Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104768 articles
Browse latest View live

Mtoto wa Mgimwa Amenifikirisha Sana Baada ya Kusema Kifo cha Baba yake Kisijadiliwe Bungeni

$
0
0
Kuna madai ya watu kuwatoa kafara watoto wao, wake zao au hata wazazi wao ili waweze kufikia mafanikio wanayotaka.

Hili la mtoto wa Mgimwa kugoma kabisa kifo cha utata cha baba yake kisijadiliwe Bungeni huku akijua kuwa anajadiliwa kama Waziri kama anavyoongelewa Hayati Baba wa Taifa ambaye pia anao watoto lakini haionekani kwamba si busara kumjadili baba wa taifa kama inavyotaka kuoneshwa kwamba ni Nongwa kumjadili Mgimwa eti kwa kuwa ameshafariki.

Hii inanitia shaka sana huenda alishirikishwa kwa malipo ya Ubunge.
Ni mawazo tu kwasababu haya mambo yapo je wewe unaonaje kuhusu hilo Swala?

Ikulu ya Tanzania Yahusishwa na Escrow

$
0
0
Bunge la Tanzania hapo jana liliambiwa kwamba afisa mmoja wa ikulu ya rais bwana Prosper Mbena aliandika barua ili kushinikiza hatua ya kutolewa kwa billioni 306 fedha za Escrow kutoka banki kuu ya Tanzania.
Bwana Mbena ambaye anafanya kazi kama katibu katika afisi ya rais aliandika barua mwaka uliopita akiiagiza wizara ya fedha kuzitoa fedha hizo kama ilivyoamrishwa na mwanasheria mkuu.
Kushirikishwa kwa ikulu ya ya rais kulizuka baada ya wabunge kujadili ripoti kuhusu kashfa hiyo ambayo imeikumba serikali ya Tanzania katika miezi kadhaa iliopita.
Kiongozi wa upinzani katika bunge,Bwana Freeman Mbowe pamoja na kinara wa bunge upande wa upinzani bwana Tandu Lissu alifichua jukumu lililochukuliwa na afisa huyo wa ikulu kushinikiza madai kwamba baadhi ya maafisa wakuu serikalini walihusika katika utoaji wa mabilioni hayo ya fedha.
Ripoti hiyo imesema kuwa fedha hizo za Escrow ni za walipa ushuru wa Tanzania na kwamba zilitolewa kwa njia ya ufisadi na kugawanywa miongoni mwa watu maarufu.

Overconfidence kwa Msichana itakufanya Usiolewe

$
0
0
  
Ukipenda kuongea na watu, kwa kweli utapata mengi sana na utaongeza maarifa.

Huu ni ukweli nilioufanyia mahojiano na wanaume mbali mbali ambao hawajaoa.

Wanadai ya kwamba msichana anayejiamini sana kupita kiasi ana safasi ndogo sana ya kuolewa. Kwa sababu wanaume waliowengi hujisikia wanyoge sana kwenye ndoa, wanawake wanapokuwa wao ni kama watawala katika familia na wenye maamuzi(tena wanawake kama hao wanakiburi sana, kutokana na kujiamini kwao.)

Wanaume walioa wanawake wanaojiamini kupita kiasi, wanadharaulika sana mbele ya jamii. 

Wasichana kazi kwenu mnaotaka kuolewa.

Helicopter ya Tanapa Yaanguka Dar na Kuuwa Watu Wote Pamoja na Rubani

$
0
0

Wakati tukiendelea kusikilizia habari za ESCROW habari za hivi punde zimenifikia toka kwa jamaa yangu wa karibu sana kuwa helikopta ya maliasili (TANAPA)  imedondoka maeneo ya Kipunguni karibu na Moshi bar na kuua wote waliokuwepo ndani yake wakiwemo polisi na Rubani.

Mbunge Lugola Awavunja Wabunge Mbavu Baada ya Kuomba Kuvaa Kininja ili Asiwatazame wahusika wa Escrow Usoni

$
0
0
MBUNGE wa Mwibara (CCM), Alphaxard Kangi Lugola wakati akichangia katika Ripoti ya PAC kuhusu sakata la Akaunti ya Tegeta Escrow bungeni jana, aliomba kuchangia huku akiwa amevaa 'Kininja' ili kutowaangalia usoni wahusika wa sakata hilo.

Mbali na kuvaa hivyo, Lugola pia aliomba kama kanuni zinaruhusu achangie tena akiwa amevaa nguo za chama chake cha CCM ili kuonyesha kuwa CCM haiungi mkono vitendo viovu japo alikataliwa na Mwenyekiti wa Bunge, Mhe. Zungu.
  
Tazama  Video  ya  tukio  hilo  hapo  chini.

Haya hapa majina yaliyoteuliwa na PAC kuandika maazimio ya kuwawajibisha watuhumiwa wa Escrow

$
0
0
Baada ya Spika wa Bunge kuahirisha Bunge mara mbili siku ya leo Novemba 29 ili kuipa nafasi kamati ya PAC iweze kufanya marekebisho ya maneno yaliyoandikwa kwenye maazimio yaliyowasilishwa na Kamati ya PAC, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Zitto Kabwe ametaja majina ya walioteuliwa na Kamati hiyo kuandika maazimio ya kuwajibisha watuhumiwa wa Tegeta Escrow.
Kupitia ukurasa wake wa Facebook (@Zitto Kabwe) ameandika majina ya wajumbe hao.

Diamond Azidi Kuwatia Wivu Team Wema, Aenda South Africa na Zari The Lady Boss

$
0
0
Diamond Amezidi kuwapa Hasira Team Wema Baada ya Kupost Picha Instagram Akiwa na Zari South Afrika  na Kuuliza hili Swali 'Otea nani yuko nyuma angu..? Guess, who is behind me...?'

Diamond Yupo South Afrika kwa muda sasa Ambapo Usiku huu Atatoa Burudani ndani ya Jumba la Big Brother Africa

Zitto Kabwe kuhudhuria kikao cha UKAWA wakati huu ni udhaifu mkubwa

$
0
0
Jana katika bunge mwenyekiti wa PAC ZITTO KABWE alisimama bungeni na kuongea kwa fahari kuwa alihudhuria kikao cha UKAWA usiku uliopita. Kwa nafasi ya Zitto kama mwenyekiti wa kamati ambayo hoja yake iko mezani inajadiliwa, halikuwa jambo la sawa kuhudhuria kikao cha UKAWA na kusuluhishana, hasa wakati huu. 

Zitto angebaki kuonesha neutrality ya ufuasi wa vyama, kwani katika kupitisha mapendekezo ya kamati yake anahitaji uungwaji mkono wa wabunge wa vyama vyote vikiwemo visivyounda UKAWA.

Zitto hakupaswa kukubali kutafuta suluhu na UKAWA wakati huu ambapo kamati yake imepewa dhamana kubwa ya kulivusha taifa katika sakata hili bila ya upendeleo wala uonevu. Kukubali wito wa suluhu na UKAWA ni sawa na matumizi ya nafasi yake kwa maslahi binafsi ya kujijenga kisiasa. Hii ndiyo tafsiri ya rushwa, abuse of public office for the private gain. 

Hata kama hakujua haya, hakukumbuka busara na akahudhuria kikao cha UKAWA , halikuwa jambo sahihi kulisema mbele ya bunge tukufu. Kufanya vile kuliashiria kuwa Zitto amechukua upande na anaitumia ESCROW kujijenga yeye binafsi na siasa yake. Anatumia nafasi yake kama mwenyekiti wa PAC kufuta makovu ya kufukuzwa CHADEMA, huku akidhihirisha kuwa yeye ni muhimu kwa uhai wa upinzani nchini. 

Zitto amefanikiwa kuonesha kuwa yeye ni muhimu kwa UKAWA, lakini pia ametumia nafasi yake ya uenyekiti wa PAC vibaya. Jambo hilo liliingiza bunge katika kufanya maamuzi kwa ushabiki wa vyama badala ya busara.

Nimemkuta Mume Wangu Akifanya Ngono na House Girl wa Jirani Yetu

$
0
0
Juzi nilikuwa naenda kazini nikamuacha mume wangu
nyumbani anaangalia TV, gari langu likazima ghafla kiasi cha
kilomita moja toka nyumbani.
Nikaona nitembee mpaka nyumbani kumwomba mume wangu aje anisaidie kutengezagari, kwa mshangao wangu nilipofika nyumbani nikamkuta mume wangu yuko chumbani na msichana wa kazi wa nyumba ya jirani. Mume wangu ana miaka 43, mimi nina miaka 39 na msichana huyo ana miaka 19 hivi.Tumekuwa katika ndoa kwa miaka 10. Nilipomuuliza mume wangu alikubali kuwa uhusiano wao umekuwa ukiendelea kwa miezi sita sasa, nifanye nini mimi?
NISHAURINI NIFANYAJE NDUGU ZANGU...
SHARE HII TAFADHALI

Hatari za kuweka picha za mtoto mtandaoni

$
0
0
Nianze kwa kukuuliza wewe mzazi; unapoweka picha ya mtoto wako kila hatua tangu akiwa mchanga hadi anaanza kutembea na kuanza shule, alikuomba au ulipata ruhusa yake?

Ingekuwa wewe umepigwa picha bila idhini yako halafu ukaikuta kwenye mtandao utafurahi?

Najua unampenda mtoto wako na ana haki zake za msingi pamoja na kuheshimiwa faragha yake popote alipo. Haiwezekani chochote anachofanya ukiweke kwenye mtandao.

Naomba kueleza madhara yanayoweza kutokea kwa kuweka picha za mtoto wako au wa mwenzako kwenye mitandao hasa mitandao ya kijamii kama facebook , instagram na mingineyo.


Kwanza fahamu kuwa kampuni karibu zote za mitandao ya kijamii zimesajiliwa Marekani, chache zimesajiliwa Ulaya na Asia, lakini karibu zote zinatumia sheria na sera za mataifa hayo.


Katika mataifa hayo wanasisitiza mtoto asijiunge kwenye mitandao ya kijamii hadi atakapofikisha miaka 13, wengine miaka 15 au 16 .


Kampuni zote za mawasiliano zina utaratibu wa kuhifadhi kila kitu kinachotokea kwenye shughuli zao za kila siku kwenye chombo maalumu cha kuhifadhi taarifa za mtandao (server). Kwa hiyo ukiweka picha za mtoto zinahifadhiwa huko hata kama utazifuta.


Hapo awali, nilisema mtoto anahitaji faragha yake, unaporusha picha za mtoto wako kwenye hii mitandao au mawasiliano yoyote, unaingilia faragha yake na huko mbele anaweza kukushtaki wewe au wengine walioingilia faragha yake.


Mtoto anatakiwa kufunzwa kuanzia mdogo kabisa kuhusu faragha yake, nini cha kusema au kutoa na nini asiseme au asitoe. Hii ni pamoja na kwenye mitandao ya kijamii, simu na huduma nyingine za mawasiliano .


Umeshawahi kuona wanasiasa wanaweka picha za watoto wao au ndugu zao wa karibu kwenye mitandao hasa ya kijamii ? unajua ni kwa nini ?


Kwa sababu kila anachofanya yeye kinamwathiri mtoto wake au watu wake wa karibu kwa ubaya au uzuri. Ni rahisi kuweka rehani faragha za watoto na ndugu zake.


Kama ni mtoto wa kike anaweza kuanza kufuatiliwa na ‘mabazazi’ kwa sababu ya picha tu. Watatafuta anapoishi, shule anayosoma na usishangae siku moja akabakwa.

Kwa hisani ya mwananchi tunapata elimu

Hoja yangu:
Kwanini hii tabia imezuka sana wanandoa siku hiyo hiyo mama anaugulia maumivu badala ya baba kumhangaikia mama na mwanae yeye anafuta kamera iko wapi tena siku hizi mchina amerahisisha anamfotoa mtoto na kupost kwenye wall yake ili iweje? kwamba watu wajue na wewe ni kudume cha mbegu au una kizazi? matokeo yake ndo wazazi mnapotofautiana na marafiki zenu mnawatukana mpaka watoto, kuna wengne sijui mtandao gani yule dada anauza pichu anamtukana mtoto wa mwenzaje eti baboon hivi mnahisi watoto wanajisikiaje? unamharibia mtoto future yake bila kujua, ukifikiri ni fahari kuweka picha ya mwanao sijui facebook, twitter, instagarma na kwingne huko ni ushamba na ujinga, labda siku hizi kwa kuwa imekuwa issue sana kupata mtoto but is not fair

Nawasilisha hoja

Dada wa Diamond, Queen Darleen Afunguka Kuhusu Mawifi zake wa Bandika Bandua

$
0
0
Queen Darleen ambaye ni dada yake na Diamond, hana tatizo na ‘bandika bandua’ ya mawifi wanaotambulishwa kwake na kaka yake huyo. Kwa mujibu wa Queen, hayo ni maisha yake na anayaheshimu.

Queen ambaye pia ni mwanamuziki, amesema kila msichana anayetambulishwa kama wifi yake, humpa heshima anayostahili.

“Mapenzi siku zote ni ya watu wawili ndio maana unaona hata mimi nina maisha yangu kama maisha yangu siingilii chochote.
Yaani mimi Diamond ukitaka kunichafua umwongelee vibaya. Jambo lolote baya kuhusu yeye, muziki yake na maisha yake binafsi. Kwa sababu kuna watu wengine wanapenda kuzungumzia mambo ya watu, ‘sijui Diamond anaringa’,

Hatimaye Diamond Amkalisha Davido Kwenye Tuzo Channel O

$
0
0
The 2014 Channel O African Music Awards

Usiku wa jana Diamond alitisha baada ya kuongoza kwa kuchukua tuzo nyingi(3).Kwenye tuzo ya most gifted afropop ndio mtu mzima davido alipokaa,big up kijana endelea kutuwakilisha kimataifa.
Diamond Platinumz walked way with the Most Gifted Newcomer, Most Gifted Afro Pop and Most Gifted East.

Alichosema Wema baada ya Diamond kupata tuzo 3 za Channel O

$
0
0
Baada ya Diamond kupata tuzo tatu usiku wa kuamkia leo, madam Wema Sepetu ktk page yake ya instagram hakusita kumpongeza kwa kuandika:
"Good night Instagramers pongezi nyingi zimuendee kaka Plutnumz kwa kupata tuzo"
Hii ni muendelezo wa series zao za mapenzi ktk kuachana na kurudiana.
Diamond aliongizana na mama yake pamoja na mpenzi wake mpya Zari, ktk khafla hiyo ilihudhuliwa pia na Vannesa Mdee, madam Rita na Salama Jabry.

Wema Sepetu azua gumzo kwenye mtandao baada ya kumuita Diamond "kaka"

$
0
0
Huku macho na masikio ya wananchi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania yakiwa kwenye bunge la katiba linalojadili lile sakata la tegeta ESCROW, mwanadada Wema sepetu ameamua naye kuzua gumzo kwenye mtandao baada ya kutoa salamu ya pongezi kwa kijana Naseeb al maarufu kama Chibu dangote ama Diamond platnumz kwa ushindi wake wa tuzo 3 kwenye tuzo za Channel O MUSIC AWARDS zilizofanyika huko Afrika ya kusini akitumia neno KAKA katika sentensi yake kitu ambacho kimezua minong’ono ya hapa na pale kwenye mtandao ule maarufu wa kijamii wa picha nchini.

Katika post yake hiyo Wema aliandika

 “…Hongera tele ziende kwa kaka platnumz... I must say he did Tanzania proud..”   na kufanya watu waanze kufunguka ya kwaio ya moyoni kuhusu kauli hiyo na baadhi yao walisema haya.


MELA : “Leo kawa kaka!!!!!! Aiseeee mapenz ya mastaa mafupi kama mkia wa kondoo”


“ LILY: “et kaka plutnums heheheheh wema bwana”


“PIERE: mara hii kaka tena?? Ohhhhhh”


ANNA: “hao ni wakuwaacha kesho.tu.watakua tena pamoja”

Katika tuzo hizo, diamond alisindikiwa na anayesemekana kuwa kipenzi chake cha sasa, mwanadada Zari ktukoa nchini Uganda, pamoja na mama yake mzazi na team ya wasafi.


Nini maoni yako mdau kuhusu ishu hii? 

Mwanajeshi Alewa Chakali na Kulala katika Mfereji wa Maji Machafu

$
0
0

KATIKA hali isiyotegemewa askari mmoja wa jeshi la kujenga Taifa (JKT) anayesadikika kuwa na wa kambi ya Mafinga wilaya ya Mufindi mkoani Iringa usiku wa leo amenusurika kuvuliwa nguo za jeshi hadharani baada ya kukutwa amelewa chakali na kulala katika mfereji wa maji machafu eneo la nje ya stendi kuu ya mabasi yaendayo mikoani mjini Iringa

Tukio hilo lilitokea muda wa saa 2 usiku baada ya wasamaria wema kumshusha askari huyo kutoka katika basi la Mgumba ambalo alikuwa amepanda kutoka Mafinga kuja mjini Iringa.

Akisimulia kisa na mkasa wa askari huyo kulewa chakali kiasi cha kushindwa kujitambua mmoja kati ya wasamaria wema aliyejitolea kumshusha katika basi hilo alisema kuwa askari huyo alipanda basi hilo Mafinga huku akiwa amelewa na wakati wote wa safari alionekana akinywa pombe kali kiasi cha kushindwa kujimudu na kuanza kutapika na kujisaidia haja ndogondani ya basi hilo.

Hata hivyo alisema baada ya kufika stendi ilikuwa ni vigumu kujitambua hivyo kupoteza fahamu na kulazimika kumpa msaada na kumzimua kwa maji kabla ya kupata fahamu kiasi na kujificha chini ya mfereji wa maji machafu .

Alisema kuwa mara baada ya kujitambua kiasi aliweza kutoa namba ya ndugu yake ambae ni askari wa FFU mjini Iringa aliyefika kumnusuru kuvuliwa nguo na kiongozi wake aliyefika eneo hilo na kumkutana akilishushia heshima jeshi kwa ulevi uliopitiliza

" Umelidhalilisha sana jeshi kwa askari kulewa hivi ukiwa katika sare .....sasa nataka kukuvua sare kisha nakupeleka kulala polisi kabla ya kesho kukuchukulia hatua zaidi " alisikika akisema kiongozi huyo ambae jina wala cheo chake hakukitaja

Maamuzi hayo ya kiongozi wake yaliwafanya mashuhuda kumuangukia na kumwomba amsamehe kwani bado ni kijana mdogo sana mambi ambayo aliyakubali na ndugu zake kumpakiza katika Taxi na kumpeleka eneo la Kihesa .

Ushauri wetu kwa askari wetu kujaribu kuheshimu nafasi hizo japo hakuna anayewakataza kunywa pombe ila watambue kuwa unywaji pombe kupita kiasi ni hatari kwa afya yako ama chonde chonde ulevi noma.

Maneno 6 Mazito ya Davido baada ya ushindi wa Diamond Platnumz Channel O 2014

$
0
0
Ushindi wa tuzo tatu za Channel O 2014 alizochukua Mtanzania Diamond Platnumz umekua mkubwa sio tu kwa Tanzania bali Afrika na kona zake ambapo miongoni mwa walioandika baada ya Diamond kushinda ni Davido.
Msanii huyu wa Nigeria ambae alifanya remix ya number one ya Diamond aliandika kwenye page yake ya instagram >>> TANZANIA STAND UP! HE DID IT na kisha akammention Diamond Platnumz.

Kwenye post hii ya Davido ambae hakupata tuzo yoyote ya Channel O japo alikua anawania, imepata likes zaidi ya elfu kumi na nne kutoka kwa followers wake ambao ni zaidi ya laki nne huku comments zikiwa ni zaidi ya mia saba.

Watoto wa Obama Ndani ya Skendo Chafu ya Mavazi Mafupi

$
0
0
Watoto wa rais wa Marekani Barrack Obama, Sasha na Malia wameshtumiwa kwa kukosa heshima na afisa mmoja wa chama cha Republican baada ya kuhudhuria sherehe za kutoa shukrani.

Elizabeth Lauten ,ambaye ni mkurugenzi wa mawasiliano wa mbunge Stephen Fincher alitoa matamshi yake katika mtandao wa facebook ambayo baadaye yalifutwa.

Baada ya kukosolewa Bi Lauten aliomba msamaha kwa kutoa matamshi hayo ya kukera.

Alikua akikosoa sketi fupi zilizovaliwa na wasichana hao wa Obama.
Bi Lauteni pia aliwashtumu wasichana hao kwa kuonyesha uchovu wakati waliposimama na baba yao katika sherehe hiyo ya ikulu ya Whitehouse. 

Maandishi yake yalisoma:
''Kwa wapendwa Sasha na Malia: najua kwamba bado mko katika usichana wenu lakini ninyi ni miongoni mwa familia ya kwanza ya taifa hili, tafadhali jaribuni kuwa na heshima.Tafadhalini jaribu kuheshimu jukumu mlilopewa.

''Mama yenu na baba yenu hawaheshimu nyadhifa zao kama inavyohitajika na taifa kwa jumla.
Kwa hivyo naona kwamba mnakosa ile hadhi ya kuwa kioo cha jamii.

Maandishi hayo yaliendelea na kuwashauri wasichana hao kuonyesha kwamba wanaishi katika ikulu ya Whitehouse.

Vaeni mavazi ya kuonyesha mnahitaji kuheshimiwa sio kama mko katika baa.

Una maoni gani juu ya hii kashfa?! Toa maoni yako hapo chini tafadhali!

Amini, Usiamini, Maazimio yaliyotokana na Maridhiano ni Makali kupita Maazimio ya Mwanzo ya PAC

$
0
0
Ukiangalia kwa makini maazimio ya kuwawajibisha viongozi wa umma walioshiriki kwa namna moja au nyingine katika sakata hili la Tegeta Escrow, utaona kwamba maazimio yaliyotokana na maridhiano kati ya CCM na wapinzani ni makali kupita maazimio ya mwanzo ya PAC.....


Maazimio ya mwanzo ya PAC pamoja na mambo mengine yalipendekeza kuwawajibisha wafuatao : wziri wa nishati na madini, naibu wake pamoja na katibu wa wizara hiyo ikiwa ni pamoja na wazri mkuu...


Pamoja na kwamba Waziri mkuu hajawajibika katika maazimio yaliyotokana na maridhiano, hao wengine wote (ukimwondoa Naibu waziri ambaye hata hivyo hakuhusika moja kwa moja), bunge limependekeza wawajibishwe na kuongeza idadi ya watu wengine wa kuwajibika ambao ni pamoja na waziri wa ardhi (Tibaijuka) na wenyeviti watatu wa kamati za kudumu za bunge...


Kwa kweli nimshukuru sana Mbowe kwa uamuzi aliouchukua dakika za mwisho wa kutishia kususia bunge kitu ambacho kimepelekea haya yote kutokea. Katika hali ya kawaida na kwa jinsi lile Bunge lilivyokuwa linaendelea, mapendekezo dhaifu yalishakuwa yamepitishwa kuhusiana na Maswi na ndio hayo hayo yaliyokuwa yanaelekea kupitishwa kwa Muhongo na Werema....Waziri mkuu obvious ange-sevu kwani trend ndivyo ilivyokuwa inaenda......The best we could get at that time ilikuwa mapendekezo ya kuwajibishwa kwa Werema na Muhongo ambapo hata hivyo CCM walikuwa karibu kushinda vita hivyo kama walivyokuwa wameshinda kwa Maswi......


Mimi binafsi (naamini hata watu wengine wengi tu) niliona hakuna kinachoweza kufanyika zaidi ya Muhongo na Werema kupata mapendekezo kama yaliyotolewa kwa Maswi !. Ungewezaje kuwa na mapendekezo tofauti dhidi ya Muhongo na Werema katika mazingira yale ambapo tayari umeshapitisha mapendekezo tofauti kwa Maswi ? Ndio maana Zitto (hata Mdee kama uliangalia vizuri - alionyesha kwa ishara) akasuggest mapendekezo hayo hayo yatumike kwa waliobaki kwa sababu hiyo ilikuwa issue ya common sense tu ! Pinda, Werema, Muhongo, Maswi wote ni wateule wa Rais.....sasa kama umeamua Maswi apelekwe kwa Rais kwa hatua yeyote ile, sioni sense ya kuamua vinginevyo kwa hao wengine......Mimi binafsi niliona alichokipendekeza Zitto kilikuwa sahihi !


CCM nao (sijui ilikuwa malicious au genuine), walitengeneza mazingira mazuri sana ya majadiliano kiasi kwamba ilikuwa ngumu kuibuka na kupinga utaratibu wote na kutishia kususa kama alivyofanya Mbowe. Binadamu ni binadamu tu, mkiwa mmekaa katika mazingira ya kuelewana na kuongea kiistaarabu na kujadiliana na kukubaliana baadhi ya mambo katika spirit hiyo na ikafika mahali kukawa na ugumu kidogo huwa inatokea tu natural mnajaribu ku-compromise....it is very natural. Na ndio maana katika mazingira yale ilikuwa rahisi kukubali mapendekezo ya Chenge ambayo yalionekana ku-accomodate position ya CCM na ya wapinzani kwa kiasi cha kutosha ukilinganisha na mapendekezo yaliyotolewa kabla. Na ndio maana mapendekezo hayo yaliweza kupitishwa kwa Maswi.....


Mbowe kuibuka na kubadilisha kabisa mwelekeo wa bunge, kama tutakuwa waungwana wengi wetu tutakiri kwamba ni kitu ambacho hatukukitegemea katika mazingira yale yaliyokuwa na majadiliano ya kiistaarabu !. Kwa kweli nashindwa kujua ushauri huu aliutoa wapi lakini kwa kweli maamuzi yake ya kusimama na kutishia kutoka yeye pamoja na wabunge wengine wa upinzani ndio ambayo yamesababisha CCM kulazimika kukaa kwenye meza ya mazungumzo na kwa kweli kwa maoni yangu mimi imesababisha viongozi ambao tulitaka sana wawajibike (Muhongo, Werema na Maswi) wamependekezwa kuwajibishwa na Rais na vile vile imesababisha na viongozi wengine kuongezwa !


Katika maridhiano hayo kitu ambacho CCM wamepata kwa maoni yangu ni kubaki kwa Pinda tu.....lakini hivyo vichwa vingine vyote tumekula !. Mimi binafsi nimeridhika sana kwa matokeo haya 

Housegirl Anafanya Mapenzi na Mtoto wa Miaka Sita

$
0
0
Nikiwa home kama weekend ndani ya chanel k24 ya Kenya kuna house girl mmoja anaduuu na mtoto wa miaka 6 

Akielezea sababu za msingi za yeye kufanya hivyo alisema:-

Ni tabia za maboss wake huwa wanshikana kimahaba mbele yake na kuanza kuchekeshana kimapenzi sasa kutokana na hali hiyo na yeye akaanza kupata hamu ya kuduu na mtu yoyote ili ajikimu kimwili 

Lakini alikosa fursa ya kutoka nje ndipo alipoamua kutembea na mtoto wa boss wake mwenye miaka Sita 
Tangia aanzishe huo mchezo na hiko kidushelele cha dogo now ni mwaka na miezi 5

Mnategema nini ninyi wasaidizi wa kazi za nyumbani mbona mnazidi kutupa stresss Jamani?

Rais Kikwete Amteua Profesa Assad Kuwa CAG Mpya

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Profesa Mussa Juma Assad kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Taarifa iliyotolewa leo, Jumatatu, Desemba Mosi, 2014 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, inasema kuwa uteuzi wa Bwana Assad ulianza Novemba 5, mwaka huu, 2014.
Taarifa hiyo imeongeza kuwa Bwana Assad ataapishwa kesho, Jumanne, Desemba 2, saa nne asubuhi, Ikulu, Dar es Salaam.
Kabla ya uteuzi wake, Bwana Assad alikuwa Profesa Mshiriki, Idara ya Uhasibu, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na anachukua nafasi ya Bwana Ludovick Utouh ambaye amestaafu kwa mujibu wa Sheria za Utumishi wa Umma.
Profesa Assad ni msomi, mwenye weledi, ujuzi na uzoefu mkubwa wa uhasibu na udhibiti wa fedha ambaye ana Shahada ya Uzamivu wa Uhasibu (PHD in Accounting) kutoka Chuo Kikuu cha Southampton, Uingereza mwaka 2001 na Shahada ya Uzamivu katika Udhibiti wa Fedha (MA in Financial Accounting) kutoka Chuo Kikuu cha Dublin City, Jamhuri ya Ireland mwaka 1991.
Profesa Assad pia ana Stashahada ya Kitaaluma ya Uhasibu (Professional Diploma in Accounting) kutoka Chuo Kikuu cha Dublin City mwaka 1990 na Shahada ya Biashara (Bachelor of Commerce) ya Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam mwaka 1988.
Pamoja na uzoefu wa kitaaluma, Profesa Assad anao uzoefu mkubwa katika eneo la uhasibu na ukaguzi. Alikuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wahasibu na Wakaguzi (NBAA) kwa miaka saba (2007 - 2014); ni Rais na Mjumbe wa Chama cha Wahasibu Afrika (Pan African Federation of Accountants) tangu mwaka 2012; na ni mjumbe wa Bodi kadhaa za Wakurugenzi nchini Tanzania.
Katika kumteua Profesa Mussa Juma ASSAD kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Rais anayo imani kubwa kuwa elimu, weledi, ujuzi na uzoefu ambao Profesa Assad anao utamwezesha kutekeleza vema majukumu ya nafasi hiyo muhimu sana katika utawala bora wa nchi yetu.
Viewing all 104768 articles
Browse latest View live




Latest Images