Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

Mwanamke yeyote Akikupa Mara Moja, Hata Akiolewa Ukimwomba Tena Atakupa Bila Shida

$
0
0
Aaahh... nilifuatilia hili hadi nimepata almost 75% wanasema kama ukishakuwa na uhusiano
na mwanamke kabla ya kuolewa/ akiwa ndani ya ndoa yaani mmekuwa mnamegana, na kuachana kwa sababu nzuri tu, labda kaolewa kahamia mbali, au kahamishwa kazi then akaja olewa au ulishalala na mwana mke mara moja na hamjagombana siku yeyote ukimwomba hawezi kukunyima, so wanaume watalaam wa mapenzi ni vigumu kugombana na wanawake wanajua siku moja wataonana na kupewa as usual, awe ameolewa au single ili mradi upate SIKU MOJA then siku zijazo hakuna kutongoza , just make a call na kupanga time utapewa......

By Chapa Nalo Jr

Jeshi la Kenya Ladai Wameua Al shabaab 100 Baada ya Shambulio liliouwa Wakenya 28

$
0
0
Makamo wa rais wa Kenya, William Ruto, anasema kuwa askari wa usalama wa Kenya wamewaandama wapiganaji wa al-Shabaab hadi kwenye kambi yao nchini Somalia, baada ya shambulio dhidi ya basi kaskazini-mashariki mwa Kenya hapo jana ambapo raia 28 waliuliwa.
Bwana Ruto alisema wapiganaji zaidi ya 100 waliuliwa katika operesheni mbili tofauti.
Alisema kambi ya al-Shabaab iliangamizwa.
Habari hizo hazikuthibitishwa na upande wa pili.
Gavana wa Mandera - ambako shambulio la jana lilitokea - amelaumu vikosi vya usalama kwa kushindwa kuwalinda raia.
Alisema polisi kawaida wanashindwa kufanya uchunguzi kamili baada ya mashambulio.

Mahakama Kuu imesimamisha mjadala wa Ripoti ya Escrow kujadiliwa Bungeni

$
0
0
Nimepata taarifa muda huu kutoka kwa mtu aliyeko Mahakama Kuu kuwa kutokana na taarifa iliyokuwa inaelezwa kuwa jopo la majaji watatu wa Mahakama Kuu watasikiliza kesi iliyofunguliwa na IPTL na PAP kuzuia bunge kujadili suala la Escrow.

Imeamriwa na Mahakama Kuu chini ya jopo la majaji watatu kuwa wamesimamisha mjadala wa Ripoti ya Escrow hadi hoja za msingi zitakapo fanyiwa kazi.

Bunge haliwezi kupewa zuio na Mahakama, Taarifa ya PAC Itawasilishwa Kwa Mujibu wa Ratiba

$
0
0
'Bunge haliwezi kupewa zuio wakati mkutano ukiendelea. Injunction itoke au isitoke Taarifa ya PAC itaingia. Majaji wasome Katiba na Sheria ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge' Zitto

DK Cheni Alishwa Sumu Tena..Kunani?

$
0
0
Stori: Imelda Mtema
Staa wa kiume wa sinema za Kibongo, Mahsein Awadh ‘Dk Cheni’, kwa mara nyingine alilazwa katika Hospitali ya TMJ iliyopo Mikocheni jijini Dar baada ya kudaiwa kula chakula kinachosadikika kuwa na sumu (poisonous food).

Akizungumza na mwandishi wetu wikiendi iliyopita Dk Cheni alisema kuwa alikuwa mshehereshaji (MC) kwenye harusi moja iliyofanyika maeneo ya Sinza jijini Dar ndipo akala chakula hicho ambapo muda mfupi baadaye alianza kujisikia vibaya ‘kichina’.

Staa huyo alisema kuwa baada ya hatua chache kutoka ukumbini, tumbo lilianza kumuuma kisha akaishiwa nguvu ndipo akaweka gari pembeni na kupiga simu kwa ndugu kuomba msaada.
Dk Cheni aliendelea kueleza kuwa baada ya kupata msaada moja kwa moja alipelekwa kwenye Hospitali ya Burhani jijini Dar.


Alisema kuwa baadaye alihamishiwa kwenye Hospitali ya TMJ ambapo madaktari walipompima waligundua alikuwa amekula chakula chenye sumu ndipo wakampatia matibabu na kulazwa.
Alisema siku ya pili yake aliruhusiwa huku akisema kitendo hicho kimemsikitisha mno.

Siyo mara ya kwanza kwa Dk Cheni kulishwa chakula chenye sumu kwani safari hii ni mara ya pili ambapo mwaka jana alilazwa tena kwa ishu kama hiyo, jambo ambalo haelewi kwa nini inakuwa hivyo.
GPL

Wema Gives a Comment on Zari and Diamond's K!ssing Photo

$
0
0
Kumekucha ...Wema Gives a Comment on Zari and Diamond's K!ssing Photo...

Aliyekuwa Mke wa Muheshimiwa Sugu Afyatua Matusi Mtandaoni

$
0
0
Mzazi mwenza wa Mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi aka Sugu, mwanadada Faiza Ally ameamua kuwatolea uvivu watu wanaodai kuwa ameachwa na mheshimiwa huyo kutokana na mavazi yake. 

Faiza ambae ana mtoto na Sugu, katika instagram ameandika:
“Sasa leo ngoja nifunguke…. Yaani nikiweka picha zangu kwa raha zangu mnaanza kusema oh ndio maana SUGU kakimbia ndio maana kaniacha Nasema hivi MIMI NDIO NIMEMUACHA mkome kunisema nimeachana na nimemuacha tukiwa kwenye process za ndoa na tulishakutana na padri na kwenye jumuiya nilisha anza ….. 

Kuna vitu vikinifanya niondoke kabla ya ndoa ambavyo vitabaki kuwa vya kifamilia ……. Nyie mna muona sugu Kama si mtu wa kawaida mm namuona Kama alie kuwa mpenzi wangu na Sasa ni baba wa mtoto wangu …. Lkn anajua ubora wangu na faida zangu Pumbavu zenu nyote mnao zani niliachwa tena kwa mavazi anajua na anapenda mavazi yangu ….. Nachukia kuamka asubuhi na kukuta comments za kusemwa vibaya…. Nyie mnajua tabia zake ????? Au mnamuona kwa mbali ?????”

Mahakama ilimshindwa Davido, inawezaje kuzuia Escrow Bungeni?

$
0
0
Oktoba 18, mwaka huu, mwanamuziki kutoka Nigeria, David Adedeji Adeleke ‘Davido’ alipanda jukwaani, akatumbuiza na kuondoka kurudi nchini kwao bila kupata usumbufu wowote.

Davido alipanda jukwaa la Fiesta wakati kulikuwa na Amri ya Zuio kutoka Mahakama ya Kisutu, ikiikataza Kampuni ya Prime Time Promotion kumtumia Davido kwenye shoo ya Fiesta kutokana na mgogoro wa kimkataba baina yake na Kampuni ya Times Promotions and Entertainment, vilevile alinyimwa kibali na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata).

Hata hivyo, Davido alipanda jukwaani na hakuna uamuzi wowote wa dharura ambao ulichukuliwa kutoa fundisho kwa wakaidi wa Amri ya Zuio. Ile adhabu ya kudharau mahakama (Contempt) haikufanya kitu.

Ni aibu kubwa kwa taifa letu ambalo linaongozwa na misingi ya sheria na dola. Ni nchi isiyokuwa na dola peke yake ndiyo alichokifanya Davido hapa nchini kinaweza kutokea na kuvumiliwa kana kwamba hakikutokea kitu. Mahakama haikuona aibu hii!

Kama kwa Davido ilitokea hivyo, nitashangaa sana kama bunge litanywea na kuamua kusitisha hoja nzito yenye maslahi mapana kwa taifa. Bunge linaweza kuendelea na kazi yake. Halafu wahusika waendelee kutapatapa mahakamani. Swali; kama kweli ni watu wazuri na walitenda kilicho halali na haki, wasiwasi wa kukimbilia mahakamani wa nini wakati Ripoti ya Escrow haijasomwa?

Jibu ni kwamba wanajua walichokifanya na wanaelewa kilichomo ndani ya Ripoti ya Escrow na wanatambua nini ambacho kinaenda kusomwa na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe, kwa maana hiyo ni waelewa wa kile kinachokaribia kuwapata. Ripoti isomwe, hata wakizuia itavuja na wananchi watachukua uamuzi. Tuache kulinda ufisadi kwa amani yetu na maendeleo ya uchumi wetu.

Mungu ibariki Tanzania.

Polisi Ang'olewa Meno Sita na Wananchi Huko Shinyanga

$
0
0
Kumetokea tukio la aina yake katika mgodi wa madini ya almasi wa Mwaduiuliopo katika wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga ambapo askari polisi wa kikosi cha kutuliza ghasia wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga Pc Idd Makame(25) amejeruhiwa vibaya mdomoni kwa kung’olewa meno sita baada ya kupigwa jiwe kwa kutumia kombeo (kwa lugha ya kisukuma Nh'ago) na watu wanaodaiwa kuwa ni wachimbaji haramu wa madini katika mgodi wa Mwadui wakati akitimiza wajibu wake wa kuhakikisha usalama wa raia na mali zao.

Tukio hilo limetokea Novemba 21,2014saa mb ili na robo usiku katika eneo la Tanex katika mgodi huo wakati askari huyo akiwa na askari wenzake wakiongeza nguvu baada ya askari wa kampuni ya ulinzi ya Zenneth inayolinda mgodi wa Mwadui kushindwa kuwadhibiti wachimbaji wadogo wa madini maarufu "Wabeshi" waliotaka kuingia kwa nguvu mgodini wakiwa na silaha za jadi. 

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema kuwa kampuni ya ulinzi ya Zenneth Security Services Limited inayolinda mgodi huo ilipata taarifa kuwa kuna wachimbaji haramu maarufu kwa jina la Wabeshi walitaka kuvamia mgodi wakiwa na silaha za jadi ikiwemo mishale, mikuki, virungu, makombeo, mapanga.

na fimbo. Kufuatia hali hiyo askari hao wa Zenneth walifika eneo la tukio kuwadhibiti Wabeshi hao lakini ghafla walianza kushambuliwa kwa silaha za jadi yakiwemo marungu, mishale, mikuki na makombeo. Baada ya kuona wanazidiwa nguvu,askari wa Zenneth walilazimika kuomba msaada wa askari wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) cha jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga. 

Baada ya askari wa FFU kufika eneo la tukio nao walianza kushambuliwa na Wabeshi hao ,ndipo PC Idd akapigwa jiwe mdomoni kwa kutumia kombeo na kung’oka meno sita mdomoni na kukimbizwa katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga kwa ajili ya matibabu. Mkurugenzi wa kampuni ya ulinzi ya Zenneth Security Services Limited Elisha Ndulu amethibitisha uwepo wa tukio hilo. 

Naye mganga mfawidhi wa hospitali ya mkoa wa Shinyanga Dkt Mfaume Salum amesema Pc Idd alipigwa na kitu chenye ubapa mdomoni na kusababisha meno sita kung’oka na anaendelea kupatiwa matibabu,hali yake inaendelea vizuri. Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga Justus Kamugisha alikiri kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa tayari wanawashikilia watu wanne kwa mahojiano zaidi na wanaendelea kufanya uchunguzi.

Sakata la wizi wa Mabilioni ya Escrow, Mkono, 'Licha ya kulishwa sumu sitohama Tanzania'

$
0
0
MBUNGE wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono (CCM), amesema licha ya kulishwa sumu na watu asiowajua hatohama Tanzania kama anavyoshauriwa.

Mkono, pia amegoma kuzungumzia sakata la IPTL na akaunti ya Escrow hadi apate kibali cha Mwanasheria Mkuu, Jaji Frederick Werema.

Kauli hiyo aliitoa jijini Dar es Salaam jana, alipozungumza na waandishi wa habari juu ya tukio la kulishwa sumu na kulazwa hospitalini nchini Uingereza.

Mkono, alisema Novemba 11 mwaka huu akiwa na wabunge wenzake wa Kamati ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala, walikwenda nchini Uingereza kwa ziara ya kikazi, ambako alipofika huko aliugua ghafla na kukimbizwa hospitali.

Alisema akiwa hospitali, wabunge wenzake wakiongozwa na Mwenyekiti William Ngeleja, waliwasiliana na ndugu zake juu ya tukio hilo na waliwapa maelekezo ya kuwasiliana na daktari wake (Mkono), Dk. Kapteni

Mkono, alisema Dk. Kapteni anayefanya kazi hospitali ya TMJ, aliwaelekeza wenzake dawa za kumpa kwa kuwa alihisi amelishwa sumu.

“Ukweli nimelishwa sumu, madaktari wameshathibitisha jambo hilo…sijui kina nani walionifanyia hivi, uchunguzi wa aina ya sumu na mtu aliyenipa bado vinaendelea…, waliotenda hivi wanajidanganya,” alisema.

Mkono, alisema akiwa jijini Dar es Salaam alitumiwa ujumbe mfupi wa maneno (sms), ikimtahadharisha juu ya safari yake na madhara atakayoyapata.

Alisema baada ya kutumiwa ujumbe huo, aliwaonyesha wenzake ambao walimtia moyo na kumtaka awe muangalifu na nyendo zake.

Mkono, alisema ujumbe huo utakuwa ni sehemu ya uchunguzi wa tukio lake aliloliita ni la kihuni, lilifanywa na wahuni wasiomtisha.

“Nimeshauriwa nihame Tanzania kwa kuwa tumefikia hatua mbaya, lakini mimi nimesema sihami kwa sababu ya wahuni wachache,” alisema.

Alibainisha kulishwa sumu kwa wabunge si jambo geni hapa nchini, kwa kuwa hata Waziri wa Uchukuzi Dk. Harisson Mwakyembe, alifanyiwa hivyo na kukimbizwa nje ya nchi kwa matibabu.

Kuhusu IPTL

Hata hivyo, Mkono hakuwa tayari kuzungumzia tukio la kulishwa sumu na sakata la IPTL linaloendelea bungeni, ingawa alisema kuna watu anawahisi kuhusika.

Alisema kuwa, alianza kushiriki kesi za IPTL mwaka 1997 akiliwakilisha Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), na kila kitu kilifanyika kwa uwazi na kipo kwenye mitandao.

Mkono, alisema hawezi kuzungumzia masuala ya IPTL bila kibali cha Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), kwa sababu kazi aliyoifanya alipewa na serikali.

Alisema kwa mujibu wa maadili ya uwakili, hapaswi kutoa siri au jambo lolote la mteja wake bila kibali kutoka kwa mhusika.

Polisi wagoma

Jana, Tanzania Daima lilipata habari kwamba polisi walimuhoji Mkono juu ya madai ya kulishwa sumu.

Gazeti hili liliwasiliana na Msemaji wa Jeshi la Polisi, Mrakibu Mwandamizi (SSP), Advera Senso, ili kufahamu kuhusu mahojiano hayo, ambako hakuwa tayari kuweka wazi na aliomba kupewa taarifa zaidi askari waliomuhoji Mkono walitokea wapi.

“Ni vyema ukajiridhisha kwanza kama hao askari wanatokea hapa kwetu au wanatoka kanda maalum …maana inaweza kuwa askari hao wanatimiza wajibu wao wa kawaida wa majukumu ya kazi hivyo jiridhishe halafu unipigie tena,” alisema.

Tanzania Daima halikuishia hapo, liliwasiliana na Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna (CP), Suleiman Kova, ambaye alitaka kujua eneo alilopewa sumu hiyo.

“Naomba unieleze mahali au eneo alilonyweshwa sumu ili nijaribu kufuatilia au ameiripoti wapi hiyo taarifa maana sasa sina taarifa,” alisema.

Tanzania Daima

Leo Ndio Leo Waliokula Fedha Escow Wanaendelea Kutajwa Laivu Bungeni Muda Huu

$
0
0

Leo Ndio Leo Waliokula Fedha Escow Wanaendelea Kutajwa Laivu Bungeni Muda Huu , Baada ya jitihada mbali mbali kufanywa ili Report ya Uwizi wa Fedha za IPTL isiweze Kusomwa Bungeni ..Ila mpaka navyoongea muda huu Report inaendelea kusomwa na Waliokula Fedha wanaendelea kuwekwa Hadharani ...
Stay Tuned....Tutarudi Baadae

Hizi ni Tabia Sugu za Wanaume wa Kibongo

$
0
0
TABIA SUGU ZA WANAUME WA KIBONGO
1. Ukali
2. Ulevi
3. Kuchelewa kurudi nyumbani
4. Kupenda marafiki kuliko familia
5. Umalaya
6. Kuficha mambo yao ya maendeleo
7. Kupenda hawara kuliko mke
8. Ubabe
9. Ubishi
10. Kusafiri bila kuaga wake zao zaidi huaga nyumba ndogo
11. Uchoyo
12. Bajeti kali nyumbani kwenye bar na nyumba ndogo ipo juu
13. Kusaidia watu baki kuliko ndugu zao
14. Kosa dogo ndani ya nyumba kelele nyingi
15. Hupenda kutoa sana ofa bar hasa akiwa na demu
16. Anapenda kuchapa nje ila akichapiwa mtajua watu wote
17. Akikusaidia mshikaji lazima akutangaze
18. hapendi kutoka na mkewe kwenye party
19. Simu yake ina nywila nyingi sana
20. Simu yake hataki iguswe lakini yeye aguse ya mkewe

Sababu ya Report ya Tegeta ESCROW Kuwasilisha Bila Pingamizi

$
0
0
Nadhani ni lazima iwasilishwe hili tupate misaada iliyofungwa. Na sio kumtafuta mchawi au kutatua tatizo, bali lengo nadhani ni kupata kitumbua kilicho sitishwa. 

Ulaya watapata taarifa ya kinachojiri na watatoa kitumbua, ili tupate ngawira za madawa au afya, elimu, .....

Ebu fikiria, jana na leo Tanga hospital wanatumia plastics badala ya gloves kutoa huduma ya kujifungua au ukunga. Bila misaada nchi haiendi. 

Unapotembea juu ya yanayojiri, angalia mbali na sio chini au unachokiona karibu. 

Chambua mwenyewe ujiridhishe. Au mnasemaje. Changia, kwanini ripoti imekubalika kusomwa.

Nani Anafaa Kuchukua Mikoba ya Pinda

$
0
0
Kwa kazi nzuri na uzalendo walio onyesha ndugu Filikunjombe na Zitto ingekuwa busara Filikunjombe apewe mikoba ya Pinda maana najua magamba hawawezi kumpa Zitto

Lakini kwasababu serikali hii wanapeana kimasirahi basi atapewa mzembe mwingine

Naomba pia tutambue juhudi za Kafulila katika ushindi wa leo kwani bila yeye huu uozo ungepita kimya kimya..kwenye kweli uongo hujitenga. Mkono wa Mungu upo juu ya taifa letu,safari Hii Hawa watu waburuzwe mahakamani

Muonekano wa Yule Msichana wa Kazi Aliye Taka Kumuua Mtoto wa Boss Wake Baada ya Yeye Kuchezea Kichapo

$
0
0
Huu ndio muonekano wa yule msichana wa kazi za ndani aliye tenda unyama wa kutaka kumuua mtoto wa bosi wake atimaye naye amepokea kipigo takatifu cha nusu kufa kutoka kwa wazazi wa uyo mtoto hii ni moja ya picha zilizo vuja ambazo wazazi wa mtoto family iyo walizificha.

Unaambiwa haya yote yasingejulikana kama Polisi isingemkamata baba mzazi wa mtoto huyu, yani baba alipoona ile video ndioakampiga Msichana huyu wa kazi ambae baada ya kipigo alikwenda kumshitaki baba wa mtoto Polisi.
Polisi walipomchukua Erick Kamanzi (Baba wa mtoto) nyumbani kwa ke na kumfikisha Polisi ambako alieleza sababu za kumpiga Msichana huyu na kuwaonyesha Polisi  video ambayo ni ya tukio la mtoto wake kupigwa.
Baada ya hapo Polisi ndio wakamwachia na kumkamata Msichana 

Sendeka Asema Tutauana Lakini Pinda Hajiuzulu Katu

$
0
0
SENDEKA asema tutauana lakini PINDA hajiuzulu katu. 
Kikao cha wabunge wa CCM kinachiendelea mchana huu kimekuwa moto mbali. Christopher Ole Sendeka mbunge wa Simanjiro amesema wako radhi kuchinjana bungeni lakini si Pinda kujiuzulu. "Ajiuzulu amekosa nini, ripoti zote hazimtaji popote kuhusika. Kama tatizo ni nia yake ya u Rais, kwani Pinda hana haki ya kugombea? Nasema niko radhi tuchinjane bungeni lakini si kuona mtu anasulubiwa kwa maslahi ya wabinafsi wachache wenye malengo yao ya kisiasa. Kwa hili nitasimama kidete. .."alisema Sendeka huku ukumbi wote ukiwa kimya

Mganga wa Kienyeji Aibuka na Kutoboa Siri Nzito Kuhusu Mwimbaji Meninah

$
0
0
Na Stori: Mayasa Mariwata na Shani Ramadhani
Mganga aliyejita-mbulisha kwa jina moja la Kimweri ameibuka na madai mazito kuwa ndiye aliyemng’arisha staa wa kike wa Bongo Fleva, Meninah Abdukareem ‘Meninah La diva’ hivyo kutoa siri nzito ambayo wengi hawakuijua.Kwa mujibu wa chanzo makini, mganga huyo amekuwa akimfanyia ndumba msanii huyo ili arudiane na aliyekuwa mwandani wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platinum’.

Kwa mujibu wa chanzo hicho, mganga huyo amekuwa akidai kwamba, huwa msanii huyo anatinga nyumbani kwake maeneo ya Mwananyamala-Komakoma jijini Dar kisha kumlilia shida yake akimtaka afanye juu chini kuhakikisha anamrudisha Diamond mikononi mwake.

Baada ya kukisikia chanzo hicho, waandishi wetu walikwenda nyumbani kwa mganga huyo na walipomuuliza ishu hiyo alikiri Meninah kufika kwake ili kufanyiwa ndumba arudiane na Diamond.

“Yule msanii anayeitwa Meninah ambaye habari zilivuma kuwa anatoka na Diamond na kukanusha, huwa anakuja hapa kufuata tiba na kikubwa anachokitaka anataka nimvute Diamond ili warudiane,” alisema.
Meninah alipoulizwa kuhusu madai hayo aliruka kimanga na kudai hakuwahi kuwa na uhusiano na Diamond na wala hamjui mganga huyo.

“Yule msanii anayeitwa Meninah ambaye habari zilivuma kuwa anatoka na Diamond na kukanusha, huwa anakuja hapa kufuata tiba na kikubwa anachokitaka anataka nimvute Diamond ili warudiane,” alisema.
Meninah alipoulizwa kuhusu madai hayo aliruka kimanga na kudai hakuwahi kuwa na uhusiano na Diamond na wala hamjui mganga huyo.

Dida Afunguka Kuhusu Ezden Kuoa Mke Mwingine Baada ya Wao Kuachana

$
0
0
Na Imelda Mtema
MTANGAZAJI mwenye maneno lukuki kutoka Radio Times FM, Khadija Shaibu ‘Dida’ amesema kuwa endapo mtalaka wake, Ezden Jumanne akitaka kuoa yeye atakuwa wa kwanza kutoa mchango wa harusi hiyo.

Dida ambaye kwa sasa yupo singo, alisema japokuwa wameacha na Ezden, lakini hana bifu naye kwa sababu anaamini kuwa yuko katika harakati za kutafuta mke bora hivyo haoni shida kumchangia.

“Ninachoamini mimi Ezden bado anasaka mke mwema na hiyo ni nzuri na wala siwezi kuwa na bifu na mtu wake yeyote atakayempata, nitapenda sana. Haya ndiyo maisha yasiyokuwa na chuki yanayotakiwa,” alisema Dida.

Hakuna Atakayeachia Ngazi Sakata la Escrow

$
0
0
Baada ya kusikiliza ripoti rasmi ya PAC iliyowasilishwa na Zitto Kabwe na Deo Filikunjombe nnadiriki kusema kuwa hakuna cha maana kwenye ripoti yao cha kuwafanya mawaziri kuwachia ngazi.

Ni drama tu lakini hakuna kipengele chochote cha sheria ambacho hakijibiki au kilichooneshwa kuwa kimekiukwa.

Hukumu ya Mahakama ni ya halali na haina utata na Zitto wala CAG wala TAKUKURU hawajaonesha kuwa ilikuwa ni batili au ya kughushi. 

Zitto kapiga porojo nyingi sana kuliko ukweli, na mwanasheria yoyote mahiri anazisambaratisha hoja zake zote ndani ya nusu saa.

Zitto ametetea sana BoT lakini alichoshindwa kuelewa ni kuwa Bot kama wakala ndiye alitakiwa aridhike na vielelezo vyote kabla hajalipa na kama havijakamilika hawezi kutoa fedha. Zitto anasema eti Mwanasheria Mkuu wa Serikali ndiye alimuamuru Gavana hizo fedha zitolewe, toka lini Gavana wa benki anatoa fedha kwa amri ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali? 

Utata wa IPTL na Standard Chartered ni huko-huko kwao si IPTL iliyokopa, iliyokopa ni Mechmar na Mechmar haiwezi jitokeza kwani imeshafilisika kisheria, Standard Chartered karata yao ya mwisho ni hii na hapa wamepata mwanya.

Nnasikitika kusema na nnaliona linakuja la Serikali kuingia gharama kubwa ya kulipa zaidi ya mara mbili au tatu hizi fedha ikiwa watafata akili za akina Zitto.

Nnashauri, wajadili hili suala bungeni lakini shauri liwachwe kesi kumi zilizopo mahakamani zinazoihusu IPTL zikamilike.

Mapendekezo ya Zitto ya watu kuachia nyadhifa zao ni ya kishabiki na hayana mshiko, watu hawaachii tu nyadhifa zao kwa habari kama hizi ambazo hazina mshiko wa kisheria.

Isitoshe, fedha zilizolipwa escrow si kamili, hizo zilizobaki zilizuiliwa kwanini? Jibu tutalipata kesho na ndilo litakalosambaratisha hoja ya kodi ya Zitto. 

Kuna mengi sana ya kuchambua lakini tusubiri leo, tusiandikie mate na wino upo. Ni matumaini yangu kuwa wote waliotajwa watapewa fursa ya kujibu. Na hapo ndipo mtamjuwa Chenge ni kichwa.

By  FaizaFoxy

Drama: Wema kuhudhuria show ya Chameleone, Diamond kuwa mgeni wa show ya Zari, zote kufanyika siku 1

$
0
0
Taarifa zilizosambaa ni kwamba Wema na Diamond wanatarajiwa kwenda Uganda December, lakini kila mmoja akiwa na mwaliko wa mwenyeji tofauti. Diamond atakuwa mgeni kwenye show ya Zari The boss lady, huku Wema atakuwa mgeni wa show ya Jose Chameleone.

Maswali ya uhusiano wa staa wa filamu Wema Sepetu pamoja na staa wa muziki Diamond Platnumz yamezidi kuongezeka kama kweli wameachana ama laa, baada ya wote wawili kujihusisha kupigia debe show hizo mbili tofauti zinazotarajiwa kufanyika siku moja, mwezi mmoja, jiji moja lakini kumbi tofauti.

Diamond ambaye amekana kuwa hana uhusiano wowote wa kimapenzi na Zari, amepigia debe show ya ‘Zari All White Ciroc Party’ huku akitarajiwa kuwa mgeni kwenye show hiyo. Kupitia akaunti zake za mitandao ya kijamii ameandika:

kama mlivyokuwa kimya wakati nasupport watu wengine… Muendelee hivyohivyo…Hasa niwaskie kwenye hii #AllWhiteParty 18th Dec 2014 at Guvnor night club in Kampala UG Usikose!… @zarithebosslady

Huku Wema naye amepigia debe show ya Jose Chameleone ‘1 Man, 1 Show, 1 Million’ huku akiahidi kwenda Uganda kuhudhuria show hiyo, ameandika:

Hatari….!!!! Hatari….!!!! Hatari….!!!!! Sijawahi kufika Uganda lakini kwa hii ntapanda ndege kabisa kwenda kumsupport my brother @jchameleone @jchameleone @jchameleone @jchameleone @jchameleone @jchameleone …. Basi tutakutana pale kati tar 18 kwenye hio show ya kufunga mwaka… Ama nene….”

Show zote mbili ya Zari na ya Chameleone zinatarajiwa kufanyika Kampala siku moja ya Dec.18.
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live




Latest Images