Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

TCRA Yakanusha Kuwa na Mpango wa Kufungia Mitandao ya kijamii

$
0
0
Baada ya Gazeti Moja Kubwa Kuandika kuwa TCRA ipo Mbioni kufunga Mitandao ya Kijamii inayotumika Vibaya ..TCRA wameibuka na Kusema :

'TCRA haina mpango huo na haikusudii kufanya hivyo na haina Mamlaka ya kufungia mtandao uliosajiliwa nje ya Tanzania.

Tumejikita zaidi kutoa elimu kwa umma juu ya matumizi mazuri ya mawasiliano. Wanaotumia mitandao vibaya ni wachache kuliko wanaotumia vizuri

Habari hii sio kweli hakuna wakati wowote ambapo yeyote katika mkutano huo alizungumzia kufunga mitandao ya kijamii. Kwa mtu anayefahamu teknolojia anaelewa madhara na hasara ya kufanya hivyo.

Waandishi wa habari wanaaswa kuwa makini wanapoandika habari kuepusha kutoa habari ambazo sio sahihi na zinazoweza kuleta mtafaruku kwa jamii'

Udhaifu wa Wanaume wa Kibongo Wawapo Kitandani na Mwanamke

$
0
0
Hapa chini ni baadhi tu ya udhaifu wa wanaume wa kibongowawapo kitandani.

1. Kudandia haraka haraka bila kumuandaa mwanamke

2. Hakuna lugha ya mwili kutwanga na kumaliza kisha kugeukia ututani nakukoroka.

3. Harufu mbaya ya kwapa au kinywa, yaweza kuwa ya pombe, sigara au kinywakichafu.

4. Kumlazimisha mwanamke kulamba koni bila ridhaa yake

5. Kujisafisha na shuka baada ya kumaliza

6. Kutupa kondom kwenye sakafu baada ya kumaliza

7. Kupiga makelele na kuuliza maswali mengi yasiyo na maana

8. Kutohakikisha kama mpenzi wake amefika kileleni au ameridhika.

9. Kuomba tendo kama vile anaomba kibarua cha kulima hakuna lugha ya kubembeleza

10. Kutosema ahsante baada ya tendo, anamalizana kukimbilia kuvaa

Kamikaze Ampiku Demu Bob Junior ! Picha na Video Wakifanya Yao Kitandani zavuja..

$
0
0
Mwanamuziki Kamikaze amezidi kupigilia msumari beef aliyonalo na Bob Junior kwa kumchukulia Demu..Demu huyo mwigizaji wa Bongo Movies anayejulikana kwa Jina la Sabby amenaswa sehemu mbali mbali akijivinjari na Mwanamuziki Kamikaze huku Bob Junior akiachwa kwenye mataa.. Picha na Video wakiwa faragha zimevuja mtandaoni zikionesha mahaba makubwa kati yao .... Angalia Video Hapa ujionee.....


Snura Adaiwa Kupora Mume wa Davina

$
0
0
Staa wa muziki wa mduara, Snura Mushi ameingia katika tuhuma nzito akidaiwa kutoka kimapenzi na mume wa rafiki yake ambae ni staa wa Bongo Movies, Halima Yahya ‘Davina’.

Kwa mujibu wa chanzo cha GPL , kwa kipindi kirefu, Snura amekuwa akionekana nyakati za usiku akiwa na mume wa Davina, wakati mwingine mwanaume huyo anaenda nyumbani kwa Snura au wawili hao kuzungumza kwa muda mrefu ndani ya gari la mwanaume huyo.

“Yaani mastaa wa Bongo bwana, wanapenda sana kuchukuliana mabwana. Huyu Snura anatoka na mume wa mwenzake. Mume wa Davina huwa anakuja nyumbani kwa Snura mara kwa mara hasa nyakati za usiku.

“Wakati mwingine anakuja na gari na kupaki jirani na nyumbani kwa Snura kisha wanakaa kwenye gari kwa saa kibao. Snura anamzunguka rafiki yake,  fuatilieni mtaujua ukweli,” kilisema chanzo chetu.

Baada ya kuunyaka ubuyu huo, GPL iliamua kuingia mzigoni kwa kumsaka Snura na alipopatikana, akasomewa tuhuma zake ambapo katika hali ya kushangaza, msanii huyo, alimwaga chozi.

Alipomaliza kulia, Snura alianza kufunguka ukweli wa kisa hicho ambapo alikiri kuwa ni kweli mume wa Davina alikuwa akienda nyumbani kwake mara kwa mara lakini ilikuwa ni kipindi ambacho Davina na mwanaume huyo walikuwa wametibuana kiasi cha msanii huyo kufungasha virago vyake na kutokomea kusikojulikana.

“Mimi nilikuwa nahangaika kuwapatanisha kwa sababu walikuwa kwenye mgogoro mkubwa, mumewe akawa ananiomba nimsaidie kumbembeleza Davina arudi wayazungumze na kumaliza matatizo yao ili kuokoa ndoa yao isivunjike.

 Davina nae alitafutwa ili kujua kwa upande wake analizungumziaje sakata hilo ambapo msanii huyo alitema nyongo. Hebu msikie:

“Watu wengine hawana kabisa kazi za kufanya, yaani walikuwa wanataka kunigombanisha na shosti wangu lakini wameshindwa. Ni kweli na mimi niliwahi kuletewa taarifa kwamba mume wangu anaonekana nyumbani kwa Snura usiku lakini ilikuwa ni kipindi ambacho nilikuwa kwenye matatizo na mume wangu.

“Kiukweli Snura hawezi kufanya hivyo kwa sababu yeye ndiye aliyepigania ndoa yangu isivunjike. Isitoshe sisi tunaishi kama ndugu, watoto wangu huwa wanaenda kushinda kwake na wakati mwingine huwa namtuma mume wangu akawachukue kwa hiyo hata kama wanamuona kwake, siyo kwa nia mbaya, watu aache uchonganishi,” alisema Davina.

Kimenuka Siwena na Nay wa Mitego, Nay Afunguka ' Sina Mke Sijaoa na sina mahusiano ya kimapenzi na Mwanamke yoyote Yule'

$
0
0
Msaniii Emmanuel Elibarick alimaarufu kama Mr Nay ameonesha dalili ya wazi kuwa hana mpango tena wa kuwa katika mahusiano na Mchumba wake huyo Siwema ambaye amezaa nae mtoto wa kiume aitwae Curtis miezi kadhaa iliyopita.


Kupitia ukurasa wake wa Instgram Nay wa mitego siku mbili zilizopita aliweka post ambayo ilikuwa inasema kuwa kwa sasa ana watoto watatu na ana mapenzi ya kweli na watoto wake lakini hana mpango wala hana mahusiano ya kimapenzi na mama wa watoto wake hao bali anawaheshimu wanawake hao kama wazazi wenzake.

"Mr_Nay Baba wa watoto watatu... Sina Mke I mean Sijaoa na sina mahusiano ya kimapenzi na Mwanamke yoyote Yule... Kati ya niliozaa nao. Nawapenda watoto wangu nawaheshim mama zao..SingleBoy am in love with my son and daughters... Rishma, Curtis na Munie"
Kwa upande wake Siwema ambaye ni mama wa Mtoto wa Nay juzi aliweka picha ya Mzazi mwenzake na kuwataka mashabiki zake wafunguke lolote juu ya picha ile ila Comment nyingi zilionesha kuwa watu hao hawapo sawa au hawapo pamoja kwa sasa kama ambavyo baadhi zinasema.

"kaysamira: Siwema Mimi nakupenda siwez kukujudge chochote sababu mapenzi upofu namuomba Mungu akupe jicho la tatu na uweze kusonga mbele,mambo kama hayo hutokea na yanapita na kama yeye hakutaki usijali kuna wanaume wengi tu wanaopenda kuwa na mtu kama wewe tena wazuri kuliko yeye labda ndio chance mungu kawapa ili uweze kukutana na prince charm wako lakini kama umeandikiwa kuwa na baba Curtis hakuna mwenye kupinga hilo lakini aache kuwadhalilisha na kutumia udhaifu wenu kama mwanamke inauma anachezea sana hisia zenu"
"Augustinasimon37: Hakuna wa kumjudge mtu hapa, mapenzi ni ya wawili tu. kabla hakuzaa walikuwa sawa wakipendana iweje sasa ndio maana tunaumia, tunawaombea wasiachane, kibinadam sio vizuri. Nakupenda bure Siwema mpende mtoto wako ndio kila kitu kwako"
Lakini pia Nay wa Mitego leo amepost picha akitoka Mwanza huku akiwa na Mwanae Curtis akimnywesha Maziwa ya kopo hali ambayo inaonyesha wazi kuwa huenda mtoto huyo yupo chini ya himaya ya baba na si mama tena kitu ambacho kinaweza kutoa majibu ya wazi kuwa watu hao huenda wameachana.

My Husband Doesn't Know How To Handle Me In The Bedroom

$
0
0
This is one issue causing serious wahala in many young marriages today. Read this one's story:

 I don't enjoy s*x with my hubby because of many reasons which I cannot state here. Its really frustrating. I have tried to subtly give him clues so I wont hurt his feelings but he never learns and would release even before I finish removing my pant.

 My elder sister bought a rabbit vibrator from the UK for me and its out of this world. I am a house wife and I now see myself looking forward to my husband's leaving in the morning so I can indulge. My problem now is that I cant seem to get enough. I cum like 2/3 tyms every day before he comes home from work.

My orgasm always knocks me out and I tend to deeply sleep off immediately. My kids are home on mid term break and I had to chase them out of my room yesterday so I can indulge. I slept from 11am to almost 3pm and my kids were hungry.

 I was so ashamed of myself when I woke up and the thing was still in my veejay. I feel as if my new rabbit is beginning to change me into something else. I rarely have strength to do any thing these days and my hubby is beginning to complain though I pretend to be sick to get him off my back. I hid it inside one old long shoe but I am never comfortable.

Whenever hubby goes to the wardrobe my heart jumps into my mouth. I really am very confused about this thing. It has taken me to heaven yet has stolen my sanity and peace of mind. I have thought about throwing it away but I really don't know if I can cope without it.

Please what do I do? 

Mwanafunzi Atekwa, Abakwa na Kuuwawa Kinyama..

$
0
0
DUNIA imekwisha jamani! Mwanafunzi wa kidato cha tatu katika Shule ya Sekondari ya Mabibo, Dar, Irene Said (15) ametekwa, amebakwa na kuuawa kikatili kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali sehemu mbalimbali za mwili huku ikidaiwa kuwa, kijana mmoja asiyejulikana alifika nyumbani kwao, Kigogo Luhanga na kutaka kiroba na mtu mmoja waongozane akabebe ndizi.

Akizungumzia tukio hilo la kusikitisha sana, mama mdogo wa marehemu, Doto Lucas alisema:
 “Siku ya tukio ambayo ni Alhamisi iliyopita (Machi 12), kijana mmoja ambaye hakuna aliyemfahamu alikuja hapa nyumbani na kumtaka mtu mmoja na kiroba ili akachukue ndizi ambazo kuna mtu aliagiza ziletwe.

“Marehemu ndiye aliyekuwa karibu akijisomea baada ya kutoka shuleni. Mtu mkubwa aliyekuwa nyumbani muda huo ni bibi wa marehemu ambaye ni mtu mzima hivyo alimwambia Irene aongozane na mtu huyo akachukue mzigo akijua uko jirani kwa mujibu wa mtu huyo.

“Baada ya muda, yule kijana alirudi akiwa peke yake na kusema anataka chombo kingine cha kubebea kwa kuwa kile kiroba kilikuwa hakitoshi.“Bibi mtu alimuonesha ndoo kwa vile hakukuwa na kiroba kingine, alipoitwaa na kuondoka nayo ndiyo  hakurudi yeye wala Irene.

“Baada ya kuona muda unayoyoma bibi wa marehemu alianza kupata wasiwasi. Ndipo akatutaarifu kilichotokea nyumbani na sisi tukaanza kumsaka Irene na kijana yule.”

KWA NINI WALIMWAMINI KIJANA HUYO?
“Sisi tuna makaka zetu wakubwa ambao wana kawaida ya kutuagizia mizigo mbalimbali kwenye magari, kwa hiyo tuliamini ni wao. Lakini tulipowapigia simu na kuwaeleza tukio hilo wote walikanusha kuwa si wao na kushangaa.

“Kauli hiyo ilianza kututia shaka zaidi hivyo tulianza kuwasiliana na ndugu na jamaa ambao wote waliishia kushangaa. Tukaenda kutoa taarifa Kituo cha Polisi, Kigogo na kuanza msako wa kumsaka binti yetu pamoja na mtuhumiwa.”

IRENE APATIKANA AKIWA AMEUAWA
Mwanamke huyo anaendelea kusimulia: “Kesho yake asubuhi  (Ijumaa) tukasikia kuna binti amekutwa ameuawa kinyama kwenye Bonde la Mto Msimbazi, eneo la Sukita. Tulipatwa na mshituko, tukaenda na kuukuta mwili, tulipoukagua tuligundua ni Irene.

“Alikuwa ameharibiwa vibaya. Sehemu za mwii alikuwa na damu, alichomwa na kitu chenye ncha kali. Kwa vyovyote yule kijana alikuwa na wenzake, walimteka huko mbele ya safari na kumbaka kabla ya kumuua. Inauma sana jamani.”

Marehemu Irene ambaye katika mazishi yake wanafunzi wenzake walikuwa wakilia sana, alizikwa Jumamosi iliyopita katika Makaburi ya Mburahati, Dar.

Katika ibada hiyo, Katekista aliyesaidiana na paroko kuendesha ibada hiyo aliyetajwa kwa jina moja la Henjewele aliwalaani vikali walioshiriki kufanya unyama huo na kuwataka wafanye toba haraka iwezekanavyo na kumrudia Mungu wao vinginevyo laana na moto wa milele utawaangukia.
Mungu ailaze roho ya marehemu Irene mahali pema peponi- Amina.
Globalpublishers

Agness Masogange Ndio Mwanamke Mwenye Makalio Mazuri Afrika Mashariki..Ushindi Huo Wamshitua

$
0
0
MODO maarufu Bongo, Agness Gerad ‘Masogange’ ameshtushwa na ushindi wa makalio yake baada ya kutojua kama ametajwa kuwa ni mwanamke mwenye makalio mazuri Afrika Mashariki.

Masogange alishinda nafasi hiyo kupitia utafiti uliofanywa na mtandao wa Media Take Out ambapo kwa kutumia vigezo vyao, walimwanika Masogange kuwa ndiye mwanamke pekee mwenye makalio bomba wakidai amejengeka vizuri zaidi.
“Daah! Mimi mwenyewe nilikuwa sijui, nashukuru kama wao wameona mimi ndiyo mwenye kiungo hicho muhimu cha kuvutia na bora kwa wanawake wengine wote,” alisema Masogange ambaye kwa sasa amehamishia makazi yake nchini Afrika Kusini.

Zitto: 'Kipengele kilichotumika kunifukuza Chadema kilitungwa kwa ajili yangu..'

$
0
0
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, amevunja ukimya baada ya kuzungumzia tuhuma mbalimbali ambazo zimekuwa zikielezwa juu yake, ikiwamo usaliti ndani ya chama chake na hatima yake ya siasa baada ya kutimuliwa.

Katika mahojiano haya, zitto anatoa maelezo yote juu ya tuhuma dhidi yake.
Swali: Mwaka 2009, ulitaka kugombea uenyekiti wa Chadema, uamuzi huo ulikuwa ni wako mwenyewe ama kuna watu nyuma yako walikushawishi kufanya hivyo?
Jibu: Chadema nilivyoingia kwenye uongozi Makao Makuu, kulikuwa na wabunge watano, wanne wa kuchaguliwa na mmoja wa viti maalumu.
Nilivyoingia pale nilipewa nafasi ya kuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi na wa Mambo ya Nje kwa ajili ya kujenga mahusiano ya chama chetu na vyama vingine vya kimataifa, hiyo kazi niliifanya kwa ubora na mpaka sasa uhusiano wote ya Chadema na vyama vya nje, niliyajenga mimi.
Mwaka 2005 niliandika mkakati wa uchaguzi tukapata majimbo mengi zaidi, tulipata asilimia nane ya kura hivyo tukapata wabunge sita wa viti maalumu.
Kabla ya hapo Chadema ilikuwa ikizidiwa hata ya UDP, pamoja na kwamba kilikuwa na wabunge tangu 1995.

Wabunge wake hawakujitanabaisha kama wapambanaji wa misingi ya kitaifa, tulivyoingia (Bungeni) sisi na kina Ndesamburo (Mbunge wa Moshi mjini, Philemon Ndesamburo), DK Slaa (Katibu Mkuu wa Chadema Dk. Willibrod Slaa), tukaanza kubadilisha hali hiyo.
Tukaanza kupambana na ufisadi, kabla ya hapo Dk. Slaa alikuwa bungeni kwa miaka 10 lakini hakuwa machachari kama ilivyokuwa kuanzia 2005.

Alivyoingia mwaka 2005 ndipo tukaanza na hoja kama zile za EPA na Buzwagi.
Baada ya hapo mimi na kina Profesa Kitila Mkumbo tukaona kuna haja ya kubadilisha chama, mwaka 2009 nilivyotaka kugombea uenyekiti nilikuwa na nia ya dhati kabisa.

Ndani ya Chadema kuna watu wanaamini katika uliberari, kama biashara na mtaji, hawa ni watu kama kina Mbowe (Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe), sisi tunaamini katika demokrasia ya jamii. Hapa kwenye kundi hili unatukuta mimi kina Profesa Mkumbo, Profesa Mwesiga Baregu, na wenginr, tulitaka kukitoa chama kwenyel mrego wa kihafidhina kwenda kwenye ujamaa.
Hata hivyo wazee walinitaka niache kugombea nikaacha, ni kweli ukiangalia chanzo cha ugonzi ni mwaka 2009, ila mimi sikudahani kama kitu kile kingeleta chuki, nilidhani mambo yangeishia pale.

Swali: Nini kilifanya iwe vigumu kumaliza tofauti zako na Chadema?
Jibu: Mara zote nimekuwa nikiwaambia Chadema kwanza waniambie kosa langu ni nini, Ndesamburo aliwahi kunifuata ili tuyamalize, Wenje naye alinifuata na siku kutaka tuyamalize, lakini upande mwingine viongozi nao wanasema yao kwa hiyo ni undumilakuwili tu kila mahali.

Swali: Kuna baadhi ya watu wanaamini kuwa wewe na Mbowe mna ugomvi binafsi, tofauti na vile ambavyo watu wanadhani kuwa mnagombea uongozi. Wengine wanasema uliwahi kutoa siri zake, juu ya kuwa na nyumba Dubai, madai haya yana ukweli?
Jibu: Kama Mbowe ana mali nje mimi kwa kweli sijui, mimi nilitoa hoja ikaundwa kamati ya uchunguzi, kama ilimkuta ana mali nje sijui.
Hata hivyo kama ana nyumba, ama mali nyingine ni kwa nini auogope? Kama una nyumba Marekani, Afrika Kusini, Dubai ama wapi hiyo siyo tabu, ilimradi kwenye tamko la maadili (Baraza la Maadili ya Viongozi wa Umma) uwe umesema kuwa unazo na TRA (Mamlaka ya Mapato Tanzania) wajue umepata wapi hizo fedha.

Swali: Lakini inadaiwa kuwa ulikaa na Mbowe wewe akakueleza kama mtu wake wa karibu kuwa ana nyumba Dubai na wewe ukatoa hizo habari kwa umma na ndicho kilichomuudhi.
Jibu: Mimi sijawahi kukaa na Mbowe kuzungumza hayo mambo. Sina ugomvi binafsi Mwenyekiti wa Chadema, siku zote nimekuwa nikimchukulia kama kaka, ndiyo maana hata akinishambulia nimekuwa nikijitahidi kukaa kimya.
Mwanzoni kabisa yeye alikuja chuo kikuu kunifuata, mwanzoni mwa mwaka 2001, nikiwa mwanachama wa Chadema lakini siyo kiongozi, yeye akiwa Mbunge wa Hai, alikuja akaniambia naomba tuzungumze utusaidie kwenye chama.

Alikuwa anataka kufanya mabadiliko ya katiba ya chama, nikatumia nafasi yangu ya uanaharakati wa wanafunzi na uwezo wangu wa uchambuzi tukafanya hivyo tulivyofanya.
Tukabadilisha chama mimi na yeye, mabadiliko makubwa ambayo yanaonekana hivi sasa Chadema ni kazi ambayo tulifanya mimi na yeye, hata gumboe mwaka 2009 niliona ni jambo la kawaida. Kilichopo ni mitizamo tofauti ya namna ya kuendesha siasa, na tofauti hizo zimesababisha yatokee yaliyotokea.
Wakati mwingine nikikaa peke yangu huwa yangu na kujiuliza, huwa sioni msingi wa ugomvi wangu na chadeama, naona ni ugomvi tu wa madaraka na juhudi za watu kutaka kuondoa wengine katika ulingo.
Katika mazingira kama hayo ni rahisi kutoa tafsiri kwamba kuna ugomvi binafsi.

Yeye (Mbowe) alikuja hapa Kigoma akafanya mkutano wa hadhara akanitukana, akasema alinisaidia sijui gari, sijui nini, yaani alikuja nyumbani kwetu kunisimanga.
Nikasema huyu mtu ananisimanga, kwanza ni mambo ya kishamba, kwamba unamsaidia mtu halafu unakuja kumsema, kwanza kuna vitu ambavyo mimi mwenyewe nimemsaidia labda kifedha ama siyo fedha, na tunajua kati ya mimi na yeye.

Siyo vitu naweza kuibuka nikasema nilimdharau sana kwa kweli, na juzi nimemsikia huko Shinyanga akisema kuwa hawezi kukaa na kuongea na mimi kwamba ni msaliti na mambo kama hayo. Huu ni undumilakuwili kwa kweli kwa sababu huku anatuma watu kwamba kina Ndesamburo (Philemon Ndesamburo), kwamba tuongee tuone namna ya kuyamaliza haya mambo alafu yeye huku nyuma akikaa anaongea yake.
Kwa hiyo binafsi naamini sina ugomvi naye sanasana ni tofauti za kiitikadi. Mimi na yeye tumekaa Bungeni miaka 10, naomba tu watu watupime.

Katika miaka yangu 10 ni hoja gani nimezisimamia na yeye ni zipi amezisimamia.
Mimi siku zote siasa zangu ni hoja na issue za kusaidia wananchi na nafurahi ninavyosimamia vitu na kuona vikienda.

Swali: Mara kadhaa viongozi wa chama chako wamekuwa wakikutuhumu kwa kusaliti chama, na kwamba kwa upande mmoja unatumiwa na CCM na upande mwingime usalama wa taifa, ni kwa nini ushutumiwe kwa tuhuma kama hizo?
Jibu: Kwenye siasa ukitaka mwanasiasa amalizike ni kumpa hizo tuhuma. Lakini waulize (Chadema), ni taarifa zipi zinapelekwa kwenye usalama wa taifa, watu haohao walisema siendi kwenye vikao vya chama, wala ofisini, sasa hizo taarifa ninazozipeleka ni zipi wakati kwenye vikao wala ofisini siendi? Mtu anayepeleka taarifa ni yule asiyekosa kwenye vikao. Anahudhuria kila kikao ili apate taarifa za kupeleka.

Lakini pia angalia, mwaka 2010 nilitoa taarifa ya kumuomboa Waziri Mkuu, hoja ile ikaungwa mkono kwa kusainiwa na wabunge wa pande zote, hivyo ikasaidia kuondoa baadhi ya mawaziri waliokuwa na shutuma.
Mwaka 2013 kulikuwa na Operesheni Tokomeza. Ripoti ya Kamati ya Bunge iliyokuwa imewasilishwa ilikuwa inamtaja waziri mmoja tu, lakini nilisimama na kujenga hoja mawaziri wengi tu wakaondolewa.

Mwaka 2014 nimepeleka hoja ya Escrow na nikaisimamia, mawaziri wameondoka, serikali imetikisika, sasa mtu anayetumika na Chama Cha Mapinduzi kwa nini aiangushe serikali ya chama hicho mara tatu ndani miaka mitano? Mtu ambaye anatumika inawezekanaje alete mjadala utakaoingusha serikali?
Ndiyo maana sipotezi muda kujibizana na propaganda za aina hiyo, watuambie ni taarifa gani zilipelekwa huko zikawaathiri?

Swali: Baada ya Mahakama kutoa uamuzi wake na Mwansheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lisu kutangaza kuwa umefukuzwa uanachama kwa kuwa kukishitaki chama ni kujifukuza katika chama moja kwa moja, tangu ukiwa kiongozi wa chama uliwahi kukitilia shaka kifungu hicho kwa kuwa hivi sasa umeonekana kukilalamikia.

Jibu: Hiki kifungu kipo kwenye kanuni na wala siyo Katiba, kilitungwa mwaka 2013. Mwaka huo kuna mabadiliko fulani fulani yalifanywa. Mabadiliko yale yalikuwa na malengo fulanifulani ikiwamo kulenga watu fulanifulani.
Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri, mamlaka ya kutoa haki iko kwenye chombo kimoja tu nacho ni Mahakama, kila raia ana haki ya kwenda mahakamani kudai haki, unaposema mwananchama wa Chadema akienda mahakamni amejivua uanachama ina maana wewe huitambui Katiba ya Jamuhuri.
Hii ina maana kama mwanachama amekipangisha chama, na chama kikashindwa kulipa kodi, yule mwanachama akienda mahakamani amejivua mwenyewe uanachama kwa kuwa haruhusiwi kwenda mahakamani.

Hicho ni kipengele ambacho hakikupaswa kuwap, Wanachama wa Chadema waende mahakamani kushtaki kipengele hicho ili kitangazwe kuwa siyo halali.
Chama kinachopambana kushika dola hakipaswi kuwa na vipengele kama hivi. Ila yote kwa yote hiki kipengele kimewekwa mwaka 2013 na mwaka 2015 kikatumika kwangu, ni wazi kilitungwa kwa ajili yangu.

Swali: Baada ya kufukuzwa Chadema, ni nini hatma yako kisiasa?
Jibu: Nina ziara ya kuzunguka na wananchi wa jimbo langu kuangalia jinsi ya kuwatumikia, leo (jana) nawaaga rasmi kwamba sintakuwa nao baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka huu, lakini ni nini kinachokuja baadaye ya hapo tutakijua vizuri wiki ijayo (wiki hii).
Hatujajua kama Chadema wameandika barua kwa Spika ili kunitangaza kuwa jimbo liko wazi, kama ndivyo tutakaa kujua ni nini cha kufanya.
Ilipaswa baada ya kesi kwisha taratibu zifuatwe, mpaka sasa sijapata taarifa zozote za kufukuzwa ndiyo maana nasema mpaka wiki kesho iishe tutajua, nitakuwa na nia ya kuendelea kutumikia kwenye jimbo lolote Oktoba.

Swali: Una mpango wa kujiunga na ACT?
Jibu: Tusijaribu kuvuka mto kabla hatujafika pa kuvukia.
Swali: Vipi hukumu ya Mahakama Kuu juu ya kesi yako na Chadema?
Jibu: Kwenye kazi yangu kuna miguu ya watu wengi naikanyaga, taarifa yangu ya Escrow nimewakanyaga mpaka mahakama. Kwa hiyo yawezekana kabisa mahakama iliona hapa ndipo kwa kunikanyaga, ama yawezekana kabisa ni taratibu.

Inaonekana kuna uhusiano wa karibu wa mahakama na wanasheria wa Chadema, sisi tulisikia kwenye vyombo vya habari kwamba hukumu ya kesi yetu imetolewa.
Hata baada ya hukumu hiyo, tulijaribu kufuatilia ili kupata hukumu, kwa siku mbili tulizungushwa, siku ya tatu tukaambiwa kuwa jalada lipo kwa jaji kiongozi.
Lakini mimi bado nina imani kwamba wakuu wa mahakama watachunguza jambo hili na kuona kama kuna cha kufanya.

Sisi tulipaswa kuitwa mahakamani, lakini hatukuitwa, kuna taratibu za mahakama hazikufuatwa, tuna imani kuwa viongozi wa mahakama watachunguza kama kuna suala la rushwa katikati hapa ama kuna nini.
Lakini pia hali hii imenifanya niwe na kiu zaidi ya kuhakikisha nikipata tena nafasi nitafanya operesheni kwenye mfumo wa mahakama kwa kuwa umekuwa na malalamiko sana ya kuwaumiza wananchi.

Aunty Ezekiel Anena Mazito Bifu la Kajala na Wema Sepetu

$
0
0
STAA anayefanya vizuri kwenye tasnia ya filamu Bongo, Aunt Ezekiel amefunguka kuwa anatamani aone mastaa wawili ambao wana bifu kali, Wema Sepetu na Kajala Masanja wanamaliza tofauti zao kwani maisha ni mafupi.
Wema na Kajala enzi wakiwa bado mashosti.
Akizungumza na gazeti hili, Aunt alisema kati ya mabifu ambayo angependa yaishe ni la Wema na Kajala kwani wapo wasanii wamefariki dunia wakiwa na bifu huku wale waliobaki ambao walikuwa na mabifu nao wakitamani waamke walau mara moja wamalize tofauti zao lakini haikuwezekana.

“Jamani maisha haya ni mafupi sana na tunatakiwa kujifunza kutoka kwa wenzetu tuliokuwa nao lakini sasa hivi hawapo tena, natamani sana Wema na Kajala wamalize tofauti zao  kwani ipo siku watakuja kujuta siku ambayo mmoja wao atakapokuwa hayupo japo siwaombei ila hilo ndilo tamanio langu kuwaona wakizungumza,” alisema Aunt.

Waraka wa wazi kwa Waheshimiwa Tundu Lissu, Mdee na Wenje Kufuatia Kufukuzwa Kwa Zitto Chadema

$
0
0
Mwishoni mwa juma lililopita uliibuka mjadala juu ya kauli za baadhi ya viongozi wa juu wa CHADEMA kuhusiana na kufutwa uanachama kwa Mbunge wa Kaskazini Mhe.Zitto Kabwe.

Mjadala mkubwa ulikua juu ya kauli za wabunge watatu wa CHADEMA ambao ni Mhe.Tundu Lissu, Halima Mdee na Ezekia Wenje.

Mjadala ulianza baada ya Lissu kueleza msimamo wa Katiba juu ya hatma ya mwanachama aliyefungua kesi mahakamani dhidi ya chama na akashindwa. Je nini kinatokea?

KWANINI LISSU ALIKUA SAHIHI.

Lissu alieleza msimamo wa Katiba. Alichokisema Lissu si mawazo yake. Ingekuwa mawazo yake bila shaka hata mimi ningempinga, lakini kwa kuwa ni msimamo wa katiba huwezi kupinga unless uombe Constitutional amendment kwa taratibu zilizowekwa.

So hata kama angesema mtu mwingine ambaye si Lissu angesema kauli ileile aliyoisema Lissu kwamba "ukifungua kesi mahakamani dhidi ya chama na ukashindwa unakuwa umejifukuzisha uanachama mwenyewe".

Kwa hiyo sio mawazo ya Lissu, ni msimamo wa katiba. Yani hata angesema Mbowe, Dr.Slaa, Mnyika au mwingine yeyote angesema vilevile alivyosema Lissu.

Wapo wanaohoji kwanini Lissu aseme na sio Mbowe ambaye ndiye mwenyekiti? Jibu lake ni kuwa masuala ya kisheria ndani ya chama yanaweza kusemewa na mwanasheria wa chama. Na wanasheria wa chama ni pamoja na Lissu, John Mallya, Mabere Marando na wengineo.

Sasa nashangaa wanaohoji uhalali wa Lissu kuongelea msimamo wa katiba ambalo ni jambo la kisheria. Mmesahau kuwa Lissu ni mwanasheria wa Chama? Sasa kama mnajua Lissu ni mwanasheria wa chama mnashangaa nini anapotoa ufafanuzi wa kisheria? Au mlitaka mambo ya sheria ayaongelee mlinzi wa Dr.Slaa?

Wengine wamehoji kwanini baada ya ile hukumu hakikukaa kikao kikaafikiana kumfukuza Zitto badala ya Lissu tu kusema. Hawa ni wale ambao hawajui hata wanachozungumza. Either ni watu wa vyama vingine so hawaijui katiba ya CHADEMA au ni wapenzi wa chadema lakini hawapendi kusoma.

Sasa kwa kuwasaidia ngoja niwaambie hivi. KATIBA ya CHADEMA ya mwaka 2006 inasema mwanachama yeyote atakayekipeleka chama mahakamani na akashindwa anakua amejifukuzisha uanachama mwenyewe. Hii ina maana kuwa baada tu ya hukumu kutoka automatically yeye sio mwanachama tena.

So bila haya Lissu kuongea lolote, Zitto alishajua yeye sio mwanachama tena. Thats legal stand.

Katiba haikusema hukumu ikishatoka kamati kuu ikae itoe tamko NO. Katiba inasema hukumu ikitoka kama umeshindwa kesi fungasha virago katafute chama kingine.

Kwa hiyo hata kama chama kisingesema lolote. Yani Lissu angekaa kimya na viongozi wengine wote wakakaa kimya, Zitto angeondoka tu.. maana hakuna namna nyingine. Na ungemfuata Zitto umuulize akaamua kuwa honesty angekuambia wazi kuwa kikatiba amejifukuza uanachama mwenyewe.

Kwa hiyo kama kuna tatizo, basi tatizo halipo kwa Lissu au Mallya au mwanasheria yeyote wa Chadema. Kama kuna tatizo basi Tatizo lipo kwenye Katiba ya chama.

Na ikumbukwe wakati kipengele hicho cha katiba kinaundwa mwaka 2006 Tundu Lissu hakuwa hata mwanachama wa CHADEMA (alikua Nccr Mageuzi), so huwezi kuhoji legitimacy yake kwenye hicho kipengele.

Labda ambaye anaweza kuhojiwa kwanini kipengele hicho kiliwekwa na akatoa maelezo mazuri ni Mhe.Zitto Kabwe ambaye wakati marekebisho ya katiba yanafanyika mwaka 2006 yeye alikuwa mjumbe wa Kamati Kuu.

Kwa hiyo yeye ndiye anayeweza kutupa logic ya hicho kipengele. Walikiweka ili iweje? Walimlenga nani? Kama alishiriki kuweka kipengele hicho mbona analalamika kinapotumika kwake? Alitaka kitumike kwa nani?

Ikumbukwe sheria ni msumeno hukata huku na huku. Unapotunga sheria yoyote jiulize hii sheria ikitumika kwangu nitajisikiaje? Sio unatunga then ikikurudia unahisi umeonewa.

Viongozi wengi wa kiafrika wanapotunga sheria kandamizi (Draconian Laws) hudhani ni kwa ajili ya tabaka la chini tu na sio kwa ajili yao. Siku zikiwageuka wanaanza kutafuta mchawi. Katika hili Zitto hapaswi kulalamika kabisa kuhusu kifungu cha katiba kinachomvua uanachwma maana alishiriki kukitunga mwaka 2006.

KWANINI MDEE ANAPASWA KUJIUZULU.

Halima Mdee alitweet kile alichokiita "mawazo yake" kuwa yeye anaamini Zitto bado ni mwanachama wa CHADEMA.

Pamoja na kuwa ni mawazo yake lakini amekosea kwa kuwa yeye kama kiongozi mkuu ndani ya CHADEMA hakupaswa kukosoa chama chake mitandaoni. Hii ni kwa sababu anazo platform nyingi za kukikosoa chama zaidi ya mitandaoni kama alivyofanya.

Yeye ni mjumbe wa Kamati kuu angeweza kuyasema huko. Yeye ni M/kiti wa BAWACHA angeweza kuyasema huko, yeye ni mjumbe wa Baraza kuu la chama angeweza kuyasema huko. Yeye ni mjumbe wa mkutano mkuu, angeweza kuyasemea huko.

Kwa kifupi Mdee alikua na fursa nyingi za kusemea hayo mawazo yake badala ya kusemea mitandaoni. Huku mitandaoni ni kwa wale wasio na fursa ya kuwasilisha mawazo yao moja kwa moja kama ilivyo kwa Mdee. So katika hili amekosea.

Pili, Mdee anajua kuwa maamuzi ya Zitto kuvuliwa uanachama ni ya Katiba si ya mtu mmoja. Si ya Lissu wala Mbowe. Ni maamuzi ya Katiba. Na Katiba hiyo Mdee alishiriki kuitunga mwaka 2006 akiwa Mbunge viti maalum na mjumbe wa kamati kuu. Leo anawezaje kupinga kitu kilekile alichoshiriki kukitunga? Huu ni wendawazimu.!

Lakini pia Mdee anajua kuwa hata kama ameona kasoro kwenye suala hili, ni kasoro za kikatiba sio za Lissu au Mbowe. Hivyo basi mahali pazuri pa kurekebisha kasoro hizo ni kwenye vikao vya chama si mtandaoni kama alivyofanya. Maana hata akitweet kila siku kuwa anamtambua ZZK kuwa mwanachama, bado Katiba iko palepale kuwa haimtambui.

Nne, Mdee ni kiongozi wa Baraza la Wanawake na alipochaguliwa alikula kiapo cha kuilinda Katiba ya chama. Katiba aliyoapa kuilinda ndiyo hiyohiyo inayosema "mwanachama akikipeleka chama mahakamani akashindwa kesi amejivua uanachama wake mwenyewe."

Sasa mbona Mdee anapingana na katiba aliyoapa kuitetea na kuilinda? Hii ni ajabu. Au alipoapa hakujua ndani kuna nini? Aliapa kuilinda katiba asiyoijua? Lakini ataachaje kuijua na alishiriki kuitunga mwaka 2006? This is paradox.!

Katika hili Mdee kadhalilisha nafasi yake kama Mwenyekiti wa Baraza la wanawake na mimi nashauri AJIUZULU ili kuonesha dhana ya uwajibikaji. Ni lazima viongozi wajifunze kuwajibika kwa kauli zao.

Hatuwezi kila siku kupigia kelele mawaziri wa serikali ya CCM wawajibike wakati sisi wenyewe dhana ya uwajibikaji inatushinda. Kipimo kilekile tunachowapimia CCM nasi tujipimie vivyo hivyo. Mdee achia ngazi maana umeikana Katiba uliyoapa kuitetea.

KWANINI WENJE YUPO SAHIHI,

Ujumbe uliosambaa ukionesha ni wa Ezekiah Wenje akichat na wabunge wenzie kwenye group la Whatsapp juu ya sakata la Zitto nao umeibua mjadala mkubwa kwenye jamii. Wengine wakisema ni wake wengine wakidai ni photoshop. Na wale waliosema ni wake nao wakagawanyika. Wengine wakasema alikua sahihi huku wengine wakiponda kuwa amekosea.

Ili kujiridhisha kabla sijacomment kuhusu ujumbe huo nilimpigia simu Wenje lakini hakupokea, baadae nikawapigia simu wabunge naofahamiana nao. Wakadhibitisha kuwa ule ujumbe ni wa Wenje alioutoa kwenye group lao la whatsapp liitwalo "CHADEMA MPs"

Baada ya kujiridhisha kuwa ujumbe ule ni wa Wenje nikawa kwenye position nzuri ya kuchangia, maana huwa najihadhari sana kuchangia taarifa ambayo siielewi vya kutosha (partial informed).

So kwa maoni yangu Wenje alikua sahihi kwa sababu alikotoa mawazo yake ni mahali sahihi. Group ya wabunge wa CHADEMA ni sawa na kikao cha wabunge wa chadema. So ni kikao kama vilivyo vikao vingine vya chama. Tofauti tu ni kuwa kikao hiki kinafanyika online.

So hiki ni kikao cha uongozi cha chama hata kama hakikua rasmi. Ndani ya vikao kama hivi ni kawaida kuwa na mawazo tofauti baina ya wajumbe. Yani kupingana kwa hoja lakini mwisho wa kikao wanatoka na msimamo mmoja na msimamo huo ndio unaoenda kwa wananchi.

Sasa Wenje ndani ya kikao kile alikua na mawazo tofauti na wenzie. Hii si dhambi, maana ni kawaida ya vikao. Na baada ya majadiliano makali Wenje na wengine waliokua na mtizamo tofauti wakakubaliana na maamuzi ya chama ya kumvua uanachama Zitto maana ni ya kikatiba.

So hadi hapo Wenje hana kosa. Kosa lipo kwa aliyevujisha taarifa hiyo ya kikao cha ndani na kuileta public. Huyu ndiye anayepaswa kuadhibiwa.

Kuvujusha taarifa ya vikao vya ndani ya mjumbe mwenzio kisa tu hujakubaliana nae mawazo, ni kosa kubwa katika maadili ya uongozi.

Mbona kuna mgogoro kwenye baraza la mawaziri na wapo ambao hawamtaki Pinda, lakini je ni waziri gani amewahi kumrekodi mwenzie asiyekubaliana nae mawazo na kurusha mtandaoni? Yani waziri anayemuunga mkono Pinda akamrekodi mwenzie anayemponda Pinda kisha akarusha mtandaoni.!

Kama hamna, sisi CHADEMA tunaojiona wakamilifu kuliko CCM hii tabia tumeipata wapi? Mbona hao CCM tunaowakosoa kila siku wanatushinda maadili?

Nashauri mbunge aliyehusika "kuscreen shot" ule ujumbe wa Wenje na kuusambaza achukuliwe hatua. Huyu hana sifa za kuwa kiongozi.

Kama ameweza kuvujisha taarifa ya kikao cha ndani kisa tu hakubaliani na aliyeitoa taarifa hiyo, huyu akipewa nafasi kubwa anaweza kuvujisha hata taarifa za kuitia nchi hatarini kisa hakubaliani nayo. Narudia, mbunge aliyehusika hafai kuwa kiongozi.!

JIPU LIMEPASUKA, SIWEZI KUWA ADUI KWA KUSEMA UKWELI.

Malisa GJ || Your Partner In Critical Thinking.!

Jinsi ya Kumtambua Mwanaume Asiye na Pesa

$
0
0

Zifuatazo ni dalili za mwanaume asiye na pesa;

1. Kila siku appointment zake yeye ni gheto kwake au anang'ang'ania kuja kwako, hakuna hata kwenda beach wala hotelin.

2. Siku ukiwa unaenda kwake, anakwambia njoo kwenye saa tisa au kumi. Ujue amekadiria hiyo mida utakuwa umeshapata lunch.

3. Ukiwa unaenda kwake hasemi ukikaribia nishtue nitoke kukupokea, ujue anaogopa akifika kabla yako itabidi alipie bajaji.

4. Ukiwa unaondoka kwake anasema sijisikii vizuri kwahiyo siwezi kukusindikiza, ujue anaogopa unapopanda bajaji itabidi akulipie.

5. Ukimwambia umefulia, anakwambia "pole mpenzi ndio maisha hayo" ujue hana cha kukupa.

6. Mkiwa mpo mahali inabidi kila mtu aondoke peke yake ukasikia anasema mi ntapanda bajaji pale mbele kuna sehemu napitia, ujue hana hela anaenda kupanda daladala.

7. Kila mkienda kula restaurant jamaa anasema "mi nimetoka kula sio mda njaa haiumi" haagizi hata maji ya kunywa ujue jamaa hana kitu.

8. Kama upo mtandao tofauti na yeye kila siku ye anatuma tu sms, siku akitaka kupiga simu anakwambia "weka line ya tigo tuongee" ujue hana kitu huyo.

9. Ukiona anasisitiza kwamba hapendi wanawake wanaopenda vitu vya gharama kama simu n.k, ujue kaishiwa huyo akaoe ma house girl.

10.Ukiona kila siku ukikaa nae anakupa wosia kwamba mapenzi sio pesa, ujue hana kitu huyo.

Posted by: SUPU YA MAWE

Kakobe :Rose Muhando Sio Mlokole Hata Kidogo Anawakatisha Wanaume Viuno Stejini

$
0
0
Kiongozi wa Kanisa la Full Bible Gospel Fellowship, Askofu Zakaria Kakobe Amewalipua baadhi ya Wanasiasa na waimbaji wa Injili wanaotumia neno uokovu katika maisha yao wakati haipo hivyo...
 Askofu Kakobe aliyasema hayo alipokuwa akihubiri kanisani kwake na kumtolea mfano Mwimbaji Rose Mhando na kusema hana sifa za ulokole kwa kuwa anawachezesha wanaume kwa kukata mauno kwenye nyimbo zake , Amesema "Hivi kweli mtu kama Rose Muhando unaweza sema ameokoka ..embu tuache utani na kumrudia Mungu Jamani"

Petiman:Bora Ninyang'anywe Mke Kuliko Kuachana na Wema Sepetu

$
0
0
Mpambe na Rafiki Mkubwa wa Wema Sepetu Petit Man Amesema Kamwe Hawezi kuachana na Wema eti kwa Sababu Shemeji yake Diamond Ana mahusiano na Mwanamke mwingine..
Kauli hiyo inaashiria kwamba Petman yupo tayari kunyang'anywa Mke endapo uhusiano wake na Wema Sepetu hautaipendeza familia ya Diamond kuliko kuvunja uhusiano na Wema Sepetu ..

Petitman ameyasema hayo akiwa na Ommy Dimpoz alipokuwa akitambulisha nyimbo yake mpya katika vyombo mbali mbali vya habari

Alisema "Mimi na Wema ni Damu Damu ...ila mambo ya mahusiano kila mtu na mambo yake hatuingiliana wala kuwekeana mipaka"


Jokate Afunguka Upya 'Hashim Thabit Mtamu Kuliko Wanaume Wote Bongo ...Diamond Ndio Hamna Kitu Kabisa'

$
0
0
Miss Tanzania Namba 2 Mwaka 2006, Jokate Mwegelo maarufu kama Kidoti amesema kuwa katika mahusiano yake ya kimapenzi alitokea sana kumzimikia Hasheem Thabit kuliko Wanaume wote aliowahi kutoka nao kimapenzi Bongo ..Akizungumza na Gazeti la Kiu , Kidoti amesema kwa sababu ambazo amezihifadhi moyoni mwake Hasheem alikuwa na vitu Adimu sana ambavyo hawezi kuvitaja.....Kuhusu Diamond Ambae pia amewahi kutoka nae Kidoti amesema hakuenjoy nae kwani yalikuwa mapenzi ya muda mchache sana.

Zari Flaunts Her Mgongo While Having Good Time in Swimming Pool

$
0
0
 Zari Flaunts her Mgongo while having good time in swimming pool with Children...
See other Photos Below and tell us if she is still hot During this time of Pregnancy

os 


Mcheza Filamu Bongo Movies Aingia Katika Kashfa Nzito ya Kuwadanganya Wadada wa Mikoani na Kuwatumia Kimapenzi

$
0
0
Ubuyu Kutoka Insta Leo hii unamuhusu Mcheza Filamu Rammy ...
Page ya Mrekebisha Tabia wamemrusha na kufichua makubwa...Jisomee Mwenyewe Hapo chini:

"Jamani @rammygalis hata wewe? Nilikupenda nilipoona ulivoigiza ile movie ya CHAUSIKU nkakuona bonge la mtanashati, kipaji kipo lkn hizi tabia unazofanya za kutongoza wasichana kupitia mitandao ya kijamii unawaambia utawapa nafasi ya uigizaji unawafanya halafu unaingia mtini zimenichefua sana!!!....wasichana wengine unawatoa hadi mikoani unawatelekeza hotelini ukishawafanya hawakuoni tena... Unabisha????? Haya sasa na yule dada mwingine mliyewasiliana kwa facebook ukamuita kutoka Mbeya akaja dar kwa lengo la kuigiza movie alipofika dar ukampangia hoteli maeneo ya Ubungo. Ulikaa nae siku hiyo moja tu akamfanya then hurudi tena pale hotelin yule dada kila alipokuwa anakupigia simu unamdanganya utaenda mwisho wa siku hukutokea wala hakukuona tena mpaka alipotafuta msaada wakurudi kwao na hotelin alikuwa anadaiwa Manager wa hotel ikabidi amsamehe tu deni lake la hotel.

This is HAPANA Rammy!!! Uache kabisa...na wengine mlio na tabia hizo chafu tutawapata tu ili iwe fundisho kwa wengine.

Pia wasichana nyie mnaniliza hadi basi why jaman!! Umvulie nguo mtu ili upate kazi...halafu unaambulia kulalwa na kazi hakuna. Hivi mnajua UKIMWI bado upo? Na mpaka sasa bado dawa haijapatikana?"

Source:Mrekebishatabia/Instagram

Baada ya Watu Kuponda, Huu Ndio Msimamo wa Wolper Kuhusu Kipini Chake Puani

$
0
0
“Wapenzi mnaotukana kisa nimevaa kipini kwa pua msipoteze muda hiko akitoki ndo kimeshafika zaidi nitakua tuu na badilisha leo cha njano kesho chekundu, why mnakua wagumu kuelewa  kinipendeze kisinipendeze ni mimi so please msinijazie comment za zamatusi nakukosoa  kwenye picha zangu kama nyie ndo wavaaji sitaki ushauri sitaki jamani pipo chilaaax me nakipini dam dam...  in love with my kipini najikuta jacq khan mwenzenu kila nikijitizama....Am so soleee. Nawapenda sana napenda ushauri lakini kipini kiacheeni pua kitasharikiana na pua na uso kushauriana kwamba leo kivaliwe au kisivaliwe lakini siyo wewe mtukanaji ok byeeeee”-Wolper amebandika andiko hilo kwenye ukurasa wake mtandaoni.

Nadhani ameeleweka, wale wanaomshabulia kwa lugha kali muache jamani.

Mzee wa Ubuyu

BONDIA Maarufu Nchini wa Ngumi za Kulipwa, Francis Cheka Atoka Gerezani..

$
0
0
BONDIA maarufu nchini wa ngumi za kulipwa, Francis Cheka aliyehukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela na kutakiwa kulipa fidia ya Sh. milioni moja kwa kosa la kumpiga na kumjeruhi meneja wa baa yake amebadilishiwa adhabu ya kifungo.

Cheka amechiwa na kutoka gerezani na sasa anatakiwa kutumikia kifungo cha nje.
Cheka alihukumiwa na Hakimu wa Mahakama ya Mkoa wa Morogoro, Said Msuya baada ya kumkuta na hatia ya kumpiga aliyekuwa meneja wa baa yake iitwayo Vijana Social iliyopo Morogoro Mjini aitwaye Bahati Kabanda ‘Masika’.

Meninah La Diva Awatamani Wema Sepetu na Kajala..Kama Angekuwa na Uwezo Asema Angefanya Hivi..

$
0
0
Mrembo na Staa wa Bongo Fleva, ambae nyota na jina lake lilianza kusikika Kupitia shindano la Bongo Star Search (BSS), Meninah La Diva amesema angekuwa na uwezo angewapatanisha mastaa wawili wa Bongo Movies , Wema Sepetu na Kajala Masanja ambao alisema kuwa anawependa sana.

Meninah aliyasema hayo leo alipokuwa akifanya mahojiano na mtangazaji Millard Ayo kwenye c kipindi cha Amplifaya, alipoulizwa kuwa angekuwa na uwezo angewapatanisha mastaa gani ambao wamegombana au hawaelewani kwa namna moja au nyingine.

“Ningekuwa na uwezo ningewapatatinisha Wema na Kajala kwasababu wote nawapenda”-Meninah alijibu

Wema na Kajala walikuwa marafiki wa karibu lakini urafiki wao ulivunjika na kwasasa sio marafiki tena.

Hakika wengi tunapenda wawili hawa waelewane na urafiki  wao urudi, wewe je?
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images