Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

NILIMFUMA MKE WANGU AKINYATIA KUINGIA KWENYE CHUMBA CHA MDOGO WANGU WA KIUME AKIWA NUSU UCHI.

$
0
0
Kumbe ilikuwa ni tabia yake kwenda kwa mdogo wangu huyo wa


kiume ambaye ni mtoto wa shangazi yangu, na kula uroda wakati mimi sipo, nilipata tetesi hizo kutoka kwa housegirl wetu lakini sikuweza kuamini. siku hiyo nilirudi kimya kimya na kujifungia chumba kimoja ambacho kilikuwa hakitumiki, na wote hawakujua kama nilikuwa nipo.

Mara ilipofika ,majira ya saa nne hivi usiku, nilimuona mke wangu ananyata huku akiwa amevaa nguo za ajabu sana, alipita chumba cha house girl na kisha kuzama kwenye chumba cha ndugu yangu huyo wa kiume. nilitoa simu yangu niliyokuwa nayo na kumpiga picha kwa ushahidi zaidi, alipoingia tu na mimi nikaingia alishindwa kuamini na gafla alianza kuomba msamaha, nilimuuliza mke wangu kwani umefanya nini alishindwa kunijibu huku akiendelea kulia na kuomba msamha, nilitoka na kwenda chumbani kwangu kulala, yule mdogo wangu wa kiume alifungasha usiku ule ule na kuondoka na mke wangu hakuweza kulala, iliniuma sana sikuweza kuamini kwani nilimuamini sana mke wangu.Kesho yake sikuweza kuvumilia nilichukua uamuzi wa kumrudisha kwao , kwani ningeweza kumfanya kitu kibaya sana kama ningeendelea kumuona.

Source: New Paradise

ALI KIBA AMUONESHA MPENZI WAKE-DUU MKALI KWELI KWELI

$
0
0
Ally Kiba anaweza kuwa hasikiki sana kwenye redio miaka ya hivi karibuni na humsikii akilalamika. Huenda mrembo huyu anaweza kuwa sehemu muhimu katika moyo wake na hivyo kumfanya azisahau stress za mainstream (kwa sauti ya Godzilla aka Zizi).

Mkali huyo ambaye hivi karibuni alikuwa Nairobi kurekodi collabo yake na Redsan, amepost picha kwenye Instagram akiwa na mrembo ambaye hakuna shaka kuwa ni ubavu wake wa pili.

Mmmh.. yummy!!

CRAZY GK "EASTCOAST IMERUDI SASA TUTATUMIA ELIMU ZETU KUFANYA MZIKI WENYE LADHA"

$
0
0
Rapper, Gwamaka Kaihula aka King Crazy GK amewataka wapenzi wa East Coast Team kukaa mkao wa burudani baada ya members wa zamani wa kundi hilo AY na Mwana FA kumpa shavu kwenye kadhaa zake kadhaa.

Akizungumza na Bongo5 leo, King Crazy GK amesema huu ni wakati wao wa kufanya kazi kama zamani kwa kutoa burudani nzuri ya muziki uliokwenda shule.

“Kwanza tumeanza kuongeza nguvu kwenye East Coast Team yetu mpya,sasa tunataka kama wanaume wawili na msichana mmoja. Pia Eastcoast Team ya zamani tumerudi tena pamoja na kuanza kufanya kazi pamoja. Tumeshaingia studio na kunapika mambo kwahiyo hivi soon utawaona AY na FA na wengine ambao wlikuwa wanaunda Eastcoast Team ya zaman,” amesema GK.

“Tutatumia shule zetu kufanya muziki wenye ladha,” ameongeza. “Sasa hivi tunatakiwa kufanya kitu kipya katika performance,tunataka kufanya vitu ambavyo watu hawataamini kama ni sisi. Unajua tunatakiwa kuwa kwenye level nyingine,sasa tukiwa kwenye ileile ina maana hakuna sababu yakurudi pamoja tena. GK wa sasa anapiga kinanda,anapiga gitaa, kwahiyo hii ni level nyingine.”
Source:Bongo5.com

NATAKA KUMSALITI MUME WANGU...

$
0
0
Habari za humu jamani
mimi ni mwanamke nimeolewa miaka 5 imepita hatujafunga ndoa mume wangu ni mtu mzima kidogo ana miaka kama 49 na mm 26 bas nlishawahi kuomba ushauri meing humu na mkanisaidia

kwa sasa tunaishi kwa amani tabia yake ya ufataki sijui anaendeleza au kaacha cjui kwani simu zote ni pin ila ananipitia ofisini kwangu kila siku tunarudi wote!
tofauti iliyopo amekuwa mvivu tunaweza kukaa mwez au hata mwez na nusu bila kunigusa kabisa muda wote yupo bize na muv akirudi nyumbani

nmefikiria najihisi mpweke sana,nahisi nahitaji mtu wa kuniliwaza me ni mrembo sana kuna watu kama wa tatu wanantaka wawe na mimi kila mmoja ana sifa zake nafikiria kumkubalia mmoja wao angalau na mm nijihisi kama wanawake wengne.namis vitu vingi

naombeni ushauri wenu katika haya maamuzi

JUX AONGEA NA MILLARD AYO KUHUSU JACKIE CLIFF KUKAMTWA [VIDEO].

$
0
0
Boyfriend wake Jackie ambae ni msanii wa bongofleva Jux ameongea kwenye Exclusive interview na millardayo.com Jan 13 2014. Baadhi ya maswali aliyoyajibu kwenye video hapa chini ni pamoja na Wameongea lini mara ya mwisho? Jack anasemaje? Jack alikua wapi wakati wanaongea? yuko nchi gani? anarudi lini bongo? na mengine…




MBOWE KUMBURUTA ZITTO KABWE KORTINI

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe anapanga kumchukulia hatua za kisheria Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe kutokana na kile alichodai kuwa ni kuzusha tuhuma zenye lengo la kumchafua yeye binafsi na chama hicho. Tuhuma hizo ni zile zilizowekwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii na kuandikwa katika vyombo mbalimbali vya habari kuanzia Januari 6 mwaka huu, zikimnukuu Zitto akieleza kuwa Mbowe amewahi kuhongwa mamilioni ya fedha na Mbunge wa Musoma Vijijini (CCM), Nimrod Mkono.
Tuhuma dhidi ya Mbowe ziliibuka baada ya Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu kumtuhumu Zitto kuwa amehongwa magari mawili na Mkono.
Hata hivyo, Mkono katika taarifa yake alikanusha madai ya Zitto kuhusu kuwapa fedha Chadema, pia alitoa ufafanuzi kwamba hakuwahi kumhonga mbunge huyo magari kama ilivyodaiwa na Lissu bali alimuuzia gari moja na kumkodisha gari la pili.
Taarifa ya kusudio la Mbowe kumburuza Zitto mahakamani ilitolewa jana na Ofisa Mwandamizi wa Habari wa Chadema, Tumaini Makene, huku ikikanusha tuhuma zote zilizotolewa dhidi ya Mbowe.
“Mbowe ameshawasiliana na mawakili walifanyie kazi suala hili kwa ajili ya kuchukua hatua za kisheria. Mwenyekiti wa chama hajawahi kupokea msaada wa fedha hizo kutoka kwa waliotajwa kwa malengo yaliyosemwa,” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo ambayo hata hivyo haikumtaja Zitto moja kwa moja.
Jana gazeti hili lilimtafuta Zitto ili aweze kuzungumzia suala hilo lakini hakupatikana.
Msingi wa taarifa
Taarifa hiyo ilieleza kuwa tuhuma hizo zinasambazwa na watu wanaotaka kuhamisha mjadala wa makosa yanayowaandama ya utovu wa maadili na usaliti dhidi ya chama hicho.
Kauli hiyo ni dhahiri inamlenga Zitto, aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Arusha, Samson Mwigamba na aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu, Dk Kitila Mkumbo, kwani walivuliwa nyadhifa zao kutokana na kuandaa waraka wa Mkakati wa Mabadiliko 2013, uliolenga kufanya mapinduzi ya uongozi ndani ya Chadema.
Taarifa hiyo imesema tuhuma zinazoshughulikiwa ni zile zinazodai kwamba Mbowe alichukua Sh40 milioni mwaka 2005  kutoka kwa Mkono ili asifanye kampeni katika Jimbo la Musoma Vijijini.
Tuhuma nyingine ni kuwa 2008 Mkono alimpatia Mbowe Sh20 milioni kwa ajili ya uchaguzi mdogo wa Jimbo la Tarime, kwamba Mbowe alizitoa fedha hizo kwenye chama kama mkopo na akalipwa.
“Wanasema mwaka 2010, wakati wa uchaguzi mkuu eti Mkono alimpatia Mbowe Sh200 milioni kwa ajili ya kampeni za mgombea urais. Mwaka huo huo eti Mbowe alipokea Sh100 milioni kutoka kwa Rostam Aziz kwa ajili ya kampeni,” inaeleza taarifa hiyo.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa hakuna ukweli wowote katika tuhuma hizo, kwamba ni uzushi  uliopangiliwa kama moja ya mikakati ya watu wenye malengo ya kutaka kuilaghai jamii kwamba viongozi wa Chadema hawana tofauti na wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
“Wanataka kuwafanya Watanzania waamini kuwa viongozi wa Chadema hawana tofauti na wale wa CCM, waamini kuwa chama hiki kikuu cha upinzani kinachobeba matumaini ya Watanzania kionekane hakina tofauti na chama kilichoko madarakani,” inaeleza.
Inaeleza kuwa lengo la watu hao ni kutaka kuisaidia CCM na kugeuza mjadala husika dhidi yao.
“Waliozusha tuhuma hizo, ni vyema wakatunza heshima kidogo waliyobakiza katika jamii kutokana na kuelemewa na mzigo wa tuhuma za utovu wa maadili na usaliti dhidi ya Chadema,” inaeleza na kuongeza;
“Wajibu masuala ya msingi yanayowaandama kuhusu mikakati yao ya kuhujumu Chadema na viongozi wake, ambayo iwapo chama kisingebaini na kuchukua hatua za kinidhamu, ingesababisha kuua ndoto na matumaini ya Watanzania kufanya mabadiliko ya kimfumo na kiutawala, kwa kuiondoa CCM madarakani.”
Ufafanuzi wa Mkono
Januari 6 mwaka huu Mkono alitoa taarifa kuhusu tuhuma zilizorushwa dhidi yake na kufafanua kuwa magari mawili aina ya Toyota Land Cruiser na Nissan Patrol yanayodaiwa kuwa alimpa Zitto, moja alimuuzia na jingine  amemkodisha.
Kuhusu tuhuma kwamba anawahonga wapinzani wake wajitoe katika uchaguzi ili apite bila kupingwa alisema katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2000, 2005 na 2010 alipita bila kupingwa kutokana na uchapakazi wake wa kiwango kikubwa.
Mkono pia alijibu tuhuma zilizotolewa na Zitto kwamba Mbowe alipewa mamilioni ya fedha na Mkono kwa nyakati tofauti na kusema hajawahi kutoa fedha zozote kusaidia Chadema.
Mvutano kati ya Zitto na Chadema ulishika kasi baada ya Mbunge huyo kufungua kesi Mahakama Kuu kuomba mahakama hiyo kuizua Kamati Kuu (CC) ya Chadema kumjadili au kuchukua uamuzi wowote kuhusu uanachama wake hadi kesi yake ya msingi itakaposikilizwa na kutolewa uamuzi.
Zitto alishinda katika shauri hilo.
Chanzo - Mwananchi

MUHUDUMU WA MUCHUARI AMPIGA MKWARA MZITO WAZIRI

$
0
0
Mfanyakazi wa Kitengo cha Kuhifadhi Maiti cha Hospitali ya Rufaa ya Mbeya, Eugene Vurugu amemtisha Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Seif Rashid kuwa ikitokea amefariki dunia akiwa mkoani Mbeya, basi maiti yake italazwa kwenye sakafu hospitalini hapo.

Akizungumza kwenye mkutano wa wafanyakazi na naibu waziri huyo mwishoni mwa wiki iliyopita, Vurugu alisema kitengo hicho kimezidiwa na wingi wa maiti zinazopelekwa hospitalini hapo.

Alisema kitengo hicho cha kina majokofu sita tu na hulazimika kuhifadhi miili kwa zamu ili angalau maiti zisiharibike.

“Hata wewe Waziri ukifa leo, hakuna pa kukuweka.

Utawekwa sakafuni kusubiri maiti nyingine zipoe halafu utaingizwa ndani kwa kuingizwa maiti mbili kwenye eneo la mtu mmoja,’’ alisema Vurugu.

Aliiomba Serikali ifanye haraka kuboresha kitengo hicho ili kuepusha tatizo la kuoza kwa miili ya marehemu.

Kumekuwa na malalamiko kuhusu uchache wa majokofu ya kuhifadhia maiti katika hospitali hiyo na baadhi ya watumishi walisema hali kuwa mbaya zaidi inapotokea ajali ambayo inasababisha vifo vya watu wengi kwa wakati mmoja.

Vurugu alidokeza pia kuwapo kwa tatizo katika Idara ya Mifupa ya hospitali hiyo, akisema wakazi wengi wanaofika hapo kwa matatizo hayo anawaona wakiondoka kwenda Hospitali za Peramiho ya Ruvuma na Ikonda ya Makete huku wengine wakienda kwa waganga wa jadi kuunga mifupa yao.

Vurugu alizungumza baada ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa hospitali hiyo, Dk Humphrey Kiwelu kusoma taarifa ya utendaji mbele ya Naibu Waziri iliyoonyesha hali iko shwari baada ya kudai kuwa hospitali hiyo imepiga hatua kubwa kiutendaji na katika utoaji huduma kwa wagonjwa.

Dk Kiwelu alisema hospitali yake ina mafanikio makubwa yakiwamo ya kuwa na maabara ambayo imekubalika katika kiwango cha kimataifa na kwamba majibu yanayotoka kwenye maabara hiyo kwa sasa yanakubalika hata Uingereza na Marekani.

Hata hivyo, alisema hospitali hiyo haina mashine ya CT Scan licha ya kuiomba kutoka serikalini tangu 2003.

Akijibu hoja mbalimbali za wafanyakazi, Dk Rashid aliwataka viongozi kujipanga na kuchangua vipaumbele kutokana na mafanikio mazuri yanayoonekana hospitalini hapo.

Alisema kwa kuwa hospitali hiyo imeongeza mapato ya ndani kutoka Sh60 milioni hadi Sh300 milioni kwa mwezi, ipo haja ya kutumia fedha hizo kuiboresha kwa kuangalia vitendea kazi zaidi na masilahi ya watumishi wote.
-Mwananchi

ARSENAL YAREJEA KILELENI LIGI KUU ENGLAND

$
0
0
Ligi Kuu ya England mwaka huu ni shughuli pevu.
Jumamosi, Chelsea alikuwa kileleni, Jumapili, Manchester City na sasa ni Arsenal. Kiasi cha pointi mbili tu kinazitenganisha timu tatu za juu.

Kikosi cha Arsene Wenger kimerejea kileleni kufuatia ushindi wa mabao 2-1 ugenini usiku wa kuamkia leo dhidi ya Aston Villa. Jack Wilshere alifunga dakika ya 34 na Olivier Giroud akafunga la pili dakika ya 35 Arsenal ikaongoza 2-0 kabla ya Cristian Benteke kuifungia Villa la kufutia machozi dakika ya 76.Arsenal inarejea kileleni kwa pointi zake 48, ikiishusha Manchester City yenye pointi 47 katika nafasi ya pili, mbele ya Chelsea yenye pointi 46.

UTABIRI MPYA WA KUTISHA-MWISHO WA DUNIA WATAJWA

$
0
0
Stori: Mwandishi Wetu na Mitandao
WAKATI binadamu wakiendelea na mipango yao ya kuifanya dunia kuwa sehemu salama ya kuishi kimazingira, kiulinzi na usalama, utabiri mpya wa kutisha unaonesha kuwa mwaka 2032 ndiyo mwisho wa sayari hii ya tatu katika mfumo wa jua.

Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali katika mitandao ya internet, sayari iitwayo Nibiru, ambayo kisayansi inafahamika kama Planet X ipo njiani kuigonga dunia na hivyo kusababisha majanga mbalimbali kutokea.

ITAONEKANA ANGANI KAMA MWEZI
Kwa mujibu wa mitandao hiyo ya kisayansi, sayari hiyo ambayo inaisogelea dunia kwa kasi kubwa, itaonekana kubwa na angavu wakati wa usiku angani na kuwa katika umbo la mwezi na hivyo kufanya miezi ionekane miwili.

DALILI KWAMBA IPO JIRANI
Taarifa zaidi za kisayansi zinasema kuwa, kadiri sayari hiyo inavyozidi kusogea, dunia itaanza kutikisika na kusababisha matetemeko ya ardhi kuongezeka sehemu mbalimbali.

Mbali na dunia kutikisika na matetemeko, milipuko ya volcano nayo itatokea huku idadi kubwa ya milipuko hiyo mipya ikiongezeka, vimbunga vikubwa kama Tsunami vitaibuka na mwishowe dunia itapigwa na bomu la miamba midogo na vimondo kutokea angani.

DUNIA ITAKUMBWA NA GIZA NENE
Wakati volcano zote duniani zitakapoanza kulipuka na zingine mpya kujitokeza, dunia itafunikwa na giza nene  na matope kwa wakati wote wa usiku na mchana huku watu wakitakiwa kusoma katika Biblia Joel 2: 1-2 na Zephaniah 1:14-17.

NI TUKIO LA AINA YAKE KARNE YA 21
Nibiru inatajwa kama kitu kinachoisogelea dunia kinachoaminiwa kusababisha madhara makubwa ambapo kama hakitaigonga dunia, kitasababisha mtikisiko usio wa kawaida kitakapopishana nayo. Baadhi ya wanasayansi wanaamini kuwa kitendo hicho kitatokea mapema katika karne ya 21 (tuliyonayo sasa).

WANASAYANSI WAPINGANA
Baadhi ya wanasayansi wanapinga kwa maelezo kwamba hakuna ushahidi wowote wa kitafiti unaoonesha wazi kwa mabingwa wa anga za juu waliobobea wa masuala ya nyota.

MWANAMKE ALIWAHI KUOTA NDOTO
Kwa mara ya kwanza jambo hilo lilitokea mwaka 1995, wakati mwanamama Nancy Lieder muasisi wa mtandao wa ZetaTalk, aliwahi kudai kuoteshwa ndoto kwamba, Mei 2003 kuna kitu kitaingilia mfumo wa jua (solar system) na kusababisha dunia kutoboka tundu litakalosambaratisha sehemu kubwa ya kizazi cha binadamu.

Lieder aliifafanua kuwa, kitu hicho kitakuwa na ukubwa wa mara nne ya dunia.

BAADA YA NDOTO
Baada ya mwanamama Lieder, mtu wa kwanza kuizungumzia Nibiru alikuwa Mark Hazlewood, mwanachama wa zamani wa mtandao wa ZetaTalk ambaye mwaka 2001 alichapisha kitabu kilichoitwa Blindsided na kusema kuwa mwisho wa dunia ungekuwa mwaka 2003 baada ya kuwasili kwa sayari ya kumi (Nibiru).

Katika mfumo wa sasa, baadhi ya wanasayansi wanasema sayari ziko 12, wakizitaja kwa namba 1. Jua 2. Mercury 3. Venus 4. Dunia 5. Luna (mwezi) 6. Mars 7. Jupiter 8. Saturn 9. Uranus 10. Neptune 11. Pluto 12. Nibiru.

IMANI NYINGINE YASEMA MWISHO WA DUNIA NI FEBRUARI 22, 2014
Hata hivyo, utabiri mpya uliotolewa na watu wa jamii ya Vikings jijini New York, Marekani umesema mwisho wa dunia ni Februari 22, mwaka huu.

Mitandao mbalimbali pamoja na gazeti maarufu la Daily Mail la Uingereza lilielezea utabiri huo uliofanywa na jamii hiyo ukidai kuwa mwisho wa dunia utatokana na Mungu Odin kupigana na kuuawa na shetani Wolf Fenrir, hivyo kuiachia dunia anayoishikilia.

Wamesema baada ya kuiachia dunia itafurika maji ambayo yatakuwa na sumu, hivyo viumbe wote watateketea.

WATUMISHI WA MUNGU TANZANIA
Baadhi ya watumishi wa Mungu nchini wamekuwa wakisimamia andiko la kwenye Biblia linalosema kuwa, hakuna mwanadamu anayeijua siku wala tarehe ya mwisho wa dunia na ni siri ya Muumba.

Makanisa mengi nchini Tanzania yana sera tofauti lakini yanaongozwa na Biblia moja. Makanisa hayo ni Romani Katoliki, Lutheran (KKKT), Anglikana na makanisa ya kiroho kama Full Gospel& Bible Fellowship la Zakaria Kakobe.

FREEMASON WABARIKI
Jamii ya Freemason tayari imebariki mwisho wa dunia kwamba umefika na dunia inatarajie tukio kubwa la pamoja.

Mitandao ya jamii hiyo inataja kama hizi ni nyakati za mavuno kwa maana kwamba, upande wa Mungu na shetani kushindania watu huku waendao upotevuni  wakiwa wengi.

MFUMO WA DUNIA TANGU KUUMBWA
Kwa mujibu wa kitabu kinachoitwa Panorama ya Biblia, ulimwengu tangu kuumbwa kwake umekuwa na matukio makubwa kila baada ya miaka 2000 (inaweza isitimie au ikapita kidogo).

Tangu kuumbwa kwa Adamu na Eva mpaka gharika inadaiwa ni miaka 2000. Gharika hadi dunia kubadili mfumo wa mawasiliano (Mnara wa Babeli) ni miaka 2000. Kuzaliwa kwa Yesu hadi saa ni miaka 2000 ambapo katika karne hii, dunia huenda ikaingia katika tukio kubwa sana ambalo halijawahi kutokea.

Source:Global publishers

NI AJABU LAKINI NI KWELI-MTOTO AISHI MAKABURINI

$
0
0
Stori: Haruni Sanchawa na Makongoro Oging’
WAKATI sehemu ya makaburi imekuwa ikiogopwa na watu wengi kutokana na ukweli kwamba ni makazi ya wafu, hali ni tofauti kwa mtoto wa kiume anayekadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 8-9 ambaye jina lake halikuweza kufahamika, kuishi katika makaburi ya Kigilagila, Yombo jijini Dar es Salaam kwa zaidi ya mwezi mmoja.

Taarifa zilizopatikana kutoka eneo la tukio na baadaye kufuatiliwa kwa karibu na waandishi wetu, zinasema mtoto huyo ambaye hafahamiki alikotokea, alionekana akishinda na kulala katika makaburi hayo kwa zaidi ya mwezi mzima uliopita, kabla ya kutoweka kuelekea sehemu isiyojulikana.

Lakini baada ya siku kadhaa za kutoweka kwake, majirani wanasema walimuona tena mtoto huyo akiendelea na maisha eneo hilo ndipo walitoa taarifa Kituo Kidogo cha Polisi Yombo kuwataarifu juu ya tukio hilo lisilo la kawaida.

Polisi walifika makaburini hapo na kumchukuwa kijana huyo lakini walipomuhoji hakuweza kuongea chochote, hali iliyowafanya askari hao kutojua cha kufanya.

Kutokana na hali hiyo, polisi wa Kigilagila walifanya mawasiliano na Kituo cha Buguruni kwa hatua zaidi, ikiwemo kubaini anakotoka na sababu za kuishi katika mazingira hayo.

Gazeti hili lilifika na kumkuta mtoto huyo akiwa katika Kituo cha Buguruni anakohifadhiwa  wakati ndugu au wazazi wakisubiriwa, kabla ya taratibu za kumkabidhi kwa Ustawi wa Jamii kuanza kuchukuliwa.

Aidha, vyanzo vyetu ndani ya kituo hicho vilisema kuna watu walijitokeza wakiwa wanatafuta mtoto wa namna hiyo, lakini baada ya kumuona, walisema hakuwa yeye.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala, SACP Marietha Minangi alithibitisha  kuwepo kwa mtoto huyo na kwamba taratibu zinafanywa ili kulimaliza tatizo lake.

“Natoa wito kwa wananchi waliopotelewa na kijana mwenye umri huo, kufika katika Kituo cha Polisi Buguruni ili kuweza kumtambua mtoto huyo,” alisema Kamanda Minangi.

ZITTO:NAMSUBIRI FREEMAN MBOWE MAHAKAMANI

$
0
0
Mbunge wa kigoma kaskazini zitto Kabwe (Chadema), amesema anamsubiri mwenyekiti wa chama hicho, Freema mbowe mahakamani.
Zitto ametoa kauli hiyo baada mbowe kutangaza kumburuza mahakamani kutokana na kile kinachodaiwa kumzushia tuhuma za uongo
Nasema sitaki malumbano na kiongozi yoyote, nachotambua masuala ya mahakama yanajibiwa mahakamani na si vinginevyo" alisema zitto.

Zitto alitoa kauli hiyo, baada ya MTANZANIA kutaka kujua msimamo wake kutokana na kauli ya Mbowe kukududia kumshitaki, kutokana na madai ya kusema uongo dhidi yake. Zitto ambaye yupo nchini Nigeria anakohudhuria vikao vya kamati za Bunge za serikali kwa nchi za Afrika, alisema pamoja na Hali hiyo mahakama ndio njia pekee ambayo haki ya mtu inaweza kupatikana.
Alisema kwa msingi huo, hivi sasa hayuko tayari kuruhusu malumbano ambayo Hayana tija kwa Taifa.

" nipo Nigeria na bahati mbaya ninaumwa sana, ila hivi Leo ninamshukuru Mungu nimepata nafuu kidogo. Kama nilivyosema mwanzo sitaki Malumbano na mtu. Pamoja na kusema anaumwa, hakuwa tayari kufafanua ni ugonjwa gani unaomsumbua.

" huu muda nahitaji kutafakari maisha yangu kisiasa na kwa vyovyote vile masuala ya mahakamani yatajibiwa mahakamani", alisisitiza zitto

Nukuu gazeti la MTANZANIA la ZITTO KABWE ndio ICON ya Chadema ndio chanzo cha kupata nguvu kwa Chadema huwezi kutenganisha Chadema na Zitto labda kwa Kabila la wachaga ambalo kwao UKABILA wameweka MBELE, ndio MKOMBOZI wa makabila mengine ndani ya CHADEMA.

NATAKA WATOTO WAWILI WA KIKE NA WAKIUME ILA SITAKI MKE.

$
0
0
Habari wakuu

Wakuu nikiwa nakaribia umri wa miaka 25, nimefanya uamuzi kwamba sitaki kuwa na mke kwa maisha yangu yote, ila nataka kuwa na watoto wawili, mmoja wa kiume na mwengine wa kike kutoka kwa wanawake tofauti, hivyo natoa tangazo hapa kwamba natafuta wanawake wawili niwatie mimba kila mmoja anizalie mtoto mmoja.
Kwa ambae yuko tayari naomba tuwasiliane kwa gogle@gmail.com ili tuweze kukaa na mwanasheria wangu kwa ajili ya makubaliano ya kisheria na malipo, mwanamke hatokuwa na mamlaka yoyote kwa mtoto

VIGEZO NA MASHARTI KUZINGATIWA

BREAKING NEWS: MWANAMUZIKI FEROUZ AKAMATWA NA BANGI

$
0
0
Add caption
Vijana ni nguvu kazi ya taifa, lakini vijana hao hao wanaweza kuwa chanzo cha taifa kutoendelea na kubomoka. Ubomoaji wa taifa huwa kwa namna nyingi ikiwemo uvivu, ufisadi, na kadha wa kadha. Lakini hapa, tuangalie hili la madawa ya kulevya na bangi
Kila kukicha kuna wasanii wa maigizo na filamu ambao tunasikia
wamekamatwa na madawa ya kulevya, "unga" katika jitihada za 'kusaka maisha', wenyewe wanasema kuna ajali kazini. Wasanii hao ambao wengi ni vijana, na pale wanapoonekana kwenye runinga huwa hamasa kwa wadogo zao na jamii kwa ujumla, wakipenda kuwa kama wao.

Na mchana huu, maeneo ya Sinza, kuna taarifa ya mwanamuziki aliyetamba kwenye muziki wa bongo fleva, Ferouz, sanasana kwa wimbo wake wa Starehe, ambao ulikuwa ukionyesha madhara ya UKIMWI na virusi vya UKIMWI. Ferouz anadaiwa kukutwa na bangi, na picha ambazo Gospel Kitaa imezipata eneo la tukio, zinamuonyesha akisindikizwa na maafande kunako mbele ya vyombo husika.

Vijana wa Tanzania tuna shida gani? Kama ni ardhi tunayo, kama ni nguvu tunazo, sasa nini shida zaidi? Ipo haja ya Operesheni ambazo Askofu Sylvester Gamanywa ameitisha za Takasika iliyomalizika hivi karibuni, na kisha kupokelewa na Operesheni Milikisha, kuwahusisha pia wasanii wa aina zote, maana wanaonekana kukumbwa na janga hili kwa sana, vinginevyo, vijana ambao ndio nguvukazi ya taifa watakuwa wakijaa jela za ndani na nje, wakiacha wageni kuja kutawala.

DJCHOKA: HIZI NDIZO SABABU ZANGU KWANINI NIMEPUMZIKA KAZI YA UDJ

$
0
0
Leo naomba niwatangazie wadau wangu na mashabiki wote waliokuwa wakinipenda kipindi nikiwa nawadj wasanii wa hapa nchini na hata wale wasanii waliokuwa wakitoka nje ya bongo. Natangaza rasmi kupumzika kazi hii ya uDJ niliyoanza nayo toka 2005 mpaka leo, sababu za kupumzika nimeona nipumzishe uDJ niendelee na kazi inayoniingizia kipato nazungumzia website yangu hii tokea ikiwa ni blog.

Kazi ya kudj wasanii ni kazi fulani nzuri lakini ni ngumu sana usipokuwa na hobby nayo, nimeifanya kazi hii kwa mapenzi yangu mwenyewe yakupenda mziki na sikuwahi kulalamika mslahi ninayoyapata kwasababu niliifanya kazi hii kwa mapenzi yangu mwenyewe hata napokuwa jukwaani nilikuwa nafurahia sana. Lakini kwa kuwa kazi hii ya kuandika habari na kuonyesha kazi za wasanii wa hapa nchini ndio inayonilipa vizuri basi naona sina budi kupumzisha kimoja ili niendelee na kimoja

Baada ya kupumzisha kazi yakudj kwenye majukwaa na kuwadj wasanii sasa nitakuwa naendelea na kazi yakuvumbua vipaji vya wasanii pia nitaendelee na mix tape zangu kama kawaida. Msanii atakayenihitaji sasa hivi basi ujue itakuwa kazi yakwenda kupiga picha show zake au kurecord show zake TU akiwa jukwaani. Mbali na hapo nitaendelea kupromoti mziki wa nyumbani na wasanii wake mpaka mwisho wangu. Nawakaribisha madj wadogo ambao mlipenda kuwa madj wa wasanii na hamkujua jinsi yakuanzia, nitawashauri na pia nitawafundisha njia za kuwadj wasanii hususani wasanii wa Hip Hop na Bongo Fleva unacheza nao vipi unapokuwa nao jukwaani.
Nawapenda sana wadau wote wa DJCHOKA MUSIC kwasababu bila nyie hakuna mimi
ONE
DJ CHOKA

KAJALA AELEZEA TUHUMA ZA KUIBA MUME WA MTU

$
0
0
Ni zile stori za town sasa hivi ambapo mwigizaji Kajala amezungumza kwa mara ya kwanza kuhusu ishu yake ya kuandikwa kwenye blogs na magazeti ya bongo kuhusu tuhuma za kuchukua mume wa mtu.

Kajala anasema picha iliyopigwa akiwa na huyo mume wa mtu, kwanza ilipigwa bila yeye kujua lakini pia anasisitiza kwenda club au kwenda sehemu na kukutana na mtu na kupiga nae picha sio kwamba ndio umemuiba.


Anasema siku ya tukio ilikua ni siku ya kuzaliwa kwa mmiliki wa club hii ndio ikawa party hivyo kila mtu alikua anapiga picha ovyo ovyo ndio maana hata yeye hakujua kama anapigwa.

Kajala ambae ni mama wa mtoto mmoja mwenye umri wa miaka 14, anasema picha hii na taarifa za kuiba mume wa mtu zimemletea tatizo na maswali kwa familia yake hasa Mtoto na Mama yake.

Anasema mama yake mzazi aliumwa kwa mshtuko alioupata kwa sababu alidhani mwanae kaenda China kikazi na sio kuchukua mume wa mtu.

B12, ADAM MCHOMVU NA DIVA WAMEPIGWA CHINI CLOUDS FM

$
0
0
Stori:  MUSA MATEJA
WATANGAZAJI maarufu Bongo wa Redio Clouds Fm ya jijini Dar es Salaam, Hamis Mandi ‘B 12’, Adam Mchomvu na Loveness Malinzi ‘Diva’, wamepigwa chini na kituo hicho, Risasi Mchanganyiko linakupa zaidi

Habari za chini kwa chini kutoka kwa chanzo chetu zinasema kuwa uongozi wa Clouds umefikia hatua hiyo baada ya kuchoshwa na tabia ya utovu wa nidhamu wa watangazaji hao.

Hata hivyo, madai ya mitaani yanasema kwamba watangazaji hao wamepigwa chini kwa kosa la kukacha sherehe za maadhimisho ya miaka 14 ya Clouds FM,yaliyofanyika hivi karibuni katika Viwanja vya Mwembeyanga, Temeke, Dar.

Risasi Mchanganyiko lilimvutia waya Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba na kumwuliza juu ya ishu hiyo ambapo alikiri.


“Ni kweli tumefikia uamuzi wa kuwasimamisha B 12, Diva na Mchomvu baada ya kukiuka baadhi ya makubaliano baina yao na ofisi hivyo kusababisha usumbufu mkubwa ambao ulitulazimu kuingia gharama ambazo hazikutarajiwa.

“Hatutakuwa nao kwa muda usiojulikana ingawa watu wengi wamekuwa wakinihoji juu ya hilo lakini watachotakiwa kuelewa ni kwamba hakuna ofisi isiyokuwa na sheria na taratibu za kuongoza watu wake, sasa hao wamevunja taratibu zetu,” alisema Ruge bila kufafanua zaidi.

Alipoulizwa ni taratibu zipi watangazaji hao walizovunja alisema: “Nashindwa kueleza kosa la kila mmoja ila naomba nieleweke kuwa hao watangazaji kwa sasa tumewasimamisha kwa muda usiojulikana wakati tukifikiria cha kufanya. Muhimu hapo ni kwamba wamekwenda kinyume na tulivyokubaliana.”

JACKIE CLIFF ARUDI URAIANI??? HIKI NDIO ALICHOPOST INSTAGRAM MUDA MCHACHE ULIOPITA!

$
0
0
Sijui ni ka mchezo gani ila ndio hivyo Jack Cliff anaye semekana alikamatwa na madawa ya kulevya chini amepost picha hiyo kwenye instragram yake.....Hata masogange ilikuwa hivi hivi alianza kupost post picha zake mara tukasikia kaachiwa.....

MSUGUANO MKALI KATI YA WAZIRI NYALANDU NA LEMBELI WAIBUKA

$
0
0
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu.PICHA|MAKTABA
Kwa ufupi
Ripoti yake imesababisha mawaziri watatu kuachishwa kazi huku mmoja akijiuzulu.

Moshi/Kahama. Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, James Lembeli amesema anawaachia Watanzania waamue mkweli kati ya kamati yake na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu.
Kauli hiyo ya Lembeli inafuatia taarifa ya
gazeti moja la kila siku (Siyo Mwananchi), iliyomnukuu Nyalandu akisema ripoti ya Operesheni Tokomeza Ujangili iliyowang’oa mawaziri wanne ilikuwa ya uongo.
Nyalandu anadaiwa kutoa kauli hiyo alipozungumza na viongozi wa taaluma mbalimbali na Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Dodoma na Manyara kuhusu mgogoro wa mipaka kati wanavijiji na Hifadhi ya Tarangire.
Pia, mgogoro huo unahusisha Pori la Akiba Nkungunero na vijiji vya jirani.
Nyalandu alikaririwa akisema kutokana na taarifa hiyo kueleza wapo watu waliobakwa wakati siyo kweli. Tanzania imeonekana kushuka kwa kiwango kikubwa katika utawala bora kutokana na ukiukwaji haki za binadamu.
Hata hivyo, Lembeli alipoulizwa na gazeti hili jana kuhusiana na kauli hiyo alijibu: “Sijaisoma hiyo habari ila nimeisikia tu, kama ni kweli ametoa kauli hiyo (Nyalandu) basi ni hatari.”
Lembeli alisema anawaachia Watanzania kupima mkweli kati yake, kamati yake na Waziri Nyalandu katika jambo hilo.
“Kwa sasa niko kijijini kwangu huku jimboni, lakini nitafafanua zaidi nitakaporejea Dar es Salaam,” alisema.
Ripoti hiyo ya kamati ndogo ya uchunguzi iliyoongozwa na Lembeli ndiyo iliyosababisha mawaziri wanne kuwajibika, kutokana na kuibuliwa kwa vitendo vya ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu. Mawaziri waliong’olewa ni Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Emmanuel Nchimbi, Waziri wa Ulinzi, Shamsi Vuai Nahodha, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Dk Mathato David na Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki alijiuzulu kabla.
Atangaza ubabe
Lembeli alikazia kwa kusema hawezi kuishi kwa kuhofia vitisho vya maisha, kwa madai ya taarifa yake ya Operesheni Tokomeza Ujangili iliyosababisha kung’olewa kwa mawaziri wanne.
Akihutubia mkutano wa hadhara Kata ya Igunda, Lembeli alisema haogopi vitisho hivyo na ataendelea kutetea masihali ya umma.
Awali, Diwani wa kata hiyo, Tabu Katoto wakati akimkaribisha, alimpa pole mbunge huyo kwa kazi ngumu na lawama aliyoifanya mwaka jana kwa faida ya taifa, hali ambayo Lembeli alisema inampa wakati mgumu kutokana na watu wenye akili ndogo kumpa vitisho. vya maisha yake.
Mwananchi: Lembeli ataka Watanzania waamue mkweli

EXCLUSIVE AUDIO KUTOKA KWA DIAMOND PLATNUMZ FT CHEGE, ISIKILIZE HAPA KWA MARA YA KWANZA

$
0
0
Zitumie hizi dakika kadhaa kumsikiliza alichokifanya Diamond kwenye hii beat ya Chegge Chigunda ya Uswazi Take away,uongozi wake umetubariki kuwapa watanzania hii kama Exclusive kwenu kuisikiliza hii nyimbo afu tupe maoni yako hapo chini kwa kucoment.

SOMA SIMULIZI HII YA KUSIKITISHA | HATA KAMA UKIANDAMWA NA MATATIZO, MAPITO KAMA HAYA USIABUDU MIUNGU MINGINE

$
0
0
Mama mmoja baada ya kukaa kwa muda mrefu bila kushika mimba, aliamua kwenda kwa mchungaji mmoja ambaye alitoka nchi ya mbali na kuja pale mtaani kwao akiwafanyia watu miujiza mbalimbali kupitia maombi yake na mama akaomba kuombewa ili apate mtoto.

Mchungaji yule alimfanyia ibada fupi na miezi michache baadae yule mama alibahatika kupata mimba na kuibeba kwa miezi tisa kisha akajifungua salama mtoto wa kiume.

Mama yule aliendelea kumtunza mwanae kwa kumnyonyesha ingawa kila alipomnyonyesha mtoto yule mama aliishiwa nguvu na kulala kwa muda kabla ya kuamka na kuendelea na kazi.

Jambo lile lilimshtua sana mama lakini akafikiri labda ni tatizo la kawaida kwani hakuwahi kuwa na mtoto.

Akaamua amwanzishie kumpa maziwa na kumwomba msichana wake wa kazi kuwa awe anampa maziwa pindi yeye yupo kazini na akawa akinunua maziwa lita tatu ili yaweze kukaa kwa siku tatu.

Maajabu ni kwamba lita tatu ziliisha kwa siku na mama kwa kuwa alipenda kwenda na bajeti hivyo alimkaripia msichana wa kazi na kumpiga sana kwa kumaliza maziwa lita tatu kwa siku.

Binti alilalamika sana na kusema mama huwa nayachemsha na kuyaacha mengine kwenye sufuria kisha kidogo namnywesha mtoto na ninaendelea na kazi kabla ya kuja kuangalia na kuona mazima yameisha kwenye sufuria.

Mama hakuamini na binti akaamua kuweka mtego ili aone kama ni majirani wanamfanyia visa au kuna kitu ambacho hunywa maziwa yale.

Siku iliyofuata baada ya kumnywesha mtoto maziwa akamlaza kitandani karibu na ile sufuria ya maziwa na kujificha nje akiangalia kila kilichokuwa kikiendelea mle ndani.

Mara akaona mtoto yule anabadilika na kuwa joka kubwa na kunywa yale maziwa na kisha kurudia umbo lake la mtoto.

Binti akakimbia mpaka kwa mama na kumwambia ingawa mama akawa mbishi kuamini na siku ya pili wakafanya kwa pamoja na baada ya dakika chache mama akamshangaa mwanae wa pekee akibadilika na kuwa nyoka.

Mama alipiga kelele na kwenda kwa mchungaji na mchungaji akasema wakamlete mtoto na alipoletewa yule mtoto, mchungaji akamkumbatia na mtoto yule kupotelea kifuani kwake.

Mama yule aliondoka na kwenda kibandani mwake ili afunge na kurudi nyumbani kabla ya kushangaa kuona kuwa yule nyoka kaja kibandani kwake ..... Akakichoma kibanda chake na kwenda kanisa lake la mwanzo ambako alifanyiwa maombi na kutolewa vitu vya ajabu tumboni mwake na kutaapishwa maji aliyokuwa akinyweshwa na yule mchungaji feki.

Sasa hivi yule mama kamrudia Mungu wake na ana mme na mtoto mmoja na yule mchungaji akiyempa yule mtoto nyoka alikimbia na haijulikani aliko.

Mama yule kila akisoma amri ya Mungu ya kwanza kwetu wanadamu hulia sana na kumwomba Mungu amsamehe kwa kupotoka kwake na amri hiyo yasema, " Mimi ndimi Bwana Mungu wako Usiabudu miungu mingine ila mimi"

Nami nakuombea rafiki yangu hata pale unapoandamwa na matatizo ya dunia, mapito magumu au kukosa furaha na amani katika maisha kamewe Usiabudu miungu mingine.
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live




Latest Images