Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

MAUMIVU "NILIYE MFUMANIA NA MPENZI WANGU KANIANGUSHIA KIPIGO CHA MBWA"

$
0
0
Nina mpenzi wangu ambaye yuko chuo fulani hapa Dar lakini kutokana na maamuzi yetu tuliamua aishi mtaani badala ya Hostel. Huyu msichana nilianza nae mahusiano kwa kipindi kirefu sana na hata tumefikia kuvalishana pete na nyumbani kwao nafahamika pia.

Kutokana na shughuli zangu nyingi kua mikoani hua tunakutana kwa baadhi ya wikiendi tu ninapokuja hapa Dar.

Basi Ijumaa hii nikaona sio vibaya kum-surprise my wife to be. Nikatoka zangu mkoani na shauku ya kujiandaa kwenda kwa P-square na mamaa.

Nilipofika pale Geto kwake hali sikuielewa. Nikaona sio mbaya kubisha hodi. Niligonga kidogo tu sauti yenye hasira na mikwaruzo ikatoka ndani. "Wewe Nani"???

Nikajibu kwa kujiamini nikijua wako discussion na wenzake.. "Mimi ni Edwin"

Ndani nikasikia kama wanabishana kidogo.

Ghafla jamaa akafungua mlango na kuniuliza huku amekasirika wewe nani? Nikajibu kwa kujiamini. "Kama Grace yupo ndani muulize Edwin ni nani?"

Basi Grace alipoulizwa akakana kunifahamu. Hapo jamaa akaanza kunishushia kipigo. Kutokana na mwili mdogo nilionao jamaa alinipga kwa kweli huku akitishia kunipigia kelele za mwizi.

Basi baada ya pale nikaenda hospital kupata matibabu. Nikaamua kumtaarifu mama yake Grace. Mama Grace alishangaa sana na kudai mbona Grace alimtaarifu tumeachana kwa Mwezi sasa?

Nikachanganyikiwa zaidi. Nilipopeleleza zaidi kwa rafiki yake mmoja, nikagundua jamaa ndio anamgharamia Grace kila kitu na kias nilichotoa kwa Grace ilikua hela ya chumvi tu..

Hapa nilipo nina maplasta usoni na sehemu nyingine.

Nisaidieni nichukue hatua Gani kisheria juu ya huyu jamaa? Je akisema nilitaka kuiba nitajitetea vipi? Ushauri wenu ni muhimu sana

Note
Nimetumia majina ya kweli ili kama Grace yupo humu ndani ujumbe umfikie na ajue ameniumiza sana moyoni kwa usaliti aliouonyesha mchana kweupe.

Asanteni

MALAWI KUNA KITU INAKITAKA TOKA TANZANIA, RAIS WAKE ATANGAZA MKOA WA RUVUMA NA WANANCHI WAKE NI MALI YAKE

$
0
0
RAIS wa Malawi, Joyce Banda ametajwa kuendeleza chokochoko baina ya nchi yake na Tanzania, huku sasa akidaiwa kutumia redio na runinga za nchini mwake kutangaza kuwa mkoa wa Ruvuma, viongozi na wananchi wa ukanda wa Ziwa Nyasa ni mali yake.
Aidha, amesitisha safari za meli ya mv Ilala iliyokuwa ikifanya safari kwenye Ziwa Nyasa kusafirisha mazao na wananchi wa ukanda huo upande wa Tanzania.
Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa soka wa Mbambabay jana, Mbunge wa Mbinga Magharibi, John Komba, alisema Rais Banda ambaye aliibua upya mzozo wa mpaka baina ya nchi hizi mbili, kuwa ni mkorofi kutokana na kufanya vitendo vinavyoonesha uhusiano baina ya nchi hizi mbili kuzorota.
Komba alibainisha vitendo hivyo mbele ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, akisema imefika mahali Rais Banda anapotosha ukweli kuhusu mpaka kati ya nchi hizo mbili na kudai sehemu ya mwambao wa Ziwa upande wa Tanzania ni yake.
Mbunge huyo alisema jimbo la Mbinga Magharibi ambalo ni Wilaya ya Nyasa, wanasikiliza matangazo ya redio za Malawi, na anazitumia kupotosha umma kuwa ukanda wa Ziwa Nyasa ni mali yake na wananchi wanaamini hivyo.
Rais Banda anatangaza kupitia vyombo vya habari vya nchi yake ambavyo vinasikika vizuri katika wilaya hiyo kutokana na wilaya ya Nyasa kutopata mawasiliano ya redio na runinga za nchini. Komba alisema kutokana na wilaya hiyo kukosa mawasiliano ya vyombo vya habari, wananchi wake wanakosa kusikiliza matangazo zikiwamo hotuba za viongozi wa Taifa.
Wananchi wanakosa kusikiliza matangazo zikiwamo hotuba ya Rais Kikwete ya kila mwezi na hotuba za viongozi wengine wa kitaifa wakiwamo Makamu wa Rais na Waziri Mkuu.
“Kutokana na kukosekana usikivu huo, Rais Banda anatumia nafasi hiyo kutangaza kuwa viongozi wote wa wilaya na mkoa na eneo lote ni mali yake,” alisisitiza Komba. Aliongeza kwamba watu wote walioko kwenye mkutano huo isipokuwa Katibu Mkuu Kinana, akiwamo Dk Asha-Rose Migiro ambaye alizaliwa Mbambabay wote ni mali ya Rais Banda.
Mbunge huyo alisema wananchi wa eneo hili nao ni Watanzania wanaostahili kusikia na kupata habari za nchi yao, badala ya kusikiliza nyimbo na matangazo ya Malawi ambayo yanakuwa na ajenda zake.
Mbunge Komba alimwomba Katibu Mkuu Kinana kwenda kuhimiza kutekelezwa haraka kwa ahadi ya Rais Jakaya Kikwete ya kuleta meli ili kuwa na usafiri wa uhakika wa mali na wananchi katika eneo hilo.
Kinana alisema ahadi ya meli ya Rais, hiyo ana uhakika itatekelezwa na kufafanua kuwa meli tatu zinatengenezwa Korea Kusini na zitakapokamilika ya Ziwa Nyasa itapelekwa kutoa huduma.
Alisema baada ya Banda kuondoa meli hiyo wananchi wa Mbambabay wanatumia boti dogo kusafirisha abiria na mizigo, hali ambayo inatia shaka.
Kinana alisema amesikia kilio cha Mbunge Komba, kwamba ahadi ya Kikwete itatekelezwa ili kuwapa wananchi usafiri wa meli, ingawa itatumia muda kutokana na kuhitaji muda mwingi kubuni na kutengeneza

PICHA ZA KIMAHABA ZA WASTARA ZAZUA UTATA

$
0
0
Na Shakoor Jongo
PICHA za aliyekuwa mke wa marehemu Juma Kilowoko ‘Sajuki’ Wastara Juma akiwa na mwigizaji Bondi bin Salim ‘Bond’ zimezua utata ambao unakazia ukweli wa taarifa ya kuwa wawili hao ni wapenzi.
Kikizungumza na Ijumaa Wikienda chanzo chetu kilicho makini, kilisema kinawashangaa sana Wastara na mwenzi wake huyo kuukana upenzi wao kila kukicha wakati picha zinajieleza.
“Wastara amekuwa akimkana Bond kuwa si mpenzi wake ila ni kaka yake sasa hebu tazama picha zao mpya, hata mtoto mdogo humdanganyi kitu,” kilisema chanzo hicho huku wawili hao wakiendelea kukanusha kuwa na uhusiano wa kimapenzi.

MAKALA:P-SQUARE WAMETUBURUDISHA NA KUTUACHIA FUNZO MUHIMU

$
0
0
Imeandikwa na Bongo5,com
Nikiwa na begi langu lenye camera ya kazi, niliwasili Leaders Club mapema mida ya saa 2 kasoro hivi usiku. Nakubali, ndio nilienda mapema mno. Si kwasababu nilikuwa nimeipania show ya P-Square, lahashaa. Nilihitaji tu kuwasili mapema ilimradi nisipitwe na kila jambo muhimu litakalotokea.
Peter akiimba wimbo kwa hisia kali

Nje ya Leaders, ulinzi ulikuwa mkali mno. Walionekana askari wengi kuanzia kwenye kona ya kwanza ya kuingia Leaders baada ya kuiacha barabara ya lami. Muonekano huo tu, ukanipa faraja kubwa kuwa mali na watu muda wote wa show watakuwa salama.
Kulikuwa na njia moja tu ya kuingilia iliyogawanishwa katika vimilango vingine zaidi ya sita vilivyosimamiwa na askari wa ulinzi waliokuwa na sare zao. Hapo nikakaguliwa kwa vifaa maalum kuanzia chini na ndani ya begi langu ili kuangalia kama nilikuwa na bomu ndani… Lol… usishtuke, nilikuwa nimebeba camera yangu tu, hakuna kingine. Itifaki ilizingatiwa.
Ndani palikuwa pameshaanza kuchangamka. Kwa mbali nilimuona DJ Sama kwenye 1 na 2 akifanya yake kama wasemavyo wenyewe wazee wa East Africa Radio. Eneo la mbele jirani na jukwaa tayari palikuwa pamejaa. Watu wengi hasa wazungu waliokuwa wamechangamka kiaina, walionekana kukunwa na burudani hiyo na kucheza kwa raha zao.
Kwa pembeni kidogo kulikuwa na sehemu ya VIP iliyokuwa imetengwa na Hennesy. Palikuwa pametengenezwa vizuri na wale walioweza kumudu walijimwaya kule.
Mwanzoni palianza kama kuboa kiaina, hivyo nikaenda pembeni kidogo kutafuta kinywaji changu kupoza koo. Kama kawaida pembezoni mwa uwanja kulikuwa na vibanda kadhaa vilivyokuwa vikitoa huduma ya bites na misosi mbalimbali.
Haukupita muda mrefu, washereheshaji wa siku hiyo, Dulla Mjukuu wa Ambua na T-Bway walivamia stage kutokea chini kwa ngazi maalumu zilizotengenezwa kupanda zenyewe kutoka chini hadi juu huku wao wakiwa wameinama kama kiumbe cha ajabu kilichoanguka kutoka mawinguni.
Shangwe zilitawala baada ya wawili hao kuanza kutangaza na kuwapandisha watumbuizaji wa kwanza, dancers walioshinda shindano la Dance 100. Sikupenda performance yao japo walipata shangwe za hapa na pale. Sababu kubwa ya kutopenda kile walichokifanya ni aina yao ya uchezaji kwa kutumia zaidi sauti za effects na si kwa kucheza kwenye wimbo unaoeleweka. Kingine ni utengezaji wao mbovu wa megamix yao iliyokuwa na nyimbo fupi na ambazo hazishiki.
Performance ya kwanza ya kueleweka ilianza baada ya Ben Pol aliyesindikizwa na msanii wake Alice kupanda. Akiwa amevaa koti la rangi ya blue bahari lilitengenezwa na mbunifu wa mavazi, Pedaih wa PSJ Couture, Ben Pol alionesha ukomavu katika uimbaji wake kwa kutumbuiza hits zake zote kwa ustadi mkubwa.
IMG_7915
Ben Pol
Alifuatia Lady Jaydee na dancers wake. Mkongwe huyo alikuwa amevalia mavazi kama askari jeshi wa kike anayeshiriki kwenye gwaride na kupendeza sana. kama kawaida yake, Lady Jaydee alizikonga vyema nyoyo za waliohudhuria kwa kutumbuiza nyimbo zake za zamani na za sasa zikiwemo Yahaya na Joto Hasira.
Lady akiwa ndani ya mavazi kama ya askari wa kike
Lady Jaydee
Wakati akiimba Joto Hasira ndipo alipomkaribisha rasmi Profesa J kuchukua usukani wa show. Profesa alikuwa amesindikizwa na rapper ambaye sijawahi kumuona lakini aliyemudu vyema kumpa tafu Mchawi huyo wa rhymes kufanya show nzuri pia.
IMG_2902 - Copy
Profesa Jay
Niseme wazi, Joh Makini ndiye aliyekuja kuipa uhai hip hop. Japokuwa yeye hakuwa akipigiwa vyombo na bendi, show yake iliwasha moto Leaders Club. Mwamba huyo wa Kaskazini alitumbuiza nyimbo zake zote zilizohit na nusu ya uwanja ulisikika ukimalizia mashairi yake. Kuanzia Higher, Stimu Zimelipiwa, Hao, Niaje ni Vipi, Manuva na zingine.
IMG_2951
Joh Makini
Baadaye, Joh alikuja kupewa kampani na Weusi, Nikki wa Pili na G-Nako na kuongezea nyimbo zingine, Nje ya Box na Bei ya Mkaa.
Nikki wa Pili baada ya kupanda kumpa shavu kaka yake Joh Makini
Nikki wa Pili
Mpaka Weusi wanaondoka kwenye stage, wapenzi wa burudani walikuwa tayari kuumudu moto uliokuwa unakuja wa P-Square.
Alikaribishwa DJ Mafuvu kuwaweka sawa kwanza na ndipo bendi yenye watu wanne tu ilipanda kuweka sawa vifaa vyao.
P-Square walipopanda, uwanja mzima wa Leaders Club ulizalisha shangwe nene kuwakaribisha. Peter na Paul wakaanza kuangusha fire. Kitu kimoja ambacho mimi kiliniacha mdomo wazi, ni muziki mzito uliokuwa ukipigwa na watu wanne tu, na kufanya uonekane kama unachezwa na watu zaidi ya 10.
Bendi ya P-Square inajua haswaaa. Ilikuwa ikipiga nyimbo zao kwa ustadi kiasi ambacho ilikuwa rahisi mno kuyadanganya masikio yako kuwa unachokisia pale huenda sio live bali ni CD. Tofauti yake ni kuwa, P-Square wanajua mno kutengeneza ladha tofauti ya nyimbo zao na kuzifanya ziwe tamu zaidi zinapoimbwa live. Kwa mfano, walikuwa wakianza kwa kuimba kama slow na baadaye kuja kuuimba wimbo kwa namna ulivyozoeleka.
Paul akivuta hisia
Paul Okoye
Kwa namna ambavyo walikuwa wakilitawala jukwaa, ni halali P-Square wawe wasanii wanaolipwa zaidi barani Afrika. Si kwa maneno tu, nimeamini kuwa, ni wasanii wachache sana wa Afrika (ukiwatoa DRC) wenye uwezo wa kutumbuiza vizuri zaidi live. Nadiriki kusema kuwa, unaweza kuwaweka Davido, Iyanya na Wizkid pamoja lakini hawawezi kufikia uwezo wa mapacha hawa.
Kuna mambo kadhaa niliyojifunza kwenye show hiyo ambayo ni pamoja na:
Kutengeneza versions tofauti za nyimbo
Hiki si kitu kipya sana, na wasanii wengi hufanya hivi pale wanapokuwa wakiimba live. Lakini P-Square walinigusa zaidi kwa jinsi wanavyofanya wao. Baadhi ya nyimbo zao za kuchangamka ambazo nilitegemea wangezikimbiza kama kawaida, walizitengenezea ladha nyingi tamu ya kusikilizika zaidi. Hakuna wasiwasi kuwa, jamaa hawa hufanya mazoezi makali na bendi hiyo na kila wimbo ulibadilishwa na kupigwa katika aina ambayo usingeweza kuona hata chembe ya kosa.
Nyimbo zilizokuwa zinagusa mapenzi na uhusiano waliziimba kwa hisia kali na kwa uwezo wao wote. Huu ulikuwa ni uimbaji kama wa msanii mchanga aliyependa kwenye stage kubwa kama ile kwa mara ya kwanza na anayetaka kuwadhihirishia watu kuwa ana uwezo mkubwa.
Paul akiimba kwa hisia
Paul akiimba kwa hisia
P-Square walitumbuiza kama si wasanii wale matajiri tunaowafahamu. Kwao kila show ni muhimu na ni lazima wazikonge nyoyo za mashabiki.
Peter akiimba kwa hisia
Peter
Bendi ni zaidi ya wafanyakazi, ni familia..
Peter alisema wapigaji wa vyombo wa bendi yao ni watu waliokuwa nao tangu enzi za utoto miaka iliyopota. Ni washkaji zao wanaotembea nao kila mahali. Uhusiano uliopo kati ya P-Square na bendi hiyo ni mkubwa kiasi cha kuchukuliana kama familia. Uhusiano huo ndio unaoleta kile nilichokishuhudia siku ile.
Kuengage na mashabiki
P-Square si wasanii tu, ni entertainers. Nilifurahishwa na uwezo wao mzuri wa kuwashirikisha watazamaji kwenye show yao. Kwa mfano walianzisha mashindano ya kizushi pale pale jukwaani ili kuonesha nani kati yao ndiye mwenye kipaji zaidi. Mwanzoni Peter alivuta juu shati lake na kuonesha six pack yake kifuani, huku Paul akidai kuwa yeye hana six pack bali anayo one pack kubwa zaidi na kutoa suruali yake kubaki na boxer, hali iliyoamsha shangwe za hatari.
Baaadaye Paul alikamata gitaa la besi akitaka aoneshe uwezo wake. Peter akasikika akisema, amekua pamoja kwenye nyumba moja na hajawahi kumuona kaka yake akipiga gitaa. ‘His name is Paul Okoye, Paul Okoye disgrace yourself,’ alisema Peter. You got one pack, show them one pack or 2 pack, go go let me see,’ aliongeza. Akiwa ameshika gitaa lake, Paul alisema ‘I am about to do 2 Pac, let’s go’ na ndipo alipoanza kupiga bass ya wimbo wa 2 Pac ‘Do For Love’, bendi ikampokea na Peter kuanza kuimba chorus ya wimbo huo.
Baada ya hapo Peter alishikaa gitaa la solo na kucharaza wimbo wa Ja Rule aliomshirikisha Ashanti, Always on Time kabla ya kupiga wimbo wa The Product G&B na Wyclef – Cluck Cluck.
Surprises
Peter Okoye ametoka kufunga ndoa hivi karibuni lakini ili kuwafurahisha zaidi watu aliamua kumkosea kidogo mkewe Lola Omotayo kwa kumfanyia surprise msichana mrembo aliyekuwa pale. Alimpandisha juu mrembo huyo na kumvalisha saa yake kabla ya kumbusu na kuibua shangwe zito Leaders Club.
Onyinye akivishwa saa na Peter
Mrembo akivishwa saa na Peter
Onyinye - Peter amkibusu
Onyinye - mrembo akifurahia
Hakuna anayeweza kuiongelea vibaya show hiyo iliyohudhuriwa na watu wa kila aina wakiwemo wazungu kibao wa mataifa mbalimbali.
Show ilihudhuriwa na watu wa mataifa mbalimbali
Ilikuwa ni show ya watu wengi lakini iliyokuwa na heshima kubwa. Kwa aina ya watu wale waliohudhuria siku hiyo, nilipata picha kuwa burudani ni kiwanda kikubwa kinachoweza kuwapa kipato kikubwa si tu wanamuziki wanaotumbuiza, bali waandaji wenyewe pia kama tu kila kitu kikifanywa vizuri.
Hakikuwa kitu cha kawaida Leaders kujaa vile ilhali kiingilio kilikuwa ni shilingi 35,000 hadi 50,000 uwanjani. Inawezekana kabisa kufanya maandalizi kama hayo kwa kutumia wasanii wa hapa hapa nyumbani na kwa kiingilio kama hicho, kwa kuweka bendi ya uhakika na wasanii wakalipwa mathalan shilingi milioni 50 kila moja.
Kwa mfano huo, waandaaji wa matamasha wanaweza kutengeneza tamasha la muziki (music festival) la hata siku tatu mfululizo na kama line up ya wasanii ikiwa ya kueleweka na muziki upigwe live, Dar inaweza kuwa na tamasha lake sawa na Sauti za Busara lilivyo.
Niwapongeze sana East Africa Radio kwa maandalizi mazuri ya show hiyo. Watu wengine wanaoandaa matamasha kama hayo, wajifunze kitu kutoka kwenye show hiyo ili tukuze zaidi kiwanda cha burudani nchini.
Bongo5,com

BARACK OBAMA AMEMFOLLOW VENESSA MDEE KWENYE TWITTER

$
0
0
Hii itakuwa ni kwa mara kwanza kwa mwimbaji wa Tanzania na pengine Afrika kuwa followed na Rais Barack Obama wa Marekani kwenye twitter ambae ana zaidi ya followers milioni 40 lakini yeye anafollow watu laki sita.
Vanessa Mdee ameingia kwenye list ya watu laki sita ambao Rais Barrack Obama ana wa-follow sasa hivi ambapo baada ya Rais huyu kufollow, kwa furaha Vanessa alishare kwenye instagram screenshot ya ukurasa wake wa twitter ukionyesha Barack Obama ameanza kum-follow.
Kama ilivyo twitter, hii inamaanisha ana Vanessa ana uwezo wa kumuandikia msg binafsi kwenye inbox Rais Obama.

HATIMAYE BAADA YA KUFUKUZWA SIMBA ADEN RAGE AONGEA NA WAANDISHI WA HABARI

$
0
0
Zifuatazo ni kauli za Ismail Aden Rage ambazo nimemnukuu akiongea na Waandishi kutokana na stori zilizochukua headlines kwa siku kadhaa kuhusu Kamati kumsimamisha kama Mwenyekiti wa Simba.
1. ‘Kwanza napenda kuipongeza kamati ya utendaji ya TFF kwa kuafiki mimi Ismail Aden Rage ndio Mwenyekiti halali wa Club hii ya Simba na nimepata barua yao jana ileile, katika katiba ya Simba kuna kitu wengi hawajui maana ya Kamati ya utendaji wanadhani ni wale watu saba… hapana!!! kamati ya Utendaji ni Mwenyekiti, Makamu wa Mwenyekiti… hamna kaimu hapo, kuna Wajumbe 7 waliochaguliwa katika mkutano halali… , Wajumbe saba wa kuchaguliwa mmoja wapo akiwa ni Mwanamke na wengine wawili wa kuteuliwa na Mwenyekiti, leo nitateua mwingine mmoja.. nimetoa mmoja’
2. ‘Kwa bahati mbaya Club ya Simba haina Makamu Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti alishajiuzulu ila ina Kaimu Mwenyekiti tu ila huku kwenye katiba hatajwi, kwenye katiba ya Simba Makamu Mwenyekiti ana kazi mbili, moja kwa kuelekezwa na Mwenyekiti na pili Makamu Mwenyekiti anafanya kazi wakati Mwenyekiti hayupo’ – Aden Rage
3. ‘Joseph Itangire ni Kaimu Mwenyekiti tu niliemteua lakini hajapata uhalali wa kikatiba kwa hiyo katiba hii inaendelea kusema, mwenye mamlaka ya kuitisha kamati ya Utendaji mara nne kwa mwaka ni Mwenyekiti, nimekua muungwana tumefanya mara 12 mwaka huu.. kama Mwenyekiti hayupo, katiba inasema anakaimu hana mamlaka ya kuitisha kikao chochote kwa mujibu wa katiba kwa hiyo kikao kile kilichofanyika hakina tofauti na kikao cha harusi’
4. ‘Maamuzi yangu kama Mwenyekiti wa Simba sasa, kwa kuwa mkutano ule ulikua ni batili… jana niliandika barua kwa TFF kwamba viongozi hawa wamevunja katiba za TFF, Simba, CAF na FIFA… ukitaka kulalamika ni lazima uwe na ushahidi wa aina mbili unaokubalika ambao ni document na video casette iliyo na sura za watu na maneno yao waliyosema, wana document ambayo kwenye barua ya Malinzi amekiri anayo na imesainiwa na Makamu Mwenyekiti wa Simba Joseph Itangire’
5. ‘Nimesikitika sana na maagizo ya TFF ya kunitaka niitishe mkutano na Wanachama wa Simba ndani ya siku 14, sijui wameitoa wapi kwenye katiba ya TFF na Simba, wamekwenda mbali na kuninyang’anya madaraka… wamenipa alafu wameninyang’anya alafu wamenipa na Ajenda ya mkutano, sasa wamenirudishia madaraka ya nini? mimi kama Mwenyekiti wa Simba… siitishi mkutano, nalindwa na katiba kwa hilo’
6. ‘Unaponipa amri unaninyang’anya madaraka yangu, katiba inasema kama naona itafaa nitaitisha… tuheshimu katiba, nilitegemea taarifa ya kwanza ya TFF mpya ingelaani mapinduzi ya kipuuzi yanayotokea’
7. Heshima yangu mimi ni Mbunge taifa linaelewa hivyo, nimekuta ofisi hii hakuna umeme miaka 18 pamoja na pazia za magunia, nimekuta uhuni mtupu.. wachezaji wameuzwa, Henry Joseph, Matole na wengine uliza wanachama wa Simba ilipata shilingi ngapi? leo imani inawatoka kusikia nimeuza Wachezaji wawili tu Congo DRC milioni 320 na nikaweka wazi hadharani sio kuwaambia Mke wangu na watoto wangu..
8. Leo nimetumiwa msg kutishia kuuwawa na tayari nimesharipoti Polisi, leo hii msg nimepata mtu kaniambia ‘Nisipotoka Simba ataniua’ alivyokua mpumbavu hajui hizi simu zinasajiliwa, nimecheki jina lake mpaka mtaa anaokaa pengine sasa yuko Lupango… why??? mpira ni burudani!! kuna mtu alikua Simba sasa yuko TFF anataka kuleta vurumai ndani ya TFF na Simba, kwa nini? kwa nini ununue watu? waandishi wa habari hebu tuache kuchochea, wewe Mwandishi ni nani ununuliwe? kuna Mwanamke Mwaandishi mmoja kalipwa milioni 2 ili anichafue, sijali.. ‘
9 Nimefanya Demokrasia sana na ndio inanitokea puani, nimeteua kamati… ziko kamati nyingi sana lakini sijaona Mwandishi hata mmoja anakwenda kuuliza kamati ya ufundi, Usajili ila kila mmoja ananishambulia mimi, leo sitaki maswali ya Waandishi wa habari, sasa mna hiari… kuandika au kuacha wala hamnipi tabu nyie, kuchafuliwa nimezoea’
10. Ukitaka kuwa kiongozi teka Ikulu kwanza, hapa ndio ikulu.

USHAURI KWA ZITTO: MAJUNGU UNAYOPIGWA YANATOKANA NA KUTOKUJENGA UHUSIANO BINAFSI NA WENZAKO

$
0
0
Tatizo la Zitto sio ukanda, udini, ukabila, usomi na siamini Waraka ambao wanasema Zitto anahusika kwasababu umeandikwa kitoto sana.

Tatizo kubwa la Zitto na Chadema ni uhusiano binafsi na watu anaofanya nao kazi. Ukweli ni kwamba kazi ni zaidi ya sera, sheria za kwenye vitabu.

Viongozi wengi ni watu wa kawaida na wana uhusiano wa karibu hata wa kifamilia tumeona Kikwete analala kwa magufuli kwasababu Magufuli amegundua uhusiano binafsi ni njia moja wapo ya kufanikiwa kwenye jambo lolote. Hivyo Zitto hayo majungu yanatokana na kutokuaminiana kwasababu hujachukua muda kuweka mahusiano ya karibu na watu unaofanya nao kazi na hili ni tatizo kila mahali hata kwenye biashara au kazi nyingine.

Je unajua familia za wenzako, unajua wameamkaje asubuhi, unajua matatizo waliyonayo kama wagonjwa nyumbani? haya yote ni muhimu kwa watu unaofanyakazi nao sehemu moja. Vitabu vipo, sera zipo na sheria zipo lakini kwenye Chama kama Chadema ambacho ndicho kinakuwa na viongozi wachache kutupiana maneno kwenye mtandao inaonyesha hakuna mahusiano binafsi ambayo mnaweza kuongea kwenye chai ya asubuhi na kumaliza.

Hakuna jambo duniani linalofanikiwa kwa sera pekee bali mahusiano ni muhimu sana. Vilevile ni lazima uelewe mahusiano ni kati ya mambo muhimu ambayo ni lazima ukubali kama ni upungufu wako na kulifanyia kazi kama alivyofanya magufuli.

Magufuli pia alikuwa anaogopwa na JK na wengine kwa misimamo lakini aligundua hilo na kujenga mahusiano.

Zitto unakipaji na huna sababu ya kuwaeleza watu hilo kwasabbau kipaji ni kutoka kwa mungu na hakuna anayeweza kukichukua hivyo focus on your weakness.

Huu ni ushauri wangu kujibizana nani yuko sawa na nani hayuko sawa haitakusaidia popote pale na kwenye chama chocote au biashara.
Kitakacho kusaidia ni mahusiano-relationship

LIL KIM APANDA JUKWAANI NA KIVAZI KILICHO MCHORA SEHEMU NYETI..WENGI WAMPONDA

$
0
0

 Kazi kweli kweli ..Mwanamuzi Lil Kim mwenye Miaka 39 akiwa anaimba Jukwanii akiwa amevaa kivazi kilichomchora ambacho kilileta sinto fahamu ikichukulia na umri wake wa sasa....hii ilikuwa ijumaa pale london kwenye Show ya 02 

Add caption



DR WA MAREHEMU MICHAEL JACKSON AELEZA SIRI NZITO KUHUSU MAREHEMU

$
0
0
Kwenye mahojiano yake ya kwanza mara baada ya kuachiwa toka gerezani kwa kuhusishwa na kifo cha nguli wa muziki wa pop duniani Michael Jackson, Dokta Conrad Murray alielezea kwenye mahojiano aliyofanya na The Mail kwamba, Michael hakuwa baba wa hata mtoto wake mmoja, aliathiriwa na madawa kiasi cha kufikia hatua ya kuhitajika kuwa anavaa condom sababu mkojo ulikuwa unatoka wenyewe kwenye uume wake.

“Unataka kufahamu ni kwa kiasi gani mimi na Michael kwa vile tulikuwa karibu? Nilikuwa nikishukilia uume wake kila usiku. Nilikuwa namvalisha condom sababu mkojo wake ulikuwa ukitoka wenyewe. Michael alikuwa hajua namna ya kuvaa condom, hivyo ilinibidi niwe namvallisha. Kilikuwa ni kitu cha kipekee sana ila aliniamini mimi. Sikumuuwa Michael Jackson, aliathiriwa na madawa, Michael Jackson kwa bahati mbaya alimuuwa Michael Jackson, naamini aliamka na kuamua kufanya aliyozoea kufanya, akajidunga sindano haraka ambayo ilisababisha kumpeleka kwenye hali iliyomfika.’’ 

Alikuwa kwenye majanga mwishoni mwa maisha yake, akiwa na msongo wa kimawazo na kupaniki … Mwishoni, Michael alikuwa mtu aliyekata tamaa. Nilijaribu kumlinda ila mwisho wa siku niliangushwa naye.

Jackson alikuwa ameingia kwenye matatizo ya kuathirika kiakili na kimwili kutokana na ziara yake ya London.’’ Alisema Dokta Conrad Murray.

DIAMOND ATANGAZA KAZI ....UWE TAYARI KUSAFIRI NAE KWENYE SHOW ZAKE

$
0
0
Je unaishi Dar-es-Salaam..? Unakipaji, Uwezo na Elimu ya kupiga picha, kushoot Video na kuedit...?
NOTE:-
1)Uwe na Uwezo wa kutumia Camera zote Old na za kisasa....
2)Uwe na sample za kazi kadhaa ulizowai fanya... (kushoot na 
Kuedit)
3)Quality ni kuanzia 1080 na kuendelea...
4)Age, kuanzia Miaka 20 hadi 35..
5)M'bunifu, Smart na uwe tayari kusafiri popote saa yoyote...

Kama unaamini unasifa hizo wasiliana nasi sasa kwa email hii diamondplatnumz@gmail.com ama kwa namba ya simu +255755700400

FLORA LYIMO HOW TO LOOK SEXY AT HOME WE ARE NOW ON WEEK NINE AND JEMBE NI LILE HOT THAN EVER

$
0
0
GO BACK TO BED ', "MONDAY IS CANCELLED''   Wakati Diamond akisema "WATUACHE TULALE" Flora yeye anasema "MBUTA NANGA"

Angalia Picha zake hizo hapo chini.
zaidi ingia hapa kwenye blog yake: Flora Lymo

 HABARI NDIYO HIYOO KWA PAMOJA'' CHUPI ZA KUSHINDIA HOME AU ZA KUVALIA KANGA MOJA NDIYO HIZO ''USIKAE BILA CHUPI JAMANI KWANI CHUPI ZINASAIDIA MAMBO MENGI SANA KATIKA MWILI WA BINADAM YOYOTE HASA KINA DADA WAKATI WAKUFIKIA UMMRI WAO WAKUTOKA UTOTONI NA KUINIA USICHANANI''MPO HAPO EEE'' YOU HAVE TO WEAR CHUPI AT ALL THE TIME MY DEARS'' 


ZITTO AJIWEKA NJIA PANDA

$
0
0
Aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe amejiweka katika mazingira magumu zaidi kisiasa ndani ya chama hicho, kutokana na shaka kubwa iliyougubika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika Dar es Salaam juzi.

Zitto pamoja na viongozi wengine wawili wa Chadema; Dk Kitila Mkumbo na Samson Mwigamba walivuliwa nyadhifa zao na Kamati Kuu ya Chadema baada ya kubainika kupanga mbinu za uasi, kupitia waraka ambao ulikuwa ukieleza mkakati wa kufanya mabadiliko makubwa ya kiuongozi wakati wa uchaguzi mkuu wa ndani.

Leo, uongozi wa Chadema umeitisha mkutano wa waandishi wa habari ambao pamoja na mambo mengine, utajibu baadhi ya hoja za utetezi ambazo zilitolewa na Zitto pamoja na Dk Kitila. Katika mkutano wa juzi, Zitto na Dk Kitila ambaye alikuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, walizungumzia kuvuliwa kwao madaraka, lakini maandalizi na uendeshaji wa mkutano huo yanazua shaka kutokana kuwahusisha watu wanaodaiwa kuwa ni wanachama wa Jumuiya ya Vijana ya Chama cha Mapinduzi (UVCCM).

Miongoni mwao, wamo waliowahi kuwa wanachama wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), Habib Mchange na Mtela Mwampamba ambao walitimuliwa kwa makosa yanayofanana na yale yalizosababisha Zitto na wenzake kuvuliwa nyadhifa zao.

Mchange na Mwampamba pamoja na aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Bavicha, Juliana Shonza, walivuliwa uanachama wa Baraza hilo Januari 5, mwaka huu baada ya kupatikana na hatia ya kutumia mitandao ya kijamii kukihujumu Chadema na kuwatukana viongozi wake wakuu. Baadaye walihamia CCM wanakoendeleza harakati zao za kisiasa.

Jana, Machange alipotafutwa, alisema: “Mimi sikuwahi kuondoka Chadema, nilifukuzwa kihuni kama walivyowafanyia Zitto na Kitila. Nimepeleka malalamiko yangu tangu Januari hadi leo sijajibiwa, hivyo siwezi kusema nimeondoka.

Nataka nimuunge mkono mwathirika mwenzangu kama ilivyokuwa mimi lakini nitabakia kuwa mwanachama mwaminifu.

“Mimi ni mwanaChadema na sikuwahi kujiunga na CCM au chama chochote, walioondoka ni Mwampamba na Shonza.” Mwampamba alisema: “Nilijitokeza pale kuonyesha mshikamano kwa sababu mimi pia ni mwathirika. Kwa hiyo nilitaka ulimwengu ufahamu kuwa mimi ni kati ya wanaopinga siasa za aina hii... Chadema ni chama kinachojiandaa kuchukua dola, sasa kama kila mwenye mawazo tofauti anaonekana mhaini itakuwaje siku wakichukua dola? Ubaguzi huu haujalishi uko chama gani, hata kama niko CCM, hilo halinizuii kuungana na mtu aliyepatwa na tatizo kama langu.”

Kuwepo kwao katika mkutano wa Zitto kunaweza kutumiwa na uongozi wa Chadema kuwa uthibitisho wa kiongozi huyo kushiriki katika uasi na kunaweza kupuunguzia nguvu utetezi unaotolewa na Dk Kitila kwamba hakuwa sehemu mpango wa kuuondoa uongozi wa sasa madarakani. Zitto, Dk Mkumbo na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba wanasubiri kukabidhiwa barua za kuvuliwa kwao madaraka na katika siku 14 wanapaswa wawe wamewasilisha utetezi wao wakieleza kwa nini wasifukuzwe uanachama kutokana na tuhuma zinazowakabili.

Dk Slaa

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbrod Slaa alisema jana kuwa ilikuwa lazima viongozi hao wavuliwe madaraka hasa baada ya Dk Kitila kukiri kuhusika na waraka ambao anasema ulilenga kushinda kupitia uchaguzi halali ndani ya chama hicho.

“Hata katika ya nchi ukihusika kutengeneza mbinu za siri lazima ushughulikiwe.Hakuna Katiba itakayokuruhusu kufanya mipango ya siri. Kwanza uchaguzi wa Chadema nani katangaza mpaka mipango ianzwe kutengenezwa sasa hivi?” alihoji Dk Slaa.
Alikiri kwamba watuhumiwa hao hawajapewa barua za uamuzi wa Kamati Kuu na alipoulizwa sababu, alisema Katiba ya chama hicho haitoi mwisho wa mtu kupewa barua, huku akihoji: “Wao nani kawaambia waende kwa waandishi wa habari?”

“Mimi ndiye Katibu Mkuu. Katiba inasema ni lini barua iandikwe? Utatokaje kwenye kikao alfajiri na wakati huohuo uandae barua za kuwapa?” alihoji Dk Slaa.

Mkutano leo

Mkutano wa waandishi wa habari ulioitishwa leo unatarajiwa kujibu  baadhi ya hoja za utetezi za viongozi hao zilizotolewa juzi. Zitto alifichua kile alichokiita tuhuma zilizotolewa dhidi yake mbele ya Kamati Kuu akimaanisha kwamba tuhuma zilizotamkwa kwenye vyombo vya habari na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe hazikuwa kamilifu.

Habari zinasema uongozi wa Chadema utaweka wazi kile kinachodaiwa kuwa ni “Zitto kujitungia tuhuma, kisha kuzipatia majibu”, badala ya kujibu hoja ambazo zilitolewa na Kamati Kuu.

Jana, Dk Slaa akizungumzia suala hilo alisema Kamati Kuu haiwezi kuchaguliwa tuhuma za kusema na za kuacha... “Hiyo hoja walete kwenye vikao, nani anayeipangia Kamati Kuu ichukue hatua gani pale inapotaka kufanya hivyo?”

Ofisa Habari wa Chadema, Tumaini Makene akizungumza jana alisema: “Kamati Kuu ilijadili mambo mengi na hayo ndiyo tunataka umma ufahamu msimamo wetu kama chama.”

Habari ambazo zimelifikia gazeti hili zinasema katika mkutano huo, huenda uongozi wa Chadema ukaweka wazi “makosa mengine” ambayo Zitto anadaiwa kuwa amewahi kuyafanya na kuonywa katika vikao vya ndani ikiwa ni pamoja na kiongozi huyo kutofika makao makuu ya chama hicho kwa zaidi ya miezi sita. “Kuna makosa mengi (Zitto) ameyafanya yenye sura ya kukiumiza chama chetu na alionywa mara nyingi tu, tena na vikao vya juu vya chama kuhusu mwenendo wake, lakini aliendelea na uasi.Sasa Kamati Kuu imechoka,” alisema mmoja wa maofisa wa Chadema Makao Makuu.

Habari zaidi zinasema katika mkutano wake wa leo, chama hicho kitatoa ufafanuzi kuhusu mikutano yote ya kichama ambayo imekuwa ikifanywa na Zitto, huku kukiwa na hoja kwamba alikuwa akifanya hivyo bila kuwashirikisha maofisa wa makao makuu wala sekretarieti ambayo kimsingi ndiyo inapaswa kuiandaa.

Wasomi wanena

Akizungumzia mgogoro huo, mtaalamu wa mambo ya siasa na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Richard Mbunda alisema hali inayoendelea ndani ya Chadema ni matokeo ya vyama vya siasa kutofanya kazi kama taasisi.

“Misingi ya vyama haiweki wazi misingi ya watu kuwa viongozi. Kwa mfano, kesho nikitaka kujiunga na Chadema nitaweza kuwa Mwenyekiti? Misingi ya wazi hakuna,” alisema Mbunda.


Alisema hali ilivyo ndani ya Chadema kwa sasa ni furaha ndani ya CCM, kwani watu wanaona kuwa chama kilichoonekana kuwa mbadala hakiwezi hata kushughulikia mambo yake ya ndani.

Mhadhiri Mwandamizi wa Sayansi ya Siasa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Alexander Makulilo alisema vyama vya siasa ni watu au kikundi cha watu wenye malengo na mitazamo tofauti.

“Ukisoma huo waraka utaona kuwa unazungumzia uongozi, upungufu uliopo kwenye uongozi na namna ya kubadili uongozi, mimi binafsi niseme ieleweke kwamba hata kwenye jumuiya yoyote mambo haya yapo hasa kwa kuwa walikuwa wanaelekea kwenye uchaguzi,” alisema. Alisema haoni kwa nini Zitto na Dk Kitila waonekane wahaini kwa kupanga mikakati yao ambayo walitaka kuitekeleza kupitia uchaguzi.


“Mabadiliko ni jambo la kawaida, hali hii ya kuwaondoa kwenye nyadhifa zao inawezekana ikawagharimu Chadema na inaweza kuwagharimu zaidi wakiwafukuza uanachama,” alisema Makulilo.

DK.KITILA "NILISHIRIKI KUANDAA NA KUHARIRI WARAKA"

$
0
0
Aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Dk Kitila Mkumbo amezungumzia mambo sita yaliyojitokeza baina yake na wajumbe wenzake kabla ya kutimuliwa katika wadhifa huo.

Aidha, alisema alishiriki kuuandaa na kuuhariri ‘Waraka wa Mkakati wa Mabadiliko 2013’ uliokuwa mahususi kumwandaa aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe kuwa mwenyekiti.

Dk Mkumbo alivuliwa wadhifa huo akituhumiwa kufanya vitendo kinyume cha katiba na taratibu za chama hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mhadhiri huyo wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alisema: “Waraka ulilenga kujenga hoja ya kufanya mabadiliko ya uongozi na kuainisha mikakati ya ushindi kwa mgombea mlengwa katika Uchaguzi Mkuu wa Chadema ambao kwa ratiba ya awali ulikuwa ufanyike Desemba mwaka huu.”

Alisema katika kikao cha Kamati Kuu kilichowavua wadhifa huo, wajumbe walisema waraka huo ulikuwa na upungufu na ulikiuka misingi na kanuni zilizoainishwa katika Katiba ya Chadema.

“Kwa kuwa dhamira yangu imekuwa ni kusukuma mabadiliko ambayo Watanzania wanayatizama nje ya mfumo wa sasa wa utawala, nilikiri makosa na niliomba msamaha na kuomba kujiuzulu nafasi zote za uongozi ombi ambalo lilipingwa na wajumbe. Mwanasheria wetu akawashauri kuwa tukijiuzulu tutaondoka na heshima zetu, akataka tufukuzwe ili tuondoke na aibu,” alisema Dk Mkumbo. Alisema kunapokuwa na uchaguzi ndani au nje ya chama, watu lazima wafanye mikakati akisema hata leo Chadema kunafanyika mikakati ya kuiondoa CCM madarakani mwaka 2015 na kwamba kitendo hicho siyo dhambi.

Alisema katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu wa ndani wa Chadema, kuna haki ya kujiandaa… “Sisi tunaamini mabadiliko, mimi na Mwigamba tulianza kutengeneza mkakati, kwanza tuainishe sababu za kutaka mabadiliko, pili tutafute nani anayefaa kuwa mgombea wetu.”

“Tuliazimia kwamba tukimpata tuchambue nguvu na udhaifu wake na pia kuchambua udhaifu wa mgombea tunayedhani atatoka upande wa pili. Tulifanya hivyo kwa siri na ilikuwa siri kati yangu mimi na Mwigamba kwa sababu mikakati ya uchaguzi ni siri.”

Alisema kuwa baada ya kukamilisha mchakato huo wangemfuata Zitto na kumwomba kuwa mgombea: “Ndiyo maana tulieleza katika waraka kwamba hatuna uhakika kama Zitto atakubali kugombea, tulitaka kufanya haraka kukutana naye, ila uchaguzi ulipohairishwa nasi tukatulia.”

Alisema kikao cha Kamati Kuu kilipokutana Zitto alikuwa hajui lolote kuhusu waraka huo, pia yeye (Dk Kitila), alikuwa hajui kama waraka huo ulikuwa umevuja kwa wanachama wa Chadema, wakiwamo wajumbe wa Kamati Kuu.

“Siamini kama kugombea nafasi yoyote ndani ya chama ni uhaini. Msingi namba moja wa Chadema ni demokrasia ambayo inatakiwa kuruhusu ushindani katika nafasi za uongozi na hasa wa juu. Wanasema uhaini kwa sababu ya wasiwasi wa siasa za ushindani katika chama chetu, hakuna uhaini wala hujuma,” alisema.

Alisema siasa za ushindani nchini hazijaanza leo na kutolea mfano jinsi uchaguzi wa Chama cha Tanu alivyokuwa na ushindani kati ya Mwalimu Julius Nyerere na Ally Sykes.

“Rais Barack Obama wa Marekani alianza mikakati mapema, waliomfikisha pale alipo ni watu wanne waliotengeneza mkakati wa kupata mgombea na kufanya ashinde bila Obama kujua,” alisema.

Alisema yeye na Mwigamba walitumia njia hiyo na kwamba baadaye wangemfuata Zitto, wangembembeleza na wanaamini kuwa angekubali, “Siasa za ushindani ndani ya vyama ndiyo huzaa ushindani wa kweli katika jamii na kujenga demokrasia ya kweli katika jamii.”

Alisema waraka huo ulioandaliwa na watu wawili unaoeleza udhaifu na nguvu ya Chadema ulikuwa siri,  lakini anashangazwa kuona viongozi wa chama hicho kuusambaza, huku akiwataka wanachama wa Chadema kuusoma waraka huo na kueleza uhaini wao ni nini.

Alisema waraka huo haukulenga kukibomoa Chadema, bali kujenga taasisi na kufafanua kuwa aliomba kujiuzulu nafasi yake si kwa sababu ya kuogopa aibu ya kufukuzwa isipokuwa kutambua jinsi wenzake walivyokosa imani naye.

Aliwataka wanachama wa Chadema kupigania kwa dhati misingi mama ya chama ikiwamo demokrasia ya ndani.

“Tutawashawishi Watanzania kwamba chama hiki ni cha demokrasia kwa sisi wenyewe kuonyesha ushindani ndani ya chama. Hakuna namna ya kuweza kudhihirisha hilo zaidi ya kuruhusu uchaguzi huru na watu washindane kwa hoja,” alisema Dk Kitila.

Alisema wanachama wa Chadema wanatakiwa kulaani tabia iliyoibuka ndani ya chama hicho kuwaita watu wenye mtazamo tofauti na viongozi kuwa ni wasaliti. “Kukataa siasa za ushindani ndani ya chama ni kuhujumu demokrasia na ndiyo usaliti, kukataa demokrasia na kukosolewa huo ndiyo usaliti wenyewe.”

Alisema lugha za kuitana wasaliti au wahaini zilitumika katika mataifa ya kikomunisti kunyamazisha upinzani na kuzaa udikteta kwenye mataifa hayo, kwamba utamaduni huo ukilelewa Chadema utajenga udikteta.

MWANAMUZIKI AMANI KUTOKA KENYA AFUNGUKA NA KUSEMA AM IN LOVE

$
0
0
Amani has been one of the most dominant women in the Kenyan music industry, lately dominating the airwaves with her collabo with Ugandan duo Radio & Weasel 'Kiboko Changu'.

She has also kept her private life very private until now that she reveals that she has indeed fallen in love. She shared the news with her fans on her Facebook page in two short words, leaving them speculating on the who and what this means....




AMANI WAIRIMU
about an hour ago
In love.
Like ·  · Share


Who is the lucky fellow?

MCHUMBA ALIYEUA NA KUJIUA ILALA, CHANZO PICHA ZA UTUPU

$
0
0
Stori: Waandishi Wetu, Dar es Salaam na Mwanza
MAPENZI ni sanaa tata sana, inawaumiza wengi, inavunja mioyo ya watu, inakatisha tamaa ya maisha, inaleta umaskini, inasababisha mauaji lakini siyo rahisi kuachana nayo na kwa mantiki hiyo, matukio mengi yataendelea kujiri.

Tukio la Gabriel Munisi kuua watu wawili kisha naye kujiua kwa kisa cha mapenzi, ni mwendelezo wa ‘sinema machafuko’ za mapenzi.
Nyuma ya tukio hilo kuna mengi yanazungumzwa, ila gazeti hili limenasa habari kuwa picha za utupu na SMS za mapenzi ni chanzo cha kila kitu.

NINI HASA CHANZO?
Gazeti hili limebaini kuwa tukio hilo la mauaji, lililochukua nafasi alfajiri ya Jumanne iliyopita, chanzo chake ni Gabriel ‘Gaby’, kunasa picha zinazomuonesha mchumba wake, Christina Newa akiwa na mwanaume mwingine.
Habari zinaeleza kuwa Gaby alichukua kompyuta mpakato (laptop) ya Christina na kuikagua, ndipo akakuta picha ambazo mchumba wake huyo alikuwa katika hali ya kustarehe na mwanaume mwingine.
“Kwanza ile laptop ilikuwa inafunguliwa kwa namba za siri (password), ikabidi Gaby awatafute wataalamu wa kompyuta waweze kumsaidia kuifungua.

“Laptop ilipofunguliwa, Gaby aliikagua na kukuta picha ambazo Christina alikuwa ufukweni na mwanaume mwingine.
“Kuanzia hapo, Gaby akawa analalamika kwamba zile picha ni mbaya sana, ni za utupu na kwamba mchumba wake amemfanyia kitendo kibaya sana,” kilisema chanzo chetu na kuongeza:
“Kama ndugu au hata jeshi la polisi, wangesoma alama za nyakati, pengine yale mauaji yasingetokea maana dalili zilijionesha waziwazi mapema.”


DALILI ZA MAUAJI
Chanzo chetu kilisema kuwa wakati Gaby anaziona picha hizo, alikuwa nyumbani kwake Mwanza, wakati Christina alikuwa Dar es Salaam.
“Kutokana na hali hiyo, Gaby alimpigia simu Christina aende Mwanza. Bila kujua anaitiwa nini, Christina alifunga safari na kwenda Mwanza.
“Christina alipofika Mwanza Gaby alimnyang’anya simu zote mbili alizokuwa nazo, akapitia SMS zote na kubaini kwamba zipo za mapenzi.

“Gaby akaunga matukio na kudai kwamba mtuma SMS za mapenzi ndiye mwanaume anayeonekana kwenye picha na Christina.
“Christina alisema kuwa hakukuwa na ubaya wowote kwa sababu zile picha siyo mbaya ni za ufukweni tu na wanafunzi wenzake,” kilisema chanzo chetu na kuongeza:
“Utetezi huo haukumsaidia chochote, maana kuanzia hapo aliendelea kupokea kichapo kila mara, kufungiwa ndani na kupewa kila aina ya mateso.”

KILICHOTIBUA NI MASOMO YA ULAYA
Habari zaidi zinasema kuwa Gaby alikuwa anawaambia marafiki zake kuwa kinachomuuma kuhusu Christina ni kumgharamia masomo kwenye Kisiwa cha Cyprus barani Ulaya.
“Alikuwa akilalamika kuwa kama asingempeleka Cyprus kusoma, yote yasingetokea, maana akiwa huko ndiko alipata mwanya wa kujirusha na mwanaume mwingine na kupiga picha alizozikuta kwenye laptop,” kilisema chanzo chetu.

Habari zinaongeza kuwa sekeseke zima lilitokea wakati Christina akiwa amerejea nchini kwa likizo.
“Aliporudi nchini aliamua kwenda Mwanza kumsalimia mpenzi wake Gaby, baadaye akaelekea Dar lakini kule Mwanza aliacha laptop ambayo iliibua kasheshe nzima,” alisema mtoa habari wetu.

DADA ASIMULIA KISA CHA LAPTOP, PICHA NA SIMU
Caroline ambaye ni dada wa Christina, alipozungumza na waandishi wetu, nyumbani kwao, Ilala, Dar, alifafanua kiundani kisa cha laptop, picha na simu, huku akisema kuwa marehemu shemeji yake (Gaby) ni katili.
Caroline, aliye Ofisa Uhusiano wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), alisema: “Julai mwaka huu mdogo wangu alikuja likizo akitokea chuoni Cyprus. Gaby ndiye alimpokea Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar es Salaam na moja kwa moja walikwenda Mwanza bila kupitia nyumbani.

“Baada ya wiki mbili, Christina alimuomba Gaby ampe ruhusa ya kuja Dar kwa ajili ya kumsalimia mama yetu, alimkubalia lakini akamtaka achukue vitu vichache ili asikawie kurudi Mwanza.

“Christina alikubaliana naye na kuchukua vitu vichache, vingi aliviacha ikiwemo laptop aliyokuwa anatumia chuoni. Alipoondoka Gaby alichukua laptop yake na kuipeleka kwa fundi ili amfungulie kwa sababu ilikuwa na password, alipofanikiwa alikutana na picha zinazomuonesha Christina akiwa amevaa nguo za kuogelea,” alisema Caroline.

Hata hivyo, Caroline alipingana na madai kuwa Christina alipiga picha za utupu na mwanaume mwingine, badala yake alisema:
“Christina alipiga akiwa beach na wasichana wenzake huko Ulaya na hazikuhusiana na suala la kimapenzi.”
Caroline akaendelea: “Gaby hakusema kilichokuwa kinaendelea badala yake alimpigia simu na kumtaka arudi Mwanza kwani amemkumbuka. Alimkatia tiketi ya ndege na kumtumia, kweli Christina akaenda Mwanza.
“Kufika Mwanza ndiyo ugomvi ulianza. Gaby alimnyang’anya Christina simu zake mbili kisha akaanza kumpiga huku akiwa amemshikia bastola.

“Christina alimwambia Gaby kuwa kama kupiga picha na nguo za ufukweni ni tatizo basi wawasiliane na mama yetu mzazi, naye aseme maana ndivyo tulivyolelewa lakini hakuelewa.
“Gaby alimfungia ndani Christina na kumpa mateso makali ambayo yalimsababishia majeraha na kudhoofu mwili. Aliendelea kuteseka bila kutujulisha ndugu zake, maana simu zote Gaby alizishikilia.
“Kila SMS iliyoingia, alipokea na kuijibu akijifanya yeye ndiye Christina. Kutokana na mateso kuzidi kuwa makali, Christina alishauri waende kwa wazazi wa Gaby kwa usuluhishi lakini kule nako hawakusuluhishwa, baba yake Gaby alisema wavumiliane kwani hayo ni mambo ya mapenzi.

“Akiwa amefungiwa ndani, siku moja Christina alipanda dirishani na kumuona kaka mmoja akipita barabarani, akamwita, akamtajia namba ya simu ya mama yetu ili awasiliane na amwambie jinsi anavyoteseka.
“Yule kijana alipiga simu, baada ya taarifa kufika kwetu ilibidi tuongee na askari wa Kituo cha Polisi Kitangiri lakini wakatujibu hawaingilii mapenzi ya watu.
“Baadaye Christina alifanikiwa kuzungumza na watoto wa mwenye nyumba ambayo Gaby alipanga ambayo ndiyo Christina alifungiwa ndani, akaomba msaada wa kuokolewa.

“Mama mweye nyumba alimpigia simu mumewe ambaye naye alimpigia Gaby, akamwambia amepata taarifa kuhusu Christina, akamweleza kama wameshindana bora waachane kuliko kumtesa.
“Gaby alikanusha, akasema hayo maneno hayana ukweli. Hata hivyo mateso yaliendelea, kitendo kilichotufanya tumweleze ndugu yetu mwingine anayeishi huko Mwanza atoe taarifa polisi, askari hao walienda na kumchukua Christina na Gaby hadi kituoni. Hiyo ilikuwa Agosti 14, mwaka huu.

“Agost 17, Christina alirejea Dar huku akiwa hana chochote, maana kila kitu kilibaki kwa Gaby. Baada ya hapo tukasikia Gaby alikuwa anazunguka kule Mwanza kwa marafiki zake na ile laptop, akionesha zile picha za Christina.
“Tukasikia Gaby anatangaza kwamba ataua familia yetu yote, sisi tulitoa taarifa Kituo cha Polisi Pangani. Kumbe Gaby alikuja Dar na kupanga kwenye Hoteli ya MM ambayo inapakana na nyumba yetu.

“Kwa maana hiyo, akiwa ghorofani akawa anatazama kila kilichokuwa kinaendelea kwenye nyumba yetu.
 “Gaby akawa anampigia simu Christina kumuomba msamaha. Christina akamjibu atafute kwanza daktari wa saikolojia amtibu, kisha baada ya miezi mitatu ndipo watarudiana. Akamshauri pia aende kanisani akatubu kwa dhambi alizomfanyia. Gaby alikubali.

“Jumanne iliyopita ambayo ndiyo siku ya tukio, ilikuwa ndiyo siku ya Christina kwenda chuoni Cyprus. Basi akawa anasindikizwa na mama, Alpha ambaye ni mdogo wetu wa kike na mume wangu, Kapteni Francis Kiranga, walipofika getini walimwona Gaby anakuja upande wa getini, alipowakaribia, alichomoa bastola. Mume wangu (Francis)  alipomuona, alishuka kwenye gari kwenda kumzuia asifanye jambo lolote baya.
“Bahati mbaya Gaby alianza kumshambulia mume wangu kwa risasi tano, kisha akampiga Alpha na Christina kabla ya kujilipua mwenyewe.

VIFO BILA HATIA
Mungu ana siri kubwa sana, maana pengine dhamira ya Gaby ilikuwa kumtoa uhai Christina lakini mhusika akapona, ila wasio na hatia ndiyo waliaga dunia.
Francis ambaye ni mume wa Caroline alifariki dunia siku mbili baada ya tukio akiwa Hospitali ya Taifa, Muhimbili wakati Alpha, mauti yalimkuta eneo la tukio, huku Christine na mama yake, wakipata majeraha ya risasi na mpaka sasa wanaendelea na matibabu.

MUNGU AWALAZE PEMA MAREHEMU
Marehemu Alpha aliagwa Jumamosi iliyopita, nyumbani kwao Ilala, Dar es Salaam kisha kusafirishwa kwenda Goba, Bagamoyo kwa mazishi.
Mwili wa Francis, unatarajiwa kusafirishwa leo Jumanne kwenda kwao Nairobi nchini Kenya.

MWANZA WAMZUNGUMZIA GABY
Habari zinasema kuwa maisha ya Gaby kwa jumla yalikuwa ya kibabe na alikuwa mwepesi kuchomoa silaha kumtishia mtu aliyegombana naye.
“Tuliwahi kumnyang’anya bastola mara tatu, sijui kwa nini alikuwa anarudisha ile silaha yake,” kilisema chanzo chetu ndani Kituo cha Polisi Kati, Mwanza.
Hata hivyo, wapo ambao walisema Gaby alikuwa mtu mzuri na wanashangazwa na tukio zima lilivyotokea.

TAHADHARI YA WANAWAKE
Gaudencia Eliona (si jina lake halisi) ambaye amejitambulisha kuwa ni mke wa mtu, alisema kuwa matukio ya wanaume kuua kwa visa vya kimapenzi, yanaibua mengi ambayo yanafichika kwenye nyumba nyingi.

“Binafsi sina amani kabisa, mume wangu kila mgogoro kidogo anatishia kunipiga na bastola,” alisema Gaudencia na kuongeza:
“Mume wangu anao marafiki zake wanne, wote wanamiliki bastola, wawili kati yao ni wakorofi sana kwa wake zao. Jamani tunateseka, tunaishi roho mkononi.
“Katika hao marafiki wawili wakorofi, siku mmoja wao alikorofishana na mkewe, akamtishia kumpiga risasi, baadaye akaweka bastola chini ya mto, basi siku hiyo yule mke wake hakulala kwa woga.”


USHAURI KWA SERIKALI
Wakili maarufu na aliye pia Mwenyekiti wa Zamani wa Chama cha Wanasheria Tanzania, Constantine Mutalemwa, alisema kuwa anashangazwa na taratibu zinazotumika ili mtu kuweza kumiliki silaha.
 “Umefika wakati kuangalia upya sheria ya umiliki silaha nchini, kwani baadhi ya wamiliki wamekosa elimu ya matumizi ya silaha,  hivyo kusababisha matukio ya mauaji ambayo siku za hivi karibuni yamekuwa yakiongezeka,” alisema Mutalemwa.

NI KAMA UFOO SARO
Tukio la Gaby, limekuja ikiwa bado Watanzania wanakumbuka lile la Anthery Mushi, kumpiga risasi mchumba wake Ufoo Saro na mama yake, Anastazia Saro kisha naye kujilipua na kufa papo hapo.
Katika tukio hilo, Ufoo alipona, huku Anastazia akifariki dunia.

Imeandikwa na Gladness Mallya, Makongoro Oging’, Issa Mnally, Dar es Salaam na Mashaka Baltazar, Mwanza.


P SQUARE WAMUUMBUA DIAMOND PLATNAM..!! HAYA NDIYO WALIYOSEMA

$
0
0
Mwanamuziki wa P square, Peter Okoye ameoneshwa kushangazwa na taarifa kwamba mwanamuziki wa bongo fleva Naseeb Abdul alihudhuria harusi yake hivi karibuni nchini Nigeria na kuhudhuriwa na mastaa mbali mbali akiwenmo msukumba gozi wa Totenham Hotspurs Adebayor.

Awali kupitia blogs mbali mbali kulisambaa taarifa kuwa dimond alikua mwanamuziki pekee afrika mashariki aliyealikwa katika sherehe hiyo iliyohudhuriwa na tajiri nambari moja afrika, Aliko Dangote.

Blogs hizo zilikwenda mbali kwa kumpamba diamond kwa vyeo vya ajabu ajabu ikiwemo Michael Jackson wa afrika mashariki jambo ambalo lilisababisha wengi kumponda.

Akihojiwa na kituo cha EATV mara baada ya kuwasili jijini Dar kwa ajili ya shoo iliyopigwa viwanja vya leaders club, Okoye alishangazwa na taarifa za dimond kuhudhuria katika harusi yake.


Okoye alikua akijibu swali aliloulizwaa na mtangazaji wa kipindi cha HotMix Adrian Hilary kuhusu diamond kuhudhuria harusi hiyo ambapo alionesha kushangazwa na jina hilo na kuhoji Diamond ni nani?

Kushangaa huko kulimaanisha licha Diamond kujichezesha mbele ya Okoye siku ya harusi yake lakini mwanamuziki huyo hakua akijua aliyekua akimzungushia viuno vya ngololo ni nani.

STEVE RnB AMVISHA PETE MCHUMBA WAKE WA TOKA SECONDARY

$
0
0
Hit maker wa ‘Jambo Jambo’ Steve RnB amefungua ukurasa mwingine wa mapenzi baada ya kumvisha pete ya uchumba mpenzi wake wa siku nyingi ikiwa ni kiashirio cha kuelekea katika ndoa.

Kwa mujibu wa VIBE, Steve ambaye pia ni memba wa bendi ya In Africa amemvisha mpenzi wake huyo anayesemekana kuwa ni wa toka enzi zao za shule.

Kwa picha hii (hapo juu) inaonekana Steve hakutaka kufanya party wala kuifanya kitu kikubwa zaidi ya kuwasilisha ombi lake wakiwa kibarazani na kumwambia kipenzi chake ‘will you marry me’? Hopefully jibu lilikuwa Yes!

Hongera kwa Steve tunawatakia safari njema ya kuelekea kwenye ndoa yeye na mchumba wake.

PICHA: VIBE

JACK CLIFF NA JUX BADO NI UTATA...WAPENZI AMA MARAFIKI

$
0
0
Kwa muda mrefu muimbaji wa kundi la Wakacha, Jux na video vixen wa Tanzania, Jackie Cliff wameendelea kukanusha kuwa na uhusiano wa kimapenzi, lakini bado picha zinazowaonesha wakiwa pamoja, zimeendelea kuzalisha maswali mengi vichwani mwa watu wanaowafahamu.

Hivi karibuni, Jux alipost picha Instagram akiwa amemshikilia Jackie mkono wakitembea pamoja kama mtu na mpenzi wake na kuandika: We jus outchea livin our mfkn lives. Siku chache kabla ya picha hiyo, Jackie naye alipost picha akiwa na Jux na kuandika: My bff is better than yours..’

Miezi mitatu iliyopita , Jackie ambaye ameonekana kwenye video ya Linex ya wimbo wake Kimugina hivi karibuni, aliweka picha ya Jux na kuandika ujumbe mrefu wa kumtakia siku njema ya kuzaliwa akisema:

I don’t like to call u a friend..To me ur just a special friend..A wonderful friend..A heaven sent,And todai its your special day..God keep showering you with lots of success and blessings cuz you deserves so much more..And your so special to me..Ladies and Gentlemen help me wish Happy Bday To this handsome friend of mine’Bongo5.com

HUSSEIN MACHOZI AWASHIRIKISHA SAUTI SOUL KATIKA WIMBO WAKE MPYA-SIKILIZA NA DOWNLOAD HAPA

$
0
0
Hussein Rashid aka Hussein Machozi aendelea kufungua njia za kujitangaza kimataifa baada ya kufanya collabo na wasanii wakubwa na wenye mafanikio barani Afrika na nje wa kundi la SAUTI SOL kutoka Kenya.

Machozi ameachia single mpya aliowashirikisha Sauti Sol inayoitwa ‘Utapenda’, iliyofanywa jijini Nairobi miezi kadhaa iliyopita.

Huu ni wimbo wa mapenzi ambao Machozi na Sauti Sol wanasifia mapenzi ya nchi zao, Hussein akiwaambia jinsi ambavyo mabinti wa kibongo wanavyojua kupenda, huku Sauti Sol wakisifia jinsi mapenzi ya Kenya yalivyo matamu, mwisho wa siku ‘Utapenda’.

Sikiliza hapa:
Bongo5.com

PICHA ZA RAYUU ZENYE UTATA ZASAMBAA MTANDAONI..

$
0
0



Haijajulikana Kama walikuwa wana Act movie ama ndio mambo yaleeeeeeeeeeeee
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images