Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Kutongoza Wanawake Walioolewa ni Rahisi Kuliko Wasioolewa..

$
0
0
Hili sasa halina mjadala au ubishi kuwa kumtongoza mke wa mtu ni rahisi sana kama kusukuma tairi katika mteremko wa mlima kitonga. Lakini ni ngumu mno kutongoza hawa wasichana wetu wa kiswaz wana mlolongo mrefu na usumbufu.

Kwanini hali hii?

Karibuni

Faraja Kota Nyalandu 'Sio Lazima Ujue Kila Kitu Kila Wakati na Hutokaa Ujue Kila Kitu Kila Wakati'

$
0
0
Sio wakati wote utakuwa na majibu. Sio wakati wote utajua kama unapatia au unakosea. Sio wakati wote utakuwa na uhakika. Ninachotaka kukuambia ni kuwa; it is okay. Si lazima ujue kila kitu kila wakati. Na hautokaa ujue kila kitu kila wakati (translation: don't be self-righteous). But it's okay. Tujue mipaka yetu, tujue uwezo wetu na tujue mapungufu yetu. Tujitambue. Tujikubali. Tuanze kujiboresha kuanzia hapo. But put your worries to rest because it's okay, we are human beings afterall...here is one of my favourite lines: Feel the fear and do it anyway! P. S 


Baada ya Mahojiano, Gwajima Aachiwa kwa Dhamana, Kwenye Hii Kesi Nani Mlalamikaji ?

$
0
0
Taarifa zimeenea kuwa baada ya Kutoka hospitalini Gwajima alikwenda moja kwa moja Kituo cha polisi Ostabey kwa ajili ya kumaliza mahojiano yake na Polisi kuhusu kumtukana Askofu Pengo...Baada ya mahojiano Askofu Gwajima Ameachiwa Huru kwa Dhamana....

Najiuliza kwa Sauti:
Katika Hili Sakata ni Nani Mlalamikaji ? Wakati kila mkubwa akijidai hausiki kwenye sakata hili
Je Pengo Amemshitaki ?


Mwanamuziki Suma Lee Akata Shauri Aamua Kuacha Mziki, Aagiza Nyimbo zake zifutwe na Redio Wasizipige Tena

$
0
0
Hit maker wa ‘Hakunaga’, Suma Lee amesema kuwa hatafanya tena muziki kwasababu ameachana kabisa na maisha hayo na ameamua kusomea dini ya kiislam

Suma ambaye alitengeneza pesa nyingi kupitia hit yake ya ‘Hakunaga’, amesema kuwa hana mpango wa kuzitoa nyimbo zake zilizoko studio ambazo hazijatoka.

“sifanyi tena muziki na nimeachana kabisa na maisha hayo, na nyimbo zote zilizobaki studio nimezisimamisha zisitoke baada ya kuzilipia, “ Alisema Suma.

“kuna wimbo mmoja nimefanya na Cp ambao ndio ulikuwa wa kurudisha kundi la Parklane, pia nimeuzuia, labda Cp auchukue yeye.Kilichobaki ni kuwaombea wazazi wetu waliotutangulia, wengine walikuwa hawataki tufanye kazi hizi, kwa kuwa hawapo na hakuna wakutukataza tena, bora tukae na kuwaombea.”

Diamond Platnumz Amvisha Pete ya Uchumba Zari Kimya Kimya..lemutuz Atoboa Siri Kwenye Letamkoz

$
0
0
Wenyewe wakiwa wamefanya siri tukio la kuvalishana pete ya Uchumba , Lesuper star Lemutuz amemwaga mchele kwenye kuku wengi kwa kufichua siri kupitia page yake ya Instagram kama ifuatavyo:

"FROM THE KING OF ALL BONGO SOCIAL MEDIA NETWORK....here is LE TAMKOZ TWO....Mwenye Mkono ni The Bosslady Zarina Hassan...ni Pete ya ENGAGEMENT RING ...from my KING ..the KING OF POP MUSIC IN EAST Naseeb Diamond Platznumz ..and the Bosslady Zarina Hasan is PREGNANT by MY KING THE KING DIAMOND PLATZNUMz and the BABY is a GIRL....thank yah my Big Sponsors Stone Block Building Materials & the Double Tree Hilton Hotel.....my people thank yah and LOV U ALL NAWAPENDAZZZ U KNOW and I am humbled! - le Mutuz

Kisha Akaandika Maneno haya Hapa Chini:

They are my Friends and they are very good people wana mapungufu yao so are we..they are the Biggest Super Stars in East Africa at this moment wala haina Ubishi loong time ago at the Birthday Party of Aunt Ezekiel I met Diamond he was Super down I told him to find a solution cause Matatizo hayampati mtu asiyekuwa na jawabu ukiona una matatizo na huna jawabu ujue ni super gademu mburulazzz dead mazafantaz.....now I saw him on Sunday the man was happy and for that I am happy for him too and he was very protective of his Woman....ukikutana na mpenzi mpya utakuwa kichaa kutaka kujua mambo yake ya zamani ili yakusaidie nini?....Baba yangu aliniambia "Mwanamke ni kisima unless umemuona mtu anakichota huwezi kujua kama kilichotwa" ...ndio maana mimi baby wangu nitaamini ana cheat only nikimkuta hana nguo na yupo kwenye act sio vinginevyo wala maneno ya mburulazzz....mapenzi sio mchezo naona kuna watu wanayazungumzia kama Yanga na Simba na binadam unaheshimika kwa msimamo ninasema tena na tena these are my people sina uadui na mtu ingawa najua kuna wanaojiita maadui zangu mimi nasema ni maadui wanaojichukia wenyewe cause HATUFANANI...mimi nina DEGREE 3 wao hawana ni FACT sio OPINION...now this case of LE TAMKOZ TWO is closed tuendelee na mengine JAMANI USIKU MWEMA SANA! - le Mutuz

Hongereni Diamond na Zari kwa Kufikia Hatua Hiyo

Mwigizaji Lulu Michael Apachikwa Ujauzito..Atupia Picha ya Kitumbo Mtandaoni

$
0
0
Staa mrembo kutoka Bongo Movies, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amewacha njia panda  mashabiki na wafuasi wake kwenye mtandao wa INSTAGARM baada ya hapo jana usiku kubadika picha ya mwanamke mwenye ujauto na kuandika maneno ambayo hayaelezi wazi kuwa ni yeye.

“Happy New Month Lovies….Si ruksa kuitana wala ku munch”-Lulu aliandika.

Kitendo cha Lulu kuchimba mkwala akiwata watu wasiitane  kuja kuona wala kufanya kijiwe cha  kujadiliana juu ya picha hiyo (Kama inavyoonekana hapo juu) ndio kuliamsha hisia yz watu kuwa inawezekana mrembo huyo atakuwa anaujauzito hata kama picha hiyo siyo yake na hiyo anajaribu kudokeza watu kiana.

Lakini pia wapo waliochukulia ni utani tu, huku wengine wakimpongeza kwa kujaaliwa kupata ujauzito.

Lulu hakuibuka kujibu komenti nying za watu ambao zilikuwa zikihoji kana ni kweli au la.

Muda utazungumza, tuvute subra...

Roho Inaniuma Sana Naomba Wema Sepetu Umsamehe Kajala..Hakuna Binadamu Aliyekamilika

$
0
0
Jambo bongo movie! Naitwa gloria, ni mukongomani naye ishi south africa. Napenda sana kazi zenu, tena sana..... Nawapendeni wote. Nina ombi moja, ninge penda muwa unganishe wasani wema sepetu,na kajala. Ahhhhh mimi nawapenda sana, na kila mara ninapo soma kwenye mitandao bifu yao iki endelea ahhhh roho ina niuma sanaaaaa. Naomba wema,amusamehe kajala. Hakuna bina damu aliye kamilika, wote tuna jaribiwa, lakini njia mbadala yaku shinda hayo niku samehe tu kwa moyo mukudjufu, maana hata biblia ina tuomba kusamehe wengini 7*70. Jo kuishi kwa utakaso.... Ijapo kuwa usani, ila tujuwe kuishi uchristu. Najuwa ombi langu lita fika. Peace and love bongo movie.

By: Gloria S. Mbobochi 

Wanaigeria Wafanya Kweli Wakipiga Chini Chama Tawala na Kumchagua Raisi wa Upinzani..Je Tanzania Tutaweza?

$
0
0
Mgombea wa upinzani nchini Nigeria Muhammadu Buhari ameibuka mshindi wa kiti cha urais dhidi ya Rais Goodluck Jonathan katika uchaguzi uliofanyika Jumapili nchini humo.

Kwa mujibu wa Reuters, Buhari wa chama cha upinzani cha APC amepata kura million 15.4 dhidi ya kura million 13.3 alizopata Jonathan.

Chama cha Rais Jonathan All Progressives Congress (APC) kimesema kuwa Jonathan amekubali matokeo na amempigia simu Buhari kumpongeza kwa ushindi huo.

Ushindi huu wa Buhari ambaye ni kiongozi wa zamani wa jeshi unaandika historia katika taifa hilo kwa kuwa ni mara ya Kwanza kwa chama cha upinzani kushinda kiti cha urais kwa njia ya kidemokrasia

Baadhi ya waangalizi wa uchaguzi huo wamepongeza namna uchaguzi ulivyoendeshwa licha ya kuripotiwa kwa hujuma katika baadhi ya maeneo ambazo zilisababisha hofu ya kutokea kwa vurugu.

Je, Tanzania tunapoelekea katika uchaguzi mkuu Oktoba 2015 tujifunze nini kutoka katika uchaguzi huu?

Majambazi Tena ! Yaua Askari Polisi Wawili Kwa Kutumia Panga na Kisha Kupora Bunduki na Kutokomea Pasipo Julikana

$
0
0

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na Polisi Mkoa wa Pwani linaendesha oparesheni kali ya aina yake ya kuwasaka majambazi waliowavamia, kuwaua askari wawili na kumjeruhi mmoja na kisha kupora bunduki aina ya SMG.

Tukio hilo limetokea tarehe 30/03/2015 majira ya saa mbili usiku huko barabara ya Kilwa Kata ya Vikindu Wilaya ya Mkuranga Mkoa wa Pwani. 
  
 Katika tukio hilo majambazI wapatao 8 hadi 10 wakiwa na mapanga na silaha zingine waliwavamia ghafla askari watatu waliokuwa kazini katika eneo la kizuizi cha Polisi kilichopo kijiji cha Kipara mpakani Kata ya Vikindu Wilaya ya Mkuranga Mkoa wa Pwani.

Majambazi hao waliwashambulia ghafla askari hao kisha kupora silaha aina ya SMG ikiwa na risasi 30 ndani ya magazine na kutokomea kusikojulikana.

Majina ya askari wa Wilaya ya Kipolisi ya Mbagala waliouawa ni kama ifuatavyo:
D.2865 SGT FRANCIS,
E.177 CPL MICHAEL,
Askari mwenye namba D5573 D/SGT ALLY amejeruhiwa kwa risasi kwenye paja la mguu wa kushoto na amelazwa katika hospitali ya Temeke kwa matibabu.
  
Askari huyu kabla ya kujeruhiwa alipambana vikali na majambazi hayo kwa kutumia bunduki aliyokuwa nayo aina ya SMG ambayo walishindwa kumpora hivyo wakatokomea kuelekea pori la Vikindu.

Katika oparesheni hiyo, nguvu na mbinu zote za kipolisi zitatumika ambapo vikosi vya Dar es Salaam na Pwani vilianza kufanya oparesheni hiyo mara baada ya tukio ili kuhakikisha kwamba majambazi hao wanapatikana haraka iwezekanavyo.

Pamoja na oparesheni hiyo kali inayoendelea, Jeshi la Polisi linachunguza ili kubaini kama tukio hili linaashiria vitendo vya ugaidi au ni ujambazi wa kutumia silaha.

Natoa wito kwa wananchi wa mikoa ya Pwani na Dar es Salaam kupitia (dhana ya polisi jamii) kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa hali na mali kwa kutoa taarifa sahihi.

IMETOLEWA NA:
S.H. KOVA
KAMISHNA WA POLISI KANDA MAALUM
DAR ES SALAM

Baada ya Mambo Kuwa Magumu Kwa Askofu Gwajima Wafuasi Wake Wameamua Kufanya Haya ili Kumnusuru Askofu Wao

$
0
0
WAKATI mambo yakiwa bado tete juu ya afya ya kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima la jijini Dar es Salaam, Mchungaji Josephat Gwajima, wafuasi wake wametangaza kufunga kwa muda wa siku 40 kuanzia juzi Jumatatu ili kuomba.

Jamaa wameona hali sasa inakuwa ngumu, wanafunga kwa vikundi, kila mmoja anamuombea apate afya njema baada ya kuzidiwa wakati akihojiwa, lakini pia wanataka haya mambo yamalizike, kwa hiyo wameona ni bora kumuachia Mwenyezi Mungu ili ayamalize,” kilisema chanzo hicho.

Picha Zingine za Wema Sepetu na Idriss Usiku Mnene Wakinong'onezana na Kufutana Jasho Zazidi Kuzua Maswali

$
0
0


Baada ya zile Picha za Mrembo Wema Sepetu akiwa na Mshindi wa Big Brother wakifanya shopping kuzua maswali mengi mtandaoni hapo juu nimekuwekea zingine wakiwa kiwanja cha starehe Escape one wakila bata kwa raha zao huku ukaribu wao ukionekana zaidi kwa kufutana jasho na muda mwingine kushikana shikana huku wakinong'onezana kwa chini chini....

Tupe Maoni yako

Siri Yafichuka Kumbe Wasanii Wengi wa Bongo Hawampendi Wame Sepetu..Wanakesha Kwa Waganga Kummaliza

$
0
0
Hii Siri Imetoka Kwa Page ya Instagram ya Mrekebishatabia....Jisomee Hapo chini Siri nzima:

"Naomba nimalizie khs Wema ntaifuta post hii....Nimejaribu kupitia maoni yoote na sijaona mtu amethubutu kusema kosa la Wema ni nini na why anatukanwa so watu wanamuonea wivu bure...achana na masuala ya msiban...amekwenda na katoa mchango wake.... Sasa naomba niweke wazi hili suala nyeti sikutaka kuweka hapa ila imenibidi ili ujumbe huu umfikie @wemasepetu na wanaomuwazia mema kumuombea... niwieni radhi nadhan mtanielewa @ssepetu @nsepetu @ssepetu ! 

Kutoka chanzo cha ndani kabisa...habari za uhakika!!! Wasanii wengi hawampendi Wema!! Wanajaribu kila njia kummaliza kisanii au hata kila atakachokifanya asifanikiwe na kujaribu kufifisha nyota yake, na asilimia kubwa za account feki zinazomtusi Wema ni wasanii au watu wa karibu wenye chuki na yeye!! Ili kumpoteza ndo maana mambo mengi yanaenda then yanakwama au saa nyingine Wema hajitambui na maisha anayoishi si yeye, wakati mwingine kama yupo yupo tu... anapambana sana..ingebidi afike mbali zaidi ya hapo au zaidi ya msanii mwingine unayemjua!!!.... anajitahidi kusogea japo ana vita kubwa sana yawezekana hajui.... 

kwa sasa anaanza kurudi lakini bado watu wanakesha kwa waganga kummaliza!! Tatizo la Wema ni kwamba anamuamini kila mtu...na ni rahisi mtu kufanya kitu chochote kwake, @wemasepetu watu ni wabaya sana mtu anaweza kukuwekea hata sumu kwenye kinywaji hatuombi iwe hivyo ila si unaona mwenyewe unavyochukiwa bila sababu?????.. kuwa karibu na ndugu zako tuu tafadhali!!! Na mpango uliopo ni kumchonganisha na dada zake ili wasipatane na asiwasikilize...japo wanafeli naamini hata Wema anapiga sala.. kikubwa sana ni maombi ndo yatamsaidia. Tatizo ni NYOTA yake.... mambo mengi ambayo amefanya ambayo hatukutegemea hakuwa yeye alifanyiziwa!! Sometimes I wish ngempeleka kwa pastor wangu aombewe.... "NYOTA" ya Wema inasakwa na Mungu amsaidie ndoto zake zisikatishwe. Amen"

Mswaada wa mahakama ya kadhi waondolewa bungeni

$
0
0
Muswada wa mahakama ya kadhi umeondolewa rasmi hivyo hautojadiliwa bungeni. Katibu wa bunge Thomas Kashilila amesema kuwa muswaada huo hautakuwepo kwenye ratiba za bunge badala yake nafasi hiyo itachukuliwa na miswaada mingine kujadiliwa.

Source: Gazeti Uhuru

Google Kuzima Simu za Watumiaji wa Android kwa siku 21 au Zaidi Kuanzia Leo Usiku

$
0
0
Android OS ni moja kati operating system iliyozidi kusambaa duniani kote huku ikiwa na mpinzani mkubwa sana ambae ni iOS mara baada ya OS nyingine kutofanya vizuri.

Taarifa zilizotelewa na Google ambao ni wamiliki wa Android OS wamethibitisha kwamba kuna malware ambao waliweza kuwa backdoored ktk Android Kernel yaani Linux kernel ambayo imeweza kusababisha security hole flow katika device hizo zitumiazo Android.

Hivyo basi Google kama wamiliki wa android wanalazimika kuzima simu baadhi zitumiazo OS yao kwa muda usiopungua siku 21 yaani wiki tatu... Au pungufu ya hapo ili kuweza kufanya marekebisho na kutoa update kwa kila device ambapo user ata update mwenyewe.

Ni taarifa yakusikitisha sana kwasabu wale wapenzi wa Instagram, Facebook na whatsapp litawacost suala hili.

Tembelea hapa kuona kama simu yako inaweza kuzimwa kupitia operation hii List of all smartphones which will face the issue

Dr Kessy Anakuletea Dawa za Kutengeneza Hips, Makalio, Nywele na Nguvu za Kiume Kwa Kutumia Dawa za Asili zisizo na Kemikali

$
0
0
Kifaa cha Kurefusha uume Kinachouzwa 160,000


Pendeza na Dr Kessy Products 
Ni dawa za Asili zisizo na Kemikali wala madhara yoyote kwa Binadamu, zimetengenezwa kwa kutumia mimea na matunda mbali mbali kukupa matokeo ya Haraka

1.Refusha Nywele na zisikatike  45,000/
2.Ondoa Mvi Sugu kichwani  45,000/
3.Toa Michirizi Mapajani, Chunusi na Madoa mwilini 40,000/
4.Punguza tumbo na Manyama uzembe 45,000/
5.Mkanda wa Kufunga Kupunguza tumbo 70,000/
6.Tengeneza Shepu Hips na Makalio  45,000/ ,Vidonge 80,000/
7.Ongeza Nguvu za Kiume  Jelly 45,000/ , Vidonge 60,000/
8.Ongeza Ukubwa wa Maumbile ya kiume Jelly 80,000/ , Mashine 160,000/
9.Kuongeza Mwili Mzima 40,000/
10.Kupunguza Mwili 45,000/
11.Kupunguza Maziwa na Kuyasimamisha 40,000/
12.Ongeza Mguu uwe wa Kupendeza 45,000/
13.Rudisha usichana ama Bikira 55,000/
14.Ongeza Hamu ya Kula 40,000/
15.Ongeza Hamu ya Kufanya Mapenzi 55,000/
16. Fanya mwili Kuwa Soft 60,000/

TUNAPATIKANA DAR NA MIKOA YOTE, HUDUMA ZINAFIKA POPOTE ULIPO , 
DAR TUPO KARIAKOO MSIMBAZI NA POSTA  MPYA

PIGA SIMU: 0719955528, 0756259180 au 0785371237

Diamond Platnumz Amnunualia Zawadi ya Ndege (Private Jet ) Mpenzi Wake Zari ..Kuzinduliwa kesho

$
0
0
Habari ya Mjini ndo Hiyo leo , Baada ya Kuhamia Kwenye Bonge la Nyumba yake huko Mitaa ya Tegeta , Diamond Amemnunulia Mpenzi wake Zari zawadi ya Ndege kama shukrani kwa Kukubali kuzaa naye......
Kumbuka leo ni Tarehe 1 mwezi wa nne...Siku ya .........

Maaskofu Wamjibu Rais Kikwete.....Watoa Tamko Zito Kuhusu Mahakama ya Kadhi......Wasisitiza Kuwa Wakristo Wote Wapige Kura ya HAPANA Katiba Inayopendekezwa

$
0
0
Siku tano baada ya Rais Jakaya Kikwete kusema kuwa tamko la Jukwaa la Wakristo (TCF) kuwataka waumini wao kupigia kura ya ‘hapana’ Katiba Inayopendekezwa lilikuwa la hasira, viongozi hao wamejitokeza tena na kusisitiza kwamba msimamo wao huo utabaki kama ulivyo.

Katika tamko pamoja walilolitoa jana baada ya kukutana juzi mjini Dodoma, viongozi hao wamemtahadharisha Rais Kikwete kuwa kuendelea kupigia debe Katiba Inayopendekezwa na kuruhusu Mahakama ya Kadhi, kunaweza kulitumbukiza Taifa katika machafuko na hali ikiwa hivyo Serikali ndiyo itakayolaumiwa.

Tamko hilo limesainiwa na viongozi walewale waliosaini lile la awali la Machi 12, mwaka huu ambao ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), Askofu Dk Alex Malasusa, Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC), Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa na Mwenyekiti wa Kanisa la Pentekoste Tanzania (CPCT), Askofu Daniel Awet.

Tamko  lao  hili  hapa:

Sisi, Maaskofu kutoka TEC, CCT na CPCT tumekutana leo tarehe Machi 30, 2015 hapa Dodoma ili kuomba kwa pamoja juu ya mgawanyiko unaodhihirika wa dini za Kikristo na Kiislamu kutokana na muswada wa Mahakama ya Kadhi.

Maaskofu tuliokutana hapa hatuna hasira na wala hatuongozwi na hasira wala mihemko katika kufikia maamuzi tunayofanya kama ambavyo wengine wanavyotutafsiri.

Tunafikia maamuzi yetu baada ya maombi na sala na tunasukumwa na upendo kwa wananchi ili kujenga taifa lenye umoja, amani, utulivu na maelewano.

Pia tumekuja kufuatilia kwa kina Muswada wa Marekebisho ya Sheria Mbalimbali ya 2014 unaopendekeza, pamoja na mambo mengine, marekebisho ya Sheria ya Tamko la Sheria za Kiislamu la mwaka 1964.

Muswada huu unapendekeza kuanzishwa Mahakama ya Kadhi  ambao utawasilishwa Bungeni April 01, 2015 kwa hati ya dharura na hivyo kuufanya umma wa Watanzania kutokujua maudhui yaliyomo katika muswada huo wakati bado hoja zetu za msingi tulizopeleka kwenye Kamati ya Katiba na Sheria ya Bunge na kwa Waziri Mkuu hazijajibiwa.

Tangu tulipokutana Machi 10, 2015 ambako tulitoa tamko letu kuhusiana na Mahakama ya Kadhi na Katiba Inayopendekezwa, tumekuwa tukiendelea kutafakari juu ya yale tuliyokuwa tumesema katika matamko yetu mbalimbali na jinsi amani na utulivu wa nchi yetu vinavyoendelea kumomonyoka siku zinavyokwenda.

Kwanza tumeshangazwa na tabia ya viongozi wa serikali ya kuitisha na kuendesha mikutano wanayodai ni ya viongozi wa dini lakini isiyo rasmi. Machi 03, 2015 Waziri Mkuu aliitisha mkutano kupitia Mchungaji mmoja ambapo hakuna hata kiongozi mmoja wa taasisi au Kanisa aliyeshiriki.

Jambo la kushangaza ni kile kilichotokea Machi 28, 2015 ambapo Mhe. Rais alishiriki kikao cha kikundi ambacho sio rasmi yaani Kamati ya Amani ya Mkoa wa Dar es Salaam.

Tunasema kamati hiyo siyo rasmi kwa sababu haina baraka za viongozi wa ngazi za juu wa kidini wa Mkoa huo na haina mwongozo wa kazi zake.

Mikutano ya jinsi hii kati ya serikali na wale ambao imewaona kuwa ndio viongozi wa dini sio sahihi kwani viongozi wa dini wana taratibu zao za kualikwa au kuwakilishwa katika mikutano na viongozi wa serikali au wa dini au madhehebu mengine.

Tunawashauri wanaohutubia na wanaoshiriki mikutano hii wajue kwamba washiriki hawana uwezo wa kuamua au kukubaliana na jambo lolote kwa niaba ya viongozi wao wa juu na pia viongozi husika wa serikali wasifurahi kwamba ujumbe wao umewafikia viongozi wa dini kwani hao washiriki sio wawakilishi rasmi na hawana uwezo wa kutoa maamuzi au kukubaliana juu ya jambo fulani la kitaifa.

Pili, tumekuwa tukifuatilia kwa karibu juu ya muswada wa Mahakama ya Kadhi na tumebainisha dhahiri kwamba kile tulichokuwa tunasema kitatokea kimeaanza kutokea bayana.

Yale yaliyotokea kwenye semina kuhusu Mahakama ya Kadhi kwa Waheshimiwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Machi 29, 2015 ambao ni wasomi, ni ishara ndogo sana ya kile kitakachotokea maeneo yote ya nchi yetu. SERIKALI KWA NIA MOJA NA KWA SABABU TUSIZOZIJUA INAANZISHA VITA VYA KIDINI KATI YA WATANZANIA WAKRISTO NA WAISLAMU.

Tunashangazwa kuona jinsi serikali inavyonuia jambo hili ovu litakaloleta balaa kwa nchi yetu wakati huu wa kuelekea kura ya Maoni ya Katiba Inayopendekezwa na baadaye Uchaguzi Mkuu wa 2015.

Kutokana na mambo hayo makuu mawili hapo juu, sisi Maaskofu wa Jukwaa la Wakristo Tanzania tunatamka kama ifuatavyo :

1.Matamshi ya Mhe. Rais akihutubia aliyowaita viongozi wa dini tarehe Machi 28, 2015 kuwa Mahakama ya Kadhi ni ya Waislamu wenyewe na serikali haitajihusisha wala kugharamia yanakinzana na kile kinachoendelea bungeni na nchini.

Hapa tunajiuliza, endapo maneno ya Rais ni kweli, mbona Bunge linaendelea kujadili kitu ambacho serikali haitajihusisha wala kukigharimia ? Kwa mantiki hiyo, tunamtaka Mhe. Rais aagize muswada huu uondolewe Bungeni na usijadiliwe tena kwa kuwa Utafiti wa Tume ya kurekebisha sheria ulishaonyesha madhara ya uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi.

 Vinginevyo, kuendelea kujadiliwa kwa muswada huu maana yake ni kwamba serikali inajihusisha na itagharimia mahakama hiyo.

2.Serikali ijue kuwa endapo Wabunge wa dini za Kikristo na Kiislamu watapigana na kisha baadaye wananchi nao wakafanya hivyo katika maeneo yao, SERIKALI ITAKUWA NDIYO CHANZO CHA MAPIGANO HAYO.

Kama tulivyotamka hapo juu, kuhusiana na jambo hili tunamtaka Mhe. Rais aiepushe nchi yetu na kuingizwa kwenye mapigano ya kidini ambayo kuyadhibiti itakuwa vigumu sana (tafadhali rejea kinachoendelea huko Nigeria).

Pia tunamwomba Mhe. Rais akumbuke na kutafakari kile kilichotokea na kinachotokea nchi ya Afrika ya Kati kati ya kundi la Seleka (Waislam) na kundi la Anti Balaka (Wakristo).

3.Tunaamini kuwa viongozi wa serikali wanafahamu viongozi rasmi wa dini na madhehebu ya dini. Kwa mantiki hiyo tunawashauri viongozi wa serikali waache kabisa kutumia vikundi visivyo rasmi kualika mikutano wanayodhani kuwa itakubalika na waumini wa dini hizo. Mikutano yote ya jinsi hiyo itakayoitishwa ni batili na maamuzi yake hatuyatambui na hatutayatambua.

4.Bado Maaskofu tunasimamia Tamko letu la Machi 10, 2015 na tunawahimiza Wakristo wajitokeze kwa wingi katika kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la wapiga Kura na zaidi wajitokeze kwenda kupiga kura ya HAPANA wakati wa kura ya maoni kwani Katiba inayopendekezwa ilifikia hapo kwa njia ya ubabe, ilikosa uadilifu na mbaya zaidi ni RUSHWA YA AHADI YA MAHAKAMA YA KADHI ya iliyotolewa na Waziri Mkuu kwa Waislamu wakati wa kupitisha Katiba Inayopendekezwa.

Tunafanya hivyo kwa dhamiri safi kwa sababu ya imani yetu na kwamba sisi ni raia wa nchi hii na tuna haki ya kueleza mawazo yetu bila woga kama Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977 inavyotupa haki.

5.Mwisho tunawaomba Wakristo wote waendelee kufunga na kuomba kwa ajili ya utulivu na amani ya nchi yetu.

Breaking News: Vurugu Zaibuka Bungeni.......Wapinzani Wamtuhumu Spika Kuilinda Serikali, Bunge Laahirishwa hadi Mchana. Video Ya Tukio Hilo Iko Hapa.

$
0
0

Kikao cha  Bunge kimevunjika muda mfupi uliopita baada ya kutokea vurugu za maneno kufuatia wapinzani kutaka Waziri Mkuu atoe taarifa juu ya mwenendo wa kura ya maoni ya katiba mpya april 30,2015.

Kutokana na vurugu hizo za dakika kama 10 hivi Spika Anna Makinda amesitisha gafla shughuli za bunge hadi mchana.

Hali likuwa hivi:

Mnyika: Nimesimama kupata idhini kwa mujibu wa kanuni ili shughuli za bunge zisitishwe badala yake tujadili zoezi la uandikishaji nchi nzima.

Mpaka sasa zoezi halijakamilika hata kwa mkoa mmoja tu wa Njombe, jambo hili ni la dharura na lilishatolewa na ukaagiza kamati ishughulikie.Tunaomba majibu tupate kikao hiki na leo tunafunga mkutano.

Spika Makinda: Hoja hii inafanana na ile ya kwanza(  Hoja  ya  mbunge wa Kisarawe Seleman Jafo ambaye  alipendekeza kura ya maoni ya katiba  inayopendekezwa isogezwe mbele  na  badala  yake  kuwe  na  katiba  ya  mpito  kuelekea  uchaguzi  mkuu)

Baada  ya  kauli  hiyo, Mnyika  na  wabunge  wa  upinzani  walianza  kupiga  kelele  bungeni  wakidai  kuonewa  huku  wakimtuhumu  Spika  makinda  kuibeba  serikali.

Hata hivyo, Spika  hakuonesha  kutishwa  na  kelele  hizo  na  badala  yake  alimtaka  katibu  wa  Bunge  atoe  mwongozo  wa  kile  kinachofuata.

Katibu  alisimama  na  kuanza  kusoma  miswada  ya  habari ambapo  wapinzani  nao  walisimama  na  kuzidisha  kelele  huku  wakisema:"Tunataka majibu..Tunataka majibu. Tumechoka kuburuzwa..Makinda kwanini unailinda Serikali.??!!!

Hali  hiyo  ikamlazima  Spika  Makinda  Kuliahirisha  Bunge  hadi  mchana.

Tazama  Video  hapo  chini. 

Masogange shows her Massive Asset....Only Men to comment..

$
0
0




Masogange shows her Massive Asset....Only Men to comment..

Bishop Piusi Erasto Ikongo Alikosoa Vikali Jukwaa la Wakristo, Asema Katiba Pendekezwa ni Nzuri Sana

$
0
0
Askofu piusi erasto amefanya press conference leo habari maelezo akitoa msimamo wake kutofautiana na maaskofu kuhusu katiba Katiba ni nzuri anatoa uhuru wa kuabudu maaskofu katiba hii inaruhusu sisi kuhubiri injiri 

Kwa mjiby wa Ibarra ya 41(1) katiba hii inaturusu maaskofu kuhubiri injiri bila kikwazo 
Nasikitika wanaingilia waumini mambo ya ukomo wa ubunge madaraka ya uraisi hayatuhusu sisi. ....

Unakuta askofu mzima anaipinga katiba eti ni mbaya kisa haina ukomo wa wabunge ukimuuliza wewe askofu ukomo wako wa madaraka ya uaskofu ni lini atakuambia yeye ni askofu wa kudumu. ...kwa nini anaingilia ukomo wa nafasi za wengine wakati nafasi yake haina ukomo. ... maandiko yanesema usitoe kibanzi kwenye jicho la mwenzio wakati jicho lako lina borit....

Kuhusu madaraka ya raisi,mambo ya wakulima muundo wa muungano Askofu ikongo anasema waachiwe waumini ambao ni ukawa ni ccm na wasio na chama
Sisi maaskofu tubebe neno la MUNGU katiba hii ni nzuri saana kwa sababu imeBEBA uhuru wa kutangaza dini jambo ambalo maaskofu tulipasa tulipongeze na kuinadi katiba. ..
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images