Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

Ni kweli Mwana FA na Diamond haziivi kisa Alikiba? FA aueleza ukweli (Exclusive Audio)

$
0
0
Weekend hii kwenye show ya uzinduzi wa Tigo Music iliyofanyika Leaders Club jijini Dar es Salaam, kulienea taarifa kutoka kwa mmoja wa mameneja wa Diamond Platnumz kuwa Alikiba aliwazuia Mwana FA na Shaa kusaliamiana na hitmaker huyo wa ‘Ntampata Wapi’.

Ni kweli?

Sijui nikwambie nini, lakini kama sitaki kulifanya hili suala liwe habari, kiukweli yaani,” FA ameiambia Bongo5.

Vipi kuhusu uhusiano wake na Diamond baada ya kumshirikisha Alikiba kwenye hit single yake, Kiboko Yangu?

“No we are very good as a matter of fact,! amesema Binamu.

He texts me (Diamond) every now and then, hivyo namcheck nini. Mameneja wake wote watatu washkaji zangu kinoma na yeye tuna mazoea ya kutosha tu hivi tumekaa one of these days tukapiga story sana, hakuna chochote kilichoharibika,” ameongeza rapper huyo.

I don’t even think Kiba anamind hiyo na anajua kuwa mimi na Diamond we cool na watu wa Diamond pia we cool, they are cool with me na as a matter of fact wananitaniaga ‘wewe team Kiba wewe’. So we good like that.

Msikilize Mwana FA akiongea hapo chini. ~Bongo5

Mwanamke Awaua watoto wake wawili na Kuwazika ndani ya Nyumba Yake

$
0
0
Mwanamke mmoja  mkazi wa mkoa wa Tabora wilaya ya Tabora mjini kata ya Chemchem amewaua watoto wake wawili  na kuwazika ndani ya nyumba yake.

Mwanamke  huyo  amedai  kuwa  kilichomfanya  awalishe  sumu  watoto  wake  ni ugumu  wa  maisha  uliokuwa  ukimkabili  baada  ya  kikimbiwa  na  mumewe.

Kwa  mujibu  wa  jirani  yake, siku  ya  tukio  mwanamke  huyo  alisikika  akichimba  shimbo  ndani  ya  nyumba  yake  kabla  ya  kutangaza  kupotelewa  na  watoto  wake  siku  ya  pili  yake.

Taarifa  ya  kupotea  kwa  watoto  hao   ilimpa  mashaka  jirani  huyo  na  kumlazimu  akatoe  taarifa  polisi  ambapo  maafande  walikuja  na  kufanya  msako  ndani  ya  nyumba  hiyo  ambapo  walifanikiwa  kufukua  maiti  za  watoto  hao.

Picha za Mwenyekiti wa Kitongoji aliyechinjwa na kupikwa ndani ya Sufuria

$
0
0
Mwenyekiti  wa Kitongoji    cha  Songambele, Kata ya Ilela Tarafa Inyonga Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi, Richard Madirisha (31), ameuawa kikatili kwa kuchinjwa  shingo na kutenganishwa na kiwiliwili na kisha kunyofolewa  viungo vya mikono na miguu na sehemu za siri  na kichwa chake na viungo hivyo kupikwa ndani ya safuria kama mboga.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari  mauaji hayo ya kikatili na  kutisha  yalitokea juzi saa 5.30 usiku nyumbani kwa marehemu.


  Kidavashari alisema, siku hiyo ya tukio marehemu alikuwa amelala nyumbani kwake akiwa na mkewe  Meklina  Mussa na  ghafla walitokea watu watano ambao hawafahamiki na  kuvunja mlango na kuingia ndani ya nyumba.

Alisema watu hao waliodaiwa kuwa na mapanga  waliingia chumbani kwa marehemu  na kumlazisha mkewe ajifiche kwa kujifunika na shuka usoni.

Alisema  baada ya mkewe kujifunika walianza kumchinja marehemu  kwa  kutumia panga huku mkewe akiwa anasikia jinsi marehemu  akilia kwa uchungu.

Kidavashari alisema baada ya kumchinja walichukua kichwa na kukiweka kwenye safuria na maji na kukipika kwenye moto uliokuwa unawaka nje ya nyumba ya marehemu.
Alisema kisha walirudi ndani na kunyofoa sehemu za siri, mikono na miguu  na  kuziweka kwenye  safuria  jingine  kwenye moto   na kutokomea kusikojulikana huku  viungo hivyo vikiendelea kuchemka  ndani ya safuria hizo.

Maswali 10 kwa Vodacom Tanzania Kuhusu Shindano la Jay Millions

$
0
0

Maswali 10 kwa Vodacom Tanzania :Leo si siku ya 12 tangu promotion yashinda mamilioni ya jaymillionsilipoanzishwa na Vodacom Tanzania lakiniimekuwa ikilalamikiwa na watu wengikwenye mitandao ya kijamii na na mitaanikuwa "vigezo na masharti kuzingatia"inatumika kuwa hadaa wananchi. Haya nimaswali tungependa Vodacom watujibu

1. Mimi naweza leta comments 150 zafacebook na twitter zilizokuwa posted kuanzia tarehe 20-25 zikilalamikia sintofahamu ya jaymillions, je Vodacom wanaweza kuleta comments 10 tuzinazosifia?

2. Kwenye radio matangazo yenu yanasema hakuna kushiriki lakini usipotuma msg ukakatwa shilingi 300 basi huna nafasi ya kushinda, je 300 ni ya nini kama si bet ya kamari husika?

3. Je kuna tangazo lolote la redio, TV au hata bango (billboard) linalosema mwananchi atakatwa shilingi 300 kwa kila msg atakayotuma kuuliza kama kashinda?

4. Tangu shindano lianze, (ambalo mlisema mtatoa milioni 100 kila siku,milioni 10 na milioni 1) leo ni siku ya 12 ambayo kwa ahadi yenu ilibidi muwemmetoa bilioni moja milioni 400 lakini mpaka leo tarehe 26 mmetoa milioni 16 tu, je ni hizi bilioni kadhaa anapewa nani?

5. Naskia vodacom ina wateja milioni 10,wateja laki moja tu ambao ni asilimia 1 tuya wanachama wakituma msg ni shilingi 300'000'000 kwa siku sawa na shilingi 3'600'000'000 na vodacom wametoa milioni 16 tu kurudisha kwenye jamii mpaka sasa, hamuoni kua mnaondoa shilingi kwenye mzunguko na kuathiri uchumi?

6. Probability ya mshindi kutokea kwenyewatu laki moja na sio kwenye watu milioni 9 na laki 9 ni sawa na kusema kila sikuku  na nafasi moja ya pesa kuchukuliwa navodacom wana nafasi 99 za kubaki nahela, je ipo ipo siku itatokea mtu atashidamilioni 100?

7. Usiri wa kuwa mshindi atatajwa baada ya yeye kuwa katuma msg hamuoni kama inaweka mwanya wa wanaochezesha promotion kupanga matokeo nakujifaidisha wao wenyewe?

8. Je si wakati muafaka kwa Vodacom kutangazia umma kuwa promotion ya jaymillions ni kamari ambayo mshindi atachaguliwa miongoni mwa walioshiriki tukwa kutuma msg ili kuwapa wanashirikinafasi sawa ya kushinda?

9. Ni sahihi kusema jana Vodacom walikata internet kwa masaa matano wakati mjadala wa kuhoji kizungumkuti cha jaymillions umeshika kasi kwenye facebook, twitter na jamii forums?

Naamini wahusika wa Vodacom maswali haya yatawafikia, wanaweza wasijibu na hawatojibu ila kwa wanachokiona sasa kwenye mitandao ya kijamii waelewe kuwa watanzania wamebadilika,  hawapelekeshwi tena.

Ni mtamu, Shape Nzuri, Lakini Namuacha kwa Hili

$
0
0
Aisee asikwambie mtu, mi ni mroho wa shape za kibantu zilizojaaliwa kalio la kutosha kumtoa nyoka pangoni. Sikosi kugeuka nikiona sampuli ya hivyo ikipita nasindikiza kwa macho hadi anakoishia ama kumfuata na kufanya application kabisa.

Juzi kati nimefanikiwa kunasa mdada mmoja mwenye vigezo kama hivyo ni nikafanikiwa kupiga naye show ya kikubwa kunako 6x6. Aisee ni mtamu ile mbayaaaa.

Baada ya kukolea nami akataka kujenga uhusiano wa kudumu japo hata kwa mchepuko ama nyumba ndogo! Kwa jinsi hata mi nilivyokolea kwake nikamkubalia.

Kitakachofanya nimuache pamoja na vigezo vyake vizuri, ni kwamba ana majini na kaniambia yeye mwenyewe , kanitajia idadi na majina ya hayo majini hadi nikaogopa.

Yaani hapo nawaza hivi siku yakicharuka hayo madude yake japo sijui huwa yanafanyaje, si itakuwa balaa.

Aisee kwa kweli naachia ngazi huku bado nalitamani hilo dada la kibantu lilioumbika vizuri, limeenea kila idara.

Breaking News: Siku Mbili Baada ya Prof. Muhongo Kujiuzulu Tume ya Ramani na Madini Duniani Yamteua Kuwa Mtendaji Mkuu wa Tume Hiyo

$
0
0
Siku Mbili tu. Baada ya profesa Sospeter Muhongo kujihuzuru nafasi ya waziri wa nishati na madini hii JanaTume ya Ramani na Madini Miamba na Mawe Duniani yenye makao makuu nchini Uingereza imemteua profesa Muhongo kuwa mtendaji mkuu wa tume hiyo pia atafanya kazi kwenye kampuni inayopasua miamba diniani kama mwenyekiti.
~Source: William Malecela Blog

Maskini:Mwanamitindo Millen Magese Alazwa Tena Hospitalini, Atoa Ujumbe Mzito Akiwa Katika Maumivu Makali

$
0
0
Mwanamitindo Maarufu Millen Magese Amepost kwenye ukurasa wake wa Instagram akiwa kitandani kwa mara nyingine tena akipata matibabu kuhusu ugonjwa unaomsumbua na kuandika ujumbe huu wa kusikitisha:

"
I didn't want to Post any pic this time because Iam exhausted ....but posting this pic today is just to insist ...Endometriosis is real. I truly don't wish to see any young girl/woman go through this pain . It's not just your period pain , it's more than that. May this remind women from all over that our women health is very important and the best investment you can ever do for yourselves. Let's continue to keep our faith higher and pray but empower ourselves by doing check ups and see doctors more often before it's too late . Don't ask God Why ask him to lead you on how you can find help and Cure . You're here for a reason 13th surgery in my body and I truly not asking rather encouraging everyone to raise awareness so we can find cure . With due respect , don't tell me which church or pastor I should see today because I obviously pray and have faith just take care of yourselves ,God knows better and he will soon get me out of this when he is done with me . Don't tell me to pray harder . Don't tell someone who is going through chronic pains to pray harder you're not helping her .Many thanks to everyone who have been here for me, pray with me since day one . It has been a long journey , may he stops it when it's time.. follow @endometriosisafrica and page awareness .its all over Google so Google it and get Knowladge about it , find out if you have any issues at all. It's better🙏#letsfindaVoice #together we can find Cure and make a difference"

NCCR-Mageuzi wataka Rugemalira, Tibaijuka, Chenge Wafikishwe Mahakamani

$
0
0
Chama cha NCCR-Magezi kimesema, vigogo wote waliohusika kutoa na kupokea mgawo wa fedha kutoka akaunti ya Tegeta Escrow wafikishwe mahakamani akiwamo Mkurugenzi wa VIP Engineering Ltd, James Rugemalira .

Kashfa hiyo imesababisha Rais Jakaya Kikwete kufanya mabadiliko madogo ya baraza lake la Mawaziri kutokana na mawaziri wawili kujiuzulu.

Mawaziri waliotajwa kwenye sakata hilo ni Profesa Anna Tibaijuka, ambaye alikuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na aliyeingiziwa Sh1.6 bilioni na mwanahisa wa zamani wa Kampuni ya IPTL, James Rugemarila.

Wengine waliopata mgao huo kutoka kwa Rugemarila na kiasi katika mabano ni Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), Andrew Chenge (Sh1.6 bilioni), Mbunge wa Sengerema (CCM), William Ngeleja (Sh40.4 milioni), aliyewahi kuwa Waziri wa Nishati na Madini, Daniel Yona (Sh40.4 milioni), Mbunge wa zamani wa Sumbawanga (CCM), Paul Kimiti (Sh40.4 milioni) na aliyekuwa mjumbe wa Bodi ya Tanesco, Dk Enos Bukuku (Sh161.7 milioni).

Akizungumza na waandishi wa habari, Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, Mosena Nyambabe alisema waliofikishwa mahakamani hadi sasa ni vidagaa lakini na vigogo mashuhuri wakiendelea kutamba.

“Mpokeaji na mtoaji wa rushwa wote ni wahalifu na wanatakiwa  kufikishwa mbele ya mahakama ili wajibu tuhuma zinazowakabili...Rugenarila naye ni miongoni mwa watu wanaotakiwa kufikishwa mahakamani.”

“NCCR tunataka kujua kwa nini baadhi waliopewa rushwa wamefikishwa mahakamani lakini watu wengine kama Profesa Tibaijuka, Chenge, Ngeleja, Yona, Kimiti na wengineo hawafikishwi mahakamani? Wote wanatakiwa kwenda kujibu tuhuma zao,” alisema Nyambabe

Hata hivyo, Mkurugenzi wa Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah alipotafutwa kuzungumzia kauli hiyo ya NCCR alisema, “Sipo ofisini hivyo nisingependa kulizungumzia hilo.”

Waliofikishwa mahakamani hadi sasa ni Mhandisi Mkuu wa Mradi wa Umeme Vijijini (Rea), Theophillo Bwakea na Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Rugonzibwa Mujunangoma, ambao kwa pamoja wanadaiwa kupokea rushwa ya Sh485.1 milioni.

Wengine ni Meneja Misamaha ya Kodi wa TRA, Kyabukoba Leonard Mutabingwa, Mwanasheria Mwandamizi wa Tanesco, Steven Roman Urassa na Mkurugenzi wa Fedha BoT, Julius Rutta Angello wanaokabiliwa na mashtaka ya kuomba na kupokea rushwa ya jumla ya Sh1.923 bilioni.


Nini Tena Kimemsibu Jacqueline Wolper? Hebu Soma Alivyofunguka Hapa

$
0
0
Kupitia kwenye page yake moja ya mtandao maarufu wa kijamii nchini, mwanadada wolper amefunguka haya yafuatayo…



"Maandishi ya uwongoo yananiharibia sana huusianao wangu plz stok na msani yoyote Tanzania wala nyege zangu azimalizwi na msani yoyote Tanzania ninamwanaume wangu namuheshm ananiheshim nasipo kuweka mahusiano yangu adharanii wala mitandaoni Maana nimtu na heshima zake.. nimeumwa na nyoka mara ya kwAnza so ata jani likinigusa ninashtuka kikubwa sina mapenz ya matangazo wala mitandaoni stak kuandikwa kwa lolote lisilolaukweli ..nawewe unaefurah me kuandikwa nawewe ikiwa ukweli unaujua kma niuwongo jua kuwa unaniharbia kwa walinizunguka cc wazazi wangu na Mahusiano yangu ..” Mwisho wa kunukuu



Jamani, kiukweli hatujui Wamemfanya nini Jacquiline Wolper wetu, ila mwenye "ubuyu" kamili wa kilichotokea tunaomba atufahamishe kupia comments hapo chini maana namba ya Jack tunayompigia ili atupe ukweli wa mambo haipatikani…

Kizuri share na wenzako

Walio Naswa Wakifanya Mapenzi ya Jinsia Moja Kumbe Walikuwa Wameoana Kabisa

$
0
0
Na Haruni Sanchawa/Uwazi
SAKATA la wasichana wawili warembo, Maua Sadick (24) mkazi wa Stakishari, Ukonga, Dar es Salaam na Lucy Fred (23) mkazi wa Karakata, Dar ambao walishikiliwa katika Kituo cha Polisi Stakishari, Ukonga jijini kwa madai ya kufanya mapenzi ya jinsia moja limechukua sura mpya.

Habari za kipolisi zinasema wasichana hao ambao walifunguliwa jalada kituoni hapo namba SKT/RB/463/2015 baada ya kukamatwa Januari 12, mwaka huu inadaiwa kuwa walioana.

“Zipo picha zinazodaiwa kuwa walioana na wanaonekana wakiwa wanavishana pete nyingine wakiwa wanafungua shampeni kwenye hafla fupi ambayo waliifanya jijini Dar es Salaam,” kilisema chanzo ndani ya jeshi la polisi.

Habari zaidi zinadai kuwa hafla hiyo waliifanyia katika ukumbi mmoja (jina tunalihifadhi) ambao upo Chang’ombe na unatumika kwa shughuli nyingi za burudani na hata michezo.“Mimi nilihudhuria sherehe hiyo na picha ninazo ambazo zinawaonesha wasichana hao wakivishana pete na walikuwepo pia waalikwa kama unavyoona kwenye sherehe za harusi katika jamii yetu,” alisema mtu mmoja ambaye jina lake tunalihifadhi.

Mtu huyo alidai kuwa mmoja wa wasichana hao anamfahamu kwa kuwa sasa hivi anaishi kwa dada yake karibu na Uwanja wa Ndege, Karakata nyuma ya msikiti mpya.Mara baada ya kukamatwa wasichana hao, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mogo, Stakishari,George Mtambalike alilithibitishia gazeti hili ofisini kwake kutiwa mbaroni kwao kwa madai ya kufanya mapenzi ya jinsia moja.

Naye Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi Ilala, SACP Mary Nzuki alisema wasichana hao bado wanapelelezwa. “Ni kwamba kesi yao ipo Stakishari na uchunguzi dhidi yao ukikamilika watafikishwa mahakamani, “ alisema Kamanda Nzuki.
GPL

Daktari: Moyo wa Mchezaji Okwi wa Simba Ulisimama Alipogongwa Kisogoni na Beki Aggrey Morris wa Azam FC

$
0
0
Sweetbert Lukonge na Ibrahimu Mussa
MOYO wa mshambuliaji Emmanuel Okwi ulisimama kwa sekunde kadhaa alipogongwa kisogoni na beki Aggrey Morris wa Azam FC.

Okwi aligongwa katika mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Azam FC iliyomalizika kwa sare ya bao 1-1 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, jana.Daktari wa Simba, Yassin Gembe, amesema moyo wa Okwi ulisimama kwa sekunde kadhaa kutokana na pigo la kisogoni karibu kabisa na ubongo katika eneo la Medullar Oblangata.

“Hakikuwa kitu kidogo, tulilazimika kufanya tiba ili kurudisha mapigo ya moyo wake kwa kuwa ulisimama kwa sekunde kadhaa. Aliumia na uliona akitoa mapovu. “Baada ya hapo, tuliona ni vema kumfikisha Muhimbili ambako vipimo vyote vimefanyika. Imeonekana hakuumia sana na ameruhusiwa.

“Lakini mimi nimeamua kumpumzisha kwa siku mbili ili kuangalia kama atakuwa katika hali gani maana mwanzo unaweza kuona yuko vizuri kumbe kuna tatizo. “Ikionekana anaendelea vizuri, basi ataanza mazoezi lakini atakuwa chini ya uangalizi wangu,” alisema Dk Gembe.

Mshambuliaji wa Simba, Dan Sserunkuma alitumia muda mwingi kumlaumu Morris kwamba alishiriki kumpiga Okwi kiwiko, hata hivyo, alikuwa akikanusha.Okwi alibebwa haraka na kutolewa uwanjani na baadaye kukimbizwa Muhimbili ikiwa ni baada ya kuzinduka.

Kugongwa huko kwa Okwi, jana jioni kulizua gumzo kwa mashabiki wa soka nchi hasa wa Simba ambao walikuwa wakipiga simu katika ofisi za gazeti hili wakidai mabeki wamekuwa wakatili kwa washambuliaji.
 Wengi walitolea mfano wa beki George Michael wa Ruvu Shooting kumkaba mshambuliaji Amissi Tambwe wa Yanga.

Aunt Ezekiel: Mimba yangu Imekuja Vizuri Haijanibadili Tabia Kama Wengine

$
0
0
Huku kukiwa na tabia kuwa baadhi ya wanawake wanapokuwa wajawazito wanakuwa na tabia za kusumbua na kubagua baadhi ya vitu, msanii wa filamu za Kibongo Aunty Ezekiel ‘Mama Kijacho’, amesema kwa upande wake yuko vile vile na wala hajabadilika.

Akiongea  na mpekuzi, Aunty alisema kuwa haoni kama amebadilika kitabia au kuwa msumbufu bali anajiona yupo kawaida ingawa mara nyingine anakuwa anachoka sana.

“Mimba wala haijanibadili maisha kwa maana sipo kama wanawake wengine wanavyokuwa wasumbufu, naamini kuwa nitaendelea kuwa hivi hadi mwisho nitakapojifungua,” alisema Aunty.

Clouds FM Yanyangwanywa Mtangazaji Mwingine na Radio Mpya EFM

$
0
0
ALIYEKUWA Mtangazaji wa vipindi vya Michezo wa radio Clouds Dar es Salaam, Ibrahim Masoud 'Maestro' leo amekamilisha usajili wake wa kujiunga na Kituo maarufu hivi sasa cha radio hapa jijini Dar es Salaam cha EFM 93.7.

Maestro ameungana na magwiji wengine katika utangazaji wa vipindi vya michezo nchini wakiwemo Maulid Kitenge na Omary Katanga ambao wapo katika radio hiyo inayokuja kwa kasi jijini.

Polisi wa Pikipiki Waporwa Bunduki 2 kwa Kushikiwa Kisu na Kujeruhiwa

$
0
0
Watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi, wamewavamia na kuwajeruhi askari mwenye no G369 PC Mansour na Hv507 PC Mwalimu, wakiwa doria ya pikipiki ambao walinyang'anywa silaha mbili aina ya SMG no 14301230 na 14303545 na watu wasio julikana mkoani Tanga.

Taarifa ya Jeshi hilo kwa vyombo vya habari imesema tukio hilo limetokea Januari 26, 2015 majira ya saa 23:30hrs eneo la barabara 04 jijini humo.

Aidha, imesema mmoja wa majeuhi askari mmoja no H 507 PC Mansour amejeruhiwa vibaya maeneo mbalimbali ya mwili na amelazwa katika Hospitali ya Mkoa Bombo.

Katika uchunguzi wa awali Polisi wamefanikiwa kumtia hatia hatiani mtuhumiwa mmoja, Ayubu Haule, (27), fundi Radio Mkazi waCorner Z Amboni Kiomoni ambaye alikamatwa eneo la tukio akijaribu kutoroka na pikipiki na mara baada ya kupekuliwa ndipo alipokutwa na mchoro wa ramani unaoonyesha matokeo ya Barabara na kufunguliwa kesi yenye no TAN/IR/322/2015.

Mtuhumiwa anaendelea kuhojiwa na Jeshi hilo huku timu ya Intel na makachero wa Polisi ikiendelea kufanya doria pamoja na Section 2 za FFU.

Picha za tukio:

Tetesi za Mwanamke Mmoja Kujiua Baada ya Kuchambwa Sana Kwenye Blog Maarufu

$
0
0

Leo Asubuhi Zimeibuka Tetesi kuwa kuwa Kuna Mwanamke Mmoja ajulikanae kama Violet amefariki Dunia baada ya Kusemwa sana na Blog hiyo, Habari ya kifo chake bado haijazibitishwa rasmi kwani kwenye mitandao  ya instagram na Facebook  kila mtu anaongea lake , Wengine wakisema kuwa mwanamke huyo anafake kifo chake ili u-turn waondoe post iliyomsema na kuweka mambo yake ya siri hadharani..Tutawaletea Updates za Habari hii Baadae tukipata uhakika wa kilichotokea

Ila kama ni kweli RIP Violet

Hivi Ndivyo Millard Ayo Alivyosherehekea Siku ya Kuzaliwa Kwake Pembeni ya Mrembo Jokate Mwegelo kama Mpenzi Wake

$
0
0
Mtangazaji wa kipindi cha Amplifaya cha Clouds FM, Millard Ayo, jana alikuwa anasherehekea siku yake ya kuzaliwa.

Kwenye party yake ndogo ambayo aliamua kuifanyia nyumba kwake, ni msichana mmoja tu special aliyepata nafasi exclusive ya kusherehekea naye – Jokate Mwegelo.

“This is what you do after you cook. You eat cake lol. Happy Birthday to the GREATEST to ever do it @millardayo,” alitweet Jokate.

Siku za hivi karibuni wawili hao wamekuwa wakidaiwa kuwa na uhusiano. Hata hivyo Jokate alikanusha.

Watoto Wanne wa Familia Moja Wafariki Kwa Sumu Iliyowekwa Kwenye Chakula, Baba yao Anusurika

$
0
0
Watoto wanne wa familia moja wakazi wa kijiji cha kibambila wilayani Kakonko mkoani Kigoma wamefariki dunia na mmoja amelazwa katika kituo cha afya Kakonko baada ya kula chakula kinachosadikiwa kuwa na sumu.

Makaburi yakiandaliwa kwa ajili ya maziko ya watoto hao

Mganga  mkuu wa wilaya ya Kakonko  Dkt. Fadhil Seleman  amewataja watoto hao waliofikishwa kituo cha  afya  Kakonko kuwa ni  Neema Joseph, Jonas Joseph, Majaliwa Joseph, Yusuph Joseph wote wakiwa na umri wa kati ya miaka 11 na 18 walifikishwa hospitalini hapo  wakiwa na hali mbaya na walipoteza maisha wakati wanaendelea kupatiwa huduma.
Amesema kwamba uchunguzi wa awali umeonesha kuwa watu hao wamekula sumu katika chakula cha ugali.

Akizungumzia tukio hilo baba wa watoto hao Joseph Kajolo ambaye alinusurika katika tukio hilo amesema hajui chanzo cha tukio hilo huku baadhi ya wananchi wa Kakonko  wameeleza kusikitishwa kwao na tukio hilo na kwamba vifo vya sumu katika wilaya hiyo  vimekuwa vikijirudia mara kwa mara

 Mkuu wa wilaya ya Kakonko Peter Toyima amesema polisi inamshikilia mtu mmoja kuhusiana na tukio hilo huku akiwataka wananchi kuacha vitendo vya kuwekeana sumu…

Demu wa Kenya Tiara Arudi Tena, Atuma Video Nyingine kwa Diamond Akiwa Anaoga na Kusema Yupo Tayari Kufanya Nae Project

$
0
0

Kuwa Staa Raha Sana: Baada ya Diamond Kutumiwa Video na Mrembo wa Kenya akimtaka Amchukukue yeye bila Malipo huku akijichezesha kwa kimahaba kwenye hiyo video, Diamond inaonekana hakupata Ujumbe wa kwanza sawa sawa , sasa Mrembo amerudi tena na kali zaidi ya ile , Mrembo huyo ajulikanae kama Tiara Ameitumia Udaku specially Video Hiyo akiwa bafuni akioga huku wimbo wa Bebe Cool unaitwa i will love you everyday ukilia kwa nyuma ili Diamond Amuone Vizuri kwani ile Video ya Mwanzo ilikuwa na Giza...

Mrembo huyo pia amesema yeye ni Mwanamuzi na Angependa kufanya Project na Diamond Platunumz
Jionee mwenyewe hapa mimi Sina Mengi :

Wema Sepetu Apigiwa Magoti na Gazeti la Mtanzania na Kuombwa Msamaha

$
0
0
“Katika gazeti letu la Mtanzania toleo No. 7709 la Alhamisi Januari 22, mwaka huu, tuliandika kimakosa stori yenye kichwa cha habari ‘Wema Sepetu ampeleka Diamond Polisi’. Baada ya kufanya uchunguzi tumejiridhisha habari ile haikuwa na ukweli, kwani chanzo kilichotupatia kilitupotosha, hivyo kuleta usumbufu kwa msanii Wema pamoja na jamii. Kutokana na hali hiyo, tunapenda kumwomba radhi Wema na familia yake. Siku zote sisi MTANZANIA tumekuwa makini katika kusimamia misingi ya habari za weledi na haki kwa jamii”. Mwisho wa kunukuu

Kitendo cha kumuomba msahani mwanadada Wema ni kitendo cha kiungwana pongezi kwenu Mtanzania natumai Wema kwa uungwana wake atawaelewa.

Shilole Amchapa Makofi Mpenzi wake Nuhu Mziwanda, Steve Nyerere na Mabausa Washindwa Kuamua Timbwili la Shilole

$
0
0
Jumamosi iliyopita ndani ya Tamasha la Kiboko Yao lililofanyika Leaders Club, Gazeti la Makorokocho lilishudia live Msanii Shilole akimchezeshea kichapo mchumba wake Nuh Mziwanda kwa madai kuwa Nuh alikua hataki kuondoka nae eneo la tukio, mchekeshaji Steve Nyerere alijitokeza kuamulia ugomvi na kufanikiwa kumtoa Shilole eneo lile lakini baada ya muda Shilole akarudi na kumdai funguo ya gari Nuh ambaye siku hiyo alionekana kuwa mpole ikabidi mabaunsa waingilie kati na kumtoa kwa nguvu shilole, baadae Nuh alionekana akitoa machozi na Malkia wa Taarabu Khadija Kopa alionekana akim'bembeleza na kumfuta machozi.
sikiliza You Heard ilivyokua ndani ya Kipindi cha Power BreakFast :


Viewing all 104712 articles
Browse latest View live


Latest Images