Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live

Taarifa ya Jeshi la Polisi Nchini Kufuatia Upotoshwaji Unaoenezwa Kwa Njia ya Mtandao ili Kuwatia Watu Hofu

0
0
Katika siku za hivi karibuni kumeibuka tabia ya baadhi ya watu wachache wasiofahamika kutunga na kusambaza ujumbe kupitia simu za mikononi na mitandao mbalimbali ya kijamii wenye lengo la kuwatia hofu wananchi, jambo ambalo ni kinyume cha sheria.
 
Aidha, watu hao wanaosambaza taarifa hizo wanajifanya kwamba taarifa hizo zimetoka kwenye taasisi za kimataifa na taasisi zingine zinazoaminika jambo ambalo siyo kweli.

Jeshi la Polisi nchini linawataka wote wenye tabia hiyo kuacha mara moja na badala yake, endapo mtu yeyote anayo taarifa ya uhalifu wa aina yoyote ama kikundi chochote cha uhalifu atoe taarifa hiyo katika kituo chochote cha Polisi au kupitia simu za makamanda wa polisi wa mikoa ama vyombo vingine vya ulinzi na usalama ili taarifa hizo ziweze kufanyiwa kazi haraka.

Aidha, Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wa taarifa zote zinazopokelewa ili kuhakikisha kwamba usalama wa raia na mali zao unaendelea kuimarika.
 
 Hata hivyo, Jeshi la Polisi halitasita kumchukulia hatua mtu yeyote atakayebainika kusambaza ujumbe wenye mlengo wa upotoshaji, uchochezi ama kuwatia hofu wananchi.

Imetolewa na:-
Advera Bulimba -SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.

Jokate Stunning New Hot Look...See Photos

0
0

These are the new photos of Jokate that have captured the eyes of many today. cHECK Out more pics

The Painful Text a Kenyan Girl (Janet Akinyi) Wrote Her Boyfriend Before Her Death at Garissa University

0
0
The survival stories from Garissa University College are horrifying. One girl hid in a wardrobe for more than 48 hours, drinking lotion to remain alive.

Not even KDFs assurances that the terrorists were defeated could make her get out, and it took the intervention of her lecturer. We’ve also heard of students who jumped over fences getting deep cuts in the process.

However, the sad stories are also many. One male student has not been found since returning to rescue his girlfriend. He had already escaped to safety but he returned inside to help the love of his life.

Another girl, Janet Akinyi (picture above), wrote this painful SMS to her boyfriend a few minutes before she met her demise.

This is extremely sad.



Auawa na Wananchi kwa Kupeleka Waganga Kijijini Kilimanjaro Kwa Ajili ya Kusindika Nyumba yake na Kupiga Ramli

0
0
MZEE mwenye umri wa miaka 68, Celestine Mushi, mkazi wa kata ya Motamburu wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro, ameuawa na wananchi wanaotajwa kukasirishwa na kitendo chake cha kupeleka waganga wa jadi kijijini kwa lengo la kuifanyia zindiko nyumba yake.

Mushi anadaiwa kuwatoa waganga hao wawili jijini Dar es Salaam na kuwapeleka Rombo kwa kazi hiyo maalumu.

Tukio hilo limethibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Godfrey Kamwela aliyesema mauaji hayo yalitokea juzi saa 2.30 usiku nyumbani kwa Mushi katika kitongoji cha Mbomai Juu, wakati waganga hao wakiendelea na zindiko lao.

Kamwela aliwataja wanaodhaniwa ni waganga wa jadi kuwa ni Ashraf Mjengwa (22) na Peter Mmaka (25), wote wakazi wa Magomeni, Dar es Salaam.

Alisema waganga hao walifika nyumbani kwa Mushi juzi saa 10 jioni, na ilipofika saa 11 walianza shughuli ya zindiko na walipomaliza, Mushi alitaka kuwapeleka katika nyumba ya mkwe wake aitwaye Priscila Hilment, ili nayo ifanyiwe zindiko.

Kamwela alisema kitendo hicho kilikataliwa na mama mkwe, ambaye alipiga kelele kuomba msaada kwa wananchi ili wawaondoe waganga hao, ambapo wananchi walifika na kuwashambulia waganga hao.

Alisema kutokana na tafrani hiyo, raia mmoja alitoa taarifa katika kituo cha polisi, ambapo polisi walifika eneo la tukio na kufanikiwa kumwokoa mganga mmoja, Mjengwa, ambapo mwenzake alikimbia na kutokomea kusikojulikana.

Kamwela alisema ilipofika saa 2 usiku, kundi la wananchi wasiojulikana idadi yake walirudi nyumbani kwa mzee huyo na kuanza kumpiga kwa fimbo kichwani na sehemu mbalimbali za mwili wake, na kisha kuondoka na kumwacha akivuja damu nyingi.

Alisema kutokana na damu kuendelea kuvuja, mtoto wa mzee huyo alimchukua baba yake na kumpeleka katika kituo cha afya cha Tarakea, ambapo alifariki dunia kabla ya kupatiwa matibabu na Jeshi la Polisi limeanza msako wa kuwatafuta wahusika.

Mwanajeshi ajinyonga Wakati hayo yakitokea mkoani Kilimanjaro, Grace Chilongola anaripoti kutoka Mwanza kuwa, fundi wa magari wa Kikosi cha Jeshi la Ulinzi la Wananchi namba 512 MTC Nyegezi, jijini Mwanza, Jacob Mponeja (55) amekutwa amejinyonga chumbani kwake kwa kutumia kamba ya katani huku akiacha ujumbe.

Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza, Joseph Lusungu tukio hilo lilitokea Aprili mosi mwaka huu majira ya saa moja asubuhi.

Alisema ujumbe huo ulioandikwa kwenye kitabu kidogo kilichokutwa kwenye eneo la tukio ulisomeka; “Kifo changu kimetokana na mke wangu kujihusisha na vitendo vya kishirikina, hali iliyosababisha kutaka kuuawa mara mbili na mtu asilaumiwe kwa kifo changu.”

Alisema kwa mujibu wa mtoto wa marehemu, ambaye ni mwanafunzi katika sekondari ya Nyabulogoya, kabla ya tukio la kujinyonga, baba na mama yake Happy Mabula (45), walikuwa na ugomvi mkubwa.

Kaimu Kamanda huyo alisema katika ugomvi huo mama huyo alikatwa shoka na mumewe na kwamba alikimbizwa katika hospitali ya Rufaa ya Bugando kwa matibabu na kwamba hali yake sio nzuri.

Alisema katika eneo la tukio kulikutwa shoka lililokuwa na damu pamoja na kitabu hicho kidogo kilichokuwa na ujumbe ulioandikwa na marehemu.

A to Z ya Mgomo wa Madereva Jana, Ulivyoanza, Vurugu na Mabomu na Mpaka Serekali Kusalimu Amri na Kukubaliana na Madereva

0
0
MGOMO wa madereva wa mabasi ya mikoani na baadhi ya mabasi ya usafiri Dar es Salaam maarufu daladala uliofanyika jana, uliambatana na vurugu katika maeneo mbalimbali ya jiji hilo na kulazimisha askari Polisi kutumia mabomu ya machozi kurejesha hali ya amani.

Awali abiria wanaokwenda mikoa mbalimbali walianza kuwasili katika Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo tangu alfajiri, tayari kwa safari zikiwemo zinazoanza alfajiri hiyo, lakini walikuta mabasi hayo yakiwa yameegeshwa bila kuwa na dalili za safari.

Ilipofika kwenye saa mbili za asubuhi, abiria waliokuwa wameongezeka katika kituo hicho na baadhi ya watu waliosadikiwa kuwa wapigadebe, walianza kufanya vurugu kuzuia magari binafsi yaliyokuwa yakipita katika barabara hiyo.

Watu hao walikuwa wametanda katika Barabara ya Morogoro, huku wengine wakirusha mawe wakizuia magari kupita katika barabara hiyo.

Katika barabara hiyo, matairi yalichomwa na vijana hao waliokuwa wakifanya vurugu katikati ya barabara, wakizuia magari ya watu binafsi pamoja na yale ya Polisi yaliyokuwa na askari.

Mbagala

Vurugu za namna hiyo zilitokea pia katika eneo la kituo cha mabasi cha Mbagala Rangitatu, ambako makundi ya vijana walikusanyika na kuzuia magari kuingia na kutoka kituoni hapo.

Mabomu ya machozi Kuibuka kwa vurugu hizo, kulisababisha askari walikuwa na mabomu ya machozi, kuyatumia kwa kurusha angani ili kusambaza watu. Katika eneo la Ubungo, abiria waliamua kukimbia huku na kule kunusuru maisha yao kabla ya kurejea kwa hali ya utulivu.

Katika eneo la Mbagala, ufyatuaji wa mabomu ya machozi ulisaidia kurejesha hali ya utulivu kwa muda ingawa baadae fujo zilianza tena na kusababisha polisi nao kuendelea kurusha mabomu hayo mpaka hali ilivyotulia.

Abiria Katika kituo cha Ubungo, wakati vurugu zikiendelea, abiria pamoja na madereva walikuwa wametulia ndani ya mabasi kusubiri hatma ya safari zao huku wengine wakiwa wamekaa pembeni mwa mabasi yao.

Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti baadhi ya abiria waliokuwa katika eneo hilo, akiwemo Abdala Ally ambaye alikuwa katika basi la Tahmeed akisubiri kwenda Tanga, alisema mpaka wakati huo saa tano asubuhi, alikuwa hajui nini hatma yake kwa sababu hakuna tarifa yoyote aliyokuwa amepewa na uongozi wa basi alilopanda.

Abiria mwingine Mwaimu Kijangwa, alisema hali hiyo inatisha kwani tangu asubuhi walikuwa wakishuhudia vurugu na milio ya mabomu ikiendelea.

Alisema walioko kwenye vurugu nje ni vibaka ambao hawaangalii watoto, wagonjwa wala walemavu na kwamba kwa asilimia kubwa hawana uhusiano wowote na mgomo huo, bali maslahi yao binafsi.

Kijangwa alitetea hatua ya Polisi kupiga mabomu na kusema wanachofanya askari kutumia mabomu ya machozi ni sahihi, ili kutuliza vurugu hizo ambazo zitasababisha maafa zaidi.

Madai ya madereva

Akizungumza na gazeti hili, Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Daladala jijini Dar es Salaam (DARCOBOA), alisema wako ambao hawakuwa na mpango wa kugoma, lakini walipotoa mabasi asubuhi walipigwa mawe wakaogopa kujeruhiwa na kuharibu magari, wakarudisha ndani kwa ajili ya usalama.

Katika kikao kilichofanyika kati ya Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudentia Kabaka na madereva hao Ubungo, walilalamikia masharti ya kutakiwa kusoma kila wanaposajili leseni zao za udereva, huku wakitakiwa kulipa ada ya Sh 560,000.

Madereva hao walidai kuwa hawapingi kupata elimu, lakini walihoji wakati wa kusoma nani atalinda ajira yao na wataishi vipi wakati wanategemea kipato kutokana na kazi yao.

Madai mengine, ni kuhusu ada kubwa ya Sh 560,000, ambayo waliitaka Serikali kuwalazimisha wamiliki kulipa ada hiyo. Mengine ni kufanya kazi bila mikataba inayoeleweka, kutolipwa mishahara na wengine kulipwa kwa utaratibu kwa huduma za simu na hivyo kuikosesha Serikali mapato na sheria isiyoeleweka ya muda wa safari.

Waziri

Akizungumza na madereva hao jana katika Kituo cha Mabasi cha Ubungo, Waziri Kabaka alisema Serikali haina nia ya kuwaumiza madereva wala abiria na hivyo imepokea kwa madai yao na kuahidi kuyafanyia kazi.

Waziri huyo na viongozi wengine walifika hapo saa 6.24 na kuanza kuzungumza na madereva ambao awali walimkataa Kamanda wa Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova wakidai hawataki kuzungumza nae.

Waziri Kabaka akianza kujibu madai madereva hao, alisema ipo haja ya kutafuta utatuzi wa kudumu wa changamoto zinazowakabili madereva na kwa kuanzia Aprili 18 mwaka huu, uongozi wa madereva hao utakutana na viongozi wa Serikali kujadili mustakabali wa madereva.

“Tumekubaliana kwa maslahi yenu tuwe na kikao kikuu Aprili 18 mwaka huu siku ya Jumamosi ofisini kwangu ili tupate madai yote kwa maandishi, mimi nitasimamia hilo,” alisema Waziri Kabaka.

Waziri Kabaka aliwaomba madereva hao kama wanamuamini, waendelee na kazi wakiamini matatizo yao yatatatuliwa siku ya Jumamosi, lakini wakadai majibu yote wanataka yapatikane hapo hapo kabla hawajaendelea na safari.

“Jana nimeongea na viongozi wenu, nilichogundua ni kwamba mikataba haiko kwa madereva walio barabarani, bali kwa watu wachache tu kwa ajili ya kuonesha kwa maofisa kazi, ili wapate leseni, kwa hiyo madereva hata mkiumia kazini hampati haki yoyote kwa sababu hamna mikataba,” alisema Kabaka na kuahidi kulisimamia suala la mikataba kwa uwezo wake wote.

Alisema katika kutatua tatizo hilo kwa muda mfupi, kuanzia sasa wamiliki wa magari ni lazima waende na madereva katika ofisi za Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kazi na Majini (SUMATRA) pamoja na picha zao ili kuhakikisha mkataba anapewa dereva mwenyewe.

Aidha Kabaka alisema Wizara ya Kazi na Ajira imeanzisha mfuko kwa watumishi wanaoumia kazini, ambao ni lazima waajiri wawalipie wafanyakazi wao ili wanufaike na mfuko huo.

Katika hoja ya kutakiwa kurudi kusoma Chuo cha Usafirishaji (NIT), Kabaka alisema kusoma madereva hawapaswi kutoa fedha zao mfukoni, ndiyo maana inaandaliwa mikataba ili mwajiri atambue majukumu yake.

Kabaka alisema atarejesha utaratibu wa zamani wa madereva wanapotaka kusajili upya leseni zao, hakutakuwa na suala la kurudi darasani na kulipa ada ya Sh 580,000, kama ilivyo sasa na inavyolalamikiwa na madereva jambo ambalo lilipokewa kwa shangwe na madereva.

Safari zarejea

Baada ya maelezo hayo, Mwenyekiti wa Umoja wa Vyama vya Madereva (TTDA), Clement Masanja, aliwatangazia madereva kuendelea na safari zao kwamba Serikali imeahidi kutatua changamoto zao.

“Serikali imepokea matatizo yetu shule imefutwa, tochi barabarani hakuna, na vituo vya ukaguzi tutatumia vya mizani tu, posho na mishahara kitaeleweka Aprili 18 mwaka huu na majibu yasipoeleweka tutaweka ‘segere’ jingine,” alisema.

Mkuu wa Mkoa Said Mecky Sadiki alitoa pole kwa madereva na abiria kwa usumbufu uliojitokeza jana.

Baada ya hapo, mgomo huo ulisitishwa na safari zikaanza saa 7.40 mchana baada ya Serikali kukubali kutatua matatizo yao waliyokuwa wakilalamikia, ikiwa ni pamoja na kuondoa dai lao la kurudishwa shule na kuwaachia huru madereva wote waliokuwa wamekamatwa.

Morogoro

Polisi mkoani Morogoro imewakamata watu saba kutokana na sakata mgomo wa madereva wa mabasi na daladala kwa tuhuma za kuwafanyia vurugu madereva wachache waliokuwa wameamua kuendelea kutoa huduma ya usafiri kwa wananchi.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Leonard Paulo, alisema hayo jana, mbele ya waandishi wa habari mara baada ya kikao cha wadau wa sekta ya usafirishaji mkoani Morogoro.

Kwa mujibu wa Kamanda huyo, aliwataja watuhumiwa waliotiwa mbaroni ni madereva wa bodaboda, daladala, makondakta wa daladala na wauza maji ambao waliamua kuwafanyia vurugu madereva wenzao waliokuwa wakipakia abiria maeneo mbalimbali ya mji wa Morogoro.

Hata hivyo aliwataja waliokamatwa kuhusiana na kufanya vurugu hizo ni Momolege Lucas (24), Mohamed Shaaban (22), Hatibu Onesmo (23), Nelson George (34), Jumanne Juma (30) Victor Costa (24) na Bakari Mohamed (19) wote wakazi wa manispaa ya Morogoro.

Hata hivyo alisema, tayari watuhumiwa hao wameshafikishwa mahakamani kwa makosa ya kuwafanyia vurugu madereva wenzao na kitendo hicho ni cha uvunjifu wa amani na ni kosa la jinai.

Mgomo huo ambao kwa madereva wa mabasi ya mikoani haukuwa na nguvu ulianza alfajiri ambapo mabasi yaliegeshwa kituoni hapo bila ya kuwa na madereva hata hivyo ilipofika saa tatu asubuhi baadhi ya mabasi yalianza kusafirisha abiria na shughuli za ukataji tiketi uliendelea kama kawaida.

Hata hivyo licha ya madereva wa daladala kuendelea na mgomo mpaka saa 9 alasiri , madereva wa pikipiki, bajaji na gari ndogo aina ya Noah walichukua nafasi za daladala kusafirisha abiria kwa kutumia vyombo hivyo vya usafiri kwa kwenda kwenye shughuli zao za kila siku.

Kwa upande wa baadhi ya madereva waliozungumza na mwandishi wa habari hii jana akiwemo wa basi la kampuni ya Stamili linalofanya safari zake Morogoro- Arusha, Lucas Chonya alisema, mgomo huo umekuja baada ya Serikali kutoa agizo la kuwataka madereva kwenda kusomo kwenye vyuo vya udereva kila baada ya miaka mitatu wanapobadilisha leseni zao.

Hata hivyo alisema, kwa madereva ni vigumu kutekeleza agizo ama utaratibu huo kwani licha ya kusababisha usumbufu , pia kwa madereva wengi hawataweza kumudu gharama za ada kwenye vyuo hivyo vya udereva.

Naye Dereva wa basi la kampuni ya Hood, Daru Dagila alisema, utaratibu wa madereva kwenda kusoma kila baada ya miaka mitatu hauwezi kupunguza ajali za barabarani. Hivyo aliwataka wadau wa sekta ya usafirishaji ambao ni kikosi cha usalama barabarani, Sumatra, Tanroads, Taboa wanapaswa kuwashirikisha madereva katika mikutano mbalimbali ili kujua chanzo halisi cha ajali.

Naye mmoja wa abiria aliyekuwa akisafiri kutoka Moro kwenda Dar , Joyce Muro aliiomba Serikali na wadau wa sekta ya usafirishaji kukaa meza moja na kuzungumza changamoto zao ikiwemo ya ajali za mara kwa mara badala ya kukurupuka kutoa kauli na maagizo ambayo yamekuwa yakisababisha migomo.

Dodoma

Usafiri wa ndani wa mkoani Dodoma uliendelea kama kawaida ingawa mabasi yanayotoka mkoani kupitia mjini Dodoma hayakuingia katika muda unaotakiwa.

Pamoja na hali ya usafiri kuwa shwari Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Usafirishaji wa Njia ya Barabarani (TAROTWU) mkoani Dodoma Lawrence Mwashinga amesema hawautambui mgomo na kwamba wao wanaendelea kusafirisha abiria kama kawaida . Akizungumza kuhusu mgomo wa madereva wa Mabasi yaendayo alisema mkoani hapa Mabasi yote yametoka.

‘’Mabasi zaidi ya 20 yanayofanya safari zake toka Dodoma hadi Dar, Mwanza, Mbeya,Iringa, Tabora, Arusha pamoja na wilayani yametoka kama kawaida’’.

Kwa upande wake Katibu wa chama hicho, Musa Nsese aliitaka Serikali na Wahusika kukaa pamoja na kujadiliana badala ya kufanya maamuzi yanayowaumiza na kuwatia hasara abiria wanaosafiri kuelekea mikoa mbalimbali.

‘’Suluhisho la mgomo ni kuwatafuta Wadau na kukaa meza moja ili kujadiliana na kupata suluhisho kwani wanaoumia ni abiria’’ alisema katibu huyo huku akisisitiza kwamba Mikataba kati ya Waajiri na Waajiriwa inatakiwa iangaliwe kwani wanaoajiriwa wamekuwa wakilalamika kuwa wanyonywa.

Naye Dereva wa basi la Champion linalofanya safari kutoka Dodoma kuelekea Dar, Steven Mauye alisema alikiri kuwa mgomo upo ila huku mkoani hauna nguvu ndio maana mpaka sasa hakuna basi lililotoka Dar es salaam.

Uchunguzi uliofanywa na Mwandishi wetu umeonesha kwamba ingawa kulikuwa na mabasi yametoka dodoma kwenda dar, hapakuwepo na mabasi kutoka mikoa ya Singida, mwanza, Kigoma yaliyokuwa yakipita Dodoma na kufanya barabara kuwa tupu kwa kukosa pilikapilika za magari ya kutoka mikoani.

Katika stendi ya Sabasaba usafiri ulikuwapo kama kawaida hukuw enye Noah na Hiace wakisema hawahusiki na mgomo huo.

Na katika stendi ya mji mdogo wa Kibaigwa wasafiri walilazimika kupanda Noah kwenda Dodoma kutokana na kutokuwapo na magari makubwa ya abiria kutoka Dar ambayo hupita mjini hapo kuelekea mjini Dodoma

Lulu Awaogopa Wachawi Kumtaja Aliye Mtundika Ujauzito Wake

0
0
MWIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amefunguka kuwa anaogopa wachawi kumtaja mhusika wa mimba aliyonayo.

Lulu alifunguka hayo juzikati wakati mwanahabari wetu alipotaka kujua mhusika wa mzigo alionao ndipo msanii huyo aliposema aachwe kwanza maana wachawi ni wengi.“Mh! Naomba mniache kwanza maana mjini hapa wachawi ni wengi, mambo yakiwa freshi kila mmoja atamjua,” alisema Lulu.   

Ali Kiba, Diamond Katika Vita Mpya ...Ali Kiba Aapa Kuwamaliza Mademu Wote wa Diamond..Ameanza na Jokate

0
0
Gazeti la Kiu Limepenyezewa Ubuyu kuwa Ali Kiba amebuni Vita Mpya Kwa Diamond Kwa kuwafyeka mademu wote walio wahi kuwa na uhusiano na Diamond..

Taarifa toka vyanzo vya ndani vinaeleza tayari Ali Kiba Ameshaanza mashambulizi kwa Jokate ..na tukio la hivi karibuni Uwanja wa Dar Live ambapo Ali Kiba Alisindikizwa na Mrembo Jokate limezidi kutia uzito Jambo hilo ambapo zimeanza kujadiliwa mitandaoni Hasa Instagram..

Mbali na Mtoko wa Hao wawili Dar live kwenye Instagram kuna akauti yenye jina la "Jokiba" ikisapoti Mapenzi ya Hao wawili ..Mtu wa Karibu wa Ali Kiba Alipohojiwa Alisema kuwa ni kweli hawa watu wapo karibu sana ila hana uhakika kama Wameanza Mchezo wa Baba na Mama...

Aidhaa kunaTaarifa nyingine kuwa Wema Sepetu ambaye naye alishakuwa ex wa Diamond siku hizi za karibuni amejaribu kujenga uhusiano wa karibu na Ali Kiba katika kile kinachoelezwa kuwa ni Kutafuta namna ya kulipiza kisasi kwa Diamond..

Mchungaji Mbaroni kwa Kumchinja Mwanaye Adai "Nilioteshwa na Mungu, Mkuu wa majeshi Nimtoe Sadaka"

0
0
DUNIA ina mambo! Mchungaji wa kanisa moja mjini Harare nchini Zimbabwe, ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja, amekamatwa na polisi baada ya kukutwa akitaka kumuua mwanaye wa kumzaa kwa kumchinja na kisu shingoni, kitendo alichokifanya nyumbani kwake mwishoni mwa wiki iliyopita.

Mchungaji huyo ambaye hata hivyo hakueleweka ni wa kanisa gani, akiwa amevaa nguo zake za kichungaji, kanzu nyeupe yenye msalaba kifuani, alimchukua mwanaye huyo wa kiume na kuanza kumchinja ndani ya nyumba yake, kabla ya kijana huyo anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka kumi, kupiga kelele za kuomba msaada.

Kwa mujibu wa mitandao, baada ya majirani kuingia ndani ya nyumba hiyo, walimkuta mchungaji huyo akiwa na kisu mkononi, ameloa damu huku kijana wake akiwa ameanguka chini akiugulia kwa maumivu makali.

Baada ya kuhojiwa sababu za kutaka kutoa roho ya mwanaye, mchungaji huyo alitoa majibu ya kushangaza;
“Nilioteshwa na Mungu, Mkuu wa majeshi. Alinitaka kumtoa sadaka mtoto wangu kama kweli nilikuwa na imani naye, sasa kwa sababu kila siku hufanya mambo yangu kwa kusikia sauti yake, nikaifuatisha. Ni kama Ibrahim alivyofanya katika Biblia.”

Hata hivyo, imeelezwa kuwa kijana huyo alikuwa bado hajafariki na aliwahishwa hospitalini ambako anaendelea na matibabu wakati mchungaji huyo ameendelea kuwa mikononi mwa polisi ambao wanamhoji kabla ya kufikishwa mahakamani kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.

Wema Sepetu: Hata Aje na Bill Gates Kamwe Siwezi Mrudia Diamond, Kwanza Sitaki Kukumbuka Kabisa Kuhusu Huyu Mtu

0
0
KIAPO! Kuonesha kwamba hana mpango wa kurudi nyuma, staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platinumz’ amefungukia msimamo wake juu ya mwandani wake wa zamani, Wema Sepetu ‘Madam’ kwa kusema kuwa kamwe hawezi kumrudia tena, Risasi Jumamosi lina mkanda kamili

Licha ya Diamond kufunguka hayo, wawili hao wamekuwa na mapenzi ya vipindi, kuna wakati waliwahi kumwagana kisha kurudiana na hakuna aliyewahi kutoa tamko zito lakini safari hii Diamond amesema ndiyo basi tena!

TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo makini kilicho karibu na staa huyo, mara kwa mara Diamond amekuwa akijiwekea nadhiri ndani ya moyo wake na kusisitiza kwamba pamoja na kuwa maisha ya sasa huendeshwa kwa msingi wa fedha lakini hata kama ‘atafulia’ kiasi gani, ni bora afe maskini kuliko kurudiana na Wema.

“Diamond amekuwa akisema kila wakati kwa msisitizo kuwa kutokana na matatizo aliyokumbana nayo katika uhusiano wake kwa Wema, ni vigumu sana kurudiana naye wala kuwaza kama ipo siku anaweza kuwa naye, maana hakuna tena jambo geni asilolijua kwake,” kilisema chanzo hicho na kufunguka zaidi:

Kama hiyo haitoshi, Diamond anasema anaposema haoni kitu kipya  kwa Wema anamaanisha ndiyo maana utaona leo hakuna hata siku moja ambayo amewahi kuwaza kurudiana naye hata kama atatumia ushawishi wa fedha kwa kumpelekea makontena ya fedha, hawezi kukubali anasema bora afe maskini kuliko kushea kitanda kimoja na Wema.

DIAMOND ATHIBITISHA
Baada ya madai hayo, Risasi Jumamosi lilifanya jitihada za kukutana na Diamond uso kwa uso ambaye alithibitisha taarifa ambazo zilielezwa na mtu wake wa karibu:

Umeambiwa na nani hayo? Sipendi kuongelea sana hivi vitu lakini huo uliousikia ndiyo ukweli. Kwa sasa nawaza maisha yangu na mpenzi wangu Zari baada ya kupitia majaribu mengi kimapenzi enzi hizo.
“Huenda wengi wasiamini ninayosema lakini nafsi yangu haijawahi kuniongoza kukumbuka ya nyuma tena kama ilivyowahi kutokea awali.

Wengi wamekuwa wakiniuliza swali kama hili lakini sikupenda kujibu kwa kuwa nilihisi litaleta tafrani kwa mashabiki wangu, sioni sababu ya kuendelea kuulizwa kwenye media hivyo ukweli ni kwamba siwezi kurudi nyuma tena,” alisema Diamond


ASISITIZA KWA KUREKODI WIMBO
Kuonesha kweli amedhamiria kutogeuka nyuma, Diamond alisema kwa sasa yuko bize studio kurekodi wimbo na Nay wa Mitego (Emmanuel Elibariki) ambao utakuwa umesheheni majibu ya maswali yote ya kila kitu ambacho kilimkera kwenye uhusiano wake na Wema.“Naomba mashabiki wangu wawe na subira kwa maswali hayo yote, majibu yake yatapatikana katika project yangu na Nay inayokuja muda si mrefu,” alisema Diamond.

WEMA AJIBU MASHAMBULIZI
Alipotafutwa Wema kuhusiana na kauli hiyo ya Diamond, naye alijibu mashambulizi kwa kusema kamwe hawezi kurudiana na Diamond, hamfai hata kidogo na hata akimshawishi na  fedha nyingi kiasi gani hawezi kurudi nyuma.

Hata aje na Bill Gates (tajiri mkubwa duniani), aje na matajiri wote anaowajua yeye duniani kamwe siwezi kulamba matapishi, kwanza sitaki kukumbuka kabisa kuhusu huyo mtu, please naomba nisimuongelee kabisa huyo mtu,” alibwatuka Wema.

WAMEFIKAJE HAPA?
Wawili hao ambao walidumu kwenye uhusiano na kupamba vyombo mbalimbali vya habari, kila mmoja amekuwa akimtuhumu mwenzake kuwa msaliti lakini sababu kubwa ambayo Diamond amekuwa akiisimamia juu ya kummwaga Wema ni baada ya mrembo huyo kuhongwa gari na mwanaume mwingine.

Tishio La Ugaidi: TANESCO Na Vyuo Vikuu Wajihami......Wanafunzi,Wafanyakazi Watakiwa Kuvaa Vitambulisho Masaa Yote

0
0
Kusambaa kwa taarifa za uwezekano wa kutokea kwa shambulio la kigaidi katika miji ya Tanzania, ikiwemo Dar es Salaam na Mwanza, kumesababisha baadhi ya taasisi muhimu kama vyuo vikuu na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), kuchukua hatua za kujihami.

Taarifa zilizotufikia jana zilieleza kuwa Tanesco na baadhi ya vyuo, vimeweka taarifa ya tahadhari na kutoa masharti kwa wafanyakazi na wanafunzi, ya namna ya kujilinda.

Mtandao huu ulimuuliza Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Felchesmi Mramba, kuhusu hatua hizo ambapo alikiri shirika hilo kuchukua hatua za ziada kujihami na uwezekano wa shambulio hilo.

Mramba alisema wamechukua hatua hizo za kiusalama baada ya kuwepo kwa tetesi za uvamizi hasa baada ya kuwepo kwa tukio la nchi jirani ya Kenya, ambako wanafunzi 148 waliuawa.

“Kutokana na tishio hilo, tumeona ni vyema tuchukue hatua mapema… si lazima yatokee ndiyo tuchukue hatua, tumeona ni vyema kujihami kwa kuimarisha ulinzi katika vituo vyetu.

 “Kuna baadhi ya maeneo yetu ni maalumu na yakiwa na athari za kiusalama ni hatari kwa nchi nzima... hivyo ni vyema tuchukue tahadhari kubwa maana kunapotokea tatizo, huathiri nchi nzima,” alisema.

Vitambulisho
Alisema wamewaelekeza na kuwasisitiza watumishi wao kuimarisha ulinzi wao na katika maeneo ya kazi. “Kwa kawaida tuna vitambulisho vya ofisi lakini kuna watu wengine walikuwa hawavai, ila kwa sasa tumesema ni lazima kila mfanyakazi avae kitambulisho wakati wote,” alisema.

Katika Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IMF)  hali ya ulinzi ilikuwa imeboreshwa, ambapo kila mwanafunzi alitakiwa kuvaa kitambulisho chake awapo katika maeneo ya chuo, ili mgeni yeyote atambulike kwa haraka.

Uongozi wa chuo hicho ulichukua tahadhari kwa kuweka tangazo kumtaka kila mwanafunzi achukue tahadhari pale anapoona mtu ambaye ana shaka naye au kitu cha kutia shaka; pia taarifa hiyo iliwataka wanafunzi kuvaa vitambulisho vyao.

Ukaguzi
Mramba alisema mgeni yeyote atakayefika katika ofisi za shirika hilo kwa sasa ni lazima akaguliwe na ajulikane anatoka wapi na anaingia ofisini kwa sababu gani. Mbali na ofisini, alisema ukaguzi pia utafanyika kwa watu wote wanaoingia kwenye mitambo.

“Tumeimarisha askari wetu ili kuhakikisha rasilimali za Tanesco ambazo ni za nchi zipo salama.”

Katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), katika lango kuu la kuingilia ofisi mbalimbali za utawala, kumewekwa ulinzi na watu wote wanaoingia na kutoka, wamekuwa wakikaguliwa kwa vifaa maalumu tofauti na huko nyuma.

Matangazo ya tahadhari
Aidha UDSM, kama ilivyo IFM pia kumebandikwa tangazo lililotolewa na Kaimu Naibu Makamu Mkuu wa Chuo hicho (Utawala), Profesa Cuthbert Kimambo, likieleza kuwa hatua madhubuti zinachukuliwa na zitaendelea kuchukuliwa katika kuimarisha ulinzi.

Alisema kutokana na taarifa za tahadhari kuhusu matukio ya uhalifu yenye taswira ya kigaidi katika maeneo yenye mikusanyiko ya watu, ni jukumu la kila mwana jumuiya ya chuo hicho kuwa macho kusaidia kuimarisha ulinzi na usalama.

“Baadhi ya hatua zinaweza kuleta usumbufu kwa wengi wetu. Taarifa zitatolewa inapowezekana, lakini tunaomba uvumilivu na ushirikiano wenu ili kuhakikisha usalama wetu,” ilisema taarifa hiyo ya Profesa Kimambo.

Mawakili wa Gwajima Wajibu Mapigo Waiandikia Barua Polisi Kuhusu Uhalali wa Kumtaka Gwajima Awasilishe Nyaraka 10 za Mali Zake

0
0
Mawakili wa Askofu wa kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, wameandika barua kuliomba Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, kuandika kimaandishi nyaraka wanazozihitaji azipeleke pamoja na vifungu vya sheria vinavyomtaka awasilishe nyaraka hizo.

Barua hiyo iliyosainiwa na Wakili Peter Kibatala iliwasilishwa jana mchana katika jeshi hilo, ikiwa ni siku moja baada ya jeshi hilo kumtaka Askofu Gwajima kuwasilisha nyaraka 10, Aprili 16 mwaka huu watakapoendelea na mahojiano.

Gwajima aliitwa kuhojiwa na jeshi hilo mara mbili kutokana na kufunguliwa jalada la malalamiko ya kumkashifu Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo.

Katika barua hiyo, mawakili hao kwa niaba ya mteja wao wanaliomba jeshi la polisi kumwandikia barua rasmi kimaandishi, Gwajima wakiainisha nyaraka wanazozihitaji pamoja na vifungu vya sheria vinavyotumika na jeshi hilo kutaka nyaraka hizo.

Mawakili hao wanasema watashukuru kupata hati hiyo ambayo hawaijui jina lakini wanaamini jeshi la polisi litafahamu jina la kisheria la nyaraka husika inayotumika kumtaka Gwajima awasilishe nyaraka wanazozihitaji.

Aidha wanasema Askofu Gwajima atakapopata nyaraka anayoihitaji atatimiza wito na kuchukua hatua stahiki za kisheria.

Tukiwaendekeza CHADEMA: Bunge Zima Litajaa Wasanii wa Bongo Fleva & Movie!

0
0
Hii tabia ya CHADEMA kutumia wasanii wa bongo fleva & movie kisiasa ni upunguani wa hali ya juu sana.

Iweje leo hii kisa tu chama kinataka ruzuku ya kutosha kione ni vyema na sawa kuokota tu vijana wasio kuwa na maadili kutoka kwenye tasnia za muziki na movie na kuwanadi ili wawakilishe wananchi bungeni!? Huu ni wehu na kukosa kufikiri!

CHADEMA wamezindua mpango uitwao "Kujaa bungeni kivyovyote" na haya ya kujaza wasanii ndio mkakati wa kufanikisha mpango huo!

Kwa taarifa sahihi kutoka CHADEMA makao makuu, wafuatao wanatarajiwa kusimamishwa na CHADEMA kwenye majimbo ya uchaguzi oct mwaka huu:

1) Irine Uwoya - Jimbo la Mtera

2) Prof Jay - Jimbo la Mikumi

3) JB (bongo movie) - jimbo la Kigamboni

4) Sugu - Jimbo la Mbeya Mjini

5) Juma Nature - Jimbo la Temeke

6) Dully Sykes - Jimbo la Ilala

7) Fid Q - Jimbo la Magu

Je, wewe Mtanzania una kubaliana na hawa CHADEMA kukupa wawakilishi wa aina hii? Maana CUF na NCCR hawana kauli huku bara ya kupanga wagombea wanaojitambua na kujua wajibu wao kwa wananchi.

Sakata la Askofu Gwajima Lina Maslahi Gani Kwa Taifa ? Lakomaliwa Kuliko Hata Waliotafuna Mabilion ya Escrow

0
0
Imetusikitisha sana kumbe nyuma ya kashfa alikuwa akidaiwa Askofu Gwajima juu ya Kardali Pengo ilikuwa ni ufunguo tu wa serikali kuingilia Imani na Utendaji wa Viongozi wa kidini (Askofu Gwajima) Iweje kashfa iliyokuwa inamuhusisha Kardinali Pengo na Askofu Gwajima ipelekee kuhojiwa na Kudaiwa alete nyaraka zinazohusiana na mapato na matumizi ya Kanisa la ufufuo na uzima, Kwani makanisa huwendeshwa na ruzuku kutoka serikalini !?, Je!

Kuna kanisa au dhehebu lolote la kidini wawe waislam au wakristo wameisha wahi kuhojiwa kuhusu mapato na matumizi ya madhehebu(makanisa/misikiti) yao?

Wanapohoji nyaraka za helicopter kwani! Iliingia nchini kwa uficho!?.... Kwanini wasiene kuuliza TRA kama helicopter hiyo haikulipiwa ushuru ?

Kumbe tumegundua serikali na wanasiasa walioko madarakani wanaajenda ya siri juu ya Askofu Gwajima. Nchi yetu ina mambo mengi ya kushughulikiwa na serikali ili kutatua matatizo ya wananchi kama vile vifo vya albino, migogoro ya wakulima na wafugaji, matumizi mabaya ya fedha(ESCROW) na mikataba mibovu isiyo na manufaa kwa mtanzania mmoja mmoja .

Mambo kama haya kama ya Sakata la Escrow na Epa  yangekuwa yanafuatiliwa kwa karibu kama anavyofuatiliwa Askofu Gwajima ingeleta tija kwa uongozi uliopo madarakani na Imani kwa wananchi juu ya serikali yao.

Kitanda cha Mtoto Mtarajiwa wa Diamond ni Madini Tupu, DIAMOND Akionyesha Hadharani na Kusema 'ANYTHING FOR HER'

0
0
Kitanda cha mtoto wa Taifa kama asemavyo mwenyewe Diamond kuwa huyo mtoto ni wa Taifa ndio icho hapo chini kwenye picha ..uujauzito sasa unaelekea miezi 5 si mchezo...


Picha: HAMISA Mobeto Ajifungua Mtoto wa Kike, MIMBA yake ilikuwa SIRI Kubwa, Azaa na Mtangazaji Maarufu

0
0
Modo maarufu na muigizaji chipukizi nchini, hamisa mobeto amejifungua mtoto wa kike. Staa huyo anayechipukia amejifungua ivi karibuni na kuwashangaza wengi kwani mimba hiyo ilikuwa na usiri mkubwa tofauti wafanyavyo mastaa wengine (zari ), Mobeto Amezaa mtangazaji maarufu Majizo ambae ni mkurugenzi wa EFM

Hongera sana, duuh!! Ila hii mimba wambea wengi walikuwa hawajaipata, khaa!! Utatuua kwa presha aisehh loh, haya sasa nawapa assignment wambea wenzangu kumtambua au kumtaja baba mtoto wa hamisa

UTABIRI: Lady Jay Dee Kuolewa na Mwanaume Tajiri..Lakini Afya yake Itadhoofu

0
0
Baada ya Kutemana na aliyekuwa Mpenzi wake wa muda Mrefu Gadner G Habash Sasa Lady Jay Dee Kuolewa na Mwanaume Tajiri.

Hayo yalisemwa na Mtabiri wake wa Nyota ambae alimkaribisha kwenye kipindi chake cha Diary ya lady Jaydee ambapo huweka wazi mambo kuhusu Maisha yake .

Mbali ya kuolewa Mtabiri huyu ametabiri Lady Jay Dee Mwaka Huu Utakuwa wa mafanikio kwake Kipesa kupitia Muziki wake lakini kiafya atakuwa na homa za mara kwa mara na kuwa dhoofu kiafya kitu ambacho kitamfanya kufikiria kifo ...

~Gazeti la Kiu

Dr Kessy Anakuletea Dawa za Kutengeneza Hips, Makalio, Nywele na Nguvu za Kiume Kwa Kutumia Dawa za Asili zisizo na Kemikali

0
0


Kifaa cha Kurefusha uume Kinachouzwa 160,000
Pendeza na Dr Kessy Products 
Ni dawa za Asili zisizo na Kemikali wala madhara yoyote kwa Binadamu, zimetengenezwa kwa kutumia mimea na matunda mbali mbali kukupa matokeo ya Haraka

1.Refusha Nywele na zisikatike  45,000/
2.Ondoa Mvi Sugu kichwani  45,000/
3.Toa Michirizi Mapajani, Chunusi na Madoa mwilini 40,000/
4.Punguza tumbo na Manyama uzembe 45,000/
5.Mkanda wa Kufunga Kupunguza tumbo 70,000/
6.Tengeneza Shepu Hips na Makalio  45,000/ ,Vidonge 80,000/
7.Ongeza Nguvu za Kiume  Jelly 45,000/ , Vidonge 60,000/
8.Ongeza Ukubwa wa Maumbile ya kiume Jelly 80,000/ , Mashine 160,000/
9.Kuongeza Mwili Mzima 40,000/
10.Kupunguza Mwili 45,000/
11.Kupunguza Maziwa na Kuyasimamisha 40,000/
12.Ongeza Mguu uwe wa Kupendeza 45,000/
13.Rudisha usichana ama Bikira 55,000/
14.Ongeza Hamu ya Kula 40,000/
15.Ongeza Hamu ya Kufanya Mapenzi 55,000/
16. Fanya mwili Kuwa Soft 60,000/
17. Dawa ya kutoa Michububuko kwenye mapaja 45,000/
18. Dawa ya kutoa maji maji sehemu ya siri na kukuacha mkavu 55,000/

TUNAPATIKANA DAR NA MIKOA YOTE, HUDUMA ZINAFIKA POPOTE ULIPO , 
DAR TUPO KARIAKOO MSIMBAZI NA POSTA  MPYA

PIGA SIMU: 0719955528, 0756259180 au 0785371237

Msanii wa bongo fleva RICH MAVOKO Ajibu TUHUMA za Kujichubua Mwili Mzima na Kuwe Mweupe

0
0
Msanii wa bongo Fleva Rich Mavoko amekanusha tuhuma za kujichubua Baaada ya blog hii kuweka Picha zake Hapa zikionyesha  Kuwa Mweupe tofauti na zamani...

Rich Mavoko amefunguka na Kusema Haya:
 “Lazima tuangalie wakati hizi picha zilipigwa, hio picha nikiwa na dred Locks ni yazamani sana na siku na simu bora wala application za kuedit picha kama sasa, Hii picha mpya nimepiga na Iphone” .
Rich Mavoko ameongezea kuwa “Hata maisha yangu yamebadilika,so ni kung’aa tu kwa mtu na sio kujichubua, wanaonijua watasema sijabadilika zaidi ya kung’aa tu“.

HAWA wa Nitarejea Afunguka "Wimbo wa Nitarejea wa DIAMOND Nauchukia Sana Umeniharibia Maisha Yangu

0
0
Unakumbuka Video ya Nitarejea ya Diamond? Basi yule msichana aliyeshirikiana naye katika huo wimbo hali yake si nzuri kisanii na kimaslahi pia kiasa cha kusema kuwa anauchukia huo wimbo kwani ndo umemuharibia Maisha
Hawa akihojiwa na Mlimani TV amefunguka na kusema kuwa Pamoja na Wimbo huo kuwa ndio uliomtoa Diamond Kimuziki lakini Diamond hakuwahi kumpa Hata Shiling 10 , Japo ameshawahi kumfuata na kumuomba msaada wakati tofauti tofauti lakini haikuwezekana kupata huo msaada ....Hawa amesema alitegemea nae angetoka lakini ameishia kuwa na maisha ya Dhiki huku mwenzake akitengeneza Hela za Maana ..

Alipoulizwa Kuhusu tuhuma za kutumia Madawa ya Kulevya baada ya kuona mambo hayaendi vizuri  Hawa amesema hakuwahi kutumia Madawa ya Kulevya bali alijiingiza katika unywaji wa pombe sana baada ya Mwanaume aliyempa Mimba Kumkimbia hivyo alianza matumizi ya pombe kupunguza Mawazo ..

Hawa anasema Hamchukii Diamond ila Anapenda kumwambia akumbuke alipotoka na Arejee Nyumbani....

AL SHABAAB May Not be Lucky next Time - See What UHURU/ RUTO’s Govt is Planning

0
0
Al Shabaab terrorists may be in for a rude shock next time they attack a university or school in Kenya like they did last week in Garissa.
The Government of President Uhuru Kenyatta and his Deputy, William Ruto, was contemplating introducing military training in schools as part of the education curriculum.

This was revealed by a senior Government official who said that the President and his Deputy were considering the proposal as a way of addressing insecurity in schools and keeping students safe.

The idea was supported by several leaders, among them Gongoni Ward Representative, Alfred Kiraga, who said that the education system should encompass a mandatory paramilitary training similar to that in Israel and other countries to make the youth patriotic and for self defence to avoid a Garissa-like situation where 147 students were massacred like flies by only 4 terrorists.

“There is need to make changes in the country’s education curriculum to make it mandatory for all citizens to undergo paramilitary studies. This will address security concerns our country is faced with,” said Kiraga.

If the proposal goes through, there would be no need for Recce Squad in case the Al Shabaab attack a school in Kenya.


Viewing all 104429 articles
Browse latest View live




Latest Images