi za Afrika kama Taibo Bacar kutoka Mozambique, David Tlale kutoka Afrika Kusini, waandishi wa habari kutoka sehemu mbali mbali za dunia na wadau wa mitindo.

Mercedes Benz Fashion Week Africa 2014 ni onyesho la kimataifa linalofanyika nchini Afrika Kusini mara moja kwa mwaka likikusanya zaidi ya wabunifu wa mavazi 35 kutoka Afrika kwa ajili ya kuonesha ubunifu wa mavazi yao ambapo kwa mwaka huu Sheria Ngowi ni mbunifu pekee aliyechaguliwa katika onyesho hilo kutoka Tanzania.

Sheria Ngowi anasifika kwa ubunifu wa mavazi aina ya suti, kanzu,sare za makampuni, mashirika, shule na hafla mbalimbali kama harusi.Mbunifu huyu alifungua rasmi ofisi zake zilizopo Masaki, mtaa wa Buzwagi mkabala na Ubalozi wa Angola mwaka mmoja na nusu uliopita ambapo alianza kazi kwa kuwatengenezea mavazi watu kutoka nchi mbalimbali duniani.

Pongezi nyingi kwa Sheria Ngowi, unaipeperusha vyema bendera ya Tanzania kwa kipaji chako na kazi zako nzuri.

Paul Makonda Akana Kumpiga Jaji Warioba, Asema Anamheshimu Kama Babake Mzazi

0
0
Katibu wa Uhamasishaji Umoja wa Vijana wa CCM, Paul Makonda akionesha kwenye simu yake picha ya video iliyopigwa wakati wa vurugu zilizotokea wakati wa mdahalo wa kujadili raismu ya Katiba inayopendekezwa, kwenye Ukumbi wa Ubungo Plaza  jana, ambapo Makonda aliyedaiwa kump[iga aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Waziri Mkuu wa zamani Jaji mstaafu Joseph Warioba, amekanusha kumpiga leo katika mkutano wa waandishi wa habari, Dar es Salaam. Pia Makonda amesema kuwa ahwezi kabisa kudiriki kumpiga kwani anamheshimu kama babake mzazi. Amesema kuwa hata leo asubuhi amezungumza na warioba kwenye simu kumjulia hali. Warioba naye amekanusha kupigwa na Makonda wala mtu yoyote kwenye vurugu hizo.

Makonda akisisitiza jambo katika mkutano huo ambapo pia aliwaambia kazi kubwa aliyoifanya wakati wa vurugu hizo, ni kumsaidia Warioba kutoka salama pamoja na Mwanasiasa mwenye ulemavu wa macho ambaye pia alikuwa anamuokoa ili asipatwe na dhahama hiyo.

Makonda akiendelea kuelezea kuwa anasikitishwa na vyombo vya habari ikiwemo mitandao ya kijamii iliyomzulia kwamba yeye ndieye aliyesababisha vurugu wakati siyo. Pia amelaani watu wote waliosababisha vurugu hizo kwamba kitendo hizho kinadhoofisha demokrasia nchini. Habari, picha na Richard Mwaikenda wa Kamanda wa Matukio blog

Rufaa ya Sheikh Issa Ponda Yatupiliwa Mbali Aendelea Kusota Mahabusu

0
0
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, leo imetupilia mbali rufaa ya Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda iliyopelekwa na wakili wake Juma Nassoro ya kupinga hatia ya adhabu aliyohukumiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akidai kuwa hapakuwa na ushahidi wa kutosha wa kumtia hatiani kwa mashtaka yaliyokuwa yakimkabili.

Kesi nyingine ya uchochezi inayomkabili kiongozi huyo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambayo inasikilizwa na Jaji Augustine Shangwa imeahirishwa hadi Novemba 20, mwaka huu.

Ndoa ya Shilole na Mchumba Wake Nuhu Mziwanda Haipo Tena

0
0

IMEGUNDULIKA kuwa uhusiano wa staa wa Mduara, Zuwena Mohamed ‘Shilole’, na mpenziwe Nuh Mziwanda ni kazi bure kwani uwezekano wa kufunga ndoa kati yao haupo kutokana na kupishana imani.Ishu hiyo imejidhihirisha juzikati nyumbani kwa wawili hao Mwananyamala-Manjunju jijini Dar, baada ya paparazi wetu kuwaibukia na kutaka kujua malengo yao zaidi kama wana mpango wa kuoana au la, msikie kwanza Nuh:

Mimi ninampenda Shilole kwa asilimia 100,  ila siko tayari kubadili dini kwa ajili yake maana kwetu ni wakristo na hapa naongea mama yangu ni mzee wa kanisa hivyo Shilole naamini anaweza kubadili maana mimi tayari nimeshafanya mengi sana juu yake.”

Msikie Shilole: Mimi siwezi kubadili dini maana Nuh ndiye alisema atabadili hata hivyo familia yangu haiwezi kunikubalia kubadili dini kwa ajili ya kufunga ndoa kama amesema naye hawezi kubadili basi tutaishi tu maana hata ndoa ya serikali yenyewe hawezi na maisha siyo lazima tuoane.

Hiki Ndicho Walichokisema Maprofesa wa UDSM Kuhusu ishu ya Diamond kupewa Shahada ya Udaktari

0
0
Ni kama wiki moja sasa tangu kuenea kwa habari ya kua Diamond Platnumz atapewa shahada ya Udaktari katika chuo kikuu cha Mlimani. Baada ya taarifa hizo kuenea sana tumebahatika kupata mahojiano ya maprofesa wawili kutoka chuo cha Mlimani wakizungumzia ishu hii.

Wote wawili wamekubali kua Diamond ni msanii mkubwa lakini hajafikia hadhi ya kupewa shahada ya heshima ya udaktari.Angepata tu endapo tu angefanya jambo ubwa na kusaidia jamii na kwamba kuimba na kupendwa na watu si kigezo kikubwa cha kupewa tuzo hizo.

Unaweza sikiliza mahojiano hayo hapa chini……

Lulu Michael 'Mambo Yakimapenzi Yamepitwa na Wakati Kwangu'

0
0
Stori: Hamida Hassan na Gabriel Ng’osha
MASTAA wana mambo! Mtoto mzuri Bongo Movies, Elizabeth Michael ‘Lulu’ ametoa kali ya aina yake kwa kusema kamwe hatumii nguvu nyingi kwenye mapenzi kwa sababu yanapoteza muda bila sababu za msingi bora nguvu zake azitunze hadi pale atakapokuwa akijifungua.

Akimwaga cheche mbele ya mwanahabari wetu, Lulu alisema siku hizi wanaume wengi wanawafanya wasichana watumie nguvu kutetea penzi kutokana na migogoro isiyokuwa na msingi.

“Bora nguvu zangu nizihifadhi za kuendea leba kuliko kuzipoteza katika mapenzi kwani hayo mambo yamepitwa na wakati kabisa,” alisema Lulu.

Aibu:Uwanja wa Ndege Dar Washika Nafasi ya Nne kwa Uduni

0
0
Mkurugenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Moses Malaki amesema uwanja wake umechakaa kiasi cha kukosa sifa za kuwa uwanja wa kisasa barani Afrika na dunia.

Kauli ya Malaki imekuja baada ya ripoti ya matokeo ya utafiti wa mtandao wa Sleeping in Airport uliyofanywa 2014 kuonyesha kuwa JNIA inashika nafasi ya nne kwa viwanja duni Afrika.

“Huo ni ukweli usiopingika kwa sababu uwanja ulijengwa zamani na miundombinu yake haikidhi mahitaji ya sasa…. hali ni mbaya,” alisema Malaki.

“Kiwanja kinakabiliwa na tatizo la miundombinu chakavu, vyoo visivyotosheleza na wakati huohuo kuzidiwa na wingi wa abiria, jambo linalosababisha huduma zake kuwa chini ya kiwango.

“Hatuwezi kuwa bora kwa uwanja huu… hebu fikiria uwanja uliojengwa kuhudumia watu milioni 1.2 kwa mwaka, sasa unahudumia watu 2.5 milioni, hapa lazima huduma zitakuwa chini ya kiwango na msongamo utakuwa mkubwa.”

Alisema katika kukabiliana na changamoto ya msongamano, ofisi yake iko katika hatua za kuongeza vizimba vya kugongea hati za kusafiria kutoka saba vya sasa na kuwa 21.

Alisema tayari wameshazungumza na Waziri wa Mambo ya Ndani kwa ajili ya kuongeza wafanyakazi, pia kuunganisha na kuwa sehemu moja kwa mlango wa abiria wanaowasili na wa ndani, kazi itakayokamilika wiki mbili zijazo.

Utafiti

Utafiti wa Sleeping in Airport ulitokana na maoni ya wasafiri waliopitia uwanja huo ambao walielezea na kupiga kura kuhusu huduma, miundombinu na uwezo wa viwanja hivyo kutumika kama eneo la kulala wasafiri inapobidi.

Nafasi ya kwanza kwa uduni ilishikwa na uwanja wa kimataifa wa Khartoum, Sudan ukifuatiwa na N’dijili, Kinshasa DRC na Tripoli Libya nafasi ya tatu.

Katika taarifa yake, mtandao huo ulisema Afrika ina sifa ya kuwa na viwanja vingi vyenye sifa mbaya duniani, ikiwemo uchafu wa sakafu, vyoo, vitendo vya rushwa, ukosefu wa viyoyozi licha ya joto kali, migahawa ya kawaida lakini ghali na michakato ya usalama inayotia shaka.

William Malecela: Jaji Warioba Anaishi kwa mlo wa CCM Kwanini Anaishambulia Serikali

0
0
Warioba ni Kiongozi wa Taifa mstaafu aliyekuwa amewahi kushika nafasi nyingi na kubwa sana za Taifa ikiwa na maana alipokuwa Makamu wa Kwanza wa Rais angeweza kushika Urais kama anything could have happened to the President. 

Kinachoshangaza na kuhuzunisha ni jinsi Warioba ambavyo amekuwa na msimamo wa kuipinga CCM na Serikali yake baada ya kuvitumikia kwa uaminifu mkubwa karibu robo tatu ya maisha yake hapa Duniani, amekuwa akililia Serikali Tatu kitu ambacho sasa kinamfanya aonekane kwamba Rasimu na Tume yake nzima walikuwa na agenda ya siri maana haiwezekani kwamba kazi yake ilikuwa kupokea mawazo ya wananchi sasa imekuwa Vita baoina yake na Serikali juu ya mawazo ambayo utafiti wote wa kisayansi unaonyesha kwamba hayakuwa mawazo ya Wananchi wote waliohojiwa kama alivyodai kwenye Rasimu. 

Wakati umefika wa Warioba kuamua aidha kujiunga na Upinzani au kuanzisha Chama chake cha Upinzani kwa sababu sijawahi kusikia Mh. Mbowe akipigwa na Wananchi kwa kuipinga Serikali ya CCM, Wananchi hawataki kuona Kiongozi yoyote wa Taifa anayeishi kwa mgongo wa CCM kuanza kuishambulia Serikali ile ile inayompa mlo. 

Wananchi wanajua kwamba Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania anapewa nyumba ya kuishi, wafanyakazi kama 5 wa kumhudumia, Nyumba ya kufikia Dodoma, 80% ya Mshahara wa Waziri Mkuu na Kusafiri Ulaya mara 2 kwa Mwaka kwa matibabu yeye na mkewe na hii ni mpaka mwisho wa maisha yake hapa Duniani, sasa kwa mutu kama huyu anayepata haki zote hizi tofauti na Wanancchi wa kawaida na anazipokea bila malalamiko leo anaposimama kuipinga Serikali ile ile ndio inaamsha hisia za Wananchi zilizopelekea matatizo yalimyomkuta jana. 

Wananchi wa Tanzania wameshaonyesha kwamba hawana muda na Viongozi wanafiki wanaokula raha chini ya Serikali ya CCM halafu wanataka kuwahadaa wananchi kwa maneno mengi ya kilaghai
Source:Jamii Forums

Si Chid Benz tu, Uteja wa Madawa ya Kulevya Bongo Flava Upo Hivi

0
0
Ni matunda ya saikolojia mgeuko, au unaweza kuita saikolojia kinyumenyume (reverse psychology). Yanayokatazwa yanavutia zaidi watu kuyatenda. Hakuna mtu ambaye hajui athari za matumizi ya madawa ya kulevya lakini kuna watu huwaambii kitu.

Madawa ya kulevya ni sumu, ni kifo, inatangazwa hivyo leo, yule aliyekuwa anasikiliza tangazo, kesho anaanza kutumia. Hiyo ndiyo inaitwa reverse psychology, na mara nyingi huwasumbua sana vijana, maana damu inachemka, nguvu ya mwili inawadanganya.

Unadhani wakati Rehema Chalamila ‘Ray C’ anaanza kutumia ‘unga’ alikuwa hajui madhara yake? Ni kama ambavyo Rashid Makwilo ‘Chidi Beenz’ alivyo na taarifa zote muhimu kuhusu sumu iliyomo kwenye mihadarati lakini hivi karibuni alikamatwa nayo Air Port.

Chidi alitangaza sana mwaka juzi kwamba ameachana na matumizi ya madawa ya kulevya. Binafsi niliamini kwa namna alivyokuwa anazungumza kwenye vyombo vya habari. Hata hivyo muonekano wake ulikuwa unatia shaka kidogo kuamini kama kweli kaacha.

Namfahamu Chidi, ni mwanamuziki wa Hip Hop aliyekamilika sana. Sauti yake pekee ni mtaji, kwani anaweza kupanda, kushuka na kuigeuza alivyotaka, vilevile anayo staili inayomfanya awe wa kipekee. Ni mkali wa miondoko (swagger) ambayo inampa thamani ya kuwa mwana-Hip Hop mwenye mvuto.

Chidi ana pumzi na nguvu (energy) akiwa jukwaani. Kwa tathmini yangu kama mwandishi wa habari, vilevile mdau katika soko la muziki (hasa kizazi kipya) na sekta ya burudani Tanzania kwa jumla, nathubutu kusema ndiye mwanamuziki wa Hip Hop ambaye hutumia nguvu nyingi jukwaani na kumudu kufanya shoo kwa muda mrefu tena kwa ufanisi.

Mara kadhaa niliwahi kujiuliza, kama alikuwa anaonesha uwezo huo jukwaani ilhali anatumia ‘madude’, je, angekuwa hatumii? Bila shaka angeweza kufanya zaidi. Jicho langu kimuziki linaniaminisha kuwa Chidi alizaliwa ili awe mwanamuziki wa Hip Hop. Ni mkali siyo siri!

Ni mmoja kati ya wanamuziki wachache wa Hip Hop nchini wenye uwezo wa kutumbuiza kwa ‘live band’ na kukonga nyoyo za hadhira kwa kiwango cha juu. Kama wewe ni shabiki wa Hip Hop, unataka nini kingine pale Chidi anapokuwa jukwaani kifua wazi?

Nimeshafanya kazi nyingi na Chidi, pamoja na sifa yake inayojulikana kwa wengi kwamba ni rapa mkorofi ambaye mara kwa mara hukwaruzana na wasanii wenzake na watu wengine lakini upande ninaoutambua ni kuwa mwanamuziki huyo si kigeugeu kwenye kazi.

Ni mtata sana, hilo hata yeye mwenyewe anajijua. Kujisema kwa watu kuwa ni mkorofi haoni tabu. Siku moja, sikumbuki tarehe ila ilikuwa mwaka juzi, nilipokuwa namtuliza asimvae mtangazaji wa EATV, Allan Lucky, aliniambia yeye ni “arnimal”, akimaanisha mnyama mkali aliye tayari kurarua mtu muda wowote.

Pamoja na sifa zote lakini hata mara moja sikuwahi kukubaliana naye halafu akaenda kinyume na makubaliano. Wakati wa mazungumzo kutofautiana lazima, ila makubaliano yakishafikiwa atatenda kama ambavyo tuliafikiana.

Ni tofauti na wasanii wengi tu ambao hawatumii ‘madude’ lakini si waaminifu katika makubaliano hata kama yapo kwa maandishi. Chidi akiwa jukwaani, anajua afanye nini kwa wakati gani kwa kuangalia sura ya hadhira ambayo anacheza nayo.

Mtazame Ray C, alilishika soko la Bongo Flava siyo Tanzania tu, Afrika Mashariki kwa jumla. Wakati huo dada yetu huyo alitambulika zaidi kwa jina la ‘Kiuno Bila Mfupa’ kutokana na uhodari wake wa kuzungusha nyonga yake, japo kizembezembe, maana huwezi kufananisha na vya wakata nyonga wa siku hizi kama Snura na Shilole.

Wakati Ray C akiwa amelegea kwa matumizi ya madawa ya kulevya, nilizungumza na mdau mkubwa wa muziki Kenya, Refigah anayemiliki lebo ya Grandpa Records, akanieleza masikitiko yake kisha akaniambia: “Pamoja na hali aliyonayo, Ray C akiwa Kenya ni biashara kubwa, Wakenya wanampenda sana, pesa zake zipo njenje.”

Mwanamuziki lulu barani Afrika, Brenda Fassie, alifariki dunia dunia mwaka 2004. Ripoti za kifo chake zipo wazi kwamba kilichomsababishia mauti ni mdawa ya kulevya, kwani asubuhi ya siku yake ya mwisho, alitumia kiwango kikubwa cha Cocaine.

Laiti kama Ray C angechukua kifo cha Brenda kama shule kwake, sina shaka kwamba pengine angekaa mbali na mihadarati. Tatizo ni kwamba akili ya binadamu hufanya kazi tofauti, mara nyingi hushawishika kufanya yanayokatazwa. Reverse psychology ndiyo sababu ya Hawa kumshawishi Adam kula tunda la mti wa katikati kwenye Bustani ya Eden.

Mwanzoni mwa miaka ya 2000, mkongwe wa Hip Hop Tanzania, Terry Msiagi ‘Fanani’ wa Kundi la HBC, alishaanza kulalamika kwamba matumizi ya madawa ya kulevya yamempotezea dira na anatamani kuacha. Yaani kadiri watu wanavyolalamika, ndivyo na wengine wanavyoshawishika kutumia.

Mkongwe Mack 2B Simba hatunaye, kifo chake kilifuata baada ya afya yake kuzorota kutokana na matumizi ya madawa ya kulevya. Mateso ya Banza Stone na hata kifo cha Ngwair ni mifano hai, sasa ni kwa nini bado zipo taarifa kwamba akina TID wanatumia unga?

Ulimwengu umeshapoteza vipaji vingi kupitia madawa ya kulevya. Kuna ambao walikuwa wanatengeneza fedha nyingi kwa vipaji vyao kama Amy Winehouse, Whitney Houston, Heath Ledger, Cory Monteith na wengineo, leo hawapo nasi. Unga uliharakisha vifo vyao.

Kuna mastaa kama Lindsay Lohan, Robert Downey Jr, Charlie Sheen, Chris Brown, Bobby Brown, Britney Spears na wengineo wengi, wamegeuka mateja. Maisha yao yanavyoharibika si kificho lakini hawajifunzi. Vipaji vinapotea, nafasi yao ya kutengeneza pesa inakuwa finyu. Mashabiki hawapendi mateja.

Ukitaka kuthibitisha hilo ni kuwa mwanamuziki hata awe anapendwa vipi, akisharipotiwa kutumia madawa ya kulevya, hupoteza chati yake haraka sana. Ndiyo maana leo hii ni kazi sana kuwarudisha sokoni wale ambao jamii iliwatema kwa sababu ya uteja. Watafanya muziki mzuri lakini mapokeo si kama zamani.

Wakati muziki wa Tanzania ulikuwa huongei kitu mbele ya Q Chiller, ikabainika kuwa mwanamuziki huyo anatumia ‘madude’. Hapa ifahamike kuwa unga husababisha ufanisi wa kazi ushuke, kisha jamii humuona mhusika kama mtu wa tofauti, maana mtumia madawa ya kulevya ni mhalifu.

Sishangai mtu anapoibiwa vifaa vya gari lake akimtaja Lord Eyez kwa sababu mwenyewe aliamua kujipa sifa mbaya. Wapo wanamuziki wakongwe wanakaa kimya na wakitoka wanarudi na heshima zao kwa sababu hawakuwahi kujiingiza huko. Hata kama walijaribu, hawakutangazwa.

KWA NINI UNGA NA WASANII?

Nimeshafafanua kuwa wasanii hawajifunzi licha ya kuwepo mifano mingi, sasa kwa nini wanaendelea kujiingiza? Zipo sababu kadhaa ambazo nitazifafanua moja baada ya nyingine kutokana na uchunguzi ambao nimeufanya.

Kwanza; kundi kubwa la wanamauziki wanajiingiza kwenye matumizi ya madawa ya kulevya kwa sababu ya kuiga. Mtu anaweza kumuona mwenzake anatumia, kwa fikra zake akadhani ana faidi sana, hivyo naye kuamua kujaribu. Wanaojaribu wengi huwa hawaachi, mwisho wanatambulika kama mateja rasmi.

Niliwahi kuzungumza na Msafiri Diouf wa Twanga Pepeta, akaniambia kuwa wakati Aisha Madinda anataka kujiingiza kwenye unga, alimuonya kwa sababu alishaona athari zake lakini mwanadada huyo aliona anabaniwa, kwa hiyo akaanza kubwia. 

Pointi ya kuiga, hutokana na kuangalia hata wasanii wa nje. Mathalan, mtu anamuona Chris Brown, kisha anaona kwamba na yeye anaweza ‘kulanduka’. Hajui kama mwenzake ana pesa, kwa hiyo anapata huduma nzuri kama chakula na hata kusafisha damu, wa kwetu akijiingiza tu, miezi miwili tayari ‘alosto’.

Nifafanue kuwa haina maana ukiwa na pesa nyingi ndiyo ruhusa kutumia, la hasha! Namaanisha kuwa akina Chris wanapata huduma ambayo angalau inawafanya wasichoke haraka. Ila kuchoka ni lazima ndiyo maana ukipima muonekano wake kabla na baada utaona tofauti kubwa.

Pili; wapo wanaingia kwenye uteja kwa sababu ya makundi. Unakuwa na rafiki ambaye anatumia lakini hujui, unamgongea sigara, kumbe mwenzake ameichanganya na unga. Ukivuta unalewa, unapata stimu, siku nyingine unaulizia kama ile, mwisho nawe unakuwa mtumiaji.

Niliwahi kumuuliza Maunda Zorro baada na yeye kusikia anatumia, kwanza alinihakikishia kwamba hatumii kabisa, ila akanipa ushuhuda wa rafiki yake mmoja aliwahi kuonja ‘fegi’ ya mwenzake studio ambayo ilikuwa imechanganywa na madude. 

Upo mfano wa mwanamuziki Kulwa wa Mapacha Maujanja (alikuwa familia ya Vinega). Yeye kwa kauli yake aliniambia kuwa aliwahi kugongea sigara ya wasanii wenzake (alinitajia majina yao) pale Maisha Club lakini alichokutana nacho kilikuwa tofauti, alilewa na siku iliyofuata aliumwa na kichwa vibaya mpaka kujihisi anataka kurukwa na akili.

Tatu; ipo imani ya wasanii kwamba ukitumia madawa ya kulevya unakuwa wa kileo zaidi na hata sanaa utafanya kwa kiwango cha kimataifa. Mwana Hip Hop anaamini akibwia unga, basi atakuwa kama Snoop Dog, The Game, Lil Wayne na wengineo wa Marekani.

Hivyo basi, mwanamuziki anaamua mpaka kujidunga kwenye mishipa akiamini ndivyo anavyokuza sanaa yake. Matokeo yake badala ya kuwa msanii mkubwa, anageuka kuwa teja wa kutupwa. Usicheze kabisa na madawa ya kulevya.
Nne; msongo wa mawazo ni sababu nyingine. Wapo wasanii soko linawakataa, pengine na majukumu ya kifamilia yanawaandama. Wakitazama kuna wenzao wanatengeneza fedha kwa kasi kubwa kama ambavyo na wao iliwahi kuwa upande wao.

Hali hiyo huwa inawachanganya vichwa wasanii kiasi cha kuamua kujiingiza kwenye matumizi ya madawa ya kulevya, wakiamini wanatafuta suluhu ya msongo wa mawazo wakati kumbe wanakwenda kujiharibia maisha yao kwa jumla.

Tano; wapo wanaoingia kwa sababu ya tamaa, mfano msanii anakubali kubebeshwa madawa na kusafiri nayo kwenda nje kuuza. Hao wanaitwa mapunda. Matokeo yake wanajiingiza kwenye kutumia wakati mwanzoni walijiapiza kusafirisha tu.
Kuna ambao waliamua kutumia baada ya kuchanganyikiwa kutokana na kudhulumiwa pesa za kusafirisha mzigo, wengine walitamani tu kuonja ili wajue wanachokisafirisha kina ladha gani. Ila yote kwa yote, mwisho ni uteja.

USHAURI

Wasanii wetu wanaweza kuepukana na matumizi ya madawa ya kulevya kama tu watazingatia kazi zao na kujiweka mbali na mambo hayo ambayo nimeyataja kuwa sababu ya wengi kujiingiza kwenye uteja. 
Muhimu ni kuzingatia kwamba kazi yao ina thamani kubwa, kwa hiyo wailinde. Na watambue kuwa kuharibika kwao, husababisha maumivu kwa mashabiki wao, maana kazi zao huingia ndani ya mioyo ya mashabiki ambao wakisikia habari zao mbaya, huumia sana na kuvunjika mioyo.


By Luqman Maloto

Janga Jingine Lamkuta Emmanuel Mbasha, inadaiwa Kaficha Habari Kuhusu Mfanyakazi wake Aliyejinyonga ndani kwake.

0
0
Majanga yanazidi kumuandama aliyekua mme wa muimbaji maarufu Frola Mbasha, akiwa bado ana kesi mahakamani akidaiwa kumbaka ndugu yake hili ndio janga jingine lilimkuta Emmanuel Mbasha. Janga hilo ni la kufariki kwa mfanyakazi wake wa ndani ambae alijinyonga ijumaa iliyopita.

Inadaiwa kua Emmanuel na mfanyakazi huyo walikua wakiishi wawili tu ndani ya nyumba ya Emmanuel, lakini kitu cha kushangaza zaidi ni pale mfanyakazi huyo alipojinyonga. Inavyosemekana Emmanuel hakutoa taarifa kwa majirani kuhusu tukio hilo badala yake alitoa taarifa polisi na kisha kuusafirisha mwili wa marehemu kwa siri sana kwenda kumzika Singida.

Tumepata ujumbe kutoka kwa mmoja wa majirani wa Emmanuel Mbasha ambae hakutaka jina lake litajwe, ujumbe huo ulisema ” Kuna kijana wa kazi toka Singida alikuwa anaishi na Emmanuel Mbasha, amejinyonga na kuacha ujumbe kuwa kwa yaliyomkuta ameamua bora ajinyonge. Walikuwa wanaishi na Mbasha tu huko ndani na baada ya kujinyonga Mbasha amefanya siri kubwa mno hawakuweka hata msiba. Kijana alijinyonga Ijumaa na ndugu wakatafutwa wakaenda kureport polisi kwa ajili ya mazishi na wamemsafirisha kwenda kuzika Singinda. Mbasha hakuta majirani tujue. Mnaweza mtafuta kwa maelezo zaidi maana nikiandika hapa yeye ndo mwenye ukweli alimfanyia nini kijana wa watu.

Bado tunafanya jitihada za kumtafuta Mbasha kwa ajili ya kuzungumzia suala hili….

Feki Kuanzia Ukucha Mpaka Unywele..Wadada Mmetuibia Sana Sasa inatosha

0
0
Kusema ukweli wanaume tumeibiwa sana na hawa wadada wenye kujifekisha kila kitu kuanzia kucha za miguu mpaka nywele kila kitu ni fake ..Kucha feki, Mahipsi feki, Makalio feki, Maziwa feki , ngozi ya uso feki..kope feki..mweeee..Tumechoka sasa embu kuweni original basi ..Ndo maana wengi wenu hamuolewi....mtu anakupenda ukiwa feki mkifika chumbani ukivua madude yako unakuwa mtu mwigine kabisa....Tumechokaaaa

By TeamWanaume


Stori Kuhusu Mtoto wa Miaka Minne Alivyompiga Risasi Mdogo Wake

0
0
Ni nadra sana kwa hapa kwetu kuona bastola zikitumika kirahisi ndani ya familia,lakini kwa wenzetu ni jambo la kawaida ambalo unaweza kulifananisha kama kumiliki simu ya mkononi ambayo unaweza kuiacha sehemu yoyote.
Huko nchini Marekani mzazi aliamua kuiacha bastola yake kitandani bila kujali kuwa ana watoto wadogo ambao hawakua na uelewa na silaha hiyo baada ya kuichukua na kuanza kuichezea.
Habari kutoka Ohio nchini Marekani zinasema tukio hilo limetokea wakati Watoto hao wakiwa wanacheza peke yao ndani ya chumba ndipo Mtoto huyo aliposhika Bastola hiyo na kumjeruhi mdogo wake kichwani.
Taarifa za Polisi zinasema Baba wa Mtoto huyo alikuwa amembeba Mtoto huyo aliyejeruhiwa  wakati Polisi walipofika eneo la tukio huku Kaka yake akilia na kuwaomba askari hao msamaha mara kwa mara.
Kamanda wa Polisi Roger Watkings amesema uchunguzi wa tukio hilo unaendelea kuona kama linaweza kuwa kosa la jinai ama vinginevyo.
Source NTNNews

Nimemkuta Mume Wangu Akifanya Mapenzi na House Girl wa Jirani Ndani ya Nyumba Yetu

0
0
Juzi nilikuwa naenda kazini nikamuacha mume wangu
nyumbani anaangalia TV, gari langu likazima ghafla kiasi cha
kilomita moja toka nyumbani.
Nikaona nitembee mpaka nyumbani kumwomba mume wangu aje anisaidie kutengezagari, kwa mshangao wangu nilipofika nyumbani nikamkuta mume wangu yuko chumbani na msichana wa kazi wa nyumba ya jirani. Mume wangu ana miaka 43, mimi nina miaka 39 na msichana huyo ana miaka 19 hivi.Tumekuwa katika ndoa kwa miaka 10. Nilipomuuliza mume wangu alikubali kuwa uhusiano wao umekuwa ukiendelea kwa miezi sita sasa, nifanye nini mimi?
NISHAURINI NIFANYAJE NDUGU ZANGU...
SHARE HII TAFADHALI

Hali ya Vengu wa The Comedy Hii Hapa Kumbe Naye Alipewa Nyumba Kama Wenzake

0
0

MUNGU mkubwa! Vengu is back from hell (Vengu amerudi toka kuzimu). Msanii staa wa Kundi la Orijino Komedi ‘OK’, Joseph Shamba ’Vengu’ ameanza kurejea katika ‘fomu’ baada ya kuugua kwa muda mrefu, Risasi Jumatano linathibitisha.

Kwa mujibu wa ndugu wa karibu wa msanii huyo (jina tunalo), Vengu ambaye kwa muda mrefu alipoteza kumbukumbu kiasi cha kushindwa kuwatambua watu, sasa amejaliwa kwani anaweza kuwafahamu watu mbalimbali wanaopata nafasi ya kwenda kumjulia hali, Kigamboni jijini Dar anakoishi.

AMEANZA KUTOA ‘HI’ KWA WATU
“Bado yupo chini ya uangalizi maalum wa kifamilia, ni watu wachache wanaruhusiwa kumuona, lakini sasa hivi huwezi kuamini, watu wanaofika kumtazama anawatambua na anawapa ‘hi’.

TATIZO USIRI
Kutokana na usiri wa hali ya msanii huyo unaofanywa na familia yake, kumekuwa na maneno chini kwa chini ikiwa ni pamoja na uzushi wa mara kwa mara kuwa, mchekeshaji huyo maarufu, amefariki dunia na kuzikwa kwa siri jambo ambalo si la kweli.

Hata hivyo, katika namna ya kusikitisha, ndugu huyo alisema kuwa kila Vengu anapomtambua mtu anayemtembelea amekuwa akimwaga machozi hali inayoonesha kuwa anarejesha nyuma kumbukumbu zake na kugundua amekuwa mbali naye kwa muda mrefu.


KUREJEA KWENYE FANI
Pia ndugu huyo alisema kwa hali ya Vengu sasa anaweza kurejea kwenye kazi zake za kuchekesha kama zamani zile.“Kwa jinsi ilivyo, Vengu atarejea hivi karibuni katika kazi yake ya kuburudisha akiwa sambamba na wenzake wa Orijino Komedi kwa sababu afya yake inaimarika sana,” alisema ndugu huyo huku akikataa katakata kutoa ramani ya nyumba anayoishi Vengu ili mapaparazi wetu wende wakamjulie hali.

APEWA NYUMBA
Kana kwamba haitoshi, wakati hali yake ikisemwa na ndugu inaendelea vizuri, kuna madai kwamba msanii huyo na familia yake wamepewa nyumba ya kisasa yenye thamani ya shilingi milioni 120, sawa na wasanii wenzake akina Wakuvanga kufuatia mkataba wa kundi hilo na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF).
“Ni kweli afya ya Vengu kwa sasa ipo vizuri, anajitambua. Pia amepewa nyumba, kubwa tu ipo kulekule Kigamboni anakoishi lakini bado hajahamia.”

KUMBUKUMBU
Vengu alianza kuugua kidogokidogo mwaka 2009, lakini Agosti, 2011 hali yake ilikuwa mbaya, akalazwa kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) jijini Dar. Rais Jakaya Kikwete ‘JK’ aliwahi kwenda kumjulia hali.

Baada ya hali yake kuzidi kuwa mbaya, alipelekwa kwenye Hospitali ya Apollo nchini India ambako alipatiwa matibabu na kurejeshwa nchini akiaendelea kuuguzwa na familia yake huku taarifa zake zikiwa ngumu kupatikana mpaka hivi karibuni ambapo ndugu mmoja aliamua kuweka wazi hali ilivyo kwa sasa.
Ugonjwa wake mkubwa ulitajwa kushambulia sehemu ya kichwa, hasa kwenye ubongo.
GPL

Sitti Mtemvu Atoweka, Gazeti Lamtafuta Bila Mafanikio

0
0
Stori: Chande Abdallah na Deogratius Mongela
WAKATI suala la kudaiwa kudanganya umri likiwa bado ‘bichii’, taarifa zinadai kuwa mshindi wa Miss Tanzania 2014, Sitti Mtemvu ametoweka na hajulikani alipo, Risasi Mchanganyiko limechimbua stori kamili.

Shughuli ya kumsaka mrembo huyo ili kujua undani wa sakata lake ilianzia Temeke ambako ilielezwa kuwa ndiko anakoishi.

Mapaparazi wetu walipofika katika nyumba waliyoelekezwa, walikuta imebadilishwa na kuwa Ofisi ya Vikoba ambapo mmoja wa wahudumu wa ofisi hiyo kwa sharti la kutoanika jina lake gazetini, aliwataka waandishi wetu kwenda Mbezi-Makonde akidai ndiko anakoishi kwa sasa.

Hapa ilikuwa nyumba ya zamani lakini kwa sasa ni ofisi na Sitti hakai hapa, kama mnamtaka nendeni Mbezi-Makonde huko nasikia ndiko anakoishi,” alisema mtumishi huyo.

Mapaparazi wetu hawakuchoka, walifunga safari hadi Mbezi-Makonde ambapo walikuta nyumba yenye maduka yaliyoandikwa Mtemvu Foundation, wakaenda moja kwa moja katika saluni mojawapo iliyokuwa na bango lililosomeka Malisa huku likiwa na picha ya Sitti sambamba na namba za simu.
Dada mmoja aliyeonekana kufanana na Sitti alizidi kutibua hali ya hewa baada ya kusema Sitti amesafiri nje ya nchi pasipo kufafanua nchi gani.“Sitti amesafiri nje ya nchi, ila kama mnamtaka nafikiri nitawapa namba zake akirudi kati ya Jumatatu au Jumatano ya wiki ijayo (wiki hii),” alisema dada huyo pasipo kutaja jina lake.

Mmoja wa majirani wa mrembo huyo alihoji inawezekanaje mrembo huyo akasafiri nje ya nchi wakati suala lake la umri halijapata ufumbuzi?“Mh! Ataondokaje wakati bado ana majanga ya umri?” alihoji jirani huyo.

Aidha, mapaparazi wetu hawakutaka kuishia hapo, Jumapili iliyopita walitia timu Buza Kipera katika Kanisa la The Revelation Church la Nabii Yaspi Bendera ambalo ilielezwa kuwa Sitti anaabudu, ili kujiridhisha kama yupo, lakini pia hakuonekana huku waumini wakidai hawajamuona kwa siku za karibuni.


Hatumuoni siku hizi, ila alikuwa anakuja katika ibada ya peke yake kwa nabii saa kumi lakini siku za karibuni hatumuoni,” alisema muumini mmoja.Katika ibada inayoendeshwa kanisani hapo ambayo mapaparazi wetu walizama ‘kiintelijensia’, Nabii Yaspi alisikika akimkingia kifua Sitti kuwa alistahili ushindi na kumtabiria kufika mbali na hata kuwa Miss World huku akiwaonya wanaomfuatilia mrembo huyo.

Mara ya kwanza nilimtabiria Sitti kushinda u-miss Tanzania na kweli akashinda, sasa wanatokea watu wakidai mara ana hipsi kubwa, ooh kadanganya umri, huu wote ni upepo tu na utapita.“Kama Sitti hatakengeuka kwenye imani yake atafika mbali zaidi na kushinda hata Miss World. Wale wote watakaoendelea kumfuatilia wataparalaizi,” alisema Nabii Yaspi.

Hadi mwishoni mwa wiki iliyopita, Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), walisema bado wanalifanyia uchunguzi suala la Ritta kudaiwa kufoji cheti cha kuzaliwa kutokana na baadhi ya nyaraka zake kuonesha amezaliwa mwaka 1989 huku yeye akidai amezaliwa 1991.

Wakati RITA na BASATA wakiwa hawajatoa tamko lolote kufuatia uchunguzi waliodai wataufanya, gazeti hili lilifanya jitihada za kumtafuta Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mukangara ili azungumzie sakata hilo.

Waziri ni mtu mkubwa sana kuzungumzia suala kama hilo, watafute wasaidizi wangu pale wizarani watakuambia kinachoendelea. Naweza kutoa tamko halafu nikaonekana mtu wa ajabu, kumbe watu wanaendelea kulifanyia kazi, nenda kamuone Mkurugenzi wa Utamaduni atakusaidia,” alisema Waziri huyo alipozungumza nasi kwa njia ya simu.
GPL

UKAWA wanyaka nyaraka juu ya Mpango wa kifisadi wa kupitisha Katiba Inayopendekezwa

0
0
Wakati wananchi wanalazimika kujichangisha fedha zao mifukoni ili wapate huduma pale Hospitali ya Muhimbili kwa sababu Serikali imeshindwa kuilipa MSD, Serikali ya CCM inapanga mipango ya hila ikitumia mabilioni kurubuni Watanzania waipitishe Katiba Inayopendekezwa!

Leo UKAWA wanahoji, haya mabilioni ambayo Rais Kikwete ameagiza kwenye mpango huu akiwa ndani ya ndege, yameidhinishwa na kikao kipi cha bunge? Yako kwenye Kasma ipi ya bajeti? Tangu lini fedha za walipa kodi maskini zikatumika kwa ajili ya kuiepusha CCM na aibu ya kura ya HAPANA?

Soma kwa makini mkakati mzima huu hapa kama ulivyoanikwa leo na viongozi wakuu wa UKAWA, walipokutana na waandishi Ofisi za Makao Makuu ya Chama cha CUF.


Source:Jamii Forums

World Trade Center is Now Open For Business

0
0
Thirteen years after the 9/11 terrorist attack, the resurrected World Trade Center is again opening for business — marking an emotional milestone for both New Yorkers and the United States as a whole.

Publishing giant Conde Nast will start moving Monday into One World Trade Center, a 104-story, $3.9 billion skyscraper that dominates the Manhattan skyline. It is America's tallest building.

It's the centerpiece of the 16-acre site where the decimated twin towers once stood and where more than 2,700 people died on Sept. 11, 2001, buried under smoking mounds of fiery debris.

"The New York City skyline is whole again, as One World Trade Center takes its place in Lower Manhattan," said Patrick Foye, executive director of the Port Authority of New York and New Jersey that owns both the building and the World Trade Center site.

He said One World Trade Center "sets new standards of design, construction, prestige and sustainability; the opening of this iconic building is a major milestone in the transformation of Lower Manhattan into a thriving 24/7 neighborhood."

The One Question You Should Never Ask a Woman

0
0
Men aren’t the only ones guilty of asking this particularly sensitive and inappropriate question. In fact, my experience is that women are way more likely to embarrass themselves on this gaff than men, at least twice as often.

The question isn’t how old are you or how much do you weigh.
The question you should never ask a woman is
“are you pregnant?

Most people assume a pregnancy is a joyous time, something to celebrate, and for the vast majority of expecting mothers it is. However, the question may be borderline disrespectful and flat out rude to ask; it isn’t really any of your business.

The sensitivity of this issue cannot be overstated.

Why would a woman care if you ask if she is pregnant?

For starters, she may be pregnant and not yet ready to make her status public. This brings up issues of how it might affect her professionally. What if she is discriminated against?

What if she is waiting to announce her pregnancy until she knows she has crossed the risk threshold of 13 weeks when the incidence of miscarriage is dramatically reduced?

What if she just recently miscarried late-term and while struggling with her loss, your nosey-a*s comes in and wants to know all of the intimate details of her life?

What if it is an unwanted pregnancy? Not to say the baby will or won’t be wanted upon birth, but you can’t assume the pregnancy is happening under positive terms.

What if she is just overweight and carries it all in the middle?

What if she is struggling to conceive, has gone through rounds of hormone therapies and has gained abdominal weight as a result of her failed attempts?

What if she has diastasis recti and you are making her feel like an alien because her body didn’t “bounce back” the way it once was?

The point is this: you should be more afraid to offend a woman by asking if she is pregnant than by not asking. Ultimately, it’s none of your business unless she wants it to be your business.
Viewing all 104414 articles
Browse latest View live




Latest Images