Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live

Vita ya Ray C na Zamaradi Yapamba Moto

0
0
Zamaradi na Ray C
Wale Mastaa waliodaiwa kuingia kwenye bifu zito, Zamaradi pamoja na Ray C, na baadae kupatana, huku chanzo cha bifu kikidaiwa kuwa ni mwanaume, bifu hilo limeibuka tena, huku chanzo kikidaiwa kuwa ni maneno ya kejeli ya mtangazaji zamaradi mketema kwa mwanamuziki Ray C.

Hivi karibuni Zamaradi aliposti picha ya mwanae kwenye mtandao wa Instagram akim wish Happy birthday, uku aki repost baadhi ya pongezi kutoka kwa baadhi ya mastaa na mashabiki mbali mbali wa mtangazaji huyo, kitendo ambacho kilitafsiriwa kuwa mwiba kwa mwanamuziki Ray C ambaye mpaka sasa hajabahatika kupata mtoto.

Mtangazaji huyo ambaye baadae tena aliandika comment kwenye page yake, akiwauliza mashabiki wake ni kitu gani ambacho wanatamani kuwa nacho katika maisha lakini hawana? Au wengine wanavyo na vinawafanya wawe na furaha?

Comment hiyo ilizua utata uku baadhi ya wadau wakidai lile lilikuwa dongo kwa hasimu wake wa mda mrefu ray c ambaye mpaka sasa hajabahatika kupata mtoto wala kuolewa, ndipo team Ray C ilipoamua kumtag boss wao huyo ambapo Ray C hakutaka kulaza damu na kuamua kujibu mapigo kwa mtindo ule ule wa vijembe, hali iliyozua balaa uko Instagram na kuziacha team hizo mbili zikishambuliana kwa matusi ya nguoni.
“Bitchez be like (Marry Me can't u see am pregnant again)????????(Players be like(In your Dreams keep popping dem kids!!!!)lol!”-Ray C aliandika

Ray C baada ya kuona hali inakuwa mbaya, alihoji kama Zamaradi ndiye mwanamke pekee aliyezalishwa bila kuolewa apa duniani? Aliwataka watu waache kuhisi vitu ambavyo hawana uhakika navyo.
Mpaka sasa bado Zamaradi ambae siku ya jana amejifungua motto wa pili hajazungumza chochote kuhusu varangati hilo.
By Warumi-on JF

Watu Wawili Wakamatwa na Mifupa ya Albino, Walikuwa Kiuiuza Shilingi Million Tatu , Wawekewa Tego na Kunaswa

0
0
WATU wawili wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Kagera kwa kosa la kukutwa na viungo mbalimbali vya mwili ikiwemo mifupa mitatu ya mtu mwenye ulemavu wa ngozi (albino).

Kamanda wa Polisi mkoani Kagera Henry Mwaibambe alisema kuwa tukio hilo limetokea juzi katika kijiji cha Kyota kata ya Kimwani wilayani Muleba mkoani humo baada ya jeshi hilo kuweka mtego kwa watuhumiwa hao ambao walikuwa wanatafuta wateja wa viungo hivyo.

Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni James Rutozi (66) mkazi wa Kimwani ambaye ndiye aliyekuwa anahifadhi viungo hivyo na Emanueli Kaloli (50) ambaye pia ni mkazi wa Kimwani aliyekuwa anatafuta mteja wa viungo hivyo.

Alisema mara baada ya kupata taarifa kuwa kuna watu wanauza viungo hivyo kwa Sh milioni 3 waliweka pesa za mitego na kujifanya wao ni wateja na ndipo walipowakamata watuhumiwa hao wawili ambao walikutwa na mfupa mmoja na walipowabana zaidi ndipo walitoa mifupa miwili.

Alisema mnamo mwaka 2006 katika kijiji cha Rushwa kata ya Mushabago wilayani Muleba, Zeulia Jestus akiwa na miaka 24 mwenye ulemavu wa ngozi (albino) alifariki dunia muda mfupi baada ya kujifungua na ndipo watuhumiwa hao walifukua kaburi hilo mwaka 2008 kwa maelekezo ya mganga wa jadi.

Alisema pia walipotaka kujiridhisha jeshi hilo liliomba kibali mahakamani ili kufukua kaburi hilo mnamo Machi 23, mwaka huu lilipofukuliwa liligundulika kuwa viungo hivyo vimetolewa katika mwili wa marehemu huyo.

Aidha, jeshi hilo linamtafuta mganga wa jadi aitwaye Mutalemwa Revocatus ambaye ametoroka kabla hajakamatwa ambaye ndiye aliyewashawishi wafukue hilo kaburi na kuwapa dawa ya kinga ili wasidhurike wakati wanafukua.

Aliongeza kuwa mnamo mwaka 2008 wananchi wa kata hiyo ya Mushabago walitoa taarifa kwa Jeshi la Polisi kuwa kaburi alilozikwa marehemu Zeulia lilifukuliwa na watu wasiojulikana baada ya kugundua tukio hilo.

Wauza Madawa ya Kulevya Tanzania Kukiona cha Moto..Kunyongwa Ama Kupigwa Risasi Hadharani

0
0
Kijana Akitumia Madawa ya Kulevya
SERIKALI imewasilisha bungeni Muswada wa Sheria ya Udhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya wa mwaka 2014, unaopendekeza wanaobainika kufanya biashara hiyo, watozwe faini ya Sh bilioni moja au kifungo cha maisha.

Hata hivyo, wabunge wameipinga adhabu huyo na kubainisha kuwa ni ndogo ukilinganisha na kosa la kukutwa na dawa hizo na kupendekeza adhabu iwe, kifo cha kunyongwa au kupigwa risasi hadharani.

Pamoja na hayo, wabunge hao, wameoneshwa kushangazwa na mamlaka za sasa kukamata watu na dawa za kulevya na kushindwa kuwachukulia hatua papo hapo, kwa madai ya kufanya uchunguzi wakati ushahidi kamili na vilelezo vipo.

Akiwasilisha muswada huo, bungeni Dodoma jana Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge, Jenista Mhagama, alisema katika kuiongezea ukali sheria hiyo, adhabu za watu wote watakaokutwa, kutumia, kufadhili au kufanya biashara dawa za kulevya zimeongezwa na kuwa kali zaidi.

Alisema kwa mujibu wa kifungu cha 12 cha Sheria iliyopo, adhabu ya kujihusisha na kilimo cha mimea ya dawa za kulevya (mfano bangi) ni faini ya Sh milioni moja au kifungo kisichozidi miaka 20 wakati Sheria inayopendekezwa imeweka adhabu ya faini isiyopungua Sh milioni 20 au kifungo kisichopungua miaka 30 au vyote kwa pamoja.

Alisema kwa kosa kubwa la kufadhili biashara haramu ya dawa za kulevya, sheria ya sasa inatoa adhabu ya faini ya Sh milioni 10 wakati Sheria inayopendekezwa imeweka adhabu ya Sh bilioni moja au kifungo kisichopungua miaka 30.

Aidha alisema kwa wale watakaokutwa na mitambo ya kutengenezea dawa hizo za kulevya Sheria imebainisha adhabu kuwa kifungo cha maisha na faini ya Sh milioni 200.

Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugola (CCM) wakati akichangia mjadala wa kupitishwa kwa Sheria hiyo, alisisitiza kuachana na adhabu ya faini badala yake, iwe kifungo cha maisha, kupigwa risasi hadharani pamoja na kunyongwa hadi kufa na kuachana na adhabu ya faini.

Alisema ana orodha ya majina na namba za nyumba wanakoishi wafanyabiashara wa dawa za kulevya nchini, lakini hawezi kuwataja bungeni hapo kutokana na hali ya sasa kuonesha kuwa mfumo mzima unawalinda wafanyabiashara hao.

Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde (CCM), pamoja na kutaka watakaokutwa na dawa za kulevya kunyongwa au kupigwa risasi hadharani wiki mbili baada ya kuhukumiwa, pia aliitaka Serikali itafute mbinu ya kuondoa dhana kuwa wafanyabiashara wakubwa wa dawa hizo wanalindwa.

Aidha, Mbunge wa Chambani , Yusuph Salim Hussein (CUF) alihoji, “Lakini pia naomba niulize inakuaje mtu anakutwa amemeza kete tumboni za dawa za kulevya, anazitoa tumboni lakini hachukuliwi hatua eti kwa sababu ya uchunguzi, uchunguzi gani? Watu kama hawa wahukumiwe palepale...,”alisisitiza.

Mbunge wa Mbozi Magharibi, David Silinde (Chadema) alisema ni wakati sasa Serikali kuanza kufanyia kazi hukumu za kunyongwa zinazotolewa na majaji kwa watuhumiwa wa mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi au kukutwa na kuuza dawa za kulevya ili kukomesha vitendo hivi.

CCM Yamuonya Tena Lowassa..Mwenendo Wake wa Makundi Kumshawishi Kuchukua Form ya Urais Watiliwa Mashaka

0
0
Lowassa
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimesema vitendo vinavyofanywa na Mbunge wa Monduli na Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa ni ukiukwaji wa Katiba na kanuni za chama hicho.

Aidha, kimesema vitendo vinavyofanywa na Lowassa ni kampeni za wazi za urais anazoendesha kabla ya muda kufika na hivyo kukiuka Katiba na kanuni za CCM na kuonya kuwa kama ataendelea na kampeni hizo haramu atapoteza sifa za kugombea nafasi ya urais.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alitoa ufafanuzi huo baada ya waandishi wa habari waliopo katika msafara wa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kutaka ufafanuzi wa kinachoendelea mjini Dodoma kwa makundi tofauti kwenda kwa Lowassa kwa madai ya kumshawishi agombee urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.

Nape akizungumzia suala hilo alisema, “Anachokifanya Lowasa ni kuvunja kanuni na kiburi, ni matendo ya wazi ya kampeni, bila shaka anajua adhabu yake. Matendo hayo yanaweza kumpotezea sifa za kuwa mgombea kupitia CCM.”

Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi CCM Taifa aliongeza kuwa Lowassa ni miongoni mwa wanaCCM ambao walipewa adhabu na CCM mwaka mmoja uliopita kwa kuanza kampeni kabla ya wakati na mpaka sasa bado wapo kwenye kipindi cha uangalizi wakati vikao husika vikiendelea na tathmini dhidi yao.

Nape alisisitiza kuwa matendo yanayoendelea hivi sasa ni dhahiri kuwa ni kiburi kisicho na maana dhidi ya CCM.

“Lowasa anajua utaratibu wa Chama katika kuwapata wagombea wake kwa ngazi mbalimbali kuanzia udiwani mpaka urais hivyo kuendelea na matendo ambayo yanatafsiri ya wazi kuwa ni kampeni ni kiburi cha wazi. “Kwa matendo hayo ya Lowassa labda dhamira iwe ni kuomba ridhaa ya kuwania nafasi ya Urais kupitia chama kingine na si CCM.”

Nape alisema ni vyema wagombea wa ngazi mbalimbali wakahakikisha wanazingatia Katiba na kanuni za chama hicho ili wasiingie kwenye kundi la kutokuwa na sifa ya kuomba ridhaa ya kugombea udiwani, ubunge na urais.

“Tunaendelea kukumbusha na kusisitiza kwamba wale wote wenye nia ya kugombea kupitia chama chetu kuheshimu kanuni na tararibu za kupata ridhaa kugombea kwa ngazi ya chama chetu,” alisema Nape.

Lowassa amedaiwa kuwa amekuwa akitumia makundi mbalimbali kufanya kampeni ambapo alianza na kikundi cha wajasiriamali jimboni Monduli mkoani Arusha ambapo walienda nyumbani kwake kumuomba agombee.

Hatua hiyo ilifuatiwa na mashehe 50 kutoka wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani ambao nao walikwenda nyumbani kwa Lowassa Dodoma kwa lengo la kumshawishi agombee urais.

Baadaye walifuata wachungaji ambao nao walifunga safari hadi nyumbani kwa Lowassa Dodoma na kusema wameamua kumuomba Lowassa agombee urais kwa madai kuwa ana maono makubwa dhidi ya Tanzania.

Baadhi ya wachungaji hao walimwambia Lowassa wanaamini kuwa yeye ndio chaguo sahihi kwao na ndio maana wameamua kufunga safari na kumshawishi huku wakieleza kuwa kila mtu ametumia nauli yake kufika Dodoma.

Kwa upande wake Lowassa, akizungumza na wachungaji hao waliofika nyumbani kwake, alisema anafarijika kuona makundi mbalimbali yakifika nyumbani kwake kumshawishi agombee.

Alinukuliwa na vyombo vya habari juzi akisema pia kuwa hakuna kundi ambalo analituma au kulipa fedha kwa ajili ya harakati za kutaka kugombea urais.

Hata hivyo, tayari baadhi ya makada wa CCM ambao wamo kwenye orodha ya kutaka kugombea urais, wametoa malalamiko yao kuwa kinachofanywa na Lowassa si sahihi.

Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba alisema kuwa kitendo cha kuandaa watu kwa ajili ya kuanza kampeni si cha kiungwana na kwamba kila mgombea anaweza kufanya hivyo, lakini wanaheshimu kanuni na Katiba za chama chao.

January amenukuliwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari na mitandao ya kijamii akieleza wazi kuwa anaweza kutengeneza makundi kwa ajili ya kuonesha Watanzania kuwa anahitajika, lakini akasema hizo ni propaganda ambazo hazina tija kwa Taifa.

“Kama mgombea anakubalika kwa Watanzania kwanini atumie fedha nyingi kutafuta makundi ili aonekane anakubalika? Alihoji January katika ujumbe wake aliousambaza katika mitandao mbalimbali ya kijamii.

Nay wa Mitego Ashtushwa na Kauli ya Siwema Kuwa Mtoto si Wake..Aamua Kuchukua Maamuzi Magumu kudhibitisha

0
0
Nay wa Mitego na Mtoto wake
Nay wa Mitego Amesikitishwa na Kauli ya Mzazi mwenzake SIWEMA ambaye wamezaa naye mtoto kwa kusema kuwa mtoto huyo si wa kwake bali ni wa aliyekuwa  Mpenzi wake wa zamani Obasanjo...Japo Wahenga wanasema Kitanda hakizai Haramu Nay wa Mitego amehabari kuwa yupo Radhi kupima DNA ili kubaini kama mtoto ni wake ama la?

Unamshauri nini Nay wa Mitego?

Mjengo wa Diamond Wazidi Kuwa Gumzo Mjini..Thamani yake Yashtusha Watu Wengi

0
0
KUKAMILIKA kwa mjengo wa Staa wa Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond’ ndiyo habari ya mjini kwa sasa ambapo gumzo zaidi ni kuhusu gharama halisi huku mkandarasi mmoja akikisia kuwa si chini ya sh. mil. 400, Risasi Mchanganyiko linakupa stori kamili.

Akiuzungumzia mjengo huo baada ya kuuona, mkandarasi mmoja ambaye hakupenda jina lake lichorwe gazetini, alithibitisha kuwa mjengo huo unafikia sh. mil. 400 kwani umechukua nafasi kubwa, na ‘material’ yaliyojengea ni ya gharama.

”Ukitazama kwa makini, material nyingi zilizotumika kwenye ujenzi ni zile ya daraja la juu na si hizi za kawaida ambazo watu wengi wamezoea kujengea,” alisema mkandarasi huyo.Jitihada za kumpata Diamond ili aweze kuzungumzia gharama halisi za mjengo huo hazikuzaa matunda kufuatia simu yake ya mkononi kuita bila kupokelewa.

Februari mwaka 2013, nyumba hiyo ikiwa haijakamilika kwa maana ya kupambwa nje na ndani, Diamond alisema imemgharimu sh. mil. 260.Diamond aliripotiwa kuhamia kwenye nyumba hiyo wiki iliyopita, habari za uhakika zinasema kuwa nyota huyo alipata mkosi namba moja baada ya sehemu ya uzio wa upande mmoja kuanguka kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha. m

Agness Masogange Flaunts Her Killing Body.....Photos

0
0
 As usually The Diva Agness Masogange Flaunts Her K!lling Body on Photos via Her Instagram Page for men to seee.....See Photos Below



Wanaume wa Kihaya Tunachunguzwa Sana Katika Mapenzi, Mademu Wengi Wanatuogopa ..Why?

0
0
Nauliza tu Jamani kwanini mimi kama muhaya, nitakapo kuwa na uhusiano wa mapenzi na Mtanzania wa kabila tofauti na mimi, scrutiny kubwa dhidi yangu has to take place, kwani sisi male wa kihaya tunatatizo? Akina dada wengi wapo tayari kutoka na kabila lolote lakini sio
muhaya, is it that our malehood una walakini?  I understand kuna certain stigma's attached to wahaya, lakini hello, for god's sake, hii ni karne mpya, and on top sisi ni generation mpya.
 Sifurahi kusikia akina dada wakisema nitatoka na muhaya as a last resort kwani tuna shida gani ?

Naombeni majibu ndugu zangu

Kutana na Mwanaume Mwenye Hips Kubwa Kuliko Wanaume Wote Dunia

0
0
20-year-old Micah is a man but his body features will amaze you! He has hips that are larger than life, the type of hips that most women will go under the knife to get.

The guy who has the eyes of many through his Instagram account says he is an upcoming singer and songwriter from Chicago. From the photos he posts on Instagram, it is obvious he enjoys and loves who he is and all the attention that comes with it.

Qoute of the Day
'You've gotta dance like there's nobody watching,
Love like you'll never be hurt,
Sing like there's nobody listening,
And live like it's heaven on earth.'

Diamond Apondwa Kusafiri na Kundi Kubwa la Watu Kwenye Show ama Safari zake za Kustarehe

0
0
Blogger Mmoja Maarufu Amemshukia na Kumshauri Diamond Kuhusu Kusafiri na Kundi kubwa la watu wasiokuwa na Ulazima Pale anapoenda kufanya show ama kustarehe ..

Ameandika hivi :

"Anyways,wewe kama mtanzania unaonaje hizi swagga mpya za Diamona kusafiri au kufatwa nyuma na kundi la watu wakiwemo mameneja wake, ndugu,mpiga picha, etc….
Kwa maoni yangu naona kama mameneja wake wanampoteza tu. Itakuwa kaambiwa akitaka kuonekana ni big star basi lazma awe anafatwa nyuma na kundi la watu everywhere he goes.,,,,,
Nimemuelewa kidogo sababu labda kaona mastaa wakubwa wakubwa duniani huwa wanakuwaga na entourage kubwa ya watu ila jamani they can afford kuwa na watu wote wale… Some of them make over 10million dollars a year sasa kulipa watu wote hao kumfata fata ni pocket change kwake. Tayari wana utajiri ambao hata wajukuu zao watakuja kuukuta ,wana majumba in every city wengine mpaka Palm Jumeirah Dubai wana mavacation home sasa huyu kijana wetu ambae mpaka leo bado anaishi kwenye nyumba ya kupanga kwanini analipa watu kumfata fata nyuma hivi? wakati it’s very unnecessary"

Je wewe unaonaje kuhusu Hili Swala?

MTAZAMO:Diamond Platinumz Huna Uwezo ni Promo Zinazokubeba Katika Muziki

0
0
Diamond Platnumz
Diamond ni moja ya wanamziki wanaojulikana lakini ukweli ni kwamba huyu jamaa hajui kutunga nyimbo nzuri na zenye mvuto nyimbo zake za kawaida sana mfano.

Nitampata wapi halafu ukisoma jina lake tu unajua ameongelea nini, hazimpi changamoto msikilizaji. huyu Diamond anabebwa sana na promo na ndio maana anatumia gharama kubwa kufanya promo huku akitumia gharama ndogo kutunga nyimbo,ajaribu kumuiga King Kiba.

Written By Lukelo Sakafu-JF

Sugu "Kikwete Studio Uliyoitangazia Dunia Kawapa Wasanii iko wapi na Umemkabithi Nani?'

0
0
 Joseph Mbilinyi aka Sugu
Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi aka Sugu, amesema hajaweza kufanya kitu chochote kuwasaidia wasanii kwa kuwa wakati anagombea Ubunge hakuna aliyekuwa nyuma yake. Sugu amelazimika kusema hayo baada ya shabiki kutaka kujua ni kitu gani alichowafanyia wasanii tangu awe Mbunge.

''Hao wanaozingua wakamuulize Kikwete studio aliyoitangazia dunia kawapa wasanii iko wapi na kamkabidhi nani, amehoji Sugu kwenye Instagram. Rais kashindwa kuwasaidia wanataka kumlaumu mbunge wa Mbeya mjini, wakati hata hao wasanii wenyewe kimsingi hawakutusapoti kwa namna yoyote wakati tunagombea huo ubunge, wote walikuwa wanajipendekeza kwenye kampeni za CCM''.

January Makamba Amjbu Tena Lowassa Baada ya Lowassa Kumponda Katika Mitandao ya Kijamii Kuwa ni Mchanga Akalelewe

0
0
Makamba
"Hapo juzi Niliandika katika mitandao ya kijamii hasa nikizungumzia mchezo mchafu wa kisiasa unaofanywa na kambi ya ndugu EDWARD NGOYAI LOWASA. na nipende kurudia tena kuita kwamba anachoendelea kufanywa na edward lowasa kuwahadaa wananchi watanzania sasa aone kwamba tunatambua mbinu hizo chafu.\

Ndugu zangu watanzania baada yangu kuyasema haya edward ngoyai lowasa ameendelea kujitetea hasa akiandika katika ukurasa wake ya twiter na magazeti akisema amenipuuza sababu ya pili akisema mmi ni mchanga natakiwa niendelee kulelewa nikue, Naomba kumwambia lowasa udogo wangu mmi si katika Ukombozi wa maslahi ya Watanzania ila kama kweli Nitakuwa mchanga basi uchanga wangu nauona katika Kutokuwa mchafu, Mla rushwa, Mlaghai,Asiyewahadaa watanzania kwa mwamvuli wa dini,Lakini mwisho uchanga wangu ni kutowapikia ubwabwa washabiki wa siasa za Kumsafisha aliye mchafu.

Hayo niliyotaja tu ndio niko mchanga bado na kwa hayo edward ni mkongwe kupitiliza.
Mwisho namshauri edward aache maigizo na taifa hili watanzania wanahitaji kiongozi muadilifu na si anayewapa ubwabwa na kuwatumia basi kuja kwake wakiwa hawajashika tiketi za gari waliyosafiri nayo."
January Makamba.

Waganga wa Jadi Wawapinga Mkwara Jeshi la Polisi, Wasema Tabia ya Kufanya Msako na Kuchukua Vibuyu vya Itawatokea Puani

0
0
Polisi na Vifaa vya waganga wa Jadi
Wakati msako wa kuwakamata waganga wapiga ramli chonganishi ukiendelea nchi nzima hasa katika mikoa ya kanda ziwa, jeshi la polisi nchini limepewa onyo toka kwa wanganga wa jadi juu ya vifaa vinavyokamatwa wakati wa msako wao.

Jeshi hilo limepewa tahadhari ya kukumbana na hatari yeyote baadaye ikiwa wataendelea kukamata vifaa hivyo vikiwamo vibuyu, vitambaa vyeupe na vyeusi, ngao, mikuki pamoja na shanga huku likitakiwa kurejesha mara moja baadhi ya vifaa hivyo ambavyo vimekamatwa.
Katibu mwenezi wa chama cha waganga wa tiba asili nchini, (Chawatiata), Steven Sebastian kutoka Mwanza, akizungumza katika mkutano wa waganga wa jadi wilaya ya Bariadi mkoa wa Simiyu, amesema kitendo cha kuchukua vibuyu vyao, kutawafedhehesha.

Sebastiani akizungumza mbele ya kamanda wa polisi mkoani hapa, Charles Mkumbo, amesema kitendo kinachofanywa na jeshi hilo cha kukamata vifaa hivyo, ni kitendo cha hatari kwani kinaweza kusababisha hali ya migogoro mikubwa kati ya jeshi la polisi na jamii.
Sebastian alieleza vibuyu, vitambaa vyeupe, na vyekundu, shanga, ngao, pamoja na mikuki ni vifaa ambavyo waganga hao walirithishwa na wazee wa zamani ambao alieleza vifaa hivyo walivitumia katika kutafuta uhuru.

Akizungumzia hilo, kamanda wa polisi Mkumbo amesema siyo kweli waganga wa jadi wanaonewa ama kusingiziwa wanapiga ramli chonganishi, bali kutokana na uchunguzi wao wamebainika kuwapo na hali hiyo.

Wema Sepetu hutoza mpaka dola elfu 2 kumuwekea mtu tangazo kwenye akaunti yake ya Instagram

0
0
Wema Sepetu Katika Pozi
Wakati wengine wanazitumia vibaya akaunti zao za mitandao ya kijamii kutukana na kudhalilisha watu, wapo baadhi ambao wamegundua fursa ana kuzitumia kuingiza pesa.

wema

Mtaji pekee unaohitajika ili uwe katika nafasi nzuri ya kutengeneza pesa kupitia mitandao ya kijamii ni kuwa na followers wengi.

Wema Sepetu ambaye ana followers 483,905 mpaka sasa kwenye akaunti yake ya Instagram amesema kuwa hivi sasa anaitumia akaunti yake kibiashara.

mi naweza kusema kwamba linapokuja swala la utangazaji (wa biashara) imerahisisha kazi Instagram sana, the more followers you got, the more money you make. So kama unataka nipost unanilipa. So imefika hivyo sababu Instagram inatumika sana kwenye matangazo sasa hivi. Mimi nimejua maduka mengine mengi labda ya nguo, accessories hata sehemu mpya za kutengeneza keki kupitia Instagram so what its matangazo.” Wema aliiambia 255 ya XXL ya Clouds Fm.

Ni kiasi gani Wema anatoza kuweka post ya mtu Instagram?

Tunakubaliana nikiiweka post yako ninaiacha kwa muda gani, masaa matano, naiacha siku nzima[…] awe kama na dola elfu moja flani elfu mbili hivi its okay its just a post its not like am appearing on billboard” alimaliza.

Hayawi Hayawi: Wema Aonyesha Pete Yake ya Uchumba

0
0
Leo katika pita pita zangu kwenye kurasa za mastaa mtandaoni nimekutana na hii picha ya madam kwenye ukurasa wa mmoja kati ya wapambe wake na kuandikiwa maneno “Ni nini Icho kwani kidolen?”.

Picha hii ya Madam imeibua komenti  kabao huku wengine wakisifia na kutoa vijembe kwa wale wanaochonga sana kuhusu madam, huku wengine wakiendelea kuponda kuwa madamu anajifariji tu kutokana na kile wanachodai kuwa mapigo ya Diamond na Zari yanampeleka puta.

Nimnyukano tu wamaneno unaoendelea huko Insta baina ya team hizo mbili.

Wale wajuzi hebu fungukeni hiyo pete ni yauchumba au? Kama ni kweli basi tumpongeze madam kwa hatua hiyo, kuhusu nani amemvisha hata mimi sijui.

Mzee wa Ubuyu

Zitto Apigwa ‘stop’ ACT-Tanzania

0
0
Act Tanzania.
Kigingi hicho, kimewekwa na Mwenyekiti wa ACT aliyesimamishwa uongozi, Kadawi Limbu, akisema Zitto aliyejiunga na chama hicho siku nne zilizopita anapaswa kusubiri mpaka atakapotimiza miezi sita ya uwanachama wake.

Limbu ambaye bado anajitambua kama mwenyekiti halali wa ACT-Tanzania, ametoa tamko hilo wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

 “Mimi bado ndiye mwanyekiti wa ACT- Tanzania kwa vile barua inayodaiwa kuniondoa katika nafasi ya uenyekiti haikuwa halali na ilinifanya nipeleke suala hilo mahakamani kwa ajili ya kupata muongozo,”amesema.

Kwa mujibu wa Limbu, katiba ya chama hicho inaelekeza wazi kwamba mwanachama yeyote anayetaka kugombea nafasi ya uongozi ni lazima uwanachama wake uwe umetimiza zaidi ya miezi sita tangu ajiunge na chama hicho.
“Mkiangalia mtaona Zitto ambaye amejiunga na chama hicho hivi karibuni katika mazingira tata, katiba haimruhusu kugombea nafasi yeyote katika chama chetu, nimuombe kwamba andelee kuwa mwanachama wa kawaida tu,”amesema Limbu.

Pia, amemtaka Katibu Mkuu wa ACT-Tanzania, Samson Mwigamba kuacha kuwapotosha wanachama kuhusu uchaguzi huo kwani sio wa halali kutokana na Limbu kufungua kesi ya kikatiba mahakamani kupinga kuondolewa katika nafasi ya uenyekiti.
Akizungumzia chanzo cha mgogoro huo, Limbu amesema yote hayo yamechangiwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, kutokana ofisi hiyo kufanya kazi kwa utashi huku ikitoa taarifa zinazokanganya.

Limbu amefafanua kuwa ameamua kumpeleka Msajili katika Ofisi za Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kwa madai kuwa amekula njama katika kumpa barua ya kumzuia kuwa mwenyekiti wa chama hicho.
Ametoa angalizo kwamba atapigana hadi kufa kuliko kuona chama hicho walichokianzisha kwa gharama kubwa, kikiangukia mikononi mwa mafisadi.
“Kuna watu wanajiita wazalendo lakini ukiwafuatilia utabaini kuwa wamejivika kofia hiyo kwa ajili ya kunyang’anya haki za wenzao. Watu hao ni sawa na majambazi,”amesema.
Hata hivyo, uongozi wa ACT-Tanzania, umesema katiba yao, iliyoko kwa Msajili wa vyama vya siasa, inaonesha kwamba mwanachama yeyote anaweza kugombea nafasi yoyote ya uongozi endapo ametimiza siku saba tangu ajiunge na chama hicho.

When A Girl Comes To Visit You And Sits Like This (photo)

0
0

When A Girl Comes To Visit You And Sits Like This ...What would you do?

Forget LUPITA NYONG’O’s fake dress… see CORAZON wearing a $1 million dress

0
0
According to Corazon Kwamboka, the dress she is wearing in the photo below is worth 1 million USD and her boyfriend will be buying it for her.

Check it out;

Million dollar dress by @smfashionhouse. OMG! The detail in this dress is crazy Swarovski stones etc, this is why a girl finna grind to be able to buy nice things. Anyway, thank God my boyfriend is getting it fi mi. He calls me #brokepikin

Happy birthday Matilda aka Wellu Sengo...Lembebez Asiye na Mpinzani Bongo Movies kwa Uzuri

0
0
Happy born day beautiful onyinye usiyekuwa na mpinzani bongo movie kwa swaga na uzuri matata.
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live




Latest Images