Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104687 articles
Browse latest View live

Zari The Lady Boss Ajibu Kuhusu Habari ya Kuvuja Kwa Mkanda Wake wa Ngono Mitandaoni

$
0
0
Mfanya biashara kutokea Uganda,Zariah Tlale aka Zari The Boss ameingia kwenye scandal nzito katika kipindi hiki  baada ya kile kinachosadikiwa ni mkanda wake wa  ngono kuvuja kwenye mitandao.
kupitia twitter mfanyabiashara huyo amejikuta katika wakati mgumu kuhusiana na scandal hiyo huku mashabiki wakitaka kujua kiunaga ubaga,na baadae kuamua kuandika ujumbe mrefu kwenye akaunti yake ya instagram.

Dearest friends, my fans all over the world, relatives and well wishers, as you may be or may not be aware, the print media in Uganda is awash with stories infringing on my fundamental inalienable human rights by attacking my modesty both as a woman and a mother to the utter prejudice of my private life and family. The clear motive of such publication is undoubtedly to deter and/or downplay my tireless efforts in my preparations for The Zari All White Party slated for 18/12/14 which to a large extent has rubbed some of my detractors the wrong way. 
I have no doubt in my mind that the pictures that appeared in today’s Red Pepper issue were leaked by someone  for their own selfish motives. Be that as it may, I would like to affirm that what goes on in my private life is absolutely my business that has no reason whatsoever to find it’s way in the public realm. Privacy to/for/of a person is not a right granted by anyone, but it’s inalienable. 
I am therefore steadfast in my resolve to hold the Zari All White Party for all my fans and friends in Uganda. And whilst I explore the option of seeking with a view of taking legal action against the  perpetrators/detractors and/or publishers, I want to assure all my family, fans and friends again to disregard such hurtful reports aimed at scoring cheap social points. 
Lastly, I call upon one and all to attend the All White Party as there’ll be incredible performances from various artists including Diamond Platinumz, whose attendance is confirmed. I’d love to see you there, I’ll be there to welcome you all and God willing, we shall have a great time like we always do. 
Bless you all, Zari.

Ripoti: Tanzania kinara wa utumwa Africa Mashariki

$
0
0
Ripoti mpya ya kimataifa kuhusu hali ya utumwa duniani imeitajaTanzania kuongoza Afrika Mashariki kwa kuwa na zaidi ya watu 350,000 wanaotumikishwa maeneo mbalimbali nchini.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba, jana alikiri kuwapo kwa tatizo hilo akisema: “Ni kweli kuwa wafanyakazi wa ndani wanatumikishwa hapa nchini ikilinganishwa na nchi nyingine.”

Ripoti hiyo ijulikanayo kama ‘The Global Slavery Index 2014’, iliyotolewa nchini Australia Novemba mwaka huu, inaonyesha kuwa Tanzania inashika nafasi ya 14 barani Afrika na kuwa ya 33 duniani.

Imeitaja Uganda kuwa ndiyo inayoshika nafasi ya pili kwa kuwa na watumwa 135,000, ikifuatiwa na Rwanda (83,600), Burundi (72,300) huku Kenya ikiwa na watumwa 64,900.

Utafiti huo uliofanyika katika nchi 167 duniani, unatafsiri utumwa kuwa ni hali ya mtu kumhifadhi mtu mwingine na kumnyima uhuru binafsi kwa nia ya kumnyonya kwa njia ya madaraka, faida au kumsafirisha.

 “Mataifa mbalimbali yanatumia maneno tofauti kuuelezea utumwa mambo leo, ikiwa ni pamoja na kusafirisha binadamu, utumikishwaji, ndoa za lazima, kuuzwa kwa watoto. Maovu yote yanazungumzia jambo moja,” inasema ripoti hiyo.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa hivi sasa kuna watumwa milioni 35.8 duniani kote, kati yao milioni 14 wapo India, milioni 3 wapo China na milioni 2 wanapatikana Pakistan. Akizungumzia ripoti hiyo Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba alisema hali imefika ilipo sasa kutokana na kukosekana kwa sheria kali na vyama vyenye nguvu vya kutetea haki za wafanyakazi hao.

Waziri Simba alisema kwa sasa ni jambo la kawaida kumsikia mtu akijisifu kuwa amekaa na mfanyakazi kwa miaka mitatu bila kwenda likizo.

“Mtu anasema ‘nimekaa naye miaka mitatu msichana huyu ni mzuri’ kwa hiyo nini? Anakaa kwako kwa sababu umeshindwa hela ya kumlipa akapange kama wafanyakazi wengine,” alisema.

Aliongeza: “Msichana anakuwa wa kwanza kuamka asubuhi na wa mwisho kulala usiku, akupikie mchana, usiku na akufungulie mlango unaporudi. Ndiyo maana wasichana wanawadhuru watoto wanaokaa nao.”

Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka na naibu wake, Dk Makongoro Mahanga hawakuweza kupatikana kuzungumzia ripoti hiyo baada ya simu zao kuita bila kupokelewa.

Kuhusu Afrika, ripoti inaonyesha kuwa Nigeria ndiyo inayoongoza kwa kuwa na watumwa 834,200, ikifuatiwa na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) (7,620, 900), Sudan (429, 000), Misri (393, 800) na Tanzania (350,000).

Kumvua Mwanamke na Kumwacha Sio Ustaarabu

$
0
0

We mwanaume mwenzangu jaribu kufikiri Mara mbili kabla ya kufanya jambo hili.

Umetumia zaidi ya mwaka mmoja kuomba mahusiano kwa mwanamke(kutongoza). Alafu baada ya kumvua nguo tu basi unakata mawasiliano apoapo hauoni ni ukatili WA kijinsia au utapeli.

Kinachonishangaza zaidi watu wenye tabia hii wanabidii kwenye kutongoza kuliko wale wanatafuta mke WA kuoa.

Ingawa inawezekana ikawa si jambo zito kwa mwanaume lakini kwa mwanamke ni majeraha makubwa moyon unayomwachia.

Unamsababishia maswali mengi kichwani kwa mfano:-
1. Labda sijui mapenzi
2. Ameniona changudoa
3.shepu yangu mbaya.

Lakini kubwa zaidi ni kwamba unasababisha ugumu kwa mwanaume atakayejitokeza kwa malengo ya kutaka kumuoa. Hataweza kutofautisha muoaji na mfunuaji.

Interview inakua ndefu na na ya mda mrefu kwa mwanaume WA kweli atakapotokea, mpaka wakati mwingine mwanaume anashindwa kwa vigezo avyopewa.

Kwakwel kama hauna malengo na mtu usimpitie na kumwacha, mnatupa shida sisi waoaji.

Karibu kwa mchango wakuu.

Diamond na Davido ndani ya BIFU Zito…..Kisa na mkasa ni Tanzania kushinda Big Brother Africa

$
0
0

Usiku wa December 07 Tanzania imechukua tena headline kwenye vyombo mbalimbali vya habari na hii ni baada ya Mtazania Idris kufanikiwa kushinda kwenye shindano la Big Brother Hot Shot 2014.

Mara baada ya Mshiriki wa Tanzania Katika Shindano la Big Brother Africa 2014 Idris Sultan kutangazwa mshindi, watanzania wengi walionekana kufurahishwa sana na Ushindi wake huku wengine wakimpongeza kupitia kurasa zao za Twitter …

Muda mfupi baadae Msanii Kutoka Nchini Nigeria Davido alionekana waziwazi kukerwa na Ushindi huu wa Mtanzania Idris na kuamua kutweet “N They Cheat Again lol”.

Tweet hii ilimfanya Msanii huyo wa Nigeria kushambuliwa kwa Maneno na watanzania wengi katika kurasa zao za twitter.

Usiku huo huo baada ya ushindi wa Idris,Diamond   naye  aliibuka  kidedea  kwenye  tuzo  za The Future Awards Africa Prize in Entertainment 2014  zilizofanyika  Lagos  Nigeria usiku wa kuamkia leo  na  kuwatupilia mbali  wakali wengine wakiwemo Panshack au Ice Prince wa Nigeria na Michael Kwesi kutoka nchini Ghana.

Baada  ya  Ushindi  huo, Diamond  aliamua  kumjibu  Davido  kwa  kuandika  “Thanks God, we have cheated another one on the future Awards Africa in Lagos Nigeria…#Samenight Thank You Allah

Ugomvi  huo  wa  maneno  haukuishia  hapo  tu, Jokate  Mwegelo  ambaye  ni  X-Girlfiriend  wa  Diamond  naye  alitoa  Onyo  kali  kwa  Davido  akimtaka  aombe  radhi  kwa  kauli  yake:

I think it’s wise that you give an apology. You don’t need Tanzanians hating you…” Aliandika Jokate



Jinsi Idris Sultan Toka Tanzania Alivyoibuka Mshindi wa Shilingi Milioni 514 za Big Brother Africa

$
0
0
Idris Sultan ndio mshindi wa Big Brother Africa Hotshots. Baada ya kutupa karata yake kwa takriban miezi miwili ndani ya jumba hilo lililopo nchini Afrika Kusini, Afrika imemchagua kuwa mshindi wa msimu huu wa Big Brother na hivyo kushinda kitita cha $300,000 ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 514 za Tanzania.

Idris ambaye ni mpiga picha katika kampuni ya I-View Studios, anarudi nyumbani kama milionea mwenye uwezo wa kuanzisha kampuni yake mwenyewe. Idris alionesha mapema kuwa mshindani mwenye nguvu na anayependwa zaidi katika shindano hilo na wengi walitabiri kuwa mshindi wa mwaka huu. 

Maisha yake katika jumba hilo yalitawaliwa na ‘uplayboy’ kama alivyosema siku anaingia kwenye jumba hilo. Akiwa mjengoni, Idris alikuwa na uhusiano na wasichana wawili, Ellah wa Uganda na Goetse wa Botswana ambao wote waliondolewa pamoja wiki iliyopita. Pia alikuwa na urafiki wa karibu na Samantha kiasi cha kupewa jina la utani, Samdris.

Hiyo ilimfanya Idris kuonekana kama mzee wa totoz na hivyo kujipatia mashabiki wengi hususan wa kike barani Afrika. 

Mastaa wa Afrika Mashariki na watu wengine waliungana kumpigia debe Mtanzania huyo ili ashinde shindano hilo baada ya kuwa mshiriki pekee kutoka Afrika Mashariki aliyesalia kwenye shindano hilo lenye mashabiki wengi.

Ushindi huo wa Idris, unaingozea Tanzania heshima kubwa katika tasnia ya burudani barani Afrika baada ya wiki iliyopita Diamond Platnumz kushinda tuzo tatu za Channel O. 

Hii ni mara ya pili ushindi wa Big Brother Afrika unarejea Tanzania. November 2011, Richard Dyle Bezuidenhout aliibuka mshindi wa Big Brother Africa 2 baada ya kukaa mjengoni kwa siku 98 mfululizo. Richard alishinda US$100,000

Download wimbo mpya kutoka kwa Lord Eyes ambapo amemshirikisha Mwasiti.

$
0
0
Download wimbo mpya kutoka kwa Lord Eyes ambapo amemshirikisha Mwasiti...Wimbo unaitwa Kwanini

Kaka Mtu Amnasa dada yake akiliwa URODA na Njemba chumbani Kwake

$
0
0
Kaka mtu aliyejitambulisha kwa jina moja la Nicholaus  amesimamia fumanizi la dada’ke ambaye ni mwanafunzi wa sekondari moja jijini Dar  ambapo alimfumania chumbani na njemba mmoja sharobaro aliyetajwa kwa jina la Abuu Ally, mkazi wa Mbagala-Charambe, Dar.

Akisimulia  mkasa  wa  fumanizi  hilo, Nicholaus alisema amekuwa akiumizwa na taarifa kwamba kila ikifika saa 2: 00 usiku kuna mwanaume amekuwa akijipenyeza na kuingia chumbani kulala na mdogo wake wa kike kisha kuchomoka alfajiri. Alidai kuwa kuwa mara nyingi vitendo hivyo hufanyika wikiendi .

Ili  kumnasa  mwanaume  huyo, Nicholaus aliandaa  vijana  kadhaa  wa  kazi  kwa  ajili  ya  fumanizi  na  kisha akamtaarifu Mjumbe wa Mtaa wa Maji-Matitu, Hawa Ally kuwa wana kazi eneo lake hivyo akatoa ushirikiano uliofanikisha kumnasa Abuu.

Baada ya kukiri kosa mbele ya kiongozi huyo wa serikali za mtaa, pande zote zilikubali kusuluhishwa ambapo Abuu alikubali kulipa faini ya shilingi laki moja na kupewa muda wa siku moja kutekeleza adhabu hiyo.

Amanda: Starehe Kwanza, Mungu Baadaye

$
0
0
Staa mwenye shepu ya aina yake ndani ya Bongo Movies, Tamrina Poshi ‘Amanda’ ameibuka na kusema kuwa siku ikifika atarejea kwa Mwenyezi Mungu lakini kwa sasa bado anakula ujana.

Akiongea na Gazeti la Ijumaa Wikienda, Amanda alisema kwa sasa umri wake unamruhusu kula ujana kwa mambo ya starehe kama kuvaa mavazi ya kuacha mwili wake nusu utupu kwa sababu muda wa kurejea kwa Mungu bado haujafika.

Jamani niacheni na mavazi yangu, ukifika muda nitarejea naona mnanisema sana, kama wewe Mungu amekujalia kusali, mshukuru mimi muda huo bado haujafika,” alisema Amanda ambaye wakati huo alikuwa ametupia kivazi kilichomuacha wazi sehemu kubwa ya mwili wake hasa tumboni.

Lemutuz Awapa Darasa Watanzania Waishio Nje ya Nchi Wanao Ogopa Kurudi Kuishi Tanzania

$
0
0
Nanukuu Kama Alivyoandikia Mwenyewe Kwenye Page ya yake ya Instagram:

'Good Morning Instagram Nation mara kwa mara huwa ninagusia mafanikio yangu madogo madogo ya Miaka 3 toka nirudi bongo nia na madhumuni yangu huwa sio bragging rights hapana......huwa ninawalenga sana ndugu zangu wengi niliowaacha Diaspora ambao wanaogopa kabisa kurudi hapa nyumbani bongo kwa kuaminishwa sana na FEAR za Super gademu mburulazzz kwamba bongo hapafai...I mean hata mimi at onetime nilikuwa na hizo FEAR ZAKUAMINISHWA NA MBURULAZZZ kwamba Bongo ni noma......please my people kama vipi unaona mbelezz hakuna mpango rudi tu ila lazima ujipange wazungu wametengeneza System yao kwa kuhakikisha kwamba mgeni hasa African ni vigumu sana kuondoka na pesa kwa sababu ya KODI so kati ya wabongo 100 ni mmoja tu anaweza kurudi na pesa so wengone 99 the best U can do ni kurudi na AKILI TOFAUTI NA ULIYOKUWA NAYO HAPA BONGO KABLA YA KWENDA MAJUU....rudi na akili people ndio utaweza hapa bongo kwa sababu utakuwa na MAAKILI MENGI SANA UTAKUWA KAMA MIMI LE MBURULAZZZ WANAPIGA PIGA KELELE.WEWE UNAPASUA KATI KATI YA UJINGA WAO U KNOW UNAVUTA PESA ILA LAZIMA URUDI NA MAAKILI MENGI SANA.....najua maisha ni popote ila ni super zaidi ukila bataz bongo na hawa wabebezz wa kibongo wasikie tu U know ni balahaa hahahah..
kabla sijaenda Majuu sikuwa na MAAKILI KAMA NILIYONAYO SASA YA KUWEZA KUANZISHA LE.TAMKOZ NA kuvuta pesa ya wadhamini huku nimelisimamisha TAIFA ZIMA kusubiri umbeya tu....inaitwa MAAKILI MENGI...JAMANI MCHANA MWEMA SANA WANDUGU!' Says Lemutuz

Hemedy: Nimebadilisha namba ya simu zaidi ya mara 50, mademu wananisumbua

$
0
0
Msanii wa filamu na muimbaji wa R&B, Hemedy PHD amesema usumbufu anaoupata kwenye simu yake ni mkubwa kiasi ambacho humfanya abadilishe namba za simu kila mara.

Hemedy ameiambia Bongo5 kuwa anashindwa kutambua watu hao wanaipataje namba yake na kuanza kumsumbua.

“Nasumbuliwa sana mwanangu, dah mpaka noma, sijui hata nisemeje,” anasema Hemedy. “Meseji 600 kwa siku ni kitu cha kawaida. Sielewi tatizo ni nini, ukiona nalalamika hivi ujue naumia. Mpaka nikipigiwa huwa nafikiria kupokea simu. Mama yangu anapata usumbufu sana kwenye kusave namba yangu. Namba hii ni ya hamsini na moja tangu nianze sanaa 2008! Wanakuwa watu tofauti tofauti, lakini mademu ndo wanakuwa wengi.”

Katika hatua nyingine Hemedy amesema kuwa wazazi wake pamoja na ndugu zao wamemshauri yeye na mpenzi wake kukaa kwanza pamoja ili kuendelea kusomana tabia kabla ya kufunga ndoa.

“Ndoa bado ipo, tena naweza sema ukaribu umeongezeka mara dufu. Lakini lakini kilichotokea ni suala la utayari kwa sababu kila mmoja anatakiwa awe tayari. Sasa watu wetu wa karibu pamoja na wazazi wametuambia ‘hebu jaribuni kufanya hivi, vuteni muda kidogo zaidi halafu tuone itakuwaje’ Pia hata mwanamke mwenyewe anahitaji kitu kidogo cha kutuhalalisha ila awe ni mke wangu.”

Busara inahitajika kutafsiri tweet ya Davido baada ya ushindi wa Idris kwenye Big Brother

$
0
0
Katika siku ambayo Davido aliwakera watumiaji wa mitandao ya kijamii nchini Tanzania ni Jumapili hii. Baada tu ya Idris Sultan kutangazwa mshindi wa Big Brother Africa, Davido alitweet kitu ambacho hakujua kingewakera Watanzania wengi walioiona. “N they cheat again lol,” aliandika Davido kwa kuongeza na ‘Emoji’ ya kipaka kilichofunika macho yake.

Dakika chache tu baada ya muimbaji huyo wa Nigeria kuandika hivyo, mastaa mbalimbali wa Tanzania na watumiaji wengine wa Twitter walianza kumshambulia kwa matusi staa huyo. Wengi waliscreeshot tweet hiyo na kuipost kwenye Instagram na kumchana vikali. Wapo walimuita shoga, wengine wamemuita snitch, wengine wanamuita hater na wengine wamefikia hatua ya kumwambia mpenzi wake anacheat na Mtanzania!

Tweet hiyo imewakasirisha wabongo kiasi ambacho Nay wa Mitego ameahidi kumtwanga DJ yeyote atakayemsikia akicheza wimbo wake.

Lakini tumejaribu kuitafsiri maana halisi ya alichokiandika staa huyo au tunakuza mambo kutokana na hasira ya kuwa na maana yenye upande mmoja? Kunaweza kukawa na tafsiri nyingi ya hicho alichokiandika. Kwakuwa hajapenda kufafanua, bado alichomaanisha anakijua yeye mwenyewe na Mungu. Lakini tafsiri maarufu iliyowafanya watanzania wengi wamtukane, ni kuwa Tanzania imedanganya kupata ushindi wa Big Brother.

Hebu tuangalie mantiki ya tafsiri hii. Big Brother ni shindano linaloandaliwa na Multi Choice na Endemol, hushirikisha kampuni maalum ambalo husimamia shughuli za upigaji kura na kuwapa matokeo waandaji hao. Hakuna uwezekano wowote Tanzania imeweza kudanganya hadi kumfanya Idris awe mshindi.

Na pia, hata kama Tanzania nzima ingempigia kura Idris (kitu ambacho hakiwezekani sababu BBA ni shindano linaloangaliwa zaidi na watu wenye DSTV nyumbani kwao ambao hatudhani kama wanafikia asilimia 5 nchi nzima, ama wale ambao ni watumiaji wa mitandao ya kijamii kujua kinachoendelea hata kama wasipoangalia TV), kwa mfumo wa shindano hilo, Tanzania ina kura moja tu.

Hivyo ushindi wa Idris umepatikana kwa mkusanyiko wa kura moja moja za nchi mbalimbali barani Afrika, kumzidi Tayo wa Nigeria.

Tunaamini hili Davido analifahamu pia, hivyo tweet yake ilikuwa ikiwaendea moja kwa moja waandaaji wa shindano hilo na sio Watanzania kama wengi walivyoitafsiri. Na katika mashindano kama haya, tweet kama ya Davido ni za kawaida kwakuwa zimekaa kishabiki zaidi.

Kama walivyopenda wanaijeria wengine, Davido pia alitamani Tayo ashinde na kwa kwakuwa walikuwa na matarajio hayo bila kugundua nguvu ya Idris kwenye shindano hilo, kilikuwa ni kitu cha kawaida kuandika hivyo. Davido na wanaijeria wengine, wameshindwa kujua kuwa Idris alikuwa na kula za uhakika kutoka Tanzania, Uganda, Kenya, Namibia, Botswana Afrika Kusini na kwingine. Hawakutaka kukubali kuwa Idris alikuwa na nguvu zaidi kumzidi Tayo.

Wanaijeria wameumizwa kwakuwa mara yao ya mwisho kuchukua taji hilo ni mwaka 2011 kwenye msimu wa sita ambapo Karen Igho alishinda. Waliichukulia Hotshots kama nafasi pekee ya kurudisha heshima ya nchi yao wanayoamini kuwa ina nguvu kuliko mataifa mengine ya Afrika.

Aliposema ‘they cheat again’ ni wazi alimaanisha Biggie amelitoa taji hilo kwa nchi nyingine zaidi ya Nigeria kwa mwaka mwingine, baada ya mwaka jana kwenye Namibia kwa Dillish na mwaka 2012 kwenda kwa Keagan Petersen wa Afrika Kusini. Hajasema Tanzania imedanganya! Kwahiyo Davido anaonewa kwa kubebeshwa mzigo kutokana na tweet yake ya kishabiki.

Tweet ya Davido haina uhusiano wowote na ushindi wa Diamond kwenye tuzo za Channel O

Tafsiri nyingine ya tweet ya Davido ni kuwa Tanzania imedanganya tena baada ya Diamond hivi karibuni kushinda tuzo mbili za Channel O. Hii ni tafsiri isiyo sahihi kabisa na hapa Watanzania tunamuonea Davido waziwazi. Hivi mnasahau kuwa ni Davido ndiye alimpongeza kwa moyo mweupe kabisa Diamond kwenye Instagram? “TANZANIA STAND UP! HE DID IT! @diamondplatnumz.” Tumesahau mapema hivi wakati ni sisi wenyewe ndio tuliompongeza kwa ujasiri wake huo? Leo hii tunarudi kwenye post hiyo hiyo na kuanza kumtukana?

Kuna wasanii wengi tu maarufu hapa Tanzania hadi leo wameshindwa kumpongeza Diamond kutokana na chuki zao binafsi lakini Davido aliyekuwa akishindana naye kwenye kipengele kimoja alimpongeza Diamond. Na pamoja na kukosa tuzo zote tano, alikuwa na kifua kipana cha kuweza hata kuandika:
Always will be grateful!!! More to come.

Kwanini tunataka kujiaminisha kuwa anamchukia Diamond? Amchukue kwa lipi wakati Davido alikuwa ametajwa kuwania tuzo tano na ni moja tu ndiyo walikuwa wametajwa kuwania pamoja na Diamond? Pamoja na jitihada zake binafsi, tunasahau kuwa Davido ana mchango wake muhimu kwa mafanikio aliyonayo sasa Diamond? Kwanini hatuna shukrani na tayari tunaanza kutukana wakunga? Leo hii mtu huyu anageuka adui yetu kwa tweet ambayo tumeielewa vibaya?

Kosa lake pengine ni kuendelea kuwa na ego na kutotaka kutoa ufafanuzi wa kile alichomaanisha lakini matusi haya tunayoyaelekeza kwake yana hasara nyingi kuliko faida.

Kama tukifuata kauli ya Nay wa Mitego kuwa redio zisipige nyimbo zake, hiyo si njia ya kupunguza ukoloni wa Naija uliotawala vituo vyetu vya redio sababu hakuuanzisha yeye. Bado redio zitaendelea kupiga nyimbo za akina P-Square na wengine ambao hata kesho wakija Leaders, lazima pajae.

Na je tunavyoendelea kutengeneza uadui huu wa Nigeria na Tanzania, vipi na wao wakiamua hizo nyimbo za wasanii wawili watatu wanazopiga kwao wazichinjie baharini, hasara itarudi kwa nani?
Kinachosikitisha zaidi ni Diamond kuwa mmoja wa watu walioitafsiri tweet yake vibaya. Labda kama kuna vitu vingine vya chini chini vinavyoendelea kati yao ambavyo sisi hatuvijui, lakini tayari uhusiano wa wawili hao unaweza ukawa umeshaingia dosari.

Thanks God, we have cheated another one on The Future Awards Africa in Lagos Nigeria… #SameDay #SameNight Thank you Allah!,” ameandika Diamond baada ya kushinda tuzo za TFA zilizotolewa jana huko Lagos.

Tunahitaji busara sana kujibu kauli za aina hii. Tunaweza tukaanza kubomoa tunachokijenga bila kujua. 
~Bongo5

Kutokujiamini ni Janga Kubwa la Wanaume wa Kibongo Mbele ya Wanawake

$
0
0
Bila hata kwenda mbali angalia Hizi Statement kadhaa za Wanaume Wasiojiamini:

1. Usimtambulishe Mkeo Utagongewa

2. Usioe mwanamke mzuri

3. Mwanamke mzuri hatulii kwenye ndoa

4. Usioe mwanamke aliekuzidi kipato

5. Usioe mchaga/muhaya

6. Usioe mwanamke aliekuzidi elimu

7. Kama wewe mfupi usitafute mwanamke mrefu

HIVI KWA NINI HAMJIAMINI?

Ukiangalia kwa wenzetu hii kitu ni tofauti sana ila hapa yaani ukidate mtu ambae hajiamini ni janga statement kama hizi hazimkauki mdomoni:

1. Sikuamini kabisa
2. I cant handle this relationship(Dude you cant handle her personality she is too smart)
3. You gat attitude(Noop ana vision ya hali ya juu wewe sio saizi yake.

NA WANAKAGUA SIMU HAO KAMA WAPELELEZI WA MAKOSA YA JINAI

Kujiamini ni credit kubwa sana kwa mwanaume wa kisasa
Hata ukiwa na ela kama hujiamini utaumwa ulcers.

~By  Masai dada

Chriss Brown Amuomba Msamaha Karruache Baada ya Kumzalilisha Mitandaoni na Kusema anashiriki Mapenzi ya Watu Watatu

$
0
0
Weekend iliyopita imeisha kwa habari za kuisha kwa penzi la Chris Brown na Karrueche, halafu story kuibwa ya pili ikawa yale madongo ambayo kila mmoja akimtuhumu mwenzake kwamba  ndiye sababu ya mapenzi yao kuisha.
Imekuwa ni kama mchezo wa kuigiza kwa wawili hao kuachana na kurudiana, lakini kupitia ukurasa wake wa Instagram Chris ameandika ujumbe wa kumuomba radhi Karrueche huku akisema hajali watu wanamchukuliaje
Ujumbe huo unasomeka hivi; 

Being young and dumb is one of my strong suits and emotional at best. I love hard and react impulsively when I’m hurt at times. I don’t think social media is a place to air out or hash out personal problems and a nigga feel hella WACK for doing it. So I AM APOLOGIZING I live in a glass house and the same sh*t that makes me great also is my curse. Everybody know I love that girl. I don’t care how my image my look to the public because I’m still gonna be the best at what I do. I just want baby girl to know I apologize!"

Hii Hapa chini ni Message aliyoandika Chriss Brown kwenye Mitandao akimtuhumu Karuache kutoka na Drake na Pia kushiriki Mapenzi ya Watu watatu



Alichokisema msichana aliyemtesa mtoto Uganda leo na maamuzi yaliyotolewa na Mahakama

$
0
0
Unamkumbuka yule mfanyakazi wa ndani aliyemtesa mtoto nchini Uganda na kuteka hisia za watu wengi duniani? leo kesi yake imeweza kusomwa kwa mara nyingine.
Mfanyakazi huyo Jolly Tumuhirwe mwenye miaka 22 aliiambia mahakama nchini humo leo kuwa anajua kile alichokifanya na anakiri kosa hivyo anaomba watu wamsamehe kwa kuwa alifanya makosa.
Mfanyakazi huyo wa nyumbani aliyenaswa kwenye kanda ya video akimpiga mtoto wa bosi wake ajulikanaye kwa jina la Arnella mwenye umri wa miezi 18 pia alikua akimkanyaga mtoto huyo bila huruma.

Licha ya taarifa ya polisi kusema Jolly atashitakiwa kwa kosa la jaribio la mauaji, kiongozi wa mashitaka alimshitaki kwa kosa la kumtesa mtoto mdogo.
Msichana huyo alikiri makosa yake na kuomba msamaha na Hakuna wakili yeyote aliyemwakilisha Jolly mahakamani hapo licha ya mmoja wa mawakili mashuhuri kusema angemwakilisha Jolly bila malipo ypyote.
Kesi hiyo imeahirishwa tena hadi keshokutwa wakati hakimu akitarajiwa kutoa hukumu dhidi yake.
Binti huyo huenda akafungwa jela miaka 15 au kutozwa faini ya dola za kimarekani 800 au adhabu zote mbili.

LULU: Bata la Watu Wa Bukoba Ni Noumer…Naendelea Kuoga Hela

$
0
0




Mwigizaji wa filamu,mrembo na mwenye mvuto wa kufanya wengi wapagawe, Elizabeth Michael aka Lulu ambae kwasasa yupo Mjini Bukoba kwa mapumziko mafupi. Akiwa katika viwanja vya kula bata mjini hapo Lulu hakusita kuwasifia watu wa kabira la Wahaya kwa njinsi alivyo furahia GOOD TIME alilopewa na kumfanya afunguke mwenyewe kwenye mitandao ya kijamii

 “Wahaya noma......
Hili Bata la Watu wa Bukoba ni Noumer...! likizo isiishe jamani”

Haikuishiahapo, alitupia picha nyingi mtandaoni akiwa "SAMUWEA" kama unavyoziona hapo juu. 

Zamaradi Mketema Atoa ya Moyoni Kuhusu Bongo Movies 'Kwanini Mmeridhika Hivi' Atamani Atokee Kanumba Mwingine

$
0
0
Leo mwanadada Zamaradi mketema ameamua kusema haya kuhusu filamu zetu nchini. Kama wewe ni mdau wa bongo movies tafadhali tusaidie kutoa maoni yako juu ya maswali haya ambayo zamaradi anauliza…

Hichi ndicho alichosema…

“…Natamani sana siku moja atokee mtu kwenye hii sekta atutambulishe hata kama sio kimataifa basi africa tu... R.I.P KANUMBA alianza kuonesha mwangaza na juhudi binafsi zilionekana na kila mtu aliona huenda angefika mbali.. lakini baada ya hapo sioni tena!!!!

Mbona hapa nyumbani ni wakubwa tu..? Nini kinawakwamisha..?  Kwanini wasanii wetu wa filamu ukubwa wao unaishia nyumbani tu....!!? Tatizo ni nini!!!????? kiukweli ni kama inakatisha tamaa na inaonekana kabisa watu wamerelax na ustar wa bongo wakati wana nafasi ya kufanya vizuri zaidi... wana bongo movie tukifika kwa wenzetu unaona kabisa tunapwaya kiasi gani.. Ujanja wetu ni nyumbani tu!!?? why!!!?? tukianza utanzania wa kufichaficha tutasifiana uongo lakini tukiwa wakweli na nafsi zetu tutaliona hilo na kuchukulia kama challenge..!!! ukweli ni kwamba hii tasnia inasikitisha!!! tena sana.. nahisi sasahivi tunafanya filamu kwa ajili ya nyumbani tu na tukiingia kwenye mabendi tukisharushwa tumeridhika!! kweli!! hapa ndio mnapotaka mfike!!? ukifika sehemu ukiwa juu nchini kwako tunachotegemea ni wewe kupasua mawimbi uende mbali zaidi nje ya mipaka!! lakini ukiamua kurelax hapo ulipo inamana unasubiri kushuka sababu kiukweli huwezi kukaa juu milele!!! kwanini mmeridhika hivi!!! kaka JB tatizo ni nini!!!??

Mi nakuangalia wewe kama mfano wa msanii mkubwa sana kwenye tasnia kwa sasa... mbona umerelax!!!??? umeridhika na ustar wa tanzania!!!? una kila kitu cha kukufikisha mbali... kinachohitajika ni juhudi binafsi tu ili kesho na sisi tufike mahala pazuri!! hebu tuongee wapenzi.. mnahisi huku kwenye bongo movie TATIZO LIKO WAPIII…!!???

JB ajibu 'post' iliyowekwa na Zamaradi kuhusu filamu za kibongo - "Tatizo liko wapi" ?

$
0
0
Baada ya mwanadada mdau wa filamu nchini, Zamaradi mketema kufunguka yake juu ya filamu za bongo – bongomovies, hatimaye mwigizaji mkongwe nchini Jacob Steven - JB ameamua kuandika haya yafuatayo hapo chini kuelezea baadhi ya mambo anayohoji Zamaradi kama ifuatavyo.

 “Kwako Zamaradi na wengine wote.

 Kwanza napenda niwashukuru wote kwa jinsi mnavyotuwazia mema. Naomba nichukue nafasi hii kuwapongeza waigizaji wote wa Tz na waandaaji wa filamuU kwa kuthubutu kutengeneza filamu hizi katiks mazingira magumu. Najua watanzania wengi wangependa kuona tukipeperusha bendera nje,lakini naomba muwape wasanii muda.

Tasnia hii ni changa na ina changamoto ambazo zinakatisha tamaa. Hebu tujiulize kwa nini wasomi wengi waliosomea filamuu UDSM na BAGAMOYO hawafanyi filamu hizi? Wasambazaji wengi wakubwa mamu,wananchi na hata hans pop walijaribu wakakimbia, kuna producer mkubwa hapa nchini JOHN RIBER ambaye ametengeneza filamuu kama NERIA na YELLOW CARD lakini naye ukimwambia njoo kwenye hizi filamu atakupa jibu.

Nakubali tuna makosa mengi kama ubora wa filamu zetu na stori lakini nataka niwaambie mazingira ya kufanya filamu bongo yanakatisha tamaa wizi wa kazi zetu umezidi na wasambazaji wengi wamekimbia. Binafsi najipanga kuwa mtayarishaji zaidi kuliko mwigizaji kwa sasa kupitia JERUSALEM FILMS na ndio maana filamu nyingi natoa nafasi kwa vijana ambao kama mabadiliko ya sera ya filamu yatafanywa watatuwakilisha nje.

Kiswahili kisichukuliwe poa kwani kina nafasi kibwa sana. Tukumbuke SHARUK KHAN ni ‘actor’ tajiri2 dunian lakini filamu zake ni za kihindi. Hebu sote tusaidiane kupambana na changamoto hizi na tuanze na EAST AFRICA kwanza huku tukiboresha, wasomi wa filamu msikimbie njooni tuanze wote na tuwape moyo wasanii wetu waliojaribu kusimamisha tasnia hii kwa vimtaji toka mifukoni mwao na vipaji walivyopewa na mungu bila msaada kutoka popote. Asanteni kwa kutuunga mkono kwemye filamu zetu.”

Alimaliza kwa kusema JB.

Nini maoni yako mdau?

Rais Kikwete aanza kufanyia kazi ripoti ya Akaunti ya Tegeta Escrow

$
0
0
RAIS Jakaya Kikwete ameanza kazi rasmi baada ya afya yake kuimarika kufuatia upasuaji wa tezi dume aliofanyiwa mwezi uliopita nchini Marekani, huku akianza kushughulikia mambo ambayo yamekuwa yanasubiri maamuzi yake.

Kazi ya kwanza ilikuwa kumwapisha Mkuu mpya wa Mkoa wa Arusha, Daudi Felix Ntibenda katika shughuli fupi iliyofanyika jana asubuhi Ikulu, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Rais atakuwa anafanya kazi za ofisini na kwa muda mchache. Muda na kasi yake ya kufanya kazi vitaongezeka kwa kadri afya yake inavyozidi kuimarika.

Pamoja na kuanza kazi kwa kumwapisha Ntibenda, Rais Kikwete pia amepokea na kuanza kufanyia kazi maazimio manane ya Bunge kuhusu sakata la uchotaji fedha katika akaunti ya Tegeta Escrow huku Watanzania wakihakikishiwa uamuzi utafanywa kwa kuzingatia misingi ya haki na uwazi.

Hayo yalithibitishwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, akisema Rais Kikwete ameagiza uchunguzi wa kina ufanyike kuhusu suala hilo kabla ya kupatiwa majibu hivi karibuni.

Balozi Sefue alitoa taarifa hiyo wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari waliotaka kufahamu ni hatua gani na lini zitachukuliwa baada ya Rais kupokea maazimio hayo juzi.

Kwa mujibu wa Sefue, maazimio hayo ni mazuri na yamempatia nafasi na fursa nzuri Rais Kikwete ya kuendeleza uchunguzi wa kina kuhusu suala hilo jambo ambalo tayari ameanza kulitekeleza na litapatiwa majibu hivi karibuni.

“Napenda ifahamike kuwa hili ni suala kubwa, lakini mfumo mzima uko wazi, kila mhimili una wajibu wake, sasa mihimili ya Mahakama na Bunge imemaliza kazi zao sasa ni Serikali Kuu, tupeni nafasi tuyafanyie kazi haya maazimio, nawahakikishia haki itatendeka,” alisisitiza Sefue. Alisema kamwe Serikali haiwezi kudharau Bunge.

Alisema maazimio yote yaliyofikiwa na chombo hicho, yamechukuliwa kwa uzito mkubwa na ndiyo maana kila azimio litapitiwa na kufanyiwa kazi baada ya uchunguzi kukamilika.

Aidha, Sefue alisema kwa sasa vyombo vinavyochunguza suala hilo ni pamoja na vilivyofanya uchunguzi awali ambavyo ni Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru).

“Si siri mpaka hapa tulipofikia vyombo hivi vimefanya kazi kubwa, tunafanya uchunguzi tena kwa ajili ya kujiridhisha na kwenda ndani zaidi ili kujua undani wa suala hili, ili hata hatua zikichukuliwa dhidi ya mhusika ziwe za haki na si kuonea,” alisema.

Chanzo: Habarileo

Tabia ya wadada/wanawake kubadilisha status kwa hitilafu ndogo za kwenye uhusiano

$
0
0
Leo naomba tujadiliane hili maana nimekua nikiliona sana,
Kwa ushahidi mkubwa nimeliona kwa rafiki zangu wengi sana na hata mimi limewahi kunitokea.

Mdada uliyenae uhusiano mkipishana kauli kidogo na ukawa kimya basi atadhani ndo keshapigwa chenga hapo ataanza kuhangaika na kubadilisha status kwenye social networks kama whatsapp, Facebook etc.

Kwa mfano mlipokua kwenye uhusiano hajawahi kuandika jambo la hivi ila leo mnakwazana jambo dogo utaona Whatsapp au Facebook ameandika: AM SINGLE AND HAPPY, I CAN MANAGE MY LIFE, NAMTEGEMEA MUNGU TU SIO MWANADAMU.

Tatizo linalonikwaza ni kwamba kitendo cha mtu kuandika haya ni kuonyesha watu wengine kua hana siri juu ya mambo yake, yaani likimkuta tu lazima aropoke kwa kuweka status ya ajabu.

Huu naona kama utoto sana watu tujifunze kua na adabu ya kutunza privacy zetu

Uchumba wa Feza Kessy na M-botswana wavunjika

$
0
0
Ule uchumba ulianza kwa kasi ya ajabu kati ya mtanzania aliyetuwakilisha big brother 2013 na mwenzake raia wa botswana kwishneyi.

Feza Kessy amekiri uchumba huo kuvunjika kwa sababu ameona jamaa siku hizi amebadilika hana tena mpango wa ndoa na yuko bize sana na mtoto wake wa miaka 8.

Pia amesema yeye ndio amemuacha aliandika kumuacha kwenye twitter na ndio ameamua hivyo.
Viewing all 104687 articles
Browse latest View live




Latest Images