Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live

Watanzania Twazidi Kuwa Juu kwenye Burudani Africa..Mtanzania Ashinda Shindano la Airtel Trace Music

0
0

Kijana anayejulika kama Mayunga ameitoa kimasomaso Tanzania baada ya kushinda shindano la music lijulikanalo kama Airtel Trace Music lililoshirikisha nchi kumi na mbili za Africa ,  shindano hilo lilifanyika jumamosi iliyopita nchini Nairobi ..Kwa ushindi huo Mayunga amepata deal la kuwa chini ya Record label ya Mwanamuziki Akon ijulikanayo kama Kon live na  Universal music Group.... Mayunga anaungana na kina Diamond na Idriss katika kuitangaza Tanzania vizuri katika ramani ya Dunia kwenye maswala ya burudani


Team Wema Wakwera na Tabia ya Watu Kumzushia Wema

0
0
Baada ya Picha za staa mrembo kutoka Bongo Movies, Wema Sepetu akiwa na mshindi wa Big Brother Africa (BBA) 2014, Idris Sultan wakiwa kwenye moja ya supermarket hapa jijini Dar kusambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii zaidi ya moto wa vifuu  huku kila mtu akiandika lake kuhusiana na kile alichokiaona, Team Wema waneoneshwa kukerwa na tabia za watu kumzushia Wema  kwenye mahusiano.

Licha ya ukweli ni kwamba Wema na Idris wanaonekana kikazi zaidi, yaani ulikuwa ni wito maarumu kutoka kwa wenye  supermaket hiyo, watu wengi wameolionekana kupakaza kuwa wawili hao ni Le Project mpya na wengi wakimtupia maneno Wema kuwa hisaa amezidiii na wengine wakimlaumu Idris kuwa ameingia chaka.

Kitendi hiki cha Wema kuzushiwa kuwa na mahusiano na watu ambao anafanyanao kazi kimewakera sana Team Wema na kusababisha timbwili la maneno mitandaoni.

Imekua kama tabia ya watu ku comment ( yani ndo umeamua kua na wema) ( wema ndo unatoka na huyu) kwa kila mtu anae fanya nae kazi.. Naomba kuwauliza inamana nyie hamuon kama hizo ni kazi?? Mme shindwa tu kwa Millard Ayo na project ya the completePackage kusema anatoka na wema . Watu wameshindwa kutofautisha kati ya X na + ntaomba Diamond awasaidie kuwapa darasa ama ASEME NA NYIYI. Ama nene".  

Mmoja kati ya team Wema aliandika mtandaoni.

Haya Ndio Maelezo ya JB Kuhusu Watu Wanaotaka Kuigiza Naye

0
0
Habari,mara nyingi nimekuwa nikipokea maombi ya watu kutaka kuigiza, jamani kuna team ya ma director ndio wanafanya kazi hii sio mimi, na hawawezi kukuchagua kwa kusema tu, mpaka wakuone ukiigiza mahali nawavutiwe.

Please  anza hata kwenye tamthilia.naamini wapo waigizaji wengi wenye vipaji lakini ni lazima uanzie sehemu kabla ya kufika kwetu.asante. JB ameandika haya kwenye ukurasa mtandaoni.

Davido Awauzi Wakenya Vibaya Alipoenda Nchini Humo Kuburudisha Jumamosi iliyopita

0
0


Today the theme is Davido. No artist has generated more hate from Kenyans in recent years than the Nigerian, and looking at the events of the past weekend, it’s clear why.

Davido started off his visit at NTV studios, and it was obvious he had no idea he was inside the largest media house in East Africa, perhaps even larger than any private media in Nigeria.

His pride and arrogance started when he met Victoria Rubadiri and Yvonne Maingi, and continued downstairs on Kimathi Street as he was being interviewed by Larry.

We have written extensively about that.

Read: Davido Angers Kenyans With His Arrogance on The Trend

Read: Hilarious Memes After Davido’s 20 Minutes Performance

On Saturday night, the Nigerian disappointed fans at Carnivore after giving a performance of less than 30 minutes. Below we have some reactions from Twitter.





Zitto aichokoza Chadema na kuwapa somo wanachama wake

0
0
KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT – Wazalendo, Kabwe Zitto ameahidi chama chake kuendesha shughuli zake kwa uwazi, ikiwa ni pamoja na kupiga marufuku viongozi kufanya biashara na chama hicho, jambo ambalo limekuwa likidaiwa kufanyika ndani ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambako aliwahi kuwa Naibu Katibu Mkuu.

Ndani ya Chadema, mara kadhaa imekuwa ikidaiwa kwamba Mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe, amekuwa akifanya biashara na chama chake.

Akizungumza wakati wa hotuba yake ya uzinduzi wa ACT-Wazalendo uliofanyika jijini Dar es Salaam jana, Zitto, bila kutaja chama wala jina la mwanasiasa yeyote, alisema chama chake kinapozungumzia wananchi kurejesha taifa mikononi mwao ieleweke kwamba wanazungumzia uwajibikaji.

“Chama cha ACT Wazalendo kimeelekeza kikanuni kwamba kila kiongozi wa chama lazima atangaze mali zake na madeni yake. Kila kiongozi lazima aweke wazi maslahi yake ya kibiashara na mengineyo wazi ili kila anapotenda au kusema jambo wananchi wajue maslahi aliyonayo au la katika suala husika.

“Viongozi wote wa kitaifa wa ACT Wazalendo wamefanya hivyo na tutaweka saini zetu mbele yenu kama mashahidi. Naomba Mwanasheria wetu aje hapa tutekeleze matakwa haya ya kikanuni.

“Fomu hizi zitakuwa kwenye tovuti ya chama ndani ya muda mfupi ujao ili kila mtanzaina aone. Kila Kiongozi wa Chama ambaye miiko ya uongozi inamtaja anapaswa kuwa amejaza fomu hizi na kuziwasilisha kwa Katibu wa Kamati ya Uadilifu katika ifikapo tarehe 30 Juni 2015.

“Tunapopinga viongozi wa umma kufanya biashara na serikali na hivyo kuwa na mgongano wa kimaslahi na kushamiri kwa ufisadi, hivyo hivyo tunapinga viongozi wa chama chetu kufanya biashara na chama. Ni marufuku serikali kugeuzwa kuwa genge la watu wachache wanaopora rasilimali za umma. Uadilifu tunaoutaka serikalini ni lazima uanzie kwetu tunaohubiri.

“Tutafanya haya kwa kubadilisha siasa zetu kuelekea kwenye masuala yanayowahusu wananchi; wakulima, wafanyakazi, wafanyabiashara ndogo ndogo, vijana, wanawake na wazee wetu.

“Tunataka kurejesha nchi yetu Tanzania kwa kujenga uchumi wa wote. Tunaporejea kwenye Azimio, hatusemi tunakwenda kutaifisha kila kitu na Serikali kuendesha shughuli zote za kiuchumi. Tunaheshimu na kuthamini sekta binafsi na mchango wake katika kukuza uchumi na kuleta maendeleo.

“Tunamaanisha kuwa ni lazima Dola isimamie uchumi. Sio kazi ya Serikali kufanya biashara. Lakini tunamaanisha kuwa ni lazima kurekebisha baadhi ya makosa yaliyofanyika kwenye ubinafsishaji na hususan ubinafsishaji holela uliofanyika kwenye sekta ya Kilimo na kupora ardhi ya wananchi wetu na kuwageuza kuwa manamba kwenye ardhi yao wenyewe. Tunataka kutomokeza ukwepaji kodi,” alisema Zitto.

CHANZO: Raia Mwema

Kaka Yake Gwajima Amtaka Amuombe Radhi Pengo

0
0


Kaka wa Askofu wa kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima aitwaye Methusela Gwajima amemtaka mdogo wake kwenda kumuomba radhi Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki Dar es Salaam Mhadhama Polycarp Kadinali Pengo kwa kutoa lugha ya kumkashifu.

 

Akizungumza na wanahabari leo Jijini Dar es Salaam, Methusela alisema ameamua kutokufumbia macho kitendo cha ndugu yake kumkashifu Pengo na kwamba anapaswa kujitathimini alipopotoka kwa kumtukana kiongozi mkubwa wa kiroho kwani ni sawa na kuidhalilisha familia nzima ya Ukoo wa Gwajima.

 

Alisema maneno yake ya kashfa ni dhahili ya kuwa hata ukoo mzima umedhalilishwa hivyo familia ya Methusela Gwajima  imemtaka  kuomba radhi mara moja.

 

Hata hivyo alisema kuwa yeye ni kada wa CCM hivyo amepata usumbufu mkubwa tokea sakata hilo liibuke maana ndugu na marafiki walioko nje ya nchi wamekuwa wakimuuliza kuhusiana na suala hilo hali inayompa wakati mgumu kuwapatia majibu.

 

Alisema kashfa hizo hazina tija kwa taifa na haileti uhusiano mwema baina ya madhehebu ya dini, bali  yanachochea  chuki, uhasama, utengano na hasira kati ya wakristo kwa wakristo.

Tamko la maaskofu na wachungaji wa kipentekoste juu ya kuugua ghafla kwa askofu Gwajima

0
0

TAMKO LA MAASKOFU NA WACHUNGAJI KUTOKA MADHEHEBU MBALIMBALI JUU YA TUKIO LA ASKOFU GWAJIMA.

Sisi maaskofu na wachungaji kutoka makanisa mbalimbali tumeshtushwa na kusikitishwa kwa taarifa ya ugonjwa wa Askofu na mtumishi mwenzetu Josephat Gwajima ambaye tarehe 27/03/2015 alifika kituo cha polisi cha kati kuitikia wito wa polisi uliomtaka kwenda kujibu shutuma za kutumia lugha ya matusi kwa kardinali Pengo.

Tumepata fursa ya kutafakari na kujadili kwa kina hali iliyompata Askofu mwenzetu hasa baada ya kuzingatia kuea Askofu Gwajima alifika polisi akiwa mzima na mwenye afya njema lakini wakati wa akihojiwa na polisi, hali yake ilibadilika ghafla kiasi cha kupelekea yeye kulazwa hospitali ya TMJ akiugua tena kwenye wodi ya wagonjwa mahututi yaani (ICU) katika chumba cha uangalizi maalum.

Maswali yetu makuu ni kitu gani kimempata mwenzetu? Tunajiuliza, je vyombo vya usalama vimekua sio sehemu salama kama zamani?

Tukiwa bado tunatafakari hill, tumeshtushwa tena baada ya kupata taarifa ya kuwa Wachungaji Wasaidizi wa Askofu Gwajima pamoja na walinzi wake waliokuwepo hospitalini hapo kwa ajili ya kumuuguza nao pia wamekamatwa kwa tuhuma za. kutaka kumtorosha Askofu Gwajima. 

Jambo hili linashangaza zaidi maana wachungaji wale wale waliokuwa naye akiwa mzima wa afya wakati anaelekea polisi ndio wale wale wanatuhumiwa kutaka kumtorosha akiwa mgonjwa.

Ni jambo la kushangaza na lisiloingia akilini kuwa wasaidizi hao wa Gwajima walitaka kumtorosha wakati Gwajima kama angekua na nia hiyo angekwisha fanya hivyo mana alikuwa na uwezo wa kutoroka alipokua Arusha kwenye kikao cha Maaskofu wakuu wa makanisa ya Kipentekoste ambao alipata taarifa za kuitwa Polisi.

Isitoshe Gwajima aliitija wito na kwenda polisi mwenyewe kwa miguu yake bila kushurutishwa, wala hakufikishwa polisi kwa nguvu.

Swali: Kama alikua anaona ugumu wa kutoroka wakati hakuna polisi anayemlinda na huku akiwa mwenye afya tele, itakuaje rahisi kutoroshwa leo akiwa mahututi na akiwa kwenye ulinzi mkali wa polisi?
Mbona hii inastaajabisha?

Jambo jingine linalotupa shida ni kuhusu mlalamikaji wa kesi hii inayomkabili Askofu Gwajima. Tumeelezwa na wasaidizi wa Askofu Gwajima kuwa pale polisi walielezwa kuwa aliyefungua kesi hii sio Pengo ila mtu mmoja aitwaye Aboubakar.

Kwa ufahamu wetu juu ya sheria unatutuma kuamini kuwa Aboubakar sio MTU sahihi wa kufungua kesi hiyo sababu hawezi kutuonyesha ameumizwa kiasi gani na matamshi ya Askofu Gwajima.

Isitoshe, Kardinali Pengo mwenyewe ametamka katika Ibada yake ya Jumapili hii ya tarehe 29/03/2015 kuwa amemsamehe Gwajima, yupi tena mwenye uchungu wa kumzidi Kardinali Pengo?

RAI YETU: 
Rai yetu ni kwamba, ni vizuri serikali pamoja na vyombo vyake vya usalama vikatumia weledi katika kushughulikia mambo ya kidini na viongozi wake kwani yanaweza kusababisha chuki dhidi ya serikali na pia kupelekea mpasuko mkubwa wa kidini katika jamii yetu iliyo na historia nzuri ya umoja na mshikamano na ushirikiano katika matukio yote ya kimaisha.

Tunaomba serikali isaidie kuondoa mkanganyiko huu na busara kubwa itumike ili kuepusha uvunjifu wa Amani katika jamii.

MAAMUZI YETU:
Jambo hili linazungumzika, maana hata hivyo tumeshaazimia kukutana na IGP ili kupata suluhisho juu ya jambo hili.

Kwa niaba ya maaskofu na wachungaji:

Mwenyekiti: Askofu Dr. Mgullu Kilimba
Katibu: Askofu Dr. Dramas Mukassa

Na mwandishi
F.A.K
30/03/2015

Wahalifu wa Mitandao, Wasambaza Picha za Utupu na Ngono na Wasambaza Uongo Mitandaoni Kwenda Jela Miaka 10 ama Faini Mil 50

0
0
WAHALIFU wa mtandao pamoja na wasambazaji wa picha za utupu na ngono, wasambazaji wa taarifa za uwongo, za kibaguzi na matusi na watu wengine ambao wanafanya udanganyifu unaohusiana na kompyuta wametungiwa sheria kali ambayo itawafanya kwenda jela hadi miaka 10 au kulipa faini isiyopungua Sh milioni 50.

Miongoni mwa miswada ya sheria utakaowasilishwa bungeni na Serikali wiki hii mjini hapa, ni Sheria ya makosa ya mtandao ya mwaka 2015 ambayo imeainisha makosa mbalimbali yanayofanywa na wananchi katika kipindi hiki ambacho matumizi ya mtandao wa kompyuta yameongezeka.

Baadhi ya makosa yaliyoainishwa kwenye sheria hiyo ni kughushi kunakohusiana na masuala ya kompyuta, udanganyifu unaohusiana na kompyuta, ponografia za watoto, picha za utupu, matusi na ngono, makosa yanayohusiana na utambuzi, uwongo, ubaguzi, matumizi ya kibaguzi, mauaji ya kimbari na unyanyasaji kupitia mtandao wa kompyuta.

Katika sheria hiyo, mtu atakayesambaza ponografia ya watoto kupitia mtandao wa kompyuta atawajibika kulipa faini isiyopungua Sh milioni 50 au mara tatu ya faida iliyopatikana kinyume cha sheria au kifungo kisichopungua miaka saba jela au vyote kwa pamoja.

Mkosaji pia ataamriwa kumlipa mwathirika fidia. Kwa upande wa kusambaza picha za ngono, matusi, uasherati atalipa faini isiyopungua Sh milioni 30 au kwenda jela miaka 10 au vyote.

Lakini mtu atakayesambaza picha za utupu atalipa faini isiyopungua Sh milioni 20 au kwenda jela miaka saba au kutumikia adhabu zote kwa pamoja.

Pia kweye muswada huo mtu ambaye atatoa taarifa, data au maelezo kwa njia ya picha, maandishi, alama au aina nyingine yoyote zikiwa ni za uongo akipatikana na hatia atalipa faini isiyopungua Sh milioni 3 au kutumikia kifungo jela kisichopungua miezi sita au vyote.

Kwa upande wa ubaguzi, sheria hiyo inakataza mtu kutumia mtandao wa kompyuta kutozalisha vitu vya kibaguzi kwa madhumuni ya kuvisambaza na iwapo atatiwa hatiani atalazimika kulipa faini ya Sh milioni tatu au kifungo cha mwaka mmoja jela.

Pia mtu akimdhihaki mtu mwingine kwa kupitia mfumo wa kompyuta kwa mwelekeo wa ubaguzi wa rangi, kabila, asili, utaifa au dini fulani akitiwa hatiani atatozwa na Mahakama faini ya Sh milioni tatu au kifungo cha mwaka mmoja jela au vyote kwa pamoja.

Pia sheria hiyo inakataza mtu kuchapisha au kusababisha kuchapishwa vitu vinavyochochea au kuhalalisha matendo yanayopelekea mauaji ya kimbari na makosa dhidi ya binadamu kwa kupitia mtandao wa kompyuta.

Mtu atakayefanya hivyo atakuwa ametenda kosa na akitiwa hatiani atawajibika kulipa faini isiyopungua Sh milioni 10 au kutumikia kifungo kisichopungua miaka mitatu au vyote kwa pamoja.

Pia muswada huo wa sheria unakataza mtu kutoanzisha usambazaji wa taarifa zinazotumwa bila ridhaa na ukitiwa hatiani utatozwa faini ya Sh milioni 3 au mara tatu ya faida iliyopatikana kinyume cha sheria au kutumikia kifungo kisichopungua mwaka mmoja au vyote kwa pamoja.

Emmanuel Mbasha Afunguka sakata la Gwajima katika Twitter, Asema Hayuko Tayari Kurudiana na Mkewe

0
0
Katika Sakata linaloendelea sasa la Gwajima Kumtukana Askofu Pengo na la Kuzidiwa na Kukimbizwa Hospitalini akiwa mikononi mwa Polisi , Emmanuel Mbasha ambae inasemakana yeye na mkewe kuachana kuna mkono wa Gwajima ametoa maoni yake kuhusu Sakata la Askofu Huyo..
Jisomee Hapa Chini:

Maoni: Alikiba Atazidi Kupitwa kila Siku, Kama R Kelly Anakujua Why Dunia isikujue?

0
0
Mi ni team Ali Kiba forever ila jamaa anazingua na sijui anajisikia au vipi maana kila siku anaambiwa hasikii kama atataka kushindana na Diamond naona kachelewa sana.

Katoa audio ya chekecha cheketua siku hizi video ndio inakutambulisha kimataifa kakaa kama mjinga fulani, Diamond katoa video ya nyimbo yake nyimbo ya kawaida sana Sema hafanyi kama Kiba kutanguliza audio. 

Dogo mjanja sana katoa video akijua itazidi kumtambulisha kimataifa. Naona Namibia, Ghana, Nigeria, Botswana wanacomment kuhusu video. Ali Kiba unalala tu.

Tuwe wawazi team Kiba Tunajua Diamond yupo juu Sema Diamond Hana kipaji kama Ali Kiba ila ukiendelea hivi utakimbiwa halafu dogo ana dharau ndo maana Hata instagram hajamfollow mtu yeyote.

Diamond big up ishu ni kujulikana kimataifa maana Tanzania umemaliza tayari Kiba ukitaka kuwa juu sikiliza mashabiki acha dharau na angalia soko linaendaje acha ujinga team Kiba tupo pamoja.

Ni ushauri maana tunataka ujulikane Dunia nzima kama R Kelly anakujua why Dunia isikujue? Jitambue.

By Vidodi

Mapya ya Gwajima yazidi kuibuka Dar, Bastola iliyokamatwa Juzi Gwajima Anaimiliki Kihalali

0
0
Mfano wa Bastola iliyokutwa
MAPYA yamezidi kuibuka katika sakata la Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Joseph Gwajima, baada ya kuthibitika kwamba bastola iliyokamatwa katika harakati za kile kinachotajwa kutaka kumtorosha kutoka katika Hospitali ya TMJ, Dar es Salaam, ni mali yake.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alisema jana kuwa uchunguzi wa kina na wa kitaalam, sasa umethibitisha silaha hiyo inamilikiwa kihalali na Askofu Gwajima.

“Kuhusu risasi 17 za short gun ni kwamba Askofu Gwajima anamiliki bunduki aina ya short gun yenye namba 102837 ambayo inatumia risasi za aina ya hizo zilizokamatwa,” alisema Kamanda Kova.

Bastola hiyo ni moja ya vitu walivyokamatwa navyo wafuasi 15 wa Gwajima, wanaodaiwa kula njama za kutaka kumtorosha usiku wa kuamkia Jumamosi iliyopita.

My Take: Najiuliza tu kwa sauti je ? Wachungaji kumiliki silaha inaingia akilini? Nilitegemea wanategemea sana ulinzi wa Mungu 

Tambua Aina ya Wanaume wenye Mvuto zaidi kwa Wanawake

0
0
Kuna aina kuu mbili zinazo wafanya wanaume wawe na mvuto mkubwa kwa wanawake, ambazo ni:-

RICH AND SUCCESSFULL MAN:- hawa kwa sasa ndiyo habari ya mujini......... ukijijua wewe mambo yako swaaafi, kuanzia kwenye pochi,,,,, nice house,,,,,,,, expensive cars....... Jua kwamba unatamaniwa mbayaaaaa, yaani hapo ukimbeep tu tayari unae!!!!!
(ila kuweni makini hapa wenye mapenzi ya dhati ni robo/kilo wengine wanatafuta watu wakuwang'arisha kimaisha tu)

GOOD SEX:- Hapa kama kitandani hujiwezi jua tayari umeshapoteza mvuto kwa mwanamke, hata kama una large penis halafu ubanjukaji ni ziro jua itabaki kuwa urembo tu hapo kati!!!!!!! You must have a right way to turn your woman on, discover her 'hot spots' and make sure she finishes first............ Atakupendajeeeeee!!!!!!!!!!!!!

SIFA NYINGINE ZA ZIADA ZINAZO MVUTIA MWANAMKE

=>mwanamme ambaye yuko strong and healthy body 

=>good haircut (sio wale wahuni waviduku,,,,, kwangu naona kama uchafu)

=>wanaume warefu nao wanamvuto wake jamani, hasa pale unapoongozana nae au pale anapokukiss.....daaaaaaaah!!!! !!!!

=>A man's cloth; mwanaume anaweza akawa anamvuto zaidi machoni pa mwanamke endapo atatupia vyema kabisa zile 'bring bring' sio mguuni una kiatu cha pink, trouser ya njano na shati lako jekundu mweeeeeee....... Hata salamu yako haita itikiwa!!!!!!!!

=>sensitive lips and kind eyes (hasa wale wenye dark eyes hao wanamvuto sana)

muscular, a six pack men, mwenye sauti nzito kiasi yakubembeleza, mwenye pua nyembamba kiasi (sio pua imezagaaa mpaka karibia na mashavu).

Nyingine wadada mtaongezea!

Tumia Bidhaa za AFRICAN BEAUTY PRODUCTS Kupata Muonekano wa Kupendeza kwa Kuongeza Hips, Makalio, Mapaja, Kurefusha Nywele na Mengine

0
0

Je unataka Kuwa Mrembo na Muonekano wa Kupendeza kwa Kuongeza Hips, Makalio, Mapaja, Kurefusha Nywele, Kupunguza Unene na Kuondoa Tumbo?Basi African Beauty Products Wanakuletea Hii:

Kabla ya Kutumia Dawa na Baada ya Kutumia Dawa zetu
1.Kuongeza Hips Makalio na Mapaja 100,000/
2.Kunenepesha Miguu iwe chupa ya Bia 70,000/
3.Kuwa Mnene Mwili Mzima 80,000/
4.Kupunguza Tumbo na Nyama Uzembe 80,000/
5.Kupunguza ama Kuongeza Maziwa 60,000/
6.Kuwa Mweupe na Soft Mwili Mzima 100,000/
7.Kuondoa Chunusi na Madoa 60,000/
8.Kuondoa Michirizi na Mabaka 70,000/
9.Kupunguza Unene Mwili Mzima  80,000/
10.Kuongeza urefu na unene wa Uume 90,000/
  
Bidhaa Zetu ni Uhakika Matokeo  Ndani ya Week Moja..
Tuwasiliane kwa Simu Namba:
0756697906 ,0716805391 au 0783300397
  
Kwa watu wa Dar es Salaam Utaletewa Popote Ulipo ..Kwa Watu wa Mikoani tunatuma kwa Basi

Gwajima Afunguka......Asema Aliagiza Bastola yake ili Ajihami Baada ya Taarifa Kuzagaa Mitandaoni kuwa Amefariki Dunia

0
0
Hii  ni  Picha  iliyosambazwa  katika  mitandao  ya  kijamii  ikidai  kuwa  Gwajima  kafariki  dunia  na  yuko  Mochwari.Taarifa  hizi  zilimpa  hofu  Gwajima  na  kumfanya  Aagize  Bastola  yake  kwa  ajili  ya  kujihami.
**********

Utata umeibuka kuhusu bastola waliyodaiwa kukamatwa nayo wafuasi wa Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Askofu Josephat Gwajima baada ya kiongozi huyo kusema anaimiliki kihalali kinyume na maelezo ya polisi.
  
Gwajima aliyetolewa kwenye chumba cha uangalizi maalumu cha Hospitali ya TMJ jana, amelitaka Jeshi la Polisi kurudisha bastola hiyo, akisema ni mali yake na aliiagiza ipelekwe hospitalini kwa sababu ya kujilinda.
 
Akizungumza na waandishi wa habari hospitalini hapo alipolazwa baada ya kuishiwa nguvu na kupoteza fahamu akiwa katika mahojiano na polisi, Gwajima alisema anashangaa kukamatwa kwa wachungaji wake waliokuwapo kwa ajili ya kumlinda.
 
Hata hivyo, katika kwa upande mwingine, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema bunduki hiyo haina umiliki halali wa Gwajima wala wa wachungaji 15 waliokamatwa lakini baadaye jioni baada ya maelezo ya Gwajima, alitoa taarifa akisema bastola hiyo ni mali halali ya askofu huyo. Pia alisema kuhusu risasi 17 za bunduki aina ya Shortgun, Gwajima anamiliki bunduki ya aina hiyo lakini akasema uchunguzi kuhusu watu hao 15 unaendelea.

Kauli ya Gwajima
Akizungumza kwa shida akiwa amejishika tumbo, Gwajima alisemaalipopata taarifa za uvumi kwenye mitandao ya kijamii kuwa amefariki dunia, aliagiza wachungaji waende hospitalini kwa ajili ya kumlinda, lakini wakaishia mikononi mwa polisi wakidaiwa kutaka kumtorosha.
 
Alisema alihofia kuwapo kwa watu wabaya ambao wangeweza kumdhuru halafu wakasingizia kitendo hicho kufanywa na polisi kwa kuwa alipata tatizo akiwa mikononi mwao.
 
“Usiku wasiwasi ulizidi, huku kila mmoja akiwa hafahamu kwa nini ujumbe wa namna ile unasambazwa kwenye mitandao, msambazaji ni nani, ana nia gani, nikaamua kuwaagiza waniletee silaha yangu iliyokuwa kwenye begi ili likitokea lolote niweze kujilinda,” alisema Gwajima.
 
Alisema alishangaa kukamatwa wachungaji wake na kuchukua silaha iliyokuwa ndani ya begi na hadi jana hakuwa ameulizwa chochote kuhusu umiliki wa silaha hiyo.
 
“Kabla sijazungumza na waandishi kueleza ukweli wa kinachodaiwa kuwa nilitaka kutoroshwa na wachungaji wangu, nilitaka kuzungumza na ZCO (Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalumu), lakini hajaja, kadi ya ile silaha ninayo,” alisema Gwajima.
 
Alisema madai kuwa alitaka kutoroka ilihali polisi alikwenda mwenyewe akitokea Arusha baada ya kusoma katika vyombo vya habari kuwa anatafutwa.
 
Alifafanua kuwa hata alipofika polisi kwa ajili ya mahojiano hakuwa na shaka hata kidogo, lakini alishangaa kuona anaishiwa nguvu kila baada ya muda na alipoona kichwa kinamuuma, akawaomba wampeleke hospitali ili mambo mengine yafuate baadaye, kitu ambacho hakikufanyika kwa wakati.
 
Wasiwasi kwa polisi
Alisema alijaribu kuomba apelekwe hospitali mara kadhaa, lakini hakuna aliyekubaliana naye hadi alipopoteza fahamu na kupelekwa hospitali ya Polisi Kurasini.
 
“Hivi hata kama ni chombo cha usalama, nimepata matatizo nipo mikononi mwao, halafu nikubali kutibiwa katika hospitali yao, sikulitaka hilo na hata waliposema nikatibiwe Muhimbili pia sikutaka, ndiyo maana nilikuja hapa, sisemi moja kwa moja kama Polisi wanahusika lakini kuna vitu vinanitia shaka,” alisema Gwajima.
 
Alieleza kuwa anatilia shaka Jeshi la Polisi kutokana na kuwapo vitu vingi vinavyoashiria wana kitu kingine wanatafuta, kwani jana tulikuwa na hofu ya kuvamiwa, waliokuja kutuvamia ni wao, sikugombana na Pengo, nilikuwa namkemea kama kiongozi mwenzangu wa kiroho wao, wameligeuza ni kesi.
 
“Sijawahi kulitilia shaka Jeshi la Polisi lakini katika hili napata wasiwasi mwingi, sina ugomvi na Kardinali Pengo, nampenda, hajanilaumu, wala kunishtaki, nilikuwa namkemea katika masuala yetu ya mabaraza ya dini na siyo vinginevyo,” alisema Gwajima.
 
Gwajima pia alionyesha wasiwasi wake kwa kile kilichokuwa kinang’ang’aniwa na polisi kwenda kupekua nyumbani kwake kuwa hakikuwa kitu kizuri.
 
Kova alipinga
Wakati Gwajima akisema hayo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema bastola waliyokutwa nayo wafuasi wa Gwajima haimilikiwi kihalali.
 
“Tumegundua kuwa katika wale watu waliokuwa pale akiwamo Gwajima mwenyewe, (bastola) haikuwa  katika umiliki wao halali, kwa hiyo hapa kuna kesi ya kupatikana na silaha bila kibali.”
 
Akizungumzia tuhuma kwamba polisi walimpekua mke wa Gwajima, Kova alisema hakuna polisi waliofika nyumbani kwake kufanya upekuzi wowote na kama wakitaka kufanya hivyo watafuata taratibu maalumu za upekuzi.
 
Akijibu swali kuhusu mahali Gwajima alipotakiwa kutoroshewa, Kova alisema uchunguzi huo bado unaendelea na utakapomalizika wahusika watafikishwa mahakamani.
 
Pia alipoulizwa kama Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo amemsamehe Gwajima, kwani polisi imng’ang’anie, Kova alisema;“amesema anamsamehe lakini haingilii mambo ya sheria.”
 
Kuhusu sababu za Gwajima kuzimia wakati akihojiwa, Kova alisema anayepaswa kuulizwa kwa nini alianguka wakati akihojiwa na polisi ni Gwajima mwenyewe.
 
“Siri za mahojiano huwa hazitolewi kabla ya ushahidi mahakamani, sababu ya kupata shock (mshtuko) atajua mwenyewe, kwa kuwa ukifanyiwa jambo ukafurahi au ukachukia wewe ndiyo unajua ilikuwaje, chochote kitakachotokea ukicheka, ukinuna, ukizimia, wewe ndiyo tukuulize ilikuwaje mpaka ukazimia kwa sababu hisia unazipata wewe,”alisema Kova.

Makonda amtembelea
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda ambaye alikuwa amemwandikia Gwajima barua akimwita ofisi kwake, jana mchana alimtembelea hospitalini hapo kwa ajili ya kumjulia hali kiongozi huyo lakini akasisitiza kuwa nia yake bado ipo palepale.
 
“Nilimtaka leo aripoti ofisini kwangu lakini kwa bahati mbaya anaugua na amelazwa. Nitakwenda kumuona ili nijue hali yake ikoje,” alisema Makonda kabla ya kufunga safari kwenda hospitali alikolazwa.
 
Alisema pia atataka kiongozi huyo wa kiroho amweleze anavyoelewa maana ya uhuru wa kuabudu unaoelezwa katika Katiba, usajili wa taasisi yake na katiba ya taasisi hiyo. 
  
“Mimi ni mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kinondoni. Niliagiza polisi wamkamate na baadaye wakimaliza kumhoji aje kwangu pia atahojiwa na jopo la watu 20,” alisema Makonda.
  

Mbunge Shyrose Bhanji Afunguka Ugonjwa Unaomsumbua

0
0
Mbunge katika bunge la Afrika Mashariki,Shyrose Bhanji amefunguka ugonjwa unaomsumbua kwa muda mrefu uliomfanya alazwe katika hospitali ya Agha Khan,jijini Dar.

Akizungumza na Clouds Fm, Shyrose alisema kuwa amekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa Pumu(asthma) kwa muda mrefu tangu akiwa mdogo lakini safari hii ugonjwa ulizidi sana hali iliomfanya kulazwa hospitali kwa siku kadhaa.

"Huu ugonjwa huwa unanisumbua kwa muda mrefu lakini hadi kufikia hatua ya kulazwa ni safari hii hali ilikuwa mbaya sana lakini namshukuru Mungu nimepewa matibabu naendelea vizuri,’’alisema Shyrose.

Aidha aliongeza kuwa mara ya mwisho kuugua hadi kufikia hatua ya kulazwa ilikuwa miaka mingi sana wakati akisoma nchini Uingereza,pia hali ya hewa ya baridi huwa ni tatizo kwake.

Video ya Davido akimponda Diamond kuwa Nyimbo zake Hazipigwi Nigeria wikii hii alipokua Kenya

0
0
When asked by Larry whether East African music receives airplay in Nigeria, Davido gave a brutally honest NO. He even admitted that this collabo with Diamond ‘Number One’ is not played in Nigeria. As true as it may be, that came out badly from a guy who was about to perform in Kenya.

Baada ya Kuhamia Nyumba Mpya, Diamond na Zari Roho Mkononi, Yabainiki Kwake ulinzi ni Sifuri, Mwenyewe Akiri Kuishi kwa Hofu

0
0
TAHADHARI ichukuliwe! Habari zikufikie kuwa, baada ya staa mkubwa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz‘ na mpenzi wake, Zarinah Hassani ‘Zari’, kuhamia kwenye mjengo wake mpya uliopo Madale jijini Dar, imebainika kuwa familia hiyo inaishi roho mkononi kufuatia ulinzi sifuri, jambo linalowafanya kuishi kwa hofu tupu

Kikizungumza kwa hofu juu ya familia hiyo, chanzo chetu makini kilipasha kwamba, pamoja na Diamond kutumia mamilioni ya fedha kujenga nyumba hiyo ya gharama kubwa, sasa changamoto imehamia kwenye ulinzi na usalama wao

“Jamani watu wanampongeza Diamond kwa kuhamia nyumba mpya lakini wale jamaa aisee wanapaswa kuombewa kila kukicha.

“Pamoja na kushusha mjengo wa maana bado changamoto ni juu ya ulinzi wao.

“Huwezi kuamini Diamond bado anaishi kizamani sana na sijui kwa nini anajiamini kiasi hicho wakati anajua wazi kuwa yeye ni staa wa Afrika na hapaswi kuishi kwa ulinzi hafifu.

MAENEO HATARISHI?

“Nasema hivi kwa sababu hata maeneo anayoishi ni hatari sana kwake hivyo anatakiwa kuwa na ulinzi mkali ili tu siku moja asije akafanyiwa kitu ambacho taifa likaingia kwenye hasara ya kumpoteza nyota mkubwa kama yeye.

“Nina uhakika asilimia mia moja Diamond hadi leo hajaanza hata kufanya process (taratibu) za kuchukua silaha (bastola).

“Mimi naijua vizuri Madale ni sehemu ambayo watu huwa wanavamiwa mara kwa mara na wanaishi kwa hofu kama Diamond anavyoishi.

HIKI NDICHO KINACHOMPONZA

“Kitu kingine kinachomponza Diamond ni ishu ya kuweka kila kitu kilichopo ndani kwake mitandaoni. Usione kila mtu anasifia lakini kuna wengine wanavitolea macho.

“Kwa mfano katupia picha za toilet (choo) ambacho kimepakwa dhahabu na kusema kimegharimu shilingi milioni 70.

“Hajakaa sawa akatupia picha za jikoni kwake kuna vitu vingi vya thamani kubwa kila mahali mpaka kwenye korido kuna flat screen (runinga). Huko si ni kuwakejeli watoto wa mbwa? Ni vizuri akaacha kufanya hivyo kwa sababu anawapa watu tamaa,” kilitiririka chanzo hicho.

ANA ULINZI GANI?

Juu ya ulinzi wa nyumbani kwa Diamond, chanzo hicho kilidai kwamba, mbali na baunsa anayewalinda aitwaye Mwarabu hakuna askari wa silaha anayelinda nyumbani hapo hivyo jamaa anatakiwa kufanya haraka kuajiri walinzi wenye silaha.


Baada ya habari hizo na uchunguzi wa kutosha, Ijumaa Wikienda lilimsaka Diamond a.k.a Dangote au Chibu ili kujua namna anavyoishi na jinsi anavyoimarisha ulinzi wake na familia kwa jumla.

Diamond, mbali na kukiri kuwa na hofu, alikuwa na haya ya kusema: “Suala la ulinzi wangu nalijua mwenyewe lakini zaidi watu wanatakiwa kujua mimi nipo na mlinzi na ninaendelea kuimarisha ulinzi wa nyumbani kwangu.

“Sidhani pia kama ni suala zuri sana kwa watu kujua siri za ulinzi wangu ila mambo mengi ya kujilinda niko kwenye michakato ya mwisho kukamilisha na soon (haraka) mambo yote yatakaa levo maana huwezi ukafanya kila jambo kwa wakati mmoja,” alisema Diamond huku akikubaliana na ushauri wa gazeti hili juu ya kuongeza ulinzi alionao wa baunsa.

ILIWAHI KUMTOKEA SUGU

Huko nyuma iliwahi kumtokea Mwanamuziki Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema) ambapo alikuwa amerejea kutoka nchini Uingereza.

Akiwa amepanga nyumba nzima maeneo ya Tegeta, Dar, Sugu alifanyiwa makala ya runingani na kuonesha vitu vya thamani vya nyumbani kwake.

Siku chache baada ya kipindi hicho kuruka runingani, jamaa huyo alivamiwa na kuporwa kila kitu lakini yeye hakudhurika.

Dark side of Fastjet: Why it’s Not Cheaper Anymore, is Fastjet is a Low-cost Airline or Not?

0
0

Is Fastjet really a low-cost airline? This question has been asked several times by passengers flying Tanzania’s budget airline, but the answers have been confusing, sometimes misleading.

 Think about these facts. If you booked your flight to Mwanza from Dar es Salaam seven days before travelling, the return ticket will cost you a whopping Sh696,000 if you don’t have any luggage weighing 20kg or more, which costs an extra Sh20,000. This means that a return ticket for a traveller with at least 20kg of luggage costs Sh716,000.

That is what happened last week, when Asha, a 34-year-old businesswoman, booked a Fastjet flight to Mwanza, hoping to travel next Sunday, on Easter, and return to Dar es Salaam on April 14, this year.

“I was shocked to hear that it would cost me that much money (Sh716,000) for a return ticket to Mwanza…is Fastjet still a low-cost airline?” she asked in a text message to The Citizen.

On the same day, Asha tried to book a flight on Precision Air (PW), which flies to Mwanza once daily, and was told to pay Sh720,000 for a return ticket. It is not clear what has pushed PW to charge Sh720,000 for a return ticket at a time when competition is stiff and fuel prices have gone down sharply.

The story is the same if you want to fly to Kilimanjaro, Mbeya or elsewhere where Fastjet, which markets itself as a low-cost airline, flies.

From Mbeya to Mwanza, Kilimanjaro to Dar es Salaam, Fastjet has been making its name as a low-cost airline, but in reality, it is not, according to various customers who have aired their complaints.

Asha is not alone. There are thousands of passengers who have not understood clearly whether Fastjet is a low-cost airline or not—thanks to the exorbitant fares charged by the airline, which currently controls the domestic market.

Mr Sadock Magai, a prominent lawyer based in Dar es Salaam, last December complained bitterly about what Fastjet was charging passengers. He described what Fastjet was charging passengers as “daylight robbery”, adding that it was a tragedy that nobody, least of all the regulator, was willing to stop what was going on.

Since then, there have been hundreds of people complaining about what Fastjet is charging, especially on the Dar-Mwanza and Dar-Mbeya routes.

Although Fastjet officials have spoken to The Citizen reporters about the matter on several occasions and defended the carrier, the reality on the ground raises one simple question – is Fastjet is a low-cost airline or not?

Nguvu na Ushawishi wa Lowassa Waongezeka Maradufu

0
0
*Tafiti Mpya Za Kitaalamu Zadhihirisha Uhalali wake Kisiasa

*Kauli ya Jk yaongezewa nguvu na Tafiti Mpya za PTT

*Kauli ya mjumbe kamati kuu Jerry Slaa Yampa majibu nape na January "Chama chetu lazima kipeleke bidhaa inayohitajika sokoni, inayouzika na inayokidhi haja ya mnunuaji"

*Tafiti zabainisha nguvu ya Wapinzani Wa Lowassa Pinda na Membe, washindwa kutumia System kumzima Lowassa Zaweka wazi ushawishi wa Lowassa Kwa Umma.

Taasisi isiyo ya kiserikali ya Positive Thinkers Tanzania imetoa ripoti yake ya utafiti kuhusu mwanasiasa anayekubalika zaidi na wananchi katika nafasi ya Rais ajaye, Lowassa aongoza na nafasi ya 2 imeenda kwa Dr. Wilbroad Slaa huku Mwigulu Nchemba aking'ara kama kijana aliyeongoza kwa kukubalika kwa kukamata namba 3.

Ifuatayo ni orodha ya wanasiasa waliongia 10 bora na asilimia ya kura walizopata.

1. Edward Lowassa 22.8%
2. Wilbroad Slaa 19.5%
3. Mwigulu Nchemba 10.6%
4. Ibrahim Lipumba 8.9%
5. John Magufuli 6.8
6. Zitto Kabwe 6.7 %
7. Bernard Membe 5.9%
8. Mizengo Pinda 3.2%
9. January Makamba 1.6%
10. Mark Mwandosya 1.2%

Tafiti hizi zimedhirisha nguvu na ushawishi aliyonayo Edward Ngoyayi Lowassa Kama Kiongozi Kwa Jamii na Umma Wa Tanzania kwa Kiwango Cha Asilimia Alichopata Lowassa Ni dhahiri Shahiri Uchaguzi Ukifanyika leo basi ana nafasi kubwa ya kushinda uchaguzi huo.

Hii ni Tofauti na Wagombea wengine ndani ya CCM ambao kama watapitishwa na chama, chama kitalazimika kutumia nguvu kubwa mno ili kupata ushindi na ushindi ambao unaweza ukawa wa asilimia moja tena baada ya uchaguzi kurudiwa ikiwa ni sehemu ya marudio baada ya round ya kwanza kuonekana kutofikia asilimia.

Tafiti hizi zinaipa kauli ya Mh mwenyekiti na Rais wa tanzania Amiri jeshi mkuu nguvu kwani alisema " ikitokea kuna mtu ananguvu ya kutosha na mnamuona anafaa kuwa Rais basi msisite kumshauri agombee, eeh mshawishini tuuh" kwa muda wa week sasa makundi mbali mbali kada na rika mbali mbali kutoka katika kila kona ya tanzania yamekuwa yakijitokeza kwenda kumuomba Lowassa agombee urais.

Kwa Tafiti hizi watu watapata majibu ni nani anafaa na kwa nini mamia ya watanzania wanajitokeza kumshawishi Edward Lowassa Agombee,Alisema hivi karibuni mjumbe wa kamati kuu ndugu jerry silaaa Yakwamba " chama lazima kipeleke mgombea anayekubalika anayeuzika na anayeweza kukipa chama ushindi" kauli hii ilikuwa mwiba na jibu kwa nape aliyewahi kutoa kauli isiyo ya kiungwana kwa kusema chama hakiwezi kumpitisha mgombea asiyesafishika hata kwa dodoki.

Kauli hii inapingwa na takwimu za tafiti za kitaalamu kwamba Lowassa Ni sawa na kiatu kilichokwisha pakwa kiwi ni kazi ya chama kukibrush tuu" pia kauli hii ni jibu linalomjibu January makamba yakwamba Lowassa Alishapita umri wa kufanya siasa ya maigizo tafiti hizi zinaonyesha namna january anatakiwa kukuza siasa yake watanzania Wamfahamu zaidi na apate uhalali wa kisiasa.

Alisema mama Sophia simba mjumbe wa kamati kuu Kumjibu januaru " kama unaona wenzio wanaigiza kwa kutoa pesa ili watu wawashawishi nawe toa pesa tuone kama kuna mtu atakuja kukushawishi"Pamoja na nguvu kubwa ya kibobezi inayotumiwa na wabobezi hawa wawili pinada na membe bado siasa yao imeonekana kukosa uhalali kwa watanzania tafiti za za kitaalamu mara kwa mara zimekuwa sio rafiki kwa pinda na membe kwa takwimu za tafiti kwa chama cha ccm kumpitisha membe au pinda ni sawa na kupeleka KOFIA YA POLICE DUKANI UKAIUZE Nguvu ya Mwigulu Lamerck Nchemba Imeonekana kuwa Kubwa Kuliko Hata Wabobezi hawa wawili wanaotumia ubobezi wao kupitia system ya serekali na dola kushinikiza makundi mbali mbali kuwaunga mkono.

Hivi karibuni kumekuwa na tabiya ya makundi mbali mbali yanayopewa na kupokea vitisho kutoka kwa wabobezi hawa wawili kwa kosa la kutumia uhuru wao na Dhamira yao njema ya kumshawishi edward atangaze nia na agombee urais.

UKIUWA KWA UPANGA NAWE UTAULIEA KWA UPANGA, TAFITI HIZI ZINAONYESHA SI RAHISI KUZUIYA MKUKI KWA SHUKA

Msichana Mtanzania Akamatwa kwa Ugaidi Kenya, Alikuwa Anaenda Kwenye Mafunzo ya Kujitoa Mhanga Somalia

0
0
Vyombo vya usalama nchini Kenya, vinawashikilia wasichana watatu akiwamo Mtanzania, kwa kile kunachodaiwa kutaka kujiunga na kundi la kigaidi la al-Shabaab huko Somalia.
Taarifa kutoka kwa Kamishna wa Polisi Jimbo la El -Wak, mpakani mwa Kenya na Somalia, Nelson Marwa amesema Mtanzania aliyekamatwa, alijieleza kuwa ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Afrika, Sudan.

Mtanzania huyo, Ummul-Khayr Sadir Abdul (19), mwenyeji wa Zanzibar, anatajwa kuwa kiongozi wa kundi hilo lililopanga kujiunga na al-Shabaab.
Wasichana wengine waliokamatwa pamoja na Ummul-Khayr, ni Maryam Said Aboud na Khadija Abubakar Abdulkadir wote raia wa Kenya.

“Hawa wasichana watatu, inaaminika kuwa walikuwa wanakwenda Somalia kupata mafunzo ya kigaidi na baadaye kufanya mashambulizi ya kujitoa mhanga,” alisema Kamishna Marwa.
Akizungumzia suala hilo, Kaimu Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai, DCI Diwani Athumani alisema: “Tunafuatilia hatujapokea taarifa zaidi ya hizo.”
Kamishna Marwa alisema raia hao wawili wa Kenya, mmoja ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mount Kenya kilichopo Thika, Jimbo Kiambu na mwingine ni mwanafunzi wa Sekondari ya Burhania, iliyopo Malindi, Kilifi.

“Serikali imepata taarifa kuhusu watu wanaokusanya watu kutoka Afrika Mashariki ili wakajiunge na makundi ya ugaidi nchini Somalia, wakala wetu wa usalama wamepata taarifa hizo na kufanikisha kukamatwa kwa wasichana hao,” alisema Kamishana Marwa.
Hivi karibuni, tovuti ya al-Jazeera ilitoa taarifa za kukamatwa kwa mkanda wa video ulioonyesha mwakilishi wa kundi la kigaidi la Dola ya Kiislamu ya Iraq na Levant (ISIL) akimtaka kiongozi wa kundi la al-Shabaab kuliimarisha kwa kufanya mashambulizi ya kigaidi katika miji ya Mwanza na Dar es Salaam.

Kamishna Marwa alisema ingawa nyaraka za wasichana hao zote zinaonyesha kuwa ni wanafunzi, lakini bado walibanwa kwa maswali kuhusu sababu inayowapeleka nchini Somalia.
Aliongeza zaidi kuwa chanzo cha habari cha kiusalama kilieleza kuwa nyaraka za wasichana hao zilionyesha kuwa walikuwa wakienda kuolewa na wanajeshi wa kundi la al-Shabaab.
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live




Latest Images