Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live

Lulu Michael Azua Jambo Kwa T-Shirt Aliyovaa Siku ya Valentine

$
0
0
Mara kadhaa tume kuwa tukiwaona  baadhi ya ndungu zetu ambao Lugha ya malkia inawapiga chenga wamekuwa wakivaa nguo zenye maandishi ambayo huwa hayafai lakini hawa mara nyingi huwa hawajui maana ya kile ambacho kimeandikwa.



Sote tunatambua kuwa watu wenye uelewa kama wa mrembo huyu, Elizabeth Michael ‘Lulu’ hawezi kuvaa ngue yenye maandishi akiwa ajui maana yake au hakubaliani na kile kilichoandikwa. Sasa je mtoto lulu ni kweli  anamaanisha hiki kilichoandikwa hadi kupiga nacho picha na kutupia mtandaoni. Au labda ni dili amepata la kutangaza kinywaji.

Kama sio,ndio tuseme kweli mrembo huyu anapenda kilaji kiasi kwamba haitaji kupendwa na mtu yoyote?

Hebu tuambie wewe umemuelewaje hapa bidada huyu.

Dude Asema Akili Yake ni Mbovu Ndiomana Anashindwa Kuoa

$
0
0
Mwigizaji nguli wa filamu za hapa Bongo, Kulwa Kikumba, amesema licha ya kuishi na mzazi mwenzie kwa zaidi ya miaka kumi, anashindwa kuoa kwa sababu akili yake siyo nzuri.



Akipiga stori mbili tatu na mwanahabari wa GPL, Dude alisema linapokuja suala la kulaumiwa kuchelewa kuoa, anastahili kwani hakuna kitu kinachomsababisha asioe zaidi ya akili yake kuwa mbovu.

“Mimi akili yangu tu bwana ndiyo mbovu, hakuna kitu cha ziada ninachoweza kujitetea, kama kuona ningeoa siku nyingi sana, nashindwa basi tu,” alisema Dude.

GPL

Gadner G Habash 'Ndugu Zangu Nawauliza Nimjibu au Nisimjibu Huyo Anayedhani Yeye Malaika Anayekosewa Yeye tu?'

$
0
0
Udaku Special blog 
Baada ya Mwanamuziki Lady Jay Dee Ambae alikuwa mke wa Gadner G Habash Kufunguka kisa cha kumuacha Habash  Hatimaye Gadner na Yeye amekuja na Hili Hapa Chini:
Hivi ndivyo alivyoandika kwenye ukurasa wake wa Instagram:


Valentine hii naishi kwa hisani ya Mungu Muumba, napendeza kwa hisani ya @robbyonefashion, nakula kwa hisani ya kazi @efm_93.7 Efm, natamba kwa hisani ya @majizzo, nna amani kwa hisani ya washkaji wangu @abdallah_gunda na @edbyamps na lavi davi kwa hisani ya #VJM.
Ndugu zangu na jamaa zangu nawauliza nimjibu au nisimjibu huyo anayedhani yeye malaika anayekosewa yeye tu??

Maswali 10 Kuhusu Magaidi wa amboni Tanga

$
0
0
Hebu tujiulize maswali yafuatayo kwa tafakuri pana:
1. Gaidi alijirushaje pangoni na pingu mkononi? Tuliambiwa polisi walimkamata gaidi mmoja na akawapeleka mapango ya amboni kuwaonesha walipoficha silaha. Eti alipofika mapangoni akajirusha ndani. Kivipi alijirusha na alikua na pingu?

2. Na kama hakuwa na pingu, polisi wanapaswa kujieleza kwanini hawakumfunga pingu gaidi? Mtu mnamshuku kuwa gaidi mnambeba kama bwana harusi? Huyu alitakiwa pingu za mikono na miguu. Au pingu zipo kwa wafuasi wa ukawa wanapoandamana?

3. Kwanini askari wamezuia waandishi kufika eneo la tukio kupiga picha na kuchukua matukio? Wanahofia nini? Waandishi wa kenya wanaingia hadi somalia "kulipo kitovu cha ugaidi" na wanacover story, wakati mwingine wanafanya interview na viongozi wa al-shabab, sembuse hawa vibarua wa amboni? Kwanini polisi wanazuia waandishi?

4. Kwanini polisi wanavujisha rekodi zao za sauti kuhusu hawa waitwao "magaidi wa amboni?". Juzi nilisikiliza clip moja ya sauti kati ya mtu aliyejiita polisi akiongea kwa simu na askari mwenzie aliyeko tanga akimueleza juu ya magaidi hao. Jana imevuja clip nyingine ya askari polisi wakiongea kwa simu juu ya mikakati waliyonayo kuwamaliza hao magaidi. Hivi inaingia akilini mikakati kupangwa kwenye simu? Hakuna radio call? Na hata kama ni simu kwanini wavujishe? Hivi hawaoni kuvujisha ni kuuza ramani kwa adui? Mi naona huu ni usanii tu.

5. Kwanini askari aliyeuawa hajatajwa jina wala waliojeruhiwa? Wanaficha nini? Luteni rajabu mlima alipofia vitani huko drc vyombo vya habari viliripoti na akatajwa majina yake kamili. Baadae akaja kuzikwa kwa heshima kama shujaa aliyefia kwny mapambanno. Vp huyu aliyefia amboni mbona hatajwi? Tunaambia tu, askari mmoja amepoteza maisha. Nani huyo? Kama mnaweza kuwataja wanaofia vitani nje ya nchi huyu wa amboni vp??

6. Hao magaidi wameingia lini huko mapangoni? Na walikua wakifanya nini huko muda wote, mbona hawakuwahi kufanya uhalifu wowote hadi askari walipowatibua?

7. Hao magaidi wanakula nini siku zote huko mapangoni? Au ndio kusema kwenye mapango ya amboni kuna shopping centre kama 'mlimani city?'

8. Halafu mapango ya amboni yanasimamiwa na mamlaka ya makumbusho ya taifa. So kuna watumishi ambao wapo kule mapangoni kila siku. Kuna wahifadhi, kuna walinzi, kuna mkuu wa makumbusho na watumishi wengine. Hivi hawa watu hawakuweza kugundua magaidi walioingia? Au labda wakati magaidi wanaingia watumishi wote walikua likizo?

9. Kwanini chagonja na igp wanapingana hadharani? Voa jana wamemnukuu igp mangu akisema askari aliyekufa alikuwa ktk mapambano na magaidi. Lakini chagonja jana kaongea na media na kusema askari aliyekufa alipigwa ambush. Yani wakati wamemkamata adui wanampeleka huko mapangoni akawaoneshe silaha zilipo; ile kufika tu wakiwa hawajui hili wala lile wakashambuliwa na risasi kutoka mapangoni hivyo mmoja kupoteza maisha na wengine kujeruhiwa. Sasa hapa tumuamini nani kati ya mangu na chagonja?

10. Taarifa za kusikitisha zilizotolewa na jeshi la polisi leo ni kuwa eti baadhi ya magaidi hao wamekamatwa na wengine wametoroka. Tehtehteh kweli hii sinema aliyeandika script atakua cha-gonja maana huyu jamaa ni hopeless kabisa. Wametorokaje? Wamepita wapi? Askari wetu wakiwa wapi? Au kuna barabara huko ndani ya mapango zinapita hadi somalia?

nashauri polisi wajipange upya wanapotunga sinema zao za kujaribu kuwahamisha watanzania kwenye mijadala muhimu. Na wakitaka sinema yao iaminike na watanzania, wamtafute mtu mwenye akili sana awaandikie script, sio kumpa 'kichaa-gonja'

i rest my case.. J.pili njema.


Malisa G.J || your partner in critical thinking.!

No.. This Can't be real...Mkorogo wa Kufa Mtu

$
0
0

This photo has been making the rounds online.. Please I want to believe it's not real. Wow!

Sikiliza na Download Diamond Platnumz Ft. P-Square

$
0
0
Unaweza Kusikiliza ama Kudownload Wimbo mpya wa Diamond Featuring P-Square

Kwa Huyu Zari Diamond Kafika Mwisho wa Reli Embu Ona Wanavyo Kula Raha, Ni Hakunaga Haijawahi Tokea Kwa Mwingine

$
0
0
 Ni ukweli usiopingika kwamba Diamond anampenda sana Zari kuliko wanawake wote aliowahi kuwa nao kimapenzi, Bata wanazokula na kuongozana kila mahali mpaka kwenye show anazopiga Diamond Sehemu mbali mbali ni Ushahidi Tosha kuwa wawili hawa wanapendana kinoma noma...

Wengine wanasema Ujauzito umechangia Mapenzi kuwa Moto moto  kwani Diamond ilikuwa ni Ndoto zake siku moja aje apate mtoto sasa hao wengine walikuwa hawataki kumzalia Diamond...



Dimaond Ameandika haya kwenye Ukurasa wake wa Instagram:

'She had never been to zanzibar so i had to take her there to experience the beauty of Tanzania...
(Alisema hajawai fika Zanzibar, imebidi nimlete ili ajionee uzuri wa Tanzania yetu...) jus #earlierToday #ValentineWeekEndInZanzibar'


Wale wa ndimu Zipo, Najua kina wauma sana!!!

Mungu ni Mkubwa: Mama yake Diamond Arejeshwa toka India......Afya yake kwa sasa inatia Moyo

$
0
0
Mungu ni  mkubwa :Mama mzazi wa Supastaa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Sanura Kassim ‘Sandra’, amerejeshwa Bongo kutoka India ambapo afya yake imetengemaa.
Habari kutoka chanzo cha kuaminika ndani ya familia ya jamaa huyo, kimesema kwamba tayari
 Sandra amesharejea katika hali yake ya kawaida na ndiyo maana akarudi Bongo baada ya kulazwa hospitalini nchini India kwa kusumbuliwa na ugonjwa wa kupooza.

Mwanafamilia huyo alisema kwamba, Diamond na mama yake walirejea nchini wikiendi iliyopita baada ya kufanyiwa matibabu ya kina na madaktari kujiridhisha kwa hali ya juu dhidi ya afya yake ambapo waligundua hali aliyonayo kwa sasa imetengemaa hivyo wakamruhusu kurejea kuungana na familia yake.

Habari zilieleza kuwa kwa sasa bimkubwa huyo yupo fiti na anaendelea na mazoezi ya kawaida huku akimalizia dawa alizopewa na wataalam hao wa afya.

Wahitimu wa JKT Watangaza kufanya Maandamano ya Siku tatu Mfululizo jijini Dar Jumatatu Ijayo.....Lengo ni Kushinikiza Serikali Iwape AJIRA

$
0
0
Vijana waliohitimu mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), wanatarajia kufanya maandamano ya siku tatu mfululizo usiku na mchana jijini Dar es Salaam kuanzia Jumatatu ijayo, kushinikiza kuonana na Rais Jakaya Kikwete kumweleza matatizo ya ajira wanayokabiliana nayo...


Wahitimu hao jana walifanya mkutano katika eneo la Msimbazi Centre, Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Vijana waliohitimu mafunzo ya JKT, George Mgoba alisema kwa muda mrefu wamekuwa wakiomba kukutana na  Rais ili wamueleze matatizo wanayokumbana nayo, lakini wamekuwa wakipewa ahadi za uongo na Katibu Mkuu wa Rais.

“Tumeomba mara nyingi kukutana na Rais na tumekuwa tukiandika barua, lakini hatujibiwi chochote. Tunajua hizi ni njama tu za watu wachache wanaozuia tusionane na Rais,” alidai Mgoba.

Alidai kuwa wameandika barua nyingine na hivi karibuni  Katibu wa Rais aliwapigia simu kuwa wafike Februari 10 ili waonane na Rais na walipofika,  hawakufanikiwa kumuona Katibu huyo.

Akizungumzia  sababu za kutaka kuonana na Rais, alidai ni kutaka kujua hatma yao ya kutopatiwa ajira kutokana na mafunzo ya kijeshi waliyoyapata. “Sisi tumepatiwa mafunzo ya kijeshi na sasa tupo uraiani kwa ajili gani? Hawa wote unaowaona ni askari tayari ” alidai.

Mkutano wao uliwakutanisha pamoja ili kuweka mikakati yao ikiwa ni pamoja na kufanya maandamano ifikapo Jumatatu kama serikali haijajibu, kama itawaajiri au hapana. Walidai endapo jibu halitapatikana, basi watafanya maandamano ya siku tatu mfululizo hadi ombi lao la kumwona Rais lifanikiwe.

Makamu Mwenyekiti, Paral Kiwango, alisema jambo hilo linaonekana kuwa na upendeleo mkubwa, kwani wenzao wa upande wa Zanzibar wote waliomaliza mafunzo ya JKT, wanapatiwa ajira. Alihoji iweje  vijana wa Bara wametelekezwa?

“Wenzetu wa upande wa Zanzibar wakimaliza mafunzo wote wanaajiriwa, lakini sisi Tanzania Bara hakuna anayetujali na kututhamini,” alidai Kiwango.

Kwa upande wake, Katibu wao Liwus Emmaneul amesema kuna fursa nyingi za ajira hapa nchini kama vile TANAPA na sehemu zingine, ambazo wao wanaweza kufanya kazi; lakini wanaoajiriwa kule ni watu wengine wasiokuwa hata na ujuzi, huku wao wakitelekezwa na wakiomba ajira kule hawathaminiwi, kama watu wenye maadili na mafunzo.

Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alipotafutwa ili atoe ufafanuzi juu ya maandamano hayo, simu yake ya mkononi iliita bila majibu.

Shule Binafsi Zatesa Matokeo Kidato cha Nne, Shule za Vipaji Maalumu Zaendelea Kuporomoka

$
0
0
Dar es Salaam. Ufaulu katika matokeo ya mtihani wa kidato cha nne umeongezeka kwa asilimia 10, chini kidogo ya viwango vya Matokeo Makubwa Sasa (BRN), lakini shule za Serikali za vipaji maalumu, kongwe na za seminari zimeendelea kuporomoka.


Katika matokeo hayo, Shule ya Sekondari ya Kaizirege ya mkoani Kagera, iliyoanzishwa mwaka 2010, ndiyo imekuwa kinara ikiwa ni mwendelezo wa mafanikio baada ya mwaka jana kushika nafasi hiyo lakini kwa upande wa shule zenye watahiniwa chini ya 40. Shule iliyoshika mkia ni Manolo iliyopo Tanga, mkoa ambao umetoa shule tano miongoni mwa shule zilizoshika nafasi 10 za mwisho.

Matokeo hayo ni ya kwanza tangu kuanza kutumika kwa mfumo mpya wa upangaji wa Wastani kwa Kutumia Pointi (GPA) ambao unaonyesha shule zote 10 za kwanza ni za binafsi.

Huyu ndio ‘Karani’ wa Benki Anayeuza Figo yake apate mtaji wa Kufanya Biashara

$
0
0
Si ajabu kusikia mtu amejiua kwa sababu tu ya ugumu wa maisha. Wengi wanafikia uamuzi huo baada ya kuhisi hawana msaada mwingine wa kupunguza makali ya maisha. Hata hivyo, kujiua siyo njia sahihi ya kupambana na changamoto.


Hali imekuwa tofauti kwa kijana Armstrong Bangili aliyeahirisha uamuzi wake wa kutaka kujinyonga na sasa anafikiria kuuza figo yake. Anasema anaishi maisha ya tabu tangu alipofukuzwa kazi katika benki moja mwaka 1998.

Kabla ya kutekeleza ‘jaribio la kujiua’ wiki iliyopita, Bangili alisoma Gazeti la Mwananchi, toleo la Januari 3. Alipokutana na habari ya Andrew Chimulimuli kutoka Morogoro aliyetangaza kuuza figo yake kwa Sh90 milioni.

Anasema alipata tumaini kuwa hata yeye anaweza kuuza figo yake na kuondokana na umaskini unaomkabili kwa sasa. Hata hivyo, anakiri kuwa hana elimu yoyote juu ya athari za kutoa figo au jinsi ya kuishi baada ya kutoa figo.

“Nimeamua kuuza figo ili nipate pesa za kufanya biashara. Figo yangu naiuza kwa Sh50 milioni tu, bei yangu ni poa kabisa, siyo kama huyu jamaa,” anasema Bangili huku akionyesha makala ya Chimulimuli ambayo ilimbadili mawazo.

Bangili mwenye umri wa miaka 45 anasema amekuwa akiishi kwa kuombaomba miaka yote, jambo linalowakera watu na yeye pia. Anaeleza kuwa amejaribu kutafuta kazi maeneo mbalimbali lakini amekosa.

Anabainisha kuwa akipata fedha hizo ataanzisha mradi wa kilimo cha mbogamboga na ufugaji wa nyuki. Anaamini kuwa ana uwezo wa kuendesha shughuli hiyo na kujiongezea kipato zaidi ndani ya muda mfupi.

“Yaani nikipata hiyo hela nitanunua shamba la ekari tano huko Bagamoyo au Tegeta, nitaanzisha kilimo cha mbogamboga na kufuga nyuki. Baada ya miaka mitatu mbona nitakuwa bilionea!” anasema huku akicheka.

Kijana huyo anayeishi Sinza, Dar es Salaam anaonekana kudhoofu mwili akisema hiyo inatokana na kula mlo mmoja na wakati mwingine kutokula kabisa. Anasema mbali na kuwa ndugu zake hawana uwezo, pia wamemchoka kwa sababu wamemsaidia kwa muda mrefu.

Bangili anatoka kwenye familia ya watoto wanne, akiwa ndiye mkubwa. Anasema wadogo zake wengine wana maisha yao na wanajimudu kwa kipato kidogo wanachokipata.

Mara nyingi amekuwa akipokea msaada kutoka kwa waumini wa Kanisa la Waadventisti wa Sabato, lakini anasema sasa amechoka kuombaomba, anahitaji kuwa na kazi ya kumuingizia kipato.

“Nataka nikipata pesa nioe, umri nao umekwenda. Nashindwa kuoa kwa sababu sina pesa za kumtunza mwanamke,” anasema Bangili ambaye ana elimu ya kidato cha nne.

Kutana na Mwanafunzi aliyeongoza kwa kufanya vizuri katika mtihani wa kidato cha nne kitaifa

$
0
0
Mwanafunzi aliyeongoza kwa kufanya vizuri katika mtihani wa kidato cha nne kitaifa mwaka jana, Nyakaho Marungu akipongezwa na mama yake Celestina Maro, nyumbani kwao Kitunda Dar es Salaam jana, muda mfupi baada ya Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), kutangaza matokeo ya mtihani huo.

Chanzo cha Kifo cha Baba Mzazi wa Dullysykes na Taarifa ya Maziko yake

$
0
0
Marehemu Mzee Abby Sykes ambaye ni Baba mzazi wa mwimbaji wa Bongo Fleva Prince Dullysykes, alifariki saa 8 mchana February 15 2015 akiwa hospitali ya taifa Muhimbili kwa ajili ya kupatiwa matibabu.


Dullysykes ameongea na millardayo.com ikiwa ni pamoja na kuelezea kitu kilichosababisha umauti wa baba yake ambapo ameanza kwa kusema

"Mzee alikua ana vidonda katika miguu na ndiyo chanzo kikubwa, sumu ikasambaa ikasababisha kifo chake, vidonda vilishindwa kupona kwa ajili ya moshi wa sigara ila zaidi hakuwa na tatizo jingine lolote manake baba yangu alikua strong"

‘Alianza kuugua vidonda miezi minne iliyopita, miezi miwili alikua anavumilia tu lakini miezi miwili ya mwishoni ndiyo vilizidi kumsumbua, mazishi tunategemea kuyafanya February 16 2015 saa kumi jioni kwenye makaburi ya Kisutu lakini safari ya kwenda msikitini tutaanza saa 7 mchana‘ – Dully.

Penzi la Aunty Ezekiel na Mcheza Dansi Moses Iyobo Lazidi Kuchanua Wakati huu wa Valentine..Soma Messeji zao

$
0
0
Wawili hawa Aunty Ezekiel na Moses Iyobo Mapenzi yao si ya kuficha Tena Baada ya kufanya siri kwa muda mrefu na hadi kupeana ujauzito licha ya Aunty Ezekiel kuwa bado katika Ndoa ..
Haya hapa ni maneno walioandikiana kwenye page zao za Instagram siku ya Valentine hapo juzi





Aunty Ezekiel
Happy Valentine Moo akee Baby akee boo boo wa mm Baba akee.....Jaden  Baba wa.....Umbea tyuu Nimemaliza waone kwanza @moseiyobo @moseiyobo @moseiyobo Aunty akee lv u
Moses Iyobo
Kabla Siku haijaisha hawa Ndio washkaji zang. ..THEY JUST SAY 🙉 MY DADY IS THE BEST @auntyezekiel @jadenjerry

Mwanamitindo Flaviana Matata Kuolewa Mwaka Huu

$
0
0
GOOD news kutoka kwa Mwanamitindo wa Kimataifa, Flaviana Matata ni kwamba anatarajia kufunga pingu za maisha Agosti 15, mwaka huu na kijana wa Kichaga anayejulikana kwa jina la Deo Masawe aishie Atlanta, Marekani.

Chanzo makini kutoka Atlanta, kimesema taratibu zote zimeshafanyika na kilichobaki ni siku ifike watu washerekehe.

“Nadhani kwa mwaka huu ndiyo itakuwa harusi ya kwanza ambayo itaacha historia kwa kuwa waoaji wamejipanga kisawasawa,” kilisema chanzo chetu huku mtu wa karibu na Flaviana akithibitisha tukio hilo na kudai litakuwa la kihistoria.

Wema Sepetu Amrudisha Ujanani Bi. Mwenda

$
0
0
Mrembo na mwigizaji wa filamu za Kibongo, Wema Sepetu amemfanyia ‘sapraizi’ msanii mkongwe, Fatuma Makongoro ‘Bi. Mwenda’ kwa kumnunulia simu ya kisasa na kumfanya awe kama kijana.



Wema alimfanyia sapraizi hiyo hivi karibuni kwa kummpeleka Bi.Mwenda katika maduka ya Mlimani City pasipo kumwambia wanakwenda kufanya nini na alipofika, akamnunulia simu hiyo yenye uwezo wa ‘internet’.

“Namshukuru sana Wema maana sikujua tunakwenda kufanya nini Mlimani City, nikashangaa ananikabidhi simu, nimefurahi na mimi kuwa kama vijana wa kisasa, kuingia WhatsApp na Instagram,” alisema Bi. Mwenda.

Picha:Bi Mwenda akiwa katika pozi

GPL

Not So Fast: Collabo ya Diamond na P-Square Bado Haijatoka, Kumbe Wimbo Uliosambaa ni wa Iyanya

$
0
0
Kama umedownload au kutumiwa wimbo unaosemekana kuwa ni wa Diamond featuring P-Square na pamoja na kuusikiliza kwa mara kibao ukashindwa kusikia sauti ya Paul au Peter Okoye, basi sikio lako halikudanganyi – hakuna collabo hiyo.



Wimbo huo unaitwa ‘Marry Me’ ni wa Iyanya ambao kipindi muimbaji huyo wa Nigeria amekuja kwenye Fiesta mwaka juzi, alimpa nafasi Diamond kuingiza kitu kwakuwa alisafiri na producer wake, Tekno aliyetembea na vifaa vya muhimu vya studio. Kwenye wimbo huo Diamond hakuimba serious na infact aliimba freestyle tu, kwa mujibu wa maelezo ambayo meneja wa Diamond ameyatoa kwa Bongo5.

Wimbo original upo kwenye album ya Iyanya iitwayo ‘Desire’ (Iyanya vs. Desire) iliyotoka February 6, 2013. Kwahiyo Iyanya alitaka kutengeneza remix ya wimbo huo ambayo hata hivyo haikuweza kujumuishwa kwenye album hiyo.

Blog kadhaa za Bongo zimeupost wimbo huo kama wimbo wa Diamond aliowashirikisha P-Square kitu ambacho si kweli. Hakuna shaka kuwa hiyo ni collabo inayosubiriwa kwa hamu sana.

Source: Bongo5

Mrembo wa Ukweli Agness Masogange Amdatisha Mwanaume wa South Africa Mpaka Ametangaza Ndoa

$
0
0
Yule mwanadada, ambaye ni video queen na role model wa teenage girls katika ka nchi ka Tanzania tena anayekumbukwa na wengi kwa kusafirisha panadol zenye thamani ya bilioni 6 kwenda South Africa anatarajiwa kuolewa karibuni

Modo Agnes Masogange ameonekana kumdatisha mwanaume aliyefahamika kwa jina la Louis Donald wa nchini Afrika Kusini baada ya jamaa huyo kuposti mtandaoni picha tofauti akiwa amepozi kimahaba na Agnes na kueleza kuwa, huyo ndiye mke wake wa kufa na kuzikana.

Jamaa huyo amekuwa akieneza habari kuwa, Masogange ni ‘mtu’ wake kitendo kilicholifanya Ijumaa ambalo awali lilikuwa na taarifa kuwa, Agnes amechumbiwa na msanii aitwaye Evance Komu limtafute mrembo huyo ili afafanue na alipopatikana alisema:
“Hiyo ishu ipotezee bwana, maswali gani hayo unaniuliza?” alihoji Masogange aliyeonekana kutotaka kuweka wazi ishu zake za kimapenzi.

Nape Nauye Amkubali Edward Lowassa kwa Utekelezaji

$
0
0
Katika kipindi cha asubuhi hii cha clouds360 Nape Mosses Nnauye amekiri haya "CCM ni chama chenye document nyingi zaidi lakini hakina utekelezaji".


Tafsiri ya Maneno haya ni sawa na ya Edward Lowassa aliyoyasema katika bunge kwa serikali ina uzito wa utekelezaji wa walio kubaliana yaani maamuzi.

Hivyo Nape Nnauye ni mhubiri wa siasa za Maamuzi Magumu ambazo kwa sasa zinaongozwa na Edward Lowassa lakini tatizo tuu ni kiburi chake cha kukimbia kivuli chake.

Chuchu Hans: Sifikirii Kuja kuachana na Ray kila Kitu Kinaenda kwa Riziki..Mtasubiri Sana

$
0
0
Mpenzi wa muigizaji wa filamu, Vincent Kigosi aka Ray, Chuchu Hans amekanusha uvumi kuwa amepigwa chini na Ray na kudai kuwa hategemei kama watakuja kuachana.
Chuchu amekiambia kipindi cha Take One cha Clouds TV kuwa wameamua ...
kubadilisha aina ya maisha yao kwa kutopiga picha hovyo na kuweka mitandaoni.

“Sifikirii hicho kitu kuachana na Ray kiukweli sifikirii na kila kitu kinaenda kwa riziki na kama riziki yangu itakuwa imeisha basi nitaikubali hali. Lakini sifikirii hicho kitu kabisa,” alisema Chuchu ambaye naye pia ni muigizaji wa filamu.

Mtasubiri Sana..
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live




Latest Images