Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Mwanajeshi wa Marekani Aliye Muua Osama Bin Laden Ajitokeza Hadharani

$
0
0
Mwanajeshi aliyemuua Osama bin Laden ametambulika kwa mara ya kwanza jana.
Anaitwa Rob O’Neill, 38, aliyewahi kufanya mission za kijeshi zaidi ya 400.

Baba yake, Tom O’Neill anasema: “Watu wanauliza kama tunaogopa kwamba ISIS watakuja na kututeka kwasababu Rob anafahamika sasa. Nasema nitachora target kubwa kwenye mlango wangu wa mbele na kusema ‘njooni mtuteke’.

O’Neill mwenyewe alipongezwa na rais Barack Obama kwa kumuua bin Laden kwa risasi tatu juu ya paji lake la uso wakati wanajeshi wa Marekani waliposhambulia kambi yake huko Abbottabad, May 2, 2011.

O’Neill amekubali kufanyiwa mahojiano exclusive na kituo cha Fox baadaye mwezi huu.

Mission zake tatu alizozifanya zimetumika kwenye filamu za action za Hollywood. Alikuwa mwanajeshi aliyeongoza wenzie huko kuokoa meli ya Maersk Alabama, iliyokuwa imetekwa na maharamia wa Somalia ambapo operesheni hiyo ilizaa filamu ya Captain Phillips.

Waziri wa Uganda Aagiza Desire Luzinda na Boyfriend wake Wakamatwe na Kushitakiwa kwa Kusambaza Picha za Utupu

$
0
0
Ile skendo ya kusambaa kwa picha za utupu za msanii wa kike wa Uganda, Desire Luzinda imezidi kumuweka pabaya, kwani sasa waziri wa maadili wa Uganda ameagiza mrembo huyo akamatwe na kushitakiwa.

Kwa mujibu wa New Vision, waziri Simon Lokodo ameagiza polisi kuwafuatilia na kuwakamata Luzinda na boyfriend, ili washitakiwe kwa kosa la kusambaza picha za utupu kinyume na kifungu cha 13 cha Sheria ya Anti- Pornography Act.

New Vision imeandika:

“STATE minister for Ethics and Integrity Simon Lokodo has directed police to question local artist Desire Luzinda for her nude pictures said to be taken by her Nigerian boyfriend that have gone viral on social media.

“Police is on track to get hold of Luzinda and her boyfriend. I have directed the Police to get her,” the minister told New Vision in a phone interview on Tuesday morning.

The minister explained that Luzinda and her boyfriend will be charged with exhibition of pornographic material contrary to section 13 of the Anti- Pornography Act.

Section 13 of the Act states that: “A person shall not produce, traffic in, publish, broadcast, procure, import, export, sell or abet any form of pornography.”

It adds: “A person who produces or participates in the production of, or traffics in, publishes, broadcasts, procures, imports, exports or in any way abets pornography contrary to sub section 1 commits an offence and is liable, on conviction, to a fine not exceeding five hundred currency points or imprisonment not exceeding ten years or both.”

Five hundred currency points is equivalent to sh10m.”

Wadada tu: Utajuaje Kuwa Wewe ni Changudoa

$
0
0
Wewe kama hujaolewa halafu unapanua miguu kwa jamaa ambae sio mume wako, yani boyfriend au mchumba kwa minajili ya kujipatia hela, ujue wewe ni changudoa. Huna tofauti na wale wanaosimama usiku kujiuza.

Japokuwa wewe husimami usiku lakini jijue kuwa na wewe ni changudoa kwasababu wote mnapewa pesa baada ya tendo. Hata kama hupewi mara tu baada ya tendo kama wanavyofanya changudoa wanaosimama barabarani, lakini unapewa pesa za matumizi na mtu ambaye si mume wako kisha ukampanulia miguu, jua wewe ni changudoa au tunaweza kukuita changudoa mwenye kiwango.

Kwa wale dada zangu ambao bado hawajaingia katika hii biashara nawashauri kufunga miguu yenu masije kujiingiza katika hii bihashara. Kwasababu mbali na kumchukiza Mungu unakuwa unajishusha thamani wewe mwenyewe. 

Halafu uzuri wake ukifanya hivi huwezi ukaja kukosa wa kukuoa dada.

Matokeo ya Darasa la Saba 2014 Bonyeza Hapa

$
0
0

Bonyeza link ifuatayo Kusoma Matokeo ya Darasa la Saba 2014 >>>>Matokeo

Penny Afunguka Baada ya Diamond Kupigwa Chini na Wema Sepetu

$
0
0
Mtangazaji aliyewahi kujiachia kimahaba na Nasibu Abdul ‘Diamond’, Penniel Mungilwa ‘Penny’ amesema mwanamuziki huyo kwa sasa alie tu kwani ameshachumbiwa na hawezi kumpata tena.

Kauli ya mwanadada huyo ilikuja baada ya kuulizwa kama anaafikiana na kauli ya mama wa Wema Sepetu, Miriam Sepetu kwamba, kwa kuwa Wema kamuacha Diomond basi staa huyo wa Wimbo wa Mdogomdogo bora akampose yeye.

Mmh! Hapa suala la Diamond kurudiana na mimi halipo kabisa maana simhitaji yeye wala mwanaume mwingine yeyote, mimi ninaye wangu tayari ambaye ameshanichumbia hivyo sitarajii kabisa kuwa na mwingine zaidi yake,” alisema Penny.

Mabeto 'Suala la Kuolewa Kwangu Silifikirii Bado Nakula Ujana'

$
0
0
Mrembo ambaye sasa amejiingiza kwenye filamu, Hamisa Hassan ‘Mabeto’ amesema kwa sasa hafikirii suala la kuolewa kwani bado anakula ujana.

Akizungumza na mwandishi wetu, Mabeto alisema bado anajiona mtoto hivyo kuliko kukimbilia maisha ya ndoa bora ale kwanza ujana.

Suala la kuolewa hapa kwangu hata silifikirii kabisa, mimi bado binti mdogo sana nitawezaje kukimbilia ndoa, hiyo ni mipango ya Mungu kila kitu kinaenda kwa wakati, muda utakapowadia nitaolewa,” alisema Hamisa.

Ziara ya Rais wa China Yaipa Aibu Tanzania, Ndege yake ilitumika kusafirishia meno ya Tembo

$
0
0
Ziara ya Rais Xi Jinping wa China aliyoifanya nchini Machi mwaka jana, imezua kizaazaa na kuitia ila sifa ya Tanzania kimataifa, baada ya maofisa waliokuwa wameambatana naye kuhusishwa na biashara haramu ya meno ya tembo.

Ripoti iliyotolewa na taasisi ya kimataifa ya Uingereza inayojihusisha na uchunguzi wa masuala ya mazingira, inadai kuwa maofisa hao walinunua kiasi kikubwa cha bidhaa hizo katika soko la Mwenge, Dar es Salaam, kisha kuzisafirisha kidiplomasia kwa ndege ya rais huyo.

Taasisi hiyo iitwayo Environmental Investigation Agency (Wakala wa Uchunguzi wa Mazingira– EIA), katika ripoti hiyo inasema maofisa hao walitumia fursa ya kidiplomasia ya kutokukaguliwa kwa mizigo yao, kupitisha  bidhaa hizo haramu katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA).

Biashara ya meno ya tembo ilizuiwa kimataifa tangu mwaka 1989 kwa kusainiwa kwa azimio la kulinda viumbe walio hatarini (Cites), azimio ambalo pia limesainiwa na China na Tanzania.

Taarifa hiyo iliandikwa kwa mara ya kwanza jana na Gazeti la New York Times la Marekani na baadaye kuwa moja ya habari zilizopewa uzito wa juu katika vyombo vingine vya habari vya kimataifa, huku Kituo cha Televisheni cha Shirika la Habari la Uingereza BBC, kikijadili kwa kina kashfa hiyo iliyopewa jina la “ndege ya rais kutumika kusafirisha meno ya tembo”.

BBC katika taarifa yake ilitumia picha za meno ya tembo na zile za maktaba ambazo zilikuwa zikimwonyesha Rais Jinping akilakiwa na Rais Jakaya Kikwete pamoja na viongozi wengine wa Tanzania alipowasili nchini kwa ziara hiyo.

Hata hivyo, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alisema jana kwamba Serikali haifahamu chochote kuhusu tuhuma hizo na kwamba hata kama zingekuwa na ukweli ndani yake waliopaswa kuulizwa ni Serikali ya China.

“Serikali haina evidence (ushahidi) wowote unaoonyesha kwamba suala la aina hii lilitokea, lakini pili mimi siamini kama kweli maofisa wa China walifanya kitendo hiki na kama hicho kilifanyika basi wanaopaswa kuulizwa ni Serikali ya China,” alisema Balozi Sefue na kuongeza:

“Siamini kama madai hayo ni ya kweli kwa sababu maofisa wanaosafiri na viongozi hukaguliwa, kwa nini wasikaguliwe na China ni marafiki zetu wazuri tu? Kwa hiyo sisi kama Serikali hilo jambo hatulifahamu kabisa.”

Baada ya kutangazwa katika vyombo vya habari vya kimataifa, maofisa wa Serikali ya China wamekanusha tuhuma hizo wakisema, “hazina ukweli wowote” wala ushahidi wa kuzithibitisha.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa China, Hong Lei alinukuliwa na Shirika la Habari la Associated Press (AP) akisema: “Ripoti hiyo haina ushahidi wowote na hatukufurahishwa kabisa na taarifa hizi.”

Mkurugenzi wa usafirishaji wa viumbe walio kwenye hatari ya kutoweka nchini China, Meng Xianlin alipuuza madai hayo akisema: “Tuhuma pasipo ushahidi haziwezi kuaminika.”

Ununuzi wa nyara

Ripoti hiyo inayoitwa “Wanatoweka: Uhalifu, Rushwa na Kuangamizwa kwa Tembo wa Tanzania,” inadai kuwa ujumbe wa maofisa wa Rais Jinping ulifika nchini wiki mbili kabla ya ujio wa Rais huyo na kununua pembe za ndovu katika eneo la Mwenge ambalo ni maarufu kwa uuzaji vinyago.

Inadai kuwa ujumbe huo ulinunua meno ya tembo kwa Dola za Marekani 700 (sawa na Sh1,120,000) kwa kilo moja, bei ambayo ni mara mbili ya ile ya kawaida na kwamba Wachina hao walinunua maelfu ya kilo za meno hayo na kuyasafirisha kwa ndege ya Rais Jinping.

Mfanyabiashara katika eneo hilo, aliyetambulika kwa jina moja la Suleiman amenukuliwa katika ripoti hiyo akisema bei ya meno ya tembo ilipanda kutokana na kuongezeka kwa mahitaji yake wakati wa ziara hiyo.

Mtu mwingine ambaye hakutajwa jina lake katika ripoti hiyo anaeleza kuwa jambo hilo lilifanyika pia hata wakati wa ziara ya aliyekuwa Rais wa China, Hu Jintao mwaka 2009 ambako maofisa waliokuwa katika msafara huo walinunua bidhaa hizo.

“Wanakuja kuchukua vitu vingi, si kwa ajili ya Hu Jintao, bali kwa ajili yao. Baada ya hapo wanakwenda uwanja wa ndege na kupita bila kukaguliwa kwa sababu VIP hawakaguliwi,” alidai.

EIA katika taarifa hiyo pia inadaiwa kuwa Wanadiplomasia wa China pamoja na maofisa usalama wa nchi hiyo kwa kushirikiana na baadhi ya maofisa wa Tanzania walifanikisha upatikanaji na usafirishaji wa meno ya tembo kwenda China.

“Tanzania ndiyo nchi inayoongoza duniani kwa kutoa meno ya tembo kwa wingi. Pia China ndiyo mnunuaji mkubwa wa meno ya tembo duniani,” inasomeka sehemu ya ripoti hiyo yenye kurasa 36.

Mwanafunzi Aliyefunika Hisabati Darasa la Saba

$
0
0
Mwanafunzi bora wa somo la Hisabati katika mitihani ya taifa ya darasa la saba iliyofanyika nchini Septemba mwaka huu, Rachel Kiunsi (13), ameeleza siri ya mafanikio yake kuwa ni kujituma katika masomo na kuwaheshimu walimu.

Akizungumza na NIPASHE kwa njia ya simu jana kutoka mkoani Singida, Rachel ambaye alikuwa anasoma shule ya msingi Kimara 'B', jijini Dar es Salaam, alisema alikuwa na bidii ya kujituma katika masomo yake hasa katika la hisabati na   ya Sayansi na kwamba alikuwa anashindwa kupata usingizi bila kujisomea usiku.

Akizungumzia jinsi alivyopokea taarifa za matokeo yake, Rachel alisema ni kwa furaha na alikuwa akitengemea kufaulu, lakini siyo kwa mafanikio kama hayo aliyoyapata.  
“Nanamshukuru sana Mungu  kwani nilikuwa namwomba atende maajabu katika matokeo yangu... nilikuwa nasali kila nikifanya mtihani na kumaliza,” alisema Rachel, ambaye alikuwa akiishi na bibi yake Kimara.

Aliwashukuru walimu wake wa masomo yote kwa juhudi za kuwafundisha vizuri wanafunzi wote katika shule hiyo kwani walikuwa wakiingia darasani kwa muda wa ziada na kutoka saa 11 jioni.

“Mimi nawashauri wanafunzi wenzangu tuliomaliza wote na kufaulu kuwa tuongeze bidii katika masomo yetu ya Sekondari kwani bila juhudi hatutaweza kufaulu kama tulivyofaulu sasa,” alisema. 


Mkuu wa Wilaya Ahmed Kipozi Aiba Mifuko 700 ya Saruji

$
0
0
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Bw Ahmed Kipozi ameiba jumla ya mifuko 700 ya sementi aliyokabidhiwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Bi Mwantumu Mahiza. Akizungumza kwenye kikao cha baraza la madiwani jana, Bi Mahiza alidai kwamba alimpa Kipozi jumla ya mifuko 1000 ya sementi kwa ajili ya ujenzi wa shule lakini Bw Kipozi alitumia mifuko 300 tu huku akiiba mifuko 700 na kuipeleka kusikojulikana.

Kipozi amepewa siku 2 (masaa 48) awe amerudisha mifuko hiyo aliyoiba vinginevyo cha moto atakiona. Haikuweza kufahamika mara moja ikiwa mtuhumiwa huyo atashindwa kurudisha sementi hiyo aliyoiba atachukuliwa hatua gani.

Source: RFA/Jamii Forums

Kumlinda Mpenzi ni Sawa na Kulinda Samaki Baharini..Ukilinda Kigamboni Wenzako Wanavua Bagamoyo

$
0
0
Jamani wanawake wengine hawajielewi, hawaelewi jinsi mahusiano yalivyo complex.Ngoja niende direct tuende kwenye point. Mke wangu ana tabia ambayo hakuna mwanaume wa aina yoyote atamvumilia. Nimechoka sasa ni muda muafaka wa action najua iko siku atajuta kunifahamu. 

Wote tunafanya kazi za kuajiriwa, hivyo tunatoka asubuhi tunarudi jioni, japo yeye anatangulia kurudi nyumbani. Sasa ana tabia ya kubeba kila umbea anaopata kutoka kwa mashosti zake na kuja kunisimulia mimi. Story za nani anatembea na nani, mke wa nani ana mahusiano na nani, mume wa nani anatembea na nani, nani ana tabia gani etc. Mimi huwa sina tabia ya kufuatilia maisha ya watu, nimejiwekea commitment kwa kazi yangu na familia yangu. Ya mtaani siyapi uzito, japo ni muhimu kujua ABC za kitaa.

Moja, Kuna jirani yetu ana duka, mke wangu akapata story kuwa yule mama na mumewe ni waathirika. Mwenzangu akatangaza marufuku kwenda kununua kitu chochote pale. Nikamweleza kuwa kama ukimwi ungekuwa unaambukizwa kwa style hiyo basi sijui kama kuna binadamu angebaki hapa duniani. Akaninunia.

Lingine linalofanana na hilo: Kuna siku alikuja akanisimulia habari za mama mwingine mwenye duka pale gengeni a.k.a. Mama J ambaye hana mume alivyo na tabia mbaya, Kuwa anawaingiza wanaume kwake anawabadilisha tu. Sikutaka kupoteza muda kwenye huo mjadala, kumbe yeye alitaka atoe ultimatum kuwa ni marufuku kwenda kununua bidhaa kwenye hilo duka. Siku moja akaniomba nimsindikize tukachukue maziwa mida ya jioni kwani mwenye kuuza hakuweza kuleta. Wakati huo, tulikuwa tunatafuta mayai ya kienyeji na upatikanaji wake ni wa shida.

Sasa tukiwa tunapita barabarani nikaona kwa duka la mama J ana mayai ya kienyeji tena mengi tuu. Saa ya kurudi nikashauri tuchukue mayai, akasema twende nyumbani. Nikamshawishi kwani upatikanaji wa mayai ni shida, tukapitia pale tukachukua mayai kumi. Pia nikanunua vocha ya tigo. Mama J akasema vocha iliyobaki ni ya kurusha. Nikamwambia poa nirushie, nikamtajia namba. Kumbe hapo ndo nikawa nimetibua nyongo bila kujua.
Tulipotoka pale njia nzima nikaona mtu kanuna hataki kuongea. Kufika home kaniita chumbani akaanza kunigombeza, eti mbona alishaniambia tabia za yule mama alafu bado naenda kununua vitu kwake?


Pili, nikipigiwa simu haijalishi ni muda gani na ni wapi, lazima aulize nani amekupigia na anasemaje. Ukweli hata nikimwambia hawezi kumfahamu kila mtu na siyo kila kitu naweza kumsimulia, mambo mengine ni ya kikazi. Kila wakati anapekua simu yangu kana kwamba niko polisi. 

Tatu, tumebahatika kuwa na usafiri, na tunapokaa daladala ni za shida kidogo. Hivyo, kila asubuhi lazima tutoke wote, tumpitishe mtoto shule, then nimdrop yeye kazini. Sasa tukiwa njiani akimwona mtu yeyote anayemfahamu ananiamrisha tumpe lifti huyo mtu. Kumbuka mimi simwulizi kuwa huyo mtu ni nani wake. Nachukulia kawaida. Sasa ikitokea mimi nimemkuta mtu ninayemfahamu au rafiki yangu, huyo mtu akishuka kwenye gari, basi nitaulizwa maswali kama vile niko polisi nahojiwa. Na bahati mbaya ikiwa ni mwanamke, basi ananuna na wakati mwingine nikitaka kusimama anasema twende bana tunachelewa. Hii imenikera sana kuliko kawaida.

Sasa, kuna shosti zake wa karibu sana, mara nyingi nawapa lifti anapotoka kazini, basi anawasifia sana kuwa wana tabia nzuri, sometimes ananiomba tuwapeleke mpaka mjini japo sina ratiba ya kwenda huko. Sasa hao mashosti zake nimetembea nao na hajui. I just wanted to prove kuwa mambo yake ya kijinga hayanizuii kufanya nikiamua. Jamani kumlinda mpenzi ni sawa na kulinda samaki baharini, ukilinda Kigamboni wenzako wanavua bagamoyo.

Anyway, nipeni wazo mbadala nimfanyeje ili aelewe hilo somo?

Jack Wolper Amsaliti Kajala Kwa Wema Sepetu, Team Kajala Waja Juu

$
0
0
Na Musa mateja
UNAFIKI 100%! Wakati kila mtu akiamini kwamba staa wa sinema za Kibongo, Jacqueline Wolper Massawe ni shosti wa Kajala Masanja ‘Kay’, ameibua mshangao baada ya kunaswa akikumbatiana na Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ ambaye kwa sasa haziivi na Kay.

TUJIUNGE KWENYE BETHIDEI
Tukio hilo lililoibua maswali mengi yasiyokuwa na majibu ya harakaharaka lilijiri hivi karibuni katika bethidei ya shosti wa damu wa Wema, Aunty Ezekiel Grayson ambayo ilifanyika kwenye Mgahawa wa Rodizio, Masaki jijini Dar.

WAKUMBATIANA
Huku paparazi wetu akishuhudia na kuwafotoa picha, Wema alipoingia tu ukumbini humo, alimkuta Wolper akila raha zake ambapo alimkimbilia kisha akamkumbatia kwa dakika kadhaa huku wakimwagiana mabusu kuonesha wamemaliza tofauti zao na kwamba walikuwa ‘wamemisiana’.
Wakati wamekumbatiana na kupigana mabusu walikuwa wakinong’onezana mambo yao ambapo walipomaliza waliachia vicheko vilivyosikika ukumbi mzima ndipo minong’ono ikaanza.

WATAALAM WA UBUYU 
Kitendo cha Wema kutumia dakika kadhaa kukumbatiana na Wolper, kilitafsiriwa na wataalam au wafuatiliaji wa mambo ya watu (ubuyu) kuwa ni usaliti mzito kwani Wolper ni Timu Kajala ambaye ni hasimu mkubwa wa Wema.

“Mh! Mwenzangu makubwa, huyu Wolper si ni Timu Kajala? Inakuwaje anatoa ushirikiano wa asilimia mia moja kwa adui wa Kajala? Hapa kuna tatizo, unafiki kwa mastaa kamwe hauwezi kuisha,” alisikika mtoa ubuyu mmoja aliyeomba hifadhi ya jina gazetini.

AKUMBUSHA VITA YAO
Kama hiyo haitoshi, mtoa ubuyu huyo alikwenda mbali zaidi kwa kusema, ukiachilia mbali Wolper kuwa karibu na Kajala lakini hata yeye (Wolper) alikuwa kwenye vita nzito na Wema kwa kudaiwa ‘kushea’ naye penzi la msanii Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
“Wolper jamani mnafiki...si ndiyo huyuhuyu aliwahi kuingia kwenye vita nzito na Wema baada ya kudaiwa kuwa anadondoka dhambini na kipenzi cha Madam, Diamond? Yaani huu ni unafiki asilimia mia,” alisema mtoa ubuyu huyo.

TIMU KAJALA WAJA JUU
Baada ya Timu Kajala kusikia kwamba Wolper ‘ali-spendi’ vya kutosha na Madam kwenye bethidei hiyo, walikuja juu kisha wakamtolea uvivu na kuanza kumshambulia katika mitandao ya kijamii na kudai hafai kuwa timu yao.

“Wolper msaliti, ataendaje kwenye sherehe ya mpinzani wetu? Tena kama hiyo haitoshi, yeye anakumbatiana na Madam ambaye kwetu sisi hatusaidii lolote,” alisema mmoja wa Timu Kajala.

KUMBUKUMBU IPOJE?
Kabla ya siku hiyo, Wolper na Wema hawakuwahi kuwa na uhusiano mzuri na kila sehemu ambayo utakumta Wolper, kamwe huwezi kuona Wema ametia maguu.

WOLPER ANASEMAJE?
Baada ya paparazi wetu kushuhudia kitendo hicho ukumbini, alimfuata Wolper na kumuuliza ni kitu gani kilichowasababisha wapatane na kuoneshana ‘mahaba niue’ wakati nyuma ya pazia wana bifu? Msikie alichojibu:

“Ujue watu wengi sana wamekuwa wakidhani mimi na Wema tuna bifu, sijui kwa kuwa mimi nina ukaribu na Kajala au kwa kuwa hatujawahi kuwa pamoja, lakini ukweli mimi na Wema siyo waongeaji sana japokuwa huwa nikiweka picha au chochote kwenye Instagram, Wema huwa ana-like na mimi huwa na-like vitu vyake hivyo sidhani kama nilikuwa na tatizo naye sana,” alisema Wolper.

TUJIKUMBUSHE
Urafiki wa mastaa huwa mara nyingi haudumu, Wema ambaye hivi sasa shosti wake mkubwa ni Aunty, kabla aliwahi kuwa na urafiki na Snura Mushi, Jamilah wa Temba, Kajala na wote hao akawamwaga.

Serekali Wakana Tuhuma za Pembe za Ndovu Kusafirishwa Kwa Kupitia Ndege ya Rais wa China

$
0
0
SERIKALI ya Tanzania imeshtushwa na ripoti inayoelezea biashara haramu ya pembe za ndovu kati ya baadhi ya viongozi wa nchi hiyo na China.

Serikali hiyo imesema imesikitishwa na ripoti iliyotolewa na taasisi ya uchunguzi ya mazingira inayodai kwamba majangili wa Kichina wakishirikiana na baadhi ya viongozi wa serikali ya Tanzania ndio wanaoangamiza idadi ya tembo kutokana na biashara haramu ya pembe za ndovu.

Inadaiwa kwamba raia wa China walitumia ziara ya rais wao, Xi Jinping ya nchini Tanzania kusafirisha kimagendo maelfu ya kilo za pembe za ndovu.
Kulingana na shirika la utafiti wa mazingira, EIA, Pembe hizo zilinunuliwa wiki moja kabla ya ziara ya rais huyo nchini mwaka jana na zilifichwa katika mifuko ya wanadiplomasia ili zisitambuliwe.

Msemaji wa Serikali Assah Mwambene amemwambia mwandishi wa BBC Aboubakar famau kwamba ripoti kama hiyo zinatatiza jitihada za serikali kukabiliana na uuzaji haramu wa pembe za ndovu.

CHANZO: BBCSWAHILI

Kadri Mwanamke Anavyojiremba Zaidi Hamu ya Kufanya nae Mapenzi Inavyopungua

$
0
0
Siku hizi limezuka wimbi la akina dada na hata akina mama kujiremba kwa namna mbalimbali kuanzia rangi ya mwili, nywele, kucha, midomo na wengine wamefikia hatua ya kunywa au kupaka dawa za kichina za kuongeza makalio na maziwa. Wengine wanasuka nywele ndefu na wanaongea kwa mbwembwe huku wanatikisa vichwa vyao na kushikashika nywele kama wafanyavyo wanawake wa kizungu. Wengine wamefikia hatua ya kubadili hata sauti na namna ya kuongea!!

Najua dada zetu wanafanya hivyo kwa lengo la kupendeza na wengine lengo lao ni kuwavutia wanaume. Lakini mimi binafsi sijui ni nini kimenitokea! Inawezekana ndiyo abnomality hiyo. Kadri mwanamke anavyojiremba zaidi ndivyo hamu ya kufanya nae mapenzi inavyopungua.

Ukweli ni kwamba nikilala na mwanamke ambaye ni natural yaani mwenye nywele za kawaida anayesuka mtindo wa 'twende kilioni' au amezibana tu, wowowo, chuchu na sauti natural huwa napata nguvu nyingi za kupanda mlima ikilinganishwa na ninapolala na mwanamke mwenye kucha za bandia, nywele za bandia, na midomo iliyopakwa rangi nyingi.

Tafadhali karibuni kwa mjadala huu

~Written By Kibo10 via JF

Utata Mkubwa Waibuka Kuhusu Mwanajeshi Aliyemuua Osama Bin Laden, Mwingine Aibu na Kudai ni Yeye

$
0
0
Utata umetanda miongoni mwa wananchi nchini Marekani kutaka kujua ni askari yupi hasa aliyefyatua risasi iliyomuua Osama Bin Laden, zaidi ya miaka mitatu baada ya kifo cha kiongozi huyo wa kundi la kigaidi la al-Qaeda, baada ya kuibuka madai tofauti.
Askari wa zamani wa kikosi cha Seal cha wanamaji wa Marekani, Robert O'Neill, mwenye umri wa miaka 38, ameliambia gazeti la Washington Post katika mahojiano mapya kuwa ndiye alifyatua risasi iliyomuua Osama.
Maelezo hayo yanapingana na yale ya Matt Bissonnette, askari mwingine wa zamani wa kikosi cha Seal aliyeshiriki katika operesheni ya kumsaka katika maelezo yaliyotolewa katika kitabu mwaka 2012.
Bin Laden, kiongozi wa al-Qaeda aliuawa mwaka 2011 katika shambulio lililofanywa na kikosi cha Seal katika makaazi yake katika mji wa Abbottabad, nchini Pakistan.
Bwana O'Neill, ambaye alistaafu jeshi mwaka 2012, alilieleza hayo jarida la Esquire bila kujitambulisha.
Alipangwa kujitambulisha katika mahojiano ya televisheni baadaye mwezi huu, lakini mtandao mmoja ulichapisha mapema jina la Bwana O'Neill kinyume na uamuzi wake wa kujitokeza hadharani, linaripoti gazeti la Post.
Bwana O'Neill amesema yeye pamoja na askari mwingine ambaye hajatambulishwa hadharani walipanda hadi ghorofa ya tatu katika makaazi yake huko Abbottabad, nchini Pakistan na alimwona Bin Laden akitoa kichwa nje ya mlango katika moja ya vyumba vya nyumba hiyo.

Obama na timu yake ya usalama wa taifa walifuatilia shambulio hilo la Marekani katika makaazi ya Bin Laden.
Komandoo ambaye hakutajwa jina, akiwa amesema katika eneo lake katika muundo wa shambulio hilo alimfyatulia risasi lakini alimkosa, kwa mujibu wa Bwana O'Neill.
Hapo hapo, Bwana O'Neill alikwenda katika chumba na kumuua kiongozi wa al-Qaeda kwa kumpiga risasi kichwani, amesema.
Hata hivyo katika kitabu No Easy Day, Bwana Bissonnette amedai alikuwa mtu wa mstari wa mbele ambaye alimuua Bin Laden.
Alhamisi, Bwana Bissonnette hakupinga moja kwa moja madai ya Bwana O'Neill, katika mahojiano na shirika la utangazaji la Marekani, NBC.
"Watu wawili tofauti wakieleza habari mbili tofauti kwa sababu mbili tofauti," Bwana Bissonnette aliliambia shirika hilo la utangazaji.
"Chochote alichosema, amesema. Sitaki kukizungumzia."
Bwana Bissonnette amepangwa kuonekana katika kipindi cha jarida la CBS dakika 60 kabla ya kuchapishwa kitabu chake cha pili, No Hero, kuhusu huduma yake katika kikosi cha Seals.
Wakati huo huo anachunguzwa kwa kufichua taarifa muhimu katika kitabu chake cha kwanza, kuhusu shambulio dhidi ya Bin Laden.

Taarifa kuhusu kile kilichotokea huenda isitolewe na serikali ya Marekani kwa miaka mingi.
Maafisa wa wizara ya ulinzi ya Marekani hawajakanusha wala kuunga mkono maelezo ya Bwana O'Neill, lakini wiki iliyopita, viongozi waandamizi wa operesheni maalum walituma barua kwa askari wote wa kikosi cha wanamaji cha Seals wakiwataka kuheshimu maadili ya kazi yao kwa kutotoa taarifa za operesheni za kikosi hicho, ikiwa ni pamoja na kuepuka kutafuta umaarufu wa umma".
"Hatutakiwi kufungamana na ubinafsi na kupuuza maadili yetu kwa kutafuta umaarufu wa umma na kujinufaisha kifedha," waliandika katika barua hiyo.
Bin Laden alithibitika kuuawa katika shambulio hilo na mwili wake ulizikwa baharini.
Giza na msongamano wa nyumba katika makazi hayo kumefanya baadhi ya askari wa kikosi cha Seals kuhoji kama inawezekana kubaini ni risasi za nani

Maimartha Awadis Mastaa wa Kike Wanaotoka Kimapenzi na Serengeti Boys

$
0
0
Stori: Na Hamida Hassan
Mtangazaji ambaye pia ni mjasiriamali, Maimartha Jesse amewaponda mastaa wa Bongo Muvi wanaotoka kimapenzi na vijana wadogo ‘Serengeti Boys’ akidai kuwa wanajichoresha.

Akipiga stori na Ijumaa hivi karibuni, Mai alisema anawashangaa baadhi ya mastaa hao kutoona aibu kutangaza kuwa wanatoka na Serengeti Boy huku wakionekana maeneo mbalimbali wakiponda raha.

“Mimi mpaka naogopa na nawaonea huruma kwani hali ni mbaya jamani, watoto wadogo wanatoka na wasanii waliowazidi sana kiumri, yani imekuwa ni kama fasheni sasa, huku ni kujichoresha,” alisema Mai.

Umesikia Kionjo cha Nyimbo Mpya ya Diamond Platnumz Kiko Hapa.

$
0
0
Bado ananijia Ndotoni...Ila nikiamka simuoni... Bado ananijia nikilala Hakiamungu sio masihara
( She's still coming in my dreams, bt when i wake up she aint there... she's still coming when am sleeping... i swear to God it's not a joke)

Post by Diamond Platnumz.

Shetta Ajitetea Baada ya Habari Kusambaa Kuwa Amekataa Kufanya Collabo na Ali Kiba

$
0
0
Ameingia kwenye vichwa vya habari Tanzania na hata wengine kuona kama amekosea kutoa kauli au kumdiss staa wa bongofleva Ali Kiba lakini ukweli anaousema Shetta ni kuwa maneno aliyoyasema yalipindishwa, yani kilichoripotiwa sicho alichokizungumza.
Kujua zaidi alichosema bonyeza play kwenye hii Exclusive video na AyoTV hapa chini.

Mwanamke Achinjwa na Kunyofolewa Sehemu zake za Siri

$
0
0
Watu wasiofahamika wamemuua kwa kumkata mapanga na kisha kumnyofoa sehemu zake za siri mkazi wa Kijiji cha Kanegele, wilayani Mbogwe, Mkoa wa Geita, Hollo Machibula (54).

Akizungumza kijijini hapo juzi, Diwani wa Kata ya Bukandwe, Henry Alphonce alisema Hollo alivamiwa na watu hao nyumbani kwake juzi saa 5:00 usiku akiwa amelala na kuanza kumkatakata kwa mapanga.

Alphonce alisema mwanamke huyo alikuwa akiishi na binti yake, Tatu Juma (25) ambaye wauaji hao walimlazimisha kuingia chini ya uvungu wa kitanda kabla ya kuanza kumshambulia mama yake.

Alisema alipata taarifa za tukio hilo saa 6:00 usiku baada ya kupigiwa simu na viongozi wa kitongoji waliofika eneo la tukio na kushuhudia mauaji hayo.

Mtoto huyo alisema alishuhudia jinsi mama yake alivyokuwa akichinjwa na kunyofolewa sehemu zake za siri walizotoweka nazo wauaji hao.

“Waliniamrisha nilale chini nisiwaagalie usoni, walipomaliza kumchinja mama walikimbia na mimi nikapata mwanya wa kupiga kelele kuomba msaada nikiamini kuwa mama atakuwa kaumizwa tu hajafa,” alisema Tatu.

Baadhi ya wakazi wa eneo hilo walidai kuwa huenda chanzo cha mauaji hayo ni migogoro iliyokuwapo kwenye ndoa ya binti yake na mumewe.

Inadaiwa kuwa Tatu alikorofishana na mumewe ambaye hawakumtaja jina na mume huyo alipokuwa akienda nyumbani hapo kumtaka arudi nyumbani kwake, mama yake alikuwa akimkataza binti huyo asirejee kwa mumewe.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Joseph Konyo alisema wanamshikilia mtu mmoja kwa mahojiano na wanaendelea kuwasaka wale wote waliohusika na mauaji hayo.

Alitoa wito kwa wakazi wa eneo hilo kuisaidia Polisi kuwasaka wauaji hao.

UKATILI! Denti wa Darasa la tano Afariki Dunia baada ya kuchapwa Viboko na Mwalimu Wake

$
0
0
Mwanafunzi wa darasa la tano katika Shule ya msingi ya Kiuu Kenya amefariki dunia baada ya kupigwa na mwalimu wake kwa kufeli somo lake la Kiswahili. 

Familia ya mtoto huyo Joseph Waburi mwenye umri wa miaka kumi imesema mtoto huyo alikuwa na nidhamu ya hali ya juu.

Mama wa mwanafunzi huyo Grace Muthoni amesema mtoto wake alienda shule Jumatatu asubuhi na aliporudi alianza kulalamika maumivu ya kichwa na shingo, siku iliyofuatia alimpeleka Zahanati ya Wilaya ya Nyagiti level 4.

Siku ya pili alilazimika kumrudisha Hospitali baada ya hali yake kuzidi kuwa mbaya, daktari akashauri ahamishiwe katika Zahanati ya Muran’ga Level 4 kwa matibabu zaidi.Wakati akisubiri gari la wagonjwa akafariki dunia.

Mama huyo amesema uchunguzi wa awali unaonyesha mtoto wake alipigwa na Mwalimu na kupata majeraha kichwani na shingoni, mwili wake umehifadhiwa kwa ajili ya uchunguzi kubaini sababu za kifo chake.

Mwalimu anayedaiwa kumpiga Mwanafunzi huyo alikimbia kujificha shimoni baada ya kusikia taarifa za kifo, huku Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Joseph Mwenda akikanusha uvumi kwamba mtoto huyo alifia shuleni.

Ommy Dimpoz Aitwa Mshamba wa Kigoma

$
0
0
“WANANIITA mshamba wa Kimanyema ila poa tu!”Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Omary Nyembo ‘Ommy Dimpoz’, amesema baadhi ya mashabiki wake wanamuita mshamba wa Kimanyema, lakini hilo halimsumbui na wala halimpi presha.

Nyota huyo anayetamba na wimbo ‘Ndagushima’, amesema hawezi kuacha kufurahia kupiga picha nyingi iwezekanavyo anavyosafiri nje ya nchi kwani ni kumbukumbu kwake na pia ni kitu alichokiota kwa muda mrefu.

“Eti wanasema mshamba wa Kimanyema kapata vihela vyake eti kaenda shopingi, nifanyaje sasa na ni kitu ninachokipenda, sitaacha kutupia picha nikiwa nje au ndani ya nchi kwa kuwa ni kitu ninachokipenda na nadhani wengi wanapenda kwani ni sehemu ya kufurahia maisha,” alisema Ommy Dimpoz.

Msanii huyo amekuwa katika ziara ya wiki mbili sasa katika nchi mbalimbali ambapo kesho Jumamosi, atatumbuiza katika Ukumbi wa La Bodega huko Ufaransa baada ya shoo iliyofanyika wiki iliyopita katika mji wa Rotterdam, Uholanzi.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images