Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

MLINZI AFUKUZWA KAZI BAADA YA KUMPIGA PICHA BOSS WAKE ALIYEKUWA AKILA URODA KWENYE GARI

$
0
0
Jamaa mmoja alijikuta kibarua kikiota nyasi baada ya kula chabo bosi wake na kumpiga picha bosi wake huyo aliyekuwa akila uroda ndani ya gari kwenye parking. Jamaa akielezea The ClickTz, kuwa boss wake huyo alipo ingia getini alikaa sana kwenye parking nikama vile alikuwa anambembeleza mtu aliyekuwa nae kuingia ndani, mara yeye mwenyewe aliingia ndani kisha kutoka nje na kurudi kwenye gari, mara nikaona gari inacheza, mara tena kidogo mlango wa gari ukafungulia nikamuona boss wangu akishughulika vibaya sana, inawezekana aliona ndani hapatoshi akaamua kufungua mlango na kushugulika akiwa nje. kumbe alikuwa ameshaniona wakati ule nikiwa nakula chabo. kesho yake asubuhi aliniita nakuniuliza ile picha niliyompiga iko wapi. mimi nilikaa kabisa kama sikufanya kitendo hicho ila aliamua tu kunitimua na ndio huo ulikuwa mwisho wa mimi kufanya kazi hapo kwake. Noma sana
-ClickTz

BINTI AGONGWA NA TRENI: HII NI AJALI MBAYA YA TRENI ILIYOWAHI KUTOKEA: INATISHA SANA

$
0
0
Ilitokea huko nigeria, binti aliyekuwa amelala kwenye reli, nakukanyagwa na treni...Inadaiwa Kisa cha binti kulala kwenye reli ni mapenzi baada ya kuachwa na boy wake aliona hakuna haja ya kuishi 

NEWZ ALERT!! HAWA NDIYO MAWAZIRI WAPYA!!

$
0
0


Saada Mkuya ni waziri wa fedha mpya, 

Asha Migiro ni waziri Katiba na Sheria

Waziri wa Ulinzi Hussein Mwinyi

Malima Waziri Mdogo Fedha

Kebwe ni Waziri Mdogo Afya

Chikawe ni Waziri Mpya Ndani 

Mhagama Waziri Mdogo elimu 

Pindi chana Waziri Mdogo Watoto Kinana Mama

Dr. Lengeya Kamani Waziri wa Mifugo 

Waziri Mdogo Telele Mifugo

LADY JAY DEE ANUNUA RANGE ROVER MPYAAA...SEE PHOTOS

$
0
0

Respect kubwa kwa mwadada Lady Jay Dee......Hiyo ni Range Rover Sport ...Nomaaaa

GARI JIPYA LA DIAMOND LAZUA UTATA..WENGI WASEMA SIO JIPYA MBONA KAZIBA PLATE NUMBER!

$
0
0


Inakwenda week sasa toka mkali wa bongo fleva Diamond Platinumz kuonekana kwenye account yake ya Instagram akiwa na ndinga hili kali V8. Mashabiki wakasema mbona lile gari la kwanza alivyolinunua tuliona mbwembwe nyingi za picha na kuliita new baby mara my new toy hili mbona hatuoni hizo mbwembwe? Shabiki mmoja akahoji mbona akipiga picha na hili gari anakaa katikati na kuziba namba za mwanzo zisionekane je ni lake kweli au…?
Na mimi ikanibidi kuzifuatilia picha hizo na kweli nikajionea mwenyewe kama hizo picha zinavyoonekana hapo juu hahaaa…
Sina jibu sahihi mpaka nitakapomtafuta na kutueleza ukweli uko wapi kama ndio new toy au new bby ameingia kwenye himaya ya Platinumz au la… stay tune.

UTEUZI WA JUMA NKAMIA NI KUUA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI-MEENA

$
0
0
Akiongea na kituo cha CHANNEL TEN leo jumapili tarehe 19/01/2014,mwandishi wa habari wa gazeti la Mwananchi ndugu Meena amelaani uteuzi wa Jumaa Nkamia kuongoza wizara inayosimamia vyombo vya habari,nanukuu,"Nkamia nimesoma naye,lakini kauli zake za hivi karibuni bungeni vinaonesha kuwa hapendi uhuru wa vyombo vya habari,kwa aliyofanya waziri aliyepita na kwa uteuzi wa Nkamia tutegemee kuminywa kabisa kwa vyombo vya habari".

Nilitegemea kuteuliwa kwa mtangazaji mkongwe Nkamia kungewafurahisha waandishi wa habari,lakini inaonekana sivyo.Je, ni kweli Nkamia hafai kuongoza wizara ya habari,au ni chuki binafsi za Meena kwa Nkamia.Nini mapungufu ya Nkamia mpaka akachukiwa kiasi hicho na Meena? Kama si Nkamia,nani anafaa kuongoza wizara husika?.
Source:Jamii Forums

OBAMA AITETEA BANGI ASEMA HAINA MADHARA SANA KAMA POMBE

$
0
0
With a majority of Americans now in favor marijuana legalization, President Barack Obama is now saying weed is no more dangerous to individuals' health than alcohol.

In an interview with the New Yorker's David Remnick published Sunday, Obama said while he believes marijuana is "not very healthy," the drug isn't as harmful as some insist.

“As has been well documented, I smoked pot as a kid, and I view it as a bad habit and a vice, not very different from the cigarettes that I smoked as a young person up through a big chunk of my adult life. I don’t think it is more dangerous than alcohol," Obama told Remnick.

When asked if he believes marijuana is less harmful than alcohol, Obama said it is less damaging "in terms of its impact on the individual consumer."

"It’s not something I encourage, and I’ve told my daughters I think it’s a bad idea, a waste of time, not very healthy," he added.

Marijuana is currently classified by the Drug Enforcement Administration as a Schedule 1 substance, which the DEA considers "the most dangerous class of drugs with a high potential for abuse and potentially severe psychological and/or physical dependence." Other Schedule 1 drugs include heroin, ecstasy and LSD.

Obama said his focus on reforming laws that punish drug users, noting the racial disparity in drug arrests.

"We should not be locking up kids or individual users for long stretches of jail time when some of the folks who are writing those laws have probably done the same thing," he said.

In August, the Obama administration announced it would not stop Washington and Colorado from legalizing recreational marijuana use, marking a major step away from the administration's war on drugs.

In the New Yorker interview, Obama said he believes these new laws are "important."

“It's important for it to go forward because it’s important for society not to have a situation in which a large portion of people have at one time or another broken the law and only a select few get punished," he said.

ANGALIA PICHA YA KWANZA YA SISTER ALIYEJIFUNGUA MTOTO WA KIUME HUKO ITALY

$
0
0
Inaelezwa kwamba sister aliyezungushiwa duara anae kwenda kwa jina la  Roxana Rodriguez ndo yule aliyejifungua mtoto wa kiume hivi karibuni na kumuita Francis. Sister huyu ameuushangaza ulimwengu pamoja na masister wenzake kwa kudai kwamba hakujua kwamba ni mjamzito. Dah bora tu waruhusiwe kuolewa.

A nun who has given birth to a baby boy in Italy said she had no idea she was pregnant.

The 31-year-old was taken to hospital on Wednesday with abdominal pains, which she thought were stomach cramps, local media reported.

The mother, originally from El Salvador, and her baby are said to be doing well and a number of other new mums in Rieti hospital have begun collecting clothes and donations for her.

Italian news agency ANAS reported that she named the baby, who weighs 3.5 kilograms (9 pounds), Francis after the current Pope.

‘I did not know I was pregnant. I only felt a stomach pain,’ the nun told ANAS.

Local pastor Don Fabrizio Borrello told journalists the nun was going to take care of the infant.

‘I guess she’s telling the truth when she says she arrived at the hospital unaware of the pregnancy,’ he said.

The woman belongs to a convent near Rieti, which manages an old people’s home. Other nuns at the convent said they were ‘surprised’ by the news.

WALIOFELI KIDATO CHA PILI KUENDELEA NA MASOMO KIDATO CHA TATU

$
0
0
Wakati Watanzania wakisubiri matokeo ya kidato cha pili mwaka 2013, imebaini kuwa Serikali imetoa agizo kwamba wanafunzi wote waliofeli mtihani huo kuendelea na masomo ya kidato cha tatu, huku wakisoma mafunzo ya kurudia mtihani wa kidato cha pili.

Licha ya matokeo hayo kutotangazwa hadi sasa, imebainika kuwa waliofaulu mtihani huo uliofanywa Oktoba 7 hadi 21 mwaka jana ni asilimia 62 tu, asilimia 31 wakitakiwa kukariri (kurudia) kidato cha pili mwaka huu, huku asilimia saba wakishindwa mtihani huo kwa mara ya pili.

Jumla ya wanafunzi 531,457 walitajwa na Wizara ya Elimu mwaka jana kuwa watafanya mtihani huo.

Uamuzi huo wa Serikali ni tofauti na ule uliotolewa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa Novemba 4, mwaka 2012, kwamba kuanzia wakati huo mtihani wa kidato cha pili utakuwa ni wa mchujo na kwamba atakayefeli atatimuliwa.

Dk Kawambwa alisema matokeo ya mtihani wa kidato cha pili yatatumika kama kigezo cha kuchuja na kukariri kidato cha pili kwa watahiniwa watakaoshindwa kufikia wastani wa ufaulu wa alama 30.

Alisema mtahiniwa ataruhusiwa kukariri kidato cha pili mara moja tu na endapo mtahiniwa atashindwa mtihani kwa mara ya pili kwa mwaka utakaofuatia, itabidi aendelee na elimu ya sekondari nje ya mfumo rasmi.

Gazeti hili limeiona barua iliyoandikwa Januari 16 mwaka huu na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na kusainiwa na Katibu Mkuu wake, Profesa Sifuni Mchome, kwenda kwa wadau wa elimu nchini, wakiwamo maofisa elimu wa mikoa na Chama cha Wamiliki wa Vyuo na Shule Binafsi (TAMONGSCO).

Katika barua hiyo, wizara hiyo imewataka wadau hao kuhakikisha kuwa wanafunzi watakaofeli mtihani huo, wanaendelea na masomo ya kidato cha tatu.

“Matokeo ya kidato cha pili yamepokewa na kufanyiwa uchambuzi ili kupata taswira ya taifa. Taarifa ya matokeo hayo imebaini kuwa watahiniwa waliofanya mtihani na kufaulu ni sawa na asilimia 62 tu,” inaeleza sehemu ya barua hiyo na kuongeza;

“Hali hii inaonyesha kuwa asilimia 31 ya wanafunzi watatakiwa kukariri kidato cha pili, 2014. Wale walioshindwa kwa mara ya pili ambao ni asilimia saba wanatakiwa kuendelea na masomo nje ya mfumo rasmi.”

Barua hiyo inaeleza kuwa wanafunzi waliofaulu kwa wastani wa alama 20 na kuendelea waendelee na masomo ya kidato cha tatu mwaka 2014, wakati awali Serikali ilitoa tamko kuwa watakaoshindwa kufikisha alama 30 watatimuliwa.

“Wanafunzi waliofaulu kwa wastani wa alama 20 hadi 39 wapewe mafunzo rekebishi ‘Remedial class’ wakiwa kidato cha tatu,” inaeleza sehemu ya barua hiyo.


Inaeleza kuwa uamuzi huo unawahusu wote wakiwamo wale walioshindwa kwa mara ya pili, “Kwa maana hiyo hakuna mwanafunzi atakayerudishwa nyumbani.”

Mwisho barua hiyo imewataka wadau hao kuhakikisha kuwa inawapa taarifa mameneja na wamiliki wa shule na seminari ili kusimamia utekelezaji wa uamuzi kuhusu matokeo hayo.

Kauli ya wizara

Akitolea ufafanuzi suala hilo, Profesa Mchome alisema, “Suala la wizara kuagiza wanafunzi wote waliofeli kuendelea na masomo ya kidato cha tatu mimi sijalisikia, ninachojua ni kwamba wapo watakaorudia.”

Alisema kuwa tayari wizara imeshapeleka taarifa za matokeo hayo na uamuzi wa Serikali katika kila kanda nchini. “Kila shule ina taarifa hizo. Wapo wanafunzi watakaorudia.”

Akizungumza kuhusu matokeo ya kidato cha pili mwaka 2013 kutotoka mpaka sasa alisema, “Ninachofahamu ni kwamba matokeo ya kidato cha pili yameshawasilishwa katika kanda zote nchini.”

“Unajua matokeo ya kidato cha pili siyo kama matokeo ya darasa la saba, kidato cha nne na sita. Matokeo ya kidato cha pili ni kama mwendelezo wa tathmini ‘Continuous assessment’ kwa mwanafunzi, hutumika pia katika mtihani wa kidato cha nne.”

Alisema ndiyo maana matokeo hayo hupelekwa katika shule husika. “Baada ya kupelekwa katika shule husika, hapo ndipo inaweza kutolewa taarifa za matokeo hayo pamoja na ufafanuzi.”

Kwa nyakati tofauti gazeti hili lilimtafuta Dk Kawambwa na Naibu wake, Phillip Mulugo ili kutolea ufafanuzi suala hilo, lakini simu zao za mkononi zilikuwa zikiita bila majibu.

Msimamo wa TAMONGSCO

Alipotafutwa Katibu Mkuu wa Tamongsco, Benjamin Nkonya kueleza kama wanakubaliana na agizo hilo la Serikali alisema, “Inaonekana Serikali haiko tayari kutekeleza mkakati wake wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN).”

“Kama wizara inalazimisha wanafunzi walio na ufaulu mdogo kuendelea na masomo katika mfumo wa vidato (formal education), lazima tutegemee kuona wanafunzi wakifanya vibaya katika mitihani ya kidato cha nne.”

Alisema kuwa asilimia 98 ya wanachama wa chama hicho ni Watanzania wazalendo kwamba hawapo tayari kutekeleza agizo la Serikali kwa sababu siyo la kizalendo na limetolewa kwa ajili ya kutimiza malengo ya kisiasa ya kujiongezea umaarufu wa muda mfupi, huku Watanzania wakiogelea kwenye dimbwi la umaskini unaotokana na ujinga.

“Wachache watakaosaliti msimamo huu watakuwa wamekubali kupoteza muda wa vijana wetu huku wakijua kwamba watafika kidato cha nne, kupata daraja sifuri na kuishia kuwa machangudoa, wauza dawa za kulevya, bangi, wizi na vitendo vingine vya uvunjifu wa sheria, kanuni na taratibu,” alisema.

Alisema ili kuwasaidia wanafunzi wanaoshindwa kuendelea na masomo yao; “Mwanafunzi ambaye ufaulu wake utakuwa chini ya asilimia 45 aondolewe katika mfumo wa elimu ya vidato (formal education) na kuingizwa katika mfumo wa elimu ya ufundi mchundo (TVET - Technical education and vocational education).”

Alisema wanachama wa Tamongsco wanamiliki vyuo 586 kati ya vyuo 750 vya ufundi mchundo (VETA) na wanamiliki vyuo 1975 kati ya vyuo 1988 vya ufundi stadi (technical institutes) ambavyo vinasimamiwa na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi Stadi (NACTE).

“Vyuo hivi vina uwezo wa kuchukua wanafunzi wote ambao wana ufaulu wa chini ya asilimia 45 kuwaendeleza hadi chuo kikuu. Kikwazo pekee kilichopo ni kwa Serikali kukubali kuchangia gharama za uendeshaji wake.”

“Kikwazo hiki kitaondoka endapo Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi itakubali kutekeleza sera, sheria na kanuni za ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi (PPP) partnership) kama ilivyopitishwa na Bunge mwaka 2010.

Kidato cha pili 2012

Katika mtihani huo mwaka 2012 wanafunzi 136,923 kati ya 386,271 waliofanya mtihani huo walifeli. Idadi ya waliofeli ilikuwa sawa na asilimia 35.5, wakiwamo wasichana 74,020 na wavulana 62,903, waliofaulu walikuwa wanafunzi 245.9,32.

CHANZO: Mwananchi

MAREKANI YAMUONYE TENA RAIS KAGAME WA RWANDA

$
0
0
WAKATI utata ukiwa umegubika juu ya kifo cha aliyekuwa Mkuu wa Usalama wa Rwanda, Kanali Patrick Karegeya, taarifa kutoka Ikulu ya Marekani zinaitaja nchi hiyo kuhusika moja kwa moja na kifo hicho. Msemaji wa Ikulu ya Marekani, Jen Psaki, amenukuliwa na vyombo mbalimbali vya habari, ukiwamo mtandao wa Yahoo pamoja na BSN, akisema kuwa Rwanda imehusika na kifo cha Karegeya.

Katika maelezo yake hayo, Psaki alisema kwamba kwa mujibu wa onyo alilolitoa Rais Paul Kagame hivi karibuni, kwenye ibada ya kuliombea taifa hilo, inadhihirisha undani wa kifo cha Karegeya.

“Tuna wasiwasi na mfululizo wa mauaji ya wanasiasa maarufu nchini Rwanda,” alisema Psaki.

Kauli hiyo imekuja wakati tayari kumekuwapo na shutuma nyingi zinazomhusisha Rais Kagame na tukio la kifo cha Karegeya, kutokana na uhasama wa muda mrefu uliokuwepo baina yao.

Katika miaka ya hivi karibuni, uhusiano wa Rwanda na Marekani umekuwa ni wa mashaka, baada ya Rais Paul Kagame kuhusishwa na matukio mbalimbali ya kihalifu, yakiwamo mauaji ya wanasiasa wa upinzani pamoja na uchochezi wa vita katika eneo la Mashariki mwa Kongo.

Licha ya kukana kufadhili waasi wa M23, mwaka jana Rais Barack Obama alimuonya Kagame kuacha mara moja kuchochea mapigano Mashariki mwa Kongo.

Katika hotuba yake aliyoitoa hivi karibuni katika ibada ya kuliombea taifa hilo, Rais Kagame alitoa onyo kali kwa watu wanaoisaliti nchi hiyo kwamba watakabiliwa na wakati mgumu popote watakapokuwa.

Rais Kagame aliwataka Wanyarwanda wote kuungana katika kusimamia misingi sahihi na msimamo wao kama taifa, bila kujali tetesi zinazotoka katika mataifa ya nje kuhusu wale waliotangaza kuisaliti Serikali yake.

Hata hivyo, hakutaja moja kwa moja kuhusu tuhuma zinazoikabili Serikali yake juu ya mauaji ya aliyewahi kuwa Mkuu wake wa Ujasusi, Karegeya, ambaye ameuawa Januari Mosi, mwaka huu.

Kutokana na hali hiyo, kiongozi huyo wa Rwanda, alitoa onyo kali kwa kusema kuwa wale wote wanaoigeuka nchi yao na kuchagua kuua raia wasio na hatia kwa sababu zao binafsi, wanastahili kushughulikiwa ipasavyo.

Akisisitiza maelezo hayo, Kagame alisema hatakuwa na huruma na watu ambao wanasahau namna Rwanda ilivyowatengeneza hadi kufika mahali walipo.

Rais Kagame, aliwataka viongozi wa Rwanda kutosumbuliwa kwa yanayowakuta ‘maadui wa taifa’, kwa kuwa Mungu aliwapa nguvu ya kujenga na kukilinda kile walichokijenga, hivyo wale wanaosahau kwamba wana dhamana kwa Wanyarwanda na kuamua kutenda mambo mabaya dhidi ya taifa lao, ni wazi kwamba wamesahau kuwa hawataweza kuwa juu ya watu wao.

“Mliponiapisha kuwa kiongozi wenu mliniagiza kwamba wakati wote niilinde nchi hii, kwa maana ya kusimama kwa ajili ya watu wake,” alisema.

Hotuba hiyo iliibua mjadala mkubwa miongoni mwa watu ambapo wengi wao waliitafsiri kama ni ujumbe wa kilicho nyuma ya utata wa kifo cha Karegeya.

Kanali Patrick Karegeya (53), ambaye alikuwa akiishi uhamishoni nchini Afrika Kusini kwa miaka kadhaa, baada ya kutofautiana na mkuu wake wa zamani, Rais Kagame, aliuawa na watu wasiojulikana ambapo mwili wake ulikutwa katika Hoteli ya Michelangelo Towers, nchini Afrika Kusini.

Ikumbukwe kuwa Kanali Karegeya aliongoza Idara ya Usalama ya Rwanda kwa muda mrefu na alikuwa ni mtu aliyeaminiwa kwa kiasi kikubwa na Rais Kagame.

Hata hivyo, kiongozi huyo alijikuta akiingia katika uadui mkubwa hata kudaiwa kuwa Ofisa Usalama huyo alikuwa akiandaa mikakati ya kumpindua Rais Kagame.

Uadui huo haukuishia kwa Karegeya pekee, bali hata aliyekuwa Mkuu wa zamani wa Jeshi la nchi hiyo, Faustin Kayumba Nyamwasa na washirika wake, walikumbwa na hali hiyo, hivyo kuwalazimu kuikimbia nchi yao.

Serikali ya Rwanda imekuwa ikilaumiwa kwa kuwaua baadhi ya wanasiasa mashuhuri nchini humo, kama John Sengati, aliyeuawa nchini Rwanda, Kanali Theoneste Lizinde na Waziri wa zamani wa Rwanda, Seth Sendashonga waliouawa nchini Kenya.

Wengine ni Kanali Shabani Rutayisire, Gratien Munyarubuga, Dk. Assiel Kabera na Andre Kagwa Rwisereka ambao waliuawa nchini Rwanda.

Pia Regina Uwamaliya na Juvenal Uwilingiyimana nao waliuawa nchini Ubeligiji, huku Charles Ingabire akiuawa mjini Kampala na Pasteur Musabe aliyeuawa Cameroon.

Mpaka sasa kumekuwa na taarifa tofauti kuhusu kukamatwa kwa watu wanaoshukiwa kuhusika na kifo hicho, huku baadhi ya vyanzo vikimtaja mmoja wa wafanyabiashara wakubwa wa Rwanda, Apollo Gafaranga, ambaye alidaiwa kujenga urafiki wa karibu na marehemu Karegeya.

Oktoba mwaka jana, aliyekuwa mlinzi mkuu wa Rais Paul Kagame, Luteni Joel Mutabazi, alitekwa na kikosi cha Jeshi la Uganda na kukabidhiwa kwa Serikali ya Rwanda.

Luteni Mutabazi alikimbilia nchini Uganda Oktoba 2011, baada ya kufanikiwa kutoroka jela yenye ulinzi mkali wa kijeshi, iliyo katika mji wa Kami, nje kidogo ya mji wa Kigali, akituhumiwa kwa kuhusishwa na kutoroka kwa mkuu huyo wa majeshi na kukimbilia Afrika Kusini.

Mlinzi huyo pia anashutumiwa na Serikali ya Rwanda kwa kutoa siri kwa Kikosi Maalumu cha Umoja wa Mataifa chini ya Majeshi ya Umoja wa Kulinda Amani nchini Kongo, (MONUSCO) na kuwezesha kuchakazwa na kushindwa kwa kikosi cha waasi wa M23.

MWALIMU GANI MKALI AMBAE ULISHAWAHI KUKUTANA NAE KATIKA MAISHA YA SHULE?

$
0
0
Katika almost shule zote hua hawakosekani wale walimu wa kali balaa ambaye ukiingia kwenye 18 zake ni lazima ueleze. kwa mfano mimi shule ya msingi lugalo niliposoma kulikua na Mwl.Chavala,Mwl.Kinyogori,Mwl. Bango,Mwl.Getwa,Mwl.Buchwa aisee hawa walimu sitawasahau kamwe. maticha,walikua wana mwaga stiki kama hawana akili nzuri aisee,
then makongo kulikua na Kisarika, Yeyeye,Malongori na Afande Miraji (thou hakua mwalimu). ebana kuna siku tulipata msala asembo baada ya kuimba vibaya wimbo wa taifa, huwezi amini marehemu Afande Miraji single-handedly alizungusha stiki shule nzima kwanzia form 1-6 pale asembo af akarudia raundi mbili. kuna jamaa kesho yake akaomba uhamisho baada ya kukamatwa tena na afande miraji hakwenda zamu akala stiki 15 za adabu. vp mwl gani ushakutana nae hadi leo huwezi msahau?
Bdonlucchese

DAVID MOYES AVUMILIKI ACHEZEA KICHAPO CHA MBWA MWIZI TENA

$
0
0
Huyu kocha wa Man u naona amekuja na Gundu kubwa kweli .....Sasa hivi Washabiki wa Man hatuongei kabisa mbele za watu hata tukicheza na team kibonde tunawasiwasi wa kufungwa ....Yaani sijui anataka kutupeleka ilipokuwa team yake kabla ya kuja Man u....Jana tumechapwa tatu moja bana sitaki kuongelea hilo sana ila jua tulifungwa ndio tumefungwa na Etoo...

SHILOLE AWACHANA MASTAA WABEBA UNGA

$
0
0
Stori: Shani Ramadhani
STAA wa muziki na filamu Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amewachana wasanii wanaojihusisha na madawa ya kulevya kuwa ni wavivu.

Akizungumza na paparazi wetu pasipo kuwataja majina, Shilole alisema wasanii wengi ni wavivu na kinachowaponza zaidi ni tamaa za kuwa na maisha mazuri, wanafikiri mafanikio yanakuja kirahisi pasipo kuhangaika.

“Wanafikiri mafanikio yanakuja kirahisi bila kujishughulisha, ninawashangaa sana kwani wanajishushia hadhi zao kwa tamaa ya kutaka kuwa na maisha mazuri bila kufanya kazi, badilikeni,” alisema Shilole.
By Global Publishers

NAMPENDA LECTURER WANGU WA CHUO ILA KUMWAMBIA NAOGOPA

$
0
0
Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 24 sasa. Ninasoma Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, mwaka wa pili.
Tatizo langu ni kwamba, kadri siku zinavyozidi kwenda nahisi kumpenda mmoja kati ya maprofesa wangu. Lakini hadi sasa ninachoona ni kwamba bado hajajua hisia zangu nifanyeje?

CHUKI ZAANZA NDANI YA CCM

$
0
0

Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM), Mkoa wa Shinyanga, Hamisi Mgeja ameonya baadhi ya viongozi wa chama hicho kuwajengea chuki wanachama kadhaa na viongozi kwa madai wako karibu na Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa.

Hatua ya Mgeja imekuja ikiwa ni siku chache baada ya Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Geita, Joseph Kasheku ‘Msukuma’ kumkana na kumshutumu, Mwenyekiti wa Wenyeviti wa CCM, Mgana Msindai kuwa anawalazimisha kuwa nyuma ya Lowassa wakati sivyo ilivyo.

Hata hivyo, Msindai alikanusha madai hayo kuwa hakuwahi kuwazungumzia wenyeviti wa CCM wa mikoa kuwa nyuma ya Lowassa zaidi ya kusema kuwa wanamuunga mkono katika masuala mbalimbali ya maendeleo.

Akizungumza katika mahojiano maalumu, Mgeja alimtetea Msindai kuhusu suala la wenyeviti wa CCM kuwa nyuma ya Lowassa katika urais. Alisema: “Nataka kutoa angalizo kwa viongozi ndani ya chama, Tanzania kwa ujumla, kumejitokeza tabia ya baadhi ya watu kuchukiana eti tu kwa sababu wako nyuma ya Lowassa,” alisema na kuongeza:

“Kumeanza watu kuchukiana, kuhukumiana kwa sababu uko karibu na Lowassa au kuwa na imani naye katika utendaji kazi wake, kumpenda na kumkubali mtu ni utashi wa mtu binafsi...tusihukumiane wala kuchaguliana marafiki,” alisema Mgeja.

Mgeja alisema: “Hakuna dhambi ya kumpenda au kumwamini Lowassa, lakini watu wanachukia, watu wananung’unika, wananuna haya yote ni majungu, woga, wivu na kutokujiamini. Inawezekana wanaofanya hivyo, wanatumwa na walio nyuma yao.

“Katika kipindi cha kuelekea uchaguzi, tusianze kusakana uchawi, muda ukifika, kila mtu atabebwa kwa sifa zake na atajibeba kwa umahiri wake.”

Mgeja alisema, kazi kubwa inayotakiwa kufanyika kwa wabunge, mawaziri na viongozi wa kada mbalimbali ni kukaa chini na kuwatumikia wananchi kwa kuhakikisha wanapata maji safi, dawa hospitalini na elimu kuliko kutumia muda mwingi kuangalia nani anampenda Lowassa.

“Kuna changamoto nyingi zinazowakabili wananchi na kila siku wanatuangalia viongozi, suala la vijana ni tatizo kubwa huduma za msingi kuliko kukaa na kuangalia Lowassa anafanya nini na yuko na nani, haileti tija hata kidogo,” alisema.

Mgeja aliwataka wanaCCM kutulia na kutafakari mambo ya maendeleo kwa kuwa hakuna mtu aliyejitangaza urais akiwamo Lowassa zaidi ya kuanzisha safari ya matumaini ambayo ndani yake kuna mafanikio katika elimu, huduma za afya, ajira kwa vijana na mambo mengi,” alisema.

Hivi karibuni, Msindai alikaririwa akisema: “Mimi ni Mwenyekiti wa wenyeviti wa CCM, lakini sikuwahi kuzungumza kuwa wenyeviti wote wanamwunga mkono Lowassa katika Uchaguzi Mkuu 2015... kikubwa tulichozungumza ni kumuunga mkono katika safari yake ya mafanikio katika kuendeleza elimu, maji, ujenzi wa zahanati.”

Msindai alisema wanamwangalia Lowassa kutokana na uwezo wake katika kusimamia mipango yake ya maendeleo na zaidi katika kupigania elimu pana kwa Watanzania.
Mwananchi

"I'M TIRED OF MEN...I'M EVEN TEMPTED TO BECOME A LESBIAN" MARYA SAYS

$
0
0
If Marya were a bird she’s be a phoenix. She is certainly as beautiful as the mythical bird


and of late has been just as elusive. No interviews not a peep. but she finally came out to receive an interview from Cate Mukei.

 When that happened, It was an interview that revealed something interesting. The songstress allegedly admited to having to fight off temptations to begin batting for the home team.

During her conversation with Cate, she made the following remark:

“I’m tired of men who can’t be in a serious relationship. Most of them just want to hit and run. I’m even tempted to become a lesbian. The grass is probably greener on the other side.” UIhh… huh… It seems uncle Chinedu might just have been right afterall!

We are left wondering, what is wrong with men?! Men keep saying that women of this generation are NOT serious in relationships FUNNY ENOUGH women say the same!!

Source: Ghafla

BREAKING NEW:AJALI MBAYA YA GARI YATOKEA SINGIDA..WATU 13 WAFARIKI

$
0
0


Habari zilizotufikia sasa hivi kutoka Singida zinasema watu 13 wamefariki dunia baada ya kutokea ajali ya magari mawili kugongana uso kwa uso eneo la Isuna mkoani humo.

Habari zinasema ajali hiyo ilihusisha gari aina ya Toyota Noah na lori ambayo namba zake za usajili hazikupatikana mara moja. Watu 13 waliofariki walikuwa katika Noah iliyokuwa ikitokea Itigi na maiti zao zimehifadhiwa katika Hospitali ya Mkoa wa Singida. 

Baada ya ajali hiyo, dereva wa lori na msaidizi wake walitokomea kusikojulikana.

"HAKUNA MWANAMKE YEYOTE MWENYE UBAVU WA KUMCHUKUA BWANA'ANGU KWANI ME NI ZAIDI YA HAO WOTE" IRENE PAUL

$
0
0
MSANII nyota wa filamu Irene Paul, amesema kwamba haoni mwanamke mwenye uwezo wa kumuibia bwanaake, ingawa hataki kumtaja hadharani kwakuwa alishaapa kutoyaanika maisha yake binafsi hata kabla hajawa staa.

Irene alizungumza na mwandishi wetu hivi karibuni ambapo alisema kwamba mashabiki wake wanatakiwa kujua kwamba anampenzi .
"Mtu anataka niweke hadharani bwana wangu wakimjua watapata nini??
Hakuna anayeweza kumchukua mpenzi wangu hilo najua lakini masiha yangu ya sanaa tofauti na yale binafsi hivyo mashabiki wangu naomba wafahamu hilo", alisema.

Hata hivyo alisema kwamba amekuwa mtu wa kuheshimu mambo yake ya ndani kwani ndiyo yanaweza kuharibu kila kitu endapo atafanya matangazo kama wengine wanavyofanya.

DIVA, B 12, MCHOMVU WARUDISHWA KAZINI CLOUDS

$
0
0
WATANGAZAJI maarufu Bongo wa Redio Clouds Fm ya jijini Dar es Salaam, Hamis Mandi ‘B 12’, Adam Mchomvu na Loveness Malinzi ‘Diva’, wamerudishwa kazini baada ya kuomba msamaha.

Watangazaji hao walisimamishwa na uongozi wa Clouds baada ya kuchoshwa na tabia yao ya utovu wa nidhamu hivi karibuni.

UMBEA:PENZI LA PREZZO NA MTOTO WA KICHAGA STARLISHA KUTOKA TANZANIA CHALI..

$
0
0
Wakati mapenzi yanaanza kuchanua kati ya Rapcellency Prezzo na mrembo wa kichaga kutoka Tanzania Starlisha Tillya a.k.a Chagga Barbie mwaka jana, wengi tulidhani huenda zile
ndramadrama zilizojitokeza kwa wapenzi wa rapper huyo waliopita zingepungua au kuisha kabisa, lakini tayari kuna bomu limeshalipuka.

Huwa wanasema penzi ni kikohozi sababu kulificha huwezi ndio maana tulishuhudia jinsi mapenzi yalivyokuwa moto moto, na kama ni hivyo pia penzi ni kama chafya yakiharibika si rahisi kuficha cheche za kutoka ndani.
Kupitia Instagram mpenzi wa Prezzo Chagga Barbie leo amevujisha moshi unaofuka ndani ya uhusiano wa wawili hao, kwa kupost ‘private message’ walizokuwa wakichat kabla ya mambo kuharibika.

Alipost picha hii na kuandika, ‘Y nime post baadhi ya chat ni kwasababu umeanza kwa kushare kwa dada zako sasa ntarusha voice note watu wakusikie live ulivyokuwa stupid mwanaume tumamu ha act Kama K*ma kaa wewe, eti hapa ulikuwaukijibabishaaaaa lol unajua hapa nilipokuangalia ndipo nilianza kustuka nikasema huyu babu mwenye rangi za blonde kaa mie nafanya nae nini?’ Ameandika Chagga Barbie muda mfupi uliopita.
Moja ya message hizo inaonesha kuwa Prezzo na mpenzi wake walikuwa wakimjadili Diamond Platnumz ambaye mwaka jana waliwahi kuwa na beef ambayo baadaye iliyeyuka.
chagga-2
Katika post hii Chagga Barbie aliandika:
‘Unatengeneza ma video yasiyonakiwango Kutwa kumponda Diamond Mara ngapi nimemtetea huyu kinara wa East Africa usie mkubali wewe unamuita mwenzio sijui Mwajuma wewe na yeye Nani Mwajuma kaa sio wewe Natafuta namna yakuweka ur voice notes watu wakusikilize kibuyu wewe @anithakajumbula ndio kaniomba nijifanye mjinga ni cool off nikuambie yaishe kuma wewe unaevaaa boxer’
Makombora yaliendelea kutoka kwa mtoto huyo wa Kichaga anayeonekana kuwa na mkwanja wa kutosha.
chagga-3
‘Wewe Serengeti Boy uki beg nikwambie nakupenda ilikuwaje?????’
chagga-4
Katika post nyingine Starlisha ameandika:
‘chaggabarbie Sasa ukibembeleza ni kuwish Happy Bday japo nikupost ilikuwaje? Sasa nitaweka msg zote mpaka ukibembeleza nikununulie hadi Giusseppe Sneakers Ukiomba Nikupe Ticket Mat*ko wewe, mwanaume gani wewe Mario wewe ulifikiri mie nahonga mburula kaaa wewe? Nimezoea kutunzwaaaaa…….siilikuwa Ukiomba nikufichie Siri Kibamia wewe……… ‘
Upande wa Prezzo kupitia akaunti yake ya Instagram ameandika:
1st they love me then they hate me then they love they love me again…. #MswatiSpeaksHisMindVolumeTwo #TrulyUnruly #Rapcellency.
Mashambulizi kutoka kwa kambi ya Prezzo hayakuishia hapo. Dada yake na Prezzo aitwaye Kay Kivile akamlipua Chagga Barbie kwa picha hii:
9dc6c79481d311e3a9720e7aedef815c_8
Kay Kivila ameandika: Mtu anaweza akawa haongei lakin ndugu zake hawawezi kukubali………… nimeshakatazwa lakin leo sina moyo wa subira ingawa juzi niliuliza kama watu mnasamehe……. Hapo enzi ni baby yake prezzo katoka kufanyiwa operation ya kutoa tumbo, ulizeni hizo hela za shughuli alitoa nan sasa,,, anaeitwa SERENGET BOY ndo alizitoa.
Source:Bongo5
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images